Search This Blog

Monday, March 23, 2020

ABEE SHEMEJI SEHEMU YA 6/10


ABEE SHEMEJI
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 6 KATI YA 10
*******

Muhimili wa maisha ya Ahmed uliyumba kwa kiasi cha kutosha,kila kitu kwake kilikuwa kimevurugika.Kuanzia maisha mpaka ndoa yake kwa ujumla,mwanamke aliyemuamini katika maisha yake yote, akaamua kumuoa na kumuweka ndani,ndiye aliyemuumiza mtima.Bado hakutaka kuamini kilichotokea,akatamani siku zirudi nyuma abadilishe kila kitu lakini hilo lisingewezekana hata
kidogo!Licha ya kuamini kwamba, ipo siku atasahau na maisha yataendelea lakini aliamini ingekuwa vigumu kusahau, kwake kitendo hiko alikifananisha na donda ndugu kamwe hakiwezi kupona,ndiyo maana saa kumi na moja ya asubuhi kulivyokucha akaamka na kuondoka zake,niya yake ikiwa ni kwenda kukaa mbali kabisa na nyumbani,ambapo huko alitaka achukuwe maamuzi kama mwanamme.
Pombe alizokunywa usiku wa jana yake,zilimfanya ahisi kichwa chake kizito lakini hilo halikumfanya ashindwe kuendesha gari mpaka Goba,Saisai.
Saa moja kamili akafika eneo hilo na kuagiza mchemsho wa kuku ambao hakumaliza kabisa kwani hamu ya kula ilipotea,kichwani kwake akawa ametawala Yusrath,kifupi alitokea kumchukia ghafla.Alivyotaka kuagiza pombe akasita kidogo,hakutaka kufanya hivyo sababu aliamini pombe sio suluisho la matatizo aliyokuwa nayo!
“Niletee Pepsi ya baridi sana”
Siku hiyo Ahmed,alitaka kukaa mwenyewe ili azungumze na akili yake mwisho wa siku atoe maamuzi ya mwisho,akafikiria kuishi na Yusrath amsamehee lakini moyo wake ukakataa akiamini kabisa ni lazima mwanamke huyo,atamfanyia kitu kibaya siku moja!Picha mbalimbali zikawa zinapita kichwani kwake,akitafakari mustakabadhi mzima wa maisha yake,mwisho wa siku akahitimisha kwamba atoe talaka ili aishi mwenyewe,alivyowakumbuka watoto wake Faad na Faisal,moyo ukamuuma zaidi.Hapo ndipo wazo hilo,akalitupilia mbali.Ilivyoletwa Soda,akaiweka mdomoni na alivyoishusha ikawa imebaki nusu.
“Mimi ni mwanamme,lazima nitoe maamuzi ya kiume”
Siku hiyo Ahmed hakutaka,kumshirikisha rafiki yake yoyote yule kama siku zote.Ndiyo maana alikaa peke yake,ilivyogonga saa tatu kasoro,akasimama kwa kasi akionekana kama mtu aliyepata wazo kabambe,akatembea kuliendea gari lakini kabla hajalifikia aliitwa,alivyogeuka akamuona dada wa jikoni anamkimbilia,akimfuata alipo.
“Umesahau kulipa”
“Oooh sorry”
Ahmed,akaingiza mkono kwenye mfuko wa shati na kutoa noti ya shilingi elfu kumi.
“Chenji,sijui kama nitakuwa nayo.Hauna hela ndogo?”
“Usijali,kaa nayo.Nitakuja kuchukua siku nyingine”
Ahmed akamaliza,akaingia ndani ya gari na kuliwasha.
Hapo hakutaka kubaki tena,wazo lililomjia ni moja tu,kurudi nyumbani na kuzungumza na Yusrath.Akiwa katikati ya safari ghafla akakumbuka kitu cha umuhimu sana,kiwanja alichomwambia Yusrath anunue akiwa jijini Mwanza.Kitu cha kwanza alichotaka kukifanya ni kuanza ujenzi mara moja na ikiwezekana aombe hata mkopo benki afanye hivyo,barabara haikuwa na msongamano sana, ndiyo maana haikuwa kazi ngumu kufika Ubungo Mataa, ambapo hapo alikunja kulia na kunyoosha,alivyofika ‘Riverside’ akalala na kona ya kulia.
Dakika tatu badaye akafika nyumbani kwake,akapiga honi, muda mfupi geti likafunguliwa na Hadima,kitendo cha kuzima gari alitoka na kupita seblen bila kuangalia popote,akanyoosha mpaka chumbani na kujibwaga kitandani.Akashusha pumzi ndefu, ndani ya sekunde mbili mlango ukafunguliwa Yusrath akaingia,hiyo ikamfanya Ahmed akae kitako kitandani.
“Mme wangu,dada ako amefika.Hata kumsalimia?”
Yusrath akauliza na kusogea karibu.
“Sikia,chukua kila kilicho chako.Pakia kwenye begi nikurudishe kwenu”
“Ahmed mme wa…”
“Nadhani umenisikia,pakia kila kilicho chako weka kwenye gari nikupeleke kwenu.Kwa sasa hivi sitaki kukuona,akili yangu ikitulia nitakuja kukuchukua”
Ahmed alizungumza kwa sauti ya chini,akiwa makini kabisa yupo siriazi hacheki.Aliongea kwa uchungu kiasi kwamba, machozi yalianza kumlenga,anamtizama Yusrath ambaye kwa wakati huo alianza kupiga magoti.
“Mme wangu naomba unisamehe”
“Nimekusamehe,siku nyingi sana.Lakini kwa sasa hivi naomba nikae mwenyewe”
“Hapana usi….”
“Yusrath please”
Kitendo cha kumalizia sentensi hiyo,alisimama na kufungua kabati ambapo huko alianza kutoa nguo za Yusrath, kuanzia moja baada ya nyingine,akatembea pembeni na kuvuta begi kubwa akaingia bafuni na kutungua chupi zake pia.
“Ahmed naomba unisamehee mme wangu,sitorudia tena”
Yusrath,tayari alianza kulia machozi!Akasimama mbele ya Ahmed,akamshika mikono ili asiendelee kufanya anachokifanya,hiyo ilimfanya Ahmed amkate jicho kali bila kumjibu chochote.
“Niache,nimekwambia niache.Usinishike…”
“Nitaenda wapi lakini?Nitakuwa mgeni wa nani?”
“Utakuwa mgeni wa baba ako mzazi,Yusrath niachie”
“Naomba nisamehe Mme wangu”
“Nilishakwambia,nimekusamehee.Nachokuomba ukapumzike kwanza kwenu,nitakuja kukufata”
“Siwezi bab..y”
“Utaweza tu”
Kile alichokuwa anazungumza Ahmed,alikimaanisha sababu hakuonesha punje ya mzahaa hata kidogo.Hapo ndipo Yusrath alipoamua kutoka na kutembea mpaka seblen huku akilia,akamuendea Hajrath akimlalamikia kwamba Kaka yake,anataka kumfukuza.
“Nio..mbee msamahaa kwa kaka yako,nakuomba Wifi yangu.Labda wewe atakuelewa”
“Kuna nini?”
“Nio..mbe msamahaa tafadhali”
Butwaa alilopigwa nalo Hajrath halikuwa na kipimo chake,hiyo ilimfanya asimame kutoka kwenye kiti na kumshika Yusrath mikono.
“Kuna nini?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Hajrath Mpilla, safari hii ilibidi achungulie kwenye korido ambayo alimuona Ahmed amepitiliza bila kuwaangalia,kuna kitu kibaya ambacho alianza kuhisi,Yusrath alilalamika huku akilia machozi akimuomba Hajrath amuombee msamahaa.
“Umefanya nini?”
Kabla ya Yusrath kujibu sentensi yake,Ahmed akatokeza seblen.Kitendo cha kumuona Hajrath kilimshtua akaganda na kuhisi kama amepigwa na ubaridi kwenye uti wake wa mgongo!
“Umefuata nini hapa?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutupiwa Hajrath.
“Nimekufuata wewe”
Hajrath akajibu kwa kujiamini,akimtizama Ahmed machoni.
“Naomba wote mtoke,Yusrath.Ingia kwenye gari nikupeleke kwenu”
Hali ya Ahmed ilikuwa tayari imebadilika,kutoka kwenye sauti ya chini mpaka juu.Macho yake mekundu,hiyo ilimfanya Hajrath aanze kurudi nyuma kidogo sababu alielewa dalili za Ahmed akikasirika na muda wowote kuanzia wakati huo,makofi yangerushwa.
“Kwani kuna nini?”
Hajrath akahoji kwa mara nyingine baada ya kuona yupo mbali na Ahmed,kilichokuwa kinaendelea ilikuwa ni kama filamu ya bongo movie!Msimamo wa Ahmed ulibaki palepale kwamba Yusrath anatakiwa kuondoka haraka iwezekanavyo kabla hajafanya kitu kibaya,hilo lilikuwa wazi kutokea sababu alidiriki kusema kwamba angeendelea kubaki, wangegawana majengo ya serikali yeye aende jela Yusrath apelekwe Monchwari.
“Sitaki kwenda Jela,please.Twende,nikupeleke nyumbani kwenu,nawewe….”
Ahmed akamgeukia Hajrath.
“Sina kumbukumbu kama niliwahi kukuonesha hapa napoishi,nachokuomba iwe mwanzo na mwisho kufika”
Kauli hiyo ilimfanya Hajrath,ashangae!Na aogope kwa wakati mmoja,Yusrath hakuwa na jinsi zaidi ya kutoka nje akiwa na watoto wake mkononi mwake,akaingia ndani ya gari! Ahmed akafuata.Hadima aliyekuwa pembeni,alishuhudia kila kitu akaingiwa na huruma akatamani aingilie kati amuombee Yusrath msamahaa lakini akaogopa kwani hakuwahi kumuona Bosi wake akiwa katika hali kama hiyo tangu amfahamu,hiyo ilimtisha zaidi maana palikuwa hapatoshi.

Siku hiyo Ahmed alikuwa ametibuka sio kawaida na alichotaka yeye ni Yusrath asiwepo eneo hilo,ndiyo maana akaanza kutembea mpaka karibu na gari!
“Hadimaaa,njoo ufungue geti”
Hadima akatokeza lakini badala ya kuelekea getini, yeye akasogea karibu na gari,kuna kitu ilielekea alitaka kumwambia Ahmed.
“Baba,msamehee Mama.Hatorudia tena”
Sentensi hiyo ilimfanya Ahmed asitishe zoezi la kuingia ndani ya gari akabana meno yake kwa hasira na kumtizama Hadima.
“Nawewe,jiandae kuondoka hautokuwa na sababu ya kubaki hapa.Anza kujiandaa nikirudi uniambie unadai kiasi gani”
“Lakini Ba…”
“Kafungue geti,nikirudi nisikukute.Nawewe Hajra nikirudi nisikukute”
Kimbelembele cha Hadima kikawa kimemponza bora angepiga kimya,akaanza kujuta ni kwanini alizungumza hakuwa na jinsi zaidi ya kufungua geti,Yusrath akaingia ndani ya gari na safari ikaanza mara moja!
“Kabla sijasahau,naomba documents”
Ahmed akavunja ukimya wakiwa ndani ya gari,anapiga gia.
“Documents zipi?”
“Za kiwanja”
“Bado sijapewa”
“Hujapewaaa?Kivipi?Mbona sikuelewi?”
“Sijajua”
“Twende kwenye hiko kiwanja”
Ghafla Ahmed akabadilisha mawazo,badala ya kutaka kwenda Ilala nyumbani kwa wazazi wake na Yusrath akataka kwenda kwenye kiwanja chake,akakione ingawa hakuwa ana uhakika kama Yusrath alinunua kweli ama pesa aliyomtumia alimpa hawara wake Sameer,japokuwa aliomba Mungu jambo analofikiria lisiwe kweli maana angepiga mtu mpaka akaua na kumzika siku hiyohiyo.
“Kipo sehemu gani?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Ahmed tena kwa ukali.
“Mbezi”
“Mbezi?!Sio tena Kigamboni?”
“Ndio Mme wangu,kipo Mbezi”
“Unapafahamu?”
“Napafahamu ndio”
Hakukuwa na mjadala mwingine zaidi ya Ahmed kutaka kuelekezwa ni wapi kiwanja chake kilipo ili aanze ujenzi mara moja,kwa kuwa Yusrath aliamini kwamba kiwanja kipo, hakukua na tatizo la kutoa maelekezo,safari ya kuelekea Mbezi ikaanza mara moja!
Hakukuwa na mtu hata mmoja kati yao aliyemuongelesha mwezake, isipokuwa sauti ya radio ilikuwa inasikika ndani ya gari,dakika arobaini na tano baadaye wakawa wamefika Mbezi Mwisho,kazi ya Yusrath ikawa ni kuonesha njia,mara kata kushoto mara panda kulia,mwisho wakatokea kwenye ukuta mkubwa kumaanisha kwamba mbele hakuna njia.
“Nahisi sio huku”
Yusrath alizungumza,kumaanisha kwamba wamepotea njia.Hiyo ilimfanya Ahmed ashushe pumzi ndefu iliyochanganyika na kero,hakuwa ana uhakika kama Yusrath anamfanyia maigizo ama amepotea kweli.
“Nikuulize kitu Yusrath?”
“Niulize Mme wangu”
“Kiwanja kipo,ama hakuna?Mimi ni mtu mzima,usinifanye fala.UMENIELEWA”
Ahmed hakutaka kuzungushwa kama mtoto mdogo,ndiyo maana akataka apewe jibu lililonyooka kuliko kuletewa maigizo kwani tangu walivyoingia mitaa ya Msakuzi,Yusrath alionekana kutokuwa na uhakika na sehemu anayoenda.
“Kipo Mme wangu,ila njia zimenichanganya”
“Zimekuchanganya kivipi?”
“Huku nilikuja mara moja”
“Mpigie dalali,aliyekuonesha kiwanja.Sijui ndugu yako huyo”
Moyo wa Yusrath ukapiga kwa nguvu,tayari kitumbua kilianza kuingia mchanga.Na endapo asingeoneshwa kiwanja hiko kilipo ni lazima ingejulikana pesa alimpa Sameer ili anunue kiwanja na sio dalali ama ndugu yake kama alivyoeleza hapo,awali.
“Kipo,kwa huku nyuma.Nimekumbuka”
Gari,likawashwa.Safari ya kuzunguka ikaanza tena,Yusrath akawa ana kazi ya kuangalia viwanja,bahati nzuri akauona mnara mrefu, hapo ndipo kumbukumbu zake zikarudi,baada ya kuukumbuka mnara huo.
“Kunja hapa”
Ahmed,akatii amri.Wakanyoosha barabara ambayo ilikuwa nyembamba kidogo,wakakunja kushoto!Ambapo pembeni kulikuwa na miti ya miarobaini na miembe mikubwa.
“Ndio hapa Mme wangu”
Ahmed,akapaki gari.Wote wakashuka,uhakika wa Yusrath ulikuwa wote ni asilimia mia moja kwamba kiwanja hiko kilinunuliwa na Sameer,ndiyo maana akapata ujasiri wa kuingia katikati wakiwa wote na Ahmed.
“Mwisho wa mpaka ni hapa”
“Heka ngapi?”
“Moja na nusu”
“Hujapewa,karatasi zozote?Mjaandikishiana?”
“Hapana Mme wangu”
“Sasa,akitokea akasema hujanunua.Utasema nini?Utaweza kutoka kweli?Inabidi nionane na mwenyekiti wa mtaa huu,umpigie simu huyo dalali sijui ndugu yako.Tuje tuandikishiane ili amaliziwe pesa zake.Yusrath usifanye mchezo na mambo ya ardhi,mpigie simu huyo aliyekuuzia”
Hakuelewa maneno hayo,yanamtisha Yusrath kwa kiasi cha kutosha.Yusrath alisimama wima lakini akahisi kama anaishiwa nguvu za miguu,tumbo la ghafla likaanza kumuuma.Kichwani kwake alifikiria vitu vingi,hakuelewa ni kitu gani akifanye kwani mipango yote ya kiwanja hiko alikuwa nayo Sameer ambaye kwa wakati huo,hakujua ni wapi alipo.Hapo,ndipo alitamani ardhi ipasuke aingie ndani,imfunike!

******
Hata siku moja hakutaka kuamini kwamba kuna siku atahukumiwa jela,kwa kosa la kuuwa.Hakukusudia lakini ilikuwa ni lazima sheria ifuate mkondo wake,japokuwa wanasheria wengi walimtetea lakini ilishindikana mwisho wa siku alihukumiwa kwa mujibu wa Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,alijuta lakini baadaye aliamini kila kitu hutokea kwa sababu maalum. NECKA GOLDEN aliamini siku moja akitoka gerezani ni lazima afunge ndoa na Ahmed, ambaye alisababisha mpaka yeye ahukumiwe.Moyo wake ulitokea kumpenda Ahmed kwa dhati kwenye kila kitu,kama alifungwa gerezani kwa ajili yake iweje aogope kupambana na mwanamke yoyote yule ambaye atagundua ana mahusiano na Ahmed.
Aliapia angerudi tena gerezani kwa ajili ya penzi la Ahmed.Siku zilizidi kukimbia hatimaye akazoea maisha ya gerezani,cha kushangaza Ahmed hakuwahi kumtembelea hata siku moja hiyo haikumuumiza sana kwa kuwa ndugu zake walisafiri kutoka Kigoma mpaka Arusha ili kumjulia hali, wakimpa moyo kwamba ni lazima angetoka kwani siku hazigandi,hilo aliliamini.
Ingawa alikuwa gerezani lakini wafungwa wote walikiri kwamba Necka Golden,alitingisha kwa urembo!Alikuwa ana mwili mdogo lakini mzuri wa sura,hiyo ilifanya wanawake wasagaji wamtake kimapenzi lakini hawakufanikiwa kwani hakutaka kabisa kujihusisha na tabia hiyo mbaya.Maisha yalizidi kusonga mbele,akiamini ipo siku angekuwa huru na kurudi tena uraiani akutane na Ahmed ili wafunge ndoa, hiyo ndio ilikuwa ndoto yake kubwa.
****
Ilikuwa ni mnamo tar 14-10, siku ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa.Ni tarehe ambayo asingeweza kuisahau kabisa katika maisha yake,Rais alivyotoa msamaha kwa wafungwa hamsini katika gereza alilokuwa na jina lake kuwepo.Hakuelewa amshukuru vipi Rais huyo,moyo wake ulipiga kwa nguvu na kuona kama hakukuchi,kitu alichokipanga baada ya kutoka ni kuchora tarehe hiyo mkononi mwake yaani ‘Tatoo’ ili iwe kama kumbukumbu katika maisha yake.
Habari za kuachiwa kwa msamaha wa Rais,zikawafikia ndugu zake wakafunga safari,asubuhi ya siku hiyo wakafika na kumchukua.
“Nahitaji kwenda Dar es salaam”
Necka Golden alisema,wakiwa katikati ya safari wanarudi mkoani Kigoma!Hiyo ilifanya ndugu zake,wamshangae.
“Dar kuna nini?”
“Kuna mtu naenda kumuona”
“Necka,subiri tufike kwanza”
Necka Golden,kwa wakati huo alimuwaza AHMED KAJEME tu,na sio mtu mwingine yoyote yule.Alikuwa yupo radhi,atoe uhai wa mwanamke yoyote yule ambaye atahisi ana mahusiano na Ahmed,barafu wa moyo wake!



Haukuwa utani kama ndugu zake walivyodhani kwamba angefika, angebadili mawazo ya kutaka kwenda jijini Dar es salaam,kumbe haikuwa hivyo.Kitendo cha kuwasili mkoani Kigoma na kusalimiana na ndugu zake, usiku huohuo akawaambia kuwa anataka kusafiri mpaka Dar es salaam kesho yake,akitoa sababu kwamba kuna jambo la muhimu anaenda kufuatilia huko,hivyo wamruhusu!Kumbe haikuwa hivyo.alitaka kwenda kumsaka Ahmed kwa wudi na uvumba,kuhusu kufikia wapi? Angekula nini? Hilo lilikuwa juu yake na ingefahamika huko mbele ya safari akifika.
“Mbona hutaki kutuambia kuna nini?”
Mama mzazi ilibidi afunguke na kuuliza swali hilo, baada ya kuona binti yake king’ang’anizi.
“Mambo ya kazi”
“Mambo ya kaziii?!”
“Ndio Mama”
“Kazi gani na leo ndio umetoka huko”
“Nilihaidiwa kazi Mama,naomba mniruhusu”
“Hapana”
“Mama,mimi nitaondoka kesho asubuhi”
Necka Golden,aliendelea kukomaa.Akitaka apewe ruksa ya kusafiri, mpaka jijini Dar es salaam na alikuwa yupo tayari hata kutoroka, endapo wangegoma kumpa ushirikiano,kilichomkwamisha ilikuwa ni pesa ya nauli ndiyo maana akawaambia wazazi wake.Kama angekua na pesa ya kusafiri, siku hiyohiyo angeaga na kuondoka zake kwa njia yoyote ile.Ubishi ulikuwa mkubwa,Mzee Golden Baba yake mzazi pamoja na ukali wake wote lakini hakuweza kumzuia Necka,kila mtu akabaki kinywa wazi.
“Hakuna kwenda,nimeshasema”
Mzee aliongea kwa ukali siku hiyo Seblen.
“Nitaenda Baba”
“Ole wako,nisisikie huo Upumbavu,umetoka kwenye matatizo.Halijatulia hili, unataka tena kuleta shida nyingine,wee mtoto una laana wewe sio bure”
Hapo Necka,alinyamaza kimya na kuingia chumbani kwake bila kujibu chochote,akimuacha Baba yake nyuma anamuita.Hakusikia,alivyofika tu chumbani kwake, akaanza kutafuta nguo zitakazomfaa,kwa kuwa aliongezeka kidogo mwili, baadhi ya nguo zilimbana,akatembea mpaka kwenye nguo za binamu yake,hapo ndipo akakumbana na nguo zinazomkaa vizuri,akatafuta begi dogo na kuanza kuziingiza vizuri ili kesho yake,asubuhi na mapema aanze safari ya kuelekea jijini Dar es saalam,akamsake Ahmed Kajeme!Mlango,ulifunguliwa Mama yake akaingia akiwa katika sura ya uzuni kidogo.
“Necka mwanangu,mimi mama yako.Nisikilize”
“Mama,niacheni”
“Sio kwamba hatutaki wewe uende huko”
“Bali nini? Mama,naomba mniache nishasema naenda”
Mama alitafsiri jibu hilo kama Kiburi,akaelewa fika kwamba binti yao ametoka jela akiwa na tabia za ajabuajabu,kama Mama hilo likamuuma sana mtima.Akaondoka zake na kunyoosha mpaka seblen ambapo huko alimueleza Mumewe.
“Ni mapepo hayo,mwache mpuuzi mkubwa”
Baba badala ya kutoa suluisho,akatoa hukumu moja kwa moja, akasonya!
“Lakini ni mtoto wetu”
“Kwahiyo?Atuburuze anavyotaka hana adabu,bora angebaki huko huko”
“Sijasema hivyo”
“Sasa una maana gani?”
“Tumruhusu afanye anachotaka”
Sentensi hiyo ilimfanya Mzee Golden amkate mkewe jicho kali,hakujibu chochote badala yake alisimama wima na kunyoosha mpaka chumbani.Mkewe,akamfuata nyuma mpaka chumbani, ambapo huko ilibidi amshawishi kama Mama,alifanya juu chini ingawa alielewa anafanya makosa.Mama ilibidi akae upande wa mtoto wake.
“Mimi siwezi,kama umemruhusu wewe.Ni wewe,mimi nitoe”
“Tumpatie hata pesa kidogo”
“Za nini?Nimesema siwezi”
Mama akanyamaza,alichokifanya ni kusimama kutoka kitandani mpaka kwenye kabati akatoa mkoba wake,akafungua zipu na kutoa pesa.
“Unataka kufanya nini?”
“Kuna karatasi nazitafuta”
Akadanganya!
“Nisisikie unampa hela yoyote”
Mama,akafinyanga shilingi elfu sitini kijanja,akatoka na kuelekea chumbani kwa Necka.Akampatia pesa hizo akisisitiza kwamba asimweleze baba yake,zaidi na hilo wawasiliane akifika jijini Dar es salaam.
“Kule kuna rafiki yangu mmoja,nitamwambia ukae kwake”
“Ahsante Mama”
Necka akamkumbatia Mama yake huku machozi yakimlenga,wakaagana.
“Uwe makini sana mwanangu”
“Sawa Mama”
Mipango ya Necka Golden,ikawa imekamilika.Pesa aliyopewa akaamini ingemsaidia kufika na kulala kwa siku moja.
Kulivyokucha asubuhi na mapema, akaelekea kituo cha basi.Bahati nzuri ilikuwa kwake,maana alivyofika Kasulu,alipata basi lililomfikisha Uvinza.Hapo akapanda basi lingine,aliamini safari yake ingekuwa ndefu sana na ingetumia masaa mengi mno!Ndani ya basi hakuacha kumfikiria Ahmed Kajeme,akiamini kwamba angefika tu, wangefufua mahusiano yao upya na baadaye wazae watoto,hiyo ilimfanya safari aione ndefu sana kwake.
“Nakupenda sana Ahmed,nina hamu sana nawewe”
Ghafla hisia za kufanya ngono na Ahmed,zikamjia akatamani wawe kitandani dakika hiyohiyo.Kutokana na kutofanya tendo hilo kwa muda mrefu ilifanya azidi kupata tabu ndani ya basi.

****
Yusrath,alisimama lakini alihisi kuishiwa nguvu za miguu kabisa kile alichoambiwa akifanye alishindwa sababu ki ukweli kiwanja hicho, walifanya mipango na Sameer,wakakinunua.Asingeweza kumwambia Ahmed kwamba Sameer ndiye alikuwa dalali na ndiye aliyefanya michakato yote ya ununuzi wa eneo hilo,akabaki anatetemeka midomo yake inamcheza amekosa jibu.
“Ule ndio mpaka?”
Ahmed akauliza baada ya kuona kuna miti imepandwa, sambamba mpaka mwisho,pembezoni mwa barabara,kimoyomoyo alimsifu mkewe kwa kuwa muaminifu lakini hakutaka kumpongeza kwa wakati huo,akatembea mpaka kando kabisa ya kiwanja akizunguka huku na kule,akijaribu kujenga picha jinsi nyumba yake itakavyokaa.
“Inabidi,igeukie huku.Kule kuwe kuna geti, chini kule Parking”
Ahmed alizungumza mwenyewe bila kujua,tayari amekalia kuti kavu na kiwanja hicho sio chake,akatembea na kumuendea Yusrath alipokuwa amesimama.
“Vipi,ushapiga simu?”
“Ndio,naona hapatikani”
“Inabidi twende kwa mjumbe,ili tumwambie kabisa”
Hapo Yusrath alibaki kimya bila kujibu chochote,akazidi kuumwa tumbo.Kabla ya kufanya chochote kile,kuna gari aina ya Prado, yenye rangi ya Silver,ikapaki kandokando ya kiwanja hiko.Akashuka mzee wa makamo, mwenye mvi nyingi kichwani,amevaa kaptula pembeni yupo na kijana mmoja,kwa harakaharaka alikuwa ni mwanaye kwani walifanana kiasi.Kilichomshangaza Ahmed,ni kumuona Mzee huyo anaingia katikati ya Kiwanja hiko na kuanza kutembea.
“Mzee Shikamoo”
Ahmed,akasalimia kwa lengo na kutaka kufahamiana zaidi.
“Marahaba kijana,hujambo?”
“Sijambo”
Mzee,akaendelea kutembea akimuonesha kijana wake mipaka ya kiwanja chake, akatembea mpaka mwisho!
“Hiki mwisho ni huku.Next Week kuna gari la matofali hapa litakuja”
Ahmed alikuwa makini akifuatilia maongezi hayo,japokuwa aliyasikia kwa mbali.Akatembea ili asogee karibu awasikie, wanazungumza nini kuhusu kiwanja chake,lakini kabla ya kuwafikia simu yake ikaita,alivyoitoa mfukoni akaona jina la Kassim!Akaiangalia kwa umakini,hiyo ilimfanya ashangae sababu haikuwa kawaida kwa Kassim, kumpigia simu, yeye hutuma meseji tu.
“Dogo”
Ahmed,akapokea na kuongea.
“Broo,shikamoo”
“Marahaba”
“Uko wapi?Kuna matatizo yametokea home”
“Kuna nini?”
“Mzee kapigwa risasi”
“Whaaat,unasemaaaa?”
“Ndio,dingi kapigwa risasi na majambazi.Tupo Muhimbili sasa hivi”
“Ilikuwaje?Amepona?”
“Broo njoo nakuomba”
“Nakuja”
Mshutuko alioupata Ahmed,haukuwa na kipimo chake.Habari za Baba yake kupigwa risasi, zilimshtua na kwa wakati mmoja aliomba awe hai,sijui angefanya nini kama angepokea habari za msiba.Bila kuuliza kitu kingine chochote,akamtaka Yusrath aingie ndani ya gari haraka.
“Kuna nini?”
“Tunaenda hospitali”
Ahmed akajibu huku akigeuza shingo yake nyuma,akarudisha gari nyuma kwa kasi, akaliweka sawa na kupiga gia.Akalitoa kwa kasi,hiyo ilimshangaza sana Yusrath na wakati huohuo ikawa neema kubwa kwake kwani kikombe kilichokuwa kinamkabili,alikiepuka.
“Ahmed,kuna tatizo gani?”
“Baba amepigwa risasi”
“Mungu wangu!”
Yusrath alishtuka,hata yeye alijikuta anaumia mtima, machozi yakaanza kumlenga kusema ukweli alimpenda sana Baba yake Mkwe, kutokana na ucheshi wake pamoja na msaada mkubwa aliowapa,hiyo ikampelekea aumie ndani kwa ndani.Walivyotokea Mbezi mwisho,wakakunja kushoto na kuchukuwa barabara kubwa,Ahmed akaonesha kuchanganyikiwa akimuomba Mungu kimoyomoyo,akachukua simu yake huku mkono mmoja ukiwa juu ya usukani kwa niya ya kumtafuta Mama yake mzazi hewani,lakini simu iliita na kukatika.
Akajaribu kupiga tena na tena lakini wapi.Haikupokelewa,alivyompigia Kassim pia hakupokea,hiyo ilimfanya azidi kuogopa zaidi.Kilichomchanganya zaidi ni baada ya kufika Kimara Suka,kulikua na msongamano mkubwa wa magari.Hakutaka kuganda eneo hilo,ndio maana akatizama ‘site mirror’ ili atanue upande wa pili,alivyoona kupo shwari akazungusha usukani bila kujali anavunja sheria za barabarani,akatembea kwa mwendo wa spidi themanini akitimua vumbi nje.
“Baby,trafiki”
Yusrath aliropoka kwa sauti akitoa taarifa hiyo lakini akawa amechelewa tayari kwani polisi wa usalama barabarani aliliona gari la Ahmed,limetanua hapohapo akalipiga mkono likasimama.Trafiki huyo Mweusi, mfupi kiasi akasogea mpaka kwenye mlango wa Ahmed,kioo kikashushwa.
“Habari yako bwana mdogo”
Afande,akamsalimia Ahmed huku akiangalia gari kwenye kioo cha mbele ili kukagua stika kama zipo.
“Salama”
“Naomba leseni yako na kadi ya gari”
Ahmed,akatii amri alichokifanya ni kutoa kadi ya gari na leseni yake ya udereva,kitendo cha Trafiki kukagua,akamtizama tena Ahmed.
“Unalijua kosa lako?”
“Ndio afande,lakini nina haraka”
“Hizo haraka zako,zimekufikisha wapi?Au ulikuwa unaniwahi mimi?”
“Hapana afande”
“Sasa hapa nakulima faini,nakuandikia”
“Afande,sikia.Tusifike huko,haina haja ya kuandikiana”
“Hapana,nakuandikia”
Alichokifanya Ahmed ni kujiongeza,akavuta pochi na kuchungulia pesa,akatoa noti ya shilingi elfu tano,akaikunja kunja na kutaka kumfinyia trafiki.
“Ngapi hii?”
“Elfu tano”
“Haupo siriazi,ngoja nikuandikie, mimi elfu tano ya nini?”
Hiyo ilimaanisha dau ni dogo,akatoa elfu kumi.Akapewa maelekezo kwamba aiweke chini ya leseni,trafiki akawa amepokea kiziba mdomo,baada ya hapo Ahmed akarudi barabarani ambapo bado kulikuwa na msongamano wa magari.

****
Walitumia lisaa limoja na nusu kufika Muhimbili, kutokana na foleni ya magari,walivyoshuka tu na kuingia mapokezi wakakutana na Zelytan mjomba mkubwa wa Ahmed.
“Shikamoo Anco,vipi hali ya Mzee?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Ahmed,akauliza akiwa anahema mwenye wasiwasi mkubwa.
“Atapona,amepigwa risasi ya mkono wa kushoto”
“Ilikuwaje?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Ahmed,kabla ya kujibiwa akatokea Kassim.Wakasalimiana,akamsalimia Yusrath juujuu.
“Dingi vipi?”
Ahmed,akamtupia swali mdogo wake.
“Yuko poa”
“Maza yuko wapi?”
“Yupo kwa dokta”
“Ilikuwaje Kassim?”
“Majambazi walikuja home,sijui walikuwa wanataka nini broo.Wakapiga risasi,hewani wote tukatoka nduki, mzee ndio akaanza kurushiana nao risasi wakampiga begani”
Kassim,akaanza kusimulia jinsi ilivyokuwa mpaka walivyompiga baba yao risasi.Kila mtu alibaki kinywa wazi lakini walimshukuru Mungu kwa kila kitu kwani uhai ndio kitu pekee walichokuwa wanaomba!
“Love,naomba simu yako mara moja”
Yusrath,akadeka makusudi mbele ya Kassim, akizungumza na Ahmed,mgongoni akiwa na mtoto mmoja mwingine begani,Ahmed hakujibu chochote, alichokifanya ni kutoa simu na kumkabidhi Yusrath,ambapo alitoka nje ili apige kwani simu yake iliisha salio.
Alivyomaliza alichotaka kufanya,kuna kitu kikamuwasha aingie kwenye meseji,akafanya hivyo!Akawa anakagua,lakini hakuna meseji yoyote mbaya aliyoikuta,moyo wake ukatulia akaamini mumewe hachepuki lakini kuna meseji moja,aliitilia mashaka, jina lililoandikwa ‘SHEM RHODA’Akaifungua,mambo yaliyoandikwa humo,yalimfanya aishiwe nguvu na ilikuwa kidogo awadondoshe watoto,moyo ulimuuma ajabu alivyogundua kwamba Rhoda na Mumewe Ahmed walifanya ngono ndani ya gari,mbaya zaidi mwanamke huyo ambaye ni rafiki yake alikuwa anatoa sifa ni jinsi gani Ahmed alivyokuwa mtamu na kumkuna ipasavyo.
Hakutaka kuliweka jambo hilo kiporo,hapohapo akapanda hewani kupitia simu ya Ahmed.Simu ikaita,ikapokelewa na upande wa pili Rhoda, akaanza kuongea!
“Niambie Shem Darling,shemela wangu mtamu,za kunisusa?”
Rhoda Denis,akaropoka bila kujua simu imepokelewa na YUSRATH.


Siku zote Mkuki kwa nguruwe, kwa binadamu Mchungu!Katika siku alizoumia katika maisha yake ni hiyo,moyo wake ulichoma kama pasi.Ikawa kama kuna mtu kaingia ndani yake,anaukamua kama nguo.Akaamini kwamba kikulacho kiungoni mwako,hata siku moja hakutegemea kama Rhoda angemfanyia usaliti wa namna hiyo wa kutembea na mume wake wa ndoa,wakati mwingine alidhani wenda Ahmed alilipa kisasi sababu ya Sameer lakini hilo hakutaka kulipa kipaumbele sababu Rhoda alijua fika kwamba Ahmed ni mumewe kwanini akubali kulala naye?Akiwa ameshika simu bado ipo sikioni tena kwenye laini, hakujibu chochote zaidi ya kuikata.Macho yake,yakabadilika rangi ghafla, ilikuwa ni bora Ahmed angetoka kimapenzi na mwanamke mwingine lakini sio Rhoda,rafiki yake kipenzi.Mikakati mbalimbali ikaanza kumiminika ndani ya kichwa chake ni jambo gani alifanye ili amkomoe Rhoda kama Sameer alivyofanyiwa unyama,ilikuwa ni lazima nayeye amfanyie unyama ili iwe ngoma ‘draw’.
“Nitamfunza adabu,hanijui mimi ni nani.Nitamuonesha,jinsi mume anavyouma”
Yusrath aliwaza,mudi yote ikamuisha.Akarudi kwa Ahmed na kumkuta wanazungumza na ndugu wengine,ambao baadhi hakuwajua vizuri.
“Simu yako”
“Ushamaliza?”
“Ndio”
Yusrath akajibu kifupi na kutembea mpaka kwenye benchi ambapo hapo,alikaa kitako akianza kutafakari ni kitu gani akifanye,mawazo yake hayakuwa hospitali tena juu ya baba yake mkwe kupigwa risasi,habari za kutaka kujua anaendeleaje akaziweka kidogo kando alichokiwaza yeye ni mpango kabambe,tena ayaratibu mambo mapema ili amfanye kitu kibaya Rhoda Denis!Kwa mbali akamuona Kassim,kuna wazo alilipata la kutaka kutembea naye alale naye makusudi ili Ahmed aumie lakini aliamini hilo lisingekuwa suluisho bali angeongeza tatizo lingine!
“Darling,subiri nipo Hospitali.Dingi anaumwa,majambazi walituvamia!Nitakupigia”
Kassim ndiye alikuwa simuni,anazungumza na Rhoda Denis akimtaarifu kwamba baba yake amepigwa risasi.
“Nakuja kukuona,unanidanganya.Upo na mademu zako hapo gesti,nakufahamu Kas..”
“Siwezi kufanya hivyo,kama unabisha nipigie video call”
“Nakuamini baby,hospitali gani?”
“Muhimbili”
“Nitakuja kumuona”
“Karibu”
Kipindi alivyokuwa anazungumza na simu,alitoka pembeni kidogo alivyoikata akageuza shingo,macho yake yakagongana na Yusrath,aliyekuwa umbali wa mita thelathini,amekaa juu ya benchi.Bila kujishauri kitu kingine chochote kile,akamsogelea.
“Shemeji vipi?”
Kassim,akaanza kutoa salam.
“Poa,Baba anaendeleaje?”
“Tunamshukuru Mungu,yuko sawa”
“Ilikuwaje Sameer? Aaah sorry Kassim”
Kassim ilibidi atulie kidogo kitendo cha Yusrath kumuita jina la Sameer, kilimfanya ashangae,kichwani akawa anajiuliza Sameer ni nani,kabla ya kujibu swali Yusrath akajihami sababu alijua kivyovyote vile ameharibu.
“Kuna ndugu yangu mmoja anaitwa Sameer,anapenda sana kuja pale nyumbani”
“Usijali,tulivamiwa leo asubuhi.Mshua,si unajua kazi zake.Nadhani alitumiwa watu”
“Poleni sana”
“Tushapoa”
Hapo Kassim hakutaka kukaa sana,alichokuwa anawaza yeye ni hali ya baba yake,akaondoka na kumuacha Yusrath anamtizama akifikiria amfanye kitu gani Rhoda Denis.Ilibidi wakae hospitalini mpaka usiku na siku hiyo,ilikuwa bahati nzuri watoto hawakusumbua.
Saa mbili usiku,Benjamin Ngowi akatokea akamuendea Ahmed kwa haraka.
“Vipi ndugu?Mzee anaendeleaje?”
Yalikuwa ni maswali kutoka kwa Benjamin Ngowi,akimuangalia swaiba wake machoni,akiwa anasubiri jibu kutoka kwa Ahmed na aliuliza huku amemshika bega la kushoto.
“Anaendelea vizuri sasa hivi,washamtoa risasi”
“Ahsante Mungu,ujue umenitumia Meseji nipo Posta.Ilibidi nipande pikipiki niache gari broo,pole ndugu yangu Mzee atapona”
“Ahsante kwa kuja”
“Usijali,sisi ni ndugu”
Mbali na urafiki wao wa kukutana sehemu za starehe lakini hata kwenye matatizo pia,ushirikiana bega kwa bega!Ndiyo maana Benjamin Ngowi, alifika eneo hilo mapema japokuwa alichelewa kupata taarifa hizo,Saa nne ya usiku ilivyofika Mzee Kajeme akawa tayari yupo wodi lingine,wakaenda kumuona, uzuri walimkuta anazungumza vizuri,mkono mmoja ulikuwa na bandeji kubwa.
“Kassim,wewe na Mama yako.Msirudi pale nyumbani tena mpaka nitakapowaambia,nenda Goba kwa anti yako Amba!Hii vita ishapamba moto,lazima watarudi tena”
Yalikuwa ni maneno ya kutisha kutoka kwa Mzee huyu Kajeme,alizungumza kwa kujiamini na alichokiongea alikuwa ana uhakika nacho moja kwa moja,hiyo ilimfanya Kassim aanze kutetemeka.
“Baba Ahmed,mbona unatutisha?”
Mama,akauliza akionekana kuingiwa na hofu,kitendo cha kusikia kuna vita kilimuogopesha hata yeye.
“Msimwambie mtu yoyote kama mnaenda huko,Kassim.Mlinde Mama yako,nitawapigia simu”
Japokuwa alikuwa ana jeraha mkononi lakini alizungumza kwa ujasiri wote na kwa umakini wa hali ya juu sana,alishaelewa ni vita gani anayozungumzia.
Alijua fika watu waliomvamia ni watu wa Florian Fredrick,hiyo ilitokana na kuunganisha matukio tofauti tofauti,hata hivyo aliwahikishia kwamba kila kitu kitaenda sawa na atawawekea walinzi kila mahali.Ahmed alikuwa pia kandokando yake,anasikiliza maelekezo yote,akatoa pole na kutaka kujua nani yupo nyuma ya tukio hilo.
“Ni mambo ya kiusalama zaidi”
“Hapa,utakuwa safe?”
“Ndio nipo safe,watu kutoka usalama wa taifa wapo,wameshafika hivyo msiwe na wasiwasi”
“Wako wapi?”
“Kuna wawili wapo humu ndani,wengine wapo nje”
Kusikia hivyo Ahmed,akaanza kugeuza shingo huku na kule.Hakumuona mtu yoyote zaidi ya madaktari waliokuwa wanazunguka huku na kule.
“Miongoni mwa hao madaktari,wawili ni usalama wa taifa sio madaktari.Msiwe na wasiwasi,nyie nendeni”
Ilivyogonga saa saba ya usiku Ahmed akalazimika kuaga, sababu alikuwa na watoto wadogo wachanga,akamfuata Yusrath wakatoka na kuelekea nje kwenye maegesho ya magari.
“Vipi wameshalala?”
Ahmed,akauliza kumaanisha watoto.
“Muda mrefu tu”
“Pole mke wangu,umengw’ata na mbu leo”
“Ahsante”
Swala la kumfukuza Yusrath na kumpeleka kwao,akawa amelisahau lakini alivyofika ndani ya gari na kuyaona mabegi,akakumbuka na kumtizama Yusrath aliyekuwa anaingia ndani ya gari.
“Samahani kwa kila kitu,kilichotokea.Zilikuwa ni hasira mke wangu,turudi nyumbani”
Yalikuwa ni maneno ya Ahmed,akiomba msamahaa kwa kitendo alichokifanya asubuhi ya siku hiyo,bado alimpenda sana Yusrath mbaya zaidi alivyowaangalia watoto wake,akaumia mtima. Hakupenda hata siku moja walelewe na mwanaume mwingine,alitaka watoto wake wakuwe wakioneshwa mapenzi ya baba na Mama,ndiyo maana Ahmed akajirudi na kusahau kila kitu kilichopita nyuma,akiamini kwamba binadamu wanateleza na hakuna aliyekamilika,licha ya Yusarth kusamehewa na kuhaidiwa mambo makubwa lakini swala la Rhoda lilikuwa lipo palepale,wivu uliomjia haukuwa wa nchi hiyo,hasira zake zilikua kama zote!Zikampanda katika kiwango cha juu kabisa.
“Nimekusamehe baby wangu”
Ahmed,akarudia tena sababu alimuona Yusrath hayupo sawa,bado anawaza.
“Umenisamehee kweli Mme wangu?”
“Ndio”
“Bado siamini”
“Nifanye kitu gani ili uamini?”
“Naamini umenisamehee Mme wangu,sitorudia tena”
“Yaliyopita si ndwele,tugange yajayo!”Ahmed,akachomekea msemo huo ili kupigilia msumari sentensi yake!
Hapo Yusrath akapachika tabasamu la Plastiki,akasogea karibu na Ahmed,wakanyonyana midomo.
“I love you My husband”(Nakupenda Mume wangu)
Safari ya kurejea nyumbani ikaanza,kilichowafanya wote wapige jicho karibu na gia ni baada ya simu ya Ahmed kuita, ambapo kioo kwa juu kilionesha jina ‘SHEM RHODA’Hiyo ikamfanya Ahmed,apotezee simu hiyo akajifanya kama hajaiona vile.
“Baby,simu yako inaita”
Yusrath akachomekea,alishaelewa kwanini Ahmed hawezi kupokea simu.
“Nimeiona,Darling.Huyu Rhoda bado sijamlipa pesa aliyokuwa anakudai,hapo atataka kusumbua”
Ahmed,akapata kisingizio akitumia deni la Yusrath kama ngao ya kujitetea!
“Ndio akupigie usiku baby?”
“Ni kweli sio mstaarabu,bora nimlipe pesa yake aache kusumbua”
“Sawa,pokea lakini”
Alichokifanya Ahmed ni kuchukua simu,akaiweka sikio la kulia ili Yusrath asisikie mazungumzo.
“Eeeeh,nitakutumia mzigo wako kesho asubuhi.Usiku mwema,kesho kesho kesho”
Hapohapo Ahmed akakata simu na kumtizama Yusrath,kuanzia hapo hakukuwa na mtu yoyote kati yao aliyemuongelesha mwenzake, mpaka wanafika nyumbani.
“Baby,nitakutumia kesho asubuhi ela ya huyu Rhoda.Umpe ili tuondokane na huu usumbufu”
Maagizo hayo aliyatoa baada ya kufika nyumbani,ambapo walinyoosha mpaka chumbani.Chakula kilikuwa tayari kipo mezani.
“Utakuja kula mezani au nikuletee Chumbani?”
Yusrath akauliza.
“Niletee chumbani”
Kitendo cha Yusrath kwenda Seblen,Ahmed akachukua simu yake na kumtafuta Rhoda hewani.
“Sikiliza wewe Rhoda,nina mke ninampenda kilichotokea siku ile zilikuwa pombe tu,mimi sijazoea kuishi maisha ya wasiwasi kama kifaranga cha kuku al..”
“Ahmed kwani nimekosea wapi?”
“Nasema kwamba achana namimi,pesa yako utapata kesho.Huna adabu,hujui kuwa nina mke au?Unanipigia simu usiku,ili iweje?Unadhani Yusrath akijua itakuaje?Nampenda mke wangu…..”
Wakati Ahmed akiendelea kufoka simuni Yusrath alinyata akasimama mlangoni ili asikilize,akiwa na hotpot la chakula mkononi,siku hiyo akaamini kwamba Mumewe anampenda sana,akatabasamu lakini kwa wakati mmoja akahaidi kwamba ni lazima angemkomesha Rhoda kwani ndiye alikuwa king’ang’anizi,hapohapo akasukuma mlango.Akamuona Ahmed,anavyotetemeka na maongezi yakabadilika.
“Sawa Kiongozi,salimia sana familia yako!Ndio nimeingia sasa hivi,nimetoka kumuona Dingi hospitalini Muhimbili,kesho nitaenda tena.Usiku mwema Kaka”
Ahmed,alibadilisha mada bila kujua mke wake,alisikia kila kitu!Hapo alijiona mjanja,kuucheza mchezo huo hatari kumbe alisikiwa,aliamini kwamba angekata simu ghafla ingetokea gumzo!Chakula kikapakuliwa,wakala na kunywa maji wakaingia kuoga, huko Yusrath alionekana kuzidiwa sana,akaanza uchokozi akitaka wafanye tendo la ndoa,wakanyonyana midomo na kubadilishana mate.
“Yusrat…th please stoop”
Sauti ya Ahmed,ilisikika.Alizungumza hivyo akiwa amelegea,hakuwa ana uhakika kama atafanikiwa kile anachotaka kukifanya maana tayari karoti yake ilikuwa imesimama na Yusrath tayari alikuwa amepandisha mori,asikiii haambiwi akili yake tayari imeshahama, kichwa chake kinafikiria tendo hilo,Ahmed akajikaza na kumshika mikono.
“Bebiiiii,nini lakiniii nina hamu naweweee”
“Subiri,subiri kwanzaa”
Ahmed,akazungumza akatoka bafuni na taulo akajifunika,Yusrath akamfuata nyuma yake akiwa kama alivyozaliwa,hajavaa chochote.
“Mme wangu ni…”
“Please,hatuwezi kufanya”
“Kwanini?”
“Hapa katikati kuna vitu vingi sana vimetokea”
“Una maana gani?”
“Maana yangu ni kwamba lazima tukapime afya zetu”
“Sijakuelewa”
“Mpaka tukapime UKIMWI”
Haukuwa utani,Ahmed alishikilia msimamo wake kwamba wapime afya zao kwanza, ndio mambo mengine yafuate kwani kwake afya ilikuwa ni bora kuliko kitu chochote kile,Yusrath aliingiwa na hofu kusikia kauli hiyo,wasiwasi ulikuwa mkubwa kwamba kama angekuwa amepata ugonjwa huo hatari wa Ukimwi ni lazima Sameer angekuwa amemuambukiza,usiku mzima alimuomba Mungu janga hilo lisije kumtokea!

****
“Nitakutumia ela nikifika ofisini,naweza nikasafiri leo narudi Moshi,niliomba ruksa ya wiki mbili.Zimeisha jana,nisiporudi nyumbani ujue nishaondoka.Tutawasiliana lakini….”
“Vipi baby,kuhusu kupima?”
“Nikirudi”
“Sawa Mme wangu”
Ahmed,akajiandaa ili apitie benki atoe pesa amrushie Yusrath ili amlipe Rhoda Denis!
“Gari atakuja nalo,Bariki”
“Bariki yupi?”
“Yule dogo wa pale Ofisini”
“Okay baby”
Ahmed,akaaga na kuondoka zake kwa kuwa alikuwa mwenye haraka,aliwasha gari na kuondoka zake,akiwa mwenye mawazo chungu mzima kichwani kwake hususani afya ya baba yake aliyekuwa hospitalini!

****
Alichokifanya Yusrath ni kumpigia simu Rhoda Denis,asubuhi hiyohiyo akimwambia kwamba afuate pesa zake nyumbani kwake Ubungo Kibangu.
“Ndio njoo,uchukuwe”
“Nakuja,asa si unitumie kwenye simu”
“Huo muda sina,unakuja au?”
Yusrath akajibu kwa swali tena kwa shari.
“Eeeh nakuja shoga angu”
Yusrath bila kujibu chochote akakata simu,tayari alimchukia Rhoda ghafla akatamani akija amuwekee sumu kwenye maji anywe afie mbali,bado alikuwa mwenye mikakati ya kinyama ya kumlipizia,akafikiria cha kufanya na kukosa jibu la haraka haraka.
Ilivyogonga saa tisa ya alasiri, Ahmed akampigia simu,akimtaarifu kwamba atasafiri na anavyoongea naye wakati huo anakata tiketi ya ndege ili arejee mkoani Kilimanjaro kikazi.
“Safari njema Mme wangu”
“Ubaki salama,nitarudi naenda kumalizia wiki mbili zilizobaki,nitakutumia pesa kidogo za kusaidia hapo nyumbani.Nisamehee,nimeondoka juujuu Bariki ataleta gari,funguo ziweke chumbani”
“Usijali baba,nakupenda sana Ahmed mme wangu”
“Mimi pia,sasa hivi nakutumia ile ela ya Rhoda.Umpe, nakuomba”
“Sawa Honey”
Yusrath akakata simu,akajisikia uchungu sana!Akajuta kwa kila kitu kilichotokea,akajishangaa hata yeye.
Ghafla akakumbuka nyuma jinsi alivyokuwa anawachomolea wanaume, iweje atembee na Sameer?Wakati Ahmed alitokea kumpenda kweli,akashindwa kuvumilia akajikuta analia machozi kwa usaliti alioufanya,Ahmed hakustahili kabisa kusalitiwa, alikuwa ni mwanamme wa aina yake,mwenye mapenzi ya kweli.Akashindwa kuvumilia,akaenda chumbani. Huko alilia mpaka kamasi zikamtoka!Hapo,usingizi ulimchukua mpaka saa kumi na moja jioni,kilichomshtua ni simu kutoka kwa Rhoda akimwambia kwamba anakaribia kufika,akaingia kuoga akaenda mezani kula na kumpa Hadima simu ili akatoe pesa nje.
Hapohapo mlango wake ukagongwa,Rhoda akaingia, akamkaribisha kwenye kiti!
“Vipi,shemeji yupo?”
Swali hilo lilitoka kwa Rhoda, likamfanya Yusrath ahisi kichefuchefu cha kutapika,akamkata jicho kali na kushusha pumzi ndefu, tayari kwa kumpa vidonge vyake lakini kuna kitu kilimwambia anyamaze kwanza.
“Kwani,hajakuaga?”
Yusrath badala ya kujibu swali,akauliza swali likawa swali juu ya swali.
“Najua umekasirika,lakini Yusrath shoga angu.Mimi ningefanya nini?Nilikuwa nina shida na pesa al..”
“Pesa yako,inakuja sasa hivi”
“Mmmh haya,mambo mengine vipi lakini?”
“Kama ulivyoyaacha”
Kwa mawazo ya Rhoda alijua kwamba Yusrath alichukia kwa kitendo cha kumtishia kwamba angemwambia mumewe kuhusu watoto kumbe haikuwa hivyo,kilichokuwa hapo ulikuwa ni wivu wa mapenzi.
Dakika mbili baadaye, Hadima akafungua mlango na kumkabidhi Yusrath kitita cha pesa.
“Pesa zako hizi hapa,zihakikishe.Baada ya hapo sasa,futa namba zangu kwenye simu yako!Naomba usimsumbue mume wangu,kumpigia simu usiku al..”
“Hee yashafika huko?”
“Nadhani nimeeleweka alafu kitu kingine sita….”
Kabla ya Yusrath kumaliza kutoa mapovu yake,wote wakageuza shingo zao baada ya mlango kufunguliwa kwa nguvu,akaingia mwanamke mmoja mwenye mwili mdogo,ameshika begi kubwa la nguo mkononi,hawakuelewa kama alikosea njia ama amechanganyikiwa.
“Habari zenu,bila shaka hapa ndio kwa Ahmed?Mimi naitwa NECKA GOLDEN,nimemkuta Ahmed?Nimechoka sanaa,naombeni maji ya kunywa jamani,Ahmed nayeee.Kuishi ndanindani huku ndio nini?Nimepata shida kupajua sana yaani”
Necka Golden,alizungumza bila kuweka nukta!Alionekana kuchoka mpaka kufika nyumbani kwa Ahmed,alichokifanya ni kuweka mabegi yake chini na kukaa kwenye kochi ili apumzike,akiwa ana uhakika kwamba hapo ndipo amefika,kama treni ishafika Kigoma!Kilichowafanya Rhoda na Yusrath,wamshangae ni baada ya kumuona anasimama na kuliendea friji mwenyewe lililokuwa karibu na meza ya kulia chakula,akachukua jagi na kumimina maji,akaanza kunywa.
“Wee dada,mbona unakua sio mstaarabu.Wewe kama nani,unakuja unaingia kwenye mafriji ya watu,una wazimu au mzima?Ukiitiwa mwizi je?”
Yusrath,akashindwa kuvumilia maji yakamfika shingoni, ikabidi ahoji ili wafahamiane vizuri,badala ya Necka Golden kujibu,akamimina maji tena kwenye glasi ili akate kiu,akanywa,akaongeza glasi nyingine ilivyofika ya tano,akamtizama Yusrath.
“Unataka kunijua mimi nani?Muulize Ahmed,bosi wako sijui kaka yako atakwambia!Bafu liko wapi,nikaoge?”
Necka Golden,alizungumza kwa kujiamini bila kusua akionesha ujasiri,hiyo ilimfanya Yusrath asimjibu, akachukuwa simu yake na kumtafuta Ahmed hewani,amwambie kinachoendelea nyumbani kwake!



Bilionea George Charles alipelekeshwa kama gari bovu!Kila alichotaka Lissa Mnzava alipewa dakika hiyohiyo bila kuchelewa,mwanamke huyo alijua kucheza na akili ya George Charles,japokuwa hapo awali ilikuwa ni ngumu lakini alichogundua kwamba George Charles anapenda sana kufikiria pesa,nayeye akatumia gia hiyo ili kumshawishi aonekane ni mwanamke anayependa maendeleo, hiyo ilimfanya George Charles,aanze kupanga mikakati ya harusi mbiombio, akiamini Lissa Mnzava ndiye mwanamke wa maisha yake,kumbe haikuwa hivyo kilichokuwa kinatokea ni kwamba alikuwa ana fuga jini ili baadaye lije kumtafuna mwenyewe mzima mzima!Licha ya hayo yote Lissa akajitahidi kumpagawisha kitandani akitumia michejo tofautitofauti,hiyo ikamfanya George Charles azidi kupagawa zaidi na zaidi,siku hiyo Lissa Mnzava sijui alitoa wapi mikao hiyo kwani George Charles, aliambiwa anyooke chali, yeye akapita katikati ya miguu yake ambapo aliitanua kidogo wakazidi kuendelea na mchezo huo wa kikubwa.
“Bebiii pleaseee”
George Charles,hakujiweza tena mpaka akaongea mwenyewe bila kutegemea,mchezo aliokuwa anaufanya Lissa haukuwa wa kawaida hata kidogo,alichokuwa anakifanya ni kumsubiria George Charles akaribie kufika kileleni kisha anatulia,hiyo ilimfanya George atahabike sana, japokuwa upande wa pili alikuwa akifurahi kwani aliamini ni moja ya njonjo ya mchezo huo,siku hiyo Lissa alikinyonga kiuno, akampeleka George huku na kule,akamrudisha kati!Mechi ilikuwa yake siku hiyo akiamini kwamba farasi umpandae hakutishi kwa mbio zake,ndiyo maana alivyokuwa juu ananyonga kiuno, ilikuwa rahisi kwake kuendesha mechi hiyo, sita kwa sita,akasogeza mdomo karibu na kuanza kulana denda,hakuishia hapo akatoa ulimi wake tena,akaupitisha sikioni mwake,akitumia ncha ya ulimi.Hapo ndipo George alipoanza kuzungumza lugha anazozijua yeye,akitoa ahadi mbalimbali kwamba atatoa kampuni moja na kumkabidhi Lissa aendeshe.
“Aaaaaaaah”
Bezi alilotoa Gerge Charles,ilimaanisha kwamba tayari amefika mshindo,akatulia na kuanza kuhema,Lissa akamuegamia kifuani sababu aliamini wasingeweza kuendelea tena kwa sekunde hiyo,ilibidi kwanza ampe mapumziko ya muda mfupi.
“Nakupenda Mme wangu”
Lissa akadeka huku akijichomoa taratibu kutoka juu,akalala pembeni!Akavuta shuka wakajifunika wote,akaweka kichwa chake juu ya kifua cha George na kuanza kumkwaruza kifuani na kucha zake zilizokuwa fupi kiasi.
“Hata mimi nakupenda Mke wangu,lile wazo ulilonipa la kuongeza mradi mwingine wa kokoto,umefanya kazi.Naona akaunti inaanza kusoma,kule nitakuachia wewe usimamie”
Hizo ndizo zilikuwa mada za George Charles siku zote,muda wote stori zake zilikuwa juu ya pesa na kampuni zake,hakuelewa kwa kufanya hivyo alimruhusu Lissa ayasome mawazo yake kiurahisi sana!Hapo ndipo alipoanza kumpa mawazo pia ili iwe rahisi kwake kumvuta karibu.Hilo likafanikiwa kwa asilimia zote mia moja,George Charles akajazwa ndani ya kumi nane tayari,hakuelewa kwa kufanya hivyo anajichimbia kaburi mwenyewe kwani mipango ya Lissa Mnzava ilikuwa ni kumuuwa.
Siku hiyo walizungumza mambo mengi hususani kuhusu maswala ya maendeleo na kufungua miradi mingine mingi,Lissa Mnzava alipiga picha na kufikiria miaka kadhaa ijayo,jinsi atakavyokuja kumiliki mali hizo zote zikawa zake, baada ya kufunga ndoa na bilionea huyo.
Alichokifanya Lissa ni kutoka kitandani,akachukua kanga moja ambayo aliiviringisha mwili mzima, kuanzia kifuani,ikafanya iwe fupi mapaja yake yakawa nje kabisa.Hiyo ikamfanya George Charles,amtizame kwa jicho la uchu!
“Usiniangalie hivyo baby, naona aibu”
Lissa akadeka kidogo,akimtizama George Charles kwa macho fulani ya kulegeaa utadhani kala kungu.
“Nije tuoge wote?”
“Baby,kuna kuoga huku tena?”
“Ndio”
“Aya njoo”
George Charles,hakuuliza tena alichokifanya ni kutoka kitandani kwa kasi,akamsogelea karibu Lissa na kumpiga denda,wakavutana mpaka bafuni.Huko wakaanza kushikana huku na kule,bafu lililokuwa chumbani kwa George Charles,lilikuwa bab kubwa.Kwanza lilikuwa kubwa mno kama chumba,kingine ukutani kulikuwa na televisheni kubwa,kando kando kulikuwa na kitu kama mtungi wa duara ambapo ndani kulikuwa na maji yenye mapovu yaani jakuzi,humo ndimo walipoingia.Badala ya kuoga,wakaanza kushikana huku na kule,alichokifanya George ni kumsogelea Lissa karibu na kuanza kumtomasa kifuani,hakuishia hapo akaupeleka mkono wake taratibu mpaka kwenye ikulu kabisa na kuanza kutalii,Lisa hakujiweza tena akafumba macho, akisubiria chochote kitakachokuwa mbeleni,haikuchukuwa muda mfupi baada ya kutomaswa mechi ikaanza humohumo ndani ya jakuzi.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa na kuanzia siku hiyo,George Charles,akamtaka Lissa awe msaidizi wake kwenye kampuni zake zote.Kwa maana hiyo kulivyokucha kesho yake,akataka kikao kifanyike ofisini kwake saa nne kamili asubuhi,jambo hilo likafanyika na wafanyakazi wote wakaitwa ndani ya chumba kikubwa maalum, chenye viti thelathini na meza kubwa katikati, yaani ‘Conference room’
“Attension”
George akasema na kusimama wima,siku zote mwanamme huyu alikuwa mtanashati na hupendelea kuvaa suti nyeusi,japokuwa siku hiyo hakuvaa koti la suti,shingoni alinyonga tai nyeusi lakini alipendeza sana.Alivyosimama tu wafanyakazi wake wote wakamtizama wakitaka kujua nini angezungumza siku hiyo!
“Kuna mabadiliko machache hapa nahitaji kuyafanya kama Managing Director,kwanza naomba niwapongeze sana kwa juhudi mnazoonesha.Let me go straight to the point,kuanzia leo ninavyoongea Lissa Mnzava atakuwa Assistance Director kwa maana nyingine.Akisema yeye ni sawa nimesema mimi,mumuheshimu na mumpe ushirikiano.Jenipha….”
George Charles alivyomaliza akaita.
“Naam bosi”
Msichana mdogo mweupe,akasimama kwa adabu zote na kumuangalia bosi wake.
“Nadhani unajua cha kufanya,jambo hili liandikwe lisainiwe liwekwe kwenye faili.Mfanyakazi mpya ameongezeka”
“Sawa bosi”
Asilimia sitini na tano,walimfahamu Lissa Mnzava kama mchumba wa bosi wao lakini wengine jina hilo hawakuwahi kulisikia kabla,kikao kilivyoisha kila mmoja akawa ana kazi ya kumuuliza mwenzake mwanamke huyo ni nani?!Saa tano ya asubuhi siku hiyohiyo,gari aina ya Rangerover Vogue yenye rangi nyeupe,lililokuwa na namba za usajili zilizoandikwa ‘GEORGE CHARLES’ likaingia nje ya gorofa hilo,vioo vilikuwa vyeusi hakukuwa na mtu yoyote aliyeweza kujua ndani kuna nani ingawa gari hilo lilifahamika na wakazi wa hapo Posta,isitoshe bilionea huyo hulitumia mara chache sana.
Kilichokuwa kinawafanya watake kujua ni nani ni baada ya George Charles kutoka nje ya ofisi,akasimama kandokando kabisa ya mlango wa gari hilo la gharama,mlango ukafunguliwa,kikatangulia kiatu kirefu yaani high hills,akashuka mwanamke mrembo,mrefu kiasi mwenye rangi ya maji ya kunde,George Charles akamkumbatia.
“Darling,umependeza”
George Charles,akamwaga sifa.
“Ahsante baby,ooh Ahsante Boss”Akaweka utani kidogo!
Wakashikana mikono na kuingia ofisini,ambapo huko wafanyakazi wote macho yao yakawa kwao,maneno ya chini kwa chini yakaanza ya kwamba huyo ndiye Lissa Mnzava.
“Yule ndiye Lissa,chakula ya bosi ile”
“Ni chomboo,mtoto kisu sana”
“Lakini kana mashauzi sana angalia mwendo wake,tutakaa kwa amani kweli humu ofisini?”
“Tuombe Mungu,maana sisi wengine tunategemewa na ukoo mzima….”
Wafanyakazi walianza kuteta,baada ya muda mfupi wakapewa maelekezo na kutambulishwa huyo ndiye Lissa Mnzava mwenyewe,mtendaji Msaidizi wa kampuni hiyo.Siku hiyohiyo Lissa akapewa ofisi aanze majukumu.

Japokuwa alipewa kila kitu,kuanzia magari ya George ya kifahari atembelee na pesa za matumizi lakini hakuridhika alitaka siku moja awe mmiliki wa mali zote,mipango yake ikawa palepale ya kutaka kumuuwa George Charles.Hakuna siku aliyofurahi kama George kusafiri nje ya Tanzania na kwenda Ujerumani,mwanya huo akautumia kuwapanga watu wake na kuwapa fomula ya namna ya kufanya.
“Huyu ni mtu mkubwa ujue,inabidi kifo chake kiwe slow but sure”
“Tunaelewa,unahitaji lini kazi hii ianze?”
“Mpaka tufunge ndoa”
“Liini?”
“Hapo ndio pagumu,hajaniambia ni lini,lakini huu mwaka hauishi”
“Sisi tunakusikiliza wewe ujue”
“Nitawaambia msijali”
Kilikuwa ni kikao kidogo lakini kizito,aliyekuwa anajadiliwa hapo alikuwa ni bilionea George Charles,mikakati ya kuuliwa kwake iliratibiwa na mwanamke anayempenda kwa dhati,anayemuamini na kutaka kufunga naye ndoa,mwisho wa siku walipanga kifo chake kisababishwe na ajali ya gari.
“Wazo zuri hilo”
“Iwe ajali,tutaongea vizuri tunaweza kubadilisha pia”
Bilionea George Charles,aliamini kwamba kwa utajiri mkubwa aliokuwa nao ingekuwa rahisi kwa mtu yoyote mbaya kumfuatilia yeye na familia yake ili kujiingizia kipato,aliufahamu mchezo ambao majambazi wengi hutumia kuteka watoto wa matajiri ama wake zao, kisha baadaye wanapiga simu na kuhitaji kiasi kikubwa cha pesa.
Ilikuwa ni siri kubwa sana kwake kutembea na walinzi, ambao muda wote walikuwa wanamfuatilia kwa nyumanyuma kama makachero wa FBI,hakutaka kuongozana nao!George Charles, alitembea na walinzi sita,ambao muda wote walikuwa na bastola zao viunoni,hakupenda kufuatana nao,walichokuwa wanakifanya walinzi hao ni kumfuatilia bosi wao na magari mawili maalum, tena ya kawaida kila anapoenda,hiyo ikawa vigumu kwa mtu yoyote kugundua kwamba Bilionea George Charles analindwa kama Rais.Hata hivyo baada ya kumpata Lissa,akawaajiri walinzi wengine kwa kazi hiyo ya kumlinda kila sehemu anayoenda, bila Lissa kugundua.
Hata Lissa alivyoingia Serena Hotel,walinzi walikuwepo pembeni yake,watatu walikuwa meza ya mwisho wawili walikuwa kulia,wanazuga wanasoma magazeti huku kila mmoja akiwa na kikombe cha kahawa mezani.Mazungumzo ya Lissa na wanaume aliokuwa anapanga wamuuwe George Charles yalichukuwa masaa mawili,ndipo akasimama!Akampita mlinzi mmoja pembeni yake kabisa bila kumjua,akaingia ndani ya gari alivyowasha,walinzi na wao wakawasha magari yao na kuanza kumfuatilia nyumanyuma!

****
Vurumai lililokuwa linaendelea nyumbani kwa Ahmed Kajeme,halikuwa la kawaida.Necka Golden,alifanya nyumba nzima itingishike, mbaya zaidi alijiamini hiyo ilimfanya Yusrath ampigie simu Ahmed ili amueleze kinachoendelea lakini matokeo yake, simu haikuwa hewani.
“Ulikuwa unampigia Ahmed?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Necka Golden,akimpandisha Yusrath juu mpaka chini akimnyali!
Yusrath hakujibu kitu,aliendelea kupiga simu lakini jibu lilikuwa lilelile kwamba haipatikani hewani,moyo wake ulimuuma ajabu,alishaelewa na kuanza kuhisi ni lazima mwanamke aliyesimama hapo anaongea kwa kujiamini ni hawara wa Ahmed,ndiyo maana alipanga ampigie simu ampe vidonge vyake,ikiwezekana aondoke siku hiyohiyo, awaachie nyumba kwani kwake jambo hilo alilitafsiri kama dharau kubwa.
“Hee!”
Ulikuwa ni mshtuko mkubwa kutoka kwa Necka Golden baada ya kuona picha kubwa ukutani,ikimuonesha Ahmed amevaa suti pembeni yupo na mwanamke ndani ya shela,akamtizama Yusrath kwa umakini zaidi na kurusha tena macho juu ya picha hiyo.
“Ina maana Ahmed kaoa?Sitaki kuamini,haiwezekani nasema.Sipo tayari kukubali hili”
Necka alizungumza kwa jazba,hasa alivyogundua Yusrath ni mke wa Ahmed.
“Samahani dada kwani wewe ni nani?”
Rhoda Denis,akatupa swali.
“Mwanamke wake,alinihaidi kunioa!Kaniacha kijijini huko,Ahmed ama kweli wanaume….”
Alivyomaliza sentensi hiyo,akamgeukia Yusrath akamsogelea karibu.
“Umeichukua furaha yangu,nitakuhakikishia katika maisha yako,hutokuwa na furaha kamwe”
Badala ya kumaliza maneno hayo aondoke kama wote walivyotegemea,alichokifanya yeye ni kukaa juu ya sofa,hakutaka kutoka kabisa akiamini hapo ndio amefika kama meli ishatia nanga!Hapo ilibidi Rhoda aage.
“Shoga,mimi naenda”
Rhoda akaondoka zake,akimuacha Yusrath na Necka Golden seblen!Haukuwa utani,Necka Golden alikaa seblen mpaka saa moja jioni,Ahmed alivyopigiwa simu akapatikana hewani lakini kitendo cha kusikia mkewe analia simuni, kilimfanya apatwe na mshtuko,mawazo yake yakamtuma wenda kuna taarifa mbaya za baba yake kutoka hospitalini lakini hakutaka kulipa hilo kipaumbele.
“Kuna nini mke wangu?”
Ahmed akauliza kwa mara nyingine.
“Ah..med,kwanini hukuniambia ukwe..li lakini?”
Yusrath alizungumza akiwa chumbani kwa kwikwi.
“Ukweli gani tena?”
“Ahmed,wewe wa kunifanyia mimi hivi?Umenidhalilisha vya kutosha,siwezi kukubali kubaki nawewe,naomba talaka yangu niondoke”
“Baby please,niambie kuna nini…”
Yusrath,hakutaka kuacha kitu chochote kile nyuma,akazungumza kila kitu kilichotokea siku hiyo tena akaanzia mwanzo tangu Rhoda Denis alivyofika,alivyomaliza kuzungumza na kulalamika akahitimisha kwamba anataka talaka yake kwani maisha ya ndoa yamemshinda, tayari ameomba poo!
“Huyo mwanamke yukoje?Bado yupo?”
“Ndio yupo”
“Wapi?”
“Seblen”
“Mpelekee simu”Ahmed akasema kwa ukali.
Yusrath bila kujibu kitu kingine chochote kile,akatoka kitandani na kunyoosha mpaka seblen ambapo huko alimkuta Necka Golden bado yupo,tena kashika rimoti ya tv,anatizama tamthilia ya Isidingo kajiachia miguu yote miwili ipo juu ya sofa.
“Simu yako,Ahmed”
Akapewa simu.
“Halloo”
Necka akaanza kusema.
“Yes,unaongea na Ahmed.Ni nani wewe unamsumbua mke wangu?”Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed,akiwa na jazba nyingi.
“Beeeeeibiiiii,it’s me NECKA GOLDEN”
Kuanzia hapo,ukimya ukatawala Ahmed akashindwa kujibu, ilielekea alipata kigugumizi cha ghafla kwani alihisi mapigo yake ya moyo yanadundia mgongoni.



Yusrath yupo pembeni,amefura! Wivu umekaa kohoni,mwanamke mcharuko aliyejitambulisha kwa jina la Necka yupo ndani kwake Seblen,anamletea fujo na kujifanya yeye ndiye Mama mwenye nyumba kwa kujiamini anatamba seblen na kuonesha yeye ndiye kila kitu, akidai kwamba Ahmed ni mchumba wake alimuacha kijijini kwa miaka mingi akimuhaidi kwamba angemuoa,Yusrath mke halali wa ndoa anachukia wivu wake unampanda mpaka katika kiwango cha juu kabisa, ndio maana akampigia simu Ahmed ili amueleze kila kilichotokea,kitendo cha ukimya kutawala baada ya Necka kujitambulisha kilimfanya Yusrath azidi kuumia mtima!
“Halloo,halloo”
Necka alizungumza,akaangalia simu na kugundua Ahmed amekata tayari, kumaanisha kwamba aliogopa kuzungumza,hiyo ilimfanya Yusrath achukuwe simu kwa hasira na kutaka kumpigia tena Ahmed lakini kabla ya hajafanya hivyo,simu yake ikaita na mpigaji alikuwa ni Ahmed tena, akaipokea kwa haraka na kuiweka sikioni.
“Halloo”
“Naniii,Yusrath mke wangu”
“Nakusikiliza”Akajibu kwa mkato!
“Nisikilize kwa umakini,nenda pale Ubungo kituo cha polisi ukatoe taarifa,ikiwezekana chukua diffenda waje kumtoa hapo nyumbani.Umenielewa?”
“Sawa mme wangu”
“Kitu kingine,huyo mwanamke ni hatari.Kuwa naye makini,ondoka kimya kimya chukua elfu hamsini kwenye draw kabatini,kawape askari wakupe diffenda.Wasimtoe lockup mpaka mimi nije”
“Nimekuelewa Mme wangu”
Kauli ya kijasiri kutoka kwa Ahmed ilimfanya Yusrath apate nguvu mpya,akavimba kichwa. Bila kumsemesha Necka, akaingia chumbani huko alivaa vizuri na kuchukua kiasi cha pesa,akamuachia dada wa kazi watoto na kumwambia angerejea baada ya muda mfupi,alivyopita seblen hakumsemesha Necka, akatoka mpaka nje ya geti ambapo huko alikumbana na pikipiki nyingi, zimepaki zinasubiri abiria wenye haraka.
“Dada,twenzetu”
Jamaa mmoja,dereva wa bodaboda alivyomuona Yusrath, akamshobokea.
“Naenda Ubungo kituo cha polisi”
“Pale Mawasiliano?”
“Ndio”
“Poa,panda mchuma twende”
Yusrath akapakia kwa nyuma,dereva akapika kick na kuanza safari,haikuchukua muda mrefu wakawa wamefika kituo cha polisi,ambapo nje Yusrath aliziona Difenda tatu na waharifu wanateremshwa wengine wakipigwa mateke na virungu!Akamlipa dereva ujira wake na kuanza kutembea mpaka kwenye kituo hicho, ambapo ndani kulikuwa na purukushani.
“Wewe kenge,vua mkanda ingia ndani.Mwizi mkubwa wewe,vua mkanda jina lako nani?”
Afande mmoja mnene kiasi, aliyekuwa zamu siku hiyo,alitoa mkwara baada ya wahalifu kufikishwa hapo.Akageuka na kumuona mwanamke mwenye mwili wa wastani, mweupe mwenye rangi ya shombeshombe na nywele za singasinga,akajitambulisha kwamba anaitwa Yusrath Kajeme.
“Una shida gani?Kuna mtu umekuja kumuona kama yupo,njoo kesho”
“Hapana,nimekuja kutoa maelezo”
“Maelezo gani?”
“Kuna mtu kanivamia nyumbani kwangu”
“Kwako?Wapi?Kakuvamia vipi?”
Kama kawaida ya maaskari kuhoji maswali na ndivyo ilivyotokea siku hiyo.Yusrath akapata kazi ya kujielezea kila kitu kilichotokea, kinagaubaga.
“Umesema,alikuwa mchumba wa mumeo?”
“Ndio alivyoniambia”
“Mumeo ulimpigia simu?Anajua?”
“Ndio ameniambia nije hapa”
“Uje hapa kufanya nini?”
“Kushtaki na kutoa maelezo”
“Ndio mara yako ya kwanza kumuona huyo mwanamke nyumbani kwako?”
“Ndio”
“Kwahiyo ni hawara wa mumeo?”
“Mimi sijui”
“Umeolewa?”
Yusrath akaanza kujuta,maswali aliyokuwa ananyeshewa hayakuwa na breki, hiyo ilimfanya achoke kidogo.
“Ndio nimeolewa”
“Una watoto wangapi?”
“Wawili mapacha”
“Mumeo anaitwa nani?”
“Ahmed Kajeme”
Mbali na kuhojiwa maswali mengi mfululizo Yusrath ilibidi ajibu sababu alikuwa ana shida na mwisho wa siku alihitimisha kwamba anahitaji usaidizi wa diffenda, wakamchukuwe Necka Golden,hilo halikuwa tatizo baada ya kusema ana shilingi elfu hamsini ya kuwapooza.
“Afande Chande,washa diffenda chukua askari ongozana na huyu mama”
“Sawa mkuu”
Ilikuwa ni amri,askari wanne wakatoka nje akiwemo dereva, Yusrath akapanda mbele kwenye diffenda askari wengine wakaruka nyuma,dereva akageuza gari kwa mikwara, namna alivyolizungusha utadhani aliambiwa kuna uvamizi wa benki mahali.
Walivyofika ‘Riverside’ Yusrath akawa ana kazi ya kuwaelekeza askari njia,kata kulia kunja kushoto nyoosha.
Mpaka walivyofika,nje ya geti.Askari wawili wakashuka,Yusrath akapita mbele na kufungua geti,akanyoosha mpaka kwenye nyumba na kufungua mlango!Wakamkuta Necka Golden yupo kwenye kochi amelala,hana habari hata kidogo!
“Ndio huyu hapa”
Yusrath akasema, askari wakamtizama Necka Golden,aliyeonekana kushtuka na kukaa vizuri kwani mbele yake alitambua wamesimama polisi, kutokana na jezi walizovaa.
“Nadhani unajua kwanini tupo hapa,leo tunaondoka wote”
“Kwa kosa gani?”
Necka Golden akauliza kwa ujasiri.
“Utajua hukohuko”
“Ni haki yangu kujua,hizo sheria za wapi mnaleta?”
Kuanzia hapo,askari hawakuwa na muda wa kujibizana naye,wakamvuta kwa nguvu mpaka nje wakimkokota,alichokifanya Yusrath ni kutoa begi la Necka pia, akaliweka kwenye diffenda,akarudi ndani mpaka alivyosikia diffenda limeondoka,akashusha pumzi nzito ya kuchoka!

*****
Ahmed Kajeme,alifanya kazi zake kwa umakini mkubwa sana wakati mwingine hakupumzika kabisa alielewa nyuma yake kuna familia inayomtegemea, alichotakiwa kufanya ni kuhakikisha inapata mahitaji yote ya msingi,ndiyo maana siku zote aliwafikiria wanaye waje kusoma shule nzuri za kimataifa.Hilo aliamini lisingeweza kutokea kimiujiza, isipokuwa ni kujituma sana!Licha ya kwamba swala la mkewe kumsaliti lilimuumiza lakini alimuomba Mungu alisahau kabisa kwani aliamini Yusrath atabadilika na ameshajifunza kutokana na makosa,akaapia kumpenda na kumuonesha mapenzi yote!Kichwa chake kilivurugika zaidi baada ya kupigiwa simu na mkewe akimwambia kwamba Necka Golden, yupo nyumbani kwake mbaya zaidi anafanya fujo,maswali aliyokuwa anajiuliza amepajuaje kwake?Na ametokaje jela?Hata hivyo alikumuumiza sana kichwa sababu alishachukua maamuzi ya kumuweka kituo cha polisi kwanza kwa ajili ya usalama wa mkewe,alimuhofia sana mwanamke huyo kutokana na tukio la mauaji alilolifanya kipindi wanasoma chuoni Makumira,akiwa ofisini kwake alitumiwa ujumbe kutoka kwa Rhoda ambao ulimshtua sana.
‘Kumbe naww umo eeh,nyie wanaume nyie.Nilikuwa nakuona wa maana sana mtaratibu kumbe ndio walewale,ndio nn kutembea na makahaba,ulivyokuwa na dharau ukamuonesha mpaka kwako’
Ahmed aliurudia ujumbe huo mara mbilimbili,akashindwa kuelewa vizuri lakini hilo halikumsumbua akapuuzia lakini baadaye meseji nyingine ikaingia,hiyo ilieleza kila kitu kilichotokea siku Necka alipofika nyumbani kwake,Ahmed akashindwa kuvumilia,hapohapo akampandia Rhoda Denis, hewani.
“Sikia Rhoda,naomba usijifanye unanijua sana.Tafadhali,kaa mbali na familia yangu,isitoshe pesa yako ushalipwa,achana na mimi achana na mke wangu”
“Etiii niachane na mke wakooo,unachekesha wewe una mke wewe sasa?Wenye wake wakiitwa utatoka nawewe?Utaishia hivyohivyo,kulea watoto sio wako mbwa weweee”
Simu ikakatwa,kijembe alichopigwa Ahmed kikamfanya atafakari kidogo kina maana gani,alivyotulia sana akawakumbuka Faad na Faisal watoto wake mapacha,akatafakari kwa muda na kupuuzia,akaendelea na kazi zilizokuwa mezani,hata hivyo hakuacha kuuliza hali ya baba yake hospitali,ambapo aliambiwa kwamba alihamishwa hospitali kutokana na usalama.

*****
Siku zilizidi kukimbia kwa kasi ya kimbunga,hatimaye zikabaki siku mbili tu ili Ahmed arejee jijini Dar es salaam,hakutaka kuondoka hivihivi bila kuwatafuta wenyeji wake Bwana Kimaro na Massawe,siku hiyo ya Jumamosi wakapanga waende Marangu mtoni,wakale Mtori,kiburu,kitawa,ngande na vyakula vyote vya asili ya Kichaga.Gari likawashwa, Ahmed akagharamia mafuta.
“Aisee Meku,pale Marangu mtoni.Nataka nikupitishe tukanywe kwanza Mbegee na Ndafu”
“Ndafu ndio nini?”
Ahmed akauliza.
“Nyama ya mbuzi mzima,anayelia mee meee”Akaweka utani kidogo!
“Mbuzi mzima?”
“Ni vigumu kukueleza Meku,sinde sinde sinde”
Bwana Masawe,alionekana kuchangamka sana asubuhi hiyo wakiwa ndani ya gari, wanashusha mlima kupitia njia ya Mamba,kona kona zilikuwa kali na nyingi,ndani ya gari walipiga stori nyingi sana,wakimsihii Ahmed arudi tena kwani Mkoa wa Kilimanjaro ni mzuri na hali ya hewa yake ni safi.
“Inabidi nikirudi nije na familia yangu,tukapande mlima Kilimanjaro”
“Utatutafuta”
“Lazima nifanye hivyo,mshakuwa ndugu zangu mjue”
Safari yao iliwachukuwa dakika arobaini na tano, mpaka kufika Marangu Mtoni,hapo walipaki kwenye kilabu cha pombe wakanunua mbege na kuanza kunywa,kila kitu kwa Ahmed kilikuwa burudani akaanza kujipiga picha za ‘Selfie’ na kumtumia mkewe akimwambia siku moja wafike Moshi kutembea kwani ni mkoa mzuri wenye watu wakarimu sana.
“Eeeeh,hiyo ndio mbege?”
Yusrath akatuma meseji akiuliza swali kupitia mtandao wa ‘WatsApp’
“Ndio mke wangu,tamu sana.Nitakuletea nawewe”
“Inalewesha sana?Mimi naisikiaga tu,hiyo uliyoshika inaitwaje sasa?”
“Hii,inaitwa Kata”
Ahmed alimjibu,akaweka simu mfukoni wakaendelea kupiga stori za hapa na pale.
“Ndio bwana,mimi nina watoto wawili”
Bwana Kimaro,alizungumza.
“Wote Mama mmoja?”
Ahmed akauliza.
“Hapana,kila mtu na mama yake.Huyu wa pili ndio naishi naye,nimekuja kugundua kitu kimoja kuhusu wanawake.Sijui kama nitakuwa sahihi sababu hawaeleweki,baadhi ya wanawake wengine ni vishoia sana”
“Kwanini unasema hivyo Kimaro?”
Kila mtu akawa makini kumsikiliza Kimaro,akapiga pafu moja la Mbege na kuwatizama wote kwa zamu.
“Wanawake unajua kwamba wametuzidi akili,hilo msikatae.Pindua huku na kule,wametuzidi akili.Mwanamke anaweza akachit kwa miaka hata mitano na usigundue,mna habari hiyo?”
Somo hilo likamuingia Ahmed,akatulia na mawazo yake yakaenda kwa Mkewe Yusrath akaona kama analengwa yeye.
“Lakini sisi ni rahisi kugundulika,dakika sifuri tunashikwa.Tangu uzaliwe,ushawahi kuona ama kusikia jamaa anamgonga mke wa mtu alafu kachukuwa simu ya huyo hawara anamtukana mwanamme mwenzake yaani mume wa huyo hawara?”
“Hapana”
“Sasa nisikilizie sasa hawa mademu,anajua una mke!Alafu anaona haitoshi anachukua namba za mkeo anamtukana matusi,ndio kilichonitokea mimi juzi kwa Mama Manka,chaaa!Niliokota Malaya mmoja pale Majengoo jimama hiloooo”
“Enheee”
“Alafu siku hiyo alinikuta nishakunywa Konyagi nusu chupa,nikampiga shoo ya kibabe Mekuu..Ilikuwa shoo shoo,mpaka Yule Malaya akaanza kusema Meku meku mekuu mekuuu mekuuu mekuuu yesuuu na Mariaaa,yewomiiii mekuu mekuuu nafyaaaa”
Hapo Ahmed na Bwana Masawe wakaangua vicheko kwani Kimaro alibana pua kidogo ili aige sauti ya mwanamke anayemzungumzia,wote wakacheka stori zikazidi kuchanganya.
Wakaaga na kuingia mjini ambapo huko walitafuta Mtori na kula,Ahmed alifurahi sana siku hiyo, alivyorudi usiku alikuwa hoi bin taaban akajitupa kitandani na kulala.

Siku yake ya kuondoka ilivyofika akaingiziwa kiasi cha shilingi milioni tisa kwenye akaunti yake,akatabasamu na hakutaka kuigusa alipanga akifika tu aanze ujenzi wa nyumba yake mara moja!Tiketi ya ndege ilikuwa tayari, alichokifanya ni kupakua kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya zawadi za mkewe pamoja na watoto wake,akamkumbuka Pia Hadima dada wa kazi,akapita kwenye maduka mbalimbali akanunua nguo,cheni,viatu na simu mpya kwa ajili ya mkewe Yusrath.Jioni hiyohiyo akaweka vitu vyake sawa,akapanda taxi iliyompeleka mpaka KIA, uwanja wa ndege,saa moja kamili jioni,akawasili baada ya nusu saa akawa tayari ndani ya ndege.

*****
“Mimi si nilikwambia,siku hazigandi baby.Hatimaye nimerudi,fungua huu mfuko kuna zawadi zenu”
“Ahsante baby”
“Huu wa Hadima”
“Wa naniii?”
Yusrath alivyosikia hivyo akauliza,wivu ukamshika!
“Hadima”
“Mmmh,umemnunulia nini?”
“Nguo,kuna sketi na viatu”
“Mpaka size yake unaijua?”
Swali hilo Ahmed hakujibu,alishaelewa Yusrath nyuma ya hayo kuna wivu,akatoa mifuko ya nguo za watoto wake wadogo mapacha na mfuko mwingine wenye simu ya gharama tena ya kisasa aina ya Iphone 5.
“This is for my beautiful wife”(Hii ni kwa ajili ya mke wangu mrembo)
Ahmed alizungumza hivyo huku akifungua boxi hilo la simu,Yusrath alipigwa na butwaa, hakutegemea kwani ndoto yake siku moja ilikuwa amiliki simu kama hiyo ili aendane na wakati,alifurahi na kum-miminia mabusu kedekede mumewe!Siku hiyo ilikuwa siku ya furaha kwao.

***
Ahmed hakutaka kuliweka swala hilo lisubiri kwani aliamini muda sio rafiki tena kwake,alichokifanya bila kumuamsha Yusrath asubuhi na mapema, aliwasha gari peke yake na kunyoosha mpaka Mbezi,Makabe kwenye kiwanja chake alichopanga aanze ujenzi mara moja!Aliwasili,akawasalimia wakazi wa eneo hilo na kuwauliza tofali zinapatikana wapi,alivyoelekezwa hakupoteza muda na wakati, akanyoosha mpaka eneo wanalouza matofali,akawasalimia vijana wa pale.
“Nahitaji tofali mia tano,nitapata?”
“Ndio Kiongozi,zinaenda wapi?”
“Hapo chini kwenye mnara”
“Zipo,gari lipo njiani linakuja.Nenda kalipie pale”
Hicho ndicho,kilichotokea Ahmed akalipia pesa kwa keshia,akapewa risiti.Hazikupita nusu saa gari likafika,vijana wakaanza kupakia matofali,kazi ilivyoisha wakaanza kuongozana mpaka kwenye saiti,wakaanza kushusha lakini walivyofika katikati akatokea jamaa mmoja,aliyenyoa kiduku kichwani akamsogelea Ahmed karibu.
“Samahani broo”
“Bila samahani”
“Wewe ndio umeagizwa na Mr.Kowero uje kushusha matofali?”
Ahmed akatulia kidogo na kumkagua kijana huyo,ambaye kwa harakaharaka alimtafsiri kama mvuta bangi na anahitaji pesa.
“Ndio nani?”
“Mwenye eneo hili,hua nalinda hapa”
Ahmed hakujibu chochote,akampuuzia na kuwapa maelekezo vijana washushe matofali mengi wayapange pembeni,matofali yakaendelea kushushwa.
Lisaa limoja baadaye, baada ya matofali kumalizika kushuka,gari aina ya Prado,likapaki kandokando ya kiwanja hiko.Akashuka mzee mwenye mvi kichwani,kavaa miwani kubwa ya macho!Sura ya mzee huyo haikuwa ngeni machoni mwa Ahmed,alishawahi kumuona eneo hilo siku aliyofika na Yusrath.
“Kijana hujambo?”
Mzee akamsalimia Ahmed.
“Sijambo,shikamoo”
“Marahaba,vipi?Itakua umekosea nini?”
“Kukosea nini?”
“Wewe sindo umeshusha haya matofali hapa?”
“Ndio Mimi”
“Sasa umeshusha,sijakuelewa vizuri.Nani amekuagiza?”
Maswali yakawa mengi,ilibidi atulie kidogo na kumtizama mzee huyo kwa umakini.
“Kuniagiza?Hakuna aliyeniagiza,nataka kuanza ujenzi nataka kujenga nyumba yangu hapa”
“Utajengaje kwenye eneo langu?”
“Eneo lako?!”
“Ndio,eneo langu.Tangu miaka ya tisini,ndio maana nakuuliza”
Ahmed akahisi kama anaishiwa nguvu za miguu,mapigo yake ya moyo yakaanza kupiga kwa nguvu,akaliangalia eneo hilo kwa umakini akidhani wenda amekosea lakini haikuwezekana hata kidogo sababu ndio hapo, walifika na Yusrath mara ya mwisho.
“Yaani,huoni hata hizi bikoni?Niliziweka mimi hizi miaka minne iliyopita”
Mzee aliyejitambulisha kwa jina la Kowero,akamuonesha Ahmed mawe yaliyopimwa na afsa ardhi yapo chini yamechimbiwa,akamzungusha eneo zima,mbaya zaidi akaingia ndani ya gari lake na kumtolea karatasi ya ramani ya kiwanja hiko,ambapo tayari kilikuwa kimepimwa na serikali na hati ya kiwanja hiko anacho!Bila kupenda Ahmed alichuchumaa chini na kuweka mikono yake kichwani,jasho jembamba likaanza kumtoka!


Kila kitu katika maisha yake kilivurugika,akahisi kama amebeba dunia nzima kichwani.Mambo yaliyokuwa yanamtokea kwa mfululizo aliyatafsiri kama mikosi na laana,hakuelewa amemkosea nini Mungu wake aliye juu!Alivyotaka kusimama akashindwa,alikosa nguvu za miguu hakuelewa ni hatua gani achukuwe kwani kwa harakaharaka alijua tayari ametapeliwa kiwanja, japokuwa jambo hilo hakutaka kulipa kipaumbele sana,sura ya Yusrath ikamjia kichwani akasimama wima kama Komandoo na kumtizama Mzee Kowero, aliyekuwa mbele yake.
“Pole sana kijana”
Mzee akatoa pole lakini hilo kwa Ahmed halikuwa na umuhimu sana,pole isingemrudishia fedha zake ama kiwanja chake,akanyoosha moja kwa moja mpaka kwenye gari lake,namna alivyolirudisha nyuma iliogopesha,tairi zilizunguka na kuchota mchanga,akaweka gari sawa na kukanyaga mafuta mengi,likatoka kwa kasi mpaka kwenye makutano ya barabara mbili,Kusini na Kaskazini hapo akashusha kioo na kumuona Mtu aliyekuwa anapita,amebeba mfuko wa nailoni mkononi.
“Samahani,naomba kuuliza”
“Bila samahani broo”
“Mambo vipi?”
“Poa tu”
“Hapa serikali za Mitaa ni wapi?”
“Serikali za mitaa?”
“Ndio”
“Kule juu,nenda moja kwa moja na hii barabara,utakuta transfoma njia inayoingia kushoto.Hapohapo”
“Sawa ahsante”
Gia ikapigwa,Ahmed akalitoa gari na kunyoosha mpaka Serikali za mitaa akifuata maelekezo,huko ndipo angejua kama ni kweli alitapeliwa ama anachezewa michezo ya kihuni,moyo wake uliuma akaomba Mungu alipite jaribu hilo salama,kwake hiyo ilikuwa changamoto kubwa sana!
Alivyokunja kona ya kushoto baada ya kuona transfoma mbele yake,akaweka gari vizuri na kushuka.
Akayafuata madarasa yalipo,ndani kulikuwa na watu wengi kiasi na wengi wao walikuwa ni wazee wa makamo.
“Habari,nahitaji kuonana na Mjumbe”
“Mjumbe?Mjumbe gani?Una shida gani?”
“Ni stori ndefu lakini ni mambo ya ardhi”
“Sawa,cha kukusaidia hapa uende ofisi za Afsa mtendaji.Tena leo Jumanne wazee wa baraza wapo pale,wahi”
“Hizo ofisi ziko wapi?”
“Pale pale Mbezi stendi,upande wa juu”
“Ahsante”
Ahmed akageuka na kuondoka zake,akaonekana kama mtu aliyechanganyikiwa vile,akalitoa gari kwa kasi ili awawahi wazee hao wa baraza,haikuchukuwa muda mrefu kufika kwani mwendo alioutumia ulikuwa wa kasi sana,alivyowasili akapaki na kushuka!Akatembea kwa haraka mpaka ofisini, ambapo huko alieleza shida na kuambiwa asubiri baada ya dakika kumi,akakaa kwenye benchi akiwa mwenye mawazo mengi sana!Hakuelewa afanye nini na msaada pekee ulikuwa ni hapo,hazikuisha dakika kumi akaitwa,akaingia ndani ambapo humo alikutana na watu watatu,mmoja mzee wa makamo wawili wamama!Akajitambulisha jina lake na kuongea shida yake.
“Unaishi wapi?”
“Ubungo Kibangu”
“Kiwanja hiko umesema kipo wapi?”
“Pale Mbezi,Msakuzi”
“Ebu jieleze vizuri ulisema ulikuwa safarini,ukamtumia mkeo pesa?Hapo sijaelewa vizuri”
Ahmed,akashusha pumzi ndefu na kuanza kujieleza tena kila kitu kinagaubaga.
“Documents alikuonesha?”
“Bado,lakini atanipa amesema”
“Samahani,naweza kukuuliza swali”
“Uliza Mzee”
“Lakini,sio kwamba nakukejeli”
“Uliza tu”
“Umesoma mpaka darasa la ngapi?”
“Chuo Kikuu,nina degree”
“Sasa mbona unafanya mambo ya kitoto?Unanunuaje Asset ya pesa nyingi kama hiyo bila kuhakikisha mwenyewe,kabla ya kununua ulienda kwa mjumbe, labda uliuliza majirani wa eneo hilo?”
“Sikununua mimi”
“Tunahitaji mtu,aliyenunua uje naye hapa ndio ataweza kutusaidia”
“Naomba mnisaidie tafadhali”
“Tukusaidie kwa kitu gani?”
“Kiwanja changu kile”
“Okay,cha kukusaidia labda pale tutakuandikia barua ukaombe STOP ORDER,kitakachofuata hapo ni mahakamani,upo tayari?”
“Ndio”
Kilichofuata hapo,Ahmed ni kuandikiwa barua ikapigwa muhuli ili akapewe stop oda sehemu husika,akashukuru na kuondoka zake!
Kitendo cha kufika nyumbani alianza na maswali mfululizo,siku hiyo Yusrath alimiminiwa maswali mengi mno!
“Ndio mme wangu ni ndugu yangu kabisa,haiwezekani kile kiwanja ni chetu”
Yusrath nayeye akaweka hoja mezani,kujitetea.
“Documents ziko wapi sasa?”
“Zipo,nitamfuata”
“Nipe namba za huyo ndugu yako aliyekuuzia”
“Nitakupa mme wangu”
“Una uhakika,hajatutapeli?”
“Nina uhakika,ni ndugu yangu kabisa.Hawezi kunifanyia kitu kama hiko”
Ahmed,akarejewa na matumaini mapya kwani Yusrath alimuhakikishia kwamba kiwanja hiko alikinunua kwa ndugu yake,hilo likamfanya siku hiyo akae mezani ale chakula cha mchana,akaingia chumbani na kujitupa kitandani kwani alikuwa amechoka sana!
Yusrath alikuwa katika wakati mgumu,usioweza kuelezeka,wasiwasi ulimjia na alianza kuchezwa na machale kwamba Sameer alimfanyia michezo ya kihuni na wenda alimtapeli pesa alizompa,akaumia moyo mno.
Hakukaa sana Seblen mlango ukagongwa dada wa kazi,akapita na kuuendea mlango!Akaufungua,mapigo ya moyo ya Yusrath yakapiga kwa nguvu, akajikuta anasimama bila kupenda,mlangoni walisimama wasichana wawili,mmoja alimtambua alitokea benki,akajua tayari kimenuka na watu hao wamefuata deni lao.
“Habari,twendeni tukaongee nje kidogo”
Ilibidi afanye hivyo,alijua nini maana yake kama Ahmed angezinduka kutoka usingizini ni lazima angehoji na hapo ndipo yangemkuta makubwa,hakutaka jambo hilo litokee ndio maana akatoka nao nje kabisa, wakasimama getini.
“Mbona tunakupigia simu hupokei?Meseji hujibu?Tukuelewe vipi?Hapa tumekufuata tu kiuungwana,ilibidi tuje na watu wa mnada”
Yusrath alitoa macho yake kusikia habari za mnada,alijua ni vitu gani alivyoweka bondi hiyo ilimaanisha wangepita mnada,seble nzima ingebaki nyeupe yaani mpaka vyombo wangechukua na vijiko, mbaya zaidi Ahmed hakuwa ana habari yoyote ile,Yusrath alihisi kutetemeka mpaka meno,sababu muda mfupi alitoka kuhojiwa kuhusu kiwanja.
“Subirini,pesa yenu keshokutwa nitawapa”
“Tumemuheshimu Sista Leah vinginevyo dada angu…Unajua hizi ni kazi,sisi tunakatwa kwenye mishahara yetu,basi ungekuwa unafanya marejesho hata ya mwezi.Hufanyi..”
Msichana huyo aliongea akilalamika akionekana mwenye gubu kuliko kawaida.
“Keshokutwa nitawalipa pesa zenu,nipeni keshokutwa tafadhalini”
“Dada usipolipa,tutakuja na watu wa mnada hapa i swear,tusilaumiane”
“Sawa msijali”
Kwa siku alizohaidi na kiasi kikubwa alichotakiwa kulipa, vilikuwa ni vitu viwili tofauti,hakuwa ana uwezo huo na hakuelewa ni wapi angepata fedha hizo mbali na hapo,hakuwa na mtu wa karibu ambaye angeweza kumkopa.
Akachoka akili,mwili mpaka mfumo wote wa fahamu ukaacha kufanya kazi vizuri!Kilichomfanya achanganyikiwe zaidi ni kitu kimoja,siku inayofuata Ahmed alimwambia atafute nyaraka za kiwanja alichonunua,jambo hilo lilimchanganya zaidi, akatamani kutoroka nyumbani lakini hakujua aende wapi.
Ahmed alilala kwa masaa mengi sana,haikuwa kawaida kwake hata siku moja hiyo ikamfanya mpaka Yusrath ashangae na kudhani wenda alifia usingizini,alivyoingia chumbani na kumuangalia vizuri akagundua bado anahema,Ahmed alilala tangu mchana wa saa nane, mpaka saa mbili ya usiku,ilivyofika saa tatu usiku ndipo alipozinduka,hata yeye alishtuka sana!Akajishangaa sana licha ya hayo yote akagundua kwamba alivyokuwa mkoani Kilimanjaro,alifanya kazi bila kupumzika.
“Nikuletee chakula huku au utakuja kula seblen Mme wangu?”
“Sijui kama nitakula”
“Kwanini baby?Kaoge basi kwanza.Ujue umelala sana leo”
“Yeah,ushaongea na ndugu yako huyo.Kuhusu kiwanja hiko?”
“Nishaongea naye”
“Amesema nini?”
“Kesho nimuone”
Yusrath alidanganya ili kumfariji mumewe lakini hakufanya jitihada zozote zile,hapo Ahmed kiunyonge akiwa bado na mawazo akatembea mpaka bafuni huko akaoga,alivyotoka akakuta ameletewa chakula chumbani tayari,akala akaletewa na juisi ya Machungwa,akashushia.
“Juisi tamu,kaniongeze tena”
Yusrath akatii amri,akachukua tena glasi nyingine!Ahmed akanywa akashukuru,alichokifanya Yusrath ni kuingia bafuni,akajimwagia maji na kuruka kitandani,hapo alianza kumchokoza Ahmed akimpapasa huku na kule,akapeleka mkono wake mpaka kwenye mjusi wa Ahmed ambaye alianza kuinuka taratibu.
Maswala ya kupima afya,hayakuwepo tena kilichofikiriwa hapo ni tendo la ndoa,hapohapo Ahmed akamgeuza mkewe na kumpindua vizuri,wakaanza kulana denda huku mkono mmoja wa Ahmed ukidarizi maeneo mbalimbali,Yusrath hakujiweza tena!Akatulia tuli,akimuacha mumewe ashughulike,alichokifanya Ahmed ni kumlaza Yusrath kifudifudi yaani akawa amelalalia tumbo,akapanda juu yake akamlalia mgongoni na kumpenyeza nyoka wake,makeke yakaanza hapohapo.Lakini cha ajabu na kilichomshangaza Yusrath ni kitendo cha Ahmed kufika mshindo ndani ya sekunde tano tu,akatulia.Haikuwa kawaida ya Ahmed hata kidogo, kuboronga kwenye mechi na kutoa boko namna hiyo,hata yeye alijishangaa.
“Baby,are you okay?”
Yusrath aliuliza,mizuka yake ilikuwa imepanda mara ghafla ilikatishwa.Ahmed akatulia na kulala chali!
“Niko poa”
“No,haupo sawa.Wewe ni mme wangu,nakujua una shida gani?”
“Niko sawa Yusrath”
“Mme wangu,tangu nikufahamu.Haijawahi kutokea hali kama hii”
Yusrath alikuwa ana kila sababu ya kulalamika sababu alimuelewa Ahmed ni mtu kazi, hasahasa katika kwichi kwichi!
“Yes nina mawazo baby”
“Unawaza nini?”
“Kiwanja kile,nahisi kama nitatapeliwa”
“No baby,usiwaze utakipata”
“Kweli?Huyo ndugu yako unamuamini kweli?Hajatufanyia mambo ya kihuni?”
“Hawezi”
Yusrath aliendelea kumpooza Ahmed kwa maneno matamu lakini hiyo haikufanya waendelee na tendo hilo.
Swala la Kiwanja kwa Yusrath halikuwa kubwa sana,kilichomuumiza akili ni mkopo wa benki, ambao muda wowote watu hao wangefika na kufanya vurugu,ilibaki siku moja baada ya kukucha akamilishe mkopo huo ambao tayari ulizidi kwa riba ya asilimia thelathini na mbili,akapiga hesabu zake na kutoa akapata jawabu!
Asubuhi na mapema akaamka,bila kumuamsha Ahmed, akanyata taratibu mpaka kwenye kabati hapo alichukuwa funguo za gari na kuzificha kwenye kanga,akatoka nje kwa staili ya kunyata mpaka nje kwenye gari,akafungua taratibu.
“Kadi iko wapi?”
Akajiuliza huku akivuta vuta vitu,akavuta draw ya kwenye dashbod akaikosa,akateremsha kidude Fulani chaa juu, ambapo hapo hukaa kadi mbalimbali,akazitoa kadi zote,akazikagua vizuri moja ilikuwa kopi nyingine original,shida yake ilikuwa ni original,akaichukuwa na kufunga gari,alivyofika seblen akaficha chini ya sofa,akarudi chumbani na kuzirudisha funguo alipozikuta!
Ahmed,alikurupuka usingizini saa mbili asubuhi swali la kwanza kuuliza ni nyaraka za kiwanja chake.
“Nilimtumia leo meseji asubuhi hii,kaniambia niende saa kumi jioni”
“Wapi?”
“Tangi bovu”
“Anazo hizo documents?”
“Kaniambia niende,nadhani atakuwa nazo”
Hapo Ahmed akamtizama Yusrath, ilielekea kuna kitu alitaka kuropoka lakini akamezea,akaingia bafuni kuoga akajiandaa akabeba na funguo za gari.
“Chai baby?”Yusrath akauliza!
“Nimechelewa,nitakunywa ofisini”
Akaingia kwenye gari na kuondoka zake!

****
Mpango wa Yusrath kuchukua kadi ya gari ulikuwa ni kwenda kuombea mkopo mwingine ili azibe pengo analodaiwa benki,ilikuwa bora afanye hivyo kuliko akumbane na aibu iliyokuwa usoni kutokea!Shabaha yake ilikuwa kwa Mr.Ezekiel Christopher,mfanyabiashara ya madini.Aliamini pesa kama hizo kwa Mr.Ezekiel ni ndogo sana,hata hivyo alielewa angepatiwa tu sababu mwanamme huyo alishawahi kumtongoza, akimtaka kimapenzi kwa maana nyingine alijipanga kwa lolote lile mbeleni ili apewe pesa,ikiwezekana atoe hata rushwa ya ngono.Siku hiyo alijiandaa harakaharaka na kupiga simu akimuomba Mr.Ezekiel waonane!
“Njoo ofisini kwangu,Masaki”
“Sawa nakuja”
“Fanya haraka naondoka na ndege ya saa kumi jioni,ukichelewa hunikuti”
“Nakuja jamani Eze”
“Nakusubiri”
Yusrath,hakuwa na muda wa kupoteza akavaa haraka na kujipodoa vizuri.Kwa kuwa alikuwa mwenye haraka,alikodi pikipiki ambayo ilimpeleka Masaki,ofisini kwa Mr.Ezekiel Christopher!Kwa kuwa taarifa za Yusrath zilikuwepo,ilikuwa rahisi kupita mpaka ofisini kwa mwanamme huyo,mfanyabiashara!
“Karibu chaurembo”
“Nishakaribia”
“Za masiku,unazidi kuwa mtamu Yusrath kama hujazaa vile”
Mr.Ezekiel akatumia Kiswahili cha geto,kukaa sana migodini kulimfanya ajue lugha zote za kihuni.Yusrath hakupoteza muda,akasema shida yake ya pesa na kuhaidi angerudisha baada ya muda mfupi,zaidi na hayo akatoa kadi ya gari ili ajiaminishe.Mr.Ezekiel akachukua kadi ya gari na kuitizama!
“Gari ni lako?”
“Hapana,la mme wangu”
“Anajua?”
“Hapana”
“Kwahiyo,unataka kuniletea mimi balaa.Unajua kabisa,usipolipa pesa hizi,mimi gari nitaliuza hutoamini”
“Sio hivyo Eze,naomba nisaidie”
“Kwanza,shika kadi yako!Kingine nina wahi,unakumbuka ulivyonijibu nyodo siku ile?Ukaniangalia kama kinyesi,dunia ni duara.Sikiliza,toka ofisini kwangu”
“Eze…”
“Toka ofisini kwangu,pesa ninazo…”
Mr.Ezekiel hakumaliza sentensi yake,alichokifanya ni kutoa begi,akafungua zipu ndani yake kulikuwa na maburungutu ya pesa.
“Hizi hapa pesa lakini kwa dharau ulizonionesha siku ile pale,sikupi hata senti tano.Uliniambia nipambane na hali yangu,nawewe leo kapambane na hali yako”
Yusrath alitia huruma,hakutegemea kabisa maneno hayo yangetoka kwa mwanamme huyo,dunia kwake ikageuka ghafla ikawa chini juu,juu chini.
Hakuamini baada ya Mr.Ezekiel Christopher kutembea mpaka mlangoni na kuufungua, akasimama kandokando, mlangoni.
“Toka ofisini kwangu,utakula jeuri yako”
Hapo ndipo Yusrath alipoamini hakuna mzaha,akasimama na kuanza kutembea!Sio siri,alijiona ni mdogo kama kidonge cha pilton,matumaini yake yakafa kabisa.Hakuelewa ni nani angempa msaada wa pesa hizo,akatafakari sana lakini akakosa jibu,ilibidi tu arudi nyumbani na kutafakari njia nyingine mbadala.Ahmed alivyofika jioni,swali la kwanza kuuliza zilikuwa ni nyaraka zake.
“Karatasi amesema anazo,anaziangalia Mme wangu!Pale alipokuwa anaishi amehama”
Yusrath,alijitetea akimpanga mumewe ili amuweke sawa!
“Mpaka lini?”
“Ameniambia kesho”
“Saa ngapi?”
“Jioni”
“Mwambie mchana awe amezipata,nishamtafuta mwanasheria tayari”
Mapigo ya moyo ya Yusrath yakadunda kwa nguvu,alishaelewa nini maana ya mwanasheria kivyovyote vile ni lazima angegundulika na kuumbuka kwani siku zote mbio za sakafuni,huishia ukingoni.
“Okay Mme wangu nimekuelewa,pole na kazi”
Ahmed akatingisha kichwa bila kusema chochote akapitiliza chumbani,akaoga na kujitupa kitandani huko alitafakari namna ya kutoa milioni nne nyingine ili ampe mwanasheria wafungue kesi atetee kiwanja chake.

*****
Saa 09;30 asubuhi,Ahmed alikuwa seblen,anavaa soksi tayari kwa kwenda kibaruani.Kichwa chake siku hiyo kilikuwa na vitu chungumzima,hakuwa ana raha hata kidogo.Kiwanja chake kilimkosesha amani, amlaani sana Mzee Kowero ambaye aliamini alitaka kumdhulumu kiwanja ambacho alikitolea jasho kukipata,hata hivyo siku hiyo ilibidi akachukue pesa ili amlipe Mwanasheria ili jarada lifunguliwe mahakamani,alivyomaliza kuvaa soksi na kutaka kuingiza kiatu kwenye mguu,akaganda baada ya kusikia geti lake linagongwa kwa nguvu bila ustaarabu.Akatulia kidogo,Hadima akatokeza seblen.
“Mwambie huyo anayegonga hivyo,akome awe na adabu”
Ahmed akasema kutokana na kero ya kelele za geti,Hadima akatoka alivyofungua geti akashangaa kuona umati wa watu sita,wawili wanaume waliojazia wanne walikuwa wasichana wakiwa katika sare za benki aliyemtambua alikuwa ni mzee mmoja huyu alikuwa mwenyekiti wa serikali za mitaa,nyuma yao kulikuwa na gari aina ya Noah,pembeni gari kubwa aina ya Canter.
“Tumemkuta Mama?”
Hilo ndilo swali la kwanza kutoka kwa mwanamme huyo mrefu mwenye misuli.
“Ndio”
Kitendo cha kujibu hivyo,akasogezwa pembeni wakaingia ndani.Bila kubisha hodi,wakazama sebleni.
“Sam,anza na tivii hiyo chomoa waya hizo.Bosco kabebe friji”
Hizo ndizo kauli walizoingia nazo kitemi, bila kusalimia.Hiyo ilimfanya Ahmed aliyekuwa kwenye sofa,asimame wima na kuwashangaa!


Ndani ya nyumba yake waliingia wageni wa ghafla mbaya zaidi walitumia utemi bila salamu,kilichomfanya ashangae ni watu hao kuanza kubeba vitu, huyu alikuwa karibu na tv,mwingine yupo kwenye friji.Hiyo ilimfanya Ahmed amsogelee mwanamme mrefu aliyekuwa kwenye tv anahangaika kuchomoa waya ili aibebe begani.
“Mbona siwaelewi?”
Ahmed akauliza huku akimvuta jamaa huyo kando,alikuwa ana kila sababu ya kufanya hivyo sababu ilikuwa ni kwake,wakati mwingine alidhani watu hao ni majambazi wamemvamia lakini kilichomtoa wasiwasi ni mjumbe wa serikali za mitaa.
“Broo,ebu niache.Kifupi hapa huna chako tuache tufanye kazi yetu.Tukitoka hapa,tunaingia jikoni kusomba”
Hakuna hata mmoja kati yao aliyetumia ustaarabu,Ahmed alikuwa njiapanda.Akamuendea Mjumbe wa serikali za mitaa na kumuuliza kulikoni.Akiwaomba awaambie vijana hao watulie kwanza ili wazungumze kwani hajui chochote!
“Wewe unaitwa Ahmed?”
Mjumbe akauliza,alikuwa ni mzee lakini sio sana!Kutokana na maisha kumchapa ilimfanya aonekane mzee wa miaka 60.
“Ndio mimi”
“Vijana,embu tulieni kidogo.Huyu ndiye mwenye nyumba kwahiyo msijali”
Hali ya hewa ikatulia,friji lililokua linaburuzwa likawekwa kwanza.
“Kuna nini?”
Ahmed akauliza tena.
“Hawa,wametoka benki.Kuna mkopo ulikopa benki,umeshindwa kulipa”
“Mimiiiiiiii!?”
Ahmed akauliza kwa mshangao,hakuwa ana uhakika kama alishawahi kukopa benki.
“Hapana mzee sio huyo hajakopa yeye.Hapa sindo anaishi Yusrath?”
Msichana mmoja mwenye mwili mdogo, akaingilia kati na kuuliza.
“Ndio,Yusrath ni mke wangu”
“Ndio huyo amekopa hizo pesa,akaweka bondi”
“Haiwezekani,sio kweli.Labda Yusrath mwingine”
Ahmed alimtetea mkewe akiamini kwa asilimia zote mwanamke wake, asingeweza kufanya jambo hilo zito pasipo kumshirikisha,ndiyo maana kwa kiburi chote akajibu huku akitabasamu, mdomo akiwa ameukunja upande kwa dharau!Hiyo ilimfanya msichana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Arafa Abdi, afungue begi lake dogo na kutoa faili,akamsogelea Ahmed karibu.
“Sindo huyu?”
Arafa Abdi,akauliza!Juu ya karatasi ya kwanza, kulikuwa na picha ndogo ya Yusrath yaani passport size,Ahmed akatulia kidogo na kuangalia picha hiyo kwa ukaribu, haikujulikana kama hakuona vizuri ama anahakikisha.
“Ndio yeye”
Jibu hilo likafanya faili lianze kufunguliwa,mwandiko wa Yusrath ukaonekana akiwa ameandika,mkopo anaotaka na kwa muda gani atarudisha,zaidi na hayo karatasi nyingine zilionesha picha za vitu vya ndani akikiri kwamba endapo asipolipa,vichukuliwe na benki ili kufidia deni.
“Mungu wangu!”
Ahmed akasema kwa sauti ya chini,bado hakuamini kama mambo hayo mazito yangefanywa na Yusrath,akahisi kuishiwa nguvu kabisa kwani kama deni hilo, lisingelipwa mali zingechukuliwa mchana huo kweupe.
“Nisubirini nakuja”
Ahmed,akasema na kunyoosha mpaka chumbani ambapo huko,alisikia maji yanamwagika bafuni kumaanisha Yusrath anaoga, bila kujali akafungua mlango na kumkuta ana mapovu mwilini!
“Baby”
Yusrath akaita na kunawa kidogo uso ili aone vizuri,akafumbua jicho moja na kumuona Ahmed amesimama,kilichomshangaza alikuwa amevaa nguo, tofauti na siku zote akiingia bafuni.
“Bado hujaondoka kumbe?”
“Jimwagie maji haraka,kuna wageni wako”
“Wageni wangu?!”
Haikujulikana kama ameuliza swali nayeye ama ameshangaa!
“Yusrath fanya haraka”
“Kuna nini mme wangu lakini?”
“Jimwagie maji,uje”
Yusrath alishaelewa kwamba hakukuwa na dalili nzuri siku hiyo,akaanza kufikiria ni msala gani tena kaufanya,akakumbuka kiwanja na kuamini ni lazima Ahmed anataka nyaraka za kiwanja chake,akanawa haraka na kuanza kufikiria jinsi atakavyompanga Ahmed,hilo halikuwa tatizo kwake alivyomaliza kunawa,akaingia kabatini na kuanza kuangalia nguo ya kuvaa!
“Vaa hiyo hapo”
Ahmed akasema huku akimuoneshea gauni lililokuwa nyuma ya mlango.
“Hilo chafu baby”
“Kwani tunaenda wapi?Vaa nimekwambia kuna wageni wako wanakusubiri seblen”
Ahmed aliongea kwa jazba kubwa,kichwa chake kilivurugika kwa kiasi cha kutosha,hakuelewa amfanye nini mwanamke huyu mpumbavu ,aliyechukuwa mkopo benki bila kumtaarifu,kilichomuumiza moyo ni kitu kimoja,pesa nyingi kama hiyo hakuona imetumiwa kwa kazi gani.
Mara mia hata angeona kuna mabadiliko nyumbani hapo,ama amenunua vitu,lakini haikuwa hivyo!Hiyo ikazidi kumuumiza zaidi,akiwa anatafakari, Yusrath akawa tayari amemaliza kuvaa,wote wakaongozana mpaka seblen!
Kitendo cha kufika seblen akahisi kama nguvu za miguu zimemuishia,watu wa benki siku hiyo walimtisha,akamwangalia mumewe ambaye alikuwa amekunja sura azungumzi kitu.
“Dada tumekuja kufata pesa yetu”
Mmoja wa wasichana wa benki,akaongea kwa mashauzi.Ahmed,akamgeukia Yusrath!
“Ulikopa benki?”
Hilo ndilo swali la kwanza,kuuliza Ahmed akitaka kuhakikisha.Hadima yeye alikuwa jikoni na watoto,anachungulia ugeni uliokuwa seblen hata yeye ulimuogopesha mno!
“Nakuuliza ulikopa pesa benki?”
Lilikuwa ni swali lingine,kutoka kwa mwanamme huyu Ahmed, safari hii macho yake yalianza kuwa mekundu, mbaya zaidi aliuliza kwa ukali.
“Ndio mme wangu”
Yusrath alijibu kwa sauti ya chini,alijisikia aibu sana!Akatamani ardhi ipasuke,imfunike akimbie aibu.
“Kwanini hukuniambia?”
“Nisamehee Mme wangu nil…”
“Nijibu swali,kwanini hukuniambia?Pesa hizo ulizokopa?Wewe unafanya kazi wapi na…?”
“Kaka samahani”
Ilibidi msichana mwingine,mrefu mnene awakatishe kidogo,ilielekea kuna jambo alitaka kuzungumza!
“Niya yetu ya kuja hapa,ni kupiga mnada hivi vitu,turudishe pesa leo saa kumi.Sasa mnavyoendelea kubishana hapo,haitoweza ku make sense!Cha kufanya,tunaomba tuchukuwe vitu,nyie mtaendelea baadaye”
Kauli hiyo ilimfanya Ahmed,atafakari mara mbilimbili,vitu vyake alivyopambana kwa muda mrefu alafu viondoke kiurahisi namna hiyo,akamtizama kila mmoja kwa zamu na kuuliza ni kiasi gani cha pesa kinadaiwa,alivyojibiwa akamrudia Yusrath.
“Unajisikiaje?Nakuuliza,unajisikiaje?Halijaisha hili unaleta ji….paaaaaa”
Kila mtu hakuamini,kilikuwa ni kibao kilichomfikia Yusrath upande wa sikio la kulia yaani kofi,likamfanya ayumbe na kurudi nyuma akapepesuka mpaka ukutani akahisi kama sikio limeziba, Ahmed alivyotaka kumfuata aendelee kumpiga mwanamme mmoja,akamshika kwa nyuma na kumvuta.
“Niachie”
Ahmed akasema kwa jazba,anahema kifua chake kinapanda juu kinarudi chini,machozi ya hasira yanamtoka.
“Kiongozi,punguza hasira.Mambo haya ya kawaida sana,kumpiga haitosaidia!Wewe mwanaume,utapata kesi bure”
Akatulizwa huku ameshikiliwa,kilikuwa ni kitendo cha ghafla,mpaka Ahmed kutulia ilichukuwa dakika kumi nzima,ndipo hasira zake zikashuka lakini hilo halikubadilisha kitu,kilichotakiwa hapo ni pesa ama vitu visombwe.
“Nisikilizeni,nina milioni moja na nusu.Nitawapa leo,nyingine kesho”
“Kaka haitowezekana”
“Naomba niji commit,hata kwa maandishi.Kesho nitawamalizia, leo nitakuja hapo benki niongee na bosi wenu”
Uhakika wa kupata pesa hiyo kesho yake,ulikuwepo ndio maana alijiamini,hakuwa na jinsi zaidi ya kufikiria kwenda benki nyingine, ambapo huweka akiba yaani ‘Fixed account’pesa hizo alipanga asiziguse lakini hakuwa na jinsi,ilikuwa ni lazima aandike barua ili benki impe pesa zake.
“Kaka,kesho tutakuja hapa.Hatutokusikiliza tena”
“Kabla hamjaja,nitakuwa nishawapa”
Ahmed akashika peni huku mikono yake inatetemeka kwa hasira,akapewa karatasi ili aandike, jambo hilo likafanyika.
“Pole sana,kaka angu”
Msichana huyo akatoa pole,wote wakaaga na kuondoka zao!Hapo ndipo Yusrath akajua tayari amekwisha na kihama kimefika kwani walibaki peke yao,akaanza kulia kwa kwikwi,akatembea kwa magoti mpaka kwa Mumewe,akiomba asemehewe.
“Unataka nini kutoka kwangu Yusrath,roho yangu?Nife ufurahi au?”
Ahmed akasema kwa uchungu,machozi yakaanza kumlenga jicho moja likaanza kudondosha chozi, likachuruzika mpaka shavuni.Akamtoa Yusrath miguuni kwake,akasimama na kunyoosha mpaka chumbani ambapo huko hakuelewa anaenda kufanya kitu gani.Alivyofika,akaegemea ukuta na kuanza kulia machozi kwa uchungu!
“Mme wangu,nisamehee”
Yusrath akiwa nyuma yake,alitokea na kuomba msamahaa!
“Naomba niache kwa sasa hivi sipo sawa. Kingine,nachokuomba! Nikirudi nisikukute.Nenda kapumzike nyumbani,ukihisi umetulia umeacha mapepe nitafute”
“Mme wangu,tayari nimeacha.Nimejifunza kuto..”
“Nenda Yusrath,sitaki kujua hizo pesa ulikopa benki ukazifanyia nini,sababu najua hukufanya cha maana. Hivi,shetani gani amekuingia mbona hukuwa hivi?”
“Ahmed na..”
“Nikirudi,sitaki kukuona”
Ahmed alimaanisha,akatoka chumbani na kwenda nje,huko aliingia ndani ya gari na kupiga honi,Hadima akatoka na kufungua geti,akalitoa gari nje bila kujua ni wapi anaelekea!

******
“Out of my office,nilishakwambia mara ngapi hunielewi.Juzi ulichelewa,do you think this is your dad’s office,nimemaliza.Mark,ondoka au niite security”
“Nisameheme Madam sito..”
“No way,Your fired”
Zilikuwa ni kelele kutoka kwa Lissa Mnzava,zilienea mpaka nje!Siku hiyo aliwaka mno,mbele yake alisimama Mackdonald Urassa,afsa manunuzi wa kampuni hiyo.Anafokewa kama mtoto mdogo na mwanamke huyo mdogo kwake, ambaye aliachiwa madaraka ya ofisi nzima na bilionea George Charles,tangu aanze kazi katika kampuni hiyo, alishawafukuza wafanyakazi kumi na mbili Mackdonald Urassa angekuwa wa kumi na tatu.Lissa Mnzava,alijisikia akajiona yeye ndio yeye,ofisi nzima ilimuogopa ikitokea siku akawahi kabla ya mfanyakazi basi siku hiyo kazi hana.
Hakujali msamahaa wowote ule,maamuzi yake yalikuwa ni hukumu moja kwa moja!Ofisi iliendeshwa kwa staili hiyo ya kidikteta,wafanyakazi wakazidi kuwa waoga walitamani hata George Charles arejee kutoka nchini China lakini hata alivyorejea,hakuwa na sauti tena.
“Mimi sina cha kuongea,kama ameamua uache kazi.I can’t help you”
Siku hiyo Maria Didas,alinyoosha mpaka kwa George Charles, akiomba asamehewee.
“Niombee msahaa bosi,sitorudia tena”
“Kwani umefanya nini?”
“Nilisahau kumpelekea kahawa ofisini kwake,nilikuwa naprint ivoices za TRA ala…”
Kabla Maria Didas,hajamaliza sentensi yake mlango ukafunguliwa akaingia Lissa,akamtizama Maria kwa jicho kali lililojaa dharau.
“Bado hujaondoka?George hawezi kukusaidia kitu,ondoka Maria nisikuone hapa”
Kauli hiyo ilimfanya George amtizame Maria kwa macho ya huruma lakini hakuwa na jinsi,mchumba wake ndio keshasema aliogopa kupinga kauli yake,hiyo ndio ikawa siku yake ya mwisho kwa Maria kufanya kazi katika kampuni hiyo!
“Baby,imiss you”
Maria alivyoondoka,Lissa akadeka akatembea mpaka kwenye kiti kikubwa cha George Charles,akaburuza kiti kwa nyuma kidogo na kumkalia mapajani.
“Wana kiss you”
Lissa akapeleka mdomo lakini George akakwepesha.
“Ofisini hapa please,show some respect”
“So what?Unaogopa nini?”
“What if mfanyakazi akiingi…..”
Lissa akalizimisha,akatoa ulimi wake wakaanza kulana denda kimahaba!

***
Maisha ya Geoge Charles na Lissa Mnzava yalikuwa ya raha mustarehee,pesa ziliongeza upendo kwani kila walipotaka kwenda walifanya hivyo,kwa Geroge Charles kutoka Tanzania kwenda Nchini Marekani ilikuwa ni sawa na kutoka Magomeni kwenda Kariakoo!Ilikuwa ni kawaida sana kwake,ndio maana siku hiyo waliamua kupanda ndege kwenda Los Angeles nchini Marekani kutembea wakageuza baada ya siku tatu,baada ya siku saba kufika George Charles akaamua kufunguka siku hiyo kwamba anataka kumuoa Lissa.
“Whaaat?”
Lissa,akauliza glasi ya wine akaigandisha kwanza,hakuelewa kama alisikia vibaya ama masikio yake yana uchafu.
“Will you Marry me?”
“Ofcourse baby,yes!When?”
“Next week”(Wiki ijayo)
Haikuwa utani,George Charles alimaanisha kufunga ndoa na Lissa Nzava kwani tayari alimpenda kutoka ndani ya moyo wake bila kuelewa anaishi na chui aliyejifika ngozi ya kondoo!Kitu ndoa ndio jambo alilokuwa anasubiri Lissa Mnzava ili amuuwe George Charles,arithi utajiri aliokuwa nao,akafurahi sana moyoni akajua tayari anaenda kuwa mwanamke bilionea.
Mipango ya harusi ya George Charles ilianza chini kwa chini,ikawa kama fununu tu kila mtu akataka kujua ukweli wa jambo hilo,hususani waandishi wa habari.Kwa George Charles hakutaka afanye sherehe kubwa, alichotaka yeye ni kuwaalika watu hamsini tu na asichange mtu yoyote yule.
“Baby watu hamsini?”
Lissa,alishtuka siku hiyo baada ya kuambiwa hivyo,alitegemea ingefanyika sherehe bab kubwa mno, kutokana na hadhi ya Bilionea George Charles alisahau kwamba George, hakuwa mwanaume wa majivuno alikuwa simpo tu.
“Yeah only fifty,tafuta marafiki zako ishirini na tano na wangu ishirini na tano.Ukumbi,Lamada Hotel”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa na ilikuwa inasubiriwa kwa hamu sana,siku ya harusi ambayo walipanga wakafunge ndoa katika kanisa la St.Joseph!

*****
Yusrath alikuwa ni mwanamke wa kulia tu,kila kukicha!Hakujua ni lini Ahmed angempigia simu na kumfuata nyumbani kwao ili warudiane,kila siku hakuacha kuomba msamahaa alichokuwa anakifanya Ahmed kwa wiki ni kutuma pesa za matumizi kwa ajili ya watoto tu na wala sio kitu kingine,Yusrath kwake hiyo haikutosha kabisa.Ahmed hakupokea simu wala kujibu ujumbe wowote ule,mwezi ukapita,miezi miwili mpaka mitatu lakini Ahmed hakutokea kumchukua.
“Mwanangu,usijali.Punguza mawazo”
Mama,akamfariji mwanaye ingawa hakujua nini kosa la mwanaye mpaka akafukuzwa.
“Siwezi Mama,nampenda mme wangu”
“Kwani ulimfanya nini?”
“Najuta sana,acha tu Mama”
“Ulifanya nini?”
Yusrath,hakutaka kamwe kusema, aliogopa aibu ndio maana akabaki kimya,akaendelea kulea watoto wake mwenyewe,matumaini yake yakawa kwa watoto hao ambao aliwapenda sana!Akajipa matumaini kwamba ipo siku Ahmed atawachukua tu.Aliendelea kukaa nyumbani mpaka inafika miezi kumi,siku hiyo asubuhi alikosa raha baada ya Faisal kuanza kulia sana,akadhani ni njaa lakini haikuwa hivyo,alivyojaribu kumpa maziwa alitapika na kuanza kuharisha mfululizo,hiyo ilimuogopesha sana!Akajaribu kumbembeleza lakini wapi.
“Ng’aaaa ng’aaaaa ng’aaaaa”
Mtoto alilia kwa sauti,alivyomgusa aliogopa zaidi, joto lilikuwa kubwa,hakutaka kuchelewa!Akatafuta usafiri ili awahi hospitalini.

******
“Beibiiiiiiiii,nimechokaaa bwanaaa twende tukalale jamani”
“Subiri,kuna mtu namsubiri”
“Aaaah,twende kwako leo”
“Nimeshakwambia kwangu siwezi kukupeleka,huwezi kulala kitanda nacholala na mke wangu.Hilo toa kwenye akili yako, tutaenda kule kwa siku ile”
“Sikuelewi Ahmed”
“Lynne,niache kwanza!Kichwa changu hakipo sawa”
Ahmed,hakuwa mwenye raha hata kidogo japokuwa aliamini kwamba kuwa na msichana huyo mrembo atafarijika lakini alijidanganya kwani pengo la Yusrath lilikuwa palepale halikuzibika,moyo ulimuuma ndio maana hata alivyokuwa amekaa kaunta viti virefu anakunywa bia, akakosa mudi kabisa siku hiyo,tangu aachane na Yusrath maisha yake hayakuwa mazuri kabisa,michongo ya pesa ikapungua!
Hakupewa tena kazi ofisini za kusafiri,pesa hakuona kabisa,ndani ya miezi kumi hakufanya kitu chochote cha maana zaidi ya kunywa pombe na kutanua na msichana huyo Lynne!Mbali na marafiki zake wakina Ngowi, kumsema lakini hakujali,alichojali yeye kutanua akinywa pombe na kufanya zinaa tu.
“Griiii griiiiii griiiiiii”
Simu yake iliita kutokea mfukoni,ilikuwa jioni ya saa moja!Lynne msichana mrembo mwenye mikogo ya kisista duu alikuwa pembeni yake,anakunywa pombe ya gharama aina ya hainesi.
“Nanii anakupigia baby sasa hivi usiku?”
Lynne akauliza huku akichungulia simu ya Ahmed,ambapo kwenye kioo aliona jina WIFE.
“Huyo kahaba,anakupigia anataka nini?”
Ahmed hakujibu,akapiga fundo moja la pombe na kuirudisha simu mfukoni,akasikia ujumbe umeingia kwenye simu yake.
‘FAISAL ANAUMWA,AMELAZWA HALI YAKE NI MBAYA,NIPO NAYE HAPA KWA DOKTA AMEER K.KOO’
Ahmed,aliusoma ujumbe huo mara mbilimbili,akatulia kidogo!Bila kujifikiria,akampigia simu Yusrath ili aulize vizuri,lakini badala ya Yusrath kuzungumza akaanza kulia machozi.
“Usilie,anaumwa nini?”
“Mwananguuu atakufaaa Ahmeeed,kwanini mimi lakinii eeeh Mungu”
Yusrath alilia simuni.
“Anaumwa nini?”
“Amepungukiwa damu na….tititi”
Hapohapo simu ikakatika,Ahmed alivyojaribu kupiga,haikupatikana hewani.Hakujifikiria,akaruka kama swala bila kuaga, akatoa funguo za gari mfukoni na kuingia,akawasha na kupiga gia!Kwa kasi akalitoa ili awahi kariakoo hospitalini,aliwapenda sana wanaye kuliko kitu chochote kile duniani.
Haikumchukuwa muda mrefu akawa amewasili,alivyofika tu akaingia ndani na kuanza kuangalia kwenye mabenchi,Yusrath alivyomuona tu akasimama na kumuendea kwa kasi, akamkumbatia kwa nguvu huku akianza kulia machozi.
“Yusrath,usilie kwanza.Kuna nini?”
“Faisal,atakufa anakufa.Mwanangu ana…kufa”
“Niniiiii,Yusrath niangalie usoni mke wangu”
Hapo Ahmed alimtoa Yusrath ili waangaliane!Hakupata maelezo ya kutosha hivyo ilibidi waingie kwa dokta ili apate maelezo ya kitaalam,hapo ndipo alipoambiwa kwamba mtoto amepungukiwa damu.
“Nipo tayari,kutoa.Mimi ni baba yake mzazi”
“Sawa,njoo maabara”
Ahmed,akasimama na kuingia maabara na daktari,ambapo huko alitolewa damu kubwa ili Faisal,aongezewe!Muda wote Yusrath alikuwa akilia tu,nusu saa baadaye dokta akafungua mlango wote wakamtupia macho!
“Samahani kidogo,wewe ndiye baba mzazi wa huyu mtoto?”
Dokta akauliza huku akimtizama Ahmed machoni.
“Ndio,mimi ni baba yake”
“Una uhakika?”
Dokta akauliza tena swali,moyo wa Yusrath ukapiga paaa!Akahisi mkojo unataka kumpenya kwani ki ukweli Ahmed hakuwa baba halali wa Faisal,bali ni Bilionea GEORGE CHARLES, alivyokumbuka hilo,akahisi kama mapigo yake moyo yameacha kutembea ghafla!Dalili za Ahmed kugundua ukweli, zilikuwa wazi siku hiyo.
“Dokta,mwanangu anaendeleaje?Mbona sikuelewi?”
Ahmed akauliza kwa jazba.
“Damu yako na mtoto,haviendani”
“Una maana gani?”
Ahmed akataka ufafanuzi wa kina!



Mshtuko alioupata Yusrath,haukuwa na mfano wake!Dalili za kila kitu kuhusu baba wa watoto mapacha Faisal na Faad, zilikuwa mbioni kujulikana siku hiyo,ndio maana alitetemeka na kujua kivyovyote vile kaburi lingemuhusu kwani Ahmed angemzika mzimamzima baada ya kumpiga mpaka kumuua,muda wote hakutulia,alitamani kumbonyeza daktari afanye analoweza ili aepuke kikombe kinachomkabili ili maisha yaendelee,lakini hiyo ilionekana kuwa ngumu sababu Ahmed alimkazia macho yake daktari,anataka jibu kamili na ufafanuzi wa kila kitu kinachoendelea,swala la damu kutoendana na mtoto wake ndilo lilimtatiza kidogo,ndiyo maana akataka kujua zaidi.
Kwa taaluma ya Dokta Yusuph Yakubu na kubobea katika kazi yake ya udaktari alishaelewa mchezo huo na alijua nini maana yake, endapo atafungua kinywa chake kuzungumza kila kitu kwani ukweli alijua mwanamme aliyekaa hapo,hakuwa baba halali wa mtoto anayeumwa,kivyovyote alijua Mwanamke huyo kambambikia mtoto!Hilo lilikuwa kawaida nchini Tanzania kwani kesi kama hizo humjia nyingi sana,ofisini kwake.Ndio maana akatulia kidogo na kuvuta kiti kabla ya kumjibu Ahmed!
“Umesema unaitwa Mr.Ahmed?”
Dokta akajifanya kuuliza ili abuni kitu cha kumueleza Ahmed.
“Ndio,imekuaje?”
“Embu,nisubirini kwanza nje,nitawaita”
Dokta Yusuph Yakubu,ilibidi atumie busara ya hali ya juu sana!Kazi yake ilikuwa ni kuhakikisha mtoto mchanga aliyeletwa kwake apone na sio kuropoka,ndiyo maana akawataka watoke kwanza nje ili afikirie ni kitu gani cha kufanya,walivyotoka nje. Akaingia nesi akitaka kujua jina la mgonjwa anayetaka kuingia atibiwe ili akamuite.
“Julia”
Dokta akamuita Nesi.
“Abee dokta”
“Niitie huyo Mama aliyetoka,hakikisha anakuja mwenyewe”
“Sawa dokta”
Nesi akafanya kama alivyoagizwa lakini alivyomuita Yusrath,Ahmed nayeye akasimama!
“We baki tu,usijali”
Ahmed,akapigwa benchi.Wasiwasi wake ulikuwa juu ya mtoto wake,dua zote siku hiyo alisali!Yusrath,aliishiwa nguvu kuzungumza hakuweza tena, alikuwa akilia tu kwa kwikwi,aliingia ndani na kukaa kiti cha pembeni akamtizama dokta.
“Nisikilize kwa makini,kama unampenda mwanao.Mtafute baba yake mzazi.Ama mtu yoyote mwenye blood group AB”
“Dokta,mbona sikuelewi?Huyo ndiye baba yake mzazi mbona”
“Sijakuita uje kubishana namimi hapa,wewe damu yako ni A mumeo AB,mtoto ana O.Kuendelea kunificha na kuendelea kulia hapo,haitokusaidia!Ndio maana nimekuita peke yako,una masaa kumi na nne,leo hii mpaka kesho asubuhi saa tatu.Mtoto awe na damu,vinginevyo utampoteza”
Moyo wa Yusrath ulidunda kama kitenesi,ukataka kutokeza nje ya kifua!Aliogopa na kutetemeka kwa wakati mmoja,hakuelewa ni kitu gani akifanye,alihisi kufakufa kuliko kawaida.
Alivyofikiria hali ilivyokuwa akatamani mambo yote yarudi nyuma lakini hilo lisingewezekana hata kidogo,alichotakiwa kufanya ni kumtafuta George Charles, popote pale alipo,angemueleza nini Ahmed?Angetumia kiswahili gani ili aeleweke?Alivyojiuliza maswali hayo akaona kama dunia yote ipo kichwani kwake,aliwapenda sana watoto wake na isingewezekana hata kidogo awapoteze kiurahisi namna hiyo,kwake watoto ilikuwa kwanza ndoa baadaye,akapiga moyo konde na kuanza kutafakari ni jambo gani alifanye.

******
Matajiri mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi walipata taarifa juu ya harusi ya bilionea George Charles,tajiri kijana!Wafanyabiashara wenzake,walivyouliza kuhusu mchango wakaambiwa hakuna kitu kama hiko,wasichange hata thumni.Waje kama walivyo,kuanzia siku hiyo George Charles alikuwa bize na simu anazungumza na wageni wake,ambao wangetoka nje ya nchi.
“Are you gona land with your private jet?”(Utakuja na ndege yako binafsi)
“Yes I have to,why are you asking?”(Ndio,kwanini unauliza)
“I just wanna know,when?”(Nataka tu kujua,lini?)
“Tomorrow Morning”(Kesho asubuhi)
“Thank you,have a safe flight”
George alikuwa simuni anazungumza na tajiri Fredinando Santiago kutokea Venezuela,kuzungumza na watu kama hao kwake ilikuwa kawaida kwani mara nyingi hukutana nao kwenye mipango ya biashara,katikati ya miguu yake alikaa Lissa Mnzava,mkononi ameshika glasi ya wine,moyo wake mweupe sana!Kila kitu alichokipanga aliona kinaenda kufanikiwa kabisa,jambo la kufunga ndoa na George Charles kwake lilikuwa kama ndoto na ilikuwa inaenda kutimia,akaona kama masaa hayaendi kwa kasi anayotaka.
Wakati George Charles anaumiza kichwa namna atakavyoandaa ndoa yake, yeye Lissa alikuwa anafikiria namna ya kifo ambacho angetumia kumuuwa George Charles ili baadaye aje kuwa bilionea.
“Nataka harusi yetu,iwe simple lakini nzuri ipendeze sana”
George Charles baada ya kukata simu,akamsemesha Lissa!
“Baby”
Akaita,baada ya kuona Lisa yupo mbali kimawazo,akamtingisha kidogo!
“Yes Darling,are you done?Vipi Antonio pia atakuwepo?”
“Yes,atakuwepo.Juzi alikuwa London,Uliongea na Asnart kuhusu bajeti nzima?”
“Not yet”
“Sasa kwanini?Please baby,keshokutwa sio mbali unajua.Nahitaji by kesho hiyo bajeti niipate,alafu mtafute pia Isaya Kibona muulize mpango wa magari umefikia wapi?”
“Usijali Darling,nitapiga!Sasa hivi nitampigia Isaya Kibona”
Baada ya mazungumzo hayo ambayo kwake hayakuwa na tija yoyote ile,akanyanyuka na kupanda ngazi.Akatembea mpaka chumbani na kufunga mlango,mpango wake ulikuwa ni lazima utimie ndiyo maana akamtafuta Minja,kwenye simu.Ili wakapange mipango na mbinu za kumjaza George Charles, wamuuwe.
“Mshatafuta njia?”
“Ndio madam”
“Njia gani?”
“Tutampiga risasi”
“Sitaki,iwe hivyo.Nahitaji auwawe kifo cha taratibu,mtu yoyote asijue”
“Sijamaliza bado,hilo ni moja”
“Malizia”
“Kuna sumu ile ya kuuwa taratibu,unamuwekea kwenye chakula”
“Si niliwaambia mara ya kwanza,kifo chake kiwe cha ajali.Ikiwezekana tutakata hata pipe za breki,ama vyovyote vile ilimradi iwe ajali”
“Basi subiri tutafanya,itakuwa kama kifo cha mke wa waziri mkuu”
“Waziri,Yule mkewe?”
“Ndio”
“Ile haikuwa ajali kumbe?”
“Haikuwa ajali ya kawaida,ilitengenezwa na watu makini kama sisi”
“Sindo ile ya kontena kudondokea gari lake dogo?”
“Hiyo hiyo”
Lissa Mnzava,alibaki kushangaa na kutoamini kama kifo cha mke wa waziri mkuu kumbe cha kutengenezwa akaanza kuamini kwamba sio ajali zote ni bahati mbaya,jambo hilo lilimfanya amuamini sana Minja.
“Usalama walishindwa kufuatilia kwani?”
“Hivi ajali kama ile usalama gani atagundua?Kila kitu kilipangwa na watu makini.Ile ajali,ilichorwa sio chini ya miezi mitano watu tulikaa vikao kama bungeni.Mpaka Yule maza akafa kwa staili ile”
“Well done”
“Nahitaji kifo cha namna hiyo”
“Lini?”
“Baada ya ndoa,anzeni kupanga.Ikiwezekana tukirudi kutoka Honeymoon”
“Limeisha hilo,ila usizingue Madam”
“Kivipi?”
“Kwenye mapene”
“Mnajua kabisa,nitakuja kuwa nani.Baada ya hiki kifo chake”
“Aminia”
Simu,ikakatwa roho ya Lissa ikawa nyeupe kabisa,alichokuwa anakisubiri kwa hamu kubwa ni siku ya ndoa,wakati mwingine roho ilimuuma lakini hakuwa na jinsi sababu ilikuwa ni lazima amalize alichokianza.

***
Zilikuwa zinahesabika siku,sasa yalibaki masaa tu ili George Charles awe mme halali wa Lissa Nzava,siku hiyo aliamini ingekuwa siku ya kihistoria katika maisha yake na isingeweza kujirudia tena!Ndiyo maana, muda wote alikuwa mwenye furaha sana!Hekaheka zilikuwa nyingi ndani ya jumba lake la kifahari,wageni kutoka nchi mbalimbali waliwasili tayari,asilimia kumi na mbili ya wageni hao,walikuwa ni ngozi nyeupe yaani wazungu.
Costa tatu zilikuwa tayari kwa ajili ya kubeba wageni waalikwa,gari aina ya marcedez benzi ilishafika kwa ajili ya kumchukua George Charles, kumpeleka kanisani.Paparazi hawakucheza mbali,sijui taarifa za Bilionea huyo kufunga pingu za maisha, walizitoa wapi,kurasa mbalimbali zilirusha picha yake huko mitandaoni kukawa gumzo.
“You look smart,my Son.Hongera sana”
Baba mzazi,Mzee Charles akatoa pongezi baada ya mwanaye kutoka chumbani akiwa tayari amevaa suti kanyonga tai shingoni,sura yake ina furaha muda wote!
“Thank you Dad”(Ahsante baba)
Wote wakaongozana mpaka nje,ambapo huko waliingia ndani ya magari na safari ya kuelekea kanisani, kuanza mara moja!

****
Usiku kucha alikuwa akihangaika,ni kitu gani akifanye ilikuwa ni lazima amuokoe mtoto wake kwani maisha ya mwanaye yalikuwa mikononi mwake mwenyewe,hakutaka baadaye aje kujilaumu kwa upumbavu alioufanya,akiwa hospitalini alihangaika sana!Kitendo cha kuambiwa na daktari amtafute baba wa mtoto ili aongezewe damu kilimnyima raha ya maisha,akazidi kufikiria!Alivyotaka kutoa damu yake,ikashindikana akaambiwa kwamba ana damu ndogo,mpaka inafika saa saba ya usiku hakuna msaada wowote alioupata!Ahmed alipagawa kwa kiasi cha kutosha,alivyowapigia marafiki zake simu wampe msaada huo walimpiga chenga,akaamua kupiga moyo konde na kumtafuta Benjamin Ngowi hewani ili amueleze tatizo hilo.
“Kaka,sipo Dar!Nipo Iringa,kuna nini Ahmed?”
Benjamin Ngowi,akauliza simuni akiwa mwenye shahuku na wasiwasi mkubwa sana,sauti yake ilikwaruza sababu ilikuwa ni usiku sana!
“Mwanangu,ana matatizo.Kama upo mbali basi,subiri nitakupigia”
Ahmed akakata simu na kuwajaribu marafiki zake wengine lakini walimtolea nje na wengine kumpa sababu zisizokuwa na miguu wala kichwa.
“Ahmed,ningekusaidia.Lakini siwezi mimi naogopa,madhara ya kutoa damu mimi nayajua broo”
“He is my son please,nakuomba nitakupa pesa yoyote ile Gelard”
“Naelewa kaka,lakini sasa daaaa!Mimi nitashindwa,nitakuja as…tititi”
Ahmed akakata simu,kuendelea kuzungumza na Gerald kusingezaa matunda,akakata tamaa kabisa akabaki akilia tu!Mpaka inafika saa kumi na moja asubuhi,kila mtu alikuwa tayari amekata tamaa,Yusrath amelia mpaka kapoteza fahamu,alivyozinduka ilikuwa asubuhi saa moja!
Akawa kama amepata akili mpya,hakujali tena, alichotakiwa kufanya ni kwenda kumsaka George Charles,kwake ikawa kama mbwai na iwe mbwai ili mradi mtoto wake apone.
“Unaenda wapi?”
Yusrath alishikwa mkono na Ahmed,baada ya kuonekana kama mtu aliyechanganyikiwa, namna aliyokurupuka kutoka kitandani iliogopesha.
“Chooni”
Akadanganya,alielewa nini maana yake angesema anaondoka.
“Nikusindikize?”
“Nitafika usijali”
Yusrath,akaweka vizuri nguo yake na kuanza kutembea akitoka mlangoni ambapo huko alijisachi na kujikuta ana noti ya shilingi elfu ishirini,akawa ana uhakika kabisa kwamba itamfikisha Masaki kwenye jumba la George Charles,hakuwa ana uhakika kama angemkuta!Alikuwa kama anabahatisha,akajilaumu sana kufuta namba zake,akatembea kwa haraka huku akitizama nyuma kama Ahmed anamuona,alivyokunja kona akaanza kuchanganya mwendo mpaka alivyotoka nje!
“Bodaa”
Kitendo cha kuita hivyo,pikipiki ikasogea mpaka miguuni kwake!
“Wapi sista?”
“Nipeleke Masaki”
“Masaki ipi?”
“Sikumbuki,ila tukifika pale aaah nimesahau.Tupitie Msasani ndio nitakumbuka”
Kilikuwa ni kipindi kirefu sana kimepita,tangia apelekwe kwa George Charles isitoshe alienda mara mbili ama tatu,ndiyo maana kumbukumbu zake hazikuwa vizuri!Pikipiki ikawashwa,safari ikaanza mara moja.
“Harakisha kaka”
Yusrath,akasema dereva akatii amri.Upepo ulikuwa mkali ukafanya mpaka Yusrath, kutokwa na machozi,kichwani aliwaza vitu vingi sana!
Jamii inayomzunguka itamfikiriaje ikijua kwamba watoto hawakuwa wa Ahmed mmewe wa ndoa,je Ahmed atamfanya nini?Jambo hilo aliliogopa sana,roho ilimuuma akazidi kuingiwa na wasiwasi mkubwa sana.Baada ya kufika Mataa ya Magomeni ilibidi pikipiki iwekwe pembeni,kulikuwa na msongamano mkubwa wa magari.
“Kuna nini?”
Yusrath akauliza,hiyo ikamfanya dereva wa pikipiki, amuulize mwenzake pembeni.
“Kuna harusi,msafara huo”
“Msafara wa harusiii!?”
“Ndio”
“Asa ndio ufanye sisi tuzuiliwe?”
“Wenye nchi bwana,si unajua tena serikali yetu hii”
Maneno hayo yalimfikia Yusrath,yalimkera sana akatamani ashuke na kutembea lakini isingewezekana sababu kulikuwa na umbali mrefu bado,bila kuelewa ndani ya magari yaliyokuwa yanapita katikati alikuwemo Bilionea George Charles,anaenda kufunga ndoa!Dakika kumi na tano baadaye safari ikaanza upya,haikuwachukua dakika nyingi wakafika Masaki,hapo Yusrath akaanza kazi ya kumuelekeza dereva njia za kupita.
“Subiri kidogo,kunja hapa”
“Wapi?”
“Kaka,sina uhakika lakini kuna gorofa Fulani hivi la kijani”
“Huku magorofa ni mengi,hapo itakuwa ngumu sista,kwani si upige simu”
“Nimekumbuka,Bringtstone street”
“Mtaa wa Bridgestone?”
“Ndio”
“Asa sista si ungesema,mbona tumeuacha kule nyuma”
“Naomba tuwahi kaka angu”
Dereva hakuwa na tatizo,akageuza pikipiki na kurudi nyuma,Yusrath akaanza kurudiwa na kumbukumbu zake,mbele yake akaliona jumba la George Charles,akashuka na kumlipa dereva ujira wake,hapo akatembea mpaka getini na kubonyeza kengele.
“Naniiiii?”
Sauti hiyo,ilisikika kutoka getini ambapo kulikuwa na spika ya kisasa.
“Yusrath”
“Una mtaka nani?”
“George”
“George,hayupo”
“Yuko wapi?Naomba nifungulie geti kwanza ni muhimu kama yupo mwambie Yustrath”
Kitu hiko kilikuwa rahisi kufanyika,geti likafunguliwa akatokeza mlinzi.
“Habari afande”
“Nzuri”
“Nimemkuta mwenyewe?”
“Nani?”
“Mr.George”
“Mr George?”
Afande akauliza kwa mshangao kidogo.
“Ndio”
“Haujapishana na msafara wowote ule?”
“Sijakuelewa”
“Yupo kanisani,anafunga ndoa St.Joseph,baada ya hapo anaenda Paris”
Ghafla akahisi kama amepalalaizi,akaishiwa nguvu za miguu kabisa.Kitu alichosikia hakutegemea,akakumbuka msafara aliopishana nao Magomeni,machozi yakaanza kumtoka!Alivyomkumbuka mwanaye aliyekuwa hospitalini,akaumia zaidi.
“Ume.. ume umesema kanisa gani?”
“St.Joseph”
Hapo Yusrath hakuwa na jinsi zaidi ya kuanza kukimbia, akitafuta usafiri wa haraka ili awahi posta,ilikuwa ni lazima afanye hivyo,hata kama angemkuta George Charles kanisani.Njia nzima alikuwa analia huku anakimbia,aliyofika kwenye barabara kubwa akaita pikipiki,akapanda juu kwa kasi.
“Dada wapi?”
“Twende tuu”
“Wapii dada?”
“Twende kaka,tweende posta St.Joseph”
Akili yake,iliruka hakuwa yeye tena!Alichokiwaza kwa wakati huo ni kumkuta George amuwahi,hakujali kwamba angevunja ndoa ya watu.
Pikipiki ikazidi kuchanja mbuga,wakafika daraja la salenda na kuzidi kusonga mbele,wakaibukia Posta mpya,dakika mbili baadaye wakawasili St.Joseph, Yusrath akashuka,akaanza kutizama huku na kule kama mtu aliyepotea kituo.
******
Kanisa lilijaza, mbele alisimama bilionea George Charles,nyuma yake yupo mpambe wake Mr.Sospeter Alfred,wamependeza, macho ya waumini wote yapo kwao,wanamsubiri bibi harusi mtarajiwa Lissa Mnzava ili ndoa ifungwe,haikuchukuwa muda sana akatokea akiwa amevalia shela kubwa linaburuzika nyuma limeshikwa,akatembea mpaka madhabauni akasimama kandokando ya George Charles,katikati yao yupo mchungaji,tayari kwa kufungisha ndoa takatifu!
Harusi hiyo haikuwa ya mchezo,nje kulikuwa na walinzi wa kutosha kwani George Charles alifahamika mpaka serikalini,usalama ulikuwepo askari waliranda kila mahali kuhakikisha shughuli hiyo inaisha salama.
“Unaenda wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa askari mmoja aliyekuwa getini baada ya kumuona Yusrath,anataka kupita.Alikuwa ana kila sababu ya kuuliza kutokana na mavazi aliyovaa Yusrath.
“Kanisani”
“Hatuwezi kukuruhusu”
“Kwanini?”
“Wewe jua hivyo,rudi nyuma”
“Hapana”
Yusrath alivyotaka kufosi kuingia akazuiwa, hapo ndipo akaanza kufanya fujo,akilazimisha aingie!
“Niachieeee,niachiee mwanangu anakufaaa, nataka kuongea na Georgeee”
Kelele zikaanza,askari wengine wawili wakatokea wakitaka kujua chanzo,kelele za Yusrath zikawafanya wamtulize na kumtoa nje! Hiyo ilifanya azidi kupiga kelele kwa sauti.
“Nataka kuonana na Georgeee,mtoto wake anakufaaaa.Niachieni nataka kuonana na George Mtoto wake,yupo hospitaliniiiii,niachieniii”
Hakukuwa na mlinzi aliye muelewa zaidi tu,walimuona ni mwehu,katika purukushani akachaniwa nguo yake ya juu.Waliokuwa kanisani, siti za nyuma walisikia kelele hizo.Wengine wakasimama na kutoka nje!Kelele za Yusrath zilikuwa kubwa,mbali na kanisa kujaza lakini sauti hiyo ilipenya na kumfikia George.
“Mtoto wake anakufaa hospitaliniiii,George nimezaaa naye!Niachieniiiii,mtoto wanguu anakufaaa nisaidieni jamanii”
Sauti hiyo ilimshtua George,akatulia kidogo ili kusikiliza sauti hiyo, haikuwa ngeni kwake!Bahati nzuri kwa pembeni kulikuwa na vidirisha vidogo vya duara,akajikuta anaganda baada ya kuiona sura ya YUSRATH, mbaya zaidi alikuwa anavutwa kwa nguvu kama mwizi,akipakiwa ndani ya Deffenda,akili ya George ikahama kabisa.
“George,are you okay?”(George upo sawa)
Mpambe wake,akauliza akiwa nyuma yake baada ya kumuona bwana harusi ameduwaa, anatizama nje!Jambo hilo likamfanya Lissa Mnzava,apate hofu kubwa sana kwani hata yeye sauti ya mwanamke huyo akitaja jina la George aliisikia vizuri,hiyo ilimaanisha kulikuwa kuna kila dalili ya ndoa kuvunjika siku hiyo!



Kwake lingekuwa pigo kubwa sana kama ingetokea angempoteza mtoto wake mdogo, baada ya kupungukiwa damu mwilini,asingeweza kuisahau siku hiyo hata kidogo katika maisha yake.Mtoto wake alikuwa ana hali mbaya kitandani,damu ndiyo kitu pekee kilichokuwa kinahitajika, hapo ndipo alipoamini kwamba unaweza ukawa na pesa lakini isikusaidie chochote kile!Marafiki zake aliowapigia simu ili wampe msaada, wote waliishia mitini na wengine kumzimia simu kabisa,akabaki analia na Mungu wake akisubiri muujiza utokee.Mabalaa yaliyokuwa yanamkuta tena yakiambatana yalimfanya ahisi wenda ana mikosi ama laana, hakuelewa alimfanya nini Mungu wake,iweje yeye afululize kukumbana na matatizo?Kifupi kila kitu kwake kikagueka tamu ikawa shubiri.Akiwa katikati ya mawazo simu nyingi sana ziliita na alivyopokea alipewa pole tu,hakuna mtu yoyote kati yao aliyesema kwamba, angejitolea damu ili mwanaye apone, hilo ndilo lililomfanya asikie uchungu ajabu.Akiwa nje,juu ya benchi anamsubiri Yusrath ambaye aliamuaga anaenda chooni, simu yake ikaanza kuita,namba zilikuwa ngeni akaipuuzia ikaita tena mpaka ikakata,mpigaji hakukoma akaendelea kupiga,akaiangalia na kuipokea ili kutoa kero!Akaiweka sikioni.
“Ahmed”
Upande wa pili wa simu ukasikika.
“Naaam,nani mwenzangu?”
Ahmed,akauliza akavuta kamasi kidogo na kufuta machozi kwani sauti hiyo aliifananisha.
“Mbona kama unalia?”
“Naongea na nani?”
“Hajrath,Ahmed upo sawa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Hajrath Mpilla,akitaka kujua kama Ahmed yupo sawa!Sauti ya mwanamme huyo ilimfanya atake kujua zaidi.
“Halloo,Ahmed”
Hajrath akaita tena baada ya kimya kirefu kutokea,hiyo ilimfanya Ahmed atafakari kwa kina akijishauri kama ni sahihi kumwambia Hajrath matatizo yake ama ndio atapewa pole kisha simu ikatwe.
“Ahmed,kuna nini?”
“Nipo Hospitali”
“Hospitaliii?Nani anaumwa?”
“Mwanangu”
“Whaaaat?Anaumwa nini?”
“Mwanangu,atakufa Hajrath”
“Please relax and tell me,wewe ni mwanamme”
“Nashindwa kujikaza”
“Upo hospitali gani?”
Shida ya Hajrath ya kutaka kumuomba Mkopo Ahmed,ikaisha hapohapo alichotaka kukifanya cha kwanza ni kujua Ahmed yupo hospitali gani ili akamuone,hakutaka kujali angefikiriwa vipi lakini alihisi kuumia nayeye,akaamini kwamba kwa njia moja ama nyingine, angemfariji Ahmed hata kwa kumpa moyo,hakutaka kuchelewa zaidi akaomba aambiwe ni hospitali gani Ahmed yupo.
“Hapo Kariakoo?”
“Ndio”
Haikuchukua dakika nyingi kuoga bafuni kama anavyofanya siku zote,siku hiyo alitumia sekunde thelathini kumaliza,akavaa haraka.Bila kupoteza wakati akachukua bodaboda na safari ya kwenda Kariakoo kwa dokta Amir kuanza dakika hiyohiyo!Hakukuwa na msongamano mkubwa wa magari,hiyo ilimchukuwa dakika kumi tu kufika Kariakoo,akaulizia hospitali ya Dokta Amir ilipo,haikuwa tabu kuipata akaelekezwa na kuingia ndani.Akaanza kushangaa huku na kule,hakupata tabu sana kumuona Ahmed,aliyekuwa kwenye benchi kainamisha kichwa chake chini,akamsogelea na kumshika bega.
“Ahmed,pole sana”
Akampa mkono ili kumuinua,akamsogelea karibu na kumkumbatia.Hapo Ahmed,alishindwa kujizuia, akiwa katikati ya mikono ya Hajrath akaanza kulia kama mtoto mdogo, akimtupia lawama zote Mungu,Hajrath alivyotaka kulia akajikaza kisabuni akitaka kumfariji Ahmed!Mbali na kumsikitikia alijisikia furaha kupata joto la Ahmed kwani miaka mingi sana ilipita.
“Ahmed,wamekwambani nini.Mtoto anaumwa nini?Usilie nakuomba”
“Amepungukiwa damu?”
“Kwanini usimtolee?”
“It's complicated,Hajra!..Sielewi nifanye nini”
“Mkeo,yuko wapi?”
Hajrath,akauliza swali hilo huku akijitoa taratibu kwa Ahmed,akajiongeza akijua kivyovyote vile, Yusrath angetokea na kuwakuta katika hali hiyo,angehoji maswali.
“Sijui,ameniambia anaenda chooni.Mpaka sasa hi..vi hajarudi al..”
Ahmed akashindwa kumalizia sentensi, baada ya kumuona Dokta ametoka,akamuendea kwa haraka ili ajue hali ya mwanaye.
“Kama nilivyokwambia”
“Dokta,hakuna njia nyingine yoyote ile?”
“Hakuna”
Kwa Hajrath,hakuelewa nini tatizo baada ya kuhoji akaambiwa kila kitu,hakujishauri chochote.
“Nipo tayari kutoa damu”
Sentensi hiyo ilimfanya Ahmed,apigwe na butwaa la waziwazi.
“Hajrath ili…”
“Twende kwa dokta”
Hakukuwa na longolongo yoyote ile,akaweka tofauti zao kando wote wakaingia kwa dokta,Hajrath akapelekwa mpaka maabara ambapo huko alitolewa damu ikapimwa,dakika tano baadaye dokta akafika akiwa na tabasamu nene!
“Damu zime match”
Ilikuwa ni furaha kubwa sana kwao,wakajikuta wanakumbatiana kwa nguvu, wakiwa katika nyuso za furaha.

*******
Waandishi wa habari,walikusanyika na kuizingira diffenda ya polisi wakijaribu kumpiga picha Yusrath, kila mwandishi alitaka kuuza gazeti kukikucha kesho yake kwani harusi ya Bilionea George Charles, waliamini ingekuwa homa ya jiji,kila mtu angetaka kusoma habari hiyo,kitendo cha Yusrath kupiga kelele akisema kwamba mtoto wa George anakufa na amezaa naye,ikafanya paparazi wamnase na kuanza kumpiga picha za mnato akiwa anasukumana na askari mpaka kwenye difenda,wakaachana na George Charles.Kilichowafanya washindwe kumchukua tena ni baada ya askari kumchukua Yusrath na kumuhifadhi kwenye diffenda, wakidhani wenda Yusrath alikuwa ni mchepuko wa George Charles,hivyo nyuma ya yote kulikuwa na wivu wa mapenzi.Ndio maana wakamtuliza!Kuharibika kwa harusi hiyo kungemaanisha vibarua vyao kuota nyasi!
“Weee mwanamke,tulia hapo.Zoezi litabadilika sasa hivi,funga bakuli lako.Ulitumwa uvue chupi yako?”
Askari mmoja aliyekuwa na mtutu begani,alipiga mkwara na kumfanya Yusrath atulie huku akilia kwa kwikwi,vitu vingi vilipita kichwani kwake.
Picha ziliendelea kupigwa mfululizo, akiwa nyuma ya diffenda,licha ya yeye kupaza sauti na kuropoka haikumfanya George Charles asitishe zoezi alilolianza, ilikuwa ni lazima amalize alichokianza japokuwa alitaka kujua ni kitu gani kinaendelea,kilichofanyika kanisani kilikuwa kama kilivyopangwa hatimaye George Charles, pamoja na Lisaa Mnzava wakawa mke na mme halali,vyeti vikaletwa wakasaini mbele ya mashahidi kama kumbukumbu zao!Kilichofatia hapo,zilikuwa ni kelele za matarumbeta na makofi,nderemo na vifijo vilikuwa vingi, baada ya maharusi kuanza kutoka nje ya kanisa hilo taratibu,huko walisimama na kuwapa mikono waumini wakiwemo wageni waalikwa.Lissa Nzava,alionesha furaha usoni lakini moyo wake ulichafukwa kwa kiasi cha kutosha,sauti ya mwanamke aliyekuwa anapiga kelele akidai mtoto wa George Charles anakufa,ilizidi kumtesa kichwani.Alichukia mno,utajiri aliokuwa anawaza aliamini George Charles keshamuandikisha mtoto wake,kwanini George anifiche?Lissa akajiuliza swali hilo na kukosa jibu.
“Hongera shoga,umependeza”
Aliyemtoa kwenye dimbwi la mawazo ni rafiki yake Martha Msoso,akampa mkono na marafiki wengine wakapita kwa staili ya kuwapa mikono maharusi,nusu saa baadaye wakatakiwa waingie ndani ya magari ili safari ya kwenda kupiga picha za kumbukumbu ianze mara moja,hilo halikuwa tatizo jambo hilo likafanyika.
“George,naomba nikuulize swali”
Lissa Nzava,akashindwa kukaa na dukuduku hilo moyoni,wakiwa ndani ya gari akataka kuhoji.Kwa namna alivyoongea kwa jazba,ikamfanya George ahisi,mwanamme huyu alikuwa na IQ kubwa sana,akamtizama mkewe na kutabasamu.
“No,hapa sio mahali pake.Subiri hili liishe mke wangu,i love you”
George Charles,alishaelewa kabisa kwamba Lissa angeanza kuhoji kuhusu mwanamke aliyesikika anapiga kelele wakati wanafunga ndoa kanisani kwani hata yeye alitaka kujua ni kwanini Yusrath alifika siku hiyo, tena mbaya zaidi alizungumza mambo mazito ya mtoto anayetaka kufa,isingewezekana hata kidogo kwake kuamini kwamba alizaa naye mtoto,hilo likamfanya azidi kuhoji na kuhaidi baada ya kurudi fungate, amsake Yusrath ili amuhoji maswali.
Swala la Lissa Mnzava,halikuishia hapo hakutaka kupotezea juujuu hata kidogo ilikuwa ni lazima ajuwe kila kitu kabla ya kupata majibu kutoka kwa George Charles sababu aliamini mwanamme huyo angemficha tu,kitendo cha kufika Mikocheni My fear, kwa ajili ya kupiga picha akaomba aende ‘washroom’.
“Naenda,washroom just one minute baby”
Lissa,akaomba ruksa huku akitoa tabasamu pana!Alichokifanya baada ya kufika huko ni kuwasha simu yake,haraka akaanza kutafuta namba za Minja,alivyopokea tu baada ya salamu akaanza kumpa mipango kabambe.
“Sijakuelewa”
“Sikiliza,kuna mwanamke nadhani ulimsikia pale kanisani leo”
“Ndio hivi ni nani Yule Malaya?Alitaka tusile ubweche?Nikajua,shughuli imeisha”
“Acha umbea.Hata mimi nataka kujua,upo wapi kwanza?”
“Nataka niende magetoni mara moja”
“Rudi pale kanisani,mfuatilie Yule kahaba nataka kujua anapoishi na ana uhusiano gani na George,umenielewa?”
“Madam,ngoja basi nikabadili nimevaa suti hapa ujue”
“No,nenda sasa hivi.Nataka ripoti hii iwe tayari leo usiku”
“Sawa madam”
“Ahsante”
Lissa Mnzava,alikata simu na kushusha pumzi ndefu.Swala la George Charles na mtoto wa nje ndilo lilimuumiza kichwa,akaapia kama ni kweli ni lazima angemuuwa na mtoto pia ili urithi uwe wake,kwenye jambo hilo alitakiwa kuwa makini sana kwani aliamini kulikuwa na ugumu mbeleni.

*****
Yusrath,aliachiliwa na jeshi la polisi saa kumi na dakika mbili jioni, baada ya kutoa maelezo ya kujikanyaga kanyaga,maelezo yake hayakueleweka vizuri hiyo iliwafanya polisi wamuachie huru kwani hawakuwa na sababu ya kumpeleka rumande,swala lao lilikuwa ni kuhakikisha ndoa ya Bilionea George Charles, inafungika bila kutokea aina yoyote ile ya vurugu.
“Naombeni simu yangu”
Yusrath,akataka apewe simu yake!Alisikitika mno na kujua tayari mtoto wake,alishafariki kwani alijua kivyovyote mtu aliyetakiwa kutoa msaada ni George Charles peke yake,alivyopewa alikumbana na ‘missed calls’ ishirini na mbili kutoka kwa Mmewe Ahmed,alivyoingia kwenye meseji akakuta nyingi, ambazo hazikuwa na idadi kamili.Akapagawa zaidi,hakutaka kusoma kwani alielewa zilikuwa niza habari mbaya,alichokifanya ni kutafuta pikipiki iliyompeleka mpaka hospitalini.Alivyoulizia,akaambiwa Ahmed na mtoto tayari wameruhusiwa na damu ilipatikana.Hakutaka kuamini,ilibidi apige kwanza kwa Ahmed huku akijaribu kubuni maneno ya kumwambia, alikuwa wapi siku nzima.
“Yusrath,upo wapi?”
Hilo ndilo swali la kwanza kutoka upande wa pili,Ahmed akiuliza.
“Nipo hospitalini hapa”
“Nenda nyumbani,nitakukuta”
“Imekuaje?Mtoto yuko wapi?”
“Nitakukuta nyumbani yupo huko”
Ahmed,alikuwa benki kwenye moja ya ATM anapakua pesa ili amsaidie Hajrath Mpilla,ilikuwa ni lazima arudishe fadhila ili aikomboe nyumba ya baba yake mzazi!Walizungumza vitu vingi sana siku hiyo,mpaka Ahmed akakubali kumsaidia japokuwa hakuwa na pesa nyingi kwenye akaunti yake.Akapakua milioni mbili na hamsini.
“Hii hapa Hajrath,nenda kawape hii kwanza.Ahsante kwa kila kitu,nakushukuru sana.Mke wangu,kanipigia kumbe alikuwa nyumbani”Akadanganya ili kumtetea mkewe,hakutaka kujazia neno lolote lile.
“Ahsante Ahmed,Ahsante sana.Ni jambo kubwa sana umenifanyia Allah atakuongezea”
“Usijali,nenda nyumbani.Kalipe hiyo pesa”
Shukrani alizotoa Hajrath, hazikuwa na mfano wake,alishukuru na kuamini kila kinachotokea siku hiyo ni ndoto na muda mfupi atashtuka,waliagana na kila mtu akashika njia yake.

*****
‘MAKUBWA YAIBUKA,MWANAMKE ANAYEDAIWA KUZAA NA BILIONEA GEORGE CHARLES KAJITOKEZA’
‘BILIONEA GEORGE CHARLES,KATELEKEZA MTOTO NA MAMA YAKE HABARI KAMILI UK.7’
‘UTATA,NDOA YA BILIONEA GEORGE CHARLES YAVAMIWA,MWANAMKE ALIYEZAA NAYE AJITOKEZA.TIMBWILI LATOKEA BIBI HARUSI AZIMIA KANISANI’
‘KIVUMBI,NDOA YA GEORGE CHARLES MASHAKANI KUVUNJIKA’
Hivyo ndivyo vichwa vya habari vya magazeti,juu yake kulikuwa na picha ya Yusrath, mbaya zaidi ukurasa wa mbele juu kabisa,kifupi karibia meza zote za magazeti ya udaku yalijaa picha za Yusrath, nyingine kukiwa na kichanga pembeni,haikujulikana mtoto waliyemweka ni kweli ama ni mbwembwe ili magazeti yauze!Kwa mara ya kwanza, tangu azaliwe kutokea kwenye magazeti,kila mtu alitaka kujua habari hiyo, ambayo ilionekana kuwa ni topiki ya jiji.
“Bei gani gazeti?”
“Mia saba”
“Nipatie”
Gazeti hilo,lilinunuliwa na Kassim Kajeme.Mdogo wake na Ahmed,hakuwa ana uhakika kama anayemuona juu ya gazeti ni Yusrath ama anamfafanisha,baada ya kupewa akafungua ili aangalie vizuri,alichokisoma kilimuacha kinywa wazi!
“Duuuu!”
Hakutaka kuchelewa,hapohapo akachukuwa simu na kumtafuta kaka yake Ahmed,hewani ili amuulize kama habari hizo,zimemfikia asubuhi hiyo, lakini badala yake akakuta simu haipatikani!


Ahmed aliendesha gari lake kwa mwendo wa kawaida kabisa, ndani ya gari lake ulisikika wimbo ya Lucky Dube unaoitwa ‘No body can stop reggae’ akaongeza sauti kidogo, akaanza kutingisha kichwa chake, akiendana na mdundo,kichwani alikuwa mwenye mawazo chungu mzima lakini baada ya nyimbo hiyo kupiga akasahau shida zote kwa wakati huo.
Mambo mengi yalipita katika akili yake akawa anawaza jinsi maisha yake yanavyoenda kwa ujumla,tangu alivyokuwa mtoto mdogo mpaka hatua alizopiga katika maisha yake!Changamoto alizokuwa nazo kwa wakati huo,muda mfupi alikuwa na Hajrath Mpilla,msichana aliyekuwa na mapenzi naye ya dhati kipindi cha nyuma,leo hii walikuwa pamoja tena akamsaidia na kumpa pesa,moyo wake ulikuwa mweupe, akili yake ikasafiri kwa kasi ya kimondo mpaka Chuoni Makumira,akakumbuka ahadi walizopeana na Hajrath kwamba siku moja wangefunga ndoa lakini mambo yakaja kubadilika ghafla,hakutaka kujilaumu kwa hilo sababu aliamini wenda Mungu hakupanga hilo lifanyike,aliamini Mungu alimpa Yusrath ili awe mkewe.
Furaha yake ilirudi upya baada ya Mtoto wake kuongezewa damu na Hajrath,ulikuwa ni msaada mkubwa sana akaamini kabisa bila Hajrath pengine mwanaye angefariki,akiwa katika mawazo hayo ndipo akapata wazo la kumnunulia zawadi nzuri Hajrath kama shukrani, kwenye jambo hilo ingawa hakuwa ana uhakika kama thamani ya zawadi hiyo, ingetosha kufafanisha na wema alioufanya!Alivyofika,Ubungo mataa akasimama kidogo ili kupokea simu ya Yusrath, akamwambia kwamba awahi nyumbani mtoto yupo tayari ni mzima.Msongamano wa magari Ubungo,ulichukua dakika arobaini nzima.Walivyoruhusiwa cha kwanza ni kwenda kwake moja kwa moja,alivyoingia seblen akamkuta Yusrath tayari amefika yupo na watoto,ameshabadili nguo kabisa.
“Ahsante Mungu”
Yusrath alisema,akasimama wima akiwa na watoto mkononi ,akamsogelea Ahmed wakakumbatiana.
“Pole mke wangu”
“Nishapoa,ahsante”
Hakuna kitu walichoshukuru kama Mungu,siku hiyo.Ahmed hakuwa na sababu ya kuuliza ni wapi Yusrath alipokuwepo kipindi wapo Hospitalini,alichojua yeye ni kwamba Yusrath alikuwa katika mipango ya kutafuta damu ili mtoto wao apone!Hata hivyo hakuwa na sababu ya kumfukuza na kumwambia arudi nyumbani,alimuonea huruma sana.
“Ushakula Mke wangu?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed.
“Hapana”
“Kuna kuku kwenye friji,mwambie Hadima akukaangie”
Ilikuwa ni kama Ahmed amesahau kila kitu kilichopita nyuma,akili yake akairudisha kwenye familia yake!Siku hiyo wakatumia muda mwingi sana kuzungumza,chakula kilivyokuwa tayari kikatengwa mezani.
“Mama,nilikumisi”
Hadima akasema,mfanyakazi wa ndani.
“Hata mimi”
Kilichosikika hapo,zilikuwa ni kelele za sahani na vijiko kugongana.Ahmed,akatembea na kuwaangalia watoto wake wachanga,kuna kitu alikigundua kisichokuwa cha kawaida.Akazidi kuwatizama vizuri,akaangalia kucha wasiwasi ukamuingia lakini hakutaka kulipa wazo lake kipaumbele kwamba watoto hao sio wake,wazo hilo akalitupitilia mbali, akaliita la kishetani tena linataka kuvunja ndoa yake,kutokana na uchovu aliokuwa nao na siku hiyo ilikuwa Jumamosi,akaingia chumbani akaoga na kujitupa kitandani,kupumzika!
Katikati ya usiku,alihisi kiuno chake,kinapapaswa. Kwa mara ya kwanza alidhani yupo ndotoni lakini alivyopata kumbukumbu nzuri akagundua ni lazima atakuwa ni Yusrath tu,akatulia kidogo na kuusikilizia mkono huo laini unavyopita,ukapita kifuani na kupapasa chuchu zake,ukazidi kushuka chini tumboni,akazidi kutulia na damu yake tayari ilianza kumwenda mbio.Mkono ulivyoshika Karoti yake,akashindwa kujizuia hapo alijigusa kidogo na kujigeuza.Yusrath alivyoona hivyo akatabasamu na kujisogeza karibu zaidi,alishajua zoezi lake linaenda kufanya kazi,akazidi kupapasa jusi kafiri!Kwaniya ya mtaro usafishwe,akaona isiwe tabu akatupa shuka pembeni na kumsogelea mumewe mdomoni wakaanza kunyonyana ndimi kwa fujo,Yusrath alionekana kuwa na moto mkali kuliko kawaida,akapanda juu ya Ahmed na kukalia karoti.Hakuchelewa,hapohapo akaanza kukinyonga kiuno chake,Ahmed akiwa chini ametulia,Yusrath akarudi chini kidogo akatoa ulimi wake wakaanza kunyonyana ndimi.Ahmed hakutaka mechi hiyo,imilikiwe mpaka mwisho akampindua.Yusrath akawa chini yeye akawa juu,akachukua mguu mmoja wa Yusrath,akauweka begani kwake na kuendeleza push up,kiuno chake kikaanza kwenda chini na kurudi juu,kwenda chini kurudi huku akikinyonga taratibu.Akamlaza Yusrath vizuri chali,akakalia tumbo akalala mgongoni kwake na kuendelea na kazi yake,sekunde tano baadaye,akamuomba apige magoti ashike kona ya kitanda yaani mbuzi kagoma,Ahmed akamshika kiuno akitumia mikono yake miwili,akazidi kupekecha pekechua.
“Aaaah shssssa aaah ssshhh beiibii aaah ilike iiiit,aaah asshss aaah aaah aashhh Mm..e wangu aaah ilike it,aaashss aaaah aaaaaah Ah..med yu killing meee,aaashsss”
Hizo ndizo kelele za puani,alizokuwa anatoa Yusrath, maana yake ilijulikana kwamba anakaribia kufika mshindo, hapo Ahmed,alizidisha majeshi kwani nayeye stimu zilikua tayari. Haikuchukuwa sekunde tatu,wote wakafika kwa pamoja na kudondoka kitandani puu!Kama mizigo,majasho yanawatoka kwa mbali.
“Baby,ahsante”
Yusrath,akashukuru sana na kumtizama Mumewe akimpongeza kwa shughuli nzito aliyofanya!Usiku huo,wakazungumza vitu vingi sana,Ahmed hakutaka kutoka chumbani,chakula akaletewa wakala na kushiba,wakawa kama wamefufua penzi lao upya!
“Nikipata pesa nataka twende kisiwani,tuka enjoy,nadhani next week on Sunday”
Ni wazo kutoka kwa Ahmed,ambalo lilionekana kuungwa mkono na mkewe!Wakapigana mabusu wakaingia bafuni kuoga wakarudi kitandani kisha kujifunika shuka,wakalala.

*****
Wa kwanza siku hiyo kukurupuka kutoka kitandani,alikuwa ni Yusrath ilikuwa ni siku ya Jumapili.Alichokifanya ni kuchukua simu yake na kuanza kuperuzi kwenye WatsApp,Facebook na Instagram!Kilichomfanya agande ni baada ya kuingia kwenye group lao la Shule,akaona picha yake ipo kwenye magazeti.Hakukaa sawa,akapigiwa simu kutoka kwa Mama yake mzazi, akimuuliza kuhusu sura yake kutokea kwenye magazeti.
“Yusrath mwanangu un..”
“Mama ngoja nitakupigia”
Yusrath alikata simu,moyo wake ulikuwa ukipiga kwa nguvu!Jambo la sura yake kuonekana kwenye magazeti na habari zilizosambaa kwamba alizaa na bilionea George, zilimuharibia siku asubuhi hiyo,akakosa raha kabisa akaanza kujuta ni kwanini aliingilia harusi ya George Charles kifupi kila kitu kiliharibika na kwa lililotokea, hakuelewa angelikabili vipi,alivyoangalia pembeni akamuona Ahmed bado amelala fofofo!Akatoka kitandani na kuanza kupiga simu mbalimbali ili aulizie kama ni kweli habari hizo, ziliandikwa kwenye magazeti,jibu lilikuwa ni lilelile halikuweza kubadilika hata kidogo,akajiona kama amevuliwa nguo yupo katikati ya soko la Kariakoo,kuanzia dakika hiyo alipokea meseji nyingi sana!
Wengine wakitaka kujua undani zaidi kuhusu sakata hilo,baadhi walimpa pole lakini wengi walimbeza,simu za ndugu jamaa na marafiki hakutaka kuzipokea kabisa,alielewa ni kwa namna gani wangezidi kumchanganya,alichokifanya ni kuzima simu kwanza ili atulie,wasiwasi wake mkubwa na hofu yake, ilikuwa juu ya Ahmed,alielewa vizuri kabisa kwamba ni lazima angeamka angekumbana na picha hizo ama kupigiwa simu,haraka akanyoosha mpaka chumbani,alivyoangalia mezani akaona simu ya Ahmed, imezimwa ipo kwenye chaji.Akatulia na kutafakari kwa muda,akamtizama Ahmed ambaye bado alikuwa amelala,akaiwasha.Meseji ziliingia nyingi,mfululizo hapohapo simu ikaanza kuita na jina lililotokea kwenye kioo lilikuwa ni Kassim,akajifikiria kwa muda kidogo, alijua ni lazima Kassim alitaka kutoa unoko huo kwa Ahmed kwani haikuwa kawaida yake kupiga simu asubuhi namna hiyo,ilivyoendelea kuita akatoka chumbani na kuipokelea seblen.
“Broo shikamoo”
Upande wa pili wa simu ulisikika,Kassim alisalimia akijua Ahmed ndiye yupo kwenye laini.
“Amelala”
“Aaah,Yusrath”
“Yes”
“Za masiku?”
“Safi tu”
“Umenitenga”
“Mimi nipo,namba yangu kwani huna?”
“Ninayo,sema si unajua tena.Naomba kuongea na Ahmed”
“Amelala,niambie tu.Nitamwambia”
“Ni mambo ya kifamilia Yusrath”
“Basi,akiamka nitamwambia”
“Haina noma,nitakupigia basi kwenye simu yako!Kuna mambo nataka tuongee”
“Mambo gani?”
“Mimi nawewe tena,tutaongea!Nitakupigia”
“Aya”
Yusrath alivyokata simu,akaingia kwenye uwanja wa meseji na kukuta yaleyale aliyowaza,meseji nyingi zilikuwa kuhusu magazeti ya siku hiyo sura yake ilivyoonekana,akatamani ardhi ipasuke akimbie aibu.Akili yake,ikaacha kufanya kazi kwa dakika,akatamani abebe kilicho chake atokomee kusikojulikana ili akimbie balaa lililokuwa mbeleni,katika kutafakari hayo, akasikia sauti ya Ahmed inamuita kutokea ndani chumbani.
“Abeee”
Akaitikia na kushusha pumzi ndefu,akatembea na kuingia chumbani!Huko,alimkuta Ahmed tayari amekaa kitandani, anapiga mihayo.
“Simu yangu unayo?”
“Yes ninayo”
“Ulikuwa unaangalia nini?Punguza wivu”
“Ndio baby,lazima niwe na wivu.Nilitaka nijue nani alikalia kiti changu,nilivyoondoka”
“Hakuna yoyote”
“Mmmmh mmmh mhhhhhhh”
Hapo Yusrath aliguna kimahaba,akamkabidhi Ahmed simu yake huku moyoni akimuomba Mungu,lisitokee la kutokea maana alishindwa kuelewa sura yake angeiweka wapi.
Simu kutoka kwa Bashir Hassan,ndio iliyomfanya Ahmed asitishe maongezi yake na Yusrath.Mtu huyo kupiga simu ilimfanya atulie kidogo sababu hakuwahi kupigiwa tangu afunge ndoa,mbaya zaidi mwanamme huyo alikuwa Mtwara,hakutaka kujiuliza akajua ni lazima kuna shida.
“Bashir”
Alivyopokea simu,akataja jina.
“Naam Ahmed,Aasalam aelekuy”
“Walekuy muslam,vipi upo?”
“Nipo Shekh,umepotea sana”
“Mimi nipo,mbona asubuhi asubuhi kwema kweli?”
Ahmed akashindwa kuvumilia,akaanza kumchimba.
“Huku salama,umesoma gazeti la leo?”
“Gazeti la leo?Huwa sisomi magazeti mimi”
“Au nitakuwa nimemfananisha basi”
“Nani?”
“Mke wako”
“Mke wangu?Nani?!”
Lilikuwa ni swali,lililoambatana na mshangao!Alikuwa na mke mmoja,anayejulikana lakini alijikuta anauliza swali hilo.
“Kwani una wake wangapi?Au umeoa mwingine?”
“Nina mke mmoja”
Wakati anazungumza hayo yote,Yusrath alikuwa pembeni yake anahisi kama mkojo unataka kumpenya.
“Basi,kanunue gazeti la leo”
“Gazeti gani sasa?”
“Udaku,Dar leo,Kumekucha na Chimbo”
“Sawa,nitanunua”
Kitendo cha kukata simu,akakumbana na meseji nyingi sana.Alivyoingia ‘WatsApp’ moyo wake ukapiga paa!Baada ya kuona ametumiwa picha ya gazeti juu kuna sura ya Mkewe Yusrath,mbaya zaidi kichwa cha habari kiliandikwa ‘MWANAMKE AJITOKEZA,KUDAI AMEZAA NA BILIONEA GEORGE UTATA WAIBUKA’Jambo lililomfanya aduawe ni picha ya Yusrath, iliyoonesha mavazi aliyokuwa nayo jana yake, kipindi wapo hospitalini.

****
Askari hawakuwa na shida tena na Necka Golden,alikaa siku kumi na tano rumande bila mshtaki wala ndugu yoyote Yule kufika na kumuona,hilo liliwafanya askari washindwe kumfungulia kesi mahakamani,walivyomuhoji alisema hana ndugu yoyote Yule, kama wanataka pesa wafute jambo hilo kichwani kwake,alijibu kwa kiburi kwani kukaa rumande kwake ilikuwa shwari tu,halikuwa jambo la kushtusha na lililomuumiza kichwa!Polisi ilibidi wamruhusu maana hawakuwa na jinsi yoyote ile,kitendo cha kutoka rumande akamfikiria mtu mmoja tu,Ahmed Kajeme mwanamme aliyemfanya afunge safari kutoka kwao kijijini mpaka Dar es salaam kwa ajili yake,ilikuwa ni lazima arudi tena Ubungo Kibangu ili amsake,ijulake zipi mbivu zipi mbichi.Alichokifanya ni kutembea kwa miguu kutoka Ubungo Mawasiliano mpaka darajani,ambapo hapo alipumzika kidogo ili aendelee na safari.Wengi,walimtupia macho na kumshangaa kwani alifanana na kichaa na alitoa harufu nzito ya jasho,nywele zake zilikuwa ndefu zimejaa vumbi.
“Necka!”
Sauti hiyo ilimfanya ageuke nyuma,amuangalie mtu anayemuita.Hakuamini macho yake,ikawa kama yupo ndotoni.
“Amney”
“Necka,ni wewe ama naota?”
Kila kitu kilikuwa kama ndoto siku hiyo kwa marafiki hao kukutana kwa mara nyingine!

****
Magazeti yalizidi kuuzwa,kila mtu alitaka kuisoma habari hiyo.Sakata la George Charles lilizua sintofahamu kwa kila mtanzania,hakuna hata mmoja aliyetegemea kama mwanamme huyo angekuwa muhuni namna hiyo,wengine walienda mbali zaidi wakadiriki kusema kwamba alitelekeza mtoto na ilibidi vyombo husika wamfunze adabu hakuna kati yao aliyejua nyuma ya pazia kuna nini.Waandishi wa habari walitaka namba yake ili wamuhoji lakini halikuwa jambo jepesi kama wanavyodhani,skendo hiyo ilimchafua vibaya sana.Ikawa kama amepakwa mavi usoni,akiwa nchini Ufaransa,ndani ya jiji la Paris Effile Tower ndani ya hotel ya kifahari anakula fungate.
Ndipo taarifa hizo zilimfikia,Lissa Mnzava aliuwasha moto usio wa kawaida,haikujulikana gazeti hilo alilitoa wapi lakini alikuwa nalo mkononi.
“George,Malaya mkubwa.Kwanini ulinificha?Kwanini hukuniambia ukweli?Naongea nawewe Son of a bitch,talk to me Motherfucker!Kumbe una mtoto nje?”
Lissa Nzava,hakukaa kitako.Aliongea kwa sauti kubwa tena akipayuka,jambo hilo lilimkera kwa kiasi cha kutosha,hasira zilimkaba kohoni.Akahisi kama kuna lidudu limemshika,moto wake haukuwa wa kawaida hiyo ilimfanya mpaka abadilike rangi kabisa.
“Please calm down my wife”(Tafadhali,punguza jazba mke wangu)
“Fuck you,Fuck you George,Fuck you”
Usingeamini kwamba huyu ni Bilionea,anayeheshimika nje na ndani ya nchi,matusi aliyokuwa anapewa kama ingekuwa mtu mwingine angewekwa jela na pengine kuhukumiwa kifungo cha maisha kama sio kunyongwa,lakini ilikuwa tofauti kwa Lissa Mnzava,ambaye alimjua tajiri huyo nje –ndani.
“Lissa,naomba tuzungumze”
“Tuzungumze nini?Wakati najua data zako zooote,I know each and everything.Huyo kahaba wako anaitwa Yusrath,ameolewa na mwanamme mmoja anaitwa Ahmed a…”
“Honey pleas…”
“No stop,listen to me.I’m still talking….Umezaa naye watoto mapacha Faad na Faisal,uwongo?”
Angekuwa mjanja,angekaa kimya!Kuliko kuropoka hakuelewa kwamba habari hizo,zilikuwa mpya kwa George Charles.
“For your information,hivi soon nitaipata namba ya Mume wake.Nitamwambia kila kitu,kwamba umezaa na Mkewe”
Lissa Mnzava,akahitimisha na kila alichokuwa anazungumza alikimaanisha.Data zote na kila kitu alikipata nchini Tanzania,kwa watu wake aliowatuma kazi hizo, ambayo waliifanya ndani ya masaa machache,alichokua anasubiri yeye ni namba za Ahmed tu,ili ampigie amwambie kila kitu.



Bilionea George Charles alihisi joto lisilokuwa la kawaida,ndani ya hoteli hiyo!Kulikuwa kuna baridi lakini alihisi kama hakuna hewa kabisa,hiyo ni kutokana na kelele alizokuwa anapigiwa na Lissa Nzava,alilalamika na kumchimba mikwara mingi akisema kwamba angemwambia Mme wa Yusrath kila kitu kilichotokea,hilo lilikuwa mbioni kutokea sababu Lissa Nzava, alionesha chuki za waziwazi.Jitihada za George kumtuliza ziligonga mwamba,alichokifanya mwanamme huyo ni kutulia,akasimama na kwenda kwenye friji, hapo alichukua mzinga wa ‘Whisky’ akamimina kwenye glasi,hilo likazidi kumkera zaidi Lissa akatafsiri kama dharau fulani,hakutaka kulifumbia macho jambo hilo.
“Kwahiyo,mimi naongea pumba?”
Lissa Mnzava akauliza na alitaka jibu.
“Niambie cha kufanya,nasubiri umalize kuongea.Waswahili wanasema,kuimba kupokezana”
Kuishi sana bongo na kukaa na masela kulimfanya ajue misemo ya geto,akasukumia msemo huo na kumimina pombe kali kwenye glasi,akachukua barafu na kuzitumbukiza.Hiyo ilimfanya Lissa atulie kidogo na kumtizama kuanzia juu mpaka chini,ilielekea aliishiwa pozi kabisa!
“Umemaliza kuongea?”
George akauliza,baada ya kuona ukimya huo!
“Bado,Yusrath ni nani kwako?”
“Unataka kujua ukweli?”
“Ndio maana nimeuliza”
“Unapenda kusikia uwongo ama ukweli?”
“George,I’m serious.Yusrath ni nani yako?”
“Nakwambia ukweli,sasa hivi.Kwanza relax,sipendi sana kuzungumza kuhusu my past lakini unanifosi”
Akapiga fundo moja la glasi,akamtizama Lissa Nzava kwa umakini na macho fulani yaliyokuwa tayari kwa kuzungumza kila kitu,bila kuficha chochote akamsimulia mkasa mzima tangu alivyoanza kumfukuzia msichana huyo akitumia gia zote na nyimbo zote akimuimbisha lakini mwisho wa siku alichezea kibuti, akatoswa!Akamuajiri katika ofisi yake kwa niya ya kumvuta karibu lakini mwisho wa siku akaja kuolewa.
Hakuacha kumsifia na kudai kwamba angetamani ampate msichana wa sampuli hiyo, bila kuelewa hiyo ilimchoma sana Lissa,akahitimisha na kusema kwamba asamehewe kwani hakujua kama siku ya harusi yao tukio lile la kutia aibu lingetokea mbele ya kadamnasi na wageni wa heshima.
“Did you fuck her?”
Lissa badala ya kuuliza kwa kauli nzuri akatumia lugha ya kihuni tena ya matusi,hakuwa mstaarabu hata kidogo na wala hakutumia tafsida!
“To be honest,yes lakini once!Ni mara moja,nilimfosi”
“Ndio siku aliyoshika mimba,right?”
“I real don’t know,baada ya hapo.Hatukuwasiliana tena alinichukia sana,we never talk.Nilimtafuta bila mafanikio and after few months nikasikia ameolewa,it was like that.Kuhusu hao watoto unaoniambia,ndio najua leo.Hata alivyokuja that day,nilishangaa sana!I’m so sorry Lissa,sina mtoto nje.I wish niwe na mtoto hata leo,naamini utanizalia watoto mke wangu”
Ilikuwa ni historia ya kugusa sana aliyoitoa George, hakujali Lissa angeumia kwa namna gani lakini alichoamini yeye siku zote ukiongea ukweli unakuweka huru,hiyo haikumfanya mwanamke huyo akubaliane naye kwa asilimia zote mia moja, akamtizama George machoni kwa umakini,akahisi kwamba anapigwa kanjanja ili alainike.Hata hivyo,bado kuna kitu alitaka kujua zaidi akashindwa kuvumilia,akataka kuuliza.
“May i ask you something?”(Naweza kukuuliza kitu)
Lissa akauliza kwa sauti ya upole.
“Sure”
“Mfano,ukigundua Yule Yusrath,amezaa nawewe.Wale watoto ni wako!Utafanya nini?”
Lilikuwa ni swali lililosikika vizuri lakini jibu lake lilikuwa gumu kidogo kutoka,katika kitu kama hiko George Charles ilibidi ajibu kwa busara sana!
“Kitanda hakizai haramu,it depends on you kama utakubali nikawachukue watoto.Tuje kuishi nao”
“Hell no,siwezi kukubali.I can’t,how?Kivipi kwa mfano?George nilee watoto wa mwanamke mwingine?Kwani mimi sina kizazi al..”
“Baby please,usitake kuanza malumbano.Umeuliza swali nimekujibu”
“Naumia baby,imagine mimi ndio nakwambia hivyo”
“Sikatai,lakini watoto hawana kosa lolote”
“Bado unampenda Yusrath?”
“Nishaoa,nakupenda wewe”
“Nakupenda pia Mme wangu”
Lissa Mnzava,akapachika tabasamu la plastiki usoni lakini moyoni alijenga chuki za waziwazi, akajua ni lazima tu George Charles,kamuongopea na anajua kila kitu kuhusu watoto wake mapacha!Alivyofikiria mali alizokuwa nazo,aliumia zaidi.Akiamini kwamba watoto hao tayari waliandikishwa mali hizo,hilo likazidi kumuumiza kichwa zaidi na zaidi.
Mkakati mpya,ukaanza kujijenga ndani ya akili yake kwamba awauwe watoto hao kisha baadaye afuate George Charles,ghafla pepo la Mauaji likamuingia akamtizama George Charles na kumbusu juu ya paji la uso!
“I’m so sorry baby,ni hasira tu na Wivu”
“Usijali Honey”
Mawazo ya Georgre Charles,hayakuwa hapo tena.Ilikuwa ni lazima amtafute Yusrath wazungumze vizuri ili ajue kama ni kweli,watoto mapacha ni wake!Huo ndio mkakati aliopanga akirejea nchini Tanzania.

*****
Ahmed alihisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi,akashindwa kusimama kutoka kitandani lakini alijikaza hivyohivyo na kutoka ndani ya shuka,picha alizoziona kwenye simu yake kwamba Yusrath alienda Kanisani kumlilia George Charles,zilimfanya achanganyikiwe, ilikuwa kidogo atoke na boxa seblen akarudi na kuvaa bukta fupi.Akachomoka kama mkuki,moja kwa moja mpaka nje, ambapo huko alitembea mpaka kwenye meza moja wanayouza magazeti kama kawaida aliwakuta watu wamesimama wanasoma vichwa vya habari,wengine sio wanunuaji.
Karibia nusu ya magazeti yalionesha picha ya Yusrath juu yake,waliomjua walimtizama na kumnyooshea vidole kwani walimtambua ndiye Mme halali wa Yusrath.Ilikuwa ni aibu ambayo alishindwa kuelewa angeificha vipi,hakutaka kuzungumza na mtu yoyote baada ya kununua gazeti,huku nyuma aliacha minong’ono.
“Yule ndio Mme wake sasa”
Sentensi hiyo aliisikia,akiwa anatembea na gazeti hilo,alijua fika kabisa yeye ndiye anazungumziwa,alivyoingia ndani akaanza kuangalia picha ya juu inayomuonesha Yusrath ameshikwa na maaskari,akafungua ukurasa wa katikati ambapo huko alikuta maelezo yenye utata.Hakutaka kukaa kimya,akanyoosha mpaka chumbani na kumtupia Yusrath gazeti kichwani.
“Nini hiki?”
Ahmed,akauliza kwa jazba na kubana meno yake kwa hasira akitaka maelezo yaliyonyooka kutoka kwa Yusrath.Kuanzia hapo Ahmed hakuzungumza tena akabaki anamtizama Yusrath anayetetemeka kashika gazeti, badala ya kushika gazeti vizuri akaligeuza,chini juu, juu-chini,alikuwa akitetemeka kwa hofu,hiyo ilimfanya alidondoshe chini.Hakuelewa aanzie wapi aishie wapi!
“Kumbe hata watoto wale,sio wangu?Yusraaaaaath”
Ahmed,akazidi kufoka akitaka kujua jibu hilo hususani kuhusu watoto,moyo wake ulichoma lakini aliendelea kujifariji watakuwa wake tu,ndio maana akatulia ili amsikilizie Yusrath, angesema nini.
“Ha..ha haa..pana baby,naomba tuzungumze”Kigugumizi kikamshika ghafla.
“Uzungumze nini?Niambie ukweli,leo nakuuua”
Kulikuwa kuna kila dalili mbaya siku hiyo ilikuwa ni wazi kabisa Yusrath, asingetoka salama kwani Ahmed alisogea mpaka mlangoni na kufunga mlango kwa ufunguo,hiyo ilimfanya Yusrath aanze kusali sala zake zote na dua zote anazozijua yeye!
“Baby nisikilize”
“Ongea”
Kila gia aliyotaka kutumia ili amdanganye Ahmed ilishindikana,wakati mwingine alitamani kuongea ukweli lakini alishindwa sababu alijua madhara yake mbeleni,hiyo ilikuwa wazi kabisa angejiweka yeye na watoto wake sehemu mbaya!
“Ahmed,naomba nikwambie uk..”
“Nijibu,watoto wa nani?”
Sauti ya Ahmed,ilienea chumba kizima ikatokeza mpaka seblen,ikamfikia Hadima.Fununu za magazeti na tatizo lililojitokeza siku hiyo, alihisi akajua ni lazima leo Yusrath atapigwa,mbaya zaidi alivyosikia mlango umefungwa,ilikuwa ni lazima achukuwe hatua sababu alimjua sana Ahmed na hasira zake,kumpiga Yusrath kilikuwa ni kitu cha kawaida sana,aliichukia tabia hiyo lakini hakuwa na jinsi,alichokifanya ni kukimbia mpaka jikoni,akachukua simu yake na kuanza kumtafuta Mama Ahmed hewani,alimpigia bila mafanikio lakini baadaye simu ilipokelewa.
“Shikamoo Mama,njoo nyumbani nakuomba Mama”
Bila kuitikiwa salamu, Hadima akasema shida yake.
“Kuna nini?”
“Nakuomba Mama njoo,fanya haraka”
“We mtoto,kuna nini huko?Nakuja sasa hivi”
Kitendo cha kukata simu,akasikia vishindo chumbani, kelele za Yusrath akilia na kuomba msaada, zilisikika lakini hakuwa na jinsi kwani mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani,hiyo ilimaanisha alikuwa anapokea kipondo kutoka kwa Ahmed.

****
Simu kutoka kwa Hadima ilimkuta Mama Ahmed yupo chumbani,ametoka kuchemsha chai na kukanda maandazi.Bila kuoga akamfuata Kassim na kumgongea mlango akimwambia aamke kuna jambo la muhimu,mlango ukafunguliwa Kassim akatoka akiwa na taulo,katoa kichwa nje.
“Nipeleke kwa kaka yako sasa hivi”
Mama alisema kwa haraka akimaanisha Kassim ndiye awe dereva wake.
“Kuna nini Mama?Shikamoo ndio nimerudi sasa hivi”
“Fanya haraka,nipeleke kwa Ahmed”
“Mama,sijaoga bado”
“Twende twende”
Kassim,alishaanza kuhisi nini kinaendelea.Magazeti ya siku hiyo yalimfanya ajuwe kwamba ni lazima Ahmed kauwasha moto na kimenuka tayari,lakini alivyofikiria hasira za kaka yake,aliumia sababu alijua ni aina gani ya kipigo kingetokea.Kwa kasi akavuta tisheti akavaa na suruali akawa wa kwanza kutoka,akakutana na Mama yake,akapewa funguo za gari wote wakatoka nje.
Moyo wa Kassim uliuma na kuchoma kama pasi,japokuwa hakuwa ana uhakika nini kimetokea lakini asilimia zote mia moja alianza kuhisi.
“Mama kwani kuna nini?”
Kassim akauliza huku akirudisha gari nyuma.
“Sijui,ebu subiri Hadima anapiga”
Mama akapokea simu.
“Ndio,unasema?Kamfungia Chumbani?Mungu wangu….Anapiga kelele,nakuja sasa hivi nipo njiani….”
Alivyokata simu akakumbana na swali kutoka kwa Kassim.
“Kaka yako,anatafuta kufungwa.Hajaacha upumbavu wake unajua”
“Kafanya nini?”
“Anampiga mkewe”
“Whaaat?”(Ninii)
Kassim aliuliza kwa uchungu na mshangao wa waziwazi,moyo ukazidi kumuuma akakanyaga mafuta mengi ili akamuokoe Yusrath, mwanamke aliyetokea kumpenda miaka mingi sana lakini Kaka yake alimzidi kete na kumpokonya tonge mdomoni.
“Endesha gari taratibu Kassim”
Mama akakemea,uendeshaji mbovu wa Kassim ulimfanya atoe onyo kali kwani gari lilipitishwa kwenye matuta na kudunda kwa nguvu,hata hivyo Kassim hakusikia alichoambiwa kiliingilia sikio la kushoto na kupitia la kulia,alivyoona kuna msongamano mkubwa wa magari,akatanua pembeni na kukanyaga mafuta mengi,hiyo ikafanya vumbi litimke nje na kufanya watu wasionane!

*****

Katika siku ambayo Yusrath alipigwa kuliko zote ni hiyo,ilikuwa ni kama Ahmed amepandwa na mashetani,kila alichokiona mbele yake alimpiga nacho Yusrath akawa kama anapiga punda,jambo lililompelekea Yusrath aanze kuvuja damu puani na mdomoni ‘lips’ zake zilichanika vibaya sana.Lakini hilo halikumfanya Ahmed, asitishe kipigo,aliendelea kumzabua makofi akachomoa na mkanda, akazidi kumkung’uta nao vibaya sana kichwani!Yusrath alilia kiasi kwamba sauti ikawa imemkauka, yupo kwenye kona ya ukuta,anasubiri kifo chake kwani ndilo jambo lililokuwa mbele yake,kila sehemu ya mwili wake ilikuwa inauma.
“Na watoto naenda kuwaua,wote.Kisha nakuja kukumaliza nawewe Malaya kahaba mbwa”
Ahmed hakutania,akageuka lakini akashindwa kupiga hatua kwani mguu wake ulikumbatiwa na Yusrath aliyekuwa chini kaung’ang’ania.
“Ahm..ed usiniulie wananguu,Ahmed nakuombaaa niuee mimiii tu,inatoshaa”
Yusrath alizungumza kwa uchungu huku akilia sana,machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni.Kitendo cha kumuachia Ahmed, kilimaanisha watoto wangeenda kufa hakutaka hilo litokee,ndiyo maana aliendelea kumshika mguu lakini badala yake alitulizwa na kibao cha uso,kichwa chake kikajipigiza kwenye ukuta,Ahmed akajivuta kwa nguvu mpaka mlangoni akafungua.
Kilichokuwa kinamtuma kwa wakati huo ni kitu kimoja tu,kuwauwa watoto wachanga ambao kwa asilimia mia moja alijua sio wa kwake!Akafungua mlango,bahati mbaya ikawa kwake na nzuri kwa watoto wachanga kwani Hadima alisikia kila kitu,akaenda kuwaficha nje huko ndani ya kikapu,akawafunika na kitambaa kikubwa cha mezani kwa juu.
Kitu cha kwanza alichokifanya Ahmed ni kuingia jikoni,akabeba kisu!Akanyoosha mpaka chumbani kwa Hadima,akawakosa watoto,akapita seblen hakuwaona.
“Wako wapi?”
Lilikuwa ni swali,lililomlenga Hadima.Kidogo aulize wakina nani lakini aliogopa kisu kikali alichoshika Ahmed mkononi, akiwa anahema juujuu majasho yanamtoka.
“Baba an..”
“Watoto wako wapi?”
“Wa wa..wawapo Chumbani”
“Hadima,nitakuuua wak…”
“Ng’aaaa! Ng’aaaa! Ng’aaaaaaa!”
Sauti ya mtoto,ilisikika akilia kutokea nje hiyo ilimfanya Ahmed agundue kwamba wapo nje,akageuza ili awafuate akawamalize,ni kweli alitokeza uwani akaona kapu limefunikwa sauti inatokea ndani yake,akashika kisu vizuri na kupiga hatua akiwasogelea, tayari kwa kuwatoboa toboa wafe.

*******
“Pipiii piiii piiiiiiii piiiiiiiiiiii”
Kassim aliendesha gari kama mtu aliyerukwa na akili,alipiga honi mfululizo kila alipoona watu mbele yake,barabara ya Shekilango ilikuwa imeziba kabisa, msongamano mkubwa!Kwa kuwa alikuwa mtoto wa mjini alizijua njia zote za Panya,akavunja sheria na kuzungusha usukani magari yanapotokea akapanda tuta la katikati na kuingia kulia ambapo huko kulikuwa na barabara ya vumbi,niya yake ilikuwa afupishe njia apitie Makaburini aibukie Shungashunga External,jambo hilo alifanikiwa.
Mwendo ulikuwa ni uleule ‘spidi 120’ akifukia matuta,mpaka alipoibuka Ubungo maziwa,akachomoka na kutokea mataa ya Extenal akakata kulia na kunyoosha!Mama yake mzazi,roho yake ilikuwa mkononi,alishaongea kuhusu mwendo anaotumia Kassim lakini ikawa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki,ndani ya dakika kumi na tano wakawa wamefika Riverside,hapo ilikuwa kidogo Kassim agonge meza za samaki za akina mama waliokuwa kandokando wanauza,hakujali alichojali yeye ni kuwahi kwa Ahmed.Haikuchukua dakika tano,akapiga breki nje ya geti akashuka kwa kasi bila kufunga mlango.Akaparamia geti na kuzama ndani!
“Uwiiii jamaaaaani,uwiiiiiiii naombeniiii msaaaaada”
Zilikuwa ni kelele kutoka kwa Hadima akiomba msaada huku akipiga piga miguu yake chini,kulikuwa kuna kila dalili mbaya siku hiyo na ilionesha tayari Ahmed ameua watoto.Kassim alivyoingia akakumbana na kelele kutoka kwa Hadima,alivyojaribu kumuuliza hakupewa jibu kamili.
“Baba ameua watotooo…Uwiiiiiiii”
“Yuko wapi?”Kassim akauliza kwa hamaki.
Badala ya Hadima kujibu,akanyoosha kidole upande wa uwani.Kassim bila kuuliza akapiga hatua tatu kubwa na kutokeza nje,alichokiona kilimtisha sana!Mama Ahmed nayeye akatokeza hapohapo kwa nyuma,wote wakaogopa na kuanza kutetemeka, hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini kilichotokea, damu zilitapakaa pembeni!


Mwili wake wote ulimtetemeka na alihisi maumivu makali sana, hiyo ni kutokana na damu kumwenda mbio na kufanya mapigo ya moyo yagonge mara mia moja kwa sekunde,ilikuwa ni hatari kubwa sana kwani mishipa yote inayopitisha damu ilizidiwa.Hiyo ilitokana na hasira mbaya sana baada ya kugundua watoto aliowalea sio wa kwake amebambikiwa,akampiga sana Yusrath hakuwa ana uhakika kama ameua ama la!Kwake hakujali kabisa,hasira ndizo zilimpeleka puta.Akaanza kuhema juujuu kama mtu anayetafuta pumzi kwa shida,alivyoingia chumbani na kuwakosa hali yake ikazidi kuwa mbaya zaidi, ghafla akaona giza mbele,akafumba macho na kuyafumbua nuru ikarudi, akaingia jikoni akiwa na kisu mkononi,akampita Hadima na kutokeza uwani baada ya kusikia kilio cha mtoto mchanga,pepo baya na chafu la kuua ndilo lilikuwa ndani yake, likampeleka puta, likitaka liue!Mbele aliona kikapu,watoto walikuwa ndani yake ilikuwa ni lazima awachome chome na kisu,kwake yeye ingekuwa mara ya kwanza kufanya hivyo,ndiyo maana alianza kutetemeka na kutandwa na hofu,akasogea kwa kasi!
Kwa hali ya kushangaza akahisi kichwa kinamuuma sana,kinavuta na kinagonga yaani kama mtu ameingia kichwani kwake na nyundo!Hiyo haikumzuia akajikaza,alivyowakaribia akahisi kama kuna kitu kinachuruzika puani,akadhani wenda ni kamasi lakini isingekuwa rahisi kwani hakuwa na mafua,akapitisha mkono puani ili kupangusa, alivyorudisha ili kuangalia,hakuamini baada ya kuona damu!Kichwa kikauma kwa nguvu,akaanza kuishiwa nguvu za miguu,akajikaza lakini alishindwa,giza la ghafla likatokea mbele yake!Akadondoka puu chini kama mzigo huku damu zikiendelea kumtoka puani!
Kitendo cha Kassim kufika na Mama yake kutokeza eneo hilo kiliwashtua sana,Ahmed alikuwa chini anavuja damu puani zimesambaa mpaka mdomoni!Kilikuwa ni kitendo kilichowafanya washindwe kujua nini chanzo,Hadima aliyekuwa jikoni alikuwa akilia tu.Wakamsogelea Ahmed mpaka karibu kabisa ili kujua kama ana uhai ama amekata kauli,tumbo la Ahmed lilikuwa linapanda juu na kushuka kumaanisha kwamba bado anahema.Kelele nyingi ziliwashtua kutokea kwa Hadima,hiyo iliwafanya wote waachane na Ahmed aliyekuwa chini na kutaka kujua ndani kuna nini,Kassim akawa wa kwanza kuingia ndani akakimbia kwa kasi mpaka chumba cha Ahmed!Walichokiona kilizidi kuwaogopesha zaidi,Yusrath alikuwa chali,amelala amevimba mwili mzima kila mahali amevulia damu,hali yake ilitisha na hakutofautishwa na mtu aliyegongwa na gari kubwa ama treni.
Tukio hilo lilimfanya Mama Ahmed achukuwe maamuzi ya haraka kwamba wapakiwe kwenye gari ili safari ya kwenda hospitalini ianze mara moja!
“Mshike kwa huko vizuri”
Kassim ndiye alitoa maagizo hayo,wakamshika vizuri Yusrath na kumkokota mpaka nje,wakampakia ndani ya gari.Ahmed akafuata nayeye akabebwa wakaingizwa ndani ya gari!Kwa kuwa ilikuwa ni asubuhi kweupe, baadhi ya majirani na wapita njia walishuhudia tukio hilo,hawakutaka kupitwa, wakaanza kuzingira gari na kushangaa, kila mtu akisema lake kama kawaida ya wabongo.
“Dada wewe baki na watoto”
Kassim akatoa ushauri baada ya kumuona Hadima kashika watoto yupo nayeye anawafuata nyuma.
“Hapana,naogopa”
“Sawa,kafunge nyumba twende wote harakisha”
Baada ya kila kitu kwenda sawa,Kassim akalitia gari moto kwa safari ya kwenda hospitalini ikaanza, ndani akiwemo Hadima pia!Kwa kuwa ilikuwa ni dharura ikambidi awashe taa za mbele ‘full’ na ‘hazard’ juu kumaanisha kwamba ana uwezo wa kukimbiza gari vyovyote anavyotaka bila kusumbuliwa na askari wa usalama barabarani.Dakika mbili baadaye wakawa tayari wametokea barabara kubwa,wakaingia kwenye lami na kuanza kunyoosha kulia.
“Hospitali gani ya karibu kubwa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Kassim akiwa ameshika usukani kwa mikono miwili,macho yote yapo mbele anakimbiza gari mno,pedeli kwenye mguu wake ipo chini kabisa kumaanisha gari linakimbia mno!Moyo wake ulimuuma kwa kiasi cha kutosha,hakuelewa ni kitu gani kilimpata Yusrath ingawa alihisi ni lazima alipigwa na Ahmed kipigo kibaya sana.Akiwa anaendesha gari alitafakari vitu vingi sana na kumshangaa kaka yake kwa tabia aliyokuwa nayo ya kupiga wanawake,alimchukulia ni mshamba tena limbukeni wa mapenzi,kutokea shamba huko!
“Ilikuwaje?”
Kabla ya kujibiwa swali la kwanza,akaibua lingine japokuwa hakumgeukia Hadima lakini ilieleweka kwamba swali hilo ni lake,akiwa katika wasiwasi mkubwa alianza kuelezea ilivyokuwa tangu asubuhi Ahmed alivyotoka na bukta kisha baadaye kurejea na gazeti,kufuata hapo alianza kusikia kelele za malumbano na mlango kufungwa.Hakuacha kusema namna Ahmed alivyotoka na kisu ili kutaka kuwauwa watoto.
“Nisikilize Hadima”
Mama,akataka kutia neno.
“Hizi habari,usimwambie mtu yoyote Yule.Kaa kimya”
“Sawa Mama”
Mmewe alikuwa mtu wa serikalini mpelelezi,ndiyo maana Mama Ahmed alikuwa mjanja,alishaelewa huko mbeleni ni lazima polisi wangetaka kujua nini kilitokea, hiyo ilimaanisha Ahmed kuwekwa rumande kama ukweli ungejulikana alitaka kuwauwa watoto hilo lisingekuwa na mjadala, jela ingemuhusu.
Maelezo yakatolewa kwamba wanyooshe Mpaka Tabata,katika hospitali kubwa inayoitwa Madona!Jina hilo halikuwa ngeni kwa Kassim akazidi kunyoosha goti, gari likazidi kuserereka mpaka walipofika Tabata Relini,akakunja kushoto na kushusha kilima alivyoibuka akakunja kona na kuingia ndani ya geti la hospitali hiyo.
“Msaada tafadhali”
Manesi walikuwa tayari nje kwani namna gari lilivyoingia kwa kasi iliwafanya wagundue kuna aina gani ya mgonjwa ndani,haraka wakatoka na kitanda chenye magurudumu kwa chini.
“Leta kingine”
Amri hiyo ikatoka baada ya kugundua kuna wagonjwa wawili ndani ya gari,wakapakiwa juu ya kitanda na kuanza kukimbizwa kwa kasi kwenye vyumba maalum!
“Wamefanya nini?”
Nesi akauliza,Hadima alivyotaka kujibu Mama akamkata jicho fulani linalosema ‘Kaa kimya’ akamezea swali hilo,akajifanya hajasikia!
“Ni mtu na mkewe,hatujui imekuaje”
Mama akajibu,vitanda vikaingizwa ndani ya chumba maalum!Dakika tano baadaye akatokeza mwanamme mrefu,mwembamba amevalia koti jeupe.Hiyo ilitosha kabisa kugundua kwamba ni daktari.
“Naitwa Dokta Mickdald Sanga,nyie ndio ndugu wa hawa wagonjwa walioletwa hapa sasa hivi?”
“Ndio, mimi ndio Mama yao”
Mama akadakia,dokta akamtizama kwa macho ya huruma.
“Ni watoto wako?”
“Hapana,huyu wa kiume ndio mwanangu!Wa kike mkwe wangu”
“Nakuomba ofisini,mara moja”
Dalili za habari mbaya zilionekana, kuna kitu alijifunza kutoka machoni mwa dokta Sanga lakini hakutaka kuyapa mawazo yake kipaumbele,akamfuata nyuma mpaka ofisini kwake na kuketi kwenye kiti cha wageni.
“Kuna nini?”
Mama akauliza,dokta akamtizama!
“Siwezi kukuhaidi kama kuna habari nzuri lakini tumuombe Mungu”
“Dokta mbona sikuelewi?!”
“Mkweo jina lake nani?”
“Yusrath,Yusrath Kajeme Mwanamme anaitwa Ahmed Kajeme”
Mama akajiongeza na kujibu swali lingine la mbele.
“Inshort wote wana hali mbaya, lakini mmoja wapo ana hali mbaya zaidi isi…”
Kabla ya dokta kumalizia sentensi yake akaingia nesi akipiga kelele na kumuomba Dokta wainuke kwani kuna mgonjwa ana kata rohoo!

****
Skendo ya Yusrath kwenye magazeti ilitapakaa jiji zima kama moshi wa kifuu,ndugu wa karibu walitaka kujua zaidi.Mama yake mzazi alipata taarifa hiyo mapema sana alivyompigia simu Yusrath akakosa jibu lenye uhakika, bado hakutaka kuamini akajua ni porojo tu ingawa sura ya Bilionea George haikuwa ngeni kabisa,akakumbuka kwamba mwanamme huyo alishawahi kufika nyumbani hapo!Hata hivyo hakuwahi kujua kwamba George Charles ni bilionea namna hiyo, ambaye angeweza kutokea mpaka kwenye magazeti.Jambo hilo hakutaka kuliweka sana kichwani,akaanza kumtafuta Yusrath kwa mara nyingine lakini matokeo yake simu iliita bila kupokelewa,akajaribu kupiga tena na tena hali ikawa hiyohiyo.Akatuma meseji lakini hazikujibiwa,alichokifanya ni kuanza kumsaka Ahmed hewani lakini ndio kabisa, simu haikupokelewa iliendelea kuita tu.Akatamani kuwa na namba za Hadima lakini hakuwa nazo,akatafakari kwa muda.
Akaona isiwe tabu kwanini aendelee kubaki wakati anapafahamu anapoishi Binti yake!Alichokifanya ni kujiandaa harakaharaka,alivyomaliza akampigia dereva taxi, ambaye siku zote alimzoea!
“Njoo unipeleke Ubungo Kibangu,ndio kwa yule binti yangu….Wahi,nakusubiri”
Mama Yusrath akawa tayari nje ya geti,ameshajitayarisha!Haikuchukuwa muda mrefu,taxi ikafika getini akapanda nyuma na safari ikaanza hapohapo!
Ghafla,akaanza kuhisi hali ya utofauti kabisa.Moyo wake ukawa mgumu akakosa raha, hiyo ilimaanisha ni lazima kutakuwa na jambo baya,lakini aliomba Mungu kitu anachofikiria kisiwe kweli sababu alimuelewa Ahmed,iliwezekana kabisa kamuuwa Yusrath kisha nayeye kujiua,hilo ndilo lilimnyima raha.Dakika thelathini baadaye wakawa wamefika nje ya geti,cha ajabu nje ya geti alimuona msichana mmoja mnene kiasi, amevaa suruali ya jeans ana makalio makubwa anagonga getini,akateremka na kusogea getini.
“Habari yako?”
“Salama Mama shikamoo”
“Marahaba”
Mama Yusrath hakutaka kuuliza zaidi nayeye akaanza kugonga geti lakini hakukuwa na dalili ya mtu yoyote kutoka,akachukuwa simu na kuanza kupiga lakini haipokelewa.
“Wenyewe wameenda hospitali”
Sauti hiyo kutoka pembeni,iliwafanya wageuke nyuma.Alikuwa ni kijana mmoja,anapita njia ikabidi wamsimamishe.
“Wameenda hospitali?”
Mama akauliza kwa mshangao.
“Ndio,ilikuja gari kuwachukua hapa”
“Gari?La wagonjwa au?”
Kijana aliyeropoka ikabidi aelezee tukio zima lilivyotokea mpaka mwisho.Akili ya Mama Yusrath ikafanya kazi kwa kasi ya mwewe.
“Hospitali gani wameenda?”
“Hapo sijui kwa kweli”
“Gari gani,lilikuja?”
“Sijui sana magari lakini ile ni Rav 4 nyekundu”
Gari hiyo haikuwa ngeni,aliifahamu sababu alishawahi kumuona nayo mkwewe Ahmed, akiitumia kumaanisha kwamba ilikuwa ni gari ya nyumbani kwao,hakuchelewa akatoa simu kutoka kwenye mkoba wake na kuanza kumtafuta Mama Ahmed hewani,simu ikaita mara mbili,mara ya tatu ya nne ndipo ikapokelewa.
“Habari shoga angu?”
Mama Yusrath,akasalimia kwanza akajifanya hajui lolote.
“Salama tu,za masiku?”
“Tunamshukuru Mungu,upo wapi?”
“Nipo hospitali hapa mara moja”
“Kuna nini?”
“Mambo tu ya kawaida”
Mama Ahmed,alionekana anataka kuficha kitu lakini hilo halikuwezekana kwani Mama huyu mwenye asili ya Kizaramo akaanza kuuwasha moto kwenye simu hapohapo,hakutaka kukwepesha.
“Nisikilize,niambie mpo hospitali gani?”
Akauliza kwa hasira na sauti ya ukali.
“Madona”
Jibu hilo lilimfanya Mama Yusrath akate simu,akaingia ndani ya taxi lakini kabla ya taxi kuondoka msichana aliyekuwa anagonga geti nayeye akaingia ndani ya texi.
“Mimi naitwa Hajrath”
Hajrath akajitambulisha,Mama Yusrath hakujibu chochote alichowaza yeye ni binti yake Yusrath na hali yake ipoje,alianza kuchezwa na machale kwamba ni lazima Ahmed kampiga kwa mara nyingine tu,akaapia kama ni kweli basi hilo sekeseke lake lisingeweza kuzuilika kiwepesi kwani asingeacha kuona rangi zote.

Ndani ya gari alizungumza mwenyewe kama mwendawazimu,mpaka wanafika hospitali alikuwa kama redio iliyowekwa mabetri ya national!Wa kwanza kuteremka ndani ya gari alikuwa ni yeye,akamuendea nesi aliyekuwa anatembea na trei lenye dawa.
“Namuulizia Yusrath,kuna mgonjwa amekuja hapa ame…”
Hakumalizia sentensi yake,akatokeza Mama Ahmed!
“Mwanangu amepatwa na nini?”
Bila salamu Mama Yusrath,akatupa swali.
“Mimi sielewi,ndio kwanza nimefika hapa”
“Usinidanganye,ujue nakuheshimu sana.Naomba tusivunjiane heshima.Mwanangu,amefanya nini?”
Mama Yusrath,akauliza kwa sauti ya ukali tena ya juu, hiyo ikafanya wauguzi pamoja na wagonjwa, waliokuwa kwenye mabenchi,wamtupie macho!




Siku zote moyo ni giza nene, huwezi kujua yupi adui yako na yupi ni rafiki yako wa kweli,laiti kama Mungu angetoa uwezo wa kujua ndani ya moyo wa mtu kuna nini.Sidhani kama pangekalita duniani,George Charles hakuwa anajua lolote kuhusu mipango ya Lissa Mnzava ya kutaka kumtengenezea ajali na kumuua,alichokuwa anajua yeye ni kwamba mwanamke huyo aliletwa na Mungu duniani ili aje kuwa mkewe kumbe alikuwa akijidanganya mwenyewe!Urembo uliochanganyika na uzuri wake vilikuwa ni tofauti na roho yake ya kinyama,moyo wa mwanamke huyu ulitisha mno.
Mipango yake,ilikuwa ya kijangili na aliisuka na watu makini.Mbaya zaidi kila kilichoendelea Tanzania nyumbani kwa Ahmed alikijua,mpaka siku Yusrath anapigwa na Ahmed kisha wote kupelekwa hospitalini habari hizo alikuwa nazo mkononi,mfano angekuwa ni mwandishi wa habari basi gazeti lake lingeuza sio masihara.
Hayo yote bilionea George Charles hakuwa anajua sababu alipewa mapenzi mazito akaleweshwa kabisa akawa kama teja.Lissa Nzava hakutisha kwa uzuri wa usoni bali hata kitandani alikuwa ni moto wa kuotea mbali,hiyo ndio ilimfanya Bilionea George Charles apagawe zaidi.Siku hiyo wakiwa ndani ya Jakuzi yaani sinki kubwa lililokuwa na mapovu kwa ndani,alipagawishwa sio kitoto.Ili kumpumbaza, Lissa Nzava aliweka mishumaa pembeni huku kando yao kukiwa na glasi za ‘wine’Mikono ya George Charles, imewekwa huku na kule,Lissa kamkalia kwa juu.Hakuna hata mmoja kati yao, aliyekuwa na akili ya kuoga bali kilichotokea ilikuwa ni mambo ya wakubwa,Lissa alikinyonga kiuno ipasavyo hiyo ikamfanya na George ajibu mapigo pia!Akamvuta Lissa karibu yake wakaanza kunyonyana ndimi kwa fujo,kwa kasi ya umeme Lissa akapinduka na kushika ukingo wa sinki,George akaelewa nini anatakiwa kufanya akajisogeza karibu zaidi na kumlalia mgongoni akawa kama anamuemea kisogoni kwa kuwa walikuwa ndani ya maji,haikuwa rahisi kuona ikulu ilipo,akaingiza mkono ndani ya maji na kumshika mjusi vizuri mkono mwingine akitumia kuisaka ikulu ya mkewe,alivyoipata akaiweka na kuanza kukinyonga kiuno mambo ya kudamshi yakaanza.
“Beiibiii aaasshsssss,yeeees fuc*** me haaaaard yesss like thaaat aashss aaaah”
Haikujulikana kama mrembo huyu anafanya kusudi ama sauti inatoka bila kupenda,hiyo ilimfanya George azidi kupanda stimu,kasi ikazidi.Wakaendelea mpaka maji yakaanza kurukaruka na kudondoka chini,haikuchukua sekunde tano.Wote wakatulia kumaanisha wamemaliza!
“You are so sweet honey”
Lissa Mzava,akamwaga sifa huku macho yake yakiwa yamelegea bado,akambusu George mdomoni na kuchukua glasi ya wine iliyokuwa pembeni,akaiweka mdomoni na kuirudisha.Hata angekuwa mwanamme gani,asingeweza kugundua kwamba Lissa ana mipango mikali,hiyo ilimfanya George adate kabisa,akajikuta anawaza dakika hiyohiyo amkabidhi nyumba moja kama zawadi.
“Nahitaji kukupa zawadi baby”
“Zawadi gani?”
“Guess what?”
“I can’t,nambie tu”
“Sorry,nilikuwa sijawahi kukwambia hiki kitu Darling”
“Kitu gani?”
“Nina apartments Mbezi beach kule,nimepangisha watu”
“Baby,are you for real?Kwanini ulinificha?”
“Kichwa changu kina vitu vingi mpenzi”
“Mme wangu,mali zako zitakuja kupotea hivihivi.Inabidi kama mkeo nijue kila kitu”
“Consider it done my wife,cheers”
George Charles alisema akitabasamu,akachukua glasi wote wakagonganisha!Kwa furaha,wakapigana mabusu.Kwa kuwa walikuwa fungate, walipata muda mwingi kutembelea jiji hilo la Paris wakaenda Effel Tower,walivyotoka hapo wakaingia chatelet kwenye maduka makubwa ya nguo na humo hawakutoka mikono mitupu,kila walipoingia ilikuwa ni lazima wanunue vitu mbalimbali.
Kwenye swala hilo George hakuwa mwenye wasiwasi hata kidogo!Wiki mbili nzima, walikuwa katika jiji hilo wakifurahia maisha ya ndoa.
“Baby,tunarudi Tanzania kesho!Tunaenda kuishi kama mme na mke”
“Naelewa baby,hatimaye ndoto yangu imetimia sasa”
“Nakupenda sana,ndio maana nimekuchagua wewe!Nahitaji unizalie watoto wazuri”
“Hilo pigia mstari”
Ndoto za George Charles zilifananishwa naza Abunuasi,hakuna hata moja kati ya hilo ambalo lingetimia na Lissa Mnzava alihakikisha sababu mipango yake ilikuwa ni kumpoteza George kwenye sura ya dunia.Usiku wa siku hiyo taarifa za Yusrath akiwa Tanzania zilimfikia kwamba amehamishwa hospitalini kwa kuwa ana hali mbaya sana na kupelekwa hospitali ya Taifa, Muhimbili.
“Na Yule Mmewe?”
Akazidi kudadisi,simuni.
“Wanasubiri azinduke”
“Atapona kweli?”
“Tangu aletwe,hajazinduka kitandani”
“Kwani wewe upo wapi?”
“Mimi nipo kila sehemu lakini naona kuna maaskari wamefika hapa”
“Kufanya nini?”
“Wanasubiri huyu jamaa azinduke,ahojiwe”
“Watoto?”
“Wapo,lakini sasa hivi siwaoni”
“Fuatilia ujue walipo,ikiwezekana uanze nao!Mimi narudi kesho nitakupa mchoro kuhusu huyu bwana”
“Nakusikiliza wewe”
“Tutaongea kesho”
Simu ilikatwa na kumfanya Bwana Minja,atulie kidogo na kuendelea kusoma mazingira ya ndani ya hospitali hiyo ya Madona,ambapo ndani yake alikuwa amemtafuta daktari anayeshughulika na wagonjwa hao akijidai nayeye ni ndugu wa familia.
Hiyo ikawa rahisi kupata data mbalimbali.Hali ya Yusrath ilikuwa ni mbaya kupita kiasi,majeraha yalikuwa mengi kichwani hiyo ilifanya ubongo wake utingishike kidogo, kutokana na kipigo alichopokea.Mama yake hakutaka kukubali kabisa, ndiyo maana akaita polisi ili Ahmed ashtakiwe akiwa hapohapo kitandani,vurugu ilikuwa kubwa na hakukuwa na mmoja kati ya familia hizo mbili,aliyemuelewa mwenzake.Bifu lilikuwa kubwa Mama Yusrath aliropoka vitu vingi sana.
“Na nitawafunga wote,naanza nawewe mama mtu.Naenda Muhimbili sasa hivi”Mama akazidi kubwata huku akibubujikwa na machozi amevimba kama chura!
Ndani ya hospitali,kukagawanyika makundi mawili wengine huku wengine kule!
Hajrath alikuwa katikati,alikuwa akilia muda wote kama mtoto mdogo,akiomba kila dua Ahmed asife, mapenzi aliyokuwa nayo juu yake aliapia kwamba ni lazima angemfuata hukohuko hata ikibidi angekunywa hata sumu.
Moyo wake ulimuuma,taswira mbalimbali walivyokuwa chuoni Makumira zilijijenga ndani ya ubongo wake,akakumbuka siku aliyotaka kujiua kisa mwanamme huyo!Kumbukumbu zake zikarudi nyuma, siku chache zilizopita,walivyokutana benki na kupewa pesa ili akaikomboe nyumba yao.
“Kum..be ulikuwa unani..aga Ahmed..Please usi..ende bado naku..penda Ah..med wanguuu eeh Mungu”
Hajrath,akashindwa kuzuia hisia zake,akajikuta anaropoka akaishiwa nguvu na kuserereka na ukuta mpaka chini akitumia mgongo, hapo alilia kwa kwikwi mpaka Manesi, wakamuonea huruma.
Wakamsogelea na kumpiga piga begani wakimpa pole wakimfariji!Mama Yusrath alihakikisha jeshi la polisi linafanya kazi yake,ndiyo maana wakaanza kumuhoji mmoja baada ya mwingine.Kwa mara ya kwanza Hadima alionesha kugoma kabisa kutoa ushirikiano lakini baadaye alivyotishiwa na kupigwa mkwara,akawa hana jinsi.
“Ujue,utaingia jela badala yake!Usitupotezee muda,tuambie ilikuwaje?”
Askari huyo,akaweka uso wa mbuzi!Hakutaka tena kuuliza kwa upole hiyo ikafanya Hadima azungumze kila kitu kilichotokea 'A to Z'.
“Kwahiyo akachukuwa kisu na kuanza kuwatafuta watoto?”
“Ndio afande”
“Baada ya hapo?”
“Mama yake akatokea,mimi nilijua kaua tayari.Kumbe amedondoka chini”
“Unamfahamu huyo George?”
“Mimi simfahamu,ndio mara ya kwanza kumuona.Tena kwenye gazeti”
“Hujawahi kumuona hapo nyumbani?”
“Hapana sijawahi”
Sakata la George kuzaaa na Yusrath halikuwa siri tena,kila kitu kilikuwa wazi sababu askari walifanya uchunguzi wao na kugundua chanzo cha ugomvi huo lilikuwa ni gazeti na nyuma ya yote kuna wivu wa mapenzi.
Kilichokuwa kinatafutwa hapo,zilikuwa ni namba za Bilionea George Charles ili ahojiwe lakini haikuwa kazi rahisi kumpata kwani alikuwa bado nje ya nchi.
“Alishawahi kumpiga kipindi cha nyuma?”
“Sijui,sina uhakika ninalala mapema”
Hadima,akadanganya alishaelewa kesi hiyo imemlalia Ahmed, hivyo kuendelea kumkandamiza ingezidisha ukali.
“Huna uhakika kivipi?Wakati Mama alisema,keshawahi kupigwa mpaka akafungiwa stoo?”
“Hapana kusema ukweli,sijawai kuona hiko kitu.Labda zamani,mimi sikuwepo”
“Ulisema unaitwa nani?”
“Hadima”
“Kabila gani?”
“Mnyamwezi”
“Sawa,tutakutafuta kwa ajili ya mahojiano zaidi”
Hapo Hadima hakujibu chochote kile,akabaki analia kwa kwikwi.

*****
Hali ya Ahmed,haikuleta faraja hata kidogo.Mbaya zaidi alikuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi yaani ICU.Huko hakuweza kuvuta pumzi bila ya msada wa mashine!Madaktari hawakuwa na majibu ya uhakika yaliyoeleweka lakini walitoa ufafanuzi wa juujuu kwamba kuna mshipa mmoja wa kichwani umepata itlafu kutokana na hasira na ‘stress’ nyingi.Hiyo ndiyo ilimfanya mpaka alale kitandani hapo, sababu ya kukorofisha mpaka mfumo mzima wa fahamu.Mama Ahmed alilia sana kwani ndiye mtoto aliyekuwa anamtegemea muda wote. Ngowi,alikuwa na kitambaa usoni.Alikuwa akilia chini chini,akimuombea swaiba wake.Alivyomuona Hajrath eneo hilo,akamuangalia kwa umakini hakuelewa kama alimfananisha ama duniani wawili wawili,hata hivyo haukuwa muda sahihi wa kuanza kuulizana wewe ni nani?Umetokea wapi?Alichokifanya Ngowi ni kumfuata Dokta moja kwa moja, ofisini kwake.
“Dokta,sisi wote wanaume.Ndiyo maana nimekufuata mwenyewe private!Nini kinaendelea?Kuna matumaini,ongea ukweli”
Benjamin Ngowi,alitaka kujua!Japokuwa hakuwa tayari kupokea majibu kutoka kwa daktari kuhusu hali ya rafiki yake kipenzi.
“Kuna mawili hapa,ngoja nikwambie ukweli”
“Yapi?”
“Mgonjwa wenu anaweza kupalalaizi ama tukampoteza kabisa,huo ndio ukweli.Maana mshipa uliopasuka ndio unatoa mawasiliano kwenye uti wa mgongo!Vinginevyo tuombe sana Mungu”
Zilikuwa ni habari mbaya tena za kutisha kwa Benjamin Ngowi,moyo ukamuuma ajabu.Kila kilichotokea alitamani kiwe ndoto ashtuke lakini haikuwa hivyo,kila kitu kilikuwa kweli kabisa!
“Kwanini imekuwa hivyo?”
“Mara nyingi hali hiyo hutokea mtu akiwa na stress nyingi sana.Ama hasira!Mtu wa namna hiyo tunamshauri apende sana kujichanganya na watu”
“Mungu wangu”
“Lakini atapona?”
Ngowi,akarudia kuuliza tena swali hilohilo.Akitamani dokta atengue kauli yake kwamba kuna kufa ama kupalalaizi.
“Hakuna anayetaka kusikia habari mbaya,lakini nitajitahidi kadri ya uwezo wangu.Pia,muombe sana Mungu”
Ngowi,akajiongeza akasimama na kutoka nje akiwa na macho mekundu.Jambo hilo lilishuhudiwa na Hajrath aliyekuwa ukutani analia kama mtoto mdogo!

******
Hospitali ilikuwa kimya na usiku ulikuwa mwingi,paka walilia sio masihara wengine walipiga kelele kama za watoto wachanga!Hiyo ilimuogopesha sana Hajrath aliyekuwa mlango wa ICU chumba alicholazwa Ahmed,hakutaka kubanduka.Ghafla akaanza kuhisi kama ubaridi mkali unampuliza shingoni.
“Nyaaau nyaauuuu nyaaaau”
Kelele za paka zikazidi,hofu ikamtanda!Akatizama huku na kule na kumuona Nesi mmoja aliyekuwa anamtibu Ahmed ameshika trei lenye dawa kwa juu,anatembea kuelekea chumba hiko alichokuwa Ahmed.Akafungua mlango!Hajrath alivyotaka kuingia akazuiwa kama taratibu zilivyo.
“Doktaaaaaaaa”
Kelele za nesi kutokea ndani ya chumba alicholazwa Ahmed zilimfanya Hajrath apigwe na mshangao,akamuona nesi katoka nje kwa kasi sekunde mbili baadaye akarudi na dokta.Wakaingia ndani,hapo walisahau kufunga mlango akapata mwanya wa kuona kila kitu.
Akamuona dokta anavyotoa kifaa cha kupimia mapigo ya moyo kwani mashine ya hewa ya oksijeni, ilikuwa ikitoa mlio usioeleweka.Hajrath akaganda kama barafu,anatizama kila kitu kinachoendelea, akahisi kama miguu yake inaishiwa nguvu tena imekufa ganzi.
“He’s gone,mfunike.Kawaambie ndugu zake,andika kwenye dirth certificate amefariki saa saba na nusu usiku”
Maneno hayo,yalipenya moja kwa moja kwenye pina za masikio ya Hajrath,akamshuhudia daktari anamfunika Ahmed usoni, kumaanisha kwamba tayari AMEAGA DUNIA!




“A..hmed usiwauwe wana..ngu….Ahmed,niue mimi tu.Usiwauwe wanangu.Ahmed,Ahmed unaniumiza.Nakufaaaa,nakufaa.Utaniuaaa Ah..med”
Tangu siku ya tano,yupo kitandani hajitambui ulikuwa ni kama muujiza mkubwa sana kwani hata madaktari waliokuwa katika hospitali hiyo ya Taifa wanamuuguza,walikata tamaa kabisa,kitendo cha Yusrath kuzungumza kwa mbali akitamka maneno hayo yalirudisha faraja kubwa sana kwao!Madaktari wakaanza kupigana vikumbo,wakihangaika huku na kule.
“Ahmed,naku..fa unaniumizaaa”
Sauti ya Yusrath ilisikika kwa mbali,bado taswira ya Ahmed akimpiga vibaya sana ilijijenga kichwani kwake,tukio baya la kupigwa kama mbwa koko lilimtesa bado.
Akajiona yupo chini, pembeni kuna kitanda wapo chumbani anapigwa mikanda kichwani na makofi huku Ahmed akiwa ameshika kisu kikali mkononi,anataka kwenda kuwauwa watoto, jambo hilo likamfanya amshike mguu asijaribu kufanya hivyo,haikueleweka ilikuwa ni ndoto ama tayari ameshaharibika kisaikolojia.Dokta Bomani,akaingia kwa haraka ili amkague mgonjwa wake ana tatizo gani.Cha ajabu sentensi za Yusrath zilikuwa ni hizohizo tu kwamba Ahmed asimuue.
Hilo halikuwa tatizo kwa dokta Bomani,mwenye taaluma za kucheza na binadamu wenzake.Purukushani za madaktari zilimfanya Mama Yusrath nayeye asipitwe,akazama ndani japokuwa walijitahidi kumzuia lakini ilishindikana.
“Mama kaa nje”
“Ni binti yangu,tafadhali naomba kumuona”
Mama Yusrath akajikaza kuongea huku akijifuta machozi,dalili zilionesha kuna habari mbaya sana kwani madaktari waligongana vikumbo mlangoni,Mama akapata mwanya na kuingia wodini ambapo huko aliangua kilio na kwa wakati mmoja alimshukuru Mungu kwani Yusrath alianza kuongea tofauti na mara ya kwanza!
Madaktari walivyofika wakamtoa nje ili waendelee na taratibu zao,nusu saa baadaye ndipo akaruhusiwa kuingia ili amuone mwanaye!Kitandani,alilala Yusrath mtungi wa hewa ulitolewa tayari,hiyo ilimaasha Mungu katenda miujiza na hali yake ina nafuu,kilichomfanya aumie ni jinsi Yusrath alivyodhoofika kiafya,Yusrath alipungua uzito mwili wake ulikongoroka kwa kiasi cha kutosha.
“Yus..rath”
Mama akamuita mwana.
“Ahme..d usiniue.Usiwauwe wanangu,Ah..med”
“Mimi mama yako”
“Ahm..ed,Mamaaa”
“Ndio,mimi mama yako”
Hapo Yusrath alitulia kidogo,akamtizama mama yake kwa sekunde kadhaa kisha kurudisha kichwa chake ukutani,hiyo ilimaanisha hakutaka kuzungumza neno lolote lile.
“Yusrath,unaendeleaje?”
“Naendelea vizuri,wanangu wako wapi?”
“Wapo nyumbani”
“Mme wangu,yuko wapi?”
Swali hilo lilimfanya Mama huyu,atulie kidogo na kumtizama Mwanaye mara mbilimbili, hakuelewa kama ana wazimu ama dishi limecheza!
“Nani Ahmed?”
Haikujulikana kama alisikia vibaya ama hakusikia swali vizuri.
“Ndio Mme wangu Ahmed”
“Yusrath,unataka kujua ni wapi Ahmed alipo?Upo sawasawa?”
“Ndio,nataka kujua.Nahitaji kumuomba msamahaa”
“Wewe umuombe Msamahaa ama yeye aombe?Tena nisikusikie,funga bakuli lako hilo.Na kwa taarifa yako,Ahmed lazima afungwe.Nachokuomba useme kila kitu,askari watakuja hapa”
“Mama lakini mi…”
“Hakuna cha lakini,nyamaza mimi na Ahmed nani zaidi?Nani bora?”
“Naomba nikuulize kitu Mama”
“Kitu gani?”
“Yule ni mme wangu lakini,mimi nikifa hawatosema nilimuacha Mama yangu duniani.Watasema marehemu kaacha Mme na watoto al..”
“Nitolee upumbavu wako,nishasema.Ulikaa humu tumboni miezi tisa kama ndiyo hivyo,Ahmed lazima afungwe”
Mama Yusrath alizungumza kwa ukali,hakujali yupo mahali gani.Alichotaka yeye ni jambo moja tu,Ahmed afungwe gerezani ili amfunze adabu, hilo lilikuwa mbioni kufanyika kwani walivyokuwa wanaongea kwa wakati huo makachero kutoka jeshi la polisi walikuwa nje wanasubiri hali ya Yusrath iwe sawa ili wakamilishe ushahidi wao.
Jambo la kumfunga Ahmed ama aachiwe huru lilikuwa mikononi mwa Yusrath,kitendo cha kuzungumza ukweli kilimaanisha Ahmed atupwe gerezani kwa kosa la kutaka kuuwa,kuna vitu vingi sana vilipita kichwani kwake akapata dakika mbili nzima kufikiria upumbavu wote aliokuwa akifanya nyuma,akakiri kwamba yeye ndiye mkandarasi wa kila kitu kutokea sababu ukweli ni kwamba Ahmed alikuwa akilea watoto sio wake,Yusrath alilia sana alihisi kujuta na kutamani arudishe siku nyuma, arekebishe kila kitu kilichotokea lakini jambo hilo lisingewezekana hata kidogo!Haukuwa utani kuhusu mpango wa Mama yake,alivyotoka nje askari wakapewa taarifa juu ya hali ya Yusrath,walichokifanya ni kuonana na daktari kwanza ili wapewe ruksa, hilo likafanyika na makachero hao wakaingia wakiwa na nguo za kiraia.
“Habari yako binti”
Afande mmoja akasalimia,shati jeupe alilovaa na suruali ya kitambaa iliyopigwa pasi vizuri ikaanyooka, ungedhani wenda ni afsa mikopo.Yusrath,alikuwa kitandani bado,anahisi maumivu ya kichwa na mgongo!
“Salama”
“Mimi naitwa Afande John Mhina,unaendeleaje?”
Afande John Mhina,akauliza kwa upole ili kumtoa wasiwasi Yusrath.
“Naendelea vizuri”
“Pole na matatizo”
“Ahsante”
“Ahmed ni nani yako?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa afande,kabla ya Yusrath kujibu akamtizama Mama yake, aliyekuwa pembeni kasimama wima.
“Ni mme wangu wa ndoa”
“Mumeo?”
“Ndio”
“Mna watoto?”
Swali hilo lilimfanya Yusrath,asijibu moyo ulimuuma sababu watoto ndio chanzo cha yeye kuwepo kitandani.
“Anyway,tuachane na hilo swali.Tupo hapa kwa ajili ya kukusaidia.Embu tuambie siku hiyo ilikuaje?”
“Siku gani?”
“Mmeo akakupiga namna hiyo?”
“Sijawahi kupigwa na mme wangu,nani amewaambia?”
Afande John Mhina,ikabidi ageuke na kumtizama Mama Yusrath.
“Yusrath,zungumza ukweli Mwanangu”
Mama akaingilia kati na kusema kwa uchungu,hakuwa tayari kuona ana umbuka mbele ya jeshi la polisi, wakati alisema kwamba binti yake alipigwa mno!
“Mama,aliyekwambia nilipigwa ni nani?Sikupigwa,naomba nipumzike kichwa kinaniuma”
Yusrath akagoma katukatu kuzungumza kitu chochote,akageukia upande wa pili na kuanza kulia machozi.
Hakuwa tayari kumfunga Ahmed na ndiyo maana alimtetea kufa kupona akimkingia kifua,hiyo ilifanya maaskari kuondoka eneo hilo.
Mama Yusrath alikasirika ajabu na kumsogelea karibu.
“Kuanzia leo,tafuta mama mwingine.Mimi sio Mama yako!Tafuta Mama yako wa kumz…”
“Mama na..mpenda Mm..e wangu bado,hata kama kanipiga.Kumbuka chanzo ni Mimiii mwenyewe,watoto sio wake ni kweli,nastahili adhabu ndio.Hata kama angeniua ni saw…a tu.Siwezi siwe..zi siwe..zi Mama”
Machozi yalimtoka kama maji,yakatiririka mashavuni na kulowanisha mashuka.Yusrath alilia mpaka basi tena mbaya zaidi alizungumza kwa kufoka,hasira zake zilimpanda mpaka kiwango cha juu mpaka Kamasi nyepesi zikaanza kumtoka puani.Ilichukuwa muda sana kumtuliza,akatulia na kulala!

*******
Saa mbili ya usiku alivyozinduka,baada ya mama yake kuzungumza naye kwa urefu na mapana akimshauri na kumueleza madhara ya kumuacha Ahmed huru,ndipo akabadili mawazo.
“Ahmed,atakuuwa.Niamini nachokwambia,hivyo kwa usalama wako.Ongea ukweli ili ubaki kuwa huru!Hii situation ni kubwa,hatoshindwa kukuua nayeye akajiua.Please Yusrath nimekuzaaa wewe peke yako,nakuomba”
Mama akaongea kwa busara,akitumia kila aina ya sera na siasa zote!Akapata muda wa kumueleza jinsi alivyomzaa kwa tabu sana kipindi wapo Geita,changamoto alizopitia na ndugu zake.
“Nilikuzaa kwa tabu sana mwanangu,sikupenda mimi kukuzaa peke yako.Lakini niliambiwa sina uwezo wa kuzaa hospitali,nilihangaika sana mpaka kwa waganga lakini sikufanikiwa kushika mimba.Mawifi,walininyanyasa,kuna kipindi hata baba yako,alikuwa upande wao!Niliteseka mno!Mpaka nimekuzaa naona kama ni miujiza,nakupenda sana mwanangu,nipo tayari kupambana na mtu yoyote Yule atakayekudhuru”
Yalikuwa ni maneno mazito na siri kubwa sana kupewa Yusrath,hata yeye alishangaa mno!Kwa mara ya kwanza mama yake kumuelezea vitu kama hivyo vikubwa.
Kidogo Yusrath akawa amelainika,dakika kumi baadaye,wakaingia makachero mkononi wakiwa na vinasa sauti.
“Naona hali yako sasa afadhali?”
Afande John,akauliza akionesha tabasamu.
“Ndio”
“Aya,tuambie”
Yusrath akavuta pumzi ndefu,akamtizama Mama yake na kumuangalia Afande John!Akaanza kutiririka kila kitu kilichotokea,tabia za Ahmed kumpiga na kumnyanyasa,akatia chumvi na kuongeza kwamba Ahmed hakuwa anaacha pesa za matumizi mbaya zaidi hata yeye wakati mwingine hulala njaa siku mbili.
“Kuna kipindi,alishawahi kunifungia bafuni siku nzima.Sikula kitu siku hiyo,sitoweza kusahau”
“Kisa nini?”
“Mpaka leo,jibu analonipa ni hanipendi.Mambo mengine niya aibu kuyazungumza najisikia uchungu sana”
Yusrath alizungumza maneno ya uongo akiyapigilia msumari wa nchi sita,nyuma ya maneno hayo kulikuwa na shinikizo la Mama yake!

******
Japokuwa,aliwatendea vibaya kipindi wanasoma chuo cha Makumira lakini haikumaanisha amchukie.Amney,alishikwa na huruma kwani Necka Golden alichoka ana ukurutu na kukondeana!Mwili wake na ngozi yake laini ikawa ngumu sana kama mamba.Siku hiyo Amney alivyomuona Ubungo darajani,akamchukua wakanyoosha mpaka kwenye duka la nguo.Huko alimnunulia baadhi ya nguo,zile za zamani chafu akamwambia azitupe kwani zilikuwa na jasho na zinanuka mikojo, sababu alitoka kituo cha polisi.
“Dada samahani,hapa hakuna bafu?”
Amney akauliza,kumnunulia nguo Necka Golden peke yake isingetosha.
“Bafu,liko kwa nyuma lakini la kulipia”
“Hakuna shida”
Baada ya maelekezo hayo,wakatafuta bafu Necka akalipiwa na kuoga vizuri kisha kuvalishwa nguo mpya,wakatoka na kwenda kununua chakula kwenye mgahawa uliokuwa pembezoni.
“Ahsante Amney,sijui nikushukuru vipi?”
Ilikuwa ni tofauti na kipindi alivyokuwa chuoni Makumira,Amney alikuwa mpana wa maneno na katika wasichana waliomchukia Necka Golden yeye ndiye alikuwa namba moja,leo hii alishangaa mambo kubadilika ghafla.
“Usijali Necka,kula chakula.Kuna kitu nimejifunza kwenye hii dunia,tuishi kwa upendo!Nilishakusamehee,kwanza ule ulikuwa ni utoto”
“Ahsante sana”
Njaa aliyokuwa nayo Necka Golden ilitisha,hiyo ikamfanya ale kwa kasi ya kimondo akaomba aongezewe sahani nyingine.
“Taratibu utapaliwa”
Amney akasema,huku akinyonya mrija wa juisi ya machungwa.Mkono mmoja ameshika simu kubwa anachati,akatoka pembeni kidogo ili kuongea na simu.
“Ndio baby ni rafiki yangu…Tutaishi naye hapo..Hakuna shida kwani si kuna vyumba viwili.Sawa sikatai,atakaa muda mfupi tuu….Usiwe hivyo Darling,nimekwambia ni rafiki yangu…Sio mtu baki,najua naelewe sijakwambia mapema…Nemesi Nemesi Mme wangu usiwe hivyo….Sawa nimekuelewa.Atakaa siku mbili ataondoka please nakuomba.Okay baby ilove you, nipo hapa Ubungo”
Amney alikuwa simuni anabishana na mtu wa upande wa pili,ambaye kwa harakaharaka alikuwa ni Mpenzi wake,hakukuwa na maelewano mazuri ndiyo maana alikunja sura na kurudi kwenye kiti akiwa kapoteza ‘appetite’ ya kunywa juisi.
“Vipi Amney?”
Necka Golden akauliza.
“Kuna mtu keshaniharibia siku”
“Nani?”
“Mambo tu ya ofisini,maliza chakula.Au wakuongeze,inabidi tuondoke tuwahi”
“Sawa namalizia”
Walivyomaliza kula,Amney akalipa na safari ya kwenda stendi ya basi kuanza!

****
Baada ya kumaliza chuo na kupata kazi,akaamua kuachana na wazazi wake na kwenda kupanga maeneo ya Magomeni mapipa,usumbufu kwa wanaume ulikuwa mwingi kutokana na uzuri na upole aliokuwa nao!Lakini katika wanaume wote ambao waliomtokea na kumuimbisha Nassib Nemesi akaibuka kinara ikawa kama bahati kwake kwani mwanamme huyo alijatambua na alikuwa mwenye akili za maisha hana utoto!Akaamini kwamba wataendana,ndani ya mwaka mmoja wakaamua kuhama na kwenda kupanga Magomeni.
Huko walipata nyumba nzuri yenye seble na vyumba viwili,kwa Amney alihesabia ni hatua kubwa sana katika maisha yake.Akaamini katika kufanya kazi,ratiba yake ilijulikana siku zote kutoka asubuhi sana na kurudi usiku saa moja ama mbili na akishapika na kula,anaingia kitandani kulala.
Hakuna mtu aliyebisha kwamba alikuwa ni msichana mchapakazi mwenye akili ya maisha na mwenye maendeleo lakini kilichokuwa kinamkwaza siku zote ni tabia ya Nemesi kumlazimisha kufanya ngono wakati akiwa amechoka usiku,jambo hilo likawa kero kwake lakini alilivumilia tu.
Amney hakuwa tayari kufanya tendo hilo akiwa amechoka sababu hata yeye alitaka kulifurahia na akilala hakutaka kusumbuliwa.Hilo halikuwa tatizo kubwa kwa Nemesi,alivumilia kwani ndege alikuwa ni wake haikuwa na haja ya kushika manati, mbali na hapo hakutaka kuchepuka hata siku moja,akielewa kwamba Amney ni msichana mwenye msimamo na kumpata kama huyo ilikuwa ni ndoto, endapo angempoteza!
Siku hiyo akiwa seblen kaweka miguu juu,mlango uligongwa na Amney aliingia ndani akiwa na mgeni pembeni, ambaye muda mfupi walitoka kugombana kwani ugeni huo ulikuwa wa ghafla sana!
“Karibu baby”
Nemesi,alimkaribisha na kumtizama mgeni huyo machoni, akarudisha macho kwa Amney.
“Baby,huyu ndiye Yule rafiki yangu niliyekwambia.Ana matatizo”
“Oooh karibu,jisikie upo nyumbani”
“Anaitwa Necka Golden,Necka huyu ni mme wangu.Anaitwa Nassib”
“Nafurahi kukufahamu shemeji”
Utambulisho ulikuwa mfupi,Amney akaenda na Necka Golden mpaka chumbani akimuelekeza kila kitu kuanzia bafu mpaka jiko lilipo.
Chumba alichotakiwa kulala Necka hakikuwa na bafu hiyo ilimaanisha ni lazima apite kwenye kordo ndipo aingie bafuni,hilo halikuwa na shida.
“Baby,ngoja nikupikie basi chap chap.Najua una njaa,mpaka umekonda ghafla”
Amney akasema kwa kuwa mpenzi wake alikua ni rafiki yake, maneno hayo yalikuwa ya kawaida wakawa kama wanataniana.
“Nina ubao baby hapa,kinoma noma yaani.Nilitaka ninunue msosi sema najua ungeni mind”
“Ndio kwanini ule nje?Wakati mimi nipo”
“Nimekuja na Season yako ile”
“Ipi baby?”
“If loving you is wrong”
“Aaaaah,usitake niunguze.Ngoja nimalize kupika nije tuangalie wote”
Walikuwa ni zaidi ya wapenzi ama ndugu,muda wote walikuwa wenye furaha.Amney alivyomaliza kupika,akatenga seblen na Nassib akaanza kula.
“Huyo rafiki yako,yeye?”
“Keshakula”
Kilichofuata hapo,kila mtu akatupa macho yake kwenye luninga wakaaanza kuangalia tamthilia hiyo,ambayo ilitamba sana na ilikuwa ndiyo habari ya mjini.
Kwa kuwa walizoea kuangalia pamoja wakiwa wamekumbatiana yaani kulaliana,wakafanya hivyo.Hata Nassibu alivyomaliza kula wakaendelea kukumbatiana kimahaba huku wakishikana taratibu.Mkono wa Amney,ukaanza kupita taratibu na kubarizi kwenye tango la Nassib,ambapo lilianza kusimama dede.Nassib nayeye hakutaka kuwa zoba,kwa kuwa ilikuwa ni kawaida nayeye akaanza mbwembwe,mkono wake mmoja akaupitisha tumboni mwa Amney,akaupandisha mpaka juu kabisa!Akaanza kupapasa kifua hususani chuchu,hiyo ilimfanya Amney ajigeuze mwenyewe na kumtizama Nassib kimahaba,macho tayari yalikuwa mekundu yamelegea kama kala kungu.
“Baby,kuna mgeni”
“Kwahiyo?Twende chumbani?”
“Lakini keshalala”
Amney akajibu mwenyewe akimwambia Nassib kwa sauti ya chini,alichokifanya ni kumtoa nyoka wa Nassib aliyekuwa mkubwa na mnene,akapiga magoti kidogo na kumbugia mdomoni akimlamba!Hiyo ilimfanya Nassib ajipinde kidogo na aupenyeze mkono wake,kwenye ikulu ambapo alikumbana na nyasi chache kiasi akaanza kupima oil.
“Aaaaashiii aaaaaah”
Amney,akaguna sababu alishikwa penyewe akazidi kupapasa kichwa cha jusi kafiri.Hiyo ilimfanya Nassib nayeye aheme ki utu uzima,walizidi kufanya mchezo huo seblen, bila kujua Necka Golden anawachungulia akiwa chumbani, kupitia kitundu cha kitasa!


Damu yake ilimwenda mbio,mwili ukaanza kumsisimka ajabu.Akatamani yeye ndiye awe Amney lakini hilo lisingeweza kutokea hata kidogo.Alivyojaribu kutoka ili asichungulie na amshinde shetani akajikuta akishindwa,bado ameganda.Akiwashuhudia Amney na Nemesi wanavuana nguo, hapo ndipo akashindwa kuzuia hisia zake,taratibu akaanza kujitomasa kifua na kuingiza mkono ndani ya ikulu yake!Hawakujua wala kuwaza kwamba Necka Golden anawapiga chabo,akili zao zote ziliruka na waliwaza ngono,Nemesi hakujiweza tena, alichokifanya ni kumpindua Amney na kumuweka sawa kwenye kochi,akaitanua miguu yake huku na kule akaingia katikati na kutoa ulimi kisha kuanza kupiga deki bahari,hapo ndipo Amney alipoanza kutoa mihemo na miguno ya ndani kwa ndani.
Waliendelea kushikana na kutomasana kwa takribani dakika kumi nzima,ndipo mchezo huo ukaanza mara moja.Mguu mmoja wa kushoto wa Amney ukawekwa begani,Nemesi akaseti mitambo na kuingia kwenye ikulu,akaanza kupanda juu na kushuka huku akikizungusha kiuno chake taratibu.
Hiyo ilimfanya Amney nayeye anyonge kiuno asteaste ili waende sawa.Hawakukaa sana, wakabinuka tena na kubadilisha mkao,mambo yakaendelea mpaka ilipofika saa saba ya usiku, ndipo kila mtu akachukua nguo zake na kuelekea chumbani kulala.
Isingekuwa Necka Golden kuwepo siku hiyo wangelala seblen mpaka kukuche kama wanavyofanya siku zote wakifanya ngono kwenye masofa! Wa kwanza kuamka,siku hiyo na kutoka kitandani alikuwa ni Necka Golden,akavaa kanga na kutoka ambapo alinyoosha mpaka bafuni.Kabla ya kuoga picha ya usiku wa jana ikaanza kumjia,Amney alivyokuwa anafaidi akifanya ngono,akili yake ikahama akaanza kujitomasa tena ili akidhi haja yake.Akitumia mikono yake kujishika kifua na ikulu akafanikiwa kujifikisha mshindo, ndipo akaanza kuoga.Alivyomaliza,akarudi chumbani akavaa nguo na kutembea mpaka jikoni ambapo huko alianza kuandaa chai.Ilikuwa ni lazima ajiongeze kwa kuwa alikuwa kwa rafiki yake,hivyo kukaa chumbani na kubweteka bila kusaidia kazi isingekuwa vizuri,hivyo ndivyo alivyofundishwa na wazazi wake.
“Ushaamka kumbe?”
Sauti ya Amney kutokea nyuma yake ilimshtua,akageuka na kutabasamu.
“Muda mrefu sana”
“Sasa si ungeacha nikuandalie chai,wewe ni mgeni”
“Acha tu,jana ulinionesha”
“Necka…”
“Amney,niache niandae.Majani ya chai yako wapi?”
“Hapo chini”
Necka Golden,akaendelea na jambo aliloanza,akaandaa chai vizuri na kutenga vikombe mezani, akimuacha Amney anajiandaa ili aende kazini.
Saa 2;45 ndipo wakatoka chumbani Amney pamoja na Nemesi, wakiwa tayari wamejiandaa,wakanyoosha mpaka meza ndogo ya chakula.Haikuwa meza kubwa sana!Ilikuwa ndogo ya wastani yenye viti vinne,kwa harakaharaka ungejua kabisa wanaoishi humo ndio kwanza wameanza maisha!Baada ya kunywa na kumaliza,wakaaga na kuondoka zao wakimuacha Necka Golden peke yake nyumbani.
Hiyo ndio ilikuwa ratiba yao kila kukicha na hakuweza kutabiri muda muafaka wa wao kurudi!Mpaka anakaa siku ya tatu hakuweza kugundua wanafanya kazi gani isitoshe nani anawahi kutoka kazini.Kwani wakati mwingine Nemesi anawahi Amney anachelewa ama Amney anawahi kufika Nemesi anachelewa.Waliishi na Necka, alipendwa na Amney akamchukulia kama dada yake ama ndugu yake na wakati mwingine alimletea zawadi mbalimbali kama nguo na viatu.Hiyo ilimfanya Necka Golden,afurahi sana akajisikia amani mno.Kutokana na matunzo pamoja na furaha aliyokuwa nayo, taratibu mwili wake ukaanza kujijenga vizuri, ngozi yake ikaanza kurudi kama awali,ule ukurutu ukapotea.Kiuno chake,kikabinuka kisawasawa kama kipindi cha nyuma!Mashavu yakaanza kurudi,kwa mwanamme yoyote Yule atakayemuangalia ilikuwa ni lazima afikirie ngono sababu Necka alivutia na alikaa kingono zaidi, kifupi alitamanisha mno!
Licha ya kusumbuliwa na wanaume waliokuwa mtaani hapo kila alipotoka lakini hakuwa tayari kuwakubalia,mawazo yake yote yalikuwa kwa Ahmed tu.Akatamani siku moja aje kuwa mkewe wa maisha,bado ndoto yake ilikuwa ni ileile na haikubadilika.
Ndani ya wiki moja kuishi na Amney pamoja na Nemesi,akajikuta amewazoea kabisa tofauti na mwanzo alivyokuwa mwenye aibu.Hiyo ikafanya awe ana uwezo hata wa kukaa seblen mwenyewe na kuangalia t.v!
“Necka”
Siku hiyo akiwa anaangalia luninga mchana, sauti ya Nemesi ikamshtua.
“ABEE SHEMEJI”
“Ushakula?”
“Bado lakini tayari nimepika”
“Sasa si ukale,unasubiri nini?”
“Sisikii njaa”
Swala la kurudi mchana kwa Nemesi halikumshtua sana Necka kwani wakati mwingine Nemesi hurudi,anakula kisha kurejea tena kazini.Hivyo ndivyo ilivyokuwa pia siku hiyo.Akala zake na kuondoka kama kawaida, akimuacha Necka Golden bize na t.v!
Sio siri,kuna sinema alikuwa anaangalia ikamfanya apandwe na hisia za ghafla sana,akatamani awepo na mwanamme kitandani ama popote pale afanye naye mapenzi.Akawehuka,akatamani mwanamme yoyote aliyekuwa nje amuite ili akate kiu yake lakini hakutaka kufanya hivyo sababu bado aliuthamini mwili wake,alichokifanya ni kukimbilia bafuni na kuanza kujitomasa kama siku zote.Lakini siku hiyo, ikaonekana kuwa bure kabisa kwani baada ya dakika tano,hisia zikampanda upya.Akabandika maji ya moto na kuoga ili azishushe lakini wapi,kila kitu kikagoma.Akabaki ana hangaika mwenyewe ndani, mara atoke mara arudi.Ni miaka mingi sana,hakuwahi kukutana kimwili na mwanamme kukaa sana jela kulimfanya apate ugumu na uchu wa kufanya ngono!Hiyo ilimfanya mpaka usiku wa siku hiyo aote ndoto nyevu kwamba anafanya mapenzi,asubuhi alivyokurupuka akawa amejichafua!
Akajisikia aibu sana,bado hali hiyo ilimsumbua sana,akajitahidi kupambana nayo na kuyatoa mawazo ya ngono kichwani kwake lakini ikawa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu yasagike!

******
Ratiba ya Nemesi kuanzia Jumamosi zilijulikana kwamba anashinda nyumbani kwani hakuwa anaenda popote pale,siku hiyo Ijumaa akaamua kupita kwenye duka la sinema akanunua nyingi ili Jumamosi akeshe nazo siku nzima.Hatimaye ilivyofika Jumamosi,asubuhi baada ya kunywa chai akapitiliza mpaka seblen!Siku hiyo walibaki wawili tu nyumbani,ghafla pepo la ngono likamvaa Necka, shetani nayeye akaanza kumnyemelea ili ampitie.Kwa kuwa alisikia sauti kutoka sebleni ya tv akajua ni lazima Nemesi anaangalia movie,akachukua kanga moja tu na kuivaa mwilini juu akavaa Tshirt mbaya zaidi ndani hakuvaa chupi.
Alifanya hivyo makusudi kwani alijua alichokuwa anaenda kukifanya,mtego aliokuwa anataka kuutega akaamini ni lazima ungemnasa Nemesi sababu alijua hata kwa mwanamme gani,asingeweza kuruka.Ghafla akasahau fadhila za Amney,hakuweza kukumbuka tena alipotoka.Kilichompelekesha kwa wakati huo zilikuwa ni hisia tu.Akatoka mpaka seblen,alichokifanya kwanza ni kutoa vyombo mezani ili kuzuga.
“Za asubuhi shemeji”
Necka akasalimia kwa sauti ya puani.
“Salama tu,sijui wewe?”
“Mimi niko poa,naona umeamkia kwenye movie leo!Nije tuangalie wote?”
Necka Golden hakutaka kukurupuka japokuwa alikuwa mwenye haraka lakini alitaka kuucheza mchezo huo,kiintelijensia.Msichana huyu alikuwa ana akili nyingi,alivyomaliza kuweka vyombo jikoni akapita kwa makusudi mbele ya Nemesi.Kisha kukaa kushoto kwake!
“Movie hii inaitwaje shemeji?”
“Temptation”
“Nani kacheza?”
“Tyller Perry, nadhani”
“Ni nzuri?”
“Ndo kwanza imeanza lakini inaelekea ni nzuri”
“Hua unapenda movie za aina gani?”
Kwa Nemesi ilikuwa kero kubwa sana,huwa hapendi kubugudhiwa akiwa katika starehe kama hiyo na mara nyingi hugombana hata na Amney.Alichokifanya ni kuchukua rimoti na kuweka ‘pause’ movie ikaganda.
“Ulikuwa unasemaaa?”
“Huwa unapenda movie za aina gani?”
“Zote huwa naangalia,lakini hua napenda sana Action.Donnie yen ndio namkubali.Love story pia napenda!Inshort movie za aina yoyote ile mimi nacheki tu ilimradi iwe nzuri”
Nemesi alivyojibu akachukua rimoti na kubonyeza ‘play’ akatupa macho yake mbele bila kujua akili ya Necka inawaza nini,alichokifanya msichana huyo ni taratibu kujivuta kwake akauchukua mkono wake na kuanza kumpapasa Nemesi shingoni,hiyo ilimfanya Nemesi ashtuke kidogo akasogea pembeni Necka akamsogelea pia na kuendelea kumpapasa shingoni.
“Kuna kipele hapa shemeji”
“Nitakitoa”
Mapigo ya moyo ya Necka Golden yalidunda kwa uwoga,hakuwa ana uhakika kama zoezi lake litafanya kazi lakini alipiga moyo konde, akiamini kwamba hakuna mkate mgumu mbele ya chai,akaendelea na zoezi lake.Licha ya yote ilikuwa ni tofauti na alivyowaza kwani Nemesi alimkwepa na kumuwekea ngumu!
“Shemeji,una tatizo gani?”
“Embu acha huo mchezo unaotaka kufanya,jieshimu”
“Mchezo gani?”
“Sikia,kama unataka tuangalie movie!Tuangalie, kama huwezi niambie niondoke”
“Lakini shemeji,si nakutumbua kipele tu,kuna ubaya gani?”
“Mwenye kazi hiyo ni Amney,sio wewe.Wewe unadhani akikukuta unafanya hivi,atakuelewa?Weee ebu niache toa mkono wako”
“Aya,basi”
Necka akatulia lakini bado aliendelea kuwashwa,akatafuta mbinu nyingine.Mkono wake akaupeleka kifuani kwa Nemesi mara aanze kumsifia hiyo ilimfanya Nemesi achukie na kuingiwa na hofu,alishaelewa ni kitu gani Necka anahitaji sababu alikuwa ni mtu mzima mwenye akili timamu lakini alichohofia ni kitu kimoja,inawezekana Necka Golden ametumwa kumpima imani na msimamo, huo ndio ulikuwa wasiwasi wake mkubwa lakini pia hakutaka kufanya jambo la usaliti.
“Necka,sijui nani.Mimi naondoka kama huwezi kutulia”
“Ungekuwa unataka kuondoka,ungeshaondoka.Najua unataka”
Necka akawaza na kujipa matumaini,akaendelea na zoezi lake la uchokozi,kuendelea kumchekea na kumpapasa bila kufanya kitu, kwake ilikuwa ni sawa na upotevu wa muda hiyo ilimaanisha Amney angeingia muda huo,ingekuwa kazi bure.Hapohapo akajitosa kimasomaso na kupeleka mkono wake kwenye tango la Nemesi!Akajivuta kwa nguvu na kumsogelea mdomoni, akilazimisha kupiga denda,Nemesi akakwepesha mdomo lakini msichana huyu Necka alishaelewa wapi pa kumshika,akaendelea kupapasa tango ghafla Nemesi akatulia kama mwanakondoo,wakaanza kulana denda kwa fujo huku wakipapasana kwa kasi!

****
*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG