Search This Blog

Monday, March 23, 2020

ABEE SHEMEJI SEHEMU YA 5/10


ABEE SHEMEJI
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 5 KATI YA 10
*******

Mguu mmoja wa Yusrath,ulikuwa begani kwa Sameer!Yupo kama alivyozaliwa,anahema ndani kwa ndani huku akitoa miguno ambayo watoto wa kike hutoa wakiwa katikati ya mchezo huo,usiohitaji hasira.Kila kitu kwake kilikuwa kimebadilika,akasahau kwamba siku hiyo mchana alipigwa makofi
na mumewe,badala yake alikuwa katika sayari nyingine ya Huba,anahisi yupo angani anapaa bila mabawa.Miguno aliyotoa ilimfanya Sameer, azidishe kasi ya kuzungusha kiuno chake,hakuishia hapo akasogeza mdomo mpaka shingoni mwa Yusrath, akatoa ulimi na kuanza kumnyonya shingo,akateleza na ulimi na kuutumbukiza mpaka ndani ya sikio la mwanamke huyo, ambaye kwa wakati huo akahisi kama roho yake inaacha mwili.
“Sa..mer I’m cummiiiing aaaaah aaashs aaaaah”
Hiyo ilimaanisha ya kwamba mwanamke huyo,anakaribia kufika kileleni ndiyo maana akaanza kukunja kunja mashuka,akiyavuta huku na kule akafumba macho yake kwa hisia kali na kumkumbatia kwa nguvu Sameer, ambaye hata yeye alizidisha majeshi majeshi,kiuno chake kikiwa kinapanda juu na kushuka,hawakuchukua dakika wote wakatulia Sameer akawa amelala kifuani mwa Yusrath,kijasho kinamtoka kwa mbali.
“Nakupenda baby”
Yusrath,alisema hivyo huku akimbusu Sameer!Alikuwa mwenye kila sababu ya kutamka maneno hayo kutoka moyoni kwani Sameer alistahili.
“Hata mimi mpenzi”
“Sijui kwanini niliolewa mapema namna hii?”
“Usiseme hivyo,wenda usingeolewa tusingekutana”
“Nataka niombe talaka,niwe nawewe uwe mme wangu.Unanipa furaha,nina enjoy kuwa nawewe”
“Mmmh baby”
“Nini Sameer,hutaki?”
“Uamuzi ni wako,baby.Mimi vyovyote nipo fresh”
“Nakupenda sana”
Penzi la miezi michache likafanya likatize upendo wa Ahmed wa miaka mingi,alichoshukuru watoto wake walikuwa tayari, wamelala na aliwapenda sababu hawakuwa wanalialia hovyo kama watoto wengine,kutokana na kunogewa siku hiyo walikula humohumo ndani.Usiku ulivyofika,simu yake ikaanza kuita mpigaji alikuwa ni mumewe, alichokifanya ni kusonya na kuzima simu,kazi ikaanza upya ya kubiduana na kuhemeana.
Asubuhi,kulivyopambazuka!Akatoka kitandani kwa haraka,kwa kuwa hoteli hiyo ilikiwa na hita,akaweka maji ya moto na kuwaogesha watoto wake juujuu,alivyomaliza akavaa na kumuaga Sameer kwa safari moja,kwenda kwa wazazi wake akawaambie kwamba alipigwa na Ahmed na baada ya hapo akamfungia ndani stoo,ndiyo maana akashindwa kufika.
“Baby,nilisahau kukupa mzigo wako”
“Mzigo gani?”
Sameer akauliza akiwa kitandani bado,alichokifanya Yusrath ni kuingiza mkono ndani ya mkoba,akatoa bahasha ya kaki iliyojaa,hilo lilikuwa wazi kabisa kwamba kulikuwa na kibunda cha pesa.
“Laki tano hizo baby”
Macho yalimtoka Sameer,hakuamini kama anapewa kiasi kikubwa cha pesa namna hiyo.Hapohapo Yusrath,akatoka nje na kutafuta bajaji ambayo haikuchukuwa muda mrefu.
Akawa amefika Ilala,nje ya nyumba yao.Kilichomfanya apigwe na butwaa zaidi ni baada ya kuona nje kuna gari aina ya Verosa,mpya kabisa rangi yake inang’aa.Gari hilo,hakuwahi kuliona kabla,akajua kabisa ndani kuna wageni lakini hakujua ni akina nani,asubuhi asubuhi hiyo.Bila kutafakari,akatembea na kufungua mlango!Sura,alizoziona zilimfanya apigwe na butwaa la Waziwazi,alikuwa ni Ahmed ametanda kwenye kochi,pembeni wajomba zake wawili.Kushoto,wameketi wazazi wake.
“Kaa hapo”
Sentensi hiyo alitoa Mzee Suleiman kwa ukali,akiwa amekunja sura hacheki.
“Ulikuwa wapi?”
Mzee Suleiman,akamdaka na swali.
“Mme wangu,muache basi mtoto akae kwan…”Mama akadakia lakini alikatishwa.
“Nyamaza,naongea na Yusrath,ulikuwa wapi?”
Sijui aliyatoa wapi machozi,hapohapo akaanza kujikamua akafanikiwa kutoa machozi mililita kumi,akamtizama Ahmed kwa hasira chafu.
“Ahmed kwa..nini umenifungia stoo?Uli…taka nifeee kwa..nini lakini Mme wangu,au kukupend…a imekuwa kosa?Ko..sa langu nini mme wa…ngu?”
Kama ungekuwa mbele yake,ungemuonea huruma wala usingedhani kama mwanamke huyo anaigiza,hiyo ilimfanya Ahmed apate kigugumizi cha ghafla sababu tayari kibao kiligeuka kwake,Mama Yusrath akamkata Ahmed, jicho kali la chuki huku midomo yake ikimcheza cheza kwa ghadhabu!


.

Ndani ya moyo wake alijua kama kila alilokuwa anasema lilikuwa la uwongo na anamsingizia Mumewe Ahmed,lakini angefanya nini?Ilikuwa ni lazima ajitetee ili apunguze makali ya kesi inayomkabili mbele na amkomeshe Ahmed, ambaye ana tabia ya kumpiga kama ngoma,upande mwingine wa shilingi alihisi kuumia baada ya kumtizama Ahmed,hakuelewa ni aina gani ya moto angechomwa huko Jehanam siku moja, akifa.
Alikuwa ana dhambi nyingi sana,watoto hawakuwa wa Ahmed na sio hivyo tu alikuwa ana mahusiano na mwanamme mwingine nje ya ndoa,anayeitwa Sameer yote hayo Ahmed hakuwa anajua,kilichomuuma ni aina ya mapendo aliyokuwa anapewa na mwanamme huyo, kifupi Ahmed hakustahili anayomfanyia hata kidogo!Ghafla akapata uchungu ajabu,kwikwi ikambana.
“Mwanahizaya,usiye kuwa na hayaa.Bazaaaaaz mkubwa”
Mama Yusrath,alitoa maneno hayo akisindikiza na msonyo mrefu wa mwendokasi,mdomo mpana wa Mama huyu uliendana na sifa yake ya uongeaji,Mama huyo hakujua kukaa kimya kwenye tatizo linalofanana na hilo.
“Lakini Ma…”
“Ahmed,nyamaza.Tulia kwanza”
Ahmed alivyotaka kujitetea na kumjibu Mama Yusrath, mjomba wake aliyeitwa Zelyatan akamtuliza ili kuepusha shali, alishaelewa kwamba kitumbua kimeingia mchanga,niya yake ilikuwa yeye ndiye azungumze na sio Ahmed aongee chochote.
“Mama,naomba tuongee kidogo!Hawa bado ni watoto”
Mr.Zelyatan akatia neno la busara niya ikiwa kusawazisha kila kilichotokea ili wayajenge lakini nayeye alikatwa ndimi.
“Huyo Ahmed,ana utoto gani?Angekuwa mtoto angemzalisha mwanangu mapacha,jitu zima hilo.Kwanza tokeni kwangu”
“Mama Yusrath,mke wangu.Ebu punguza ukali wa maneno kidogo”
Mzee Suleiman alivyoona mkewe anaropoka akamtuliza ili aingilie kati, kama mwanamme ilibidi amtulize mkewe kwani alimuelewa na alijua alikuwa mbioni kutoa matusi ya nguoni. Kifupi siku hiyo sable haikutosha,kila mtu akashikwa na ghadhabu, dakika mbili nzima wakatumia kujibizana.
“Enhee,endelea”
Mr.Zelyatan akamtaka Yusrath kwanza azungumze kila kitu kilichotokea,hapo ndipo Yusrath alipoanza kujielezea kila kitu kilichotokea, akasema namna Ahmed alivyompiga.
“Kwanini alikupiga?”
Mr.Zelyatan akahoji.
“Muulize mwenyewe”
Swali hilo likageuka kwa Ahmed,hiyo ilimfanya Yusrath ajiandae vizuri kwani alishaelewa ni kitu gani Ahmed ataenda kujibu na ataongea kila kitu kuhusu mwanamme aliyemkuta,ndiyo maana akaanza kupangilia uwongo mwingine wa kujitetea.
“Anco,pamoja na Baba na Mama…”
Ahmed akaanza kuongea,akaweka pozi kidogo na kushusha pumzi.
“Mke wangu,nakupenda sana!Naomba unisamehee,nakubali nimekupiga.Anco,ni kweli nilimpiga Yusrath tulipishana maneno kidogo,ni hasira tu hata hivyo sikuwa vizuri jana!Nilivyofika nyumbani hatukuelewana vizuri,mkono ukateleza bahati mbaya na isitoshe pia,nilikuwa nimekunywa”
Kumegewa siku zote ni siri ya ndani,Ahmed hakutaka kusema kwamba alimfuma na mwanamme ndani ya nyumba yake,aliamini kwa kusema hivyo ingekuwa aibu kubwa na skendo hiyo ingeenea,angeidhalilisha ndoa yake, ndiyo maana akataka jambo hilo liwe siri na kuzitupia lawama zote pombe,pia alifanya hivyo ili kumkingia kifua Yusrath, asionekane muhuni na Malaya kwani aibu ya mkewe ingekuwa yake pia,Yusrath hakuamini. Alichokitegemea kutoka kwa Ahmed kilikuwa ni kitu tofauti na alichosikia,hiyo ikamshangaza na kumfanya ashindwe kujazia neno lolote lile.
“Kwahiyo ndiyo umfungie stoo?Hujui kama ana watoto wadogo?”
Mama Yusrath,akauliza kwa shali.
“Ni hasira Mama,naomba mnisamehee”
“Hatuwezi”
Ghafla ukazuka mjadala mkubwa,ikatokea vuta n’kuvute!Ahmed akasisitiza asamehewe na alimpenda mkewe, akahitimisha kwamba jambo hilo halitojirudia tena,haikuwa rahisi kama anavyodhani.Hapo ilibidi Yusrath,ageukiwe na kuulizwa kama amekubali kumsamehee mumewe ama achape lapa.Alichokisema ni kitu kimoja tu,anahitaji Talaka na si vinginevyo.
“No,mke wangu usifike huko.Nakupenda bado”
“Siwezi Ahmed”
“Nisamehee sitorudia tena”
Ilikuwa ni aibu kubwa kwa Mwanamme kama Ahmed kulengwa na machozi mbele ya wakwe zake,alihisi uchungu wa ajabu sana!Hakutaka kuamini kwamba kuanzia siku hiyo yeye na Yusrath, ndiyo ingekuwa mwisho wao,japokuwa hakutaka kukubali jambo hilo litokee, ndiyo maana aliendelea kubembeleza,alivyowaangalia watoto wake wachanga moyo ulimuuma zaidi.Hiyo ikamfanya azidi kuongeza kasi ya kumuimbisha na kumwambia maneno matamu,kwa mwanamke yoyote Yule angeambiwa maneno anayosema Ahmed, hakika angetulia na kutoa msamahaa hicho ndicho alichokifanya Yusrath,ghafla akasahau yaliyopita akafuta machozi na kumtizama Ahmed.
“Nimekusamehee Mme wangu lakini usirudie tena”
Ulikuwa ni ushindi mkubwa kwa Ahmed baada ya kupoteza matumaini ya kumkosa mkewe,hiyo ilimfanya Mama Yusrath asiseme kitu chochote kile akabaki kimya.Ahmed hakuishia hapo,kwa busara alizokuwa nazo akaendelea kuomba msamahaa kwa wazazi wa Yusrath, kwa kila kitu kilichotokea,hawakuwa na sababu ya kuendelea kuweka kinyongo, wote wakaridhia na kumsamehee!Hiyo ilimaanisha Ahmed aondoke na familia yake,hicho ndicho kilichotokea.

******
Siku zote,wanaogombana wanapatana na utamu wa penzi huzidi mara mia yake, mbali na hapo heshima huongezeka.Familia ikarudi upya kwenye mstari,Ahmed akazidi kuwa mwenye furaha zaidi, akasahau yote yaliyopita hakuwa na sababu ya kuendelea kubaki na vitu moyoni mwake,akakubali na mkewe wagange yajayo!Sambamba na Yusrath ambaye hata yeye muda wote,alikuwa mwenye furaha iliyozidi kifani, hasa katika swala la gari jipya aina ya Verosa, lililonunuliwa na mumewe.
“Una tabia mbaya baby”
Yusrath akasema huku akicheka,akiwa ndani ya gari jipya juu ya mapaja, kawapakata watoto wake mapacha!
“Sasa,si nilitaka kuku surprise siku ile,ndiyo shetani akafanya yake”
“Gari zuri sana,hii sehemu ya kuwekea glasi?”
“Ndio Darling”
Gari lilikuwa zuri la kisasa,pembeni chini karibu na gia kuna sehemu maalum ya kuwekea glasi ama chupa.
“Kwahiyo utakuwa unaweka glasi ya bia hapa?”
“Hapana ya soda”
“Hahahaha,Wewe huyo?”
“Ndio baby”
“Sawa baba paroko”
“Inabidi mwezi ujao nikufundishe kuendesha gari”
“Nitafurahi nikijua,barabarani watanikoma huko!”
Ahmed,hakuwa mwanamme mwenye longolongo kwake yeye aliamini siku zote ahadi ni deni,mwezi mmoja baadaye ikawa kila siku ya Jumamosi lazima watoke wote kwenda kwenye kiwanja kikubwa cha mpira,hapo ndipo akaanza kumfundisha Yusrath gari kwa staili ya kumpakata na kumuonesha jinsi ya kukanyaga mafuta na kubadili gia.
“Ukiwa unaendesha gari,especially barabarani.Usiwe kama roboti,angalia vioo vyote kila baada ya sekunde tatu.Site mirrors za nje na hii ya ndani!Concetrate baby”
“Sawa mwalimu”
“Ndio,hapa mimi naongea kama mwalimu sio baby.Ukikosea makonzi”
Ahmed akaweka utani kidogo wote wakacheka na kupigana mabusu ya mdomo,zoezi likaendelea kama kawaida.

****
Kama mwanamme ama kichwa cha familia ilikuwa ni lazima atimize wajibu wake,akili yake aliisumbua kuwaza kuongeza miradi mingine, akiamini siku moja watoto wake watahitaji kwenda shule, hiyo ilimaanisha mshahara peke yake,ungeshindwa kukidhi mahitaji hayo yote, isitoshe mkewe alikuwa mama wa nyumbani tu,alichokifanya ni kuendelea kufanya kazi kwa bidii zote.Kuna vitu akavipunguza kama pombe na matumizi yasiyokuwa ya lazima.Lengo lake likiwa ni moja tu,pesa ikipatikana anunuwe kiwanja kisha baada ya hapo atumie kiwanja hiko kuombea mikopo.Hiyo ndiyo mipango iliyokuwa ndani ya kichwa cha mwanamme huyu Ahmed.
“Leo uko bize kweli,unapiga ova time nini?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Aneth baada ya kuingia ndani,ofisini kwa Ahmed.
“Inabidi nifanye hivyo”
“Kweli,ndoa sio mchezo.Leo Ijumaa Ahmed akae mpaka sasa hivi?”
“Nilikuwa nasikia tu kwa watu”
“Hongera sana,gentleman anatakiwa awe hivyo.Hiyo inakupunguzia kukaa kwenye vikundi,ukiwa bize kama hivyo utapata muda saa ngapi?”
“Yes it's true”
Ni kweli,Ahmed alikuwa bize mezani kwake juu kuna makaratasi mengi sana, anajaza ‘Tax Invoice’ na kutoa risiti za EFD mashine.
“Hivi ulisikia lile sakata la TRA?”
“Lipi?”
“Walikuja majuzi hapa,wanataka risiti za sales”
“Kwanini?”
“Ahmed,usicheze na TRA.Cheza na vitu vyote lakini sio wale jamaa,unamkumbuka Kim?”
“Kim yupi?”
“Aaah,yule chaliii.Alikuwa basa,anaringa ringa hivi.Mwembamba mrefu”
“Yeees,hivi yuko wapi?”
“Kapigwa chini na bosi,alimuweka ndani siku tatu”
“Acha bwaaana,ilikuwaje?”
“Kumbe alikuwa anapewa pesa na bosi,atume returns za kampuni.Pesa alikuwa anakula.Z report hatoi,wale jamaa wakaja…Ahmed sikia,alafu nina shida…Nilisahau kukwambia”
“Shida gani tena?”
“Nina shida na ela”
“Shilingi ngapi?”
“Laki na hamsini,nikopeshe”
“Duuu”
“Ahmed,nisaidie.Nitakulipa mwisho wa huu mwezi”
Pamoja na Anneth kupiga stori nyingi siku hiyo lakini shabaha yake ilikuwa ni hiyo,akopwe pesa na Ahmed, aliamini kivyovyote swaiba wake huyo,asingeshindwa kumuazima kiasi hicho cha pesa!Ni kweli,hilo halikuwa tatizo kwa Ahmed.
“Nitakupa kesho,lakini usisahau kurudisha”
“Hilo ondoa shaka”

******
Kurudiana na Mumewe kwa kishindo, haikumaanisha kwamba waachane na Sameer, hapana.Kilichobadilika ni kitu kimoja tu.Kwa kitendo cha Ahmed siku chache zilizopita kurudi ghafla mchana na kumkuta Shotola seblen kilimaanisha ipo siku moja Ahmed angeingia na kumkuta Sameer ndani,hiyo ingemaanisha ungekuwa ni mwisho wa maisha yake duniani.Alichokifanya ni kutokubali Sameer awe anafika nyumbani kwake, kumaanisha kwamba watakuwa wanakutana huko hotelini,kilichomfanya apate afadhali ni baada ya kupata dada wa nyumbani yaani housegirl,ambaye huyo muda wote alikuwa ana kazi ya kuwaangalia watoto,kuwafulia nguo na kuwaogesha.
Hapo ndipo Yusrath hupata mwanya wa kuchomoka na kwenda hoteli ya Sinza, kufanya mavituzi na Sameer,hawakuishia hapo bali Sameer alihongwa pesa na vitu vya gharama sana!Hakuna siku ambayo Yusrath alionyeshwa utundu kama hiyo,Sameer alimnyongea viuno,akamlamba kila sehemu ya mwili wake.Siku hiyo alijituma sio kawaida,hiyo ilimfanya Yusrath apagawe zaidi na zaidi!Alitoa miguno na maneno ya kila aina, jioni hiyo.
“Nakupenda sana baby wangu,alafu mme wangu kanunua gari”
Yusrath akashindwa kukaa na jambo hilo kifuani.
“Acha utani Darling.Namimi utaninunulia lini langu?”
“Hayo mambo madogo,usijali laaziz wangu”

*****
‘AHMED KWEMA,MUDA HUU MKEO HAYUPO NYUMBANI,YUPO HOTELINI NA MWANAMME MWINGINE,SIKU NJEMA’
Ulikuwa ni ujumbe mfupi,ulioingia kwenye simu ya Ahmed akiwa ofisini kwake.Moyo wake ukapiga kwa nguvu,kitu kilichomshangaza namba hiyo ilikuwa ngeni,akatulia kidogo akajua wenda mtu huyo amekosea namba lakini isingewezekana akosee mpaka jina lake, hapo ndipo akapata uhakika kwamba meseji hiyo ni yake,hakutaka kukurupuka kama siku zote, alichokifanya ni kumpigia simu dada wa nyumbani,hapohapo simu ikapokelewa.
“Hadima”
Akaita jina, baada ya simu kupokelewa.
“Abee Baba,shikamoo”
“Marahaba,mpelekee Mama simu. Nataka kuongea naye”
Ulikuwa ni mtego ili ajue kama Yusrath yupo nyumbani.
“Nani Mama?”
“Ndio,mpelekee simu”
“Mama hayupo,ametoka”
“Tangu saa ngapi?”
“Saa tatu”
“Saa tatu,asubuhi?”
“Ndio Baba”
Ahmed alivyoangalia saa yake ya mkononi, ilionesha ni saa kumi ya jioni.
“Hajakuaga anaenda wapi?”
“Hapana baba”
“Sawa,baadaye”
Kitendo cha kukata simu,akahisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi mkali,akaanza kuisaka namba iliyomtumia ujumbe huo,alivyopiga haikupatikana hewani.Alichokifanya ni kumpigia moja kwa moja mkewe,matokeo yake simu iliita bila kupokelewa,ikaita tena na tena.Mara ya nne,ndipo ikapokelewa!
“Mme wangu”
Upande wa pili wa simu ulisikika,Yusrath alikuwa kwenye laini.Hiyo ilimfanya Ahmed ashikwe na hasira ajabu,akajikaza kisabuni.
“Yes baby,nimekumisi.Nimekupigia muda mrefu mbona hupokei?”
“Nilikuwa nimelala baby wangu,nilichoka sana”
“Upo chumbani?”
“Mimi?”
“Ndio”
“Nipo chumbani Darling,nilikuwa nimelala”
“Okay,kwenye draw hapo ya chini kabisa.Kuna karatasi nimeacha,naomba uchukuwe nisomee majina yaliyokuwepo.Kuna mtu anayataka”
Ki ukweli hakuwa chumbani,alikuwa hotelini na Sameer wapo uchi wa mnyama.Sentensi hiyo kutoka kwa Ahmed ilimfanya atetemeke,jasho likaanza kumtoka, hakuelewa ni kitu gani akifanye.
“Ushafungua draw?”
Ahmed akauliza kwa sauti ya ukali kidogo ingawa alijitahidi kujikaza lakini alishindwa.
“Hapana,hapana Mme wa..ngu.Ndio nashuka kitandani”
“Nasubiri”
Macho ya Ahmed,tayari yalikuwa mekundu na alizungumza hivyo akiwa ana uhakika wa asilimia mia moja kwamba Yusrath hayupo nyumbani,alichotaka kukifanya ni kuaga ofisini wakati huohuo,achukuwe pikipiki awahi nyumbani ili ahakikishe kwa macho yake,hakuelewa ni hatua gani achukuwe endapo angemkosa Yusrath nyumbani,alichomuomba Mungu ni kumpa nguvu na hekima ili asifanye jambo lolote la kipumbavu, sababu alizijua hasira zake!


Hakuwa yeye tena bali hasira zilianza kumpanda taratibu na kufika katika kiwango cha juu kabisa,sura ya mkewe kulazwa juu ya kitanda yupo uchi wa mnyama na mwanamme mwingine ndiyo ilikuwa inapita kichwani kwake,moyo wake ukauma ajabu.Kifupi Ahmed alikuwa kama mkandarasi anayeezeka mabati alafu Yusrath chini anabomoa kwani alijitahidi kulijenga penzi lao lisije hata siku moja kubomoka lakini hiyo ikawa kama kutwanga maji kwenye kinu!
Akiwa juu ya kiti anatafakari, hapohapo akasimama na kuvuta koti lake lililokuwa juu ya kiti,akaliweka mwilini na kuanza kutembea kwa hatua mbilimbili,akatokeza mpaka kwa sekretari.
“Bosi,akiniulizia mwambie nimeenda hospitali sijisikii vizuri”
“Nitamwambia”
Ahmed alitoka nje, baada ya kutoa sababu hiyo ya uwongo.Hakuwa sawa hata kidogo mapigo yake ya moyo yalimwenda mbio akapata presha kubwa,hakuelewa ni kitu gani akifanye endapo akimkosa mkewe nyumbani,alivyotaka kupanda pikipiki ili awahi, akaghaili na kutoa funguo za gari ndani ya koti,akaingia ndani ya gari lake na kuanza kulitoa taratibu kabisa,alivyoingia barabarani akafunga mkanda akiwa mwenye msongo mkubwa wa mawazo!

****
Hakuna siku iliyomchanganya akili kama hiyo,kitendo cha Mumewe kupiga simu na kumuuliza ni wapi alipo kisha kumdanganya na baadaye kuambiwa atafute karatasi chumbani kilimfanya aogope,alitetemeka sababu aliongea uwongo ambao uligundulika.Muda wote, alikuwa mwenye wasiwasi, akamtizama Sameer aliyekuwa pembeni yake akamchukia ghafla akiamini huyo ndio chanzo,kilichomchanganya zaidi ni baada ya Ahmed kukata simu, hiyo ilimaanisha amechukia na kivyovyote vile kitu kibaya kilikuwa mbioni kutokea,alichokifanya ni kumpigia simu dada wa nyumbani na kumuuliza mumewe kama amefika.
“Hajafika”
“Hayupooo?”
Yusrath aliuliza mara mbilimbili.
“Ndio Mama”
“Alikupigia simu?”
“Ndio”
“Kaniulizia?”
“Alitaka kuongea nawewe al..”
“Ameniuliziaaaa?”
“Ndio Mama”
“Ukamwambia nini?”
“Kama ulivyoniambia”
“Kukwambia nini?Kwani mimi nilikwambia nini?”
“Umetoka utarudi,baaday..”
Jambo hilo likamfanya Yusrath akate simu,jasho jembamba lilianza kumtoka, akahisi tumbo linamuuma hakujua nila kuharisha ama uwoga,kwa kasi akaanza kuvaa nguo zake kwani alishaelewa ni aina gani ya kipigo ataenda kuchezea,kifupi alijua kabisa kwamba, ataenda kupata tabu sana!Hakukumbuka kumuaga Sameer,akafungua mlango na kuanza kuteremsha ngazi mbilimbili,alivyofika nje akatafuta pikipiki ambayo ilimfikisha mpaka nyumbani kwake,Ubungo Kibangu.
Japokuwa hakukuwa na jua kali lakini mwili wake ulilowa jasho,hakuelewa ni aina gani ya mbinu atakayoenda kutumia ili mumewe amuelewe,kila alivyozidi kupiga hatua kulisogelea geti, ndivyo uwoga wake ulizidi,alivyofungua geti alistaajabu baada ya kutoona gari nje,hapo aliamini kwamba Ahmed hajarudi bado ingawa swala hilo, hakutaka kulipa kipaumbele,akadhani wenda alifika nyumbani kwa usafiri mwingine na yupo ndani.Akatembea taratibu na kufungua mlango,macho yake yakakumbana na Dada wa nyumbani akiwa na watoto anawapa maziwa ya kopo.
“Baba amerudi?”
Namna Yusrath alivyouliza swali,ilimfanya mpaka Dada huyo agundue ni namna gani anavyoogopa!Yusrath alitia huruma na aliuliza kwa sauti ndogo ya unyenyekevu, akiwa mwenye wasiwasi mkubwa sana.
“Bado”
“Una uhakika?”
“Ndio”
Bado hakutaka kuamini,akatembea mpaka chumbani lakini hakukuwa na dalili yoyote ile ya Ahmed kuwepo,humo hakukaa sana akatoka na kumuuliza dada wa kazi jinsi Ahmed alivyopiga simu na kumuulizia.
“Ilikuwa saa ngapi?”
Ni swali lingine kutoka kwa Yusrath.
“Mchana,mchana hivi”
“Ulisema,alikuuliza nini?”
“Alitaka kuongea nawewe”
“Ukamjibu nini?”
“Umetoka tangu asubuhi”
“Mungu wangu,sasa kwanini ulimwambia?”
Hapo Hadima alikaa kimya kidogo kwani tajiri yake alitia huruma, machozi yalionekana kumlenga,kwa akili ya ki utu uzima akaelewa kabisa alishatia doa ndoa ya watu ni bora angekaa kimya, kuliko kusema aliyoongea!Hiyo ilimfamya Yusrath aweweseke,akajua kabisa simu aliyopigiwa na Ahmed akitaka achukuwe karatasi kwenye ‘draw’ ulikuwa ni mtego na sio vinginevyo,akahisi kujuta kwa kila kitu kilichotokea sababu miezi michache iliyopita walipelekana kwa wazazi kisa kesi ya staili hiyo,akajilaumu sana kwa upumbavu ambao ameanza.
“Kwanini nisitulie kwenye ndoa yangu lakini?”
Yusrath alijiuliza kimoyomoyo na kuapa kama hilo likipita salama ni lazima atatulia kwani alishaelewa, matatizo yote yanayotokea yeye ndiye mkandarasi na siku zote mwanamke mjinga, ataivunja ndoa yake kwa mikono yake ye mwenyewe!Hayo yote aliyajua siku hiyo,akaingia chumbani na kukaa kitako kitandani lakini akaona haitoshi,akatoka seblen akaanza kutembea huku na kule,moja haikai mbili haikai.
“Watoto wamelala?”
“Ndio Mama”
Hiyo haikusaidia chochote,alichowaza yeye ni kitu gani atamjibu Ahmed akirudi, hata hivyo wasiwasi ulianza kumuingia,haikuwa kawaida kwa Ahmed kufumbia macho jambo kama hilo zito, ilikuwa ni lazima siku hiyo angechezea vitasa lakini mpaka wakati huo mwanamme huyo hakutokea,jambo hilo ndilo lilimtia mashaka zaidi.
“Bora aje basi,anipige yaishe”
Hilo ndilo alilokuwa analitegemea,alikuwa yupo tayari kwa makofi akajiandaa vizuri,kazi yake ikawa ni kutega sikio kama atasikia mlio wa honi ya gari lakini mpaka inafika saa mbili usiku, hakukuwa na dalili yoyote ile ya Ahmed kutokea,mbaya zaidi hata simu hakupigiwa,alivyotaka kumpigia yeye moyo wake ukasita,akaogopa ataharibu.
Upande mwingine wa shilingi ulimwambia wenda Ahmed kapata ajali mbaya ya gari sababu ni lazima angeendesha gari kwa kasi kutokana na mawazo,akaanza kupata hofu mpya!Ikafika saa tatu usiku,saa nne,saa tano,saa sita ilivyofika saa saba akaamua kuchukua simu na kumpigia Ahmed lakini matokeo yake iliita bila kupokelewa,saa nane ikagonga ilivyofika saa tisa,akapiga simu lakini iliendelea kuita tu.

*****
Hasira za Ahmed Kajeme zilikuwa ni mbaya na chafu,hilo alilijua na wakati mwingine alidhani wenda hasira zake zilisababishwa na mapepo wabaya,ndiyo maana alivyokuwa darasa la saba baba yake alishawahi kumpeleka msikitini ili akasomewe dua mapepo hayo yatoke,hiyo haikusaidia kwani alivyoingia kidato cha kwanza, alikasirishwa shuleni baada ya kuchapwa fimbo ishirini bila sababu, kwa hasira akampiga mwalimu wake na kokoto la utosi,mwalimu huyo alilazwa hospitali kwa takribani miezi saba kitandani,Ahmed alifanya matukio mengi sana yaliyosababishwa na hasira zake mbaya, hilo wazazi wake walilijua mbaya zaidi akikasirika sana macho yake yanakuwa mwekundu na kuanza kutetemeka mikono, dalili hiyo huwa mbaya kwa maana anaweza kumpiga mtu yoyote yule na kitu chochote kilichokuwa karibu yake.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa siku hiyo baada ya kumpigia simu mkewe,mikono yake ilikuwa inatetemeka akiwa ndani ya gari,hawezi kushika usukani vizuri akawa kama mtu mwenye ugonjwa wa degedege,alivyojiangalia kwenye kioo akaona ni kwa namna gani macho yake yalivyokuwa mekundu.
Hiyo ilikuwa ni dalili mbaya endapo Yusrath angekuwa mbele yake akaogopa kufungwa sababu angemuua siku hiyo ili kuepusha hilo,alichokifanya ni kuendesha gari taratibu ili hasira zake zishuke huku akijaribu kadri awezavyo kuzishusha mwenyewe,jambo hilo likaonekana kuwa gumu.Alivyofika,Kariakoo Kongo!Akakunja kushoto mpaka kwenye baa inayoitwa Matako bar!Akanyoosha mguu na kukunja kushoto ambapo kulikuwa na magari mengi sana yamepaki,mwenye bar hiyo aliita Makutano bar lakini kutokana na wahudumu wote kuwa na makalio makubwa,wadau mbalimbali na walevi wakaibatiza jina na kuiita Matako bar,kama mumeo kakudanganya anaenda kuangalia kombe la dunia basi utamkuta, Matako Bar.
Sio siri wanawake wa bar hiyo,walivutia na walivalia vimini walijua kutega wanaume,wanawake wengi waliichukia bar hiyo sababu waume zao walitekwa na mashangingi.Hapo ndipo Ahmed,alitaka kwenda kutulia na kutuliza hasira zake!Alivyopaki gari na kushuka,akalakiwa na mwanamke mnene kiasi,shepu kubwa,amevalia kimini,nyuma ana mzigo wa kuvunja chaga!
“Karibu sana,kinywaji gani?”
Mwanamke huyo aliuliza kwa mikogo na madoido akiwa katika tabasamu pana.
“Ndovu na Valuer,chupa kubwa”
“Sawa”
Hazikupita hata dakika tano,vinywaji vikawa mezani.Hapo Ahmed hakuchelewa akamimina bia yake na kuchanganya na pombe kali,akashushia taratibu huku akitafakari mambo yake ya ndoa!Ilivyoisha,akaongeza tena, taratibu hasira zake zikaanza kushuka,akaanza kuona nyota nyota na kuhisi kizunguzungu kwa mbali,hiyo ilimaanisha tayari pombe ilianza kupanda kichwani.Licha ya kuhisi kizunguzungu lakini moyo wake bado uliendelea kumuuma.
“Kuna mbwa koko mmoja juzi,nilimfuma na mke wangu!”
Kwa nyuma ilisikika,sauti ya mwanamme ikiongea akatega sikio ili kusikia vizuri kwani stori ya namna hiyo ilimuhusu yeye pia.
“Aaaaacha,mwanamke yupi?”
“Kuruthum”
“Chumu?”
“Huyo huyo,yupo na mpemba mmoja falafala.Chumbani kwangu,Mamaaaaae!Nilichokifanya,nikafunga chumba..”
“Ikawajee?”
“Sio poa,huyo Mpemba huko alipo,hawezi kunisahau yaani mpaka anaingia kaburini”
“Ulimfanya nini?”
“Niliwapigia simu wakina Tino,pale Tandale.Nikawaambia njoeni pandeni hata pikipiki,mjeee.Hawakuchelewa,wakaingia mpaka kwangu.Nikawaambia sikilizeni,kuna kazi hapa.Kila mmoja nampa laki laki….Wale jamaa wakasema poa,tukafungua mlango ule.Mpemba,anatetemeka.Nikamuuliza,mke wangu.Umegongwa bao ngaapi na huyu mbwa kokoo?”
“Duuu,aise kama nakuona vile”
“Hasira zilinifika kohoni mzee mwenzangu.Yule jamaa nilikuwa napewa stori zake tu mtaani.Kwamba anakula mke wangu,kila nikiweka mitego yangu,anaruka.Siku hiyo ikafika arobaini yake.Mpemba kaomba sana msamaha,nikawaambia wale njemba,mshikisheni ukuta huyo.Mpemba yule akadhani utani,walimshikisha ukuta wakamla samvu la kopo”
“Walimfi*****?”
“Ndiooo,tena laivuu naonaa”
“Ndio dawa yao,wapenda wake za watu.Hiyo ndio dawa yao.Sasa mkeo yuko wapi?”
“Siku zote,anayekumegea ndiyo unatakiwa ule naye sahani moja!Sio mkeo”
“Lakini pia sisi sometimes,tumezidi ndio tunafanya wake zetu wachepuke.Kuna rafiki yangu mmoja,mke wake anatembea na Muuza nyama buchani.Kisa tu mumewe,aachi pesa za matumizi”
“Hilo nalo neno,wanawake wengine ni hulka tu.Anaona raha kuchepuka,yaani bila kuchepuka hasikii rahaa”
Maongezi hayo yalimfanya Ahmed ajifunze kitu,akageuka kidogo ili kuangalia sura za wanaume wanaozungumza,alivyowaona alichoka,walikuwa ni wazee wenye mvi.Hapo ndipo akapata akili mpya ya kuanza kumtafuta mwanamme anayetembea na mkewe Yusrath,akaapia atamfanya kitu kibaya ambacho angeenda kusimulia ulimwengu mzima,pia kitu kingine alichotaka kujua ni mwanamme huyo anafanana vipi.
Siku hiyo alikunywa pombe za kutosha huku akifikiria ni aina gani ya mitego amuwekee mkewe,akafikiria njia tofautitofauti na nyingi lakini hakupata jibu kamili.
“Nitamjua tuuu”
Ahmed alijisemea na kuweka glasi ya pombe mdomoni,akizidi kutafakari mbinu.Mwishowe akapata mbinu moja na kutabasamu,mwanamke mwenye makalio aliyepita mbele yake alimtamanisha,akamuangalia vizuri kuanzia juu mpaka chini,karoti yake ikaanza kusimama.
“Psiiiiiii”
Akapiga mluzi,mwanamke huyo akageuka.
“Mamboooo”
“Poaa”
“Leo,unatoka saa ngapi hapa?”
“Sasa hivi tu”
“Vipiiii?Tuondoke wote?”
“Mmmmh”
“Mbona unagunaaaa?Bei gani kwanii?”
“Elfu thelathini”
“Sawa,tweeende”
“Wapi lakini?”
“Wewe unataka kwendaa wapiii?”
“Hapo nyuma kuna gesti,hatulali lakini”
“Hakuna shakaaaa”
“Nikimaliza,nitakwambia”
Kilichomuweka hapo tena sio pombe bali ni mwanamke huyo aliyemtamani ghafla,akili yake tayari ikahama,akaanza kuwaza ngono tu!Akabaki anamtizama mwanamke huyo anayetingishika kwa nyuma yaani hamsini,hamsini mia Ahmed akabaki anakula kwa macho bila kuamini baada ya muda mfupi, atakuwa naye kitandani.Hilo halikuwa na longolongo,mwanamke huyo alivyoaga wenzake, akamfuata Ahmed na kumtaka waondoke, kwa kuwa hakukua na umbali na gesti ilipo.Wakaenda na kupewa chumba,hakuna maongezi yaliyoendelea hapo baada ya kufika chumbani.
“Subiri,nikuvalishe Condom”
“Ya nini sasaaaaa kwanini nile pipi na magandaa?Wakati nimetoa pesa?”
Ahmed akataka kugoma lakini mwanamke huyo nayeye akaweka ngumu,hakutaka kuongea akatoa pakiti ya Condom na kumvalisha Ahmed,aliyekuwa na stimu na mori.Akamkunja vizuri mwanamke huyo mwenye mwili mkubwa na kuanza mashambulizi hapohapo.Kwa kuwa ilikuwa ni kama biashara,hakukuwa na mbwembwe nyingi,Ahmed hakutaka kuweka ufundi wowote ule!Akafika kitonga na kutulia,akatoa pesa na kumlipa!
*****
Muda ulikuwa umekwenda sana,akawasha gari na kuanza safari ya kurudi nyumbani,hapo ndipo simu yake ilipoanza kuita,alivyoangalia akaona ni mkewe ndiye anapiga,akaipotezea!Ahmed,hakuishia hapo, akaenda kwenye bar nyingine na kuongeza bia nyingine akaweka kwenye gari na kuondoka zake!Usiku ulikuwa mkubwa,barabarani kulikuwa na magari machache!
Saa 9;57 Usiku ndipo aliwasili nje ya geti,hakutaka kupiga honi.Alichokifanya ni kuingia ndani ya geti na kujifungulia mlango huku akipepesuka,akaingiza gari ndani na kulifunga geti vizuri.Akiwa anayumba,akatembea mpaka mlangoni na kuanza kugonga!
“Ngo! Ngoo! Ngoooo”
Ni katikati ya Usiku Yusrath,alikurupuka kutoka kwenye kochi akiwa amelala seblen, alivyoangalia saa ya ukutani alishtuka zaidi,akatembea akiwa na mawenge kabla ya kufungua mlango akachungulia dirishani,moyo wake ukapiga kwa nguvu baada kuona sura ya Ahmed,tena akiwa amelewa chakali,akajua tayari ugomvi ungeenda kuanza!Akajishauri na kuufungua kisha kurudi nyuma akijiandaa kupokea kibao sababu alijua ndilo jambo linalofuata,lakini badala yake Ahmed akapitiliza ndani bila kumuangalia usoni,akanyoosha mpaka chumbnani bila kusema chochote,hivyohivyo akiwa na viatu akajitupa kitandani puuu!Kwa uwoga aliokuwa nao Yusrath,akaogopa kuingia chumbani,alichokifanya ni kunyata mpaka chumbani.Ahmed,alikuwa kitandani,kalala kifudifudi na viatu halikuwa jambo la kawaida,alichokifanya yusrath ni kusogea karibu na kuanza kumvua viatu taratibu.
“Weweee naniiiii,unatakaaaa kuniibiaaa viatuu,sogeaa sogeeaa.Mwiziii wewee nishakuonaa.Sijalewaaa ujuuee”Ahmed,aliongea kilevi.
Hiyo ilimfanya Yusrath,atabasamu kidogo kwani mambo aliyokuwa anazungumza Ahmed yalimfurahisha.Hakuelewa mwanamme huyo ni aina gani ya pombe alikunywa sababu hakuwahi kumuona katika hali kama hiyo tangu wafahamiane,akahakikisha kamvua suruali na shati,akajisogeza karibu na kumkumbatia kisha wote wakalala huku akiwa anatafakari ni majibu gani ampe mumewe kukikucha,endapo akiulizwa alikuwa wapi mchana kutwa!

Kitu usingizi kwa Yusrath, kilikuwa ni kitu hadimu kupatikana usiku huo,alitamani kusikuche.Aliwaza vitu vingi sana,hususani majibu atakayompa Ahmed kukipambazuka,alishaelewa kipigo kilikuwa halali yake sababu alimuelewa Mmewe,ana mkono mwepesi na makofi yangehusika asubuhi yake,hata hivyo alitamani kukuche mapema apigwe ili yaishe, kuliko Ahmed kukaa kimya,akiwa anatafakari ni kitu gani akifanye,Ahmed akajigeuza, hapo ndipo akahisi tumbo linaanza kumuuma upya,sio siri mpaka kunakucha hakupata usingizi kama binadamu wa kawaida,saa 12;45 akaamka na kutoka kitandani akimuacha Ahmed bado anakoroma,alichokifanya ni kuwachukuwa watoto wake,akanyoosha mpaka chumbani kwa Hadima,dada wa kazi.
Huko,alitumia muda huo kuwanyonyesha maziwa na kuwalaza tena walale,akatembea mpaka seblen na kukaa,akisubiri hatma yake!Hapo hakuweza kukaa sana macho,kutokana na uchovu ukichanganya na usingizi aliokuwa nao,akajikuta amesinzia!

Pombe bado zilikuwa nyingi kichwani,asingeweza kuamka asubuhi na mapema kama afanyavyo siku zote kwani usiku wa jana, alichanganya pombe kali, kutokana na msongo wa mawazo akiamini angetoa mawazo,kichwa chake kilikuwa kizito na kilimuuma sana!Alitambua sana kwamba huo sio ugonjwa bali ni ‘hangover’alichokifanya cha kwanza ni kulazimisha macho yake yafunguke kwani yalikuwa mazito kuliko kawaida,alivyoangalia ukutani moyo wake ukapiga paaa kwa nguvu, baada ya kuona ni saa 4;28 Asubuhi,kwa kasi akatizama huku na kule ili kuangalia simu yake ilipo,akajisogeza mpaka karibu na meza akaichukua,moyo wake ukazidi kwenda mbio baada ya kukuta ‘missed calls ‘19 za bosi wake na meseji zisizokuwa na idadi kamili,kitu alichokumbuka ni kwamba siku hiyo alikuwa ana kikao cha bodi,mbaya zaidi alikuwa ni kiongozi, ambaye angeongoza timu hiyo.
“Jesus christ”(Yesu Kristo)
Alikuwa ni muislam lakini alijikuta anamtaja Yesu bila kutarajia,sio siri alihisi kuchanganyikiwa kupita kawaida,akajua kabisa ni lazima bosi wake atakuwa amekasirika na siku hiyo kulikuwa na hati hati ya kibarua chake kuota nyasi ama kupigwa lidandasi, kutokana na uzembe alioufanya,kwa kasi ya ajabu bila kuoga wala kupiga mswaki akaanza kufungua makabati ili achague shati avae,cha ajabu hakukuta nguo hata moja iliyopigwa pasi!Kwa wakati huo hakuwa na muda,akavaa shati moja wapo, lililojikunja kunja na kuvuta tai yake,akaiweka shingoni kwa kasi na kuvuta koti,alivyotaka kuvuta suruali,mlango wa chumbani kwake ukafunguliwa Yusrath,akaingia.
“Mme wangu”
Akaita kwa mahaba huku akisogea karibu,akamuona namna Ahmed alivyokuwa ana haha.
“Nimechelewa kazini nina kikao”
“Sasa utafanya nini?”
“Itabidi nichukuwe pikipiki niwahi”
“Ndio unaenda hivyo?”
Yusrath ilibidi aulize kwani koti na shati alizovaa mumewe,vilikuwa vimejikunja kunja utadhani vimetoka mdomoni mwa Ng’ombe!
“Ndio,si hujaninyooshea.Acha niende hivi hivi”
Ahmed akajibu kwa hasira kidogo huku akimtizama Yusrath,ilielekea bado ana hasira naye.Alivyotaka kufungua kinywa chake aulize kitu,akasita na kunyamaza!
“No,usiende kazini baby”
“Una maana gani?”
“Bora uwende hospitalini,ukahonge pesa.Wakuandikie karatasi,uzuge ulikuwa unaumwa,ulizidiwa love.Kuliko kwenda hivi,ukiulizwa kwanini umechelewa,utajibu nini?”
Ulikuwa ni mkakati kabambe kutoka kwa Yusrath,Ahmed hakufikiria hata siku moja kufanya kitu kama hicho cha kugushi,alichokifanya ni kuunga mkono hoja ya mkewe,hakuchelewa!Kwa kuwa kulikuwa na hospitali kubwa maeneo ya Ubungo,akapanda pikipiki na kwenda huko!Ambapo alikutana na Dokta Mbwilo,hakutaka kuficha akafunguka kila kitu anachotaka ili asaidiwe!
“Unajua,ni hatari hii?”
Dokta Mbwilo akajifanya kuleta ugumu kidogo lakini akatulizwa na kibunda cha shilingi laki moja ili agushi cheti na kuandika kwamba mgonjwa huyo alidondoka na kulazwa hospitalini,pesa ikawa imefanya kazi yake na kubadilisha mawazo ya daktari,kwa mbwembwe za Dokta Mbwilo,akachukua bandeji na kumuwekea kwenye mshipa wake wa damu.
“Hapo utasema,uliwekewa dripu,kingine akti kama unaumwa kweli”
“Sawa dokta”
Dokta akawa amekula laki moja, ya bure bure!Alichokifikiria Dokta kwa wakati huo ni kwenda kununua baadhi ya mabati ili amalizie nyumba yake.
Ahmed,hakutaka kubaki maeneo hayo tena,alichokifanya ni kurudi nyumbani,akakuta tayari Yusrath kapiga pasi nguo,akavaa na kutoka bila kuongea kitu chochote.
Alivyofika nje,akapanda pikipiki iliyompeleka mpaka Posta ofisini kwake,kila aliyemuona aliangalia chini!
“Kuna barua yako”
Sentensi hiyo ilimshtua kutoka mapokezi,Ahmed akageuka na kupewa baasha ndogo ya kaki.
“Bosi,anakuita.Kaniambia ukifika upite ofisini kwake moja kwa moja”
Mapigo yake ya moyo yakabadilika,yakaanza kupiga kwa nguvu kiasi kwamba jasho likaanza kumtoka,hakuelewa apitie ofisini kwake kwanza ama anyooshe ili kuitikia wito!Kutokana na mazingira yaliyokuwepo alijua kabisa hakukuwa na dalili nzuri,hata hivyo alipiga moyo konde na kunyoosha mpaka mlango wa bosi wake,akagonga na kuambiwa aingie ndani.Sura aliyomkuta nayo bosi wake,iliogopesha kumaanisha hakukuwa na habari njema hata kidogo,bosi wake hakuongea kitu zaidi ya kumuoneshea ishara akae kwenye kiti,Ahmed akafanya hivyo kwa adabu zote.
“Naona kazi imekushinda,barua yako umeipata?”
Zilikuwa ni tuhuma zilizoambatana na swali kwa wakati mmoja.
“Ndio,nimeipata”
Bora asingejibu chochote,kinywa cha Ahmed kilitoa harufu mbaya ya pombe, hiyo ilizidi kumtia bosi wake hasira,akapata jibu moja kwa moja kwamba Ahmed alikesha bar akilewa kama sio siku hiyo basi usiku wa jana.
“Umeisoma?”
“Hapana”
“Ulikuwa unajua kwamba leo una kikao?”
“Bosi nili…”
“Shut up stupid,nimekuuliza swali nijibu swali”
Sauti ya mkuu wake wa kazi Mr.Kibangala,ilienea chumba kizima,akapiga meza kwa hasira,hiyo ilionesha ni kwa kiasi gani amechukia.
“Ndio nilikuwa najua nina kikao”
“Kwahiyo ukafanya makusudi kisa baba yako ni rafiki yangu?Listen Ahmed,nina uwezo wa kukubadilikia dakika mbili usiamini,kilichokufanya uchelewe ni kitu gani?”
Hapo Ahmed akatulia kidogo,mkononi alikuwa ameshika baasha kubwa akaanza kuifungua huku akijitetea na kusema kwamba aliamka asubuhi, wakati yupo njiani,alidondoka ghafla na kupoteza fahamu,akapangilia uwongo huku akimuangalia bosi wake machoni, yupo siriazi.
“Ulidondoka sababu,ulikunywa pombe.Ahmed unanuka sijui gongo,ulitaka uje asubuhi ukiwa hivyo?Are you serious,out of my office!GET OUT…”
“Lakini bos..”
“I said GET OUT”(Nimesema toka nje)
Mzee Kibangala alifoka kwa hasira huku akiwa amesimama wima,amenyoosha kidole kumaanisha kwamba Ahemd atoke nje ya ofisi hiyo mara moja,hakuishia hapo akamwambia endapo angeendelea kubaki mahali hapo, angeitiwa polisi na kuwekwa mahabusu,Ahmed hakuwa nala kufanya alivyotaka kuzungumza kwa niya ya kujitetea haikuwa rahisi,ikambidi asimame na kutoka nje.Ambapo huko kila mtu alimshangaa!
“Ahmed”
Ni sauti ya Aneth,ndiyo iliyomshtua baada ya kutoka nje.Badala ya kuitikia aligeuka na kumuangalia kwa macho yaliyotia huruma.
“Naam”
“Usijali,bosi ndio alivyo.Hapo alipo ana stress,cha kufanya njoo kesho.Atakuwa keshatulia tayari”
“Ameniambia nisirudi tena”
“Ahmed,nisikilize mimi nachokwambia.Huyu mzee mimi namjua,nimefanya kazi hapa, huu mwaka wa tisa,nachokwambia njoo kesho umevaa vizuri.Ingia ofisini kwako fanya kazi kama kawaida”
“Kweli?”
“Ndio Ahmed,na pole kwa kila kitu”
“Ahsante”
Hapo hakuwa tena nala kuongeza wala kuzungumza kitu kingine,alichokifanya ni kutafuta pikipiki,impeleke mpaka nyumbani ili akapumzike,njiani hakuacha kuzilaumu pombe!

****
Shida ya Rhoda Denis,haikuisha.Aliendelea kuteseka akiranda randa huku na kule,akitafuta kiasi cha pesa alichokuwa anadaiwa na Baba mwenye nyumba sambamba na mzigo wake ulioshikiliwa na TRA alipie kodi,ilikuwa ni lazima aukomboe ili maisha yake yaendelee.Kila rafiki yake,aliyemtafuta alimtosa na kumchinjia baharini, baadhi walimpa pole lakini wengine walimsaidia kwa kumtumia pesa,hiyo haikutosha.
Mtu wa pekee ambaye aliamini atakitoa kitanzi hiko shingoni kwake ni Yusrath peke yake,aliamini hilo kwa asilimia mia moja!Lakini cha ajabu alivyomtumia meseji,alijibiwa kwamba hatoweza kumsaidia sababu pesa hizo hana.Akazidi kumpigia zaidi na zaidi lakini wapi,mwisho wa siku simu zake hazikupokelewa kwa hasira akatuma meseji ya kwamba angesema kila kitu kuhusu siri nzito ya watoto mapacha,lakini hilo pia lilikuwa bure.
“Lazima nipajue kwake na atanikoma,naenda kuharibu”
Siku hiyo aliapia kufanya jambo hilo,mikakati ya kuanza kupasaka kwa Yusrath ikaanza mara moja,hilo halikuwa tatizo akamtafuta msichana mmoja rafiki yake anayeitwa Shakira,akiamini kabisa kwamba ni lazima atakuwa anapajua.
“Yusrath,nilisikia anaishi Kibangu lakini sijawahi kufika kwake”
“Aise nina shida naye”
“Kwani namba zake hauna?”
“Nina shida ya kupajua kwake”
“Mpigie simu,akuelekeze”
“Sitaki kumpigia”
“Sawa,ngoja nikupe namba za dada mmoja hivi”
“Nani huyo?”
“Anaitwa Marcelina”
“Ndio nani?”
“Ndio mtu wa karibu,anayepafahamu kwake.Kama sio huyo basi atakupa mtu mwingine”
“Sawa Ahsante,nitumie namba zake”
“Nakutumia”
Mchakato wa namba ukaanza mara moja,hazikupita dakika mbili akawa tayari amepewa namba za Marcelina,bila kupoteza muda akampandia hewani na kumueleza shida yake, hakutaka kuzunguka mbuyu na kuleta hadithi nyingi.
“Ubungo Kibangu,ngoja nikuandikie kwenye meseji.Nipo kwenye kelele”
“Shukrani sana,nashukuru mno”
Marcelina akawa amemuuza mwenzake bila kujijua,laiti angejua angempigia simu kwanza Yusrath na kumwambia kinachoendelea.Bila kupoteza wakati akashika simu yake vizuri na kuanza kuandika akitoa ramani ya kufika anapoishi Yusrath,mchana huo huo Rhoda Denis, akatafuta daladala mpaka Ubungo,ambapo hapo ili iwe rahisi kwake akatafuta pikipiki na kumuelekeza mmoja wa madereva.
“Hapo,napafahamu sista.Panda mchuma twende,shika helment”
Jambo hilo lilimfurahisha sana Rhoda,akatamani kufika mapema!Hata hivyo haikumchukua muda mrefu akawa amewasili,nje ya geti la rangi jeusi.Akachukua simu yake ili kuangalia maelezo.
“Yes,ndio hapa kaka”
Akateremka kwenye pikipiki na kumpa dereva ujira wake,akatembea mpaka getini na kugonga mara moja.Alivyoangalia vizuri akagundua kwamba geti lipo wazi,akaingia taratibu mpaka ndani ya uwanja akaona gari limepaki nje,akatembea adoado mpaka mlangoni,hapo aligonga na kusubiri ambapo baada ya sekunde kama tatu hivi,akatokeza msichana mdogo wa makamo.
“Shikamooo”
“Marahaba,nimewakuta wenyewe?”
“Mama yupo,baba hayupo.Karibu ndani”
Dada wa kazi badala ya kumuita bosi wake kwanza, yeye alimkaribisha Rhoda Denis,ambaye alipitiliza mpaka ndani.Vitu vya gharama alivyovikuta ndani ya nyumba akapata jibu tosha ya kwamba Yusrath asingeshindwa kumsaidia kiasi cha pesa alichohitaji,niya ya kufika hapo ilikuwa ni lazima atumbue jipu na kama mbwai iwe mbwai na ikiwezekana urafiki ufe siku hiyohiyo, kifupi siku hiyo alikuwa mahali hapo kwa shali.
“Haaa,Rhoda!”
Yusrath alipigwa na bumbuazi la waziwazi,hakutegemea kuuona ugeni kama huo nyumbani kwake,kilichomfanya ashangae sio kumuona Rhoda, kilichomstusha, kajuaje anapoishi? Nani kamuelekeza.
“Ndio mimi”
Rhoda akajibu,bila kucheka hiyo ilimaanisha hakukuwa na dalili yoyote ya amani eneo hilo.
“Nilitaka nikupigie leo”
“Ili iweje?”
“Nikutumie pesa unayotaka”
“Sina shida na pesa,kilichonileta hapa.Nataka kumwambia mumeo ukweli wote”
Baada ya kumalizia Sentensi hiyo,ghafla mlango ukafunguliwa kila mtu akageuka,Rhoda akashtuka Yusrath akahisi kama mapigo yake ya moyo yamesimama kwa muda.

****
Hasira zilimpanda katika kiwango cha juu kabisa,akaanza kutetemeka kama mgonjwa mwenye homa ya usiku,hali hiyo ilikuwa ni mbaya sana.Kitendo cha bosi wake kumfokea kama mtoto mdogo ndiyo kilimfanya ahisi uchungu ajabu,mbaya zaidi barua aliyosoma ilimfanya ahisi kuchanganyikiwa alikuwa amesimamishwa kazi kwa muda usiojulikana,hakuelewa angefanya nini bila kazi.Mbele yake aliona giza kubwa,akiwa juu ya pikipiki aliwaza vitu vingi sana,sura ya mkewe Yusrath ikamjia kichwani, moyo wake ukazidi kumuuma baada ya kuunga unga matukio,akapata jibu la kwamba kila kilichotokea Yusrath ndiye aliyesababisha sababu bila kuchepuka wenda asingeenda kunywa pombe na matokeo yake,kusimamishwa kazi.Hiyo ilimaanisha lazima amueleze siku iliyopita alikuwa wapi na nani,kifupi hasira zote siku hiyo zingeenda kumuangukia Yusrath,pikipiki ikazidi kupepea mpaka walivyofika kwake,Ubungo Kibangu!Ilivyosimama,akamlipa dereva ujira wake na kuanza kutembea kwa kasi,aliomba sana Mungu, amuepushe sababu hasira zake zilifanya mpaka macho yake yabadilike rangi,yakawa mekundu kama mtu aliyevuta cha Arusha,kwa kasi akafungua mlango!
“Sina shida na pesa tena,kilichonileta hapa.Nataka kumwambia mumeo ukweli wote”
Hiyo ndiyo sentensi aliyokumbana nayo Ahmed baada ya kufungua mlango na kuingia ndani seblen!Rhoda alikaa kimya baada ya Ahmed kutokeza.
“Shikamoo Shemeji”
Rhoda,akasalimia.Wakati huo wote Yusrath alitetemeka akahisi kama mwili wake umepalalaizi,akatamani ardhi ipasuke aingie ndani, imfunike.
“Ukweli gani unataka kuniambia?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed huku akihema kwa jazba,mikono yake inatetemeka!Macho yake yanazidi kuwa mekundu.



Kama siku hiyo Yusrath,angepimwa mapigo ya moyo yangeonesha yanadunda mara mia saba kwa sekunde!Hofu ilimtanda,akashindwa kuongea wala kumeza mate,kitendo cha Rhoda Denis kutaka kuropoka kuhusu siri ya watoto mapacha,mbele ya Ahmed ingemaanisha kwamba uhai wake ungekuwa ni asilimia ishirini kuishi kwani alimuelewa sana Ahmed,dalili za kupigwa kipigo cha mbwa koko mpaka apasuke zilikuwa mbioni kutokea siku hiyo,hakuelewa sura yake angeiweka wapi baada ya hapo.Kimoyomoyo alimuomba Mungu wake, Rhoda Denis asiropoke chochote kile,akapiga dua zote anazozijua yeye.
“Nakusikiliza”
Ahmed akasema,bado macho yake yalikuwa mekundu!Sentensi aliyoongea Rhoda ilimuweka njia panda na alitaka kujua ni kitu gani mkewe amefanya.
“Shemeji…”
Rhoda akaita na kumuangalia Yusrath,akamuona namna gani anavyohaha na kutetemeka mbali na hapo alitia huruma akawa mdogo ghafla kama kidonge cha ‘Pilton’
“Mkeo nilimkopesha pesa mwaka juzi,kipindi yupo dukani pale Kariakoo!Aliv….”
“Shilingi ngapi?”
Ahmed akamkatisha,hakutaka kusikia stori nyingi za abunuasi na hadithi za hapa na pale.
“Milioni mbili”
“Ikawaje?Wewe,hiyo milioni mbili ilikuwa ya nini?”
Swali hilo lilimlenga Yusrath ambaye hakuamini kama soo hilo limepinduliwa,hiyo ilimaanisha nayeye ajiongeze ili kuepuka kikombe kinachomkabili.
“Niliibiwa pesa za mahesabu,pale dukani Mme wangu.Nikaogopa kumwambia baba ndio nikamuomba Rhoda anikopeshe”
“Yaani uliibiwaje?”
“Baby,sijui itakuwa chuma ulete”
“Chuma ulete!Ndio nini?”
Ahmed akataka ufafanuzi kidogo,mazingira ya kishua naya geti kali, aliyokulia hakuelewa nini maana ya chuma ulete.
“Ni mambo ya kishirikina baby,nguvu za giza”
“Yaani nini,mbona sikuelewi?Sijawahi kuona mimi mchawi anaiba pesa,walikuja usiku au?”
“Sio hivyo baby”
“Kumbe nini?”
Siku hiyo Yusrath,aliulizwa maswali kama polisi.Hakutofautishwa na mtuhumiwa aliyekuwa kizimbanni anajibu mashtaka.Ikabidi kwa utaratibu na utulivu aanze kuelezea jinsi Chuma ulete inavyokuwa,akasema namna pesa ikichanganywa na nyingine zinachukuliwa zote,Kwa Ahmed ilikuwa ni vigumu kuamini vitu kama hivyo lakini hakuwa na jinsi, ilibidi aitikie ili asifanye mambo yawe marefu.
“Jina lako nani?”
Swali hilo aliulizwa Rhoda.
“Mimi,mimi naitwa Rhoda Denis”
“Hiyo pesa nitakulipa mimi,leo nina kiasi kidogo cha pesa.Nitakupa laki tano,hiyo nyingine tuwasiliane.Naomba usimsumbue mke wangu”
“Nimekuelewa shemeji”
Kwa Yusrath ilikuwa kama mazingaombwe kwake kwani jambo kama hilo hakulitegemea hata kidogo,moyo wake ulipiga sambasoti kwa furaha, baada ya Ahmed kuelekea chumbani.
Ahmed hakuwa na jinsi,ilikuwa ni lazima alipe deni la mkewe ili kuepuka fedhea,hata siku moja hakutaka mkewe adhalilike ndiyo maana akaamua kulivaa jambo hilo kama lake,ni mkewe?Angefanya nini?Ilibidi acheze nafasi ya mume,ndiyo maana akaingia chumbani,akanyoosha moja kwa moja mpaka kwenye kabati ambapo huko alivuta ‘draw’ la chini,alipoweka pesa za akiba kwa ajili ya Yusrath nayeye.
Kwa hesabu ya haraka alikumbuka aliacha kiasi cha shilingi milioni moja na nusu,lakini ilibakia laki tisa sababu Yusrath alitoa pesa za matumizi ya watoto.Kitendo cha kuvuta kilimfanya ayatumbue macho yake kama mjusi aliyebanwa na mlango,hakukuwa na pesa yoyote ile,akajipa moyo na kudhani wenda kabati la juu yake,akafanya hivyo lakini hakukuwa na pesa pia,mapigo yake ya moyo yakaanza kuongezeka zaidi kudunda!
“Yuuuuuusrath”
Sauti hiyo,ikatoka ikafika mpaka sebleni.Yusrath akaelewa nini maana yake, kitendo cha kuitwa jina lake kamili kilimaanisha Ahmed amechukia sana,akamtizama Rhoda kwa macho ya wasiwasi kisha kuanza kutembea akaingia mpaka chumbani,aliyoyaona akajua tayari amekwisha,milango ya makabati yalikuwa wazi ma ‘draw’ yamevutwa vutwa,tayari alishajua ni kitu gani ameitiwa.
“Pesa ziko wapi?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kuuliza Ahmed huku akiwa amekunja ndita,anamtizama Yusrath kwa macho makali.
“Pesa!?”
Haikujulikana kama ameuliza nayeye swali ama hakusikia vizuri,Ahmed hakujibu akabaki anamtizama akiamini kwamba swali alilouliza limeeleweka sababu aliuliza kwa sauti, ndiyo maana akaendelea kumuangalia akisubiri jibu la wapi pesa zilipo?
“Pesa,Mume wangu.Nilimtumia Shangazi alipata shida,mtoto wake alitakiwa kufanyiwa operesheni ya moyo nikamtumia,samahani lakini sikukwambia Mme wangu”
Kila alichozungumza Yusrath kilikuwa cha kubuni na alifanya hivyo akiwa katika harakati za kujitetea ili msalaba huo wa moto usimwangukie,hapo alipo alikuwa anazidisha makosa na alishaelewa kilikuwa ni kifo cha nyani,miti yote imeteleza siku hiyo.
“Unasemajeeee?”
Ahmed akauliza kwa mshangao, ulioibua hasira zingine.
“Mtoto wa Shangazi alilazwa,nikamtumia kwa ajili ya matibabu.Hakuwa ana pesa ya dawa”
Tayari Yusrath akawa amechanganya mlenda na kachumbari,akawa ameongea vitu viwili tofauti.
“Mbona sikuelewi,Yusrath.Pesa ziko wapi?”
“Mme wangu..”
“Nachotaka kujua,pesa zipo wapi?”
“Baby,nilishakwambia zilipo…”
Kitendo cha kuongea hivyo akaanza kurudi kinyumenyume kama gari la mizigo lililofeli breki kilimani,hiyo ni kutokana na Ahmed kuanza kumfuata. Kuendelea kusubiri hapo,ingemaanisha kipigo chake kingekua cha paka shume,hilo ndilo lilikuwa linaenda kutokea sababu Ahmed alipandwa na hasira ajabu,alivyounga matukio ya kufukuzwa kazi,kupiga simu jana yake Kwa Yusrath hayupo nyumbani na vilevile,pesa kupotea katika mazingira ya kutatanisha.
“Au unataka kuniambia Chuma ulete alikuja humu ndani?Akachukua pesa eeeh”
Ahmed aliuliza huku akimsogelea Yusrath,chumba hiko kilikuwa kikubwa ndiyo maana Yusrath aliweza kurudi kinyumenyume akajikuta amejigonga kupuu!Kwenye mlango wa bafuni,hapo hakuwa na jinsi zaidi ya kuingia bafuni na kujifungia kwa ndani na funguo.
“Yusrath,toka huko bafuni.Uniambie pesa zilipo”
Kuanzia hapo Yusrath hakuongea chochote,alibaki bafuni akitamani kila kitu kibadilike,aliogopa kwa kiasi cha kutosha,alichokifanya Ahmed ni kutoka mpaka seblen.
“Rhoda”
“ABEE SHEMEJI”
“Ngoja,nikupe namba zangu za simu.Tuwasiliane,by next week nitakutumia nusu ya pesa zako!Samahani kwa usumbufu”
“Usijali shemeji ni mambo ya kawaida,ilikuwa nimsamehee sema kuna mambo yamenikaba”
“Nipigie simu,next week”
“Sawa ahsante,niagie kwa Yusrath”
Ahmed,hakujibu kitu alichokifanya ni kuingia jikoni na kuwaangalia watoto wake wanavyonyonyeshwa maziwa ya kopo.
“Wakitoka hapo,unaenda kuwalaza au?”
Ahmed akamuuliza Hadima.
“Ndio Baba”
“Hakikisha,wanashiba.Hawajakusumbua?”
“Hapana baba”
“Akija,mtu kuniulizia mwambie sipo”
Ahmed alivyomaliza kutoa maagizo hayo,akashusha pumzi ndefu na kuangalia mlango wake wa chumbani,akatembea na kunyonga kitasa!Alivyoingia hakumkuta Yusrath kumaanisha kwamba bado yupo bafuni,alivyojaribu kufungua mlango ukawa bado umefungwa.
“Yusrath,fungua mlango”
“Ahmed,siw..wezi…Sitaki”
“Kwanini?”
“Utani..piga”
Yusrath alijibu kwa kwikwi,alikuwa tayari analia.
“Kwanini nikupige?”
“Ahmed,siwezi kufung…ua”
“Naomba ufungue,tuongee tafadhali”
“Sitaki,siwe..zi niache nikae humuhumu”
Hakukuwa na dalili yoyote ile ya Yusrath kutoka bafuni,alichokifanya Ahmed ni kutoka chumbani,akabeba funguo za gari.
“Hadima natoka,make sure.Mama ako anakula”
“Sawa Baba”
“Njoo,unifungulie geti”
Ki ukweli alimpenda sana Yusrath,sababu alielewa ni wapi wametoka.Kuendelea kubaki nyumbani ingemaanisha kumjeruhi vibaya sana mkewe, ndiyo maana alitaka kukaa sehemu iliyotulia,ikiwezekana amtafute Benjamin Ngowi, amueleze kila kilichotokea ili apate ushauri.Akiwa anageuza gari,akachukuwa simu yake na kuanza kutafuta namba za rafiki yake huyo ili walau apate ushauri.

*****
Tangu aonane na Ahmed hotelini,mahusiano yao hayakuwa mazuri tena!Kuna vitu vingi sana alivikumbuka,mapenzi yao ya dhati waliyokuwa chuoni Makumira,hata hivyo Ahmed alikuwa ndiye mwanamme aliyemuonesha mapenzi ya dhati!Vitu vingi sana vilipita kichwani kwake,akawa anatafuta kila sababu ili aachane na Dokta Sajo,japokuwa Ahmed alikuwa tayari ni mume wa mtu lakini hilo hakujali,aliamini Ahmed ni wake na hivyo ndivyo walivyohaidiana tangu wanasoma chuoni Makumira.Dokta Sajo,hakulijua hilo.
“Nilishakwambia,siwezi kurudi Afrika Kusini,subiri kwanza nikae na wazazi wangu.Alafu bado kuna upelelezi unaendelea,tangulia mimi nitakuja”
Hayo ndiyo yalikuwa majibu ya Hajrath,tena hakuongea kwa ustaarabu.Alimwambia Dokta Sajo kwa kufoka na hasira,hakumchukulia tena kama zamani, kwa wakati huo alimuona kama kaka yake tu,mbali na hapo hakuwa ana hisia naye tena,kichwani mwake alikuwepo Ahmed tu na wala sio mtu mwingine.Akatumia kigezo cha kwamba ana kesi anatakiwa akamilishe ushahidi ili Florian Fredrick, pamoja na watu waliohusika kutaka kumuuwa wawekwe mikononi mwa sheria.
Siku hiyo Hajrath alilia kama mtoto mdogo baada ya kuonana na Florian Fredrick mahabusu,hakutaka kuamini kama mwanamme huyo ndiye aliyemuuza na kutaka kumuua,moyo wake ulichoma kama pasi ya mkaa!
“Ndi..o yey..e”
Hajrath alizungumza huku akibubujikwa na machozi,akakumbuka kila kitu kilichotokea nyuma,akawa kama anaangalia mkanda wa filamu ya kutisha akajiona, alivyokuwa anasafirishwa na kuchomwa madawa ili alale,sio hivyo tu alivyokumbuka risasi alizopigwa akalia na kushindwa kuendelea kuongea,akabaki analia machozi kuna kama lidudu lilimkaba kohoni ndiyo maana akashindwa kuongea tena.
“Usilie dada,futa machozi”
Sirgent Abdallah Mafutaa,aliyekuwa na jezi za kipolisi.Alionekana kuguswa na mkasa huo,akampa kitambaa ili ajifute machozi,ikaonekana kama amechochewa akazidi kulia zaidi.Historia ya Hajrath kama ingeandikwa vitabuni na waandishi maarufu nchini Tanzania kama Eddazaria Msulwa ama Hussein O Molito basi wangeuza nakala mia moja kwa siku,mkasa wa Hajrath ulikuwa wa aina yake,kila aliyekuwa ndani ya chumba hiko,alikaa kimya akimsikiliza wengine walishindwa kuvumilia Kamanda wa kituo cha polisi Oysterbay Neema Masud nayeye alikuwepo,akashindwa kujizuia akatoka nje.
“Huyo mtuhumiwa,kesho apandishwe mahakamani.Faili lake,liende mahakamani”
Kamanda Neema Masud,alitoka huku nyuma akiacha maagizo hayo na hilo halikuwa ombi bali ni amri.
“Sawa,mkuu”
Hilo likaisha,kilichotakiwa ni utekelezaji tu nasi vinginevyo!Bila kujua kwamba nyuma ya kila kitu kuna mwanamke hatari aliyesuka mipango hiyo na yupo hai, anayeitwa SPORAH TREVEZ.

********
Ahmed hakuweza kukaa na dukuduku hilo ndani ya kifua chake,ilikuwa ni lazima apate ushauri wa jinsi ya kulitatua.Hakumficha Benjamin Ngowi,akamwambia kila kitu kilichotokea kuhusu ndoa yake mpaka alivyofukuzwa kazi na misukosuko yote,jambo hilo lilimshangaza sana Benjamin Ngowi na alisikitika kwa wakati mmoja sababu alimchukulia Ahmed kama ndugu yake wa damu.
“Pole ndugu yangu,ni changamoto kwenye maisha.Usiumie sana,kubali kwamba lishatokea.Kingine wazungu wana msemo unaosema, What doesn’t kill you,make you stronger”
Benjamin akaanza kutoa lisala.
“Alafu kitu kingine Ahmed,kama unahisi pombe haikufai.Achana nayo,sio lazima unywe”
“Ndio maana leo nataka ninywe soda”
“Sijakwambia uache,kama unahisi haikufai acha ama punguza”
“Nitajitahidi kuacha,sasa utanisaidiaje?”
“Kwenye lipi kazi?Ama Familia?”
“Yote”
“Well,kwenye familia sio mzuri saaana sababu sijaoa bado ingawa nina mawazo tu ya hapa na pale”
Benjamin Ngowi,siku zote alipewa busara,katika swala la kutoa ushauri mwanamme huyo alikuwa nambari moja,hakuwa mtu mzima sana alikuwa kijana wa makamo kati ya miaka 27-32 wengi waliamini karama hiyo alipewa na Mungu.
“Nakusikiliza Benja”
“Usimfuatilie Mkeo,mwache awe free.Give her freedom!Kwanza unamfuatilia ili upate nini?Ngoja nikwambie ukweli,i have a girlfriend,nipo naye huu mwaka wa nne,sijawahi kushika simu yake!Wala kumfuatilia fuatilia”
“Inawezekana vipi hiyo?”
“Sababu sitaki stress,najua nikishika simu yake.Kuna vitu ambavyo sivipendi,nitakuta kwenye simu yake,nitaumia.Ngoja nikwambie kitu Ahmed,kuna vitu kama unaweza kuviepuka,epuka kushika shika simu ya mkeo,hakuna kitu kinachovunja mahusiano kama simu”
“Ni kweli”
Siku hiyo Ahmed akawa yupo darasani,anasikiliza somo yupo makini kabisa na chupa yake ya Coca- cola mezani,hakuwa ana uhakika kama angetekeleza anayoambiwa ama atarudia tabia yake ileile ya kumchunguza mkewe maana wivu wake haukuwa na kipimo.
“Nina rafiki yangu mmoja,nadhani unamjua”
“Yupi?”
“Alikuja kwenye harusi yako,nilishawahi kukwambia nina rafiki yangu ni daktari yupo South Afrika,alikuwepo kwenye harusi yako”
“Alikuwepo?”
“Ndio,sasa nayeye ana demu wa kibongo.Anamzingua kishenzi.Atakuja leo hapa na demu wake”
“Leo?”
“Ndio,muda sio mrefu wataingia hapa.Jamaa kafa kaoza kwa huyo demu,aliniambia akisikia siku huyo mwanamke ana mchit,ataua mtu”
“Sasa atamuua nani,demu au?”
“Huyo jamaa,atakayemchukulia.Lakini jamaa ana haki,huyo demu ana wezeree balaa”
“Acha bwana”
“Alafu sasa ana swaga,ana sura nzuri.Inshort jamaa kachagua,utamuona mwenyewe”
Ahmed akawa ana hamu ya kumuona mwanamke huyo mlimbwende, anayemwagiwa sifa,stori za hapa na pale ziliendelea kama kawaida,Benjamin Ngowi akasimama huku akiwa ameshika simu yake mkononi, kumaanisha kwamba ilikuwa inaita,alivyorejea baada ya dakika moja, akamwambia kwamba wageni wake tayari wamefika, wapo nje,hivyo anaenda kuwapokea!Mawazo ya Ahmed bado yalikuwa kwa mkewe moyo wake uliendelea kumuuma,alimpenda sana Yusrath lakini kwake ilionekana kama fungu la kukosa,akiwa katikati ya mawazo mengi nyuma yake, alisikia kelele nyingi na moja ya sauti alizosikia ilikuwa ya Benjamin Ngowi,moja kwa moja akajua wageni hao tayari wamefika lakini hakutaka kugeuka nyuma,akaendelea kuwapa mgongo.Kabla ya sekunde kuisha Benjamin akawa amefika mezani.
“Ahmed,huyu ni rafiki yangu anaitwa Dokta Sajo.Doctor Sajo,meet my Friend Ahmed”
Benjamin akatoa utambulisho mfupi na kusimama kwa heshima ili atoe mkono,wakapeana mikono huku wote wakitabasamu.
“His fiance”(Mchumba wake)
Moyo wa Ahmed ukapiga paa!Akahisi kama yupo ndotoni,mwanamke aliyemuona mbele yake alimuogopesha,bado hakuamini macho yake kama anayemuona mbele yake ni Hajrath,akajikuta anamuangalia bila kuongea chochote.Hajrath ndiyo usiseme,alihisi kama damu yake imeacha kutembea kwa muda,akabaki ameganda kama sanamu anamtizama Ahmed!


Ulikuwa ni mshtuko mkubwa uliojenga sura tofauti kwa watu hawa wawili ambao walishawahi kuwa wapenzi miaka kadhaa nyuma iliyopita chuoni Makumira, kila mmoja alikuwa anawaza vitu vyake kichwani,Hajrath akahisi kama ameishiwa nguvu za miguu kabisa mapigo yake ya moyo yalimwenda mbio sana,akabaki bado ameganda anamtizama Ahmed, jinsi alivyokuwa bado mtanashati,tena mbaya zaidi alikuwa amenenepa mashavu yametokeza yamevimba yakawa kama mimba ya panya,kitambi cha wastani kimetokeza shati alilovaa lilionesha hilo,ngozi ya mwanaume huyo ilibadilika akawa mweupe kiasi chake, tofauti na alivyomuona mara ya mwisho hotelini ama alivyokuwa chuoni Makumira,kifupi Ahmed bado alikuwa ‘Handsome boy’Hajrath hakuishia hapo,moyo ukamuuma baada ya kuangalia kidole cha Ahmed akaona kina pete ya ndoa inayong’aa, ikionesha kwamba bado ni mpya.
“Ahmed…Huyu ndiye Yule shemeji yako”
Benjamin Ngowi, ilibidi aingilie katikati,kuna kitu alianza kuhisi hiyo ni baada ya kuangalia chupa ya Ahmed iliyokuwa na soda ya Coca Cola,akajua ni lazima Ahmed alichanganya Konyagi ama kilevi chochote kwani alishaelewa ni lazima pombe zake zimtume kwenye ngono,hivyo ndivyo Benjamin Ngowi alivyodhani na picha alilopata ni kwamba Ahmed amemzimia mwanamke huyo ambaye alitambulishwa kama shemeji, bila kuelewa historia ya watu hao wawili,kuingilia kati kulimfanya Hajrath ashushe pumzi na kukosa amani,japokua alikaa kwenye kiti lakini mawazo yake yalikuwa kwa Ahmed,mwanamme aliyetokea kumpenda kuliko yoyote yule chini ya Jua la Mungu ndiyo maana alikunywa sumu kwa ajili yake,hakuelewa ni kitu gani akifanye!Alikuwa katika giza nene ambalo asingeweza kuiona nuru mbele daima kwani Ahmed alikuwa tayari ni mme wa mtu,hilo hakujali sana sababu aliamini kivyovyote vile atafanya juu chini ili siku moja awe wake kwani hakuna linalo shindikana chini ya Jua.
Dokta Sajo hakuwa mwenye habari japokuwa tabia za Hajrath zilimkera lakini alipanga kwenda naye hivyohivyo sambamba,akiamini kwamba ipo siku moja ambayo haina jina Mwanamke huyo angebadilika na kuwa kama zamani,alikuwa yupo radhi kuvumilia hata ingemchukua miaka mingapi.
Hakuhisi kabisa kama mwanamme aliyekuwa jirani yake ndiye mkandarasi wa penzi lake kuyumbishwa,hata hivyo hakutaka kulikuza jambo hilo na kumfaidisha kila mtu,ndiyo maana mtu wa kwanza kumwambia tatizo hilo alikuwa ni Benjamin Ngowi tu,akiamini ndiye mtu pekee mwenye busara na msiri ambaye angempa ushauri wa kitu gani akifanye.
“What do you prefer?What is your name again?”(Unatumia nini?Jina lako nani tena)
Swali hilo lilimlenga Ahmed,sababu muda wote alionekana kimya hajachangamka hata kidogo,hiyo ikamlazimu Dokta Sajo atake kumdadisi, hata hivyo upole wa Ahmed ulimvutia kwa kiasi cha kutosha,hapo ndipo akapata wazo la kwamba ikiwezekana mwanamme huyo asimamie harusi yake.
“Are you Married?”(Umeoa)
Lilikuwa ni swali lingine la nyongeza lililomlenga Ahmed,hata kabla hajajibu la kwanza,hiyo ikamfanya ababaike na kutoelewa ajibu lipi aanze na lipi,akatulia kidogo na kujibu swali kwanza akisema kwamba kichwa kinamuuma na muda wowote angeaga na kuondoka zake,swali la pili akaitikia ndio ameoa na ana watoto tayari.
Jibu hilo kwa Hajrath likawa kama bomu lililolipuka ghafla,moyo wake ukachoma kama pasi akatamani kulia lakini akajizuia,alihofia angeyaruhusu machozi yake, kungeibuka maswali mengi sana hasa kutoka kwa Dokta Sajjo!Ahmed hakuwa mwenye raha hata kidogo,kuna vitu vingi sana vilimsumbua sana kichwani,aliwaza kuhusu kibarua chake kilichoota nyasi na kingine juu ya mkewe kumzingua, hata hivyo uwepo wa Hajrath ulimfanya ajisikie hali ya utofauti.Hiyo ilimfanya akose raha ya maisha,alivyoangalia saa yake ya mkononi ilisoma saa tano usiku tayari,ilikuwa ni lazima awahi nyumbani ili kesho yake asubuhi na mapema awahi kazini kama alivyoshauriwa na Anneth,hapohapo hakutaka kupoteza wakati akamtizama Benjamin.
“Mimi naona,niwaache.Sijisikii vizuri.Naomba mniruhusu nikapumzike”
“What is he saying?”(Anasema nini)
Dokta Sajjo,akataka kufafanuliwa kwa Kiingereza, akitaka kujua Ahmed amezungumza nini,Benjamin akageuka siku hiyo na kuwa mkalimani wake,akatafsiri. Jambo hilo likamfanya Dokta Sajjo achukie kwani alipenda Ahmed abaki mahali hapo,akaomba wakae kidogo lakini Ahmed alisimamia msimamo wake,akitumia ndoa yake kama ngao na gia ya kuondokea,akaingiza mkono mfukoni na kutoa funguo za gari, akatembea na kutoka nje bila kumuaga Hajrath.
“I wan’t to susu”(Nahitaji kukojoa)
Hajrath nayeye akasimama,hakuwa na niya yoyote ya kwenda msalani lengo lake lilikuwa ni moja tu,kumfuata Ahmed kwa nyuma.Akapiga hatua mbilimbili mpaka nje ambapo huko alianza kutizama huku na kule,akamuona Ahmed anafungua mlango wa gari,akatembea kwa haraka na kumshika bega.
“Ahmed”
Hajrath akaita kwa upole huku akimtizama Ahmed machoni.
“Yes”
“Nilikukosea nini?Mbona siku ile ulinipa namba feki?Ahmed kweli,tumefikia huko?”
Hajrath alilalamika,akaikumbuka siku waliyokutana Hotelini, akamuomba Ahmed namba ,hatimaye namba hiyo haikuwa hewani miaka nenda rudi,hiyo ikamfanya agundue moja kwa moja ya kwamba alipewa namba za treni.
“Hajrath,naomba niende tafadhali”
“Ahmed,nimekukumbuka sana”
“Hata mimi lakini acha tu,ibaki historia”
“Usiseme hivyo Ahmed”
“Unataka niseme nini?”
“Bado unaishi kwenye moyo wangu”
Hapo Ahmed alitabasamu na kuangalia pembeni kwa mapozi,haikueleweka kama alicheka kwa dharau ama nyodo!
“Unanichekesha ujue,si una jamaa ako?”
“Ndio ninaye,lakini sifurahii mapenzi”
“Hilo sio swala langu”
“Ahmed please”
Hapo Hajrath alizungumza kwa hisia kali sana,moyo wake ulimuuma lakini hakuwa na jinsi!Hakujali Ahmed atamchukuliaje lakini ilimradi keshautoa mzigo uliokuwa unamsumbua moyoni mwake,hiyo ikawa haitoshi akamsogelea Ahmed karibu kabisa na kumpiga busu shavuni.
“Nakupenda Ahmed,daima nitakupenda”
Hapo Ahmed hakujibu chochote,akaingia ndani ya gari akaliwasha na kuondoka zake,kurejea nyumbani kwake akiwa anatafakari maneno ya Hajrath kama yalikuwa yana ukweli ama ni usanii na kanjanja za kibongo,ghafla tukio la Florian Fredrick likamjia kichwani siku moja wakiwa kantini chuoni Makumira,alimnyonya mdomo mbele yake.
“Wanawake wengine bwana”
Ahmed akajisemea huku akiangalia ‘site miiror’ ya nje ahakikishe kama hakuna magari ili aingize gari barabarani.

*****
Ukimya wa Florian Fredrick ulizua maswali mengi kichwani kwake,kiasi kwamba alikosa raha ya maisha.Simu za mwanamme huyo hazikuwa hewani,wasiwasi ukawa mkubwa sana,aliamini kitendo chake cha kuwasili nchini Tanzania,angepigiwa simu lakini ilikuwa tofauti kabisa,akajipa moyo wenda atapigiwa simu ama kutumiwa ujumbe kwamba Frolian Fredrick amefika salama,lakini wapi,haikuwa hivyo miezi kadhaa ikapita hapo ndipo taa nyekundu ikawaka kichwani kwake kwamba ni lazima Frolian wake,amepatwa na tatizo kubwa sababu haikuwa kawaida ya mwanamme huyo kukaa kimya kwa kipindi kirefu namna hiyo,mbali na hapo alimmisi mwanamme huyo kitandani sababu alikuwa ni fundi na hodari kwenye sita kwa sita,hiyo ilizidi kumfanya atake kujua nini kinaendelea.
“Au kapata Malaya wa kitanzania,kampagawisha”
Sporah Trevez alijiuliza maswali lukuki yaliyokosa majibu,kukaa kimya bila kuchukua hatua yoyote kusingeleta majibu yakinifu,hapo ndipo akapata wazo la kumtafuta mwanamme mmoja gaidi anayeitwa Tiger,akiamini kwa kumtumia mtu huyo angepata jibu lake ndani ya masaa yasiyopungua arobaini na nane,Sporah Trevez siku zote alipenda kukaa kihasarahasara,wenda kuishi sana ughaibuni kulimfanya ajenge mazoea hayo ya kukaa nusu uchi,ungebahatika kuitwa nyumbani kwake ungedhani wenda anakutega kumbe hakuwa na mpango huo, wanaume wengi walipata tabu sana.Siku hiyo akiwa na chupi peke yake ndani huku akiwa amejifunga mtandio kiuoni, juu amevaa sidiria akamtafuta Tiger hewani,akimwambia kwamba anamuhitaji nyumbani kwake mara moja.
“Sasa hivi?”
“Ndio,njoo nyumbani kwangu”
Hilo halikuwa tatizo,alichokifanya mwanamke huyo ni kuwataarifu walinzi wake kuhusu ugeni wa Tiger hivyo wasimhoji maswali mengi,baada ya hapo akaliendea jokofu na kuchukua pombe kali,akaimimina kwenye glasi na kujitupa juu ya sofa,sio siri mwanamke huyu alikuwa tajiri na mwenye pesa chafu hiyo ilitokana na harakati zake za kufanya dili chafu za kuuza madawa ya kulevya na mara nyingine silaha za moto pale ikibidi,urembo wake ulikuwa ni tofauti na roho yake!Sporah Trevez jambo la kuuwa kwake lilikuwa ni kawaida sana,yaani ilikuwa ni sawa na kuweka kikombe cha chai mdomoni.Haikuchukuwa dakika nyingi sana,akasikia geti lake linafunguliwa akajua bila shaka atakuwa ni Tiger,akatembea mpaka dirishani.Kwa kuwa alikuwa juu gorofani aliweza kuliona gari la Tiger linaingia,hiyo ilimfanya ashushe ngazi mpaka seblen na kufungua mlango.
“Karibu ndani”
Tiger,akaishia kumuangalia na kumeza mate ya matamanio,alikuwa mwanamme lijali ndiyo maana alisisimka, mwili wa bosi wake Sporah Trevez, ulikuwa na mvuto wa aina yake na ulimpandisha mori kwa kiasi cha kutosha,karoti yake ikaanza kusimama taratibu lakini akili yake,akaihamisha haraka sana kwani alijuwa hapo kusingekuwa na ngono bali aliitiwa kazi.
“Kuna kazi nataka nikupe”
Sporah Trevez,hakutaka kuleta stori nyingi akaenda moja kwa moja kwenye pointi ya msingi.
“Kazi gani Madam?”
“Nahitaji uende Tanzania,ukamtafute Florian Fredrick!Nina uhakika kuna tatizo amelipata”
“Liini?”
“Swali zuri,leo jioni.Nitakuwekea pesa kwenye akaunti yako”
“Lakini Tanzania ni kubwa,nitaanzia wapi?”
“Unahitaji kazi ama hutaki?”
“Nataka”
“Fika Tanzania,Dar es salaam.Nitakupa maelekezo ukifika huko”
“Sawa,nitaenda”
Hapo Sporah Trevez alitembea mpaka karibu na Tiger,akamsogelea kabisa mpaka sikioni.
“Hakikisha,unaenda leo”
Akanong’ona kwa sauti ya chini ya mahaba na kurudi kwenye sofa alilokalia mwanzoni,hiyo ilimfanya Tiger azidi kusisimka mwili lakini hakuwa na jinsi,akakubali wito na kugeuza kuondoka zake, bila kujua kwamba Sporah Trevez alikuwa ana midadi ya kufanya ngono na niya ya kumsogelea sikioni ilikuwa ajiongeze lakini akashindwa kufanya hivyo.

*****
“Aaaaash aaaah aaaaah,Beibiii aaaaashss aaaah beiiibii aaashss aaaah”
Mkono wake mmoja ulishika kona ya kitanda mbuzi kagoma majanini,anatoa miguno ya puani, haikufahamika kama raha zilizidi kipimo ama anaumia lakini kelele ziliongezeka mara dufu,kiuno chake kilikuwa kimeshikwa vizuri tena kwa mikono miwili,anapelekewa majeshi majeshi.Alichokihisi hakikuwa kitu cha kuelezeka hata kidogo!Kifupi alihisi yupo angani, anaviangalia viumbe vyote kwa chini,alisikia raha siku hiyo na kitu kingine ni kwamba aliamini mambo yote yamekwisha sababu aliyekuwa nyuma yake wanafanya tendo hilo lililohalalishwa kwao alikuwa ni mumewe Ahmed,amepiga magoti anaendelea kukizungusha kiuno chake.Kuna mambo mengi aliyamisi kama hayo kipindi cha nyuma,ndiyo maana akafanya kila jitihada na utundu wote ili amfanye Ahmed asahau yote yaliyopita.Ndiyo maana baada ya hapo,akageuka na kumtupa chali,akapanda juu yake akaendelea kumzungushia kiuno.Ni kweli kwa wakati huo Ahmed, alisahau kila kitu,kwake ulikuwa ni usiku mfupi na mtamu tangu aingie kwenye ndoa,hakuelewa ni kwanini Yusrath hakuwahi kumpa vitu hivyo hadimu tena vipya.
****
Asubuhi ya saa kumi na mbili,akashtuka kutoka kitandani kwani aliweka saa yake ‘alarm’ tofauti na siku nyingine.
“Vipiii?”
Yusrath,akauliza kwa sauti ya uchovu akiwa bado kitandani, alishtuka kutokana na Ahmed kuutoa mkono wake uliokuwa kifuani mwake.
“Nawahi kazini”
“Si uliniambia ume..”
“Ndio lakini inabidi nikaombe msamahaa,acha nikajaribu kucheza karata dume”
“Natakuombea Mme wangu,Mungu akupe wepesi”
Ahmed,akanyoosha mpaka bafuni ambapo huko alipiga mswaki na kuoga.Akafanya kila linalotakiwa kufanywa chooni kisha kutoka kuliendea kabati,siku hiyo alitaka kuwa mtanashati kuliko siku zote,ndiyo maana akachagua shati jeupe na suruali nyeusi,akavuta tai na kuiweka kohoni.Hilo alilijua kabisa kwamba akivaa namna hiyo anatoka chicha,kwani kitambi chake cha wastani, kilichochomoza kilifanya shati limbane kidogo na kufanya watu wajue kabisa mwanamme huyo anakula mambo matamu ya ndoa!
“Baby baadaye”
“Kazi Njema mme wangu,nakuombea ufanikiwe”
Ahmed akawa tayari keshatoka akatembea mpaka nje na kuingia ndani ya gari lake!
***
Wasiwasi wake ulikuwa ni mkubwa akiwa nyuma ya kompyuta yake,akakosa raha kabisa siku hiyo hata kazi alizozikuta hakuweza kufanya kabisa akajua kwamba ni lazima bosi wake akija atamfokea kama mtoto mdogo,hiyo ilimfanya ajawe na uwoga.Wakati mwingine alitamani kuondoka na kuanza kujuta ni kwanini alifika ofisini wakati tayari alifukuzwa kazi,hakutaka kabisa bosi wake aje amtukane na kumfokea kama siku iliyopita.
Muda wa kuingia bosi wake ulikuwa saa mbili asubuhi, hiyo ilimaanisha zilibaki dakika chache awasili.
Mapigo yake ya moyo,yakazidi kwenda mbio kila dakika ilivyozidi kwenda mbele,hatimaye saa mbili ikagonga.Nusu saa baadaye akasikia sauti ya bosi wake akiitikia salamu za wafanyakazi, hapo ndipo akahisi mwili wake umeporomoka na kuwa mdogo kama mchanga,akakosa nguvu kabisa.Akaacha kubonyeza ‘keyboard’ ya kompyuta na kutulia kama mtu aliyekuwa anasikilizia kitu fulani kutoka nje,akasikia hatua za mtu zinakuja ofisini kwake, mlango wake ukafunguliwa.
“Ahmed,unaitwa na Bosi”
Moyo wake ukapiga kwa nguvu,akajua kabisa anapoenda huko ni lazima bosi wake angemfokea kama kawaida,hata hivyo alijikaza kisabuni na kupiga moyo konde!Akanyonga kitasa na kutoka nje ambapo alitembea mpaka mlangoni,akagonga.
“Get in”
Bosi huyu,alipenda sana kutumia kiingereza mara nyingi,haikujulikana kama anataka aonekane ni msomi ama alikulia sana nje ya nchi.
“Ahmed,Uko smart sana leo.Have a seat”
Tabasamu la bosi wake lilimfariji ingawa hakuwa ana uhakika sana na hilo,akakaa na kumsalimu kisha kushusha pumzi ndefu.
“Kuna emergence imetokea,unatakiwa kusafiri na ndege ya leo usiku.Kifupi unatakiwa Mkoani Kilimanjaro kesho asubuhi na mapema, you gona be there for two months,DEAL NO DEAL?”
Lilikuwa ni jambo ambalo hakulitegemea na kwa wakati mmoja lilimshtua,hakuyaamini masikio yake hata kidogo ndiyo maana akabaki ana bung’aa,hakujua aseme ahsante ama yupo tayari,ndiyo maana akatafakari kwa muda.
“Deal,nipo tayari bosi”
“Kitu kingine Ahmed,punguza pombe.Usiendekeze,what you did yesterday was not right at all, it was very bad to me.Wewe ni kama mtoto wangu,I have a son ni makamo yako,so nakuchukulia kama yeye.Cha msingi,saa kumi jioni nenda nyumbani kajiandae na safari.Saa nane mchana tiketi yako itakuwa tayari,una swali?”
“Hapana Bosi”
“Have a safe flight”
“Thank you”
Ahmed hakuelewa amshukuru vipi Mungu wake alitamani kupiga kelele za furaha,alitabasamu na kutoka nje.Akayakumbuka maneno ya Anneth kwamba bosi wake ana visirani na angetakiwa kuzipuuza hasira zake,hiyo ilimfanya anyooshe mpaka ofisini kwa Anneth.
“Ahmed,umenishtua”
Namna Ahmed alivyofungua mlango iliogopesha,alikuwa kama mwizi anayevamia.
“Pole,siamini bosi kanyooka.Nasafiri leo usiku”
“You can’t be serious,unanitania”
“Kwanini nikutanie?Anneth shukrani sana.Nilikuwa nishakata tamaa”
“Mimi nilikwambia”
“Sasa nikifika Moshi,nitakutoa kidogo!”
Ahmed alimaanisha,atamtumia pesa!
“Usijali Ahmed”
Furaha aliyokuwa nayo Ahmed,haikuishia hapo.Akampigia mkewe Yusrath akimwambia kila kitu kilichotokea,shukrani zake zote akampa mkewe akiamini yeye ndiye alimuombea pia,hakuishia hapo akamwambia kwamba atawahi kurudi hivyo apike chakula kingi.
“Sawa Mme wangu”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,saa nane mchana Ahmed akawa tayari ana tiketi yake mkononi,akarejea nyumbani ambapo huko alikula na mkewe na baada ya hapo akamtaka amuandalie nguo za kuvaa akiwa safarini.
“Moshi kuna baridi baby,lazima nikuwekee masweta”
“Ndio baby,ni mwezi wa sita huu”
Nguo zikapangwa vizuri,Ahmed akaoga na siku hiyo wakaagana kitandani wakifanya tendo la ndoa,kila mtu alijitahidi kumridhisha mwenzake,saa mbili usiku haikuwa mbali.
Wakasindikizana mpaka uwanja wa ndege,Yusrath akabaki hapo mpaka alivyoshuhudia ndege imepaa angani,ndipo alipotoa simu yake na kumtafuta Sameer.
“Twende club leo,una leseni baby?”
“Leseni ya nini?Ya biashara au?”
“Ya gari”
“Siwezi kukosa kitu kama hiko”
“Jiandae uje nyumbani kwangu uchukuwe gari,twende Club.Sijawahi kwenda Club,nahitaji leo mpenzi tufurahi wote.Unipeleke club zote za hapa Dar,tule kuku kwa mrija”
Ghafla Yusrath,akabadilika.Akawa sio tena yeye,hisia zake zote zikahamia Kwa Sameer RAJAB!



Mbali na kupewa kila kitu na mumewe,kuanzia pesa mapenzi na upendo wote ambao ulioneshwa juu yake lakini kwake ikawa sio kitu kabisa,bado alihisi kumpenda Sameer ingawa hakumchukia mumewe.Ingetokea siku moja wangesimama mbele wanaume hao na kuambiwa achague mmoja abaki na mmoja,angeshindwa kutoa jibu la harakaharaka,kila mmoja alikuwa na nafasi yake.Hakuna siku aliyokuwa na furaha kama hiyo,kusikia kwamba Mumewe Ahmed atasafiri na isitoshe atakaa mkoani Kilimanjaro kwa Takribani miezi miwili,kwake ilikuwa ni sherehe kubwa sana.Aliamini kwamba angetanua na kufanya kila aina ya starehe akiwa na Sameer bila bugudha yoyote ile,hilo lilikuwa kichwani kwake.Ndiyo maana alivyohakikisha ndege aliyopanda Ahmed, ipo angani inatoboa mawingu,akampandia hewani Sameer na kumpa habari hizo nzuri.
“Nije kwako,saa ngapi?”
Sameer aliuliza simuni,ilielekea hata yeye alikuwa ana mchecheto na mtoko huo.
“Saa nne nne hivi ama tano”
“Poa”
Yusrath,akakata simu na kurudi ndani ya texi iliyowapeleka uwanjani hapo,Ahmed alikuwa tayari amelipia pesa ya kuwapeleka na kumrudisha mkewe mpaka nyumbani, safari ikaanza.
Akiwa njiani alikuwa mwenye mawazo mengi sana,hakumfikiria tena Ahmed na kukumbuka,usemi wa asiyekuwepo na lake halipo.Kwa kuwa ilikuwa ni usiku,ilifanya barabara iwe nyeupe,dereva alizidi kukanyaga pedeli za gari akizidisha kasi,haikuwachukuwa muda mrefu wakawa wamewasili Ubungo,Kibangu.
“Ahsante kaka,Mungu akubariki”
“Amen dada angu”
Yusrath alizungumza kwa furaha,iliyotokana na kwenda disco siku hiyo akiwa na Sameer,kwa kasi akaingia ndani na kunyoosha mpaka chumbani.Akatembea mpaka kabatini,akitafakari ni aina gani ya nguo apigilie siku hiyo,mavazi ya disco hakuwa nayo, hiyo haikumpa tabu sana.Akachukuwa sketi ya kipindi cha nyuma,akiamini ni lazima itakuwa haimtoshi na kuijaribisha, kifupi alitaka kuvaa nguo inayombana.
“Hii inanibana sana”
Alijisemea mwenyewe huku akiwa mbele ya kioo kikubwa,ghafla akaanza kuchukia kwa jinsi, alivyonenepa na kufanya nguo zisimtoshe!Akaingia tena kabatini na kuanza kupekuapekua nguo, mwisho akaliona gauni lake refu ambalo aliamini akilivaa ni lazima lingemchonga na kumuonesha umbile lake, gauni hilo alinunuliwa na Ahmed siku moja wakiwa wanaenda ‘Dinner’ yaani chakula cha usiku,alivyoridhika akaingia bafuni na kujimwagia maji,alivyotoka tu akakaa juu ya ‘dressing table’hapo alitumia masaa mengi kujiremba,hata siku moja hakuwahi kujiremba kwa dakika nyingi namna hiyo,alivyomaliza hapo akachukua ‘foundation’ na kuanza kujipaka nayo usoni ili uso wake ung’ae.Alivyohakikisha hilo lipo sawa,akachukua ‘lip bum’,akajipaka mdomoni.Alivyoridhika akasimama ili kujikagua vizuri,siku hiyo alikubali kwamba ametokelezea akanyoosha dole gumba kumaanisha amejikubali.Hakutaka kuchelewa,akachukuwa simu yake na kumtafuta Sameer, hewani.
“Nipo njiani nakuja”
Upande wa pili,ukasikika baada ya simu kupokelewa.
“Baby,muda wote huo?”
“Kuna foleni”
“Chukua boda”
“Nakaribia kufika lakini”
“Harakisha”
Muda wote alikuwa mwenye mchecheto wa kuona club kunafananaje,alitamani Sameer afike waende dakika hiyohiyo,akatembea mpaka seblen.
“Ng’aaaaaa! Ng’aaaaa! Ng’aaaaaaaa!”
Sauti ya mtoto wake mmoja,ilisikika akilia kwa sauti kubwa sana.Hiyo ilimfanya atulie kidogo na kumuita Hadima, akimwambia ahakikishe watoto wanakunywa maziwa kwani yeye ana mtoko.
“Lakini mama”
Hadima akawa ana kitu anataka kuzungumza huku akiwa na Faisal mkononi mwake,analia kwa sauti.
“Zungumza”
“Mtoto anaumwa”
“Anaumwaaaaa?Umekuwa daktari siku hizi?Hujampa maziwa ya kutosha, ndio maana analia”
“Hapana Mama,amekuwa wa moto tangu jioni.Nilitaka kuwaambia ulivyokuwa na Baba lakini mlikuwa mshatoka tayari”
“Nimekwambia mpe maziwa ya kutosha,mimi natoka.Baba yako akikupigia simu mwambie nimelala!Kwaheri,tutaonana kesho”
Ilikuwa ni kauli iliyomfanya Hadima asijue ni kitu gani akifanye,alimuonea huruma mtoto huyo mchanga anayelia kwa sauati,mbaya zaidi alikuwa anachemka yaani wa moto mno, kifupi ilielekea alikuwa ana homa kali,angefanya nini?Wakati mama wa mtoto,hatoi ushirikiano akajaribu kuingia ndani na kum-bembeleza, akimpa maziwa lakini wapi mtoto alichachamaa akalia, mpaka sauti ikaanza kumkauka.
“Ng’aaaaaa ng’aaaaaaaaa, ng’aaaaaaaaaa ng’aaaaaaaaa”
Kelele za mtoto huyo zilikuwa kubwa sana,kiasi kwamba alibadilika rangi na kuwa mwekundu, cha ajabu alisikia geti linafunguliwa na gari linawashwa,jambo hilo lilizidi kumuumiza akili.Akasikia muungurumo wa gari linatoka nje kisha geti kufungwa.Mtoto alizidi kulia kwa sauti kali,hiyo ilimfanya Hadima alengwe na machozi,akashikwa na hasira na chuki za waziwazi kwa Yusrath akashindwa kumuelewa ni mama wa aina gani,kilichomfanya aumie zaidi, aliamini kabisa ni lazima yupo na hawara wake kwani sentensi ya kwamba akipigiwa simu na Ahmed aseme amelala,ilitosha kabisa kumpa jibu hilo.
Kuendelea kubaki hapo na kum-bembeleza mtoto kusingesaidia ilikuwa ni lazima aokoe maisha ya malaika huyo asiyekuwa na hatia kwani aliamini kama lolote baya lingetokea asingejisamehee kwani alikuwa ana uwezo wa kufanya jambo, alichokifanya ni kungia ndani chumbani kwake na kuchukua akiba yote ya pesa aliyokuwa nayo ndani ya begi lake,akambeba na Faad,ambaye alikuwa bado amelala, akawabeba wote kwa safari moja tu,hospitalini ili kuangalia ustaarabu wa matibabu.

****
Sameer alikuwa nyuma ya usukani,amevimba utadhani gari lake vile.Mkono mmoja upo juu ya usukani mwingine nje,kioo kafungua kaweka kishoka!Maisha kwa upande wake yalikuwa ya mteremko kwani kila alichotaka kwa Yusrath alitimiziwa,hiyo ilimfanya aringe na kuamini kwamba anapendwa kwa kiasi cha kutosha!Kwake dunia akaona kama kaiweka mfukoni,matanuzi aliyokuwa anafanya tangu ampate Yusrath yalitishia amani,kwa siku alikuwa ana uwezo wa kutumia mpaka laki moja, bila kujuta sababu aliamini akitaka nyingine atapata, kifupi Yusrath alikuwa kama benki yake,akitaka pesa anachota anavyotaka!Pembeni ya gari kushoto,alikaa Yusrath,moyo wake ulikuwa mweupe kwake aliona kila kitu kipo sawa kabisa,Sameer kwake alikuwa kila kitu,aliamini hata ikitokea siku moja Ahmed akimpiga chini haitakuwa tatizo atabaki na Sameer kwani ndiye mwanamme mwingine anayempa furaha,ndiyo maana aliwaza kumpa kiwanja ili taratibu waanze kujenga na baadae kikinuka,wawe wamepata pa kuishi tayari.Hiyo ndiyo ilikuwa mikakati ya Yusrath kichwani kwake.
“Hilo gauni,kama muimba kwaya.Baby,huna nguo kabisa ya Club?”
Sameer alivunja ukimya na kupiga kijembe, baada ya kumtizama Yusrath kwa kipindi kirefu.
“Darling,sijawahi kwenda club.Yaani sijawahi hata kuwaza kama ipo siku moja nitaenda”
“Leo kimekusibu nini?”
“Hata sijui,basi tu.Maruwani yangu, yamenipanda”
“Sijui twende club gani?Kuna kiwanja kimoja kwanza kinaitwa Spirit Sinza pale.Sema pale,hawana kibali cha kukesha,twende Club Next Door”
“Baby,popote pazuri twende.Ikiwezekana tupite kote tu”
“Poa baby”
Hapo Sameer akasogea karibu na Yusrath,wakaanza kunyonyana ndimi kimahaba,kwa kuwa hakukuwa na magari mengi barabarani hawakujali.Wakazidi kusonga mbele mpaka walipofika Club Next Door,Masaki.Hapo ndipo Sameer alipopanga kumpeleka Yusrath afurahi.Wakashuka ndani ya gari na wote kuingia ndani,ambapo bosi na mtoa pesa alikuwa Yusrath.Mazingira ya ndani yalimshangaza Yusrath,hakutaka kuamini kama kuna watu wanaishi namna hiyo,alizoea kuona mambo hayo kwenye luninga sanasana kwenye sinema za kifilipino,wasichana walikuwa wengi wamevalia nguo za nusu utupu wakicheza katikati,kana kwamba hakuna kufa tena.Jambo hilo lilimfurahisha sana Yusrath,akajutia sana kwa kitendo cha kubaki nyumbani kila siku.
Mkononi alikuwa na chupa ya bia ya Windock,hakuwa mlevi sana lakini siku hiyo alipania kunywa mpaka atambae.
“Baby,kumbe una smoke?”
Yusrath alimuuliza Sameer baada ya kumuona mwanamme huyo ana kipisi cha sigara mkononi.
“Yes,shika jaribu”
“Nononono,sitaki”
“Come on baby,piga pafu moja.Kama hivi”
Sameer akaweka sigara modomoni,akavuta moshi ndani na kuutolea puani kama kumuoneshea mfano Yusrath,akamshawishi nayeye apige pafu moja!Kwa kusua,Yusrath akashika sigara,akaiweka mdomoni na kuvuta,kilichofuata hapo kilikuwa ni kikohozi kwa kwenda mbele sababu moshi ulimpalia,hakutaka kuendelea kuvuta tena alichotaka yeye ni kunywa pombe,hilo halikuwa tatizo.
Nyimbo iliyomfanya aingie katikati kucheza ni ya 50 cent aliyomshirikisha Olivia 'Candy shop',spika zilikita kwa sauti kubwa.Yusrath akawa kama mtu aliyepagawa kazi yake ilikuwa ni kuweka mikono yake hewani,pombe zilikuwa zinafanya kazi yake.Sameer akafika na kumshika kiuno,wakaanza kucheza akimbambia kwa nyuma wanaenda mpaka chini na kurudi juu.
“Bebiiii ilove you…Uuuuu, I'll take you to the candy shop.
Boy, one taste of what i got,
I'll have you spending all you got.
Keep going till you hit the spot, wuuuuuuuu”
Yusrath,akawa ana kazi ya kufatisha maneno ya mziki huo huku mengine akiyamung’unya mung’unya ya uwongo na kweli ilimradi furaha tupu.

*****
Tangu maisha yake ya kunywa pombe akiwa mdogo kidato cha kwanza,hakuwahi kupoteza kumbukumbu ama ‘network’ lakini siku hiyo,akahisi wenda amekunywa pombe nyingi sana!Baada ya kufika Masaki,Club Next Door na kuona gari ya rafiki yake ipo nje ya ukumbi huo wa disco,hakutaka kukubali akafikicha macho ili aangalie vizuri namba za usajili kwa umakini.
“Ina maana Ahmed,hajasafiriiii.Asa kwanini kanidanganya”
Benjamin Ngowi,alijisemesha mwenyewe baada ya kuwa ana uhakika kwamba gari lililopaki nje ya ukumbi huo lilikuwa la swahiba wake,Ahmed Kajeme!Kilichomjia kichwani ni kwamba Ahmed kamdanganya ana safari kwenda Mkoani Kilimanjaro.
“Kwanini anidanganye,atasafiri leo!No,namfuata ndani wala simpigii simu”
Benjamin Ngowi,akatizama huku na kule ili kuangalia nafasi ya kuweka gari lake kisha aingie ndani ya club hiyo, aanze kumsaka Ahmed Kajeme na akimkuta anakunywa pombe basi waunganishe kwani hakua na rafiki wa kufa na kushibana kama Ahmed,ndiyo maana akaghaili safari ya kwenda kulala na kutafuta sehemu nzuri ya kupaki gari lake,alivyopata nafasi akaliweka vizuri kisha kuteremka!Akachukuwa simu zake na kuweka mfukoni,akafunga gari na kuanza kutembea hatua za taratibu kisha kuingia mlango wa club.
Kilichompeleka ndani humo,sio kunywa tu bali kuonana na mshkaji wake Ahmed wapige stori.Kazi yake ilikuwa ni kutizama huku na kule,akiangalia watu wanaocheza katikati akaangalia upande wa kaunta,lakini Ahmed hakuwepo.Kilichomfanya atabasamu ni baada ya kumuona Shemeji yake Yusrath,akaamini kwamba ni lazima atakuwepo na Ahmed,jambo hilo lilikuwa ni ajabu sana kwa Ahmed kutoka na mkewe usiku namna hiyo, tena eneo kama hilo isitoshe ana watoto wadogo wachanga,licha ya kuwaza hayo lakini hakutaka kulikuza aliliacha kama lilivyo,sababu lilikuwa ni la kifamilia zaidi hakupaswa kuhoji wala kuingilia sababu halikumuhusu,kilichomleta hapo ni kunywa tu na sio kuhoji maswali,akaanza kuwapangua watu ili amfikie Yusrath aliyekuwa upande wa kushoto lakini cha kushangaza,kilichomfanya apigwe na butwaa ni baada ya kumuona kijana mmoja aliyevalia kofia kichwani,tshirt nyeupe na jeans,amemfuata Yusrath karibu kabisa,hapo alisita kidogo kwani picha aliloliona hakulielewa vizuri,mbaya zaidi sura ya kijana huyo haikuwa ngeni machoni kwake.Hiyo haikutosha,akapigwa na butwaa baada ya kuwaona wawili hao wanapigana denda,mapigo yake yakamwenda kasi,akadhani wenda anaota ama amemfananisha Yusrath lakini hilo alilipinga.
“Bebiiiiii,I’m horny..Pleaseeee,I’m dying”
Kutokana na kutomaswa tomaswa kifuani na kushikwa shikwa kiuno na Sameer ilimfanya Yusrath,apandishe midadi.Akitaka kufanya mapenzi dakika hiyohiyo bila kuchelewa,swala hilo lilikuwa jepesi kwa Sameer,wakashikana viuno huku wakiyumba mpaka nje kwenye maegesho ya magari,wakaingia ndani ya gari wakafunga milango na kubinua viti.Kwa kasi ya umeme Yusrath akavua nguo zake!Bila aibu yoyote wakaanza kufanya mambo ya ajabu ndani ya gari.Mbaya zaidi kila kitu kilishuhudiwa na Benjamin Ngowi,moyo wake ukawa unamuuma ajabu,ukachoma kama pasi ya mkaa,hakuamini kama gari la Ahmed leo hii limegeuzwa na kuwa gesti bubu,ilikuwa ni dharau iliyozidi kipimo chake!



Shirika la ndege ya Tanzania Airways,ilikuwa karibuni kukanyaga ardhi ya Mkoa wa Kilimanjaro!Juu ya uwanja unaoitwa Kilimanjaro International Airport(KIA),taratibu zilifahamika kwamba abiria wote wafunge mikanda yao ili ndege iweze kutua,hicho ndicho kilichofanyika.Abiria wakafanya hivyo, akiwemo Ahmed,ambapo ndege hiyo ikaanza kutoa matairi yake kisha kichwa kikaanza kuangalia chini,hapo marubani kwa ufundi wao wakaanza kuiteremsha,kitendo cha matairi kugusa lami ikatingishika kidogo kisha kukaa sawa,ikakimbia kwa kasi ya risasi kisha baadaye kusimama.Ilikuwa ni safari fupi ambayo haikuzidi lisaa limoja,lakini ilionekana kumchosha sana Ahmed kwani hakupata nafasi ya kupumzika tangu siku iliyopita, ndiyo maana muda wote alipiga mihayo ya usingizi isitoshe ilikuwa ni usiku tayari.Ndege ilivyosimama,akafungua mkanda na kulishika begi lake dogo la mgongoni na kuanza kutembea kwenye korido ambapo huko alipishana na abiria wenzake,alivyotoka nje kabisa ya lango.
Akahisi kuna mtu amemshika bega.
“Mr.Ahmed Kajeme,nadhani ndio wewe?”
Mwanamme huyo mrefu,mweupe mwenye meno ya kichaga aliuliza akiwa ana mtizama Ahmed kwa umakini.
“Ndio mimi”
“Mimi naitwa Massawe,karibu Kilimanjaro”
Jina hilo halikuwa ngeni katika masikio yake sababu alivyotoka Dar es salaam, alipewa maagizo ya kwamba angepokewa na vijana wawili,akatizama huku na kule ili amsubiri kijana mwingine lakini hakutokeza.Bwana Masawe akawa mbele yake, kumaanisha Ahmed amfuate nyuma,ambapo huko safari yao ilikomea kwenye gari aina ya Prado,lililokuwa linaunguruma kumaanisha ndani kuna dereva.
“Nimempata”
Bwana Masawe,alimwambia mwenzake aliyekuwa nyuma ya usukani.Jamaa huyo akageuka na kumtizama Ahmed.
“Ahmed,karibu”
“Ahsante”
“Jisikie upo nyumbani,Meku.Mimi naitwa Praygod Kimaro!Tukupeleke ukapumzike ama tupite sehemu?”
“Naomba nikapumzike”
“Hakuna shaka,ndio mara yako ya kwanza kufika Moshi?”
Praygod Kimaro,alianza usaili huku akipiga gia,akageuza shingo yake nyuma ili aangalie namna ya kulichekecha gari,akafanikiwa kuliweka sawa na safari ikaanza.Wanaume hao,walionekana kumchangamkia sana Ahmed kuliko kawaida,hapo ndipo alipogundua vijana hao pia ni wafanyakazi wenzake hivyo angekuwa nao ‘site’ jambo hilo lilimfurahisha sababu wote walikuwa ni makamo yake,isitoshe walikuwa wacheshi na stori zao zilikuwa za kupiga madili ya pesa.
“Aisee,Mekuu…Juzi bwana nilikuwa pale Same,Yesu na Mariaaa.Nilikuwa na tajiri mmoja hivi,aliniuliza kama ninaweza kuendesha lori….”
Praygod Kimaro,alizungumza na kwa mbali alikuwa ana rafudhi ya kichaga,hiyo ilimfanya Ahmed asikilize kwa makini akiwa siti ya nyuma.
“Si unajua mimi Meku nilivyo sasa,kila kitu nataka kujaribu.Nikamwambia ndio,nikajua yameisha.Yule mdosi,akapiga simu.Lori likaletwa,akaniambia niingie niendeshe”
“Hahahahahahaha”
“Kuingia ndani,naona vitu vya ajabu.Nikaweka funguo,jasho linanitoka,nikapiga gia.Ilikuwa kidogo nimgonge huyo mdosi nikaliingiza lori kwenye mtaro…..”
“Hahahahahaha”
Stori hiyo ilimfanya Ahmed atabasamu,nayeye ilimfurahisha kidogo.
Ghafla,akamkumbuka mkewe Yusrath,akatoa simu mfukoni ili amtafute!Kilichomshangaza na kilichomfanya ajilaumu ni baada ya kugundua simu yake haina chaji,yaani imezima kabisa,akahaidi akifika hotelini atafanya utaratibu wa kuchaji simu kisha kumtumia ujumbe mfupi mkewe,akimtaarifu kwamba amefika salama.
Safari ilizidi kusonga mbele na dakika 45 baadaye, wakawa wamefika Njia panda,hapo walinyoosha na kutokea Himo,safari ilizidi kwenda mbele zaidi,wakakutana na barabara ya Makerere,ambayo ilikuwa na kilima cha wastani,wakapandisha.Nusu saa baadaye,wakatokeza soko la Mwika.Ahmed,alikuwa kimya anashangaa, baridi lilimkung’uta kisawasawa lakini alijikaza kisabuni,hatimaye gari likasimama nje ya nyumba ya wageni.
“Meku,tumefika”
Ahmed,hakuwa ana uhakika kama anaambiwa yeye sababu hakuelewa nini maana ya neno Meku.
“Tumefika eeh?”
Akauliza huku akishika begi lake vizuri,akavuta kitasa na kuteremka, ambapo mbele yake walikuwa wanaume hao wawili,ndani ya nyumba hiyo ya wageni kulikuwa na baa moja iliyoandikwa kwa Juu Mandela,jambo hilo lilimfurahisha sababu alikuwa mwenye kiu ya bia.Kila kitu kikaenda sawa, baada ya kuoneshwa chumba chake cha kulala akiambiwa kwamba asubuhi,kukikucha watampitia ili waende ‘Site’ huko Rombo!
“Sawa,ahsanteni kwa kila kitu”
“Usiku mwema”
“Na ninyi pia”
Wenyeji wake walivyotoka,cha kwanza kukitafuta ilikuwa ni soketi ili achaji simu yake,alivyofanya hivyo akaingia bafuni kujimwagia maji ambayo yalikuwa ya baridi kwelikweli,baada ya hapo akavaa nguo pamoja na sweta zito ili kushindana na baridi.
Baada ya kutulia akaanza kufikiria jinsi gani apangilie pesa atakazolipwa,zilikuwa fedha ambazo, aliamini baada ya kutoka hapo angenunua kiwanja ili aanze kujenga,hapo alitabasamu na kuona moja ya ndoto zake itatimia,akaanza kupiga picha atakavyoanza kuishi kwake na familia yake,aliamini kabisa furaha ingeongezeka!Hakutaka kukaa sana,akatoka nje ambapo huko aliyoosha mpaka kaunta kulipokuwa na vinywaji vingi.
“Dada mambo”
“Safi kaka,karibu”
“Ahsante,nipo ndani chumbani.Naweza kunywea chumbani?”
“Bila shaka,bia gani?”
“Ndovu”
“Ngapi?”
“Tatu”
“Sawa,upo chumba namba ngapi?”
“1O”
“Utaletewa”
Hapo alitoka na kuingia moja kwa moja chumbani,kutokana na baridi kuwa kali, akanyoosha moja kwa moja mpaka kitandani na kujifunika na blanketi zito,dakika moja baadaye mlango wake ukagongwa akawa ameletewa bia zake,akaziweka mezani na kufungua moja!Akapata wazo la kumpigia mkewe simu,alivyoangalia vizuri alikereka sababu aliiweka vibaya na kufanya isiingie chaji,hakuwa na jinsi zaidi ya kunywa bia yake akisubiri simu ipate chaji kidogo, amtumie meseji mkewe,akiamini kivyovyote vile Yusrath ni lazima alikuwa akimtafuta hewani, saa saba ya usiku ndipo,alipochomoa simu kwenye chaji,akaiwasha na kuanza kumsaka Yusrath hewani.
Matokeo yake,simu iliita bila kupokelewa.
“Griiii griiiiii,griiii griiiiii”
Alikuwa katikati ya raha,mguu wake mmoja umewekwa kwenye kiti cha mbele mwingine upo karibu na gia,Sameer yupo juu yake wanafanya tendo baya la usaliti!Simu iliita lakini hakuweza kuisikia hata kidogo,alichohisi yeye ni raha ya ajabu,hiyo ilimfanya Ahmed ajuwe ni lazima mkewe atakuwa amelala, alichokifanya ni kutuma ujumbe mfupi ‘Mke wangu,nimefika salama.Simu haikuwa na chaji.Usiku mwema,nakupenda mke wangu’hakuelewa kwamba mkewe analiwa uroda, tena ndani ya gari lake, alilonunua kwa jasho lake.Yusrath aliendelea kupewa raha za dunia,kukurukakara za ndani ya gari, zilifanya mpaka gari lianze kunesa nesa kwa nje,kwa watu wazima waliokuwa wanapita nje walielewa nini kinaendelea ndani ya gari hilo,mmoja wapo alikuwa ni Benjamin Ngowi.
Alitamani kusogea karibu na gari ama kumpigia simu Ahmed lakini aliona hiyo isingetosha,akatulia mpaka alivyomuona kijana huyo anatoka ndani ya gari, anafunga zipu,kumaanisha kwamba keshamaliza mchezo!Akarudi nyuma kidogo na kujificha pembeni ya gari, baada ya kumuona Yusrath nayeye kashuka,anaweka nguo yake sawa.
“Bebiii,thank youuuu….Ilove you.Nipeleke nyumbaniii,wewe baki na gari,kesho uje kunichukua.Hili gari ni lakooooo bebiii,mimi ndio nimekupaaaa”
Yusrath,alizungumza kwa sauti ya kilevi huku akipepesuka,akaingia ndani ya gari wakaanza kuondoka,hata Ngowi nayeye akaingia ndani ya gari lake na kuanza kuwafuata kwa nyuma.
Hakutaka kuwasogelea karibu sana akiamini Yusrath analifahamu gari lake,safari yao ikakomea Ubungo Kibangu,nyumbani kwa Ahmed hapo Benjamin Ngowi akiwa umbali wa mita mia moja,akazima taa za gari na kuangalia kila kitu kinavyoenda,cha kushangaza badala ya gari kuingizwa ndani liliondoka tena!Hapohapo nayeye akaanza kulifuata kwa nyuma,mpaka walipofika Kinondoni studio,gari lilisimama,akaingia msichana mwingine aliyevalia kimini cheusi.
Gari halikufika mbali,likasimama tena na kuanza kunesa nesa kumaanisha kwamba wanafanya ngono,msichana huyo akashuka na kuondoka zake.
“Siwezi kukubali rafiki yangu afe kwa magonjwa,this is too much”Ngowi,alisema kwa uchungu.
Kulifumbia jambo hilo macho kulimaanisha kumuuwa rafiki yake,akiamini kwamba kama Kijana huyo angepata magonjwa,angepeleka kwa Yusrath na ingekuwa rahisi kumfikia Ahmed,hakutaka kitu kama hiko kitokee ndiyo maana akazidi kumfuatilia mpaka walivyofika Sinza,Mori.Hapo wakaingia ndani ndani na gari kusimama nje ya nyumba ndogo,akaamini hapo ndipo kijana huyo anaishi sababu baada ya kugonga geti likafunguliwa.

********
Benjamin Ngowi,hakutaka kulifumbia swala hilo macho!Aliamini kwa kufanya hivyo atamuokoa rafiki yake kipenzi kwani alijua nini maana ya ugonjwa mbaya wa Ukimwi,unavyotesa kitandani mpaka kukutoa duniani.Hilo ndilo alilohofia,hakutaka kumkosa rafiki yake kwani alikuwa bado mdogo kufa, ndiyo maana kulivyokucha tu,akamtafuta hewani,bahati nzuri simu ikapokelewa akamsalimia na kumpa pole ya safari.
“Naona upo uchagani”
“Kuna baridi sana,mpaka meno yanagongana.Ndio naelekea site sasa hivi,vipi huko Bongo?”
“Huku kama ulivyotuacha na jua letu hili,joto sana”
“Ndio nyumbani kwetu,tutafanyaje unadhani.Tukubali matokeo tu”
“Kweli,hakuna jinsi.Uliniambia utarudi lini?”
“Baada ya miezi miwili”
“Lakini Moshi,si hapo tu.Pua na mdomo,unaweza hata ukaja na kurudi week end”
“Tatizo huku,nasimamia vitu vingi lakini nikipata nafasi nitakuja.Jumamosi moja”
“Uwe unakuja”
“Ondoa shaka”
“Kuna jambo nataka kukwambia”
“Jambo gani?”
Hapo Benjamin Ngowi,akatafakari kwa muda kidogo na kukaa kimya,kuna wazo la ghafla lilimjia kichwani.Akaelewa ni kwa namna gani Ahmed angepata jazba na maumivu,hiyo ilimlazimu akae kimya kwanza akitafakari njia ya kumwambia bila kumuumiza.
“Nataka,nikutambulishe shemeji yako rasmi.Nataka tukachumbie”
“Wacha wee,karibu sana chama letu,wapi huko?”
“Ahsante,nitakupigia simu baadaye.Kukupa mchakato mzima,inabidi ukirudi twende wote”
Benjamin Ngowi,akawa tayari ameua soo!Kwa kuwa siku hiyo hakua na shughuli nyingi nyumbani kwake,aliamua kutumia mwanya huo kwenda Sinza Mori,kukabiliana na kijana,mchepuko wa Yusrath.Akawasha gari!
Baada ya kufika,akaliona gari aina ya Verosa, akajua ni lazima kijana huyo bado yupo,hajatoka.Akamsubiri kwa kama dakika kumi nzima,ndipo alipomuona!Akateremka ndani ya gari na kumfuata.
“Mambo vipi?”
Benjamin,akamsalimia Sameer aliyekuwa anafungua mlango wa gari anataka kuingia ndani.
“Poa”
Sameer akaitikia lakini alionesha hakuwa na muda na Benjamin kwani aliendelea kufungua mlango na kuingia ndani ya gari.
“Nina mazungumzo nawewe”
“Mimi?!”
“Ndio,wewe hapo”
“Samahani kidogo,kwani tunafahamiana?”
“Haijalishi,sikia…wewe ni kijana mdogo sana…”
Hapo Benjamin Ngowi,akasonya kwa hasira na kumkazia macho Sameer.
“Kitu unachofanya,kitakucost..”
“Mbona siku…”
“Hili gari lako?”
“Oya kaka eh,sikujui hunijui.Chukua time,mbona unaniletea uchuro.Au umetumwa?”
“Achana na Yusrath ni mke wa mtu kama ulikuwa hujui,Mumewe akijua unatembea naye.UTAPATA TABU SANA”
Benjamin Ngowi,hakutaka kujazia mengi zaidi ya kumuonya,akaondoka na kuingia ndani ya gari lake akimuacha Sameer anamuangalia kwa dharau!

****
Baada ya mwezi mmoja kupita, Ahmed alifanikiwa kutengeneza pesa nzuri,kwani alikuwa akilipwa kwa siku kumaanisha kwamba yupo Mkoani Kilimanjaro kwa siku sitini yaani miezi miwili.Pesa yake,haikuwa ya kawaida, hiyo ikamfanya afanye kazi kwa bidii kubwa ili asimuangushe na kumtia aibu bosi wake,wazo la kununua kiwanja hakutaka kulifanya siri, lilikuwa la kifamilia kumaanisha kwamba ni lazima amwambie mkewe ili walijadili.
“Baby,habari nzuri sana hizo.I’m proud of you babyboy”
“Nafurahi kukupata wewe Mke wangu,Faisal na Faad wanaendeleaje?”
“Vizuri tu,Faisal anaendelea vizuri alikuwa anaumwa kidogo.Lakini sasa hivi,anaweza mpaka kula.Tumekumisi”
“Bado mwezi,mmoja tu.Mtaniona”
“I can’t wait to see you my husband,imiss you”
“Me too sweartheart”
Waliongea vitu vingi sana siku hiyo na kutakiana usiku mwema,kuna wazo lilimjia Yusrath kichwani, baada ya siku mbili akamkumbushia Ahmed inshu ya kununua kiwanja ili wajenge.
“Nikirudi baby,tutaenda wote kununua”
“Mme wangu”
“Yes”
“Kuna ndugu yangu,anauza kiwanja bei rahisi kabisa. Tuwahi mapema kabla hajakiuza,kama unaweza nitumie hizo pesa nikanunue”
“Darling,mambo ya viwanja haya sio rahisi kama unavyodhani.Kuna utapeli mwingi”
“Honey ni ndugu yangu,namuamini”
“Heka ngapi?”
“Heka moja na nusu”
“Bei gani?”
“Nitaongea naye,nimuulize”
“Kipo wapi Kiwanja?”
“Kigamboni,Mji Mwema”
“Ni sehemu nzuri,ebu jaribu kuzungumza naye.Utanipa jibu”
“Sawa Mme wangu”
Hatari aliyokuwa anataka kuifanya Yusrath, ilikuwa ni kubwa mno,alitaka kuchukua pesa kutoka kwa Ahmed anunue kiwanja kwa jina lake kisha amkabidhi Sameer ama ikiwezekana amtumie pesa anunue kiwanja wajenge,mwanamke huyu haikujulikana kama alipewa dawa ama ni akili zake mwenyewe,siku tatu ilivyopita akamseti mumewe na kumwambia amtumie milioni saba ili kiwanja kinunuliwe,Kwa Ahmed mara ya kwanza alikuwa mgumu kidogo kutoa kiasi hicho kikubwa cha pesa,kulalamika sana kwa Yusrath kukamfanya ajisikie vibaya.
“Acha basi kulalamika baby,nakutumia.Usiwe unalalamika hivyo mke wangu,sijakataa kukutumia nilikuwa nahoji tu,uniweke sawa.Ni pesa nyingi hizo,hapa nilipo nina nusu yake.Mpaka nikatoe akiba nyingine benki”
“Sawa baby,nimekuelewa.Nitaacha kuongea basi”
“Sijasema hivyo,nikutumie wapi?”
“Tigo pesa”
“Hapana,haitokuwa salama.Nitakuingizia kwenye akaunti yako”
“Okay baby,lini?”
“Kesho jioni,itakuwa tayari”
“Okay baby kazi njema.Nakupenda sana”
Mlolongo wa kutuma pesa,haukuchukuwa muda mrefu.Alichokifanya Ahmed ni kuvuta pesa zake kutoka akaunti nyingine, akazichanganya na zake alizolipwa kisha kwenda benki kutuma,alifurahi sana kupata kiwanja na kumshukuru mkewe kwa kupambana,hakuamini kama mambo yangekuwa rahisi namna hiyo na angepata kiwanja Kigamboni.Alivyotuma pesa akampigia Yusrath ili kuhakikisha kama zimeingia kwenye akaunti yake,jibu alilolipata likamfanya ashushe pumzi ndefu na kumsisitiza mkewe awe makini kwani kuna matapeli.

******
Sameer,alikuwa amepaki gari nje ya benki ya CRDB tawi la vijana,Mnazi mmoja.Hakuamini kama siku hiyo angeenda kupewa kiasi cha shilingi milioni nane taslim,pesa kama hizo hakuwahi kuzimiliki tangu azaliwe.Kitendo cha kuhaidiwa anapewa ili anunuwe kiwanja kilimtia kiwewe,akapanga mikakati mikubwa kichwani,ghafla wazo jingine likamjia,amdhurumu Yusrath akimbie mbali na pesa hizo.Lakini nafsi nyingine ikamzuia,akatafakari kwa muda kiasi akiwa anaangalia watu wanavyoingia na kutoka nje ya benki,akimsubiri Yusrath atoke na maburungutu ya pesa.
Nusu saa baadaye akamuona Yusrath anatoka kwenye mlango wa kioo, akiwa na begi mgongoni,akafika mpaka kwenye gari.
“Baby,nimekuweka sana?”
Yusrath akauliza huku akilitupia begi la pesa viti vya nyuma.
“Hapana,ulifanikiwa?”
“Ndio,pesa hizo hapo”
“Nakusikiliza”
“Wewe ndio uniambie cha kufanya,juzi umeniambia kuwa kiwanja umepata”
“Yes,Vikindu huko”
“Ndio wapi?”
“Ukivuka Mbagala”
“Milioni nane hizo,baby nakuomba.Usije ukanifanya nijute,nimeamua kujitoa muhanga kufa ama kupona kwa ajili yako!Namfahamnu mme wangu,akija kujua,Sijui itakuaje nahitaji mapema tufanye hili jambo,akija kugundua tayari tuna nyumba yetu”
“Hilo usijali mpenzi nitacheza kama Michael Scolfied,ngoja niongee na rafiki yangu mmoja anaitwa Sagasa,ni dalali”
“Sawa baby,mimi nawahi nyumbani.Nakuachia gari,leo jioni unipe jibu”
Hilo ndilo jambo la msingi ambalo Sameer alilisubiria kwa hamu kubwa kukabidhiwa gari.Alivyomfikisha Yusrath kwake,akageuza gari na kulipaki sehemu tulivu ili achungulie pesa kama ni kweli ama anaota,alivyozifungua alidata vilikuwa ni vibunda vya shilingi elfu kumikumi, vilivyofungwa vizuri na rababendi,akatabasamu na kuona maisha tayari ameyapatia.
Alichowaza sio kingine bali ni msichana anayeitwa Vaileth,mrembo huyo alikuwa ana nyodo sababu alikuwa yupo kimaslai zaidi,aliamini siku hiyo angemuonesha jeuri ya pesa.Akachekelea na kumtafuta simuni ambapo alimuuliza ni kiwanja gani kizuri,angeweza kuonana naye anywe na kula nyama choma mpaka ajinyee.
“Sameer,acha drama”
“Nipo siriazi,wapi unataka kwenda?”
“Aya,nikikwambia Kempiski unaweza kunipeleka?”
“Nasema hivii,nisikilize.Chagua kiwanja chochote kile”
“Leo una pesa sana?”
“Nina mavumbaaa,zungumza mrembo”
“Ngoja nifikirie,nitakupigia”
Usiku wa siku hiyo walichagua kwenda Vampino Cassino maeneo ya Oysterbay, akiwa na Vaileth,mwanammke wa kitasha!Siku hiyo walizunguka kumbi zote kubwa kubwa,bosi alikuwa Sameer,mpaka inagonga saa nane ya usiku Sameer na Vaileth walikuwa chakali,hiyo ilimfanya Sameer ashindwe kuendesha gari vizuri kwani akiwa barabarani aliyumba huku na kule,kilichomfanya apoteze muhimili kabisa ni baada ya Vaileth kuchezea koki yake,akafungua zipu ya suruali na kuanza kuichua karoti yake bila kujali wapo barabarani,alivyoiweka mdomoni na kuanza kuinyonya ndipo kabisa Sameer,alihisi kama anasimamia ukucha.
Hapo ndipo akajisahau kwamba yupo barabarani,gari likawa linahama upande taratibu, likiwa katika mwendo kasi.Hakuweza kuliona gari linaloingia kutoka upande aliopo,hapohapo wakasikia puuuu!Kilikuwa ni kishindo kikubwa sana,wakajigonga kwa mbele vioo vikawarukia,kitendo cha kuangalia mbele kiliwashtua.Tayari,walikuwa wamesababisha ajali mbaya,boneti la mbele lilifumuka na kioo kimevunjika vibaya sana!
“Shukeni kwenye gari”
Ilikuwa ni kauli ya mwanamme mmoja mrefu, aliyeongea kwa jazba nje mlangoni,ambaye gari yake aina ya Alteza ilikuwa imegongwa na kuumia vibaya mno,kitendo cha dakika tano watu wakaanza kusogea karibu na eneo la tukio,mmoja kati ya wahuni waliosogea walianza kufungua milango ya Verosa,akaliona begi kubwa siti ya nyuma, hapohapo akalichukua begi lenye pesa na kuingia nalo mitini,kimbembe kikabaki kwa Sameer kwani alikuwa ana kesi nyingi za kujibu,hapohapo pombe zikamwisha na kutulia akiangalia gari lilivyopondeka, vibaya sana kwa mbele!



Usiku kucha alifanya kazi bila kuchoka,baridi lilimpiga lakini hakujali. Akiamini kwamba siku zote mtaka cha uvunguni sharti ainame!Hata hivyo nyuma ya kila kitu, alisukumwa na familia yake ambayo ilimtegemea yeye kama muhimili,hakutaka iishi kwa kuteseka hata siku moja,ndiyo maana alijinyima na kuhangaika usiku kucha ili baadaye asipokuwepo duniani waje kuishi vizuri wasiteseke.Alimpenda sana Yusrath na watoto wake mapacha akiamini, hao ndio kila kitu katika maisha yake,usiku wa siku hiyo alifanya kazi sana akiwa saiti mpaka akawa anasinzia kwenye kiti,baridi lilimpiga.
“Meku,nenda ukalale”
Bwana Massawe,alimshtua Ahmed aliyekuwa kwenye kiti,anasinzia alionekana kuchoka!
“Acha tu”
“Kapumzike”
Ahmed hakutaka kukubali, sababu aliamini baada ya kutoka hapo na kwenda kusaini kwamba alifanya kazi ‘overtime’ pesa yake ingeongezeka na hilo ndilo lilimfanya akeshe mpaka usiku kila siku.Ilivyogonga saa sita kamili, ndipo akaamua kwenda kupumzika Mwika,akamuita dereva ili ampeleke anapolala.Sura ya mkewe ilivyomjia akashika simu yake na kutaka kumpigia lakini akasita kidogo, sababu ilikua ni usiku sana,alichotaka kumuuliza ni kuhusu pesa alizomtumia kununua kiwanja,imefikia wapi sababu tangu amtumie mchana, hakupata jibu la kueleweka.Akapata mcheche,akatafakari tena na kupiga simu hapohapo,simu ikaita na kukata.Akapiga tena,ikapokelewa sauti ya kichovu ikasikika upande wa pili, kumaanisha kwamba Yusrath alikuwa katikati ya usingizi mkali.
“Wife”
Ndio neno la kwanza kulisema Ahmed,simuni.
“Baby,kumbe ni wewe.Nimepokea simu bila kuangalia!Nimechoka sana”
“Samahani,nimekusumbua usiku”
“Wala,usijali.Wewe ni mume wangu”
“Mzima lakini?”
“Mimi ni mzima baby,pole na kazi mme wangu”
“Nishapoa,ndiyo narudi sasa hivi nipo njiani.Mke wangu,nafanya haya yote kwa ajili yenu”
“Naelewa Mme wangu,nakupenda sana”
“Hata mimi,alafu hukuniambia umefikia wapi”
“Kufikia waaaapi,niniii?”
“Kuhusu kiwanja”
“Ooooh,nilisahau kukwambia baby.Nilienda kukiangalia,nimekiona love wangu”
Yusrath,akadanganya hakutaka kuonekana mzembe, aseme kwamba hakuenda hata hivyo hakuwa ana mpango wa kununua kiwanja kwa ajili ya Ahmed,alitaka kununua kwa ajili ya Sameer.
“Good,ndiyo maana nakukubali mke wangu”
“Sasa nitaachaje kwenda,ni kiwanja chetu kile baby”
“Walikwambia nini?”
Ahmed,akataka kujua zaidi.
“Kesho,tutaenda tena.Ndio tutaenda na mjumbe kutoka Serikali za mitaa kama shahidi,tutaandikishiana pale na mambo mengine yataendelea”
“Umefanya la maana sana mke wangu,kuwa makini tu.Matapeli wengi siku hizi,nadhani unajua kesi za viwanja zilivyokuwa nyingi.Ukitoka hapo,hakikisha unatembelea majirani,unawauliza historia ya hapo”
“Sawa mpenzi wangu”
“Mimi ndio naingia,kesho nitakupigia ili unipe feedback”
“Okay baby”
Yusrath alianza ghafla kujibu kwa mkato ili Ahmed amalize,sababu alisikia simu nyingine inaingia na alivyochungulia aligundua mpigaji alikuwa ni Sameer,hapo ndipo akapoteza ‘appetite’ ya kuzungumza na mumewe.
“Faisal na Faad,wanaendeleaje?”
“Hawajambo,wanakusalimia baby”
“Haya,Mke wangu.Nikutakie usiku mwema.Alafu….”
Ahmed akawa kama anataka kuongeza kitu kingine,hiyo ilimfanya Yusrath abenue mdomo, akionesha kuchukizwa na jambo hilo.
“Lakini basi,tutaongea kesho,usiku mwema”
Yusrath,hakujibu kitu.Alichokifanya ni kukata simu ili apokee simu ya Sameer ambayo iliita mfululizo.
“Hallooo baby”
Yusrath,akapokea simu kwa mapozi yote lakini habari aliyosikia ilimfanya atake kudondoka chini,Sameer alizungumza akisema kwamba amepata ajali ya gari.
“Gari limepona?”
Hapo hakutaka kujua tena hali ya Sameer,alitaka kujua gari limekuaje.Aliomba Mungu mara mia Sameer aumie lakini sio gari la Ahmed lakini matokeo yake ilikuwa kinyume chake,gari liliumia vibaya Sameer hakuumia hata kidogo!
“Sameer,upo wapi?”
“Naenda kituoni,nipo na maaskari”
“Kituo gani?”
“Sijui,nadhani ni Mabatini”Hapohapo,simu ikakatika!
Yusrath,akahisi kuchanganyikiwa mapigo yake ya moyo, yalidunda kiasi kwamba yalitaka kutokeza nje ya kifua,hakuelewa angemweleza nini mumewe.Kwamba gari limepata ajali?Kivipi?Nani alikuwa anaendesha?Hayo ndiyo maswali aliamini kwamba angekumbana nayo kutoka kwa Ahmed,yakiambatana na kipigo kikali sana.Alivyopiga simu ya Sameer,iliita bila kupokelewa. Asingeweza kulala mpaka asubuhi,usingizi wote ulikata akakaa kitandani kitako, akitafakari ni jambo gani alifanye,hapohapo akapata wazo la kwenda hukohuko,kituo cha polisi,mabatini!

*****
Sameer alishikiliwa na polisi kwa makosa mawili,kulewa na kufanya uzembe barabarani.Askari wa usalama barabarani wasingeweza kumuacha hivihivi hata siku moja kwani kwao kesi hiyo ilikuwa na maslai makubwa sana!Ndiyo maana wakapiga simu,kituo cha polisi cha kati ili difenda ije impakie huku askari hao, wakipima ajali hiyo,hakukuwa na mjadala ikaonekana wazi kwamba mwenye makosa ni Sameer,ndiyo maana wakamtupa kwenye Diffenda ili asubuhi ya kesho yake, kukipambazuka ndipo aeleze na kutoa faini,katikati ya safari askari walimtisha.
“Wewe Segerea,unaendesha gari.Umelewa?Nyie ndio Serikali,inawatafuta sisi tunazuia ajali nyie ndio kwanza hamsikii.Unaenda kufungwa miaka Thelathini Jela”
Askari aliyekuwa pembeni yake nyuma ya Difenda, aliongea kwa mikwara mizito na kuzidi kumtisha ili kuiweka kesi hiyo ionekane ngumu sana,akazidi kuongea maneno mengi, walivyokaribia kituoni ndipo Sameer akaomba ruksa apige simu,kwa mara ya kwanza haikuwa rahisi lakini baadaye alikubaliwa.Hapo ndipo akampigia simu Yusrath na kumuelezea hali halisi,dakika ishirini baadaye wakawa wamefika kituo cha polisi Mabatini,alichoambiwa ni kuacha simu na kuvua mkanda.
“Vua mkanda huo haraka,hatujaja kucheza mdako hapa.Pumbavu”
Amri hiyo ilimfanya Sameer aharakishe kuvua mkanda,akawekwa nyuma ya nondo!
****
Yusrath alihisi kuchanganyikiwa,ubaridi uliokuwa unampuliza kwenye uti wa mgongo hakuelewa umetokana na nini.Kila kitu kwake,kilivurugika kwa kiasi cha kutosha, akatamani yaliyotokea yawe ndoto.Hakujua ni kitu gani akifanye zaidi ya kutembea huku na kule akionekana kama mtu anayetafuta kitu,chumbani.Mara afungue kabati mara afungue mkoba,ghafla akakumbuka kwamba anahitaji kuchukua nauli ili awahi,kituo cha polisi mabatini.Haraka akavaa na kutoka nje mkuku mkuku,akatafuta taxi ili amuwaishe eneo hilo,akiwa njiani alihisi tumbo linamuuma hakuelewa la uwoga ama kuharisha.
Hawakuchukuwa dakika nyingi wakawa tayari wamewasili,kituo cha polisi.Akamlipa dereva ujira wake na kunyoosha moja kwa moja mpaka kituoni.
“Habari yako afande”
Akamsalimia,polisi aliyekuwa zamu siku hiyo usiku.Amevaa jezi za kipolisi,mnene kiasi ana kitambi cha kiaina.
“Salama”
Afande huyo alijibu huku akiendelea kuandika andika vitu kwenye karatasi akijifanya yupo bize.
“Samahani afande”
“Bila samahani”
“Kuna ndugu yangu ameletwa hapa na..”
“Njoo kesho”
“Afande,naomba nimalizie”
“Nakusikiliza”
“Kilichonileta hapa,kitu kingine alikuwa ana gari langu.Ndio kapata nalo ajali”
Hapo afande huyo,akatulia kidogo na kumuangalia Yusrath kwa kitambo.
“Jina lake nani?”
“Sameer”
“Sameer nani?”
“Sameer Rajab”
“Yule ni ndugu yako?”
Afande akauliza,kwa mshangao kidogo ingawa haikujulikana ni kwanini kashtuka namna hiyo.
“Ndio ni ndugu yangu”
“Kivipi?”
Yusrath,akaona kero akaamini kabisa maswali anayoulizwa, hayahusiani na tukio lililokuwepo lakini alielewa kwamba hulka ya mapolisi ni maswali akakumbuka ile nyimbo ‘Una maswali mengi kwani we ni polisi’
“Binamu yangu”
“Hivi binamu,ni mtoto wa shangazi ama Baba Mkubwa?”
“Shangazi”
“Umeolewa?”
Afande akauliza,lakini alipata jibu baada ya kuangalia kidole cha Yusrath kilichokuwa na pete.
“Basi,umeolewa kumbe.Binamu yako unajua ana kesi gani?”
“Hapana”
“Anaendesha gari amelewa,kasababisha ajali.Alafu kitu kingine,walikuwa wanafanya mapenzi ndani ya gari”
Sentensi ya Mwisho ilimfanya Yusrath atulie kidogo na kumtizama Afande huyo kwa umakini zaidi.
“Umesema walikuwa wanafanya mapenzi kwenye gari?”
“Ndio”
“Na nani?”
“Unaniuliza mimi?Lakini inaelekea yule ni Kahaba wa barabarani,hata hivyo gari yako inaletwa italala hapa,utaikuta kesho”
Nguvu zilimuishia kusikia kwamba gari italala kituo cha polisi,aliogopa na alitetemeka kwa wakati mmoja,akaomba kuonana na Sameer,akazuiwa.Alivyojaribu kupenyeza noti ya shilingi elfu kumi kama hongo, Afande huyo akagoma akimtaka arudi kesho asubuhi sana.
“Kesho saa kumi na moja asubuhi,ndio utamuona.Kama una chai,uje nayo”
Hakukuwa na mjadala,Yusrath akaondoka kishingo upande!

****
Hakuamini kama mbele yake,lilikuwa gari la Mumewe, limeharibika vibaya sana!Mbele hakutamaniki,hakujua atamueleza nini Ahmed amuelewe.Alifikiria akachoka akiwa kituo cha polisi nje,analitizama gari hilo kwenye maegesho ya magari mengi yaliyokuwa hapo,mengine yamepata ajali.Kushoto kwake kulikuwa na pikipiki nyingine, zimefungwa akajua hizo nazo zina kesi,machozi yalimlenga kwani kuikomboa gari hiyo ilitakiwa atoe shilingi laki sita taslim,mbali na hapo alitakiwa alipe gari aina ya Alteza ambayo iligongwa kisha amtoe Sameer kituo cha polisi,zilikuwa ni pesa nyingi tena zaidi ya milioni.Alivyopiga hesabu hizo,akahisi utumbo mkubwa unamuuma.Akatembea mpaka kaunta,kituoni.Akataka kuonana na afande aliyeshikilia faili lenye kesi hiyo,hilo halikuwa tatizo akaitiwa wakatoka nje ili kujadili.
“Nachotaka mimi ni kulitoa hili gari kwanza”
“Na huyu mtuhumiwa sijui,ndugu yako?”
“Huyo atajijua mwenyewe,shauri yake”
Yusrath,alizungumza kwa hasira za waziwazi akiwa mwenye wivu kohoni,kitendo cha kuambiwa Sameer alikuwa na mwanamke kahaba ndani ya gari wanafanya zinaa, kilimfanya amchukie Sameer ghafla.
“Na dereva wa gari,Yule aliyegongwa?”
“Nitamalizana naye”
“Basi hilo halina shaka,cha msingi tufanye taratibu za kulitoa gari lako.Nadhani unajua cha kufanya”
Afande alizungumza hivyo,akimaanisha kinachotakiwa ni mafaranga ili gari litolewe eneo hilo yaani Yusrath atoe fedha,hilo ndilo jambo lililoanza kumuumiza kichwa,akafikiria harakaharaka, kichwani kwake akamjia mtu anayeitwa Habiba Seif,afsa mikopo katika benki mojawapo iliyokuwa jijini Dar es salaam.Msichana huyo alikuwa ni rafiki yake,wazo lililomjia aombe mkopo ili akomboe gari kisha akalitengeneze kwenye gereji za wachina, akiamini huko ndipo litarudi kama lilivyokuwa mara ya kwanza, bila kugundulika na Ahmed kwamba lilipata ajali,hakutaka kupoteza muda akasogea pembeni na kuisaka namba ya Habiba Seif,baada ya kuhakikisha, akampigia hapohapo.
“Halloo,Habiba.Unaongea na Yusrath”
“Yusrath,namba yako ninayo za masiku?”
“Nzuri tu,sijui wewe.Familia haijambo?”
“Sisi huku wote wazima”
“Sijui,upo frii tuongee”
“Zungumza tu”
“Nina shida”
“Shida gani?”
“Mkopo”
“Mimi mbona,nishatoka kwenye mikopo siku nyingi sana Yusrath.Siku hizi nimeacha nina biashara zangu”
“Mungu wangu,sijui itakuaje”
“Usijali,kuna mtu nitakuunganisha naye,unahitaji kiasi gani?”
“Milioni tatu hivi kama na nusu”
“Lini?”
“Hata leo”
“Kwa leo,nitakudanganya.Si unajua process za mikopo zilivyo na mlolongo”
“Ndio maana nikakupigia wewe simu unisaidie kwa haraka”
“Ngoja nikuunganishe na dada mmoja anaitwa Leah Evarist,atakusaidia”
Hilo halikuwa tatizo, kupitia mgongo wa Habiba Seif,mambo yakawa marahisi kwa Yusrath,wakafanya mawasiliano na Leah Evarist, ambaye hata yeye alizungumza na mabosi wake akawaambia kwamba mtu atakayemkopesha hana longolongo yoyote na hatokuwa msumbufu na kiasi hiko cha pesa kingerudishwa kwa wakati ikiwemo na riba ya asilimia kumi,mambo yakaenda haraka.
Yusrath akatakiwa aoneshe anapokaa ili wathaminishe vitu alivyokuwa navyo, wavipige picha kama kuviweka bondi,hiyo ndiyo ilikuwa taratibu ya kwamba endapo atashindwa kulipa mkopo huo ndani ya miezi sita basi vitu vyote vya ndani, vitakuwa halali ya benki na vitapigwa mnada.
Mbele ya mashahidi, Yusrath aliweka sahihi yake ambapo juu ya maelezo hayo kwenye karatasi kuliandikwa mali zitakazochukuliwa na benki kama t.v,meza,jiko,kitanda,vyombo,kabati,friji na vingine vingi,mbaya zaidi Ahmed hakushirikishwa kwenye mkopo huo.Kifupi,kama Yusrath angeshindwa kulipa deni hilo kwa wakati,wangepukutisha kila kitu bila huruma na kubaki kweupe.
“Basi,hakuna shaka.Mkopo uje uchukuwe kesho asubuhi,hii ni copy yako.Sisi tunaondoka na Original,tukutakie siku njema”
Afsa Mikopo Leah Evarist pamoja na wasaidizi wake,waliaga huku wakiangalia vitu vya thamani, vilivyokuwa ndani ya nyumba hiyo.Yusrath,akawasindikiza mpaka getini, kisha kurudi mpaka seblen,akashusha pumzi huku akitabasamu baada ya kila kitu kukamilika,mzigo uliokuwa kichwani kwake sasa aliutua!


Usiku wa siku hiyo kwake ulikuwa mrefu kukucha,masaa yalijisogeza mwendo wa ajuza akitamani kupambazuke mapema akachukuwe mkopo wa pesa alizohaidiwa atapewa kisha akatoe gari na kwenda kulikarabati kwenye gereji za kichina,akiamini huko kuna mafundi wenye taaluma zao!Aliliamini hilo sababu alisikia sifa za wachina hao waliokuwa Mikocheni kwamba wanatengeneza na kunyoosha magari vizuri,ndiyo maana sehemu ya harakaharaha iliyomjia ni hiyo.
Nyuma ya kufanya hayo yote alitaka Ahmed, akirejea kutoka safarini asijue lolote lile juu ya gari kwamba lilipata ajali,usingizi kwake siku hiyo ulikuwa ni wa mang’amung’amu.
Lakini, hata kama usiku uwe mrefu vipi ni lazima kukuche,hicho ndicho kilichotokea.Ilivyogonga saa kumi na moja asubuhi,alitoka kitandani na kuanza kujiandaa.Saa kumi na mbili kamili,akaanza safari ya kuelekea benki ili akachukuwe mkopo wa pesa,alitumia usafiri wa bodaboda ili awahi kufika.Ni kweli aliwahi sababu alifika na kukuta bado benki haijafunguliwa,ikamlazimu asubiri mpaka saa tatu kamili ndipo ilifunguliwa,akaingia moja kwa moja na kueleza shida yake.
“Sawa,subiri pale kwenye kiti”
“Nishaongea na Leah Evarist”
“Taarifa zako tunazo,subiri dakika kumi,atakuja”
Kitendo cha kupigwa benchi kilimfanya afure kwa hasira,aliona kama kukaa hapo ni kupotezewa muda, wakati yeye alitaka kutatua tatizo lake siku hiyohiyo,akomboe gari kituo cha polisi na kulipeleka gereji akiamini siku hiyohiyo lingetoka.
Dakika kumi zikawa kama mwaka kwake,ndiyo maana hakutulia juu ya kiti,akawa kama mwanafunzi aliyekali banseni bana kwenye daladala,mara abadili mkao huu mara akae upande upande ili mradi muda uwende tu,akaona kama anacheleweshwa vile.Alivyomuona Leah Evarist akasimama kwa haraka na kumuendea kwa kasi.
“Umefika muda?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa mwanamke huyo mnene kiasi,mwenye rangi ya maji ya kunde, mrefu wa kimo mkononi ameshika funguo za gari,kwa harakaharaka alikuwa ni mwanamke mwenye uwezo kifedha.
“Sio saana”
Hakutaka kusema ukweli na kuonekana ana shida.
“Nifuate ofisini kwangu”
Wote wakaanza kuongozana, mpaka ofisini, ambapo huko hakukuwa na muda wa kupoteza,Yusrath akapewa pesa na kuambiwa asaini baadhi ya karatasi, akithibitisha kwamba amepokea pesa,kuanzia hapo hakuwa na muda wa kupoteza tena,akatoka nje na kuchukua bodaboda, ambayo ilimpeleka mpaka Kituo cha polisi mabatini.Hapo,alimtafuta askari aliyeshikilia faili la gari na kesi ya Sameer,akampa kiasi cha shilingi laki moja na nusu,mambo yakaenda haraka sana.Gari likaachiwa,kilichomuumiza kichwani jinsi gani angelipeleka Mikocheni,hakuweza kuendesha gari.
“Kuna kijana hapa,ngoja nimuite.Lakini inabidi umpe kifuta jasho”
Askari huyo,alipendekeza akionekana yupo upande wa Yusrath na anataka kumsaidia,hiyo yote ni baada ya kupewa kitita cha pesa.
“Hilo halina shida,ilimradi anifikishie gari langu Mikocheni kwa wachina”
“Nampigia simu sasa hivi,ngoja nikakuchukulie funguo zako za gari,alafu vipi huyo kijana?”
Askari,alihitimisha na swali akimaanisha Sameer.
“Ngoja,nitengeneze kwanza gari”
Jambo lililotakiwa kufanyika,halikuchukuwa muda mrefu.Baada ya dakika kumi akatokea kijana mmoja mrefu,mwembamba.Ambaye kwa muda mfupi tu Yusrath aligundua kwamba anaitwa Kavishe.
“Habari,dada”
Kavishe,akasalimia akiwa na funguo za gari mkononi kwa kuwa alipewa maelezo yote,hakukuwa na haja ya kuuliza zaidi.Alichotaka kujua kwa wakati huo, gari liko wapi,wakatembea pamoja mpaka kwenye gari na kulikagua vizuri.
Uzuri alivyoliwasha liliwaka,akapewa kibali maalum kutoka kituo cha polisi ili awaoneshe maaskari wa usalama barabarani endapo wangemletea usumbufu, wa aina yoyote ile.
Safari ilianza mara moja, bila kupoteza wakati,licha ya hayo ndani ya gari hakukuwa na maongezi ya aina yoyote ile,Yusrath alijikita kwenye mawazo mazito sana!Alimuwaza Ahmed na familia yake kwa ujumla,akatumia muda huo kufikiria makosa aliyokuwa nayo,mara ghafla akakumbuka pesa alizompa Sameer ili anunue kiwanja,mapigo yake ya moyo yakabadilika ghafla,yakamuenda mbio.
Hakuwa mwenye uhakika kama mwanamme huyo alinunua kiwanja kweli ama pesa hizo alimuhonga kahaba ambaye, aliambiwa walikuwa wote ndani ya gari.
Kutokana na msongamano wa magari,iliwalazimu watumie lisaa limoja na dakika kumi na tano kufika Mikocheni kwa Warioba.Nje,kulikuwa na geti kubwa pembeni kuna magari mengi ya kisasa,Kavishe akapiga honi, geti likafunguliwa na mbele yao walikumbana na uwanja mkubwa sana,kandokando kulikuwa na magari mengine, mengi yakisubiri huduma ya ukarabati lakini pembeni pia kulikuwa na magari ambayo tayari yalikarabatiwa ipasavyo, yakawa kama mapya vile.
“Kaka,ahsante nadhani mimi nishafika.Chukua hii,utakunywa supu”
Yusrath,alitoa shukrani huku akitoa shilingi elfu ishirini kutoka kwenye mkoba wake,akampa bwana Kavishe kama shukrani.
“Poa sista,aminia.Mimi ngoja,nidandie gari hapo.Naenda Buguruni kuna jamaa naenda kumuona one time”
Bwana Kavishe,akajisemesha mwenyewe hata hivyo hakuulizwa anapoenda,Yusrath hakujibu chochote badala yake alifuatwa na Mwanamme mmoja mnene kiasi,alionekana kuwa ni muhusika,akamuuliza maswali ya hapa na pale kuhusu gari,alivyolitizama akamuhakikishia kwamba Verosa hiyo, ingekuwa kama imetoka ‘Show room’ jamaa huyo alizungumza kwa kujiamini.
“Itakuwa kama Mpya,hapa ndio cheng Garage,njoo kesho asubuhi,ufate gari yako”
“Itakuwa shilingi ngapi?”
“Njoo,ofisini uongee na bosi”
Wote wakaongozana,huko Yusrath alipewa bili nzima ya marekebisho ya gari.
“Kunyoosha hii gari,kupigwa putty ya kisasa na rangi yake ni metaliki hii,niamini.Hii itarudishwa mpyaaa”
“Nitashukuru kaka angu”

****
Wachina hawakuwa watu wenye longolongo,siku iliyofuata Yusrath hakuamini baada ya kufika na kuoneshwa gari,macho yalimtoka pima.Akalisogelea karibu na kulishika vizuri.Hakuamini kama gari lingerudi na kuwa kama lilivyonunuliwa,akazidi kustaajabu.Furaha aliyopata,haikuwa na mfano wake,akiamini kwamba hata kama iweje Ahmed asingejua kwamba gari yake, ilipata ajali na ilipondeka vibaya sana!Akazunguka,mpaka mbele kabisa na kuitizama kwa umakini,gari ilipigwa rangi vizuri na kunyooshwa ipasavyo,haikuwa rahisi kwa mtu yoyote yule kugundua.Hiyo ilimfanya atabasamu na kumtizama kijana huyo,ambaye kwake alimfananisha na mkombozi wa maisha yake.
Kilichofuatia hapo ni kutoa malipo ya marekebisho na kuuliza kama kuna mtu anayeweza kuendesha gari,hilo halikuwa tatizo,akapewa msaada huo ambapo gari, lilipelekwa mpaka Ubungo Kibangu.
“Paki hapo,sogea mbele kidogo”
Yusrath,alimuelekeza dereva aliyemsaidia ili aliweke gari vizuri sehemu ambayo, Ahmed alipaki mara ya mwisho,kumaanisha kwamba baada ya hapo lisingetoka tena,lilivyoweka sehemu yake akashukuru na kumpa jamaa huyo noti ya shilingi elfu kumi kama ahsante.
“Usijali Mama,nitalipwa na ofisi”
“Sikatai lakini,hii ni yako weka mfukoni mdogo wangu”
“No,nimekufanyia tu bure.Ubinadamu,shika funguo zako!Siku njema”
Yusrath,hakuamini kama jamaa huyo amegoma kupokea pesa,ilikuwa ni tofauti na wanaume wengine wa kibongo ambao wakitoa msaada ni lazima wadai pesa,hakuwa na haja ya kumlazimisha,akampa shukrani na kumsindikiza mpaka getini kisha kurudi ndani,ambapo huko alipitiliza mpaka chumbani,akavua nguo zote na kuingia bafuni kujimwagia maji.
Saa saba mchana,simu ilimshtua akiwa kitandani na watoto wake mapacha, Faisal na Faad,aliyekuwa anapiga ni mumewe Ahmed,akapokea na kutabasamu.
“Sweart heart”
Hilo ndilo neno la kwanza,lililomtoka Ahmed kinywani.
“Yes baby”
“I miss you,nawamisi sana”
“Hata sisi mme wangu”
“Mpo salama lakini?”
“Ndio,tunakusubiri kwa hamu kubwa”
“Natamani kuwaona,nina zawadi zenu nyingi hapa”
“Wooow baby,zawadi gani?”
“Utaziona mke wangu,punguza mushkeli”
“Mushkeli ndio nini baby?”
“Punguza,mcheche”
“Moshi,huko.Watu wa huko wamekuharibu na maneno hayo,muone vilee”
“Hahaha,nakutumia laki mbili baby,ya hapo nyumbani.Mle kuku mnunue stock ya ndani”
“Sawa Mme wangu,ahsante sana”
“Vipi Kiwanja,ulifatilia?”
“Baby,nilifuatilia lakini nilivyoenda kule Mjumbe hakuwepo.Nikashindwa”
Yusrath alidanganya,kusema ukweli swali hilo lilimfanya aogope sana,mapigo yake ya moyo yakapiga kwa kasi.
“So far,kesho atakuwepo?”
“Yes”
“Sawa,Darling.Ukikwama niambie”
“Nitakutaarifu,mme wangu”
Baada ya kukata simu,sura ya Sameer ikamjia.Ilikuwa ni lazima amuhoji kama alinunua kiwanja na kama bado, amuulize ni kwanini?Ili kufanya hivyo ilikuwa ni lazima awasiliane na Kamanda Akida,ili Sameer aachiliwe amuulize,japokuwa alitaka kwanza Sameer asote rumande ili amfunze adabu.
Hilo halikuwa tatizo kwa Kamanda Akida,akapewa pesa kidogo ili alegeze uzi,hatimaye saa kumi jioni Sameer akaachiwa huru.Akapewa simu na kitu cha kwanza kukifanya Yusrath ni kumpigia simu mwanamme huyo ili kumuuliza ni wapi amefikia kuhusu kiwanja.
“Achana na mimi”
Hiyo ndiyo sentensi ya kwanza kujibu Sameer kwa jazba.
“Sameer, unasemajee wewe Mbwa?”
“Nimekwambia achana na mimi,tena unikome”
“Sio kirahisi hivyo,nadhani hunijui mimi vizuri Malaya mkubwa,sikutegemea kama ungeweza kutiana na kahaba ndani ya gari langu”
“Unasemajeee?”
“Hujui,ulichokifanya ama?”
“Yaani badala ya kunipa pole,unaniuliza kuhusu kiwanja na vitu vya ajabu,sikuelewi unajua.Mimi na kiwanja,kipi bora kwako?”
“Kiwanja,kiwanja ndio bora kwangu.Ndio maana nimeuliza kilipo,na ninataka kujua,kilipo nipo siriazi”
Yusrath,alizungumza kwa jazba tena kwa sauti kubwa, iliyojaa hasira za waziwazi,rangi yake ya mwili ikabadilika na kuwa nyekundu ghafla.Hiyo ilimfanya Sameer,apoe kidogo lakini sio sana, hata hivyo hakutaka kuonesha kwamba ana babaika.
“Kiwanja,kipo”
“Wapi?”
“Mbezi,Msakuzi”
“Mbona unanichanganya?”
“Kivipi?”
“Mara ya kwanza uliniambia sijui wapi kule mbele ya Mbagala”
“Kile kimeuzwa tayari”
“Okay,nitakiona lini hiko kiwanja?”
“Hata sasa hivi”
“Sasa hivi,siwezi.Labda kesho”
“Tufanye kesho kutwa”
“Poa”
*****
Yusrath hakukoma,akawa kama Kuku.Akasahau majanga yote yaliyomkuta, baada ya kukutana na Sameer siku hiyo jioni saa kumi na mbili,hata yeye alijishangaa kwani aliapia hatoweza kufanya tena ngono na Sameer na kuapia kwamba wangeachana lakini badala yake,walivyokutana walitafuta gesti moja iliyojificha,huko walifanya ngono kisawasawa.
“Aaaah bebii,ashsssi aaaah”
Yusrath,alitoa miguno yake kama kawaida,akasahau kila kitu!Akahisi kama yupo bahari ya Hindi,anaogelea.Sameer akamuweka kila mkao,akamshughulikia barabara,akimuweka kila staili na kumtomasa kila mahali,mara amnyonye shingo,amtomase chuchu.
Ambidue bidue huku na kule,ili mradi rahaa duniani.Mpaka inafika saa mbili ya usiku kila mtu alikuwa ameridhika,wakaagana.
“Njoo,uchukuwe gari kesho,unipeleke huko Mbezi msakuzi.Nikaone hiko kiwanja”
Yusrath,alisema wakiwa wanaagana, wakikumbatiana kwa mahaba,hilo halikuwa tatizo kwa Sameer sababu aliamini kumuonesha kiwanja Yusrath lilikuwa ni jambo dogo sana,usiku wa siku hiyo akazungumza na dalali mmoja anayefahamika kwa jina la David Mwasha,akampanga na kumpa picha halisi!
“Unataka kumpiga au?”
David Mwasha,akauliza simuni akitaka kujua mchakato mzima.
“Nitakuchana,cha kufanya wewe poa kidogo!Mimi nitakuja na huyo manzi,nitajifanya kama nimepanunua”
“Freshi,kwahiyo lini utakuja?”
“Kesho mchana,nitakuvutia waya kamanda”
“Aminia,uje mapema sababu kiwanja hiko.Kina maseke,nimewauzia watu karibia watano tayari”
“Nitakupooza kidogo,usije uka devela tu lakini utaniangusha kinyama yaani”
“Siwezi”
“Poa”
Sameer akawa tayari,amempanga mshkaji wake ili kesho yake,ampumbaze Yusrath akimdanganya kwamba ndicho kiwanja alichonunua.

*****
Masaa ishirini na moja,yakawa yametimia.Yusrath na Sameer wakawasili siku hiyo mchana Mbezi,msakuzi.Wakaingia barabara ya vumbi wakanyoosha moja kwa moja na kutokea huko Msakuzi,ambapo kulikuwa na majumba mengi ambayo watu walikuwa wanajenga.
“Ilibidi niongezee pesa yangu,ela uliyonipa haikutosha baby”
Sameer,alivunja ukimya baada ya kupunguza spidi na kupanda tuta, akazidi kusonga mbele zaidi.
“Ahsante baby,nitakulipa usijali”
“Usiwe na wasiwasi,hiki ni kiwanja chetu sio mbaya”
Kwa mara nyingine tena Benjamin Ngowi,aliliona gari la Ahmed Kejeme maeneo ya Mbezi.Siku hiyo uvumilivu ukamshinda yakamfika shingoni,akaamua kulifuatilia mpaka mwisho lilivyopaki,nayeye akateremka kutoka ndani ya gari lake,akawaendea mpaka walipo.
“Shem mambo vipi?”
Sauti hiyo,ilimfanya Yusrath,aishiwe nguvu kwani hakutegemea kumuona Benjamin Ngowi,eneo kama hilo isitoshe pembeni yake alisimama na Sameer.
“Sikia shem,ebu achana na mambo unayofanya.Huyu kijana,atakupotosha!Wewe ni mke wa mtu,una watoto wadogo kwanini unamfanyia Ahmed hivi?Unakosa nini kwake?”
Benjamin alitoa ya moyoni,akazungumza kwa hisia kali sana tena kwa uchungu!
“Umemaliza?”
Yusrath,akauliza kwa dharau.
“Nitamwambia Ahmed,lazima nitamwambia siwezi kulifumbia macho hili swala”
“Okay mwambie,tuone mimi nawewe nani zaidi”
Yusrath alizungumza kwa kujiamini kuliko kawaida,hiyo ilimfanya Sameer amtizame Benjamin kuanzia juu mpaka chini kwa nyodo.
“Kaka,ebu acha kufuatilia maisha ya watu.Mbona unanifuatilia sana?Achana na sisi fanya mambo yako,mind your own business bro”
“Kijana,achana na huyu mwanamke ni mke wa mtu.Nadhani unajua mke wa mtu ni sumu”
“GETO NINA MAZIWA”
Benjamin hakutaka kujibizana,akatembea mpaka kwenye gari lake na kuchukua simu kwa niya moja tu,amtafute Ahmed amwambie kila kitu kwani kitendo hiko kilimuuma sana,hakuelewa kwamba Yusrath kamzidi akili kwani wakati huohuo, alitoka pembeni na kumtafuta Mumewe Ahmed hewani alivyompigia tu simu ikapokelewa,akajifanya analia.
“Baby,are you okay?Mbona unalia?Kuna nini?”
“Ba…by…Why me?Kwani..ni hivi lakini?”
“Kuna nini?Sikuelewi ujue?Kuna msiba?”
“Baby pleas..e rudi Da..r nateseka sa..na.Nimeumia”
Hapo Yusrath,akajifanya kuvuta kamasi ili atengeneze mazingira ya kuonekana analia kwa uchungu.
“Yusrath,relax uniambie. Kuna nini kwani Mke wangu?”
“Rafiki ya..ko baby”
“Rafiki yangu?Nani?”
“Leo..nilivyokuwa nyu..mbani alikuja”
“Naniiii?”
“Benjami..ni Yule Benjami..ni Ngowi”
“Benja Ngowi?!”
“Ndi..o baby”
“Kafanya nini?”
“Alivyoku..ja,akanikuta jiko..ni,dada aliku..wa sokoni ananunua vitu vya nyum…bani tukabaki wawili tu…Baby najua atakuambia mambo ma..baya sababu ameniambia atafanya kila awezalo kututenganisha...”
“Honey,mbona sikuelewi,Kuna nini?”
“Benja..min alitaka kunibaka”
Yusrath,alisema maneno hayo huku akijifanya kulia kwa uchungu sana!
“Whaaaaaaaaaaaaaaaaat?”(Niniiiiii)
Ahmed,akauliza kwa ghadhabu!Moyo wake,ukapiga paa kwa mshtuko,hasira zake zikampanda mpaka kiwango cha juu kabisa, baada ya kusikia rafiki yake Kipenzi Benjamin Ngowi,alitaka kumuingilia kimwili mkewe wa ndoa Yusrath,akaapia siku hiyohiyo atapanda ndege na kurudi jijini Dar es salaam!


Presha ya Ahmed ilipanda kwa kiasi kikubwa sana,hiyo ikafanya mapigo yake ya moyo yapige kwa nguvu na kupeleka damu mbiombio,hali hiyo haikuwahi kumtokea tangu azaliwe, ndiyo maana akajishangaa.Maneno ya Mkewe yalimshtua sana kwamba Benjamin Ngowi alitaka kumbaka,japokuwa hakuwa ana uhakika na tuhuma hizo lakini moja kwa moja alichukulia jambo hilo litakuwa la kweli sababu isingewezekana hata kidogo, Yusrath amsingizie Benjamin Ngowi.Kilichomfanya aamini jambo hilo moja kwa moja,ndiyo huyo rafiki yake mwenye mazoea ya kufika nyumbani kwake,mara kwa mara.Swali alilokuwa anajiuliza likapata jibu lake,hapohapo akakata simu na kumpigia tena Yusrath na kuanza kumuhoji akimfariji kwamba asijisikie vibaya, kila kitu kitakuwa sawa na siku hiyohiyo, angerejea jijini Dar esa salaam.
“Bab..y utakuja leo?”
Yusrath akauliza akiigiza kutoa sauti ya kwikwi,alikuwa anataka kupata uhakika ili awahi kurudi nyumbani.
“Ndio,nitakuja leo”
“Afa..dhali baby,please naomba uje.Naogopa kukaa nyumbani”
“Nakuja mke wangu”
Wakati akiwa anazungumza na Mkewe,simu nyingine iliingia akatoa sikioni ili kujua ni nani mpigaji.Akaitizama simu hiyo kwa umakini baada ya kugundua mpigaji ni Benjamin Ngowi,akashusha pumzi ndefu akaendelea kuitizama bila kuipokea.
“Okay,baadaye mpenzi”
Alivyosema hivyo akakata simu na kuipokea simu ya Benjamin akitaka kumsikiliza.
“Ahmed,mambo vipi kaka”
“Safi tu”
Ahmed,alijibu kifupi tofauti na siku zote ambapo akipokea simu huchangamka,tukio hilo lilimshangaza sana Benjamin Ngowi.
“Vipi,unaumwa?”
“Ninasumbuliwa tu Malaria”
“Pole sana ndugu yangu,ushaenda hospitali”
“Ndio”
“Upo sehemu nzuri ili tuweze kuongea?”
“Zungumza tu”
“Kuhusu Mkeo”
Hapo,Ahmed hakujibu kitu chochote kile,akakumbuka maneno ya Yusrath akimueleza mbinu alizopanga Benjamin Ngowi kwamba angefanya juu chini ili awagombanishe,licha ya kuwaza hayo yote lakini hakutaka kutia neno lolote lile.
“Mke wangu,amefanya nini tena?”
“Kuna mambo ya ajabu sana,anafanya”
“Mambo yapi?”
“Unarudi lini?”
“Mambo gani kafanya Benjamin?”
Hapo Ahmed akauliza kwa sauti ya ukali kidogo.
“Ukirudi tutaongea vizuri lakini kuwa makini na Mkeo,mambo anayofanya niya aibu sana”
“Benjamin Ngowi”
Ahmed akaita tena akitumia majina yote mawili,hiyo ilimaanisha kuna jambo la muhimu anataka kumueleza.
“Naam”
“Ujue mimi nawewe tunaheshimiana sana”
“Naelewa hilo”
“Sasa mb….”
Alivyotaka kumalizia anachotaka kukisema, akasita na kuupiga mdomo wake ‘stop’ asiropoke ili asije kuharibu ushahidi,ilikuwa ni lazima kwanza arudi Jijini Dar es salaam ampe Benjamin Ngowi vipande vyake,hilo alilipanga baada ya kukata simu na kumpigia Bosi wake akimuomba ruksa, akidai mkewe anaumwa sana yupo hospitalini.
“Unahitaji kusafiri lini?”
Bosi,aliuliza simuni.
“Leo bosi kama ikiwezekana”
“Unajua huo mradi simuamini mtu yoyote yule,isipokuwa wewe.Unatarajia kukaa huko siku ngapi?”
“Wiki hivi bosi”
“Wiki ni nyingi Ahmed,fanya siku tano.Andika vocha ya nauli,ufanye utaratibu wa kurudi”
“Ahsante bosi”
Ahmed,hakutaka kupoteza hata sekunde moja!Alichokifanya ni kupanga nguo zake, ndani ya begi lake dogo,alilosafiri nalo.Akaweka kila kitu sawa na kutoka nje!Safari hiyo hakutaka kumuaga mtu,alichokifanya ni kutoka barabarani ili atafute usafiri.Kwa kipindi hiko,gari aina ya Noah ndizo zilitumika kupakia abiria.
“Wapi hiyo?”
Amed,akamuuliza Kondakta mmoja baada ya kufungua mlango wa Noah.
“Moshi,Mjini”
“Naenda Uwanja wa Ndege”
“Panda twende,K.I.A?”
“Huko huko”
Kitendo cha kuingia ndani ya gari na abiria kutosha,gari ikaanza safari mara moja.
*****
Kitendo cha kusikia Ahmed anarudi siku hiyohiyo kilimfanya afanye mambo yake harakaharaka,alielewa ni lazima jioni hiyo angerejea pengine asingepiga hata simu.Alichokifanya ni kumuomba Sameer warudi nyumbani haraka iwezekanavyo,hilo halikuwa tatizo, baada ya kuoneshewa kiwanja feki na kuridhika wakarudi nyumbani,hapo Sameer alipaki gari kama alivyolikuta mara ya mwisho, kisha kuingia ndani,ambapo hapo alikula chakula kilichoandaliwa na dada wa kazi.
“Kula,harakaharaka.Mme wangu anaweza kuingia hapa,muda wowote ule”
“Kwani,hajakupigia simu?”
“Anaweza asinipigie simu”
“Atakupigia”
“Kula baby haraka,nakuomba,Moshi na hapa sio mbali”
“Sasa mpaka nikabwe,niache basi nile taratibu.Kula ni ibada”
Wasiwasi mkubwa ulikuwa kwa Mumewe, endapo angerudi na kumkuta Sameer ndani ya nyumba yake, tena mbaya zaidi anakula chakula,akakumbuka kipigo cha siku moja baada ya Mumewe kumkuta Shotola ndani,hiyo ilimaanisha kuna makosa mengi ya kufanya lakini sio kurudia yaleyale.
Sameer alivyomaliza kula,akaletewa na juisi akashushia. kila kitu kwake kilikuwa sawa,hakuwa mwenye wasiwasi wa aina yoyote ile,akamuaga Yusrath kwa mabusu motomoto na jambo hilo lilishuhudiwa na mfanyakazi wa ndani Hadima,akiwa jikoni alitingisha kichwa na kusikitika sana lakini hakuwa nala kufanya, kilichomleta hapo ni kufanya kazi,sio kufuatilia maisha ya wengine.
Kitendo cha kuagana na Sameer kutoka nje,hazikupita dakika tatu mlango ukagongwa,Yusrath alivyofungua mlango mapigo yake ya moyo yakapiga kwa nguvu,hiyo ni baada ya kumuona Ahmed mbele yake,amevaa begi dogo mgongoni.
“Karibu mme wangu”
Yusrath,akasema huku akiwa kama mtu aliyepigwa na butwaa,hakuwa ana uhakika kama Sameer alionana naye nje wakati anatoka getini ama walipishana.
“Za hapa?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Ahmed huku akiingia ndani.
“Sio nzuri wala sio mbaya”
“Kwanini?”
“Kama nilivyokwambia baby,naogopa”
“Faisal na Faad,wazima?”
“Ndio,wamelala”
Ahmed,akatembea mpaka seblen alivyotaka kukata kona ili apite kwenye korido,akasita kidogo baada ya kuona mezani kuna vyombo na pembeni kuna glasi yenye juisi nusu.
“Leo umekula mapema sana,sio kawaida yako”
Yusrath,akashtuka alivyoangalia mezani hapohapo akapata jibu la haraka.
“Tangu jana mchana sijala baby,ndio maana nimekula mapema leo”
Akabuni uongo kwa sekunde hiyohiyo sifuri,Ahmed hakutaka kuuliza maswali mengine zaidi.Alichokifanya ni kunyoosha moja kwa moja mpaka chumbani kwake,Yusrath hakutaka kubaki nyuma nayeye akaunga mkia,akaingia chumbani na kufunga mlango.
“Nini kimetokea?Ilikuwaje?”
Kitendo cha Yusrath kukaa kitandani,akakumbana na maswali ya Ahmed hiyo ilimfanya ababaike kidogo.
“Ni ngumu kuamini baby,lakini hata mimi nashindwa kuelewa”
“Ndio maana nimekuja,ili unieleweshe”
“Siku hiyo ilikuwa mchana baby nipo jikoni,nimemtuma dada dukani.Mlango ukawa umegongwa.Nilivyofungua,nikamkuta ni Benja.Sikua na uhakika kama alikufuata wewe,nadhani ulimwambia kama umesafiri?”
“Endelea”
Ahmed,alikuwa makini kusikiliza maelezo ya Yusrath hasira zikaanza kumpanda taratibu kwani hakuamini kama Ngowi angeweza, kufikia hatua hiyo ya kutaka kumbaka mkewe,Yusrath hakuishia hapo akazidi kuongeza chumvi akisema kwamba Ngowi alikuwa akimtaka tangu siku nyingi sana.
“Kwanini hukuniambia kama anakutaka?”
“Niliogopa”
“Alinipigia simu leo aka…”
“Pia alisema atafanya juu chini,uniache”
Yusrath akajiwahi ili ajihami,bomu alilokuwa anatengeneza aliamini lilikuwa kubwa na muda mfupi lingeenda kulipuka sababu alimjua fika Ahmed,ni kweli alikuwa kama ametabiri vile.Ahmed akaomba funguo za gari na kutoka nje,akafungua mlango alivyoingia tu.Akahisi kuna kitu cha tofauti,kwanza kiti cha dereva, kilivutwa sana kwa nyuma,alivyoangalia geji ya mafuta akakuta ni tofauti na alivyoyaacha.Alama ya kiulizo ikaja kichwani,nani aliyetoa gari?Hapohapo akashuka ili kujiridhisha akaangalia chini,akaona kuna alama za matairi,hapo ndipo akapata jibu la swali lake kwamba gari lake lilitoka nje,akamezea na kuingia ndani kisha kupiga honi,Hadima akatoka na kufungua geti.Alivyofika getini kabla ya kutoka,akasimamisha gari na kushusha kioo.
“Nani alitoa gari?”
Lilikuwa ni swali,lililomlenga Hadima.Hakujibu chochote,akabaki anamtizama Ahmed!
“Sijui Baba”
“Lakini lilitoka?”
“Sina uhakika”
Sio kwamba Hadima hakuelewa kila kinachoendelea, bali hakutaka kuongea chochote.
“Okay”
Ahmed,akakanyaga mafuta na kuchukua simu yake ambapo hapo, alimtafuta Ngowi hewani akitaka waonane,Mikasa.
“Umerudi?”
Ngowi,akauliza kwa mshangao.
“Ndio,mbona unashangaa?”
“Sikutegemea,sawa nakuja.Ngoja nimwachie kijana duka hapa”
“Utanikuta”
Hakukuwa na maongezi marefu sana, simu ikakatwa.Kama alivyotarajia ndivyo ilivyokuwa,Ahmed akawa wa kwanza kufika eneo la tukio,dakika kumi baadaye Ngowi,akafika nayeye.
“Pole na safari”
Ngowi,akasema lakini Ahmed hakuonesha uchangamfu kama siku zote.
“Najua ulitamani nife ili umchukuwe mke wangu”
Sentensi hiyo ilikuwa mshale wa moto,Benjamin akapigwa na butwaa la waziwazi.
“Sikiliza Benjamin,wewe ni rafiki yangu sana.Lakini nachokuomba kuanzia leo,sitaki ukanyage kwangu.Namba yangu kwenye simu yako futa,tusiwasiliane tena al..”
“Ah..”
“Nyamaza,nimalize”
Hali ya hewa ikawa tayari imebadilika,Ahmed aliongea kwa kufoka hio ikafanya wateja waliokuwa ndani ya bar hiyo,wawaangalie,alivyomaliza kutoa dukuduku lake akasimama lakini Benjamin akamzuia kwa kumshika mkono.
“Ahmed kaa chini,uniambie tatizo nini?”
“Siwezi kukwambia,kwani hujui ulichokifanya?”
“Ahmed,ebu kaa chini”
Benjamin akatumia busara zote,hakutaka kuonyesha jazba akitaka kujua nini tatizo.Hapo ndipo Ahmed akafunguka bila kukwepesha,akasema yote kwamba Benjamin alitaka kumbaka mkewe,akahitimisha kwa kusema kwamba anamtaka kimapenzi.
Jambo hilo lilimshangaza sana Benjamin,hata hivyo alipanga asiropoke lakini ilibidi afunguke na kusema ukweli kilichotokea.
“Na niliwakuta wanafanya mapenzi,ndani ya gari lako.Kwa macho yangu”
Yusrath akawa amemwaga mboga Benjamin Ngowi kamwaga ugali na maji ya kunawa,japokuwa Ahmed alisikia maneno hayo,lakini badala ya kukasirika akatabasamu.
“Benjamin,usinifanye mimi mtoto mdogo!Kwahiyo unatunga ili nimuache mke wangu,kwa taarifa yako siwezi kumuacha”
“Ahmed,kama kweli unataka kumjua mwizi wako.Fanya jambo moja ngoja nikwambie cha kufanya”
Benjamin Ngowi,akatoa mbinu.Akamwambia jinsi ya kuweka mtego ili wamnase Sameer.Japokuwa Ahmed alionesha kugoma lakini baadaye alikubali.
*****
Siku tatu zilipita Yusrath akijua kila kitu kipo sawa na hali ya hewa tayari imetulia,mbaya zaidi Ahmed akampumbaza akimuonesha kila aina ya mapenzi,akajifanya kila kitu kimeisha na tayari alimfunza adabu Benjamin Ngowi,siku ya nne ilivyofika akamuaga mkewe akimwambia kwamba atasafiri na kurudi kazini Mkoani,Kilimanjaro!
“Okay baby,mimi napanda pikipiki ili niwahi ndege naona nimechelewa sana”
Ahmed alimwambia mkewe siku hiyo mchana,akaangalia saa yake akionekana mwenye haraka sana.
“Darling,muda wote ulikuwa wapi?”
“Sikuangalia vizuri tiketi kama ndege inaondoka muda huu”
“Sawa baby safari njema”
Akiwa mwenye haraka,akatoka nje na kutafuta pikipiki.Pembeni upande wa pili kulikuwa na magari mawili moja ni Landcruiser lingine Nissan Patrol,magari hayo yalikuwa yapo kwa ajili ya kazi maalum, ambayo Ahmed aliisuka.Ahmed hakupanda pikipiki ili aende uwanja wa ndege kama alivyomuaga Yusrath bali alienda kusimama Riverside, hapo alishuka na kuingia kwenye kibanda kimoja cha muuza chips na kukaa.
“Mtaniambia kinachoendelea”
“Poa”
Ulikuwa ni ujumbe mfupi,alioutuma Ahmed kwa watu wake, aliowaweka nyumbani kwake ili wamkamate Sameer.Hakuelewa ni kitu gani akifanye akimshika mwanamme huyo,anayemmegea mkewe.Dakika ishirini baadaye,akatumiwa meseji kwamba Sameer amefika tayari.Akakaa vizuri,kujua kinachoendelea.

Habari ya kusafiri kwa Ahmed ilikuwa njema sana kwake siku hiyo,akamtaarifu Sameer simuni baada ya Ahmed kutoka,akimwambia akodi pikipiki ili awahi.Sameer bila kujua kwamba anaingia ndani ya kumi na nane za Mke wa mtu na siku zake arobaini tayari zimefika,akawasili kama siku zote na kupewa funguo za gari akaliwasha huku pembeni akiwa amekaa Yusrath,kila kitu kwao kilienda kama kawaida,kitendo cha kulipita gari aina ya Landcruiser,hapohapo magari hayo yakawashwa kwa safari ya kuwafuatilia nyuma,baada ya kufika Riverside wakampakia Ahmed.
Ndani ya gari hilo kulikuwa na wanaume sita, walioshiba na miili imejazia kama wacheza mieleka,hawakua wanaume wa mchezomchezo na walikuwa siriazi, hawacheki.Mbele,nyuma ya Usukani alikaa Emmanuel Raymond Kikwabi,rafiki yake na Ahmed wa miaka mingi sana.Na ndiye huyo aliyeratibu mchakato mzima na kuwatafuta wanaume maalum kwa ajili ya kazi hiyo.
“Kama tulivyoongea kwanza pole Kiongozi”
Emmanuel Kikwabi,akatoa pole huku macho yake yakiwa mbele anatizama Verosa ya Ahmed ambayo ilikuwa inaendeshwa na Sameer.
“Siwezi kupoa,mpaka nimkamate mwizi wangu.Ushawaambia vijana cha kufanya?”
“Wanajua tayari,ndio maana nipo nao.Kwenye Nissan kule kuna wengine sita.Huo Mku** wake leo,utawaka moto sijui kama ataweza kukaa mwaka huu wote”
Emmanuel Kikwabi,alizungumza kwa uchungu.Unyama waliopanga kumfanyia Sameer ulitisha mno,ilikuwa ni lazima wamuingilie kimwili wamfanyizie kwenye haja kubwa huku wakimchukuwa video,huo ndio mpango uliopangwa.
Muda wote Ahmed alikuwa mwenye hasira,hususani gari lake lilivyokuwa linaingizwa kwenye mashimo.
“Aendeshe gari langu,anigongee mke wangu.Bullshit hizi ni dharau,Emma nipe bastola yako”
Ahmed akaona anashindwa kuvumilia,akataka Bwana Emma amkabidhi silaha yake.
“Ahmed,ukikurupuka.Unamkosa,hili swala niachie mimi.Kuwa mpole,ukikosea stepu hata moja!Una haribu ushahidi,huyu anatakiwa akamatwe,kiintelijensia.Yeye si muhuni, inabidi akamatwe kihuni”
Hapo Ahmed akapoa kidogo.

****
Ilikuwa ni lazima kwanza wapite Sinza,hoteli waliyozoea kukutana na kufanya ngono ndipo wazunguke mji,hawakujua kwamba nyuma yao wanafuatiliwa, sio kwamba Sameer hakuliona gari aina ya Landcruiser bali alijua ni magari tu ambayo yapo barabarani, akaliipuzia.Walivyofika Sinza,wakapaki gari na kuingia hotelini,huko wakala raha zote za dunia.Yusrath alibiduliwa biduliwa huku na kule,kila kitu kikawa burudani kwake,hakukaa sana simu yake ikaita na mpigaji alikuwa ni mumewe.
“Nimefika Mke wangu,upo wapi?”
Ahmed alizungumza na kuuliza simuni baada ya simu kupokelewa,hiyo ilimfanya Yusrath amtizame Sameer.
“Nipo nyumbani baby wangu,pole na safari”
“Ahsante nishapoa,ndio natafuta taxi niende Mwika”
Ahmed hakuwa Mkoani Kilimanjaro kama walivyoongea bali alikuwa nje ya hoteli hiyo ndani ya Landcruiser,hasira zimemshika kohoni baada ya mkewe kumuongopea yupo nyumbani, akatamani kushuka akaue mtu lakini alizuiwa asifanye hivyo,moyo ulimuuma sababu alijua ni kitu gani anafanya Yusrath ndani ya hoteli hiyo.
Dakika thelathini baadaye akamuona anatoka na mwanamme,tena kijana mdogo!Akamtizama kwa hasira,chozi la uchungu likamtoka.
Sameer na Yusrath walipanga siku hiyo wazunguke sehemu mbalimbali lakini kabla ya yote, walitaka waende Quality Center,wakashangae shangae kidogo.Ni kweli,waliwasha gari na kuelekea huko!Walivyofika wakaingia ndani na kupewa kadi,kisha kupeleka gari moja kwa moja kwenye maegesho.
“Baby,tumefika.Twende tukatembee”
Sameer alisema lakini kabla ya kumalizia sentensi yake,kioo chake cha mlango kikagongwa.Akashusha kioo na kumuona mwanamme mmoja mrefu kiasi mweusi.
“Mambo vipi Chif?”
Jamaa huyo,akasalimia.
“Fresh”
“Umeangalia tairi lako la nyuma,halina upepo”
Sameer,akashtuka kidogo akafungua mlango lakini badala yake,akakutana na mdomo wa bastola kwa chini usawa wa tumbo lake,jamaa huyo akawa ameshika bastola hiyo.
“Rudi ndani ya gari,usipige kelele.Sitaki kukuua lakini ukienda kinyume,nakuuwa.Ingia ndani ya gari”
Ni kitendo ambacho haikuwa rahisi kwa mtu yoyote yule kuelewa,hata Yusrath alishindwa kuona lakini baadaye akawekewa bastola Kichwani.
“Nawewe Kahaba,pita nyuma”
Baada ya zoezi hilo,akatokea jamaa mwingine,akafungua mlango akakaa na Yusrath nyuma.
“Msiniue tafadhali”
Sameer alisema kwa uwoga.
“Washa gari,tutoke humu ndani”
Gari likawashwa wakaanza kutoka nje,ambapo hapo Sameer alitoa kadi wakatoka nje ya eneo hilo.
Jamaa aliyekuwa pembeni yake mwenye bastola,akatoa simu na kubonyeza namba fulani kisha kuweka simu sikioni.
“NIPO NAO HAPA,ndio wote wawili….sawa nawaleta”
Hapohapo simu ikakatwa,hiyo iliwafanya Sameer na Yusrath wazidi kutetemeka kwa uwoga wakishindwa kuelewa waliowateka ni majambazi ama wametumwa.


Ndani ya gari kila mmoja alisali sala yake ya mwisho,akijua huko wanapoenda hakukuwa na usalama wa aina yoyote ile kwani wanaume waliokuwa mbele yao hawakuonesha aina yoyote ile ya mzaha,sura zao muda wote zilikuwa na makunyanzi kumaanisha walikuwa ni watu wa kazi,miili yao ilikuwa mikubwa mno.Mmoja aliyeshika usukani alikuwa mwenye misuli mpaka shingoni, mrefu mwenye mwili kama wa mcheza filamu wa kimarekani, Rambo!Aliyekaa nyuma ya kiti huyu ndiyo usiseme mikono yake ilikuwa imejazia mfano wa viazi mbatata,akafanana na mcheza mieleka, John Cena.Hilo tu liliwafanya waone hakukuwa na dalili nzuri mbeleni,akili ya Yusrath ikamtuma moja kwa moja ni lazima watu hao ni majambazi na wanataka pesa.
“Nitawapa ela mnayotaka,mnataka bei gani?”
Akaongea kwa uwoga huku akitetemeka akijaribu kunusuru maisha yake kwani uhai kwake ndio ulikuwa kila kitu kwa wakati huo.
“Mme wangu,ana ela nyingi.Mpigieni simu,atawapa pesa”
Aliendelea kujiongelesha mwenyewe mpaka mwanamme aliyekuwa mbele, nyuma ya usukani kugeuza shingo yake.
“Kaa kimya”
Zilikuwa ni sentensi mbili tu,lakini ni nzito na alizungumza kwa kutisha.Muda huo Sameer alikuwa akitetemeka nguo yake ya ndani ilikuwa imelowa,hakuelewa ulikuwa ni mkojo ama jasho kwani kwa wakati huo alihisi mkojo unataka kumpenya,alivyoangalia nje akagundua wapo Kyembe Mbuzi na kuanzia hapo kilichotokea wote walivalishwa vitambaa usoni ili wasijue ni wapi wanaelekea!

*****
Ahmed alitetemeka kwa hasira,midomo yake ilikuwa ikimcheza muda wote, ana uchungu wa kumegewa mke,hata siku moja hakuwahi kufikiria kama Yusrath angeweza kumsaliti tena mchana kweupe,hakuelewa ni shetani gani, alimuingia mpaka akabadilika namna hiyo,wakati mwingine alidhani wenda hafanyi naye mapenzi vyema kwani kama kuhusu majukumu anatimiza yote.Akiwa ndani ya gari alitaka apewe bastola.
“No,Ahmed.Punguza hasira,kumegewa najua inauma.Ili mradi umempata mwizi wako,lakini trust me huyo Mseng*** nakuapia kila akiona mke wa mtu atakaa mbali”
“Bado haitoshi,inaniuma Emma”
“Naelewa,ni jinsi gani una feel”
“Naomba bastola yako”
“Nitakupa usijali”
Ahmed alikuwa kiti cha mbele,kulia kwake nyuma ya usukani alikaa mwanamme huyo Emmanuel Raymond Kikwabi,nyuma wanafuatiliwa na magari mengine mawili, moja likiwa la Ahmed wakipanga kuelekea Chanika,nje kidogo ya mji. Huko ndipo walipanga kumfanyia unyama Sameer kisha wamtelekeze misituni,licha ya mwanamme huyu Emmanuel kuwa mzuri wa sura lakini alikuwa ana roho nyingine mbaya upande wa pili,ndiyo maana alimshauri Ahmed afanye unyama huo wa aina yake.
Magari yalizidi kusonga mbele,wakatokea Tabata Barakuda hapo walikunja kushoto na kupanda barabara ya kuelekea Segerea, ambapo huko waliingia majumba Sita.Wakakamata barabara ya kuingia Gongo la Mboto!Walifanya hivyo kuzunguka zunguka ili Yusrath na Sameer wasijue ni wapi wanapelekwa,walizidi kusonga mbele na mwisho wakasimama kituo kinachoitwa Buyuni huko Chanika,wakakunja kushoto na kuchukuwa babarabara ya vumbi.
Nyuma yao zikafuata Nissan Patrol na Verosa ya Ahmed,namna waliyoongozana ungesema kuna harusi fulani lakini haikuwa hivyo,mbeleni kulikuwa na tukio baya linaenda kutokea,wakaachana na barabara kubwa wakaingia kushoto ambapo kandokando kulikuwa na majumba yanaendelea kujengwa,mbele kidogo gari, likasimama nje ya geti kubwa.
“Piii piiiiii”
Honi ikapigwa,haikuchukuwa hata dakika mbili geti likafunguliwa, gari zote zikaingia.Geti likafungwa,Ahmed alishangazwa na wanaume wengine aliowakuta humo, wote walikuwa na miili mikubwa utadhani vyakula vyao vilikuwa kokoto, wakashuka na kusubiri magari mengine yapaki vizuri.
“Shukeni”
Sameer alishikwa kwa nguvu kwapani,akatolewa ndani ya gari huku Yusrath yeye akiwa ameshikwa shingoni kwa nyuma.
Ahmed alivyomuona mkewe,akadondosha chozi la uchungu,huruma ikamuingia jinsi mkewe alivyoshikwa kama mtuhumiwa,akamsogelea karibu kabisa na kumtizama bila kusema chochote,hata hivyo Yusrath hakujua mbele yake kuna nani sababu machoni alikuwa ana kitambaa lakini alianza kuhisi sababu alisikia marashi, anayopaka mumewe,lakini hakutaka kulipa wazo lake kipaumbele kwamba Ahmed ndiye mkandarasi wa kila kitu kutokea,alichokiwaza yeye ni lazima hao walikuwa ni majambazi,wakati mwingine alienda mbali zaidi na kudhani wenda Sameer ndiye, amesuka mpango huo ili avune pesa.Wakakokotwa mpaka Seblen ambapo huko walipitishwa mpaka ndani ya chumba kidogo,wakasukumizwa na mlango ukafungwa kwa nje.
“Tayari”
“Kazi nzuri,kawaandae vijana waanze kazi.Kamera ipo tayari?”
“Ipo kwenye chaji,nadhani itakuwa tayari imejaa”
“Kaiangalie”
Mazungumzo hayo yalimfikia Ahmed akiwa pembeni,akawasogelea karibu.
“Emma,namimi naruhusiwa kuona?”
“Unaruhusiwa ndio,Mkeo inabidi ajue.Wewe ndio umefanya hivi”
“Naweza nikamuona sasa hivi?”
“Subiri kwanza,waandae mazingira”
Ndani ya chumba hiko,kulikuwa na kitanda kikubwa.Pembeni kuna meza ya mbao kushoto kuna kiti kilichotengwa upande wa kushoto kwenye kona.Humo ndipo Sameer na Yusrath, waliwekwa kwa ajili ya zoezi maalum,wakiwa wanatetemeka mikono yao imefungwa kwa nyuma vitambaa vipo usoni,wakasikia parakacha za watu wanakuja,wakasikia mlango unafunguliwa.
Vitambaa vyao vikatolewa usoni,Yusrath alikuwa wa kwanza kupigwa na butwaa baada ya kumuona Mumewe Kipenzi mbele yake,pembeni amesimama mwanamme mwingine mrefu kiasi.
Alivyotaka kuongea akashikwa na kwikwi na kuanza kulia hapohapo,Sameer akaogopa zaidi licha na hayo sura ya Ahmed haikuwa ngeni kwake.
“M..me wang..u naomba unisamehee”
Hayo ndiyo maneno yaliyotoka kinywani mwa Yusrath,akiamini msamahaa ndiyo ngao, pekee na ndiyo kitu anachostahili kwa wakati huo.Ahmed hakujibu chochote,akabaki anamtizama kwa hasira kama Simba aliyejeruhiwa na mkuki,akamuangalia Sameer aliyekuwa pembeni,macho yake akayarudisha tena kwa Yusrath.
“Kwanini nikusamehe?”
Ahmed akauliza huku akijizuia na kubana meno yake kwa hasira.
“Nisamehe..e kwa niliyokufany..ia mme wangu,sito..riudia tena ni Shetani tu”
Hapo Ahmed,akashindwa kujizuia akaangalia pembeni na kuanza kulia machozi,kila kitu kilichotokea kwake kilikuwa kama ndoto,leo hii mkewe amemsaliti, maumivu aliyokuwa anahisi moyoni mwake hayakuwa na mfano wa kuyafananisha na kitu chochote kile.
“Ahmed,njoo nje”
Emma Kikwabi,alivyoona rafiki yake analia.Akamtoa nje,ilielekea kuna jambo fulani alitaka kumshauri.
“Sikia,usilie.Wewe ni mwanamme,usioneshe udhaifu mbele yao,hii kazi tumeanza inabidi tuimalize…”
Emma,alivyomaliza kuongea hivyo, akatoa bastola kiunoni kwake.
“KACHA KACHA”
Akaikoki na kumkabidhi Ahmed.
“Kill them”(Wauwe),Akasema kwa umakini.
Ahmed,alitetemeka kusikia hivyo lakini kwa wakati mmoja alipata ujasiri,akafuta machozi na kukamata bastola vizuri.Hakuwahi kutumia silaha kabla lakini siku hiyo alipewa na alichotakiwa kukifanya ni kumuuwa mkewe pamoja na Sameer, jambo hilo lilikuwa liko mbioni kutokea sababu hasira ndizo zilimuongoza,wakaongozana na Emma Kikwabi mpaka chumbani ambapo huko kitendo cha kuingia tu,kilimfanya Yusrath atetemeke.Mapigo yake ya moyo yakazidi kwenda kasi akajua tayari mwisho wake wa kuishi unakaribia tena anaenda kuuliwa na mumewe kwa risasi.
“Nianze na nani?”
Hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa Ahmed akiwa na bastola mkononi,siku hiyo ilikuwa ni kama sinema ya kihindi.Yusrath akazidi kumwaga machozi,katika hali ya kushangaza Sameer akawa amemwaga mkojo,kwenye suruali yake.Mkojo ukapenya mpaka chini ukalowanisha malumalu.
“Mbona unajikojolea,mtu mzima?”
Emmanuel kikwambi,akauliza baada ya kuona tukio hilo.
“Nisa..mehe kaka.Nao..mba msiniue,mimi nimekosea ndio”
“Kwanini unatembea na mke wa mtu?Hukujua?”
“Nili..jiua kaka,nisamehee sitorudi tena.Nikitoka hapa,nitaokoka.Nitamrudia Mungu”
“It’s too late,umechelewa.Lakini,ulionywa,tatizo nyie mkiambiwa mnasema geto mna maziwa,tumia maziwa leo”
Emmanuel Kikwabi alizungumza na wakati huo Sameer alikuwa akijibu kwa hofu, iliyofanya apate kigugumizi cha ghafla,kila kitu kwake siku hiyo kilibadilika.Akaapia baada ya kutoka hapo,ataokoka ama atakuwa Shekh lakini hilo halikumfanya Ahmed,abadili mawazo.
“Nimeuliza,nianze na nani?”
Ahmed akauliza tena safari hii,akiwa amemuelekezea bastola Mkewe Yusrath, usawa wa kichwani kumaanisha kwamba kitendo cha kuvuta triga,Yusrath angefumuliwa na risasi na hapohapo angedondoka chini na kufariki dunia, sababu bastola hiyo ilikuwa tayari imekokiwa.
“Noo,naanza nawewe.Uliambiwa,hukusikia”
Ahmed akahamisha bastola na kumsogelea Sameer karibu kabisa,mlango wa bastola ukagusa kichwa chake,hasira na uwoga vikazidi kutawala kwa Ahmed huku kidole chake kikiwa taratibu kinasogea kwenye kifyatulio,kimoyomoyo alianza kuhesabu ilivyofika tatu, akavuta triga akafumba macho yake ili auwe.
“Karakacha! Karakacha!”
Ulikuwa ni mlio wa bastola kumaanisha hakukuwa na risasi ndani yake,hiyo ilimfanya Emmauel Raymond,apigwe na mshangao na kumuangalia Ahmed,hakutarajia kama ni kweli kama asingetoa risasi ndani ya bastola siku hiyo angeua,akamsogelea karibu na kuchukuwa bastola yake.
“Haina risasi,njoo”
Sameer kwa wakati huo,aliloa jasho kama mtu aliyetoka kumwagiwa maji,anahema jujuu akiwa anasubiri mwisho wake,kichwa chake kilikuwa kinatafakari, kifo kinafanana vipi.Baada ya kusikia bastola haina risasi,akaishiwa nguvu.
Mambo hayakuishia hapo,Ahmed na Emma wakatoka nje!
“Kwanini ulitoa risasi?”
“Ni kesi,Ahmed”
“Ungeniacha,nipate kesi.Ni mimi sio wewe”
“Namimi ningeshtakiwa,Ahmed una hasira sana,punguza”
“Nataka nikawauwe”
“Hapana,lazima tufanye tulichokipanga”
Baada ya hapo,wanaume walioshiba tisa wakaitwa wenye miili ya miraba minne.
Walikuwa tayari kwa kufanya kazi hiyo,mmoja kati yao alishika boxi kubwa la Condom na mwingine kikopo cha mafuta,wote wakaingia chumba alichokuwa Sameer,kamera ikawekwa kwenye kiti na kutegwa vizuri ambayo ilitegwa usawa wa uso wa Sameer, uonekane vizuri.Kwa mara ya kwanza hakuelewa nini maana yake lakini alivyoona wanaume hao wanajishika sehemu za siri huku wakiamuangalia kwa macho fulani ya mahaba,akaanza kupata picha na kujua kinachotaka kutokea kwani dalili ya mvua ni mawingu,akazidi kuomba anachofikiria kiwe tofauti,lakini haikuwa hivyo sababu aliona mafuta yanawekwa mezani na Kondomu zinatolewa kwenye maboxi,Ahmed na Emmanuel Kikwabi wakaingia pia, mlango ukafungwa.
“Mchumba,una vitu viwili vya kuchagua.Tutumie nguvu,ama ukubali kwa hiyari yako.Yote yanawezekana,tukitumia nguvu tukakuumiza alafu tutakula mavi hayo vilevile”
Mmoja wa wanaume hao alizungumza huku akimuangalia Sameer,wakati huo Yusrath aliwekwa pembeni nayeye atizame. Ahmed na Emma walikaa kama watu wanaosubiri sinema ianze!
“Chagua kimoja”
Sameer hakujibu,kilichofuata hapo ni mwanamme huyo kumsogelea karibu na kumfungua kamba,akamshika vizuri na kuanza kumvua suruali lakini hapo Sameer akaonesha ubishi kidogo.
“Ooooh,kwahiyo tutumie nguvu?Tompooo,njoo”
Hakukuwa tena na maongezi mengine zaidi,Sameer asingeweza kushindana nguvu na wanaume hao,wakamshika mikono mmoja akaanza kumvua shati mwingine suruali,wakamtoa boxa yake akabaki kama alivyozaliwa,wakamgeuza na kumlaza Kifudifudi kitandani,miguu yake ikatanuliwa wakachukuwa mafuta na kumpaka kwenye makalio yake.Mmoja wa mabaunsa hao,akashusha suruali yake,uume wake mkubwa ukawa umesimama imara,akauvalisha Condom.
“Mwekeni vizuri nione tundu,tegesha kamera vizuri”
Sameer alizidi kukukuruka lakini ilishindikana kalio lake likapanuliwa huku na kule,jamaa akaingia katikati ya Sameer na kupitisha mashine,maumivu aliyosikia Sameer, hayakuwa na kipimo chake,akapiga kelele lakini hiyo haikusaidia alivyomaliza wa kwanza akaingia wa pili,huyo hakutoshekwa akarudia mzunguko mwingine.Kila kitu kilishuhudiwa na Ahmed,aliyekuwa pembeni amekunja mdomo wake kwa hasira,alivyofika mwanamme wa tano Sameer akaanza kutoa damu kwenye makalio,hilo hawakujali wakazidi kufanya kazi,mashuka yakazidi kuchafuka damu.Wakati huo Yusrath alikuwa akilia machozi,lakini hilo halikusaidia!Wanaume wakaendelea na kazi yao,Sauti ya Sameer ikawa imemkauka kabisa,amelegea na kuishiwa nguvu.Hilo halikufanya wamuache,wakaendelea kumuemea kisogoni, tena kwa zamu,mpaka alivyopoteza fahamu zake!



Ulikuwa ni kama msiba mkubwa sana kwake,machozi yalimtiririka mashavuni yakalowanisha mashavu yake na kupita shingoni,akawa analia kwa kwikwi.Kila kitu katika ndoa yake kikawa kimevurugika,akatamani siku zirudi nyuma abadilishe kila kilichotokea.Kifupi alijiona ni mpumbavu na kugundua kwamba mwanamke mjinga huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe.Ndiyo maana alibaki akilia kwa uchungu,akiwa amekaa kwenye kona ya ukuta,baada ya Sameer kufanyiwa unyama huo wa kuingiliwa kimwili mbele yake akishuhudia mpaka kuzirai,hakuelewa nini hatma yake.Wanaume waliokuwa mbele yake,aliwaona wanamchukua Sameer na kumteremsha kutoka kitandani,kitanda kizima kililowa damu.Ahmed alikuwa pembeni,anatizama mchezo mzima moyo unamuuma ajabu wakati mwingine akaona kama adhabu hiyo haikutosha kwa Sameer.
Baada ya tukio hilo kuisha,akamtizama mkewe Yusrath kwa macho makali,akasimama na kumsogelea karibu kabisa,akachuchumaa na kumshika kidevuni wakawa wanatizamana.
“Ulikosa nini kwangu?”
Hilo ndilo swali la kwanza kuliuliza Ahmed.
“Nakuuliza,ulikosa nini kwangu?”
“Na..omba nisam..ehe Mme wangu,sikukosa kitu”
“Kumbe nini?Tamaa au?Kwanini ulitaka kunigombanisha na Benjamin Ngowi?”
Swali hilo lilimfanya Yusrath akae kimya,hakuweza kujibu chochote kuanzia hapo, badala yake alikuwa akilia kwa kwikwi tu,bila kuacha.Ahmed akaachana naye,wakatoka nje na Emmanuel Kikwabi ili ampe utaratibu mwingine.
“Cd,moja nitakupa ukae nayo.Nyingine tutabaki nayo kwenye laptop,huyu sijui amekufa.Atajijua mwenyewe,tutaenda kumtupa porini huko”
“Ahsante Emma,nitakutumia pesa uwape vijana”
“Haina shida na mkeo?”
“Nitaondoka naye”
“Kuwa makini,nina amini amejifunza.Hatorudia tena”
“Hata mimi nina amini hivyo”
Alichokifanya Ahmed ni kurudi ndani ya chumba cha mara ya kwanza,akamkuta Yusrath na kumwambia kwamba wanatakiwa kurudi nyumbani,hiyo ikamfanya Yusrath agome na kukataa katukatu,alishaelewa kitendo cha kufika nyumbani angeweza kupigwa mpaka akauliwa, ndiyo maana akatingisha kichwa ishara ya kugoma.
“Nimekusamehee mke wangu”
“Si..wezi kurudi Ahmed,please niache”
“Siwezi kukuacha,mimi ni mumeo.Twende nyumbani”
Ilichukuwa dakika kumi na tano nzima,kumuimbisha Yusrath akubali kuondoka,ndipo akakubali wakatoka nje na kuingia ndani ya gari.Ambapo humo,hakukuwa hata na mmoja kati yao aliyemuongelesha mwenzake,safari nzima walinuniana, kila mtu akiwa anatafakari kilichotokea, kifupi ndoa yao tayari iliingia doa ambalo lisingeweza kufutika kirahisi.
Saa 11;45 jioni, wakawa wamefika nyumbani tayari,kila mtu akashuka,hata walivyofika hakukuwa na mazungumzo ya aina yoyote ile, isipokuwa Ahmed kujitupa kitandani.Yusrath,akaingia moja kwa moja bafuni,huko alilia sana akihisi kujuta kwa kila kitu kilichotokea katika ndoa yake na maisha yake kwa ujumla!Alivyomaliza kwikwi, akawasha bomba la mvua, maji yakawa yanam-mwagikia,akatoka bafuni na kuingia chumbani,hapo alivaa na kutoka kisha kwenda kuketi seblen.

*****
Kiasi alichokuwa anadaiwa na benki kilikuwa ni kikubwa sana,hiyo ilimfanya achanganyikiwe sababu aliweka nyumba yake kama bondi, endapo mkopo usingerudishwa kwa wakati ichukuliwe ili kufidia deni.Wakati wa marejesho ukawa umefika,akajitahidi kupeleka asilimia kumi ya malipo,nyingine tisini akashindwa kulipa.Hiyo ilimaanisha Benki ifike kwa mwenyekiti wa Serikali za mitaa apewe barua kisha baada ya siku chache nyumba yake ipigwe mnada,sio siri Mzee Mpilla alionesha kuchanganyikiwa kwa kiasi cha kutosha,hata hivyo kwa upande mwingine hakujilaumu sana sababu pesa alizokopa benki zilikuwa ni kwa ajili ya kumkomboa na kumtafuta mtoto wake Hajrath,hilo lilifanikiwa na kilichobaki ni kurudisha pesa alizokopeshwa na benki,jambo hilo likaonekana kuwa kama mtihani mkubwa sana katika maisha yake,pesa hizo zilikuwa nyingi kulipa.Mbali na hapo hakuwa ana uhakika kama angeweza kuzilipa, ndiyo maana akakata tamaa kabisa,alivyomwambia mkewe akahisi kuchanganyikiwa, nyumba ikakosa amani, hiyo ikamfanya Hajrath aingilie kati na kuuliza.
“Baba yako anaumwa,ndiyo maana hata mimi sina raha kabisa”
Mama,akadanganya hakuwa mwenye sababu ya kumshirikisha binti yake juu ya swala kama hilo zito,akiamini ni lazima lingemuumiza mtima.
“Anaumwa nini?Si angeenda hospitalini sasa?”
Hajrath akazidi kudadisi.
“Keshaenda.Atapona lakini”
Maswali yalikuwa mengi siku hiyo, kutoka kwa Hajrath Mpilla akitaka kujua,kinachoendelea.Hata hivyo kuna kitu kisichokuwa cha kawaida alianza kuhisi,ni wanaume waliokuwa wanafika nyumbani kwao mara kwa mara.Siku moja,wazazi wake hawakuwepo, akafika mjumbe mmoja aliyetumwa kutoka Benki ili apeleke barua kwao,bahati mbaya ama nzuri wakamkuta Hajrath,hapo ndipo alipoanza kudadisi baada ya kufungua barua hiyo,moyo wake ulichoma kama pasi.Aliumia sana na kujiuliza ni kwanini wazazi wake wanamficha jambo hilo zito.Siku hiyo alilia machozi,wazazi wake walivyofika akawaeleza kila kitu kilichotokea akawatupia lawama,walivyojaribu kumtuliza wakawa wamechelewa.
“Ni kweli baba yako,alichukuwa mkopo Hajrath”
Mama,akafunguka!
“Kwanini,hamkuniambia?”
“Tusingeweza”
“Mnadhani,siwezi kuwasaidia?”
Hapo Mama,akakaa kimya hakuwa na lingine la kuongeza zaidi.Kitu cha kwanza kumjia kichwani Hajrath ni mwanamme anayeitwa Dokta Sajjo,huyo alikuwa ni mpenzi wake ingawa hawakuwa na maelewano mazuri licha ya hayo,hakuwa ana hisia naye kabisa.Siku hiyo ilibidi amtafute na kumueleza shida yake,akamtajia kiasi cha pesa kinachotakiwa kulipwa vinginevyo nyumba yao itapigwa mnada.
“Kwahiyo,umenitafuta leo sababu una shida?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Dokta Sajjo,simuni.Alikuwa ana kila sababu ya kuuliza hivyo kwani Hajarth,alibadilika kwa kiasi cha kutosha,wakawa hawawasiliani tena kama siku zote,mpaka anarudi nchini Afrika Kusini hawakuwa na maelewano mazuri.
“Sina maana hiyo”
“Bali?”
“Nina matatizo”
“Nikwambie kitu Hajrath”
“Nakusikiliza”
Namna Dokta Sajjo alivyouliza,kulikuwa kuna kila dalili za shali mbeleni, ndiyo maana Hajrath nayeye akajibu kwa kibuli chote.
“Ahsante kwa kila kitu lakini,naomba nikwambie kitu kimoja.Mimi nawewe kuanzia leo tuwe marafiki tu wa kawaida,kila mtu afanye mambo yake…”
Dokta Sajjo,akaongea kutoka moyoni.Akamuelezea Hajrath jinsi alivyokuwa anaumia na asingeweza kuendelea kuumia tena, bora waachane ibaki historia bila kuelewa kwamba hiyo kwa Hajrath ilikuwa ni sawa na kumpiga chura teke,hakuwa ana muda wa kubembeleza, wakaachana siku hiyohiyo.
Kwa Hajrath,haikumuumiza sana sababu ndicho kitu alichokuwa anakitafuta kwa siku nyingi sana!
Siku hiyo,aliumiza kichwa chake kupata shilingi milioni kumi na moja,ni wapi angezipata?Hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza kujiuliza,akaanza kuwafikiria marafiki zake na kuchambua waliokuwa na uwezo wa kumsaidia,sura ya Mr .Filbert Kimaro,ikamjia kichwani.Mkurugenzi mtendaji katika kiwanda cha Tanzania Breweries Limited(TBL),hapohapo bila kuchelewa.Akamtafuta kwenye simu na kupanga wakutane siku inayofuata,asubuhi kulivyokucha bila kunywa chai.Akatafuta daladala lililompeleka katika kiwanda hicho cha Bia.
“Namuulizia Mr.Filbert Kimaro”
“Andika jina lako hapo,saini pia”
Hajrath akafanya hivyo,hilo halikumshangaza sababu zilikuwa ni taratibu za ofisi zote, kuingia na kusaini,baada ya hapo akaruhusiwa kuingia ndani ambapo huko alisubiri juu ya sofa mpaka alivyoitwa.
Kitendo cha kuingia ofisini,alikumbana na ubaridi mkali,kiyoyozi kilikuwa kikali mno!
“Karibu Hajrath,za masiku?Ndo umenenepa namna hiyo?”
“Ah wapi,mbona hapa nimepungua sana Filbert”
“Basi ulikuwa kibonge kumbe,anyway!Niambie,kuna nini tena?”
“Nina shida,unikopeshe pesa”
“Pesa?”
“Ndio”
“Bei gani?”
“Milioni tisa hivi”
“Milioni tisa?”
“Yes,milioni tisa Filbert.Nitakurudishia”
Kusema ukweli,hakuwa ana uhakika kama ataweza kulipa pesa hizo,alichofikiria kwa wakati huo ni kuikomboa nyumba yao, ambayo ilitakiwa kupigwa mnada, wiki moja baadaye.
“Ya nini?Mbona pesa nyingi namna hiyo?”
“Mama angu,anaumwa.Alafu pia,kuna mambo yangu fulani hayaendi sawa!Tafadhali nisaidie,nitakulipa”
“Nikikutafutia Milioni tano, vipi?Itakusaidia?”
“Itanisogeza kidogo”
“Basi,tuonane kesho”
“Ahsante sana Filbert,Mungu akubariki”
Hakukuwa na maongezi mengine zaidi ya Hajrath kusimama na kuondoka huku nyuma akimuacha Filbert Kimaro,anamsindikiza kwa macho.Akiyaangalia makalio ya mwanamke huyo, yanavyotingishika kwa nyuma,ghafla pepo la ngono, likamuingia akaanza kum-mezea mate!
“Mbuzi,kafia kwa mpika supu”
Akasema maneno hayo huku kichwani kwake,akiandaa mikakati ya kumvua Hajrath nguo yake ya ndani.
****
Hilo halikuwa utani,kesho yake akatafuta hoteli nzuri akampigia Hajrath simu ili wakutane eneo hilo,tena mbaya zaidi akamwambia amechukuwa chumba tayari.
“Filbert”
“Yes,Hajrath”
“Hivi,unanichukuliaje?”
“Ah,kama rafiki yangu”
“Naomba unisikilize,kama huwezi kunisaidia niambie!Mimi sio mtoto mdogo,kwani hakuna sehemu nyingine mpaka hotelini?Tena unaniambia upo room!Listen to yourself”
“No Hajrath,sio kama unavyofikiria”
“Kumbe?”
“Ni ni nilitaka tu,tuongee tukiwa faragha”
“Basi,sina shida na pesa zako!Ahsante”
Hapohapo,Hajrath akakata simu!Kwake mwili wake ulikuwa na thamani kuliko pesa,ni kweli alikuwa ana shida lakini hakuwa tayari kuvua nguo yake ya ndani na kupanua miguu yake kisa shilingi milioni tano,ambazo hakuwa ana uhakika kama angepata ama angenyimwa!Aliendelea kuhangaika usiku na mchana bila kukoma,wanaume wengi aliowatangazia shida walimtaka kingono!Akajichukia,kwanini aliumbwa mwanamke?Akawalaani wanaume wote kiujumla.
Siku moja,akiwa amekata tamaa akamkumbuka mwanamme mmoja,anayeitwa AHMED KAJEME,akapanga kumsaka popote alipo,hata nyumbani kwake apajue au amuibukie ofisini kwake ili aombe msaada huo!

*****
‘SHEM,ILE PESA VIPI?NAONA KIMYA,NINA SHIDA SANA,NIMEBANWA.KAMA UNAWEZA KUNISAIDIA,NITASHUKURU SANA.MIMI RHODA’
Meseji hiyo ilisomeka juu ya kioo cha simu ya Ahmed,hakuwa ana uhakika kama aliiona vizuri sababu aliona nyota nyota na kizunguzungu kikali sana,akaweka sigara yake mdomoni akavuta na kutoa moshi mdomoni.Juu ya meza yake kulikuwa na mzinga mkubwa wa Chupa ya pombe kali, aina ya Konyagi pembeni kuna glasi iliyojaa bia!Akiwa katika ‘bar’ maarufu Viva Park,Tabata Bima.Kichwani alikuwa mwenye ‘stress’ nyingi sana ndio maana akatumia mpaka sigara,usiku huo wa saa mbili.Kila alivyofikiria kuhusu mkewe Yusrath,akahisi kama bado ana maumivu makali sana moyoni.
Akapiga fundo moja lililokuwa kwenye glasi,akamaliza bia yote!Akashika simu yake na kuanza kuangalia meseji hiyo,akaisoma kwa mara nyingine tena,safari hiyo alikuwa anasoma kwa sauti kana kwamba anamsomea mtu pembeni,ghafla akabonyeza bonyeza na kuweka simu sikioni, kumaanisha kwamba alitaka kuzungumza na Rhoda sio kujibu meseji hiyo.
“Mambo,shemeeeji”
“Poa Shemela,pole kwa kazi”
Rhoda,akasema kwa unyenyekevu.
“Ahsantee,nipo kwenyee kelelee ngoja nitoke pembenii kidogo tuongee”
Ahmed akasimama,akatembea mpaka nje barabarani ili waelewane vizuri na Rhoda Deniss.
“Hapo,unanisikiiaaaa vizuriii?”
“Ndio Shemela..”
“Upo wapi sasa hivi?”
“Nipo Segerea huku,nataka kupanda daladala.Niende kulala”
“Kwanini usipitiee hapa,hapaaaaa….”
Ahmed akawa kama anavuta kumbukumbu la eneo alipo.
“Hapaa Viva Park,Tabata Bima”
“Upo Bima?”
“Ndioooo”
“Sawa,nitapita hapo Shemela”
“Poa,nakusubiri”
Ahmed alirudi kwenye meza yake huku akipepesuka,akavuta kiti na kukaa ambapo hapo aliagiza chupa nyingine ya bia.
“Weee muhudumuuu,psiiii psiiii.Ebuu njoo”
Ahmed akaita kwa ukali kidogo huku akiwa amekunja sura.
“Abee”
“Mbona bia ya moto?Mimiii si nimekwambiaa ya baridiiii,unanijua mimi weweee?Nimekwambia bia ya moto kitimoto wewe, un…”
“Kaka samahani nil…”
“Acha nimalizeee kuongeaa,hivi mnafanya vipi kazi?Niletee bia ya motoo aah ya baridi nimesema”
Mhudumu akampuuzia na kuchukua chupa ya bia ili abadilishe,kwake kushinda na walevi wa aina hiyo, ilikuwa kawaida,akabadilisha bia na kuendelea kuhudumia.
Dakika kumi baadaye,Ahmed akapokea simu kutoka kwa Rhoda Denis kwamba tayari amefika,akamuelekeza alipo kisha wakakutana.
“Kaaribu shemejii”
Ahmed,akamkaribisha.Wakapeana mikono, Rhoda akakaa pembeni!
“Nilijua upo na Yusrath”
“Hapana,yeye yupo nyumbani”
“Msalimie sana ukifika,mimi sikai sana”
“Pata hata moja basi”
“Nitakunywa moja tu”
Rhoda,akaagiziwa pombe.Chupa moja ilivyoisha,akapewa nyingine,ilivyoisha akaongezewa nyingine.Zikaanza kumpanda kichwani,ikawa kata mti panda mti!
“Shemeelaaaa,mimiiii naondokaa bwanaaa,nina usingizii”
“No,acha nikupelekeee unaishii wapi kwaniii?”
“Mabibooo,alafu mzigoo wangu.Hukunijibu,utanipaa liniii?Maana Shemelaa,nina madeni hapa,ni sheeeedaaaaa”
“Unaogopa kudaiwa,nchi yenyewe inadaiwaaa hiii.Sembuse weweee,embu tuongeze moja moja,kisha tuondoke”
Hapo wakaagiza tena,licha ya kwamba walikuwa wapo bwii, mtungi.Ilivyogonga saa 5;56 Usiku,viti vikaanza kutolewa kimoja baada ya kingine, kumaanisha kwamba ‘bar’ ilikuwa inakaribia kufungwa kama sheria za nchi zinavyotaka kwani diffenda za polisi, zilikuwa tayari zipo doria.
“Hii nchiii bwanaaa,matakoo ya Mbuziii.Tutafute pesa sisiiii,tupangiwe kuzitumiaaa na kulewaa.Inakeraa sana,nitaongea na Rais,kuhusuuu hili. Ujue walevii sisi tunaonewa sana wakati ndio tunaiiingizaaa patoo kubwaa sana serikaliniii”
Maneno hayo yalimtoka Ahmed,huku akicheua cheua.Wakaanza kukokotana na Rhoda wakatembea kwa kuyumba mpaka lilipo gari,gizani chini ya mti.
“Shemeelaaa huku”
Ahmed alitaka kuingia mlango wa nyuma,siku hiyo alikuwa tilalila.Wote wakaingia ndani ya gari.Lakini badala ya Ahmed kuwasha gari,akaegamia usukani.
“Vipi shemelaaaa,gari haina mafuta?”
“Weeeee,gari yanguu.Ina full tank mudaa wotee,pumbavuu”
Ahmed akasema akimtizama Rhoda Denis machoni,macho yake akayapitisha kifuani kwa mwanamke huyo,mwili ukaanza kumsisimka.Macho yake,alivyoyatupa mapajani mwa Rhoda,ndipo akashindwa kujizuia akajikuta anaweka mkono wake juu ya paja la Rhoda na kuanza kumpapasa.
“Mmmmh shemelaaaa,Tabia mbayaaa.Ebuu tuondokee please,niache bwanaaa”
“Aaaah,samahani.Nilijuaaa nashika gia,lakini una miguu lainiii kama umeumbwa kwa pambaaa”
“Kuliko Mkeooo?”
“Nooo,hujamfikia mke wanguuu.Mke wanguuu mzuri bwanaaaa,thubutuuu.Lakini ana…Tuachanee na hayo Shemeji,unakaa wapi umeniambia?”
“Mabibooo,Mwishooo”
“Okay,twende”
Ahmed,alikuwa anaongea hovyohovyo,akataka kuwasha gari akasita na kumuangalia tena Rhoda Denis,vitu fulani vikaanza kupita ndani ya mwili wake, damu yake ikaanza kuchemka.Akamshika Rhoda mapajani na kusogea kwake, akaanza kumnyonya shingo,bila kuelewa hapo ndipo udhaifu wa mwanamke huyo ulipo,akajikunja kidogo sababu alihisi kutekenywa Ahmed,hakuishia hapo.Akapitisha mkono wake,kifuani kwake,kupitia blauzi chini ya tumbo,akakumbana na blazia akaipachua na kuanza kutekenya chuchu.Kwa wakati mmoja akipeleka mdomo wake taratibu, mpaka kwa Rhoda,akatoa ulimi, Rhoda akafungua mdomo wake na kuachanisha meno,ulimi wa Ahmed ukapita ndani,wakaanza kulana denda.
“Mmmmmmh”
Rhoda,akaguna kwa rahaa baada ya vidole vya Ahmed, kupenya ndani ya sketi na kushika ikulu yake!


Mambo yaliyokuwa yanaendelea ndani ya gari,yalikuwa ya kikubwa yanayopaswa kufanywa na watu wazima.Msimamo wa Rhoda Denis,ulionekana kuyeyuka kama barafu na kila kitu kilichokuwa kinaendelea kuanzia hapo, kilimfanya ahisi rahaa za ajabu.Hiyo ikampelekea mpaka mwenyewe kwa hiyari yake aanze kuvua nguo zake,akanyanyuka juu kidogo na kuvuta sketi yake chini, ambapo Ahmed alimsaidia kutoa mpaka miguuni,ikawa juu.Akainua kidogo mgongo wake na kutoa blauzi,akabakiwa na chupi na sidiria peke yake!Damu yake ilimwenda kwa kasi kiasi kwamba akatamani mechi hiyo ianze mara moja,jambo ambalo Ahmed hakutaka kulifanya.Alichokifanya mwanamme huyo ni kumuandaa kwa kumshika shika kila sehemu ya mwili wake,hususani alivyojua udhaifu wa Rhoda upo shingoni,akawa anamnyonya shingo mara kwa mara!Japokuwa alikuwa amelewa lakini alikuwa makini katika mchezo huo mpaka mwenyewe akajishangaa,dakika tatu baadaye,akawa tayari ametoa suruali yake,akabinua kiti kikalala akaitanua miguu ya Rhoda huku na kule,akaweka mpira kati na mechi kuanza mara moja!Hakuna mechi iliyokuwa ndefu kama hiyo kwani walicheza dakika tisini zikaisha,lakini bado mpira uliendelea.Hiyo ni kutokana na Ahmed kutumia kinywaji aina ya Konyagi.
“Aaaah assshs aaaaah aaaah”
Hizo zilikuwa ni kelele za Rhoda,akimmkwaruza,Ahmed mgongoni hakutaka kuonekana gogo ndiyo maana akajitahidi kuzungusha kiuno chake,ili waende sawa!Sio siri,katika mechi alizowahi kucheza hiyo aliikubali mno sababu alienda mizunguko mingi sana kwa kipindi kifupi.Waliokuwa nje wanapita haikuwa rahisi kuona gari kwani lilikuwa kwenye giza chini ya mti,ingawa lilikuwa linanesa.Hakukuwa na mtu aliyemuongelesha mwenzake.Baada ya mtanange huo kuisha,kila mtu akavaa kimya kimya nguo zake,Ahmed akawasha gari na kuanza safari ya kuelekea Mabibo,Mwisho!Ambapo huko,aliambiwa kwamba Rhoda anaishi,alivyofika Kigogo,Mburahati akamgeukia!
“Mabibo,mwisho palepale au?”
“Ukiniacha pale kituo cha polisi,nitakuwa nimefika”
“Hakuna shaka”
Hawakuchukuwa dakika nyingi,wakawa wamefika Mabibo Mwisho,Ahmed akaweka gari pembeni na kutoa lock milango,Rhoda Denis bila kusema chochote akashuka na kumuacha Ahmed anamtizama,bila kuamiini kwamba wametoka kufanya tendo hilo la kuzini!
Kila mtu alionekana kabisa kumuonea aibu mwenzake!
“Wanawakeee bwanaaa,yaaaani….”
Ahmed akataka kumalizia sentensi yake lakini akakosa neno la kujazia,kitendo cha kufanya ngono na Rhoda Denis,kilimfanya ashangae.Mbaya zaidi hakuwahi kumtongoza hiyo ilimfanya awaweke wanawake katika kundi fulani la micharuko na mapepe,akawasha gari na kuanza safari ya kuondoka,mwendo wake haukuwa wa kawaiada kama siku zote.Siku hiyo alikanyaga pedeli za gari sana,hiyo ikafanya likimbie kasi.Alivyofika Riverside,akalala na kona mzimamzima,hakukuwa na watu usiku huo, ndio maana ilikuwa rahisi kupenya,akaingia barabara ya vumbi kwa mwendo uleule,haikuchukua muda akawa amekaribia kufika,yupo umbali wa mita kumi,akaanza kupiga honi kuanzia alipokuwa,alivyolifikia geti akaweka mguu kati gari likapiga msele, vumbi likatimka.
“Piiii piiiiiiiiiiiiiiiii”
Ulisikika mlio mkali wa honi,gari likiwa linaunguruma akaona haitoshi,akaweka gia kwenye herufi ‘P’ na kukanyaga mafuta ili apige resi.
“Vuuuuuuum”
Sekunde kumi na tano baadaye akasikia,kufuli linatekenywa.Geti likafunguliwa,mbele akamuona mkewe ametoka, akiwa amevaa Kanga,chini na juu kajifunika.Kabla ya kuingiza gari ndani,akamtizama kwa makini kidogo na kubana meno yake kwa hasira,akakanyaga mafuta mengi na kuingiza gari ndani kwa kasi ya ajabu,hiyo ilifanya mpaka akanyage maua ya bustani iliyokuwa nje.Akazima gari na kushuka huku akipepesuka.
“Karibu Mme wangu,pole na kazi”
Yusrath,akasema kwa adabu zote.Tofauti na siku zote ambazo hulala mapema hata kama Ahmed yupo nje,siku hiyo ilikuwa ni tofauti kwani alimsubiri mpaka usiku huo mzito.Sio kwamba Ahmed hakusikia,hakutaka kujibu alipita moja kwa moja mpaka ndani,Yusrath akafuata nyuma yake.
“Karibu chakula Mme wangu”
“Karibu chakula Mme wangu”
Ahmed alirudia maneno hayo huku akiwa amebana pua yake,akimkebehi.
“Kahabaaaaa mkuuubwa wewe!Tena Kichecheee,kwahiyo unaonaa uniwekee sumu kwenye Chakula nifee.You wan’t to kill me?You waaaant to kiiiill mee?”
Ahmed alizungumza kwa sauti akipepesuka huku na kule,yupo mlango wa chumbani anataka kuingia lakini akaghaili na kumrudia Yusrath.
“Ulikooosa nini kwaaangu,wewe mwanammke?Kisa kukupeendaa,najuuutaaaa.Najuuuuta,nimeoaa bomu la machoziiii,shiiiiiiit.Blood fool”
Yusrath,alibaki kimya machozi yakimbubujika mashavuni, amesimama ameegemea ukuta anaogeshwa matusi,hakutaka kujuta wala kujibu sababu aliamini kwamba anastahili kwa yaliyotokea,mbali na hapo aliumia sababu alijua kwamba kila kitu kimekwisha,iweje Mumewe aanze tena kumuwashia moto?
“Usinitizameee kama unaangaliaa tangazooo ama mjusi guluguja aliyebanwaa na mlango,njee mzuuuuurii lakini ndaniii,shwetaaaani takatakaaa Malaya mchafuuu.Tena shetaani lenye mapembee”
Hapo Ahmed,aliongea kwa vitendo akiweka mikono yake kichwani ili atoe mfano wa mapembe,akatembea mpaka seblen kwenye meza ya chakula akakaa.
“Njooo,unipakuliee nileee.Ilaa nakuchukiaa vibaya saaana,unadhani watanichukuliaje sasa hiiivi,uko nje?Ahmed,kamegewa mke wake,bora basiii ungetembea na kibabu kuliko Yule cheki bobuuu”
Yalikuwa ni maneno ya Ahmed,tena akizungumza kwa sauti ya juu iliyochanganyika na ulevi ndani yake,kazi ya Yusrath kwa wakati huo ilikuwa ni kupakua chakula,akafunika ‘hotpot’ lililokuwa na wali,akafungua bakuli lenye samaki,akapakua pia.
“Kinakutosha?”
Yusrath akauliza huku akipangusa machozi,akitumia viganja vyake vya mikono.
“Onja chakulaaa hiko,siiiweziii kufaaa.Umeniwekeaa sumu kwenye chakulaa nifee..Hahahaha,onjaa”
“Siwezi kufanya hivyo Mme wangu”
“Kama uliwezaaa kutembeaa na Yule mpumbaavu mwenzako,utashindwajee kuniwekea sumu?”
Bila kujibu kitu kingine chochote,Yusrath akachota chakula na kukiweka mdomoni ili kupingana na maneno ya Ahmed kwamba chakula kina sumu,hilo lilimfanya Ahmed amtizame.
“Ngojaa,tusubiri kwa dakikaa kumi.Uliwekaa sumu ya panyaa ama mendee?Mbonaa hufiii?”
Maneno aliyokuwa anayasema ni kweli,aliyamaanisha.Matukio yaliyotokea yalimfanya ajenge wasiwasi mkubwa sana na mkewe,ndiyo maana akaweka mashaka kwenye chakula akijua ni lazima mkewe kamuwekea sumu ili afe kwa niya ya kulipiza kisasi.Ahmed,badala ya kula akasimama, akatembea na kunyoosha mpaka chumbani ambapo huko,alijitupa kitandani na kulala hivyohivyo na viatu.Alichokifanya Yusrath ni kumuamsha Hadima,akamwambia atoe vyombo vyote asafishe na meza!
“Sawa Mama”
“Watoto,wamelala?”
“Ndio Mama”
Yusrath alizungumza akitia huruma,akatembea taratibu akielekea chumbani kwake ambapo huko aliamini anayafuata matusi kutoka kwa Mumewe na dalili za yeye kupigwa siku hiyo ilikuwepo,cha kushangaza alivyoingia chumbani akamkuta Ahmed amelala,fofofo anakoroma anatoa mlio wa ajabu utadhani trekta linalopanda mlima,akasogea karibu akapiga magoti na kuanza kumvua viatu,akamfungua shati na kumtoa suruali,akamsogeza vizuri pembeni kisha kumfunika na shuka!Kuanzia hapo,akaanza kuwaza ni kitu gani akifanye kwani asingeweza kuishi kwenye ndoa yake isiyokuwa na amani.

*****
Mkono wake,ulianza kupapasa kitanda upande wa kushoto, ambapo siku zote Mumewe analala.Akazidi kupeleka mkono mbele zaidi hakukuwa na dalili ya mtu kuwepo,hapo ndipo alipofumbua macho baada ya kugundua Ahmed hayupo!Akatulia kidogo ili kusikilizia kama bafuni kuna maji yanamwagika,huko napo hakukua na dalili ya mtu yoyote kuwepo.Alivyotupa macho kwenye saa ya ukutani,akashangaa baada ya kuona ni saa 1;36 asubuhi,mbaya zaidi siku hiyo ilikuwa ni Jumamosi kumaanisha kivyovyote vile Ahmed asingeweza kuamka asubuhi namna hiyo!Hata hivyo hakutaka kuyapa mawazo yake,kipaumbele sana kwamba Mumewe ameondoka,alichokifanya ni kutoka kitandani na kuliendea dirisha,akafungua pazia,hakuliona gari.Hiyo ilimpa jibu kwamba Ahmed hayupo,akatembea mpaka kabatini na kuvaa kanga,akatoka mpaka seblen.
“Hadimaaaaaa”
“Abee Mama,shikamoo”
“Marahaba,baba ametoka saa ngapi?”
“Saa kumi na mbili”
“Alisema anaenda wapi?”
Lilikuwa ni swali la kijinga kwa Yusrath kuuliza,tena kumuhoji msichana wa kazi.
“Hajaniambia”
Hapo Yusrath,hakujibu kitu chochote akarudi chumbani.Alivyotaka kuchukua simu ili ampigie akaziona simu za Ahmed mezani,akachoka zaidi!Mawazo kwake,yalikuwa ni mengi sana hakuelewa ni mtu gani amtafute amshauri,alivyofikiria kurudi kwao akalitupitilia wazo lake mbali sababu angeshindwa kujibu maswali ya wazazi wake,kwanini umeondoka kwa mumeo?Hakuwa tayari kuanika mambo aliyofanya, kwake ilikuwa ni aibu kubwa ukizingatia alikuwa ni mtoto aliyetoka kwenye familia ya kiislam,swala tano!Akakosa kabisa raha ya maisha,hakuelewa changamoto hiyo angeitatua vipi.Akawakumbuka rafiki zake tofauti tofauti wenye busara,kuna taasisi moja inayohusika na ushauri wa ndoa na changamoto za maisha lakini jina lilimtoka!Alivyomkumbuka Witness Kafifi,akapata wazo kabambe.Hakuchelewa akachukua simu na kumtafuta msichana huyo hewani,simu ikaita kisha kupokelewa.
“Za asubuhi,Witness”
“Salama dada shikamoo”
“Marahaba,vipi familia?”
“Haijambo,sijui wewe huko?”
“Huku Insha Allah,tunamshukuru Mungu,Witness nina shida na kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Unakumbuka siku ile tulivyokuwa Bestbite,ulikuwa na rafiki yako mmoja hivi.Alikuwa amevaa ushungi na miwani?”
“Unamsemea,Roshban?”
“Sijui,lakini alikuwa analalamika kuhusu ndoa yake.Akasema sijui kuna kampuni sijui tahasisi,something like that”
“Yes yes yes,nakumbuka”
“Nahitaji,jina lake”
“Jina la hiyo taasisi?”
“Ndio,wanapatikana wapi?”
“Story za Kway Therapy?Si unasemea wanaotoa ushauri?”
“Ndio”
“Mimi nawajua hao,wako vizuri sana.Wapo Posta pale lakini Makao makuu yao yapo Mikocheni”
“Siwezi kupata namba zao za simu?”
“Mpaka ufanye booking,ngoja nikupe link yao.Una peni hapo?”
Yusrath,akatembea mpaka chumbani kwake,akafungua mkoba na kutoa kalamu.
“Ninayo”
“Andika www.facebook.com/STORYZAKWAY. Ingia kwenye huo mtandao,wafuate inbox,utapewa utaratibu”
“Ahsante”
Yusrath,akakata simu.Akaingia kwenye mtandao wa ‘google’,akaanza kuandika ili kuutafuta,kabla hajamaliza mlango wa chumbani kwake, ukagongwa.
“Mama kuna mgeni wako”
Sauti ya Hadima,ilisikika kutokea nje!
“Mgeni gani?”
“Simjui”
Yusrath,akasitisha shughuli aliyokuwa anaifanya.Akaingia bafuni akanawa uso na kuvaa dera ili akaonane na mgeni wake,asubuhi hiyo ambaye alifika bila taarifa.Kichwani,aliwaza ni aina gani ya mgeni.Akatembea mpaka seblen,ambapo huko alikutana na mwanamke mnene kiasi,amevalia gauni la kitenge,akamuangalia kwa umakini kama anayemfananisha lakini ilionekana kama picha inakuja na kupotea.
“Habari yako”
Mwanamke huyo alisalimia na kumpa Yusrath mkono kwa niya ya kumsabahi,hiyo ikamfanya Yusrath agande kidogo lakini libidi atoe mkono wake huku akizidi kudadisi,wakasalimiana.
“Naitwa HAJRATH MPILLA,nina muulizia kaka angu Ahmed.Nadhani wewe ndio wifi yangu?”
Hajrath alizungumza huku akitabasamu,akimchangamkia Yusrath.
“Karibu sana,jisikie upo nyumbani..Weee Hadimaa,Hadimaaaaaa”
Yusrath akamuita dada wa kazi,akatokeza.
“Muwekee mgeni chai,mkaangie na Soseji.Wifi yangu karibu,lakini sijakufahamu vizuri”
Hakuna siku ambayo Yusrath alionesha uchangamfu kama hiyo,hata yeye hakuelewa ni kwanini ametokea kumpenda Hajrath, ghafla namna hiyo.
“Ni mtoto wa Mama yangu mdogo,naweza nikasema Mpwa.Kwenye harusi yenu mbona nilikuja,lakini baada ya hapo nilisafiri”
Kila alichokuwa anazungumza Hajrath hakikuwa na ukweli hata kidogo ndani yake,hakuwa ana undugu wowote ule na Ahmed na ilimpa tabu sana kupajua anapoishi,niya ya kufika hapo ilikuwa aseme shida zake lakini kabla ya yote ilikuwa ni lazima atumie uwongo ili kumlainisha Yusrath.
“Karibu mezani”
“Ahsante,lakini nimemkuta?”
“Ametoka,atarudi.Tafadhali msubiri”
Hajrath,akasimama na kwenda mezani ambapo huko juu ukutani, aliona picha ya Ahmed akiwa ndani ya suti kushoto Yusrath amevaa shela,moyo wake ukachoma kama pasi,akaumia ajabu lakini ilibidi ajikaze kisabuni.
“Mlipendeza sana”
Hajrath,akatia neno!
“Ahsante”
Kilichosikika hapo,zilikuwa ni stori za hapa na pale,dakika mbili baadaye wakasikia mlio mkali wa honi, kutokea nje ya geti.
“Pipiiiiiiiiii”
Hiyo ilimfanya Yusrath atulie kidogo mapigo yake ya moyo, yakaanza kubadilika. Wasiwasi ukaanza kumjia, akakumbuka matusi ya usiku uliopita, akakosa raha kabisa.Hadima akatoka na kuelekea nje ili afungue geti.
“Kaka ako ndio huyo anaingia”
Yusrath akamwambia Hajrath!Akiwa kama mwenye wasiwasi usoni.
*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)



0 comments:

Post a Comment

BLOG