Search This Blog

Monday, March 23, 2020

ABEE SHEMEJI SEHEMU YA 10 MWISHO


ABEE SHEMEJI
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 10 KATI YA 10 MWISHO
*******

Familia nzima na baadhi ya ndugu wa Yusrath waliendelea kusota rumande na walishafikisha siku kumi na mbili bila kuachiwa huru ama kupata dhamana,walilia na kusaga meno huku wakimlaani Yusrath popote alipo lakini hilo halikuweza kubadilisha chochote kile kilichotokea,ilikuwa ni lazima waseme ni wapi Yusrath alipo ama wataje walipozificha milioni Mia tano za Bilionea George
Charles, kitu ambacho kwao kilikuwa ni kitendawili kikubwa,hakuna mtu yoyote kati yao aliyeelewa pesa hizo nyingi zilikuwa wapi,hata hivyo askari hawakuwa tayari kuwaamini hata kidogo,wakiwa hakikishia kwamba ni lazima wangeenda gerezani!Mama Yusrath alilia kuliko kawaida na aliumia mtima kwani hata siku moja hakuwahi kuwaza kama angeingia katika mkasa huo hatari wa aina yake,taswira ya milango ya gereza ikifunguliwa na kutupwa ndani huku akihukumiwa kifungo cha miaka kadhaa jela ilijijenga kichwani kwake kila kukicha akiwa ndani ya chumba hiko kidogo ambacho hakuelewa majira nje yanaendaje!Alitamani mambo yote yawe ndoto lakini muujiza huo usingeweza kutokea hata kidogo!Msako wa msichana anayeitwa Yusrath uliendelea kimya kimya,maaskari kanzu na makachero kutoka jeshi la polisi walimwagwa kila mtaa wakimsaka Yusrath,kiasi hiko kingi cha pesa kiliwatoa udenda na kila askari alitamani amkamate yeye,wakaanza kuwasaka marafiki zake wote wa karibu na wengine walichukuliwa ili kutoa maelezo vizuri kituoni.
“Afande,nimebandika maharage jikoni”
“Nenda kazime jiko,tunakusubiri”
Mmoja wa marafiki zake,ilibidi akasaidie kutoa maelezo kituo cha polisi baada ya askari kumkuta maeneo ya Kigamboni,Mji mwema!
Siku zilizidi kukatika bila mafanikio,wakawa wana uhakika wenda Yusrath ametokomea mikoani,hata hivyo mawazo hayo hawakutaka kuyapa kipaumbele sana!

*****
Kulikuwa kuna uwezekano mkubwa kwa Yusrath kunusurika kuonekana na maaskari kama asingegeuka nyuma baada ya kuona gari,kitendo hiko kilimfanya Kamanda Sudy,apige breki na kumtizama vizuri.
“Tunayemtafuta yule pale”
Kamanda Sudi akasema,akiwa mtu mwenye uhakika wa moja kwa moja!Sura ya Yusrath haikuweza kumtoka kichwani hata hivyo alikuwa na picha yake mkononi ili kuhakikisha akaitizama kwa makini,hawakutaka kuchelewa wakaweka diffenda pembeni na kumsogelea,ambapo mmoja wapo akamshika bega!Kassim alikuwa pembeni,tukio hilo lilimshangaza hata yeye,hakuelewa ateremke ama abaki ndani ya gari baada ya kuona askari wamemzunguka Yusrath, wanamuhoji maswali kitemi na askari hao walihoji maswali wakitumia ubabe wa hali ya juu sana!
“Wewe ndio Yusrath na utaondoka na sisi”
Kamanda mmoja aliyekuwa na cheo cha Sirgent,alichimba mkwara sura yake ilikuwa mbali na mzaha,macho yake mekundu mdomo wake mweusi kama pua ya mbwa alionekana kabisa alikuwa ni mvutaji hodari wa bangi!
“Kwenda wapi?”
Yusrath akauliza kwa sauti ya kitetemeshi,Kassim alivyoona hivyo akashuka ili ajaribu kuzozana nao!
“Kuna nini afande?Mbona mnakuwa sio wastaarabu”
Kassim,akataka kujifanya mwamba ili achukue ujiko kwa Yusrath hata hivyo alitulizwa!
“Tulia mtoto wa Mama,usipoangalia utaongozana na sisi!Huyu ni mwizi,tunaenda naye pale Central.Kwa maelezo zaidi,utamkuta pale”
Kwa picha ya haraka bila kuhoji kitu kingine chochote kile,akajua kosa lake lipo wapi ndiyo maana akabaki kimya,ilikuwa ni lazima ataje milioni Mia tano zilipo na hakupata muda wa kusema lolote, zaidi ya kuongozana na maaskari mpaka kwenye difenda!
“Panda juu hapo,fanya haraka!Kabla sijakuzabua makofi”
Askari akapiga mkwara kama kawaida,Yusrath akashika chuma la juu na kujivuta huku machozi yakimlenga kila kitu kwake kikawa kama sinema ya kuhuzunisha,mambo yaliyomtokea alijua kabisa anastahili sababu siku zote ni lazima uchume ulichopanda!Hiyo ilimfanya Kassim,abaki akiduwaa bila kuamini kinachoendelea,alitamani kuwaungia askari hao lakini hakutaka kujiingiza katika mkasa wowote ule kwani alijua tabia za maaskari zilivyo si ajabu angeishia kulala kituo cha polisi!

*****
Furaha aliyokuwa nayo Ahmed,haikuweza kuelezeka kiwepesi ama kwa maandishi!Ndoto ya muda mrefu ya kutaka kuitwa Baba ilimfanya ajione kama simba msituni na hakuna kama yeye,muda wote meno yake yalikuwa nje!Yupo wodini kambeba mtoto wake mdogo mchanga!Bila kupima DNA yoyote alikuwa ana kila sababu ya kusema kwamba mtoto ni wake,japokuwa alikuwa bado mdogo sana lakini kuna vitu kama vidole,kucha za miguu viliendana!Wakati akiwa mikononi mwake,aliweza kuchunguza pasipo mtu yoyote yule kugundua!Pembeni,alisimama mama yake mzazi,kushoto aliketi Mama yake Hajrath wote walionekana wakiwa wenye furaha mno kupata mjukuu,alikuwa ni mtoto mwenye afya njema na kila mtu alitamani kumbeba!
“Hongera Mwanangu”
Mama Hajrath,akatoa pongezi!Ahmed hakukaa sana, Benjamin Ngowi akawa amefika,mkononi ameshika mfuko uliojaa matunda mengi,wakasogea kando ili watete kidogo!
“Ndugu yangu,sasa huyu ni wako kweli”
Ngowi akaanza kuchombeza huku akipiga jicho kwa mtoto mchanga!
“Kwanini kaka?”
“Naona,mmefanana!Nimeona tu,bichwa lile.Na kichwa chako hiko kilivyokaa kakaaa”
“Hahaha”
“Sio wale wa siku ile,mimi nilianza kuhisi uju…”
“Aaah,tuachane na hayo!Vipi mambo”
“Safi mzee,nimeona nipite chap hapa!Niwahi home,nimetoka mzigoni”
“Pole Mkuu,bwana wee!Hapa katikati nilipata shida mzee,ulivyokuwa China”
“Weee,nini zaidi?”
“Basi tu,mambo yalienda vibaya vibaya”
“Si inshu ya Yusrath ile au?”
“Noo,kuna mengine yalizuka kaka,nitakupa mkanda nikitulia.Lakini Dunia hiii,asikwambie mtu ni kisanga,sogea karibu nikwambie”
Ngowi,akasogeza sikio karibu ili aambiwe jambo na rafiki yake!
“Nilinusurika kupata umeme”
“Umeme!?”
“Ndio,Ukimwi mzee”
Ngowi,akatoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango!Akamtizama rafiki yake kuanzia juu mpaka chini na kumuangalia kwa macho fulani,yanayotaka kusema kitu!
“Sijakuelewa”
“Hilo tisa kumi sasa….Anywei Ngowi,nitakutafuta!Nenda home msalimie shem”
Kufuatia hapo,wakaagana vizuri na kila mtu akiwa na furaha ya kumuona mwenzake!Ilibidi Ahmed akae hospitalini mpaka saa tano ya usiku,alihisi kuchoka lakini hakua tayari kumuacha Hajrath mahali hapo!
“Nenda tu baba angu,atakua salama”
Ni Mama Hajrath ndiye aliyetoa pendekezo hilo,macho ya Ahmed yaliyojaa uchovu yalimfaya amuonee huruma,hapo ndipo Ahmed akaaga na kuondoka zake akihaidi kwamba angepita asubuhi kabla ya kwenda kazini!
Usiku wa siku hiyo kwa Ahmed,ulikuwa mrefu, alimzoea Hajrath akiwa pembeni yake wanapiga stori na joto lake wakikumbatiana lakini siku hiyo ilikuwa ni tofauti kabisa,kila alipolala alijigeuza huku na kule,wakati mwingine alihisi joto kali na muda ulijisogeza taratibu mno!Hata hivyo kulikucha alichokifanya ni kupita kwenye moja ya migahawa,akanunua uji mzito na kuuweka ndani ya gari na safari ya kwenda hospitalini kuanza!Huko aliacha uji na baadhi ya pesa za matumizi kisha kuwahi kibaruani kutafuta mkate wa kila siku,furaha yake iliongezeka kwa kiasi cha kutosha kwani aliamini baada ya hapo ndoa ingefuata sababu kilichokua kinasubiriwa ni Hajrath ajifungue ili achukue jiko jumla jumla,hata alivyowasili ofisini alionesha tabasamu la waziwazi kama mtu aliyeshinda mamilioni ya pesa kwenye bahati nasibu!
“Ahmed,uliandaa ile tenda ya juzi!GPSA wanahitaji,deadline ni keshokutwa”
Sekretari ama mfanyakazi aliyefahamika kwa jina la Christina,alikua ofisini kwa Ahmed!Alikuwa ni binti mdogo anayependa anachofanya,muda wote alikuwa bize kuliko mfanyakazi yoyote ndani ya kampuni hiyo,kwake yeye ilikuwa kazi kwanza ndiyo maana muda wote aliulizia mikakati na mfumo mzima wa ofisi unavyokwenda!
“Tina,karibu ukae kwanza!”
“Ahmed,nimeacha wateja kule”
“Naelewa,kaa basi kwani kuna tatizo gani?”
Ushawishi wa Ahmed ukazaa matunda Tina akatembea mpaka kwenye kiti cha wageni,akaweka sketi yake vizuri,akaketi.
“Mbona juujuu hivyo?Leo umependeza”
“Acha utani wako basi Ahmed,nimeshakaa niambie!”
“Tenda tayari,bado nasubiri watume akaunti namba ili nikalipie benki”
“Unafanya mchezo na Vero wewe,naona hutaki kazi”
Tina,aliogopa! Namna alivyozungumza ilionesha wazi kwamba anamgwaya Veronica mno na anamuogopa ndiyo maana akajitahidi kumuogopesha Ahmed pia.
“Acha nidhamu ya uwoga”
“Sio hivyo Ahmed,yule Mama ni mtata sana!Basi tu,kwa kuwa hujamjua vizuri!We subiri ipo siku utamjua”
Tabasamu la Ahmed lilichanua,akacheka kwa dharau sababu alijua kivyovyote vile Veronica hatoweza kumfanya lolote kwani walikuwa na ajenda yao ya siri,licha ya hiyo hakutaka kulionesha hilo waziwazi,akamezea na kumruhusu Tina akaendelee na kazi!Lakini Tina alivyofika mlangoni,akakumbana na Veronica akiwa katika harakati za kuingia ofisini kwa Ahmed,akamkata jicho kali!
“Shikamoo Bosi”Tina,akasalimia kwa uwoga!
Salamu hiyo iliitikiwa baada ya sekunde tano kupita,Tina alivyopita Veronica akafunga mlango nyuma yake!Kupitia macho yake,ilionesha ni kiasi gani alishikwa na wivu mkali,akamtizama Ahmed na kwenda moja kwa moja kwenye kiti!
“Mlikua mnaongea nini?”
Lilikuwa ni swali lilionesha wivu wa waziwazi kabisa!
“Mambo ya tenda yale”
“Tenda wapi!Muda wote huo?Mlikua mnatongozana hapa,mimi sio mtoto”
Veronica,akaongea lililokuwa moyoni mwake!Alihisi kumpenda Ahmed ndiyo maana moyo wake ulimuuma ajabu,akatulia kidogo na kumtizama machoni!
“Bado una deni langu”
Veronica,akafunguka.
“Lipi?”
“Mara hii umesahau,nakupenda Ahmed”
“Hata mimi mbona nakupenda”
“Sio kama unavyofikiria,nahitaji uwe wangu!Mbona unaninyanyasa,nilishakwambia.Sitoharibu mahusiano yako yoyote yale,sitokusumbua nachohitaji niwe nawewe tu,sijawahi kumtongoza mwanamme na kumlilia namna hii,nionee huruma”
Kila shetani na mbuyu wake,Veronica alikufa akaoza kwa Ahmed hilo lilikuwa wazi na alizungumza bila kupepesa macho wala kope,kile alichokisema kilitoka ndani ya mtima wake hakujali Ahmed angemfikiria vipi, yeye alichojali ahueni ya moyo wake ili upate pumziko la milele na aliapia kama angempata Ahmed,angetulia kabisa ingawa alimpenda mumewe pia!
“Una mume lakini”
“Ndio maana nikawa mkweli kwako,sikutaka kukuficha.Nina mume nina watoto vilevile”
“Sasa kwanini usitulie?”
“Ahmed,tunarudi kule kule sasa”
“Poa,nitakufikiria!Nipe muda”
“Mpaka lini?”
“Nitakujibu”
Veronica,alisimama wima macho yake yakiwa yamelegea mno anamtizama Ahmed, bado haamini kama ni yeye ametoka kumtongoza kijana mdogo kama huyo,akaona aibu na kuangalia chini kwa upole kabisa,akatembea na kutoka nje huku akimuacha Ahmed nyuma anayaangalia makalio yake yanavyotingishika!
“Huu sasa mtihani huu,hizi lawama kabisa!Lakini tutajua mbele ya safari”
Ahmed,akajikuta anaropoka mwenyewe kisha kutupa macho yake juu ya kompyuta akiedelea na kazi!

******
Jioni ya siku hiyo baada ya kutoka kumuona Hajrath hospitalini,akaamua kupitia moja ya baa ili akate kiu kwa bia mbili tatu walau apate usingizi kutokana na uchovu aliokuwa nao!Wakati mwingine imani yake ilimtuma bia hufaa kwa mtu aliyechoka na kazi hivyo ili apate usingizi mwanana alihitaji kupata bia kama tatu hivi kisha kuoga na kulala!Hivyo ndivyo alivyotaka iwe,akapaki gari kwenye baa moja inayoitwa PK,karibu na Ubungo maji,mkabala na gorofa la TANESCO,hakukua na vurugu nyingi sana,baa ilipooza na jambo hilo alilipenda sababu siku hiyo hakutaka sehemu yenye vurugu!
“Niletee Kilimanjaro ya baridi”
Ahmed,akaagiza bia kwa Mhudumu aliyefika dakika moja ikawa nyingi,mezani kukawa na chupa kubwa ya bia,akamimina kwenye glasi na kunywa kidogo!Hapo alipata muda wa kutafakari mambo mawili matatu,jinsi atakavyoitwa baba badaaye akiwa kama mwanaume mwenye majukumu katika familia,dakika kumi baadaye chupa moja ikawa imeisha akanogewa na kuongeza nyingine,akiionya nafsi yake hiyo ingekua ya mwisho lakini ilivyobaki kidogo akaagiza nyingine!
“Dada,ebu niongezee ya mwisho!Alafu niletee bili yangu niondoke zangu”
Alisema hivyo kumaanisha kwamba baada ya hapo,aondoke kwani alitaka kurudi mapema kwake apumzike hata hivyo alielewa udhaifu wake upo wapi baada ya kunywa pombe,hakutaka shetani ampitie!Alivyotafakari kidogo,akamkumbuka Veronica jinsi alivyo, weupe wa mwanamama huyo,ukamfanya afikirie vitu chungumzima!Taswira ya kunyonywa tango,ikamjia akajiona alivyosimama tango lake likiwa limeshikwa linalambwa,mwili wake ukamsisimka ghafla na karoti ikaanza kufurukuta kiasi!Alivyojitahidi kushindana na ibirisi,akashindwa hapohapo akasimama na kwenda kando ambapo alichukua simu na kumtafuta Veronica hewani.
“Upo wapi?”
Ahmed,akauliza bila salamu,jinsi alivyouliza ni kama anayemuuliza mkewe!
“Ahmed,nipo Mwenge vipi kwani?”
“Njoo hapa,Ubungo maji.Tunywe!”
“Ubungo Maji?Ndio wapi?”
“Kuna baa moja,nipo hapa”
“Ahmed,baa?!Hua sikai,baa mimi.Wee njoo Mwenge!”
“Kwahiyo hutaki?”
“Sio kwamba sitaki,baa sikai!Inshort sikai sehemu loko loko!Nipo hapa Mwenge,kama unaweza tukutane Samaki samaki”
“Mlimani?”
“Yes,tukutane hapo”
Ahmed,akaguna!Akaangalia mazingira aliyopo na mfanano wa Veronica vilikuwa ni vitu viwili tofauti,Veronica alionekana ni mwanamama mwenye uwezo kifedha na matawi ya juu,kukaa sehemu kama hizo asingeweza,ilibidi amuite muhudumu na kumlipa pesa zake,akaingia ndani ya gari na kuondoka!
Kutoka Ubungo mpaka Mwenge kwa usafiri binfasi ilikuwa ni sawa na pua na mdomo.Dakika kumi na saba,alikuwa Mlimani City,anaegesha gari!Akashuka na kutembea mpaka samaki samaki,ilikuwa ni sehemu iliyotulia yenye ustaarabu wa hali ya juu!Sasa hapo,aliamini ndio hadhi ya Veronica,kwanza asilimia ya watu waliokuwemo ndani walikuwa wazungu,waliobaki walikuwa waafrika lakini walionesha kujiweza kiuchumi,isitoshe kila mtu alikunywa pombe kwa ustaarabu huku mziki mzuri wa Celine Dione unaoitwa ‘Power of love’ ukiwa unatumbuiza,sehemu hiyo hakuwahi kuingia hata siku moja,hupita tu nje,siku hiyo akajihisi nayeye ni miongoni mwa matajiri kuingia mahali kama hapo!Katika kushangaa kwake,nyuma akaona kiti kirefu kiasi,kilichochongwa kwa mtindo wa mbao ukafanana na samaki,kimerembwa vizuri huku taa hafifu zikimulika mulika,akatembea mpaka hapo na kukaa!Mhudumu akamfikia,alikuwa ni kijana aliyevaa tai shingoni aina ya ‘Balltie’ amechomekea vizuri, msafi.
“Kuna kinywaji gani?”
“Kuna bia,wine,cocktail,Mocktail,shots za takira,vodka na vingine vingi”
“Niletee Red wine”
“Sawa”
Jinsi ya kulipia eneo hilo,ulimshangaza kwani kijana huyo alienda kwenye kimashine maalum,akabonyeza bonyeza ikatoa karatasi,akanyoosha mpaka kaunta!Akafuatilia kila hatua,mpaka pale aliposhtuliwa na Veronica!
“Umekuja muda mrefu?”
Veronica akauliza kwa uchangamfu huku akiachia tabasamu mwanana,akamsogelea Ahmed karibu na kumkumbatia kimahaba!
“No,sasa hivi nimeingia”
“Ahmed,ulitaka uniite baa?Hizi ndio sehemu unazotakiwa uje mtu kama wewe,ukikaa hapa kwanza utapata akili mpya…Kaka,naomba Heinken”
Veronica alivyomuona kijana wa vinywaji ameweka wine ya Ahmed,nayeye akamchomekea!
“Muongeze na huyu Wine nyingine”
Alivyoacha maagizo hayo,akamgeukia Ahmed na kumtizama!
“Nakupenda Ahmed,ahsante kwa kuniita!Nilikuwa hapo Mwenge,kuna mradi mmoja nimefungua ndio nilifika kupiga hesabu”
“Mradi gani?”
“Vyakula,inshort nafaka!Nauza jumla na rejareja”
Ahmed,alitokea kuvutiwa sana na maongezi hayo,akaanza kumdadisi Veronica kwa kumuhoji maswali mpaka ilivyoletwa vinywaji.
“Cheers Ahmed”
Wakagonganisha glasi na kuziweka mdomoni!
“Ngoja nikwambie kitu kimoja Ahmed,I mean baby wangu!Maisha haya ni mafupi sana,katika maisha sijazoea kujinyima!Natafuta pesa,ili iweje?Ni enjoy,alafu ukitaka kufanikiwa siku zote don’t sale your self so cheap!Usiwe mrahisi,kwanza kuwa expensive! Utaheshimika alafu pili utapata marafiki wapya wenye uwezo wa kuku challenge,sasa unakaa baa nani ataku challenge?”
“Unaongea pointi sana ujue Veronica”
“Kitu kingine nakupa mfano tu,mtu anayeendesha Range na Vits.Ni watu wawili tofauti,mwenye Range atafikiria kupata laki moja ya mafuta Vits elfu kumi!You get?”
“Yes,nakupata Veronica”
“So focus,siku moja moja unaenda hata pale Kempiski unaenda kupata lunch!Lazima upate exposure ya maisha,utapata marafiki wapya”
Siku hiyo Veronica aliongea vitu vya msingi na vilimuingia Ahmed kichwani,akajikuta nayeye amekua tajiri ghafla.
Hata hivyo kuna kitu alikumbuka,akatoka na kumpigia Hajrath simu akimwambia anaingia kulala hivyo,ataweka simu chaji ulikuwa ni uwongo lakini hiyo ingemsadia kujiweka katika mazingira mazuri na salama.Alivyorudi akamkuta Veronica yupo kwenye kiti,sketi yake imepanda kidogo paja lake jeupe lipo nje!
“Kwenye maisha yangu mimi Ahmed,sipendi kua tegemezi.Eti nimtegemee mwanaume!Hell no,nimeolewa fine.Lakini sijawahi kumuomba Mme wangu pesa hata senti tano,labda anipe mwenyewe wakati mwingine ananiita mimi kiburi lakini walaaa”
Akamaliza na kuweka glasi ya bia mdomoni.
“Vizuri sana”
Pombe zilianza tayari kufanya kazi yake,mbaya zaidi alichanganya wine na bia pamoja na yote mbele yake alikuwa Veronica,mwanamama mrembo ambaye alimfananisha na ndege mzuri kasuku anayeimba kwa sauti nzuri!Samaki samaki ilikuwa sehemu ya wastaarabu sana,hakukua na kelele za fujo na nyimbo zake zilikua za kiingereza na sio singeli.
Kwa kuwa Veronica,alikaa kwenye pembe ya kona kulipokua na giza,Ahmed nayeye akasogea bila kuuliza chochote,akamfikia mdomoni mwake wakaanza kulana denda kwa fujo,wakaachiana na kutizamana kimahaba!Veronica akapandwa na midadi zaidi baada ya nyimbo anayoipenda kupigwa,ilikuwa ni nyimbo ya Rihana inayoitwa ‘pon de replay’hiyo ilimfanya aanze kukizungusha kiuno chake huku akiwa juu ya kiti,jambo hilo lilimfanya Ahmed apagawe kama fisi aliyeona mfupa,udenda ulimtoka mwanamama Veronica alikuwa na kiuno chepesi kukizungusha,uvumilivu ukamshinda Ahmed, akajikuta kamshika kiuno na kumfuata karibu na kuanza kumnyonya mdomo tena yaani denda, bila aibu!Aliyewakatisha stimu alikuwa ni yule kijana muhudmu aliyewaletea vinywaji.
“Samahani,hapa haturuhusu kupiga picha”
Sentensi hiyo iliwakera na kuwakata morari kwani kati yao hakuna hata mmoja aliyeshika kamera!
“Kwani nani kapiga picha?Hakuna mtu aliyepigaa picha,mbona unakata stimu za watu kiongozi”Ahmed,akabwata kwa hasira!
“Hapana,kuna mtu alikaa pale muda mrefu alikuwa anawapiga picha,nilivyomuuliza akaniambia mmemtuma”
Kila mtu aliganda na kukaa kimya kwa sekunde kadhaa,macho yao yote wakatupa nyuma kufuatisha kidole cha muhudumu huyo ili waone mtu anayewapiga picha,kitu kilichowashangaza hadi muhudumu hakukua na mtu yoyote kwenye meza,isipokuwa chupa mbili za bia ambazo zilikuwa zimeisha!Jambo,hilo liliwafanya waogope zaidi na kuhisi kama wamepigwa sindano ya ganzi!




Kila mtu alikosa raha ya kukaa eneo hilo tena,macho yao yalikuwa yanaangalia nyuma kumtafuta mtu aliyesadikika kwamba aliwapiga picha,baada ya kumkosa ilibidi wamgeukie tena Mhudumu na kumuhoji.
“Wewe,una uhakika?”
Veronica aliuliza akiwa mwenye sura ya wasiwasi kama mtu mzima anayeoga nje!
“Ndio dada,alikuwa pale”
“Kavaaje?”
“Tshirt nyekundu na jinsi,mnene hivi”
Katika kumbukumbu za kichwa chake akajaribu kumfikiria mtu ambaye angeweza kumpiga picha,taswira ya mumewe ilivyomjia kichwani na maelezo aliyotoa mhudumu vilikuwa ni vitu viwili tofauti kwanza Muwewe hakuwa mnene cha pili hakuwa jijini Dar es salaam,jambo hilo likamfanya atoe fikra hizo potofu kwamba mumewe anamfuatilia na kumuangalia Ahmed!
“Tuondoke Ahmed”
Hakukuwa na kipingamizi na hakukua na haja ya kubaki mahali hapo tena,wakatembea mpaka kwenye maegesho ya magari.
“Sikia,napeleka gari Warioba pale.Nifate nyuma kisha tutatumia gari yako!Hii gari inajulikana sana,sitaki kutembea kwa mashaka”
Veronica alitoa wazo akimwambia Ahmed namna ya kufanya huku yeye akitembea kuelekea upande wa kushoto alipoacha gari yake,Ahmed akasubiri mpaka alivyoona gari ndogo ya kifahari aina ya JAQUAR linasimama kando yake, kioo kikashushwa!
“Nifate nyuma”
Veronica alitoa maelezo hayo huku taratibu akiliondoa gari lake,hiyo ilimfanya Ahmed afate maelekezo wakaanza kuongozana mpaka Mikocheni,hapo Veronica alipaki gari vizuri akaenda kuzungumza na mlinzi wa ukumbi huo kisha kuingia ndani ya gari la Ahmed!
“Mbona unaacha gari hapa?”
“Nitakwambia baadaye,Ahmed umeoa?”
Lilikuwa ni swali lililomfanya Ahmed amtizame Veronica mara mbilimbili,hakuelewa swali hilo lina maana gani ndiyo maana alitafakari kidogo!
“Kwanini umeniuliza hivyo?”
“Aaah aaah,nina maana yangu!Kumbuka kuna mtu katupiga picha isije ikawa mkeo katuma watu ikawa kizai zai,katika maisha yangu sipendi kashfa kama hizo”
“Usijali kuhusu hilo,kua na amani!Labda mumeo,lakini sidhani kama tumepigwa picha itakuwa yule Mhudumu Kivuruge”
Ahmed aliongea kwa namna ya kumtoa wasiwasi Veronica aliyeona kabisa kapoteza mudi ya kuzungumza!Kufuatia hapo,ukimya kidogo ulitawala lakini Ahmed akauvunja kwa kuuliza swali.
“Tunaelekea wapi?”
“Pikolo Hotel”
“Ndio wapi?”
“Ahmed,wee mwanaume hutembeagi kabisa!Pikolo hupajuiii?”
“Sasa mimi Pikolo Hotel nikafanye nini?”
Ahmed hakutaka kuonekana mshamba,akatengeneza hoja ya kujitetea!
“Kutembea kuswim pia,ni sehemu nzuri.Siku nyingine nitakupeleka Golden Tulip,nina uhakika napo hupajui”
“Sasa nikafanye nini huko?”
Stori zilikuwa nyingi,Veronica alitabasamu na kuanza kuuliza maswali ya hapa na pale akimtania Ahmed,akasahau kabisa huyo alikuwa mfanyakazi wake ofisini!Dakika kumi baadaye wakawa wameingia kona ya Pikolo Hotel,Veronica akamuelekeza ilipo wakasimama nje ya geti kubwa ambapo walifunguliwa na mlinzi aliyevaa sare za kazi,wakanyoosha mpaka nje ya gorofa kubwa ambapo kando yake kulikuwa na bwawa la kuogelea!Kutokana na usiku kuingia hakukua na mtu yoyote aliyekuwa anaogelea,isipokuwa wazungu wachache waliokuwa wamekaa wanapiga stori!Mandhari ya eneo hilo ilimfanya Ahmed,ashtuke kidogo ilikuwa ni sehemu iliyotulia mno!Mtu wa hali ya chini isingekuwa rahisi kufika hata kuingia,kwa muonekano paliogopesha kabisa!Wote wakashuka ndani ya gari na kuongozana mpaka mapokezi,ambapo hapo walipewa kadi ya hoteli na kukaribishwa vizuri!Bado Veronica hakuamini kama siku hiyo anaenda kukutana na Ahmed kwenye sita kwa sita,ndiyo maana akaona kama anachelewa kufika chumbani,kichwa chake kilijaa vitu vingi sana,alipanga ampe vitu hadimu Ahmed ili siku nyingine akimuita asidengue!Kwa hatua za haraka kiasi wakafanikiwa kufika mlangoni,ambapo hapo waliweka kadi na kuusukuma,Veronica akazama ndani Ahmed akafuata mlango ulivyofungwa tu!Ahmed akarukiwa mdomoni wakaanza kulana denda,kilichosikika hapo ilikuwa ni miguno mithili ya mtoto anayenyonya maziwa kwenye kopo!Ndani ya chumba kukawa na patashika,wakaanza kuvutana huku na kule huku midomo yao ikiwa imegandana,Veronica alikuwa na moto usio kawaida na mikono yake haikutulia,mara iende masikioni mwa Ahmed mara amkwaruze mgongoni,alivyoona amepata engo nzuri,akaingiza mkono wake ndani ya shati la Ahmed,akaanza kumpapasa kifua akafika mpaka kwenye chuchu na kuanza kuzipalaza,hapo ndipo Ahmed akahisi kupagawa,mwanamama huyu hakuishia hapo akashuka chini zaidi na kutoa mkanda wa Ahmed,akamfungua kifungo na kumtoa nyoka aliyekuwa tayari amesimama dede,bila kupenda akapiga magoti na kumshika vizuri, akamuweka mdomoni na kuanza kumlamba!Kuendelea kukaa bila kuonesha jitihada zozote zile,angedharaulika ndiyo maana akaanza kumtioa Veronica nguo moja baada ya nyingine!Hiyo ikawapandisha midadi na kwa kasi wakaanza kuvuana nguo wakabaki kama walivyozaliwa,wakatupana kitandani!Alichokifanya Ahmed cha kwanza ni kuishika miguu ya Veronica huku na kule,akaingia katikati ulimi wake akajaza mate na kuanza kupiga deki bahari,jambo lililomfanya Veronica aweweseke kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa!Kazi yake ilikuwa ni kukunja kunja mashuka,hakika alihisi raha ambazo katika maisha yake hakuwahi kuzipata kabisa!Akaanza kuvuta vuta mashuka mara kadhaa akitaja jina la Ahmed na kuzungumza kiingereza,hiyo ilimpa ujiko Ahmed!
“Ahmed Fuc**** me now please, i’m wet”
Akalalamika baada ya kuona maji ya shingo kwani tayari alikuwa amelowa hajiwezi tena,ilikuwa ni kama ametoa ruksa,Ahmed hakuchelewa akapanda juu kidogo na kuyakamata mapaja yake vizuri, yaliyokuwa meupe,mguu mmoja akauweka begani mwingine kando kidogo!Taratibu sana kwa mapozi akaanza kumuingiza nyoka wake,mpaka akazama kabisa!Hiyo iliimfanya Veronica afumbe macho yake,akihisi kama ameota mbawa!Kushughulika kwa Ahmed na zoezi zima la kupanda juu na kushuka huku akikinyonga kiuno chake kilichukua dakika tano nzima,ndipo wakabadili staili,Veronica alikuwa hoi ameshapanda milima mitano na wakati huku alikuwa anakaribia kufika kilele cha mlima kwa mara ya sita!
“Ahmeeeed,nishiiiike kiuno….”
Akiwa chini kifo cha mende,alilalamika huku akijitahidi kukinyonga kiuno, Ahmed akatiii amri akamshika kiuno kwa mtindo wa kukipapasa!Veronica akajinyonga vizuri huku akiguna ndani kwa ndani,akamshika Ahmed vizuri kiuno ambapo kwa sekunde kadhaa akafika kileleni na hapohapo Ahmed,akamwaga risasi zake kisha kutulia juu ya kifua cha Veronica,wote wakawa wanahema kwa mbali.
“Pole mpenzi”
Veronica,akawa wa kwanza kuvunja ukimya!Akaangalia pembeni akiwa mwenye aibu fulani.
“Nawewe pole”
“Nishapoa”
Kufuatia hapo Veronica akasimama na kuvuta taulo,akalifunga kifuani!Hapo ndipo Ahmed,akapata kuliona vizuri umbo la bosi wake,lilikuwa umbo matata ambalo halikuchosha kulitizama,Veronica alibinuka kwa nyuma kidogo,makalio yake yakafanana na muinuko wa kichuguu,miguu yake ilikuwa minene na mapaja meupe ambayo hayakuwa na michirizi yoyote ile isitoshe alikuwa na rangi moja,tofauti na wanawake wengine wanaotumia karolaiti huku wanakuwa weusi kule weupe kama Pundamilia!Mwendo wa Veronica ulikuwa wa madaha mpaka alipolifikia friji na kutoa chupa kubwa iliyoandikwa kwa pembeni DOMPO,akabeba glasi mbili akafungua na opena maalum,kisha kumimina akamfuata Ahmed na kumpa glasi moja wapo!
“Karibu baby”
“Ahsante mpenzi,ulikuwa umeiweka humu kwenye friji?”
“No,nilivyoenda kupaki gari niliwapigia simu waniwekee”
“Kumbe ulijipanga?”
“Maandalizi ni muhimu siku zote na huwa sipendi kufanya vitu vya kubahatisha hata kidogo”
Kila mtu akaweka glasi kinywani na kuzidi kupiga stori za hapa na pale!
“Siku ile kwanini ulinidanganya?”
“Kukudanganya kivipi?”
“Nikaja hapa,nakupigia simu hupokei?”
“Nilipata majanga”
“Majanga yapi?”
Ahmed akawaza kidogo na kujishauri kama ingekuwa sahihi kueleza ukweli ama kudanganya,akabaki njia panda asijue ajiteteee vipi.
“Au mwenzangu,alikubania kutoka?”
Jibu hilo likawa afadhali kwa Ahmed,akaunga humohumo!
“Hahahahaha”
Ahmed akatabasamu na kukaa vizuri kitako,akavuta shuka na kujifunika!
“Siku ile unapiga simu, nilikua bafuni naoga”
“Enheeee”
“Hapo nimeshampiga fix naenda kwa washkaji!Sasa ulichoharibu ukatuma meseji ile upo Pikolo hotel!Kitimu timu kikaanza”
“Pole sana,mimi sikujua sasa”
“Subiri nimalize,alichofanya akafunga na ufunguo akauweka mfukoni!Kilichofuata hapo,Mungu anajua”
Veronica alitabasamu lakini dhahiri alionekana kuweka wivu kiasi, moyo ulimuuma lakini akajifanya kutoa pole ya kinafki,akashusha pumzi na kumtizama Ahmed kwa makini akaipiga jicho karoti ambapo muda huo ilikuwa kwa mbaaali,inaanza kusimama!
“Leo umemdanganya nini?”
“Alafu,sijakwambia!Yuko hospitali sasa hivi,amejifungua”
Ahmed,akafunguka kila kitu kwenye maisha alijifunza kitu kingine kuwa mkweli na muwazi kwenye mahusiano ili likitokea la kutokea awe upande salama!
“Hongera,nina uhakika nitapata nafasi nzuri ya kuenjoy nawewe”
“Kwanini?”
“Unafikiri uta sex naye?Mpaka miezi sita ama saba ipite kwa maana hiyo,mimi nitakuwa mlinzi wake,ole wako utuchiti nitaua mtu”
“Acha vituko”
“Alafu kitu kingine,ukitoka hapo hakikisha kabla hujamshika mwanao,oga na utakate”
“Kwanini?”
“Ndio hivyo nakwambia,hairuhusiwi kwa mwanaume aliyetoka kuchepuka aende direct kumshika mtoto wake,utambemenda shauri yako”
“Weee mambo hayo ya Kiswahili umeyajulia wapi?”
“Hiyo ni reality,wala sikudanganyi”
“Imani tu hizo”
“Nipo siriazi,kwahiyo leo tutalala hapa?”
“Mmmh,kesho kazini”
“Mimi ni bosi wako lakini”
“Kwahiyo unataka unipe likizo ya mapenzi au?”
“Ndio lakini andika barua”
Kufuatia hapo wote wakacheka,wakanywa wine kisha kuingia bafuni ambapo huko hekaheka na kukurukakara ilianza upya na kilichosikika huko ilikuwa ni miguno ya Veronica,akilalamika kwa raha anazopata!

******
Mapenzi ya Veronica na Ahmed yaliendelea kwa siri kubwa sana,hakuna hata mmoja kati ya mfanyakazi yoyote Yule aliyehisi jambo hilo kwani walifanya kazi kwa weledi mkubwa na heshima juu,kila mtu akilinda na kuificha siri hiyo ingawa mara kwa mara walipigana mabusu ofisini na kutekenyana wakiwa wawili tu kisha baadaye jioni kukutana hotelini wakila raha za dunia!Penzi kwa Hajrath lilikuwa palepale ili kumpumbaza zaidi, aliongeza upendo mara mia yake!Wiki moja baadaye,Hajrath aliruhusiwa kutoka hospitalini,lakini kutokana na wazazi wake kukaa na kujadili wakaona ingekuwa hatari sana kukaa nyumbani peke yake kwani hawakua na mfanyakazi yoyote Yule nyumbani,uamuzi uliotoka ni kwamba Hajrath akakae nyumbani kwa wazazi wake kwa muda wa miezi miwili!Kwa mara ya kwanza Ahmed aligoma na kukataa lakini wazee walimsihisi na kumuomba wakitumia hoja kwamba kuna mila na deturi za ukoo, zinatakiwa zifuatwe!
“Lakini,itachukua muda gani kurudi nyumbani?”
Ahmed akauliza,haikumuingia akilini hata kidogo!
“Mwezi mmoja”
“Mwezi mmoja?Mbona atakaa sana?”
“Usijali,kuna taratibu pia za mila inabidi afanyiwe”
“Kila kitu kipo sawa lakini?”
“Usijali”
Ni mazungumzo kati ya Ahmed na Mjomba wake Hajrath,aliyefahamika kwa jina la Abdallah Miraji,rika lake na Ahmed lilikuwa sawa ndiyo maana Ahmed akazungumza naye bila uwoga,baada ya kuachana na Ahmed akatafakari kidogo kwa muda kisha kushusha pumzi ndefu, kabla ya kumtafuta Veronica na kumuomba siku inayofuata walale mpaka asubuhi!
“Mpaka asubuhi?”
Veronica akauliza kama mtu asiyeamini.
“Ndio Baby”
“Siamini,aya ngoja nitengeneze mazingira nitakujibu kesho ofisini”
Kwa Ahmed asingeweza kuvumilia mpaka mwezi upite ndiyo akutane na Hajrath kwa maana nyingine asifanye tendo la ndoa jambo hilo aliamini angeshindwa kabisa!
“Bado kijana mimi alafu mbichiii,nikae mwezi bila kunginja na kudinyana….Haitowezekana mimi sio Padri”
Ahmed akazungumza kisha kuingia chumbani kwake,huko alipitiwa na usingizi mzito sana!

*****
Bahati nzuri ilikuwa kwao,siku hiyo ilikuwa Ijumaa kumaanisha siku inayofuata ni Jumamosi,kumaanisha kwamba wangepata muda mzuri wa kupumzika na kutoa ‘stress’ Veronica alifurahi sana kumpata Ahmed kwani alijua kumkuna vizuri hata hivyo Ahmed alikuwa ni mwanamme mcheshi na muongeaji kila wakati,jambo hilo lilimfanya Veronica atambe na kujiona mwenye furaha,habari za mume wake hakua nazo tena japokuwa aliwasiliana naye mara kwa mara simuni!Siku hiyo usiku ilikuwa ni lazima watoke kwenda kujivinjari kwenye hoteli moja yenye hadhi inayoitwa Golden Tulip iliyopo Masaki!Jioni muda wa kutoka ofisini, Veronica alimuita Ahmed kwake ili ampe mikakati yote jinsi watakavyo kula kuku kwa mrija katika hoteli hiyo iliyokuwa na kila sifa ya binadamu mwenye pesa kupumzika na kutoa mawazo!
“Leo utakuja kwangu”
“Mimii?!Nije kwako?”
“Ndio,unaogopa nini kwani?”
“Kwanini nisiogope,wewe mke wa mtu ujue!Sitaki kufa kinywa wazi hapa nilipo kwenyewe naishi kwa mashaka alafu nije kwako”
“Hauwezi,mimi nipo hakuna mtu yoyote leo”
“Veronica,mimi sitaki matatizo ujue!Mimi naelewa uchungu wa mke”
“Acha uoga,mimi ndiye nayetakiwa kuogopa sio wewe”
Veronica alizungumza kwa kujiamini mno!Akimuhakikishia Ahmed usalama wake,akamtoa wasiwasi kabisa akimuhaidi kwamba mumewe hakuwepo yupo safarini!
“Unaishi wapi?”
“Mbezi mwisho”
“Sasa sipajui”
“Nitakuelekeza baby,usiwe na wasiwasi kabisa”
Ahmed akatafakari kwa sekunde kadhaa,katika hali ya kushangaza Veronica akamvaa mdomoni na kuanza kumla denda kwa fujo,Ahmed akamtoa kidogo!
“Tuko ofisini Vero”
“Kama nina hamu je?”
“Sio mahala pake hapa”
“Mmmmh”
Veronica akaguna huku akipeleka mkono wake kwenye mkongojo wa Ahmed!
“Vero tulia bwanaa”
Akaweka msimamo kidogo na kuutoa mkono wa Veronica,hakutaka kupoteza muda zaidi ya kuaga na kuondoka zake huku kichwani kwake akiwa na mihadi ya kwenda Mbezi beach usiku huo!

*****
“Hizi hapa picha”
“Sioni vizuri”
“Hapa ilikuwa usiku,nilishindwa kuwapiga vizuri!Kulikua na giza,ilikuwa kidogo wanione hata hivyo niliweza kufanikisha zoezi”
“Umefanya vizuri,walikuona?”
“Hapana,lakini ilikuwa kidogo mkeo anione nikawahi kuondoka fasta nikasepa”
“Ilikuwa wapi?”
“Samaki samaki Mlimani city”
Mazungumzo hayo yalifanyika ndani ya ofisi ndogo lakini yenye vitu vya samani,kulikuwa na hewa ya kiyoyozi kali, kando kulikuwa na friji dogo,pembeni kushoto kulikuwa na masofa mawili!Ilikuwa ni ofisi ndogo lakini nzuri kwa kuitizama,meza kubwa ilikuwa na kompyuta mbili,pembeni kuna printa!Nyuma ya kiti kikubwa cha kuzunguka alikaa mzee mrefu,mwenye mvi moja moja kichwani!Uso wake ulionekana wa kinyama baada ya kutizama picha iliyomuonesha Mkewe Veronica,akiwa na kijana mmoja wameshikana viuno na nyingine akamuona wanapigana madenda kimahaba,kitu hiko kilimfanya akunje sura yake ilikuwa ni dharau kubwa mno,macho yake yakawa makubwa huku akitetemeka kwa hasira akavuta droo na kutoa bastola aina ya Revolver A46,akaiweka mezani.
“Cheza na mali zangu,pesa zangu lakini sio Mke wangu!Nitaua mtuu”
Mzee akapiga meza kwa hasira na kusimama,akabeba bastola na kutoka nje tayari kwa kwenda kuua!

*****
Saa 2;30 usiku,baada ya kutoka kutuma pesa Tigo pesa kwenda kwa Hajrath ambayo ingetumika kwa ajili ya matumizi ya mtoto,akaingia ndani ya gari ili aelekee Mbezi,kuonana na Veronica walale usiku huo mpaka asubuhi!Hata hivyo usiku huo alipigiwa simu sana na Benjamin Ngowi,akimtaka waonane kwani ana mambo mengi wangependa waongee,Ahmed hakuwa tayari ikambidi amdanganye ili Benjamin Ngowi,asiendelee kumsumbua!
“Nipo nje ya mji,huku Bagamoyo kaka”
Ahmed alijibu simuni,alidanganya ili amfanye Benjamin aghaili.
“Utarudi leo?”
“Hapana,kesho nadhani”
“Poa,ukirudi nambie!I hope ni kwema huko”
“Ni kwema kabisa”
Ahmed akakata simu,maelezo ya Veronica yakamjia kichwani!Kwamba akifika Mbezi mwisho,asonge mbele baada ya kituo cha polisi akunje kulia.Haikuwa sehemu ya kupoteza ndiyo maana alivyofika Mbezi Mwisho,akapunguza mwendo na kukunja kulia ambapo hapo aliona miti ya mikorosho,akapiga simu ili apewe maelekezo ya kina!
“Umefika kwenye mikorosho?”
Upande wa pili wa simu,ulisikika Veronica aliuliza!
“Ndio”
“Sasa usikate simu nyoosha,moja kwa moja!Mkono wako wa kulia geti la kwanza kushoto hapohapo!Sio mbali na hapo”
Akasogeza gari karibu na kukunja kona,akaona geti kubwa na refu lenye rangi nyeusi!
“Nimefika”
“Okay,subiri”
Akiwa katika harakati za kumsubiri Veronica,akaona geti linajisogeza lenyewe kwa mara ya kwanza alidhani ni mlinzi lakini baadaye akagundua ni geti la umeme lenye matairi kwa chini,mbele yake akaona jumba kubwa la kifahari ambapo nje kulikuwa na magari matatu,mawili aliyajua sababu alishawahi kumuona nayo Veronica lakini moja aina ya Marcedez Benz,ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kuliona,bila shaka Mme wa Veronica alikuwa tajiri!Akaingiza gari ndani,kabla ya kuliweka vizuri akamuona Veronica ametoka akiwa na dera zito,bado alikuwa na wasiwasi wa kushuka ndani ya gari.
“Ahmed karibu,mbona una wasiwasi?”
“Tunaondoka sasa hivi au?”
“Karibu kwanza ndani”
“Mimi naogopa,kavae nakusubiri”
“Ingia kidogo bwanaa”
Ahmed hakuweza kupinga tena hoja hiyo,akatembea taratibu kisha wote kuingia ndani!Kulikua na ukimya mkubwa ndani ya seble hiyo ya kisasa iliyokuwa pana mno,televisheni kubwa mithili ya ukuta!Ahmed hakua ana uhakika kama alishawahi kuona tv yenye ukubwa wa namna hiyo!Seble ilirembwa na kilichomfurahisha zaidi ni kwelamu la kioo ndani lilikuwa na samaki wanapita pita huku na kule!Akiwa katikati ya mduwao,Veronica akafika na kumkalia juu ya mapaja.
“Unaona sa…..”
Ahmed hakuweza kumaliza sentensi yake baada ya mdomo wake kumezwa akabaki anamumunya maneno, mithili ya mtoto mdogo anayejifunza kuongea!
“Unaongea sana baby,punguza mdomo”
Veronica akazungumza kimahaba na kusimama,akaliendea friji na kutoa chupa kubwa ya pombe!Akatembea mpaka jikoni,hapo ndipo alipopigwa na butwaa na kuganda kama barafu baada ya kusikia mlango wa seblen unafunguliwa kitemi,Ahmed alikuwa seblen anatetemeka kwa hofu jasho linamtoka,mlango ukafunguliwa mtu aliyemuona mbele yake alimuogopesha na kumfanya atetemeke kwa uwoga akahisi kama mapigo yake ya moyo yanadundia mgongoni!



Moyo wake ulikosa utulivu kabisa,akahisi kama unataka kutokeza nje ya kifua!Lilikuwa ni fumanizi la waziwazi,alihisi kujuta ni kwanini alikubali!Ni bora angeshikilia msimamo wake uleule lakini kutokana na kushawishiwa na Veronica akajikuta amekubali mwenyewe matokeo yake,akajikuta yupo katika wakati mgumu mno!Hakuelewa ni kwa njia gani angejitetea!Bado aliganda huku akimshuhudia msichana mdogo wa makamo akimaliza kufunga mlango,akabaki ameganda kama sanamu!Kutokana na giza lililokuwa mlangoni hakuweza kumuona vizuri msichana huyo,mpaka aliposogea karibu!Akajikuta amepigwa na butwaa,hakuwa ana uhakika kama alikua ndotoni ama anachokiona mbele yake ni mzimu!Taswira ya msitu unaoutisha,alioufananisha na Jehanam ukajijenga kichwani kwake,bado kumbukumbu zake zisingeweza kumsahau msichana huyo Ruth!Hakika aliamini milima haikutani lakini binadamu wanakutana,japokuwa hakuwa mwenye uhakika wa asilimia zote mia moja kama msichana aliyesimama mbele yake ni Ruth lakini hilo aliliamini,haikuwezekana hata kidogo binadamu wafanane namna hiyo.Ingawa Ruth hakuwa kama yule,safari hii mashavu yake yalikuwa manene kiasi mwili wake umeongezeka,ukawa na nyama!
“Mungu wangu!”
Ruth ndiye alikuwa wa kwanza kushangaa,jinsi alivyoshtuka iliogopesha ikapelekea mpaka kuweka mikono yake mdomoni!
“Ruth”
Ahmed akaita!
“Ndio mimi,siamini bado”
Ruth nayeye akazungumza,akiwa bado ameduwaa haamini anachokiona!Hata yeye alikumbuka vitu vingi, kipindi wapo katika msitu wa kutisha,Ahmed alivyomkomboa hakuna mtu hata mmoja kati yao aliyeamini kama mwenzake angekuwa hai kwa kipindi hiko!Ruth hakuweza kujizuia,akajikuta anabubujikwa na machozi akamsogelea Ahmed kwa kasi wote wakakumbatiana wakiwa wamesimama,hiyo ilimfanya Veronica ashtuke na kupigwa na bumbuazi baada ya kuona tukio hilo la ajabu mbele ya macho yake,maswali mengi yaliyokosa majibu yalipita kichwani kwake!Akadhani wenda Ahmed na Ruth ni wapenzi,swali hilo likabaki kuwa kitendawili mpaka alipowashtua!
“Ruth,umekuja saa ngapi?”
Hapo ndipo msichana huyu akitumia kiganja chake cha mikono,akajifuta machozi huku akimtizama Veronica!
“Nilikuja muda mrefu Anti,nilikuwa swimming kule nimekaa”
“Mbona hukuniambia?”
“Nilikupigia lakini simu yako haikuwa hewani”
“Ulikuja saa ngapi?”
“Jioni”
“Sasa,ulipitia wapi?”
“Mchana nilimkuta dada,akanifungulia lakini ndio naondoka hivyo”
Majibu ya Ruth hayakumridhisha alitaka kupewa historia akiambiwa kiundani zaidi wamejuana vipi na Ahmed,ndiyo maana akamtizama Ahmed na kumrudia Ruth bila kuzunguka wala kupindisha swali, akauliza!
“Ulimjulia wapi Ahmed?”
“Ni hadithi ndefu sana Anti,lakini nilikutana naye kule nilipotekwa”
Jambo hilo lilimfanya Veronica,amtizame Ahmed kwa mara nyingine kwani hadithi hiyo ilikuwa ngeni ni kweli alijua fika kwamba Ruth alitekwa lakini hata siku moja,hakusikia kuwa Ahmed nayeye alitekwa!Ilikuwaje?Kwanini atekwe?Ni maswali ambayo yalipita kichwani mwa Veronica hata hivyo hakutaka kulifanya jambo hilo liwe topiki kubwa sababu alielewa usiku huo angekuwa na Ahmed mpaka asubuhi.
“Mlikuwa wote huko?”
“Ndio,hajawai kukwambia?!Alinisaidia kabla makomand….”
“Poleni sana”
Veronica hakutaka stori ziwe ndefu ndiyo maana akamkatisha ili kuokoa muda,alichokifanya ni kuingia chumbani!Akiwaacha Ruth na Ahmed wakiwa hawaamini,wakabadilishana namba sababu kila mtu alikuwa na kiu ya kumuhadithia mwenzake mambo aliyopitia,hakika lilikuwa ni jambo la kushukuru Mungu!Dakika tano baadaye Veronica,akatoka chumbani akiwa amejiandaa vizuri mkoba kauweka kwapani,wakatoka nje!
“Nitakuacha Mwenge pale”
“Hakuna shida anti nitachukua taxi”
“Utamsalimia sana Baba ako,mwambie asinitupe hivyo”
“Nitamwambia”
Ndani ya gari,kukawa na ukimya wa ajabu!Ruth alitafakari vitu chungu mzima,katika kuwaza kwake akatamani kuuliza Ahmed na anti yake wana uhusiano gani kwani ulikuwa ni usiku mno!Maswali mengi yalikosa majibu yakaunyanyasa moyo wake licha ya hiyo hakutaka kulivalia kibwaya jambo hilo,alivyofika Mwenge akateremka na kuwaaga!Huku nyuma akimuacha Veronica anamtizama mpaka alivyoishia kwenye moja ya kona!
“Mlikutana wapi?”
Veronica,akauliza swali huku akikunja kona ya kuingia barabarani!
“Mimi mwenyewe siamini kama yupo hai mpaka leo,Vero!Mungu ni mkubwa sana,huyo Ruth nilikutana naye huko sijui wapi!Tulitekwa”
“Ndio najua alitekwa,baba yake waziri Mkuu sasa hivi!Baba yake huyo mtoto mimi kaka yangu!Kuna kipindi alipotea,ndio mlikuwa wote huko?”
“Tulikua wote ndio”
“Nawewe ulitekwa?”
Ahmed kabla ya kujibu,akashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani!Hakutaka kukumbuka mateso na unyama uliotokea katika msitu wa kutisha,akamtizama Veronica na kukaa kimya!
“Tunaelekea wapi?”
“Golden Tulip”
“Ndio wapi?”
“Masaki”
Safari ikazidi kusonga,ndani ya gari kukawa na mziki wa taratibu wa mapenzi ulioanza kuamsha hisia zao kwa mbali.Kila mtu akatamani kufika haraka wawe sita kwa sita,Kwa mwendo wa taratibu wa dakika ishirini walikuwa tayari wamefika Msasani kituo kinachoitwa Macho!Hapo wakakunja kulia na baada ya muda mfupi wakatokea fukwe za Koko,wakakunja kushoto na kunyoosha barabara, ambapo baada ya muda mfupi walikuwa nje ya geti kubwa la kisasa ambapo ndani kulikuwa na gorofa zuri la kuvutia,Veronica alionekana kuwa mwenyeji wa eneo hilo ndiyo maana moja kwa moja akapitiliza upande wa kushoto kwenye maegesho ya magari!Akapaki vizuri wakashuka!
“Sasa gari yangu ujue,nimeacha nyumbani kwako!Itakuaje?”
“Utaondoka na langu,nitakuletea ofisini gari yako Jumatatu”
“Unadhani ofisini watatufikiria vipi?”
“Achana nao,hilo niachie mimi”
“Nawewe utaondoka na usafiri gani sasa?”
“Usijali kuhusu mimi,lakini mambo hayo tuongelee kesho baby”
Mbali na uzuri wake uliobebwa na weupe lakini Veronica alijua kujilegeza,hakuwa na macho makubwa lakini aliweza kuyatumia kimahaba kwani aliyalegeza kwa kiasi cha kutosha hiyo ikamfanya Ahmed azidi kupagawa zaidi,walivyoshuka wakatembea taratibu ambapo walishuka ngazi tatu!Kushoto kulikuwa na uwazi mkubwa,jiko la kisasa ndani yake kulikuwa na watu maalum wa kuchoma nyama,kandokando kulikua na kaunta iliyosheheni vinywaji vya kila aina,Ahmed akatokwa na udenda mithili ya fisi aliyeona mzoga wa nyama!
“Utakula nini?”
Veronica,akageuka na kuuliza!Mbaya zaidi alimsogelea karibu kabisa na mdomo akitaka kuwaonesha wahudumu wa kike kwamba Ahmed alikuwa mpenzi wake hivyo wasimkodolee macho!
“Chochote tu”
“Mmmh baby,sema bwana!Hapa kuna kila kitu”
“Nitakula nyama choma”
“Vinywaji?”
“Wine kama ya siku ile”
“Aya”
Kuanzia hapo Veronica akawa bize jikoni kuwapa maagizo wapishi akasogea kaunta na kutoa maagizo pia kisha baada ya hapo wakaelekea upande wa kushoto!Mandhari ya eneo hilo ilikuwa nzuri,kushoto kulikuwa na bwawa la kuogelea,upande wa kulia kuna bahari iliyotenganishwa na kingo ngumu,vikiambatana na viti vya kupendeza mno!
“Hapa wapi?Haki ya Mungu,sikua najua kama Dar kuna maeneo kama haya,kumbe watu wanakula maisha,aisee”
Ahmed akavunja ukimya,hakika siku hiyo aliosha macho sio mchezo!Kila kitu kwake kikawa kigeni.
“Hapa ni Masaki Golden Tulip”
“Umepajuaje?”
“Acha wivu baby,kuna kipindi nilikuwa napenda kufanya kikao mule ndani.Kuna conference room”
“Huyu jamaa kajipanga”
“Mbona kuna sehemu nyingi mpenzi,kuna hapo mbele Coral beach!Wanapaita The beach club”
Veronica,jinsi alivyoongea ilikuwa dhahiri kabisa ni mtu wa viwanja na matawi ya juu!Walivyomaliza kutembea wakaelekea mapokezi kutafuta chumba,ambapo huko walipata na kupewa kadi maalum ya umeme!Ilikuwa ni hoteli iliyotulia.Kiyoyozi chenye ubaridi wa wastani kinachotoa hewa safi kilipuliza,wakafika mpaka chumba walichopewa,wakafungua mlango!Mbele yao,walitizamana na kitanda kikubwa mno,ambapo pembeni kulikua na safu mbili ya masofa,tv pana!
“Pazuri sana”
Ahmed akatoa sifa,katika maisha yake alikiri mwenyewe kwamba siku hiyo kila kitu kwake kilikuwa kigeni,katika kutafakari akashtukia ameshikwa kiuno na kuvutwa karibu,hakukaa sawa akadakwa mdomoni ulimi wa Veronica ukapita kinywani mwake,wakaanza kulana denda na kilichosikika hapo ilikua ni miguno mithili ya mtoto mdogo anayenyonya kidole gumba!Damu ya kila mtu ilienda mbio,wakiwa bado na nguo tena wamesimama walizidi kupapasana huku midomo yao ikiwa bado imegandana!Mgongo wa Ahmed upo ukutani Veronica yupo mbele yake,Ahmed akapapasa mkono wake mpaka nyuma,akabinya kidogo makalio ya Veronica,taratibu akaanza kuingiza mkono ndani ambapo huko alikumbana na mgongo laini sana,akashusha mkono mpaka kwenye makalio,sasa akawa anayashika vizuri huku akiyabinya taratibu mithili ya mtu anayechagua embe gengeni,aste aste wakaanza kuvuana nguo mpaka walipomaliza, wakatupana kitandani,Ahmed chini Veronica juu alichokifanya ni kukamata maiki na kuanza kuimba nayo taratibu mdomoni,alivyoitoa akapanda juu na kuanza kuendesha farasi ambapo kiuno chake kilikuwa kinapanda juu na kushuka huku akikinyonga kwa ufundi wa hali ya juu,hiyo ilimfanya Ahmed azidiwe nguvu,akamshika vizuri kiuno ili amthibiti lakini alikuwa kama amempandisha mashetani,Veronica alizungusha kiuno sio mchezo!Hiyo ilimfanya Ahmed nayeye ashughulike ili asitoe boko katika mchezo huo wa kukata na shoka,hazikupita sekunde mbili Veronica akapiga magoti na kushika kingo ya kitanda,Ahmed akafika nyuma yake na kuanza kupeleka majeshi!Ambapo baada ya hapo Veronica akalalia tumbo,Ahmed akawa juu yake,hakika ilikuwa ni mechi ya kipekee!Ndani ya dakika kadhaa,kila mtu akawa hoi ingawa hawakuwa na uhakika kama wangeendelea ama wangelala!
“Ahmed,Mkeo anafaidi sana!Natamani kuwa yeye?”
“Kwanini?”
“Sio kwa ufundi huo”
“Hapana,chakula ni kile kile tofauti ni mapishi”
“Hata kama lakini mapishi yako wewe kiboko,kama chumvi ipo mahala pake,umekatia nyanya vizuri!Kifupi,unaweza kupika vizuri mtu akala na kufurahi”
“Wewe ndio unasema mlaji”
“Kwani wewe hujijui?”
“Wala”
“Acha zako,mkeo hakwambii kwani?”
“Hajawahi kuniambia”
“Toa uongo,anakwambia sana!Lakini mimi nina wivu baby,nina wivu sana”
“Punguza,utakufa na presha”
“Naanzaje kupunguza sasa?”
“Jitahidi basi”
“Ngoja nipige simu jikoni kama tayari,naona ushanitia njaa mwanaume wewe”

******
Japokuwa alikuwa nyumbani akilea mtoto lakini moyo wake ulikuwa kwa Ahmed,alihisi kuna kitu kimepungua kikubwa sana katika maisha yake nayo ni uwepo wa kipenzi chake Ahmed!Alitamani angekuwa pembeni yake ili angalau amshike mtoto usiku wacheze wote na kupiga stori lakini hilo lilikuwa ni gumu kwa kipindi hiko akawa kama mkiwa!Hata hivyo aliwasihii wazazi wake kwamba anataka kurudi kwake kwani angekuwa huru kama angepata ukaribu na mumewe!
“Mwanangu,mimi nawajua wanaume!Ukikaa naye sana,hatoweza kukuoa mapema!”
Mama Hajrath siku hiyo akafunguka baada ya Hajrath kulalamika kwa muda mrefu!
“Kama ananipenda atanioa mama alafu ndio muda mzuri wa sisi kugundua madhaifu yetu,tukikaa hivi mbalimbali itakuwa ngumu kujuana”
“Ni kweli mwanangu hata hivo pale nyumbani nani atakuangalia?”
“Mpaka hapa nilipofikia ninaweza mwenyewe mama usijali,tutatafuta hata dada wa kutusaidia”
“Mimi sina neno,nitaongea na baba yako!Si unajua mila zetu,asikawie sana basi akupose”
“Hilo ondoa shaka kabisa Mama”
Siku hiyo usiku Hajrath alikuwa na hamu kubwa ya kuzungumza na Ahmed simuni ampashe habari nzuri kisha wazungumze na kupanga mikakati ya kumpa jina mtoto,lakini matokeo yake alivyopiga simu iliita bila kupokelewa!Akapiga tena na tena,lakini hakukuwa na majibu yoyote yale!
Simu ya Ahmed iliita akiwa juu ya kiuno cha Veronica,amemkunja vizuri kitandani miguu yote miwili kaishika, yeye yupo katikati ananyonga kiuno chake huku mara kadhaa wakipigana madenda,hakua na habari kwamba simu yake inaita wakati huo alihisi yupo angani anapaa bila mabawa!Veronica alikuwa mtamu kwake,kilichomfanya apate stimu zaidi ni baada ya kushiba na kupata glasi tatu za wine!Jasho jembamba lilimtoka,akamvuta Veronica vizuri na kumlaza kiupande upande,kisha yeye akapita mgongoni kwake,mechi ikaendelea kama kawaida!
“Aasshsss aaasshsss yesss aashss aaahsss sssshh”
Veronica alitoa miguno ya kila aina ili mradi raha tupu,alivyohisi anafika akanyonga kiuno na kuomba denda huku akitetemeka hiyo ilimfanya Ahmed akoki bastola yake vizuri sekunde moja baadaye akamwaga risasi wote wakatulia tuli.Kilichowashtua ilikuwa ni simu iliyokuwa karibu na meza,Veronica akapapasa mkono na kuishika alivyoona jina ‘WIFE’ akaingiwa na wivu ingawa hakutaka kupokea,akampa Ahmed!
“Nyamaza usiongee kitu”
Ahmed akatoa onyo kali,akapokea simu na kuweka sikioni!
“Baby ulikuwa wapi?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka upande wa pili wa simu.
“Nimelala mpenzi,hapa nimeshtuka kwenda chooni ndio naona simu yako inaita”
“Nitanuna ujue”
Hajrath akazungumza kwa sauti ya kudeka.
“Usinune mke wangu,nimekumisi.Unarudi lini?”
“Wee si utaki kuja kutuona?”
“Sio hivyo,huko ni kwa wakwe ujue!Kuja huko,inabidi nijipange”
“Usiogope,baby nitakuja huko next week nadhani!Naomba uje kunichukua”
“Lini mke wangu?”
“Nadhani kuanzia Jumatatu,nitakupa jibu Kesho asubuhi”
“Nitafurahi kukuona,nimekumisi sana!Nimechoka kulala mwenyewe kitanda kikubwa”
“Usijali,nitakuja”
Wakati mazungumzo ya Ahmed na Hajrath yanaendelea simuni,Veronica alikuwa pembeni!Anaangalia kwa macho yaliyojaa wivu,alichokifanya ni kusimama kutoka kitandani mpaka kwenye glasi ya wine akanywa na moja kumkabidhi Ahmed,ambapo tayari alikuwa amekata simu!
“Naona mwenye nyumba anarudi”
“Ndio”
“Tutapata kweli nafasi?”
“Kwanini tusipate?Kama kawaida”
Stimu ziliwapanda baada ya kupata kileo,wakaingia tena ndani ya kitanda sita kwa sita na kuanza kukunjana huku na kule,ilikuwa ni mechi ya aina yake na mpaka ilivyofika saa tisa za usiku kila mtu alikuwa hoi,amegeukia upande wake!

*****
Kitu alichokifanya Ahmed ni kununua kila mahitaji ya mtoto,kama baba ilibidi afanye hivyo,vitu kama nepi,sabuni,beseni la kuogea na pampas!Alijaza ndani ya gari lake jioni ya siku hiyo alivyorejea kutoka kazini,badala ya kwenda kwake akapitiliza moja kwa moja kwa wazazi wa Hajrath,bahati nzuri ikawa kwake na ndio jambo alilokuwa analiomba kila saa kwamba asiwakute wazazi wa Hajrath,hata hivyo kitendo cha kufika hawakukaa sana,Hajrath na mtoto wakaingia ndani ya gari!
“Punguza ac ni kali”
Alichokifanya Ahmed ni kupunguza makali ya kiyoyozi kisha kumgeukia Hajrath!
“Mtoto anaitwa nani?”
“Bado sijampa jina”
“Kwanini sasa?”
“Nilikuwa nakusubiri wewe Dad”
“Nalipenda sana jina la Babrah”
“Babrah?”
“Yes Babrah”
“Jina zuri,umelitoa wapi?”
“Juzi nilikuwa na google majina nikalipenda,limekaaje?”
“Limekaa bomba”
“Sawa Mama Babrah”
Hajrath akatabasamu na kumpiga Ahmed kingumi fulani cha mahaba begani,safari ikaanza hapohapo!Walipofika tu,kazi ilikuwa ni kushusha mizigo ya mtoto Babrah ambaye kwa wakati huo alikuwa tayari amelala,hakuwa mtoto msumbufu anayelialia hovyo!Wote wakaingia chumbani na kukaa kitandani,ambapo walianza kuongea na kupanga mikakati ya maisha,kilichowakatisha ilikuwa ni simu ya Ahmed,mbaya zaidi ilikua kitandani!Ahmed,alivyopiga jicho akaipotezea kwani juu ilitokea namba ya simu peke yake,namba hiyo aliifahamu ilikuwa ya Veronica alidiliti jina makusudi ili tukio kama hilo likitokea ajitetee!
“Si upokee simu baby!”
Hajrath akasema baada ya kumuona Ahmed,anasua sua!Hiyo ilimfanya Ahmed,apate kitete akaitizama simu mpaka ikakata,ikaanza kuita kwa mara nyingine!
“Huyu jamaa ni msumbufu sana,tuachane naye!Tufanye yetu mke wangu,nyumbani hawajambo?”
Sura ya Hajrath ilibadilika ghafla,akamtizama Ahmed kisha akatabasamu kiupande kwa dharau!
“Ahmed,hiyo namba usidhani siijui!Huyo ni Veronica,Malaya wako!Pokea simu weka loudspika la sivyo nitapokea mimi”
Hajrath alizungumza kwa sauti ya chini lakini kavu,iliyojawa na hasira pamoja na wivu!



*****
“Anyway,shauri yako!Utajua mwenyewe”
“Baby”
“Nini?Nimekwambia utajua mwenyewe,kumbuka una mtoto mdogo!Bado tunakuhitaji”
Ilikuwa ni hali ya kushangaza kwa Hajrath kuwa mpole ghafla,hakutaka kuongeza neno lingine zaidi ya kutabasamu na kumwangalia Ahmed kwa macho fulani hivi yasiyo ya kawaida,akatoka kitandani na kutembea mpaka seblen!Hapo ndipo Ahmed akapata mwanya wa kupokea simu hiyo kwa haraka!
“Usipige subiri Vero,utaharibu”
“Poa,usiku mwema nakupenda”
Ahmed alizungumza kwa wasiwasi mkubwa, macho yake yote yakiwa mlangoni anamtizama Hajrath kama angerejea,baada ya kukata simu na kuhakikisha amesawazisha mambo akatoka na kuelekea seblen ambapo huko alimkuta Hajrath yupo kwenye kochi anaangalia sinema!
“Nikuletee juisi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Hajrath kana kwamba hakuna kitu chochote kinachoendelea!
“Hapana,baby yule sio Veronica lakini”
“Ahmed,mimi mbona nishapotezea!Wala lisikusumbue kabisa,nishasahau kwanza!Awe Veronica asiwe Veronica,shauri yako”
Ki ukweli Ahmed alikuwa katika wakati mgumu sana ni bora Hajrath angeongea ili ajue kama yameisha kuliko alivyokuwa kimya,hakujua mpango wa mwanamke huyo ni nini hasa ndiyo maana alihaha kama bata aliyekula pumba kavu!Hata walivyorudi kulala Hajrath hakuonesha chuki ya aina yoyote ile.
“Nimekumisi mpenzi”
Ahmed akasema huku akijivuta karibu kabisa na Hajrath aliyekuwa ukutani.
“Bado nina maumivu lakini”
“Hakuna shida,kama unahisi maumivu basi tulale nitavumilia”
“Lakini usijali mme wangu”
Alichokifanya Hajrath ni kumgeukia Ahmed,akamshika kidevu akatoa ulimi wake na kuutumbukiza kinywani mwa Ahmed wakaanza kubadilishana mate,hakuishia hapo mkono wake laini ukapita taratibu kwenye tumbo la Ahmed ukashuka taratibu mpaka kwenye karoti ambapo tayari ilikuwa imesimama dede,akaanza kuichua adoado alivyoona imesimama imara,akarudi kidogo chini akaishika kwa mikono miwili na kuiweka mdomoni akaanza kulamba mithili ya koni,tukio hilo lilimfanya Ahmed apandishe midadi na kulegea kabisa,karoti yake ilikuwa inateleza kama kambale kwenye tope!Utundu wa Hajrath ulimfanya afumbe macho yake,akakikamata kichwa cha Hajrath akawa kama anakipandisha juu na kukishusha ilimradi stimu,ghafla akaanza kukakamaa na kunyoosha miguu!Dalili hiyo Hajrath aliifahamu akajiandaa vizuri na kuzidisha kasi ya kulamba koni,akajichomoa na kumkumbatia Ahmed kwa nguvu,ambapo risasi ziliruka na kumfikia Hajrath kwenye kitovu!
“Pole baby”
Hajrath akasema huku akichukua kanga safi na laini ili kusafisha risasi zilizomwagika,baada ya hapo akaingia bafuni kuoga ambapo Ahmed pia alifuata!
“Natamani maumivu yapungue baby,I’m hot”
Hajrath akadeka kumaanisha kwamba nayeye ana mizuka lakini asingeweza kufanya chochote kwani alitoka kujifungua siku chache zilizopita, hiyo ilifanya bado ayahisi maumivu,hata hivyo alishauriwa na madaktari asifanye tendo hilo kwa muda!
“Honey,nataka kuanza taratibu za ndoa!Nataka kuleta posa kwenu”
Ahmed akavunja ukimya,jambo hilo likamfanya Hajrath atabasamu kidogo!
“Lini mpenzi?”
“Ngoja mambo yakae sawa,nadhani mwezi ujao”
“Nitafurahi sana,kua mke halali wa Ahmed Kajeme”
“Nafanya hivi sababu nakupenda,pia samahani kwa kila kitu!Sisi ni binad…”
“Baby,nishakusamehe!Usijali,najua unanipenda kila unachofanya najua nipo kwenye akili yako”
“Ahsante kwa kulijua hilo Mama Babrah”
“Sawa,Dadiyoo”

******
Swala la Mr.Mbogo kumtafuta mtu anayetembea na mkewe lilikuwa dogo sana na alielewa zoezi hilo lingekuwa rahisi kama angetumia akili, tena akienda taratibu mno la sivyo asingeweza kumbaini mwizi wake,hasira zilimjaa na jazba ilimpanda!Hakuelewa hata kidogo Veronica anakosa nini kwake kwani kila kitu alimpa ndani ya nyumba,akiwa njiani akaanza kufanya mkakati, moja kwa moja kwa kuwasiliana na msichana mmoja anayeitwa Jaqlin Lucian,akiamini huyo ndiye angeweza kumsaidia katika hatua yake ya awali sababu tu mkewe hutumia mtandano wa kampuni hiyo!
“Nisaidie kitu kimoja Jaqlin”
Mr.Mbogo alianza kuzungumza baada ya salamu za hapa na pale.
“Kitu gani?”
“Nakutumia namba ya mke wangu,nataka kujua kwenye simu yake anaongea na nani mara kwa mara!”
“Si unajua ni risk,hairuhusiwi vipi humuelewi nini?”
“Kuna mambo siyaelewi”
“Usinitaje lakini ujue namuheshimu sana Mkeo,akijua mimi ni…
“Usijali kuhusu hilo kuna ya maji pia hapa nitakupa”
“Lakini mmh,anyway!Tuma namba hizo”
Pesa ikawa tayari imebadilisha mawazo yake,akiwa juu ya kompyuta msichana Jaqlin akaingiza namba na kuanza kupekua huku na kule akafanikiwa kupata namba tatu ambazo mara nyingi zinawasiliana na Veronica!Akafanya kama alivyoambiwa,akarudi kwenye laini na kumpasha habari Mr.Mbogo!
“Nitumie na majina yao”
“Lakini kuna huyu mmoja,imezidi juzi usiku waliongea kwa dakika ishirini,wiki iliyopita pia!Leo mchana vile vile”
“Huyo anaitwa nani?”
“Ngoja kidogo niangalie……Ahmed Kajeme”
“Anaishi wapi?”
“Hapo itakuwa ngumu kujua,sitoweza kutresi!Mpaka utaratibu maalum kutoka polisi ama ngazi za juu,msaada wangu umeishia hapo”
“Ahsante sana,nitakutumia laki moja kwa kazi hiyo the rest nitafanya mimi”
“Nitashukuru sana”
Hatua ya kwanza ikawa tayari imekamilika jina la Ahmed Kajeme likamuingia kichwani,akawa tayari ana namba zake!Alichokifanya kwanza ni kuziandika namba hizo kwenye simu kisha kuangalia kama kwenye ‘watsApp’ ipo!Ghafla moyo wake ukakosa utulivu,mwili wake ukachemka kwa hasira baada ya kuona sura ya mwanamme mwenye ndevu kiasi zilizokuwa katika mtindo wa O,Sura hiyo haikuwahi kumtoka hata mara moja!Picha aliyooneshwa kwenye simu ya mwanaume akiwa na mkewe samaki samaki ndiyo iliyokuwa kwenye ‘WatsaApp’ sasa akawa ana uhakika Ahmed ndiye anakula tunda lake kiulaini,moyo wake ulimuuma na kutaka kumfata huko huko alipo!Akashindwa kuelewa angeanzia wapi!Kwa busara na mwendo wa taratibu akaanza kufanya uchunguzi katika biashara zote za mkewe,akapiga simu kwenye duka la nguo kumuulizia mtu huyo lakini hakupata majibu!
“Nilikuwa nina shida na nguo,hapo hakuna kijana huyo?Anayefanya kazi hapo dukani?”
“Hakuna shemeji,umesema Ahmed Kajeme?”
“Ndio”
“Sijawahi kumsikia”
“Okay”
Simu ya nne kuipiga ilienda moja kwa moja kwenye kampuni aliyoajiriwa kama bosi,ikapokelewa na msichana wa mapokezi!
“Habari,unaongea na Machupa hapa”
Bwana Mbogo,akaficha jina lake hakutaka kuweka wazi kuhofia kushtukiwa hata hivyo aliamini kwa kufanya hivyo ingekua rahisi kupata ushirikiano,ndiyo maana akabadili sauti licha ya hiyo mpaka namba akatumia nyingine!Kilichomfanya aamini kwamba asingeshtukiwa mapema simu aliyopiga ilikuwa ya mezani.
“Tukusaidie nini?”
“Kuna bwana mmoja,nimeambiwa niwasiliane naye anaitwa Ahmed Kajeme!Sijui yupo hapo?”
Mr.Mbogo akawa kama anacheza kamari la bahati na sibu,kutafuta jina hilo!
“Ahmed Kajeme yupo ndio ni shida ya kiofisi au?”
“Ndio ya kiofisi,ngoja nitakupigia baadaye”
Mr.Mbogo akapata uhakika asilimia mia moja kwamba Ahmed Kajeme anafanya kazi na mkewe ofisi moja,alichotakiwa kufanya ni kumtafuta kwa wudi na uvumba! Mchakato wa kumfuatilia na kujua anapoishi ukaanza mara moja.

*****
Kitu cha kwanza kukifanya Ahmed kwa siri kubwa ni kuanza harakati za kutafuta kiwanja,bahati nzuri ikawa kwake baada ya kukutana na mzee mmoja aliyefahamika kwa jina la Kazabuti!Akamueleza shida yake,siku iliyofuata wakafunga safari mpaka Kimara,bunyokwa!Huko ndipo mzee huyo alikuwa na hekari tisini.
“Mzee uliwezaje kupata heka zote hizi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed,kuna kitu alitaka kujifunza!
“Hakuna utajiri mkubwa kama ardhi,nina viwanja vingi sana!Kila nikipata pesa nilikuwa nanunua viwanja!Hapa Dar nina viwanja ishirini na mbili,Arusha ninavyo na Moshi,sema nilinunua miaka mingi sana iliyopita enzi za ujana wangu”
“Hongera sana”
“Hapa nilinunua miaka ya themanini,kulikuwa na kichaka kikubwa”
“Naona sasa hivi kumekua mjini”
“Kuna marafiki zangu niliwashauri wanunue,nilivyonunua waliniona mwehu napoteza pesa.Walinishangaa sana,sasa hivi wanajuta kiwanja chako hiki hapa nataka nikukatie hapa,ulisema heka moja?”
“Nataka kuongeza nimebadili mawazo,heka moja na nusu”
“Hakuna shida,nataka kukupa hapa barabarani!Hapa juu,utajenga fremu kama hutojali alafu kule chini nyumba,paking ya gari hapa pembeni yake”
“Kama tulivyoongea kwenye simu,nitakupa nusu nyingine nitamalizia”
“Mara nyingi wateja wangu hufanya hivyo”
“Tutaenda serikali za mitaa kwanza”
“Hilo la Muhimu,kuna kesho na keshokutwa siwezi kufanya biashara kama hii kubwa kiholela”
Siku zote aliyegongwa na nyoka akiguswa na jani hustuka!Swala la kutapeliwa kwa mara nyingine hakutaka litokee, ndiyo maana wakaongozana na mzee Kazabuti mpaka ofisi za Serikali za mitaa ambapo huko,waliandika makubaliano kwa njia ya karatasi kisha kupigwa muhuri,hatimaye Ahmed akafanikiwa kulipa nusu ya pesa,muamala uliobaki akahaidi atalipa miezi miwili baadaye!
“Ahsante sana Mzee wangu”
“Sawa kijana,tuzidi kuwasiliana”
Furaha aliyokuwa nayo Ahmed hakutaka kuimalizia peke yake,akamtafuta Benjamin Ngowi hewani ili ampashe habari kuhusiana na hatua aliyopiga!Hilo halikuwa tatizo saa moja ya jioni wakakutana baa moja inayofahamika kwa jina la 5N, Mwenge.Hapo ndipo walipanga wakutane maswahiba hao wa siku nyingi!
“Naona ushaanza kutoka shavu,ndugu yangu”
Ngowi,akaweka utani kidogo huku akivuta kiti na kukaa!
“Shavu wapi bwana,majukumu yameongezeka”
“Naelewa,ushakuwa baba sasa!Inabidi vitu vingine upunguze”
“Vitu gani hivyo?”
“Kama ulikuwa unakunywa bia saba kunywa tano”
Mhudumu akafika na kuagizwa vinywaji,hakuchelewa sana akaweka chupa za pombe mezani,zikafunguliwa Ngowi na Ahmed wakamimina kwenye glasi na kupiga ‘cheers’kama ishara ya kushukuru kukutana tena kwa mara nyingine!
“Kuna kitu sijakwambia Ngowi…”
“Kitu gani?”
“Nataka kuoa”
“Kuoa?!Umesema kuoa?”
“Ndio”
“Nani tena?”
“Unadhani nani?Zaidi ya Hajra”
“Mbona ghafla hivyo,si amejifungua juzi tu kwanini usisubiri mpaka mtoto akue kue kidogo,ndio mfunge ndoa”
“Naona muda unakimbia sana,muda sio rafiki tena”
“Nakubaliana nawewe,utaweza lakini?Sio umpige mtoto wa watu,maana nakujua wewe!Bondabonda”
“Nishaacha,huwezi amini Hajra sijawahi kumpiga hata mara moja,tangu niwe naye”
Ahmed hapo,alidanganya hakutaka kuonekana limbukeni.
“Ndio inavyotakiwa,siku zote uwe mtu wa kupotezea!Hakuna adhabu nzuri kwa mwanamke kama kumsumbua kisaikolojia”
“Kivipi?”
“Yule Pendo Yule,nipo naye huu mwaka wa nane!Na nilishawahi kumfumania ujue live bila chenga siku moja”
“Weee!Acha utani, ikawaje?”
“Sikumfanya chochote,nilitulia kama fala.Wala sikumpiga hata kumtukana,nikamwacha lakini moyo uliniuma ile kishenzi yaani,nikajiuliza hapa nikimpiga atajua tayari yameisha alafu nitapata kesi!Nilichokifanya nilipiga buyu,narudi home freshi.Pendo siku tatu halali usingizi usiku,siku ya nne akaondoka mwenyewe kwao,unajua kwanini?”
“Sijui”
“Alikua anajiuliza maswali mwenyewe huyu ana niya gani namimi,alikonda siku mbili ujue!Alivyokua kwao anapiga simu napokea freshi tunaongea,akachoka”
“Duuuuu kaka,una moyo mimi sasa hivi sijui ningekua wapi!Nadhani jela!Nadhani ulisikia timbwili la Yusrath”
“Sasa,ungefaidika nini kwenda jela?Baadaye kabisa,akamuhadithia dada yake!Kila kitu,wakaniita tukayaweka sawa”
“Wewe jembe,labda hauna moyo haki ya Mungu!Mimi ningeua,hapa kwenyewe bado namsaka Yusrath popote pale duniani,hata kama nikisikia amekufa nafukua mwili wake”
“Haina maana,puuzia!Ukitaka kuishi vizuri hapa duniani,kila kitu puuzia usiweke moyoni!Ukisemwa vibaya puuzia,ukitukanwa puuzia yaani take it easy”
“Nitajaribu ushauri wako,sijui lakini kama nitaweza”
Siku hiyo walikunywa pombe wakaagiza nyama choma,Ahmed alivyoanza kuhisi amelewa akajihami na kuomba kuondoka nyumbani muda huohuo!
“One for the lord broo…Angalau moja ya mwisho”
Ngowi,akapendekeza bia zikaongezwa hapo ndipo Ahmed akaanza kuita wahudumu na kuwatongoza kama kawaida yake akilewa pombe!
“Yule demuuu,ana upaja mzuriii sanaa Ngowiiii.Naondoka nayee leoleo nikampige paipuuu”
“Ahmed,malizia tusepe”
Ngowi alivyoona hivyo,akajua kivyovyote vile Ahmed angeharibu na kuunguza picha,alichokifanya ni kumuinua huku akipepesuka akamuingiza ndani ya gari.
“Kwahiyooo,unaona nitafaidi Ngowi,au unamtakaaaa wewe yule gashiii?Niache basi nishuke niende”
“Nenda kapumzike Ahmed,saa sita hiii!Una familia tayari”
“Aaaaaah,bloodfool!Okay,naendaaa homeee mimi ndio Baba Babrah one way hiyooo”
Ahmed,akapandisha kioo cha gari na safari ya kurudi kwake kuanza mara moja huku akiwa na furaha tele, hasa alivyokumbuka kwamba amenunua kiwanja,magari hayakuwa mengi usiku huo barabarani!Akanyoosha mguu,mpaka alivyofika getini kwake ambapo alishuka na kujifungulia,akaingiza gari ndani kisha kufunga geti!Hofu ilikuwa kwa Hajrath,akaanza kutunga tenzi za kujitetea endapo angeulizwa alikuwa wapi,alivyofika mlangoni alipigwa na butwaa na kushtuka huku wivu taratibu ukianza kumpanda hiyo ni baada ya kuona sandozi za kiume!
Hakuwa ana uhakika kama ni zake ama amelewa,akazitizama vizuri akajua ni lazima ndani kulikuwa na mwanaume!Akaapia kama ingekua hivyo,Hajrath asingeacha kuona kila rangi!Kwa jazba akafungua mlango kwa hasira,moyo wake ukapiga paa kwa nguvu baada ya kukutana na mwanaume mrefu amekaa kwenye sofa amekunja nne,anavuta sigara bila wasiwasi,pembeni yupo Hajrath analia kwa uchungu mbaya zaidi amevaa kanga moja tu!Sura hiyo haikuwa ngeni hata kidogo,mwanaume huyo alishawahi kumuona kwenye picha ofisini kwa Veronica,yaani mme wa Veronica!Mapigo yake ya moyo akahisi kama yameacha kudunda kwa sekunde tano,akahisi joto la ajabu!
“Karibu,Ahmed Kajeme”
Mr.Mbogo akasema huku akimtizama Ahmed kwa macho yaliyojaa unyama,akachomoa bastola yake kutoka kiunoni akaiweka mezani,jambo lililomfanya Hajrath atetemeke na kujisogeza pembeni akitumia makalio,Ahmed aliyekuwa amesimama mlangoni pombe zikamwisha, akahisi kama nguo yake ya ndani imelowana,hakuelewa ni mkojo ama jasho!




“Ahmed una mke mzuri sana,ulikosa nini kwake?”
Mr.Mbogo aliuliza swali,mguu wake akiwa amechora nne anamtizama Ahmed Kajeme jinsi anavyotetemeka!Uchungu aliokuwa nao mzee huyu,haukuelezeka kiwepesi!Moyo wake ulimuuma,mbaya zaidi alijinyima ili mkewe apate furaha alafu kiulaini Ahmed,akawa anajilia!Siku hiyo alimuomba Mungu,asije kuua ingawa hilo ndilo lilikuwa kusudio lake,ndiyo maana akaweka bastola mezani akimtizama Ahmed!
“Alafu umerudi usiku umelewa?Unatoka wapi sasa hivi?”
Mr.Mbogo akauliza kana kwamba ni mke wa Ahmed.
“Wewe ni nani?”
Ahmed,akajikakamua na kuuliza swali huku sauti yake ikionesha kabisa alikuwa mwenye wasiwasi mkubwa!
“Unataka kunijua mimi ni nani?”
“Ndio”
Hakuongeza neno lolote badala yake,akachukua simu kutoka mfukoni na kuiweka mezani akafungua upande wa picha na kumuonesha Ahmed picha aliyopigwa akiwa Samaki samaki,baada ya hapo akachukua simu na kumuwekea Hajrath pia,jambo lililofanya msichana huyo aangue yowe la kulia,alilia kwa uchungu mno,hakutaka kuamini kama Ahmed amefanya jambo hilo la usaliti.
“Dada,huyu mwanamke hapa kwenye picha ni mke wangu!Anafanya kazi ofisi moja na mumeo”
“Ana…itwa nani mke…o?”
Hajrath akauliza kwa sauti iliyojaa kwikwi,alikua ana kila sababu ya kutaka kujua jina!
“Veronica”
Jina hilo halikuwa ngeni,masikioni mwa Hajrath!Akamtizama Ahmed aliyekua bado amesimama kama mlingoti,amepigwa na butwaa hajui afanye kitu gani!Mbaya zaidi siku chache zilizopita alitoka kumkanya kuhusu Veronica,alivyotaka kujazia neno akashindwa kwikwi kali ikamshika!
“Ningekua mimi ndio wewe,ningeanza kusali sala za mwisho!Nimekuja kwa lengo moja tu,kukuua baaasi!Ushahidi ninao,tarehe kumi na saba mlilala Pikolo, last week mlikuwa Golden Tulip mkalala mpaka asubuhi”
Hakuongea kama mtu anayebashili mechi ya mpira,alikuwa ana ushahidi wote sababu alitoa risiti na baadhi ya picha zilizowaonesha Ahmed na Veronica wakiwa mapokezi,hiyo ilizidi kumfanya Ahmed awe mdogo kwani hakuweza kutoa neno lolote la kujitetea,akabaki kimya mdomo ukawa mzito ghafla kama mtu anayekunywa uji wa magimbi akatamani ardhi ipasuke atumbukie ndani akimbie aibu inayomkabili mbele yake,hakika hakuelewa ni hatua gani achukue!
“Unaweza kukanusha?Naongea nawewe kabla sijakuua!”
“Ninini samehee brooo,hiy…”
“Siwezi kukusamehe adhabu yako wewe ni kifo,ili wapuuzi wengine kama wewe wajifunze”
Hakukua na nukta ya mzaha kutoka kwa Mr.Mbogo sura yake ilibadilika ghafla akavuta sigara fundo refu na kukitupa kipisi chini,akakizima kwa kukinyaga na kuokota bastola huku akimtizama Ahmed kwa macho yaliyojaa unyama wa hali ya juu,dalili ya kifo na harufu ya kaburi ndio vitu alivyokuwa anahisi Ahmed,bila kutegemea akahisi nguo yake ya ndani imelowa,kuja kutahamaki mkojo ukawa unamtoka,aliogopa kufa kuliko kawaida na siku hiyo aliamini kwa asilimia mia moja zote,angepigwa risasi na kufa!
“Na..kuomba Baba an…ngu”
Hajrath alikua wa kwanza kumshika mzee Mbogo mguu,akimsihii asifanye hivyo,akapiga magoti huku akisaga meno na kulia kumuombea Ahmed msamahaa!
“Tuna mto..to mdogo,bado anatuhitaji al…Ng’aaaa ng’aaaa ng’aaaaaaa”
Alikuwa ni kama amemwambia mtoto alie vile kwani muda wote Babrah,alikuwa kimya amelala kelele za kilio zilimfanya Hajrath ahisi uchungu usiokuwa na mfano wake,akapiga picha jinsi mtoto huyo atakavyopata malezi bila baba,akazidi kumsihii Mr Mbogo abadili mawazo yake atoe adhabu nyingine yoyote lakini sio kifo!
Kilio kilichotoka chumbani kilifika seblen na kuenea nyumba nzima,hiyo ilimfanya Mr.Mbogo ashushe pumzi, ghafla akaanza kuingiwa na huruma,jambo ambalo alishindwa kuelewa linatokana na nini!Alichokifanya ni kumtizama Ahmed kwa macho makali,akamsukuma Hajrath na kumfuata Ahmed karibu kabisa!
“Kaa mbali na mke wangu,NITAKUUA”
Zilikuwa ni sentensi za kutisha kufuatia hapo Mr.Mbogo,akafungua mlango na kuondoka zake,akimuacha Ahmed anahema kwa pupa,bado hakuamini kama amepona kwenye tundu la sindano!Cha kwanza kufanya Hajrath, ilikuwa ni kukimbia chumbani kumuangalia mtoto,anayelia mfululizo cha pili ilikuwa ni lazima apaki kila kitu kilichokua chake,aende kwao!Kitendo kilichotokea muda mfupi,kilimfanya aamini yeye ni fungu la kukosa,akaapia asingerudi tena kwa Ahmed,Hajrath alidhamiria kuondoka zake na mpaka alipofikia na maamuzi aliyochukua aliamini angekua sahihi kabisa,akiwa chumbani anamnyonyesha mtoto huku akilia,akakumbuka jinsi alivyowakataa wanaume,akahisi kujuta kuzaa na Ahmed!Tukio la kinyama lililotokea,lilimfedhehesha kuliko kawaida.Machozi,yalimbubujika alivyohakikisha kamaliza kumnyonyesha mwanaye,akasimama na kuanza kupanga kila kitu kwenye begi kisha kuvaa nguo tayari kwa kuondoka,akamuweka mtoto vizuri na kuvaa begi dogo mgongoni!Mlangoni alikutana na Ahmed,ambaye alianza kumuhoji,anaenda wapi!
“Niache nio…ndoke,usinishike Ah..med!Nakuacha ubaki na maisha yako.Nimesha..choka nimechoka siwezi kua nawewe ten…a”
Machozi yaliteleza na kuchuruzika mpaka shingoni,yakalowanisha dera alilovaa uchungu ulimshika akapata kwikwi,ambayo ilimshinda mpaka kumjibu Ahmed!
“Nisamehee Mke wang…..Paaaaaa”
Kibao kikali kilimfikia Ahmed shavuni,kikalia kwa sauti!Na kilimuingia vizuri,tangu amjue Hajrath hakuwahi kupigwa kibao cha namna hiyo,akahisi kama kichwa kinamuuma akalishika shavu lenye maumivu huku akiona maluwe luwe.Licha ya kupata maumivu akazidi kumshika Hajrath mkono kumsihii asiondoke, matokeo yake mkono wake ukang’atwa kwa nguvu,ukweli mwanamke huyu alikuwa mwenye hasira kuliko kawaida!Haikuwa rahisi kuuteteresha msimamo wake,akatembea mpaka seblen huku akiwa na simu mkononi,akabonyeza namba fulani na kuipiga,akaiweka sikioni!
“Njoo unichukue”
“Waaapi?”
“Huku Kibangu”
“Sawa,nakuja hapo!Upo sawa?”
“Njoo unichukue nimekwambia”
Kufuatia maongezi hayo na simu kukatwa,sasa Ahmed akawa ana uhakika kwamba Hajrath hakua katika utani,kila kitu alimaanisha!Akaendelea kumuimbisha nyimbo zote akitumia saundi ili amtulize lakini ikawa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki!Mzozo ulikuwa mkubwa,ikatokea vuta n’kuvute,mpaka Hajrath anatoka nje ya geti alitumia nusu saa lizima,hiyo ilitokana na Ahmed kumvuta vuta!
“Mama,nisamehee!Nimekiri kosa langu ni kosa gani lisilosamehewa mke wangu?”
“Siwez..i kukusamehee!Siwezi Ah..med nitakuja kufa siku sio zangu”
“Huwezi kufa”
“Niache,niende zangu ili ubaki na amani!Ndio jambo unalotaka,kwanini unaning’ang’ania?Kwanini lakini,please niache niende zangu”
Haukuwa utani,majirani wakaamka baadhi wakafungua mapazia ili kujua kuna nini kinaendelea nje!
“Kuna nini hapa wanangu?”
Mzee mmoja mwenye busara akatoka nje na kuuliza!
“Hakuna kitu mzee”
“Hakuna kitu vipi bwana?Wakati namsikia Mama analalamika muda mrefu,haya mambo inatakiwa kumalizana ndani!Mama,ingieni ndani mmalizane.Sio vizuri,mnawapa watu faida”
Mzee alizungumza,ikaonekana kabisa alikuwa upande wa Ahmed ingawa hakujua chanzo cha ugomvi huo ni nini,Hajrath alimtafsiri mzee huyo kama mchawi na nuksi ndiyo maana akabaki kimya ili amlindie heshima yake,katikati ya mzozo huo taxi nyeupe ikatokea na kusimama kandokando yao!Wakamuona Hajrath anaisogelea taxi,kabla ya kufika Ahmed akamshika mkono kwa mara ya mwisho akizidi kumuomba msamaha!Hata hivyo hakufanikiwa,Hajrath akafungua mlango wa nyuma na kuingia ndani,alichokifanya Ahmed ni kuzunguka upande wa dereva!Akachomoa funguo za gari.
“Hauendi popote na mke wangu,unamjua wewe huyu?”
“Kaka tueshimiane,hapa mimi nipo kazini.Mkeo akiwa kwako,mse*** nini”
Ilikuwa ni kama dereva amevurugwa na kitendo hiko,kingine hakua mstaarabu hata kidogo ndio maana akatoa tusi zito!
“Nani Mse***?”
“Wewe ni Mse***!Tena Mse** baridi,nipe funguo zangu”
Dereva taxi,akapandisha mori akafungua mlango na kushuka kabla ya kutoka Ahmed akamtuliza na ngumi ya mdomo,hiyo ilimtia hasira na kumpandisha jazba akashuka kwa kasi na kumvaa Ahmed ambapo hapo walidondoshana chini na kupigana misumbwi,Ahmed alikuwa chini dereva taxi yupo juu yake akampiga makonde ya tumbo ya nguvu!
“Toa funguo zangu Ku*** wewe”
Hakukua na kitu kingine zaidi ya dereva kuchukua funguo zake na kurudi ndani ya gari,akalipiga moto na kugeuza ambapo alimuona Ahmed yupo chini anajizoa zoa,akashusha kioo!
“Siku nyingine usichezee koki,utalowa bwege wewe”
Dereva,akakanyaga pedeli ya mafuta na kuondoka zake!

*****
Kimbembe kilianza katika swala zima la kuomba msamahaa,Hajrath hakupokea simu wala kujibu meseji za Ahmed!Hilo lilipelekea atume ndugu jamaa na marafiki ili wajaribu zoezi hilo lakini hakuna hata mmoja aliyeambulia kitu,mawazo kwa Ahmed yalizidi na hata alivyoenda kazini hakuwa makini hata kidogo mbaya zaidi hakumuona Veronica siku tatu mfululizo,hakuelewa kwamba alikufa ama yupo wapi!Hata hivyo hakutaka kuuliza chochote,akaendelea kufanya kazi kwa unyonge huku mara kadhaa akijaribu bahati ya kumpigia Hajrath kila siku jambo ambalo,lilikuwa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu!
“Ahmed,tafadhali achana na mimi,fanya maisha yako huo ndio msimamo wangu!Siwezi kubadilisha”
“Lakin… tititi”
Siku hiyo simu ilipokelewa lakini badala yake ikazidi kumuumiza mtima,Hajrath alivyomaliza akakata simu na kuizima kabisa!Jambo lililomfanya aumie moyo zaidi,akiwa kwenye sofa anatafakari zaidi ndipo akapata wazo la kumtafuta Mjomba wake ili akamuombee msamahaa wenda angeeleweka!
“Usiku sasa hivi,nipigie asubuhi Ahmed,sawa?”
“Nitakupigia”
“Usiku mwema”
Hakukua na haja tena ya kuwasumbua watu usiku huo!Hata hivyo hakutaka kuelekea chumbani kulala akiamini kwa kufanya hivyo angejitesa kwani alikuwa mpweke mno!Kulivyopambazuka asubuhi na mapema,akajiandaa kama kawaida na kuelekea ofisini ambapo huko!Hakufikiria kingine zaidi ya kumuwaza Hajrath.
“Kaka,naomba tuonane leo”
Ahmed alikuwa simuni,anazungumza na swaiba wake, Benjamin Ngowi.
“Leo?Wapi?”
“Popote tu lakini Blue pearl Garden ingefaa sana”
“Maongezi gani hayo twende Garden Ahmed,unataka kuiteka nchi nini?”
Benjamin alishangazwa kwani mara nyingi maongezi yao hufanyika Baa ama kwenye kumbi za starehe ndiyo maana akachomekea utani huku akimaanisha!
“Maongezi ya kawaida tu”
“Saa ngapi?”
“Kumi hivi jioni,itakuwa poa sana!Ni muhimu tafadhali usikose”
“Mimi saa tisa nipo pale,utanikuta!”
“Poa,baadaye”
Simu ikakatwa,ajenda iliyokuwa inataka kuzungumziwa ilikuwa ni Hajrath na ni lazima wamjadili siku hiyo ili wajue watatumia gia gani arudi nyumbani,Ahmed aliteseka vya kutosha na alimpenda sana Hajrath ndiyo maana alitumia muda mwingi sana kumfikiria bila kufanya kazi ya aina yoyote ile.
Muda ulikimbia kwa kasi hatimaye saa tisa alasiri juu ya alama ikafika,akatoka nje na kuingia ndani ya gari na kuanza safari ya kwenda Blue pearl Garden iliyokuwa Ubungo!Ni sehemu iliyokuwa na utulivu mkubwa sana na watu wachache walipafahamu hiyo ilifanya iwe na ukimya mno!Hakukuwa na msongamano mkubwa sana wa magari, ndiyo maana akawahi kufika,hata hivyo alishangaa na kutabasamu baada ya kuona gari la Ngowi lipo kando!Akaamini kweli Benjamin ni mzungu sana!Alivyoshuka,moja kwa moja akanyoosha mpaka ndani.
“Nimeamini wewe ni mzungu”
“Hata wewe inatakiwa uwe hivyo,muda ni mali Ahmed,mambo vipi lakini?”
“Fresh tu,za siku kibao?”
“Mungu ni mwema karibu,hapa hakuna bia lakini”
“Naelewa,leo sitaki kabisa”
Walivyomaliza kusalimiana,Ahmed hakuwa na lingine zaidi ya kuweka hoja yake mezani,akaelezea kila kitu kilichotokea, hakuficha.
“Sisi wote wanaume,sina sababu ya kuficha ficha!Nahitaji msaada wako”
“Ulisema ulitembea na mke wa mtu?”
“Kaka,jamaa alikuja na bastola ndani kwangu.Ilikuwa kidogo nitoe mavi,Benjamin kifo kisikie tu kwa jirani.Katika maisha yangu,sijawahi kuwa na hofu namna ile.Nilipiga dua zote siku hiyo!”
“Inauma ndio,si una kumbuka ulichomfanyia yule sharobaro wa Yusrath”
“Basi ndio siku hiyo nilijua jamaa angepiga simu,waje kunila samvu la kopo aisee sijui ningeweka wapi sura yangu”
Ngowi akacheka na kumtizama Ahmed kwa masikitiko makubwa sana!
“Nahitaji msaada wako,nampenda sana Hajrath nataka arudi nyumbani!Nataka nifunge naye ndoa kaka,nampenda nakuhaidi sitomkosea tena naapa mbele yako Mungu shahidi wa hili”
Masononeko aliyoonesha Ahmed yalimfanya Benjamin Ngowi aingiwe na huruma,alichomuhakikishia kwa asilimia mia moja ni kwamba angezungumza na Hajrath,kwa kudhibitisha kuwa yupo siriazi akachukuwa simu yake na kumuendea hewani,akaweka laudispika ikaanza kusikika ikiita!
“Shem”
Wa kwanza kuzungumza alikuwa ni Ngowi.
“Abee”
“Upo?”
“Nipo”
“Wapi hiyo?”
“Nipo Kigoma”
“Aaah shem,acha zako”
“Kwanini nikudanganye sasa?!Nipo Dar,niambie”
“Nahitaji kuongea nawewe”
Kuanzia hapo,ukimya ukatawala!
“Halloo shem”
“Nakusikiliza”
“Nataka kuzungumza nawewe”
“Ndio nakusikiliza,zungumza”
Moyo wa Ahmed kwa wakati huo,ulikuwa ukidunda kwa nguvu,akahisi kama joto kali limempiga kwenye uti wake wa mgongo!
“Mambo haya sio kwenye simu ujue,inabidi tuonane”
“Kama kuhusu Ahmed,please usinipotezee muda wangu”
“Sio wala,ni mambo mengine tofauti kabisa”
“Benja,mimi nawewe tunaheshimiana sana.Nisije nikakuvunjia heshima”
“Usijali,hatutofika huko”
“Sawa,lini?”
“Kesho Jumamosi,ndio siku nzuri tukutane Kawe Club”
“Kawe Club?”
“Ndio,Kawe Club! Nitakuja kukupitia”
Baada ya simu kukatwa akamtizama Ahmed,aliyekuwa kaduwaa kama mtu anayesoma tangazo!
“Sasa bratha,hapa kazi kwako!Mimi nitaenda kuongea naye hakuna mkate mgumu mbele ya chai”
“Sawa kaka,utanijulisha!Nakuaminia Ngowi”
“Hakuna tabu”
Siku hiyo hawakunywa pombe,kila mtu aliagiza Mirinda Nyeusi, walivyomaliza wakaingia ndani ya magari yao,wakaondoka zao!

*****
Jumamosi haikuwa mbali,hatimaye kulikucha na kama Benjamin Ngowi alivyohaidi jioni ya siku hiyo angempitia Hajrath ili wakafanye mazungumzo ambayo bado Hajrath hakuelewa ingawa alihisi ni lazima ajenda kubwa ingekuwa juu ya Ahmed lakini hakutaka kulipa jambo hilo kipaumbele sana!Saa kumi ya Jioni,akawa tayari amejiandaa vizuri!Akatoka nje huku akimuacha mtoto wake na msichana wa kazi,roho ilimuuma lakini aliapia angewahi kurudi baada ya muda mfupi!Alivyotokeza nje ya geti,akakutana na gari la Ngowi linaunguruma,akatembea na kuvuta kitasa cha mlango kisha kuingia ndani.
“Za siku?”
Hajrath akatupa salamu huku akivuta mkanda wa siti kwa ajili ya usalama!
“Nzuri tu”
“Tunaenda wapi?”
“Kama tulivyoongea jana,Kawe Club”
“Aya, lakini hayo ni mazungumzo gani?”
“Usijali ukifika utajua”
Kuanzia hapo hakukuwa na maongezi mengine zaidi ili kufupisha njia Ngowi akaamua kupitia njia ya Coca Cola,akaibukia Mikocheni na kutokezea katika mzunguko wa barabara ya Mbezi,hapo akanyoosha na kukunja kulia barabara ya vumbi!Dakika tano baadaye,akapunguza spidi ili atafute sehemu ya kuegesha gari.Moyo wa Hajrath ukapiga kwa nguvu,kuna kitu alikiona akamgeukia Benjamin!
“Benja,nimeona gari la Ahmed hapa.Niambie ukweli kama yupo!”
“Hayupo,niamini”
“Gari lake nalijua”
“Magari yanafanana”
“Mpaka namba?!”
Hapo Ngowi,akashindwa kujibu kitu hakuweza kutengeneza hoja ya kujitetea kwani kuna mambo nyeti walipanga na Ahmed,wakateremka lakini Hajrath macho yake yote yalikuwa kwenye gari aina ya ALTEZA kwa namna ya kulikagua,asilimia zote mia moja akajua Ahmed yupo eneo hilo!
“Mimi narudi”
Hajrath,akasimama na kusita!
“Tafadhali nakuomba,lile gari sio la Ahmed hata mimi nilidhani hivyo”
Benjamin Ngowi,akatumia diplomasia ya ki utu uzima ili kumshawishi!Wakatembea sambamba mpaka ndani ambapo kazi ya Hajrath ilikuwa ni kukagua mtu mmoja baada ya mwingine kama angemuona Ahmed, matokeo yake hakumuona!Wakatembea mpaka kwenye moja ya siti ambapo kando kidogo kulikuwa na uzio wa seng’eng’e iliotenganisha bahari iliyofanya upepo wa eneo hilo uwe mzuri wa kuvutia!
“Karibuni”
Dada wa vinywaji akafika kuwasikiliza!
“Niletee,red wine”
Benjamin akaagiza!
“Fanta orange ya moto”
Mhudumu alivyoleta vinywaji,Hajrath akavunja ukimya!
“Enhee,niambie”
“Nini kimetokea?”
“Kuhusu nini?”
“Wewe na Ahmed”
“Hakuna kitu,kwani yeye amekwambia nini?”
“Hajaniambia kitu”
“Basi hakuna kitu”
“Shem,sikia nikwambie.Nyie mshakuwa watu wazima,ni wazazi sasa hivi.Atakayeumia ni mtoto sio nyie”
“Ndio alivyokutuma?Nilijua tu!”
“Hajanituma,Ahmed hana uwezo wa kunituma mimi!Unajua shem,hata kwenye kabati vikombe vinagongana!Msamehee,yaishe”
“Kwanini asije kuomba yeye msamahaa?”
“Anadai hupokei simu”
Benjamin akasahau kama alidanganya,tayari akawa amechanganya kachumbari na mlenda!
“Si ulisema hujaongea naye?”
Hapo Benjamin akaishiwa pozi,mbaya zaidi Hajrath alimtizama machoni bila kupepesa kope!
“Nijibu”
“Tuliongea kidog…….”
Hakuweza kumalizia sentensi yake,Ahmed akatokea pembeni hiyo ilimfanya Hajrath atake kusimama lakini Ahmed alimzuia na kumrudisha taratibu kwenye kiti!
“I’m sorry mke wangu,naomba nisamehee nakupenda bado!Naomba urudi nyumbani”
Ahmed alizungumza kwa hisia zote na kwa sauti ya chini,hakutaka kumpoteza Hajrath moyo wake ulikuwa ukiumia ajabu,bila Hajrath ilikuwa ni sawa na gari bila mafuta,lisingetembea!
“Nakupenda Hajrath,sijawahi kupenda hivi katika maisha yangu!Niliteleza tu,bahati mbaya shetani alinipitia ndio maana ikawa vile”
Maneno ya Ahmed,yalimuingia Hajrath moyoni lakini hakutaka kuuruhusu mtima wake kumsamehee baada ya kukumbuka jinsi alivyodhalilishwa kwa kushikiwa bastola,hakika asingeweza kusahau hata kidogo hata hivyo kuna nafsi ilimwambia ‘Msamehee’akajaribu kupingana na nafsi hiyo lakini alishindwa kabisa!Hapo hapo,Ahmed akapiga goti moja chini bila kuuliza chochote,akaingiza mkono mfuko wa nyuma na kutoa pete!Jambo lililomfanya Hajrath azidi kupagawa zaidi.
“Will you marry me?”
Ahmed akauliza,huku akimtizama Hajrath na wakati huo mwanamke huyo alikuwa akilengwa na machozi!Akatulia kwa muda akahisi kama mashavu yake yanaanza kulowana yalikuwa ni machozi yanambubujika.
“Ahmed,I love you so much”(Ahmed,nakupenda sana)
Akajikuta ameropoka bila kupenda,akatoa mkono wake kisha Ahmed akamvalisha pete ya uchumba,hiyo ilimfanya Benjamin Ngowi apige kelele na kunyanyua mikono juu kwa furaha kama shabiki wa mpira,anavyoshangilia baada ya kuona goli.


Utaratibu wa kuhamia nchini Sweden,akale kuku kwa mrija ulianza mara moja baada ya kupata wazo la kwenda kutafuta maisha huko katika nchi hiyo ya ‘Scandnavia’ aliamini baada ya kufika huko,angetafuta kazi ama kufungua biashara yoyote ile kisha akajenga nyumba kubwa ya kifahari yenye hadhi yake!Kilichokuwa kikwazo kikubwa ni hati ya kusafiria,ndiyo maana kwa haraka akaanza mchakato huo na kila alipoona kuna ugumu akatumia msemo wa ‘Penye uzia penyeza rupia’ pesa ikapeleka mambo kwa haraka akapata barua kutoka serikali za mitaa,akapeleka uhamiaji alivyoona muda unakwenda bila majibu akahonga maafisa wa polisi,ndani ya siku tatu akawa tayari ana hati ya kusafiria mkononi mwake!Kimbembe kilianza kwenye swala zima la kupata viza,hapo ndipo kulikuwa na ugumu mkubwa.Alidhani mambo yangekua rahisi kumbe haikuwa hivyo,kila alipojaribu kutoa pesa ilishindikana hapo ilibidi awe mpole sana!Ukapita mwezi mzima akiwa mkoani Arusha,bila kupata chochote!
“Halloo naongea na Martha?”
Upande wa pili wa simu,ulisikika siku hiyo akiwa kitandani amelala!
“Ndio,nani mwenzangu?”
“Mtu wa Immagration,si ulikuwa unahitaji viza ya kwenda Sweden?”
Martha Msoso baada ya kusikia hivyo,akakaa kitako kwani hizo zilikuwa habari njema sana kwake!Moyo wake ukapiga sarakasi kwa furaha kubwa, akajua tayari safari inanukia!
“Ndio,nina shida nayo kweli”
“Njoo Sakina hapa,tuongee vizuri nimetoroka ofisini kwa ajili yako”
“Sawa,sawa sawa nakuja sasa hivi”
Safari ya kwenda Sweden na shilingi milioni mia tano ilikuwa ni kama ndoto na ilikuwa ni lazima itimie,alichokifaya ni kutembea mpaka kabatini akatungua nguo kwa haraka na kuweka mwilini!Kwa kuwa alikua amekodi hoteli,alifunga chumba na kutembea mpaka mapokezi!
“Dada nitarudi”
“Sawa,karibu sana na leo tukuwekee chakula?”
“Nitakupigia simu”
“Hakuna shida dada”
Alikuwa ana kila sababu ya kufika haraka eneo la Sakina,ndiyo maana akachukua pikipiki ili awahi,bahati nzuri akawa ndani ya muda baada ya kufika akatoa simu na kumtafuta mtu aliyempigia simu muda mfupi uliopita akidai anafanya kazi uhamiaji.
“Nishafika”
“Mbele yako,unaona hilo kontena?”
“Ndio”
“Kwenye hiyo baa ya kushoto”
“Sawa,nakuja”
Hakutaka kupoteza wakati kwa hatua mbilimbili,akatembea mpaka kwenye baa hiyo na alivyofika akaanza kuangalia huku na kule kwa namna ya kumtafuta mwenyeji wake,alivyopiga simu kwa mara nyingine akamuona mwanamke mtu mzima yupo kwenye kona, kushoto anampungia mkono,akawa ana uhakika ndiye mwenyewe,akamsogelea mpaka alipo!
“Ndio wewe?”
“Yes,Martha?”
“Ndio mimi”
“Karibu kiti”
“Ahsante”
“Ulikuwa unataka viza?Mimi nitakusaidia”
“Nitashukuru sana mama angu,utakuwa umesaidia balaa”
“Mambo madogo hayo,sasa umejipangaje?”
“Kuna laki tano”
“Hapana,swala lako ni zito.Nitafungwa ujue”
“Basi laki saba”
“Hapana”
“Unataka ngapi?”
“Milioni moja na nusu”
Hapo Martha,akatulia kidogo na kumuangalia mwanamama huyo!
“Hapana,mbona nyingi sana!Nakupa laki tisa.Ndio mwisho wangu”
Wakahitimisha,mwanamama huyo ambaye mpaka wakati huo hakujitambulisha jina lake, akaonekana kama anachezea simu baada ya dakika mbili,wanaume watatu wakafika eneo hilo,warefu wa kimo.
“Martha Msoso,upo chini ya ulinzi.Sisi ni maafisa kutoka jeshi la polisi”
Japokuwa alikuwa amekaa kwenye kiti lakini alihisi kudondoka,akahisi kapigwa na joto la ajabu mwilini!Alivyomwangalia mwanamama mwenyeji wake,akazidi kuchanganyikiwa kwani mkononi alikuwa tayari na kitambulisho cha jeshi la polisi.
“Tuongozane”
“Nimefanya nini?”
Martha akauliza kwa sauti ya kupwaya,ilielekea alizijua sheria za nchi kwamba askari haruhusiwi kukuchukua bila kukwambia kosa lako!
“Twende kituoni”
“Siwezi kwenda bila kujua nimefanya nini”
“Una kosa la kushiriki ujambazi,RB yako hii hapa!Imefunguliwa Dar es salaam staki Shari na Yusrath Suleiman”
Martha akaishiwa nguvu,mbaya zaidi hakuelewa ni kwa njia gani jeshi lilijua yeye yupo mkoani Arusha,hapo ndipo akaamini kwamba Serikali ina mkono mrefu sana!

*****
Maisha yaliendelea kana kwamba hakukuwa na kitu chochote kilichowahi kutokea nyuma,matukio yote ya nyuma yaliyopita ya kuumiza moyo yakageuka na kuwa historia,wakasahau yaliyopita na kuganga yajayo!Mapenzi yao yote wakayadondoshea kwa mtoto wao mdogo aliyekuwa mrembo,Babrah!Ahmed aliwahi kurudi na alijirekebisha hata kiwango cha kunywa pombe alipunguza, kwa wiki alikunywa mara moja tena wakati mwingine alifika nazo seblen na kunywa mbele ya Hajrath!
“Hii movie inatisha baby”
Siku hiyo wakiwa seblen,Hajrath akavunja ukimya usiku huo wakiwa wenyewe wanatizama luninga!
“Inaitwaje?”
“Wrong turn”
“Unapenda mambo ya kutisha,angalia usiku usije kupiga kelele”
“Wala siwezi”
“Shauri lako”
Ilikuwa ni familia bora,yenye upendo wa hali ya juu sana!Siku zilisogea kwa kasi ya ajabu,sijui wazo hilo Ahmed alitoa wapi lakini lilionekana kumuingia Hajrath na bila kupinga akamuunga mkono!
“Kabla hatujafunga ndoa, naomba nikufungulie biashara”
“Baby,biasharaaaaa?!”
“Ndio,unapenda biashara gani?”
“Mmmh,nipe muda nifikirie kwa sasa hivi!Nitashindwa kukupa jibu mpenzi”
“Nakupa wiki mbili,mshahara wa mwezi huu nataka kuuweka then mwezi ujao uwe ushanipa matokeo”
Kuanzia siku hiyo Hajrath alikuwa akihangaika huku na kule akifikiria,akaona haitoshi na kuamua kuwashirikisha marafiki zake ili wampe mawazo,kila mtu akaja na wazo lake.Wengine wakamwambia vitenge,kuna waliomshauri na kumwambia maji ya jumla baadhi yao wakamwambia afungue mgahawa wa chakula!Akachoka na kushindwa kuchagua mbichi na mbivu!
“Ndio hivyo,Kanei!Nashindwa kuelewa,nifanye biashara gani”
Siku hiyo aliamua kumualika rafiki yake Kanei ili amshauri alikuwa ni msichana mdogo lakini mwingi wa busara hata hivyo alikuwa ni mjasiriliamali.Ndiyo maana Hajrath akampa mualiko huo nyumbani kwake,niya na madhumuni ilikuwa ni kupata ushauri!
“Vipodozi,sasa hivi nafanya vipodozi!Biashara hiyo inalipa ukiwa siriazi!Nikisema vipodozi sio viwili vitatu!Vya jumla,alafu sasa baadaye unaweka nguo pia unachanganya biashara”
“Mmmh,hizo akili za kichaga umezitoa wapi besti?”
“Mjini hapa,siku hizi wanaume wenyewe hawahongi lazima ujiongeze!Ukitegemea wanaume utachakaa”
“Ama kweli vyuma vimekaza”
“Alafu siku hizi walivyokuwa washenzi,hawatoi pesa wanakupa ushauri ooh mara fuga kuku wa kutotolesha,sijui wekeza kwenye ukulima tabu tupu!”
“Lakini ndio vizuri”
“Juzi,kuna libaba nilikua nalo.Linanitongoza,shemeji yako akaona meseji”
“Ikawaje sasa?”
“Kalalamika sana”
“Sipati picha angekuwa Ahmed,ungekoma”
“Kwanini?”
“Basi tu”
“Shoga,mimi sijawahi kupigwa na mwanaume.Hivi inakuaje?Yule shemeji yako ujue kama zoba hivi,akifuma meseji kwenye simu analia kama bwege!Nina hamuu wewe siku moja anipige,natamani kupigwa pigwa ili kujua inakuaje”
“Usiombe Kanei”
“Natamani hata siku moja,anipige hata vibao vitatu lakini nafasi hiyo sipati.Vipi mwenzangu,ebu niambie siri ya kupigwa ili namimi nijaribu”
“Kanei kuwa siriazi basi,umesema vipodozi eeh?”
Hakuelewa kwamba Kanei anamaanisha kwani hata siku moja hakuwahi kupigwa kibao,ndiyo maana alitaka kuonja radha ya kupigwa na mpenzi wake!Hata hivyo siku hiyo walizungumza mengi sana kuhusiana na biashara na mambo mbali mbali ya maisha!Ilivyofika saa moja jioni, akaaga na kuondoka zake!

****

Maisha yalizidi kusonga,Ahmed kwenye swala la kumfungulia Hajrath biashara halikuwa longolongo alifanikisha hilo na baada ya siku moja alimrudia ili apate mrejesho,hilo halikuwa tatizo!
“Umesema vipodozi?”
“Ndio baby”
“Okay,anza kufanya research utafute fremu”
“Honey,ahsante sana!Wewe ni mume bora”
“Wewe ndio umenifanya niwe hivi”
“Ilove you”
Siku iliyofuata mchakato ukaanza mara moja,akapatikana dalali ambapo alimuonesha fremu tatu tofauti tofauti,fremu aliyoipenda ilikuwa maeneo ya Tabata, Liwiti.Kwa hofu ya kuitumia pesa,Ahmed akachota na kulipia kodi ya miezi sita,ukarabati ukaanza bila kupoteza wakati rangi ikapigwa taa zikawekwa kilichokuwa kinasubiriwa ni mzigo wa vipodozi!Kichwani mwa Ahmed kulikuwa na mambo mengi sana,mtoto wake mdogo ndiye aliyemfanya aumize kichwa namna hiyo sababu aliamini kuna kesho na keshokutwa, hata hivyo wazo la kufungua kampuni yake binafsi lilikuwa kichwani kwake,lakini isingewezekana bila ya kuanza kumfungulia biashara Hajrath hata ingetokea amekwama basi duka lingeendesha vitu vidogo vidogo vya nyumbani!Hakuelewa akili hiyo ya kuwaza mambo ya mbele kaitoa wapi.Siku chache baadaye,akapakua shilingi milioni tatu,akamchukua Hajrath ili waende kununua mzigo wa Vipodozi kwa bei ya Jumla,hilo likawezekana na kila kitu kilikuwa kama ndoto kwa Hajrath!Siku mbili baadaye,duka likawa limefunguliwa wakaliita AHB Cosmetics,yaani kila herufi lilisamama badala ya majina yao!
“Nimekuja kukupitia baby wangu”
Siku hiyo Ahmed alitokeza ghafla dukani bila kumwambia Hajrath,alifanya hivyo makusudi kutokana na wivu aliokuwa nao moyoni.
“Sawa,tuondoke love”
“Babra amelala?”
“Huyo hapo amelala ndio”
Fremu haikuwa kubwa sana,lakini ilijaa vitu mbalimbali kuanzia mafuta,manukato,sabuni na vingine vingi!Katikati kulikuwa na kiti kikubwa cha kuzunguka na meza,hiyo ilikuwa kwa ajili ya Hajrath kukalia,siku hiyo walifunga mapema na kuondoka zao!Hakutaka mchezo kabisa,baada ya kufanikisha hilo!Akaanza kupanga mipango ya harusi,hilo halikuwa siri wajomba wakaitwa na kukaa kikao kwa mara nyingine!
Wakakubaliana ili mahali itolewe,hata hivyo walipigwa faini kutokana na Hajrath kuzalishwa,hilo halikuwa tatizo!Wakalipa na michakato ya ndoa ikaanza mara moja!
*****
“Yes,naoa keshokutwa!Kadi,muone Salome!Broo,kichwa kinauma hapa!Sina hata shilingi mia mfukoni”
“Aya,hakuna shaka!Nitakuja huko”
“Usikose kaka,nitafurahi kukuona kwenye harusi yangu”
Taratibu za ndoa zilifuatwa,siku ya siku ikafika shekh akaitwa Ahmed pembeni Hajrath kushoto ubani ukachomwa,Ahmed akiwa ndani ya kanzu iliyonyooka kama muumini wa msikitini vile kumbe mara ya mwisho kuswali ilikuwa sijui lini!Hata hivyo,ndoa ilifungwa watu wakala ubwabwa na kusaza,wengine walilewa mpaka basi,mpaka watoto wa uswahili wakabeba pilau kwenye mashati!Haikuishia hapo.Siku ya Jumamosi ilibidi wafanye sherehe nyingine kubwa ukumbini, ilikuwa pambe!Watu walifurika sana,kila mtu alikuwa mwenye furaha isipokuwa Kassim,muda wote alikuwa amekunja sura,anamtizama Hajrath mbele jinsi alivyokuwa mrembo, moyo ulimuuma ajabu!Hata hivyo hakutaka kukubali,ulivyofika muda wa kutoa zawadi,watu wakaanza kupita kwa mtindo wa kupanga mstari wengine wakitoa mikono!Ilivyofika zamu ya Kassim kumpa mkono Hajrath,akaganda kidogo na kumtekenya kiganjani kisha kusogea karibu ya sikio lake kama wengine wanavyofanya kumpa pongezi lakini yeye badala ya kufanya hivyo,akatoa ulimi wake na kumnyonya sikio bila mtu yoyote kuona,hiyo ilimfanya Hajrath apigwe ganzi mwilini, akahisi kama amepararaizi mwili mzima,damu yake ikamwenda mbio mno!Akabaki ameganda kama sanamu,hajui afanye nini kwani nguvu zote zilimwishia.



“Nakupenda sana”
Kassim alimalizia kwa maneno hayo akiwa sikioni mwa Hajrath kisha kuondoka zake huku nyuma akimuacha Hajrath akiwa katika butwaa kubwa,alitamani kumueleza Ahmed kila kilichotokea lakini akasita kwani aliamini angeharibu furaha nzima ya siku hiyo!Muda wa zawadi ulivyoisha,mshehereshaji wa shughuli hiyo akawaomba wageni waalikwa wajongee kwenye maakuli yaani chakula.Kitendo hiko kilifanyika mara moja,watu wakala na kunywa wanavyotaka!Hakika kamati ya vinywaji na chakula walijipanga vizuri!Saa sita kamili kama sheria za nchi zinavyotaka,harusi ikawa imeisha!Gari maalum lililowapakia maharusi likasogea karibu!
“Hongera sana mzee”
Ngowi,hakuwa mbali akamfuata Ahmed nje na kumpa mkono akiwa mwenye furaha tele moyoni huku pembeni akiwa na kipenzi chake,Pendo Jonas!
“Ahsante bado wewe tu”
“Mimi mwezi ujao”
Siku hiyo kila mtu alitaka kupiga picha na Ahmed,ghafla akageuka na kuwa maarufu kwa usiku huo!
“Tupige picha kidogo ya kumbukumbu”
Hayo ndiyo yalikuwa maneno ya wadau mbalimbali baada ya Ahmed kutoka nje ya ukumbi huo,kila kitu kilikuwa ni furaha!Wakaingia ndani ya gari na Hajrath,kitendo cha kufika tu akapokelewa na busu motomoto!
“Nakupenda mme wangu,hakika tumetimiza ndoto”
“Nakupenda pia,mke wangu!”
Hajrath kwa kudeka,akalala kifuani kwa Ahmed na kutulia, gari likageuzwa na safari ya kwenda Serena Hotel kuanza mara moja,ambapo hapo walichagua kulala usiku huo kisha siku inayofuata waende kisiwani Zanzibar,kwa ajili ya fungate!Kila mtu alikuwa mwenye furaha sana usiku huo!Gari ya kifahari aina ya BMW X6 iliyopambwa na Maputo kila upande,iliingia ndani ya Serena Hotel kisha wakafunguliwa milango kama watoto wa mfalme,Ahmed akashuka mkewe akafuatia!Hawakufanya kazi yoyote wala kubeba mizigo sababu walisaidiwa na wapambe wao,mpaka mlango wa chumbani.
“Jamani usiku mwema”
“Nawewe pia,shemeji!Mfike salama”
Hajrath akaitikia,hakuna jambo alilokuwa anasubiria kama hilo la kuwahi kufika hotelini kwani damu yake ilimwenda mbio kuliko kawaida!Akili yake iliwaza kufanya tendo la ndoa ambalo kwake kwa mara ya kwanza ingekuwa akiwa ndani ya ndoa,hakuelewa utamu wake upoje ndiyo maana muda wote alikuwa mwenye kiwewe!Ilikuwa ni hoteli ya kisasa tena ya nyota tano!Mkononi Ahmed alishika kadi maalum ya umeme,akagusisha kwenye mlango ukajifungua!Kitendo cha kuingia ndani,Hajrath hakufikiria lingine zaidi ya kumgeuza Ahmed kwa kasi na kuanza kumnyonya mdomo huku akimpapasa kila sehemu ya mwili,ilikuwa ni wazi kabisa alikuwa mwenye midadi iliyozidi kipimo!Hata hivyo Ahmed akajiongeza sababu alijua ni kitu gani kinachotakiwa kufanyika kama mume,akaupitisha mkono wake taratibu nyuma ya mgongo wa Hajrath na kushusha zipu ya shela,lote likaachia na kudondoka chini kilichoonekana lilikuwa ni umbo zuri la Hajrath akiwa ndani ya ‘skintight’ fupi na sidiria nyeupe,mikono ya Ahmed,ikaanza kuteremka chini kwenye kitovu na kukutana na tight laini,akapata nafasi kidogo na kupenyeza vidole viwili ambavyo vilikutana na chupi,akazidi kuingiza zaidi mpaka akakutana na kitu anachokitafuta,kwa ufundi wa hali ya juu akaanza kucheza na mgodi kwa namna ya kuupapasa!
“Mmmmh”
Hajrath akaguna huku akifumba macho yake hiyo ilimaanisha tayari gari limewaka,Hajrath nayeye hakutaka kuonekana mzembe!Nayeye akaanza kumvua nguo Ahmed,kuanzia koti mpaka shati,ikafuata vesti mpaka boxa ikatolewa,mwili wa Hajrath ukazidi kusisimka baada ya kukutana na muhogo uliosimama imara kabisa,akauchua kidogo ili anogeshe mchezo!Hata hivyo alikuwa amechelewa kwani alitupwa kitandani,Ahmed akapanda juu yake!Akachojolewa nguo moja baada ya nyingine,wote wakabaki watupu kama walivyozaliwa,hakukuwa na muda wa kupoteza zaidi ya mineso ya kitanda kusikika!

******
Siku iliyofuata kama walivyopanga ndivyo ilivyokuwa kwani waliamka asubuhi na mapema ili kujiandaa na boti ya saa nne asubuhi,ilikuwa ni furaha kubwa sana kwao baada ya Babrah kuletwa,ilikuwa ni lazima Asia,binamu yake na Hajrath aende pia Zanzibar kwa ajili ya kumuangalia mtoto,hilo liliwezekana baada ya muda mfupi wakawa na tiketi zao tayari kwa safari!Ambapo hapo walichukua taxi mpaka bandarini,safari ikaanza mara moja!Ingekuwa ndiyo mara yake ya kwanza kufika kisiwani Zanzibar,ndiyo maana alikuwa mwenye hamu kubwa sana ya kupaona,alisikia jinsi watu wa huko walivyokuwa wakarimu na wenye upendo!
“Asaalam aelekuy”
Hizo ndizo salamu walizokumbana nazo ndani ya boti!Ahmed na familia yake walikaa juu kabisa ili kutizama maji na kuona mandhari ya bahari ya Hindi,kila wakati Hajrath alideka kwa mumewe,akawa mwenye furaha kuliko kitu chochote kile!Ndani ya masaa mawili na nusu,boti ikatia nanga bandarini!Kila kitu kiliwashangaza kuanzia mavazi ya huko mpaka mandhari,watu wa Zanzibar walijua sana kujitunza,wengi wao walivaa baibui na sketi ndefu,kifupi ulikuwa ni mji uliotulia!
“Karibuunii zenjiiii,mwataka usafiriii!Mwatokea Bara,siooo?”
Mzee mmoja dereva taxi aliwapokea kwa rafudhi ya kwao!
“Ndio lakini kuna mwenyeji wetu,anakuja”
“Ayaaaa,miyee naitwa Mudriiiick!Taxi yangu ileee paaleee.Kama hamtojalii tawapeleka popote mwapotakaa”
“Tuna ndugu yetu atakuja”
Ahmed,akarudia jibu lake akatoa simu mfukoni na kuonekana kuna mtu anamtafuta hewani,baada ya muda mfupi akamrudia Hajrath!
“Amefika,amesema yupo hapo nje”
Wote wakabeba mizigo yao mgongoni na kutoka pembeni,ambapo hapo walisimama kidogo!Costa ya abiria ikapaki kandokando yao!
“Ahmeeeeed”
Sauti ya dereva,ikamuita!Hiyo ilimfanya Ahmed apigwe na butwaa,alikuwa ni rafiki yake wa siku nyingi sana!Waliosoma wote,ambaye huyo ndiye angemtumia kama mwenyeji wake!
“Daah,Hamidu!Ndiyo umenenepa hiviii?!”
“Aaah,weyee acha mas-haraa!Weye ndiye wanenepa sana!Karibuni Zenji,shemejii asaalam aelukuy”
Hamidu,akamgeukia Hajrath ili ampe salamu!Wakasalimiana wote kisha kuingia ndani ya Costa!
“Mwezako nilikuwa napeleka chombo nyumbaniii,ulivyonipigia simu n’kaona hata ngoja nije kwanzaaa!Vipi huko baraa,mwasemaje?”
Rafudhi ya Hamidu,ilimshangaza sana Ahmed kwani alikuwa tayari anaongea kama watu wa huko,lakini hata hivyo alielewa kwamba Hamidu aliishi Zanzibar takriban miaka kumi!
“Harusiii yakoo,sikuweza kuja bwana!Nilipatwa na maradhiii kidogoo,kifuaa chaaaanguuuu!Kilileta shida na watoto na skuli basi tafranii!Sasa hivi,wacha niwapeleke hoteli kwanza kisha baadaye,nije kuwatembeza”
Hamidu alizungumza kama watu wa huko kabisa na mara kadhaa alisalimiana na marafiki zake kwa njia ya kuwapungia mkono akiwa ndani ya Costa,hata hivyo Hajrath muda wote alifurahi kwani Hamidu alionesha kuchangamka na kuwafurahia kwa kiasi cha kutosha!Walivyofika Maisara,wakapunguza mwendo na kuingia mtaa mmoja uliogawanyishwa na kuta mbili,wakapita katikati na kutokezea upande wa pili ambapo huko mbele yao walikumbana na hoteli,Costa ikaingia ndani na kuegeshwa!
“Mmefikaaaa,wachaa niwakaribishee!”
Kilichokuwa cha kwanza ni kufika mapokezi ambapo hapo walipewa vyumba viwili,kimoja cha Asia na Babrah kingine cha Ahmed na Mkewe Hajrath,ilikuwa ni hoteli nzuri inayonukia harufu ya ubani kila mahali,walivyoingia ndani wakapigana mabusu na kurukiana kama watoto wadogo!
“Nakupenda Mme wangu”
“Hata mimi love,una enjoy sana?”
“Yaani kungekuwa na neno lingine,zaidi ya sana ningelitumia!Sijui nisemeje jinsi navyojisikia sasa hivi”
“Nielezee kidogo”
Hapo Hajrath akashusha pumzi na kuzishikashika kidogo ndevu za Ahmed kwa mtindo wa kuzipapasa kimahaba!
“Najihisi ni mwenye bahati sana”
“Kua namimi?”
“Yes kuwa nawewe Ahmed,sio siri tumetoka mbali sana!Nakumbuka mambo mengi kuhusu wewe,tukiwa Chuoni pale Makumira”
“Hatimaye,milima na mabonde tumevuka na tumeshinda”
“Sema ulijua kuninyoosha wee mwanaume na demu wako Yule Necka,snitch sana Yule”
“Wewe je?Florian?”
“Nani aliyeanza,wewe ulimwaga mboga nikamwaga ugali.Hakuna mtu kula”
“Alaf…”
Ahmed hakuweza kuzungumza tena matokeo yake kilichosikika hapo ni kama sauti ya mtoto anayenyonya kopo la maziwa,walikuwa wakipigana madenda wakatupana kitandani,wakiwa wenye moto wakitomasana!Hajrath akatoka kitandani,akasimama na kushuka kitandani hiyo ilimfanya Ahmed atoke aende nyuma yake amshike kiuno vizuri, hakukuwa na maswali mengine ya ziada zaidi ya kufanya tendo la ndoa,walivyotoka hapo wakahamia bafuni ilionekana mechi hiyo waliipania sana!Sababu ilichezwa kwa kipindi kirefu sana!
Jioni ya siku hiyo Hamidu aliwafuata wakatembea tembea maeneo kama Mwembe mimba,soko la Mombasa na Mwanakwerekwe!Saa moja wakafika Forodhani,sehemu iliyomfanya Hajrath atabasamu kwani kulichangamka mno,watu walikuwa wengi!Mbele yao kulikuwa na meza nyingi sana juu yake kuna vyakula mbalimbali vya pwani.
“Chei chei,karibuni”
“Baby hii ni nini?”
Hajrath akauliza baada ya kuona kitu kigeni kwenye macho yake!
“Shawarma”
“Shawarma?!”
“Ndio shawarma”
“Ndio nini?”
“Nadhani ni kuku hawa,si ndio Hamidu?”
“Ndiooo ni kuku haoooo”
Hajrath hakutaka kupitwa,akanunua!Akatengenezewa na kupewa,hakika alifurahia,wakatembea mpaka kwenye meza ya pweza hapo wakadokoa vipande kadhaa,wakakunja kwenye meza ya mishkaki ya bata!Wakakatiza kwenye ngisi mwisho wakamalizia kwenye urojo,hapo ndipo Hajrath akahisi kuchoka wakarejea katika hoteli waliyofikia!
Fungate ilienda vizuri siku iliyofuata wakaenda Zanzibar Park,kushangaa wanyama ambapo huko pia walipiga picha za kumbukumbu walivyomaliza hapo wakaenda kutembelea kwenye mnara Mapinduzi square,hakika ilikuwa fungate na kumbukumbu nzuri sana kwao!
Wiki moja baadaye wakawa tayari wametoshekwa walichotakiwa ni kuanza kufunga kila kitu na kurejea Dar es salaam wakihaidi kwamba Zanzibar wangerudi kwa mara nyingine tena kwani ni kisiwa kilichotulia mno!
Safari ya kurudi haikuwa ndefu sana kwani walikata tiketi za ndege ndogo aina ya Coastal,ambapo ndani ya dakika arobaini na tano ilitua Mwalim Nyerere Terminal One!Kwa kuwa walirudi kimya kimya,hakukuwa na mtu wa kuja kuwapokea wakakodi taxi mpaka Ubungo Kibangu,ambapo huko walianza kufanya usafi wa hapa na pale sababu nyumba ilikuwa na vumbi kiasi!
‘Hajrath,nakupenda sana.Nielewe,unautesa moyo wangu’
Ilikuwa ni meseji ya mapenzi,ambayo Hajrath aliisoma asubuhi ya siku inayofuata!Hakua ana uhakika na namba hiyo lakini alianza kuhisi,hata hivyo alipata majibu ya maswali yake baada ya ujumbe mwingine kutumwa kisha chini akaona jina la Kassim,moyo wake ulipiga kwa nguvu kumbukumbu zake zikamrudisha siku ya ndoa yake,alivyonyonywa sikio!Mbali na hapo,hakutaka kuijibu meseji hiyo,akasonya na kuendelea kupika jikoni!
Hakuwa tayari kabisa kutoka kimapenzi na Kassim shemeji yake na kila alipotamani kumshtaki kwa Ahmed kuhusu usumbufu wa mdogo wake,aliogopa kuwagombanisha!

****
Duka alilofunguliwa Hajrath lilipamba moto,pesa walizopata kwenye harusi wakaongeza mtaji!Ndugu,jamaa na marafiki hawakukauka dukani, wengine walifika kumuungisha baadhi walienda kumpongeza na kuchunguza ili wakapige umbea,hata hivyo Hajrath hakujali kwenye biashara yake alikuwa mkali,mkopo hakutoa hata kidogo!
“Hajraa”
Sauti ya kiume ilisikika kutokea mlangoni,hiyo ilimfanya Hajrath ainue shingo yake kumuangalia mtu huyo!Hakuamini alikuwa ni Hillary,mwanaume waliyesoma wote sekondari!Hata yeye alionesha kushangaa,akatoa tabasamu la kirafiki.
“Hillary!”
“Ndio mimi”
Wote wakatabasamu na kupeana mikono!
“Umekuwa Mama sasa, nimesikia”
“Yeah ndio,nishaolewa tayari”
Hajrath akazungumza kwa mapozi huku akionesha kidole chake chenye pete ya ndoa!
“Kweli duu,maisha haya yanaenda kasi sana!Nilisikia,lakini nilikuwa mbali.Nilikuwa mafia kikazi,nilivyojaribu ruksa kazini.Bosi,akanibania”
“Pole mwaya,usijali kabisa”
“Hata hivyo nimekuletea zawadi,nikaona leo nipite maana nasema kesho nitapita kesho nitapita, boxi lako hilo utafungua baadaye”
“Jaamaaani,wooow!Ahsante Larri al…”
Hajrath alishindwa kumalizia sentensi yake baada ya kuona gari aina ya Alteza nje,mbaya zaidi Hillary alikuwa amemsogelea karibu yake,hali hiyo ilimfanya amsogeze Hillary pembeni lakini alikuwa tayari amechelewa kwani Ahmed alifungua mlango wa gari na kushuka!
“Hajra,una nini?Mbona umechenji ghafla?Unaumwa?”
Hillary akauliza,alichoharibu ni kumshika bega kwa niya ya kumuuliza!Ahmed alikua nyuma yake,kila kitu anakishuhudia kaweka mikono mfukoni,akajawa na wivu pamoja na jazba,hakutaka kuamini kama Hajrath angeweza kufanya jambo hilo ndani ya duka lake katika akili yake akajua kwamba mwanaume huyo anatoka kimapenzi na Hajrath,akazidi kutembea mpaka karibu kabisa huku akibana meno yake kwa hasira!
“Hillary,huyu ni mme wangu!Anaitwa Ahmed”
Kabla ya kuulizwa,akajihami kwa kuonesha msisitizo ili kupigilia sentensi yake msumari akamsogelea Ahmed karibu na kumshika kiuno!
“Oooh,Mr Ahmed nafurahi kukufahamu”
Hillary akaachia tabasamu la kulazimisha na kutoa mkono lakini matokeo yake mkono wake,ukabaki umeganda hewani kwani Ahmed hakutoa mikono yake mfukoni,akabaki anamtizama kwa macho makali mwanaume huyu anayejichekesha kama Malaya aliyeona pesa.
“Mimi naitwa Hillary,nimesoma na Hajrath”
Kabla ya kutambulishwa akajitambulisha mwenyewe kwani sura ya Ahmed ilimtisha,ilikuwa mbali na mazoea!
“Toka”
Ilikuwa ni sentensi moja iliyotoka kwa Ahmed,moyo wa Hajrath ukapiga paa akahisi tumbo linamuuma,alishaelewa nini kinachofuata baada ya hapo!
“Ahme…”
“Nawewe nyamaza,nitakuzabua sasa hivi.Hili duka sio dangulo,umenielewaa?”
Kwa sauti ya juu Ahmed akapayuka,ilikuwa ni aibu kubwa mbele ya Hillary.
“Kijana toka hapa dukani,nisikuone tena”
Sentensi hiyo ilivyoisha,akaona kiboxi cha zawadi pembeni bila kuuliza akakichukua na kumtupia Hillary, aliyekuwa mlangoni anatoka nje kikampiga mgongoni!Baada ya hapo,akamgeukia Hajrath na kumkata jicho kali la hasira!




Kilikuwa ni kitendo kilichomfanya Hajrath achukie na kukasirika kwa wakati mmoja,jambo alilolifanya Ahmed lilikuwa la kitoto na ndiyo maana alikunja sura,hakutaka kuzungumza chochote kitu!Akabaki anamtizama kwa macho makali yaliyojaa hasira,kifua chake kinapanda juu na kushuka kutokana na aibu hiyo!Hakuzungumza kitu kingine zaidi ya kukaa kwenye kiti na kuchukua simu!
“Yaani mimi naongea unachat?”
Ahmed akaibua hoja nyingine,akamsogelea Hajrath akiwa bado mwenye jazba nyingi!
“Naongea nawewe”
“Hajraa,si nakuongelesha”
Ahmed akageuka ghafla na kuwa kama dikteka kwenye mapenzi,akitaka Hajrath amsujudu jambo ambalo halikuwa rahisi kwa mwanamke nuyu ambaye tayari alikuwa nunda!
“Ulitaka nifanye nini labda?”
Hajrath akajibu kwa swali.
“Unisikilize nachoongea”
Alichokifanya Hajrath ni kuweka simu chini kisha kumtizama Ahmed!
“Aya ongea”
“Siku hizi umekuwa na dharau sana”
“Nakusikiliza,ongea Ahmed”
Ki ukweli,hakuwa na mudi ya kuzungumza alikuwa tayari kwa lolote lile ndiyo maana akamjibu Ahmed jinsi anavyotaka!Hata walivyofunga duka na kuondoka ndani ya gari hakuna hata mmoja kati yao aliyemuongelesha mwenzake!Hajrath alinuna,akaingia bafuni kuoga na kujitupa kitandani akiangalia ukuta, tofauti na siku zote!Hiyo ilimaanisha hakutaka kuguswa usiku huo!
“Geukia huku basi mke wangu”
Ahmed alizungumza kwa sauti ya chini,akiwa yupo kitandani anampapasa Hajrath akijaribu kuomba chakula cha usiku!
“Ahmed niache, nimechoka”
“Naomba nisamehee”
“Nishakusamehee mbona”
Hakugeuka nyuma,alizungumza akiwa amempa mgongo Ahmed!
“Basi geuka tuongee”
“Nakusikiliza,ongea”
“Sasa tutaongeaje hivyo?”
“Ahmed,utamuamsha mtoto amelala!Naomba niache nimechoka,sijisikii kufanya chochote”
“Usiseme hivyo,mwenzio nina hali mbaya”
Ni kweli,mnara wa Ahmed ulikuwa umesimama wima shuka alilojifunika lilituna na dawa yake ilikuwa ni Hajrath!
“Nishakwambia,sijisikii kufanya chochote!Alafu ukiendelea kunisumbua nitakuachia chumba,niende seblen”
“Najua nimekukosea,ile yote ni hasira na wivu”
“Wala usijali,nishakuzoea”
Hajrath alishikilia msimamo wake,hata hivyo hakuwa na hamu yoyote ile ya kufanya tendo hilo kwani alikuwa bado mwenye hasira na dukuduku rohoni,hiyo ilimfanya Ahmed azidi kulazimisha mwisho wa siku akapanda juu ya Hajrath kama jogoo lakini aliambulia kusukumizwa kwa nguvu.
“Ahmed,unataka kufanya nini?”
Hapo Hajrath alishikwa na hasira,akakaa kitako na kumkata Ahmed jicho kali la hasira,lililojaa chuki!Kitendo alichotaka kujaribu kukifanya kilimfanya akasirike zaidi.
“Nina hamu,angalia”
Tango la Ahmed,lilikuwa limesimama mpaka misuli ikatokeza lakini hilo halikumfanya Hajrath arudishe moyo wake nyuma,akatoka kitandani na kuuendea mlango!
“Ili nisikupe tabu inabidi niende seblen”
Ilikuwa ni wazi kabisa,bila utani Hajrath akaenda seblen na kulala!Japokuwa moyo ulimuuma lakini hakutaka kubadili msimamo wake,alivyotulia alijishangaa hata yeye mwenyewe roho hiyo ameitoa wapi wakati kipindi cha nyuma hakuwa hivyo!
Usiku wa siku hiyo kwa Ahmed ulikuwa wa tabu mno,damu yake ilimwenda mbio,akahisi kama yupo baharini anazama na kufa kwa kukosa pumzi,haikuwezekana mtu kama yeye kunyimwa unyumba!Ghafla sura ya Veronica ikamjia,mwanamama ambaye kila kukicha alikuwa analilia penzi lake!Akatafakari kwa muda lakini wazo la Veronica likayeyuka baada ya kukumbuka kwamba alinusurika kupigwa risasi!Alivyofikiria wasichana wengine wa kando akakosa kabisa,hapo ndipo akajua umuhimu wa kuwa na mchepuko!
“Laiti ningekuwa na demu sasa hivi,ningemfata!Siwezi kupata mateso ya namna hii na nitamkomesha!Subiri,nitalala hivi hivi lakini atajuta”
Ahmed,alijisemesha mwenyewe huku akisononeka vya kutosha,bado hakuamini kama amenyimwa chakula cha usiku,wakati mwingine alidhani Hajrath amekuwa kiburi na tayari kaota pembe sababu amemuoa!
“Na talaka nane zinamuhusu,huyu!Wee subiri muone”
Akasema kana kwamba anahadithia watu,kinagaubaga akajifunika huku tango lake likiwa juu limesimama hivyo hivyo kwa tabu,akapitiwa na usingizi!

*****
Saa moja kasoro asubuhi,Ahmed alitoka kitandani bila kusalimia wala kumuongelesha Hajrath alivaa nguo na kuingia ndani ya gari lake tayari kwa kuondoka!
“Pipipiiiii”
Niya ya kupiga honi ilikuwa ni Asia,atoke ili afungue geti lakini matokeo yake aliyetoka ni Hajrath!Akatembea mpaka getini na kulifungua ili Ahmed atoke!Hata hivyo ilikuwa ni tofauti na alivyotegemea sababu alijua Ahmed angefika getini angeshusha kioo na kumsabahi matokeo yake,alinyoosha mguu na kulitoa gari nje kwa kasi!Hiyo ilimuumiza sana Hajrath,akajuta kwa kitendo alichokifanya usiku wa jana, akajilaumu ni kwanini alimtesa mumewe namna ile usiku wa jana.Kwa akili ya ki utu uzima na jinsi alivyomjua Ahmed alijua fika siku hiyo ni lazima aende kutafuta mwanamke mwingine wa nje,ghafla akaanza kuhisi wivu na kumpigia simu ili aombe msamahaa lakini matokeo yake simu haikupokelewa,akajaribu kutuma meseji bila mafanikio yoyote yale!Ilivyogonga saa tatu,akamuita Asia ili amuachie maagizo juu ya mtoto na kumpa pesa kidogo ya matumizi kisha nayeye kuondoka zake kwenda dukani kwake huku kichwani akiwa na mawazo chungu mzima!
“Sasa kosa langu nini?”
Akiwa njiani,alijiuliza maswali kama hayo bila kupata muafaka wa majibu yoyote yale,akajaribu kumpigia Ahmed kwa mara nyingine lakini simu haikupokelewa,akahisi kuchanganyikiwa mawazo yaliyomjia kwa haraka kichwani ni lazima Ahmed atakuwa gesti na mwanamke, wanafanya ngono ndiyo maana hapokei simu,akatuma meseji ya kuomba msamahaa lakini hakukuwa na majibu ya aina yoyote ile!
Hesabu za dukani,hazikwenda vizuri kabisa siku hiyo na mara nyingi aliweka kichwa chake juu ya meza,akijikita kwenye mawazo!Kila kitu kilivurugika ndani ya mtima,hata alivyorejea nyumbani na kukutana na Ahmed hakusemeshwa kitu chochote kile,hata alivyojichekesha akajikuta anacheka mwenyewe!Akili yake ilifika mwisho kabisa kuwaza,akashindwa kuelewa jambo hilo amshirikishe mtu gani wa karibu ili alitatue,alipotaka kuwashirikisha marafiki zake moyo wake ukasita,akaona bora awatumie ndugu zake na Ahmed ili ajue ni kitu gani alichokifanya.Hakua na chaguo lingine zaidi ya kuanza kuisaka namba ya Kassim,bahati mbaya ikawa kwake akawa ameifuta!Hakua na jinsi zaidi ya kumsubiri Ahmed arudi usiku!Hata hivyo hawakuongeleshana,akamngoja aingie bafuni kuoga,akachukua simu na kuziingiza kwenye simu yake!
“Sasa, tutaishi hivi mpaka lini?”
Hajrath akauliza,vitimbwi vya mumewe vilimfanya aulize!Hilo halikumfanya Ahmed ajibu,akabaki kimya akapitiliza mpaka kwenye kitanda na kulala chali.
“Mme wangu”
Hajrath akaita lakini kukawa kimya,alichokifanya Hajrath ni kuvua nguo na kupanda kitandani,hapo alilala akiwa na mawazo mengi sana! Kulivyokucha asubuhi na mapema akamtafuta Kassim hewani.
“Kassim,mambo”
Hajrath alianza salamu baada ya ukimya kutokea, simu ilivyopokelewa!
“Hajrath,ni wewe!?”
“Ndio, za masiku?”
“Poa tu,niambie”
“Nina shida nawewe”
“Namimi?Mimii umesema?”
Kassim,akauliza kama mtu asiyeamini kile anachosikia,kila kilichotokea siku hiyo ulikuwa kama muujiza mkubwa sana kwake,kupigiwa simu na Hajrath!
“Ndio wewe”
“Shida gani?”
“Kwanza nataka kuonana nawewe”
“Lini?”
“Hata leo kama upo frii”
“Mimi nipo frii hata sasa hivi”
“Lakini nisikilize,yale mambo yako mimi sitaki.Sipo huko kabisaaa,kama upo frii tukutane sijui wapi?”
“Njoo hata geto kwangu”
“Huko siwezi kuja”
“Aya,tukutane Mkuki house pale Pizza Hutt”
“Ndio wapi?”
“Ukifika Kamata,niambie nitakuelekeza”
“Aya,ahsante sana”
Hakua na chaguo lingine zaidi ya kumshirikisha Kassim, kwenye jambo hilo linalomsumbua kutoka moyoni mwake,alielewa kabisa Kassim ndiye suluisho la tatizo hilo ingawa alikuwa akimsumbua na kumtongoza!Baada ya kila kitu kukamilika,akajiandaa vizuri huku nyuma akiacha maagizo ya mtoto na pesa kidogo ili ikitokea dharura aambiwe mapema,alivyohakikisha kila kitu kipo sawa!Akatoka nje na kutafuta daladala za kwenda Mnazi mmoja,akiamini huko ingekuwa rahisi kwake kufika sehemu inayoitwa Kamata!Akiwa njiani aliwaza vitu chungu mzima, hususani juu ya kuanza kuzungumza na Kassim,angeanzia wapi? Alielewa kwamba angefunguka kila kitu lingekua kosa kubwa sana tena la jinai kwani kwao alifundwa mambo ya ndoa asiyatoe nje!
Alivyofika Mnazi mmoja,akateremka na kumlipa kondakta pesa yake kisha kuanza kutizama huku na kule,kwa kipindi kirefu sana hakufika eneo hilo!Mabadiliko makubwa yalimshangaza,hususani magorofa yaliyopanda juu kabisa.Alichokifanya ni kutembea mpaka kandokando kidogo ambapo kulikuwa na pikipiki zimepaki pamoja na bajaji, zilizokuwa zinawasubiri abiria wenye haraka kama yake,jua lilikuwa kali na linachoma mno hiyo ilimfanya atoe leso na kujifuta jasho lililokuwa linamtoka!
“Sista,bajaji hii ina Ac mwanzo mwisho,njoo tuondoke”
Dereva mmoja,akainadi bajaji yake kwa kuongeza chumvi, baada ya kumuona Hajrath anaelekea upande huo!
“Nataka niende hapo Kamata”
“Kamata sehemu gani? Pale mataa?”
“Nooo! Subiri kidogo”
Hakuwa ana uhakika na sehemu anayoenda,alichokifanya ni kumpigia Kassim simu ili apate maelekezo ya kina,alivyokata simu baada ya maelekezo akamtizama dereva!
“Mkuki House”
“Anhaa,twenzetu”
Hajrath akaingia ndani ya bajaji huku nyuma akiwaacha wanaume wenye uchu wakim-mezea mate,kutokana na mzigo aliofungasha nyuma!
“Oyaaa,chukua namba.Usiyumbee mzee baba kazi hiyo”
Mmoja wa madereva,akatupa neno hilo!Bajaj,aliyopanda Hajrath ikaanza safari ya kuondoka ambapo ilipita,mtaa wa Kongo mataa na kukunja kushoto ikanyoosha moja kwa moja!
“Umesema,Mkuki House dada?”
“Ndio,Mkuki house”
“Pale pale nje”
“Ndio hapohapo,alafu hujaniambia bei”
“Hapo buku tatu tu”
Hakukuwa na maongezi mengi ya ziada,walivyofika nje ya jengo hilo refu Hajrath akashuka na kumlipa dereva ujira wake huku nyuma akimuacha anamtizama jinsi anavyotingishika kwa nyuma,suruali ya ‘jeans’ aliyovaa ilifanya watu wote macho yawe kwake!Muda,haukuwa rafiki tena akachukua simu na kumtafuta Kassim hewani.
“Mimi nipo ndani tayari”
“Sawa,nakuja nipo nje”
Kwa Hajrath ndiyo ingekuwa mara yake ya kwanza kufika katika jengo hilo,lililokuwa zuri kwa nje!Mtu yoyote wa hali ya chini,angeogopa kulisogelea jengo hilo akidhani wenda kuingia na pesa lakini ilikuwa ni bure!Alivyoingia ndani,akakumbana na kiyoyozi kikali hali ya hewa ilikuwa safi na wengi waliokuwa ndani ya mkahawa huo,walikuwa wazungu na waarabu,alivyopiga jicho kulia mwisho akamuona Kassim akimpungia mkono,akamsogelea mpaka alipo!
“Karibu,karibu sana”
Kabla ya Hajrath kukaa,Kassim hakutulia moyo wake ulimwenda mbio hakutaka kuamini kama aliyesimama ni Hajrath,mwanamke aliyetokea kuunyanyasa mtima wake kwa siku nyingi sana!Leo iweje ajilete mwenyewe tena akitaka mazungumzo,kichwani alijiuliza maswali mengi sana ni mazungumzo ya aina gani huku akianza kumkagua kuanza usoni jinsi alivyojiremba vizuri,topu aliyovaa iliyobeba maziwa yake madogo kiasi,akazidi kushuka chini na kupagawa na kiuno kilichonyooka na kutenganishwa na ‘hips’ iliyojichora namba nane,akashusha pumzi ndefu na kutoa tabasamu la kirafiki!
“Karibu ukae”
“Ahsante Kassim,umekuja muda sana?”
“Ah wapi,nimeingia sasa hivi!Kwangu mimi hapo mbele”
“Unaishi mwenyewe?”
“Yeah,nimepanga Kurasini.Wee si hutaki kuja,usinifanyie hivyo bwana,nishakuwa siku hizi!Sina yale mambo”
Kassim,alitengeneza hoja akionekana keshapotezea na hapo alipo,hana hisia zozote na Hajrath!
“Sijui nianzie wapi?Kwanza,nisamehee kwa kila kitu kilichotokea nyuma”
“Usijali,never mind!Kila kitu,kipo okay.Just forget ngoja nikaagize pizza,unakunywa soda gani?”
Ili aonekane ana swaga Kassim akachombeza maneno akiingiza na ung’eng’e!
“Sprite ya baridi”
“Okay”
Kassim,akasimama na kuvuta ‘jeans’ yake juu kidogo akaweka t shirt yake vizuri akaelekea upande wa juu!
Maongezi yalitakiwa yafanyike siku hiyo ili Hajrath ajue nini hatma yake lakini matokeo yake,ikashindikana simu kutoka kwa Asia kwamba mtoto analia sana ilimfanya aghaili kila kitu,wakapanga siku nyingine ama ikiwezekana baada ya siku mbili zijazo!
Jambo hilo lilimfanya Kassim akasirike kwa kiasi cha kutosha lakini alijesemea moyoni ipo siku Hajrath atajaa ndani ya kumi na nane zake,kuanzia siku hiyo walianza kuwasiliana rasmi wakiwa kama marafiki,licha ya kupanga wakutane kila siku lakini ilipita wiki nzima bila kuonana!
“Sasa utaniona lini?Mimi nasafiri keshokutwa”
Kassim siku hiyo alipima maji!Baada ya kupigwa kalenda kila siku iendayo kwa Mungu!
“Utarudi lini?”
“Naweza kukaa mwezi mzima”
“Nitajitahidi kesho tuonane,popote pale Kassim! Pole kwa usumbufu”
“Usijali,ukishindwa kesho basi hutoniona”
Moyo wake ulidunda mara mia moja kwa sekunde baada ya kusikia siku inayofuata,ataenda kuonana na Hajrath angejisikia amani sana kama angekutana na mwanamke huyo ambaye alimfananisha na Malaika,akaenda mbali zaidi na kuapia angempindua kaka yake, hata kama bifu na undugu ufe ilimradi Hajrath awe wake,aliwaza vitu vingi mno mpaka akashindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani aliyokuwa nayo!
Kulivyo pambazuka siku hiyo,akafanya usafi wa kina,akadeki kila mahali akafuta vumbi lote,akatumia masaa mawili kulipamba geto lake!Alivyoliangalia akastaajabu,haikuwahi kutokea geto lake kuwa safi namna hiyo,akajipigia makofi na kushangilia!Alivyoingia jikoni,akaona kuna vitu vimepungua akaenda dukani na kununua baadhi ya vyakula ili Hajrath akija ampikie wale!Hesabu zake,zilikuwa ndani ya muda sababu ilivyogonga saa sita na nusu,simu yake ikaita!
“Ndio natoka hivyo!Kurasini sehemu gani?”
“Ukifika Uhasibu nipigie simu”
“Sawa,nitafika hapo muda sio mrefu”
“Poa poa”
Mwili wa Kassim,ukasimama kama miba ya nungunungu!Mwili wote ukapata joto la ghafla,akaanza kuvuta picha jinsi Hajrath atakavyofika, aanzie vipi kuingizia gia zake ili amle mtoto aliyejileta mwenyewe kwenye anga zake!
“Sijui nimuwekee madawa?No,hapana.Nitatumia sound zangu mwenyewe,mbuzi kafia mwenyewe kwa mpika supu!Inabidi nitembelee gia kubwa leo”
Kassim,aliwaza na kupanga mikakati ya namna atakavyomuingia Hajrath,alimuelewa ni kwa namna gani mwanamke huyo alivyokuwa mgumu mwenye msimamo mkali katika mapenzi,hata hivyo alijipa moyo kwamba lazima angemvua samaki huyo bila ndoano!Dakika ishirini na tano baadaye,akapokea simu kutoka kwa Hajrath!
“Nishafika,nipo stendi hapa Uhasibu”
“Maraa hii?!”
“Hakuna foleni”
“Sasa,hapo inabidi uchukue boda boda!Mtafute bodaboda yoyote hapo karibu mpe simu”
Ukimya,ukapita wa kama sekunde tano!Hajrath akarudi kwenye laini!
“Ongea na boda boda huyu hapa,shika kaka!”
Dereva wa pikipiki akapewa simu ili apewe maelekezo!
“Kiongozi vipi mambo?”
“Freshi tu,sasa sikiaaa…”
“Eeeeeeh….”
“Kabla ya kufika Sabasaba hapo,unaingia kushoto!Unaujua msikiti wa Chaurembo?”
“Yes,naujua”
“Enhee,mbele kuna mgahawa hapohapo!”
“Poa mkuu”
Dereva wa pikipiki baada ya kupata maelekezo,akamtaka Hajrath apande kwenye pikipiki!
“Ni mbali sana kaka?”
Hajrath akauliza huku akipandisha sketi yake juu kidogo ili apande,mapaja yake yakaonekana dereva wa bodaboda akampiga jicho la uchu!
“Hapana,hapo mbele tu.Jishike vizuri njia ina mashimo”
Safari ikaanza mara moja,hawakutumia dakika tatu wakawa tayari wamefika Hajrath akashuka na kumpa dereva pesa yake,alivyoangalia nyuma akamuona Kassim anamuangalia!
“Nilijua utapotea”
“Ningepotea kweli ujue njia zinachanganya”
“Karibu ni huku”
“Tunatembea tena?!”
“Hapo nyuma tu”
Mguu kwa mguu,Mbele Kasim nyuma Hajrath mpaka nje ya nyumba kubwa kiasi,ambapo nje kulikuwa na geti la grili!Wote wakaingia ndani,ambapo hapo Hajrath alipata nafasi ya kuangalia seble ya Kassim ilivyopangiliwa vizuri ukutani kaweka ‘wallpaper’ za kisasa,ilikuwa ni seble ndogo lakini yenye kila kitu cha muhimu ndani!
“Nikuletee nini mgeni?”
“Maji ya baridi”
Kassim kwa mbwembwe na mikogo akatembea mpaka kwenye ‘water dispenser’ yaani mashine maalum ya kuwekea maji ya kunywa,akabinya na kumsogezea Hajrath!
“Ndio nilikua napika pika hapo jikoni”
“Unaweza kupika wewe?”
“Kwanini nisiweze?”
“Unapika nini?”
“Ugali kuku”
“Mmmh,utaunguza hakuna mpikaji hapa”
“Njoo uone”
Moja ya gia namba moja ikakubali kuingia,hiyo ilikuwa mipango ya Kassim kumzoea kwanza Hajrath,akafanikiwa kumuinua kutoka kwenye kochi, wakaingia jikoni!Ambapo kulikuwa na jiko la gesi la mchina,kuku wamebandikwa!
“Kassim,ndio nini sasa?Una Royco?”
“Ndio”
“Leta na maji”
Hajrath,akaingia jikoni kupika!Akasonga ugali na kuuweka mezani,wote wakaanza kula huku wakicheka kwa furaha!Mtihani,uliofuata ni kumtoa Hajrath kwenye kiti mpaka chumbani hapo ndipo kimbembe kilipokuwa,alifikiria mpaka basi hata hivyo alipata jibu alivyokunywa maji,akaingia chumbani ambapo huko alichukua stuli,akapanda juu na kutoa balbu ya chumbani!
“Hajraaaa”
“Beee”
“Nakuomba mara moja”
“Wapii?”
“Wee njooo”
Hajrath akasimama kidogo akachungulia na kuona mlango wa chumbani,upo wazi!
“Njoo,kuna kitu unisaidie”
“Kitu gani Kassim?Usianze balaa lako!Siwezi kuja huko”
“Njoo unishikie stuli hapa,niweke taa mara moja tu”
Kwa hofu Hajrath akatembea mpaka chumbani,huko kulikua na kitanda stuli ipo katikati!
“Nishikie stuli nipande,nibadili hii klopu imeungua”
Kassim akapanda juu,Hajrath ameshika stuli!Lakini katika hali ya kushangaza na kushtua,Kassim akashuka kwa kasi na kumshika Hajrath kiuno kabla ya kujinasua,akawa amechelewa tayari kwani shingo yake ilinyonywa na kulambwa,ikamfanya ajikunje na kuishiwa nguvu kabla ya kujibu chochote mkono wa Kassim ukawa tayari umeshika kifua,unapapasa maziwa huku mwingine taratibu akiyapeleka chini kwenye mgodi!
Hajrath alijitahidi kufanya anachoweza ili kujitoa lakini hisia zake zilikuwa karibu,akashindwa kabisa akatupwa kitandani puuu!Kassim,akapanda juu yake akaanza kumpiga madenda huku akimvua nguo moja baada ya nyingine kwa kasi,alivyoifikia sketi akashika na chupi kwa pamoja akavishusha chini,bila kupoteza muda akaipanua miguu ya Hajrath huku na kule akatoa ulimi wake na kuanza kupiga deki bahari.
“Aaasssshhhsssss mmmmh”
Hajrath akaguna,kumaanisha hajiwezi tena!
“Kasiiiim,Kaassssimm. Ngooo!Ngooo! Ngo Ngoo Ngoooo”
Kelele za mlango zilimshtua Hajrath kwa mbali aliyekuwa hana nguo hata moja yupo chali,analambwa mgodi akatulia kidogo na kumsukuma Kassim aliyemganda!Hata hivyo kilichomuogopesha ni sauti anayoisikia!
“Kuna mtu anaaagongaaa”
Hajrath akasema kwa sauti ya chini!
“Kassim,uko wapi?”
Sauti hiyo ikazidi kusogea karibu ikikaribia kuingia chumbani,moyo wa Kassim ukapiga kwa nguvu kwani sauti hiyo ilikuwa ya kaka yake Ahmed,alitetemeka kwa kiasi cha kutosha,akaruka kama swala mpaka mlangoni,akakutana na Ahmed mlangoni,yaani angechelewa kidogo tu Ahmed angeingia chumbani kwani waliacha mlango wazi!
“Vipi dogo?Mbona nagonga muda mrefu hufungui?”
Ahmed akauliza kwa jazba!Kuna kitu Kassim alijifunza kupitia macho ya kaka yake,kulikuwa kuna kila dalili mbaya ya fumanizi siku hiyo na kivyovyote vile Ahmed alifika hapo kwa ajili hiyo!Hajrath aliyekuwa chumbani alihisi tumbo linamuuma jasho linamtoka akavuta sketi,taratibu akajichomoa kitandani na kujificha kando kando ya kabati ana sali sala zote anazojua.
“Kuna jambo nataka kuongea nawewe na uniambie ukweli”
Ahmed,akaongea kwa kufoka hiyo ilimfanya Kassim azidi kuhaha,akijua tayari moto unawaka siku hiyo kwani alizielewa vurugu na hasira za Ahmed, hasa linapokuja swala la mapenzi!



Jasho jingi lilimtoka mwilini,moyo wake ulimwenda mbio na alihema kwa wasiwasi mkubwa!Alielewa nini maana yake endapo Ahmed angeingia chumbani na kumkuta,ilikuwa ni bora ukutane na simba mwenye njaa kuliko Ahmed akiwa mwenye hasira!Akiwa,kandokando ya kabati ameshika nguo zake,alijuta kwa kiasi cha kutosha, kitendo cha kufika kwa Kassim na kumkubalia amvue nguo kilimfanya ajute kupita kiasi,wakati mwingine alianza kujiuliza maswali ilikuaje mpaka akavuliwa nguo wakati alikuwa ni mtu mwenye msimamo mkali,mbaya zaidi angewagombanisha ndugu hawa wawili waliozaliwa tumbo moja!Sala zote anazojua yeye alisali siku hiyo na kupiga dua za kila aina akimuomba Mungu isitokee Ahmed akaingia ndani ya chumba hiko kwani hisia zake zilimwambia ni lazima Ahmed alifika mahali hapo ili kuwafumania isitoshe anajua kila kitu!Swali lililokuja kichwani kwake ni amejuaje?Au alisoma meseji?Alijiuliza na kujijibu mwenyewe huku akiwa makini kumsikiliza Ahmed akiwa na Kassim mlangoni,maongezi yao aliyasikia vizuri sana na yalimtisha kwa wakati mmoja!
“Jambo gani?”
Kassim akauliza kwa hofu,sura ya Hajrath aliyekuwa chumbani ilimjia hata yeye aliogopa endapo Ahmed angeingia chumbani kwake kupiga msako,siku hiyo angemezwa mzima mzima bila kutafunwa hilo alilijua ndiyo maana hofu ilimtanda mno.
“Kuna mwanamke umemtia mimba,Maza ameniambia nije kuongea nawewe!Wazazi wake wanakutafuta”
Lilikuwa ni jambo la kushtusha lakini sio sana kama uzito wa Hajrath kukutwa ndani ya chumba chake,hiyo ilimfanya ashushe pumzi kidogo na kumtizama Ahmed!
“Nani?Demu gani?”
“Sada,pale jirani”
“Ndio alivyokwambia?”
“Maza,ameniambia!Juzi nilikuwa nao pia,walitaka kuja hapa nikawaambia wasifanye hivyo ngoja nije kwako kwanza”
“Kama kuhusu hilo,mimi shega tu!Nitaonana nao”
“Dogo kua makini,kama mimba yako kweli.Usikane”
“Broo mimi sijakana mimba sema yule demu,nishai sana miyeyusho kishenzi”
“Ndio ana mimba yako sasa”
Wakati Kassim akizungumza hayo,alikuwa akifanya jitihada za kumtoa Ahmed waende seblen kwa staili ya kutangulia yeye mbele,wakafika mpaka seblen!Moyo wa Ahmed ukapiga paa baada ya kuona mkoba wa rangi ya kaki,hakua ana uhakika kama wa Hajrath ama aliufananisha,akagandisha macho yake kwa muda kisha kumgeukia Kassim!
“Alafu kumbe una demu ndani,si ungeniambia tu!Endelea,nitakupigia simu baadaye”
“Poa,nitakuja ofisini kwako hata hivyo tuongee vizuri”
“Njoo nyumbani leo usiku,tutaongea”
Kuanzia hapo Ahmed hakuwa na sababu nyingine ya kubaki,akatoka nje na kuingia ndani ya gari huku nyuma akimuacha Kassim dirishani anachungulia mpaka alivyohakikisha gari limepotea kwenye upeo wa macho yake,ndipo akafunga mlango na funguo, kwa kasi akaingia chumbani!
“Hajraaaa”
Akaita,hiyo ilimfanya Mwanamke huyo atoke haraka kabatini na kuanza kuvaa nguo kwa kasi ya ajabu,hakuamini kama ameponea kwenye tundu la sindano!
“Sasa unaenda wapi?”
Kassim akauliza!
“Naenda kwangu,Kassim niache kwanza!Siwezi kukaa hapa tena”
“Hakuna kilichoharibika tumalizie”
“No,niache niende zangu!Hapana hapana hapana,sitaki”
Msimamo wake ulikuwa pale pale,hakukuwa na uwezekano tena wa kubadili maamuzi aliyochukua tayari,Kassim akashindwa kumshawishi ndege huyu mzuri abaki ili amnyonyoe mabawa,kila alipojaribu kumuimbisha hakufua dafu!Hajrath,akabeba mkoba wake na kuchukua viatu chini ya kiti,haraka akatoka zake nje na kutafuta pikipiki ambayo ilimpeleka mpaka nyumbani kwake Ubungo Kibangu,bahati nzuri hakumkuta Ahmed!
“Baba alirudi?”
Swali hilo alitupiwa Asia.
“Hapana”
“Tangu alivyotoka asubuhi?”
“Ndio hajarudi”
“Babrah,yuko wapi?”
“Amelala”
“Akiamka niambie,nipo chumbani”
Alichokifanya Hajrath ni kuingia moja kwa moja chumbani,akajitupa kitandani na kupumzika huku akitafakari hatari aliyonusurika muda mfupi uliopita!

******
Mikausho ya Ahmed kwa mkewe ilizidi kiwango chake,wiki nzima hakumuongelesha hata kidogo alinuna lakini aliacha kodi ya meza yaani pesa za matumizi mezani kila siku!Siku hiyo akiwa ofisini,amenyonga tai shingoni kavaa shati jeupe simu moja ilimshtua,ikamfanya akae vizuri kwenye kiti!
“Umesema,wewe nani?”
“Waziri mkuu Isaack Nyaulingo”
“Ndio nani?”
“Waziri wako mkuu, humjui?”
“Namjua”
“Ndio mimi hapa,njoo kesho Magogoni!Saa nne kamili,usikose Ahmed”
Simu ikakatwa,ikimuacha Ahmed anatizama simu yake haamini kama kapigiwa simu na Waziri mkuu,ni kweli sauti hiyo haikuwa ngeni kwani mara nyingi huisikia kwenye vyombo vya habari!Kilichomfanya aamini ni kweli Waziri Mkuu Mh.Isack Nyaulingo ni baada ya kumkumbuka Ruth hapo ndipo akapata jibu la waziwazi,swali lililobaki alikuwa anataka nini na kuna mazungumzo gani!Hata hivyo siku hiyo alifanya kazi kama ratiba yake inavyotaka,akarudi nyumbani na kuingia chumbani!Akamkuta Hajrath,amelala akavua nguo na kuingia bafuni ili aoge,alichokiona bafuni kilimfanya atabasamu!
Juu ya sinki kulikuwa na maua pamoja na kadi zilizoandikwa ‘I’m sorry my Husband’ pembeni kuna saa nzuri,wallet,tisheti na viatu aina ya NIKE,ilikuwa ni ‘surprise’ iliyomfanya Ahmed alengwe na machozi kwani vitu kama hivyo alizoea kuviona kwenye filamu za kifilipino!Siku hiyo alifanyiwa na Hajrath mke wake wa ndoa,swala la kuoga akaliweka kwanza kando akarudi chumbani na kumtizama Hajrath kwa macho fulani yaliyoonesha majuto kwa mambo aliyofanya,akasogea karibu!
“Nakupenda mke wangu”
Ni maneno aliyosema Ahmed,akiwa wima amesimama hiyo ilimfanya Hajrath afumbue macho,aachie tabasamu mwanana akatoka kitandani na kumkumbatia mumewe kwa furaha,wakapigana mabusu na kuanza kutomasana kwa hisia kali sana!
“Nakupenda Ahmed”
Hajrath,akanong’ona kimahaba na kumbusu sikioni Ahmed!
“Nakupenda pia”
“Twende bafuni tukaoge”
Kilichoendelea huko hakika ilikuwa ni furaha iliyozidi kifani,wote walikuwa watupu bila nguo hata moja mwilini,wanabadilishana mate!Kwa kuwa kila mtu alijua ni wapi udhaifu wa mwenzake ulipo hakukua na haja ya kuulizana,chuchu za Hajrath zilitomaswa vizuri na kulambwa vibaya mno!Koni ya Ahmed,ilichuliwa ipasavyo na kunyonywa shingo kwa kiasi cha kutosha!Kila mtu alikuwa na kibarua cha kumpapasa mwenzake anapopajua yeye,mpaka pale Hajrath mwenyewe alipolisogelea ‘sink’ na kulishika,Ahmed akaelewa nini maana yake akamshika kiuno na kumuingiza nyoka pangoni kilichofuata hapo ilikuwa ni miguno na mihemo ya raha,mpaka walivyomaliza tendo hilo na kuoga iliwachukua dakika arobaini na tano nzima!
“Jifunike vizuri Love”
Ahmed akasema huku akimfunika Hajrath vizuri wakiwa ndani ya shuka moja bila nguo yoyote ile ndani!
“Sawa”
Wakajifunika na kukumbatiana,Hajrath akaweka kichwa chake juu ya kifua cha Ahmed huku mkono wake mmoja ukiwa juu ya kifua pia,anadeka kimahaba!
“Leo nimepigiwa simu baby,sijui matapeli wale”
“Na nani?”
“Jamaa kasema yeye waziri Mkuu,matapeli bwana alafu sauti kama waziri.Kweli bongo nyoso”
“Hahahahaha,akasema nini?”
“Niende Magogoni kesho kuna mazungumzo”
“Wakuteke huko baby,matapeli hao baby!Kua makini”
Jambo hilo hata Hajrath halikumuingia akilini hata kidogo,haikuwezekana hata kidogo kwa Ahmed kupigiwa simu na Waziri mkuu kwani hata Mjumbe wa nyumba kumi hajawahi kumpigia,jambo hilo akalipuuzia lakini akaanza kulitilia maanani baada ya kuamka asubuhi na mapema na kukuta ujumbe mfupi kutoka kwa Ruth,akimsihi asikose saa nne asubuhi ya siku hiyo!Kwa kuwa Hajrath alikuwa amelala bado hakutaka kumsumbua, alichokifanya ni kupiga simu moja kwa moja ofisini akiwataarifu kwamba asingefika siku hiyo kwani ana changamoto za kifamilia!Hakutaka kufanya siri,akamueleza Hajrath kila kitu na alivyotumiwa meseji!
“Wamenitumia meseji hapa”
Amed hakutaka kusema aliyetuma meseji ni nani,akasingizia imetoka ofisi ya waziri mkuu!
“Basi itakuwa kweli”
“Kwahiyo niende?”
“Nenda Baby”
Mapigo ya moyo ya Ahmed yalipiga bila mpangilio,hakuelewa ni kwanini hali hiyo imemtokea siku hiyo lakini alivyotulia akagundua kwamba ana kitete cha kuonana na mtu mzito kutoka serikalini,jambo ambalo hata siku moja hakuwahi kuliota katika maisha yake!Hakuelewa avae nini lakini alipewa wazo na mkewe,akalichukua kama lilivyo!Mwisho wa siku akaonekana mtanashati,suruali ya kadeti,shati jeupe alilochomekea na koti jeusi vilimfanya awe nadhifu na kuendana na ofisi anayoenda!
“Mimi naenda,muda unakimbia kweli”
“Unazijua hizo ofisi zilipo?”
“Magogoni,pale nyuma ya Ikulu!Ofisi ya waziri mkuu naijua ilipo”
“Sawa baby,kila lakheli!Utaniambia kinachoendelea huko”
“Okay”
Ahmed akaondoka akiwa na mawazo chungu mzima kichwani,hata alivyoendesha gari barabarani alikuwa akiwaza vitu vingi sana,hakuelewa kwanini anaitwa na mwanasiasa mkubwa namna hiyo lakini alivyotuliza akili,akaanza kuhisi wenda ni sakata la kutekwa kwake lilikuwaje hata hivyo hakutaka kuyapa mawazo hayo kipaumbele sana, kilichotakiwa hapo ni kweli kusikiliza wito na kuwa tayari kwa lolote lile!Ndani ya dakika sitini na mbili alikuwa nje,ameshawasili Magogoni akaegesha gari kando na kutoka nje.
“Unaelekea wapi?”
Askari mmoja wa usalama,akahoji baada ya kumuona Ahmed ameegesha gari eneo hilo karibu na ikulu.
“Ofisi ya waziri Mkuu”
“Unaijua ilipo au unajiendea endea tu kama una tafuta gesti?”
“Ndio napajua”
“Una miyadi naye?”
“Ndio”
Askari hakuwa na swali lingine la ziada zaidi ya kumruhusu apite,ambapo huko alikutana na kimlango kidogo maalum akaambiwa atoe vitu vyote vya chuma kuanzia wallet saa na mkanda,kila kitu kikaenda sawa akaandikisha jina lake na kusema kilichompeleka!
“Jina lako Ahmed Kajeme umesema?”
Msichana wa mapokezi akauliza huku akikagua daftari lenye orodha ya wageni wanaotakiwa kuonana na waziri mkuu siku hiyo!
“Ndio mimi”
“Tunaomba kitambulisho chako”
“Kipi?”
“Chochote kinachotambulika na Serikali”
“Hata Leseni?”
“Hiyo itafaa,nipatie”
Hakukuwa na shida yoyote baada ya kukabidhi akapewa kadi yenye namba na kukaribishwa ndani!Ilikuwa ni sehemu yenye ukimya wa hali ya juu sana,mpaka alivyofika mlango alioelekezwa na kuingia!
Mbele yake kulikuwa na ofisi kubwa sana,moyo wake ukapiga kwa nguvu baada ya kumuona Waziri Isaack Nyaulingo, mubashara! Kando kando yake aliketi Ruth hapo ndipo akaamini kweli Ruth alikuwa ni mtoto wa Waziri mkuu na haikuwa kanjanja hata kidogo,akakaribishwa vizuri kwa uchangamfu mkubwa jambo lililomfanya ajisikie ni binadamu kamili!
“Karibu kiti Ahmed”
Ruth akasema tena!Hapo hapo waziri mkuu akainua mkonga wa simu!
“Leta Kahawa”
Alivyoweka mkonga chini,akamtupia macho Ahmed!
“Ondoa shaka kabisa ni mambo ya kawaida!Nataka kufahamu vitu fulani fulani,utakuwa umenisaidia sana Ahmed”
Waziri mkuu alizungumza kwa upole na maneno ya ushawishi mkubwa sana!
“Upo tayari kunisaidia?”
“Yes nipo tayari”
Alivyojibu hivyo mlango ukafunguliwa na kuwekewa kahawa mezani kwake na mmoja wa wafanyakazi wa ofisi hiyo!
“Nadhani mnafahamiana vizuri na Ruth?”
“Ndio”
“Mlikutana wapi?”
Lilikua ni swali la mtego,lililomfanya Ahmed akumbuke msitu wa kifo ambao aliufananisha na Jehanam!Akamtizama Ruth kwa kitambo na kutamani kuzungumza kitu,alivyokumbuka alivyoonywa juu ya kusema chochote akabaki kimya!
“Najua unaogopa kuzungumza,tusipoteze muda!Ruth aliniambia mlikutana msituni,ukamsaidia!Nachotaka kufahamu,ulifikaje kule?”
“Kule msituni?!”
“Ndio,ulifikaje?Ilikuwaje?Unaweza kukumbuka?”
Hakika alikuwa katika wakati mgumu kuliko kawaida,hakua ana uhakika kama aliyekuwa mbele yake anamjaribu ama alikuwa siriazi,hofu ya kifo ilimtanda baada ya kukumbuka namna ya watu waliomteka walivyokuwa wanatisha hawana sura za mchezo hata kidogo!
“Nahitaji kuwashikilia waliohusika kwa njia moja ama nyingine,nahitaji vyombo vya dola vifanye kazi yake!Ahmed ukiendelea kuwaficha,kesho watakusumbua tena watalisumbua taifa letu!Tafadhali niambie ukweli”
“Ninaogopa hapa nilipo Mheshimiwa Waziri Mkuu,nimetishiwa uhai wangu”
“Sikiliza kijana,nitakupa ulinzi wa kutosha na hakuna mtu yoyote atakayejua!Mengine niachie mimi”
“Naogopa sana”
“Naelewa,nachotaka kujua hawa wanaharamu ni akina nani?Tafadhali,nitakupa zawadi kubwa sana”
Ahmed,akabaki njia panda akamtizama Ruth anayetia huruma hata yeye ilielekea alitaka Ahmed azungumze ukweli.
“Mke wangu ndiye aliyehusika”
“Mke wako?!”
“Hapana,aliyekuwa mke wangu pamoja na pamoja na na na na yule Bilionea George Charles”
Waziri Isack,aliganda kidogo na kumuangalia Ahmed mara mbilimbili,jina la Bilionea George Charles lilimtisha kwani alielewa ni mtu wa aina gani,kumshika bilionea George Charles kulimaanisha kuitingisha nchi ya Tanzania,hata hivyo hakutaka kuonekana anatetereka!
“Kivipi?Ilikuaje?”
“Naomba nifupishe,alikuwa na mahusiano na Mke wangu,akamzalisha bila mimi kujua!Nilivyogundua,ikatokea vurugu kubwa, siku hiyo nipo nyumbani kwangu ikaja diffenda ya polisi kunichukua akiwemo huyo Mke wangu na George Charles,nikajua labda wananipeleka kituoni!Kumbe haikuwa hivyo,matokeo yake nikafunikwa kitambaa nikajikuta nipo kwenye huo msitu”
Hadithi hiyo ilimsisimua sana Waziri Isack na kusikitika kwa wakati mmoja,moyo wake ulimuuma na akapandwa na hasira kwa wakati mmoja!Bila kuuliza kitu kingine chochote,akainua mkonga wa simu!
“Naomba niunganishe na ofisi ya Rais,sasa hivi!Baada ya hapo,nahitaji kufanya Press conference na waandishi wa habari mpigie IGP mwambie namuhitaji ofisini kwangu,sasa hivi”
Yalikuwa ni maelekezo mafupi lakini mazito mno,hiyo ilimfanya Ahmed atetemeke hasa alivyosikia Rais anapigiwa simu,picha lililomjia ni kwamba Bilionea George Charles hakuwa mtu wa kawaida ndiyo maana hata Rais akashirikishwa!
“Rais yupo kwenye laini”
Upande wa pili wa simu ukasikika,kumaanisha Waziri Isaack anatakiwa kuzungumza!
“Nahitaji kuzungumza nawewe mheshimiwa Rais”
“Sawa,kwenye simu?”
“Hapana,naomba nije ofisini kwako”
“Njoo baada ya dakika ishirini”
“Ahsante”
Waziri mkuu alivyokata simu,akamtizama Ahmed!
“Ahsante Ahmed,nitajie akaunti namba yako!Ili uingiziwe shilingi milioni Mia moja hamsini sasa hivi kama ahsante,hujui ni kwa namna gani umeisaidia serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,nakuhakikishia hawa watu wote waliohusika tunaenda kuwakamata leo leo tukianza na George Charles”
Mapigo ya moyo ya Ahmed yakaacha kudunda kwa muda,akahisi kama amepalalaizi baada ya kusikia anaingiziwa kiasi cha shilingi milioni mia moja hamsini kwenye akaunti yake,zilikuwa ni pesa nyingi mno kwake kuzimiliki kwa mkupuo, kwa upande wake ikawa ni sawa na kulala maskini na kuamka tajiri!



Kuanzia wakati huo simu zilipigwa,huku na kule!Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akapewa picha nzima na jukumu la kumuweka chini ya Ulinzi bilionea George Charles akapewa IGP,hilo halikuwa gumu kufanyika saa kumi ya jioni siku hiyo Bilionea George Charles alikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi akiwa uwanja wa ndege anataka kusafiri kwenda nje ya nchi,jambo hilo lilimshtua mno akashindwa kuelewa ni kitu gani akifanye lakini alivyofikishwa kituoni akasomewa mashtaka yake,alihisi kujuta na kumlaumu sana Yusrath kwa kumshikia akili zake!Baba yake alipojaribu kumkingia kifua hakuweza sababu Serikali ilichachamaa hakua na jinsi zaidi ya kusema kila kitu kilivyoenda!
Hakupinga,alikiri kosa lake na kufanya kesi hiyo iwe rahisi sana,siku inayofuata Yusrath alitafutwa na kufunguliwa tena kesi nyingine akawa ana kesi juu ya kesi!Maaskari walioshirikiana kumteka Ahmed walivyotafutwa walikana lakini haikuwa rahisi sababu George Charles alikuwa na kamera nyumbani kwake pamoja na kinasa sauti,ushahidi ukakamilika baada ya wiki moja askari wakavamia msitu uliokuwa karibu na Mzinga!Ilikuwa ni ambush kubwa iliyofanya majambazi wengine wauwawe huku wengine wakikimbia!Askari watano walijeruhiwa kwa kupigwa risasi lakini hakuna hata mmoja wao aliyepoteza maisha!Mpango wa majambazi kuvamiwa na watu wasiojulikana kupatikana ukageuzwa na kufanywa kama siasa fulani,kila kiongozi aliipongeza Serikali kwa kufanya juhudi hizo!Raisi akiwa katika hotuba ya kulipongeza Jeshi la polisi yeye Ahmed alikuwa nyumbani kwake anatizama kwenye televisheni,pembeni yupo Hajrath, kamuwekea miguu juu!
“Baby,kuna kitu nimejifunza kwenye haya maisha”
Hajrath akavunja ukimya!
“Kitu gani?”
“Kama una uwezo wa kumsaidia mtu,fanya hivyo!Asa usingemsaidia yule binti sijui ingekuaje”
“Baby,huo msitu unatisha sana usiombe!Sitaki hata kuukumbuka”
“Pole Mme wangu,hata mimi nilipitia kashkash nzito!Si unakumbuka?”
“Naanzaje kusahau mke wangu?”
Kiwanja alichonunua Ahmed tayari kilianza kujengwa na ramani ya nyumba yake ilikuwa ni gorofa mbili kwenda juu,hakika ingekuwa nyumba ya kifahari sana!Pesa nyingine iliyobaki,wakaamua kuanza kujenga hosteli za wanafunzi wakiamini ingekuwa ni biashara nzuri ya kudumu!Hakika ilikuwa ni kama bahati kwao,Ahmed akafanya kazi kwa muda wa miezi mitano na kuandika barua ya kuacha kazi kwani tayari aliweza kujiajiri mwenyewe, kwa haraka na kasi ya ajabu akafungua ofisi ya kukata Bima akawa miongoni mwa mawakala,Mungu sio Athuman pesa ikaanza kuingia taratibu huku adoado akisubiria gorofa lake liishe,kwa kuwa pesa ilikuwepo Mafundi walifanya kazi kwa kasi usiku na mchana na baada ya miezi saba kuisha wakawa tayari wamehamia kwenye jumba lao jipya la gorofa!Ilikuwa ni nyumba nzuri,iliyojengwa kisasa sana!Geti kubwa,uwazi wa kupaki magari na bustani nzuri iliyoendana na nyumba yao!
“Mungu ni mwema”
Ahmed alisema siku hiyo!Wakiwa chumbani,juu ya kitanda kikubwa cha kisasa,mbele kuna luninga kubwa sana wanatizama!
“Ni kweli mme wangu,hatimaye tumepiga hatua kubwa sana!Nimesikia watu wanasema sijui sisi tumejiunga na Freemason”
“Walimwengu,hawatoacha kuongea hata ufanye nini!Waache wanachofikiria,siri tunaijua sisi wenyewe na haina haja ya kumwambia mtu yoyote yule nini kimetokea”
“Najua,itakuwa ni hatari kwetu”
“Kumbe unajua hilo”
Walikuwa wote kitandani,Hajrath kavaa kanga moja tu ambayo kwa pembeni ilitoka na kuonesha paja nje, juu ikawa imeshuka chini,Ahmed alivyomuangalia kwa umakini akahisi joto la ghafla,sio siri mkewe alijaaliwa mapaja manene yanayovutia!Akakohoa kidogo na kumuangalia usoni!
“Hua sichoki kukuangalia mke wangu,ndio maana wakati mwingine nakua na wivu nawewe!Sogea nikwambie kitu”
Kwa mwanamke na mtu mzima kama Hajrath alielewa ni kitu gani Ahmed anahitaji kwani boxa yake ilianza kutuna kwa mbele,akajilegeza taratibu na kumsogelea, hakukua na maongezi mengine zaidi ya kupigana mabusu kedekede kwa fujo na kuanza kutomasana kwa kasi ya ajabu,siku hiyo Hajrath akataka kuonesha ufundi wake,akapanda kwa juu na kujipachika na kuanza kukinyonga kiuno chake adoado huku akimpapasa Ahmed kifuani,hakika zilikuwa ni raha kwa wanandoa hawa!Mchezo uliendelea,wakizidi kubinuana huku na kule ndani ya mashuka,ilimradi kila mtu afurahi na katikati ya mechi hiyo kila mtu alimuongelesha mwenzake!
“Bebiiiii,nikushikeee wapiiiii?”
Hajrath akauliza na kupewa maelekezo,hakucheleweshwa akawekwa mbuzi kagoma mechi ikaendelea bila kukoma,kwa kuwa ndani kulikuwa na ki ubaridi fulani cha uchokozi ikafanya mechi hiyo iwe kabambe mno!Sio siri,walienjoy mno mpaka wanamaliza walitumia sio chini ya dakika hamsini,majasho kwa mbali yanawatoka!
“Nime enjoy baby”
Hajrath akavunja ukimya!
“Hata mimi,mke wangu”
Jinsi jumba hilo lilivyojengwa ilikuwa rahisi kutoka nje na kupunga upepo,Ahmed alivaa taulo akafungua mlango na kwenda kukaa kibaraza cha juu ambapo aliona chini,gari lake alilopaki na mbwa mkali anayefuga jinsi anavyozunguka kukagua usalama wa nyumba hiyo,kifupi akiwa kibaraza cha juu huona mpaka nje ya geti mtu anayetaka kuingia!Hajrath akaja nyuma yake na kuizungusha mikono yake shingoni mwake!
“Unawaza nini Darling?”
“Maisha tu,jinsi yalivyo”
“Usiwaze sana maisha ndio haya haya baby”
“Babrah,tunaenda kumchukua lini kwa bibi yake?”
“Sasa nikuchekeshe,kila nikitaka kumchukua Mama hataki!Nikimwambia Babrah tuondoke nayeye hataki,anamtaka bibi yake!Nikaona niwaache tu”
“Ambao tusiokuwa na bibi tuna comment wapi?”
Ahmed akasema kiutani Hajrath akatabasamu hakika ilikuwa ni familia yenye upendo na amani sana!

****
Kila kitu kilienda sambamba na biashara zilienda vizuri na ratiba zao zilijulikana kuondoka wote asubuhi na kurudi jioni pamoja,hata hivyo kwa Ahmed hakutaka kumbana sana Hajrath akapata wazo la kumpeleka katika mafunzo ya kuendesha gari yaani ‘driving school’ hilo likafanikiwa bila kipingamizi baada ya mwezi mmoja,Hajrath akatunukiwa cheti cha udereva ikawa furaha kubwa!Siku hiyo asubuhi Jumapili,Hajrath alipigwa na bumbuazi pamoja na mshtuko baada ya kutoka kibarazani kwa juu!
“Baby,hii gari nyingine ya nani?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Hajrath akiwa amevaa taulo moja,anatizama gari jipya kwa chini!
“Lipo kwetu!Ni la kwetu mke wangu”
“Muongo baby,ebu ngoja”
Hajrath hakutaka kuamini kwa fuaraha akiwa na taulo akashuka ngazi na kutoka mpaka nje!Akalizunguka gari na kulikagua,lilikuwa ni gari aina ya Landcruiser Vx,imepanda juu na mpya kabisa na mara nyingi magari ya namna hiyo hupenda kuendesha wabunge!
“Baby”
Hajrath akaita akiwa chini anaangalia juu gorofani,Ahmed akasimama kwa juu akawa anamtizama kwa chini!
“Nimekufanyia surprise eeh”
“Ndio maana jana nikashangaa hujaniamsha,una tabia mbaya!Hongera mme wangu”
“Hili nakuachia wewe sasa,sawa Darling”
Furaha ya gari jipya ikafanya siku hiyo watoke na kwenda kupata chakula cha usiku kwenye moja ya hoteli nzuri sana!Hata hivyo waliwahi kurudi na kilichoanza kumnyima raha Hajrath ni usumbufu alioanza Kassim, kwa mara nyingine baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu sana!
“Kassim,nielewe kilichotokea kwanza kifute!Kichwani kwako”
Hajrath alikuwa simuni siku hiyo anazungumza na Kassim,amesimama kwenye ngazi!
“Kwanini nifute? Wakati bado nakupenda”
“Mimi ni mke wa kaka yako”
“Hilo unadhani silijui sasa?”
“Kumbe unalijua?Basi niheshimu basi”
“Unaninyanyasa sana,siwezi kufanya chochote bila wewe Hajrath!Nipo radhi kukufanyia chochote kile unachotaka hapa duniani”
“Umechelewa,vyote nishafanyiwa na kaka yako”
“Hawezi kukupa vyote”
“Basi sikia,iwe hakunipa vyote au kanipa nimeridhika naye!Kama hauna mambo mengine ya msingi ya kuongea,naomba nikafanye shughuli zangu”
Hapo ilibidi Hajrath azungumze kwa ukali kidogo,hakutaka kuweka mazoea tena na Kassim akahisi kujuta baada ya kukumbuka tukio la kumvulia nguo!Alivyokata simu,akashuka ngazi na kutoka nje ambapo huko aliingia ndani ya gari na safari ya kwenda dukani kwake kuanza mara moja!Kwa kweli maisha yake yalimnyookea,akawa ni mwanamke mwenye furaha, hiyo ikamfanya aongezeke kidogo, mashavu yakamtoka kuna baadhi ya marafiki zake wakawa wanayatamani maisha yake, baadhi walimuonea wivu kutokana na mafanikio aliyokuwa nayo!Swala la Hajrath kupanda daladala au bodaboda likageuka na kuwa historia!
******
“Baby,unatoka saa ngapi?”
Hajrath siku hiyo alipendeza kuliko kawaida,gauni fupi la kimini alilovaa lilifanya umbo lake matata lijichonge vizuri,mapaja yote yalikuwa nje!Nywele kabana vizuri kwa nyuma,amejipamba usoni hakika siku hiyo alitumia dakika sitini nzima kujiremba hata alivyojiangalia kwenye kioo alikiri kwamba ametokelezea na asilimia mia moja aliamini angeenda kufunika watu wote huko waliokuwepo kwenye ‘party’ siku hiyo walipanga waende na Ahmed na mpaka dakika hiyo nguo zake zilikuwa kitandani,kilikuwa ni kitendo cha kufika kuvaa na kuanza wote safari lakini mpaka wakati huo Ahmed hakuonekana,akavuta subira kidogo!Baada ya lisaa limoja kupita akapiga tena simu!
“Nakuja mke wangu,namalizia”
“Nakuomba,muda umeenda tutachelewa baby”
“Nakuja nakuja,kuna stock taking nafanya hapa”
“Au niende mwenyewe utanikuta?”
“Hapana nisubiri”
Mpaka inafika saa tatu ya usiku Ahmed hakuonekana,mbaya zaidi marafiki zake walimpigia simu na baadhi walimfuata nyumbani wakimsihii waanze kwenda Ahmed atafika baadaye!
“Nyie nendeni tu Gully,mimi nitakuja”
“Hapana,muda unaenda!Ahmed atakuja mwenyewe mimi nitampigia simu”
“Atakasirikia sana,namjua”
“Usijali,sisi tutaongea naye”
“Kweli?”
“Ndio”
“Mpigieni sasa hivi”
Hajrath hakutaka Ahmed akasirike ndiyo maana akataka apewe taarifa,matokeo yake simu ya Ahmed iliita bila kupokelewa!
“Hapokei,nitaongea naye Hajra”
“Sawa kama ndio hivyo”
Hatimaye akakubali lakini kishingo upande kwani alielewa ni kwa jinsi gani Ahmed angekasirika kwa kiasi cha kutosha,wote wakatoka na kuingia ndani ya gari la Gulshan!Msichana shombeshombe wa kiarabu,safari ya kwenda Kinyerezi ikaanza mara moja!
Kulikuwa kuna uwezekano mkubwa wa Ahmed kuwakuta endapo wangesubiri kwa dakika tano nyingine kwani walipishana kidogo Ahmed akaingia na kuanza kuita huku akipanda ngazi!
“Baby I’m sorry,nilichelewa kidogo”
Alianza kuomba msamahaa kwani alielewa kosa lake lakini matokeo yake kulikuwa kimya,akafungua milango yote!Akazidi kuita bila mafanikio yoyote yale!Akakaa kitandani na kuwaza vitu chungumzima,kuondoka kwa Hajrath peke yake alitafsiri kama dharau kubwa sana!Akashuka ngazi mpaka seblen na kufungua friji,hapo alichukua chupa ya pombe kali na kuanza kunywa kwa fujo,wivu ukampanda na akili yake ilimtuma moja kwa moja ni lazima Hajrath atakuwa na mwanaume tu huko alipo,akachukua simu na kuanza kumpigia lakini haikupokelewa,akapiga tena na tena!Hasira zikampanda zaidi,akaanza kutetemeka mikono huku midomo yake ikimcheza macho mekundu,akapiga fundo la mwisho na kusimama hivyo hivyo kwa kupepesuka,akaingia ndani ya gari kwa safari moja tu, kumfuata Hajrath hata hivyo aliomba Mungu asifanye jambo lolote la kipumbavu kwani hasira alizokua nazo,zilichanganyika na wivu!

*****
Kila mtu alimsifia Hajrath,wanaume mafisi na mabaaria waliofika kwenye ‘party’ kutafuta vimwana, walivyomuona Hajrath walimtizama kwa macho ya uchu kila mtu akatamani alale naye walau kwa usiku mmoja wakaanza kumlia mingo,mbaya zaidi alionekana yupo mpweke muda wote yaani hana mwanaume,kama kawaida ya wanaume, mmoja akajitosa na kumsogelea ili ajaribu kucheza karata yake!
“Mambo mrembo”
Jamaa akatoa salam!
“Safi tu”
“Umependeza sana,usiku wa leo!Kuliko watu wote hapa, Malkia!Kama umeshushwa vile”
“Ahsante”
“Upo peke yako?”
“Hapana!Na mme wangu”
“Aaah,hayupo lakini”
“Yupo”
“Ningemuona,anyway naitwa Moris”
“Ahsante kwa kukufahamu”
“Wewe unaitwa nani?”
Hajrath badala ya kujibu akatoa simu yake na kumtafuta Ahmed hewani,hakika hakuwa mwenye raha hata kidogo, alielewa ni kwa namna gani Ahmed atakuwa amechukia kwa kitendo cha kuondoka bila kumwambia na jamaa aliyefika anamuongelesha alizidi kumtia kichefuchefu cha kutapika!
“Unaitwa nani?”
Jamaa akauliza tena,alivyoona Hajrath anapiga piga simu!
“Aaah jina langu aaah Hajrath,naitwa Hajrath!Kaka samahani,sipo sawa unaweza ukaniacha kidogo”
“Yes naweza,sisi ni binadamu naweza kukusaidia hata kwa mawazo!Nini tatizo?”
Wakati jamaa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Moris akiwa anachombeza Ahmed alikuwa getini anapaki gari,akashuka kwa kasi na hasira na kubamiza mlango wa gari!Marafiki zake na Hajrath walivyomuona wakamsalimia lakini hakujibu,akaingia mpaka ndani na kumkuta Hajrath amesimama na mwanamme,hapo ndipo kichaa chake kikampanda zaidi na zaidi!Hakuongea chochote zaidi ya kumshika mkono Hajrath na kumvuta!
“Tuondoke”
Sentensi hiyo ilimfanya Moris ashangae na Hajrath atetemeke,akamshika shati Ahmed!
“Broo kwani… puuuuuuu”
Ahmed hakujibu chochote zaidi ya kugeuka na ngumi nzito iliyomfikia Moris shingoni, akatupwa na kudondokea majani!Kufumba na kufumbua,watu wakaanza kusogea!
“Huyu ni mke wangu,niacheni niondoke naye!”
Ahmed tayari alipandwa na hasira,akamvuta Hajrath na kumuingiza ndani ya gari,akarudi upande wa pili na kufungua mlango akaingia na kumkuta Hajrath analia kwa kwikwi!
“Acha kujiliza liza”
Gia ikapigwa,gari ikarudi kinyume nyume kwa kasi,kabla ya kuweka gari sawa wageni waalikwa wakawa wametoka nje wanatizama gari linavyogeuzwa wakashuhudia linaondoka,wakabaki wanalitizama mpaka taa nyekundu za nyuma zilivyoishia kwenye kona!
“Ah…med kwanini.. umenifanyia hivyo la..kini kosa langu ni kitu gani?”
Hajrath aliuliza kwa kwikwi huku akibubujikwa na machozi,yakafika mpaka shingoni!Hilo halikumfanya ajibu kitu chochote, zaidi ya kumkata jicho kali na kukunja kona ya kuingia majumba sita,ambapo kulikuwa na barabara ya vumbi pembeni kuna vichaka vingi akazidi kusonga mbele,katikati ya safari akaweka mguu kati,gari ikapiga msele na kusimama! Kama mbogo akateremka na kuzunguka upande wa Hajrath!
“Shuka ndani ya gari,kahaba wewe!Shuka nimekwambia shuka haraka nisije nikakuua”
Alichokifanya Ahmed ni kumvuta Hajrath na kumtoa ndani ya gari,bila kujali chochote akarudi ndani ya gari na kulitia moto,akamuacha!Hajrath bado hakuamini kama ukatili huo anafanyiwa na mumewe,akalishuhudia gari linaondoka akiwa katikati ya vichaka hivyo vinavyotisha!Akashindwa afanye nini zaidi ya kutembea kwa miguu huku akilia kwa sauti,alivyofika mbele kidogo akasikia kelele za watu,alivyowakaribia akagundua ni vibaka wametoka kupora,akasimama kwa niya ya kujificha lakini alishachelewa, wakamuona!
“Oyaaaaa”
Wakamshtua na kuanza kumkimbiza,Hajrath alichanganyikiwa na kuingia katikati ya vichaka bila kujali kama kuna miba lakini vibaka hao watano walimkimbiza,walivyofika sehemu wakasimama!
“Yuko wapi,yule gashi?Au jini?”
“Yupo humu humu,pita kule mtoto mzuri huyo tumchede”
Yalisemezana bila kujua Hajrath yupo nyuma ya mti amejificha ameziba mdomo wake asipige kelele machozi yanamtoka,kilichowashtua vibaka hao wenye uchu ni meseji ya simu kutoka kwa Hajrath, wote wakageuka!
Hiyo ilimfanya Hajrath aanze tena kukimbia huku akipiga kelele,hakuelewa ni wapi anakimbilia lakini alizidi kusonga mbele,akiwa anakimbia alipata wazo lakini hakuelewa kama lingefanya kazi,mtu wa haraka ambaye aliamini angefika wakati huohuo alikuwa ni Kassim,akatumia kama fimbo ili apate msaada,kazi yake ilikuwa ni kukimbia huku anatizama simu akaipata namba ya Kassim na kuipiga akaiweka sikioni,lakini matokeo yake iliita bila kupokelewa akapiga tena!
“Kassim upo waapii?Nahihaji msaada wako nabakwa”
Simu hiyo ilimfikia Kassim,akiwa kitandani katikati ya usingizi,jicho likamtoka kwa mshtuko!
“Uko wapiiii?”
“Sijui sijui,nipo huku majumba sita!Segerea njoo Kassim nakimbizwa”
“Kassim naomba nisaidie nabakwaa,njoo nakuomba…”
Hapohapo simu ikakatika baada ya kujikwaa kwenye jiwe, akateleza na kudondoka chini,akabiringika na kufikia mgongo!Hiyo ikafanya vibaka hao wafike eneo hilo wakamzunguka,mmoja akaokota simu na kuizima wengine wakaanza kumpekua,wakachukua mkoba wake na kumtizama kwa kummulika na tochi,kimini alichovaa kiliwafanya wahuni wakabaji waingiwe na tamaa!
“Tumchedee huyu Jeshi”
“Poa,lala chali”
Hajrath,akashikwa vizuri ili wafanikishe zoezi lao lakini haikuwa rahisi kama wanavyodhani kwani alibana miguu yake,mmoja alivyotaka kumshika mikono akamwagiwa mchanga machoni,hata hivyo alitulizwa na kofi kali la uso,hakutaka kukubali akapapasa pembeni na kushika jiwe,akambamiza nalo mmoja wapo aliyeshika gauni lake,ikatokea patashika kubwa sana walivyoona wanachelewa!Mmoja akampiga ngumi ya pua Hajrath,hapo ndipo alipotulia,wakaanza kumchania sketi yake huku wakishusha suruali zao, tayari kwa kufanya ukatili huo!Hajrath alilia machozi na lawana zote alimtupia Mumewe Ahmed kwa kitendo cha kumtelekeza katikati ya kichaka hiko ambacho matokeo yake,yalikuwa ni kubakwa, kwake ingekuwa hasira hasara na aliapia asingeweza kumsamehee katika maisha yake yote!
“Lala vizuri”
Mmoja wa mateja,akasema huku akijitahidi kumlalia Hajrath kwa juu,ambake!



Simu kutoka kwa Hajrath ilimkuta Kassim akiwa getoni,yupo katikati ya usingizi. Isingekuwa Hajrath kupiga kwa mara ya pili wenda angeizima!Habari alizopewa zilimshtua na kumuogopesha kwa wakati mmoja,ndiyo maana alikurupuka kutoka kitandani na kibukta chake na kuvuta shati kwa kasi!Gari lilikuwa nje lakini hakutaka kutumia akiamini kwa kufanya hivyo,ungekuwa ni upotevu wa muda!Bahati nzuri ikawa kwake,nje kulikuwa na pikipiki inapita kwa kasi,hakujali akaipiga mkono ikasimama.
“Nipeleke,Majumba sita Segerea kaka!Sasa hivi fanya fasta”
Kassim akazungumza bila kumeza mate!
“Twende”
Ilikuwa ndiyo dereva aende kupeleka hesabu na kulala lakini akaona ni vyema,achukue pesa ya lala salama,akageuza pikipiki Kaasim akapanda akiwa na mawazo mengi,kilichokuwa kinamuumiza kichwa ni Hajrath aliyekuwa anaomba msaada usiku kama huo mnene!Kwa mwanamke kama yeye aliyeolewa haikuwa hali ya kawaida hata kidogo!
“Kaka ongeza mwendo”
Kassim akaamuru, mwendo wa dereva wa kusuasua ulimnyima raha!Dereva akatii amri ya abiria wake,haikuchukua dakika nyingi wakawa wamekunja tayari kona ya Majumba sita,kazi ya Kassim ilikuwa ni kutizama kwa makini huku na kule,pikipiki ilikuwa katika mwendo ule ule,kuna kitu alikiona ambacho hakukielewa hata kidogo!Vimuli muli vya tochi vilimfanya amuombe dereva asimamishe pikipiki,akashuka kwa haraka!
“Oyaa pesa yangu,vipi?”
“Nisubiri nakuja”
Japokuwa alikuwa mwenye hofu lakini hakua na jinsi,namna Hajrath alivyopiga simu akiwa anahema anadai kwamba anabakwa ilimfanya ayalinganishe na mazingira hayo ya pori zito,akaanza kufatisha taa za tochi zilipo!Kulikua na giza nene la kutisha,taratibu akaanza kukanyaga miti ya michongoma,alivyofika mbele kidogo akasikia kelele na yowe za Hajrath,akaotoka kipande kinene cha gogo ili ajihami ingawa hakujua watu hao wamejipanga vipi,akapiga moyo konde akaanza kutembea kwa kasi,akamfikia mmoja wapo aliyeshika tochi na kumpiga na gogo la kichwa,kibaka mwingine aliyekuwa juu ya Hajrath anataka kuanza zoezi la ubakaji,akapigwa na gogo la shingo!Hakuna mtu yoyote aliyebaki,vibaka wakatimua mbio huku wakiwa na hofu kila mtu ameshika njia yake isipokuwa mmoja wao aliyepigwa na gogo la kichwa,huyo alikimbia na kudondoka kandokando kama mzigo kutokana na maumivu makali,aliyokuwa nayo kichwani!
“Hajrath”
Kassim akaita baada ya kumuona Hajrath yupo hoi chini,amelala chali amekata tamaa analia machozi nguo zake tayari zimechanwa,moyo ulimuuma mno!Akamuinua taratibu na kumuweka sawa.
“Pole”
“Ahs…nte”
Hakutegemea kumuona Kassim mahali hapo,ndiyo maana hata alivyoitikia alibaki anamshangaa bila kutegemea muujiza huo mkubwa uliotokea usiku huo,hakuelewa ni aina gani ya shukrani ampe japokuwa alibaki analia kwa kwikwi,alichokifanya Kassim ni kumpukuta majani na michanga iliyokuwa kichwani na kumuweka nguo vizuri,wakaanza kutembea mpaka walivyotokea barabarani!
Ukiachana na unyama aliofanyiwa na Florian baada ya kufanywa kama kontena la kusafirishia madawa ya kulevya kwa mara nyingine tena alifanyiwa ukatili wa aina yake,hakutegemea kitu kama hicho kingetokea ndani ya ndoa yake!
Akawakumbuka baadhi ya wanawake wanaoenda kushtaki ustawi wa jamii,akaapia kesho yake ni lazima aende huko ili amfunze Ahmed adabu na katika maisha yake yote asije kumsahau,wakati mwingine alianza kujuta kuolewa na mwanaume huyo katili mwenye roho ya kinyama!Hakuelewa ilikuwaje akampenda!Mpaka wanapanda kwenye pikipiki ili safari ianze mawazo yake yalikuwa mbali kabisa hana hili wala lile,hajui anapokwenda!Mpaka wanafika Kurasini,alikuwa ameganda tu anamuwaza Ahmed haamini unyama aliofanyiwa wakati mwingine alidhani yupo kwenye ndoto ya kutisha,walivyofika Kassim akamkaribisha ndani kisha yeye kutoka na pesa,akamkabidhi dereva wa pikipiki kama posho ya kazi yake,akarejea ndani na kumkuta Hajrath analia, alichokifanya ni kutembea mpaka kwenye friji na kutoa maji ya baridi!
“Karibu maji”
Aliamini kwa wakati huo hata angemuuliza Hajrath nini kilimsibu isingekuwa rahisi kuelezea, ndiyo maana akamtaka kwanza anywe maji ili baadaye amsaili,hivyo ndivyo ilivyokuwa!
“Nitakunywa”
“Kunywa sasa hivi”
Kassim aliendelea kumfariji Hajrath,akimtaka anyamaze na anywe maji ili apunguze hasira zake lakini hilo halikuwa rahisi hata kidogo kumfanya mwanamke huyu atulie,hasira zilimkaba bado alikumbuka tukio la kutaka kubakwa na ingekuwaje kama Kassim asingetokea usiku huo na kumkomboa jambo hilo lilimuumiza sana ubongo wake!
“Kassi…m ahsan..te sana”
“Sawa,kunywa maji!Ingia bafuni ukaoge,ngoja niingie jikoni nikupashie chakula ule”
Aliingiwa na huruma mno!Licha ya kumpenda kutoka moyoni lakini pia aliumia kwa kiasi cha kutosha akitaka kujua ilikuwaje mpaka Hajrath akaingia ndani ya kichaka hiko kizito usiku huo,alichokifanya ni kumsindikiza Hajrath chumbani ambapo huko kulikuwa na bafu,akampa taulo nayeye kurudi jikoni ambapo huko alipasha chakula joto akakitenga mezani na kumkuta Hajrath tayari kamaliza kuoga,akamkabidhi moja jezi za mpira ya timu ya ‘Manchester’ akaivaa!
Jinsi ilivombana ilifanya umbo lake lijichore vizuri ndani ya kaptula hiyo fupi, kwa aibu na haya akachukua na kanga ili kujifunika,hata hivyo hakuficha kitu chochote kile bado figa yake ilionekana,ikawa tabu sana kwa Kassim akabaki anakula kwa macho!
“Karibu mezani,chakula tayari”
“Nashukuru”
Ingawa hakuwa na mudi ya kula lakini alihisi njaa,taratibu akaanza kula wali na nyama aliondaa Kassim,hata hivyo hakumaliza sababu chakula hakikushuka vizuri kutokana na msongo mawazo mengi aliyokuwa nayo kichwani kwake!Hasira zilivyopungua,akamtizama Kassim na kumshukuru kwa mara nyingine kwa kila kitu alichokifanya!
“Naweza kuondoka?”
Hajrath akauliza,haikueleweka lilikuwa ni swali ama hoja!
“Kwenda wapi?”
“Kwangu”
“Usiku sasa hivi ni hatari,ilikuwaje nikakukuta pale!Ulikua unafanya nini?”
Lilikuwa ni swali lililomfanya Hajrath aanze kulengwa na machozi,hakua tayari kuongea chochote kuhusiana na ndoa yake,akiamini kwa kufanya hivyo angeitia doa na kuwapa sababu za walimwengu kuzungumza madhaifu yao, hata hivyo nafsi nyingine ilimsukuma aseme kila kitu kilichotokea,akiwa juu ya kiti anamtizama Kassim,sura ya Ahmed ikamjia akiwa anampiga na mara nyingine akimtukana matusi ya nguoni!
“Najuta kuolewa na kaka yako”
Sentensi hiyo ilitosha kabisa kumfanya Kassim,agundue kuna shida kubwa kwenye ndoa yao!
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kaka yako ananitesa sana”
Hatimaye Hajrath akaamua kufunguka lakini hakutaka kuweka kila kitu wazi,akaishia hapo akidai kwamba amechoka anataka kupumzika kichwa kinamuuma sana!
Kila kitu katika maisha yake kilivurugika na aliapia akitoka hapo ni lazima akadai talaka yake licha ya kwamba alishazaa na Ahmed,hilo halikumfanya ageuzwe ngoma alitaka kuachana naye ili asonge mbele na maisha yake,hakutaka kujali jamii ingemuonaje!
“Sawa,utalala chumbani!Mimi nitalala hapa seblen”
“Kwanini sasa?Mimi nitalala seblen”
“Hapana Hajra,lala chumbani!Mimi napenda kulala seblen”
Kassim alijifanya muungwana,hata hivyo hakutaka kuleta habari za mapenzi na kutaka ngono katika wakati kama huo wa matatizo aliyokuwa nayo Hajrath,ilikuwa ni lazima kwanza aweke ubinadamu mbele ili Hajrath asidhani kwamba alitoa msaada wake ili apate ngono,kitu alichoamua ndicho kilichotokea Hajrath alilala chumbani akafunga mlango na funguo,hata hivyo usingizi haukumjia!Mara kwa mara alifungua macho yake usiku akidhani wenda Kassim angemjia usingizi na kumfanyia ushenzi jambo ambalo hakutaka litokee hata kidogo,alikuwa mwenye mawazo mengi sana na mwisho wa siku akahitimisha kwamba ni lazima aombe talaka yake na baada ya hapo ampeleke Ahmed kwenye vyombo vya sheria kwa kitendo cha kinyama alichomfanyia!Hata hivyo alitaka kujipa subira kwanza akidhani wenda zilikuwa ni hasira,akiwa katikati ya mawazo mengi akapitiwa na usingizi mzito sana!

******
Alikuwa ni kama amerudiwa na fahamu zake baada ya kurudi nyumbani na kupaki gari,hakushuka badala yake aligeuza na kurudi alipotoka ili amtafute Hajrath njiani alipomuacha!Hakua ana uhakika kama angemkuta usiku huo mnene,hata hivyo alijipa moyo kwani aliamini kwamba Hajrath angekuwa sehemu fulani ya kichaka alichomuacha amekaa sababu asingekuwa na ujanja wa kwenda sehemu yoyote ile,kitendo cha kufika majumba sita,akapunguza mwendo na kuanza kuangalia huku na kule akimtafuta mkewe,alihisi kujuta kwa hasira na wivu wa kipumbavu aliokuwa nao!Alijilaumu mno na kuapia kwamba hatojisamehe kama angemkuta Hajrath amepatwa na matatizo makubwa,aliomba sana Mungu amlinde Hajrath alipo,kwa mwendo wa taratibu alitizama huku na kule,akimtafuta mpaka anatokea upande wa pili uliokuwa na lami,hakukuwa na dalili yoyote ile ya Harath kuwepo!Akarudia kwa raundi nyingine,akapita njia ile ile lakini hakukua na dalili ya mtu yoyote,akarudi tena kwa mara nyingine ya tatu!Ilivyofika mara ya nne bila mafanikio yoyote akateremka kutoka ndani ya gari,akaanza kutembea kwa miguu na kuliacha gari,akaingia vichakani huku akiita kwa wasiwasi!
“Hajraa,mke wangu!Hajraa nisameehee mke wangu,sitorudia tena!Twende nyumbani nimekuja kukufata”
Alisema kana kwamba anamuona,hata hivyo kulikuwa na ukimya wa hali ya juu sana!Alivyoona mbele kuna giza zito,uwoga ukamuingia akatembea na kurudi mpaka kwenye gari lake,akaanza kutafakari kwa kina ni kitu gani akifanye akampigia Hajrath lakini simu haikuwa hewani!Hapo ndipo akapata wazo lingine la kumpigia simu Gully,rafiki mkubwa wa Hajrath aliyeandaa sherehe siku hiyo!
“Gully upo wapi?”
Ahmed akauliza baada ya simu kupokelewa!
“Sikusikii vizuri ngoja nitoke pembeni”
Upande wa pili wa simu kulikuwa na kelele sana,ndio maana hawakusikilizana kabisa!
“Unasemaje shem?”
“Upo wapi?”
“Mimi?!”
“Ndio”
“Nipo Bulls park hapa,Club”
“Upo na Hajra?”
“Hapana,shem si mliondoka wote?”
Gully,akarudisha swali.
“Sawa,nitakupigia”
Simu ikakatwa,Ahmed hakuwa na jinsi zaidi ya kuanza kuwapigia simu rafiki zake Hajrath mmoja baada ya mwingine,hakuambulia kitu chochote mpaka inafika saa kumi na moja asubuhi,alichoka kabisa na kurudi nyumbani kwake akiwa hoi bin taaban!

****
“Umeamkaje?”
“Salama tu”
“Mimi ndio naondoka!Sasa?”
Kassim,alikua seblen anamuuliza Hajrath! Swali lake lilikuwa na maana kubwa sana kwanza alitaka kujua kama Hajrath angeendelea kubaki alafu la pili alitaka kuelewa mchakato mzima wa siku hiyo utakavyoenda!
“Wewe nenda utanikuta”
“Kama ndio hivyo sawa,nikuletee nini nikirudi?”
“Chochote tu”
Alidhamiria kukaa kwa Kassim!Hata ikiwezekana ajifiche hukohuko!
“Sawa”
“Alafu Kassim”
“Naam”
“Naomba usimwambie mtu yoyote kua nipo hapa”
“Hilo usijali kabisa,inabidi uniambie kwanza imekuaje?”
“Nitakwambia ukirudi”
“Baadaye,poa”
Kassim,akaondoka zake!Huku nyuma akimuacha Hajrath akiwa na mawazo mengi sana!Hakuelewa ni kitu gani akifanye lakini alichoamua yeye ni kujificha ama kukaa mbali na Ahmed,asijue mahali alipo alielewa ni kwa namna gani angemtesa lakini hilo hakujali,alivyomfikiria Mtoto wake Babrah,moyo ukamuuma sana akatamani kurudi lakini akasita!Saa kumi na mbili jioni Kassim alirejea akiwa na mifuko iliyojaa matunda,pamoja na zawadi kadhaa za nguo.Hajrath alitabasamu na kushukuru kwa ukarimu aliouonesha Kassim,siku hiyo walizungumza vitu vingi sana,hapo ndipo Hajrath akaamua kufunguka kila kitu kilichotokea,akasema jinsi anavyoishi na Ahmed hasira alizokua nazo na namna anavyopigwa kutokana na wivu aliokuwa nao!
“Siku akijua nipo hapa,ataniua”
“Hawezi,ananiheshimu sana!Na siku hiyo,tutapigana kweli”
“Sio, Ahmed namfahamu!Nimesoma naye,ni mkorofi hakubali kushindwa hata kidogo”
“Sasa wewe umesoma naye mimi nimezaliwa naye tumbo moja!Ni kaka yangu huyo,ana hasira sana pole lakini”
“Nishazoea”
“Hivi,anadiriki vipi kumpiga mwanamke,hapo ndipo namshangaa sana!Ni ushamba”
Kassim akaanza kumkandia kaka yake na kumponda jinsi alivyokuwa mshamba na limbukeni hajui kumtunza mtoto wa kike,waliongelea mambo mengi sana!
“Hivi,Kassim demu wako yuko wapi?”
“Mimi hardcore”
“Kwenda huko,muongo ile siku ile nilisikia umemtia demu gani sijui mimba”
“Yule demu jau sana,mimba ilitoka ile!Sijui katoa,atajua mwenyewe”
Moyo wa Hajrath ulipata utulivu mkubwa mno,japo sio sana!Saa mbili ilivyofika Kassim akasimama na kwenda jikoni ambapo huko alianza kupika chakula cha usiku ili wale,hata hivyo Hajrath hakukubali swala hilo litokee,nayeye akaingia jikoni ambapo huko walipika wote huyu alikata nyanya yule vitunguu!
“Punguza moto huo ni mkali sana,utaunguza”
Hajrath akasema Kassim,akatii!Chakula kilivyokuwa tayari wakaweka mezani,wote wakaanza kula huku wakipiga stori nyingi sana kuhusiana na maisha!
“Unafanya kazi wapi Kassim?”
Hajrath akaibua swali.
“Nipo bandarini pale TPA”
“Kwenye mahela!?”
“Hela wapi,hakuna chochote”
“Nasikia bandarini kuna pesa mno”
“Kawaida sana”
Baada ya kula,Kassim akashukuru wakatoa vyombo mezani!Hajrath akaingia chumbani lakini kabla ya kufunga chumba,Kassim akagonga!
“Kuna bukta naitaka,mara moja!Nilale”
“Ingia”
Kassim,akaingia na kuchukua kila anachotaka kisha kutoka!
“Usiku mwema”
“Nawewe pia”
Hali ya hewa,ilianza kubadilika taratibu wingu lilitanda angani na baridi kuongezeka ghafla huku upepo mkali ukivuma,bila shaka ilikuwa ni dalili ya mvua kubwa sana ni kweli kwani siku zote dalili ya mvua mawingu,hapohapo ikaanza kunyesha kwa kasi!Baridi lilimpiga Kassim,akiwa seblen amejifunika juu ya kochi huku televisheni inawaka,hata hivyo usingizi ulimpitia akalala fofofo!Lakini katikati ya usiku,alishtuka baada ya mlio mkubwa wa radi kupiga,akafungua macho yake,alishtuka sana!Mbele yake alimuona Hajrath,akiwa amesimama na kanga moja peke yake,iliyoanzia kifuani na kufanya mapaja yake manene na malaini kuwa nje!Ni jambo lililomfanya Kassim,apigwe na mshtuko wa waziwazi!Akashindwa kujua ni kitu gani akifanye zaidi ya kuduwaa akimshangaa Hajrath akiwa ndani ya kanga moja,tena mbele yake!



Biashara zake ziligonga mwamba,akili yake haikufanya kazi kabisa kitu kilichokuwa kichwani kwake ni mkewe Hajrath, wapi alipo!Kila alipojiuliza aliishia kujijibu mwenyewe tu,kulivyokucha hakuweza kwenda kazini alichokifaya ni kuendelea kupiga simu kwa ndugu,jamaa na marafiki ili ajue ni wapi alipo!Simu kutoka ofisini kwake siku hiyo alizipotozea na hakutaka kujibu hata moja!
“Insurance ya Scania boss,kuna mtu anahitaji”
Sauti ya upande wa pili ilisikika ikimkuta Ahmed yupo katikati ya kichaka, alichomuacha Hajrath usiku wa jana,mvua inamnyeshea hilo hakujali kabisa!
“Nitakupigia Jesca”
“Lak..”
“Nitakupigia nimekwambia”
Alichotaka kujua ni wapi Hajrath alipo na sio kitu kingine,akazidi kusonga mbele mpaka chini ya mti hapo alishtuka baada ya kuona kipande cha nguo kimechanika,akainama kidogo na kukichukua ingawa hakuwa mwenye uhakika wa asilimia zote mia moja kwamba nguo hiyo aliivaa Hajrath lakini jambo hilo lilimuumiza moyo,hakupata jibu alipojiuliza nguo hiyo ilikuwa chini kwa sababu gani,taa nyekundu ikawaka kichwani kwake kuashiria kwamba kuna hatari ilitokea!Lawama zote alijitupia mwenyewe akajiona ni jinsi gani alivyokuwa mpumbavu asiyekuwa na akili hata kidogo!
Kwa kuwa udongo wa eneo hilo ulikuwa tepetepe ikawa vigumu kupita,ikamlazimu atumie akili nyingi kuruka na kukanyaga majiwe, mpaka alipolifikia gari lake na kuliwasha kwa safari moja tu,kuelekea kwa Benjamin Ngowi ili waanze mchakato wa kumtafuta Hajrath popote pale!

*****
Mbele yake alisimama Hajrath akiwa katika vazi la kanga moja peke yake,umbo la mwanamke huyo lilimpagawisha, akashindwa mpaka kumeza mate,Mungu katika kumuumba Hajrath alimjazia udongo mwingi kwa nyuma,umbo lake likafanana na kibuyu!Kanga aliyovaa ilikuwa laini kiasi kwamba chuchu zake dede kifuani zilitokeza zikajichora,mpaka hapo Kassim hakujua nini maana ya Hajrath kufika Seblen akiwa katika vazi hilo la mitego,mapigo yake ya moyo yalimwenda mbio kiasi kwamba akahisi joto kali mwilini,akajivuta taratibu na kukaa kitako kwenye kiti huku tango lake taratibu likianza kusimama,kutokana na mvua kubwa inayonyesha na baridi linalovuma akavuta shuka na kujifunika kidogo!
“Maji ya kunywaa”
Hajrath akavunja ukimya lakini macho yake yalivyolegea na jambo alilolitaka vilikuwa ni vitu viwili tofauti!
“Ma..maji umesema?”
Kassim akauliza akiwa amepata kigugumizi ambacho hakuelewa kilitokea wapi!
“Ndio”
“Huko jikoni,subiri kidogo”
Kassim akasimama wima lakini hapo uvumilivu ulimshinda akakumbuka ule msemo ‘Ukifa na kiu baharini we ni mzembe’,akajikuta anamshika Hajrath kiuno kwa niya ya kutingisha kiberiti hata hivyo hakukuwa na upinzani wa aina yoyote ile,Hajrath akatulia hiyo kwa Kassim ilikuwa ni sawa na ‘kosa kwa difensi’akapeleka mdomo wake mdomoni cha ajabu Hajrath aliupokea kwa mbwembwe wakaanza kubadilishana mate kwa fujo wakinyonyana ndimi,mkono wa Kassim ukashuka taratibu na kuanza kutomasa kifua cha Hajrath, ambapo baada ya muda mfupi,akaivuta kanga ikadondoka chini,Hajrath akabaki kama alivyotoka tumboni mwa mama yake!Hata hivyo mwanamke huyo hakuwa gogo,alijua kucheza mechi akaanza kufanya madoido mara amnyonye Kassim shingo mara achue tango,mwisho wa habari akamtupa juu ya kochi nayeye kupanda juu yake,mzuka ulimpanda ajabu, mvua iliyokuwa inanyesha ilizidi kumpandisha wazimu na kukinyonga kiuno huku mara kadhaa akiinuka juu na kurudi chini,kutokana na mvua kuwa kubwa miguno haikusikika lakini mechi hiyo ilikuwa cha ndimu sababu wachezaji hawakujipanga vizuri,ilikuwa ni mechi ya kushtukiza ingawa ilichezwa dakika tisini na nyongeza juu,ambapo Hajrath kwa mara ya mwisho alienda na kushika stuli,kumaanisha kwamba Kassim afike nyuma yake!Kassim hakuremba kwani kwake hiyo ilikuwa ni bahati ya mtende,ndiyo maana alipeleka mambo haraka sana sababu aliamini angemkosa siku hiyo Hajrath asingempata tena,akiwa nyuma yake amemshika kiuno anapeleka majeshi majeshi,akauzungusha mkono wake mmoja kwa chini ambapo alikutana na chuchu za Hajrath na kuanza kuzitomasa kimahaba huku akishughulika na kuzungusha kiuno chake,alihakikisha mechi hiyo ya kwanza hatoi boko, ndiyo maana alifanya kila awezalo,kuonesha utundu!
“Be…bii I’m cumming,yeeees aaaaah aaaashaa haapooo hapooooo,yes aashhhsss”
Kelele hizo zilitoka kwa Hajrath akihisi raha za ajabu kiasi kwamba akajiona yupo juu angani vitu vyote anaviangalia kwa chini,hiyo ilimaanisha anakaribia kufika safari yake!
Jambo hilo ilimfanya Kassim apandishe mori kama masai,akamvuta kwa nguvu na kumwagia risasi,ambapo Hajrath nayeye alijikunja kidogo na kutulia!Kassim akarudi kinyume nyume na kukaa juu ya kochi,Hajrath hakuweza kumgeukia alichokifanya ni kuibeba kanga yake na kuingia chumbani bila kusema kitu chochote kile alihisi aibu sana!Bado Kassim hakuamini kilichotokea,kwake jambo hilo lilikuwa kama ndoto!

*******
Ahmed alikutana na Benjamin Ngowi nyumbani kwake,jioni yaa saa kumi na mbili baada ya kutoka kumsaka kwa mara nyingine Hajrath kila pembe ya mji, bila mafanikio!Matumaini yake yakaangukia kwa Ngowi akiamini huyo ndiye angempa msaada mkubwa wa mawazo kwani walikuwa ni marafiki, walioshibana!Hakukuwa na haja ya kuficha mambo,Ahmed akafunguka kila kitu na mambo yote yaliyotokea uso wake ulionesha kujuta na wasiwasi wake mkubwa ulikuwa wenda Hajrath amekufa tayari,japokuwa hilo hakutaka kulipa kipaumbele sababu mathara yake yangekuwa makubwa sana kwani angehusishwa kwa njia moja ama nyingine na mwisho wa siku gereza lingemuhusu!
“Kwanza pole,alafu kwa sasa sitaki kukulaumu japokuwa naweza kusema Ahmed unazingua sana,rafiki wa kweli ni yule anayekuchana ukweli.Ahmed,hasira hasara!”
“Naelewa bro nakuhaidi,nikimpata sitofanya tena upuuzi niliofanya!Najuta sana”
“Naelewa hilo,naona hata unavyoonekana haupo sawa kabisa!Ndugu zake wanajua?”
“Hapana”
“Ndugu zako?”
“Hamna anayejua zaidi tu ya marafiki zake”
“Rafiki yake mkubwa ni nani?”
“Hajra hana rafiki mkubwaa,mara leo yupo na yule kesho na huyu!Kila mtu ni rafiki yake kutokana na nyakati”
“Kuna sehemu yupo nina uhakika,kwa rafiki yake mmoja wapo”
“Yupi sasa?”
“Mimi nawee ndio hatujui,mara ya mwisho alikua na nani?”
“Na binti mmoja wa kiarabu Gully anaitwa”
“Basi huyo huyo wa kumuhoji”
“Ngoja nimpigie sasa hivi”
“Hapana,unajua anapoishi?”
“Ndio”
“Inabidi tumfate,kama Hajra yupo huko utamuona ukienda ghafla”
“Ni wazo zuri”
Wote wakainuka,mguu kwa mguu mpaka kwa Gully jinsi walivyofika kwake Kigamboni,Mji mwema!Iliogopesha,hawakupiga simu wala kutoa taarifa jambo lililomfanya Gully ashangae sana hata hivyo ilibidi wafunguke na kumueleza kila kitu kinagaubaga,jambo lililomfanya hata Gully ashangae!
“Siku ile nasikia ulifanya fujo shemeji,baada ya pale nikaondoka mimi sikukaa tena”
“Sasa kuanzia siku hiyo,sijamuona tena”
“Sasa atakua wapi?”
“Hata sijui”
“Kwao umeenda?”
“Ndio”
Ahmed,akadanganya hakupenda kuhojiwa maswali mengi sana!
“Zamda,ulimuuliza?”
“Hapana”
“Wenda atakuwa kwake,muulize!Mungu wangu Hajrath atakuwa wapi”
Zilikuwa ni habari za kusikitisha kwa mtu mzima kupotea katika mazingira ya kutatanisha kama hayo,licha ya yote Ahmed hakukoma kuzunguka kwa marafiki wakubwa wa Hajrath usiku mzima lakini hakukua na dalili yoyote ile ya kuonekana kwake!
“Ahmed,Hajrath atakuwa kwao!Nina uhakika,nina anza kuhisi kitu”
Benjamin akatoa wazo baada ya kumrudisha Ahmed nyumbani kwake,alikuwa ana kila sababu ya kusema hivyo sababu walizunguka kwa marafiki wote!
“Kwanini unasema hivyo?”
“Unadhani atakuwa wapi?Kote tumezunguka”
“Sawa,sikatai atakua kwao!Kama hayupo?Naanzaje kujielezea kwao,hawatonielewa!”
“Ahmed kwenye jambo kama hili zito usiogope,wewe ni mwanaume!Sifa ya mwanaume ni ujasiri mwanaume hakimbii tatizo analikimbilia ili alitatue,weka uoga pembeni kesho nenda kwao”
“Nitajaribu kufanya hivyo”
“Usiku mwema mimi naondoka”
“Bro,ahsante kwa kila kitu”
Ngowi akaaga,akaingia ndani ya gari lake akiwa na masikitiko makubwa sana,uzito wa jambo la rafiki yake Ahmed alilivaa kama lake,ndiyo maana akawa bega kwa bega naye akimuhaidi kwamba kesho atarejea tena ili waendeleze msako huo kimya kimya, kabla ndugu hawajagundua!

*****
Ushemeji kati ya Kassim na Hajrath ukafa,sasa wakawa kama mume na mke yaani kupika kupakua,lilikuwa ni jambo la hatari endapo Ahmed angegundua mchezo huo!Japokuwa wote wawili walilifahamu hilo lakini hakuna hata mmoja kati yao aliyejali madhara yake,badala ya Kassim kulala seblen kama awali akawa analala chumbani na Hajrath na huko walifanya mapenzi kila saa kila dakika,kila mtu alimuona mwenzake mtamu!Walijitahidi kupeana mahaba wakihaidiana kwamba ingekuwa siri kubwa sana!Hajrath kuishi kwa Kassim ilikuwa sawa na magendo ndiyo maana hakutoka ndani kuhofia angeonwa na taarifa kusaambaa kwa kasi!
“Unajua sana mapenzi Kassim”
“Hata wewe”
“Jana usiku,nili enjoy mno!Ile wine ilete tena”
“Nitaileta leo”
Mguu wa Hajrath ulikuwa juu ya tumbo la Kassim wapo kama walivyozaliwa,chumbani peke yao hakuna anayejali kwao kila kitu kilikuwa sawa!Kwa raha alizopewa Hajrath alidiriki kusema ni bora angefuga nyoka kuliko kuishi na binadamu katili kama Ahmed,alihisi kujuta na wakati mwingine kujilaumu ni kwanini alimzungusha Kassim!
“Ni bora ningeolewa nawewe”
“Hata hivyo,hujachelewa!”
“Kwanini?”
“Omba talaka”
“Alafu?”
“Tunaanza kuishi wote”
“Sio rahisi kama unavyofikiria,Ahmed ni kaka yako!Hatokuelewa”
“Mimi sitojali”
Wakati Kassim anazungumza hayo,mdomoni alikuwa na kipande cha ‘chocholate’ akakitoa mdomoni na kuanza kukipakaza kwenye mgodi wa Hajrath taratibu huku mkono wake ukidarisi adoado,hiyo ilimfanya Hajrath aanze kufumba macho yake kwa raha!Zoezi halikuishia hapo kumbe Kassim alikuwa na mipango yake kabambe,alichokifanya ni kujivuta chini mpaka mapangoni,akaitanua miguu ya Hajrath huku na kule na kuanza kupiga deki bahari kwa namna ya kulamba ‘Chocholate’ iliyokuwa juu ya mgodi!Ilikuwa ni mara ya kwanza Hajrath kufanyiwa utundu huo tangu azaliwe,alihisi anapaa angani na kusimamia ukucha,akaanza kunyonga nyonga mashuka huku akivuta pumzi nzito na kuishusha,alichokua anahisi hakikuweza kuelezeka kiwepesi!Mpaka ikafika wakati akaanza kumshika Kassim kichwa chake,akimkandamizia kwa ndani azidishe mbwembwe,hiyo ilimfanya Kassim azidishe kasi mpaka Hajrath alivyobana miguu kumaanisha tayari ameshafika kitonga,Kassim akamuwahi juu kwa juu,mpira ukapigwa kati mechi ikaanza hapohapo!Ilikuwa ni jioni tulivu,iliyofanya mechi hiyo ichezwe vizuri na uzuri kila mtu alijua tayari udhaifu wa mwenzake ulipo,mechi ilikua pambe na kuisha taratibu!Kassim,akiwa juu ya kifua bado, Hajrath yupo chini wakaanza kupongezana!
“Nimekupelekesha eeh?Mpaka unahema”
Ahmed akauliza kwa kujigamba!
“Usijisifu kwa mbio,msifu na anayekukimbiza”
Hajrath hakukosa neno,wote wakatabasamu na kuingia kuoga!
“Utakula nini leo Mme wangu?”Huko huko bafuni,Hajrath akauliza huku akiwa nyuma ya Kassim anamsugua mgongo!
“Leooooo,wali samaki”
“Okay,nitakupikia wali mtamu ule mpaka ushangae”
“Nitafurahi, si unajua mimi mambo ya chini ya pua hua sirembi”
Majina yao yakabadilika ghafla wakaanza kuitana mme na mke,penzi lao likanoga Kassim hakukubali Hajrath aondoke na Hajrath hakutaka kubanduka, akaona hapo ndio mwisho wa reli,raha alizokuwa anapata zilimsahaulisha matatizo ingawa mara kwa mara alimkumbuka sana mtoto wake mdogo Babrah,alijua fika ni jinsi gani pia ndugu zake wangeteseka kumtafuta kila pembe ya mji!

*****
“Hivi una habari,mke wa kaka yako amepotea?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mama Ahmed,akimuuliza Kassim simuni!
“Kapotea!?”
Kassim akajifanya kushangaa kana kwamba hajui be wala che!
“Ndio,wiki ya pili hii wanamtafuta!Wameenda mpaka monchwari zote”
“Ilikuaje kwani?”
“Ahmed hataki kusema lakini nina uhakika alimpiga mkewe,si unamjua kaka yako alivyo na mahasira yake”
“Ninamjua sana,sasa itakuaje?”
“Amechanganyikiwa,hajui afanye nini!Kesho anataka kupeleka taarifa kwenye magazeti na redio”
“Mwambie asiende kwanza”
“Kwanini?”
“Nitakupigia Mama ngoja sasa hivi,wee mwambie asiende kwanza”
Habari hizo zilimuogopesha mno,akampelekea Hajrath kama zilivyo akamwambia ni kwa jinsi gani alivyokuwa anatafutwa mji mzima kama shilingi,hakuacha lolote nyuma kila kitu akakiweka wazi!
“Mpaka monchwari wameenda?!”
Hajrath akauliza kwa mshangao,hakutegemea kama jambo hilo lingekuwa kubwa namna hiyo!
“Kesho wanaenda kwenye tv na redio pia”
“Mungu wangu,kwahiyo itakuaje?”
“Ebu subiri,Ahmed anapiga”
“Anapiga?!”
“Ndio”
Kassim akashusha pumzi kidogo na kuipokea simu ya Kaka yake!
“Dogo vipi?”
Upande wa pili wa simu ukasikika!
“Safi shikamoo broo”
“Marahaba,upo wapi?”
“Nipo geto”
“Fungua mlango nipo nje”
Akatoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango,kitu kama hicho hakukitegemea kabisa,akasimama wima na kuvuta pazia alichokiona kilizidi kumuogopesha,gari la Ahmed lilikuwa nje!Alichokifanya ni kumgeukia Hajrath!
“Nenda chumbani,fanya haraka”
Akasema kwa sauti ya chini,hiyo ilimfanya Hajrath akimbie na kuingia chumbani ambapo huko,aliingia bafuni moja kwa moja na kutulia!Alivyohakikisha kila kitu kipo sawa,akafungua mlango na kutoka nje,akamkaribisha Ahmed ndani!
“Kassim,Hajrath yuko wapi?”
Lilikuwa ni swali la moja kwa moja,lililomfanya Kassim apigwe na bumbuazi na kubabaika!
“Hajrath?Hajrath gani?!”
“Mke wangu”
“Mimi kwa kweli sijui,kwanini unaniuliza kwani amekwambia anakuja hapa?”
“Kumbe,sijakwambia!Hajrath wiki ya tatu hii inaenda,haonekani nyumbani”
“Sema ukweli”
“Kassim,nimeongea na Mama leo acha usanii!Kakupigia,kaniambia nije kuongea nawewe!Kuna mambo mmeongea,nilikuwa karibu hapo nikaona nipitie hapa!”
“Mbona Mama sijaongea nayeye chochote”
“Kassim,niambie shemeji yako alipo!Hata kama alikwambia usiseme alipo,wewe niambie tu sitomwambia!Najua ni rafiki yako mkubwa sana”
Jambo hilo lilimfanya Kassim,ashushe pumzi kidogo na kumtizama Ahmed kwa umakini anayeropoka maneno hayo kirahisi rahisi kama mlevi wa gongo, wakati tayari hata yeye alikuwa amekufa ameoza kwa penzi Hajrath!




Hakuwa tayari kuzungumza ukweli wowote kuhusu Hajrath alipo,japokuwa alikuwa yupo ndani chumbani kwake alikuwa tayari siri hiyo abaki nayo kifuani mpaka atakapofukiwa mavumbini lakini sio kuzungumza chochote!Hakuelewa ni kwa namna gani anautesa mtima wa Ahmed,hilo lilikuwa wazi kwani macho ya Ahmed yalikuwa mekundu mno!Yalionesha kuchoka kwa kila kitu,hata hivyo hakuonesha kukata tamaa,alimuangalia Kassim akiamini huyo ndiye ingekuwa rahisi kumsaidia!
“Sijui alipo”
“Hakuna rafiki yake yoyote unayemjua labda?Wa karibu”
“Hapana”
“Au nimekumbuka kitu kimoja,Instagram una followers wengi, nitakutumia picha yake umposti”
“Nimposti Hajrath?”
“Ndio”
“Nitafanya hivyo”
Alikuwa ana kila sababu ya kumshauri Kassim afanye hivyo kwani aliamini sana mitandao ya kijamii ina nguvu mno na watu wengi hutumia kupata habari mbalimbali,hata hivyo aliondoka akimsisitiza kuwa angerudi kwa mara nyingine ili ajue mchakato mzima umefikia wapi!Ahmed alikuwa nyuma ya pazia, hakuelewa kabisa kwamba mdogo wake ni mkia wa fisi na kila kitu alichokua anazungumza Hajrath aliyekuwa bafuni anasikia,alimuonea sana huruma mumewe akatamani kutoka ili ajisalimishe lakini alijionya akiamini kwa kufanya hivyo, ingekuwa hatari kubwa!Akiwa bafuni mlango ukafunguliwa akamuona Kassim amesimama mbele yake!
“Vipi, ameshaondoka?”
Hajrath akahoji,akionekana ni mtu mwenye wasiwasi sana!
“Ndio,kasema atarudi tena”
“Lini?”
“Mimi sijui”
“Kwani unaogopa?”
“Siogopi lakini…”
“Lakini nini Kassim?Hutaki mimi nikae hapa?”
“Sio kwamba sitaki,nakupenda Hajrath nataka sana ubaki hapa!Tutaishi hivi mpaka lini?”
“Una maana gani?”
“Kwanini usiombe talaka ili tuishi kihalali?”
Kassim akatoa dukuduku lake,hakutaka kuendelea kuishi kwa wasiwasi kama kifaranga cha kuku kikimuona mwewe!
“Kassim sio rahisi,unadhani Ahmed atakubali?”
“Msimamo wako tu”
“Unataka vita vya tatu vya dunia lakini niache nifikirie kwanza”
“Au bado unampenda?”
Maswali mfululizo,aliyonyeshewa Hajrath yalimfanya akasirike na kuchukizwa,akatoka bafuni na kuelekea chumbani ambapo huko alikaa kitako na kumtizama Kassim anayeendelea kuhoji maswali magumu ambayo majibu yake yalihitaji utulivu wa kutosha!
“Sitaki huyu jamaa ajue kabla hujaomba talaka”
“Nitajitahidi”
“Lakini nina wazo,kwanini sasa hivi usijitokeze kwanza ili upunguze kasi yake!Maana ataenda polisi,mbele kutakuwa kugumu”
“Kassim,sijakuelewa”
“Urudi nyumbani kwanza”
Kuanzia hapo Hajrath alitulia kimya,akijaribu kutafakari maneno ya Kassim ambayo kwa wakati huo alimfananisha na mtu anayebwabwaja tu,ki ukweki hakuwa tayari kurudi kwa Ahmed hata angetokea mtu amuwekee kisu shingoni!
“Siwezi kurudi kwake,mara mia nikaishi msituni na masokwe”
“Nina mipango nawewe”
“Ipi?”
“Rudi kwanza mimi nitakuja huko huko”
“Kassim,ushapata unachokitaka tayari!Kukuvulia nguo im…”
“No please usiende huko tafadhali”
“Kumbeee?Kumbe nini?”
Moyo wake ulimuuma,hakuwa tayari kurudi kwa Ahmed lakini pia Kassim alimuumiza mtima kwa wakati mmoja kwani alimuamini na kujipa matumaini kwamba hapo ndipo yangekuwa makazi yake milele,akili yake ikashindwa kufikiria nje ya boxi, japokuwa mara kadhaa alimkumbuka mtoto wake,Babrah!
“Sawa,nitaondoka”
Hatimaye akazungumza maneno hayo,akiwa katika sura ya upole na utulivu wa hali ya juu!
“Sio kwa maana mbaya lakini”
“Poa”
Akajibu na kusimama wima,haikueleweka kama ndiyo safari ama anaenda seblen!

****
‘AHMED MAMBO,SAMAHNI KWA KILA KITU.NIPO SALAMA,KILA KITU KIPO SAWA NIPO ARUSHA NATAKA KUKUTOA WASIWASI KWAMBA MM MZIM,NAKUTAKIA MAISHA MEMA,MIMI VERONICA’
Ahmed alisoma ujumbe huo wa simu akiwa ndani ya gari lake mataa ya Mwenge usiku wa saa saba,anarejea nyumbani kwake!Moyoni alikosa utulivu,kichwani alitawala Hajrath!Hiyo ilifanya mpaka mfumo wake mzima wa fahamu ushindwe kufanya kazi vizuri,akashindwa kufanya kazi kabisa kila kukicha akawa anazunguka sehemu mbalimbali kumuulizia Hajrath!Japokuwa Hajrath hakuwa mtu wa kupenda starehe na mla bata lakini siku hiyo alizunguka kwenye club zote jijini kuanzia Club lemambo,Bill canaz,Maisha club lakini huko kote alimkosa na kuamua kurudi nyumbani kwanza ili atafakari ni njia gani atumie,ghafla akapata wazo la kwenda kwa waganga wanaopiga Ramli ili wamtajie ni wapi alipo lakini akalitupilia wazo hilo mbali akijua fika angeenda kutapeliwa kwani hakuna mganga wa namna hiyo,alivyofika nyumbani kwake akapaki gari na kuteremka lakini alishtuka baada ya kukuta taa za seblen zinawaka!
“Stress hizi,zitaniua”
Kivyovyote aliamini kutokana na msongo wa mawazo hakukumbuka kuzima taa asubuhi alivyotoka,lakini kitendo cha kuingia ndani moyo wake ulipiga kwa nguvu kwa mshtuko alichokiona mbele yake, kilimfanya asiamini,akabaki ameganda kama barafu!
“Nimemleta huyu hapa”
Kassim alisema,akionesha kama mtu mwenye wasiwasi akajaribu kulificha hilo, pembeni yake alikaa Hajrath,anaangalia chini!
“Kassim,ahsante sana!Mungu akubariki”
Kutaka kujua Hajrath alikuwa wapi ingeamsha hisia nyingine tofauti,hata hivyo hakutaka kuhoji jambo hilo mbele ya Mdogo wake Kassim bila kujua anachokifanya kilikuwa ni afadhali kwao!
“Hajrath”
Kassim akaita!
“ABEE SHEMEJI”
Hajrath akaitikia kichwa kikiwa chini bado,hakutaka kumuangalia mtu yoyote usoni kwani wote walikuwa wanaume zake,alihisi aibu!
“Kwani kuna nini?Ahmed kuna nini?Nini kimetokea?Muda wote huo kumbe alikua kwa Tausi”
Kassim akazungusha maneno,aliongea hivyo makusudi ili atengeneze picha nzuri,hakutaka kabisa Ahmed aanze kuhisi kwamba alikuwa kwake kwani hiyo ingeibua maswali mengi sana!Ndiyo maana akazuga kwamba hajui chochote,alivyohakikisha kaweka na kusawazisha kila kitu akajifanya kuaga na kuondoka zake huku nyuma akiwaacha wanandoa hawa wanatizamana!
“Hajrath I’m so sorry”(Hajrath nisamehee)
Ahmed akavunja ukimya lakini badala yake Hajrath akasimama na kupandisha ngazi ambapo huko aliingia bafuni akaoga na kujitupa kitandani,akianza kutafakari na kujilaumu ni kwanini amerudi nyumbani hapo!

Siku hiyo usiku Ahmed alirudi na zawadi kedekede,mfuko mzima ulijaa nguo na kadi pamoja na maua chungu mzima,akijaribu kurudisha penzi lake akiomba msamahaa kwa kila kitu. kilichotokea,jambo hilo lilimfanya Hajrath afurahi na kusahau kila kitu kwa muda mchache ingawa bado aliendelea kumuwaza Kassim na raha alizompa kwa muda mfupi waliokutana!Waliendelea kuchati na kupigiana simu usiku na mchana,wakijuliana hali bila Ahmed kujua akatamani ahame kabisa nyumbani mbaya zaidi siku moja akiwa katikati ya tendo la ndoa na mumewe alilitaja jina la Kasim jambo lililomfanya Ahmed,ashtuke sana lakini alimezea baada ya Hajrath kujitetea hata hivyo Ahmed alikubali lakini kishingo upande!
“Nimekumisi,laaziz”
Siku hiyo usiku,Hajrath akiwa katika nguo ya kulalia inayoonesha kila kitu yupo kitandani anazungumza na Kassim,alikuwa amelala chali umbo lake limebinuka na alikaa mkao wa kutega na wakati mwingine alivyokuwa katikati ya mazungumzo alikuwa akijitomasa maziwa!
“Mimi pia mpenzi wangu”
“Kesho naomba nikuone Kassim wangu,natamani tuishi wote!Najutia kwanini nilikuzungusha,nani kakufundisha mapenzi?”
“Si wewe hapo”
“Mmmh muonee,aku sio mimi”
Hajrath alijilegeza macho yake makubwa kiasi,yakawa kama yanataka kudondoka akajigeuza kwa mapozi lakini ilikuwa kidogo apige kelele baada ya kumuona Ahmed yupo nyuma yake,mlangoni anamtizama!Hakuelewa ni kwa muda gani alikuwa anamsikiliza,hakuwa ana uhakika kama mazungumzo yote yalisikiwa,alibaki ameganda akahisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi mkali,alichokifanya Ahmed ni kusogea taratibu mpaka alipo Hajrath akaichukua simu na kuiweka sikioni!
“Hallooo”
Akasema,hakuwa ana uhakika kama Kassim mdogo wake ndiye anazungumza na Hajrath ama mwingine kwani katika maongezi hayo alisikia jina hilo!
“Hallooo”
Ahmed akasema tena lakini matokeo yake,simu ikakatwa!Alichokifanya ni kuitizama namba ya simu,akachukua simu yake na kuziiingiza kwake,alichokiona kilimfanya apigwe na butwaa lisilokuwa na mfano wake,jasho jingi lilimtoka puani!Mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu,bado hakuamini kama mdogo wake angeweza kumfanyia jambo kama hilo la kishetani,kifua chake kikaanza kupanda juu na kushuka taratibu,macho yake yakaanza kubadilika rangi akaweka simu sikioni ili azungumze na Kassim ingawa hakuelewa ni kitu gani amwambie.
“Kassim…..”
Ahmed aliita lakini alishindwa kumalizia sentensi yake,machozi yakaanza kumtoka yakapita mashavuni na kulowanisha shati lake,haikueleweka zilikuwa ni hasira ama uchungu wa kumegewa mke na mdogo wake!
“Mmeanza lini mahusiano na Kassim?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed huku akipangusa machozi yake akitumia viganja vyake vya mkononi!
“Nakuuliza mmeanza lini mahusiano na Kassim?Ni mdogo wangu lakini,kwan…ni?Kwa…nini mmenifa..nyia hivi?”
Mikono ya Ahmed ilianza kutetemeka kama mtu mwenye kifafa,hiyo ilimaanisha hasira zake zimepanda mpaka kiwango cha juu kabisa,alishindwa kuhema!Mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu,haamini alichokishuhudia wakati mwingine alijilaumu kunyata na kufungua mlango kimya kimya!
Hajrath alivyoona hivyo,akaanza kurudi nyuma akitumia makalio mpaka kwenye pembe ya kitanda, Ahmed nayeye akapanda kitandani na viatu,akarusha kofi lakini lilimkosa kosa Hajrath kwani aliruka kama swala upande wa pili,akatoka kitandani na kusimama kwenye kingo ya kitanda,Ahmed akamfuata Hajrath akarudi upande wa pili,kwa kuwa kitanda kilikuwa katikati hiyo ilifanya waanze kuzungushana,Ahmed akienda huku Hajrath anaenda kule!Bahati nzuri ilikuwa kwa Hajrath akawa upande ulipo mlango wa kutokea,akachomoka kwa kasi na kuanza kukimbia,kutokana na hofu badala ya kukanyaga ngazi ya kwanza akakanyaga ya pili na kuteleza,akabiringika kama mpira mpaka chini akahisi maumivu makali shingoni na mgongoni,alivyotaka kusimama Ahmed akawa tayari amemfikia akamvuta na kumtandika kibao cha uso,kilichomtupa mpaka juu ya kochi,hasira za Ahmed zikapanda akavua mkanda na kuanza kumchapa nao!Kelele alizopiga Hajrath hazikuzaa matunda kwani Ahmed alizidi kumshambulia mpaka akaanza kutoa damu puani!
“Leo nakuua,kahaba wewe”
Kifo kilikuwa mlangoni,hasira za Ahmed zilimpanda kiasi kwamba misuli ya shingo ikasimama uso ukawa mwekundu misuli ya kichwa imesimama,anamkaba Hajrath aliyekuwa chali juu ya kochi!
“Arghhsaarhh Ah…med naaku…fa”
Hajrath alijaribu kutoa sauti lakini alishindwa,shingo yake ilibanwa kwa nguvu mno akaanza kuishiwa nguvu taratibu na hewa,katika hali ya kushangaza mlango ukafunguliwa kwa nguvu!Haikuleweka ilikuwaje mpaka Kassim akafika kwa muda mfupi,akamvaa Ahmed na kikumbo ambapo alipepesuka!Akasimama wima akamtizama Hajrath aliyekuwa juu ya sofa anahema kwa mbali,damu zinamtoka puani!
“Wewe ndio nilikuwa nakutaka”
Ahmed akasema akiwa na hasira bado,akamvaa Kassim mzima mzima wakatupana chini!Ahmed,akawahi kuamka na kumpiga teke kali Kassim bila kujali ni mdogo wake waliyezaliwa tumbo moja hasira zilimuongoza,hiyo ilimfanya Kassim ashindwe kuvumilia kwani kuendelea kutulia ilimaanisha kipigo kisingekoma,Hajrath alitamani kusimama aamulie ugomvi akashindwa, hakua na nguvu hizo tena,akarudi kwenye kochi mzima mzima na kutulia tena,akishuhudia mtu na kaka yake wanapigana!
Kassim yupo chini,Ahmed yupo juu anampiga mdogo wake kama mwizi,kwa hasira alizokuwa nazo kitu kuuwa kilikuwa mbioni kutokea hata hivyo Kassim hakukubali maumivu aliyohisi hakutaka yaendelee tena ndiyo maana kwa nguvu za ajabu,akajikusanya na kumsukuma Ahmed,akadondokea upande wa pili!
“Ahmed tuliaaa…”
Kassim akasema kwa Jazba huku akimsogelea akitaka kumshika lakini alichelewa,akapigwa ngumi ya pua iliyomfanya aone nyota na maluweluwe,akapigwa kikumbo na kudondokea meza kubwa iliyokuwa na poti la udongo la kuwekea maua,vyote vikadondoka!Ahmed,akapanda juu ya Kassim ili amshambulie lakini bahati mbaya akateleza na kudondoka,hapo ndipo ukawa mwanya wa Kassim kuchukua poti la udongo na kumpiga nalo utosini,kilichosikika ulikuwa ni mguno wa Ahmed hapohapo ukimya ukatawala!Ahmed,hakujitingisha tena akabaki ametulia chini!
“Ahmed punguza hasira broo,ngoja nikwambie”
Akiwa anahema akawa anamuongelesha Ahmed lakini matokeo yake kulikuwa na ukimya!
“Ahmed….”
Akaita na kumsogelea karibu,akainama na kumshika kwa namna ya kumtingisha lakini hakukuwa na dalili yoyote ya Ahmed kujigusa!
“Ahmed,Ahmed”
Kassim akazidi kuita,akainama kidogo na kumgeuza,moyo wake ukapiga kwa nguvu akaomba Mungu isiwe kama anavyofikiria,akasogeza sikio lake kifuani kwa Ahmed hapo ndipo alipopigwa na butwaa baada ya kugundua mapigo ya moyo ya Ahmed,hayadundi kumaanisha kwamba amefariki dunia!


Mwili wa Yusrath Suleiman ulikongoroka kwa kiasi cha kutosha,ukiachana na ‘stress’ za kesi iliyokuwa inamkabili mbeleni lakini kuna jambo lilianza kumsumbua akiwa maabusu!Kukohoa na kutapika mara kwa mara kulimfanya,awe na mawazo chungu mzima!Wazazi wake walishindwa kuelewa kwanini hali hiyo inatokea,ilibidi siku moja wamuombe mmoja wa maaskari wakampime. Haikuwa kazi rahisi ikabidi wapenyeze noti ya shilingi elfu kumi ili kusukuma mchakato huo kwa haraka!Jambo hilo likafanyika na siku mbili baadaye majibu yakapatikana kwamba Yusrath ana ujauzito wa miezi miwili!Jambo lililowafanya wazazi wake washike tama!Walichoka sababu hawakuelewa ingekuwaje mbeleni,walitambua ni kwa jinsi gani Yusrath angeteseka akiwa maabusu akiilea mimba,hakika angekuwa katika wakati mgumu sana na kwenye mateso mengi!
Mbali na kuomba dhamana wakitumia mimba hiyo kama ngao lakini haikuwa rahisi hata kidogo,kuna jambo liliwaumiza sana vichwa vyao!Kuhusu baba wa mtoto huyo aliye tumboni,asilimia kubwa ya fikra zao walidhani ni lazima mimba hiyo ingekuwa ya Bilionea George Charles,ambaye kwa wakati huo hata yeye alikabiliwa na kesi nzito mno,hawakuelewa ni wapi wangeomba msaada, wakatamani kumtafuta Ahmed popote alipo lakini walishindwa wangeanza vipi kwa mabaya waliomfanyia!
Siku zote mkono akiunyea mtoto haukatwi,Mzee Suleiman na Mkewe hawakuacha kumtembelea Yusrath maabusu,ambapo hawakuelewa hatma ya kesi yake ingekuaje!Waliendelea kumpelekea chakula kama kawaida bila kuchoka,wakati mwingine walifanya zamu!Mchana kaenda huyu asubuhi kapeleka chai yule.Tumbo la Yusrath lilianza kuwa kubwa na hali yake ilizidi kuwa mbaya zaidi,midomo yake ilikauka na wakati mwingine ilianza kutoa uteute mweupe!Mbali na hapo mara kwa mara alikuwa akiharisha,hizo zilikuwa dalili mbaya sana iliyofanya mpaka mmoja wa maaskari alipeleke jambo hilo kwa wakubwa zake wa kazi!
“Yupi?”
Kamanda,Elias Chacha aliuliza siku hiyo akiwa ofisini kwake baada ya kuletewa taarifa ya mmoja wa maabusu ana hali mbaya!
“Yule, Yusrath Suleiman”
“Ukiniambia Yusrath Suleiman nakuwa sikuelewi,njoo na faili lake”
“Sawa mkuu”
Swala la faili halikuwa tatizo na baada ya hapo,Kamanda Elias Chacha akasimama mpaka maabusu ili kumuona mgonjwa huyo anavyoendelea na hali yake,hata yeye alivyomuona alijisikia huruma!
“Fanyeni fasta,aende hospitali!Piga simu kwa ndugu zake,mkutane huko huko”
Jambo hilo likafanyika kwa haraka,Yusrath na tumbo lake akapakiwa kwenye gari maalum mpaka hospitalini,ambapo huko alianza kuchekiwa kipimo kimoja baada ya kingine!Dakika sitini baadaye majibu yakawa tayari na bahati nzuri wazazi wake,wakawa tayari wamewasili ili wazungumze na Dokta Bernald Mwakatobe,alikuwa ni daktari kijana ambaye kila wakati alionesha tabasamu lakini baada ya kuisoma karatasi hiyo mpaka mwisho,sura yake ikabadilika kidogo akaonekana kama mtu mwenye simanzi,kuna kitu wazazi wa Yusrath walijifunza kupitia sura ya Dokta, Bernald Mwakatobe!
“Nyie ndio wazazi wake?”
Dokta Bernald Mwakatobe,akavunja ukimya baada ya Yusrath kumaliza kukohoa kikohozi kikavu!
“Yes ndio sisi”
“Okay”
“Mme wake huyu yuko wapi?Au anayehusika na hiyo mimba”
Swali hilo likawa gumu kidogo,hapo ilibidi wote wamgeukie Yusrath atoe majibu yaliyo nyooka!
“Yusrath,jibu swali”
Baba akasema!
“Mumewe ana matatizo kidogo,hayupo nchini”
Mama,akatia neno kwa namna ya kumkingia binti yake kifua!Alichojua yeye mimba niya George Charles na kwa wakati huo yupo gerezani,isingekua busara kuyaanika hayo mbele ya daktari.
“Well,tumechukua vipimo vyote!Mtoto yupo salama,bp ipo vizuri!Lakini kitu kimoja hakipo sawa”
“Kitu gani dokta?”
Dokta Bernald akamtizama kila mmoja wapo kwa zamu,akaitizama karatasi iliyokuwa mezani kwake kisha akakohoa kidogo!
“Yusrath ni HIV Positive,ana maambukizi ya virusi vya ukimwi”
Hakuna mtu aliyekuwa tayari kupokea majibu hayo,wakabaki wameganda kama barafu!Yusrath aliangua kilio kikubwa sana,akashindwa kuelewa ugonjwa huo kautolea wapi na nani alimuambukiza,fikra zake zikamtuma kwa Ahmed,lakini alivyotulia hakukubaliana na hilo alivyomkumbuka George Charles,akaishiwa nguvu kabisa,ghafla mawazo yakampeleka kwa Samir lakini hilo lisingekuwa rahisi!
Alivyotuliza kichwa vizuri,akakumbuka siku aliyobakwa baada ya kutoka kumuibia pesa bilionea George Charles na baada ya hapo Martha Msoso akamtosa maporini,hapo ndipo akabakwa na kupata mimba pamoja na virusi vya ukimwi kwani wabakaji hawakutumia mpira waliingia peku peku bila ndala,Yusrath alihisi kujuta akalia kwa uchungu!Hakuelewa angeishi vipi na ugonjwa huo pamoja na mtoto ingawa daktari alimpa moyo na kumhakikishia kwamba mtoto angezaliwa akiwa salama kabisa, alichotakiwa kuzingatia ni mfumo wa kumeza dawa na aina ya vyakula!
“Mto..to wa..ngu hana baba”
Yusrath akasema kwa uchungu kwikwi ikiwa imembana,akakumbuka siku zote mkataa pema pabaya panamwita,akalia na kusaga meno akijuta na kujuta zaidi jinsi alivyokuwa na Ahmed,akatamani siku zirudi nyuma abadilishe kila kitu kilichotokea lakini hilo lisingeweza kutokea,mwisho wa siku akakubali kila kitu kilichotokea akayaacha mambo kama yalivyo!

****
Swala la Bilionea George Charles, lilikuwa gumu sana,kesi yake ilifikishwa ngazi za juu na kumfikia Raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania,jambo lililomfanya ashindwe kupenyeza kitita cha shilingi billion moja kama hongo ili hakimu alegeze kesi,alichokifanya ni kuwatafuta wanasheria mbalimbali ili kumtetea lakini mwisho wa siku kesi ikawa ngumu,akahukumiwa kifungo cha miaka mitatu gerezani,alijisikia uchungu mno na alivyomkumbuka Yusrath moyo wake ulimuuma sababu ndiye mwanamke aliyemuingiza shimoni,akajuta kushikiwa akili na mwanamke huyo shetani mwenye mapembe!Hata hivyo sheria ni msumeno hukata huku na kule ndiyo maana, haikumuacha Martha Msoso salama,nayeye akasukumwa ndani na kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani,kwa kosa la kuiba pesa!

****
Mwili wa Sporah Trevez,uliwatatiza maaskari na usalama wa taifa kwa ujumla!Mgongoni alikuwa na mchoro mkubwa wa tatuu wa nyoka aina ya ‘dragon’ kwenye mikono kuna michoro mbali mbali ya maua pamoja na samaki!Kilichowachanganya zaidi wapelelezi ni baada ya kupekua begi lake na kukuta ana passpot nane za nchi tofauti tofauti huku yakiwa na majina tofauti,jambo lililowafanya wasijue ni raia wa nchi gani!Hata hivyo,waliendelea kumuhifadhi monchwari kwani mwili uliharibiwa na risasi za maaskari waliokuwa katika ‘ambush’ kali pamoja na walinzi wake!Florian Jackson,haikuchukua muda sana kesi yake kuisha,akahukumiwa kifungo cha maisha katika magereza ya Ukonga,hakuna mtu yoyote aliyemuonea huruma kutokana na ukatili aliofanya!Kutokana na operesheni hiyo kwenda kikomandoo na kwa haraka,Mzee Kajeme akaitwa kitengo cha usalama wa taifa,akatunukiwa cheo na kupandishwa ngazi!Hiyo ilimaanisha angekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa taifa,jambo hilo lilimfurahisha sana na alijisikia amani kupita kawaida!Lakini akiwa ofisini kwake,alishtuka baada ya kusikia simu inaita.Akatoka pembeni,akaitizama namba ilikuwa ngeni,akaiweka sikioni!
“Naongea na Mr.Kajeme?”
Upande wa pili wa simu ulisikika!
“Nani mwenzangu?”
Mr.Kajeme akauliza swali,likawa swali juu ya swali.
“Ni mkazi wa Kurasini,njoo alipopanga mwanao kuna matatizo kidogo”
“Hallo sikusikii vizuri”
Simu ilikatika,kilichomshangaza Mr.Kajeme ni kelele zilizokuwa upande wa pili!Wengi walikuwa wakisema neno ‘Moto moto moto’Mzee Kajeme akatafakari na kutulia kidogo,jambo la kwanza lililomjia lilikuwa ni mwanaye, Kassim.

*****
Ahmed,alikuwa chini sakafuni,amelala hajigusi!Kulikuwa kuna dalili zote kwamba amefariki tayari!Kila kitu kikabadilika,ulikuwa ni msala mkubwa endapo swala hilo lingegundulika hivyo ilikuwa ni lazima wachukue uamuzi mgumu wa kuuweka mwili wa Ahmed ndani ya gunia ili wakautupe mbali wapoteze ushahidi,Kassim alitetemeka ilikuwa ni lazima wafanye jambo hilo hatari bila kugundulika usiku huo!Hajrath akiwa analia,akamshika Ahmed upande wa kichwani Kassim upande wa miguu wakaanza kumbeba na kumuweka kwenye gari,viti vya nyuma!
“Tuna..enda kumtupa wa..pi?”
Hajrath aliuliza huku akilia machozi,moyo ulimuuma akamtizama Ahmed ambaye alikuwa amefumba macho haongei tena,hakutegemea siku moja kama angekuja kuingia kwenye mkasa kama huo hatari!
“Sijui Hajrath,yote umetaka wewe!Malaya wewe”
“Nim…efanya nini?”
“Nimemuua kaka yangu!”
Kassim alizungumza akitetemeka,hofu ilimtanda na alimuangalia Hajrath bila kummaliza,walichokifanya ni kuchukua gunia,Kassim akawasha gari safari ya kuondoka ikaanza mara moja!Usiku huo waliomba Mungu,wasishtukiwe kwani ungekuwa ni msala mkubwa kwao!Bahati nzuri ikawa kwao kwani walivyofika Mbweni walisimama baada ya kuona kichaka kizito. Kassim,akachepuka upande wa pili na kuingiza gari katikati ya msitu huo wenye miti mirefu huku akizima taa za gari!
“Tutamtupa huku,inabidi siri hii ibaki kifuani!Hakuna kusema chochote”
“Sawa”
Wakala kiapo,wakamteremsha Ahmed kwa namna ya kumburuza na kumvalisha gunia mwili mzima,wakambeba mpaka katikati ya pori na kumuweka huko chini ya mti mkubwa ambapo pembeni kulikuwa na kichuguu,giza lilikuwa nene lakini kilichowasaidia ni mwanga wa mbalamwezi!
“Tuondoke sasa hivi,twende Kurasini kwangu kule”
Hakuna mtu aliyekuwa na raha hata kidogo,wakaingia ndani ya gari na kuondoka zao,wakiamini kwamba tayari Ahmed amefariki dunia!
Dakika thelathini zilikuwa nyingi,gunia likaanza kucheza,haikueleweka kama ulikuwa ni muujiza ama kiini macho sababu kilichoanza kuonekana ni mkono wa Ahmed,ukiwa umetokeza nje!Akajigusa gusa na kujitoa nje,maumivu ya kichwa aliyohisi hayakuwa na mfano wake,mwili wake ulikuwa mzito kwa kiasi cha kutosha na kila alipojitahidi kuvuta kumbukumbu zake sehemu aliyopo alishindwa kabisa.Tukio lililomjia mara ya mwisho ni meseji alizokuta kwenye simu ya mkewe mbaya zaidi zilitoka kwa mdogo wake,Kassim!Hata hivyo walimshambulia,wakidhani amekufa wakamuweka kwenye gunia hakuamini hata kidogo kama mdogo wake angeshirikiana na mkewe kufanya unyama kama huo!Akajikongoja adoado na kutokeza barabarani,kila sehemu alihisi maumivu,bahati nzuri ikawa kwake akaona pikipiki inakatiza akapunga mkono,bodaboda ikampita na kusimama mbele kabisa lakini baadaye ikageuza na kurudi mpaka miguuni kwake!
“Nipeleke Kurasini”
“Usiku huu kaka”
“Nisaidie tafadhali,nilivamiwa na majambazi wakanitupa huku”
Ahmed akaingiza mkono mfukoni na kutoa noti sita za shilingi elfu kumi,dereva akaingiwa tamaa bila kujiuliza chochote akamruhusu Ahmed apate nyuma!
“Pole ndugu yangu,ilikuaje tena?”
Dereva akahoji lakini Ahmed hakujibu chochote,alivyofika Kurasini kazi yake ilikuwa ni kumuelekeza dereva mpaka kandokando ya Msikiti ambapo hapo aliamini angeshuka isingekuwa rahisi kwa Kassim na Hajrath,kumuona!Alivyompatia dereva ujira wake tu,akaanza kutembea huku akichechemea,mpaka nje ya nyumba aliyopanga Kassim,akashangaa kwani hakuna gari nje kumaanisha kwamba bado hawajafika,aliamini wangefika eneo hilo lazima sababu kwa mbali aliwasikia wanazungumza baada ya kumtupa porini!Mlango ulikuwa wazi,akasukuma na kuingia ndani akatembea kwa tabu mpaka kwenye sofa na kukaa akiwa anahema juujuu kwa hasira,hakuelewa ni kitu gani akifanye lakini baada ya kuangalia kushoto akaona mlango wa jikoni, ambapo kando kulikuwa na mtungi mdogo wa gesi juu kuna jiko,bila kujifikiria akatembea na kuufungua ukaanza kutoa kimlio mithili ya tairi la gari linalotoa upepo,akachukua kiberiti cha gesi na kutulia juu ya kochi akiwasubiri Hajrath na Kassim!
Kitendo alichokuwa anaenda kukifanya kilikua ni hatari lakini hilo hakujali kabisa akiamini kwamba watakaobaki wasingeweza kujua nini mkasa wa hadithi hiyo ya kusisimua!
“Buriani”
Akasema huku akihisi harufu kali ya gesi inayozidi kusambaa nyumba nzima!Hazikupita dakika sita,akasikia muungurumo wa gari akanyanyuka na kuvuta pazia!Moyo wake ukazidi kupiga kwa nguvu baada ya kuwaona Kassim na Hajrath wanateremka kutoka ndani ya gari tena wanabembelezana kimahaba na kumtaja taja,akarudi kwenye kiti na kutulia akisali jaribio lake lifanikiwe bila kikwazo!
“Mungu wangu,Kassim!Sijui kama nitaweza Ahmed kul…”
“Hajrath,naomba usimwambie mtu yoyote yule kilichotokea iwe siri yetu hili lishatokea,mimi mwenyewe nimechanganyikiwa”
Kassim alizungumza,bado walikuwa na wasiwasi mkubwa baada ya kudhani wamemuua Ahmed,kila mtu alikuwa na mashaka na hofu!Wa kwanza Kassim akasukuma mlango na kugeukia nje,akimwambia Hajrath aingie ndani kitendo cha Hajrath kufika,alipiga yowe kali la mshangao baada ya kumuona Ahmed amekaa kwenye sofa,anavuja damu mdomoni nguvu zilimuishia akajua ni lazima ulikuwa mzimu,Kassim alivyogeuka akahisi amepigwa na ganzi,akaganda kama sanamu haelewi kinachoendelea,Ahmed alikuwa mbele yao analia machozi tena kwa kwikwi,bila kupoteza muda na kutafakari mara mbilimbili,akawasha kiberiti cha gesi!
Kilichotokea hapo ulikuwa ni mlipuko mkubwa wa moto mithili ya bomu la kutegwa.Wakazi na majirani wa eneo hilo,walitoka mbio mbio kuangalia kilichotokea,moto ulikuwa mkubwa sana na haikujulikana chanzo cha moto huo,hata hivyo walijitahidi kuzima bila mafanikio,mpaka kunakucha baada ya kupata msaada wa gari la kikosi cha kuzima moto!Nyumba hiyo haikuwa ngeni machoni mwa Mr.Pascal Nyanda,ilikuwa ni lazima ampigie simu mzee Kajeme amueleze kila kilichotokea!
Saa tano ya asubuhi ndipo walifanikiwa kuzima moto huo mkali,watu wengi walizingira nyumba,askari wakaingia ndani ili kuangalia kama watapata masalia yoyote yale!Hawakuambulia chochote zaidi ya majivu tu.
“Kulikuwa na watu humu?”
Askari mmoja,akamuuliza mwenzake!
“Sidhani,inabidi tuwaulize majirani hilo swali”
Hakukuwa na dalili yoyote ya mtu kupona ndani ya moto huo,Hajrath,Kassim pamoja na Ahmed waliteketea na kugeuka majivu kabisa!Huo,ndio ukawa mwisho wao duniani.

********MWISHO********

*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG