Search This Blog

Monday, March 23, 2020

ABEE SHEMEJI SEHEMU YA 3/10


ABEE SHEMEJI
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 3 KATI YA 10
*******

Uzuri na muonekano wa kuvutia wa msichana Yusrath ulizidi kuunyanyasa mtima wa Mtoto wa Bilionea George Charles,ambaye kwenye mamilionea waliokuwa kwenye chati pia kijana huyo mdogo aliwekwa.Lakini wachache sana waliijua sura yake,pesa alizokuwa nazo na mali alizomiliki
vilikuwa tofauti na muonekano wake hakuwa mtu anayejionesha kwa watu,mbali na hapo alivaa kawaida na kuendesha magari ya kawaida tu.Hilo lilifanya watu wabishane mtaani kama ikitokea wakiambiwa ‘Yule ndiye milionea George Charles!’Kitu ambacho kiliwafanya wafanyakazi wake wa kike ofisini, wamzoee na kujigonga kwake, baada ya kusikia hajaoa yaani hana mke wala mtoto,wengi walitamani nafasi hiyo!Kama kawaida ya wanawake wengi wa kibongo, hupenda wanaume wenye pesa na uwezo,walijipitisha kila kukicha lakini hawakuambulia kitu.
“Boss kahawa”
Mwanamke huyo,ambaye alikuwa sekretari wa George, siku hiyo aliingia ofisini kwa bosi wake.
“Ahsante Monica,baadaye”
Katika wanawake waliokuwa na ndoto ya kutembea na George Charles kimapenzi ni huyu Monica,kila kukicha aliendelea kumuwinda lakini hakufua dafu kwani akili ya George, ilikuwa kwa Yusrath siku zote.Ndiyo maana siku hiyo hakumaliza kazi zake.
“Niitie Emmanuel Bruno Ndunguru”
Monica,akakatishwa mazungumzo alichukizwa lakini hakuwa nala kusema,akanyoosha moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya mkurugenzi msaidizi,akagonga na kuingia!
“Unaitwa na boss”
“Sawa,nakuja”
Mkurugenzi msaidizi Emmanuel Ndunguru,alisimama wima na kujiweka vizuri akanyoosha mpaka kwa bosi wake.
“Simamia ofisi,hakikisha kila kitu kinaenda sawa!Natoka kuna suppliers watakuja wale Hamaka,wakifika nipigie simu”
“Sawa boss”
George Charles,hakuwa mtu mwenye maneno mengi sana!Hiko ndio kisa cha wenzake akiwa chuo kumbatiza jina la Baba Paroko,sura yake ilikuwa ya kipole sana!Siku hiyo alipanga baada ya hapo,anyooshe moja kwa moja mpaka Kariakoo akaonane na Yusrath,kwake kumuona tu angefarijika!Akatembea mpaka kwenye maegesho ya magari akawasha na kuanza kutembea,kichwani kwake alimuwaza Yusrath tu na wala sio kitu kingine,alivyowasili Kariakoo,akaweka gari vizuri na kushuka!Akatembea mpaka dukani ambapo hapo, kulikuwa na mkusanyiko wa wateja wengi! Akasubiri mpaka wapungue,ndipo akasogea karibu kabisa!
“Mambo”
George Charles,akatoa salamu huku akimtizama Yusrath aliyekuwa katika tabasamu mwanana,hilo ndilo lilifanya mapigo ya moyo ya George Charles yapige kwa nguvu!
“Nilikusubiri juzi,hukuja”
“Nilisafiri”
“Leo,kuna mizigo mipya imeingia.Perfume nzuri kutoka Dubai,si unajua Dubai walivyo na marashi mazuri,kuna zingine zimetoka Oman”
Yusrath akaanza kupiga debe,fikra zake zilimtuma George yupo mahali hapo kama mteja lakini haikuwa hivyo bali mwanamme huyo alikuwa eneo hilo kimawindo!
“Ebu nipatie ile”
“Subiri,chukua hii hapa ni nzuriiii hiyooo”
Wakiwa katikati ya maongezi yao mwanamme mmoja aliwakatisha baada ya kusimama pembeni ya George, alikuwa ni Ahmed amefika na kusimama pembeni,hiyo ilimfanya Yusrath ashtuke bila kutegemea.

******
Umbali mrefu waliokuwa, haikuwa rahisi kwa mtu yoyote kuwakuta,japokuwa alikuwa hoi bin taaban lakini alikaza mwendo,mwanamke aliyembeba mgongoni mwake hakuwa na undugu naye lakini alijisikia kumsaidia!Akazidi kusonga mbele, mpaka alipotokeza barabara ya lami,ambapo huko kulikuwa na magari yanapita kwa kasi,akajaribu kusubiri ili aombe msaada,kutokana na mavazi aliyovaa haikuwa rahisi kwa mtu yoyote, kuhatarisha maisha yake na kusimamisha gari katika eneo hilo lenye msitu mnene na mzito!Alivyoona zoezi hilo ni gumu,akamlaza Hajrath pembeni na kusimama katikati ya barabara lakini hapo ndipo alipoharibu kabisa,kwani madereva waliokuwa ndani ya magari walimpita kando na kutimua mavumbi,hakukata tamaa!Akazidi kupunga mkono,gari lililokuwa linakuja mbele yake limewasha taa kali lilimfanya aogope sababu lilikuwa katika mwendo wa kasi.
“Chino,angalia mbele!Kuna mtu Yule umemuona?”
Ndani ya gari kulikuwa na wanaume watano waliokuwa na silaha za moto,wana hasira kwa kiasi cha juu kabisa,hiyo ni kutokana na kumkosa mwanamke waliyekuwa wanamsaka kwa muda mrefu,walichoamua kufanya ni kuchoma kijiji cha Nazareth moto na kutimua kwa kasi ya ajabu!Wakiwa katikati ya safari yao, wakitumia mwendo wa kilomita ishirini kwa dakika,ghafla walimuona mwanaume amesimama mbele katikati ya barabara umbali wa kama mita mia mbili,mavazi aliyovaa yaliwaogopesha ndiyo maana walikoki bastola zao ili kujihami kwa lolote litakalo tokea.
“Atakuwa kichaa tu,katokea huko porini”
“Sio jambazi kweli?”
“Kama ni jambazi,basi itakuwa ni sawa na mbuzi kufia kwa mpika supu”
“Unataka kufanya nini?”
“Nasimama”
“Tuna haraka lakini”
“Niachie mimi”
Mwanamme anayeitwa Chino,ndiye alikuwa nyuma ya usukani anaendesha gari,akapunguza mwendo na kusimama bastola yake ikiwa katikati ya miguu yake,akiwa tayari kwa kufanya lolote lile!Akasimama na kufungua kioo
“Naomba msaada”
“Wewe ni nani?Usiku unafanya nini hapa?”
“Nisaidieni,kuna watu wanataka kutuuwa”
Mwanakijiji huyo bila kujua,anaingia kwenye mdomo wa mamba akasema maneno hayo!
“Msaada gani sasa unataka?”
“Nina mgonjwa,nataka tufike hapo mjini”
“Hakuna nafasi,tupishe”
“Nisaidieni,sina pa kwenda nitakufa”
“Mwambie aingie”
Jamaa mmoja aliyekuwa nyuma aliyeonekana mwenye mamlaka kuliko wote akaamuru,akawa kama ameingiwa na huruma!Chino,akakubali,akateremka na kutembea kwa hatua chache na kumuweka Hajrath mgongoni,akampakia ndani ya gari, safari ikaanza mara moja,kwa umbali kidogo walivyotembea barabarani.Mmoja akamtizama Mwanamke aliyekaa kushoto kwake,amelala!
“Ndio huyuuuuuuu!”
Jamaa huyo akaropoka kwa sauti baada ya kumuona Hajrath,yupo kandokando yake tena ndani ya gari.



“Weka bia nyingine,waongeze na hao wotee!Kwenye bili yangu”
“Tutafika kweli?”
“Niamini mimi,ngoma lazima ifikee”
“Wewe ni mgeni wa barabara lakini”
“Nimeendesha magari mengii sanaaaa,Scania za kila aina.Malori yalee,Masaa machache hapo!Tunaingia Mbeya Tanzania,niamini mimi…Kabla ya kuamsha popo, inabidi nipunguze kichupa kwanza”
“Tutaondoka sasa hivi kweliii?”
“Tatizo lakoo nini hasaa Mjuni,au wewe mgenii kwenye hizi kazi?”
“Hapanaa”
“Sasa?”
“Basi tu.Safari ni ndefu sana,tukianza kunywa mapema hivi!Majanga”
“Acha uwoga,dada muongeze nyingine!Wewe kaziii yako kutuliiaaa kaziii na dawaa”
Bwana Solomoni Kibwenzi,hakutaka kubanduka katika kilabu cha pombe, kabla ya kuweka vitu vyake kichwani,ilikuwa ni lazima kwanza anywe pombe kwani kwake ilikuwa ni kazi na dawa!Hakuwa peke yake, pembeni alikuwa na utingo wake ambaye siku zote humsaidia akiwa safarini na lori.Tabia ya Bwana Solomoni ilikuwa ni ulevi wa pombe, yaani pombe nayeye yeye na pombe!Japokuwa huendesha gari vizuri kwa masafa marefu, akitokea Afrika Kusini Mpaka Tanzania,ambapo kabla ya kufika ni lazima apitie nchi kama Zambia na Zimbabwe!Huendesha safari ndefu mno na yenye kuchosha!Bwana Solomoni siku hiyo alikunywa pombe nyingi mno usiku wa siku hiyo,alivyotaka kusimama akarudi kitini!Hiyo ilimuogopesha mpaka utingo wake!
“Solo,tutafika kwelii?”
“Shut up!I said shut up,funga bakuli lakoooo,mimi nimeanza kuendesha gariii.Enzi na enzii.Sasa hiili ni gariii,tuondoke kwanzaaaa.Tusepe!”
Bwana Solomoni,alianza kupepesuka hatua moja mbele, kumi nyuma! Akatembea mpaka kwenye lori aina ya Scania,lililokuwa na tela. Nyuma limebeba makontena mawili.
“Hilii garii ni puliiiing aiseee,ingia kwenye gari bwashee!Tuamshe poopoooo!Breki ya kwanza Namibia hapa,ngoma imesimama kideteee”
Pombe alizokunywa dereva huyo aliyefahamika kwa jina la Solomoni, usiku huo zilikuwa nyingi mno!Hiyo ilifanya mpaka kichwa chake kiwe kizito,anahisi kizunguzungu kikali lakini hakutaka kukubaliana na hali hiyo.Akapiga lori funguo likaanza kuunguruma,akaweka gia na kulitoa! Hapohapo akaliingiza barabarani.Macho yote yalikuwa mbele ya barabara ya lami ambapo hakukuwa na magari mengi, hiyo ilifanya abadili gia namba kumi,lori lilikuwa katika mwendo wa kasi usio wa kawaida.Kilichompa bichwa ni barabara hiyo kuwa nyeupe, hiyo ilimfanya akae katikati ya barabara, akazidi kupandisha gia na kunyoosha mguu!Lori lilikuwa katika kasi ya ajabu,mbaya zaidi lilibeba makontena nyuma!
“Uwogaaa tuuu,hapa tunafikaaa zetuuuu….Salamaaa kabisaaaa,Mimi ndioo Solomoniii!Raisi wa Madereva wote dunia hii na hata nikifa,kama huko mbinguni kuna magariii,nitapewa cheo!Niwaongozee maderevaaa wengiineee marehemuu”
Solomoni alijiongelesha akijitapa mwenyewe huku akibadili gia na kucheza na usukani.Ni kweli alikuwa dereva makini, ndiyo maana waliweza kuzikata kilomita arobaini bila kupata shida yoyote ile.Alivyofika katika barabara ya tambalale,akaendeleza mwendo wake uleule!Akiwa katikati ya barabara,mbele yake kulikuwa na kona kali,ambapo hapo alikunja kwa kulala nayo akafanikiwa kuikunja!Akapandisha gia na kusonga mbele zaidi!Spidi ikazidi kuongezeka na kuwa kubwa sana.
“Weweeee,una lala?Unakuwa kama Mwanamkeee bwaaaana,amkaaaa”
Solomoni alikuwa amegeuka nyuma,ambapo kulikuwa na kitanda!Akasahau kuangalia mbele,kitendo cha kurudisha shingo yake mbele na kutupa macho barabarani,hakuamini macho yake umbali wa mita kumi kulikuwa na gari ndogo aina ya Pajero,mwendo wa kasi aliokuwa nao, ilikuwa ni vigumu kupiga breki, alichofanya ni kutoka saiti yake lakini hiyo ilishindikana sababu nyuma alibeba makontena,alichoharibu ni kupiga breki, hapo ndipo alipofanya lori lianze kuserereka!

*****
Majambazi waliokuwa ndani ya Pajero,walishtuka baada ya kusikia mwenzao anapiga kelele kwamba mwanamke waliyekuwa wanamsaka wapo naye ndani ya gari,hiyo ilimfanya dereva ageuze shingo!Ni kweli mwanamke aliyelala alikuwa ni Hajrath.
“Muuwe”
Dereva,akasema sentensi hiyo na kugeuza shingo mbele!Alichokiona kilimshtua,mbele yake kulikuwa na Scania kubwa,lipo katikati ya barabara linakimbia kwa kasi kuja upande wake kumaanisha kwamba asingechukua maamuzi ya haraka basi ilikuwa ni lazima wakutane uso kwa uso!Kwa kasi ya mwewe akazungusha usukani ili kuikwepa ajali hiyo!Lakini alikuwa tayari amechelewa,lori lililobeba makontena ambalo lilikuwa linaserereka liliwafikia na kontena zote kudondoka,moja liliponda ponda gari hilo, vibaya sana,ilikuwa ni ajali mbaya ya kutisha.Iliyosababishwa na uzembe wa madereva kutokuwa makini barabarani,kutokana na picha iliyokuwepo hakukuwa na dalili ya mtu yoyote yule kutoka hai ndani ya gari ndogo,damu zilitapakaa kwenye vioo zikaanza kusambaa juu ya lami,hakika ilikuwa ni ajali ya kutisha, usiku huo!

******
Siku zote wivu unahusika kwenye mapenzi ya kweli,lakini ukizidi unakuwa karahaa na kero!Kitendo cha Ahmed kutokeza dukani na kumuona Yusrath anacheka na kutabasamu na wanaume kilimuuma mno!Fikra zake zikamwambia moja kwa moja, kwamba wanaume hao wanakula naye sahani moja,isitoshe mwanamme aliyesimama kando yake.Amevaa kawaida,huyo ndiye alifanya moyo wa Ahmed utibuke kwa kiasi cha kutosha,ndiyo maana akaanza kumtizama kuanzia juu mpaka chini.Hakuelewa ni mwanaume wa aina gani kasimama naye,hakuelewa mwanaume aliyesimama pembeni yake ana wadhifa gani.
“Nimekuja kukutoa lunch leo”
Ahmed akasema kwa sauti ili George Charles, asikie.
“Sasa hivi?”
“Ndio”
“Ngoja basi nimalizie”
“Sawa nakusubiri”
Ahmed,akaganda eneo hilo akawa amekaba mpaka penati.George alivyoona hivyo akashindwa kuongea maneno mengine zaidi,akaaga na kuondoka zake huku akimtafakari Ahmed ni nani mbele ya Yusrath,wakati mwingine alidhani wenda ni kaka yake,moyo ulimuuma lakini hakuwa na jinsi!Hata hivyo aliapia ni lazima amwambie ya moyoni Yusrath na ikiwezekana wafunge ndoa haraka iwezekanavyo,hizo ndizo zilikuwa ndoto za Mtoto wa Bilionea,aliyeitwa George Charles!

****
Japokuwa walifika mgahawani na kuanza kula lakini kwake bado kuna kitu kilianza kumsumbua,hakutaka kubaki kimya ilikuwa ni lazima aulize.
“Baby,Yule nani?”
Ahmed akaibua swali akimtizama Yusrath, machoni.
“Yupi baby?”
“Yule niliyemkuta pale dukani”
“Mteja tu”
“Mbona alivyoniona,akaondoka?”
“Nilikuwa nishamalizana naye!Baby acha wivu,utakufa kwa presha”
“Lazima nijue Darling”
“Yes ni haki yako.Naona leo,ukaamua kunifanyia ziara ya kushtukiza”
“Ndio maana yake,nilikuwa ofisini.Muda wa lunch ulivyofika nikasema no!Ngoja nije kula nawewe!Unajua nakupenda sana”
“Naelewa hilo Sweatheart”
“Ahsante kwa kulijua”
Siku hiyo Yusrath,alitia fora!Kila mtu alimwangalia,hakuwahi hata siku moja kuonekana na mwanamme wanakula pamoja tena wakicheka kimahaba namna hiyo,waliokuwa wanamtaka msichana huyo waliingiwa na wivu hawakuacha kumkodolea macho,mpaka wanamaliza kula na Ahmed anamuachia pesa Yusrath yote waliona.
Wakajua wenda msichana huyo amempendea Ahmed pesa!Siku iliyofuata na wao wakajaribu kuiga,wakaingia kwa gia za pesa lakini wakatolewa nje,wakatoswa!Hakuna hata mmoja kati yao,aliyeambulia kuwa na Yusrath msimamo wa binti huyo,ulikuwa ni palepale,mtu yoyote yule hakuweza kumyumbisha na kuutingisha msimamo wake,moyo wake ulikuwa tayari umedondoka kwa Ahmed!Mwanamme aliyeonesha niya ya kuwa naye katika maisha yake yote,hilo aliliamini kwa asilimia zote mia moja!

*****
Mingo na misele aliyokuwa anapiga George Charles,ilikuwa ya kiu utu uzima.Hakutaka kufanya papara!Alishajiwekea ni lazima kabisa Yusrath angekuwa wake siku moja,hata kama ingemchukuwa miaka mia moja mbele,kila siku alikuwa akiwaza ni mbinu gani atumie.Akanunua mpaka ‘diary’ yake ndogo ya kuandika njia atakazotumia.Kwa utu uzima aliokuwa nao na kuishi sana Marekani kulimfanya awe mjanja na kufuata mambo hatua kwa hatua,siku zote aliamini ya kwamba asingeweza kulala na kuamka kesho asubuhi akawa na Yusrath,ilihitajika mipango na mikakati mathubuti.Ndiyo maana akaandika kwenye ‘diary’ hatua tano atakazofanya ili kumnasa Yusrath!
“Nampenda Yusrath,atakuwa wangu siku moja”
George Charles aliapia kimoyomoyo huku sura ya Yusrath ikiwa kichwani kwake,ikajenga kama taswira!Akamuona alivyokuwa katika tabasamu,akaenda mbele zaidi na kuwaza siku ambayo, watakuwa pamoja wapo na watoto wao wanacheza kwenye bustani ya maua,mara wanakimbizana!Kifupi alikuwa ni kama anaangalia sinema ya kihindi.Kama kawaida siku hiyo kazi,hazikufanyika!Ilibidi amuite msaidizi wake kwa mara nyingine ili amsaidie kufanya kazi zake,akatoka na kuingia ndani ya gari lake!Safari ikaanza hapohapo ya kuelekea Kariakoo!Alivyofika dukani,akachungulia huku na kule lakini akamkosa,akapata jibu la haraka hapohapo, baada ya kuangalia saa yake ya mkononi,akagundua kwamba muda huo ulikuwa wa kula.Akatembea kwa hatua chache mpaka kwenye mgahawa ambao jana yake alimuona Yusrath anaingia,akazama ndani!Ni kweli,alikuwa ni kama ametabiri vile kwani alimuona akiwa meza ya mwisho,akasogea mpaka alipo!
“Mambo”
George Charles,akasalimia.
“Safi”
“Naweza nikakaa?”
“Yeah,karibu”
George Charles,akavuta kiti na kuketi pembeni yake!Akatabasamu kidogo na kumuangalia Yusrath usoni aliyekuwa na sura ya kipole,macho madogo kama mchina!Mashavu yametokeza kiasi kama mdoli,hiyo ilimfanya George aendelee kumkagua kwa kitambo kidogo,Yusrath akaangalia chini kwa aibu.
“Inaelekea una aibu sana”
George akavunja ukimya.
“Ndio,sipendi mtu aniangalie sana machoni”
“Unaweza vipi,kuwamudu wateja sasa?”
“Kama umegundua,siwaangalii sana usoni kwa muda mrefu”
“Nitalichunguza hilo”
“Usijali,umejuaje kama nipo hapa?”
“Jana nilikuona unaingia na jamaa mmoja smart sana,sijui ni nani?”
George,akauliza swali kwa mtego!
“Kumbe uliniona?”
Yusrath akaelewa yupo mtegoni,hakutaka kuingia akazuga.Hapohapo chakula kikaletwa!
“Mimi niletee Juisi”
George Charles,nayeye akaagiza.Kilichofuata hapo ukimya kutawala,walivyomaliza kula.George akaomba azungumze,mawili matatu!
“Hilo duka lako?”
George,akataka kujua zaidi.
“Hapana”
“Umeajiriwa?”
“Hapana,kwa wazazi wangu”
“Wazazi wako wapi?”
“Wapo,hapahapa!Kuna duka lingine kule mtaa wa nyuma”
“Well, vizuri sana…Nimependa uchapakazi wako.Una elimu gani?”
Swali hilo lilimfanya Yusrath,anyamaze kidogo na kumtizama George, ilielekea maswali sasa yashaanza kuwa kero kwake,kuna jibu la shombo alitaka kujibu lakini akaupiga mdomo wake ‘stop’ kwanza!
“Sorry,unaishi wapi?”
George Charles,akabadili mada alishaelewa swali lake lilikuwa kero!
“Ilala”
“Lini upo free?”
“Niko bize,sina free”
“Mfano,nikikutafutia kazi nyingine ufanye!Utaweza?”
“Kazi gani?”
“Marketing manager,kwenye kampuni”
“Yeah nitaweza,kwanini nishindwe?”
“Nimependa ukarimu wako,nataka nikuweke sehemu”
“Sehemu gani?”
“Posta,Mpya!Samora Avanue pale.Kuna nafasi pale nadhani itakufaa kuna kampuni moja inaitwa Hajreymer”
Moyo wa Yusrath,ukapiga kwa nguvu!Hakuelewa ni furaha ama mshtuko,kirahisi rahisi namna hiyo anapata kazi, tena kwa mtu ambaye hamjui.Wakati mwingine kuna vitu alianza kuhisi, wenda mwanamme huyo ni fisadi tu mpiga porojo,anamtaka hivyo anaingia kwa sera ya kumtafutia kazi ili amvue nguo yake ya ndani.Baada ya kutafakari sana,akalitupilia wazo hilo mbali.
“Lini nije kuiona kwanza ofisi?”
“Siku yoyote ile ukiwa tayari”
“Mmmh,Vipi Ijumaa itafaa?”
“Saa ngapi?”
“Nikitoka msikitini,saa saba”
“Njoo”
George Charles akasimama kidogo na kutoa kadi,akamkabidhi ambayo juu iliandikwa HAJREYMER INVESTMEST chini imeandikwa dealers in Furnitures,home appliance,stationeries and impoters of all kind of used car.Kwa chini kidogo Managing Director George Charles,macho yake hayakuishia hapo!Yakashuka chini na kuona namba za simu.Hakutaka kuliweka kichwani kwamba George Charles ndiyo huyo anayezungumza naye,kwa kuwa hakulikumbuka jina lake.
“Namba zako hapa ni zipi?”
“Zozote zile”
Yusrath,akamtizama George Charles na kushindwa kummaliza,mambo yaliyoandikwa kwenye kadi yalikuwa tofauti nayeye,ndiyo maana hakuzingatia sana!Akajua tu,ni wale wale matapeli wanaochonga vitambulisho feki ili wawatongozee wanawake hata baada ya kuwaza hayo yote,hakutaka kupuuzia.
Siku hiyo walivyoachana akarudi dukani kama kawaida,hakutaka kuwaambia wazazi wake wala Ahmed, juu ya jambo hilo,ilivyofika siku ya Ijumaa baada ya kutoka kuswali,akatafuta bajaji,iliyompeleka mpaka Posta.Hapo baada ya kushuka,akatafuta kadi na kuanza kupiga namba za simu,ya kwanza haikupokelewa akajaribu namba ya pili iliyokuwa chini!Ilivyoita,ikapokelewa wakati huohuo!
“Habari,unaongea na HAJREYMER, INVESTMENT, tukusaidie nini?”
Sauti nyororo,upande wa pili,ilisikika!Yusrath akatulia kidogo,hakuelewa ajitambulishe vipi.
“Nahitaji kuzungumza nana na na…”
Jina likawa limemtoka,akachukua kadi na kuangalia.
“George Charles”
“Jina lako nani?”
“Yusrath Suleiman”
“Zungumza tu,tunaweza kukusaidia”
“Amesema,nionane naye”
“Yupo kwenye kikao.Subiri kidogo”
Hakukaa sana baada ya dakika tano,simu yake ikaita!George akawa tayari amepewa taarifa,ndiyo maana akampigia.
“Upo wapi?”
“Hapa,Samora Avanue!Kwenye hili lisanamu”
“Sawa nakuja”
Yusrath,akasimama na kutulia ili kumsubiri mwenyeji wake!Akiwa amesimama,akahisi kuna mtu kamshika bega,alivyogeuka akapigwa na butwaa la waziwazi!
“Ahmed!!”
Yusrath,akasema kwa mshtuko akiwa ameyatumbua macho yake haamini!Kilichomuogopesha zaidi,pembeani kwa mbali George Charles alikuwa anakuja,hapo ndipo mapigo yake ya moyo, yakazidi kudunda kama kitenesi,hofu ikamtanda!Akazidi kumuona George anazidi kumsogelea alipo.



Moyo wake ulipiga kwa nguvu,ukataka kutokeza nje ya kifua!Wasiwasi wake ulikuwa katika kiwango cha juu kabisa,alishaelewa nini maana yake kama Ahmed angemuona George Charles mahali hapo,akahisi kutetemeka mpaka mkojo ukataka kumpenya ndani kwa ndani!Lakini hapohapo,akili yake ikafanya kazi kwa kasi ya kimbunga.
“Darling,umenionaje?Njoo huku nikwambie kitu”
Yusrath akamvuta Ahmed kandokando ya barabara,akamuweka pembeni kabisa!Kazi ya Yusrath ilikuwa ni kusali kimoyomoyo, Ahmed asigeuke nyuma kwani angemuona George.
“Unafanya nini huku Love?”
Yusrath akaibua swali,akimwangalia George kwa jicho pembe, ambaye alisimama akiwa anaongea na simu.
“Ofisi yangu ipo pale mbele”
“Wapi?”
“Pale Benjamin”
“Nipeleke nikapaone”
Yusrath akasema kwa haraka huku akimvuta Ahmed mkono,lengo la kufika Posta halikuwa hilo hata kidogo,ilikuwa aonane na George, ambaye alimuhaidi atamtafutia kazi lakini badala yake, akakumbana uso kwa uso na Ahmed,alijisikia vibaya lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima aepushe ajali hiyo ambayo chanzo angekuwa ni yeye, wakavuka barabara upande wa pili lakini Ahmed akasimama na kumuangalia Yusrath!
“Baby,ofisi yangu ile pale juu”
“Sawa twende”
“Kwa sasa hivi,haitoleta picha nzuri!Isitoshe bosi yupo.Itakuwa ngumu kidogo kuanza kuingiza wageni alafu ndio kwanza kazi nimeanza juzi”
“Baby,usijali.Lakini ningependa kujua ofisi yako”
“Hilo ondoa shaka,siku moja utafika”
Wakiwa katikati ya mazungumzo simu ya Yusrath ikaanza kuita,akaitoa kiuwoga kuangalia juu ya kioo!Aliyekuwa anapiga ni George Charles,akatafakari kwa muda na kutulia kidogo,akamtizama Ahmed, ambaye alikuwa akimuangalia.Simu ikaendelea kuita mpaka ikakata,ikaanza kuita kwa mara nyingine!Swala la kuacha simu hiyo mpaka ikate kwa mara ya pili,lingezuia hali ya sintofahamu kwa Ahmed,hapohapo akapokea na kuiweka sikioni.
“Nakuja sasa hivi”
Kitendo cha kuzungumza maneno hayo,akakata simu na kumtizama Ahmed ambaye macho yake yalionesha kutaka kujua simu hiyo ,ilipigwa na nani.
“Kuna mteja pale dukani,ananisumbua!”
“Dukani umemuacha nani kwani?”
“Hafsa”
“Sawa,muwahi basi huyo mteja!Mimi bado nipo kazini,ulikuja kufanya nini Posta?”
“Kuna mtu nilikuja kumuona”
“Acha niwahi tutawasiliana”
Ahmed,akatembea na kuingia ndani ya ofisi akimuacha Yusrath nje!Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake kuchukua simu na kumtafuta George hewani,akimwambia amsubiri upande wa pili!Baada ya kumaliza hapo,akavuka barabara mpaka upande aliomuona George Charles, ambapo huko alimkuta,amesimama! Akaachia tabasamu kidogo na kumsalimia kwa staili ya kupeana mikono.
“Nilikuona hapa,mara ukapotea ghafla.Ulienda wapi?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka Kwa George Charles.
“Nilienda pale Benjamin”
“Okay,twende ofisini.Nikakuoneshe”
George Charles na Yusrath wakaanza kutembea kwa miguu mpaka walipolifikia jengo moja kubwa na kuingia ndani,ambapo nje kulikuwa na walinzi wamesimama wakampa heshima kubwa, George!
“Mgeni wangu huyu,siku yoyote mkimuona hapa!Msimsumbue hata kidogo”
Maagizo hayo aliacha langoni akiwaambia walinzi wake,ambao bila kubisha wakaitikia.Alivyoingia ndani akakumbana na heshima zisizokuwa na idadi kamili.
“Anaitwa Yusrath,mkimuona hapa!Mruhusuni apite”
Siku hiyo Yusrath alijihisi kama malaika, jinsi George alivyokuwa anampitisha ofisini akimtambulisha mbele za watu kama mgeni mmoja maalum,hiyo ilifanya wafanyakazi wake wampe heshima!Bado alishindwa kuelewa kama George ndiye mmiliki wa ofisi hiyo nzima ama aliwapanga watu wajifanye kumpa heshima ili ampumbaze.
Mbele yake kulikuwa na wasichana warembo wamevalia sare zilizofanana, wapo nyuma ya kompyuta zao,Yusrath akazidi kustaajabu, juu kabisa akaona kombe kubwa chini limeandikwa pongezi alafu jina la George Charles pembeni yake.
“Boss,kuna haya mafaili.Wanahitaji TPA yapo tayari”
Mmoja wa wanawake,akatokeza na kumsogelea George!
“Niletee ofisini baadaye”
“Alafu,alikuja Philipo!Anadai,keshakutumia kwenye akaunti yako!Anasubiri Quotation”
“Hilo swala lipo kwa Fredy,analishungulikia nenda ofisini kwa Fredy,muulize alafu uje kunipa jibu”
Yote hayo yalisemwa mbele ya Yusrath,George akapiga hatua nyingine mbili akiwa na Yusrath pembeni akafuatwa na mwanamme mmoja aliyevaa tai shingoni,kachomekea mkanda nje!
“Nimetumiwa email,utahitajika tena kwenye kikao kesho asubuhi sana Boss, Tata Investment”
“Nitumie kwenye email,nitaikuta!”
“Sawa boss”
Ubize aliokuwa nao George ulimfanya Yusrath atake kuuliza maswali mengi lakini kwa wakati huo alinyamaza kwanza mpaka walivyofungua mlango mkubwa, ambapo ndani kulikuwa na uwazi mkubwa,masofa ya gharama!Na pembeni kuna meza kubwa iliyonakshiwa vizuri, juu yake kuna kompyuta mbili, nyuma yake kuna kiti kikubwa cha kuzunguka juu pembeni ya kuta hizo kuna picha kubwa ya George, akiwa katika tabasamu,alivyoichunguza vizuri akagundua kwamba haikupigiwa sehemu yoyote ile barani Afrika,picha hiyo ilionesha akiwa amesimama juu ya mabarafu.
“Have a seat”(Kaa kitini)
George akasema na kunyoosha mkono kwenye moja ya viti viwili, vilivyokuwa pembeni yake,Yusrath akataka kukaa kwenye sofa.
“No,njoo hapa!Feel free,relax”
George akasema,akachukua rimoti ya kiyoyozi na kubonyeza,chumba kizima kikajaa ubaridi.
“Coffe ama Chai?”
“Hapana nina haraka”
“No,weka Baraka kwenye ofisi”
Hapo,Yusrath akashindwa cha kujibu.
“Silence means yes”(Ukimya unamaanisha ndio)
Alichofanya George ni kuinua mkonga wa simu,akaagiza kahawa vikombe viwili.Ndani ya dakika moja,mlango ukafunguliwa akaingia mwanamke ameshika vikombe viwili,akitumia trei,akaweka mezani na kuondoka zake!Katika vitu ambavyo hakuwahi kuviona ni hivyo,mambo kama hayo kwa Yusrath yalikuwa mageni kabisa,alizoea tu kuangalia kwenye filamu jinsi mabosi wanavyosalimiwa na kuagiza wakipewa heshima,akajua wenda ni maisha ya kuigiza lakini haikuwa hivyo!Yusrath akaenda mbali zaidi na kutamani siku moja awe na mamlaka kama George,awe anaheshimika kila kona!
“George”
Yusrath akaita baada ya kushusha kikombe cha kahawa mdomoni na kukiweka mezani.
“Yes please”
“Ofisi hii ni yako?”
“Ndio”
“No sio kweli,you are kidding”
“Why should i?”
“Hongera,hongera sana!”
“Ahsante,by the way.Maliza Kahawa,uwende ukaone ofisi yako!Ukiwa tayari uje uanze kazi”
“Kumbe ulikuwa siriazi”
“Ndio,ulijua utani?”
Hiyo ilifanya Yusrath,amalize kahawa yake haraka haraka ili akaoneshwe ofisi hiyo kwani jambo hilo kwake lilikuwa kama zali la Mentali!Hilo halikuwa tatizo kwa Mwanaume huyu George Charles,wakasimama na kutoka nje ambapo huko upande wa pili mlango wa tatu kulikuwa na mlango,walivyofungua wakakutana na ofisi yenye meza mbili!Lakini bado rangi,haijapakwa vizuri kumaanisha kwamba ilikuwa katika marekebisho fulanifulani.
“Hii ndio itakuwa ofisi yako,by keshokutwa itakuwa tayari.Are you ready?”
George akasema na kuuliza swali.Furaha aliyokuwa nayo Yusrath,haikuweza kuelezeka kiwepesi, akatamani amrukie George ambusu lakini hilo asingeweza kulifanya,shukrani alizotoa hazikuweza kuelezeka kiwepesi!
Swala hilo halikuishia hapo,akalipeleka mpaka kwa wazazi wake kama lilivyo,akaeleza kila kitu kilichotokea na mtu anayetaka kumpa kazi.
“Na shule je?”
Baba akauliza,akataka kujua mpango mzima wa binti yake!
“Nitasoma pia”
“Sasa utawezaje kupanda farasi wawili kwa wakati mmoja?”
“Sio farasi wawili baba, naenda kufanya kazi”
“Huyo mwanamme unamfahamu?”
“Ndio,alinipeleka ofisini kwake”
“Dunia,imebadilika sasa hivi.Kuna matapeli wengi mwanangu”
Mama nayeye,akatia neno!Siku hiyo walikuwa seblen, wanakula chakula cha usiku.
“Kabla ya kuanza.Tunahitaji kumuona huyo kijana hapa”
“Hilo halina tatizo wazazi wangu”
Huo ndio mkakati wa wazazi hawa,waliokuwa makini na binti yao!Kulivyopambazuka tu,akamtafuta George Charles hewani na kumpasha habari juu ya kila kitu kinagaubaga.
“Hilo jambo dogo sana kwangu,labda kama kuna lingine”
“Ni hilo tu George”
“Sawa,saa ngapi nije?”
“Jioni saa kumi na moja ama mbili”
“Nipe utaratibu”
“Tutakutana,Ilala Boma”
“Okay”
Yusrath,akazidi kuwa mwenye furaha!Akiwa dukani akataka kumpigia simu Ahmed ili amueleze kila kitu kilivyotokea,ghafla mteja akatokea,akasahau na kuanza kuhudumia!

******
Niya yake,haikuwa kumtafuna kama ‘big g’ kisha baadaye kumtema,alitaka awe mkewe wa maisha azae naye watoto,wajenge familia.Ndiyo maana alipambana usiku na mchana ili ahakikishe kwamba anamuweka Yusrath kwenye himaya yake,kitendo cha hatua yake ya kwanza kufanikiwa ilikuwa shangwe ndani ya mtima wake!Lilivyokuja swala la kutaka kwenda kwa wazazi wa Yusrath wamjue, likawa ndio dogo kabisa,akaamini hilo ndilo lingekuwa lina umuhimu zaidi kufahamiana na wazazi wa mwanamke anayempenda.Siku hiyo alivyokuwa ofisini, alitafakari vitu vingi sana, hususani nguo atakayotakiwa kuvaa.Ilikuwa ni lazima avae nguo ya heshima.Ndiyo maana ilivyotimu saa kumi jioni akawasha gari na kuelekea nyumbani kwake Masaki,huko alivyofika tu!Akanyoosha mpaka chumbani kwake kabatini na kuanza kuangalia nguo yenye heshima!Akafanikiwa kutungua suti ambapo,alitafuta na shati jeupe!Akatoka mpaka seblen na kumpa mmoja wa wafanyakazi wake.
“Nipigie pasi hiyo”
“Sawa bosi”
Alivyotokeza dakika mbili baadaye akakuta tayari nguo zimenyooka,akavaa na kuweka tai yake vizuri shingoni.Alivyotaka kuvaa koti,nafsi ikamwambia hapana.Hivyo ulivyo,umetoka chicha!Akanyoosha mpaka kwenye kioo kikubwa na kujitizama.Kila kitu kikawa kimekamilika,kilichomchanganya ni aina ya gari.Hakuelewa atumie gari ya aina gani kwani kwenye maegesho ya magari kulikuwa na magari nane ya kifahari na manne ya kawaida.Jumla alikuwa na magari kumi na mbili ya kutembelea!Hapo ndipo alipochanganyikiwa na siku hiyo hakutakiwa kwenda nyumbani kwa wazee hao kizembe, ilikuwa ni lazima aende amevimba ndiyo maana akapata wazo hapohapo na kumuita mfanyakazi wake.
“Nitolee,Vogue kwenye parking.Ifute vumbi”
Akiwa juu gorofani,alimwambia mfanyakazi wake!Jambo hilo likafanyika wakati huohuo!Lilikuwa ni gari la gharama,hakupenda kulitumia isipokuwa kwenye vikao vyake vikubwa ndio hupenda kutumia gari hilo la kifahari.Mambo yalivyokwenda vizuri akaingia ndani ya gari,akalirudisha kinyume nyume na kulitoa ndani ya geti,akatoka nje huku akianza kufanya mawasiliano na Yusrath.

******
“No,mimi sijaafiki”
“Ahmed please,nimekwambia nimepata kazi”
“Sio ghafla hivyo,mimi sio mtoto mdogo”
“Sasa ulikuwa unatakaje mme wangu?”
“Bado hujamaliza shule huna vyeti,inawezekana vipi?Hapo kuna namna,hakuna kitu chochote!Huyo jamaa anakutaka tu,niamini nachokwambia”
“Ahmed mme wangu,sio kama unavyofikiria.Hana hata mpango namimi kabisa sio wanaume wote wapo hivyo”
“Mh! Mh!Hutujui sisi wanaume,hizo ni njia tu za kukuweka karibu.Naelewa kila kitu hapo”
“Sasa nifanye nini?”
“Achana na hiyo kazi,sitaki”
Yusrath alikuwa simuni,anajaribu kumuelewesha Ahmed,mchakato mzima wa kazi ulivyokuwa na jinsi,itakavyokuwa lakini ilikuwa ni tofauti na alivyotegemea!Ahmed,aligoma na kukataa katukatu hiyo ilitokana na wivu.Jambo hilo likamfanya Yusrath apate kibarua kingine cha kumshawishi.
“Basi, chagua kimoja!Mimi ama kazi”
Yusrath akatamani kulia machozi,kila kitu kwake kilikuwa kigumu kuchagua.Ni kweli,siku zote alimsikiliza sana Ahmed na kumtii lakini katika swala hilo akawa mgumu kidogo.
“Nakupenda Ahmed,lakini pia usichukulie hiyo kama advantage ya kuniburuza buruza unavyotaka”
Yusrath,akaongea kwa ukali kidogo!
“Nadhani swali langu,hujalielewa.Kuna mawili, kubaki na mimi ama hiyo kazi?”
“Vyote…tititi”
Yusrath,akajibu na kukata simu kwa hasira!



Yusrath alikuwa amekasirika kwa kiasi cha kutosha,kitendo cha Ahmed kumnyima asifanye kazi alikitafsiri kama ubinafsi fulani hivi,japokuwa upande wa pili wa shilingi alikiri kwamba Mwanamme huyo ana haki ya kumzuia lakini haikuwa mapema namna hiyo kwani bado hakuwa mumewe wa ndoa,kuna vitu alikuwa ana uwezo wa kuvipiga vita lakini sio katika swala la kutafuta maisha!Yusrath hata siku moja hakutaka kuja kuwa mwanamke tegemezi,alitaka siku moja aheshimiwe aitwe ‘Bosslady’awe na pesa nyingi kwenye akaunti.Atembee nchi anazotaka,asafiri siku yoyote anayojisikia, ndiyo maana alivyosikia George anataka kumpa kazi,aliichangamkia fursa hiyo haraka iwezekanavyo,akawashirikisha hadi wazazi wake, ambao hata wao walimuunga mkono!Iweje Ahmed akatae?Yeye kama Nani?Mpenzi?Hayo ndiyo maswali yaliyokuwa yanazunguka kichwani mwa Yusrath.Licha ya hayo, moyo wake ulimuuma kumkatia simu,akatafakari tena upya!Akanyanyua simu na kumtafuta Ahmed hewani,matokeo yake simu iliita bila kupokelewa!Hakukoma, akapiga tena,alivyoona haipokelewi akatuma ujumbe mfupi ‘POKEA SIMU MME WANGU’Akajaribu kupiga tena lakini haikupokelewa,alivyotulia kwa kama dakika tano simu yake ikaita,akashtuka!Aliyekuwa anapiga si mwingine bali ni George Charles,Yusrath akajifikiria kidogo,akapokea na kuiweka simu sikioni.
“Ndio nakaribia kufika,upo wapi?”
“Mimi ndio nataka kutoka”
“Basi sawa,nikifika Ilala Boma nitakwambia”
Simu ilivyokatwa,Yusrath akaanza kujiandaa ili akaonane na George Charles kisha waelekee nyumbani,akamtambulishe kwa wazazi wake kama muajiri wake!Akiwa katika harakati za kutaka kuondoka akachukua simu na kumtafuta Ahmed kwa mara nyingine tena!
“Darling,I’m so sorry”(Mpenzi,nisamehee)
Hilo ndilo neno la Kwanza kulitamka Yusrath, baada ya simu kupokelewa.
“Usijali”
“Umekasirika?”
“No,nipo okay”
“Ahsante Mme wangu,samahani kwa kukukatia simu”
“Baby,usijali.Kuna kazi namalizia hapa!Nitakutafuta”
“Okay, Darling!I love you”
“Me too”
Ahmed,aliitikia kwa unyonge na kukata simu,moyo wake uliuma ajabu!Wivu ukapanda na kuwa katika kiwango cha juu kabisa,maongezi aliyokuwa anazungumza na Yusrath kwenye simu kwamba yupo shwari ilikuwa sio kweli,sababu alikuwa anaumia ndani kwa ndani.Kitendo cha Yusrath kumkatia sumu katikati ya maongezi, kilimuuma mno,akatafsiri moja kwa moja jambo hilo kama dharau.Hata hivyo hakuwa nala kufanya zaidi ya kufanya kazi zilizokuwa mezani kwake,jioni ilivyofika akafunga hesabu vizuri na kuweka kila kitu mahali pake.
Siku hiyo hakutaka kwenda nyumbani,alitaka kwenda sehemu moja iliyotulia apumzike na kutoa mawazo yanayomkabili,wazo lililomjia ni kwenda Texas Pub.Huko ndipo aliamini atapoteza mawazo na kufikiria mambo mengi, kuhusu maisha yake kwa ujumla!Akakodi Bajaj,iliompeleka Msasani,karibu na kituo cha macho!Akaingia ndani ya pub,ambapo hapo kulikuwa na wazee kwa vijana wanakunywa pombe wakifurahi,hapakuwa na vurugu sana eneo hilo,ndiyo maana alipapenda!Akatembea mpaka kaunta na kukaa kiti kirefu.
“Nipe Red wine”
Akamwambia dada mmoja wa kaunta,wine ikapimwa akapewa kwenye glasi!Akachukuwa simu yake na kuanza kuingia kwenye mitandano ya kijamii kama Instagram na Facebook ili kuperuzi,peruzi mambo mbalimbali.Glasi ya kwanza ilivyoisha akaagiza nyingine.Kuna kitu alikikumbuka cha ghafla,akaanza kutafuta namba mpaka alipofikia Kassim,akamtafuta hewani.
“Dogo,uko wapi?”
“External hapa”
“Una mishe gani?”
“Nipo tu naenda home”
“Sasa sikia,tafuta pikipiki uje hapa Texas.Msasani”
“Kuna nini broo?”
“Njoo dogo,ule bata”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaa! Broo bwana!Poa nakuja,lakini mtonyo wa bodaboda sina”
“Nitalipa,njoo”
“Poa”
Siku hiyo Ahmed alitaka kufurahi na mdogo wake,kwani tangu aanze kazi hakuwahi kumtoa wakiwa sehemu,akaagiza tena glasi ya tatu ya pombe!Baada ya hapo,akaanza kuhisi vitu vinapanda kichwani taratibu.Hakuwa na hili wala lile,akahisi kuna mtu kamshika begani,alivyogeuka hakuamini macho yake!Sura ya mwanamke huyo,isingeweza kumtoka hata kidogo, akasimama kwa heshima na kumpa mkono.
“Amney!”
“Ahmed!”
“Sasa naanza kuamini,milima haikutani lakini binadamu wanakutana”
“Kabisa,ujue nimekuona tangu kule.Nikawa nakufananisha,huyu sio Ahmed? Sasa ulivyogeuka kule nikasema ndio wewe”
“Wacha bwanaaa,naona sasa ushamaliza chuo?”
“Nashukuru Mungu,kitabu kimeisha.Nimepata sehemu ya kujiegesha”
“Wapi hapo,namimi unipe kibarua?”
Ahmed akaweka utani kidogo!
“Ah,acha masihara.Nasikia sasa hivi umekuwa mkurugenzi Posta huko,sijui ofisi gani.Hongera sana bwana”
Habari hizo zilimshtua kidogo Ahmed.
“Nani amekwambia?”
“Hapa Duniani,utanyimwa chakula lakini sio maneno”
“Una maneno wewe,unakunywa nini?”
“Reds”
Ahmed,akamuagizia kinywaji anachokunywa.Hawakukaa sana,Simu ya Ahmed ikaita akatoka nje sababu aliyekuwa anapiga ni mdogo wake, Kassim.Haikuchukuwa dakika nyingi,wakawa wameonana tayari,akamlipa dereva wa pikipiki.
“Dogo vipi?Nimekuita uje kuenjoy maisha”
“Shukrani”
“Usiwaze,mimi ni kaka yako!Nikipata,nakutafuta tunafurahi.Sina ndugu mwingine unajua”
“Ni kweli”
Wakanyoosha mpaka kaunta ambapo huko Amney,akatambulishwa kwa Kassim.
“Mmefanana!”
Amney,akatia neno.Kassim akaagiza kinywaji chake wakaanza kunywa.
“Umemwambia Dingi kuwa tupo wote?”
“Nitamwambia”
“Sababu tukitoka hapa,tunaruka sehemu nyingine ujue.Mpaka majogoo dogo”
“Duu,leo hatulali!”
“Kasema nani?Hakuna kulala leo”
Maongezi yaliendelea wakiwa na furaha,lakini kwa wakati huo mawazo ya Kassim hayakuwa hapo,yalikuwa kwa Amney,pepo lake la ngono likamvaa akaanza kumuangalia kwa macho ya kuibia akimthaminisha jinsi ya kumuingia!Alivyomuona anaelekea upande wa chooni,nayeye akamuungia hukohuko!Kisha kurudi,kuketi akiwa anatabasamu.Hapo hawakukaa sana,walimuaga Amney na kuondoka wakielekea kiwanja kingine.Wote kichwani walikuwa tayari wamewaka,yaani bwii.
“Nataaaka nimuoee Yusrath,mdogo waanguu alafu nikupee kamati ya vinywajii”
Ahmed,akaropoka akimwambia mdogo wake, hakuelewa sentensi hiyo ilikuwa kama mshale wa moto kwake,ili kudhihirisha hilo akaanza kumtafuta Yusrath hewani lakini simu iliita bila kupokelewa,akapiga tena.Ikapokelewa!
“Halloooo”
Ahmed,akapigwa na butwaa akahisi kama pombe zimeisha kichwani kwani sauti aliyosikia ilikuwa ya mwanaume,usiku huo.Jambo lililomfanya,apatwe na mshtuko mkubwa sana moyoni!

******
Mateso aliyokuwa anapata Jambazi anayeitwa Jitu Baya,yalizidi kipimo chake askari walimsulubu vya kutosha ili tu atoboe siri na kusema ni wapi mwanafunzi anayesoma chuo cha Makumira alipo.Katika kituo cha Central ndipo,alipohifadhiwa akipewa kila aina ya mateso, usiku na mchana lakini wapi!Hakuwa tayari kutoboa siri hiyo iliyokuwa ndani ya kifua chake.
“Umegoma kusema,sio?”
Afande Mkumbo,siku hiyo aliingia ndani ya chumba hiko kidogo, ambapo majambazi sugu huifadhiwa kwa ajili ya mahojiano!
“Kusema ukweli,mnanionea sijui chochote”
“Utajua tu.Na leo,ndio utajua kwanini kachumbari sio mboga lakini ina umuhimu kwenye pilau”
Urefu wa afande huyo na weusi wake,uliendana na maneno yake!Alikuwa mwenye sura mbaya ya kutisha,ilielekea kabisa ndiye waliyemtegemea kwenye shughuli kama hizo za kutesa majambazi sugu.Hilo lilikuwa wazi na sio mkwara sababu walimtoa katika kituo kikubwa cha Oysterbay.
“Naomba nikuhakikishie kwamba,utanitajia wenzako”
Afande Mkumbo,akatoka nje!Alivyoingia tena ndani ya chumba hiko, alikuwa ameshika plaizi na mkasi.
“Hakuna mtu yoyote Yule,aliyetoka humu akiwa na siri kifuani mwake!”
Kile alichokizungumza,hakikuwa mkwara ulikuwa ni ukweli mtupu, kwamba Afande Mkumbo,alikuwa ana roho ya kinyama,kwake yeye kumkata mtu masikio ama vidole, lilikuwa ni jambo la kawaida sana,ilimradi tu ukweli utajwe.Alichokifanya ni kusimama,akashika plaizi,bila kuuliza akamsogelea Jitu Baya na kuanza kubinya sehemu zake za siri.Mkononi akawa ameshika picha ya Hajrath Mpilla.
“Unamjua huyu bintiii?”
“Hapanaaaaaaa,simjuiiiiii”
Sehemu zake za siri ziliendelea kubinywa kwa nguvu,Jitu baya alijikaza kisabuni.Afande Mkumbo hakuishia hapo,akaendelea na zoezi hilo!Dakika mbili baadaye,adhabu ikabadilika!Mkono wake ukachukuliwa na kuwekwa mezani,bila kuulizwa chochote kidole kimoja,kikakatwa na kudondoka chini damu zikaruka.Kidole kinachofata kikashikwa!
“Florian,Florian Fre…drickiiiiii”
“Sikusikiiii”
“Florian Fredri….ckiiii”
“Kafanya nini?”
“Ndio anaj…ua”
“Yuko wapi?”
“South Africa,lakini anaingia Kesho kutwa tarehe mbi….li”
Jitu Baya,akazungumza kila kitu!Akamtaja Florian Fredrick ndiye mkandarasi wa mambo yote.Askari wakachukuwa maelezo na picha yake.

*****
Tarehe mbili mwezi wa saba saa kumi na moja jioni,wakawasha Diffenda na kwenda moja kwa moja Uwanja wa ndege Mwalimu Nyerere,ili kumuweka chini ya ulinzi Florian Fredrick.Askari wote wakawa wamevaa kiraia,haikuwa rahisi kuwagundua!Wakajigawa wakiwa makini kabisa kutizama lango la abiria, wanapotoka ili wamtie Mikononi Florian Fredrick,kivyovyote vile waliamini kupitia yeye wangejua ni wapi Hajrath Mpilla alipo!



Ilikuwa ni ajali mbaya,tena ya kusisimua.Kuna wengine walishika vichwa baadhi yao waliogopa na kuziba midomo kwa mshtuko,wanawake walikuwa waoga hawakuweza kuangalia mara mbilimbili.Mbele yao kulikuwa na gari lililopondeka pondeka na kilichoonekana hapo zilikuwa ni damu nyingi, pamoja vipande vya nyama.Kwa picha tu,hakukuwa na dalili ya mtu yoyote yule kutoka akiwa hai ndani ya ajali hiyo.Waandishi wa habari hawakutaka kucheza mbali,walifanya kazi yao ipasavyo,jeshi la polisi lilikuwa tayari limewasili eneo la tukio.Ajali hiyo ilisababisha barabara zifungwe na kufanya msongamano mkubwa wa magari.Kilichofanyika ni simu kupigwa ili gari maalum lenye winchi lije kuinua kontena lililolalia gari ndogo,haikuchukua dakika nyingi sana!Gari kubwa, likatokea na kuanza kunyanyua kontena taratibu.Hapo ndipo wenye roho nyepesi waliangalia pembeni,walichokiona hakikuwa rahisi kuandikika.Vichwa vya watu wawili vilikuwa pembeni vimekatika,mikono mitatu ilikuwa kandokando!Licha ya ajali hiyo kutisha namna hiyo lakini kwa askari ilikuwa kawaida sana kwao kushuhudia matukio kama hayo,ndiyo maana waliendelea na kazi yao!
“Fanyeni mvute hayo magari pembeni,maiti zipakieni kwenye gari!Zoezi hili liishe, mambo mengine yaendelee”
Sauti hiyo ilitoka kwa Kamanda Mtambwa Kialo,kiongozi wa operesheni hiyo, alitaka kwanza magari yaliyopata ajali yatolewe pembeni ili magari mengine yaendelee na safari.Katikati ya zoezi hilo,gari la wagonjwa likafika tayari kwa kupakia maiti ili ziende kuhifadhiwa monchwari.
“Afande”
Askari mmoja aliita kwa nguvu huku akionekana kushtuka baada ya kuchunguza huku na kule ndani ya gari ndogo,hiyo ilifanya askari wawili wasogee karibu yake.
“Kuna nini?”
“Embu tizama”
Wote wakatupa macho yao chini ya siti ambapo waliuona mwili wa msichana ukiwa umelowa damu,kilichowashangaza zaidi ni bastola za moto walizoziona ndani ya gari hilo.Tukio hilo, wakaliunganisha moja kwa moja na ujambazi.Kila askari akaanza kutafsiri jinsi alivyoelewa ajali hiyo.
“Huyu ni mzima,ana hema”
Afande mmoja akasema baada ya kumshika msichana waliyemkuta kifuani,walifanya hivyo kwa tahadhari sababu walikuwa wamevalia ‘gloves’ maalum.Haraka Msichana huyo akaingizwa ndani ya gari la wagonjwa ambapo ndani yake kulikuwa na madaktari watatu,ambao hapohapo walianza kushughulika naye!Uchunguzi ukazidi kuendelea,lakini hawakufanikiwa kumpata dereva wa lori na Utingo wake,wote walikimbilia kusikojulikana!Gari maalum la kupakia wagonjwa,liliendelea kupiga king’ola kuashiria magari yote yapishe barabarani,hiyo ilimaanisha ndani ya gari hilo kuna mgonjwa anayehitajika awaishwe hospitalini haraka iwezekanavyo.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwani walifika katika Hospitali ya St.Theresa ndani ya dakika chache,mgonjwa akashushwa kwa kasi na kuwekwa juu ya kitanda chenye magurudumu kwa chini,akaanza kukimbizwa kwa kasi mpaka ndani ya wodi ambapo huko,madaktari walimshambulia wakimpa huduma ili kuokoa maisha yake!Kilichowashangaza madaktari ni vidonda alivyokuwa navyo,kwa taaluma waliyokuwa nayo walielewa kabisa majeraha hayo,yalisababishwa na risasi sababu yalikuwa kama matundu matundu madogo.Hiyo ikafanya ilete hali ya sintofahamu,licha ya yote hawakuacha kumtibia sababu walipewa oda hiyo kutoka jeshi la polisi,ambapo baadaye maasakari wakafika na kumfunga pingu Msichana huyo akiwa hapohapo kitandani.
“Huyu ni jambazi,katika gari alilokuwepo.Tumekuta bastola nyingi,inaelekea walikuwa wanaenda kufanya uhalifu,wakapata ajali.Ana kesi ya kujibu”
Kamanda mmoja akasema,alikuwa ana kila sababu ya kuamini jambo hilo,sababu ya tukio zima aliloliona!Kwa takribani siku tatu nzima,waliendelea kumshughulikia mgonjwa huyo ambaye hata jina lake hawakulijua,mbaya zaidi hakuna ndugu yake hata mmoja aliyefika kumuona,jambo hilo likawapa jibu tosha kwamba ni jambazi na ilikuwa ni lazima baada ya hapo,wamuhukumu gerezani,hilo lilikuwa halina mjadala kabisa.

*****
Kumbukumbu zilianza kumjia taratibu sana,kichwani kwake kulikuwa na matukio ya kila aina ya kutisha,yakawa yanakuja na kupotea!Mara ya mwisho alijikuta amezinduka katika kijiji chenye binadamu wa ajabu,alivyofumbua macho yake na kutizama huku na kule,akamuona mwanaume mrefu kwenda hewani,amevalia koti jeupe shingoni amezungusha kifaa cha kupimia mapigo ya moyo!Hapo,bila kuuliza chochote alijua kabisa yupo hospitalini lakini bado hakuelewa amefika vipi eneo hilo na nani amemfanya afike mahali hapo,hilo ndilo swali lililomtesa.Mkononi mwake alikuwa na dripu ya maji ambayo ilikuwa nusu tayari.Daktari alivyomuona mgonjwa wake,amefungua macho alitabasamu na kumuendea kwa kasi.
“How do you feel?”(Unaendeleaje)
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Dokta Sajo Mlendwa,daktari bingwa ambaye kazi yake ilikuwa ni kukarabati miili ya binadamu wenzake,uhakika aliokuwa nao ni kwamba msichana huyo angepona na alikuwa tayari keshamuwekea dawa ya kuondoa sumu ya risasi alizopigwa,licha ya yote alitamani kujua tatizo la mgonjwa wake,licha ya kwamba hata yeye aliamini kuwa ni jambazi.Badala ya Msichana huyo kujibu,akageuza shingo yake upande wa pili,hapo ndipo aliposhtuka zaidi baada ya kuona ana pingu mkono wake mmoja, ambayo ilifungwa na chuma za kitanda.
“Kwanini mmenifunga pinguuu?”
Aliuliza kwa sauti ya mbali kidogo lakini iliyosikika.
“What did you just say?”(Unasema nini)
Ilielekea ni wazi kabisa ilikuwa ni lugha gongana!Daktari hakuelewa mgonjwa huyo anazungumza lugha gani.
“Why did you handcuff me?What did i do?I’m asking you what’s wrong,don’t you hear me?”(Kwanini umenifunga pingu?Nimefanya nini?Nakuuliza kosa langu,unisikii)
Akauliza kwa ukali kidogo,ingawa kwa mbali alikuwa anahisi maumivu ya kichwa,swala la kufungwa likamchanganya akili yake!
“Relax”(Pumzika)
“Why I’m i even here?Who brought me here?”(Kwanini nipo hapa,nani kanileta hapa)
Yalikuwa ni maswali mengi mno, aliyouliza kwa mfululizo.
“Relax you are safe here,just calm down and i will explain everything to you.Police brought you here unconscious, two days ago!They actually saved you from the car accident an….”
Kabla ya Dokta Sajo Mlendwa kumalizia anachotaka kusema,akaingia askari mmoja!Akatembea mpaka kandokando ya kitanda,wakasalimiana na daktari nayeye akaanza kuhoji maswali kuhusu hali ya mgonjwa.Akamgeukia mgonjwa na kuanza kumuuliza maswali.Hapo ndipo walipojua jina lake anaitwa, Hajrath Mpilla!

*******
Lilikuwa ni gari la gharama lililofanya kila mkazi wa eneo hilo la Ilala Boma,aoshe macho kwa kulitizama tu.Abiria waliokuwa wanapita kwenye madaladala hata wao waligeuza shingo zao,wakalisifia.Lilikuwa gari zuri la kifahari,ambalo kwa kipindi hiko lilikuwa vigumu kwa mtu yoyote kulimiliki.Mbaya zaidi lilikuwa linaunguruma na vioo vilikuwa vyeusi sana yaani ‘tinted’ kumaanisha kwamba mtu aliyekuwa ndani hataki kuonekana.Hilo lilikuwa wazi kabisa sababu George Charles hakutaka kuonekana ni tajiri,hata hivyo gari hilo hulitumia mara chache mno!Tangu aliagize, hiyo ilikuwa mara yake ya tatu kuliendesha.Akiwa ndani ya gari,wakati wote alikuwa anatizama huku na kule,akimsubiri Yusrath ili ampeleke kwa wazazi wake Ilala,dakika kumi na mbili baadaye simu yake ya mkononi ikaita akaipokea haraka sababu ilitoka kwa Yusrath,namna mapigo yake ya moyo yalivyodunda, ilimuogopesha mpaka yeye mwenyewe,sio siri kuna hali alijihisi ndani ya mtima wake, ambayo ilikuwa niya utofauti kabisa.Alihisi kumpenda kwa dhati Yusrath lakini bado hakumwambia,sio kwamba hakuwa na uwezo wa kumuelezea kile kilichokuwa moyoni mwake,la hasha!Alitaka kufuata taratibu zote.
“Range Rover Vogue,nyeupe!Hapa karibu na sheli”
“Gari nyeupe ipo moja”
“Ndio hiyohiyo”
“Mmmh,haya”
Mguno huo wa mshtuko,ulikuwa wazi kabisa ya kwamba Yusrath ameshtuka baada ya kuliona gari hilo,hazikupita hata sekunde mbili.Akawa amefika,George akafungua mlango Yusrath akaingia ndani wakasalimiana.
“Tunaelekea wapi?”
George Charles,akauliza.
“Tunaingia mtaa ule katikati kule,twende nitakuelekeza”
Safari ikaanza hapohapo,ndani ya gari ukimya ukatawala lakini kulikuwa na nyimbo nzuri laini inapigwa taratibu,walivyoingia katikati ya mtaa,Yusrath akawa ana kazi ya kumuelekeza njia za kupita.Walipofika waliteremka wote na kushuka,wakaingia ndani!Wazazi wa Yusrath walimpokea vizuri,wote walionesha tabasamu na jinsi walivyomuona tu,wakawa wenye uhakika kabisa Mwanamme huyo hakuwa mbabaishaji na tapeli,kilichowaaminisha zaidi ni jinsi alivyokuwa anazungumza kwa umakini na sera zake kwa ujumla!Kitu kingine alichobarikiwa George ni namna anavyozungumza na watu,alikuwa akiongea taratibu,hiyo ilifanya kila mtu atamani aongee zaidi.Kila kitu kilivyokuwa sawa,nayeye akawataka wazazi hao wajumuike awapeleke nyumbani kwake.
“Hapana,sio leo baba angu”
Mama,akaweka kidogo mkazo!Mualiko huo ulikuwa wa ghafla.
“Nawaomba,wazazi wangu”
George Charles,akawashawishi!Haikuwa kazi ngumu sababu sifa yake kubwa ilikuwa kutokubali kushindwa kitu anachotaka,alitumia kama nusu saa mpaka wazazi hao wakakubali kufika kwake!Hapohapo,akapiga simu nyumbani kwake waandae chakula cha usiku kwani kuna wageni angeenda nao!Kila mtu alijiandaa na baadaye wakaingia ndani ya gari,safari ya kwenda Masaki ikaanza, hapohapo!Ndani ya gari,kila mtu alikuwa anawaza lake.
“Ulisema una kampuni?”
Mzee Suleiman,akaanza usaili wakiwa ndani ya gari.
“Nina kampuni na viwanda pia”
Wakati mwingine mzee huyo hakutaka kuyaamini maneno hayo,sababu maneno aliyosema George yalikuwa mazito kulingana na umri wake.
“Hongera sana.Elimu yako,ipo vipi?Samahani kwa maswali lakini”
“Nina PHD ya uchumi”
“Hongera kijana,hongera”
Baba hakutaka kuuliza maswali mengine zaidi,kichwani kwake ilimjia taswira fulani hivi wenda George Charles ndiye mkwe wake, japokuwa jambo hilo alitamani liwe kweli.Walivyofika Masaki,wakaingia katikati ya mitaa!Huko walisimama nje ya geti kubwa,ambapo George Charles alibonyeza rimoti iliyokuwa ndani ya gari lake,geti liliokuwa na magurudumu chini taratibu likaanza kusogea.Watu wote wakatupa macho ndani, kushangaa jengo kubwa la gorofa tatu,hawakuishia hapo!Wakaangalia vizuri nje na kuona bustani ya maua,iliyopambwa vizuri kabisa.Kandokando kulikuwa na magari yamepaki,hiyo ilifanya wazidi kuduwaa.Hata kwa Yusrath ilikuwa hivyo,bumbuazi alilopigwa,halikuwa na kipimo chake.Taratibu gari,likaenda kuegeshwa sehemu maalum na wote wakashuka.
“Karibuni kwangu”
Kila mtu alikuwa akishangaa kwa staili yake,wakaingia ndani.Seble ndio usiseme,ilipambwa kwa vitu vya gharama sana na ilikuwa kubwa mno!Kabla hawajakaa vizuri wakaletewa vinywaji ili wasuuze makoo yao!Kilichowashangaza nyumbani hapo,ni kutoona dalili yoyote ya mtoto ama mwanamke ambaye angewakaribisha yaani mke wa George Charles,badala yake George Charles ndiye alikuwa bize kuwahudumia.
“Jisikieni huru kabisa,hapa ndio kwangu!Japokuwa sio mkaaji sana”
“Ahsante sana,jumba lote hili unaishi mwenyewe?”
Mzee akauliza swali la mtego akitaka kujua kama George Charles ameoa ama yupo ‘single’
“Naishi na wafanyakazi,ndio wanaonisaidia saidia”
“Mama yuko wapi yeye?”
“Mama yupi?”
George Charles,akarudisha jibu!Ilielekea swali hilo hakuweza kulichambua vizuri.
“Anamaanisha wifi”
Yusrath,akapigilia msumari ili kumuelewesha George Charles!Hiyo ilimfanya Mwanamme huyo atabasamu kidogo.
“Bado sijabahatika kumpata mwenzangu,nipo mbioni lakini”
Kauli hiyo iliwaacha midomo wazi,hakuna aliyekuwa tayari kuamini kwamba Mwanamme kama huyo mwenye uwezo kipesa,akawa yupo peke yake! Ilivyofika saa mbili wote wakaingia mezani kula chakula,saa nne usiku wakaaga na kushukuru ambapo hapo ilibidi George awarudishe kwao Ilala Boma.
Alivyokuwa njiani katikati ya safari anarudi kwake baada ya kuwafikisha!Akasikia simu inaita nyuma,alivyoangalia akagundua ni simu ya Yusrath,ikaita tena na tena!Ikaita na kukata,ikaita tena.Jina lililoonekana juu ya kioo ni MY LOVE,George Charles aliumia moyo lakini alitaka kupokea na kumpa taarifa kwamba simu imeachwa.
“Halloo”
George akapokea na kusema,upande wa pili ukawa kimya kidogo.
“Naomba niongee na mwenye simu”
“Sipo naye karibu hapa”
“Wewe ni nani?”
“Ndugu yake”
“Naweza kuongea naye sasa hivi?”
“Nipe dakika kama kumi hivi”
Hapo hapo George Charles,akakata simu na kuweka gari kando.Ilikuwa ni lazima ageuze gari kurudi Ilala Boma ili amkabidhi Yusrath simu yake,hicho ndicho kilichotokea!Akafanya hivyo,bahati nzuri alivyogonga geti likafunguliwa na yusrath mwenyewe.
“Simu yako”
“Oh My God,Thanks!Nilitaka nikupigie simu sasa hivi.Ulikuwa umefika mbali?”
“No,nilikuwa jirani hapo.Have a good night”
George Charles akasema na kumuangalia Yusrath machoni,yalikuwa ni macho fulani hivi tofauti kabisa,hiyo ilifanya msichana huyu aangalie chini kwa aibu za kikekike,wakaagana na Yusrath kuingia ndani,chumbani kwake.Cha kwanza kabisa ni kumpigia Ahmed simu,hapohapo ikapokelewa.
“I miss you?”
Yusrath akasema.
“Ahsantee,thank you”
“Kwani baby,hujanimisi?”
“Muda wote ulikuwa wapi,ndio unanitafuta sasa hivi?”
“Nilitoka Darling”
“Wapi?”
“Kuna sehemu nilienda”
“Okay,sawaaaa!Kesho”
“Ahmed,upo sawa?”
“Sijui”
“Mbona sikuelewi?”
“Mimi ndio sikuelewi”
“Nimeafanya nini?”
“Ulikuwa na nani leo?”
“Wapi baby?”
Yusrath akajibu kwa swali.
“Nijibu swali Yusrath,siku hizi sikuelewi unajua.Ulikuwa wapiiiii?”
“Nilitoka”
“Na nani?”
“Na marafiki zangu”
“Usinidanganye,kuna mwanamme alipokea simu yako”
Sentensi ya Ahmed ilifanya mapigo ya moyo ya Yusrath,yahame njia!

*******
Jeshi la polisi la Tanzania,siku zote lilikuwa makini sana!Na kila kitu kilikuwa kimepangwa kuanzia mavazi mpaka mbinu za kumtia mikononi Frolian Fredrick,walivaa nguo za kiraia na walikuwa makini sana kuangalia langoni!Hawakuwa karibukaribu,kila askari alitawanyika na kusimama kwa mahesabu!Saa 12;15 Jioni,ndipo wakaona abiria wengi wanatokeza kwenye lango kubwa.Umakini wao ulikuwa ni mkubwa mno,wakamuona mwanamme mmoja amevaa miwani mikubwa ya rangi nyeusi.Afande mmoja,aliyekuwa karibu na mlango akatoa picha na kuangalia,akamuangalia na mwanaume anayetokeza,akageuka pembeni na kumpa ishara afande mwenzake kwa njia ya kichwa!Kilichowaaminisha zaidi ni kitendo cha Florian Fredrick kuvua miwani,hapo ndipo walipomuungia nyuma nyuma, wakitembea kumfuata,mpaka alivyofika kwenye maegesho ya magari.Kabla ya kuzifikia taxi akasimamishwa.
“Kijana,upo chini ulinzi.Unahitajika!Kituo cha polisi”
Afande mmoja,akasema na kutoa kitambulisho,akamuonesha. Florian,akatizama huku na kule na kutabasamu kana kwamba hajashtuka,kabla ya kufanya chochote askari wengine watano, wakasogea karibu na kumuweka chini ya ulinzi,hakika siku hiyo ilikuwa ndio AROBAINI YAKE!



Bado hakutaka kuamini ya kwamba siku hiyo amekamatwa kirahisi namna hiyo kama kuku aliyekuwa ndani ya banda,akawatizama maaskari waliomzunguka na kuwaangalia mmoja baada ya mwingine kwa zamu.Na kudhani ni utani tu,mbali na hapo alijiuliza maswali mengi sana, ni nani aliyewataarifu polisi juu ya ujio wake siku hiyo!Licha ya kutafakari hayo yote ilikuwa ni wazi kabisa kama angekutwa na hatia ya utekaji basi gereza lingemuhusu.Hata hivyo hakutaka kulipa kipaumbele sana wazo lake,alitaka kwanza ajue ni kwanini askari hao wamemzunguka namna hiyo.
“Kuna shida gani Afande?”
Florian Fredrick,akahoji huku akitabamu kama mtu ambaye hana wasiwasi wowote ule.
“Upo chini ulinzi,tunakuomba kituoni kwa mahojiano zaidi”
“Hapana,mpaka nijue kosa langu”
Florian Fredrick,alikuwa ni msomi na alijua ni haki yake ya msingi kujua ni kosa gani analoitiwa kituo cha polisi, ndiyo maana akahoji kwa kujiamini.
“Hatuna muda wa kupoteza bwana mdogo,utajua kituoni”
“Siwezi kwenda popote,nishasema.Mpaka nijue kosa langu!Kama hamna kitu kingine,naomba mnipishe”
“Unajibu kiburi,sio?”
“Ukweli ndio huo”
Swala la Florian kujibishana na maafande hao, kwa Sirgent Mahugo alilichukulia kama upotevu wa muda,akachomoka na kumfunga pingu hapohapo,akaanza kumburuza kwa nguvu.Urefu wa polisi huyo ambaye mikononi alikuwa na misuli mingi kama mpiganaji ulifanya aweze kummudu Florian kwa kiasi cha kutosha,ndiyo maana alimburuza mpaka kwenye deffenda, iliyokuwa katika maegesho ya magari.
“Hatuna muda wa kuchekeana,hatujaja kuuza sura hapa na kucheza makiri kiri.Embu kaa vizuri, kabla sijakupiga mabuti”
Sirgent Mahugo alizungumza kwa ghadhabu,hakuna askari yoyote kati ya hao aliokuwa nao aliyejuwa ni jinsi gani walisumbuliwa kumtafuta Florian Fredrick,usiku na mchana!Ndiyo maana hakutaka kuremba,polisi wote wakaingia ndani ya diffenda na safari ya kwenda kituoni kuanza mara moja,kituo cha kwanza kumpeleka ni Urafiki, ambapo huko alichukuliwa maelezo yake.
“Umesema unaitwa nani?”
“Manase Kavishe”
“Usituchezee akili,sawa!”
“Kivipi?”
“Jina lako nani?”
Ilielekea askari walilijua jina lake, ndiyo maana walimuhoji mara mbilimbili.
“Manase Kavishe”
“Manase Kavishe?!”
“Ndio”
“Ulikuwa wapi na unaelekea wapi?”
“Niambieni kosa langu kwanza,siwezi kujibu chochote”
Florian Fredrick,alijibu kila kitu kwa kujiamini huku akimuangalia afande huyo aliyekuwa mapokezi bila wasiwasi wa aina yoyote ile.
“Siwezi kuongea chochote zaidi bila mwanasheria wangu”
Alihitimisha Florian Fredrick na kubaki kimya,hata afande huyo alivyojaribu kumuuliza maswali mengi zaidi, hakupata ushirikiano wa aina yoyote ile.

*****
Moyo wa Ahmed,haukutulia hata kidogo!Maelezo ya Yusrath yalimtatiza,akapata wivu ajabu.Haikuwezekana hata kidogo mwanaume, apokee simu usiku kama ule alafu atoe maelezo yasiyoeleweka,taa nyekundu ikawaka kichwani kwake!Jasho jembamba likaanza kumtoka,hakutaka kufikiria kitu kingine zaidi ya kudhani kuna mwanamme anamlia tunda lake.Ndiyo maana usiku huo ulizuka ugomvi mkubwa, ambao haukuweza kufikia muafaka.
“Ongea ukweli Yusrath”
Ahmed,aling’aka!
“Ukweli gani?”
“Mimi sio mtoto mdogo”
“Ahmed,unataka kuujua ukweli gani lakini?”
“Kuhusu huyo mwanaume”
“Nimekwambia ni ndugu yangu”
“Sio kweli,ndiyo apokee simu?”
“Sikuwa nayo karibu!Niliisahau”
“Muongo mkubwa,tabia hiyo ulianza lini?Au sababu nakupenda?Kama hunitaki niambie mapema kabla hatujafika mbali”
“Ahmed nakupenda, tambua hiko kitu,nakupenda kutoka ndani ya moyo wangu!Ndio maana, mpaka leo tupo pamoja”
“MNAFKI,sio kweli.Siku hizi umebadilika,sikuelewi kabisa.Una mwanaume mwingine,hilo nalijua”
Ahmed,alizungumza kwa kufoka,kile alichoambiwa na Yusrath hakusikiliza tena,zilizokuwa zinamuongoza ni hasira,wala hakutaka kusikiliza somo ndiyo maana alimgombeza Yusrath kama mtoto wake wa kumzaa,hiyo ilimfanya Yusrath nayeye aanze kuchemka taratibu kwa hasira.
“Mimi mnafki?!”
Yusrath,akauliza kwa sauti ya ukali kidogo.
“Ahmed,nakuuliza mimi mnafki?”
“Nimekwambia ndio”
“Sawa,ahsante!Nashukuru,usiku mwema”
“Al….tititi”
Ilielekea Ahmed alitaka kuzungumza kitu lakini simu ilikatwa,hiyo ilimfanya achanganyikiwe zaidi.
“Halloo,haloo”
Akawa anahakikisha kama ni kweli amekatiwa simu,akajaribu kupiga lakini haikupokelewa.Akajaribu kwa mara nyingine lakini matokeo yake,simu ya Yusrath ikawa haipatikani tena kumaanisha imezimwa!Sio siri,usiku huo kwa Ahmed, ulikuwa mgumu kuelezeka na ulikuwa ni mrefu kuliko siku zote zile,alivyojitahidi kujizungusha huku na kule ili kuusaka usingizi,ikawa kazi bure!Kichwani kwake, alimuwaza Yusrath na mapenzi yao kwa ujumla,hisia zake zilimtuma ni lazima atakuwa na mwanamme mwingine tu.
“Lakini kwanini sikumuuliza kistaarabu?”
Ahmed,akahisi kujuta kwa kitendo alichokifanya.Kuuliza kwake kwa hasira kulimfanya ajitupie lawama zisizokuwa na idadi kamili,mpaka inagonga saa saba ya usiku simu ya Yusrath haikuwa hewani hata kidogo!

*****
Mbali na msichana huyu Yusrath kuwa mtaratibu lakini upande mwingine wa shilingi alikuwa ni mkorofi na mwenye hasira za karibu vilevile,hususani mtu yoyote akimpigia kelele!Kitendo cha kumkatia simu Ahmed bila kumpa vipande vyake ilimaanisha kumuheshimu sana,vinginevyo siku hiyo Ahmed angejuta kuzaliwa.Hilo alilijua wazi ndiyo maana akachukuwa maamuzi magumu ya kumkatia simu na kuizima kabisa ili aepukane na jambo ambalo alijua ni lazima lingetokea mbeleni,kifupi akafunika kombe ili mwanaharamu apite.Ukweli ni kwamba, alimpenda sana Ahmed na mambo mengi sana alipanga kufanya naye,licha ya hivyo kuna vitu ambavyo alianza kuvichukia kutoka kwa mwanamme huyo.
“Kwanini Ahmed anifanyie hivi?”
Yusrath alijiuliza maswali mengi usiku wa siku hiyo,akakosa jibu la kitu gani amfanye Ahmed!Alivyotaka kuwasha simu na kuandika ujumbe mrefu ya kwamba waachane nafsi nyingine ikamkataza na kumwambia hizo ni hasira zikipoa utamtafuta!
Usiku wa siku siku hiyo, alilala akiwa na mawazo chungu mzima,licha ya kuwaza hayo yote.Alikumbuka kwamba kukipambazuka alitakiwa awahi kazini ambapo huko,bosi wake angekuwa George Charles!Akaapia kwamba atafanya kazi kwa bidii zote na kutafuta pesa kwa wudi uvumba ili baadaye aje kuishi maisha ya raha mustarehee!Huo ndio ulikuwa mpango wake,ndiyo maana usiku huohuo alikuwa akiwaza ni aina gani ya nguo aivae ili asubuhi awasili nayo ofisini!
Kutokana mawazo kuwa mengi sana,muda ulikwenda harakaharaka!Kulivyopambazuka tu,cha kwanza ni kwenda bafuni kujimwagia maji,ambapo huko alifanya kila kitu na kunyoosha mpaka chumbani kwake akiwa na kanga moja, ambayo ilimfunika kifuani,mapaja yake manene yalikuwa wazi!Moja kwa moja mpaka kwenye kioo kikubwa, ambapo hapo hata yeye alijishangaa!
“Mmh,kumbe nimenenepa hivi!”
Alijishangaa!Ni kweli,unene wake uliongezeka kiasi!Pembeni akawa kama anavibunduki,badiliko hilo aliliona siku hiyo akiwa kwenye kioo,hata hivyo aliendelea kuangalia mbele yake akaona nyonga yake ilivyokatika vizuri,kifua chake kimesimama ambacho haikuwa na haja ya yeye kuvaa sidiria.
Hakutaka kupoteza muda mwingi katika kioo,akafungua kabati na kuchagua gauni refu,ambalo aliamini lingekuwa la heshima kwa kazi atakayoenda kuanza!Akalivaa mwilini,hiyo ilimfanya ashtuke sababu lilimbana kiasi, tofauti na mara ya mwisho kulivaa,hapo ndipo alipata jibu la swali lake kwa uhakika zaidi ya kwamba,ameongezeka!Alivyomaliza kila kitu,akabana nywele zake vizuri.Akavaa kitambaa cha kitenge juu ya kichwa chake!Alivyojikagua vizuri na kuhakikisha yupo sawa,akavaa viatu na kutoka nje,ambapo huko huko aliwasalimia wazazi wake,akatafuta daladala lililompeleka mpaka Posta,hapakuwa na umbali sana na anapoishi.Ndiyo maana ndani ya dakika thelathini akawa amefika tayari Posta,akatembea mpaka kwenye jengo kubwa lililokuwa mkabala na sanamu la Mwanajeshi aliyeshika mtutu.Hapo hakuulizwa na maaskari,hiyo ni kutokana na George Charles kuweka maagizo hayo!Alichofanya Yusrath ni kunyoosha mpaka mapokezi,akamsalimia dada aliyemkuta.
“Nimemkuta George?”
Dada wa mapokezi alimtizama Yusrath kwa umakini kidogo,sio kwamba sura hiyo ilikuwa ngeni kwake lakini ni namna alivyolitaja jina hilo, wakati ofisi nzima humuita ‘Boss’Iweje yeye amuite jina lake kamili?Licha ya kuwaza hayo lakini hakutaka kuhoji maswali mengine zaidi.
“Ndiyo yupo”
“Naweza kumuona?”
“Sawa,jina nani?”
“Mwambie Yusrath Suleiman”
Kama itfaki za ofisi zilivyo ni lazima simu ipigwe kwanza, ndipo mgeni aruhusiwe kupita.George akiwa ofisini kwake bize kwenye kompyuta.Simu yake ya mezani ikaita,moja kwa moja akajua imetoka kwa sekretari.Akaangalia ukutani ambapo kulikuwa na televisheni kubwa,nje ilikuwa inaonesha mgeni gani yupo yaani kulikuwa na CCTV camera kuanzia mlangoni,alivyomuona ni Yusrath moyo wake ukapiga kwa nguvu mno!Akachukuwa mkonga na kuuweka sikioni.
“Mwambie apite”
Bila hata ya kumsikiliza Sekretari,akasema maneno hayo.Hakukaa sana,mlango ukafunguliwa akamuona Mrembo Yusrath mbele yake,akahisi kama amepata kigugumizi.Akamkaribisha kiti!
“Ndio umekuja kuanza kazi?”
George Charles,akauliza swali la kitoto kwani ilieleweka wazi kwamba Yusrath hakufika mahali hapo,kucheza ngoma bali kufanya kazi.
“Chai ama Kahawa?
“Hapana”
“Okay,follow me”(Sawa,nifuate)
George akasimama Yusrath akamfuata nyuma yake,wakafungua mlango na kutembea hatua kama sita hivi,ambapo kulikuwa na mlango mwingine!Wakaingia,ofisi ilikua tayari imekamilika.Hiyo ilimfanya Yusrath ashangae kwa kiasi cha kutosha,kila kitu kilikuwa tayari kuanzia kompyuta na meza za kisasa.
“Hii itakuwa ofisi yako,kiti chako kitakuwa kile pale!Nitakutafutia someone ambaye atakuwa anakuelekeza kufanya mambo mawili matatu,is that okay for you?”
“Ndio boss”
Yusrath akaweka utani kidogo wote wakacheka.Hatua ya kwanza kwa George ikawa tayari imekamilika,swala la kumuweka karibu alifaulu kabisa!Licha ya yote hayo,alijaribu kumfanya awe na furaha kwa maana hiyo kila jioni alimrudisha kwao!Taratibu Yusrath akaanza kuzoea mazingira ya ofisi na ndani ya wiki moja,akawa tayari amejua kufanya kazi zote!

******

Lilikuwa ni pigo lingine kubwa,kwake.Mawasiliano yake na Yusrath hayakuwa mazuri kabisa tangu alivyomtibua,Yusrath alikuwa akijibu kifupi simuni na wakati mwingine alipokea simu zake kwa kujisikia.Hiyo ilimaanisha kwamba Yusrath bado ana hasira,ikazidi kumnyima raha ya maisha Ahmed,maisha kwake yakawa machungu,akakosa mtu wa kumshauri ni jambo gani alifanye!Akapiga moyo konde akijaribu kuomba msamaha kila kukicha.
“Siwezi kuwa na mtu ambaye,haniamini period!So p’se just leave me,niache kwa sasa,niko busy”
Siku hiyo Yusrath akajibu meseji ya Ahmed simuni,ilikuwa meseji ya kuchoma moyo.Ahmed aliiangalia mara mbilimbili akiitafakari kila wakati,baada ya sekeseke hilo kufikia siku tano.Akapata wazo lingine la kwenda Kariakoo,dukani ambapo Yusrath hukaa hapo kila siku.Huko aliamini angempata na wangeyajenga lakini matokeo yake,alimkosa!Alisimama eneo hilo mpaka jioni!Mbaya zaidi alivyopiga simu,haikupokelewa.
Hilo ndilo likamvuruga zaidi na zaidi.Siku hiyo ikapita bila ya kuongea naye,kilicho mshangaza zaidi ni tabia iliyoibuka ghafla ya Yusrath kuzima simu usiku, jambo ambalo halikuwa la kawaida kabisa.Siku zikaenda hivyo hivyo,kilichokuwa kinamsaidia kwa wakati huo ni kazi ambazo zilikuwa zinamuweka bize.
“Ahmed,unaitwa na Bosi”
Baada ya kuweka mkonga wa simu sikioni,sauti ya Anneth Kasera ilisikika hiyo ilimshtua kidogo, sababu tangu aanze kazi katika ofisi hiyo,hakuwahi kuitwa na tajiri yake bali huachiwa maagizo mezani kwake juu ya mambo anayotakiwa afanye.Bila kupinga,akasimama na kuweka tai yake vizuri,akafungua mlango na kutembea mpaka mlangoni kwa tajiri yake!Akagonga na kuruhusiwa aingie ndani.
“Ahmed,karibu.Have a seat”
Mr.Tumain Kibangala,mkurugenzi wa kampuni alimkaribisha ingawa aliongea kwa uchangamfu lakini hakuonesha sura ya kutabasamu.
“Ahsante boss”
“Vipi?Kazi zinaendeleaje?”
“Zinaendelea vizuri”
“Nimefurahishwa sana na utendaji wa kazi zako,I’m proud of you!Kukusifia hivyo,haimaanishi kwamba ubweteke.Nimekuita nina sababu kubwa sana,naelewa kwamba una polite language.Nahitaji kupata tenda ya kampuni nyingine,inshort wasiliana na hii kampuni tupate hii tenda,ikikubalika utapata ten pasenti, kwenye mshahara wako”
Ahmed,alikuwa makini akimsikiliza bosi wake!Sifa alizopewa hazikuwa za uwongo,kilichomchanganya ni kivipi bosi wake, amezifahamu.Maelezo hayo yalivyokamilika akapewa namba za simu.
“Ofisi ipo hapo jirani,unaweza ukaenda kwa muda wako”
“Hata sasa hivi?”
“Kama una nafasi”
“Sawa bosi”
Ahmed,akatoka akiwa ana mawazo mengi kichwani kwake!Hakuwahi kupewa kazi ya kwenda kuomba tenda,akafikiria ni gia gani aitumie!Alivyofika ofisini kwake tu,akachukuwa namba na kupiga ambapo ilipokelewa na sauti ya kiume.
“Sawa,unaweza ukafika saa kumi jioni.Ili uonane na Marketing Manager”
“Ahsante”
“Karibu tena”
Ahmed,alikuwa katika wakati mgumu kiasi lakini alipiga moyo konde sababu alijiamini.Ilikuwa ni lazima amfurahishe bosi wake ili pia mshahara wake upande kama alivyohaidiwa.Kitengo alichopewa kilikuwa ni tofauti na jambo analoenda kulifanya,kitu kilichomjia kichwani ni kwamba bosi wake, anampima ili ajue uwezo wake.Ilivyotimu saa kumi jioni,akavaa koti lake jeusi akatoka nje na kuvuka barabara upande wa pili,ambapo huko alikumbana na jengo kubwa upande wake wa kushoto.Alivyofika mlangoni,walinzi wakamsaili,akaandikisha jina lake na kuacha kitambulisho,akazama ndani.
Ndani alikumbana na ofisi kubwa mno,iliyopambwa na vitu vya gharama sana!Akanyoosha moja kwa moja mpaka mapokezi,ambapo hapo alizungumza shida yake kinagaubaga!
“Unataka kwenda kwa Marketing Manager?”
Dada wa mapokezi akauliza.
“Ndioo”
“Binafsi ama kiofisi?”
“Kiofisi”
“Nyoosha pale,mlango wa kwanza wa pili.Juu umeandikwa Marketing Manager”
“Okay,shukrani”
Ahmed akaweka koti lake vizuri,akakohoa kidogo ili kuweka sauti yake sawa.Vitu vingi vikawa vinapita kichwani mwake,hususani vya kuongea na je angezungumza nini?Hata hivyo,aliamini angetumia kila aina ya ushawishi,alivyofika mlangoni,akagonga na kuruhusiwa kuingia!Alivyofunga mlango na kugeuka mbele ili asalimie,akahisi kama mwili wake umepararaizi,msichana aliyemuona mbele yake alifanya ashtuke!Macho yake hayakumdanganya,alikuwa ni YUSRATH.
“YUSRAAATH!”


Butwaa alilopigwa Yusrath halikuwa na kipimo chake,hakuelewa ni kitu gani akifanye.Akabaki ameganda kama barafu,anamtizama Ahmed mbele yake,hakuwa ana uhakika kama alishawahi kumuelekeza ofisi yake ilipo.Na kama hakumuelekeza,je nani kamwambia?Maswali kama hayo ndiyo yalikuwa yanazunguka ndani ya kichwa chake!Haikueleweka kama ni aibu ama uwoga sababu baada ya hapo, akainamisha kichwa chake chini,hiyo haikumfanya Ahmed asite kutembea mpaka karibu kabisa na meza yake.
“Bado siamini,Yusrath!”
Ahmed, akazungumza akiwa makini kabisa hacheki yupo siriazi.Hakuelewa alizungumza akiwa mwenye hasira, ama wivu.
“Ahmed please,naomba tuongee nje ya hapa.Nakuomba tafadhali”
“Tuongee nini sasa?”
“Kitu unachofikiria sio kabisa”
“Sio nini?Sikutegemea”
“Ahmed,nakuomba.Nipo chini ya miguu yako,hii ni ofisi ya watu”
“Bosi wako hajambo?”
Ahmed akauliza makusudi ili kumtingisha Yusrath,fikra zake zilimtuma wazi kabisa ni lazima bosi wa kampuni hiyo ana mahusiano naye ya kimapenzi.
“Yupo ofisini kwake”
“Okay,siku njema”
Ahmed hakutaka tena kubaki eneo hilo,kwa kufanya hivyo, aliamini kabisa angeendelea kuumia moyo,akasahu kabisa kilimchompeleka mahali hapo.Lakini kabla ya kuufikia mlango, akamgeukia Yusrath na kumtizama kwa jicho fulani kali,lililojaa machungu mno!
“Ahsante kwa kila kitu”
Hayo ndiyo maneno aliyozungumza Ahmed kisha kufungua mlango huku nyuma akimuacha Yusrath akiwa njiapanda!Moyo ulimuuma ajabu,kwa wakati huo akili yake ikashindwa kufanya kazi, kabisa.Kuendelea kubaki juu ya kiti bila kuchukua hatua yoyote, kungemfanya azidi kuumia zaidi, ndiyo maana akakurupuka na kuuendea mlango kwa kasi,akauvuta na kutoa kichwa nje!
“Ahmed!”Akaita.
Kwa kuwa hakuwa mbali sana,ilimfanya ageuke.Wakatizamana macho kwa macho,kuna kitu Ahmed alijifunza machoni mwa Yusrath,mapenzi mazito tena ya kweli.Msichana huyu hakuigiza hata kidogo,alikuwa mwenye mapenzi ya dhati, kutoka ndani ya mtima wake.
“Nakuomba mara moja please”
Hapo Ahmed hakuwa na jinsi tena,akaanza kutembea kwa taratibu mpaka karibu kabisa na Yusrath.
“Sema”
“Nahitaji tuzungumze ofisini”
“Sawa”
Kwa upole na heshima kubwa,akawa yupo tayari.Japokuwa moyo wake ulimuuma ndani kwa ndani,kitendo cha kusukuma mlango ili aingie.Mlango wa tatu kutoka upande wake ukafunguliwa,akatokeza mwanamme mrefu kiasi,akamtizama kwa umakini, hakuwa na uhakika kama aliwahi kumuona sehemu japokuwa sura hiyo haikuwa ngeni kwenye macho yake.
“Yusrath,nakuomba mara moja”
Hapo ndipo kumbukumbu za Ahmed,zikawa zimekaa vizuri.Mwanaume aliyesimama mbele yake,alishawahi kumuona dukani kwa Yusrath tena wanachekeana.Kuna kitu kisichokuwa cha kawaida alianza kuhisi na moja kwa moja, jambo hilo alikuwa ana uhakika nalo.Jinsi alivyokuwa anamtizama George Charles ilifanya Yusrath,aanze kuhofia.
“Sawa bosi”
Ilibidi aitikie hivyo ili kumpoteza Ahmed kwani alishaelewa ni vitu gani mwanamme huyo anawaza kwa wakati huo,hakuishia hapo akasogea karibu na bosi wake George Charles kisha kumgeukia Ahmed.
“Ahmed,huyu ni bosi wangu.Anaitwa Mr.George Charles”
Yusrath akatoa utambulisho huo mfupi huku akimtizama Ahmed.
“Bosi,huyu anaitwa Ahmed”
“Mr. Ahmed,nafurahi kukufahamu karibu sana,karibu ofisini kwetu”
George Charles,akatoa mkono ili kusalimiana na Ahmed huku akitabasamu lakini ulibaki hewani, hiyo ni kutokana na Ahmed kuingiwa na wivu,alimtizama George Charles kwa macho fulani ya chuki za waziwazi,akamuangalia kuanzia chini mpaka juu.Kuna neno alitaka kulitoa lakini akaupiga mdomo wake ‘stop’hiyo ilimfanya Yusrath amkanyage mguuni ili atoe mkono wasalimiane na George lakini badala yake,akamkata jicho kali Yusrath. Hapohapo akaondoka zake bila kusema chochote,hiyo ilimshangaza sana George Charles ikapelekea kutaka kujua, mwanamme huyo ni nani na kwanini kafanya vile.
“Yusrath,huyu ni nani?”
George akauliza,alikuwa ana kila sababu ya kuuliza swali hilo.Sababu katika maisha yake,hakuwahi kukutana na tukio kama hilo la kushangaza,isitoshe ndani ya ofisi yake!
“Anaitwa Ahmed”
“Ni nani?”
Yusrath akabaki kimya kidogo,akashindwa kujibu swali hilo, hakuelewa kama angekuwa sahihi kumjibu bosi wake Ahmed ni nani yake,ama isingekuwa sahihi kufanya hivyo.
“Ni mchumba wangu”
Moyo wa George Charles,ukapiga kwa nguvu.Akahisi kama amesikia vibaya,hakutegemea kusikia jibu hilo kutoka kwa Yusrath,wivu ukamuingia ghafla!Akakunja sura na kubadilika hapohapo, hiyo ilimfanya Yusrath aogope na kuanza kujuta kutoa jibu hilo kwa bosi wake,moja kwa moja akajua ameenda tofauti na itfaki za kiofisi,hakuelewa kwamba George Charles, anamuwinda tangu siku nyingi!
“Njoo ofisini kwangu,sasa hivi”
Akasema kwa hasira, iliyochanganyika na wivu.

******
Ghafla penzi likabadilika,badala ya kuwa tamu likawa shubiri.Ahmed alihisi kuchanganyikiwa kuliko kawaida,akaamini tayari amepokonywa tonge mdomoni na George Charles!Hata alivyorudi ofisini hakuonekana kuwa sawa hata kidogo,muda wote alikuwa akimuwaza Yusrath wake.Hakutaka kuamini kama penzi lake baada ya muda mfupi, lingeota mbawa,hakuwa yeye tena bali ni wivu wa mapenzi ndiyo uliompeleka puta.Mawazo ya Yusrath yakafanya hata mfumo wake wa hewa usifanye kazi vizuri,akaanza kuhema kwa kasi!Mapigo yake ya moyo,yakawa yanadunda kwa nguvu sana!Macho yake yakabadilika rangi nakuwa mekundu ghafla,mkono wake mmoja unatetemeka hiyo ilikuwa ni hasira, iliyofika kiwango cha juu kabisa,hapohapo akasimama na kufungua mlango ambapo huko aliomba ruksa ya kuondoka,akisingizia kwamba hayupo sawa kiafya.
Hakutaka kuchelewa,akatafuta bajaji ambayo ilimpeleka nyumbani kwao,huko alivyowasili tu.Akavua nguo zote na kujitupa kitandani,japokuwa alitamani usingizi uje lakini hakupata hata kidogo,kichwa chake kilijaa Yusrath akawaza vitu vingi sana walivyopanga,iweje ghafla amsaliti.
Kilichomuuma zaidi na kumsononesha moyo ni namna alivyotambulishwa kwa George Charles,hiyo ikampa picha tosha kwamba George Charles anakula tunda lake,akiwa katikati ya mawazo mengi.Simu yake ikaanza kuita,alivyoangalia akaona ni Yusrath anapiga,akaiweka pembeni na kuanza kutafakari kama ni sahihi kuipokea ama aipotezee,ikakatika na kuanza kuita tena lakini bado hakupokea.Ilivyoanza kuita kwa mara nyingine,ndipo akaipokea na kuiweka sikioni lakini badala ya kuongea,yeye alikaa kimya.
“Love”
Ni upande wa pili wa simu ndiyo uliosikika,Yusrath akiwa kwenye laini.
“Nakusikiliza”
“Baby please,naomba nijue kwanini umeondoka ofisini ukiwa na jazba vile?”
“Nakusikiliza,sema shida yako”
“Nataka nijue kwanza mpenzi wangu”
Yusrath,alizungumza kwa upole simuni alikuwa ana kila sababu ya kufanya hivyo kwani Ahmed alikuwa katika hasira mbaya,hivyo ilibidi acheze sehemu yake kama msichana mwenye akili hakutakiwa kukurupuka,kwa maana hiyo ilibidi amtulize kwanza na kumuelewesha, hiyo yote ni kutokana na tayari alishamuelewa Ahmed ni mwanamme wa aina gani.
“Ujue nini?Unachotaka kujua ni kitu gani Yusrath?Hivi unataka nini kutoka kwangu?”
“Nakupenda Ahmed,nahitaji kuwa nawewe.Hiyo ndio shida yangu”
“Kuwa na mimi?!”
“Ndio”
“Na Yule baasha ako je?”
Ahmed,akatumia Kiswahili cha kihuni hiyo ilitokana na hasira alizokuwa nazo!
“Sio kama unavyodhani ni..”
“Achana namimi,ndiyo maana hutaki nije kwenu wanijue.Nishaanza kupata picha,una mwanamme mwingine.Ushachumbiwa tayari namimi siwezi,kwanini hukuniambia mapema lakini?”
Ahmed,akamuhukumu moja kwa moja Yusrath,hakutaka kuzunguka mbuyu!Akaeleza kila kitu na kufunguka jambo linalomsibu.
“Mme wangu nisamehee,alafu naomba ujue kitu kimoja.Wewe ndiye mwanamme wangu.You are my one and only,amini hicho nachokwambia.Kama unataka kujitambulisha nyumbani sawa,njoo hata kesho.Nadhani ndio utafurahi.Ahmed,I do love you,nakupenda kutoka ndani ya moyo wangu,hakuna mwanamme nitakayempenda zaidi yako!Nambie upo tayari kuja lini nyumbani kujitambulisha?”
Yusrath alizumgumza kwa hisia kali za mapenzi na ilikuwa ni wazi kabisa,kila alichokuwa anakisema kilikuwa na ukweli ndani yake,hakuwa anatania hata kidogo!Kumpenda Ahmed ili baadaye aje kuwa mmewe ndio zilikuwa ndoto zake siku zote,hakutaka kumpoteza hata kidogo.Sio kwamba hakutaka kuolewa ama kumpeleka nyumbani kwao wamtambue,lakini alitaka kumzoea na kuzijua tabia zake kabla ya kujiingiza ndani ya ndoa, hata hivyo aliamini kwamba bado ni mdogo sana kuishi na Ahmed kama mme na mke.Hilo halikuwa sawa kwa Ahmed,yeye alitaka kupeleka mambo kwa kasi bila kusubiri kwanza na kuzijua changamoto za ndoa,japokuwa alijitahidi sana kumshawishi lakini mwisho wa Siku Ahmed akadhani wenda anamsaliti,hapo ndipo aliamua kukubali kumpeleka nyumbani kwao,wamfahamu.
“Ahmed,nijibu Mme wangu,unataka kuja lini nyumbani ili niwaambie wazazi wangu?”
Yusrath,akauliza tena hiyo ni kutokana na Ahmed kukaa kimya simuni bila kujibu chochote.
“Naomba tukutane face to face”
“Lini?”
“Jumamosi”
“Ahmed,unanipenda?”
“Ndio nakupenda”
“Ahsante kwa kunipenda”
Mawasiliano kati ya Yusrath na Ahmed yalizidi kushika hatamu.
Kuanzia siku hiyo Ahmed akawa ana kazi ya kuomba ushauri juu ya kufunga ndoa,jambo la ndoa hakuwa na utani nalo, akafunga safari mpaka mtoni Kijichi kwa Baba yake mdogo ili kumpasha habari hizo njema za kutaka kujitambulisha kwa wakwe.
“Ni jambo zuri sana,baba yako anajua?”
Baba yake mdogo aliyefahamika kwa jina la Said Kajeme,akaanza kumuhoji maswali mawili matatu.
“Bado hajui”
“Huyo binti kabila gani?”
“Amezaliwa huko Tanga,mtu wa Tanga lakini amekulia sana Dar es salaam”
“Cha kufanya,nitaongea na Mshua wako!Tutajadili vizuri,tutajua namna ya kufanya”
“Hakuna shaka Anco”
Swala hilo akaliacha mikononi mwa Baba yake mdogo Mr.Said Kajeme,akiamini kila kitu kitaenda sawa,atapigiwa simu ili waanze kujipanga wafanye taratibu zote za kufunga ndoa ili baadaye wachukuwe jiko,kihalali.

******
Kila kitu kilipangwa vizuri,simu zilifanya kazi yake kikamilifu.Ahmed na Yusrath walipanga kukutana kwenye moja ya hoteli iliyokuwa Ubungo maziwa,Green Palm hotel.Siku hiyo walipanga kulala wote mpaka asubuhi, kumaanisha kwamba ilikuwa ni lazima wafanye juu chini watumie ujanja wa sungura!Siku zote mapenzi yana nguvu kuliko ‘break down’kazi hiyo haikuonekana kuwa ngumu hata kidogo,swala hilo likafanikiwa kabisa. Yusrath akakubaliwa kulala nje kwani alitoa sababu kubwa,akawasiliana na shangazi yake ambaye alimpanga vizuri.Akapiga simu kwao,kwa Ahmed halikuwa tatizo lolote lile,akasema tu hatorudi siku hiyo kwani anasafiri nje ya mkoa, kutafuta fursa nyingine za kazi.Kumbe haikuwa hivyo,siku hiyo alipanga kukutana na Yusrath hotelini,waongee vitu vingi hususani swala lao la ndoa, ambayo tayari ilikuwa katika mipango!Siku hiyo saa kumi jioni,kulikuwa na hali ya hewa fulani ya uchokozi,baridi sio baridi,giza sio giza.Lakini kivyovyote vile ilikuwa ni lazima mvua inyeshe sababu wingu lilikuwa kubwa angani.Kitendo cha kukabidhiwa chumba tu,Yusrath akanyoosha moja kwa moja, mpaka kitanda kilipo,ambapo alikuwa anapiga hatua huku anavua nguo yake moja baada ya nyingine,mwishowe akabaki na chupi pamoja na sidiria peke yake!Ahmed,akachanganyikiwa akawa kama fisi aliyeona mfupa,akatembea kwa kasi ya umeme na kumvaa,akaiviringisha mikono yake kiunoni na kumsogelea mdomoni,hapo alitoa ulimi wake,wakaanza kulana denda aste aste!Hakuna hata mmoja kati yao, aliyekuwa mwenye haraka na mwenzake,japokuwa wote walikuwa na moto na damu zao zilitembea kwa kasi ya kilomita mia kwa sekunde,shati la Ahmed,likaanza kufunguliwa vifungo taratibu kimoja baada ya kingine.Akatupwa kitandani,Yusrath akapanda juu yake akainama kidogo na kuanza kumnyonya mdomo,hiyo ilifanya Ahmed ajihisi kama yupo juu ya maji, anatembea bila kuzama.Huo haukuwa mwisho,mkanda wa suruali ya Ahmed, ukashikwa na kuvutwa,ukatupwa chini,suruali yake ikateremshwa.Shati likafuata,akabaki na boxa peke yake.Hapo ndipo Yusrath,akaanza kuupapasa mkongojo wa babu ambao tayari ulikuwa umesimama kama mnara,kwa Ahmed kuendelea kuganda kama sanamu ingempunguzia ‘point’ ndiyo maana akashika chupi ya Yusrath na kuanza kuishusha taratibu,ilivyotoka kabisa miguuni.Akaanza kumpapasa,hususani maeno ya mapango,alivyotoka hapo!Akapitisha mkono mmoja nyuma ya sidiria na kutoa vishikizo,hatimaye sidiria ikaachia!Yusrath akabaki kama alivyozaliwa,hiyo haikumaanisha Ahmed,amfakamie!Akazidi kumshika huku na kule,hususani juu ya chuchu.Mara azilambe chuchu za Yusrath mara,amnyonye masikio na shingo.Akashuka chini zaidi,akambinua kidogo,akakamata miguu ya Yusrath huku na kule.Akatoa ulimi wake na kuanza kudeki bahari,hapo ndipo Yusrath akaanza kuhisi kama moyo wake, umeacha kudunda.
“Aaah aaaah yes…s ba..by aishiii aaaah Ahm..ed,Ilo..ve you aaah aaaah”
Ni Yusrath,ndiye alikuwa anatoa miguno hiyo huku mikono yake ikiwa kichwani mwa Ahmed,anamkandamiza kwenye mgodi,ilielekea hakutaka Ahmed aache zoezi hilo, lililoonekana kuwa tamu kwake,zoezi lilidumu kwa takribani sekunde ishirini nzima na kadri sekunde zilivyozidi kwenda mbele, ndio kelele za mahaba kutoka kwa Yusrath zilikuwa zikiongezeka huku akinyonga kiuno chake,kwa Ahmed alikuwa anaelewa nini maana yake!Kitendo cha Yusrath kubana miguu, hapohapo akamdaka juu kwa juu,akaiweka huku na kule,akaingia katikati yake na kuseti mitambo vizuri.Kilichofuata hapo,ni mguu mmoja wa Yusrath kukunjwa na kuwekwa begani,ndani kwa ndani Ahmed akawa ana kazi ya kuzungusha kiuno chake taratibu,hapo ndipo Yusrath akahisi kama yupo angani, vitu vyote anaviona kwa chini!Kifupi usiku wa siku hiyo ilikuwa ni kama wameambiwa ndio mwisho wa kukutana kwani hawakufanya makosa,mpaka saa tano ya usiku ndipo kila mtu alikata kiu yake.
Hapo waliagiza chakula na kuanza kula humohumo chumbani,wakioneshana mahaba kama kulishana na kutaniana,kifupi siku hiyo ikawa kama wapo fungate.Walizungumza mambo mengi sana,hususani juu ya maisha yao ya ndoa yatakavyokuwa.Ahmed,hakutaka kuamini kama anaenda kummiliki Yusrath awe mkewe halali,aishi naye watumie shuka moja kila siku.Kwake,ikawa kama muujiza,ndiyo maana muda wote akawa hatuliii,anambusu Yusrath kila wakati.
“Baby,hayo mabusu leo sikuelewi...Mbona mengi?”
Yusrath,akauliza kiutani.Wakiwa wamesimama dirishani,kwa kuwa hoteli hiyo ilikuwa ya gorofa, wote walikuwa wakiangalia chini jinsi jiji la Dar es salaam lilivyokuwa zuri lenye kuwaka,mji mzima ukawa unawaka taa.Kwa hiyo ikawa kama burudani,ndiyo maana wakawa wamesimama dirishani, wameshikana kimahaba,Ahmed kavaa taulo,Yusrath kikoi ambacho kilionesha nusu nzima ya mwili wake kwa maana nyingine alikuwa amekivaa,kihasara hasara.Hawakukaa sana,mvua kubwa ikaanza kunyesha,wakatizamana na kuanza kutabasamu,hiyo ilikuwa ina maana kwamba wapashe na kutafuta joto,hapohapo wakatupana kitandani na kurudia tendo hilo, kwa mara nyingine,walivyomaliza wakakumbatiana na kulala!

*****
“Griii griiii,griii griiiii”
Mlio wa simu,ndiyo uliokuwa unasikika asubuhi na mapema,baada ya kupambazuka!Wa kwanza,kuisikia alikuwa ni Yusrath,japokuwa haikuwa simu yake inaita.Akatulia kidogo lakini ikaanza kuita tena,hapo ndipo akaanza kumtingisha Ahmed taratibu.
“Baby,simu yako inaita”
“Mmmmh”
Badala ya Ahmed kujibu,akaguna na kujigeuza upande wa pili.
“Baby simu yako”
“Mmmmmh”
Ahmed akaguna tena,ilielekea alikuwa amechoka bado ana usingizi mzito.Hiyo ilimfanya Yusrath atulie kidogo,moyo wake ukamwambia achukuwe simu na kuipokea lakini upande mwingine ukamkataza kufanya hivyo,simu ikaendelea kusumbua.Akaichukua ili kuangalia juu ya kioo mpigaji ni nani,akaona kuna namba ngeni.
“Baby simu yakoo,amka upokee.Au nipokee?”
“Naniii,anapiga…aa?”
Ahmed akauliza huku akipiga mihayo.
“Namba ngeni baby”
“Pokea,mwambie nimelala”
Kufuatia kauli hiyo,Yusrath akaipokea simu na kuiweka sikioni, bila kuongea chochote,akasikia sauti ya mwanamke.
“Baby,mimi Necka Golden.Upo wapi?Tabia mbaya Ahmed,hata kuja kuniona? Nakupenda bado,naomba uje kuniona…Halloo Ahmed Hallooo…..”
Hapohapo Yusrath aliganda,akahisi kama amechomwa sindano ya ganzi mwilini.Maneno aliyokuwa anasikia upande wa pili,yalimvuruga mwili wake ukaishiwa nguvu,simu ikadondoka kitandani,kifua chake kikaanza kupanda juu na kushuka mapafu yake yaka jaa hewa,hakutaka kuamini kama Ahmed alikuwa ana mwanamke mwingine.Mbele yake,akaanza kuona kama vitu viwili viwili,hiyo ni kutokana na machozi ambayo tayari yalianza kumtoka na kutiririka mashavuni,kitendo cha kuvuta kamasi na kutoa sauti, hiyo ndiyo ilimfanya Ahmed ageuke!
“Yusrath,kuna nini?”
Ahmed,akauliza kwa mshangao baada ya kuona hali hiyo.Badala ya Yusrath kujibu,akatoka kitandani na kusimama wima,hapo akaanza kuvaa nguo zake kwa kasi,dalili zilionesha hakukuwa na amani tena.Ahmed nayeye akasimama wima na kumfuata kwa kasi.
“Yusrath,mbona unalia?”
“Ahmed niacheeeee,usini…shike”
Yusrath akaropoka kwa sauti ya ukali huku akimkaripia Ahmed kwa kufoka,kwa wakati huo hakutaka kushikwa!Hasira zilimkaba kohoni,akashindwa kuhema vizuri akawa kama ana kitu,anataka kuzungumza lakini kwikwi ilimbana sana!



Haikuwa kawaida kwa mtu yoyote yule kuingia gerezani na kuchangamka, ingawa kwa mara ya kwanza ilikuwa ni vigumu kwake,hata siku moja hakuwahi kudhani kama angekuja kutupwa nyuma ya nondo.Kitendo cha kumuua Gabriel kwa kumpiga chupa kichwani akiwa disco ndicho kilimfanya atupwe ndani ya gereza hilo la Kisongo!Baada ya kuzoea, akachukulia kila kitu kinatokea kwa sababu maalum,ndio maana akakubaliana na hali.Ndugu zake waliofika kumtembelea walimshangaa sana kwani badala ya kukonda na mwili wake kupauka, yeye alinawiri kabisa tena muda wote alikuwa akitabasamu kama vile kila kitu kipo sawa kabisa maishani mwake.
Kutokana na uchangamfu wake akiwa gerezani ilifanya apendwe na wafungwa wenzake!Kwani akiwa humo hakutaka kumuona mtu yoyote yule anaonewa,kila kitu kikawa shwari kabisa kwa Necka Golden!Hatimaye mwaka,ukawa umeisha kiutani utani,akajipa moyo kwamba ipo siku angetoka gerezani kwani siku hazigandi, licha ya hayo yote hakuacha kumsahau Ahmed Kajeme,mwanamme aliyetokea kumpenda kutoka ndani ya mtima wake,aliamini akitoka gerezani tu na kuwa huru, watafunga ndoa na baadaye wawe mke na mme,aliamini hilo sababu alivyoingia gerezani, alipewa za chini ya kapeti kwamba Ahmed na Hajrath sio wapenzi tena,japokuwa aliumia kwa kitendo cha kumsaliti rafiki yake, Hajrath!Siku zikazidi kujisogeza adoado,mpaka ilipofika tar 17 March.Siku hiyo ilikuwa siku ya kuona wafungwa,ndugu,jamaa na marafiki huenda kuwaona wapendwa wao na kuwafariji huku wengine wakifika na vyakula.Siku hiyo ilikuwa ni tofauti kabisa na siku nyingine zote kwani sura aliyokutana nayo,ilimfanya ashtuke na wakati mwingine aliangalia chini kwa aibu kubwa.
“Amney”
Necka Golden,hakuwa ana uhakika kama ni kweli Amney yupo mbele yake ama yupo kwenye njozi ya mchana.
“Necka,mambo vipi?Pole”
Hakuonesha kuwa na kinyongo chochote kile badala yake alitabasamu kama hakukuwa na kitu kilichotokea kati yao.
“Safi tu,umenisusa”
“Hamna,kwanza I’m so sorry.Sikuja kukuona tangu ulivyohukumiwa,pole sana!Mungu ni mwema,hilo ni jaribu tu la kukuimarisha”
“Ahsante,nishazoea”
Mbali na Amney kuonesha tabasamu kubwa usoni lakini Necka Golden bado alijihisi ni mkosaji mkubwa,kwa upande wake alijua kabisa hayo yalikuwa ni malipo ya duniani hivyo akitoka ni lazima amtafute Hajrath popote pale amuombe msamahaa,lakini alichoapa ni kwamba hakuwa tayari kumuona akiwa na Ahmed,alikuwa yupo radhi kukosa yote lakini sio mwanamme huyo ambaye sasa alimpenda kweli.Siku hiyo walizungumza vitu vingi sana.
“Nishamaliza chuo,nimechaguliwa kufanya kazi hapa Arusha,kwenye kampuni moja ya Tumbaku”
“Hongera sana,nikitoka inabidi unipe japo kibarua”
“Usijali Necka,sisi bado ni marafiki.Mambo ya nyuma tuyaache ulikuwa utoto tu ule,nimekuletea vitu vya kula kula hapa”
“Ahsante”
Siku hiyo Necka Golden,akahisi kama kuna mzigo fulani kautua kutoka moyoni mwake ingawa kuna jambo alitaka kuuliza lakini alishindwa,hata hivyo alipiga moyo konde na kuhoji.
“Ahmed yupo wapi siku hizi?”
Lilikuwa ni swali,lililomshangaza Amney lakini hakutaka kuonesha mshtuko wa waziwazi.
“Yupo,Yupo Dar!Anafanya kazi,kanenepa huyo”
“Mmmh,mbona haji kuniona?”
“Yupo bize labda kazi”
“Anafanya kazi siku hizi,kazi gani?”
“Sina uhakika lakini mara ya mwisho kumuona ilikuwa miezi kama miwili hivi iliyopita,atakuja tu usijali nitamwambia”
Necka Golden,akashusha pumzi na kutafuna kipande cha kuku kisha kumtizama tena Amney!Kuna vitu alitaka kujua zaidi,akamtizama Amney kwa macho fulani ya kutaka kujua jambo zito.
“Bado yupo na Hajrath?Wamerudiana?”
Sio kwamba hakusikia fununu juu ya kupotea kwa Hajrath lakini alitaka kuhakikisha kwanza,taarifa hizo zina ukweli ndani yake ama skendo tu.
“Hivi hujui?”
“Kujua nini?”
“Hajrath,haonekani chuoni.Inasemekana ametekwa”
“Sijakuelewa”
“Hata mimi sielewi,kila mtu anasema lake.Wengine wanasema,alitoroka na bwana ake wengine kajiua.Cha kushangaza pale Makumira kuna kipindi walijaa askari saaaaana,sikuwa na rahaa.Walinisumbua sikupenda kwa kweli.Sijui Hajrath yuko wapi,maskini ya Mungu”
Amney alizungumza kwa simanzi kubwa sana,urafiki wao na Hajrath ulikuwa ni wa karibu kiasi kwamba wakawa kama ndugu wa tumbo moja,alikumbuka vitu vingi sana nyuma, ndiyo maana alikuwa ana kila sababu ya kuzungumza akiwa mwenye simanzi mno!Habari hiyo, ilimfanya Necka Golden atafakari vitu vingi sana,alitamani siku moja akutane na Ahmed uso kwa uso,amueleze namna anavyompenda.Mbaya zaidi aliapia kimoyomoyo, angekuwa yupo tayari kurudi gerezani kwa mara nyingine ili kutetea penzi lake na Ahmed,alimsikitikia sana mwanamke yoyote huko alipo, ambaye kwa wakati huo ana mahusiano ya kimapenzi na Ahmed kwani alipanga kumfanya kitu chochote kile kibaya hapa duniani,stori zilikuwa ni nyingi sana siku hiyo na mwisho wa siku Necka Golden akaomba apewe namba za Ahmed,swala hilo kwa Amney halikuwa tatizo akafanya hivyo bila kinyongo!Kwa kuwa Necka Golden,alizoeana na baadhi ya maaskari magereza, kulivyopambazuka kesho yake akaomba apewe simu!
“Fanya haraka,piga kabla Kamanda hajafika”
Askari magereza,akamwambia Necka Golden!Hapo ndipo akaipiga namba ya Ahmed.
“Baby,mimi Necka Golden.Upo wapi?Tabia mbaya Ahmed,hata kuja kuniona? Nakupenda bado,naomba uje kuniona…Halloo Ahmed Hallooo…..”
Necka Golden hakutambua kwamba simu hiyo haikupokelewa na Ahmed bali ilikuwa sikioni mwa Yusrath.

*****
Japokuwa alijitahidi kumuimbisha Yusrath akijaribu kumshawishi ili amwambie ni kitu gani kinamliza lakini ilikuwa ni kazi bure,badala yake Yusrath alitaka kuondoka zake na aliapia ya kwamba hatomsamehe tena Ahmed na swala la ndoa alifute kichwani mwake kwani hawezi kuolewa na mwanamme malaya,hilo lilikuwa wazi kabisa sababu aliongea kwa hasira.
“Achana na..mimi ma..laya mkubwa”
Yusrath akaropoka akiwa katikati ya mikono ya Ahmed,ameshikiliwa kwa nguvu asiondoke!Ahmed alitaka kujua ni kitu gani kilimfanya Yusrath apandishe mori namna hiyo,hakuwa tayari kumuachia aende zake,ndiyo maana akamshika kwa nguvu zake zote.
“Yusrath,kuna nini?”
“Ahmed,achana namimi..Naomba niache”
“Siwezi kukuachia”
“Huwezi nini sasa?Nimekwambia sitaki,baki na Malaya zako,nenda kamuone!Si anakuita,hujamuona siku nyingi.Mimi sio fala,hivi unanichukuliaje?”
Hapo ndipo Ahmed akapata picha wenda mtu aliyepiga simu ndiye kachafua hali ya hewa,kwa kasi akaruka mpaka kitandani na kuikwapua simu,akaiweka sikioni.
“Halloo,halloo…”
Hakukuwa na mtu yoyote yule hewani,kumaanisha kwamba simu ilikuwa imekatika.
“Yusrath,Yusrath,Yusraaaath”
Msichana huyu mwenye hasira mbaya akawa tayari keshafika mlangoni,kitendo cha kunyonga kitasa ili atoke nje, Ahmed akawa tayari keshamvaa,akamvuta na kumkumbatia kwa nguvu.Hiyo ilimfanya Yusrath alie kwa kwikwi kifuani mwa Ahmed,alihisi uchungu ajabu pamoja na wivu.Akashindwa kuongea kabisa kutokana na kuhisi kama kuna kitu kimejaa kohoni,akabaki na kwikwi.
“Futa machozi mke wangu,uniambie nini tatizo”
Swala la Yusrath kunyamaza likachukuwa dakika kumi nzima,hapo ndipo alianza kumuhoji maswali Ahmed ambayo yote yalijibiwa kwa ufasaha kabisa,mwisho akahitimisha ya kwamba apige namba ya simu iliyompigia kisha aweke loudspika.
“Kwelii?”
Ahmed aliuliza kama mtu asiyejiamini,akaanza kupiga hesabu ni mchepuko gani ambaye anao,akawaza na kuwazua.
“Ndio piga simu Ahmed,usipopiga mimi nawewe ndio mwisho,sitanii”
Yusrath alizungumza kwa kumaanisha.
“Kwahiyo nipige sasa hivi?”
“Ndio”
Ahmed kwa upole,akachukua simu na kuzitizama namba za simu!Bado namba hizo zilikuwa ngeni machoni mwake,licha ya hayo alihisi kama kinyesi kinataka kumtoka!Akawaza atafanya nini kama simu ingepokelewa na mwanamke ambaye alishawahi kuwa naye kimapenzi,kwa kasi akaanza kuwafikiria wanawake aliotembea nao,akashusha pumzi ndefu na kupiga namba kisha kuweka simu sikioni.
“Weka loudspika nimekwambia”
Yusrath,akaamuru Ahmed akafanya hivyo akawa ameshika simu mkononi anasikilizia,mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu.Simu,iliendelea kuita kwa kama sekunde nne nzima,ikapokelewa!
“Halloo wewe nani?”
Hilo ndilo swali la kwanza kuuliza Ahmed simuni baada ya simu kuwa hewani tena,aliuliza kwa ukali.
“Una akili sawasawa?Wewe ndio umepiga simu,unam…”
“Ebwana,usinipotezee muda niambie wewe nani?Umetoka kupiga simu sasa hivi”
“Sijampigia mtu simu”
“Umepiga”
“Unanimalizia chaji, mpuuzi nini”Simu ikakatwa!
Jambo hilo likamfanya Yusrath ashindwe kuelewa,akamwangalia Ahmed na kutizama simu, ambapo namba zilikuwa ni zile zile.
“Baby”
“No Ahmed.Sio yeye,aliyepiga ni mwanamke”
“Au kakosea namba?”
“Hapana,kataja jina lako”
Yusrath hakuwa tayari kuamini kile anachoambiwa,bado moyo wake ulimwambia ni lazima Ahmed ana mwanammke mwingine pembeni,licha ya yote hakuwa na jinsi ya kufanya akaitikia kishingo upande huku ndani ya moyo wake akiapia ni lazima atafanya uchunguzi ili ajue kila kitu ingawa hakuwa ana uhakika kama angeweza kubaki na Ahmed ama mkataba wao ungevunjwa,endapo angetambua kwamba Ahmed ni ndumi la kuwili!

*****
Askari waliendelea kumshikilia Florian katika kituo kikubwa cha polisi Staki shali,hapo walimuweka kwa takribani siku mbili wakimuhoji maswali juu ya uraia wake na biashara anazofanya,jambo lililowatia mashaka jeshi la polisi ni kudanganya jina lake.Moja kwa moja,wakajua ndiye yeye mtuhumiwa namba moja ambaye angeweza kutaja ni wapi Hajrath Mpilla alipo,sio hivyo tu.Florian,alihusishwa kwenye matukio mengi tu kama kutumia madawa haramu ya kulevya aina ya Coccaine na Herroin!Mbaya zaidi kilichowatia maaskari hasira ni kitendo chake cha kukana kwamba hakuwahi kusoma Chuoni Makumira,kitendo hicho kilifanya askari wapige simu chuoni hapo.Wanafunzi watano walifikishwa na kumtizama Florian, wote walikiri kumtambua.
“Namfahamu,anaitwa Florian Fredrick”
“Unamfahamu vipi?”
“Chuoni Makumira,nilikuwa nikimuona”
Huyo alikuwa ni mwanafunzi wa tatu kusema jambo hilo hilo,hivyo walikuwa wana kila sababu ya kumtia hatiani ili ataje ni wapi Hajrath alipo,swala hilo kwake likawa gumu sana,hakuwa tayari kutoboa siri hiyo, kutoka ndani ya kifua chake.Licha ya kukaa kimya na kutokuwa tayari kuzungumza chochote lakini maaskari walimuhakikishia, angesema kila kitu kwani kulikuwa na watu watata kama yeye lakini walivyofikishwa mahali hapo,walitaja mpaka majina yao ya utotoni.

******
Taarifa za Ahmed kutaka kuchukuwa jiko,hazikuwa tena siri kama hapo awali.Baada ya siku mbili. Baba yake akafikishiwa habari,akamuita Ahmed na kumuweka chini kitako!Jambo hilo lilimshtua lakini hakutaka kumvunja moyo,alikuwa mwenye kila sababu ya kumzuia kijana wake asioe sababu ilikuwa ni bado mapema mno, kujitwisha majukumu ya ndoa,ukizingatia hana kiwanja wala nyumba,mbaya zaidi alikuwa bado anaishi kwake.Hiyo ilimfanya Mzee Kajeme amnyeshee mvua ya maswali.
“Ndio,sijakukataza kuoa!Je,una uhakika na uamuzi wako?”
“Ndio Baba,nina uhakika”
“Kuoa,sio jambo rahisi kama unavyodhani.Najua vijana mnadhani kuoa ni fashion!Inabidi ujenge kwanza maisha yako Mwanangu,jenga weka mambo yako sawa”
“Nikiwa naye baba,nitajenga maisha yangu!Ni mwanamke mpenda maendeleo”
“Kumbuka,bora ukosee njia wasamalia watakuelekeza.Usije ukakosea kuoa, Ahmed”
“Ndio baba,nimekuelewa”
“Huyo binti ni wa wapi?”
“Ni mtu wa Tanga”
“Anafanya nini?”
“Anafanya kazi huku anasoma”
“Una muda naye gani?”
Mzee Kajeme,alianza kumfanyia usaili mwanaye!Alikuwa mwenye kila sababu ya kufanya hivyo sababu alitaka mwanaye aoe mwanamke,anayejielewa!Hata hivyo maswali yalijibiwa ipasavyo,halikuwa tatizo lolote lile.Siku iliyofuata,akaitwa mshenga barua ikaandikwa, ndani ikawekwa shilingi laki moja,akatumwa awapelekee wazazi wa Yusrath ili kusubiri majibu ya barua hiyo kama waliridhia ama wamekataa!

******
Kulala pamoja na matibabu ukichanganya na chakula alichokuwa anahudumiwa na madaktari iligharimu zaidi ya milioni tisa za kitanzania,hizo zote ilitakiwa Hajrath alipe!Hakuwa mwenye uwezo wa kupata pesa popote pale,ukizingatia alikuwa ana kesi pia inayomkabili nchini humo Afrika Kusini tena kesi mbaya ya ujambazi.
Zaidi na hayo alikuwa anatibiwa akiwa na pingu mkononi,kumaanisha kwamba yupo chini ya ulinzi.Katika kuhojiwa sana,ikagundulika kwamba ni raia wa Tanzania,hiyo ilikuwa siri yake yeye pamoja na Dokta Sajo Mlendwa ambaye alikuwa yupo tayari kumsaidia, hivyo ilibidi kwanza,aukane uraia wake ili kesi hiyo iwe rahisi.Hata hivyo ilibidi amwambie hivyo kwani alijuwa askari wangeenda ubalozi wa Tanzania ili kesi hiyo iendeshwe na hapo ndipo watu hao wabaya, wangeweza kujua yupo nchini humo.Dokta Sajo Mlendwa,alikuwa yupo tayari kwa lolote lile!Ndiyo maana akamtafutia mawakili wenye nguvu, waliopo nchini humo.
“Nitakutafutia kadi ya uraia,sawa?Usiongee chochote na maaskari,usiwajibu lolote lile.Ikiwezekana,jifanye unaumwa sana”
Hivyo ndivyo Dokta Sajo,alivyomshauri Hajrath!Hakuwa na jinsi ilikuwa ni lazima afatishe kile alichoambiwa kufanya,aliogopa kurejea nchini Tanzania hata kupiga simu pia alihofia, alijuwa kivyovyote vile Florian angejua na kumteka tena na safari hiyo angemuua!
Siku hiyo usiku,askari walivyofika walijaribu kuchukuwa maelezo yake lakini walishindwa sababu alibaki akiwaangalia bila kujibu chochote kile.Dokta Sajo,aliendelea kumkingia kifua,akapata wakili wa kujibu, sambamba na kitambulisho cha taifa hilo,Hajrath akawa tayari amepata karatasi ambayo ilimuonesha ni raia wa nchi hiyo.Kutokana na maelezo aliyotoa kwamba alitekwa na kwenda kutaka kuuliwa, ilifanya askari waamini lakini haikuwa kazi rahisi kwani siku zote mkono mtupu haulambwi.Dokta Sajo, akajiongeza!Akawapooza na kuwafinyia Dolla elfu moja na mia tano za Kimarekani,faili ya Hajrath,likachomwa moto na kuanzia siku hiyo hakuna polisi hata mmoja aliyefika eneo hilo la hospitalini.

***
Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele matibabu ya Hajrath yalizidi kuendelea na hali yake ilionesha matumaini sababu alianza kutembea na wagonjwa wenzake akifanya mazoezi,Dokta Sajo hakuwa mbali,alikuwa naye bega kwa bega!Akajitahidi sana kuwa naye karibu mpaka mwezi mmoja unaisha, hali ya Hajrath,ikaimarika zaidi.
“Naweza kurudi Tanzania sasa”
Siku hiyo Hajrath alisema baada ya kuhisi hali ipo shwari.
“Hapana,tafadhali.Hata kwangu hupajui,kweli?Itakuwa sio vizuri”
“Ahsante kwa kila kitu,una ubinadamu sana Dokta”
“Usijali,watu wengine Mungu alituumba kuwapa furaha watu wengine”
Hapo Hajrath alitabasamu kidogo,alikumbuka vitu vingi akiwa nchini Tanzania na alijisikia kurudi huko!
“Twende,ukapaone kwangu.Ukae japo wiki kisha,utarudi Tanzania.Ingawa sikushauri saaana”
“Nyumbani ni nyumbani”
“Upo sahihi”
Jioni ya siku hiyo Hajrath alipelekwa kwenye mgahawa ili ale chakula,hapo walikula na kisha kuingia ndani ya gari, safari ikaanza hapohapo.Njiani walizungumza vitu vingi sana,Dokta Sajo alikuwa mchangamfu kuliko kawaida,hiyo ilimfanya mda wote Hajrath acheke na kutabasamu.Alijisikia amani na huru.
“Nitakukumbuka sana dokta”
“Hata mimi”
Safari ya kutoka kijiji walichokuwa mpaka mjini Capetown, iliwachukuwa zaidi ya masaa matano kwa gari binafsi,walivyofika mjini minerton, wakachukua barabara ya kuingilia Century city,mji ulikuwa mzuri.Magorofa yalikuwa marefu sana!Magari yalikuwa yanapita juu na chini yaani barabara za ‘fly overs’,treni za umeme pia zilikuwa juu.Sio siri,jiji hilo lilimfanya Hajrath azidi kutupa macho yake!
“Huwa unatoka huku mpaka kule kila siku?”
Hajrath akauliza,baada ya kuona safari imezidi kuwa ndefu.
“Hapana kule nakuja kwa wiki mara tatu.Lakini kazi zangu nyingi nafanyia Capetown,nina hospitali yangu huku”
“Hongera sana.Bado sana kufika?”
“Hapana,ni hapo nyuma.Nataka nipite nichukuwe vitu vya kupika”
“Kupika?”
“Ndio”
Hajrath,alitamani kuuliza jambo lakini akasita kidogo!Wakasogea mbele kidogo na kuingia kupaki nje ya supamaketi kubwa,Dokta Sajo akashuka na alivyorejea baadaye akawa na mifuko mingi!Safari ikaanza upya,ambapo baada ya dakika kumi!Wakawa,wamesimama nje ya geti dogo lakini la kisasa!Mlinzi akafungua,gari likaingia ndani.Haikuwa nyumba kubwa sana,ilikuwa ni ndogo lakini yenye mvuto,rangi ilikuwa imestadiwa vizuri.Pembeni kuna banda kubwa ambapo ndani kulikwa na mbwa wawili wakubwa,hiyo ilimfanya Hajrath aogope.
“Naogopa mbwa”
“Usiogope,lakini wakali.Hapo wakikuona lazima watabweka”
Ilikuwa ni wazi,kitendo cha Hajrath kushuka ilikuwa kidogo mbwa wavunje banda kwani walibweka kwa hasira lakini walitulia, baada ya Dokta Sajo kuzungumza nao.
“Papiiiii, shut up”
Mbwa wakatulia,Dokta Sajo akatembea mpaka mlangoni ambapo hapo alitoa ufunguo na kuingia ndani.
“Jisikie upo nyumbani”
“Ahsante”
Kilichofuata hapo ni Dokta Sajo,kumpitisha Hajrath kila chumba akimuonesha mandhari,kila kitu kilivyokuwa sawa,akamuonesha na chumba chake cha kulala ambacho kilikuwa na bafu pia,siku hiyo walikuwa na kazi ya kujuana vizuri.Hajrath akapata mwanya wa kumuuliza kuhusu familia yake.
“Niliishi Uingereza mimi,nilioa mzungu.Lakini tumetengana!Nikaamua kurudi South”
“Kwanini sasa mlitengana?”
“Ni stori ndefu lakini ni mambo ambayo sitaki kuyakumbuka,mpaka leo imenifanya niwe naishi mwenyewe”
“Pole sana”
“Ahsante,nishapoa”
Maongezi yalizidi kupamba moto,Dokta Sajo akaingia kupika wakala na kulala.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yao,walikuwa kama kaka na dada,lakini kadri siku zilivyozidi kwenda mbele!Hisia zao,zikazidi kubadilika,Hajrath akajisahau, hakutaka kurejea nchini Tanzania,alitaka abaki na Dokta Sajo ambaye alitokea kumpa furaha kila wakati.
Alitamani siku moja,wawe zaidi ya kaka na dada.Alizuia hisia zake lakini hilo likawa gumu,siku hiyo usiku ilikuwa ni lazima ajitoe ufahamu tu na ajichetue.Ndiyo maana walivyoagana kulala, yeye hakufanya hivyo,aliingia chumbani kwake na kuchukua nguo ya kulalia yaani ‘Night dress’akatoka na kwenda mpaka mlangoni kwa Dokta Sajo!Kilikuwa ni kitendo cha ujasili mkubwa sana,akagonga.
“Naniiii?”
Dokta Sajo akauliza akiwa ndani.
“Hajrath”
“Kuna shida gani?”
Hapo Hajrath,akashindwa atoe jibu gani, damu yake ilizidi kumwenda mbio.
“Njoo kwanza,wewe toka nje tu.Kuna kitu nataka kukwambia”
Dokta Sajo,akasimama na kujifunga taulo.Hakuelewa ni shida gani aliyokuwa nayo Hajrath usiku huo,alivyofungua mlango alishtuka sana,moyo wake ulipiga kwa nguvu.Mbele yake alisimama Hajrath akiwa na nguo ya kulalia, mbaya zaidi ndani hakuvaa kitu chochote kile,kila kitu alikiona mubashara, kuanzia kifua hadi mwili mzima.
“Dooookta”
Hajrath akaita kwa sauti ya puani,hapohapo hakutaka kupoteza wakati, akaingia ndani mzimamzima na kumrukia Dokta Sajo midomoni,kabla dokta huyu hajachukuwa uamuzi wowote karoti yake ikawa tayari imeshikwa,akahisi kulegea,akatupwa kitandani puu!Hajrath akapanda kwa juu, akiwa na morari ya kufanya, tendo hilo la kuzini!


Mapigo ya moyo ya Dokta Sajo yalipiga kwa nguvu,yakafanya damu yake iende kwa kasi ya kiwango cha juu kabisa,akawa hajiwezi tena yupo juu ya kitanda anatomaswa tomaswa.Tendo hilo hakulifanya siku nyingi, ndiyo maana akawa kama mtu aliyepalalaizi,kujigusa hawezi tena,isitoshe alishindwa kufanya kitu chochote kile.Hajrath akazidi kumpagawisha sababu alianza kumlamba kila mahali,akamtoa taulo ambalo alikuwa amelivaa,Dokta akabaki kama alivyozaliwa.Mwanamke huyu sijui shetani gani lilimpanda,alichofanya ni kuchukua koni ya dokta iliyokuwa tayari imesimama akaitumbukiza mdomoni na kuanza kuilamba,hiyo ilifanya Dokta huyu apagawe zaidi na zaidi,hajielewi tena!Hajrath hakuishia hapo,akajitoa na kuanza kumlamba tumboni kwa ulimi.Alivyoona dokta kapagawa zaidi,akapanda juu tayari kwa kuendesha farasi,sio siri alikuwa ana kasi mno ndiyo maana kitendo cha kupanda juu tu,akaanza kunyonga kiuno chake.Hiyo ilimfanya dokta azidi kuchanganyikiwa,bila kujua ni kitu gani akifanye akaanza kuguna ndani kwa ndani.Ilikuwa ni aibu kubwa kwa Dokta kumaliza mechi hiyo katikati ya safari tena kabla ya dakika moja kufika,alivyojitahidi kwa kila hali ili swala hilo lisitokee akawa amechelewa tayari kwani alikuwa hoi na alifika mshindo,hakuweza kuendelea tena!Akabaki anahema kwa mbali,akahisi aibu lakini hakuwa na jinsi hiyo ni kutokana na Hajrath hakuwa amefika mlima kitonga.
“Thank you”(Ahsante)
Hajrath akashukuru, hakutaka kuwa wazi na kuonesha ya kwamba hajaridhika,akachukulia ya kwamba wenda ni sababu siku ya kwanza tu kwani kuna baadhi ya wanaume kama hawajafanya tendo hilo kwa muda mrefu,hufika mapema kitonga!Kwa aibu kubwa na haya,akasimama na kuweka nguo yake ya ndani vizuri,hapo akatembea mpaka chumbani kwake,akajifungia mlango kwa ndani!Alichokifanya ni kunyoosha moja kwa moja mpaka bafuni kwake,bado alikuwa anahamu kubwa na maruwani yake yalikuwa yamepanda kwa kiasi cha juu kabisa,ilikuwa ni lazima ayashushe kwa namna yoyote ile.Hapo ndipo alipoanza kuyatomasa maziwa yake huku akivuta picha za wanaume mbalimbali akiwa nao kitandani,hiyo haikutosha akaingiza mkono wake kwenye ikulu!Akazidi kufanya zoezi hilo hisia kali,zikampanda kwa kasi ya ajabu akahisi kama kuna vidudu vinatembea kupitia mgongoni mwake,nguvu za miguu zikaanza kumuishia akajikunja kidogo!Kuna vitu vikatoka,akahisi raahaa ya ajabu.Akashusha pumzi ndefu na kujitupa kitandani,kichwani alikuwa ana mawazo mengi baada ya kukamilisha jambo lililokuwa linampeleka puta,akajiona ni mkosaji!Akajitupia lawama,akahisi aibu kubwa!Hakuelewa angemuangalia vipi usoni Dokta Sajo asubuhi kukikucha,usiku mzima alikuwa mwenye mawazo tele.Hapo ndipo akapata wazo,aondoke zake!Japokuwa usiku wa siku hiyo kwake,ulikuwa ni mrefu mno lakini kulikucha!Akaingia bafuni ili kujimwagia maji,alivyotoka akaanza kupanga nguo zake,ukweli ni kwamba hakutaka kabisa kukaa ndani ya nyumba hiyo, wakati mwingine akatamani ardhi ipasuke aingie ndani akimbie aibu lakini hilo halikuwezekana.
“Ngo!Ngoo!Ngoo!”
Akiwa katikati ya hekaheka za kuweka kila kitu sawa ili aende kuaga kwa Dokta Sajo,mlango wa chumbani kwake,ukagongwa!Mapigo yake ya moyo yakapiga kwa nguvu,akaanza kutetemeka kwa wasiwasi mkubwa!Akajua huyo ni lazima angekuwa ni Dokta Sajo tu na wala si mtu mwingine,sababu ndani ya nyumba hiyo waliishi wawili tu!Akaelewa fika kwamba asubuhi hiyo angeambiwa aondoke kwa kitendo kichafu alichokifanya usiku wa jana yake,akashikwa na hofu kubwa!Hakuelewa ni aina gani ya msamahaa aitumie ili Dokta Sajo ambaye siku zote alimchukulia kama dada yake,amsamehee!Akatembea taratibu kwa unyonge na kuzungusha funguo,akanyonga kitasa!Dokta Sajo,akawa yupo mbele yake,kwa aibu kubwa akaangalia chini na kutoa salamu.
“Umeamka salama?”
Dokta Sajo,akauliza huku akimtizama alishindwa kumuangalia usoni sababu Hajrath aliinamisha kichwa chake chini,akiona aibu!
“Ndio”
“Twende,ukanywe chai.Nimepika leo!”
“Hapana kaendelee tu”
“Hapana,nimezoea kunywa nawewe!Twende tafadhali”
“Dokta Sajo…”
Hajrath akaita,bado kichwa chake kilikuwa chini.
“Naam”
“Nahitaji kwenda nyumbani”
“Nyumbani?!”
“Ndio”
“Wapi?”
“Tanzania”
“Hapana,njoo tuongee tafadhali.Nakuomba”
Dokta Sajo kwa taaluma yake na kusomea mambo ya saikolojia alishajua tatizo la Hajrath,hivyo ilikuwa ni lazima autibu ugonjwa unaomsumbua kwa wakati huo!Akamshika mkono na kuanza kutembea naye,ambapo walifika mpaka seblen kwenye meza ya kula chakula.Hapo Dokta Sajo,akamimina chai na kufungua sahani, iliyokuwa na kuku wa kukaanga,pembeni kulikua na soseji pamoja na mayai,akamtengea Hajrath kwenye sahani yake.
“Karibu”
“Ahsante”
Bado hakuonesha kuwa mwenye amani kama siku zote,wasiwasi wake ulikuwa ni mkubwa kwa kiasi cha kutosha!Jambo lililomjia ni jinsi Dokta Sajo alivyomchukulia,kivyovyote vile ni lazima angemhisi ni mwanamke Malaya,hilo ndilo likamuumiza zaidi na zaidi sambamba na kumnyima raha ya maisha,akashindwa kumaliza kabisa chai.
“Alafu,nina zawadi yako”
Dokta Sajo akasema.
“Yangu?”
“Ndio,yako Hajrath”
Hapo hapo Dokta Sajo,hakutaka kukaa zaidi akasimama na kutembea mpaka chumbani kwake,ambapo baada ya kurejea alikuwa ana mfuko mkubwa!Moyo wa Hajrath ukaanza kudunda kwa nguvu,hakuelewa hali hiyo ilitokana na hofu aliyokuwa nayo ama shahuku ya kutaka kujua ni kitu gani kilichokuwa ndani ya mfuko huo!Hapohapo,akaufungua. Alichokiona kilizidi kumfanya azidi kufungua na kuchungulia,lilikuwa ni gauni refu kiasi lenye maua maua ya kuwaka, akachungulia ndani akakumbana na viatu vizuri,haikuishia hapo kulikuwa na kikopo kingine kidogo, alivyokifunua akaona mikufu na bangili zinazong’aa!Hakuwa ana uhakika kama ni dhahabu ama shaba!
“Zawadi zako hizo,nahitaji tutoke jioni ya leo”
“Wapii?”
Hajrath akauliza huku akimtizama Dokta Sajo!
“Sun city,nataka nikutembeze pia jiji zima!Kajaribu nguo kwanza,tuone kama zimekutosha!Kama zinakubana,nikabadilishe”
“Ahsante”
“Usijali”
Hajrath,akasimama wima akanyoosha mpaka chumbani kwake ambapo huko alivua nguo zake zote na kuanza kulivaa gauni hilo zuri,alivyomaliza hatua hiyo akavaa mikufu na kutembea mpaka mbele ya kioo!Kitendo cha kujiona alishtuka,kiasi kwamba alikiri moyoni mwake tangu azaliwe hakuwahi kupendeza kwa kiasi kikubwa namna hiyo,akajigeuza geuza!Akaona namna ambavyo Mungu alivyokuwa fundi na alimpendelea wakati wa kumuumba,ambapo alimuwekea udongo mwingi kwa nyuma,ikafanya apate kimlima!
“Nimependeza!”
Alijisifia kabla ya kusifiwa na hilo halikuwa utani hata kidogo,mwanamke huyu alitoka chicha sio masihara,hapohapo akafungua mlango na kutembea mpaka Seblen!Butwaa alilopigwa Dokta Sajo, halikuwa na kipimo chake,hiyo ilimpelekea mpaka asimame na kuweka mkono wake kinywani!Kama uzuri alikiri kwamba Hajrath ni mrembo,sio hivyo tu bali hata shepu alikuwa nayo,gauni alilovaa lilimchonga na kumchora umbile lake la nambari nane!Dokta Sajo akameza fundo la mate huku akizidi kumshangaa mwanamke huyo mrembo, aliyekuwa mbele yake.
“You are beautiful”(Wewe ni mrembo)
“Thank you”(Ahsante)
Jinsi ambavyo Hajrath alivyoitikia kwa mapozi na kurembua macho yake ikafanya moyo wa Dokta Sajo,utikisike kwa nguvu akahisi kama kapigwa sindano ya ganzi, akabaki ameganda kama sanamu la michelini.
“Umejuaje size yangu?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Hajrath.
“Nimekaa nawewe kwa muda mfupi lakini nimejua vitu vingi sana kuhusu wewe”
“Kweli umenipatia,hizi ni Gold?”
“Ndio,pure Gold”
“Ahsante”
“Jioni,ujiandae.Tutatoka”
Dokta Sajo hakuwa mwanaume mwenye longolongo ama mbabaishaji,jioni ya siku hiyo aliporejea kutoka katika mihangaiko yake,akamtaka Hajrath ajiandae ili wakatembee na kushangaaa mambo mengi ya jiji hilo la Afrika Kusini, hususani sehemu inayoitwa Sun City,mji wa jua!Hapo watalii wengi hupenda kwenda kupumzika.Wote walivaa na kupendeza,kwa heshima kubwa Dokta akazunguka kushoto na kumfungulia Hajrath mlango wa gari,siku hiyo Hajrath akajihisi kama ni malkia vile.Baada ya kuingia ndani ya gari, safari ikaanza hapohapo!

***
Kila kitu kwake kiligeuka ghafla na kuwa furaha iliyozidi kifani,akasahau mateso yote yaliyopita nyuma!Mbaya zaidi alishawahi kukutana na mwanamme anayeitwa Florian Fredrick,akamlaghai kwa kumpa raha kama anazopewa wakati huo lakini hilo hakujali,akajikuta ameingia kwa Dokta Sajo mzima mzima bila kupima akahisi kumpenda kweli,wakati mwingine aliulaumu sana moyo wake kwa kupenda ghafla namna hiyo ingawa alikuwa bado anaona aibu,Dokta Sajo siku hiyo alikuwa ana kazi ya ziada!Kumzungusha Hajrath jiji hilo na kutembelea sehemu nyingi za kifahari,kwa Dokta Sajo pesa hazikuwa chochote mbele ya Hajrath, ilimradi tu atampa furaha,zaidi na hayo alihisi kuna kitu kisichokuwa cha kawaida ndani ya mtima wake,alihisi kumpenda Hajrath kutoka ndani ya moyo wake,ndiyo maana kwanza alijaribu kumzoea na kumuweka karibu ili wawe kama marafiki kisha baadaye wawe wapenzi!Hiyo ndiyo ilikuwa mipango kabambe ya Dokta Sajo na aliamini kwa asilimia kubwa lingefanyika,usiku wa saa mbili uliwakutia wakiwa katikati ya jiji la Johannesburg,hawakutaka kuondoka bali ni kula chakula cha usiku!Kila kitu kwa Hajrath kilikuwa ni furaha tupu,akajihisi kama yupo paradiso!Saa nne ya usiku, ndipo walipoingia ndani ya gari na safari ya kurudi jijini Cape town kuanza,umbali ulikuwa ni mkubwa lakini ilikuwa ni lazima warudi nyumbani!Dokta Sajo aliendesha gari kwa masaa mengi sana barabarani,walipofika waliingia ndani na kilichofuatia hapo ni Hajrath kushukuru mno kwa mambo aliyofanyiwa,akaaga ili akalale!Kitendo cha kugeuka ili aondoke mkono wake ukadakwa kwa kasi akavutwa karibu na Dokta Sajo,akajikuta yupo katikati ya mikono yake, midomo yao ipo karibu sana,hakuna kilichofuata hapo zaidi ya kupigana madenda kwa fujo!
“Mmmmh mmmh”
Miguno ndiyo ilisikika baada ya Hajrath kunyonya shingo yake,mkono wa Dokta Sajo ukapita nyuma ya gauni akashusha zipu gauni lote likashuka,kwa kasi akaanza kuvua shati lake!Akamvua Hajrath nguo na kumtupa juu ya kochi,yeye akapanda juu yake!Kwa hatua aliyofikia kilichofuata, kilijulikana kwa maana hiyo hakutaka kufanya makosa ya kizembe kama ya mara ya kwanza ndiyo maana alitaka kwanza aanze kumuandaa Hajrath kwa staili ya kumtomasa na kumshika kila mahali,ndani ya sekunde tano wakabaki kama walivyozaliwa,damu zao zilikwenda mbio kwa kiasi cha kutosha!Siku hiyo Hajrath,aliandaliwa kwa takribani dakika mbili nzima!
“Aaaah aaaah,ashii aaaah aaah aaaah”
Hajrath,alitoa sauti za puani huku akiwa amefumba macho yake akiwa katika sayari nyingine ya Huba!

******
Swala na mpango mzima likiwemo jukumu la ndoa ya Ahmed Kajeme,lilisimamiwa na Mjomba wake Mr.Zilyatan Humudi,katika wajomba zake wakubwa ambao waliheshimika huyo ndiye alikuwa mmoja wao na hata kwenye ukoo wao yeye ndiye alikuwa msemaji mkubwa!Taarifa za ndoa ya Ahmed akalivaa kama lilivyo,alichokifanya ni kumtafuta shemeji yake Mohamed ili watete jambo hilo kwa ukubwa zaidi.Hapakuwa na mahali pengine zaidi ya nyumbani kwa Mohamed,baba mzazi wa Ahmed.
“Shemeji,karibu sana”
Mzee Mohamed alimkaribisha shemeji yake kwa tabasamu pana na heshima nyingi.
“Ahsante sana”
“Umehadimika mno”
“Majukumu yamekuwa mengi,waswahili wanasema maji yamezidi unga”
Wote wakacheka,hapo Mke wa Mohamed ambaye ni mdogo wake na Mr. Zilytan Humud akatokeza,akamsalimia kaka yake kwa heshima kubwa na baadaye akamkaribisha kinywaji.
“Nimekutengenezea Juisi unayopenda Kaka angu”
“Ahsante,alafu ulijuaje?”
“Khaa!Nakumbuka sana,tulivyokuwa watoto, ulikuwa huambiwi kitu kwenye juisi ya Miwa”
“Usinikumbushe mbali”
Baada ya utani wa hapa na pale,ilibidi waanze mada iliyowaleta hususani kuhusu Ahmed na ndoa yake kwa ujumla,barua ilikuwa tayari imetumwa kilichokuwa kinasubiriwa ni majibu kutoka upande wa wazazi wa Yusrath kisha baadaye, wajomba waende kusikiliza swala zima la mahali itakavyokuwa.Wakati mikakati ya ndoa na kusubiri majibu ya barua iliyotumwa yeye Yusrath alikuwa bize na George Charles,Yusrath alizoeshwa vibaya kwani kwa siku alikuwa anapewa shilingi laki tano kila walipoachana na George Charles!Tabia za Yusrath zikaanza kubadilika, ghafla pesa ikafanya kazi yake,mawasiliano na Ahmed yakaanza kupungua taratibu na kila alipoulizwa kulikoni alijibu mkato kwamba yupo bize na kazi, hivyo anachoka sana!Pesa zikamlewesha zaidi, George Charles hakuwa mwanaume bahili,alimpeleka kila kumbi ya starehe ili kumuweka sawa!Hiyo ikamfanya Yusrath atakate ndani ya wiki moja tu,hakuna ‘fashion’ iliyompita kila nguo alijua kuivaa!Sio kwamba hakuelewa kwamba aliletewa barua ya uchumba,alitambua kila kitu lakini alipuuzia.
“Yusrath unajuwa nakupenda sana”
Siku hiyo Ahmed alisema kwa hisia simuni,tabia za Yusrath zilimfanya ahisi hali ya hatari mbeleni!
“Hata mimi”
“Umebadilika sana lakini”
“Nimekuwaje?”
Akajibu kwa mkato,hiyo ilimaanisha kwamba hajisikii kuzungumza na Ahmed.
“Sikuelewi siku hizi”
“Ahmed,nilishakwambia nipo bize!Nachoka sana,narudi usiku.Hapo bado sijaosha vyombo,sijapika,sijadeki.Nionee huruma basi,alafu isitoshe kama unaona nakunyanyasa,mlango upo wazi”
Moyo wa Ahmed ulichoma kama pasi,Yusrath alizungumza kwa sauti kali ya hasira tena iliyojaa ghadhabu kubwa.
“Nimekosea wapi?”
“Hujakosea kitu”
“Tatizo nini mke wangu?”
“Sina tatizo”
“Si unajua nimetuma barua kwenu?”
“Najua,naelewa!Usinikumbushe kumbushe kama mtoto mdogo”
“Itajibiwa lini?”
“Kesho kutwa”
“Majibu yatakuwa mazuri?”
“Wazazi wangu,ndio wanajua”
“Yusrath,unanipenda?”
“Ahmed,una nini lakini?Mbona kila siku unaniuliza kitu hikohiko?”
“Nahitaji kujua”
“Nakupenda”
Mazungumzo yao hayakuwa ya kawaida hata kidogo,kuna mambo yalibadilika sana!Hakuwa Yusrath yule wa kipindi kile ambaye kila sentensi anaweka neno ‘baby,Darling ama Honey,hiyo ilimfanya Ahmed ashindwe kuelewa ni kwanini mwanamke huyo, kabadilika namna hiyo,akawaza wenda sababu ameanza kushika pesa ndiyo maana ana kiburi,akalitupilia mbali wazo lake na kudhani labda kuna mwanamme yupo nyuma yake,anataka kuharibu kila kitu!Siku hiyo, hakuwa ana furaha hata kidogo,alisononeka kwa kiasi cha kutosha akaamini kwamba ‘Sikitiko la mahaba linashinda msiba’

******
Ilikuwa ni siku ya Jumatano tarehe 11 June,kila mtu alikuwa akiisubiri kwa hamu siku hiyo,hususani Mr.Zelytan Humudi.Barua waliyotuma wiki moja nyuma walikuwa wakiisubiri kwa hali na mali,kila mtu alitaka kujua ingejibiwa vipi.Ni kweli,kama walivyohaidiwa baada ya wiki moja ingejibiwa!Jioni ya siku hiyo,geti likagongwa na kijana mmoja aliyevalia kanzu na kibalaghashee kichwani.Akajitambulisha kwamba ameagizwa na Wazazi wa Yusrath kuleta barua ya majibu.Wakaipokea na kumkaribisha ndani!
“Hapana,nawahi msikitini sasa hivi!Siku nyingine,acha niwatakie usiku mwema!Insha Allah”
“Nawewe pia usiku mwema, Insha Allah”
Wote wakaingia ndani wakiwa na barua hiyo mkononi,wakitaka kujua kama wamekubaliwa kuchukua jiko ama wamechomolewa!Haraka,wakaichana bahasha kwa kihoro,macho yao yote wakatupa juu ya barua hiyo!


Mioyo yao ilipiga kwa kasi kiasi kwamba wote wakajikuta wanaisoma barua hiyo kwa pamoja wakiwa watatu wamesimama wima seblen,hawakuamini kile walichokiona, baada ya kuimaliza wakatizamana na kutabasamu hiyo ilimaanisha kwamba kuna habari njema na wamekubaliwa kuchukuwa jiko,utaratibu uliofuata hapo ulieleweka ya kwamba wajipange kwenda katika familia hiyo ya akina Yusrath Suleiman ili wawasikilize ni vitu gani wanahitaji na wakamilishe mahali,hilo halikuwa tatizo kwa kuwa kila kitu kilipangwa na watu makini,utaratibu ukaanza mara moja.Siku hiyo hiyo ilibidi wakae chini ili kulizungumzia swala hilo zito!

******
Hayakuwa kwa mapenzi yake bali ni shinikizo kubwa kutoka kwa Ahmed ambaye ni kweli, alimpenda kuliko binadamu yoyote yule chini ya jua la Mungu,swala la kufunga ndoa akiwa katika umri huo aliamini ni mapema sana,ndoto zake zilikuwa atengeneze maisha awe ana uwezo kidogo ili asinyanyaswe kwani alielewa kabisa usipokuwa na kitu ni lazima mwanamme atakudharau, hilo ndilo lilifanya kila siku amkatalie Ahmed kuhusu mpango mzima wa ndoa,kwa nguvu ya penzi akakubali kishingo upande!Barua ikaletwa kwao, akaitwa na kuulizwa kama anamtambua Ahmed,hiyo ikampa wakati mgumu kidogo kwani alielewa nini maana ya kusema ‘ndio’akatafakari kwa muda kidogo na ilikuwa kidogo amkane lakini hiyo isingekuwa dawa,alichokifanya ni kukubali,hakutaka kumpoteza Ahmed na wakati huohuo hakutaka ndoto zake ziyeyuke, akabaki njiapanda!
Kilichofanyika ni wazazi wake kumuhoji maswali kadhawa kadha,akajibu bila tatizo. Hapo ndipo wazee wa ukoo wakaitwa ili kujadili jambo hilo la binti yao Yusrath kutaka kuchumbiwa,hawakuwa na tatizo lolote wakajibu barua na kumtuma mtu arudishe majibu hayo!Tangu siku hiyo Yusrath alikuwa katika mawazo mengi sana,kazi hakuweza kufanya kiufanisi.Mambo chungumzima yalimiminika ndani ya ubongo wake,alifikiria vitu vingi hususani ndoa yake ambayo aliamini alikuwa bado mdogo sana kujiingiza,alielewa fika anaenda kuishi kwa mipaka na masharti mazito,hilo lilikuwa wazi zaidi na hayo aliamini kwamba ni lazima ndoto zake za kutaka kuja kuwa mfanyabiashara mkubwa zizimike kama mshumaa uliopulizwa na upepo!Sababu alimfahamu vizuri Ahmed ni mwanamme mwenye wivu,asingekubali afanye kazi kirahisi rahisi namna hiyo.Wakati akiwa katika mawazo hayo kazi za ofisi hazikwenda vizuri kama kuandaa ‘bid documents’ na kutoa tenda mbalimbali.Swala hilo lilimfanya George Charles,amuibukie ofisini kwake moja kwa moja.
“Naruhusiwa kuingia?”
George,aliuliza akiwa ameingiza kichwa chake ndani ya ofisi kiwili wili kipo nje,sio kwamba hakuwa ana uwezo wa kuingia anavyotaka yeye bali alitaka kumuonesha Yusrtah kwamba anaheshimu ofisi yake.
“Ndio,karibu bosi”
“Ahsante”
George Charles,akatembea taratibu mpaka kwenye kiti kimoja wapo cha wageni,akakaa na kumtizama Yusrath,kwa kumuangalia tu aligundua kwamba binti huyo hayupo sawa hata kidogo,jambo hilo likafanya atake kumdadisi zaidi!
“Are you okay?”(Upo sawa?)
“Ndio”
“Hapana,sijakuzoea ukiwa hivi!Nambie ukweli”
“Nipo sawa George,nipo sawa!”
“Una uhakika?”
“Yeah”
“Kuna mambo fulani nataka kuzungumza nawewe sasa hivi,upo tayari kunisikiliza?”
“Nipo tayari ndio”
Hapo George alimtizama Yusrath kwa macho fulani ya kutaka kumuuliza maswali lakini akashusha pumzi kidogo,vitu alivyotaka kumuhoji vilipotea kichwani, uzuri wa Mwanamke huyo ulimchanganya akili kuliko kawaida!
“Saa kumi,nitakuchukuwa tutaenda sehemu”
Ukaribu wa George Charles na bosi wa kampuni hiyo ulizua maneno ya chini kwa chini kwa wafanyakazi,kila mtu alianza kuhisi ni lazima watu hao wanatoka kimapenzi ikawa skendo kubwa kuna baadhi ya wanawake waliokuwa ndani ya ofisi hiyo wakaanza kumchukia Yusrath,wakidai kwamba ameleta kauzibe.
“Wewe subiri,nitamkomesha!Malaya yule,sijui katokea wapi”
Ilisikika sauti ya mwanamke huyo,akimpasha habari shoga ake!
“Wewe una uhakika gani?”
“Nina uhakika saana tu,hili jambo limenifika hapaaa!Unajua kwa muda gani,nilikuwa nampenda Boss,from no where atokee huyo kigagulo,amchukuwe inahusu!Ukisikia vita vya tatu vya dunia kuanza usishangae yaaa…Naomba hii Document niipin kwenye mafaili”
Mada ilibadilika ghafla,George Charles mkurugenzi wao alikuwa ametokeza.Hiyo ilifanya atetemeke kuliko kawaida, ndiyo maana akaangalia chini bila kujua kwamba amesikiwa ama la!

****
George Charles,alikuwa ni mwanamme makini, wenda kusoma sana kwake ama kukaa nje ya nje kulimfanya awe mjanja na ajuwe kucheza na viumbe hawa wanawake,hakutaka kwenda kwa pupa kwani alishaelewa ya kwamba Yusrath ana tatizo lina msumbua na ilikuwa ni lazima akae naye faragha, aanze kumchimba kwa kumuimbisha nyimbo nzuri za kila aina ili ajae ndani ya kumi na nane zake!Ndiyo maana, ilivyogonga saa kumi ya jioni, akamchukua na kumpeleka moja kwa moja kwenye mgahawa mkubwa wa kifahari, yaani watoto wa mjini wanasema mgahawa wa kitasha!Hapo ni ngozi nyeupe tu ndio zilisheheni ndani ya mgahawa huo kwa maana hiyo,Yusrath na George walitia fora sababu ya ngozi zao nyeusi!Kitu cha kwanza walisikilizwa na kuletewa chakula pamoja na vinywaji.
“Nimepapenda hapa,sio siri”
Yusrath akasifia,hakutania.Sehemu hiyo ilistahili sifa kedekede sababu ilitulia na kulikuwa na mandhari mazuri ya kuvutia sana,kulikuwa na upepo mwanana.Hiyo ilimfanya Yusrath ajisikie huru kuliko siku zote,akala akamaliza na kuanza kunyonya juisi akitumia mrija.
“Ahsante,George”
“Usijali”
Huo ndio ulikuwa muda muafaka wa George kuanza usaili wake,alitaka kujua kitu kinachomsumbua Yusrath ndani ya mtima wake,ndiyo maana akamtoa nje kabisa ya ofisi ili ajuwe kila kitu kinagaubaga!
“Najua haupo sawa haupo sawa Yusrath usinifiche,ukiwa hivyo mimi nakosa raha kabisa.Niambie nini tatizo?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa George,kwa mara ya kwanza ilikuwa ni vigumu kwa mwanamke huyo kusema kinachomsibu akamtizama George kwa kitambo kidogo hakuwa ana uhakika kama mwanamme aliyekuwa mbele yake, alikuwa sahihi kuelezwa changamoto alizokuwa nazo,jambo lililokuwa linafanyika ndani ya ubongo wake ni kuchuja vitu mbalimbali.
“Yes,ni kweli George.Nina shida inanisumbua”
Hatimaye,akakubali kilichobakia hapo ni kusema ni aina gani ya tatizo linalomsibu na hilo ndilo George Charles, alikuwa anasubiria,kwa maana kwamba alikuwa yupo tayari kumsaidia kwa gharama yoyote ile.
“Nina ndoto kubwa sana katika maisha yangu,kwanza napenda kukushukuru sana!Nina amini kwa njia moja ama nyingine,utafanya ndoto zangu zitimie”
Yusrath akaanzia mbali kidogo,hakutaka kuanzia nyuma kwenda mbele, alitaka kila kitu akipangilie kuanzia mwanzo mpaka mwisho!
“Kivipi?Fafanua”
“Ndoto zangu,siku zote nahitaji kuwa mwanamke independent,mwanamke anayejitegemea.Nina kwangu,nina pesa za kutosha!Magari ninayo nina biashara zangu.Nahitaji kuja kuwa kama wewe George,nina kampuni kubwa kama yako!Mwenye mamlaka,nisafiri popote pale napotaka kwenda”
“Jambo hilo linawezekana sana tu,maisha ni kuchagua siku zote!Everything is possible under the sun,hususani ukishaelewa ni kitu gani unahitaji!You should focus,ujuwe unataka nini”
“Ni kweli upo sahihi,sijamaliza lakini….”
“I’m listening”(Nakusikiliza)
Hakuwa na jinsi,ilikuwa ni lazima aweke kila kitu wazi!Akazunguka kote lakini mwisho wa siku,akasema kwamba ana mchumba na keshapeleka barua nyumbani kwao,zaidi na hapo tayari imejibiwa hivyo kilichobaki ni kufunga ndoa tu,akahitimisha kwamba hilo ndilo jambo linalo mtatiza na kumpa mawazo kila kukicha.
“Jambo hilo kwangu ni kikwazo George,nishauri nifanye nini?”
Yusrath akahitimisha na kuomba ushauri,hakuelewa ni kwa jinsi gani George Charles ameumia moyo,sio siri rohoo ilimuuma ajabu!Akashindwa kutoa jibu la harakaharaka.Ilibidi atumie kwanza akili ya kuzaliwa na sio kukurupuka kama wanaume wengine wanavyopaniki,ni kweli na ilikuwa wazi aliumia na wivu ulimkaba kohoni lakini jambo hilo hakutaka kulionesha waziwazi.
“Kwani huyo mwanaume unampenda?”
George akauliza kwa sauti ya chini,tena kwa upole zaidi.
“Ndio nampenda sana”
Yusrath,akafunguka bila kigugumizi wala kusita.
“Well,nayeye anakupenda?”
“Ananipenda ndio”
“Ulishamwambia kuhusu swala lako,i mean kuhusu ndoto zako?”
“Nilishawahi kumwambia zaidi ya mara moja”
“Akasemaje?”
“Yeye,anataka kunioa!Anasema,nisijali.Atashughulikia hilo”
“Una amini atafanya hivyo?”
“Sina uhakika,ndio atafanya hivyo”
“Okay,kwa mfano ukiambiwa uchague kitu kimoja sasa hivi.Kutimiza ndoto zako,ama kuolewa.Utachagua nini?”
Maswali hayo yaliulizwa na mwanamme huyu Makini George Charles,ilikuwa ni lazima afanye mambo kidiplomasia, katika swala hilo ilikuwa ni lazima acheze na akili ya Yusrath kwanza!Swali hilo lilimfanya Yusrath abaki njiapanda.
“Nitachagua vyote”
“Mshika mawili,moja humponyoka”
George Charles,akachomeka misemo ya kibongo japokuwa alikuwa ana muda mfupi sana nchini humo.
“Naelewa George,sasa nifanye nini?”
“Pick one,kuolewa ama kutimiza ndoto zako”
“Lakini kuolewa pia ni moja ya ndoto zangu”
“Kipi unataka kianze?”
“Hapo,ndio nachanganyikiwa zaidi wangu”
Yusrath akaropoka,kila kitu kwake kilikuwa kama kimevurugika kwa kiasi cha kutosha!
“Usichanganyikiwe,relax kila kitu kitakuwa sawa”
Udhaifu wa Yusrath,alikuwa tayari kaufahamu hivyo kazi ilikuwa kwake kutengeneza mazingira ya kumvuta karibu,namna ya kumpata Yusrath alishaelewa na ilibidi mikakati hiyo ianze mara moja!

****
Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele,mawasiliano kati ya Ahmed na Yusrath yalipungua sana!Moyo wa Ahmed uliuma ajabu,hakuelewa nini tatizo la Yusrath kwani mara nyingi alimpigia simu na ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa na akipokea atajibu kwa kifupi ‘Nipo bize nitakupigia’jambo hilo lilimuumiza sana mtima Ahmed,ukizingatia chereko chereko za harusi zilikuwa mbioni kutokea!Ahmed akahisi kuvurugwa akaumia ajabu, ingekuwa tiba hiyo inapatikana hospitalini angeenda,kifupi maumivu yake hayakuweza kutulizwa kwa vidonge, sababu panapomchoma akipapasa alikuwa hapaoni!
“Yusrath,ananijibu shit ujue.Simuelewi”
Malalamiko hayo,siku hiyo alimpelekea rafiki yake mkubwa Benjamin Patrick Ngowi!Urafiki wao haukuwa wa muda sana lakini walitokea kubadilishana mawazo mbalimbali ya kibiashara na harakati za maisha,Ahmed alikuwa msiri lakini maji yalikuwa shingoni siku hiyo.
“Yusrath yupi?Sindo huyu unayetaka kumuoa?”
“Ndio”
“Humuelewi kivipi?Amefanya nini broo?”
“Hapokei simu zangu,hatuongei vizuri kama zamani!Ananijibu anavyojisikia”
“Hiyo tabia kaanza lini?”
“Hivi karibuni”
“Kaa naye chini,muyaweke sawa.Nadhani atakuwa ana presha za ndoa”
“Sio kweli,nahisi kuna kitu”
“Kitu gani?”
“Kuna mwanamme amempata”
“Usipende kuhisi”
“Nakwambia ukweli Ngowi,nimeanza kupata picha.Nipe siku tatu,nitakupa jibu kamili”
“Ahmed,sikiliza nikwambie.Mwanamke hachungwi kama unavyodhani,utajitia presha bure!Kama unadhani huna uwezo wa kumuacha,usimchunguze kabisa!Ndio maana wazee wetu wa zamani,walikuwa wana dumu kwenye ndoa zao,wewe unadhani kwanini?”
“Kwanini?”
“Walikuwa wakiwa wanarudi majumbani,wanapiga miluzi.Walikuwa wana maana kubwa sana!Kifupi kama unahisi hauna ubavu wa kumuacha Yusrath,usimchunguze sijui ushike simu.Sababu mwisho wa siku utaumia”
Huo ndio ulikuwa ushauri wa Mr.Ngowi,mwanamme huyu alikuwa mpole mtaratibu na asiyependa kuona watu wanagombana hovyo,ndiyo maana alimshauri Ahmed aachane na faili hilo la kuhisi Yusrath ana kimada pembeni.
Kwa Ahmed alimsikiliza kwa makini lakini alichokuwa ana shauriwa kilipitia sikio la kulia na kutokea kushoto!

*******
Jumatatu asubuhi,alivyokurupuka kutoka kitandani akanyoosha moja kwa moja mpaka Posta,kwenye ofisi anayofanyia kazi Yusrath, kwakua walimfahamu kama ‘Supplier’ hivyo ilikuwa rahisi kwa walinzi wa getini kumruhusu aingie ndani,alichokifanya ni kunyoosha moja kwa moja mpaka mapokezi.
“Dada habari”
Ahmed,akamsalimia mwanamke mrembo aliyemkuta nyuma ya kompyuta.
“Salama, karibu”
“Ahsante”
“Nikusaidie nini?”
“Nahitaji kuonana na Yusrath,sijui nimemkuta”
“Yusrath?!”
“Ndio,Yusrath”
“Bado,hajafika!Unaweza kumsubiri hapo”
Ahmed akasubiri kwenye sofa kubwa lililokuwa kando kando!Alikuwa mwenye hamu kubwa ya kumuona Yusrath,dakika thelathini baadaye akatokeza, Ahmed akasimama na kumuendea kwa kasi.
“Yusrath”
“Ahmed!”
Yusrath akashtuka,hakutegemea kumuona Ahmed mahali hapo, siku kama hiyo tena asubuhi bila taarifa.
“Nimekuja tuzungumze”
“Sio hapa Ahmed,nakuomba.Hii ni ofisi ya watu”
“Naelewa Yusrath,nakupenda sana!Tafadhali tambua hilo”
“Ahmed hata mimi nakupenda,tutaongea leo jioni nakuomba”
“Kweli?”
“Ndio”
Ingawa mazungumzo yao yalikuwa kwa sauti ya chini lakini yalisikika moja kwa moja na mwanamke anayeitwa Zuwena,akatega sikio vizuri.Ahmed akaridhika na kuanza kuondoka, alivyotaka kufika mlangoni ili atoke nje, nayeye akasimama wima!
“Wee mkaka!”
Zuwena akaita,hiyo ilifanya Ahmed asimame na kugeuka nyuma!Hakuwa ana uhakika kama niyeye anaitwa ama nani.
“Mambo”
“Poa”
“Mimi naitwa Zuwena”
Bado Ahmed,aliendelea kukaa kimya alitaka kumsikiliza mwanamke huyo na ajue kilichomfanya amsimamishe.
“Wewe ni mchumba wa Yusrath?”
“Ndio”
“Sitaki kukuficha wala nini kaka angu..Yusrath anatembea na…..”
Kabla ya kumalizia anachotaka kuongea George Charles, akatokeza mlangoni,macho yake yakagongana na Ahmed!



Sura ya George Charles mwanamme aliyetokeza mbele yake,haikuwahi kumtoka hata kidogo!Katika watu ambao aliwahisi wana mahusiano na Yusrath basi George Charles alikuwa ni nambari moja,alikuwa ana kila sababu ya kumtuhumu kwani mazingira na matukio mbalimbali aliyojaribu kuunga, ilimfanya alipe wazo lake asilimia mia moja kwamba mwanaume huyo, anakula naye sahani moja,haikuwezekana hata kidogo Yusrath aajiriwe moja kwa moja bila kuwa na vyeti,mbaya zaidi alipewa cheo kikubwa!Zaidi na hilo, penzi lake lilikuwa katika mgogoro mkubwa,hiyo ikafanya amkate jicho kali George Charles akampandisha juu mpaka chini,akashindwa kuelewa ni kitu gani amwambie!Kila kitu kilionekana kuharibika katika maisha yake.
“Zuwena Niprintie zile Documents za jana”
George Charles, akazungumza baada ya kufika karibu kabisa na Zuwena,akamtizama Ahmed kwa sekunde tatu kisha kumvuka, ilielekea kuna vitu chungumzima vilikuwa ndani ya kichwa chake na vilitakiwa vitatuliwe siku hiyo,ndiyo maana baada ya agizo hilo akanyoosha moja kwa moja mpaka ofisini kwake.
Alichokifanya Zuwena ni kutafuta kalamu kwa kasi na karatasi ndogo,akaandika kitu juu ya karatasi hiyo na kumshikisha Ahmed!
“Namba yangu,utanipigia”
Zuwena akasema kwa sauti ya chini huku akiweka mikono yake sikioni kwa ishara ili kuitilia msisitizo sentensi yake!Ahmed hakutaka tena kubaki eneo hilo,akatoka nje na kutembea taratibu mpaka ofisini kwake ambapo huko alianza kutafakari vitu vingi sana.Muda mwingi aliutumia kumfikiria Yusrath,mwanamke anayempenda kuliko wote,vitu vingi vilianza kutiririka kichwani mwake, akawa kama anaangalia filamu ya kusisimua,akajiona kipindi cha mwanzo mapenzi walivyoanza,walivyokuwa wenye furaha kupita kawaida.Lakini iweje alivyoajiriwa tu tabia yake ibadilike?Hilo ndilo swali alilokuwa anajiuliza bila kupata jibu,kilichokuwa kinamvuruga akili yake na kufanya ashindwe kufikiria vizuri, iweje maseke hayo yatokee dakika za ukingoni? Ni bora tabia hiyo ingetokea kipindi cha mwanzoni na sio kipindi hicho ambacho kila ndugu,jamaa na rafiki walijua kuhusu ndoa yake!Hakuelewa sura yake angeiweka wapi, endapo Yusrath angegoma kuolewa naye.
Siku hiyo muda ulikimbia kwa kasi ya maporomoko ya maji,kufumba na kufumbua ilikuwa imegonga saa tisa ya alasiri,akakumbuka kuna namba alipewa kwenye karatasi,akatoa na kuanza kuipiga!Ambapo,iliita na kupokelewa na sauti ya kike,bila shaka alikuwa ni Zuwena!
“Mambo”
“Poa!Nani?”
“Ahmed”
“Ahmed gani?Wa wapi?”
“Nilikuwa asubuhi hapo ofisini kwenu,kumuulizia Yusrath ak…”
“Nimeshakukumbuka kaka angu,upo wapi sasa hivi?”
“Nipo ofisini”
“Namaanisha upo wapi?”
“Posta”
“Posta,hapa hapa?”
“Ndio”
“Ulisema wewe ndiye mchumba ake na Yusrath?”
“Ndio mimi”
“Mmmh”
Zuwena akaguna,hiyo ikafanya mapigo ya moyo ya Ahmed yapige kwa nguvu!
“Mbona umeguna?”
“Una kazi,nina ubuyu.Lakini una moyo,una kifua rafiki yangu?”
“Una maana gani?”
“Nataka kukwambia Mambo ya Yusrath”
“Amefanya nini?”
“Usinitaje lakini Kaka,sitaki kibarua changu kiote nyasi”
“Siwezi kukutaja niambie tu”
“Mimi sitaki kukwambia,nataka ushuhudie mwenyewe kwa macho yako”
“Kushuhudia nini?”
“Ikifika saa kumi,njoo ofisini hapa.Hakikisha,Yusrath hakuoni”
“Kwani huwa anatoka saa kumi?”
“Hapana,wewe njoo”
Moyo wa Ahmed,ulikuwa ukidunda kwa nguvu sana!Kijasho chembamba kilianza kumtoka,jinsi mwanamke huyo alivyokuwa anazungumza simuni, ilitosha kabisa kumwambia kwamba hakukuwa na jambo zuri japokuwa alimuomba sana Mungu kisitokee kitu anachofikiria sababu alizielewa hasira zake na wivu wake ulikuwa mkubwa mno dhidi ya Yusrath,kuanzia dakika hiyo tangu apewe taarifa hiyo masaa yakawa yanasogea kwa mwendo wa ajuza,hiyo haikuwa shida aliendelea kusubiri mpaka ilivyogonga saa kumi kamili jioni,akasimama na kutoa taarifa kwamba hajisikii vizuri hivyo bosi wake akimuulizia,isije ikaleta tatizo lolote lile.Akachomoka moja kwa moja,akavuka barabara akiwa mwenye mawazo mengi sana kichwani kwake!Hakutaka kufika kabisa katika jengo hilo analofanyia kazi Yusrath alichofanya ni kuvuka upande wa pili,akasimama kandokando ya banda la magazeti.
“Nipatie gazeti la Mwananchi”
Ahmed hakuwa mwenye niya ya kusoma,lengo lilikuwa ni kuzuga kwanza ili kutafuta pozi!Asingeweza kusimama eneo hilo bila kutafuta kitu cha kuzugia,alivyomlipa muuza magazeti pesa yake, akalifungua na kujifanya anasoma gazeti,akalivuta mpaka usoni kwake huku jicho moja likiwa makini kwenye lango la kutokea upande wa pili.
Alikuwa makini sana kuangalia upande huo,wafanyakazi walikuwa wakitoka na kuingia!Akasubiri kwa nusu saa lizima,ndipo akamuona Yusrath anatokeza, hiyo ilimfanya avute gazeti usoni kabisa,akasubiri kidogo baada ya dakika mbili nyuma akafuatia George Charles!Hakutaka kukurupuka na kuchukua hatua yoyote!Alichotaka kujua ni wapi watu hao wanaenda ingawa alianza kuhisi kuna hali ya hatari ipo mbioni kutokea,akawashuhudia kwa macho yake mawili Yusrath na George Charles wanaingia ndani ya gari aina ya Lancruiser V8,hilo lilikuwa gari la mtoto huyo wa bilionea,moyo ulimuuma ajabu hakuwa mwenye uhakika kwamba siku kama hiyo angekuja kuisahau katika maisha yake,ghafla akaanza kujichukia na kuuchukia umaskini kwa ujumla,hakutaka kuamini kwamba leo hii Yusrath,anamsaliti mchana kweupe!Alichokifanya ni kusogea mpaka zilipokuwa taxi nyingi,akasimama nyuma ya moja wapo!Mzee mmoja akatokeza,hakuwa mzee sana lakini kutokana na hali ya maisha kuwa ngumu alionekana kama mtu aliyepitia msoto!
“Mzee kwema?Shikamoo”
“Marahaba,twende tajiri”
Ahmed akaingia ndani ya gari,akaketi siti ya mbele!
“Wapi,tunaenda?”
“Unaona ile gari pale?”
“Ipi?”
“Landcruiser nyeusi”
“Ile kule mbele kabisa?”
“Ndio!Nina shida nayo,ifuate mpaka inapoishia”
“Hata kama inaenda Rombo?”
Mzee akaweka utani kidogo huku akiwasha gari,akaweka gia na safari ikaanza mara moja!
“Popote pale,wewe kaa nayo nyuma”
Mzee alikuwa makini sana,mikono yake miwili ipo juu ya usukani,anatizama kwa umakini gari aina ya Landcruiser v8, lisimpotee kwenye upeo wa macho yake,wakaingia Kisutu na kutokeza moja kwa moja katika hospitali ya Regency,wakakunja na kutokea katika shule ya Zanaki!Bado walikuwa sambamba,mbele yao kulikuwa na Kirikuu mbele ya Kirikuu ndio gari aina ya Landcuiser V8 lilisimama,humo ndimo Yusrath na George walikuwemo!Kila kitu kwa Ahmed hakikuwa sawa kabisa,alihisi angepoteza kila kitu kama angemkosa Yusrath,bado hakupata picha kamili ni kitu gani akifanye,hapohapo pepo baya likamvaa likamfanya atake kuwauwa George na Yusrath kisha nayeye ajiue lakini akalikemea lishindwe,wakasonga mbele mpaka walipofika maeneo ya Upanga karibu na Chuo Kikuu cha Mzumbe kilichokuwa na tawi jijini Dar es salaama,gari alilokuwa anaendesha George likazidi kusonga mbele mpaka walipotokeza daraja la Salenda.
Ndani ya gari Ahmed alitamani kuruka kutokea dirishani,wivu ulikuwa umefika katika kiwango cha mwisho kabisa,ukajichanganya na hasira, akaanza kutetemeka kama mtu mwenye homa kali ya usiku,hiyo ilimfanya dereva taxi alione hilo.
“Vipi kaka ,upo sawa?”
Mzee huyo dereva taxi akauliza lakini hakujibiwa kitu chochote kile.

*****
Siku zote pesa ni sabuni ya rohoo!Hakuna kitu alichoharibu kama kumueleza George ndoto zake, hilo lilikuwa ni sawa na kuteleza ndani ya kumi na nane!George Charles alitaka kuitumia fursa hiyo ipasavyo,hakutaka kufanya makosa.Kila kitu alikipangia mahesabu,hakutaka kwenda pupa hata kidogo.Ndoto za Yusrath siku zote, alitaka kuja kuwa mwanammke anayemiliki miradi mingi na mfanyabiashara mkubwa sana nchini, kwa George swala hilo lilikuwa ni dogo kulitimiza,alikuwa ana uwezo wa kumsafirisha Yusrath nchi yoyote ile anayotaka,alikuwa mwenye pesa za kumnunulia gari lolote analohitaji,pesa zake zilitosha kabisa kumjengea nyumba Yusrath ama vyote kwa pamoja.Lakini hakutaka kutengeneza mazingira hayo kwa kasi,alichokifanya ni kumuhaidi kumpeleka katika moja ya machimbo yake ya kokoto yaliyokuwa huko Kunduchi,kumaanisha kwamba Yusrath ndiye angekuwa kila kitu katika kusimamia mradi huo wenye pesa nyingi,hiyo ilikuwa na maana kwamba mshahara wake ungeongezeka mara nne yake,siku hiyo walikuwa njiani kwenda kutembelea machimbo hayo ya kokoto.
“Nimekuamini sana,ndiyo maana nataka kukupa huku usimamie”
George alizungumza wakiwa ndani ya gari.
“Ahsante sana boss na ofisini je?”
“Kila kitu utafanya huku utakuwa unakuja kukagua,kwa wiki mara moja!Unaandika ripoti,unanitumia”
Yusrath alikuwa mwenye furaha ajabu,hakuelewa kwamba yupo kwenye mtego na yupo mbioni kuingia katika anga za George Charles,ambaye alikuwa anayasoma mawazo yake na kutumia diplomasia ya hali ya juu sana!Akajiona ni mwanamke mwenye bahati kuliko wote,akamshukuru sana Mungu,hakuelewa hesabu za George zilikuwa ni kumuweka kwanza mbali na Ahmed wake,ambaye alimchumbia tayari.
“Wiki ijayo,nitakuagiza Arusha.Ukifanya vizuri.Nitakutuma South Africa!”
Maneno hayo yalipenya kwenye masikio ya Yusrath,akatabasamu.Akahisi kama tayari ametajirika akaanza kuzipigia hesabu pesa atakazolipwa kama posho na mshahara,kichwani mwake akaanza kuchanganua aina ya biashara atakayoanza,akamtizama George mara mbilimbili bila kuamini,shukrani alizompa hazikuwa na mfano wake!Safari hiyo ilikomea Mwenge kwenye mgahawa mkubwa ambao ulikuwa unauza juisi na chakula,hapo wakashuka ili wakale kidogo kisha baadaye waendelee na safari yao.Kitendo cha kuingia ndani,taxi aliyopanda Ahmed ikafika!Kwa presha aliyokuwa nayo,akafungua mlango bila kusahau kumlipa dereva ujira wake.
“Broo..Brooo..Oyaaa..Kiongozi”
Dereva taxi,akamuita huku akifungua mlango wa gari,Ahmed akageuka.
“Umesahau,kunilipa”
“Aaah,samahani.Bei gani?”
“Twenty”
Bila kuhoji chochote Ahmed akatoa pesa hiyo na kuingia ndani kwa kasi kama mshale,kiti cha mwisho kabisa akamuona Yusrath amekaa,alivyoangalia kushoto akamuona George Charles yupo sehemu maalum ya kuagiza juisi.
“Yusrath,kwanini unanifanyia hivi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed,akiuliza kwa uchungu sana.
“Ahmed,ume…”Bumbuazi,alilopigwa Yusrath,halikuwa na mfano wake!
“Kwanini unanifanyia hivi?
“Kukufanyia nini?”
Badala ya Yusrath kujibu swali,akauliza swali.Likawa swali juu ya swali,hiyo ilifanya Ahmed azidi kupandisha mori.Mbaya zaidi hakutumia ustaarabu hata kidogo,kilichomuongoza zilikuwa ni hasira na sio kitu kingine,hiyo ilifanya mpaka macho yake kubadilika rangi na kuwa mekundu.Kulikuwa kuna kila dalili mbaya kutokea siku hiyo,kelele hizo zilimfikia George akiwa mbele kabisa,akashika glasi mbili zilizokuwa na juisi akasogea mpaka karibu kabisa na meza ya Yusrath kwa niya ya kumtuliza mwanaume huyo,anayemfokea!
“Yusrath,kuna nini?”
George akauliza kiustaarabu akiwa bado ameshika glasi za juisi.Alichofanya Ahmed ni kumnyang’anya glasi moja wapo na kumwagia usoni,akamgeukia Yusrath na kumshika mkono na kumvuta kwa nguvu.
“Tuondokeee”
Hali ya hewa ilikuwa tayari imebadilika,George Charles kamwagiwa juisi usoni dharau ambayo hakuwahi kufanyiwa tangu azaliwe,Yusrath akazidi kuvutwa kwa nguvu.
“Tuondokeee”
“Siendi Ahmed,achana na mimi.Niachiee….paaaaa”
Haikujulikana ilikuwaje lakini kilichosikika,kilikuwa ni mlio wa kibao kikali kilichomfikia Yusrath shavuni,akayumba na kuparamia meza,kila mtu ndani ya mgahawa huo akabaki kushangaa!Ahmed,alikuwa tayari amepandisha mori kwa hasira anahema,kifua chake kinapanda juu na kushuka.



George Charles alikuwa kimya,hasemi chochote anatafakari dharau aliyooneshwa ndani ya mgahawa huo!Kwa heshima kubwa na pesa alizokuwa nazo haikuwa rahisi kubaki kimya ilikuwa ni lazima Ahmed akaozee jela lakini kwake ilikuwa kinyume chake.Kitu kingine kilichomfanya ajiulize maswali mengi kichwani ni kosa gani amefanya?Mbele yake alisimama mwanamme ambaye sura hiyo haikuwa ngeni machoni mwake,japokuwa huwa anakutana na watu wengi sana kwa siku!Cha ajabu alimuona Yusrath anavutwa kwa nguvu kutoka nje,hakuwa nala kufanya zaidi ya kuweka glasi yake juu ya meza!Akaangalia mlango ulipo ili atoke,macho ya watu wote yalikuwa kwake,hakutofautishwa na mtu aliyekuwa jukwaani anatizamwa,hali ya hewa tayari ilikuwa imechafuka.Ahmed alizidi kumvuta Yusrath kutoka nje huku akimfokea kama mtoto mdogo.
“Ahme…d niacheee”
Yusrath alizungumza kwa uchungu huku akibubujikwa na machozi ya hasira,kitendo hiko kilikuwa cha udhalilishaji wa hali ya juu sana,isitoshe hiyo ilikuwa ni mara ya pili.Alihisi kujuta kumsamehee na kurudiana na Ahmed,kitendo cha George Charles kupita mbele yake akamshika shati.
“George please nisaidi…e,nao..mba unisaidie”
George akawa amesimama,hakuweza kutembea sababu shati lake lilikuwa limeshikiliwa na Yusrath analia, akimuomba msaada.
“Broo,achana na hii kesi!Usije ukajitafutia matatizo”
Ahmed akachimba mkwara akiwa katika jazba kubwa lakini Yusrath alizidi kumng’ang’ania shati George,sio siri ilikuwa kama sinema ya kusisimua.
Kila mtu katika mgahawa huo alisimama ili kushuhudia tukio hilo la aina yake,kuna wengine walidhani labda watu hao wapo kwenye maigizo lakini haikuwa hivyo,kilichotokea mbele yao kilikuwa kina uhalisia mtupu.Alichokifaya George ni kuitoa mikono ya Yusrath kwenye shati lake na kutembea kuelekea kwenye gari lake,alikuwa ana hasira zilizofika katika kiwango cha juu kabisa lakini hakutaka kuziruhusu zimuendeshe, alivyotaka kuingia ndani ya gari!Yusrath akawa tayari amemfikia,akasimama nyuma yake!Ahmed akatokea mbele yake.
“Broo,huyo ni mke wangu!Hiko kigari chako cha kuazima kisikufanye umdange mke wangu”
Hayo yalikuwa ni maneno ya Ahmed bila kujua,anazungumza na bilionea mwenye magari mengi kuliko kawaida,George hakusema kitu chochote akageuka na kufungua mlango,akamsogeza Yusrath pembeni ili aingie ndani ya gari lake lakini cha ajabu Yusrath akaingia yeye tena upande huohuo wa dereva,akaruka upande wa pili.Hiyo ilimfanya Ahmed achukie zaidi,kwa hasira alizokuwa nazo pamoja na wivu akajikuta anamkunja shati George Charles, ambaye kwa wakati wote alikuwa kimya haongei kitu.
“Namuomba mke wangu,achana naye!Sawa,nadhani mimi hunijui vizuri.Namuomba mke wangu nimesema”
George Charles, badala ya kukasirika,akatabasamu kwanza!Hiyo ndiyo ilikuwa sifa ya mwanamme huyu akikasirika,kwanza anatabasamu alafu sekunde hiyohiyo anakunja sura,hivyo ndivyo ilivyokuwa.
“Bwana mdogo,niachie.Usije ukatafuta shida,sitaki tufike huko”
George akasema kwa ghadhabu.
“Nimekwambia mshushe mke wangu ndani ya gari”
Kwa kuwa hakutaka ugomvi na shari,alichokifaya ni kufungua mlango na kuingiza kichwa ndani, akamtizama Yusrath
ambaye wakati huo alikuwa akilia kwa kwikwi.
“Yusrath,shuka ndani ya gari.Mmeo anakuita”
“Si..wezi kushuka,sio Mme wangu!Ahme..d naomba niache,acha…na mimi”
George hakuwa na jibu lingine zaidi,akaitoa mikono ya Ahmed na kuingia ndani ya gari,kabla ya kufanya chochote akaweka kichwa chake juu ya usukani.Alifanya hivyo ili ashushe kwanza jazba zake asingeweza kuendesha gari akiwa katika hali kama hiyo,hasira alizokuwa nazo zilitisha kingine kilichomfanya aumie zaidi ni kusikia kwamba Yusrath alikuwa mke wa mtu tayari,hilo hakuweza kukaa nalo moyoni.
“Kumbe umeolewa?Mbona hukuniambia?”
Kichwa chake kikiwa juu ya usukani,akauliza kwa uchungu.
“Sija..olewa”
“Usinidanganye”
Katika maisha yake,hakuwahi kuja kufikiria kutembea na mke wa mtu, zaidi na hayo hakujua kama Yusrath tayari ameolewa ingawa jambo hilo hakutaka kulipitisha ndani ya kichwa chake moja kwa moja.
“Please Georg..e niamini.Mimi sijaolewa”
Ahmed alikuwa nje,anagonga kioo cha gari anatamani kukivunja.Ili kuepusha watu kujaa eneo hilo.alichokifanya George ni kuliwasha gari na kulitoa eneo hilo.
“Psiiiii,boda boda”
Ahmed akaita pikipiki moja wapo iliyokuwa pembeni,ikafika mpaka kwenye miguu yake.
“Fatilia hiyo gari”
“Poa broo,chukua elementi”
Ahmed,akavaa kofia hiyo maalum kwa ajili ya usalama wake, safari ya kuifuatilia Landacruiser V8 ikaanza mara moja.
“Yule mkeo nini kaka?”
Dereva wa pikipiki akaanza mazungumzo,tukio lililotokea alilishuhudia hivyo alitaka kujua nini kimetokea, watoto wa mjini wangesema anataka ubuyu.
“Ndio”
“Imekuaje tena?Ungetuita wahuni tumfanyizie!”
Kuanzia hapo Ahmed hakujibu chochote,machozi ya hasira yakaanza kumbubujika.

***
“Shut up,i said shut your mouth”(Nyamaza,nimekwambia nyamaza)
George Charles alimnyamazisha Yusrtah kwa sauti ya ukali mno wakiwa ndani ya gari,hakuwahi kuwa hivyo kabla,udhalilishaji aliofanyiwa ndani ya mgahawa bado ulimsumbua kichwani.Aliamini hakustahili kufanyiwa kitu kama hiko,alivyoangalia shati lake lilikuwa limechafuka na limeacha mabaka ya juisi,mbali na macho yake kubadilika rangi lakini Yusrath hakuacha kuomba msamahaa kwa kitendo alichofanya akijaribu kujielezea,alielewa kabisa yeye ndiye chanzo!Lawama zote akamtupia Ahmed akijitetea kwamba hakuwa ameolewa,hiyo haikumfanya George ajibu kitu chochote kile mikono yake ilikuwa juu ya usukani anaendesha gari macho yake yote kayatupa mbele,hageuki!Yusrath akazidi kuongea mwenyewe bila kujibiwa,hiyo ilikuwa wazi kabisa baada ya hapo kibarua chake kingeota nyasi na ndoto za kupelekwa ili akabidhiwe mradi wa machimbo ya kokoto zingeenda kuzimika kumaanisha kwamba ndoto zake zote asingeweza kuzitimiza.
“George i’m so sorry”(George,nisamehee)
Mambo yaliyokuwa yanamiminika ndani ya ubongo wa George, yalikuwa ni mengi mno,aliwaza vitu chungu mzima!Akazidi kusonga mbele na safari yao ikaishia nje ya geti kubwa la kisasa, lililokuwa na matairi madogo kwa chini,likaanza kusogea lenyewe Landcruiser v8, likaingia ndani mlinzi aliyekuwa na gobole mgongoni akasukuma geti ili alifunge lakini kabla ya kumalizia kufunga,mwanamme mmoja akatokeza na kutaka kuingia ndani.
“Mke wangu,kaingia humu”
Ahmed alivyowasili akapiga kelele akilalamika lakini akazuiwa na kusukumizwa kwa nje.Roho ilimuuma zaidi sababu alimuona Yusrath anashuka kutoka ndani ya gari,mbaya zaidi jumba hilo la kifahari likamfanya akose raha,nje kulikuwa na magari mengi ya kifahari,hapo akaamini kwamba mwanamme huyo hakuwa mtu wa kawaida na kivyovyote vile alielewa mali hizo ndizo zilimchanganya Yusrath wake,akalia kwa uchungu huku akijipiga piga kifuani.
Hakuamini kama leo hii amepokonywa tonge mdomoni,sio siri siku hiyo alilia kama mtoto mdogo,kamasi zikamtoka.Akajua tayari Yusrath hakuwa wake tena!
“Kijana kalilie huko mbali,unapiga kelele”
Mlinzi wa getini akatoka nje akiwa na gobole mkononi,ilielekea alipewa maagizo kutoka kwa tajiri yake!Hiyo ilimfanya Ahmed,asimame kinyonge na kuanza kutembea, wakati mwingine alianza kujuta ni kwanini amechukua hatua hiyo mkononi ya kumpiga Yusrath,akajilaumu na kujichukia,akaelewa kabisa kama Yusrath angemuacha basi chanzo angekuwa niyeye sababu aliamini siku zote mwanamke apigwi,bali analiwazwa na kubembelezwa!

****
Hata baada ya kuingia ndani, George Charles hakutaka kuongea chochote,alikaa kimya akitafakari vitu vingi sana kichwani mwake!Yusrath nayeye alikuwa nyuma akimuomba msamahaa bado kwa tukio baya sana lililotokea,aliamini alistahili kusamehewa ndio maana alikuwa akihangaika.Akawa anamfuata George, nyuma mpaka walipofika Seblen ambapo huko mwanaume huyo alinyoosha mpaka kwenye friji na kuchukuwa glasi ya maji ya kunywa,akanywa ili kushusha hasira zake.Bado,hakutaka kuzungumza chochote,alichokifanya ni kupanda ngazi ili aingie chumbani kwake,Yusrath hakutaka kubaki. Nayeye akaanza kupandisha ngazi harakaharaka,bila kujali kitu chochote.George Charles alivyoingia chumbani,Yusrath nayeye akazama ndani ya chumba hiko,Mlango ukafungwa!

****
Kitu alichokifanya Ahmed kilikuwa ni kibaya sana,hilo alianza kujuta mwenyewe baada ya kutulia na kutafakari.Uhakika ulikuwa ni kwamba mkataba wake na Yusrath ulikuwa tayari umevunjika,hilo lilikuwa ni wazi kabisa sababu kitendo kama hicho ilikuwa ni mara ya pili kutokea,usiku wa siku hiyo hakulala kabisa aliweweseka usiku,moyo wake ukamtuma ajaribu kumpigia simu Yusrath ingawa hakuwa ana uhakika kama jambo hilo lingefua dafu,bila kutafakari zaidi akachukuwa simu yake na kumuendea hewani!Simu iliita bila kupokelewa,akajaribu tena na tena lakini mwisho wa siku,haikupatikana kabisa hewani kumaanisha kwamba Yusrath amezima simu, hataki kuzungumza naye tena.Hapo ndipo akahisi kama moyo wake,unawaka moto ajabu!Mpaka hapo,hakujua ni jambo gani alifanye,hakuna kitu ambacho alikuwa anasubiri kama kukuche haraka,usiku huo alitafakari vitu chungu mzima ndani ya kichwa chake,hususani swala zima la ndoa yake,itakavyokuwa.Hakujua sura yake ataiweka wapi kwani mipango ya ndoa ilikuwa ukingoni na kila mtu alikuwa akijua tayari.Kulivyokucha tu,akajaribu kumtafuta Yusrath simuni lakini simu iliita bila kupokelewa,baada ya muda mfupi ukaingia ujumbe wa meseji ‘Sahau kuhusu ndoa,siwezi kuwa mkeo.Naomba usinisumbue’Yalikuwa ni maneno makali ya kuchoma kutoka kwa Yusrath,hiyo ilimfanya Ahmed aishiwe nguvu za miguu akiwa kituo cha daladala, anasubiri usafiri aelekee ofisini kwake Posta.Alichofanya ni kusogea kandokando ili ajaribu kupiga tena simu kwa mara nyingine,lakini haikupokelewa.Alichofanya ni kutuma meseji ‘Naomba unisamehee Mke wangu,naomba tuonane tuzungumze tuyamalize sitorudia tena’ Kuanzia hapo alikuwa akisubiria meseji kutoka kwa Yusrath,macho yake yote yakiwa juu ya kioo cha simu yake, akisubiri majibu kwa hamu,mapigo yake ya moyo yakapiga kwa nguvu baada ya kusikia muungurumo wa meseji kuingia.
Alivyotaka kufungua daladala la Posta,likawasili mahali hapo.Akaingia na kukaa kwenye siti ya nyuma kabisa ili aweze kusoma ujumbe huo,mapigo yake ya moyo yaliendelea kukita kwa nguvu zote,akafungua meseji ‘Huna salio la kutosha kutuma ujumbe huu….’ Almanusura atukane ndani ya daladala, ulikuwa ni ujumbe uliomtaarifu kwamba hana salio la kutosha kutuma ujumbe aliotaka kutuma, hivyo ilibidi anunue vocha na kuweka,kwa kuwa alikuwa ana salio kwenye simu yake Tigopesa,akanunua hapohapo na kurudia kutuma ujumbe kwa Yusrath.Akasubiri ili ajibiwe lakini hakukuwa na dalili ya aina yoyote ile ya Yusrath kujibu kitu cha aina yoyote ile.
Vitu vingi sana alivitafakari,hakupata jibu kamili.Kitu alichokuwa anakiwaza siku zote, kilikuwa kina ukweli ndani yake,kwamba ni lazima George Charles anatoka kimapenzi na Yusrath,alivyokumbuka hayo moyo ukamuuma ajabu.Wakati mwingine alidhani wenda kutokana na kipato duni alichokuwa nacho kwani mjengo wa George Charles,haukuwa wa mchezomchzeo!Akaapia kwa Mungu wake ni lazima atafute pesa ili baadaye asije kunyanyasika hiyo ikampa hasira sana!Nusu saa baadaye akawa ameingia Posta tayari,akanyoosha moja kwa moja mpaka mlango wa ofisi yake ilipo,alivyopishana na Aneth Kasera kwenye korido akamshika mkono.
“Nina shida nawewe”
“Saa ngapi?”
“Sasa hivi”
“Subiri kidogo,bosi yupo kuna kazi hapa nishavurunda.Nitakuja ofisini kwako”
“Poa,nitakusubiri”
Hakukuwa na msaada mwingine zaidi ya kumuingia Aneth Kasera kwa mara nyingine ili ampe mbinu kama za mara ya kwanza alizofanya ingawa hakuwa ana uhakika kama atasamehewa na Yusrath wake,akajitahidi kufanya kazi alizozikuta mezani kwa siku hiyo lakini haikuwezekana hata kidogo!
Mawazo yote yakawa kwa Yusrath,akatamani atoke nje amuibukie ofisini kwake lakini asingeweza kufanya hivyo,aliogopa sababu alijua hasira zake zilivyo wenda angeweza kuharibu kila kitu!Kwa kawaida huwa ana kunywa chai ama kahawa lakini siku hiyo hakuna kitu chochote kati ya hivyo vilivyopanda,saa tano mlango wake ukafunguliwa Aneth Kasera akawa ameingia na kuketi pembeni ya kiti cha wageni.
“Ahmed,nambie boss wangu”
Aneth akaanza maongezi,ni mwanamke pekee ambaye alimzoea kuliko mfanyakazi yoyote yule.
“Sio shwari”
“Nini tena?”
“Wifi yako”
“Kafanya nini?Ushambutua tena nini?”
Aneth akauliza kimasihara masihara, hakuelewa kwamba ni kweli alichosema,hiyo ilifanya Ahmed akae kimya.
“Sijui itakuwaje?”
“Ahmed please,don’t tell me umempiga tena mtoto wa watu”
“Subiri kwanza”
“Nini sasa?”
Aneth akaonekana kukerwa kidogo, ndiyo maana akauliza kwa jazba akiwa makini anamtizama Ahmed.
“Bahati mbaya..”
“Bahati Mbaya nini?”
“Mkono uliteleza”
“Ilikuwaje?”
Aneth Kasera,akataka kupewa mkanda mzima ajuwe jinsi ilivyokuwa.Ahmed,akashusha pumzi.Akamtizama Aneth akaanza kumuhadithia tangu mwanzo, ilivyokuwa mpaka timbwili lilivyotokea kwenye mgahawa,akahitimisha kwa kusema anajuta sana.
“Ahmed,unakosea sana!Mwanamke hapigwi hata kidogo,kuwa gentleman.Sio siri,umenikera.Hata ningekuwa mimi,nisingekusamehee!Hii mara ya pili,unampiga.Hapo hujamuoa..Hizo ni zama za kale”
Sio siri siku hiyo Aneth Kasera alitoa povu sio la kawaida,akamdharau Ahmed kwa kiasi cha kutosha akamsema na kumpa vidonge vyake,hiyo ilimfanya Ahmed atulie na kujuta kwa kila kitu alichokifanya.
“Sasa ningefanya nini Aneth?”
“Kwahiyo kumpiga ndiyo suluisho?Ungetulia,ungekuwa mpole!Sasa ungeitiwa mwizi je?Ungemlaumu nani Ahmed,vitu vingine uwe unatafakari mara mbilimbili wewe ni msomi.Sasa ngoja nikwambie ukweli kama ndio jamaa alikuwa anatupa mawe,ndio atachukuwa advantange ya kumchukuwa,sikufichi”
“Amchukuwe mara ngapi?”
“Una uhakika gani?”
“Ninao”
“Usipende kuhisi,alafu nishakujua kinachokusumbua wewe.Ni wivu tu,huna lolote”
“Ni kweli.Naomba nisaidie Anneth”
“Nitajitahidi”
“Lini?”
“Nipe muda”
“Hapana,naomba leo”
“Itakuwa ngumu kidogo”
“Nakuomba,nipo chini ya miguu yako”
“Ha! Haa! Haaa! Kumbe Ahmed unakuwaga mpole namna hiyo,kweli mtoto kakuteka!Sasa sikia,umesema yupo Posta hapo Hajryemer Investment?”
“Ndio”
“Twende wote saa nane”
“Na mimi?”
“Ndio”
Jambo hilo lilikuwa ni zito kidogo lakini hakuwa na jinsi ilikuwa ni lazima aonane na Yusrath,amuombe msamahaa na warudiane amani itawale.
Saa nane juu ya alama,ilivyofika Aneth akawa tayari amewasili wakasimama na kutoka nje ya ofisi, ambapo huko walivuka barabara mpaka upande wa pili.Aneth alikuwa tayari kujitolea kwa lolote lile,ndiyo maana alikuwa mstari wa mbele na hata walivyofika katika jengo hilo kubwa,akajitambulisha kama ‘supplier’ akaingia. Ahmed nayeye akazama ndani,moja kwa moja wakapitiliza mpaka mapokezi.
“Tumemkuta Yusrath?”
“Yes yupo”
Dada wa mapokezi akajibu.
“Tunaweza kumuona?”
“Kiofisi ama?”
“Ndio”
“Okay,subirini hapo”
Hapohapo simu ikapigwa mpaka kwa Yusrath, bila kujua ni wageni gani,akatoa ruksa wapite ndani.Majonzi yalitawala kwa mwanamke huyu,binafsi hakuweza kufanya kazi vizuri,kuna vitu vingi sana alikuwa akiwaza ndani ya kichwa chake,hususani kitendo cha Ahmed kumpiga kwa mara nyingine,aliapia hatoweza kumsamehee japokuwa hakuwa ana uhakika kama ataweza kusimamia msimamo wake huohuo!Mlango wake wa ofisini ulivyofunguliwa,akaingia Aneth Kasera nyuma yake akafuatia Ahmed,moyo wake ukapiga kwa nguvu,akamtizama Ahmed kwa hasira.
“Naomba mtoke nje,sasa hivi”
Ilikuwa ni kauli kutoka kwa Yusrath,hakutaka kuwasikiliza sababu alielewa shida yao.
“Tokeni nje please”
Akasema tena kwa ukali,hapohapo mlango ukafunguliwa kwa mara nyingine, George Charles akaingia na kumtizama Ahmed kwa macho makali,kuashiria kwamba hakukuwa na dalili nzuri ya amani kwani alikumbuka kila kitu kilichotokea siku iliyopita.



Katika watu walioonesha kutetemeka ndani ya chumba hiko, ambacho kwa wakati huo kilionekana kidogo ni mwanamke huyu Yusrath,mbele yake walisimama wanaume wawili,bosi wake George Charles na pembeni yupo mpenzi wake ambaye hawakuwa na maelewano mazuri, huyu aliitwa Ahmed Kajeme.Moyo wake ulikuwa ukipiga kwa nguvu sababu alijua ni kitu gani kingetokea sekunde chache zijazo.Alimuelewa Ahmed,ngumi mkononi mwenye hasira chafu sana tena za kutisha!Hivyo sekunde yoyote kuanzia hapo kingenuka,hilo lilikuwa wazi kutokea sababu sura yake ilianza kuchora makunyanzi akimuangalia George Charles kwa chuki za waziwazi kumaanisha kwamba muda wowote angemvaa kama chui mwenye njaa kali sana,matukio mbalimbali yalipita kichwani kwa George Charles!Alikumbuka dharau aliyooneshwa na mwanamme huyo siku iliyopita,kisasi alichokuwa nacho ndani ya mtima wake kilikuwa kikubwa lakini hakutaka kuchukuwa hatua hiyo mapema namna hiyo.Akakwepesha macho yake kwa Ahmed na kumtizama Yusrath,ambaye kwa wakati huo alionekana anahenya!Alishaelewa nini maana ya Ahmed kuanzisha vurugu ndani ya ofisi hiyo.
“Bos…..”
“Nipatie lile faili la Kuki’s Oil”
George Charles,akajua ni namna gani Yusrath anavyotetemeka, hivyo ilibidi amkatishe!Kutokana na kutetemeka kwake ilifanya mpaka asione faili lenyewe, kazi yake ikawa ni kuvuta madroo yote,akaanza kuangalia mezani bila kuona chochote.
“Sio hilo hapo?”
George Charles,akahoji.Ni kweli Yusrath alivyotupa macho yake mezani akaona faili hilo,akalichukua na kumkabidhi.Kitendo cha kulishika na kugeuka ili atoke,Ahmed akasimama mbele yake,akamuangalia machoni kwa hasira kali huku akiyabana meno yake,wivu umemkaba kohoni kuliko kawaida,chochote kibaya kilikuwa mbioni kutokea sababu Ahmed alianza kuhema kwa juujuu akimtizama George wakawa kama majogoo wawili wanaovimbiana.
“Ahmed…..”
Aneth nayeye akasimama,akamshika mkono Ahmed ili asijaribu kufanya jambo lolote la kipuuzi.
“Ahmed,nakuomba usifanye hivyo!Naomba ukae chini”
Yusrath nayeye akaingilia kati ili kumtuliza Ahmed,hapo ndipo mwanaume huyo akageuka kwa ujasiri.
“Chagua kimoja,mimi au huyu?Nani unampenda?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Ahmed,akiuliza akiwa ndani ya ofisi hiyo bila uwoga wowote ule kwani alitaka kujua kama Yusrath ni fungu lake,japokuwa aliongea kwa hasira lakini alimaanisha kile anachokiuliza,hakutaka kubaki na dukuduku akiogopa kupata kiungulia,hiyo ndiyo ilikuwa sifa ya mwanaume huyu jasiri.
“Yusrath naongea nawe…”
“Hapa sio mahali pake Ahmed”
“Niambie mahala sahihi”
“Ahmed,sikia…”
Aneth Kasera akamkatisha,ilielekea kuna kitu cha ziada alitaka kuchangia.
“You should behave, hii ni ofisi ala…”
“Aneth,kaa chini hili niachie mimi…Yusrath,talk to me”Aneth akatulizwa!
Ahmed hakutaka kuelewa somo,alitaka kujuwa msimamo wa Yusrath upo wapi siku hiyohiyo,moyo wake ulikuwa ukichoma kama pasi,ndiyo maana hakutaka kubaki na mzigo huo moyoni alitaka kuutua ingawa alijua baada ya hapo angejifungia chumbani na kulia machozi,hakuelewa na hakupata jibu ni wapi angempata mwanamke kama Yusrath,atakayekuwa anamshauri,mbali na hapo mazoea ndiyo yangempa taabu.
Hakuna siku aliyokuwa katika wakati mgumu kama hiyo,Yusrath alikuwa njiapanda,japokuwa hakuwa ana mahusiano na George Charles bali kilichomuweka hapo lilikuwa ni jambo moja tu,kutimiza ndoto zake na mwanamme pekee aliyekuwa na uwezo huo alikuwa ndiye huyo George!Kwa wakati huo alitakiwa kuchagua kitu kimoja ndoto zake ama hisia, kitu ambacho kilikuwa kigumu sana.
“Ahmed nakupenda lakini pia naomba ujuwe kitu kimoja,George sina mahusiano naye ya aina yoyote ile.He’s my boss swallow it, vomit it i don’t care.Enough is enough! I’m sick and tired of this bullshit. I do realy love you.Kukupenda isiwe makosa usiniburuze unavyotaka wewe.Ahmed wewe ni mbinafsi sana,hutaki nifanye kazi.Una wivu,hupendi maendeleo yangu!Hutaki nitimize ndoto zangu…..”
Hakuwa Yusrath yule anayezungumza kwa sauti ya upole na utaratibu siku zote,siku hiyo aliuwasha moto!Akapayuka kwa sauti, hiyo ikafanya sauti yake isambae na kutoka nje ambapo wafanyakazi wengine walitega masikio yao vizuri ili wasikie nini kinaendelea.
Mishipa ya shingo ya mwanamke huyu ilisimama na kutokeza,misuli ya usoni ikaanza kuonekana kumaanisha kwamba aliongea huku akiwa ana hasira, mbaya zaidi machozi yalianza kumtoka.Mshtuko na jazba alizokuwa nazo Ahmed,zilitulia kwa wakati huo,hakuwahi kumuona Yusrath akiwa katika hali kama hiyo tangu amfahamu ndiyo maana akabaki akimshangaa.Kitendo cha Yusrath kumaliza kuzungumza dukuduku lake lililokuwa moyoni siku zote, akaketi juu ya kiti na kuinamisha kichwa chake juu ya meza,hapo hakuweza kuzuia tena hisia zake,akaanza kulia kama mtoto mdogo.
“Chaguo ni lako,by the way....Mnaweza mkaenda.Huu ni muda wa kazi”
George akasema na kutaka Ahmed na Aneth waondoke mara moja mahali hapo,wivu ulimshika hakutegemea kitu kama hiko kutokea mbaya zaidi kwa Yusrath kutamka waziwazi anampenda Ahmed mbele yake,jambo hilo kwake akalichukulia kama dharau fulani, ndiyo maana hakutaka kumuona Ahmed mahali hapo.
“Nitaondoka kwa Muda wangu”
Ahmed akajibu kwa kiburi huku akimtizama George Charles kwa dharau kubwa sana.
“But this is my office, leave now.Both of you”(Lakini hii ni ofisi yangu,ondoka.Wote ondokeni)
Hiyo ilikuwa ni amri sio ombi,George Charles alikuwa ana mamlaka ya kufanya kitu chochote kile sababu hiyo ilikuwa ofisi yake!Ndio maana akawataka wapotee eneo hilo mara moja,akarudia tena kwa mara nyingine akisema kwamba ndani ya dakika mbili wawe wamefutika eneo hilo vinginevyo,angewafunga mara moja ama awaitie polisi.
“Ahmed tuondoke”
Isingekuwa Anneth kuingilia kati,siku hiyo Ahmed asingetoka eneo hilo.Alikuwa yupo tayari kwa lolote lile ndiyo maana alibaki amesimama anamtizama George aite polisi wake.
“Aneth…”
“Ahmed,tuondoke nakuomba”
“Alafu huyu koloo eeh...Mwache aite polisi wake,ananitishia polisi mimi?Stupid,mimi naogopa polisi?Alafu jiangalie Ke…”
“Ahmed,nini lakini..Nakuomba baba angu”
Mwili wa Aneth ulikuwa ukitetemeka sababu alijua nini maana ya polisi kuitwa mahali hapo,ilikuwa ni lazima wangelala ndani kumaanisha kwamba kibarua chake kingeota nyasi, hivyo hakutaka jambo hilo litokee sababu ndugu zake wote waliokuwa kijijini walimtegemea yeye isitoshe Mama yake alikuwa ni mgonjwa,kifupi yeye alikuwa ndiye muhimili wa karibia ukoo wao mzima.Kwa heshima ya Aneth ilibidi Ahmed ashushe pumzi kidogo,akamuangalia Yusrath aliyekuwa mezani bado analia,akamgeukia George Charles na kutoka nje,staili aliyotoka nayo ilitisha sababu alimpiga kikumbo kikali George Charles akayumba, kidogo adondoke,akaubamiza mlango kwa nguvu na kuanza kupiga hatua kwa haraka, akielekea nje,wafanyakazi wote wa ofisi hiyo walibaki kumshangaa,Aneth nayeye hakuwa mbali alikuwa nyuma nyuma anatembea,alitamani kumuongelesha Ahmed lakini alishindwa, akihofia angeweza hata kupigwa makofi kutokana na hasira chafu za mwanaume huyu,Ahmed.

********
Kishingo upande ilibidi Ahmed akubali Yusrath afanye kazi kwa George Charles,hayakuwa kwa mapenzi yake lakini hakuwa na namna nyingine ya kubadilisha kitu hiko,kwa kuwa alimpenda Yusrath hakuwa na jinsi,kila kitu alikiacha kama kilivyo lakini akimsisitiza Yusrath kwamba anampenda sana na anafanya hayo yote kutokana na wivu wa mapenzi juu yake!Hata hivyo Yusrath alimsamehee na kila kitu akakisahau kabisa akakubali wagange yajayo,kilichomfurahisha zaidi ni kitendo cha Ahmed kukubali afanye kazi.
“Najua umeniruhusu kishingo upande Mme wangu,lakini nikuhakikishie Ahmed wangu.George sio mtu wangu,niamini mimi.Sio kama unavyonifikiria”
“Sawa naelewa lak…”
“Lakini nini Baby?Lakini nini?Nakupenda Ahmed,nafanya hivi kwa ajili yetu.Sipendi kuja kuwa mzigo kwako,nataka tufanye maendeleo Mme wangu!Ukinikataza mimi kufanya kazi,haimaanishi siwezi kuchepuka ama kuwa na mwanamme mwingine pembeni,mimi ninajiheshimu.Naelewa nachokifanya”
“Ndio Honey lakini mimi nina wivu”
“Hilo naelewa tangu siku nyingi,punguza”
“Nitajitahidi”
“Sio utajitahidi,usikubali upelekwe na hisia.Wewe ni msomi,usikurupuke”
“Basi yaishe”
“Acha nimalize kwanza,nataka kukwambia ukweli.Jirekebishe mme wangu”
“Nitafanya hivyo”
“Neno lingine,nakupenda sana!Nimechoka kuishi mwenyewe,nimechoka kulala mwenyewe kitandani”
“Una maana gani love?”
“Nataka unioe”
“Upo tayari lini?”
“Siku yoyote ile”
Kwa Ahmed ilikuwa ni kama ndoto ya mchana,hakutaka kuamini kama Yusrath amekubali kirahisi namna hiyo wakati hapo nyuma alikuwa analilia kutimiza ndoto zake kwanza,hiyo kidogo haikumuingia Ahmed akilini.
“Baby,si umesema mpaka utimize ndoto zako?”
Ahmed,akatupa swali.
“Ndio,sasa umekubali nifanye kazi.Nitatimiza ndoto zangu nikiwa nawewe”
“Sawa Darling,nakupenda sana!Ahsante kwa kila kitu”
Moyo wa Ahmed siku hiyo ulilipuka kama bomu la ‘Nuclear’ furaha yake ikazidi mara mia yake,hakutaka kufanya kitu kingine zaidi ya kumpigia simu rafiki yake kipenzi Benjamin Patrick Ngowi,akampasha habari juu ya kila kitu kilivyokwenda lakini kabla ya hapo akamgusia kwanza kuhusu kumvalisha Yusrath pete ya uchumba.
“Kwahiyo unataka kumvalisha kwanza pete?”
“Hilo jibu,uliza swali”
“Liini?”
“Siku yoyote ile”
“Kwanini usifanye iwe siku ya Valentine Day,mwezi ujao”
“Ebwana eeh,bonge la idea.Ngoja,niandae mambo sasa!Inabidi tukutane,tupange bajeti”
“Tatizo lako Ahmed una mcheche,ebu tuliza kwanza akili.Bado tuna mwezi mzima”
“Lakini kitu kimoja,nataka kum surprise usimwambie”
“Usijali,tuliza akili.Tupange kitu,kiwe kikubwa bwanaa.Usikurupuke navyokujua wewe,utamwambia”
“Siwezi,nakuaminia bwana mipango miji”

*****
“Noo George,nishakwambia siwezi.Tushafanya kosa,tusiendeleze!Wewe ni bosi wangu.Fanya kama hatujawahi kufanya kitu chochote kile,yalitokea siku ile sahau”
“No please bu…”
“Kuwa mwelewa,I have a Man,soon atanioa!Mimi naumia sana,kufanya kile kitendo.So please kama unataka niendelee kufanya kazi hapa kwako, naomba uziache hizo habari”
“Nisikilize…”
“Naomba unielewe bosi,ukiendelea kunigasi hivi.I swear,nitaacha kazi.I feel guilty kukuangalia usoni,sijui unanichukuliaje right now”
Yalikuwa ni malumbano kati ya Yusrath na George Charles,ofisini.Namna walivyokaribiana iliogopesha, kama angetokea Ahmed na kuwakuta angem-meza mtu mzimamzima bila kumpika.Mazungumzo yao yalikuwa ni mazito mno kwa watu kama hao kuyajadili.Yusrath alijihisi ni mkosaji mbele ya Ahmed,alijuta kuliko siku zote zile,kumvulia nguo yake ya ndani George Charles akauona mwili wake,kosa hilo lilikuwa la jinai.
Siku ambayo alipigwa na Ahmed kwenye mgahawa ndiyo siku aliyoingia chumbani kwa George Charles ili kumsihi asimfukuze kazi,hapo ndipo alipojikuta anaingia mpaka chumbani kwake bila breki, kilichofuata huko ndicho kilichomfanya ajute mpaka dakika hiyo.Wakati mwingine alitamani siku zirudi nyuma,abadilishe kila kilichotokea lakini hilo halikuwezekana hata kidogo,maji yalikuwa tayari yameshamwagika ilikuwa ni vigumu kuzoleka.Mbali na kufanya kosa hilo kubwa hakutaka kurudia tena,ndiyo maana akagoma kabisa kushiriki tena ngono na George Charles,alivyoona bosi wake huyo anazidi kumsumbua akasimama kutoka kitini akimwambia kwamba angeacha kazi dakika hiyohiyo.
“Nitakuongeza mshahara”
“Ukiwa una maana gani George?Mimi sio Malaya.Alafu nisikilize,mimi sio kama unavyonichukulia.Nakuheshimu sana,naomba nisikuvunjie heshima yako”
“Kiasi gani niwe nakulipa kila siku,sitaki kukuchezea Yusrath”
“Nina mwanamme,nadhani unamfahamu.Ninampenda sana”
“Kitu gani Yusrath?!I have deep pocket”
Kwa mara ya kwanza George kujigamba kwamba ana pesa nyingi sana,hiyo ilimfamya Yusrath amtizame kwa umakini zaidi.Hakuamini maneno hayo yanatoka kwa George!
“Kumbe Ahmed,alikuwa sawa!Listen,sitaki tena kazi yako.I’m done”
Ilikuwa kama utani vile lakini ndio ukweli,Yusrath akawa amejuwa tayari shabaha za George zilikuwa ni kitu gani,ndiyo maana akachukuwa uamuzi huo wa kuacha kazi,George alivyotaka kumuwahi ikashindikana,huo ndio ukawa mwisho wa Yusrath kufanya kazi katika ofisi hiyo kwani aliamini thamani ya mwili wake ni zaidi ya pesa!

***

Wiki moja ilikatika,kila alipojaribu kuulizwa kuhusu kazi alijibu kwamba alikuwa likizo kumbe alikuwa akitafuta kazi, sehemu nyingine tofauti,haikuwa kazi rahisi kama alivyodhani sababu hakuwa na vyeti,mabosi wengi walimtaka kingono binafsi hakuwa tayari kutoa rushwa hiyo ili apate kazi.Siku zilizidi kwenda akiwa bize sana,siku moja akiwa barabarani baada ya kuzunguka kwa muda mrefu alihisi kizunguzungu kikali sana,ilikuwa kidogo adondoke chini!Isingekuwa kujishika kwenye gari, lililokuwa pembeni yake,wenda angedondoka chini.Hali ya kizunguzungu iliendelea kumkumbuka kila mara,mpaka siku moja alipoamua kwenda hospitalini ili kupima afya,majibu aliyoyapata yalimfanya ahisi kama amepigwa na shoti ya umeme,alikuwa ni mjamzito wa wiki tatu!Alihisi mwili wake unaishiwa nguvu kabisa,kitu cha kwanza kumjia ni sura ya George Charles, ilikuwa ni lazima mimba hiyo ni yake kwani hakushiriki tena na Ahmed tendo hilo kwa muda mrefu,jasho jembamba lilimtoka akashindwa ni kitu gani akifanye,alitamani kuitoa mimba hiyo lakini alivyokumbuka vifo vya marafiki zake,akaogopa sana!Hiyo ilimfanya azidi kutiririkwa na kijasho chembamba hasa alivyomkumbuka Ahmed,hakutaka kumkosa mwanamme huyo,alichokifanya baada ya kutoka hospitalini akanyoosha moja kwa moja mpaka kwa rafiki yake kipenzi,Rhoda Denis.
Jambo alilokuwa nalo kifuani, lilikuwa ni zito sana hivyo alihitaji ushauri.Alivyowasili Mabibo Mwisho,akaanza kutembea kwa miguu mpaka alivyotokea Relini,hapo akakatiza katikati ya vichochoro na kugonga nyumba moja iliyokuwa na geti la grili,baada ya dakika moja ukafunguliwa.
“Heee!Umepotea njia,ama?”
Rhoda Denis,mwanamke wa maji ya kunde aliuliza kwa mshangao!Ilielekea alishtuka kumuona Yusrath mahali hapo.
“Wala sijapotea”
“Kumbe?”
“Nimekufuata wewe,nikaribishe ndani.Maana nimechoka sana”
“Karibu,pitaa”
Yusrath,akazama ndani.Ambapo pembeni kulikuwa na kochi kubwa,akaketi na kushusha pumzi ndefu,hakuelewa aanzie wapi aishie wapi.
“Vipi maandalizi ya harusi,shosti.Usinisahau maana mimi kwenye mambo ya chini ya pua,kwanza inabidi unipe kamati ya chakula na vinywaji”
“Ha! Haa! Haaaa! usijali,Rhoda….”
Yusrath akalazimisha kuweka tabasamu usoni kisha akaita,akakaa vizuri na kumtizama Rhoda kwa umakini.
“Nambie”
“Nina shida hapa,kubwa sana”
“Shida gani?”
“Sijui,nianzie wapi”
“Anza popote,mbona unanitisha tenaa”
“Kifupi nina mimba”
“Mimba?Unachoogopa nini?Hilo ndilo linakutisha?!"
Hapo Rhoda Deniss alitabasamu na kucheka,kwake jambo hilo akalifananisha na kibonzo!Kwa Mwanamke kama Yusrath kuhofia mimba lilimshangaza.
“Sio kama unavyofikiria”
“Mbona sikuelewi?Jamaa si anataka kukuoa kwani tatizo liko wapii?”
“Sio mimba yake”
Kufuatia jibu hilo,Rhoda akabaki kimya anamtizama Yusrath, ilielekea alishtuka kidogo.
“Sio mimba ya bwana harusi?”
“Ndio Rhoda,naogopa sijui nifanye nini.Hapa nimechanganyikiwa.Nataka kuitoa lakini naogopa”
“Usiogope,wala usiitoe”
“Rhoda hiii…”
“Nisikilize,usitoe hiyo mimba…”
“Nisitoeeeeee?!”
“Ndio”
“Sasa nifanye nini?”
“Unampenda jamaa?”
“Jamaa gani?”
“Mumeo mtarajiwa?”
“Ndio”
“Sasa naomba hii iwe siri yetu,usimwambie mtu yoyote Yule.Hivi wewe unadhani peke yako ndio una tatizo kama hilo,mbambikie tu wanawake wengi wanafanya hivyo siku nyingi,asilimia tisini ya wanaume hapa duniani wanalea watoto sio wao,sana sana Tanzania”
“Kivipi?”
“Wewe ni mtoto wa kike,unajua cha kufanya.Chakalika kabla haijawa kubwa,kazi kwako.Chagua moja,kuwa sahihi ama unataka kuwa na amani”
Rhoda Denis,alihitimisha kwa swali.Akimuacha Yusrath njiapanda!

Hakuna siku aliyokuwa katika wakati mgumu kama hiyo,kila kitu katika maisha yake kilivurugika kwa kiasi cha kutosha, akatamani siku zirudi nyuma abadilishe kila kitu kilichotokea lakini jambo hilo lisingeweza kutokea hata siku moja.Mawazo ya Rhoda Deniss yakamuingia akilini kwa asilimia hamsini na moja,licha ya kumsikiliza hakutaka kuyatilia maanani moja kwa moja,ilikuwa ni lazima ahoji mchakato utakavyokwenda.
“Lakini sasa Ahmed akijua?”
Yusrath,akauliza swali maana alizijua fujo za Ahmed kama angegundua mpango huo batili,kifo kingekuwa halali yake maana angepigwa kipigo cha mbwa koko!
“Sasa,atajuaje?”
“Kwa mfano ndio amejua”
“Hakuna cha mfano,hawezi kujua kamwe.Labda wewe ndio umwambie”
“Atanizika mzimamzima,namuelewa yule.Ana hasira,anaweza hata akaninyonga usiku kitandani”
“Sio huyo Ahmed tu,wanaume wote.Lazima utokee mpasuko mkubwa hapo!Ndio maana nakwambia ufanye maamuzi mapema kabisa kabla haijawa too late,umwambie sasa hivi ama kama nilivyokwambia”
“Nimekubali”
“Umekubali nini?”
“Nampenda Ahmed,sitaki kumkosa”
Jibu hilo lilimaanisha kwamba Ahmed,abambikiwe mimba hiyo ailee hakuwa tayari kumkosa kwa njia moja ama nyingine kwani tayari alimpenda kutoka uvunguni mwa moyo wake!Alichosisitiza ni kwamba jambo hilo libaki kuwa siri hiyo,isivuje kwa mtu wa aina yoyote ile.
“Yusrath,usiwe na wasiwasi kabisa!Ondoa shaka,kila kitu kipo sawa.Fanya nilivyokwambia”
Ushauri wa Rhoda Deniss siku hiyo kwake ukawa na maana kubwa sana,akatabasamu na kuingiza mkono kwenye mkoba wake na kutoa noti mbili za shilingi elfu kumi,akamkabidhi Rhoda kama shukrani.Akafungua mlango na kuondoka zake,hakutaka kula chakula chochote isipokuwa ni kuonana na Ahmed siku hiyohiyo, wafanye ngono ili amuuzie mbuzi kwenye gunia,ilikuwa ni lazima mpango huo ufanyike haraka iwezekanavyo!Akiwa ndani ya daladala akaanza kutuma meseji za mapenzi.
“Daaaaaarling….”
Yusrath,akaandika ujumbe huo katika mtandao wa ‘WatsaApp’mbele yake akaweka emoji za kopa kopa nyingi sana,haikuchukuwa hata sekunde mbili Ahmed,akajibu.
“Yes sweartheart”
“Imic you”
“Me too bby”
“Ushakula Mme wangu mie?”
“Nop bado,kuna kazi namalizia hapa bby”
“Mmmh,sio kwamba upo na mwanamke hapo?”
“N’po ofisini Kipenzi,acha wivu”
“Ndio,nitaua mtu Mme wangu”
Yusrath,alianza mazungumzo hayo kwa makusudi ili kumseti vizuri Ahmed,mwanamke huyu alikuwa mjanja kama Sungura,ilikuwa ni lazima atumie akili nyingi sio kukurupuka kama nyumbu, ndiyo maana akaanzia mbali kidogo.
“Wivu tu,uko peke yako baby wangu”
“Alf lv…”
“Yes bby…”
“Naona aibu kukwambia bby…..”
Yusrath alivyotuma meseji hiyo akaweka kiemoji cha ngedere kimeweka mikono machoni.
“Darling niambie,mimi ni mmeo”
“Nimemmic Ahmed mdogo………”
Baada ya kutuma meseji hiyo akaweka Emoji nyingine ya kutia huruma,kwa akili ya Ahmed akajua nini kinachotaka kufanyika,hakuchelewa hapohapo akapanda hewani.Kwa Yusrath akaamini tayari mtego wake umefanya kazi,kwa kuwa alikuwa kwenye siti ya mwisho kwenye daladala, alivyopokea simu tu,akaanza kuongea kwa sauti ya mahaba,hiyo ilimfanya Ahmed ashindwe kuvumilia!Hata yeye damu yake ilimwenda mbio mno kwani tendo hilo hakulifanya siku nyingi, kutokana na ubize aliokuwa nao Yusrath.
“Bebiiii please,leo nakuomba.Siwezi kulalaa hiviii,natesekaaaa aaaah”
“Okay love,nitachelewa kutoka lakini, tuna kikao cha bodi leo”
“Nitakusubiri mme wangu”
“Sawa mke wangu,tutawasiliana”
“Okay baby,ilove you”
“Ilove you too”
Tayari Yusrath akawa amemjaza Ahmed kingi,kazi ilikuwa kwake kucheza kama Ronaldo, alichokifanya ni kuanza kufikiria ni hoteli gani nzuri naya kisasa ambayo angeweza kulala na Ahmed wafanye tendo hilo kisha baadaye apewe mzigo huo wa mimba ailee, aliamini kivyovyote vile mpango aliosuka, Ahmed asingeweza kuchomoka,japokuwa alihisi moyo wake kuuma.
Akakumbuka kwamba kuna hoteli moja aliwahi kuiona karibu na Ubungo Maziwa,hiyo ilimaanisha aende na kujua bei kisha kutoa pesa ili baadaye alale na Ahmed, kifupi kila kitu alikipanga kiakili sana,alivyofika Shekilango akashuka na kuchukua pikipiki iliyompeleka mpaka Ubungo Terminal,alivyoshuka akamkabidhi ujira dereva wa pikipiki,mbele yake kushoto kulikuwa na hoteli ya rangi ya machungwa,akatembea taratibu mpaka nje ya gorofa hilo.Akatizama huku na kule na kuingia ndani!
“Dada habari”
“Nzuri za kwako?”
“Vyumba vipo?”
“Yes vipo,kuna vya thelathini na tano arobaini na Hamsini”
“Vipoje hivyo?”
Dada wa mapokezi,akaanza kuelezea sifa za vyumba hivyo na bei zake.Chumba alichokitaka Yusrath, kilikuwa cha shilingi elfu hamsini,akaomba aoneshwe!Wakapanda ngazi mpaka gorofa namba tatu,ambapo huko chumba kilifunguliwa.Kilikuwa ni kikubwa cha kuvutia,kilichompagawisha zaidi ni aina ya bafu la jakuzi yaani sink kubwa la kuingia ndani na kuoga ndani kwa ndani,akaanza kupiga picha atakavyooga na Ahmed ndani ya jakuzi hilo.
“Nahitaji hiki hiki”
“Sawa”
“Hii tv inawaka,Ac pia?”
“Vyote vinafanya kazi”
“Sawa Ahsante”
“Unalipia sasa hivi,ama utakuja baadaye?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Dada wa mapokezi.
“Nalipia sasa hivi”
“Twende mapokezi”
Hakuwa mwenye sababu yoyote ile ya kurudi nyumbani kwao kwani hakuwa na kitu chochote kile cha kufanya,alivyolipia akakabidhiwa kadi maalum ya kufungua mlango!Alivyoingia tu ndani,akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine,akajitupa kitandani na kulala hapohapo!Kutokana na uchovu mwingi aliokuwa nao,usingizi haukumchelewesha ukamchota akalala fofofo!

*****
Maisha yake hayakutofautishwa na peponi,Kila kitu alichokitaka alikipata kutoka kwa Dokta Sajo!Maumivu aliyoyapata huko nyuma, yakageuka na kuwa historia tu katika maisha yake.Jiji la Afrika Kusini lilimpenda,likamfanya anawiri.Ngozi yake ikarudi na kuwa nyororo zaidi na hayo Dokta Sajo alijua kumgharamia,alijua kumkarabati.Hajrath hakutofautishwa na gari inayofanyiwa ‘service’ kila baada ya mwezi mmoja kwani ilikuwa kila baada ya wiki tatu ni lazima Dokta Sajo arudi na mifuko ya nguo,manukato na mafuta ya kisasa kumaanisha kwamba vya zamani viwekwe kando.Moyo wa Hajrath,ukafa ukaoza kwa Dokta Sajo!Kunenepa kwake na kunawiri kwa Hajrath,hakukumuacha Mwanamme yoyote yule salama kila mtu alimmezea mate,akatamani japo apewe penzi kwa usiku mmoja tu lakini hakuna yoyote kati yao aliyefanikiwa!
“Kwanini,hatukujuana mapema?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Hajrath,siku hiyo akiwa ameletewa mfuko wa zawadi kutoka kwa Dokta Sajo.
“Kila jambo na wakati wake.Tungejuana mapema wenda,tusingefika hapa!”
“Naamini hivyo”
Siku hiyo Hajrath akawa ana kazi ya kujaribu nguo,ikitoka ile inaingia hii.Akibadili hii anachukuwa ile.Dokta Sajo akiwa kitandani alikuwa akimuangalia,nguo zote zililetwa siku hiyo zilimkaa Hajrath mwilini kisawasawa,nguo zilimchonga na kilichofanya nguo hizo zimkae vizuri ni kutokana na umbo lake nambari nane na nyuma alikuwa ‘Mashallah’ Mungu kamjaalia.Baada ya kujaribisha nguo ya mwisho,Dokta Sajo akasimama na kumuendea akamshika kiuno kwa nyuma, wote wakawa wanajiangalia kwenye kioo kikubwa kilichokuwa mbele yao.
“Tumependezana sana”
Hajrath,alisema akageuka na kumtizama Dokta Sajo!
“Mmmh mhhh”
Dokta Sajo alijibu lakini alishindwa kutoa sauti sababu mdomo tayari ulikuwa umemezwa,wakaanza kunyonyana ndimi.Dokta Sajo akatupwa kitandani,alichokifanya Hajrath ni kutoa nguo moja baada ya nyingine akapanda kitandani,akamsogelea karibu dokta Sajo.Kilichofuata hapo,ni kitendo ambacho watoto waliokuwa na umri wa chini ya miaka kumi na minane,hawaruhusiwi kutizama!

*****
Saa kumi na moja jioni,alikurupuka kutoka kitandani.Muda ulikuwa umekwenda kwelikweli na alikiri kwamba alilala sana siku hiyo,alivyoangalia simu yake.Akakuta ‘missed calls’ ishirini, nyingi zilitoka kwa Ahmed,meseji zilikuwa hazina idadi huyo pia alikuwa ni Ahmed,hapohapo akamtafuta hewani akamwambia yupo hotelini tayari na alipitiwa na usingizi,akahitimisha kwa kuomba msamahaa!Halikuwa tatizo kubwa sana,siku hiyo Ahmed alitakiwa kuhudhuria kwenye kikao,hivyo kwenye saa kumi na mbili angekuwa tayari ametoka kazini.
“Alafu baby,kuna kitu nataka kukwambia”
Yusrath,alisema simuni.Alitaka kumwambia Ahmed habari za George Charles alivyomtongoza akamkatalia.
“Kitu gani hiko love?”
“Wewe njoo”
“Nitakuja,nitachelewa lakini”
“Kwanini?”
“Foleni,kutoka jioni huku jam inakuwa kubwa”
“Utachukuwa pikipiki nitakulipia”
“Kwani upo wapi?”
“Ubungo Maziwa hapa Golden Palm Hotel”
“Nikitoka,nitakwambia Baby”
Hayo ndiyo yalikuwa mazungumzo yao,baada ya hapo Yusrath akavua nguo zake zote na kuingia moja kwa moja bafuni, huko akaoga vizuri na kunyoosha mpaka kwenye simu ya mezani.
“Chumba namba 103,kuna nini jikoni?”
“Ugali Kuku,nyama choma!Wali kuku,wali Maharage”
Upande wa pili wa simu ukajibu,kutoka jikoni Yusrath akatafakari kidogo!
“Ugali Kuku,itachukuwa muda gani?Na maji ya kunywa”
“Nusu saa”
“Okay”
Yusrath akakata simu,ni kweli.Hoteli hiyo walikuwa makini sana,ndani ya nusu saa akawa ameletewa msosi tayari.Akanawa na kuanza kula,akiwa amevaa taulo moja pekee,amejiachia kihasara hasara,vitu vingi sana vilimiminika ndani ya kichwa chake!Alimfikiria Ahmed na kitendo anachoenda kukifanya.
Alivyomaliza kula akanawa na kunywa maji,mpaka hapo akawa ameshiba mpaka mwisho,akatulia kidogo na kuwasha t.v ili apoteze muda.Ilivyogonga saa moja juu ya alama simu yake ikaanza kuita,akajua ni lazima atakuwa ni Ahmed.Ni kweli,alikuwa ni kama ametabiri vile kwani mpigaji alikuwa ni Ahmed,akapokea na kuanza kuongea kwa sauti ya mahaba.
“Chukua pikipiki Darling,nitakulipia”
“Usijali,nakuja.Hiyo pesa ya Pikipiki unayotaka kunilipia,weka mfukoni baby”
“Sawa love,take care.Nipo hapa Golden Palm hotel, room no103 Ubungo maziwa”
Mcheche aliokuwa nao Yusrath,haukuwa wa kawaida hata kidogo!Mbali na kutaka kutimiza jambo alilolipanga,alikuwa na hamu ya kufanya ngono,damu ikaanza kumuendea mbio.Akatamani Ahmed afike sekunde hiyohiyo,mpaka hapo akawa hatulii mara akae mara asimame,ili mradi moja haikai mbili haikai!Ndani ya dakika 45,simu ya mezani ikaita.Alivyopokea akaambiwa kwamba ana mgeni wake anaitwa Ahmed.
“Mruhusu apite”
Hazikupita hata sekunde saba,mlango wa chumba chake ukagongwa,akajua tayari mambo yameiva,akaweka taulo vizuri.Akalipandisha juu kifuani huku chini mapaja yake yakawa nusu nje,akafungua mlango.Akalegeza macho yake na kumkaribisha Ahmed!
“Karibu baby”
Ilikuwa ni sauti moja laini,iliyotoka kwa Yusrath.Ahmed akasisimka mwili,akaingia mzimamzima mlango ukafungwa,hali aliyokuwa nayo Yusrath na jinsi alivyovalia haikumfanya Ahmed aulize mara mbilimbili,akamvaa hapohapo na kuanza kumnyonya mdomo,kwa kuwa Yusrath alikuwa ana taulo peke yake hana kitu chochote ndani, ilikuwa rahisi kwake kuanza kumtomasa kila sehemu ya mwili wake,akianzia kifuani,shingoni mpaka kwenye ikulu.Mambo hayakuwa mazuri kwa Yusrath lakini pili akili yake haikuwa hapo,alitaka Ahmed aanze mara moja.Alichokifanya ni kuanza kumvua Ahmed shati,akamvua mkanda na kuitoa suruali yake,hakuishia hapo.Akaivuta boxa!Nyoka wa Ahmed alikuwa amesimama dede tayari,tofauti na siku zote huwa wanaandana kwa takribani dakika kumi,siku hiyo Yusrath alipanda juu harakaharaka na kukaa juu ya tango, hapohapo akaanza kukinyonga kiuno chake akainama kidogo na kuanza kumpiga denda Ahmed,kasi iliendelea hawakuchukuwa dakika nyingi Ahmed akawa tayari amefika mshindo,Yusrath akatabasamu akajua tayari jambo lake limetimia.Licha ya yote hayo waliongea mambo mengi sana siku hiyo na kila mtu alikiri, kumpenda mwenzake.
“Nakupenda Ahmed,katika maisha yangu.Sitokuja kukusaliti hata siku moja,nitakutunzia tunda lako!Mimi nawewe mpaka kifo”
Yusrath alizungumza kwa hisia kali sana huku akimtizama Ahmed kwa macho ya huba,wakahaidiana vitu chungu mzima!Kuhusu swala lao la ndoa pia,siku hiyo waliondoka hotelini hapo saa nne ya usiku!Walitumia Bajaj moja,Yusrath akashuka Ilala.Ahmed akawa amebakia kwenye bajaj!
“Baby kesho,ilove you”
Yusrath aliaga.
“Ilove you too Darling,nikifika nitakutumia meseji”
“Okay Darling”
Bajaj ikawashwa,Yusrath akabaki anaitizama kwa macho mpaka ikapotelea gizani,akagonga geti likafunguliwa na mlinzi kisha kuingia ndani,kwa kuwa wazazi wake walisafiri hakuwa mwenye wasiwasi wowote ule.Alivyoingia seblen,akala chakula,akaingia bafuni kuoga na kupitiliza moja kwa moja, kitandani.Hapo akaanza kuchat na Ahmed.
“Ndio nimefika,nakaribia kufika home Darling,nime enjoy”
“Hata mimi Mpenzi wangu”
“Reaaal?”
“Yeah…”
Baada ya kutuma meseji hiyo,ghafla sura ya Rhoda Denis ikamjia kichwani,akaweka simu yake ili amtumie meseji ya kumshukuru.
Kwa haraka akaanza kuandika ‘Ahsante sana Rhoda,tayari sasa mambo yako poa!Ahmed lazima atajua mimba ni yake,nimetoka kufanya naye mapenzi muda sio mrefu.Kuna zawadi yako lazima nikupe best’ baada ya kuandika hivyo akatuma ujumbe huo.
“Haaaaaa!”Akapiga yowe la nguvu kwa sauti.
Butwaa alilopigwa Yusrath,halikuwa na mfano wake, moyo wake ukapiga kwa nguvu kwa mshtuko!Baada ya kugundua meseji hiyo, imeenda kwa Ahmed sio kwa Rhoda na mbaya zaidi, ikaonesha kwamba imefika tayari.


Yusrath Suleiman alichanganyikiwa kwa kiasi cha kutosha,mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu akatamani apae na kuzuia meseji lakini jambo hilo lisingewezekana,ukweli ni kwamba meseji ilikuwa tayari imeenda,akaingia tena kwenye simu yake ili kuhakikisha kama ni kweli alikosea na kumtumia Ahmed,akakuta ni kweli!Akashusha pumzi ndefu na nzito huku akiwa na wasiwasi mkubwa,alishajua nini maana yake baada ya Ahmed kuipata meseji hiyo.Hakuelewa sura yake,angeiweka wapi. Wakati mwingine alitamani ardhi ipasuke aingie ndani imfunike ili akimbie aibu,alivyowakumbuka wazazi wake akaumia zaidi,ilikuwa ni lazima ndoa isitishwe na Ahmed atoe sababu ya jambo hilo.Alivyofikiria hayo,akazidi kuumia moyo.Lawama zote, akamtupia Rhoda Deniss kwa ushauri aliompa,akiwa katikati ya mawazo hayo, simu yake ikamshtua iliyokuwa kitandani,mapigo yake ya moyo yakazidi kwenda mbio,akajua ni lazima atakuwa Ahmed na endapo angepokea angekumbana na maswali mazito mno,taratibu akapeleka mkono wake na kuchukua simu, alivyoangalia kwenye kioo akahema ndani kwa ndani, baada ya kugundua simu inatoka kwa rafiki yake Rehema Mponzi,hakutaka kuipokea akarudi tena kwenye mawazo!Simu ikaita na kukatika,bado alikuwa akitafakari ni kitu gani angemjibu Ahmed amuelewe,sio siri siku hiyo alikuwa katika wakati mgumu kuliko kawaida,alivyomkumbuka George Charles, akahisi kichefu chefu cha kutapika,akayakumbuka maneno ya Ahmed ya kwamba mwanamme huyo ni lazima alikuwa anamtaka kingono tu na wala sio kitu kingine,muda ulizidi kwenda akisubiria simu iite kwani alijua ni lazima Ahmed angempigia tu na kuanza kumuhoji maswali yasiyokuwa na idadi kamili.
Akaanza kujipanga mwenyewe ni kitu gani angemjibu,hapo hapo akapata wazo na kumpigia simu Rhoda Denis ili aombe ushauri wa kitu gani akifanye,matokeo yake simu ya Rhoda haikuwa hewani, akaishiwa pozi hakuelewa ni kitu gani akifanye kingine,akatamani hata Ahmed atume meseji lakini hakutumiwa,akataka mwenyewe ampigie lakini moyo wake ukampiga ‘Stop’ asifanye hivyo kwani angeharibu kila kitu,ilikuwa ni lazima kwanza Ahmed aanze kumpigia simu yeye.
Usiku huo ikawa subiri,subiri nawewe lakini simu haikupigwa, wala hakutumiwa meseji ya aina yoyote ile,siku hiyo usingizi ulikuwa ni kitu hadimu kupatikana, hata alivyolala ulikuwa ni usingizi wa mang’amung’amu!Kulivyopambazuka tu,moja kwa moja akaenda kushika simu yake ili akutane na meseji za Ahmed lakini wapi,haikuwa hivyo!Hapo ndipo kijasho chembamba kilianza kumtoka,Ahmed hakuwa mwanamme wa kukaa kimya katika jambo kama hilo zito,alikuwa ni mwanamme mwenye hasira na wivu,mkorofi hapendi kunyanyaswa.Iweje jambo hilo limfanye akae kimya?Hayo ndiyo maswali aliyokuwa anajiuliza Yusrath kichwani.
“Sijui nifanye nini?”
Yusrath,akabaki na maswali hayo kichwani!Jambo hilo, lilimuumiza ndani kwa ndani, akashindwa kunywa chai kwa amani. Muda wote macho yake yalikuwa kwenye simu ya mkononi.Alivyorudi chumbani kwake, akamtafuta tena Rhoda Denis ili ampe ushauri wa jambo gani alifanye,akatabasamu kidogo na kufarijika baada ya kusikia simu hiyo inaita.
“Rhodaa”
Ilivyopokelewa tu,Yusrath akaita jina.
“Halloo Yusrath,vipi ulifanikiwa?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Roda Denis.
“Rhoda,nina matatizo rafiki yangu”
“Nini tena?Una shida gani?”
“Kuna meseji nilitaka kukutumia wewe,nikamtumia Ahmed”
“Meseji gani?”
“Ngoja nakufowadie sasa hivi”
Hapo alichokifanya Yusrath ni kutoa simu sikioni na kuanza kubonyeza bonyeza, akaituma kama ilivyo kwa Rhoda.
“Umeona?”
“Subiri,bado haijafika”
Sekunde mbili baadaye Rhoda Denis,akawa anasoma ujumbe huo!Hata yeye mapigo yake ya moyo yalimwenda mbio lakini ilikuwa ni lazima amshauri rafiki yake ni kitu gani akifanye.
“Yusrath,nimeona meseji”
“Ndio,naomba nisaidie nifanye nini”
“Hiyo meseji ulituma lini?”
“Jana usiku”
“Ikawaje,alikupigia?”
“Hapana”
“Meseji alikutumia?”
“Hapana”
“Sasa,usifanye chochote!Wala usimpigie,acha akupigie yeye kwanza”
“Hata mimi ndio nilikuwa nafikiria kufanya hivyo”
“Subiri mpaka kesho,asipokupigia nitajua cha kufanya”
“Kweli?Kwahiyo sasa?”
“Yusrath,Relax!Najua una presha lakini tulia,fanya shughuli zako kama kawaida.Sawa?”
“Sawa,sasa akipiga?”
“Pokea”
“No,siwezi!Please Rhoda,nitamjibu nini?”
“Ngoja,nifikirie cha kufanya.Lakini naomba usipaniki,ukipaniki utaharibu kila kitu”
Yusrath akaitikiwa kishingo upande huku roho ikimuuma ajabu,hakutaka hata siku moja ampoteze Ahmed sababu kwake ilikuwa ni sawa na kula Ng’ombe mzima lakini kabakisha mkia kwa maana kwamba ndoa ilikuwa ukingoni kufanyika,hakutaka aibu hiyo imtokee hata kidogo!
Kwake siku hiyo, ilikuwa ni ngumu kusogea,mshale wa dakika ulikuwa unasogea kwa taratibu mno,hakutulia wala hakwenda sehemu yoyote, alikuwa akizunguka huku na kule akisubiri simu ya Ahmed iite.Jioni ya siku hiyo, uzalendo ukamshinda akasema ‘Liwalo na liwe’hakutaka kuendelea kubaki katika hali ya namna hiyo,akapiga moyo konde na kuanza kutafuta namba ya Ahmed simuni,alivyotaka kupiga moyo ukasita sababu hakujipanga na maswali ya Ahmed,akaweka simu chini na kuanza kutafakari.
“Nitamwambia simu sikuwa nayo mimi”
Akajaribu kutunga uwongo lakini akagundua porojo hizo zilikuwa za kitoto,na Ahmed hakuwa fala kama wanaume wengine.Ilikuwa ni lazima amuingie na hoja nzito sana,kwa ujasiri bila kutafakari kitu kingine zaidi, akapiga simu na kuiweka sikioni.
“Griii griiiii”
Upande wa pili wa simu ulisikika kumaanisha simu ya Ahmed ipo hewani,mapigo ya moyo ya Yusrath yalidunda kwa nguvu kama kitenesi huku kijasho chembamba, kikimtoka.
“Hallooo!”
Ahmed ukapokea simu,moyo wa Yusrath ukapiga paa!Akapata kigugumizi cha ghafla na kushindwa kuongea!

******
Muda wote alikuwa mwenye furaha,akitabasamu mwenyewe akiamini ya kwamba Yusrath ndiye mwanamke wa maisha yake,kumaanisha ya kuwa yeye na Yusrath mpaka kifo!Haikuwa rahisi kwa binadamu kuwatenganisha, hivyo ndivyo Ahmed alivyoamini siku zote,alikuwa yupo tayari kwa lolote lile isitoshe alimuamini ndiyo maana hata alivyokuwa anafanya naye ngono, alienda pekupeku bila ndala yaani nyama kwa nyama,hiyo ilitosha kudhihirisha asilimia mia moja, yupo tayari kwa lolote lile,alikuwa akiwaza mengi na kutafakari vitu chungu mzima akiwa ndani ya bajaj baada ya Yusrath kushuka nyumbani kwao,Ilala.Picha mbalimbali zilikuwa zinampitia kichwani kwake usiku huo,hususani walivyokuwa kitandani wapo uchi wa mnyama, wanashiriki tendo la ndoa!Akaona haitoshi akaanza kuchat na Yusrath,akajihisi ni mwenye bahati sana kupendwa na Mwanamke mzuri kama Yusrath.Hakutaka kuliweka hilo ndani ya moyo wake,akaanza kuchat naye akimsifu kwamba yeye ni fundi kitandani,waliendelea kuchat hivyo akiwa ndani ya Bajaj, usiku huo!Walivyofika Manzese,Tiptop bajaj ikasimama kwani kulikuwa na foleni ndogo.
“Foleni sasa hivi usiku,inakuwaje?”
Ahmed akamuuliza dereva huku akiwa ameshika simu yake, kihasara hasara.
“Kutakuwa kuna ajali mbele lakini inasogea”
“Poa”
Ahmed akaachana na hilo,akazidi kuchat na Yusrath wake.Kuna meseji ndefu iliingia kutoka kwa Yusrath,akakaa sawa alivyoifungua tu na kuanza kuisoma,akashtukia amepigwa kibao kikali cha uso kupitia dirishani,ndani ya sekunde sifuri simu ikakwapuliwa na kibaka mwingine.Akiwa mwenye maumivu ya kibao cha uso anaona nyota,akachungulia nje ya bajaj na kuona mateja wawili wanakimbia upande wa pili wa barabara.
“Dereva,simamisha bajaj.Nimeibiiiwaaaa”
Ahmed akaachia kelele kali akimwambia dereva.
“Umeibiwa nini?”
“Simu”
“Saa ngapi?”
“Simamisha bajaj”
Kabla ya Bajaj kusimama,Ahmed akaruka kama swala na kuanza kukimbilia upande wa pili alipowaona mateja,hakuogopa chochote!Moyo ulimuuma kwa kitendo hicho kilichotokea,akazidi kuelekea gizani lakini hakukuwa na dalili ya aina yoyote ile ya mateja hao kuonekana,akarudi kwenye bajaji, akiwa anahema.
“Umewapata?”
“Alafu acha ufala,au umekula nao njama!Nirudishieni simu yangu”
“Siwezi kukufanyia hivyo kaka”
“Wewe boya nipe simu yangu”
Tayari Ahmed,akashikwa na hasira akamkunja shati dereva wa bajaj akamtingisha tingisha,kutokana na mwili wa dereva huyo kuwa kimbaombao hakuweza kufurukuta.
“Kaka niachie,mimi wale siwajui.Unanionea tu”
“Unawajua”
“Siwajui”
Walioamua ugomvi huo ni wapita njia,ambapo waliwagombelezea.Hiyo ilifanya Ahmed atafute bodaboda, mpaka nyumbani kwao akiwa na mawazo tele kichwani kwake!Mawazo yalikuwa mengi sana,akatafakari namna ya kununua simu mpya na kusajili laini nyingine siku inayofuata,hakukaa kwa raha kabisa mawazo yalitawala kichwani kwake,siku hiyo alikuwa mnyonge akamuhadithia mpaka mama yake jinsi ilivyokuwa,Mama akatabasamu kidogo na kusikitika kwa mbali,akachukulia hiyo kama changamoto.
“Ulivyoambiwa kuwa uyaone sio kushangaa magorofa,ndio ukubwa huo”
Mama,akatia neno huku akicheka lakini ki ukweli aliumia moyo pia.
“Nitaongea na Baba yako,ama nina pesa kidogo nitakupa uongezee, ukanunue simu nyingine”
Ahmed alionekana kuchoka na mwenye mawazo tani zaidi ya elfu moja kichwani kwake,vitu vingi sana vilikuwa ndani ya simu yake.Alivyoingia kitandani bado alitafakari,alizoea kuzungumza na Yusrath usiku, kifupi usiku huo kwake ungekuwa kama mwaka mzima,alijigeuza geuza kitandani bila kuupata usingizi.Kulivyopambazuka tu,akaanza kujiandaa lakini kabla ya kutoka nje ya mlango, mama yake alimuita.
“Mama shikamoo”
“Marahaba”
Mama akasogea mpaka karibu,alimpenda sana mwanaye!Akaangalia huku na kule na kumfinyangia noti za pesa mkononi.
“Usimwambie baba yako kama nimekupa”
“Ahsante Mama”
“Akikuuliza mwambie sijakupa pesa yoyote,nimemwambia umeporwa simu”
“Ahsante Mama,ubarikiwe sana”
“Aya Baba angu,kazi njema”
Ahmed akaondoka akiwa mwenye furaha tele moyoni,akafika kituo cha daladala na kupanda basi la Posta.Kutokana na msongamano wa watu, ndani ya basi hakuweza kuhesabu pesa hizo ni shilingi ngapi.Saa tatu kamili akawasili kazini,akanyoosha mpaka ofisini kwake.Huko ndipo alipata muda wa kuhesabu,moyoni alijawa na furaha kwani zilikuwa ni laki mbili na hamsini.Akapiga hesabu za harakaharaka, kwenye akaunti yake,ilikuwa ni lazima aongezee naza kwake baadaye ili anunue simu kisha baadaye asajili laini.
Kutokana na kazi alizokuta mezani, jambo hilo asingeweza kulifanya kwa wakati huo,kwake ilikuwa kazi kwanza.Ilivyogonga saa kumi juu ya alama akaingia kwenye moja ya ATM, zilizokuwa jirani na kuchota pesa,akanyoosha moja kwa moja kwenye duka la simu.
Jambo alilokuwa analifanya lilikuwa ni kinyume na ndoto zake,pesa alizokuwa amehifadhi zilikuwa zina mipango mingine na sio kununua simu,kifupi akawa amerudishwa nyuma kwa hatua tano.Alivyonunua simu akatoka na kunyoosha makao makuu ya mtandao!Hapo alijielezea na kutoa kitambulisho chake,haikuwa kazi ngumu ndani ya dakika chache laini yake ikawa hewani,kitendo cha kuiweka kwenye simu!Hapohapo ikaita,akapokea.
“Hallooo”
Bado hakujua ni nani anapiga ingawa alikuwa anahisi ni Yusrath,namba ziliingia bila jina!Kilichomfanya ahisi ni Yusrath ni tarakimu za mwisho za namba hizo zinazoishia na 009.
“Baby,mambo”
Kitendo cha kuzungumza hivyo,moja kwa moja akajua ni Yusrath.Kitu alichokosea Ahmed ni kuanza kuomba msamahaa kwa kutokumtafuta Yusrath hewani kwa takribani siku nzima,akaanza kuomba msamahaa akajielezea kila kitu kilivyotokea kinagaubaga.
“Kwani hakuna simu nyingine Ahmed?”
Yusrath,akatumia mwanya huo kujifanya kukasirika, alifanya hivyo kwa makusudi ili kupima kina cha maji!
“Nilichanganyikiwa”
“Kwahiyo?Ukanisahau hadi mimi,eti?”
“Sina maana hiyo mke wangu”
“Ila?”
“Nililibiwa simu”
“Kwani hapo ndani,hakuna mwenye simu?Kassim simu anayo.Simu unazo,Ahmed hunipendii”
Alichokuwa anafanya Yusrath ni kutingisha kiberiti ni kweli akagundua kwamba hakina njiti,akazidi kufoka mwisho akakata simu!Akijua ni lazima Ahmed angepiga,hicho ndicho kilichofanyika kwani Ahmed alipiga simu akiomba msamahaa japokuwa hakustahili kufanya hivyo.Yusrath akapata uhakika tayari kwamba meseji hiyo haikusomwa,akamshukuru sana Mungu akiamini ni lazima alimtumia kibaka huyo kupora simu.
Penzi lao,likachipua tena kwa mara nyingine!Ahmed akawa hapindui tena kwa Yusrath,ilikuwa kitu kidogo tu lazima Yusrarth aulizwe kwanza na kutoa ruksa.Penzi lao kila siku likaonekana kama ni jipya vile,siku zilisogea kwa kasi ya ajabu sana!Baada ya mwezi mmoja na nusu kukatika ndipo Yusrath akaamua kufunguka na kumwambia Ahmed kwamba ana mimba yake.
“Unasema kweli?”
Ahmed akauliza kama mtu asiyeamini kile anachoambiwa.
“Ndio,nina mimba Ahmed”
“Ya nani?”
“Are you serious?Na swali lako”
“Sina maana hiyo baby,yaani mambo yamekuja ghafla”
“Ghafla kivipi?Ahmed sikuelewi ujuwe”
Yusrath,akapaza sauti kidogo.
“Sasa itakuaje?”
“Ahmed,unaniuliza itakuwajeee?Hivi,unajisikia.Itakuaje?Nitakuja kwenu kuwaambia wazazi wako.Ndivyo itakavyokuwa”
“Tutaongea mke wangu,usijali kuhusu hilo!Sawa mamii”
Ahmed,hakuonekana mwenye furaha hata kidogo hakuelewa ni kwanini hali hiyo imejitokeza!Siku hiyohiyo baada ya mazungumzo hayo kumalizika,akampigia simu rafiki yake wa karibu Mr.Benjamin Patrick Ngowi,akamueleza kila kitu kilichotokea.
“Kwahiyo mtoto ana kibendi?”
“Yes broo!”
“Home wanajua?”
“Hapana”
“Wasijue kwanza,sikilizia.Cha kufanya kama tulivyoongea mpige pete ya uchumba mengine yatafuata baadaye”
“Poa,hiyo sekta nakuachia wewe.Nakuelewa,wewe ni mtoto wa mjini.Downtown kitambo”
“Sawa,ahsante kwa kunipa heshima hiyo,cha msingi usimueleze chochote kile”
Hiyo ndiyo mipango waliyofanya wawili hawa,kilichofanyika jambo hilo lilianza chini kwa chini.
Walitaka kufanya jambo hilo kizungu,ndiyo maana wakaalikwa marafiki wachache tu.Tukio hilo lilipangwa kufanyika tarehe 24 April,kumaanisha kwamba walibakisha wiki tatu tu ili tukio hilo lifanyike,marafiki mbalimbali walitoa michango kwa ajili ya shughuli hiyo iende vizuri,Benjamin Ngowi alilivaa swala hilo kama lake,alikuwa ni mtu wa watu ndiyo maana ikawa kazi rahisi sana kwake kuikamilisha.
“Sikiliza Moses,hili swala ni langu.Ndio,ni pale Kawe Club!Kwahiyo leo jioni utatuma?Nitashukuru sana,inaruhusiwa kama una rafiki yako ama marafiki.Ndio Moses,shukrani”
Ngowi,alihangaika usiku na mchana kuhakikisha shughuli ya rafiki yake inaenda vizuri kwa maana hiyo ilibidi amtafute Mc maarufu wa kimataifa, anayeitwa Swai G,hakutaka kupoteza muda.Akamtafuta na kumuweka sawa,wapishi wakatafutwa,vinywaji vikapigiwa hesabu kila kitu kikaenda sawa,kilichokuwa kinasubiriwa ni siku hiyo ambayo Yusrath,alikuwa hajui kabisa.

*****
Tarehe 24 April,siku ya Jumamosi mchana Ahmed na Yusrath walikuwa wanazungumza mambo mengi kuhusiana na mapenzi yao pamoja na ndoa yao kwa ujumla,kila mtu alionekana kuwa mwenye furaha sana siku hiyo!
“Naomba nikutoe outing leo”
“Baby,ghafla namna hiyo?Leo sitoweza”
“No,please!Nakuomba,chonde chonde”
Ahmed alimsihii sana kwani hiyo ndiyo siku ambayo aliipania kuliko siku zote zile.
“Kuna sehemu naenda”
“Baby nipo chini ya miguu yako.Nitakupeleka unapoenda”
“Kweli?”
“Ndio,usafiri leo nitakuwa nao”
Mambo aliyopanga Ahmed yalikuwa makubwa na Yusrath hakuwa anaelewa lolote lile,jioni ya siku hiyo Ahmed akafika na gari lenye wazfa, ambalo alipewa na rafiki yake!Siku hiyo asingeweza kutumia daladala ama bajaj ingawa aliapia ipo siku atanunua usafiri wake binafsi,safari ilianza na baada ya dakika arobaini na tano walikuwa mataa ya Mwenge,taa zilivyoruhusu wakanyoosha mpaka Coca Cola!Wakakunja kulia na kutokea Mikocheni wakazidi kusonga mbele zaidi,walivyopita ‘round about’ wakakunja kulia.
“Baby,huku wapi?”
Yusrath akauliza,uzalendo ulimshinda.Ahmed akabaki kimya mpaka aliposimamisha gari nje ya ukumbi mkubwa.
“Kuna nini leo hapa?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Yusrath.
“Kuna sherehe nadhani”
Ahmed alivyojibu tu,wakashuka akamshika mkono Yusrath na kuanza kuingia ndani.Kitendo cha kufika watu wote wakapiga makofi na kusimama kwa heshima,jambo hilo lilimshangaza sana Yusrath, ikamfanya aanze kutetemeka,aibu ikamshika hakuweza kuwaangalia watu machoni.
“Baby,mbona sielewi?”
Yusrath akaongea kwa sauti ya chini,umati wa watu ulimchanganya.
“Ahmed please niambie”
Mc Swai G,akaongea na kuwakaribisha Yusrath na Ahmed!Bado Yusrath alikuwa ndani ya giza nene lakini baada ya dakika tano,Ahmed akapiga goti moja chini na kuingiza mkono mfuko wa nyuma,akatoa pete.
“Baby,will you marry me?”
Ahmed akauliza huku goti moja likiwa chini,aliuliza kwa hisia kali sana.Kilichotakiwa hapo ni Yusrath kusema ‘YES’ ili wageni waalikwa wapige ‘cheers’ lakini badala yake Yusrath alianza kulia machozi,yakatiririka mpaka mashavuni.
Picha iliyokuwepo ilionesha kabisa alikuwa analia kwa furaha lakini ilikuwa kinyume chake sababu Yusrath alilia kwa uchungu,alimsikitikia sana Ahmed na kutamani kuomba msamaha,wakati huohuo akitaka kukataa jambo hilo lisitokee.Akapiga moyo konde na kujifuta machozi.
“Ah..med,naomba unisam..eheee.Kwa haya,nitakayo..kwambia”
Yusrath,akajikaza akitaka kutoa siri kubwa iliyokuwa ndani ya kifua chake!



Sherehe ilikuwa ni ndogo lakini ni nzito,kila aliyekuwepo ndani ya ukumbi huo, alijua ni kitu gani kinaenda kufanyika, isipokuwa Yusrath ambaye alikuwa nyuma ya kila kitu.Tukio hilo lilifanywa na watu makini, likawekwa kuwa siri kubwa mno, ndiyo maana mpaka Yusrath anafika eneo hilo hakuelewa ni kipi hasa, kinaenda kutokea usiku wa siku hiyo,mpaka pete ilivyotolewa na Ahmed akapiga goti moja chini kumaanisha kwamba akubali kuvalishwa pete ya uchumba,hapo ndipo moyo wake ukapiga kwa nguvu ukataka kutokeza nje ya kifua.Aliogopa,moyo ulimsuta endapo angekubali kuvalishwa pete na Ahmed, wakati tumboni ana kiumbe cha George Charles.Kitendo cha kusita kutoa mkono kilimfanya Ahmed aishiwe nguvu,sababu alielewa nini maana yake!Aliomba Mungu Yusrath asikatae mbele kadamnasi,kwake ingekuwa aibu kubwa mbele ya wageni na marafiki anaowaheshimu!Mbali na hapo, hakuelewa kichwani mwa Yusrath kuna nini zaidi ya kumuona anabubujikwa na machozi na kulia kwa kwikwi akisema, asamehewe.
“Nimeshakusamehee Mke wangu kwa kila kitu,kubali kuvaa pete hii”
Ilibidi kidogo Ahmed atumie akili ya ziada kwa kuchukua mkono wa kushoto wa Yusrath, akashika kidole chake na kuingiza pete kidoleni,hapo ndipo Yusrath alizidi kuachia machozi!Watu wengi na wageni waalikwa walishangazwa na kufurahi sababu walijua mwanamke huyo, analia kwa furaha.Hapo ndipo ‘Dj’ hakufanya makosa,akaweka nyimbo ya Bushoke aliyomshirikisha K-lynn
‘Mbona wanitazama kisha waanza kulia,kama nimekukosea naomba unisamehee!
Hapana hujanikosea ninalia kwa faraha,mapenzi unayonipa sijawahi kupataaa’
Ahmed akasimama na kumkumbatia Yusrath kwa nguvu,kilichofuata hapo zilikuwa ni kelele za furaha nyingi sana za watu kushangilia tukio hilo.
“Usilie baby,nakupenda sana.Nimekusamehee kwa kila kitu”
Laiti kama Ahmed angejua ni aina gani ya kosa analomsamehee Yusrath siku hiyo sherehe hiyo ingevunjwa na Yusrath angetolewa ngeu, sababu angepigwa vibaya sana kwani hasira za mwanamme huyu zilikuwa kali kuliko kawaida,hapo ilibidi Yusrath afute machozi na kupiga kimya kwani moyo wake ulimwambia ayaache mambo kama yalivyo na aliapia siri hiyo angekaa nayo kifuani kwake,akaomba Mungu mambo yasije kuharibika mbele ya safari.
Alichokifanya ni kumtizama Ahmed na kumvuta karibu,akaomba mdomo na kuanza kumpiga denda!Kilichosikika hapo,zilikuwa ni kelele nyingi za watu kupiga makofi,wenye simu wakaanza kuchukua tukio hilo la aina yake.
“Nakupenda Ahmed,lakini una tabia mbaya…Mbona hukuniambia?”
Yusrath akauliza kwa kudeka huku akimuangalia Ahmed machoni,ambaye alionesha kuwa na furaha muda wote.
“Nilitaka niku surprise”
“Surprise,hata ndugu zangu hawajui?Baby please”
“Nitawaambia,tutafanya party nyingine”
“Mmmmh baby”
“Nini sasa?”
“Ilove you”
Akajitahidi sana kupachika tabasamu la plastiki mbele ya umati wa watu,sherehe ilienda vizuri na ilivyogonga saa tano kila mmoja akaanza kuchukua njia yake,wasiokuwa na usafiri waliita bajaj na bodaboda, waliofika na magari waliingia taratibu na kuondoka zao!Siku hiyo ilikuwa ni furaha sana kwa Ahmed na ni siku ambayo asingeweza kuisahau katika maisha yake.Hata hivyo alikuwa ana jukumu la kumrudisha Yusrath nyumbani kwao.Jambo hilo likaanza kufanyika mara moja sababu ya usiku kuwa mwingi,alivyofika getini nyumbani kwa akina Yusrath, akasimamisha gari na kumtizama machoni.
“Mama Kijacho”
“Abee Baba kijacho”
“Nakupenda sana”
“Mimi pia”
Kilichofuata hapo ni kupeana mabusu ya mdomo yaani denda,kila mtu alikuwa ana hisia na mwenzake ndio maana kwa dakika moja nzima, walitumia kunyonyana ndimi, wakibadilishana mate.
“Baby,utanipandisha bwaaanaaaa!Stoooop”
Yusrath,akazungumza kwa sauti ya kudeka kama kawaida yake, macho yake yamebadilika rangi na kuwa mekundu hiyo ilimaanisha kwamba Ahmed angeendelea kufanya hivyo, basi hali ya hewa ingebadilika,kutokana na muda kuwa umeenda sana wakapanga kesho wangekutana ili wafanye tendo hilo la ngono,wakaagana na Ahmed akatoa gari eneo hilo huku nyuma akimuacha Yusrath, analisindikiza kwa macho!

******
George Charles,aliumia mtima kwa kiasi cha kutosha.Alijilaumu sana kwa kitendo cha kukurupuka bila kufata itfaki alizozipanga!Akakosa raha kabisa ya maisha,kazi kwake zikawa hazifanyiki tena akaamini misemo ya wahenga kwamba, kupenda ni maradhi ya moyo! Kitu kilichomjia kichwani ni mwanamke anayeitwa Yusrath, hakuelewa ni kwa njia gani nyingine aitumie ili amrudishe kwani kila alipojaribu kupiga simu hazikupokelewa na meseji zake hazikujibiwa,ofisi ikawa ya moto hapakukalika hata kidogo kila kitu kikasimama!Akafunga safari mpaka Kariakoo, kwenye duka la vipodozi ili akaonane na Yusrath, wazungumze kidogo lakini alivyofika hakumuona pia,hakutaka kukubali hata kidogo akapiga gari moto na kunyoosha mpaka nyumbani kwa wazazi wa Yusrath,maeneo ya Ilala.Lakini huko pia aliambiwa kwamba Yusrath hayupo na muda wake wa kurudi ni usiku.
“Akija,mwambie nilipita hapa”
George Charles,akaacha maagizo kwa kijana wa getini.
“Nimwambie nani?”
“Mwambie George Charles”
“Nitamwambia”
“Ahsante,mwambie anitafute.Usisahau”
“Nitamwambia kiongozi,siwezi kusahau”
George Charles akawasha gari na safari yake ilikuwa ni moja kwa moja mpaka nyumbani kwake,Masaki.
Hapo alipaki gari na kunyoosha mpaka chumbani kwake,akajitupa na kulala chali akiangalia juu kwenye paaa!Kutoka moyoni alimpenda sana Yusrath,hakutaka kumchezea hata kidogo alitaka wafunge ndoa siku moja watengeneze familia,alitafakari vitu chungu mzima, akakumbuka siku waliyofanya ngono juu ya kitanda hiko, akatamani jambo hilo litokee kwa mara nyingine!Muda ulizidi kukimbia,akachukua simu ili ajaribu kumpigia Yusrath kwa mara nyingine.Simu ikaita,moyo wake ukapiga kwa nguvu baada ya simu hiyo kupokelewa,hakuamini. Hapohapo akawahi kuzungumza ili simu isikatwe!

*****
“Aaaaaah aaaaashss aaaah beibiiiii,aaaaaah Ahmed,ilooove youuuu”
Sauti ya puani aliyokuwa anatoa Yusrath,ilisema kabisa kwamba alikuwa katikati ya raha za ajabu sababu Ahmed alijua kucheza na mwili wake,akajua sehemu zote ambazo akiguswa ni lazima apige kelele kama hizo.Wakati huo shingo yake ilikuwa inanyonywa na kupigwa mabusu hiyo ilifanya asisimke zaidi,miguu yake yote miwili ipo begani kwa Ahmed,tango lipo ndani ya Ikulu.Ahmed anazungusha kiuno chake taratibu mno!Mpaka dakika hiyo tangu waanze,alikuwa amefika mshindo mara sita!Jambo lililomfanya atokwe na kijasho chembamba lakini hiyo haikufanya atulie,hata yeye alijitahidi kunyonga kiuno chake aste aste hakutaka kuwa gogo kitandani!Akazidisha kelele na kuanza kumkwaruza Ahmed na kucha mgongoni hiyo ilikuwa na maana ya kwamba tayari anakaribia kufika mshindo kwa mara nyingine tena.
“Baby I’m cumming aaah aaaah A..hmed”
“Bab..y Cumm…Yeah aaaaaah”
Yusrath alikuwa akisema kwamba anakaribia kufika mshindo,kwa wakati huo pia Ahmed nayeye alikuwa njiani,hawakuchukua hata sekunde nne Ahmed akazidisha kasi na kuguna ndani kwa ndani kisha kutulia kifuani kwa Yusrath!Kila kitu kwao kilikuwa furaha,kila mtu aliridhika.Ahmed akatoka kifuani kwa Yusrath taratibu na kulala chali ambapo hapo walijifunika shuka moja, wakaanza kuzungumza mambo mengi kuhusu ndoa yao pamoja na jinsi watakavyomtunza mtoto.
“Sasa baby,mfano umenioa.Aya,tutaishi wapi?”
Yusrath,akauliza swali.Alitaka kujua mchakato mzima wa maisha yao na mawazo ya Ahmed.
“Tutapanga”
“Tutaishi kwenye nyumba ya kupanga?”
“Ndio”
“Ushafikiria kuhusu kujenga,ama kununua kiwanja labda baby?”
“Kusema ukweli badoo”
Hapo Yusrath alikakaa kimya kidogo,akashindwa ni kitu gani amjibu Ahmed.
“Unachowaza wewe ni nini?Katika maisha haya.You are a Man.Uanaume haupimwi kwa kuvaa vizuri,uanaume unapimwa katika maamuzi yako na maendeleo.Ahmed,utaniudhi kwa kweli,nahitaji mwaka huu uwe una kiwanja tayari”
Haukuwa utani katika swala la maendeleo, mwanamke huyu alikuwa ni mkali kuliko pilipili mbuzi,licha ya Ahmed kuchukia kwa kuambiwa maneno hayo lakini yalimwingia akilini, akayatafakari mara tatutatu, kwake ulikuwa ni ukweli mchungu!
“Nakupenda sana Yusrath,please naomba usiniache.Nitakufa maskini”
“Siwezi kukuacha lakini ufanye juu chini,huu mwaka usiishe uwe una kiwanja tayari.Huu ni mwezi wa nne”
“Okay baby,nimekuelewa.Lingine?”
“Hama kwenu,anza kujitegemea”
“Sawa mke wangu”
“Ala…..”
Kilichomkatisha Yusrath katikati ya maongezi ni simu yake iliyoanza kuita ikiwa pembeni, juu ya meza.
“Atakuwa Mama nini?Maana tangu asubuhi sijaongea naye”
Yusrath alisema hivyo huku akijivuta kwa juu,akachukua simu na kuangalia juu ya kioo!Namba zilikuja kama zilivyo lakini aliijua namba hiyo niya George,kutokana na kuifuta kwenye simu yake.
“Bebiii”
Yusrath akaita na kumtizama Ahmed.
“Yes”
“George anapiga”
“George?George gani?!”
“Yule bosi wangu,baby ananitaka naomba upokee umwambie aachane namimi”
“Tangu lini?Nipe simu”
Kukabidhiwa simu kwa Ahmed ilikuwa ni sawa na chizi kupewa rungu,hapohapo akachukuwa na kuiweka sikioni tayari kwa kutoa mapovu.
“Yusrath,mbona hupokei simu zangu?Nisamehee yaishe,nahitaji kuzungumza nawewe.Jaribu kusahau yaliyotokea siku ile, ni shetani tu”
Upande wa pili wa simu ulilalamika,aliyezungumza alikuwa ni George Charles bila kujua simu ipo sikioni mwa Ahmed,ambapo kwa wakati huo hasira zake zilianza kupanda taratibu.Swali lililomjia kwa harakaharaka, ni jambo gani lililotokea mpaka shetani akahusishwa?



Sura ya Ahmed,ilibadilika hapohapo akawa kama mtu aliyelamba ndimu!Maneno kutoka kwa George yalimfanya aumie ajabu,ilikuwa ni lazima kuna jambo zito lilifanyika kati ya watu hao wawili George na Yusrath,kitendo cha George kumtaja shetani kwenye maelezo yake ilimpelekea moja kwa moja kupata jibu la kwamba ni lazima walifanya ngono,hilo halikuwa na mjadala!
“George!”
Ahmed akaita,simu ilikuwa bado kwenye laini.
“Nisikilize George,tena kwa makini.Nachokuomba uachane na mke wangu…”
“Sio ka…”
George akamkatisha ilielekea kuna kitu alitaka kujazia kwenye mazungumzo yake,mwanamme huyo alionekana kujiamini sana, ndiyo maana hakuogopa wala kukata simu.
“Achana na Mke wangu George,nitakufanya kitu mbaya hutoamini”
“Naomba niongee na mwenye simu”
“Hivi hunielewi?”
“Naomba niongee na Yusrath..”
George Charles,hakuonesha hofu ya aina yoyote ile alichotaka yeye ni kusikia sauti ya Yusrath tu na wala sio kitu kingine,ujasiri huo ulimfanya Ahmed azidi kuchanganyikiwa akamkata Yusrath jicho kali,akaweka loudspika na kumtaka azungumze.
“Ongeaa”
Ahmed akafoka kwa sauti.Yusrath asingeweza kufanya kitu chochote kile zaidi ya kumfokea George, akimwambia akome kumpigia na kuanzia siku hiyo,asimtafute kwa njia moja ama nyingine.Hiyo haikusaidia kumpumbaza Ahmed kwani simu ilivyokata,alishushiwa mvua ya maswali.
“Mlifanya nini wewe na George?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Ahmed akimtizama Yusrath machoni,tayari alikuwa mwenye jazba nyingi.
“Baby mbona sikuelewi”
“Hunielewi?Hunielewi?Yusrath,mimi sio mtoto mdogo!”
“Ahmed,relax.Niambie,nini tatizo.Nieleze,George amekwambia nini?”
Hapo Ahmed akashusha pumzi ndefu,moyo wake ulimuuma wivu ukapanda katika kiwango cha juu kabisa,akamueleza kila kitu alichoambiwa.Mapigo ya Moyo ya Yusrath yalipiga kwa nguvu,akaanza kutetemeka hakuelewa ni kitu gani akijibu,alichokifanya ni kujivuta na makalio mpaka ukutani, sababu alielewa muda wowote Ahmed, angerusha kibao,ndiyo maana akajihami mapema.
“Baby,ngoja niongee ukweli”
“Nakusikiliza”
“Ile siku uliyonipiga Pale Mwenge niliondoka naye mpaka kwake,kusema ukweli siku ile uliniumiza sana nilikasirika.Nika apa,sitokuja kukusamehee kamwe maisha yangu yote.Nililia sana siku ile,nikamueleza George, jinsi gani navyokupenda.Akaanza kunifariji na kunipa pole nyingi huku akinilazimisha nichukue kinywaji ninywe.Nakumbuka ilikuwa ni waini….”
Mambo aliyokuwa anazungumza Yusrath yalikuwa ya kubuni,Yusrath alianza kuhadithia hadithi ndefu ili kumtengeneza Ahmed kisaikolojia,mwanammke huyu alikuwa ni mjanja,aliongea akiwa mkavu na mwenye kuonesha majuto makubwa sana.
“Ikawaje?Ebu fupisha maelezo”
“Ahmed I’m so sorry,bora ningekusikiliza…George alitaka kunibaka siku ile”
“Whaaaaat?!”
Ahmed,alishtuka akitumia kimombo kuonesha jambo hilo lilimshangaza kwa kiasi cha kutosha,akatamani dakika hiyohiyo avae nguo, amfate George Charles, bila kujua hapo alipo tayari amelishwa matango pori na alichoambiwa ni uwongo kwani Yusrath alikubali kwa hiyari yake, kufanya ngono,akidhani wenda angetoa mawazo licha ya yote alijuta kwa kitendo alichokifanya.
Siku hiyo hakufanya makosa,akaendelea kumuaminisha Ahmed na kukazania msimamo wake huohuo,ili kuupigilia uwongo wake msumari akakamua machozi mililita kumi yakaanza kutoka,hapo Ahmed hakuchomoa akamsogelea Yusrath na kumkumbatia.
“Usijali Yusrath,najua yote nimetaka mimi.Naomba unisamehee”
“Nipromise hutorudia tena”
“Siwezi,nakuhaidi”
Hivyo ndivo ilivyokuwa,hatimaye Ahmed akawa ametulia, Yusrath akayaacha mambo kama yalivyo,akiapia ya kwamba hatokuja kufungua kinywa chake kuongea lolote juu ya mtoto atakayezaliwa.

****
“Nilidhani utakuja”
“Wapi, Tanzania?”
“Ndio”
“Kuna mambo yaliingiliana,lakini nitakuja.Jamaa anaoa lini?”
“Bado sina uhakika lakini keshamchumbia mwanamke nadhani mambo ni hivi karibuni tu”
“Anaoa Mtanzania?”
“Mtanzania ndio,lakini kwa mbaliii ana uarabu Fulani.Afrikasti”
“Hongera zake,hata mimi natarajia kuoa hivi karibuni”
“Lini tena?”
“Bado sasa tulia,inabidi nifanye utaratibu na shemeji yako”
“Kwahiyo nitakuja huko?”
“Tatizo una haraka,ngoja nikupe siri.Shemeji yako anatoka Tanzania”
“Acha utani”
“Nakwambia ukweli,sina sababu ya kukudanganya”
“Sasa chombo kipo huku ama huko?”
“Nipo naye huku”
“Habari njema hizo”
“Lakini kabla ya harusi,nitakuja naye huko kutembea.Tuweke mambo sawa kwa wazazi wake!Maana ni stori ndefu kidogo”
“Nitakusubiri kwakweli”
Yalikuwa ni mazungumzo kwa njia ya simu kati ya Dokta Sajo na Benjamin Patrick Ngowi,ungeyasikiliza maongezi yao ungedhani wenda ni ndugu kumbe walikuwa ni marafiki wa karibu sana,hiyo ni kutokana na kusoma chuo kimoja wote!Stori zilikuwa nyingi siku hiyo kupitia simu ya mkononi.Dokta Sajo siku zote alitamani kumuoa Hajrath,awe mkewe wa ndoa!Tabia za mwanamke huyo, zilitosha kabisa kumuweka ndani,hata hivyo hakutaka kufanya mambo hayo kienyeji alitaka aende Tanzania akajitambulishe,jambo hilo lilikuwa gumu sana kwa Hajrath kulikubali.Hakutaka kuisikia tena nchi inayoitwa Tanzania katika maisha yake,alikumbuka mateso aliyopitia!Alimkumbuka mwanamme anayeitwa Florian akili yake ikasafiri na kurudi nyuma na kumuona Ahmed ambaye alifanya siku moja atake kunywa sumu ili ajiue,kifupi aliichukia Tanzania nzima na watu wote wanaoishi ndani ya nchi hiyo.
“Kwanini sasa hutaki kwenda mpenzi?”
Siku hiyo Dokta Sajo,alitaka kujua zaidi.
“Ina maana hujui kwanini?”
“Ndio sijui”
“Kila siku nakwambia kitu hiko hiko,unataka nirudi tena Jehanam?”
“Hapana,mambo yamebadilika tayari.Naamini kila kitu kimetulia inabidi tufanye utaratibu tufunge ndoa yenye baraka”
“Kwani hatuwezi kuishi hivi,nawatumia meseji nyumbani nawaambia nipo salama.Wasinitafute”
“Unadhani,ni wazo zuri?”
“Ndio”
“Hapana,inabidi twende.Isitoshe kuna rafiki yangu,amenipa mwaliko wa ndoa.Huko Tanzania,kwanini pia tusitumie nafasi hiyo”
Mvutano mkubwa sana ulitokea kati ya Dokta Sajo na Hajrath siku hiyo usiku wakiwa mezani, wanakula chakula.Japokuwa Dokta Sajo, alitumia ushawishi mkubwa lakini haikuwa rahisi kwa Hajrath kukubali kirahisi namna hiyo,lakini mwisho wa siku alikubali kuingia Tanzania kwa sharti moja tu,iwe siri kubwa sana kwani alikubali kumpa Kampani Dokta Sajo, siku hiyo ya harusi.

****
Siku zilizidi kwenda na miezi ikazidi kusonga mbele,tumbo la Yusrath lilianza kukuwa taratibu, akajaribu kulificha wazazi wake wasigundue lakini hilo halikuwezekana sababu mimba ni pembe la Ng’ombe,halifichiki.Hata hivyo,alijitahidi kushindana na hali kwa kuvaa Madera pamoja na nguo kubwa kubwa ili kuficha tumbo lake lisionekane kiurahisi,miezi mitano ilivyofika Mama akaanza kuhisi.Alichelewa kujua kutokana na Yusrath kujifungia chumbani muda wote ama kutoka asubuhi na kurudi jioni.
“Haa Yusrath,kumbe una mimba?”
Mama akauliza kwa mshangao ingawa hakuonesha ukali wa aina yoyote ile.
“Mama hapanaa sinaa”
“Kumbe hiyo nini?”
“Nimeshiba tu”
Haikujulikana kama anasikia aibu ama hakuwa tayari kumueleza Mama yake kuhusu hali hiyo,Mama hakuonesha ukali wowote, akasogea karibu akitaka kujua mimba ya nani,japokuwa alikuwa ana uhakika asilimia mia moja niya Ahmed,mme wake mtarajiwa lakini alitaka kupata uhakika zaidi.

*****
Tabia ya Kassim,haikuweza kubadilika hata kidogo!Aliendelea,kutembeza dudu na kuwavua wanawake nguo zao za ndani,hakuremba na hakujua kitu kubembeleza katika maisha yake.Japokuwa kaka yake,alikaa chini na kumkanya atulie lakini ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki,mwanamme huyo aliendelea kuwachanganya wanawake kama pilau na kachumbari,haikujulikana tabia hiyo ya kupenda vimwana aliitolea wapi,kila siku alikuwa akigombana na wanaume wakati mwingine wazee walimuonya kwamba wangemtoa busha,yeye hakujali aliweka masikio pamba na kuzidi kupita nao!Na sifa yake ilikua moja tu,harudii mwanamke zaidi ya mara mbili.Laiti kama kila mwanamke aliyetembea naye angekuwa anamtoboa usoni basi sura yake ingekuwa chandarua ama nyavu ya kuvulia samaki,kifupi Kassim alikuwa fagio la chuma!
“Baby,huyu nani?”
Siku hiyo mwanamke anayeitwa Sakina,aliwaka baada ya kukuta meseji ya mwanammke ndani ya simu ya Kassim.
“Mwanammke”
“Sina maana hiyo.Ni nani yako?”
“Aliyekwambia ushike simu yangu nani?”
“Yaani badala ya kujibu swali,unauliza swali.Kassim,huyu kahaba ni nani?”
“Sakina,unanipigia kelele”
“Nakupigia kelele?”
“Ndio”
“Nakupigia kelele?”
“Ndio….paaaaa”
Kassim,alipigwa kibao kikali cha shavu kilicholia kwa sauti kubwa!Kilimuingia lakini katika maisha yake,hakuwahi kumpiga mwanamke na aliapia hatokuja kufanya hivyo kamwe,ndiyo maana akatulia na kumuangalia Sakina.
“Ondoka”
“Badala ya kunibembeleza kwa upuuzi uliofanya,unanifukuza”
“Nikubembeleze nini?Nikubembeleze,una kunya keki wewe!Nenda toka,achana namimi”
Kimasihala masihala,huo ndio ukawa mwisho wa penzi lake na Sakina,Kassim hakutaka kurudi nyuma, maisha yake katika mapenzi yalikuwa kama samaki,hayarudi rivasi.
“Umeona wapi samaki anarudi rivasi?”
Siku hiyo Kassim,alimwambia Sakina alivyokuwa anajaribu kumuomba msamahaa ili penzi lao lirudi,haikuwezekana ikabaki kuwa historia.
Maisha yake yalikuwa hivyohivyo,mpaka alivyompata mwanammke mwingine anayeitwa Rhoda Denis,penzi lao lilianza kama utani mwisho wa siku wakajikuta wapo chumba kimoja, wanafanya ngono,kilichowafanya wanawake wavutiwe na mwanamme huyo ni mbinu anazotumia.
Kwanza,alikuwa anajua kupiga domo akitongoza,ana maneno malaini na matamu,pili alijua kuvaa muda wote alikuwa msafi, tatu alinukia manukato mazuri sana!
“Kassim,nani amekufundisha haya yote?”
Siku hiyo Rhoda Deniss, aliuliza wakiwa kitandani uchi wa mnyama, baada ya mwanamke huyo kupewa dozi ya 5G,haikuwahi kutokea kupewa penzi kama hilo.Mchezo wao ulikuwa huohuo,ilikuwa kila siku mwanamke huyo aombe penzi.Ilielekea nayeye alinogewa na mchezo huo,akawa anahonga.Vitu kama pesa,nguo na zawadi mbalimbali alimpatia Kassim kama zawadi kwani hakutaka kumpoteza hata kwa sekunde!
Siku moja wakiwa kitandani wanapiga stori,sijui ilikuwaje Rhoda Denis akashika simu ya Kassim,akaingia kwenye picha.Moyo wake ukapiga kwa nguvu kuna kitu alikiona.
“Darling, huyu Ahmed umemjuaje?”
Moyo wa Kassim,ukalipuka kama bomu maana hakutegemea hata yeye, kusikia swali kama hilo!Kilichomjia kichwani ni kwamba ni lazima kaka yake, alipita na Rodha Denis.
“Wewee umemjuaje?”
Kassim,akajibu kwa swali.
“Baby nijibu bwanaa”
“Ni mshkaji wangu tu,hatujuanii kiviiiile”
Kwa wakati huo Kasim hakutaka kuropoka,alitaka kumsikiliza kwanza Rhoda kitu gani angetaka kuongeza.
“Duniani hapa mmmmh”
“Kuna nini?”
“Wewe utamwambia lakini”
“Kumwambia nini?Ahmed,simjui kivile nimekwambia.Yaani nina ndugu yangu fulani,huyo ni rafiki yake alikuja naye home”
“Anataka kuoa”
“Nani Ahmed?”
Kassim,akajifanya kushtuka akiuliza kwa mshangao.
“Ndio,hajakwambia?”
“Ah wapi”
“Mwanammke anayetaka kumuoa sasa ni rafiki yangu sana”
“Anaitwa nani?”
Kassim,akajifanya hajui lolote.Ili kuzuga zaidi akajifanya na jina hajui,kila kitu akakifanya kuwa kigeni kwake.
“Yusrath,ni rafiki yangu sana!Lakini wanawake sisi,Mungu anatuona sijui kilimsibu nini yule mwanamke”
“Kivipi?”
“Huyu Yusrath ana mimba,kuna siku alikuja analia hapa.Kama mtoto mdogo,nimsaidie.Kwamba hiyo mimba sio ya Ahmed.Mimba ya mwanamme mwingine akataka kutoa,nikamwambia asiflash.Ambambikie Ahmed, jamani loooh sisi wanawake”
Moyo wa Kassim,ulipiga kwa nguvu.Hadithi anayopewa hapo ilikuwa ngeni,kwanza alishtuka kusikia Yusrath ana mimba.
“Una picha ya huyo Yusrath?Kama unayo ebu nimuone”
“Wa nini baby?”
“Nataka nimuone tu”
Kassim,akataka kuhakikisha kama ni Yusrath anayemfahamu.Rhoda Deniss hakuwa mwenye hiyana,akachukuwa simu kubwa na kumuonesha Kassim picha,hiyo ilimfanya Kassim atoe macho yake,hakuamini kama Yusrath ni muhuni tena mshenzi wa tabia,ilikuwa ni lazima amwambie kaka yake,kila kitu.



Laiti kama angejua Kassim ni nani,angefunga bakuli lake na kupiga kimya.Rhoda akawa tayari amevujisha siri nzito bila kutarajia,ahadi aliyompa Yusrath kwamba angeitunza siri hiyo mpaka atakapofukiwa chini mavumbini ikawa imeyayuka,akashindwa kutimiza ahadi hiyo hata kabla mtoto ajazaliwa,Kwa Kassim alitabasamu na wakati huohuo akashikwa na hasira,haikuwezekana hata siku moja kaka yake afanywe zoba,alee mimba isiyokuwa yake.Kuna vitu vingi sana vilipita ndani ya halmashauri ya ubongo wake,ndiyo maana akakaa kimya akijaribu kutafakari ni kitu gani akifanye.Hiyo ikamshangaza sana Rhoda Denis, ambaye kwa wakati huo alizidi kuongeza mambo mengine na chumvi nyingi,akizungumzia maisha ya watu.Alikuwa kifuani kwa Kassim akiamini kwamba kila kitu kipo shwari kabisa.Licha ya hayo yote, moyo wake ulikuwa mweupe, niya ya kuzungumza hivyo pia, alihitaji mawazo ili stori ziendelee.
“Au nilimshauri vibaya?Mbona upo kimya?Mimi sipendi baby,naongea peke yangu”
Rhoda,akauliza kwani alihitaji hoja yake ipewe kipaumbele.
“Ni wazo zuri sana,kwahiyo huyo Dada alikuja hapa kwako?”
“Ndio,ni rafiki yangu.Unajua rafiki yangu.Siri yake,siri yangu…Sema siku hiyo alikuja hapa,anatetemeka huyoo,nikamwambia relax”
“Sasa hiyo mimba,hajakwambia ya nani?”
“Hajaniambia”
“Nyie wanawake bwana..Kwahiyo jamaa,analea mimba sio yake?”
“Ndio maana yake”
“Sasa na mtoto akizaliwa?”
“Atalea vile vile”
“Huo mchezo mimi bado,sijachezewa”
“Unaongea tu wewe”
“Bado sijafanyiwa huo uboya aise.Hivi unanichukuliaje baby?”
“Wanawake wana akili wewe”
“Kwa mafala labda wengine,sio kwangu.Yaani heeee,ujanijua vizuri,jaribu siku huo mchezo uone.Mtoto azaliwe uniambie kafata kwa Babu thubutuuuu”
“Haa! Haaa! Haaaa! Haaaa!”
“Hakuna cha kufata kwa babu wala nini,unapachikiwa vizuri tu bila kujua”
“Kama havijatokea vita vya tatu vya dunia”
“Wanabambikiwa wanajeshi,sembuse wewe.Wanapachikiwa watoto Maraisi,sembuse wewe.Baby omba Mungu tu,upate mwanamke muaminifu”
“Waaaaaaapi,nenda zako.Mimi sio fala wala lofaa!Tuachane na hayo,nimekumisi”
Simu ya Kasssim ilikuwa tayari imepata moto,ilikuwa inachaji hivyo ilimaanisha anataka kuitumia, ndio maana akaanza kumtomasa Rhoda Denis kila idara,kila sehemu ya mwili wake mambo yalivyokuwa tayari,mechi ikaanza hapohapo.

*****
Muda wote Ahmed alikuwa mwenye mawazo tele,mbali na kuwa mwenye furaha ya Yusrath kuwa mjamzito.Kilichomuumiza ni kwamba hakuwa amejipanga kwa hilo.Kwa maana hiyo jambo hilo lilitokea ghafla,alivyolifikisha wazo hilo kwa rafiki yake wa karibu Benjamin Ngowi,akapata kitu kipya na kuingiwa na faraja.
“Sikiliza Ahmed kwani ana mimba ya miezi mingapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Benjamin Ngowi.
“Mitano,inaenda sita”
“Sasa hivi kuna vitu unatakiwa upunguze,punguza pombe na starehe zisizokuwa na lazima.Tenga pesa ya mtoto na Mama yake.Kama unashindwa fungua akaunti kila wiki unaweka ishirini”
“Ni wazo zuri lakini n..”
“Lakini nini Ahmed,you are a Man.Tena anza kumuhudumia sasa hivi,ikiwezekana kila baada ya siku mbili unamtumia elfu kumi.Najua ni ngumu lakini lazima iwe hivyo”
“Ngowi,kuna vitu vingi sijafanya.Naona kama jambo hili litafanya mambo yangu mengi yakwame”
“Hakiwezi kukamwa kitu,fanya juu chini kila kitu kiende.Huo ni uanaume!Eti sio kisa Shemeji ana mimba ndiyo ushindwe kujenga ama ushindwe kununua kiwanja.Get serious,mambo yote inabidi yaende kama kawaida plans zote zifanyike”
“Nahisi kichwa changu kinaanza kupata moto”
“Ndio,uanaume huo.Hapo ndio tutapima uwezo wako wa kufikiri na kuamua”
“Nilitaka kununua kiwanja,inabidi sasa ni stop”
“No don’t ,nunua”
“Na Shemeji yako?”
“Timiza wajibu wako kama kawaida”
“Nitafanya nini?”
“Unaniuliza mimi tena?…Ahmed”
Ahmed alikuwa katika wakati mgumu kuliko kawaida,mambo aliyoambiwa yalimwingia akilini kama yalivyo kwamba ni lazima kila kitu kiende kama kilivyopangwa,ndiyo maana akamtizama Benjamin Ngowi,alivyotaka kuchukuwa glasi ya bia ili aweke mdomoni akashindwa,hiyo ilitokana na mawazo mengi, kutawala kichwani kwake.
“Psiii weitaaa,muongeze nyingine tatu.Kwenye bili yangu”
Benjamin Ngowi,akaagiza vileo.Chupa zikaletwa nyingine kwa ajili ya Ahmed ili azidi kutafakari vizuri,usiku ulivyokuwa mwingi akanyoosha mpaka nyumbani kwao ambapo huko alijitupa moja kwa moja kitandani,akaendelea kutafakari.Kabla usingizi hujamchukua akasikia kwa mbali, mlango wake unagongwa.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Akasikilizia kwa mbali.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Ukagongwa tena kwa mara nyingine.
“Brooo”
Sauti hiyo kutokea nje ya mlango ndiyo ilimwambia kwamba huyo ni Kassim,alishangaa sababu haikuwahi kutokea usiku kama huo akagongewa mlango na mdogo wake.
“Dogoo”
Ahmed alisimama na kutembea mpaka mlangoni,akaufungua.
“Ingia,Vipi mbona usiku usiku dogo?”
“Aaaah,siku nyingi sijakuona”
“Poa,ingia ndani”
Kassim,akaingia ndani.Akakaa kwenye moja ya kiti cha pembeni,akamtizama kaka yake kwa masikitiko makubwa sana,alielewa kabisa hakuwa anaelewa lolote lile, kuhusu mimba aliyobambikiwa.
“Fresh,hatuonani broo”
“Nipo”
“Au ndio ubize wa ndoa?”
Kassim,akaanza kumchimba kaka yake.
“Pilika tu”
“Alafu shem,simpati siku hizi hewani.Kabadili namba nini?”
“Mbona muda sana”
“Kwahiyo ana namba mpya?”
Kassim alitaka kujua hilo kwanza,kwa maana namba ya Yusrath haikupatikana hewani kwa kipindi kirefu sana,hata hivyo kwake haikumsumbua alimuweka kiporo na kujua ni lazima siku moja angemvua nguo yake ya ndani na kutimiza ndoto yake,kitendo cha kaka yake kutaka kumuoa, kilimfanya ajipe moyo kwamba atakuwa karibu naye zaidi yaani ‘Shemeji zima taa,kaka hayupo’huo ndio ulikuwa mpango wa mwanamme huyu.
“Anayo mpya”
“Siku nyingi sijaongea naye”
“Nikupe namba zake?”
Sio kwamba Ahmed hakuwa anaelewa kwamba mdogo wake huyo,alikuwa akimsumbua Yusrath akimtongoza na kumtaka kimapenzi mbaya zaidi Kassim hakutumia ustaarabu hata kidogo,alitumia gia za kitoto za kumkandia kaka yake,hilo Ahmed alilijua lakini hakutaka kulionesha waziwazi.
“Hizi hapa”
Ahmed,akaonesha simu yake!Kazi ya Kassim ikawa ni kuzihamishia kwenye simu yake.
“Hapa,kifaa umepata broo”
Kassim, akasanif.
“Ahsante sana”
“Acha niende”
“Fresh,mimi nipo”
Kassim,akanyoosha moja kwa moja mpaka chumbani kwake huko akajifungia na kuanza kupiga namba za Yusrath,bahati mbaya kwake akakuta inatumika.Alivyotega sikio lake vizuri akasikia Ahmed anaongea,akajiongeza na kujua kwamba ni lazima Ahmed ndiye yupo kwenye laini anazungumza naye.Hakuchoka,akazidi kupiga zaidi na zaidi!Hiyo ndiyo ilikuwa hali halisi wakati Kassim anahangaika kumpigia simu Yusrath yeye kwa wakati huo alikuwa akideka simuni,akimueleza Ahmed jinsi anavyompenda,hakumficha jinsi ilivyokuwa, Mama yake alivyogundua ujauzito aliobeba.
“Mtoto wako,ananisumbua tumboni”
“Anafanya nini?”
“Ananipiga mateke”
“Anakupiga mateke?”
“Ndioo bwanaaaaa”
Yusrath akadeka simuni,hiyo ilimfanya Ahmed atabasamu kidogo.
“Ndio anakuwa,alafu litakuwa jembe hilo”
“No bebii,mimi nataka awe wa kike”
“Mmmmh”
“Ndioooo”
Wakati Yusrath,anazungumza akatoa simu sikioni ili kuangalia namba iliyokuwa inampigia simu na kumsumbua muda wote,namba hiyo haikukoma.Ilikuwa ni ngeni,akaipotezea na kuendeleza mazungumzo na Ahmed,saa nane za usiku ndipo walipoagana.
“Baby,mimi nawewe.Huwa hatumalizi mazungumzo yetu, hata siku moja”
“Ni kweli”
“Naomba niruhusu nilale Mme wangu”
“Sawa,Mama kijacho wangu”
Hiyo ndiyo staili waliyotumia kuagana,kila mmoja akampiga busu mwenzake wakaagana simuni.Kwa kuwa Yusrath hakutaka usumbufu mwingine zaidi,ilibidi azime simu na kulala akitafakakari maisha yake kwa ujumla.

*****
*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG