Search This Blog

Monday, March 23, 2020

ABEE SHEMEJI SEHEMU YA 1/10


ABEE SHEMEJI
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 1 KATI YA 10
*******
 *******
“No Kassim.Hapana!Si..wezi,Mungu wangu….”
“Hajrath,nisikilize.Huwezi kufanya nini?Ndio ishatokea sasa”
“Ni mme wangu lakini”
“Namimi ni Kaka yangu,Hajrath.Niangalie usoni”
“N..o Siwezi,Eeeh Mungu wangu.Ahmed Ahmed amka basi”
Kila mtu alionekana kupigwa na butwaa usiku wa siku hiyo,siyo Hajrath wala Kassim.Kila mtu alipagawa vya kutosha.Lakini mmoja wapo kati ya watu hao wawili, alionekana kuchanganyikiwa zaidi,huyu ni Hajrath alikuwa mara azunguke mara ashike hiki.Hakuamini kama mme wake wa ndoa
yupo chini,amelala katulia.Kichwani kwake ilikuja taswira ya milango ya gereza,inafunguka nayeye kutupwa ndani, jambo hilo lilionekana kumchanganya zaidi.Sio yeye tu,hata Mwanamme huyo Kassim,aliyekuwa pembeni yake.
Aliyekuwa amelala chini ni kaka yake,tumbo moja!Ni wazi kwamba endapo siri hiyo ingevuja wasingetoka salama, ndiyo maana walikuwa wanahaha,kutafakari ni kitu gani wakifanye.
“We..we ndio umesababisha,shemeji”
“Huu,sio muda wa kulaumiana.Wewe ndio chanzo”
“Hapana wewe ndio umemuua”
“Sasa tutafanya ni..ni?”
“Siju..i”
Haikuwa kazi rahisi kutoa maamuzi,mtu aliyekuwa amelala chini alikuwa ahemi wala hajigusi.
“No,Ahmed please.Wake up mme wan..ngu”
Hajrath,bado hakuamini kama mmewe amelala sakafuni haongei kitu, ndio maana alikuwa akimwaga machozi,anaongea kwa kwikwi.Alitamani walau mwanamme huyo aseme japo neno la mwisho,wakati mwingine alijilaumu kwa upumbavu wake ikapelekea mpaka mmewe kufariki dunia,kifupi yeye ndio alikuwa mkandarasi wa kila kitu kutokea.
“Shemeji”
Kassim akamuita Hajrath huku akimuangalia kaka yake, aliyekuwa chini sakafuni amelala.Badala ya Hajrath,kuitikia alimuangalia tu kumaanisha kwamba anamsikiliza,anaweza kuongea.
“Inabidi hii ibaki kuwa siri yetu”
“Kassim,sijakuelewa…Hili swal..a lazima nilipeleke polis..i”
“Polisi?Ukaseme nini?Wewe ndio chanzo”
“Kwanini umemuua kaka yako?”
“Mimi,sijamuuwa wewe ndio umemuua”
Hajrath na Kassim walizidi kubishana,juu ya kitu gani wakifanye.Ki ukweli ulikuwa ni msala mkubwa endapo jambo hilo lingefika kituo cha polisi.Ni dhahiri kwamba hakuna hata mmoja kati yao angeachwa salama, kutokana na tukio hilo lililotokea,hiyo ilifanya kila mtu amtupie mpira mwenzake.Baada ya kulumbana sana,wakiwa seblen wakaamua kutoka na wazo kwamba wakaitupe maiti hiyo mbali,ili kupoteza ushahidi.
“Kassi..m,Oooh My God,kwanini mimi?”
Hajrath alilalamika huku akiweka mikono yake kichwani na kupiga piga miguu yake chini,baada ya kumuona Shemeji yake anatoka nje na funguo za gari.
Roho ilimuuma vilevile, mwanamme huyo kwa kitendo alichomfanyia kaka yake,sambamba na kuumia moyo alimlaumu sana Shetani.Licha ya yote hayo hakuwa na jinsi zaidi ya kuingia ndani ya gari na kulirudisha kinyumenyume kwa kasi mpaka karibu na mlango kabisa,akaretemka na kuliacha linaunguruma.Alivyoingia ndani,akatembea kwa kasi mpaka karibu na maiti ya kaka yake.Akaitizama maiti hiyo iliyokuwa chini sakafuni,moyo ukamuuma ajabu, lakini hakuwa na jinsi ilikuwa ni lazima apige moyo konde kwani maji yalikuwa tayari yashamwagika, ni vigumu kuzoleka!
“Nisaidie tum-bebe”
Hapo,ndipo Hajrath alipozidi kuchanganyikiwa zaidi.Ilikuwa ni lazima wakubali kilichotokea ili wasonge mbele kwani hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa tayari kuingia kwenye matatizo makubwa na ilikuwa ni lazima wafanye jambo hilo wasionekane na wabaki na siri hiyo nzito mpaka kifo chao.
“Mnyanyue kwa huko.”Kassim,akaamuru.
Hajrath akapiga moyo konde,akamnyanyua mme wake wakambeba.Yeye akamshika kwa upande wa kichwani,Kassim chini upande wa miguu wakaanza kumtoa nje.Walivyofika huko wakasaidiana kumuingiza ndani ya gari.
“Shem”
Kassim,akaita kabla ya kuingia ndani ya gari.
“ABEE SHEMEJI”
“Hatuwezi kumtupa hivi,inabidi tumuweke ndani ya gunia.Una gunia lolote?Ama mfuko mkubwa?”
“Ngoja,nikaangalie stoo.Nisubiri”
Roho ya uwoga ikamtoka Hajrath,akavaa ujasiri ambao hata yeye mwenyewe alijishangaa kabisa.Akatembea mpaka jikoni.Huko aliingia stoo,akaanza kutupa macho yake huku na kule,akaona gunia alivyolishika na kulifunua akaona kuna viazi,akavimwaga chini vyote kwa haraka na kutoka mbiombio mpaka nje.
“Liweke gunia hilo ndani,fanya haraka ingia twende”
Kitendo cha Hajrath kuingia,gari ikapigwa moto na safari ikaanza mara moja.
“Tunaenda wapi?”
Hajrath,akauliza huku akimuangalia shemeji yake, bado hakuamini kama mmewe amekufa tayari na yeye pamoja na Kassim walikuwa wakandarasi wa jambo hilo kutokea,wakati mwingine alidhani yu ndotoni japokuwa alitamani iwe hivyo ashtuke ili amkute Ahmed wake,yupo hai lakini jambo hilo halikuwezekana kwani kilichokuwa kimetokea kilikuwa ni ukweli,sio siri usiku huo kwake ulikuwa ni sawa na Jehanam.
“Bado sijajua”
Ni kweli Kassim,alikuwa katika dimbwi la mawazo mengi sana!Hakutaka kuamini kama Kaka yake kipenzi amekufa kisa Mwanamke huyo shetani aliyekuwa kushoto kwake,mara ghafla roho chafu ikamvaa ikamwambia ammalize pia na Hajrath kwani bila mwanamke huyo wenda asingejikuta katika matatizo makubwa namna hiyo.
“Kwanini uliniita?Kwanini umenifanya nimuuwe kaka yangu?Wewe Malaya naongea nawewe”Kassim,akauliza kwa ukali na kufoka.
“Kwa sababu nakupenda”
“Nyamaza,Kahaba wewe.Tena funga bakuli lako!Wema wangu umeniponza,bora ningemuacha akuuwe tu,ona sasa ulichokifanya”
“Kassim,lakini in..”
“Lakini nini?Lakini nini?Yote umetaka wewe?Kwanini lakini,umetumwa au?Najuta kukufahamu.Yaa…”
Ghafla ukazuka ugomvi mkubwa,Kassim alifoka kwa sauti ya juu,akionekana kujuta.Akatamani muda urudi nyuma,arekebishe kilichotokea lakini muujiza huo kamwe usingetokea, hata angeenda kwa Mganga yoyote yule!Kifupi maisha yake yasingekuwa na amani hata kidogo kuanzia siku hiyo.Damu ya kaka yake ilikuwa mikononi mwake,kilichomfanya akatishe sentensi yake ni baada ya kuangalia ‘site mirror’ za pembeni,akaona gari linamulika mulika taa,kuashiria kwamba asimame,alivyoangalia vizuri akagundua ni gari ndogo aina ya Vitz.
“Kuna gari inatuwashia taa nyuma,unaifahamu?”
Kassim,akauliza.Hiyo ilimfanya Hajrath ageuke nyuma.
“Mungu wangu!”
“Nini?”
“Gari ya Tonny hiyo”
“Tonny!Ndo nani?”
“Rafiki yake Ahmed,please simama”
“Nisimame!?Hivi una wazimu wewe mwanamke?”
“Hapana,nakuomba simama.Alafu niachie mimi,nakuomba.”
Kwa hofu na mashaka ilibidi Kassim,aweke mguu kati na kuweka gari kando.Gari la nyuma yake pia likasimama,akashuka mwanamme mmoja mrefu kiasi,mwenye rangi ya maji ya kunde.Akatembea mpaka karibu kabisa na gari ndogo aina ya Verrosa,kwa kuwa vioo vilikuwa vyeusi sana hakuweza kujua ni nani anaendesha gari.Akagonga kioo!Kikashushwa taratibu,sura ya Kassim ikaonekana,pembeni kushoto yupo Hajrath.
“Tonny,mambo”
Hajrath akawa wa kwanza kusalimia.
“Poa shem,nilijua upo na Ahmed.Yuko wapi?”
“Ndio tunaenda kumchukua,amenipigia simu.Si unajua mimi siwezi kudrive usiku.By the way.Huyu ni shemeji yangu,mdogo wake na Ahmed,anaitwa Kassim”
Hajrath aliongea kwa pupa,kwaniya ya kutaka Tonny aondoke ili yeye na Kassim wamalize walichokianza.
“Niaje broo”
Tonny,akamsalimia Kassim.
“Poa”
“Anywei.Nitamcheki kwenye simu kesho.Msalimie sana”
Hata kabla ya Tonny kumalizia kuaga vizuri,Kassim akawa tayari amepiga gari moto na kuliondosha mahali hapo kwa kasi.
Aliamini kuendelea kubaki eneo hilo,wenda ungeibuka msala mwingine kwani Tonny angechungulia kidogo ndani angeuona mwili wa Ahmed na huo ndio ungekuwa mwisho wao!Ndani ya gari kukatokea ukimya wa ajabu,Kassim alikuwa akitafakari ni wapi, akautupe mwili huo ili mtu yoyote yule asijue ulipo.Hapo ndipo alipopata wazo la kwamba waende kumtupa katika pori lenye miti lililokuwa Mbweni,kwa kufanya hivyo waliamini hakuna mtu yoyote Yule angejua ni wapi Ahmed alipo.

Dakika kumi baadaye, wakawa tayari wamelifikia pori hilo,wakazima taa na kushuka,wakateremsha gunia na kuushusha mwili wa Ahmed chini,hapo ndipo walipoanza kuuweka ndani ya gunia huku wakitizama huku na kule kama wanaonwa.
Walivyohakikisha wamemaliza shughuli hiyo nzito,wakalifunga gunia kwa juu na kamba,wakalibeba gunia.Wakatembea nalo mpaka katikati kabisa ya pori,lililokuwa lina giza kuliko kawaida,wakamtupa chini.
“Naomba hii ibaki kuwa siri yetu”
“Sasa tutasema nini?Akiuliziwa?”
“Nitakwambia cha kufanya,tuondoke”
Hakuna hata mmoja kati yao aliyekubali kuamini kwamba Ahmed,amefariki tayari. Mbali na hapo wao ndio walikuwa wakandarasi wa kila kitu kutokea,kwa haraka wakatembea mpaka walipoacha gari,wakaingia na kuondoka zao kwa kasi!
Gunia,lililokuwa limetupwa porini ndani yupo Ahmed,lilianza kutingishika kwa nje, baada ya dakika thelathini kupita tangu liwekwe eneo hilo, kumaanisha ya kwamba,Ahmed hakuwa
amekufa kama walivyodhani.

********
TANZANIA ARUSHA(Ngulelo) 1999.

“Darling,unajua wewe ni mzuri sana”
“Ahsante baby”
“Nakupenda,naomba usije ukaniumiza”
“Siwezi mpenzi”
Haukuwa utani hata kidogo,ungebahatika kumuona mwanamke anayesifiwa wallah,usingebisha.Ungekiri kwamba mwanamke huyo hana kasoro yoyote ile,ni wazi kabisa Mungu alimpendelea katika uumbaji wake.Rangi yake haikuwa ya kung’aa, bali maji ya kunde,hakuwa mwenye macho makubwa wala madogo bali ya wastani lakini wakati wote yalikuwa yamelegea,midomo yake ndio usiseme,alikua ana ‘lips’ pana.Zilizofanya mwanamme yoyote Yule atamani kuzinyonya.Kuongezea hapo,alikuwa amejaaliwa katika maumbile.Hiyo ndio ilifanya mwanamme yoyote rijali ageuze shingo yake nyuma, endapo akipita mbele yake.Ahmed,alikuwa amelala kitandani,anamuangalia Mpenzi wake jinsi alivyoumbika,mbaya zaidi alikuwa ametoka kuoga,amevaa kanga moja tena imelowana.Hiyo ikafanya damu yake ianze kumwenda mbio kwa mara nyingine.
“Hajrath”
Ahmed,akaita huku akimeza mate ya uchu.Japokuwa alikuwa ndege ni wake lakini alionekana kuwa na ugwadu kana kwamba ndio siku yake ya kwanza kukutana naye kingono!
“Abee Mpenzi”
Hajrath,akaitikia.Namna alivyozungumza ni wazi kabisa ungedhani ana mapozi ama maringo,kumbe ndivyo alivyo.Akamuangalia Mpenzi wake aliyekuwa bado yupo kitandani,amejifunika na shuka hana nguo hata moja.
“Njoo nikwambie kitu”
“Uniambie nini?Huna lolote,najua unachokitaka”
Kwa hali ilivyokuwa na jinsi ambavyo Ahmed,alivyokuwa akimuangalia Mpenzi wake, ilionekana wazi kabisa kuna zoezi pevu anataka kulifanya.Hajrath aliligundua hilo, baada ya kuona shuka alilojifunika Ahmed limetuna kwa mbele,kama mwanamke mtu mzima akajua ni kitu gani,anatakiwa kukifanya.Akadondosha kanga chini na kupanda kitandani,akamsogelea Ahmed midomoni wakaanza kulana denda.Ilikuwa ni wazi kabisa kila mtu,alikuwa ana moto kwani walianza kushikana huku na kule taratibu sana,wakabinuana kitandani huku wakikwaruzana migongoni.Hajrath,akawekwa chali,akawa anaangalia juu kwenye paa.Hapohapo,Ahmed,akajisogeza kidogo na kutoa ulimi wake,akaugusisha kwenye chuchu za Hajrath.
“Aaaah! Aaaaah! Aaaaah!Mmmh Aasssh Beeeeibiii”
Kilichosikika hapo ni miguno na Hajrath hakuwa anajielewa tena,zaidi ya kufumba macho na kuvuta vuta mashuka,ni dhahiri kwamba alikuwa yupo katika dunia nyingine ya huba!


Haukuwa utani hata kidogo kwani Hajrath,aliota mbawa akajiona yupo juu angani anaviangalia viumbe hai vyote kwa chini.Hali yake ilikuwa mbaya kabisa,bila kuulizwa akashika tango la Ahmed na kuliweka ndani ya mgodi wake,kilichofuata hapo!Mimi nawewe hatujui.

*******
“Oyaa,Tizzo!”
“Nambie”
“Hivi Ahmed,ndio anamkaza Hajrath?”
“Hajrath gani?”
“Leo humjui Hajrath?”
“Namjua ndiyo,inawezekana ninayemfahamu mimi siyo huyo unayemzungumzia”
“Hajrath,wewe humjui Mzee Baba.Anayechukua Civil Engineering”
“Si Yule mwenye matako matako makubwa?”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaaa!Ndio huyohuyo”
“Sasa unacheka nini?”
“Namna ulivyosema hayo matako,jinsi ulivyoniangalia.Sasa ndio huyo bwana,leo si nimemkuta anatoka getoni kwa Ahmed”
“Sio kweli,utakuwa umemfananisha”
“Sasa mimi nisimjue Hajrath,kweeli?”
“Sio bwana”
“Kama hutaki basi,ndio hivyo sasa.Ule mzigo wa Ahmed”
Mazungumzo hayo yaliendelea!Siku hiyo, skendo hiyo ilienea ya Msichana huyo Hajrath, kuonekana anatoka chumba alichopanga Ahmed yaani getoni,uvumi huo ukasambaa kwa kasi kama moshi wa kifuu.
Haikuwezekana hata kidogo kwa mwanafunzi yoyote Yule kukubali ya kwamba Hajrath,kaonekana ametoka chumba cha Ahmed,kila mwanafunzi wa chuo hiko cha Makumira aliyepewa habari hizo alionekana kushtuka na kupigwa na butwaa la waziwazi.
“Hapana,labda sio yeye.Mimi nakunya kwa mafungu mafungu hapa mpaka Ngaramtoni”
Jamaa mmoja alisikika akibisha na kuwaambia wenzake, baada ya kupewa habari hizo ambazo yeye alizichukulia kama uvumi.
“Sasa unachobisha ni kitu gani?”
“Yule demu,katosa watu kibao hapa chuoni.Alafu ni mgumu kinoma yaani,sio mrahisi namna hiyo!”
“Watu na nyota zao arifu”
“Embu nenda,mimi nitabisha mpaka kufa kwangu”
Ligi ilikuwa kubwa,bado wanafunzi wa chuo cha Makumira waliendelea kubisha na wengine waliweka mpaka dau la pesa!Hakuna mtu yoyote aliyekuwa tayari kukubali kwamba Hajrath ana mahusiano ya kimapenzi na Ahmed.Mbali na msichana huyo kuwa mrembo chuoni hapo,kilichomfanya azidi kuwa wa kipekee ni swala moja tu.Hakuwa kama wasichana wengine;micharuko, wapenda mabuzi na madanga!Yeye alikuwa ni wa tofauti kabisa na hata marafiki zake wa karibu walivyomfuata na kumuuliza kuhusu skendo hiyo ya kutoka na Ahmed kimapenzi,akajifanya kushtuka.
“Mimi?Ahmed?Ahmed yupi?Nilikuwa kwake?Lini?”
Hajrath,akaonekana kuwa mkali siku hiyo baada ya kuulizwa swali hilo,hiyo ikafanya marafiki zake wasiendelee kumuuliza zaidi.
“Alafu nimezisikia hizo habari,sipendi nimesema.Sitaki kabisa.Mnikome,tusifuatiliane”
“Lakini hatukukuuliza kwa ubaya shoga”
“Ndio,kwani hakuna mada nyingine.Course work hamjafanya bado kazi kuuliza habari zangu”
Hatimaye wakawa wamekatwa ndimi,licha ya Hajrath kuendelea kubisha lakini iliendelea kuaminika ya kwamba yupo kimapenzi na Ahmed, mwanamme aliyekuwa mwaka wa mwisho katika chuo hicho.Siku hiyo Hajrath alikasirika na kuondoka eneo hilo lakini huku nyuma alivyokuwa akitembea alikuwa akitingishika, jambo lililozidi kuwatoa wanaume udenda,alivyofika hostel ndani ya chumba chake akafunga mlango na kumtafuta Ahmed hewani.
“Baby mambo”
Akasalimia kwanza,ili kumjulia hali kabla ya kutaka kusema dhumuni la simu hiyo.
“Poa,vipi?Upo wapi baby?”
“Nipo hostel”
“Alaf baby….”
“Yes baby”
“Kwanini sasa umewatangazia watu kuwa sisi ni wapenzi?”
“Mimi?Lini?”
Ahmed badala ya kujibu swali,akaibua swali likawa swali juu ya swali.
“Chuo kizima sasa kinajua”
“Mimi sijasema chochote,kwani Darling ni vibaya watu kujua?”
“Sio vibaya”
“Sasa mbona kama umekasirika?”
“Sijakasirika Darling”
“Kwani unataka mapenzi yetu yawe siri?”
“Ikiwezekana mpenzi”
“Kwanini?”
“Basi tu”
Kuanzia hapo,ukimya ukatawala wa kama sekunde moja nzima.Ilielekea Ahmed alikuwa akitafakari kitu fulani ndani ya ubongo wake,picha iliyomjia mbele ni kwamba wenda Hajrath ana mwanamme mwingine, ndiyo maana alitaka yeye awekwe kuwa siri.
“Halloo baby”Hajrath,akaita simuni kwa sauti ya chini baada ya kuona ukimya huo!
“Halloo Honey”
“Nakusikia Hajrath”
“Mbona huongei?”
“Sasa unataka niongee nini?Sina cha kuongea,amua unavyotaka”
Staili aliyotumia kujibu Ahmed ilimfanya Hajrath,aumie.Akajitahidi kum-bembeleza lakini swala hilo halikuwa rahisi,mbaya zaidi simu ilikatwa bila hata yeye kujielezea vizuri.Angefanyaje?Wakati alikuwa akimpenda kweli Ahmed,japokuwa walikuwa hata hawajafikisha mwezi mmoja katika penzi lao.Hapohapo,akafungua mlango na kutembea kwa hatua za harakaharaka mpaka stendi ya mabasi. Safari ya kutoka Usariva mpaka Ngulelo,ilimchukua dakika arobaini na tano nzima,hapo aliteremka kwa kasi na kuanza kutembea,ilikuwa ni lazima akaonane na Ahmed,amuweke kitako wazungumze vizuri.
Isingewezekana kwa yeye kupata usingizi siku hiyo hata kidogo bila ya kuzungumza na Kipenzi cha roho yake,ilikuwa ni lazima mtima wake uwe mweupe, ndiyo mambo mengine yaendelee.Akiwa anatembea barabarani alikuwa akiwaza vitu vingi sana kichwani mwake,hakuelewa ampe sababu gani Ahmed ili amuelewe kwani kwa wakati huo hakutaka penzi lake lijulikane kwa mwanafunzi yoyote Yule,mpaka muda muafaka utakapofika.Mwendo wa mita kama kumi,akawa ametokea kwenye uwazi mkubwa wenye miti ya michongoma,akaingia kichochoroni.Mbele yake,akaona milango ya vyumba tisa vimepangana,akapitiliza mpaka cha mwisho ambacho Ahmed,ndipo alikuwa amepanga.Akasimama na kuanza kutafakari.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Hatimaye,akagonga!
“Ngo! Ngoo! Ngooo! Ngoooo!”
Akagonga tena kwa mara nyingine baada ya kuona kuna ukimya umetawala.Akaamua kusubiri kwa kukaa chini,juu ya kibaraza.Hakutaka kubanduka siku hiyo mpaka azungumze na Ahmed,amuombe msamahaa japokuwa hakuelewa ni kosa gani amefanya.Mapenzi aliyokuwa nayo juu ya mwanamme huyo ilifanya mpaka ajione amefanya kosa la jinai kumkasirisha, ndiyo maana alikuwa yupo radhi kusubiri eneo hilo mpaka usiku,ikiwezekana angelala hapohapo.Kwake yeye ilikuwa potelea mbali.Lisaa limoja,likawa limekatika kiutani utani akiwa bado anamsubiri Ahmed arejee,mbaya zaidi alivyomtafuta hewani simu yake haikupokelewa,akajaribu kutuma meseji lakini pia hazikujibiwa.
“Ahmed,p’se pokea simu.Natk kuzungumza nawewe.Nisamehe bebiii”
Hajrath alituma ujumbe huo mfupi pia haukujibiwa,akapiga simu.Haikupokelewa vilevile!

*******
Haikujulikana ni jambo gani lilimchukiza namna hiyo.Wivu na hasira vilimpanda kwa wakati mmoja,baada ya kuzungumza na Hajrath,moyo wake uliuma ajabu.Akahisi ni lazima kuna mchezo atakuwa anachezewa na Hajrath!
“Mapenzi ya siriiii?”
Ahmed,alijiuliza mwenyewe na kushindwa kupata jibu la swali lake kwa muda huo.Bado kauli ya Hajrath ilimpitia kichwani na kumfanya azidi kupandwa na jazba!
“Haiwezekani,hapa kuna kitu na lazima nitajua tu”
Baada ya kutafakari kwa muda wa kama dakika mbili nzima,ghafla akapata wazo kabambe!Hapohapo,akachukua simu yake na kuanza kutafuta majina mpaka alipolifikia jina ‘GEBO’baada ya kuliweka jina hilo sawa,akaipiga.
“Gebo,mambo vipi kaka”
Ahmed,akasalimia.
“Fresh,nambie Ahmed”
“Uko wapi?”
“Nipo Chuo”
“Ninaweza nikakuona leo?”
“Saa ngapi?”
“Sasa hivi,ikiwezekana”
“Wapi?”
“Tengeru,pale pa siku ile”
“Kuna nini?”
“Kaka,nitakwambia”
“Haina noma,ngoja nikaweke begi hosteli.Nitakuja hapo”
“Poa poa”
Ahmed,hakutaka kitu kingine zaidi kwa rafiki yake aliyeitwa Gabriel bali ni ushauri,akiamini kwamba angeweza kupata mawili matatu juu ya kitu gani akifanye,bila kupoteza wakati.Akafunga chumba chake na kuanza kutembea kuelekea stendi ya mabasi.
Jazba ilimkaba kiasi kwamba alitamani afike Tengeru,aonane na Gabriel atoe dukuduku lake.Kama mwanamme hakutaka kutoa maamuzi ya hapohapo ilikuwa ni lazima apewe ushauri na mwanamme mwenzake,kwani katika jambo hilo hakupaswa kukurupuka hata kidogo!Alichoshukuru ni baada ya kuona daladala ya Usariva,hakupoteza wakati,akarukia na sekunde tisa baadaye dereva akaondosha gari.Baada ya kupita Kwa Mrefu,Ahmed akaanza kujiandaa kushuka kwani kituo kilichokuwa kinafuata kilikua ni Tengeru.
“Konda Tengeru”
Baada ya kuongea hayo,akajisachi mfukoni na kutoa nauli.Alivyoteremka kutoka ndani ya daladala.Akavuka barabara upande wa pili,ambapo hapo alipitiliza mpaka sehemu iliyokuwa na ‘grocery’ ndogo,akakaa na kuanza kumtafuta Gabriel hewani kwa mara nyingine!Haikuchukuwa muda sana,wakaonana na kusalimiana.
“Nini shida kiongozi?”
Gabriel,akahoji baada ya kumuona Ahmed hayupo kwenye mudi nzuri.
“Nitakwambia.Leo hupigi vyombo?”
“Napiga,niagizie basi.Maana nina kiu kweli Mkuu”
Muhudumu akaitwa muda huohuo.
“Niletee Faru John,mkubwa”
Dakika moja baadaye,mzinga mkubwa wa Konyagi ukawekwa mezani.Kwa Ahmed,aliagiza soda!Ahmed taratibu,akaanza kufunguka jambo lililofanya kikao hiko kidogo kitokee, japokuwa alianzia mbali kidogo.
“Unamsemea,Hajrath yupi?!”
Bwana Gabriel,haikufahamika kama anauliza ama amepigwa na mshangao sababu staili aliyotumia kumuangalia Ahmed haikuwa ya kawaida.
“Mwaka wa pili”
“Yupi huyo?”
“Kwani kuna Hajrath wangapi?”
“Huyo ninayemjua mimi ndio huyo huyo.Kwani ndio huyo unayemsemea wewe?”
“Ndio”
“Ndio gashi wako?”
“Ni shemeji yako”
Hapo,Gabriel akafungua chupa ya Konyagi na kumimina kwenye glasi yake mpaka ilivyofika nusu,akaiweka glasi mdomoni alivyoitoa akawa amekunja sura kama mtu aliyekula ndimu changa.Akaweka glasi chini,ikiwa haina kitu!Akamtizama Ahmed kwa kitambo kidogo!
“Anakwambia Mapenzi yenu yawe siri?Yaani hujui tu ni kwanini?”
“Hapana sijui”
“Mkuu,achana na huyo demu.Ni Malaya,ni kicheche hafai.Usione pale chuoni mtaratibu,ana mabalaa yuleee.Ni malayaaa mchafu.Hata juzi nilivyosikia ni demu wako.Nilitaka nikufate nikwambie.Kakaaa Yule demu maharage ya Mbeya,maji mara mojaa”
Maneno aliyokuwa anazungumza Gabriel,yalikuwa ni kama mishale ya moto!Hiyo ikafanya mpaka Ahmed ajute kumuita kwani Bwana Gabriel aliendelea kutoa maneno makali mno.
“Yule manta hakufai hata kidogo,mademu mbona wapo kibao mshkaji wangu.Kuna akina Veronica Denis,Asimwe Kato.Vigoli kibao vipo,kuna vitoto vibichi vipo year one.Wewe unahangaika na huyo bibi.Atakuuwa kwa presha,achana naye”
Gabriel,akazidi kumkandia Hajrath.



Maneno aliyokuwa anaambiwa Ahmed,yalikuwa ni mazito mno kuyasikia.Sio hivyo tu, bali yalikuwa niya kuchoma mtima.Hata siku moja hakutegemea kwamba angekuja kuelezwa vitu kama hivyo kutoka kwa mtu yoyote yule.Alitokea kumuamini sana Hajrath, japokuwa walikuwa wana kipindi kifupi tu tangu waingie katika mahusiano ya kimapenzi.Jambo moja ambalo mwanaume huyu alikuwa dhaifu,akipenda huwa anapenda kweli,sambamba na hayo anaingia na miguu yote miwili.Sura ya mwanamke aliyempenda kuliko wanawake wote Duniani, ikaanza kumjia.Akajisikia uchungu ajabu hasa alivyojenga picha kichwani kwake siku hiyo alivyosalitiwa mbele za watu.
“Jaqlin Lucian”
Ahmed akasema kwa uchungu,Hajrath akawa amemkumbusha vitu vingi sana, tayari alimtonesha kidonda kilichoanza kukauka!Akaanza kuwachambua wanawake wote aliowahi kuwa nao katika mahusiano,akaja kugundua kitu kimoja.Hakuna mwanamke muaminifu hata kidogo!
“Siwezi kuwalaumu,wanawake hawaridhiki.Kabisa yaani”
Ghafla akili yake ikasafiri na kupiga rivasi kipindi anasoma shule ya Msingi,Uhuru Mchanganyiko!Akamkumbuka msichana mmoja anaitwa Monalisa Japhet,alivyomsaliti kisa tu aliona mvulana mwingine ana kichongeo kipya,akatoswa kwa staili hiyo.
“Sikilizaaaa.Nikwambie Jembe!Yule demu piga chii,piga chiniii babaaake.Kuna mademu kibao hapa Chuo,wanakufagilia ile mbaya.Sitaki kuamini umri kama huu bado unateeeswa na mapenzi shenziii”
“Gebbo,nampemda Hajrath”
“Utakufa na presha kenge wewe.Achana naye,ujue ngoja nikupe siriii ya mademuu.Mwanamke haridhiki,unaweza ukawa unampa kila siku mia tano,lakini akatokea mbwiga mmoja,akampa Elfu tano.Na siku hiyohiyo,akamdinya. wanawakee wotee matakoo yao kasoro Mama zetu”
Ahmed hakutamani kusikia maneno hayo hata kidogo,wakati mwingine aliona ni bora asingemtafuta Gabriel ili amshauri.Wivu ulikuwa umemkaba kohoni,hakuelewa angemfanya nini Hajrath endapo angeonana naye,ana kwa ana!Mapenzi yao tangu yaanze hayakuwa yametimiza hata mwezi mmoja,hiyo ilimaanisha bado yalikuwa motomoto.Moyo wa Ahmed ulijawa na chuki kwani tayari penzi lake lilikuwa limeingiliwa na jini kisirani.
Siku hiyo alipanda daladala akiwa mwenye mawazo chungu mzima akiwa anarudi geto kwake,daladala lilivyofika Ngulelo,aliteremka na kuanza kufata barabara ya vumbi, ambayo ilimfikisha mpaka kwenye kichochoro kidogo,kinachoelekea eneo analoishi.Sio siri kichwa chake kizima kilijaa Hajrath tu,yale mahaba yote yakawa yameisha,akawa hana hamu tena na Hajrath.
Zaidi na hayo yote hata alivyokuwa anaona anapigiwa simu na Hajrath,aliipotezea!Kitu kilichomfanya apandwe na jazba zaidi ni baada ya kumuona Hajrath,mbele yake amekaa nje ya mlango, chini.Hakusema chochote zaidi ya kutoa funguo na kuingiza ndani ya kitasa!
“Ahmed,ina maana hujaniona au?”
Hajrath ilibidi aulize,hakumzoea kumuona mpenzi wake akiwa katika hali kama hiyo.
“Ahmed,naongea nawewe.Una nini?Mbona hupokei simu zangu mpenzi wangu?”
“Simu gani?Achana namimi”
Ahmed,alisema kwa ukali kidogo huku akihangaika kufungua mlango,hakutaka kumuangalia Hajrath usoni,aliogopa kufanya hivyo kwani angefanya kitu kibaya mno!Alielewa namna alivyokuwa mwenye hasira na mwenye mkono mwepesi,siku hiyo kulikuwa kuna kila dalili mbaya za yeye kuachana na mpenzi wake kwani siku zote dalili ya mvua ni mawingu.
“Ahmed,naomba tuongee”
“Uongee na nani?Ahsante Mungu,nimekujua mapema”
“Ahmed,mbona sikuelewi?”
Swali hilo kutoka kwa Hajrath lilimfanya Ahmed,aachane kwanza na mlango.Akamgeukia Hajrath na kumtizama machoni kwa sekunde kama moja.Jicho lake halikuwa la kawaida,lilikuwa jekundu kwa ndani, mbaya zaidi lilikuwa moja la kushoto.Mkono wake ulikuwa ukitetemeka kama mtu mwenye homa ya usiku.Hajrath aliliona hilo,akaanza kuingiwa na uwoga kwani hakuwahi kumuona Ahmed akiwa katika hali kama hiyo ingawa hawakua wamejuana mapema kiasi cha kumfahamu kiundani zaidi.
“Ahmed”
Hajrath akaita tena, akiwa mwenye wasiwasi kwa mbali,alihisi moyo wake unamuuma ajabu.Ni dhahiri kwamba alimpenda mwanaume huyo kuliko kitu chochote kile chini ya jua la Mungu.
“Naomba kuanzia leo,iwe mwanzo na mwisho.Kuliita jina langu”
kwa mara ya kwanza,Hajrath alidhani wenda ni utani lakini haikuwa hivyo,alichofanya Ahmed ni kuingia ndani na kufunga mlango kwa ufunguo.
“Ahmed,fungua mlango”
Usingekubali hata kidogo ungepita na kumuona mrembo kama Hajrath,akiwa nje ya dirisha anaita huku machozi yakianza kumlenga.Ni wazi kwamba kila mwanamme aliyemuona alim-mezea mate,lakini hakuna hata mmoja kati ya hao aliyefanikiwa kumnasa isipokuwa Ahmed peke yake.Huyo ndiye mwanamme aliyeamua kuwa naye katika ulimwengu wa mapenzi.
Ndiyo maana baada ya muda mfupi tu tangu wajuane,akakubali kumvulia nguo yake ya ndani wakafanya ngono.Kwa kitendo hiko alikitafsiri moja kwa moja,tayari amekufa ameoza.Ndiyo maana mpaka wakati huo alikuwa dirishani kwa Ahmed,anamuita bila mafanikio yoyote yale.
“Ahmed,I’m so sorry”(Ahmed,nisamehe)
“Hajrath,toka.Nitakumwagia maji ya moto!Nadhani hunijui vizuri”
Sauti hiyo ya Ahmed ilisikika kutokea ndani ya chumba chake,haikuwa na chembe ya mzaha hata kidogo.Hiyo ilimfanya Hajrath aanze kulia machozi.

*******
Kila kitu kikawa kimevurugika katika maisha yake,sio upande wa masomo tu.Hajrath,alikumbwa na msongo wa mawazo.Kila siku alimuwaza Ahmed, hakuweza tena kujisomea kama alivyofanya kila siku na wanafunzi wenzake.Japokuwa alijitahidi kuificha hali hiyo isitokee lakini wapi.Jambo hilo likawa kama pembe la Ng’ombe,halifichiki.Siku ya kwanza ilipita bila kugundulika lakini siku iliyofuata marafiki zake wawili wakaingia hostel,chumba anacholala kumuuliza.Kulikoni?Maana haikuwa kawaida ya rafiki yao kusononeka namna hiyo na kutega vipindi darasani.Ucheshi wake pamoja na kuongea na watu, kulifanya ukimya wake uzue alama ya viulizo.
“Kulikoni,shoga?”
Mpangw’a akahoji.Yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia chumbani,alizungumza bila hata ya kuweka begi lake chini.Hali ya rafiki yake ilimshangaza sana.
“Nimepumzika tu”
“Hujaingia darasani tangu jana.Vipi mwenzetu?Unaumwa?”
“Ah wapi,uchovu tu”
“Hapana Hajra,una nini?Sio kawaida yako”
Msichana huyu aliitwa,Necka Golden.Nayeye hakuwa nyuma alitaka kumdadisi rafiki yake kipenzi.
“Nipo sawa lakini,vipi class.Nani kaniulizia?”
Hajrath,alisema na kuuliza huku akimtizama kila mmoja wapo,akajivuta kutoka kitandani na kukaa sawa!Majibu aliyowapa marafiki zake na hali yake vilikuwa ni vitu viwili tofauti.Ni wazi kwamba, moyo ni sawa na kichaka chenye giza nene,kuna jambo lilikuwa linamsumbua Hajrath lakini hakujuwa ni kwa namna gani,aliseme.Alitamani kuwaambia rafiki zake lakini hakuelewa aanzie wapi kwani tangu mara ya kwanza alikuwa akiwaficha kuhusu uhusiano wake na Ahmed.Hiyo ilimfanya abaki njia panda,kuna nafsi moja ilimwambia aseme wenda angepata ushauri lakini upande wa pili wa nafsi ulimpiga ‘stop’
“Temba kakuulizia”
“Kasema nini?”
“Alitaka kutoa test,nadhani alivyogundua haupo akawa anazuga”
“Mmh,nawewe Necka,mpana sana.Umejuaje?”
“Kusoma hatujui hata picha tusione,inawezekana vipi?Nani asiyejuwa Temba anakutaka sema anashindwa kukwambia tu”
“Hayo yako sasa”
“Ndio ukweli huo na nina uhakika kakutongoza”
“Ah wapi,sio kweli”
“Hajrath,tatizo lako wewe msiri sana.Jambo hilo litakucost”
“Bwana wee,tuachane na hayo”
Hadithi na stori za hapa na pale ziliendelea.Niya ya Hajrath ilikuwa ni kutoa mawazo lakini jambo hilo lilionekana kufeli kwani kila baada ya sekunde mbili sura ya Ahmed,ilimjia.Akajiona alivyokuwa naye,wanacheka wote.Ghafla akajiona alivyokuwa juu ya kitanda na mwanamme huyo!Kifupi, hakutofautishwa na mtu anayetizama sinema ya kusisimua,picha zikawa zinajichora na kutengeneza taswira kwenye ubongo wake.Akasahau kama yupo na marafiki zake,akili yake ikawa imesafiri maili nyingi sana,akabaki ameduwaa.Mazungumzo ya marafiki zake,hakuyasikia tena wala kuchangia lolote,mbele yake alimuona Ahmed tu.
“Mamiii,Hajrath.Haaaash hallooo”
Mmoja wa marafiki zake alijaribu kumuita na ilionekana alikuwa akimuongelesha lakini yeye hakusikia,ikabidi amtingishe.
“Abee,Yes nawasikiliza.Temba hawezi bwana kufanya kitu kama hiko”
Hajrath,akawa kama amekurupushwa kutoka katika usingizi mzito sana.Hiyo ilifanya mpaka wenzake wamshangae!Hiyo yote ni kutokana na wao kuongelea kitu kingine,stori ya Temba ilikuwa ishapita tayari!
“Hajrath,unawaza nini?”
“Sio kitu”
Alijaribu kuwadanganya lakini hilo liligundulika, sababu machozi yalikuwa tayari yanaanza kumlenga,tukio hilo liliwashtua marafiki zake, waliokuwa wamemzunguka.
“Hajrath,una nini?”
Wote wakajikuta wana muuliza kwa pamoja huku wakimsogelea karibu kabisa,wakaketi juu ya kitanda chake na kumtizama usoni.
“Nini kinakusumbua?Sisi ni marafiki zako.Usiwe msiri namna hiyo”
Huyu aliitwa Amney,alizungumza kwa upole na utulivu wa hali ya juu sana.Hata hivyo katika kikundi hiko cha wasichana hawa watatu,Amney ndiye aliyeonekana kama ndiye mkubwa wao, sababu tu alikuwa ana busara na mtoa ushauri,hiyo ilifanya wampachike jina na kumuita, Mama ushauri.
“Am..ney naum..ia”
Hajrath,akazungumza kwa kwikwi,hapo ndipo alipoanza kumwaga machozi mfululizo.Kazi ya marafiki zake ikawa ni kumpiga piga mgongoni ili atulie lakini ikawa kinyume chake,akazidi kulia kwa uchungu.
“Nyamaza mamii,una shida gani?Sisi ni kama ndugu zako.Shika kitambaa jifute machozi”
Sekunde saba baadaye Hajrath akawa ametulia,anatafakari aanzie wapi amalizie vipi jambo hilo la mapenzi, linalomtesa mtima wake na kumnyima raha ya Maisha.
“Mapenzi yananitesa”
Jambo hilo lilimshtua kila mtu aliyemzunguka.
“Mapenzi yamefanya nini?”
Necka akamdaka na swali sambamba na mshangao!
“Ahmed ananitesa”
“Ahmed?Ahmed?Ahmed huyuhuyu?”
“Ndio”
“Kakufanya nini?”
Hakukuwa na sababu nyingine yoyote ya kuendelea kubaki na siri hiyo kifuani,ilikuwa ni lazima aseme kila kitu kuanzia A-Z,tena bila kuficha chochote kile,akawaambia kila kitu kilivyokuwa na mpaka walipofikia.
“Hash,mbona ulituficha sasa?Anyway,usikubali hata kidogo!Mfuate Ahmed umwambie ukweli,ngoja nina namba zake hapa.Subiri nimpigie sasa hivi”
Amney,akatoa wazo.
“Umpigie? Umwambie nini sasa?”
Mpangw’a akaonekana kupinga hoja hiyo.
“Nimwambie aje hapa”
“Kabla ya yote inabidi tumfuate tumuulize,nini tatizo”
“Mimi nina amini anachozungumza Hajra,ni kweli”
“It doesn’t make sense,yaani kisa tu.Ulisema unataka mapenzi ya siri?Hainiingii akilini”
“Ukiwa una maana gani?”
“Alikuwa ana tafuta sababu tu,ana demu mwingine.Nakwambia ukweli”
“Lakini hauna uhakika”
“Picha,linaonekana kabisa.Mimi sio mgeni wa mapenzi.Wanaume mimi nawajua!Haswa haswa mbuzi wa chuo cha Makumira,wanaume wa hiki chuo wote Malayaaaa”
Gafla,ukaibuka mgogoro mkali mno!Huyu alisema hiki huyu alidakia kile, mwisho wa siku walikubaliana ya kwamba Ahmed afatwe na kuulizwa nini tatizo.
Katika warembo hao watatu,mmoja kati yao hakuonesha kuwa na furaha kabisa.Hasa aliposikia jina la Ahmed,kichwani kwa Necka Golden kulipita vitu chungu mzima.Hakuwa ana uhakika kama wanamzungumzia Ahmed,anayemfahamu yeye.
“Niacheni mimi nikaongee na huyo Ahmed”
Necka Golden,baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kidogo akaibuka na wazo hilo.Kila mtu akamgeukia yeye!
“Utaongea naye nini?”
“Nitamwambia ukweli,ni rafiki yangu”
“Utazungumza naye leo?”
Hajrath,akauliza huku akiwa kama mtu aliyerejewa na matumaini.
“Ndio,leo leo.Tena nikitoka hapa”
“Mwambie,nampenda sana.Naumia kwa ajili yake, please please Necka”
“Hilo limeisha”
Necka Golden,akamuhakikishia rafiki yake kwamba kila kitu kitaenda sawa na Ahmed atarudi tena kwenye himaya yake ya mapenzi.
Necka Golden,alikuwa ni msichana mwenye rangi ya kitasha,mfupi kiasi.Macho yake yalikuwa ya duara,hata yeye alikuwa ana mapozi fulani ya kutembea!Siku hiyo Hajrath akahisi kama ameutua mzigo wa kilo kumi kichwani,kitendo cha kuhakikishiwa kwamba Ahmed atarudi tena kwake ilikuwa ni sherehe kubwa moyoni,akatamani asimame ashangilie kama mashabiki wa Simba wanavyoshangilia wakiwafunga Yanga ama Kinyume chake.
“Necka,ahsante sana”
Shukrani alizotoa Hajrath,hazikuweza kuelezeka kiwepesi.
“Usijali,sisi ni marafiki.Jioni nitakupa jibu”
“Namba yangu si unayo?”
“Eeeh Shosti,nitakosaje namba zako kwenye simu yangu?”
“Jioni nitakupigia”
“Okay”
Wote,wakatoka ndani ya chumba anacholala Hajrath,wakimuachia kazi, Necka Golden ya kuzungumza na Ahmed.

********
Kumpa kazi Necka Golden ya kuzungumza na Ahmed,ilikuwa ni sawa na kumkabidhi fisi bucha alinde minofu.Kwani katika wasichana wa chuoni hapo, waliokuwa wanamtamani Ahmed kimapenzi,ni huyu Necka Golden, alikuwa ni miongoni mwao!Kitendo cha Hajrath kutaja jina la Ahmed kwamba ni mpenzi wake,lilimtia kichefuchefu cha kutapika.Akajikuta anaanza kumchukia Hajrath,wivu ulimkaba kohoni!
“Huyu Malaya,anachekesha.Subiri nimuoneshe picha.Anajifanya mzuri sana!”
Necka,aliwaza huku akitembea harakaharaka,akatoa simu yake mfukoni na kuanza kusaka majina, mpaka alipolifikia jina Said Sangu,akairuhusu simu itoke.
“Mtoto mzuriiiii”
Sauti ya upande wa pili,ikasikika.Baada ya simu kupokelewa!
“Upo wapi Sangu?”
“Nipo Hostel,vipi unataka kuja nini?Njoo basi ule, nimepika leo Kuku”
“Nitakuja,hivi Ahmed.Unajua anapoishi?”
“Ahmed?”
“Umenisikia Sangu,anaishi wapi?”
“Ngulelo”
“Nitumie namba zake,sasa hivi”
“Kwenye WatsApp, au?”
“Nitumie hata kawaida”
“Alafu Dp yako,kaliii hiyooo chaurembo”
“Nitumie namba za Ahmed,sasa hivi”
Ilikuwa ni lazima siku hiyo aende anapoishi Ahmed,azungumze naye kwanza.
Damu yake ilikuwa inamwenda mbio mno,moyo wake ulikuwa ukimdunda.Haikuwa hali ya kawaida kutokea,vitu vingi alikuwa akivitafakari.Hakujua ni kitu gani amwambie Ahmed,baada ya kumpigia simu.Baada ya kupiga hatua kama sita hivi,ujumbe kwenye simu ukawa umeingia.Alivyoitoa akakuta namba ya Ahmed,tayari imetumwa bila kuchelewa akaipiga hapohapo.
“Griii griiiii”
Upande wa pili wa simu,ukasikika.Simu ilikuwa ikiita,mapigo yake ya moyo yakazidi kupiga kwa nguvu!Akiwa anatafakari juu ya kitu gani akiseme simu ikipokelewa,upande wa pili wa simu ukasikika.Ahmed,akawa yupo kwenye laini.
“Halloo”
“Samahani,nazungumza na Ahmed?”
“Ndio,nani mwenzangu?”
“Mimi Necka Golden,Ahmed.Kuna mzigo wako nimepewa.Uko wapi?”
“Town”
“Tunaweza kukutana?”
“Yes,njoo Town”
“Hapana,huko siwezi kufika.Naomba tukutane kwako,nina mazungumzo nawewe pia.Please nakuomba”
“Wewe ni nani kwani?”
“Necka,Necka Golden!Second year”
“Okay,upo wapi?”
“Chuo hapa”
“Nipigie baada ya dakika kumi hivi”
“Sawa”
Moyo wa Necka Golden,ukapiga mkambo.Akatabasamu kwa furaha na kimoyomoyo akasema ‘Umekwisha Hajrath’Dakika alizopewa zilitosha kabisa kwa yeye kwenda mpaka, Hostel na kujipamba vizuri,ilikuwa ni lazima atumie nafasi hiyo vizuri bila kufanya makosa.
Kifupi siku hiyo Necka alijifananisha na Merci uwanjani,akatembea kwa mwendo wa haraka mpaka alipofika hostel.Akatoa funguo na kufungua mlango,akavua nguo kwa kasi ya umeme na kupitiliza mpaka bafuni,akaoga vizuri.Kazi ya kujimwagia maji ilivyoisha,akazama kwenye kabati kuchagua viwalo.Siku hiyo hakutaka kuvaa kiboya,alitaka kupigilia pigo za kumtingisha Ahmed.Kichwa chake kikaanza kutafakari nguo gani avae,ghafla akalikumbuka gauni lake fupi la rangi ya bluu,alilopewa zawadi na shangazi yake aliyekuwa anaishi nchini, Oman.
“Sijui,litanitosha lile gauniiii”
Necka,akajiuliza.Akalivuta gauni kutoka ndani ya kabati,akalichukua na kuanza kulipiga pasi.Jambo alilotaka kulifanya siku hiyo, lilianza kumuogopesha mpaka yeye mwenyewe lakini alipiga moyo konde.Ilikuwa ni lazima aifurahishe nafsi yake kwa kufanya jambo gumu namna hiyo na hakujali,Hajrath na marafiki zake wangemchukuliaje.
“Kwani nilizaliwa naye tumbo moja?Potelea mbali”
Necka Golden alisema hivyo huku akiwa mbele ya kioo kikubwa,anavaa gauni.Alivyomaliza,akajitizama vizuri jinsi gauni hilo lilivyomchora,akajishika kifuani vizuri na kuyaweka maziwa yake kwa juu,yakawa yanaonekana nusu yaani ‘boobs’ kwa kimombo!
“Hapa,hatoki”
Siku hiyo Necka,alijifananisha pia na Ndoano!Ahmed ni samaki,hivyo ilikuwa ni lazima amvue samaki wake, ambaye kwa muda wa siku nyingi alikuwa akimtamani.
“Mimi ndio Necka Golden”
Akajitapa kwa madoido,kabla ya kufanya kitu kingine zaidi.Simu yake,ikaita.Alivyoiangalia akagundua ni HAJRATH,anapiga.Akasonya na kuitupa kitandani!Ilivyokata,akamtafuta kwa mara nyingine Ahmed, hewani.
“Uko wapi jamani Ahmed?Bado hujatoka mjini jamaani?”
Namna alivyozungumza,hata kama ungekuwa mwanaume kauzu namna gani,ilikuwa ni lazima usisimke mwili.Necka,alizungumza kwa sauti ya puani tena ya mahaba, akijilegeza!
“Ndio.Ndio ndio hapa Ngulelo,nitakupigia sasa hivi”
Upande wa pili wa simu ulisikika,ni wazi kwamba sauti ya Necka ilimchanganya Ahmed mpaka akapata kigugumizi cha ghafla.
“Sawa,Ahmed”
Simu ilivyokatwa,ikamuacha Necka Golden anatabasamu.Akiamini tayari ushindi ni wake!



Jambo alilokuwa anaenda kulifanya lilikuwa ni hatari sana, endapo rafiki zake wangelijua.Sio kwamba, alikuwa hana fahamu na kitu alichokuwa anaenda kukifanya,lakini hakuwa ana jinsi. Ilikuwa ni lazima asikilize nafsi yake inataka nini kwa wakati huo.Aliamini kwamba akibaki na dukuduku atapata kiungulia.Ndiyo maana, siku hiyo aliipania vilivyo.Necka Golden, hakutaka kumtongoza Ahmed siku hiyo iishie hapo,kama ikiwezekana siku hiyohiyo alale naye wafanye ngono,hayo ndiyo yalikuwa mahesabu ya msichana huyu aliyetumwa kurekebisha tofauti, kati ya Ahmed na Hajrath,lakini yeye alitaka kwenda kinyume chake.
Licha ya kutafakari juu ya mambo yote hayo,alipiga moyo konde.Akiwa katikati ya mawazo hayo,simu ikamzindua.Akapiga jicho juu ya kioo cha simu na kugundua kwamba ni Hajrath ndiye alikuwa akipiga kwa mara nyingine.Ilikuwa ni lazima apokee simu,kwani bila kufanya hivyo wenda angeanza kushtukiwa na mambo yote yangeharibika,ilikuwa ni lazima kazi hiyo afanye ki- intelijensia.
“Halloo shosti”
Necka Golden,akapokea simu na kuanza mazungumzo hapohapo huku akiwa katika tabasamu la plastiki.
“Vipi?Ushaenda?”
“Bado best,ndio najiandaa hapa”
“Jitahidi sana kumwambia kuwa nampenda”
“Usijali,nitamwambia.Hayo yote niachie mimi”
“Kila la kheri”
Simu ilivyokatwa ikamuacha Necka Golden,anasonya.Alivyohakikisha amekamilisha kila kitu,akachukua tena simu ili kumtafuta Ahmed hewani,bahati nzuri ikawa kwake, simu yake ikaita kabla ya yeye kupiga na aliyekuwa anapiga alikuwa ni Ahmed mwenyewe,moyo wake ukapiga kwa nguvu ingawa hakuelewa ni kwanini hali hiyo imetokea ghafla namna hiyo.
“Halloo”
Necka Golden,alitoa sauti ya puani baada ya kupokea simu.
“Nimeshafika,nipo geto”
“Hivi ni wapi ulisema?”
“Ukifika Ngulelo niambie”
Ahmed,alikuwa tayari amefika.Yupo chumbani kwake anasubiri ugeni huo wa ghafla,hivyo kabla ya yote ilikuwa ni lazima aweke chumba chake vizuri.Ingawa chumba hiko kilikuwa kisafi,kimepangwa vizuri lakini bado hakujiamini.Ndiyo maana akaanza kuweka kila kitu vizuri,sio siri alikuwa ni mwenye shauku ya kujua ni kitu gani alitaka kuambiwa na msichana huyo anayeitwa Necka Golden,kitu kilichomfanya ashangae zaidi, hakuwa ana mahusiano naye ya karibu.Katika kutafakari sana,akakumbuka kitu kimoja tu na hicho ndicho, aliamini kilikuwa mbioni kutokea.
“Hajrath,itakuwa ametumwa.Lakini ngoja nimsikilize”
Ahmed aliwaza na kujijibu mwenyewe, hisia zake zilimtuma na kudhani hivyo sababu ya ukaribu wa msichana huyo na Hajrath.Kila kitu akakiweka mahali pake,viatu aliviweka vizuri.Meza akaiweka sehemu yake,hakuwa na haja ya kuingia chumbani kwani aliamini ugeni huo ungeishia seblen peke yake.

Alivyomaliza kila kitu alichotaka kukifanya kwa wakati huo,akajitupa juu ya sofa na kuanza kutafakari vitu vingi,hususani masomo yake.Ghafla picha ya Hajrath ikamjia kichwani kwake,maneno aliyoambiwa na Gabriel yakaanza kupita ndani ya ubongo wake,akaumia ajabu.Bado alihisi kumpenda lakini hakuwa na jinsi,asingeweza kuishi na msichana Malaya hata siku moja,japokuwa hakuwa ana uhakika lakini alijuwa fika kwamba lisemwalo lipo,binafsi hakutaka kufanya uchunguzi wa kina zaidi, akiamini angezidi kuumia.Kilichomjia ndani ya kichwa chake ni kitu kimoja tu,aachane na Hajrath.Ashikilie masomo kwani ndilo jambo lililomfanya awepo ndani ya chuo hicho,japokuwa aliamini haikuwa kazi rahisi, kumsahau Hajrath.Akiwa katika dimbwi la mawazo simu yake ikaita,hakuwa mwingine bali ni Necka Golden.
Simu hiyo ilikuwa ikimtaarifu kwamba tayari Necka Golden, alikuwa amefika kituo kinachoitwa Ngulelo.
“Unaona hiyo barabara ya vumbi,baada ya sheli hapo?”
Ahmed,aliuliza simuni baada ya kusikiliza maelezo ya Necka Golden.
“Ndio,naiona”
“Njoo nayo moja kwa moja!Tutakutana njiani”
“Sawa nakuja”
“Okay”
Simu ilivyokatika,ilimuacha Ahmed anasimama na kuanza kufungua mlango,akafunga chumba chake vizuri kwa funguo.Akaanza kutembea kutafuta barabara kubwa ya vumbi huku macho yake yakiwa mbele, tena kwa umakini kama dereva anaye endesha gari kubwa lenye makontena kwani kazi yake kubwa, ilikuwa ni kutizama huku na kule.
Kuna wasichana wengi walikuwa wakipita na wengine wanatokea upande wa barabarani lakini umakini wake ulikuwa kwa Necka Golden,kwa sura alimfahamu.Macho yake yakatua kwa mrembo aliyevalia gauni la rangi la bluu,lililokuwa fupi.Mapaja yapo nje,moyo wake ukapiga kwa nguvu.Kutokana na wenge lililompiga ilimfanya asigundue kabisa kama aliyekuwa akimtizama ndiye Necka mwenyewe,mpaka alivyosogea karibu yake kabisa.
“Oooh Necka”
Ahmed,akaita na kumpungia mkono, hiyo yote ni kwa sababu alikuwa yupo upande wa pili wa barabara hiyo yenye vumbi.Kwa Ahmed,alijisikia aibu na haya kwani wanaume wote waliokuwa kandokando yake walikuwa wakimkodolea macho ya uchu Necka Golden.Hivyo kwa yeye kumuita ilikuwa ni lazima macho ya wanaume hao wote yamjumuishe pia nayeye.
“Ahmed,mambo vipi?Nilikuwa napitiliza hivyoo,bila kuniita ningepotea”
“Na ungepotea kweli, cause simu nimeacha ndani”
“Mungu wangu sijui ingekuwaje?”
“Kupotea mara moja moja sio mbaya”
Ahmed alisema lakini alikuwa katika hali ya utani,sababu alikuwa akitabasamu.
“Twende kwangu,au tukakae sehemu tuongee?”
Ahmed,akauliza swali.Akitoa pendekezo.
“Kwako,Ahmed.Sababu nina maongezi marefu kidogo na mazito”
“Poa”
Hapo,Ahmed na Necka wakaanza kuongozana.Wakachukua barabara ya vumbi.Macho ya wanaume hayakuwaacha salama kabisa.
“Huku umehamia lini?”
Necka Golden akavunja ukimya,kutoka walipokuwa mpaka kwa Ahmed ulikuwa ni mwendo usiozidi dakika kumi lakini siku hiyo, walitumia zaidi ya dakika kumi na tano kutokana na mwendo wa Necka,sio siri alitembea kama anaogopa ardhi,mwendo wake haukujulikana kama ndiyo pozi ama alizaliwa nao.
Hiyo ilimfanya mpaka Ahmed nayeye atembee mwendo wa ajuza.
“Mwaka wa pili,semista ya kwanza”
“Mara ya kwanza ulikuwa unaishi wapi?”
“Kilala kule”
“Sasa kwanini umehamia huku?Mbali kote huku?”
“Sikutaka kukaa karibu na chuo”
“Au ndiyo uchoyo,hutaki wageni?”
Necka Golden,siku hiyo alikuwa mwenye maswali ambayo hayana maana, hiyo yote alitaka kumzoea Ahmed kwa haraka zaidi ili baadaye asipate shida,watakavyoingia geto.Kila hatua aliyokuwa anaifanya aliipangilia kwa umakini wa hali ya juu sana,alielewa kivyovyote vile asingeweza kufanikisha lengo lake, bila kuanza kumzoea ki undani zaidi,kifupi ilikuwa ni lazima aanze na moja kisha baadaye mbili ifuate.Stori za hapa na pale ziliendelea,hatimaye wakapita kwenye kichochoro kimoja, kilichokuwa na michongoma,hapo walitokea nje ya nyumba zilizopangana.Mbele kulikuwa na vyumba vingi.
“Hizi nyumba ni hostel?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Necka.
“Wapangaji”
“Hakuna wanafunzi wanaoishi huku?”
“Hapana,hakuna”
“Bora,basi namimi nitafutie chumba niwe jirani yako”
“Upo siriazi?”
“Sina utani nawewe”
“Sawa nitajaribu.Anyway Karibu kwangu”
Ahmed,alimkaribisha mgeni wake na kuanza kufungua mlango,walivyoingia ndani.Macho ya Necka yakawa yana kazi ya kuangalia kila pembe ya chumba hiko,akakumbana na friji kubwa la kisasa.
Makochi mazuri,televisheni kali, iliyokuwa ukutani imetundikwa.Kifupi chumba hiko kilikuwa kama cha mfanyakazi ama muajiriwa la wala sio mwanafunzi wa chuo,jambo hilo likazidi kumpagawisha Necka mara mbili yake zaidi,akabaki amesimama ameduwaa.
“Karibu kiti”
Ahmed,akasema huku akimuonesha moja ya sofa kwa kutumia mkono ili kuonesha msisitizo,kufuatia hapo Necka hakuwa na kipingamizi chochote kile,akaketi.
“Kinywaji gani,unatumia?”
“Chochote tu”
“Chochote ndio kinywaji gani?”
“Namaanisha,kilichokuwepo nitakunywa”
“Sawa,kuna juisi”
Ahmed,akapendekeza lakini ilielekea Necka hakufurahishwa na kinywaji hiko hata kidogo,niya yake ilikuwa apige ulabu ili akate mshipa wa aibu kichwani,aanze kujichetua na lolote likitokea pombe iwe kama ngao ya kujitetea,mbali na kuchukizwa na jambo hilo lakini hakutaka kulionesha waziwazi,kwani bado hawakuwa na mazoea sana na Ahmed,kitendo cha yeye kuanza kuropoka ropoka siku hiyo, aliamini kisingeleta picha nzuri mbele ya barafu wa moyo wake,hivyo ilibidi kidogo awe mwenye stahaaa na mnyenyekevu kuliko kitu chochote kile na hivyo ndivyo alivyoamua kuutega mtego wake kwa staili hiyo.
Wakati akiwa ametulia juu ya kochi yeye Ahmed,alikuwa mara apite hivi mara aingie kule ili mradi anaweka vinywaji sawa.
“Samahani kidogo,ngoja nioshe glasi mara moja.Rimoti hizo hapo, washa tivii,uangalie”
Hivyo ndivyo Ahmed,alivyosema huku akiliendelea friji, lililokuwa seblen hapo,alivyokamilisha kila kitu akatoka nje kabisa,ambapo baadaye alifika na glasi mbili.Akamimina juisi kwenye glasi nayeye, akafanya hivyo kwenye glasi yake,kisha akaketi sofa la pembeni kabisa.Jambo hilo pia likaonekana kuwa ni kero kubwa kwa Necka kwani hakulifurahia kabisa.
“Nambie.Hivi,umeniambia unaitwa Necka eeh?”
Ahmed,akavunja ukimya na kuweka glasi ya juisi mdomoni,akapiga fundo la kwanza na kuweka glasi juu ya meza.
“Mara hii umeshalisahau jina langu?”
“Majina ya kizungu hayo,inakuwa tabu kidogo”
“Ndio, naitwa Necka”
“Necka,nambie sasa.Leta sera”
Sentensi hiyo ilimaanisha ya kwamba Necka aseme kilichomleta na ana habari gani,hiyo ilifanya Ahmed akae vizuri ili asikilize.Hata hivyo alijuwa vizuri sana kwamba hakuna jipya zaidi tu zilikuwa ni habari za Hajrath, kuombewa msamaha.Lakini hakutaka kuongea chochote, ilikuwa ni lazima amsikilize kwanza!
“Ahmed”
“Yes”
“Nina ujumbe wako”
“Ujumbe wangu?!”
“Ndio”
“Kutoka kwa nani?”
“Sio ujumbe,actually.Nina jambo nataka kukwambia”
Ghafla,Necka akabadili kauli. Badala ya kusema anataka kutoa ujumbe sasa alisema ana jambo.Kitu hiko kikamfanya Ahmed,atege masikio yake yote mawili kusikiliza.
“Kuhusu Hajrath”
Alikuwa ni kama ametabiri vile kwani alitegemea sana katika mazungumzo hayo ni lazima Hajrath angehusishwa na kitu alichokuwa anakitegemea baada ya hapo ni Necka kusema ‘Hajrath anahitaji msamaha wako’ ama ‘Hajrath anahitaji kuzungumza nawewe’ Mbali na kuwaza hayo yote lakini alitaka kumuacha Necka amalize kile alichokianza.
“Sitaki,kuanzia mbali lakini ujuwe tu.Mimi najua una mahusiano na Hajrath ya kimapenzi”
Necka,akaanza kufunguka.Baada ya kuongea hayo,akaweka pozi kidogo na kushusha pumzi ndefu.
“Kwanza labda nikuulize kitu,unampenda?”
Necka akatupa swali.Ili kwanza kutingisha kiberiti kama kina njiti,hiyo ilimshangaza sana Ahmed,hakuelewa ni ujasiri gani aliokuwa nao binti huyo aliyekuwa pembeni yake,swali hilo lilimfanya Ahmed atulie kidogo akawa kama anatafakari.
“Kwanini umeniuliza hivyo?”
Ahmed,badala ya kujibu swali nayeye akauliza swali, likawa swali juu ya swali.
“Nataka kujua kwanza,kabla sijaendelea”
“Nampenda lakini ameniumiza sana”
“Kivipi?”
“Hilo jambo siwezi kulisema lakini juwa hiko kitu”
“Sawa,sio muhimu sana mimi kujua!Lakini ukweli nakupa,Hajrath hakufai.Hakufai, hakufai,kabisaaaa.Unajua kwanini anakwambia anataka mapenzi yenu yawe ya siri?”
Moyo wa Ahmed,ukapiga paaa!Akashindwa kuelewa azungumze nini.Kwani kila alipotaka kujibu hoja hiyo, alihisi mdomo wake umejaa mate.

******

“Geboo,mbona umeingia bila kupiga hodi?”
“Samahani,sikujua si.. si kujua”
Namna Hajrath,alivyokuwa ilikuwa ni lazima kama mwanamme aliyekamilika apigwe na butwaa la waziwazi ama apate kigugumizi,hakuwa na kitu juu zaidi ya blazia.Kitovu kilikuwa nje,chini alikuwa amevaa nguo inayobana yaani ‘skin tight’ zaidi ya hapo, umbo lake lilikuwa kubwa,sio siri mtoto huyo alijaliwa kuwa na miguu minene na mapaja yenye supu nyingi.Achilia mbali nyonga yake iliyojipinda na kufanya nyuma abinuke.Hapo ndipo macho ya Gabriel yalipoganda,mapigo yake ya moyo yalimuenda kasi moyo wake ulikuwa kidogo utokeze nje ya kifua,akatamani hapohapo amrukie amlaze juu ya kitanda afanye naye ngono, ghafla akatamani kuwa jogoo ili ampande.
Ni kweli kwamba macho hayana pazia,kwa mara ya kwanza Gabriel kuona maumbile ya Hajrath kiundani zaidi,kilichomshangaza zaidi ni mchoro wa ‘tatouu’ wa msichana huyo wa samaki anayeitwa Dolphine,pembeni ya nyonga upande wa kushoto.Aibu aliyoshikwa nayo Hajrath,haikuelezeka kiwepesi,japokuwa alikuwa tayari amechelewa lakini ilimbidi achukuwe Kanga iliyokuwa juu ya kitanda na kujistili.
“Siku nyingine usirudie kuingia humu ndani bila kupiga hodi”
“Sawa”
Gabriel,akaketi juu ya kiti kilichokuwa pembeni ya kitanda bila kukaribishwa.Akabaki kimya, anatafakari bado!
“Za masiku?”
“Safi tu,Hajra”
“Leo mbona ghafla hivyo?Kama ugomvi”
“Hapa nina haraka sana,kuna mambo nahitaji nikwambie”
“Mambo gani?”
“Kumbe wewe ni shemeji yangu?”
Haikujulikana kama Gabriel,aliuliza swali ama anatoa tuhuma.
“Kwa nani?”
Hajrath, akajibu kwa swali.
“Ahmed”
“Yes,ndio.Kwani ulikuwa hujui?”
Hajrath,alizungumza maneno hayo akiwa ana maana yake kichwani.Alifanya hivyo kwa makusudi ili kumuumiza moyo Gabriel ambaye kwa muda mrefu alikuwa akimtaka kimapenzi lakini moyo wake haukuwa tayari kukubali swala hilo litokee.
“Nilikuwa nasikia tu,lakini sikuwa na uhakika”
“Ndio hivyo,Ahmed ni boyfriend wangu”
“Lakini Hajra,mbona unapenda kuniumiza moyo.Nakupenda na unajua kabisa,nilianza kukwambia jambo hili tangu upo hapa mwaka wa kwanza,naumia.Sikuwahi kupenda kama hivi.Nielewe”
Gabriel,akaanza kusema yaliyokuwa moyoni mwake kwa mara nyingine.Kumtongoza Hajrath kama angekuwa anaimba kuna uwezekano mkubwa kabisa angekuwa ametoa ‘Album’ tisa kama sio kumi,ni wazi kwamba katika wavulana wa chuo hiko waliokuwa wakimgasi Hajrath bila kuchoka ni jamaa huyu anayeitwa Gabriel,alimfukuzia kwa takribani miaka miwili lakini kwake ikawa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki,hakukata tamaa akajuwa wenda msichana huyo ataingilika kwa gia ya pesa,akawa anafanya hivyo.Pesa za ada akawa anatumia kwa kukodi magari ya kifahari ili kuutingisha moyo wa Hajrath lakini wapi,kuhusu zawadi ndio usiseme alihonga na kuendelea kutoswa kama kawaida.
Sio siri Gabriel alijituma sana kumfukuzia na kumpigia misele Hajrath lakini jitihada zake hazikuzaa matunda hata kidogo.
Kitendo cha kusikia yupo na Ahmed,kilimuuma mtima, ndiyo maana alijaribu kuharibu,kifupi Gabriel alikuwa ni mnafki anang’ata na kupuliza.Siku hiyo akajaribu tena kukumbushia swala lake lakini kazi ikawa ni ileile,msimamo wa Hajrath haukutetereka!
“Nampenda Ahmed”
“Lakini mimi ndio wa kwanza.Kukuimbisha kote miaka yote hiyo, nionee huruma jaribu kunipa hiyo nafasi,nikuoneshe jinsi gani nakupenda”
“Ahmed please,sorry Gebbo naomba uniache.Sipo kwenye mudi nzuri siku ya leo”
Ni wazi kwamba,Hajrath hakuwa katika hali ya kawaida, ndiyo maana hata ubongo wake ulikuwa ukichanganya mafaili,akalitaja jina la Ahmed.
“Ahmed hakufai,atakuchezea atakuacha tu.Mimi ni rafiki yake,namjua vizuri.Sikiliza,sisemi hivyo ili kumuharibia,nakupenda ndiyo maana”
“Gabriel”
Hajrath,akaita.
“Yes,nakwambia ukweli”
“Unanipenda?”
“Ndio”
“Basi naomba uwende,sasa hivi sipo vizuri.Please nakuomba”
“Lakini Haj…”
“Niache kidogo please please”
Huo ndio ulikuwa msimamo wa Msichana huyu mrembo,kitu kilichomtibua zaidi ni kusikia kwamba Ahmed anapondwa na kupigwa majungu,ni jambo ambalo hakutaka kulisikia na aliamini angeendelea kumsikiliza Gabriel,angeumia zaidi mtima.Ili kuepusha hilo,akaamua kumfukuza.
“Sawa,mimi naenda.Lakini,ndio ujue,Ahmed hakufai”
“Aya”
Hakuwa na sababu ya kuendelea kubaki,ilibidi aanze safari ya kuondoka hivyo hivyo, kishingo upande.Kuna jambo moja lilimshtua na kumshangaza Gabriel kwa wakati mmoja,ni baada ya kukumbana na mwanaume mrefu,aliyevalia suti nyeusi,yupo mlangoni kwa Hajrath anataka kuingia.
Kilichomuogopesha zaidi ni kitendo cha jamaa huyo,kuzama ndani ya chumba cha Hajrath na kilichosikika baada ya hapo ni mlango kufungwa na ufunguo.Kwa akili yake,akaelewa ni kitu gani kinaenda kufanyika,mbaya zaidi mavazi aliyokuwa amevaa Hajrath yalitosha kabisa kumpa jibu la swali lake.
“Kwahiyo amenifukuza ili huyu jamaa aingie amgonge?Ni lazima hili jambo Ahmed alishuhudie wote tuumie”
Gabriel alisema akionesha wivu na hasira za waziwazi.


Kanga ilikuwa tayari ipo chini,mguu wake mmoja upo juu kabisa.Mdomo wake unanyonywa,kifua chake kinatomaswa.Hakuwa anahisi kingine zaidi ya kufumba macho huku akivuta vuta mashuka,raha alizohisi hazikuwa na mfano wake,ndiyo maana alikuwa anatoa miguno ya puani bila ya yeye mwenyewe kujielewa.
“Aaah aaah aaashii aaahsh aaishiii yeees aaaah aaah”
Hiyo ndiyo miguno iliyokuwa inatoka ndani ya chumba hiko.Ni dhahiri mtu huyo alikuwa anakaribia kufika kileleni,akazidi kujinyonga nyonga kwani Mwanaume aliyekuwa juu yake alikuwa amemkamatia vilivyo,zaidi na hapo mguu wake mmoja ukawekwa juu begani.
“Aaaah”
Pumzi hiyo ilimtoka mwanamme huyo,baada ya kumwaga oil chafu.Hapohapo, akatulia kifuani akiwa amechoka kiasi,baada ya ushindi wa mechi hiyo.Ukimya wa ajabu ukatokea kila mtu alionekana kuchoka.
“Sijui nifanye nini ili abadilike?”
Mwanamke huyo alikuwa akiwaza,wakati mwingine alijilaumu mno kwani tangu aolewe hakuwahi kufurahia tendo hilo la ndoa,ilikuwa ni lazima akitaka kufika kileleni, mumewe anawahi kumaliza anamwacha, njiapanda.Tatizo hilo liliendelea kumtesa kwa kiasi cha kutosha,alimuogopa sana Mmewe.Hakutaka kumuelezea tatizo hilo, akiogopa kufokewa ama kununiwa.
Hata hivyo alimvumilia sana huku akijaribu kutafuta tiba mbalimbali kutoka kwa makungwa kwenye sekta hiyo ya ndoa,hasa katika swala la tendo la ndoa.Akakumbuka namna alivyozunguka sana mpaka kwa Mwanamke maarufu anayetingisha jiji la Dar es saalam, anayeitwa Samira Suleiman ili kupata tiba lakini wapi,akaona haitoshi akafunga safari mpaka Zanzibar ili kuonana na Salma Super Woman,akashauriwa awe mvumilivu na akae chini amueleze mume wake.Lakini kwake swala hilo likawa gumu.
“Naomba nikaoge”
Marry Frank,alizungumza kwa sauti ilioonesha kutofurahia kabisa, hakuongea kimahaba, bado alikuwa ana moto kwani hakufikishwa kitonga na alimuelewa sana mume wake hata kama angebustiwa na waya wa kuchajia betri la gari,asingeweza kuingia mzunguko wa pili kwa wakati huo.
Baada ya mumewe kujisogeza na kujitoa juu yake,akavuta kanga na kuiviringisha, kihasarahasara mwilini,akashuka kitandani na kunyoosha mpaka bafuni.Huko akajifungia kwa ndani na kujiangalia kwenye kioo,hakuwa na jinsi zaidi ya kuanza kujishika mwenyewe na kuutomasa mwili wake,akivuta hisia ili ajiridhishe mwenyewe.Haikuwa mara ya kwanza kufanya kitu kama hiko,tabia hiyo aliichukia lakini hakuwa na jinsi kwani bila kufanya hivyo,nyonga zingemuuma mno.
“Aaaaah! Aaaah”
Alifumba macho yake huku akiwa anasikilizia utamu,kichwani kwake walikuja wanaume tofautitofauti.Akiwa nao anafanya mapenzi,akazidi kuishika ikulu yake ambapo hapo alihisi kama kuna majimaji yanayoteleza kama mlenda,akazidisha kasi, mpaka alivyohisi vitu kama utitiri vinatembea kwa kasi ya ajabu,hapohapo akatulia kidogo sababu alikuwa amekidhi haja yake.
Akajiangalia kwenye kioo,jinsi alivyokuwa akajitizama vizuri,akili yake ikasafiri kwa kasi ya risasi kipindi cha nyuma, alivyokuwa anaridhishwa na Mmewe kabla ya ndoa yao.Akashindwa kuelewa ni kitu gani kilimkumba,wakati mwingine alidhani wenda mumewe kamchoka ama kamkinai.Vitu vingi sana vilipita kichwani kwake,ghafla sura ya mwanamme wake wa zamani, anayeitwa Jonathan Ermas ikampitia kichwani,akamuona namna ambavyo alikuwa akiridhishwa naye kitandani, kipindi bado wapo wapenzi,akatamani arudishe siku nyuma huyo ndiye awe mume wake wa ndoa lakini hilo halikuwezekana,akabaki anajutia na kulia machozi.Kifupi Marry Frank,alijichukia mwenyewe kwa kukubali kuolewa mapema.
“Kwa..ni..ni mimi?”Alilia kwa kwikwi.
Sio kwamba alishindwa kuchepuka,la hasha!Aliogopa kufanya hivyo sababu alimuheshimu sana Mumewe na hata siku moja, hakupanga kuja kufanya kitu kama hiko.
“Maaaryyyy”
Sauti ya mumewe kutoka chumbani,ikamshtua.Kwa kasi akafuta machozi akitumia viganja vyake vya mikono,akafungua bomba la maji na kuanza kujimwagia maji harakaharaka,akatoka na kanga moja bila kujifuta, niya yake ikiwa kumtega mumewe.Lakini wapi,mtego wake haukufanya kazi kwani Mumewe alimpita na kuingia bafuni kwa niya ya kuoga,dakika mbili baadaye akatokeza na kupitiliza mpaka kwenye kabati.
“Naenda ofisini mara moja,kuna kazi naenda kumalizia”
“Sawaa”
“Are you okay?”(Upo sawa)
Lilikuwa ni swali.
“Ndio”
“Okay”
Ukweli ni kwamba Marry, hakuwa mwenye furaha hata kidogo,kuna mengi yalikuwa yanamuumiza kwa kiasi cha kutosha,kama kungekuwa na mzani wa kupima mawazo basi mzani huo ungevunjika, kutokana na uzito wa mawazo,sio siri kuna mambo mengi sana yalikuwa yakimtesa mwanamke huyu mdogo kuingia ndani ya ndoa!Mume wa Marry,ama kwa jina Erasto!Baada ya kuvaa,nguo akatembea mpaka nje,akafunga mlango na kutoka nje,ambapo huko aliingia ndani ya gari.
“Piii piiii”
Akapiga honi,kuashiria mlinzi afungue geti.Kabla ya kuanza safari akasikia simu yake imeingia ujumbe wa meseji,akafungua na kuisoma.
‘AU MPAKA MAMA YAKO NIFE,BILA KUMUONA MJUKUU WANGU?’
Huo ndio ujumbe uliokuwa unasomeka juu ya kioo cha simu ya Erasto,akashusha pumzi ndefu na kutulia kidogo.
Hakutaka kuutilia ujumbe huo,maanani.Akawasha gari ili kuanza safari moja tu,chuo cha Makumira ili kuonana na msichana anayeitwa Hajrath kwani ni siku nyingi alikuwa akimfukuzia bila mafanikio yoyote yale,ilikuwa ni lazima aende kwa mara nyingine tena, akajaribu bahati yake.Hakutaka kuamini ya kuwa msichana kama huyo wa chuo,amtolee nje kizembe.
“Leo nitampata tu”
Erasto,akajisemea huku akibadili gia,akitokea Ngalamtoni,alipojenga nyumba yake.Mapenzi kwa mkewe yalipungua kabisa,hakutaka tena kumsikia Marry.Aliendesha gari akiwa na mawazo chungu mzima,katika maisha yake siku moja alitamani kuwa na mtoto,ndiyo maana alijitahidi kufanya kazi kwa bidii ili awe na familia bora,aitwe baba bora.Lakini mambo yalibadilika na kuwa kinyume kwani swala la kupata mtoto likageuka na kuwa ndoto ya mchana,hiyo ni kutokana na Marry kushika mimba kisha ikifika miezi mitano inaharibika, kwa mara ya kwanza alidhani ni kawaida lakini mimba zaidi ya kumi zilitoka,jambo hilo lilimfanya aumie zaidi na kuanza kutafuta wanawake wengine wa nje ili wamzalie mtoto!Ilikuwa ni jioni,barabara haikuwa na msongamano wa magari sana, hivyo ilimchukua muda mchache kufika chuo hiko cha Makumira,akaegesha gari na kuanza kutembea kuelekea hostel anazoishi Hajrath,kwa kuwa alikuwa anajua ni majengo yapi,hakuuliza akanyoosha na kupitiliza mpaka chumbani.Kitendo cha kuingia tu,akafunga mlango na ufunguo kwa ndani.
“Umefuata nini humu Erasto?”
Hajrath,aliuliza kwa jazba.Ugeni huo wa Erasto ulimkera mbaya zaidi mwanaume huyo pia, aliingia bila kupiga hodi.
“Nimekufuata wewe”
“Unanitakia nini lakini?”
“Nakupenda, Hajrath”
“Fungua mlango kwanza,ndio tuongee”
“Siwezi”
Damu ya Erasto,ilianza kumwenda kasi.Hiyo ilisababisha na mazingira yaliyokuwepo, hususani namna ambavyo Hajrath alivaa,juu hakuwa na kitu chochote kile bali sidiria tu.Sio siri,umbo lake lilikuwa na mvuto wa aina yake,ukiachilia hilo ndani walikuwa wawili tu,kitanda kipo pembeni.Hiyo ilitosha kabisa kuhamisha hisia za Erasto,hakuwaza kitu kingine zaidi ya kufanya ngono.Ndiyo maana suruali yake ikaanza kutuna taratibu.Kwa kasi ya mwewe,akavua koti lake la suti akalitupa pembeni na kumrukia Hajrath, mithili ya Chui mwenye njaa kali, anavyomrukia Swala,akamvutia kitandani na kumziba mdomo.Kitendo hicho kilikuwa ni cha ajabu kwa mwanaume kama Erasto mwenye heshima zake kukifanya,haikuwa akili yake.Hisia kali ndizo zilimuongoza na kumpelekea atake kufanya kitendo hicho cha ubakaji.
“Era..sto niachie”
Hajrath alijitahidi kupiga kelele lakini hazikuweza kutoka kwani tayari mdomo wake ukawa umezibwa,Erasto akawa anang’ang’ana kuivuta ‘skin tight’ ya Hajrath, iliyokuwa imem-bana sana,hapo ndipo zoezi hilo likaonekana kuwa gumu,hakutaka kushindwa akaishika vizuri na kuivuta kwa nguvu,hiyo ilifanya skin tight ichanike,kwa namna nguo hiyo laini ilivyopata mpasuko wa kuchanika, ilikuwa rahisi kwa Erasto kupitisha tango lake ili afanye anachokitaka,akafungua zipu na kulitoa tango lake likiwa tayari limesimama.
Hapo ndipo kibarua kilianza kuwa kigumu kwani hakuweza kufanikisha sababu Hajrath,aliibana miguu yake.Kwa nguvu za ajabu na kwa kutumia vidole ambavyo aliviingiza machoni mwa Erasto,ilimfanya apate upenyo akaruka na kujibiringisha mpaka upande wa juu wa kitanda,akadondoka puu, sakafuni.

*******
“Kaka,njoo fasta.Uko wapi?Gheto?Njoo Hostel, kwa Hajrath.Ufumanie mwenyewe,nilikuwa nakwambia unabisha..Hapana kaka usichelewe sasa hivi,wewe njoo tu.Chukua hata boda,mimi nitalipa,usichelewe sasa!Njoo ufumanie mwenyewe,nilikwambia huyu demu malaya,hutaki”
Maneno hayo yalitoka kinywani mwa Gabriel,tena bila nukta.Alikuwa akizungumza harakaharaka simuni kama mtu aliyemeza kaa la moto,akimpasha habari Ahmed baada ya kumuona Mwanaume, anaingia chumbani kwa Hajrath.Wakati anazungumza hayo,alikuwa amejificha kwenye ngazi anautizama mlango wa Hajrath na kutamani Ahmed,atokee sekunde hiyohiyo.Ashuhudie kwa macho yake fumanizi hilo,kivyovote vile aliamini huo ndio ungekuwa mwisho wa mahusiano yao.Alivyohakikisha habari hizo zimemfikia na Ahmed,atafika muda si mrefu,akasogea kidogo ili auone vizuri mlango wa Hajrath bila kugundulika.

*****
Simu kutoka kwa Gabriel,ilimshtua na kumpa presha.Akapata kitete cha ghafla,akamtizama Necka Golden, aliyekuwa pembeni yake.Mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu sana!Hakuelewa ni kwanini,hali hiyo imejitokeza ghafla, wakati hapo awali alisema hampendi Hajrath.
“Nakuja,nisubiri”
Yalikuwa ni maneno mawili tu,yaliyomtoka Ahmed.Akachomoka na kufungua mlango.
“Ahmed una…”
Necka Golden,ilibidi asimame na kuuliza lakini alikuwa keshachelewa tayari kwani Ahmed alikuwa tayari ametoka nje, hiyo ilimfanya ashindwe kuelewa ni kitu gani kimempata,japokuwa alihisi mtu aliyempigia simu ndiye aliyesababisha kila kitu kutokea lakini hakuelewa chochote kile,alichofanya ni kutulia na kukaa kwenye sofa.Kasi ya Ahmed ya kutembea iliogopesha,moyo wake ulikuwa juu juu kama mtu aliyeambiwa nyumba yako inateketea na moto,akatamani afike mapema ashuhudie fumanizi hilo.
Japokuwa ingekuwa ni kweli,angeumia mara mbili yake zaidi.Kila alipogeuka nyuma kuangalia kama kuna pikipiki inakuja hakuona dalili yoyote ile,akaendelea kuchapa mwendo akitembea hatua mbilimbili,mpaka alipofika stendi.
“Nipeleke Makumira”
Ahmed,akamwambia mmoja wa madereva waliokuwa eneo hilo bila ya kutoa salamu.
“Poa chalii anguu”
Ahmed,akapanda nyuma.Dereva akapiga kiki, safari ikaanza mara moja.Ingawa pikipiki ilikuwa katika mwendokasi lakini Ahmed,alitamani dereva aongeze gia.Kichwani alikuwa mwenye mawazo chungu mzima,hakuelewa angemfanya nini Hajrath kama angeshuhudia fumanizi hilo,hakupata picha atakuwa katika pozi gani.Akaanza kujenga picha kichwani ya Mwanaume akiwa na Hajrath hostel kisha yeye kutokea,kila kitu akawa anakijengea picha kichwani kitakavyoenda kutokea, kifupi alifika eneo la tukio, kifikra.
“Kaka vipi?”
Ahmed,akamuuliza dereva baada ya kuona pikipiki inapungua mwendo.
“Naingia hapo sheli,arifuu”
“Sasa muda wote ulikuwa wapi usijaze mafuta?Unazingua mshkaji”
Ili kuepusha shali na abiria wake ilibidi akae kimya,kwani namna alivyoulizwa ilimuogopesha mpaka yeye mwenyewe.Ahmed,aliuliza kwa hasira za waziwazi huku akifoka kwa ukali.Hiyo haikufanya dereva wa pikipiki,aghaili kuingia sheli kwani bila kujaza mafuta wasingefika popote pale.
“Sasa kwanini hukuweka mafuta?Hivi mnakuaje nyie bodaboda?Huo ni upumbavu, yaani mambo yenu ya kuunga unga tu”
Ahmed,alizidi kuzungumza akiwa na hasira za kufumania.Hapo walipoteza dakika tano nzima, ndipo safari ikaanza upya,dakika kumi baadaye Ahmed,akawa amefika Chuo cha Makumira,akampa dereva ujira wake!

********
Isingekuwa Hajrath,kujitupa chini wenda yangekuwa mengine.Kujitetea kwake kulimfanya anusurike na zoezi hilo la kutaka kubakwa, ambalo hata yeye hakutegemea kama lingetokea,akiwa sakafuni alimuona Erasto anamfuata alipo,hapo ndipo alijivuta kwa kasi na kunyoosha mkono,akachukua kisu kilichokuwa chini ya meza,akakishika vizuri mkononi.
“Erastoo, nakuuuuwa kaa mbali namimi”
Hajrath akaropoka kwa nguvu huku akitetemeka kwa hasira,haukuwa utani.Kulikuwa kuna kila dalili za hatari siku hiyo, kutokana na hasira alizokuwa nazo ghafla!Kifua chake kilipanda juu na kushuka,mapafu yake yalijaa hewa pua zake zikawa zinamcheza,jasho linamtoka anamsubiri Erasto asogee ili amtoboe toboe na kisu.Kwake yeye ilikuwa ni bora akafungwe kuliko kukubali kufanyiwa kitendo cha kinyama namna hiyo.Kisu alichoshika Hajrath, kilimfanya Erasto aogope na kushindwa kusogea kwani alielewa nini maana yake, endapo angeendelea na zoezi lake la kutaka kujaribu kubaka.Ghafla akili yake ikaanza kurudi taratibu,akatulia kidogo na kuanza kujishangaa mwenyewe kwa kitendo alichotaka kukifanya.
“Hajrath,naomba unisamehee”
“Tokaaa”
Hajrath,akaropoka kwa hasira huku akiwa bado ana kisu mkononi,hiyo ilifanya Erasto aishiwe pozi,akatembea mpaka lilipokuwa koti lake akalibeba.Akafungua mlango na kutoka huku akitembea kwa haraka,alivyopiga hatua tatu,akawa anajiangalia kama yupo sawa.Akagundua kuwa hajafunga zipu ya suruali yake,akaivuta juu na kuanza kuchomekea vizuri kisha kuvaa koti lake.

******
Moyo wa Ahmed,ulichoma kama pasi!Tangu mlango wa Hajrath unafunguliwa alishuhudia,akamuona mwanaume huyo anavyotoka,mbaya zaidi alivyokuwa anafunga zipu na kuvaa koti.Tafsiri iliyokuja kichwani kwake harakaharaka ni kwamba mwanaume huyo,ametoka kujisevia tayari,akajikuta anapiga ukuta ngumi kwa hasira.
“Kaka,punguza jazba”
Gabriel,alimtuliza kinafki.Moyoni alifurahi kwani alitaka kwa makusudi kitu kama hicho kitokee.
“No!No!No.Haiwezekani”
Bila kuongeza kitu kingine chochote,Amed akachomoka kwa kasi kama mkuki,akauparamia mlango wa Hajrath lakini alikuta umefungwa na funguo.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Ahmed akagonga mlango kwa fujo kana kwamba baba mwenye nyumba anadai kodi yake ya miezi kumi.
“Erastoo,naomba uniache”
Hajrath alisikika akiongea kutokea ndani.
“Fungua Hajra”
Moyo wa Hajrath ukapiga kwa nguvu,hakuwa ana uhakika kama sauti aliyosikia kutoka nje ni yenyewe ama kasikia vibaya,akavuta kanga na kujifunika vizuri.
“Wewe nani?”
Akauliza,akiwa karibu na mlango ili kupata uhakika zaidi.
“Fungua mlango Hajrath”
Hatimaye akapata uhakika ingawa namna alivyokuwa anazungumza Ahmed,ilimtisha.Akazungusha funguo na kunyonga kitasa,Ahmed akazama mzima mzima, mpaka chumbani na kumuangalia Hajrath kwa jicho kali la hasira,lililojaa wivu na chuki.
“Ndio maana ulitaka mapenzi yetu yawe ya siri”
Haikujulikana kama lilikuwa ni swali ama shtaka la kwanza kusomewa.Ahmed alizungumza huku sura yake ikiwa imejikunja,anatizama kitanda cha Hajrath kilivyovurugika,akaamini kabisa kwamba muda mfupi Hajrath alikuwa kitandani anacheza mechi na mwanaume aliyeondoka.
“Ahm..ed nisikilize”
“Nikusikilize nini?Nikusikilize nini Malaya mkubwaa”
Kila kilichotokea kwa Hajrath kilikuwa ni kama sinema ya kusisimua,akashindwa kuongea na kuanza kulia kwa kwikwi lakini kwa Ahmed,alitafsiri jambo hilo kama maigizo.
“Usiniletee maigizo ya kifilipino hapa,kuanzia leo usinijue tena.Kwa mach..”
Ahmed,akashindwa kumalizia sentensi yake, baada ya kumuona Hajrath anaenda chini kwa magoti na kumshika miguu.
“Ahmed na..kupenda saaa….na.Naomba usifanye hivyo.Naku..penda mpenzi.Nipe dakika moja t..u…yaa kuni..sikiliza”
Hajrath,alizungumza huku akitiririkwa na machozi!Yakashuka na kulowanisha shingo nzima,hakuwa ana uhakika kama siku hiyo penzi lake litaendelea kwa jinsi alivyokuwa anampenda Ahmed,alikuwa yupo tayari kukosa vyote duniani lakini sio kumpoteza, AHMED!


Ni wazi kwamba aliwahi kuumia lakini sio siku kama hiyo,moyo wake ulimuuma. Ndiyo maana akawa analia machozi kama mtoto mdogo, aliyeachwa na Mama yake!Ungemwangalia urembo aliokuwa nao,ungesema wenda alikuwa anaigiza.Kumbe haikuwa hivyo,ukweli ni kwamba alikuwa akimlilia Mwanaume kwa uchungu huku akiwa amepiga magoti, jambo ambalo hakuwahi kulifanya kwa mwanaume yoyote yule tangu azaliwe.Hajrath,alikuwa kiburi kwenye swala zima la mapenzi lakini hakuelewa kwanini anamnyenyekea Ahmed kwa kiasi hicho,hata yeye mwenyewe alijishangaa!Machozi aliyokuwa anatoa Hajrath yalimfanya Ahmed,atulie kidogo na kumtizama kwa kama sekunde tano nzima,hakuelewa ni kitu gani akijibu lakini alihisi kumuhurumia msichana wake.Lakini upande wa pili,ukamwambia no!Msichana huyu hakufai,utakufa na presha.Alizidi kupembua mambo akijaribu kutofautisha tui la nazi na maziwa,machozi ya Hajrath hata yeye yalimshangaza mno,akaingiwa na huruma na kumshika mkono.
“Ahmed,tusepe!Achana na huyo malaya.Utakufa na ngoma”
Hiyo ilikuwa ni sauti ya Gabriel, aliyekuwa akitizama sinema hiyo kwa muda mrefu,aliropoka hivyo baada ya kuona Ahmed,anaanza kulegeza!
“Twenzetu,tusepe Kaka!Achana naye.Hayo machozi,anaigiza tu huyo”
Gabriel,alivyoona anazungumza bila kufanya vitendo!Alimsogelea Ahmed na kumshika mkono akiwa anamvuta kumtoa nje,hiyo haikuwezekana sababu Hajrath aliung’ang’ania mguu wa Ahmed.Kilichotokea ni vuta,n’kuvute!Gabriel anamvuta Ahmed,Hajrath ameung’ang’ania mguu wake huku akilia machozi, akisihi asamehewe.
“Ahm..ed plea..se!Nipe nafasi,nisikilize Mpenzi wangu.Bado nakupenda”
“Ebu,muache.Kicheche mkubwa,huoni hata aibu”
Gabriel,akamchamba Hajrath aliyekuwa analia huku amepiga magoti.
“Mwana,tuondoke.Achana na huyu Malaya”
Hajrath,hakuelewa kama masikio yake ni mabovu ama amesikia vibaya,maneno aliyokuwa anazungumza Gabriel yalizidi kumuuma zaidi,kitendo cha kuitwa Malaya kilifanya achukie ajabu kwani tangu azaliwe hakuwahi kusimama barabarani na kuuza mwili,alielewa sana hiyo ilitokana na kumtosa na kumkataa kimapenzi.
“Mwache mguu wake baki na mabw….”
“Naaani Malaya?”
Hajrath,akasimama kwa hasira zilizochanganyika na jazba alizokuwa nazo,ndiyo maana akainuka wima na kumuangalia Gabriel kwa macho makali,yaliyojaa chuki.
“Nakuuliza wewe Gabr..iel nani malaya?”
Hajrath,akauliza tena huku akifuta machozi yake.Ilikuwa ni lazima sekunde hiyohiyo amtolee uvivu, ndiyo maana alikuwa akisubiri jibu,litakalo mpandisha mashetani yake,amchambe na amtolee mapovu yote!
“Wewe ni malaya,ulikuwa na nani humu ndani?Hata Ahmed mwenyewe kaona kila kitu”
Gabriel,nayeye akasema na kutengeneza hoja ili kumkandia Hajrath!Alikuwa ni kama anasubiri jambo hilo litokee.
“Gabriel,wewe wa kuniambia mimi hi..vyo?!Kisa nimekukataa ulikuwa unanitaka”
“Yewomiii,muone huyu.Wewe unaweza kutongozwa namimi wewe?”
Ghafla ukaibuka mgogoro mkubwa,kila mtu alipandisha sauti ya juu,chumba kikageuka na kuwa kama soko dogo la Tandika.Hakukuwa na maelewano hata kidogo,huyu alizungumza hiki yule alijibu kile.Jambo hilo likafanya wanachuo wengine watoke vyumbani ili wajue ni kitu gani kinaendelea.Tukio hilo,liliwashangaza watu wengi.Hakuna aliyetaka kuamini kama Hajrath ni mkorofi namna hiyo, akiwa mwenye hasira.
“Wewe mwanaume ni mnafki sana,kichwa kama kibuyu”
Sijui alitokea wapi msichana huyu anayeitwa Amney,rafiki mkubwa wa Hajrath,hakutaka kuona jambo hilo linaendelea.Kwake alilitafsiri jambo hilo ni kama udhalilishaji,ndiyo maana hakutaka kuona linaendelea.
“Nawewe Amney,funga bakuli lako”
“Usininyamazishe,kenge wewe.Mwanaume mzima mbeya.Ungekuwa mwanamke wewe,ungeshatiwa mimba siku nyingi”
Amney,alizungumza kwa hasira za waziwazi huku akimtizama Gabriel kwa macho makali yaliyojaa chuki,ilielekea siku hiyo alikuwa akiisubiri kwa muda mrefu sana!
“Kwanza ulikuwa unamtaka Hajra,kakukataa nani asiyejua.Ahmed,huyu rafiki yako ni chui.Usitembee naye.Ku**** la mamako Gebo”
Amney,akamaliza na tusi zito la nguoni.Ni wazi kwamba alionekana kukerwa kuliko kawaida,ilikuwa ni bora ufanye kitu chochote kile lakini sio umguse rafiki yake Hajrath,ndiyo maana siku hiyo alilivalia swala hilo kibwebwe.
“Kwanini unanitukania Mama yangu?Mama yangu kafanya nini?”
Gabriel nayeye akapandisha Mori,akamsogelea Amney karibu zaidi ili amzabe makofi lakini alishindwa sababu alishikwa na wanaume waliokuwa pembeni wanaangalia,mzozo huo.
“Masatu,niache nimuoneshe huyu Malaya”
Gabriel alizungumza huku akijaribu kujitoa mikononi mwa wanafunzi wenzake.
“Achana naye kaka!Haifai,wewe mwanaume”
“Mwache,mwache ajaribu kunipiga nimuoneshe..Msen** wewe!”
Amney,bado alikuwa anawaka ilikuwa ni kama moto uliomwagiwa mafuta ya petrol vigumu kuuzima,sio siri siku hiyo alicharuka mno!
“Masatu,niachie!Niachie kaka,nimfunze adabu”
Badala ya kusuluisha ugomvi wa Ahmed na Hajrath, sasa mambo yakawa kinyume.Amney na Gabriel wakawa kama wamenunua sakata hilo!Jambo hilo likazidi kuwajaza wanafunzi,wengine wakasimama kwenye ngazi,kelele zikawa nyingi.Hakuna mtu aliyemuelewa mwenzake!
“Nina meseji hapa,nyingi ulizokuwa unanituma nikutongozee kwa Hajrath,mwanaume gani wewe?Mnafkiiii hujui kutongoza domo zege”
Kitendo cha Amney kuropoka maneno hayo,ikafanya Gabriel apate aibu na ilikuwa wazi kabisa,angeendelea kubaki eneo hilo angeumbuka kwani Amney alikuwa amegusa mshono,kila alichokuwa anaropoka kilikuwa kina ukweli na alikumbuka sana kwamba alishawahi kumtumia meseji Amney,akimsihi ampigie pande kwa Hajrath.
“Ahmed,tusepe”
Hivyo ndivyo alivyofanya Gabriel,akamvuta Ahmed.Wakaanza kupangua pangua wanafunzi wengine mpaka walivyotoka nje kabisa!Huko walitafuta usafiri wa pikipiki na kuelekea moja kwa moja mpaka kituo kinachoitwa madukani,hapo walitafuta ‘grocery’ iliyokuwa karibu wakaagiza vinywaji.
“Mimi niletee faru John,mwenzangu sijui anakunywa nini”
Gabriel alimuagiza muhudumu,baada ya hapo ikawa ni zamu ya Ahmed kuagiza, ambaye alionekana kuwa katika msongo mkubwa wa mawazo!
“Sijisikii kunywa chochote,subiri kidogo nitakuita”
“Dada leta glasi nyingine na soda”Gabriel,akadakia.
“Soda gani?”
Muhudumu akauliza.
“Fanta”
“Ya baridi ya Moto?”
“Baridi”
Baada ya maagizo hayo,haikuchukuwa muda mrefu, vinywaji na glasi vikawa mezani.Alichofanya Gabriel ni kumimina mzinga wa Konyagi kwenye glasi yake,akachakachua na soda kidogo ili kupunguza machungu ya pombe hiyo.Akafanya hivyo kwenye glasi nyingine ya pembeni.
“Gebo,unataka kufanya nini?”
Ilikuwa ni lazima Ahmed,aulize sababu tukio la Gabriel kumimina pombe kwenye glasi nyingine, lilimshtua kidogo ingawa hakutaka kuyapa mawazo yake kipaumbele ya kwamba glasi hiyo ilikuwa ya kwake kwani tangu azaliwe hakuwahi kunywa pombe!
“Subiri utaona,nataka utoe mawazo.Tuanze maisha mapya”
“No! No! No! No! Hapana,sijisikii fresh, si unajua mimi na pombe ni vizuri tofauti”
“Hii itakufanya uwe fresh,mambo yote yatakuwa bomba.Onja kidogo broo!Naelewa namna unavyojisikia sasa hivi,machungu unayopata, toa mawazo kata nyagi, haya ni machozi ya simba”
Ahmed,alikuwa kimya kidogo!Akijaribu kutafakari na kuyachuja maneno anayoambiwa na rafiki yake,akayapima kwenye mzani wa ubongo wake.Utu uzima aliokuwa nao, ukichanganya na usomi wake,haikuwa rahisi kumshawishi na hoja ya kitoto kama hiyo eti’Pombe inatoa mawazo’akabaki akimtizama Gabriel machoni.
Maneno ya Amney yalikuwa yakijirudia kichwani kwake!Kwamba Gabriel alikuwa akimtongoza Hajrath,akataka kuuliza kama ni kweli ama Amney alikuwa katika hoja ya kutengeneza utetezi lakini mdomo ukagoma, akaupiga ‘stop’ kwa wakati huo,alitaka kuepusha vitu vingi sana ukizingatia alielewa namna Gebo,alivyokuwa katika hasira za waziwazi.
Ndiyo maana hakutaka kukumbusha kitu kama hiko,akakiweka kiporo akihaidi ipo siku angemuuliza.
“Nimiminie kidogo nionje”
Hatimaye,Ahmed akasema amiminiwe kidogo pombe hiyo aina ya Konyagi.Sio kwamba alitaka kutoa mawazo,alitaka kuonja na kujua inafanana vipi!Ilikuwa ni kama Gabriel anasubiri kitu hiko kitokee,kwa kasi ya umeme akafungua chupa na kumimina kwenye glasi ya Ahmed,akachanganya na soda!
“Piga pafu moja”
Gabriel,akamshawishi mwenzake!Ahmed akafanya hivyo,akaweka glasi mdomoni na kuonja kidogo,akakunja sura kama mtu anayekunywa dawa ya Muharobaini.
“Piga pafu lingine”
“Mbona chungu namna hii?Unaipendea nini?”
“Piga pafu,utazoea tu!”
Ahmed,akawa kama mwanafunzi anayefundishwa darasani.Akawa anatii amri,hatimaye glasi ya konyagi ikawa imeisha,akamiminiwa nyingine.Hiyo ilivyofika nusu, akaanza kuona maluweluwe na nyota,kichwa chake kikawa kizito.Kila kitu alikiona tofauti, kuanzia mazingira mpaka Gabriel, aliyekuwa mbele yake.
“Geboooo.Wewe Gebooo ndio wewe kweliii?”
Ahmed,akaita kwa sauti ya kilevi!Gabriel,alilijua hilo.
“Nambie,ndio mimi kakaa”
“Let me tell you one thing Meeen.Love is unfair,nampeeenda sana Hajraaath,kwanini anifanyie mimii hiviii?Au kisaa mimi bado nasomaaa,one day namimi nitakuwa biliooneaaa!”
“Ndio hivyo kaka,mapenzi pesa siku hizi.Bila pesa,hakuna kitu chochote!Kama ningejua unatembea na Hajra tangu mara ya kwanza,nisingekubali.Yule demu,kila siku pale chuoni anashushwa na magari tofauti tofauti.Huyo mtu sio wa kushindana naye kabisa”
“Mapenzi mimi baasiiiiiiiiiiii.Basiiii,kushneiiiii.Nasema Kushneiiiii”
Ahmed,alizungumza huku akijipiga piga kifuani kama mtu mwenye hasira,kila kitu katika maisha yake,kilivurugika kuliko kawaida.Kichwa chake kikawa kizito ghafla,akahisi kama ameibeba dunia nzima kichwani,moyo ulizidi kumuuma mno.Tukio aliloshuhudia kutoka ‘hostel’ anazoishi Hajrath, lilimfanya azidi kuumia zaidi,akatabasamu. Ilielekea kuna kitu alikikumbuka.
“Mbona unacheka kaka?”
Gabriel,akahoji.Haikuwezekana hata kidogo,mtu aanze kucheka kwenye msiba, ndiyo maana akahoji.
“Nayakumbuka maneno yake,siwezi kukuacha mpaka kifo!Mimi ni wakoooo”
Ahmed,alizungumza kwa masikitiko makubwa mno!Muda,uliyoyoma,wa kwanza kuaga alikuwa ni Gabriel hiyo ni baada ya kutumiwa ujumbe mfupi na mwanamke ambaye alikuwa akimsubiri, Ngaramtoni.
“Broo,chumba changu sijafunga mlangoo.Mimi nakuachaa hapaaa!Tutawasiliana basi”
Kazi ya kuwatenganisha Hajrath na Ahmed,ilikamilika hivyo hakuwa mwenye haja tena ya kubaki eneo hilo,tofauti na siku nyingine ambazo anamsindikiza Ahmed mpaka Ngulelo anapoishi.
“Thanks,tuwasiliane mimi mwenyewe naondoka sasa hivi”
Ahmed,akasema huku akionesha dole gumba,kuashiria kila kitu kipo sawa kabisa.

*******
Ulikuwa ni kama msiba,Hajrath alilia kuliko kawaida.Mpaka sauti ikamkauka,pembeni yake alisimama Amney,kushoto Mpangw’a walikuwa wakimpooza na kumpa pole kwa kila kitu kilichotokea,kila kitu kikageuka na kuwa majonzi.Moyoni alijuta kujihusisha tena kwenye maswala hayo ya mahusiano,hakuelewa kosa lake liko wapi.
“Hajrath,nyamaza.Usilie, sawa?”
Amney,alizungumza kwa sauti ya upole iliyojaa uchungu mno!Alimuonea sana huruma, rafiki yake kipenzi.
“Kwani kitu gani kimetokea?”
Mpangw’a akauliza.Yeye alikuwa nyuma ya kila kitu kwani ugomvi ulimpita sababu alikuwa darasani kwenye kipindi.
“Hujui?Alikuja Ahmed na yule Gabriel, mbuzi kasoro mkia”
“Nani?Ahmed,alikuja hapa?”
Mpangw’a akauliza kwa mshangao.
“Ndio,alifika hapa!”
“Kufanya nini?”
“Sielewi,mimi nimekuta ugomvi mkubwa hapa”
“Kisa nini?Ilikuwaje?”
Mpangw’a akauliza,hapo alimgeukia Hajrath aliyekuwa ameinama amefunika macho yake na kitambaa,analia kwa kwikwi.
“Nam...penda Ah..med”
Hajrath akasema huku akilia,sauti yake ilitoka kwa mbali hiyo ilitokana na kulia kwa muda mrefu.Kwa kujikaza hivyohivyo,alianza kusimulia kila kilichotokea kuanzia Erasto alivyoingia mpaka songombingo, lililotokea baada ya Ahmed kutokea,historia hiyo fupi ilimfanya kila mtu abaki kinywa wazi.
“Pole sana,sasa itakuwaje?”
Mpangw’a akahoji,jambo hilo lilikuwa zito mno kulisuluhisha.
“Inabidi tumsaidie rafiki yetu”
“Sawa,kwanza ale aoge alafu twende sehemu iliyotulia tujue tutafanya nini.Mimi ndiyo maana nachukia mapenzi,sitaki hata kuyasikia.Kisa hizi stress ndogo ndogo”
Siku hiyo,wakawa wana kazi kubwa ya kum-bembeleza mwenzao ambaye hakuwa ana hamu ya kufanya kitu chochote kile,kifupi Ahmed aliharibu mfumo mzima wa mwili wa Hajrath,kuanzia mzunguko wa damu,mfumo wa fahamu,hewa, mpaka mfumo wa moyo,hiyo ilifanya mpaka ashindwe kufanya kitu chochote kile.
******
Mbele yake aliona nyotanyota, kizunguzungu,lakini njia aliikumbuka kazi yake ilikuwa ni kumuonesha dereva wa pikipiki,anapoishi.Walivyofika kituo cha Ngulelo,wakaingia barabara ya vumbi upande wa kushoto.
“Nyoosha tu Mkuu”
Ilikuwa ni jioni,mishale ya saa 12;45.Ahmed alikuwa yupo mtungi,ametoka kulewa Konyagi,nyuma ya pikipiki, anazungumza mwenyewe,lakini ilikuwa kila baada ya sentensi saba ataje jina la Hajrath.Dereva wa pikipiki, kazi yake ilikuwa ni kukunja kona,kunyoosha ilimradi anatii amri za abiria wake aliyempakia, sababu ndiye alikuwa bosi wake kwa wakati huo.
“Paleee,kwenye mitiii ya michongomaaa.Utasimama paalee njeee okeiiiiii?”
Ahmed,akaelekeza tena!Baada ya kufika,pikipiki ilisimama akashuka huku akipepesuka kidogo,akajisachi mfukoni na kutoa noti.
“Shikaaaaaa,nasubiri chenjiiii”
Ahmed,akasema.Dereva wa pikipiki akawa kama amepigwa na bumbuazi,ilikuwa ni noti ya shilingi mia tano!Ilibidi kwanza azime pikipiki yake na kushuka kabisa ili apambane na abiria huyo mlevi,ambaye kwake yeye kitendo hiko alikitafsiri kama dharau.
“Ebu,usinizingue.Umenipa jero!Kutoka kule mpaka huku buku sita”
“Whaaaat,oooh.Niwieee radhiii.I’m sorry my friend.Nipeee hiyooo”
Alivyochukuwa noti ya mia tano,akaingiza tena mkono mfukoni na kutoa noti ya shilingi elfu kumi.
“Nisameheee kiongoziii.Nilijua nimekupa kumi,niwie radhiii sana!Sijalewaa lakini,nipo ngangaliii”
Dereva,akarudisha chenji akapanda kwenye pikipiki na kuondoka zake,akimuacha Ahmed anapepesuka,akatembea kwa kujishika shika mpaka alivyofika mlangoni kwake,baada ya kujisachi akajikuta hana funguo cha chumba,alivyonyonga kitasa mlango ukafunguka.Ilikuwa kidogo apige kelele baada ya kugundua kuna mtu ndani kwake.
“Umeingiiiaje humuuu?Talk to me”
Ahmed,aliuliza huku akimshangaa Necka Golden, aliyekuwa juu ya kochi!Memori kadi iliyokuwa ndani ya ubongo wake,ilifuta faili la Necka Golden kutokana na pombe kali aliyokunywa.Akawa anakumbuka na kusahau.
“Aaah,ulikuja leoooo mchana”
Haikujulikana kama lilikuwa swali ama anazungumza.Hiyo ilimfanya Necka Golden atulie kidogo na kumtizama,akaishiwa pozi!Alishajua tayari kwamba Ahmed amekunywa pombe, kutokana na harufu kutapakaa eneo zima la seble.
“Karibu,nimekusubiri sana”
Necka Golden,akasema.Ahmed hakujibu chochote badala yake, akapitiliza mpaka chumbani huko alijitupa kitandani kama mzigo!Kutokana na pombe kali aliyokunywa,ilimfanya apate usingizi mzito!Akiwa katikati ya usingizi,kuna kitu kisichokuwa cha kawaida akahisi kinamlamba sikioni mwake,kwa mara ya kwanza alidhani yupo ndotoni,akajilazimisha kufumbua macho yake na kumuona Necka Golden,yupo sikioni kwake kapenyeza ulimi ndani kabisa.Anachokonoa sikio,alifanya kitu hiko kiuwoga lakini ilibidi akate mshipa wa aibu.
“Ahmeed tuliaaaaaa”
Necka,alisema maneno hayo kimahaba akiwa sikioni kwa Ahmed amejilegeza,mikono yake inapapasa mgongo,hakuishia hapo.Akamsogeza kidogo na kuanza kumfungua vifungo vya shati.Akamsogelea mdomoni na kuanza kumla denda.Mpaka inafikia hatua hiyo,Ahmed alikuwa kimya kabisa,hakuwa ana ubavu wa kupinga hoja kama hiyo nzito.Mbaya zaidi alikuwa kesha kunywa pombe, hakuweza kuchukuwa maamuzi ya haraka,damu yake ikawa inatembea kwa kasi ya ajabu!Huo ndio ulikuwa mwanya wa Necka Golden,kuitumia nafasi hiyo bila makosa!Namna alivyokuwa anamtomasa Ahmed iliogopesha,akaingiza mkono mpaka ndani ya zipu na kutoa tango lililokuwa tayari limesimama,akajaza mate mengi mdomoni na kulitumbukiza tango mdomoni.
“Aaaaah”
Ahmed,alitoa mguno mzito wa ndani kwa ndani,hakujielewa tena!Mtoto huyu Necka,hakuishia hapo.Akaanza kutoa suruali ya Ahmed,yote na kumvua shati,akaitoa na boxa yake pia.Ahmed,akabaki kama alivyozaliwa.Kwa kasi ya ajabu nayeye akaanza kuzitoa nguo zake,alivyohakikisha yupo mtupu,akaweka mguu mmoja wa Ahmed Mashariki na mwingine Magharibi,akapita katikati na kuiweka maiki ya Ahmed mdomoni huku akiwa anampapasa papasa kifuani,akatoka hapo na kuibana miguu kwa pamoja.Tango,lilikuwa limesimama dede nene na refu,Necka Golden!Akapanua miguu na kupanda kwa juu ili aanze kuendesha farasi,akaanza kukaa taratibu.Tango likawa linaingia asteaste ndani ya mgodi, mpaka likafika mwisho kabisa!Akaanza kuzungusha nyonga zake taratibu,akiwa juuu.
“Aaaasssh! Aaah! Aaaah!”
Hio ndio miguno,iliyokuwa ikitokea kwa Necka Golden huku akiwa ameyafumba macho yake,akisikilizia tango lililokuwa ndani ya mgodi wake!Hakutofautishwa na mtu anayejichokonoa na pamba,masikioni.


Raha aliyokuwa akihisi haikuweza kuelezeka kiwepesi,kifupi hakutegemea kama mambo yangekuwa marahisi namna hiyo!Alishukuru sana kwa Ahmed kunywa pombe kwani vinginevyo kibarua cha kufanya anachokifanya kingechelewa ama asingeweza kufanikisha!Aliendelea kukizungusha kiuno chake,akajisogeza karibu na mdomo wa Ahmed akatoa ulimi na kuutumbukiza kinywani mwa Ahamed,wakaanza kunyonyana ndimi kwa fujo.Mambo hayakuishia hapo,Ahmed hakutaka kuonekana mzembe, nayeye akaonesha ushirikiano, akam-binua Necka Golden na kumlaza vizuri chali,hakuchelewa apanua mdomo na kufakamia kifua cha Necka, ambapo alianza kulamba chuchu,hapo ndipo Necka alihisi kama roho yake inaacha mwili,akahisi kama yupo angani vitu vyote anaviona kwa chini.Mechi hiyo ilidumu kwa kipindi kirefu hiyo ni kutokana na Ahmed kutumia kilevi aina ya Konyagi!Mtanange ulikuwa mkali na kufanya Necka aende mizunguko takribani mitano, ndipo Ahmed,akawa amefika safari yake.Akatulia kidogo juu ya kifua cha Necka,wakiwa hivyo hivyo wakapitiwa na usingizi mzito.

*******
Kichwa chake kilikuwa kizito kama kobe! kinamuuma kupita kiasi,tumbo halina kitu.Hakuwa ana uhakika kama usiku wa jana yake kabla ya kulala alikula ama la.Bado akiwa amefumba macho,alijaribu kuvuta kumbukumbu za siku ya jana ilivyoenda,akamkumbuka Gabriel walivyokuwa wote wanalewa pombe.Wakati akitafakari mambo hayo na kuwaza, akajigeuza kitandani,hapo ilibidi ashtuke sababu alihisi hana nguo hata moja!Akafumbua macho yake,akili yake ikarudi nyuma kwa kasi ya ajabu,akamkumbuka Necka Golden!Kilichomuogopesha zaidi alivyoangalia chini akaona chupi ya kike, kumaanisha bado yupo!Huo ulikuwa ni ukweli kwani hapohapo Necka Golden alifungua mlango akatanda mlangoni,akiwa amevaa kanga moja tu peke yake.
“Chai ipo tayari Mpenzi,sukari iko wapi?Siioni”
Kulala na Ahmed mpaka asubuhi alijihesabia moja kwa moja tayari ni wapenzi,hicho ndicho kitu alichokiamini,ndiyo maana asubuhi na mapema akaamka kutoka kitandani na kuandaa chai nzuri,kifupi akavaa uhusika wa Mke na Ahmed ndiye mumewe.
“Necka,unafanya nini hapa?”
Lilikuwa ni swali la kitoto, kuliuliza mtu mzima mwenye akili zake timamu.
“Sukari iko wapi?Tutaongea baadaye”
“Juu ya friji,kwenye kontena la kijani”
“Okay,kaoge uje kunywa chai sasa”
Necka akazungumza kwa kujilegeza huku akimtizama Ahmed, aliyekuwa yupo kitandani bado,akageuka na kuanza kutoka.Nyuma,alivyokuwa anatingisha ilimfanya Ahmed amtizame!Alikuwa mwenye vitu vingi sana kichwani kwake anavitafakari,alijaribu kukiumiza kichwa chake na kukisumbua ilikuwaje mpaka akalala na Necka Golden,jibu alilopata ni moja tu,pombe!Dakika mbili baadaye akatokeza tena Necka, mlangoni.
“Jamaani Ahmed,chai tayari nenda kaoge basi”
“Sawaaa,kichwa kinaniuma”
Ahmed,akatoka kitandani akiwa na aibu akimsubiri Necka atoke ndipo apite bafuni.
“Nataka kuvaa taulo”
“Vaaa tu kwani kuna shida gani?Alafu humu ndani hauna panadol umeze”
“zipo”
“Meza tafadhali,kunywa maji mengi.Hizo ni hangover”Ahmed,akafanya hivyo,akainua mkono wake akiwa amelala hapohapo,Necka akampa maji ya kunywa ili ameze dawa!Bado alikuwa ametanda mlangoni,anamsubiri Ahmed aingie bafuni.Chumba hiko kilikuwa kina bafu la ndani kwa ndani yaani ‘self contained’ kwa lugha ya kitaalam,alichofanya Ahmed ni kuliviringisha shuka mwilini mwake vizuri na kuzama bafuni, ambapo huko alikuta mambo mageni,maji ya vuguvugu.
Pembeni kuna sabuni amewekewa tayari,choo kisafi.Hakukuwa na swali la kujiuliza hapo, jibu likaja hapohapo ya kwamba Necka ndiye kafanya hayo yote.Akajimwagia maji na kupiga mswaki,akafanya kila kitu!Akavuta taulo na kujipangusa maji mwilini,alivyofungua mlango akaona kitanda,kimetandikwa vizuri kimewamba kama ngoma!Kifupi vitu hivyo vilikuwa vigeni kwake,kuna vitu Hajrath aliwahi kuvifanya lakini Necka Golden alimzidi,sio siri binti huyo siku hiyo alitia fora,Ahmed akajisikia vizuri akapita mpaka kabatini ili kuangalia nguo safi,itakayomfaa siku hiyo.Alivyovaa,akapaka mafuta na kujipulizia marashi, akafungua mlango ili atokeze seblen!Huko ndipo alipigwa na bumbuazi la waziwazi,seble ilikuwa safi, vitu vimepangwa vizuri.Juu,ya meza kuna hotpot,pembeni kuna sahani juu ina mayai ya kukaanga na mikate iliyopakwa siagi!
“Karibu chai”
Necka akasema na kuchukuwa vikombe viwili,akaanza kumimina chai.
“Ahsante”
Kuanzia hapo kazi ya Necka ikawa ni kumimina chai,mara aweke sahani vizuri mara akate mayai, ilimradi mahaba niue.Baada ya hapo akaweka sukari kwenye chai kisha kukoroga,kila kitu kilivyokuwa sawa akamtizama Ahmed!
“Karibu Mme wangu”
Ahmed,hakusema chochote alichofanya ni kuchukuwa chai!Njaa ilimuuma ndiyo maana akaanza kufakamia mayai na kuchukua mikate na kula huku bado akiendelea kuutafakari ukarimu wa msichana huyo mrembo aliyekuwa pembeni yake,bado hakuelewa kama ndiyo mahaba ya mwanzo mwanzo,anafanya hivyo ili amteke ama ndivyo alivyo,alishindwa kupata jibu la kitendawili hiko kizito.
Japokuwa alikuwa hapo lakini akili yake ilisafiri umbali wa maili mia moja,akaanza kumtafakari Hajrath,jinsi walivyokuwa wakiishi kwa furaha!Ghafla ikamjia picha ya mchana wa jana,namna alivyomfumania ‘hostel’ na mwanaume mwingine,moyo ukamuuma ajabu!
“Jana ilikuwaje?”
Ahmed,akavunja ukimya!Alitaka kujua tukio la usiku wa jana lilivyokuwa,alielewa vizuri sana walichokifanya lakini alitaka kupata mkanda kamili.
“Kula kwanza bwaaana,nitakwambia”
“Mmmh,unanitisha”
“Kwanini nikutishe?”
“Maana sielewi”
“Utaelewa tu”
Jibu hilo hakulisema kwa sauti bali kimoyo moyo huku akimtizama Ahmed kwa macho ya husda.Zoezi la kupata kifungua kinywa lilivyokamilika, Necka akatoa vyombo na kupangusa meza,akapitiliza mpaka jikoni.
Alipopanga Ahmed,hakukutofautishwa na mfanyakazi aliyeajiriwa kwani alikuwa ana sehemu ya jiko,chumba kimoja na seble kubwa kiasi.Necka aliingia jikoni na kuosha vyombo vyote!
“Leo huendi chuo?”
Ahmed akauliza.
“Sina kipindi leo,nitaenda hostel tu”
Sauti kutokea jikoni ikafika mpaka Seblen alipokuwa ameketi Ahmed,alivyosikia jibu hilo akaingia chumbani.Haikupita hata dakika moja,Necka akiwa ana kanga yake akatokeza na kuufunga mlango!
“Ahmeeed”
Ilikuwa ni sauti ya Necka ikiita.
“Yes”
“Nakupenda sana,naomba nikubali niwe mpenzi wako.Nitajiita mwenye bahati”
Haikujulikana kama ni kigugumizi ama mdomo wake ulijaa mate,Ahmed alishindwa kutoa jibu hilo moja kwa moja na kubaki anamtizama Necka Golden aliyekuwa mbele yake ana kanga moja peke yake,macho yake amelegeza kama mtu aliyekula kungu,anazungumza kwa mahaba na mikogo!Kwa kweli,Ahmed alikuwa katika wakati mgumu kuliko kawaida,hakuelewa ni kitu gani akiseme, ndiyo maana akabaki kimya akimtizama Necka.Ambaye alianza kutembea akimfuata kitandani alipo!
“Nijibu Mpenzi,usinitese naumia Ahmed.Wewe ni Handsome”
“Na Hajrath akijua je?”
Ahmed,akaropoka kitu ambacho hakupanga kukizungumza kwa wakati huo!
“Hawezi kujua”
“Sasa sasa ita ita ku..”
Hakuelewa kigugumizi kilitokana na nini lakini alikuwa tayari yupo karibu, akamsogelea midomoni,akatoa ulimi wake na kuupitisha kinywani kwa Ahmed,ambao ulipokelewa wakaanza kulana denda,Necka hakuchelewa akatupa kanga yake kando na kuanza kujisogeza vizuri kitandani ili aanze kufaidi tunda!
******
“Nishasema,kama huwezi niambie nikutafutie mwanamke mwingine.Mwanamke hazai.Huuu mwaka wa tatu sasa,mimi nasubiri mjukuu.Kama mwanamke hazai sasa ni wa faida gani?Atakusaidia nini?”
“Lakini Mama,hiyo ni mipango ya Mungu”
“Hakuna cha mipango ya Mungu.Yule mwanamke ni mgumba.Na nina uhakika,keshatoa sana mimba.Ndio maana kizazi chake kimelegea,kila akishika mimba watoto wanakufa.Au anawatoa kafara?”
“Mama umefika mbali,hilo swala niachie mimi na mke wangu,tutazungumza.Alaf isit…”
“Kelele Erasto,mimi ni Mama yako!Nikuachie wewe na mkeo?Kwa mantiki gani?”
Ilikuwa ni asubuhi na mapema,nje ya uwanja wa kuegesha magari alisimama Mama Erasto,anaongea kwa sauti kubwa sana!Mbaya zaidi sauti yake ilikuwa kali mno, kiasi kwamba nyumba za jirani walikuwa wanasikia kinachozungumziwa.Erasto alijaribu kujitetea lakini ilishindikana, sauti yake ilizidiwa na kelele za Mama yake mzazi, ambaye kila siku alikuwa akimpigia kelele kuhusu yeye kupata mtoto. Marry Frank, Mke wa Erasto.Alisikia kila kitu.Moyo wake ulimuuma ajabu,akashindwa kuvumilia akabaki analia machozi ya kwikwi akiwa chumbani,hakuelewa ana mkosi gani. Wakati mwingine swala hilo la watoto wake kufia tumboni, alilihusisha moja kwa moja na ushirikina japokuwa hakutaka kuyapa mawazo hayo kipaumbele.
“Eeeh Mu..ngu nime..kosea wapi?”
Marry,alimlalamikia Mungu wake huku akibubujikwa na machozi kama mtoto mdogo,maneno aliyokuwa anayasikia yalikuwa ni kama sumu kali ya mdudu tandu!Hakutegemea kama ipo siku moja Mama yake mkwe, angetamka maneno kama hayo mazito kwani siku zote walikuwa wakicheka wote vizuri zaidi na hayo walikuwa ni marafiki wakubwa sana,alibakia kujuta kuolewa!Kifupi,maisha yake kila siku yalikuwa ya kulialia kila kukicha.
“Erasto,ninaondoka!Lakini tambua Mama yako,nataka mjukuu”
Mama alimaliza kutoa yake ya moyoni,akafunga geti na kutoka zake nje.Huku nyuma akimuacha Erasto,akiwa na mawazo mengi sana.
Upande mwingine wa shilingi, jambo aliloambiwa aliliona lina mantiki,ndiyo maana akageuka na kuingia ndani, badala ya kuingia ndani ya gari ili aanze safari ya kwenda kazini,akazama mpaka chumbani na kumkuta mkewe analia machozi ya kwikwi.
“Nadhani,umemsikia Mama alichoongea!”
Sijui siku hiyo Erasto alipandwa na shetani gani,sababu alizungumza kwa hasira za waziwazi, hakuwa Erasto wa siku zote,anayempa moyo mkewe,hakuwa Erasto wa siku zote anayemwambia mkewe ‘Usijali Mungu yupo’hakuwa Erasto anayemfuta machozi mkewe akimkingia kifua na kumpa moyo!Siku hiyo ilikuwa kinyume chake,hakuongeza lingine zaidi.
Akaondoka zake kuelekea kazini.Huku nyuma akimuacha Marry,analia kwa uchungu akitafakari juu ya ndoa yake kwa ujumla.
Siku hiyo, hata chai haikupita kabisa,machozi yalimtoka.Kitu cha kwanza kukikumbuka ni Mama yake mzazi,hapohapo akampigia simu na kumueleza kila kitu kilivyotokea!
“Njoo nyumbani tuongee Mwanangu,usilie”
Upande wa pili wa simu,ulisikika mama akimwambia Mwana.
“Ma…ma inauma,naumi..a”
“Usilie,njoo nyumbani nitakwambia cha kufanya.Tatizo lako litaisha”

*******
Siku zote kwenye msafara wa mamba ni lazima kenge watakuwepo tu!Hajrath aliamini kwa asilimia zote mia,kupitia rafiki yake Necka Golden ataweza kurudiana upya na Ahmed ingawa jambo hilo linazidi kuwa gumu sana baada ya Ahmed kulishuhudia tukio la Erasto kutoka chumbani kwake,kichwa kinazidi kumuuma.Akashindwa kabisa kuhudhuria vipindi darasani,akitoa visingizio na sababu zisizokuwa na kichwa wala miguu. Mara aseme anaumwa mara ana dharura ni wazi kwamba alikuwa ananyanyaswa na ‘stress’ za mapenzi.Zaidi na hayo alikuwa akimuwaza Ahmed muda wote,mategemeo yake yote yakaegamia kwa Necka Golden, ambaye alimuhakikishia ya kwamba kila kitu kitakuwa sawa!
“Nitazungumza na Ahmed,wala usijali besti. Kwanza nishazungumza naye.Bado anakupenda lakini subiri nimuweke sawa”
Siku hiyo Necka,alimhakikishia Hajrath jambo hilo,zaidi na hilo akamuhaidi ya kwamba atafanya juu chini,awakutanishe na Ahmed.Hajrath hakuelewa kwamba rafiki yake ni mkia wa fisi,anamzunguka na kumlamba kisogo!
“Jitahidi,leo pia uwende.Umwambie nampenda sana msisitize.Mwambie siwezi kula, kila siku nalia”
Hajrath alizungumza kwa upole na unyenyekevu wa hali ya juu sana.Macho yake yakiwa mekundu mno kwa ajili ya kulia kila kukicha.
“Lakini uwe unaenda darasani sasa”
“Alafu mbona unanukia harufu ya Ahmed?”
Swali hilo lilitoka kwa Hajrath,marashi ya Ahmed, aliyatambua ingawa aliuliza swali hilo kiutani lakini jibu lilikuwa ni kwamba Necka Golden, usiku wa siku hiyo alilala na Ahmed kitanda kimoja,akajipulizia na marashi yake pia, siku hiyo asubuhi.
“Perfume sasa hivi zipo nyingi.Hii Dolby,mbona hata Latifa anayo”
“Basi hapa moyo unadunda mwenzako,perfume hiyo nimezoea kumsikia Ahmed ananukia”
“Utakufa kwa presha”
“Lazima,si unajua ninavyompenda.Akikubali tu,nitafanya sherehe.Nitatangaza chuo kizima kuwa nipo naye”
“Utasubiri sana mwaka huu”
Necka Golden,alijisemea kimoyomoyo huku akipachika tabasamu la plastiki usoni,akamkumbatia Hajrath na kumpiga piga mgongoni kidogo akimpa pole,kisha kusimama na kuaga!Alivyotoka nje tu,akatoa simu yake na kumtafuta Ahmed hewani.
“Baby,upo wapi?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kuuliza.
“Nipo geto bado”
“Ushakula?”
“Mmmh,lunch au?”
“Yes Darling,lunch”
“Bado”
“Sasa,usitoke leo nataka kukupikia maanjumati,usiende kula popote pale Sweatheart”
“Sawa,mimi nakusikiliza wewe Kipenzi”
Tayari walikuwa katika mapenzi mazito,Necka alihakikisha na kuapia kumteka Ahmed mazima,ampe dozi kamili.
Kitu kingine kilichomfanya ampende mwanaume huyo ni namna anavyofanya mapenzi vema,sio siri katika sekta ya sita kwa sita Necka,alinyanyua mikono juu, ndiyo maana muda wote akatamani awe kitandani anafanya tendo hilo lililowaleta duniani.

********
Siku zilizidi kukimbia,mapenzi kati ya Necka Golden na Ahmed yakazidi kuwa motomoto,siku hadi siku.Kilichompagawisha zaidi Ahmed ni namna msichana huyu alivyokuwa anamjali,ilikuwa haipiti siku bila kuletewa zawadi,kama sio shati basi vest ama viatu.Vitu vidogo kama hivyo vilifanya akili ya Ahmed,imfute kabisa Hajrath kichwani.Akamsahau mazima,hakutaka tena kumsikia wala kumuona.Siku zote penzi ni kikohozi kulificha huliwezi,mbali na kujificha ficha na kufanya mambo yao mbali na chuoni hapo Makumira lakini uvumi ukaanza kutapakaa na mwanafunzi wa kwanza kuzidaka habari hizo, alikuwa ni Mpangw’a rafiki yake mkubwa sana na Hajrath,hakutaka kukaa na jambo hilo kifuani.
Ilibidi ampashe habari hizo rafiki yake kipenzi.
“Mmmh,haiwezekani.Necka hawezi kufanya hivyo.Wewe hujui wanafunzi wa hapa chuo kwa kuzusha vitu,hayo ni maneno tu”
Hajrath,alikataa katukatu.
“Lisemwalo lipo lakini”
“Watu wana majungu sana,Necka ananiwekea mambo sawa!Leo nitaonana na Ahmed”
“Ndivyo alivyokwambia?”
“Ndio”
“Basi,makubwa hayo!Maana mimi nimesikia sikia huko, huo ubuyu”
“Wapi?”
“Kwa akina Christopher,huyu nani huyu Irene Mriba, nayeye kaniambia”
“Achana nao,Necka hawezi kufanya kitu kama hiko ni rafiki yangu sana”
Hajrath aliongea,akijifariji ki ukweli alikuwa nyuma ya kila kitu.Aliendelea kuamini ya kwamba Necka asingeweza kumzunguka hata kidogo,ndiyo maana maneno aliyoambiwa aliyatupilia mbali na kuyatafsiri kama majungu na fitna za wanachuo, wanaopenda kila siku alielie na kuumia.
“Watu wengine bwana,eti Necka anatoka na Ahmed.Kitu hiko hakiwezekani hata kama Yesu arudi sasa hivi”
Hajrath,alizungumza kwa kujiamini.
“Mkude,kakuulizia leo”
“Wapi?”
“Class, kaingia”
Ilibidi Mpangw’a abadili mada alivyoona,jambo alilolileta, Hajrath halisapoti.
“Anasemaje?”
“Katoa,assignment na group work ya watu kumi kumi”
“Umenitafutia group?”
“Tumesaini,nilikuombea group la akina Grace Charles.Baadaye aka register majina yote.Na anahitaji hiyo kazi kesho,kwa hiyo hauna group”
“Sasa itakuwaje?”
“Inabidi umfate ofisini kwake.Atachukuwa asilimia thelathini kwenye hiyo kazi,fanya umuone Mkude, Hajrath”
“Sawa,nitamfata leo ofisini kwake”
“Usiache kumuona si unajua test zinakaribia”
Mambo mengi walizungumzia siku hiyo,lakini mada hiyo ilivyoisha na Mpangw’a alivyoondoka sura ya Ahmed ilimjia kichwani tena,akaanza kuumia kwa mara nyingine.Hapohapo,akachukua simu akapiga moyo konde na kumtafuta Ahmed hewani lakini simu haikupokelewa,akajaribu tena na tena lakini hakikubadilika kitu.

********
Sio siri,Necka Golden alipenda mapenzi kuliko chakula.Ndiyo maana kila wakati akatamani awe na Ahmed,wafanye ngono.Siku hiyo alikuwa kitandani yupo uchi wa myama.Miguu yake imechanuliwa huku na kule.Ahmed kaishika miguu, ulimi wake upo nje,anaulamba mgodi mithili ya paka anavyolamba maziwa juu ya kisosi.Mkono mmoja,upo juu ya kifua cha Necka,unatomasa chuchu.Hapo ndipo msichana huyu mdogo alihisi moyo wake unaacha mwili,kazi yake ikawa ni kushika mashuka na kulamba midomo,macho ameyafumba,raha alizohisi hazikuwa za kawaida hata kidogo,Ahmed akaona haitoshi akamsogeza vizuri.
Safari hiyo alitumia kidole chake kucheza na mgodi,ulimi wake ukawa unalamba chuchu za Necka,zilizokuwa zimesimama wima kama mwiba!Alivyohisi kidole chake,kina ute ute.Akashuka kidogo na kuseti mitambo ili aanze kazi ya uchimbaji mgodi.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
“Ngo!Ngooo!Ngooo!Ngoooo”
Sauti ya mlango kugongwa ilisikika lakini hakuna hata mmoja kati yao aliyesikia, kutokana na jambo walilokuwa wamelianza,ukaendelea kugongwa tena.Ahmed,akaanza kusikia kwa mbali kelele hizo za mlango, alivyotaka kuchomoka,akavutwa ili zoezi hilo liendelee.
“Ahmed pleaseeee”
Necka Golden,alizungumza kwa sauti ya puani,macho yake yakiwa yamelegea huku akimvutia Ahmed kiunoni kwake ili ndizi izame ndani ya mgodi,hakuwa tayari kukatishwa utamu na kumuacha atoke aende kufungua mlango, uliokuwa unagongwa kwa wakati huo!


Mlango uliendelea kugongwa lakini hakuna mtu yoyote aliyejishughulisha nao!Kilichosikika hapo kwa mbali ni kitanda kunesa,Ahmed na Necka Golden walikuwa wakipinduana pinduana.Kila mtu alitaka kumuonesha mwenzake yeye ndiye yeye,ilielekea siku hiyo kila mtu alimpania mwenzake, ndiyo maana tendo hilo lilidumu kwa nusu saa lizima.Hata hivyo baada ya kuingia bafuni na kuoga waliendelea na mechi hiyo ya kukata na shoka.Saa kumi na moja ya jioni, ndipo kila mtu alipata nafasi ya kuzungumza na mwenzake wakiwa wote ndani ya shuka moja,Necka amekiweka kichwa chake juu ya kifua cha Ahmed,anadeka kama mtoto mdogo!
“Nakupenda Ahmed”
“Hata mimi,umejuwa kuniweza leo”
“Kukuweza kivipi?”
“Wewe hujui?”
Ahmed akajibu kwa swali.
“Sijui,ndio uniambie sasa”
“Upo vizuri kila idara”
“Hata wewe Darling”
Necka alivyozungumza hivyo,akapitisha mkono wake chini ya shuka,akamshika nyoka wa Ahmed, ambaye alikuwa ametulia kidogo baada ya kutoka kutema sumu ndani ya shimo.
“Tabia mbaya hiyo”
Ahmed akasema kiutani huku akichezea nywele za Necka,mashine yake ilikuwa ikiguswa na taratibu ilianza kuvimba.
“Tabia gani?Wakati nimeshika utamu wangu”
Kila kitu kilikuwa burudani kwa wawili hawa,mambo yalikuwa mukide mukide!Wakajihisi kama wapo pepo ndogo,kwa raha na burudani walizokuwa wanapeana.Baada ya maongezi ya hapa na pale,wakapasha na dakika mbili baadaye kilichosikika ni sauti za mahaba.
“Ahmeeeeed,yeees aaah aaah,haaapo haaapo hivyooo hivyoo assshiiii”
Necka alilalamika akitolea sauti yake puani,ilielekea amekamatika vilivyo,hakuwa anaongea hivyo kwa kupenda lakini raha alizohisi zilimfanya aropoke huku akikinyonga kiuno chake kwa fujo!

********
Mawazo yalikula akili yake pamoja na Mwili,uzito wake ulipungua ghafla kutokana na ‘stress’ za mapenzi alizokuwa nazo kichwani.Kula kwa wakati lilikuwa ni jambo hadimu kulifanya.Mawazo yake yote yalikuwa kwa Ahmed,hakuelewa ni kwa njia gani angempata tena arudi katika himaya yake!Kitu kingine kilichomuumiza zaidi ni uvumi uliokuwa unazidi kila kukicha ya kwamba Necka Golden na Ahmed ni wapenzi.Jambo hilo lilimuumiza sana akili na kuuchoma mtima wake,japokuwa aliamini kwamba kitu kama hicho hakiwezi kutokea lakini ilifika kipindi, moyo wake ulijawa na wivu,alivyojaribu kumuuliza Necka Golden, hakupewa jibu la kumridhisha!
“Haiwezi kuwa hivyo,kazi yako ndio inafanya watu wahisi mimi na Ahmed ni wapenzi,wanafunzi wa hiki chuo ni wachonganishi sana.Wasione kitu,watakikuza”
Hilo ndilo lilikuwa jibu la Necka Golden kila kukicha.
“Mbona juzi hukuniletea taarifa?”
“Taarifa zipi?”
“Si ulisema Ahmed anataka kuonana na mimi?”
“Hata mimi nashangaa,sijui ilikuwaje.Tangu jana sikumpata”
“Siku hizi hapokei simu zangu kabisa,nilienda kwake kugonga hakufungua.Jana ulikuwa naye?”
Baada ya kuhitimisha maneno hayo,akaibua swali.Mawazo ya Necka Golden, yakarudi nyuma kwa kasi ya umeme ama mithili ya kompyuta isiyokuwa na mafaili.Akakumbuka jioni ya siku iliyopita,alivyokuwa kitandani na Ahmed,moyo wake ukapiga kwa nguvu akaanza kutetemeka, japokuwa hakuelewa ni kwanini.
“Uli uli ulienda kwake jana?”
Akauliza akiwa mwenye kigugumizi,japokuwa hakujua ni wapi kimetokea.
“Ndio,nilienda kwake.Niligonga kwake,nikakaa sana nje!Muda ukawa umeenda nikaamua kurudi hostel”
“Pole sana!Niachie mimi,nitarekebisha kila kitu”
“Kwani ulivyomwambia,nahitaji kuonana naye.Alisemaje?”
“Hakusema kitu,aliniambia sawa.Atafanya hivyo”
“Necka,Ahmed atanirudia?Unavyoona wewe, atanisamehee?”
Laiti kama angejua mtu anayezungumza naye moyoni yupo vipi,angemuogopa kama ukoma.Hajrath alikuwa katikati ya giza nene lililozungukwa na simba wakali,alichokuwa anakosea ni kumwambia kila kitu kuhusu Ahmed,sijui ni kwa nini alitokea kumuamini namna hiyo.
Kuanzia siku walivyotoka hapo,akawa msumbufu!Kila kukicha alimtafuta Necka hewani akimuuliza ni wapi alifikia,siku za mwanzoni alipewa ushirikiano lakini siku zilivyozidi kwenda mbele,mawasiliano yakaanza kukatika taratibu, wakati mwingine Necka alitoa majibu ya mkato kwani jambo hilo kwake lilikuwa kama kero.
“Niko bize Hajrath”
Siku hiyo Necka alijibu kwa ukali simuni.
“Uliongea na Ahmed?”
Hajrath,akarudia swali lilelile.
“Nimekwambia nipo bize,mpigie kwenye simu yake”
“Hapokei simu zangu”
“Shauri yako,mimi nifanye nini sasa?”
Simu ikakatwa,ikimuacha Hajrath kwenye mataa.Hakuelewa kama Necka alikuwa amelewa pombe ama kuna mambo fulani fulani yanamchanganya,hakutaka kumfikiria vibaya.Akajipa moyo na kudhani wenda msichana huyo yupo bize.

Siku zikazidi kujongea,mawasiliano kati ya Necka Golden na Hajrath,yakakatika kabisa,hapo ndipo taratibu akili yake ikaanza kufunguka na kupata picha ya maneno yaliyokuwa yanazungumziwa,akaamua kuvaa ujasiri na kuanza kulifuatilia kiundani zaidi.Hakutaka kujua ataumia moyo kiasi gani, endapo angegundua Necka Golden, amemzunguka japokuwa jambo hilo hakutaka liwe kweli.

********
Ahmed na Necka Golden,waliongozana kila mahali kama kumbikumbi.Jambo hilo halikuwa tena siri,chuo kizima cha Makumira kilitambua.Lakini kuna wanafunzi wengine,hawakuamini walilichukulia jambo hilo kama skendo na uvumi tu,wengine hawakutaka kuliamini moja kwa moja!
“Haiwezekani,Ahmed huyuhuyu?”
“Ndio,anamgonga Necka”
“Ahmed?”
“Bwege nini,ndio”
“Inabidi Ahmed,nimtafute nimuulize vizuri kama kweli anamkaza yule gashi”
“Unaambiwa juzi,Ahmed kapigiwa magoti na Hajrath”
“Hajrath ganii?”
“Yule mwenye choo,anayejambia mbali”
Kiswahili walichotumia kilikuwa cha geto.
“Si,yule mwenye msambwanda?”
“Kuna Hajrath zaidi yake hapa chuo?Huyo huyo.Sasa kapiga magoti,analia kama mtoto unaambiwa, Ahmed anatumia kizizi sio bure”
“Weeee!Acha masihara,kisa nini?”
Walikuwa ni wanaume lakini wenye tabia za kike,kwa wanaume kama hao haikuwa kawaida kukaa vigenge na kupiga hadithi za umbea,lakini hiyo ilikuwa topiki namba moja siku hiyo na walizungumziwa watu watatu,Ahmed,Necka na Hajrath.Sio genge hilo tu,kifupi kichwa cha habari cha wiki hiyo ndani ya chuo cha Makumira, kilikuwa ni juu ya watu watatu.Licha ya chuo kizima,kufanya habari hiyo kuwa kichwa cha habari lakini kwa Hajrath hakutaka kuamini moja kwa moja, alikuwa kama Thomaso,ilikuwa ni lazima ashuhudie mwenyewe eitha kwa kumuuliza Ahmed mwenyewe ama kuwafumania ‘live’,hapo ndipo angeamini vinginevyo hakutaka kuamini, maneno ya kuambiwa!Siku hiyo kulivyopambazuka tu akafunga safari,mpaka Ngulelo!
“Ahmed yupo?”
Siku hiyo alifika geto la Ahmed,asubuhi na mapema.Akamuuliza Msichana mmoja aliyemkuta nje,amebeba ndoo ya maji anaelekea bafuni.
“Dada,hata salamu!”
“Samahani dada,siko sawa.Nisamehee,za asubuhi?”
“Nzuri tu”
“Namuulizia Ahmed,sijui nimemkuta?”
“Sina uhakika saaaana,nilirudi jana nimechelewa.Nilimsikia usiku akiingia,jaribu kumgongea”
“Sawa ahsante”
Hajrath,akatembea mpaka karibu na mlango ili agonge,mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu.Alikuwa mwenye hofu mno,japokuwa hakuelewa hali hiyo inatokana na nini,mbali na hapo hakujua ni sentensi gani ya kwanza, aiseme endapo Ahmed,angeufungua mlango!

******
Ilikuwa ni asubuhi ya saa kumi na mbili kasoro mbili,kulikuwa kuna kibaridi fulani cha uchokozi,ambacho kilimfanya Necka Golden ajivute karibu na Ahmed,akamkumbatia na kuendelea kuuchapa usingizi.Dakika tatu baadaye,akahisi kama mlango unagongwa,akasikiliza vizuri. Hakuwa ana uhakika kama ni mlango wa Ahmed ama ni jirani kwani ilikuwa ni asubuhi sana!Akaanza kumtingisha Ahmed,aliyekuwa amelala fofofo kando yake!
“Baby,baby,baby”
Necka,aliita.Kwa mbali Ahmed,alianza kujigeuza geuza.
“Mmmmh”
Akaguna na kugeukia upande wa pili,akamkumbatia Necka kwa nguvu!
“Baby,kuna mtu anagonga”
“Kafunguee”
“Hapana,nenda wewe”
Ahmed,akashusha pumzi kidogo.Akatega sikio lake ili kuhakikisha kama jambo hilo lilikuwa lina ukweli au ni mawenge ya usingizi.
“Nani tena asubuhi subuhi aah”
Ahmed,akazungumza.Akionekana kukerwa na tukio hilo alilolitafsiri kama ni usumbufu,akajizoa zoa na kuvaa bukta,akavuta na flana nyepesi, iliyokuwa kitandani.Akatembea na kufungua mlango,akapita mpaka seblen,akaingiza ufunguo na kuuzungusha.Akafungua mlango,sura aliyoiona ilimfanya ashtuke na kuyatumbua macho yake kama mjusi,aliyebanwa na mlango!
“Umefuata nini hapa?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kwa Ahmed kulitupa,sura yake ikiwa imejikunja.
“Nimekuja tuongee,Ahmed wangu”
“Utaongea nini na mimi?”
“Naomba nipe nafasi,dakika moja tu.Nijielezee mpenzi wangu”
“Hapana Hajrath,sitoweza!Sitoweza kabisa,naomba uwende.Nimeumia vya kutosha”
“Ahmed please,hujui navyokupenda.Just one minute,I’m begging you.Unachofikiria sicho kabisa”
Hajrath,aliomba na alizungumza huku akitia huruma akilipigania penzi lake,hiyo ilimfanya Ahmed atulie kidogo na kushusha pumzi ndefu ya kuchoka,kichwani alikuwa ana vitu vingi anaviwaza!Ndani alimuacha Necka Golden,lakini aliamini kivyovyote vile asingemruhusu Hajrath aingie chumbani.
Hakuelewa kwamba maongezi yao,yalimfikia Necka Golden akiwa chumbani kuna msemo ukamjia kichwani’Kama umechoka kuiba,fumaniwa yaishe’,msemo huo ukampa nguvu na kiburi!Akatoka kitandani na kuvuta kanga moja,akaiviringisha mwilini.
“Nakupa dakika moja tu.Dakika hiyooo moja tu,ukimaliza kuongea tafadhali uwende”
Ahmed,alizungumza kwa msisitizo.Hajrath kwa upole akainama ili kuvua viatu,alivyoinua sura yake!Moyo wake ukapiga paa!Baada ya kumuona Necka Golden yupo nyuma ya Ahmed,amevaa kanga moja peke yake.




Ukiachana na siku ambayo,hatokuja kuisahau katika maisha yake baada ya kumshuhudia mama yake mzazi anapigwa na Baba yake!Siku nyingine ambayo ilimuuma ni siku hiyo,hakuelewa ni kitu gani akifanye.Kwanza aliganda,pili hakuelewa ni kwanini ameishiwa nguvu na kushindwa hata kutembea.Kwake tukio hilo lilikuwa ni kama ndoto ya kutisha ambayo alitamani ashtuke ili akute jambo hilo sio kweli,haikuwezekana hata kidogo kumshuhudia Necka Golden, akiwa amevaa kanga moja tena ndani yupo Ahmed,jibu hilo lilitosha kabisa kujua ni kitu gani kinachoendelea.Butwaa alilopigwa halikuwa na kipimo chake,hiyo ilimfanya mpaka Ahmed nayeye ageuke nyuma.Moyo wake ulipiga kwa nguvu mno,jasho jingi likaanza kumtoka, japokuwa hakuelewa ni kwanini hali hiyo inatokea siku hiyo.Nyuma yake alisimama Necka Golden!Msichana mdogo mrembo,aliyevalia kanga moja ambaye kwa kipindi kifupi,penzi lao lilikuwa limenoga barabara,akageuza shingo yake mbele!Akamuona Hajrath, msichana aliyekuwa anatembea naye kimapenzi!Ambaye, walihaidiana vitu chungu mzima katika maisha yao,wakadiriki kwenda mbele zaidi na kula viapo ya kwamba wangefunga ndoa wazae watoto,Ahmed awe Baba, Hajrath awe Mama!Ahmed,akawa kama amepararaizi,akashindwa kujua ni kitu gani akifanye kwa wakati huo!
“Nee…ckaa”
Lilikuwa ni neno moja tu,alilotamka Hajrath. Haikujulikana kama anaita, ama anashangaa. Mbali na hapo alikuwa anahema juu juu,kifua chake kinapanda juu na kushuka!
“Unasemaje?”
Necka akajibu kwa madoido huku akibenua mdomo kwa dharau,akampandisha Hajrath kuanzia juu mpaka chini kwenye miguu.Hakutofautishwa na mtu anayetizama Kinyesi,bado Hajrath hakuamini jambo hilo.Akili yake ilimwambia wenda watu hao wanafanya maigizo na baadaye wangemwambia ‘Ingia ndani tulikuwa tunakupima’lakini jambo hilo halikutokea!
“Baby,tuingie ndani”
Necka Golden,akamwanbia Ahmed kimahaba huku akimvuta mkono!
“Ebu,niachie kidogo”
“Baby,kwani bado unampenda Hajrath?Niambie ukweli”
Ni wazi bila kupinga Necka Golden, alikuwa anatingisha kiberiti kama kina njiti,swali alilouliza lilimfanya mpaka yeye aogope,hakutaka kusikia jibu ‘Ndio nampenda Hajrath’,ndiyo maana hata yeye majasho yalianza kumtoka, baada ya kumuona Ahmed anavyomuangalia Hajrath.
“Hajrath..”
Ahmed akaita huku akimtizama machoni.Badala ya Hajrath kuitikia alibaki akimuangalia,sio kwamba alipenda lakini kulikuwa kuna kitu kama jinamizi limemkaba kohoni.
“Nasikitika kwamba,nimechelewa kukwambia.Huyu ndiye mpenzi wangu mpya,amechukuwa nafasi yako.Najua itakushtua, lakini amini nachokwambia”
Maneno ya Ahmed,yalikuwa ni kama mishale ya moto.Na alizungumza akiwa mkavu kabisa,hacheki yupo siriazi.Hakukuwa na nukta ya mzaha ndani ya maneno aliyoyasema.
“Nadhani umesikia,tafadhali nenda”
Necka Golden,akadakia maneno ya Ahmed akipigilia msumari kwani yalimpa nguvu akamsogelea karibu kabisa akamlalia begani kisha kumuangalia Hajrath kwa nyodo,kitu alichokuwa anakifanya alijua kabisa kwamba sio sawa na kilikuwa ni kitendo cha kinyama kwa kumfanyia mtu kama Hajrath,mpole,mnyeyekevu na mtaratibu.
Hasira na wivu vilimkaba kwa wakati mmoja,ilikuwa bora angehadithiwa ama kuendelea kusikia kwa watu habari hizo za Ahmed na Necka,kuliko kushuhudia kwa macho yake mwenyewe!Wakati mwingine alianza kujilaumu ni kiranga gani kilimtuma adamke asubuhi na mapema siku hiyo.
“Bor..a nimejua ma..pema”
Yalikuwa ni maneno matatu kutoka kwa Hajrath,machozi yalikuwa yanamtoka kama maji.Katika maisha yake hakuwahi kuumia namna hiyo katika swala la mapenzi,maumivu aliyokuwa anahisi moyoni mwake yalikuwa ni zaidi ya kidonda kilichomwagiwa spirit.
Mbele yake walisimama watu wawili,Ahmed na Necka Golden!Ki ukweli hakuamini picha aliyoiona, ndiyo maana akaanza kurudi kinyumenyume kama gari lililofeli breki, likiwa linapanda mlima,akajikwaa kwenye jiwe,alimanusura adondoke chini.
Alivyogeuka alianza kutembea kwa kasi huku akimwaga machozi,hakuwa anajali kama yupo barabarani ama la,kichwa kizima kilijaa mawazo,machozi yalikuwa yanamtoka,kwikwi imem-bana!Hasira ipo kiwango cha juu kabisa!Akaanza kukimbia ili awahi kufika hostel, ambapo huko hakujua ni kitu gani akifanye akiwasili!Ghafla,pepo baya likamvaa baada ya kuona duka la dawa,kushoto kwake karibu na stendi ya mabasi!
“No,hapana siwezi kuishi”
Hakuwa tayari kukumbana na aibu itakayompata baadaye,suluisho alilolichukua ni moja tu.Kujiua ili akimbie aibu,mbali na kujua ya kwamba vitabu vya dini vinakataza kujitoa uhai lakini hakujali.
“Eeeh Mungu,naomba unisamehe!Mungu hata kama ungekuwa wewe,ungefanya nini?”
Hajrath aliwaza huku akisukuma mlango wa duka la madawa,akafuta machozi haraka haraka ili muuza duka asimuhisi vibaya.Ilikuwa ni asubuhi sana kwani ndiyo kwanza Mama huyo, alikuwa akifagia duka hilo lililokuwa linauza dawa za binadamu.
“Karibu dada”
“Ahsante,una panadol?”
Hajrath aliuliza akiwa amejikaza.
“Ndio zipo”
“Nipe za elfu mbili”
“Za elfu mbili?”
Ilielekea Mama huyo kama alianza kuchezwa na machale,ndiyo maana akajibu kwa swali lililoambatana na mshangao!
“Ndio za elfu mbili,hata za elfu tano naomba”
“Unaumwa nini?”
“Kichwa,kinanisumbua sana”
“Mbona unachukua nyingi namna hiyo?”
“Nataka nyingine niweke akiba hostel,kuna wenzangu pia wamenituma”
“Mmmmh,sawa”
Mama hakuwa na jinsi,swala lake lilikuwa ni kupokea pesa sio kuhoji wateja maswali ndiyo maana hakutaka kuendelea na maswali yake, akiogopa mteja wake kuondoka na kukosa pesa,hapohapo akaingia kabatini na kuanza kutafuta vidonge aina ya Panadol,alivyoweka kwenye kifuko maalum,akapokea pesa!Hajrath akachukua dawa zake,akafungua mlango na kuanza safari ya kutembea, kuelekea pasipo julikana,ni kweli alidhamiria kujiua.
Ndiyo maana alianza kutafuta,sehemu salama ya kufanya kitendo hiko cha kujitoa uhai bila kubugudhiwa na mtu,ghafla picha ya Wazazi wake ikamjia kichwani,akawaona wanavyomlilia akiwa ndani ya jeneza,akawaona marafiki zake siku ya msiba wake.Aliamini kabisa kifo chake,kingewaumiza na kuwagusa watu wengi sana atakaowaacha duniani.Mbali na kuwaza vitu hivyo vyote lakini hakutaka kuurudisha moyo wake nyuma,ilikuwa ni lazima amalize alichokianza.
Akatizama huku na kule, akaona kuna kichochoro chembamba ambacho kwa mbali kulikuwa na miti michache,huko ndipo aliamini angefanya jambo lake kwa usalama zaidi.Alivyotembea hatua tatu akaona kiduka kidogo,akasimama ili anunue maji ya kumezea vidonge!
“Una maji ya kunywa?”
Hajrath,akauliza alivyofika dukani.
“Ndio,makubwa madogo?”
“Nipe makubwa”
“Buku hayo”
“Poa”
Hajrath,akaingiza mkono mfukoni na kutoa noti ya shilingi elfu kumi.
“Dada,chenji sina”
Muuza duka akalalamika,akiwa amekunja sura, ilielekea kitendo hiko kilimkera na mteja huyo alikuwa wa kwanza kufika na pesa kubwa.
“Dada nimekwambia sina chenji,huna pesa ndogo?”
“Sina”
“Basi sina chenji”
Jibu hilo lilimfanya Hajrath ajifikirie mara mbilimbili.’Sasa Chenji mimi ya kazi gani?Si naenda kufa’ Kitu hiko kikampitia kichwani,hakuwa ana sababu ya kuchukua chenji sababu alijua baada ya hapo,anaenda kufanya kitendo gani.
Aliganda kwa kama sekunde mbili nzima.
“Kaka,baki na chenji nitakuja kuipitia baadaye,nakaa mtaa wa nyuma hapo”
“Sawa,kingine nini nikupe?”
“Maji tu”
Alivyopatiwa anachohitaji,alianza safari ya kuelekea bondeni ambapo huko kulikuwa na miti pamoja na mbogamboga,hakukuwa na makazi ya watu!Eneo hilo aliliona litamfaa kabisa kufanya tukio hilo.Japokuwa aliamua kujiua lakini alikuwa ni mwoga kwani hakuelewa,akifa baada ya hapo anaenda wapi,akaanza kujaribu kukitafakari kifo kinafananaje lakini alishindwa sababu hakuwahi kufa kabla.
Akatembea hatua mbilimbili na kuruka mtaro wa maji,akasimama chini ya mti wa m-buyu mkubwa,akatizama huku na kule kisha kukaa chini.Hapo hakuwa anafanya kitu kingine zaidi ya kulia machozi,kifupi alianza kuulilia msiba wake mwenyewe.
“Ah....med”
Hajrath aliita huku akitoa vidonge mfukoni mwake,ni kweli.Alidhamiria kujiua!Na kivyoyote vile aliamini Necka Golden pamoja na Ahmed ndio walikuwa wakandarasi wa kila kitu kutokea.Akamuomba Mungu wake msamahaa na kuvikusanya vidonge vyote juu ya kiganja chake,akatizama huku na kule.Bado alikuwa haamini kama baada ya muda mfupi atakuwa anajikunja kunja akiiaga dunia kisha kuwa marehemu.Hakutaka kufikiria zaidi ghafla,akabwia vidonge vyote thelathini na nane mdomoni,akafungua maji ya kunywa na kuanza kuyamimina mdomoni,vidonge vilikuwa ni vingi ndiyo maana vilikuwa vinapita kwa shida shingoni,akazidi kunywa maji mengi.Ulikuwa ni ukweli mtupu kwamba binti huyo, alidhamiria kujiua siku hiyo,sekunde moja baadaye akaanza kuhisi tumbo linamkata, akahisi kama kuna mtu yupo ndani ya tumbo lake ameshika viwembe analichanachana kwani lilimuuma mno!Akajua tayari muda wa kwenda Jehanam umewadia kwani kwa kosa alilolifanya alijua huko pangekuwa halali yake,akaanza kujikunja kunja.
Maumivu aliyokuwa anahisi hayakuwa na mfano wake,alishawahi kuumwa tumbo mara nyingi lakini la siku hiyo halikuwa la kawaida,kazi yake ilikuwa ni kughala ghala kwenye mchanga,akitafuta walau msaada wa mtu amsaidie lakini haikuwa hivyo,kifupi kifo chake alikiona.Kwa mbali,akaanza kumuona mnyama wa ajabu anamfuata,mnyama huyo alikuwa ana mabawa,jicho moja na mapembe mawili.Alikuwa akija kwa kasi upande wake,hiyo ilitosha kabisa kupata jibu la swali lake ya kwamba, Israel Mtoa roho za watu yupo karibu kufanya kazi yake!

********
Asubuhi ya siku hiyo Ahmed hakuwa mwenye furaha hata kidogo,kila kitu kilikuwa tofauti kabisa!Hakuelewa ni kwanini, sababu mapenzi yote yalihamia kwa Necka Golden!Kitendo alichomfanyia Hajrath, kilikuwa ni cha kinyama mno!Akajiweka chini ya viatu vya Hajrath,akagundua ni namna gani alivyokuwa ameumia mtima.
“Baby una nini?”
Necka Golden,akauliza kwa furaha wakiwa chumbani,hali ya Ahmed ilimshangaza sana ingawa alihisi ni kwa kitendo alichokifanya kwa Hajrath.Jambo hilo alilitafsiri bado ana mapenzi na Msichana huyo!
“Bado unampenda Hajrath?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Necka Golden,badala ya Ahmed kujibu akamtizama machoni.
“Ebu niache kidogo.Nina mawazo”
“No,Ahmed.I love you,nakupenda sana!Nimefanya hayo yote sababu nakupenda,sitaki kukupoteza”
“Naelewa”
“Nipende kama navyokupenda baby”
Hapo Necka Golden hakuweza kumshawishi Ahmed kwa njia yoyote ile zaidi ya kuanza kumtomasa kila sehemu ya mwili wake ili amuhamishe kimawazo.
“Hajrath stooop”
“Umeniiitaje?”
Necka Golden,akafura kwa hasira iliyochanganyika na wivu.
“Sorry”
“Kwahiyo unanifananisha mimi na yule Changu wako?”
“Hapana nisamehee”
Siku hiyo Necka Golden alikuwa anapima maji! Akitaka kujua kama ni kweli Ahmed anampenda ama la,kitendo cha kumfokea akawa mdogo kilimfanya ajione mshindi na kujiona yeye ni bingwa!Hapo ndipo akachukua nafasi hiyo na kuanza kumtomasa upya Ahmed,akafanikiwa kumlainisha,akamlaza chali na kuanza kumpapasa!Moyo wa Necka ulijawa na furaha ajabu,akajua tayari Ahmed ni wake wa maisha.

********

Kupotea kwa Hajrath katika mazingira ya kutatanisha ndani ya chuo cha Makumira kiliwafanya rafiki zake waanze kuingiwa na wasiwasi, isitoshe kilichowatisha zaidi namba yake haikuwa hewani.Wakamuulizia kila mahali lakini hawakupata majibu yaliyo waridhisha hata kidogo,jambo hilo likawafanya wazidi kupagawa zaidi.Ikapita siku ya tatu,lakini hakukuwa na dalili ya Hajrath kuonekana chuoni,wakaanza kumuulizia huku na kule.Hawakuwa na jinsi,ilibidi siku ya saba ilivyofika tangu apotee waanze kuulizia ni wapi Ahmed anaishi,hilo halikuwa na tatizo lolote lile.
Siku hiyo wanafunzi sita wakapanda daladala mpaka Ngurelo,waonane na Ahmed.Waliamini wenda Ahmed atakuwa ana fununu ni wapi alipo Hajrath, japokuwa jambo hilo hawakulipa sana kipaumbele,walikuwa kama wanabahatisha tu!Walivyofika hawakutaka,kuzunguka wakasema kilichowafanya wafunge safari yao mpaka kwake!
“Hajrath?Tangu lini?Hamjamuona chuoni?”
Ahmed akauliza,hata yeye jambo hilo lilimuogopesha kiasi.
“Ana wiki sasa”
“Wiki?”
“Ndio.Hukuwasiliana naye?Hauna namba za wazazi wake ama ndugu zake,usikute yupo kwao!”
“Walaa lakini inawezekana yupo kwao,sina namba yoyote ile ya ndugu yake”
“Mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni lini?”
Hapo Ahmed,hakutaka kujibu.Akaanza kutafakari ni jibu gani alitoe kwa wakati huo.
“Hapa hajafika kabisa”
“Mmmh,kweeeli?”
“Ndio,hapana”
“Ahmed!Hajrath ulimuona lini mara ya mwisho? Tuambie basi alipo,kama yupo kwa ndugu zake tujue.Kuliko kuwa hivi,tunabaki rohoo juu”
“Alikuja hapa.Hiyo wiki iliyopita,hatukuongea kiviile!Akaondoka”
“Hamkuongea?”
“Ndio”
“Hakusema anaenda wapi?”
“Ha…”
Kabla ya Ahmed kumalizia sentensi hiyo,simu ya Amney ikaita.Alivyoitoa ilikuwa ni namba ngeni.Akaipokea na kuiweka sikioni.
“Yes,ndio Mimi.Naongea na nani?Unasemaaa?Hajraaath!Mungu wangu,amekufaaaaa?Uwiiiiiii”
Kila mtu alikuwa kimya,kitendo cha Amney kuropoka sentensi hiyo, kilimfanya kila mtu apatwe na mshtuko lakini aliyeonekana kupagawa zaidi si mwingine bali ni Ahmed.


“Martiiin,Martiin,Martiiin”
“Naaaam”
“Amka,dada amezidiwa”
“Nakujaa”
Sauti hiyo ilisikika ndani ya nyumba ya matofali kubwa kiasi,hali ilionekana kuwa mbaya, ndiyo maana walikurupushana.Kila kitu kilionekana kuvurugika siku hiyo,ndiyo maana Martin, mtoto mkubwa wa Mzee Phares,akakurupuka kutoka usingizini.
Haukuwa utani hata kidogo kwani siku hiyo usiku kabla ya kulala, dada yake alikuwa mwenye hali mbaya ya kutisha,kuamshwa kwa fujo ilimpa jibu tosha ya kwamba kama asingewahi kuchukua hatua basi,angempoteza dada yake kipenzi.
“Martiin,fanya haraka”
Safari hiyo mlango ulikuwa ukigongwa.Martin alikuwa anamalizia kuvaa kaptula ndogo, akavuta fulana iliyokuwa nyuma ya mlango na kuufungua mlango kwa kasi.
“Vipi Monica?”
“Dada kazidiwa,anaumwa sana”
Kama mkuki, Martin akachomoka mpaka chumba alichokuwa analala dada yake,akafungua mlango kwa nguvu na kuzama ndani.Hali aliyomkuta nayo dada yake ilimuogopesha kwa kiasi cha kutosha,akamshika kichwani.Joto lilikuwa kubwa mno!Zaidi na hayo alikuwa akitoa majasho na kutetemeka mwili,hali ingezidi kuwa mbaya zaidi kama wangeendelea kubaki na kumtizama kama wanashangaa tangazo bila kuchukua hatua yoyote,kama mtoto mkubwa wa kiume, ilibidi achukuwe maamuzi ya sekunde sifuri,hapohapo akainama na kumbeba dada yake mikononi.
“Kachukuwe funguo chumbani kwa Mzee”
Martin alisema,dada yake akatii na kuanza kutembea kwa kasi!Wazazi wao siku hiyo hawakuwepo,hivyo ilikuwa ni lazima watumie akili ya kujiongeza.Akaingia ndani na kutoka na funguo za gari ameshika mkononi,hakukuwa na muda wa kupoteza. Wakampakia mgonjwa ndani ya gari na safari ya kuondoka ikaanza hapohapo!
“Rachel,tunaenda hospitali sawa?”
Monica alimfariji mdogo wake ambaye kwa wakati huo alikuwa ana weweseka,hali hiyo ilizidi kuwatisha mno, ndiyo maana Martin akalitoa gari kwa kasi ya ajabu,akitokea maeneo ya Ilboru, ambapo huko ndipo walipokuwa wanaishi.Haikuchukuwa muda mrefu sana,wakawa wamewasili Zahanati ya karibu ili waangalie tatizo la Rachel,Mungu alikuwa upande wao sababu walifanikiwa kumfikisha na wauguzi walitoka mkuku mkuku ili kumuhudumia, alfajiri hiyo ya saa kumi na moja.Wodi lilikuwa kimya,hiyo iliwalazimu Martin na Monica,wasubiri mpaka wapate majibu.Dokta akatokeza mlangoni,wakamuendea kwa kasi.
“Mlikuwa wapi muda wote mpaka mgonjwa amekuwa na hali mbaya namna hii?”
Dokta aliuliza kwa jazba,kitendo cha mgonjwa kuletwa akiwa katika hali mbaya kilimfanya afoke.
“Ilikuwa ghafla”
“Nani mkubwa kati yenu?”
“Mimi”
Monica,akadakia.
“Hapana,wewe wa kiume njoo.Binti baki”
Kauli hiyo ilikuwa ya kutisha kuliko kawaida,kulikuwa kuna kila dalili ya msiba kutokea siku hiyo.Martin akapiga moyo konde na kumfuata daktari kwa nyuma ambapo huko,alipewa taarifa mbaya zaidi ya kwamba,dada yake anatakiwa kulazwa siku hiyo.Hivyo wamuache,kama alivyopokea habari na ndivyo alivyoenda kumfikishia dada yake Monica!
“Ebu nenda nyumbani,katengeneze chakula”
Monica akatoa wazo.
“Chakula?”
“Uji,kuna uji pale kwenye semothi.Uje nao,mimi nitabaki na mgonjwa”
Ilikuwa ni lazima mmoja aende mwingine abaki.Kama Monica angekuwa ana uwezo wa kuendesha gari basi zoezi hilo angelifanya mwenyewe,jukumu la kwenda kutengeneza uji akalivaa Martin,akawasha gari na kuanza safari ya kurudi IIboru.Kitu alichokiona Martin, alivyofika karibu na Ngurelo kilimshangaza,kwa mara ya kwanza alijua wenda ni mnyama lakini alivyotuliza akili akagundua ni mtu,akatizama vizuri kwa mbali.Akadhani wenda haoni vizuri akashusha kioo ili kutizama vizuri upande wa chini, kulipokuwa na miti mingi.
“Mungu wangu!”
Hakujua nini kilitokea, ghafla aliweka gari kandokando ya barabara,akafungua mlango kwa kasi na kuanza kushuka bonde akikimbia kama mwehu, hiyo ilifanya ajikwae na kuanza kubiringika kama mpira,alivyofika chini akasimama na kuanza kukimbia tena mpaka alipomfikia msichana aliyekuwa chini,anaghalaghala.
Alivyotathmini vizuri,akaona baadhi ya vidonge vipo pembeni, akaelewa msichana huyo yupo katika jaribio la kujiua.Hakuchukuwa jukumu lingine zaidi ya kuanza kupiga kelele za kuomba masaada,akiamini swala hilo hatoweza kulifanya mwenyewe,akaanza kukimbia kama mtu aliyepoteza akili zake.
“Kuna nini?”
Mzee mmoja mpita njia,aliuliza baada ya kusikia kelele hizo,asubuhi na mapema namna hiyo.Ilielekea alikuwa anawahi kibaruani.
“Kuna mtu anakufa”
“Unasemajeee?Wapi?”
“Huku njoo”
Kelele hizo hazikuishia hapo,kufumba na kufumbua watu wakaanza, kumfuata nyuma Martin mkuku mkuku,kama kawaida ya wabongo, hawawezi kukubali kupitwa na kitu.Walichokikuta kiliwashtua wakazi wengi wa eneo hilo,msichana alikuwa chini ana tapatapa huku anatoa mapovu mdomoni.Wengine bila aibu wakaanza kupiga picha wakitumia simu zao.
“Kafanya nini huyu?”
“Kanywa vidonge anataka kujiua”
“Anakufa huyu,mwiteni mjumbe”
Lilikuwa ni wazo la kipuuzi kulitoa mzee mwenye mvi kichwani kama yeye ingawa lilikuwa ni wazo la busara,kusubiri mpaka mjumbe afike, kulimaanisha kumuacha binti huyo afie hapohapo.
“Hapana tumuwaishe hospitali,nina gari nimeliacha kule juu”
“Wapi?”
“Kule juu barabarani”
Kila mtu aliangalia juu,ambapo kulikuwa na kilima kikali,hiyo ilimaanisha kulikuwa na kibarua kingine kizito cha kum-beba msichana huyo aliyekuwa chini,ana hangaikia uhai wake.
“Jamani twendeni”
Vijana wenye huruma wakam-beba Hajrath ambaye kwa wakati huo alikuwa anakoroma kama kondoo aliyechomwa kisu cha shingo,hali ya msichana aliyekuwa amebebwa siku hiyo, ilikuwa inatisha hakuna hata mmoja kati yao aliyetegemea kama angekishinda kifo.Walipata taabu kidogo kupandisha kilima, kuna wengine waliteleza,mpaka walipolifikia gari aina ya Mark II, walikuwa tayari wamekula dakika moja nzima.
“Muingize siti ya nyuma,fanyeni haraka.Gari nimepaki vibaya”
Kazi ya kumpakia Hajrath ndani ya gari ilifanyika muda huohuo,Martin akaingia ndani ya gari.Akalitoa mbio kama mtu asiyekuwa na akili vizuri,kazi aliyotumwa ya kutayarisha chakula cha dada yake aliisahau, alichokuwa anakumbuka kwa wakati huo ni kuokoa maisha ya binti huyo mdogo kufa.
Hakuwa na jinsi zaidi ya kukimbiza gari mpaka hospitali ya karibu na Ngurelo,ambapo huko alipokelewa na wauguzi na haraka wakampakia juu ya kitanda chenye magurudumu chini,wakaanza kukimbizana ili kuiweka afya yake vizuri.
Ukitoa Martin Phares,kulikuwa na wasamalia wema wengine watatu ambao waliambatana na Martin kuhakikisha mgonjwa huyo,anafika salama hospitalini hapo!Madaktari,walimvaa Hajrath akiwa anatoa mapovu,hali hiyo ilikuwa ni mbaya sana endapo wangefanya mzahaa.Ndiyo maana,walijitahidi kadri wanavyoweza ili kuutetea uhai wake.

*******
Ndani ya wodi ya wagonjwa mahututi,madaktari walipigana vikumbo.Kila daktari alijitahidi kwa taaluma aliyokuwa nayo, kuyaokoa maisha ya binti huyo mdogo mwenye ndoto nyingi katika maisha yake, aliyeletwa baada ya kutaka kujiua,ilikuwa ni lazima wafanye juhudi za kuyaokoa maisha yake.
“Sasa si bora,angekufa tu.Ni kheri tukawahangaikie wagonjwa wengine,kule leba”
Ni sauti ya Nesi mmoja aliyeonekana kukerwa na mgonjwa huyo, aliyetaka kufanya jaribio la kujiua.
“Kwanini unasema hivyo?”
Nesi Mwenzake akauliza.
“Si kalilia wembe,mwache umkate”
“Lazima uulize,kwanini alitaka kujiua.Ni matatizo ujue Rehema”
“Sina muda wa kuuliza,angekufa tu.Tuna wagonjwa wengi wanataabika, kupambana na uhai lakini wengine wanataka kujiua,hivi binti kama huyu mdogo.Anataka kujiua kisa nini?Kwa maisha yapi magumu anayopitia?”
Yalikuwa ni malumbano usiku wa siku hiyo baada ya dripu ya Hajrath kuwekwa dawa itakayomsaidia kumpa nguvu.
Hilo halikuonesha nafuu yoyote ile kwani siku iliyofuata hali yake ilizidi kuwa mbaya, ukilinganisha na alivyoletwa awali na wana usalama,kilichowachanganya madaktari zaidi ni jambo moja tu,hakukuwa na ndugu yoyote wa kumpa taarifa za mgonjwa huyo!
“Sasa,tutafanya nini na huyu mgonjwa?Ujue nishachanganyikiwa hapa,sijui hata nifanye nini.Embu niache kidogo”
Yalikuwa ni maneno kutoka kwa Dokta Sumari,alionekana kuchoka akili mpaka mwili. Msululu wa wagonjwa aliokuwa nao siku hiyo ulikuwa ni mkubwa,habari ya msichana aliyetaka kujiua aliamua kuiweka kwanza kapuni.
“Hali yake ni mbaya sana”
“Sasa nifanye nini mimi?Nimejitahidi kadri ya uwezo wangu,naomba unipe lile faili la Mrs Mshana!Yule mama mjamzito aliyejifungua mtoto njiti”
“Lakini Dokta…”
“Nishasema,siwezi kushughulika na huyo aliyetaka kujiua,tafadhali get out”
Huo ndio ulikuwa msimamo wa Dokta Sumari,siku hiyo alionesha kutingwa mno.Swala hilo lilikuwa ni tofauti kwa Nesi aliyeitwa Neema kwani alifanya juu chini ili Hajrath apatiwe matibabu mpaka nukta ya mwisho,hakuelewa kwanini anafanya hivyo sababu mgonjwa huyo hakumjua na wala hakuwa ana uhusiano naye.Hakutaka,kukubali swala hilo litokee ndiyo maana akanyoosha mpaka mlango wa Dokta Mlungu,daktari bingwa ambaye walikuwa wanamtegemea!
“Shida nini Neema?”
Dokta Mlungu akauliza.
“Nina matatizo”
“Kaa kitini,nini tatizo?”
“Nina mgonjwa wangu,ana hali mbaya sana”
“Mgonjwa gani?”
Nesi Neema ilibidi aseme kila kitu kilivyoenda, kinagaubaga.
“Dokta Sumari,leo hayupo sawa ndio maana!Yupo wodi gani huyo mgonjwa?”
“Namba mbili”
“Sawa twende”
Kwa Neema hakutegemea kama mambo yangekuwa marahisi namna hiyo,Dokta Mlungu akawa amempa matumaini mengine mapya,haraka akatoka ofisini kwake wakaongozana mpaka wodini.
Haukuwa utani,jambo alilolisema Nesi Neema lilikuwa na ukweli mtupu,hali aliyomkuta nayo binti huyo ilikuwa ni mbaya tena ya kutisha.
“Kwanini mmemuacha mpaka akafika kwenye hali mbaya kiasi hiki?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kuhoji,Hajrath alikuwa amevimba mwili,rangi yake ya ngozi imebadilika kulikuwa kuna kila dalili za kumpoteza kama wasingechukuwa hatua nyingine mbadala.Hapo ndipo Dokta Mlungu,alipoanza kutafuta madaktari wenzake kutoka katika hospitali ya Mount Meru ili apatiwe msaada zaidi kwani huko waliamini, ndipo kuna matibabu yenye uhakika.
Hakuna muda uliopotezwa,simu ikapokelewa na Dokta Shitindi.Akaambiwa mchakato mzima ulivyoenda mpaka dawa alizopewa mgonjwa huyo.
“Mleteni sasa hivi Dokta Mlungu,hii ni kwa heshima yako.Vinginevyo nilikuwa naondoka sasa hivi,fanyeni haraka”
Upande wa pili wa simu ulisikika,Dokta Shitindi akakubali.Taratibu za kumuhamisha Hajrath hospitalini, zilifanyika wakati huohuo.
“Ina maana huyu mgonjwa hana ndugu yoyote Yule?”
Dokta Mulungu akauliza wakiwa na Nesi Neema ndani ya gari lake binafsi.
“Sijui”
“Fanyeni,utaratibu ili tujue ndugu zake wanapatikana vipi”
“Sawa nitafanya hivyo”
“Hakuwa na kitambulisho chochote kile mfukoni?”
“Hapana,lakini nilimkuta na vikaratasi fulani hivi”
“Viko wapi?”
“Sijui niliviweka wapi”
“Fanya ufuatilie,wenda tunaweza kujua ni wapi tutaanzia”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa.Hajrath alifikishwa hospitali ya Mount Meru, akiwa mwenye hali mbaya bado,hakuweza kuongea na wala hakupata fahamu yoyote ile.Ilibidi wamuweke ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi.Siku zilizidi kwenda na hakuna hata mtu mmoja aliyefika kumuona,siku ya saba ilivyofika ndipo Nesi Neema akaibuka na vikaratasi ambavyo alivikuta mfukoni mwa Hajrath, kipindi anakabidhiwa hospitalini.
“Hizi karatasi naona ni summary tu,ebu hizo nyingine.Wale vijana waliomleta hawakufika tena?”
“Walifika juzi lakini sikuwepo”
“Nipatie hizo karatasi”
Vikaratasi vikaanza kufunguliwa kimoja baada ya kingine.
“Naona kuna namba za simu hapa”
“Jaribu kupiga ili tujue”
Kabla ya kujaribu kupiga namba hizo,ghafla akaingia nesi mmoja akiwa anahema juujuu.
“Njoo Dokta”
Dokta Shitindi akatembea kwa kasi na kuongozana na nesi aliyemuita mpaka ndani ya chumba alicholazwa Hajrath,hali aliyomkuta nayo ilikuwa mbaya.Alikuwa akitingisha miguu kama kuku anayetaka kukata roho.
“Mwite Dokta Rwaichi sasa hivi”
Miguu ya Hajrath kutingishika ilifanya Dokta Rwaichi,mchaga huyo mtaalam katika taaluma nzima ya mfumo wa fahamu kuitwa.Haikujulikana ni kwanini anaitwa lakini alihitajika ndani ya wodi hilo mara moja,sekunde moja baadaye.Akaibuka,akamuona mgonjwa,akamuendea na kumuangalia vizuri hapo ndipo alipoanza kutafuta dawa za kumtuliza lakini kwa wakati huo ilionekana alikuwa ameshachelewa tayari sababu miguu ya Hajrath ilitulia.
Dokta Shitindi akatafsiri moja kwa moja kwamba binti huyo teyari kapoteza maisha,akatoka nje ya chumba na kuchukua simu ya mkononi pamoja na karatasi aliyopewa yenye namba ambazo juu ziliandikwa Amney,hapohapo akapiga simu.Akitoa taarifa ya kifo cha rafiki yao!



Taarifa za kifo cha Hajrath kutoka kwa dokta,zilikuwa za kutisha kwa wote!Kila mtu alibaki akiyatumbua macho yake bila kuelewa ni kitu gani wafanye.Ahmed alihisi kuchanganyikiwa zaidi,hakuelewa ni kitu gani akiseme.Picha ya Hajrath ikamjia kichwani siku aliyofika kwake asubuhi na kumkuta Necka Golden,akajuta mno akatamani Hajrath afufuke, ama jambo hilo liwe ndoto ashtuke.
Kubaki hapohapo na kushangaa kusingebadilisha kitu chochote kile,walichofanya ni kutafuta usafiri mpaka hospitali ya Mount Meru ili kuhakikisha taarifa hiyo mbaya,ambayo kila mmoja wapo alitamani isiwe kweli kwani walielewa nini maana ya kifo,wasingemuona tena Hajrath maishani.
Haikuwachukuwa muda sana wakawa wamewasili hospitali ya Mount Meru,wakajielezea na kuambiwa wasubiri juu ya benchi.Sio siri kila mtu siku hiyo,alimuomba Mungu wake.Amney alikuwa akilia kama mtoto mdogo,akizunguka huku na kule.Mbili haikai tatu ndio kabisa,Ahmed ndio usiseme,aliganda kama barafu hawezi kuongea kitu,hakuelewa angelia kilio gani siku ya msiba wa Hajrath,kitu kingine kilichovuruga akili yake, alitaka kujua ni kitu gani kilimuua Hajrath wakati siku hiyo aliondoka akiwa mzima kabisa, japokuwa aliamini moyo wake uliuma alivyomfumania na Necka Golden.Taa jekundu ikaanza kuwaka kichwani kwake,akahisi wenda aligongwa na gari kutokana na mawazo aliyokuwa nayo, mbali na kuwaza hayo lakini hakutaka kuyapa kipaumbele sana,akayatupitilia.

*****
Mambo makubwa mawili aliyofanya Dokta Shitindi yalikuwa ni tofauti na taaluma yake,Moja alikurupuka kutoa taarifa za msiba bila kuwa mwenye uhakika lakini jambo la pili, hakutakiwa kutoa taarifa za kifo moja kwa moja, alichotakiwa kufanya ni kumuuliza anayempigia yupo katika mazingira gani.Ni kweli alimuacha Hajrath atingishiki lakini mapigo yake ya moyo yalikuwa yanapiga kama kawaida,hilo lilithibitishwa na Dokta Rwuachi,ambaye alionekana kushughulika na mgonjwa huyo mpaka hali yake ilivyokuwa sawa!Ndipo alipotoka nje na kumtaarifu Dokta Shitindi.
“Mwacheni kidogo”
“Si amefariki”
Haikujulikana kama Dokta Shitindi anauliza swali ama ameshtuka.
“Hapana,yupo sawa ni mzima”
Dokta Rwaichi hakuwa mwingi wa maneno,alitembea mpaka ofisini kwake ili kuendelea na shughuli nyingine huku nyuma akimuacha Dokta Shitindi amepigwa na butwaa la waziwazi na kugundua ya kwamba tayari amebugi stepu na asingeangalia kibarua chake kingeota nyasi siku hiyo, kwa kosa la kutoa taarifa za uwongo.
“Dokta”
Muuguzi wa kike alimuita,akitokea nyuma yake.
“Yes”
“Kuna wanafunzi wametoka Chuo cha Makumira.Wanasema wamepigiwa simu leo”
“Na dokta nani?”
“Hawamjui,walichoniambia ni mwanafunzi mwenzao”
“Sijapokea mgonjwa mwanafunzi mimi, kutoka chuo cha Makumira”
“Sawa,ngoja nikamuone Dokta Makalla”
Muuguzi akaanza kutembea lakini alivyopiga hatua mbili mbele,akasimamishwa.
“Ebu njoo kidogo”
“Abee Dokta”
“Inawezekana ni huyu binti,wako wapi?”
“Wapo reception pale”
Dokta shitindi alikuwa ni kama ametabiri vile,kitendo cha kupiga hatua tatu simu yake ikaita na alivyoiweka sikioni ili kujua ni nani,akagundua ni watu aliowapa taarifa za msiba,dakika kama kumi zilizopita nyuma.
“Sawa nakuja”
Dokta Shitindi akatembea na kutokeza mpaka mapokezi,akatizama huku na kule kisha kuanza kupiga simu.Ambapo, Amney alipokea!
“Njoo huku”
Dokta Shitindi alisema simuni na kukata simu huku akimpungia mkono Amney,wanafunzi wote wakasimama akiwepo Ahmed.
“Aje mmoja tafadhali ili kuhakikisha kama ni yeye?”
Sentensi hiyo ilimtisha kila mmoja wao na kuitafsiri ya kwamba mmoja kati yao,aingie monchwari kuangalia kama maiti ni kweli ilikuwa ya Hajrath.
“Mimi hapa nipo tayari”
Amney akazungumza kwa ujasiri wa hali ya juu,hiyo ilifanya wanafunzi wenzake wamshangae kwani hakuwa na roho ya kawaida, swala la kuingia monchwari halikuwa jambo la mchezomchezo,lilihitaji moyo mgumu.
“Wewe ndo Amney?”
Dokta Shitindi akavunja ukimya wakiwa wanaongozana katikati ya kordo ambapo walipishana na madaktari wengine pamoja na wagonjwa tofautitofauti.
“Ndio mimi”
“Mlikuwa wapi muda wote mpaka Mgojwa wenu analetwa hapa Mount Meru?”
“Tulikuwa tunamtafuta sana bila mafanikio”
“Mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni lini?”
“Yapata wiki sasa”
“Jina lake nani?”
“Hajrath”
Maswali ya hapa na pale yalimfanya Amney,alengwe na machozi upya, japokuwa alijikaza kisabuni lakini jambo hilo lilionekana waziwazi.
“Kwanini alitaka kujiua?”
Dokta akauliza swali lililomfanya Amney,apigwe na butwaa la waziwazi.Akamtizama Dokta huyo aliyekuwa kushoto kwake, mrefu kwenda hewani.Tukio la kutaka kujiua kwa Hajrath lilikuwa ngeni kabisa, ndiyo maana moyo wake ukawa kama umelipuka.
“Kwani,mzima?”
Amney akauliza swali akijaribu kuthibitisha kauli ya Dokta kama ni kweli ama alikosea kumuuliza swali ‘Kwanini sasa alitaka kujiua?’Sentensi hiyo kwake aliichambua vizuri.
“Ndio ni mzima.Lakini ana hali mbaya sana!”
Hali ya Hajrath kuwa mbaya hakujali alichoshukuru Mungu ya kwamba Hajrath bado anavuta pumzi ya Mungu,moyo wake ukapiga sarakasi kwa furaha.Ingawa mpaka hapo hakuwa mwenye uhakika kama majibu ya Daktari yana ukweli ama anataka kumfariji tu.Walitembea mpaka wodi la wagonjwa mahututi,wakaingia.
Alivyotupa macho yake kwenye kona ya kushoto akamuona Msichana amelala,kwa mbali hakuweza kumtambua lakini alivyosogea karibu, akagundua kwamba ni Hajrath,uso mzima ulikuwa umemvimba.Mwili wake umebadilika rangi.Hiyo ilimfanya ashindwe kuzuia machozi yake,akamsogelea karibu na kumshika rafiki yake kipenzi juu ya paji la uso.
“Eeeh Mungu,Hajrath kwanini ulitaka kujiua?Do…kta ilikuwaje?”
Baada ya kusema maneno hayo ,machache akamtupia swali dokta!Hata hivyo hakupata maelezo yaliyojitosheleza kwani Hajrath alipokelewa kwenye hospitali hiyo baada ya kutoka hospitali nyingine.
“Nachojua mimi alitaka kujiua,alikunywa vidonge vingi sana!Bahati nzuri wakamuwahisha hospitali,hali yake ndio kama hivyo unavyoiona.Una namba yoyote ile ya ndugu yake?”
Dokta alijaribu kutoa maelezo juujuu na kuhitimisha na swali.
“Hapana”
“Huyu ni rafiki yako huna hata namba yoyote ya ndugu yake?Hujui hata anapoishi?”
“Anaishi Dar es salaam!Simu yake kwani iko wapi?Na namba zangu,ulizipata vipi?”
Dokta akaelezea kila kitu kinagaubaga,namna alivyopata namba za Amney!
“Hakuwa na simu?”
“Itakuwa walimuibia”
“Ngoja kidogo,naweza kuwasaidia kupata namba.Nisubiri kwanza”
Jambo hilo lilitakiwa kufanyika mara moja, ndiyo maana Amney,akajikaza na kufuta machozi.Akatoka nje, akatoa simu yake ya mkononi akatafuta jina Mpangw’a,alivyompata,wakasalimiana.
“Sikia Mpangw’a…..Ndio nenda hostel,anapolala Hajrath….Kwani uko wapi?Nakuomba ni emergency…ndio.Please please utafanya baadaye...Noo,nitakwambia ukifika.Sawa,ndio!Cha kufanya,nenda hostel asa hivi, chumba cha Hajrath ndani ya kabati lake,kuna kile kikopo kidogo.Anachoweka laini za simu.Njoo nacho,hapa Mount Meru Hospital...Usijali Mpangw’a, nitakwambia kila kitu.Sawa ahsante”
Alivyomaliza kuongea maneno hayo akaenda mpaka mapokezi ili kuwapasha habari,akaelezea kila kitu alichoambiwa na daktari.
“Alitaka kujiuaaaaaaaa?”
Lilikuwa ni butwaa la waziwazi,huyu aliitwa Abela John,hakuna msichana anayeongoza kwa kushtuka kama huyu.Hata kama akiwa usingizini,ukimuamsha ni lazima ashtuke asipo piga kelele, basi ni lazima akupige ngumi.Maneno hayo yalipenya kama yalivyo kwenye ngoma za masikio ya Ahmed,picha ya tukio zima lilimjia na alijua sana Hajrath kwanini alifanya kitendo hiko,alijisikia uchungu na kuangalia chini akajiona kama ni muuaji,astahili kuishi. Kama Hajrath angekufa asingejisamehee habadani.Kuhusu kutaka kujiua kwa Hajrath kilikuwa ni kitendawili kikubwa sana,hakuna hata mmoja kati yao aliyejuwa kwamba Hajrath alitaka kujiua kisa Ahmed na Necka Golden.Dakika Ishirini baadaye,Mpangw’a akawa ameingia hospitalini hapo,taarifa alizopewa zilimshtua mno akaweka mikono yake mdomoni kwa mshangao!Akabaki kinywa wazi.Hata hivyo ilibidi muda huohuo watumie nafasi hiyo kupachika laini nyingine ya Hajrath kwenye simu ili kujaribu kama wangepata namba yoyote ile ya nyumbani kwao.
“Hii ya Voda,alikuwa anatumia mwezi uliopita”
Simu ya Amney iliwaka,wakazama kwenye ‘Phonebook’jina la ndugu wa karibu kulipata lilikuwa ni ‘Bro Hussein’.
Hapohapo,hawakutaka kupoteza wakati.Wakapiga!Simu iliita kama mara mbili bila kupokelewa, wakajaribu tena,ikapokelewa. Upande wa pili wa simu ukasikika, sauti ilikuwa nzito kidogo.
“Halloo,samahani.Nazungumza na Kaka yake na Hajrath?”
Amney alianza kuhoji ili apate uhakika.
“Ndio,wewe nani?”
“Mimi naitwa Amney,shikamoo”
“Marahaba!Hajra yuko wapi?Mbona simpati hewani?”
Upande wa pili ukauliza swali.
“Hajrath yupo Hospitali,anaumwa”
“Anaumwa nini?Wewe nani?Ebu kata nakupigia”
Ilikuwa ni habari nyingine nzito pia.Hazikupita hata dakika tatu,simu ikaanza kuita.Amney akapokea na kuanza kutoa taarifa za ugonjwa wa Hajrath, japokuwa hakuweza kuliweka wazi swala la Hajrath kutaka kujiua.
“Sawa nakuja,mimi nipo Tanga,nakuja leoleo.Umesema ni Mount Meru?”
“Ndio”
“Okay”
Bahati nzuri ndani ya dakika moja,akatokea kijana mmoja mrefu kiasi.Akawasogelea na kuwasalimia.
“Naitwa Martin Phares,poleni sana.Kuna nesi kanielekeza hapa kwenu”
Baada ya salamu hiyo,kijana akaanza kujielezea na kusema alivyomsaidia Hajrath mpaka akamfikisha hospitalini.Ilibidi kila mtu atege masikio yake vizuri.
“Ulisema ulimkuta wapi?”
“Ngurelo,kule darajani”
“Alifata nini Ngurelo?”
Lilikuwa ni swali lililoulizwa na Amney,hapohapo kuna kitu akakumbuka akamgeukia Ahmed.
“Ahmed….”
Akaita huku akimtizama usoni.
“Umemfanya nini Hajrath?”
Lilikuwa ni swali la moja kwa moja!Hakukwepesha.
“Kuhusu nini?”
“Ngurelo alienda kufanya nini?Wewe si unaishi Ngurelo?”
“Ndio”
“Hajrath hakuja kwako?”
“Unajua m…”
Kabla ya Ahmed kumaliza kujitetea Dokta akatokeza na kumuita Amney,ambapo huko alimuuliza kama alifanikiwa kuwapata ndugu wa Hajrath.
“Nilifanikiwa”
“Wamesamaje?”
“Wanakuja”

*******
“Baby nina shida”
“Shida gan?”
“Kama laki mbili hivi”
“Ya nini?Juzi tu.Nilikutumia laki tano,imeisha?”
“Nilitumia Darling,si unajua matumzi ya hp hostel.Nywel,nyingine nikanunua stock ya chakula.So,nimebaki na pesa kidog sn.Hainitoshi love”
“Okay,subiri nitoke ama namtuma mtu akutumie.Sasa hivi nip kweny kikao”
“Sawa,love u Darling”
“Me too”
Juu ya kioo cha simu,msichana huyu alikuwa anachat.Ungeambiwa ya kwamba ana mahusiano na mzee wa miaka hamsini na mbili, habadani ungebisha.Mbali na kuwa na Ahmed, Necka Golden alikuwa ana mahusiano na Mzee mmoja mfanyabiashara,mbaya zaidi alikuwa mme wa mtu.Isitoshe alikuwa ana watoto watano,msichana huyu hilo hakujali.Alichotaka yeye ni kuchota na kumchuna pesa ili atumie chuoni hapo.
Kifupi ,Mr.Mwapongo ndiye alikuwa anamuweka mjini na kumfanya avae viwalo vya bei mbaya sana!Necka alijua kuzitumbua pesa za Mr.Mwapongo kisawasawa,zaidi na hayo alimpagawisha kitandani.Ndiyo maana mzee huyo alikuwa yupo radhi familia yake ile mboga za majani hata mwezi mzima lakini Necka Golden, ale kuku kwa mrija.Necka Golden alikuwa ni msichana mmoja makini na mjanja sana,hakutaka kuacha meseji kwenye simu yake!Akazifuta zote, akiwa mwenye furaha baada ya kumpiga kizinga kibopa huyo!Hapohapo,akampigia simu Ahmed,akitaka kujua ni wapi alipo.
“Nipo Mount Meru hospital”
Upande wa pili wa simu ukajibu,Ahmed alisikika akisema.
“Baby,kuna nini?”
“Nitakwambia,upo wapi kwani?”
“Nataka nielekee kwako.Funguo umeacha palepale au?”
“No,angalia dirishani”
“Sawa Sweatheart”
Necka Golden,akakata simu.Ndani ya dakika tatu,akapokea ujumbe wa muamala kutoka kwa Mr.Mwapongo, uliosoma shilingi laki mbili na hamsini za kitanzania.


Alichokuwa anafanya Necka Golden ni kupanda farasi wawili kwa wakati mmoja, hakuelewa ya kwamba atachanika msamba,hakuwa na njia nyingine ya kufanya ili kuvuna pesa kirahisi kwani alitamani maisha ya starehe.Na alikuwa msichana mpenda viwanja na kula bata.Hilo ndilo lililomfanya ajue kucheza na wanaume wenye pesa jijini hapo, Arusha.Na tangu aanze mchezo huo, hata siku moja hakuwahi kukosea.Kwa maana nyingine alikuwa mjanja kuliko Sungura.Ungemuona kwa sura na kuambiwa matendo yake,habadani ungebisha na kukataa katukatu.Alikuwa ni binti mdogo,mrembo kwelikweli,mnyenyekevu kuliko kawaida.Baada ya kukamilisha kila ratiba aliyopanga siku hiyo,akaingia bafuni kujimwagia maji ambapo huko,alinawa na kufanya kila kitu.Akatoka na kanga yake moja mpaka kwenye kabati, ambalo lilikuwa na kioo kikubwa sana mbele yake.Utaratibu wake ulikuwa ni uleule siku zote, kukaa juu ya kiti na kuanza kujipaka vipodozi tofauti tofauti,alivyomaliza kile anachokifanya.Akavaa nguo zake na kujipulizia marashi,alivyohakikisha kila kitu kimeenda sawa!Akaanza kutembea kuelekea stendi, ambapo huko aliamini angepata usafiri utakaompeleka Ngurelo anapoishi Ahmed ili amsubiri,ki ukweli siku hiyo alikuwa ana kiu ya kufanya ngono.
Ndiyo maana akatembea harakaharaka ili afike mapema,aoge kwa mara nyingine na kulala kitandani amsubiri Ahmed afike.Kifupi alianza kufikiria vitu atakavyovifanya kabla ya kufika.Alivyowasili kituoni,kuna sauti ilimshtua kutokea upande wa pili.
“Necka,unaenda wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa msichana anayeitwa Linda Mwacha, mwanafunzi wa chuo cha Makumira mwaka wa pili,jambo hilo lilimfanya Necka abaki anamuangalia kwani tangu wajuane, hakuwahi kuulizwa kitu kama hiko.Ilielekea swali hilo,lilimkera lakini hakutaka kulionesha jambo hilo waziwazi.
“Naenda hapo mbele.Vipi kwani?”
“Wapiii?Kwani hauna habari kama Hajrath yupo hospitali”
Kauli hiyo ilimfanya Necka amuangalie Linda machoni,hakuwa ana uhakika kama alisikia vizuri.
“Yupo hospitaliii?Kuna nini?Nani anaumwa?,”alijifanya kushtuka.
“Mimi sijui lakini nimeambiwa juujuu,alitaka kujiua”
Siku hiyo msichana huyo Linda Mwacha,alikuwa mwenye hekaheka kupita kawaida.Namna alivyoongea harakaharaka bila kuweka nukta, ilimfanya mpaka Necka ashindwe kuyasikia maneno mengine vizuri.Hata hivyo habari za Hajrath kutaka kujiua alifanya ajumuishe na tukio la kumfumania yeye na Ahmed,kwake yeye aliona ni bora angekufa tu moja kwa moja.
“Hali yake vipi?Anaendeleaje?”
Sio kwamba Necka Golden aliuliza swali hilo akitaka kujua hali ya Hajrath ipoje,niya yake alitaka kusikia ‘Hajrath ana hali mbaya sana,hawezi kupona’
“Mimi sijui,nisindikize.Yupo Mount Meru hapo”
Safari ya kwenda kwa Ahmed ikawa imevunjwa tayari,hata hivyo alianza kupata picha kamili ya kwanini Ahmed alimpigia simu na kumwambia yupo Mount Meru hospital,alijua ni lazima tu.Ahmed yupo Hospitali ili kumjulia hali Hajrath,jambo hilo likamuumiza kichwa.
“Atanikoma,mshenzi”
Necka aliropoka kwa sauti kubwa bila kujua ya kwamba yupo nyuma ya pikipiki,ilibidi dereva atege sikio akidhani wenda abiria wake anamsemesha.
“Dada unaongea na mimi?”
Dereva akahoji.
“Endesha pikipiki,acha umbea”
Dereva,akashushuliwa jambo,lililomfanya awe mdogo na kuzidi kuendesha pikipiki hiyo.Hakutaka kuuliza maswali mengi,kazi yake ilikuwa ni kumfikisha abiria wake hospitali ya Mount Meru.Walivyowasili wakakuta tayari pikipiki aliyopanda Linda Mwacha,imefika.
“Hapana Necka,nitalipa mimi”
Linda Mwacha,akaingiza mkono ndani ya mkoba wake mdogo na kutoa noti ya shilingi elfu kumi,alivyorudishiwa chenji akaanza safari ya kulifuata jengo la Hospitali hiyo lilipo.Huko walitembea harakaharaka mpaka mapokezi,bila kuuliza chochote walivyoangalia upande wa pili wakaona wanafunzi wenzao,wakawaendea kwa kasi.
“Imekuwaje?Hajrath anaendeleaje?”
“Sijui,ana hali mbaya”
Msichana mmoja,aliyeweka mikono shavuni alijibu.Ilielekea aliguswa mno na kitendo cha Hajrath kutaka kujiua, japokuwa hakuwa na urafiki naye wa karibu namna hiyo.
“Imekuwaje kwani?”
“Sisi hatujui,tumepigiwa simu.Ndio tumefika muda sio mrefu”
“Anaendeleaje?”
“Ana hali mbaya sana”
Siku hiyo ilikuwa siku ya majonzi mno!Kila daktari alivyofika kuwaona hakutoa majibu yanayoeleweka.Macho ya Necka wakati wote yalikuwa kwa Ahmed,hakuelewa ni kitu gani haswa kilimfanya awepo hospitalini hapo,jambo lililomfanya apatwe na wivu,akamsogelea mpaka karibu kabisa bila aibu.
“Njoo tuongee Ahmed”
Necka,alikuwa sikioni kwa Ahmed.Anamnong’oneza,Ahmed akasimama kisha kutoka pembeni.
“Njoo nje huku kabisa”
“Necka kuna nini?”
Ilibidi Ahmed ahoji,alikuwa ana kila sababu ya kuuliza kwani Necka alimburuza msobemsobe,wakatoka mpaka nje kabisa!
“Unafanya nini hapa?”
Necka akatupa swali,hakuwa ana punje ya masihara hata kidogo!
“Nimekuja kumuona mgonjwa”
“Wewe ana kuhusu nini?”
“Ni mwanafunzi mwenzangu”
“Mwanafunzi mwenzaaaakoooo!!!”
“Ndio,Necka.Ebu tuache masihara,Hajrath alitaka kujiua.Sisi tumesababisha”
“Unaumwa kweli wewe!Ana shida zake zinamsumbua.Tena,bora angekufa tu”
“Angekufaa?Hivi,unakisikia unachokiongea?”
“Ndio,bora angekufa.Mimi nibaki nawewe”
“Necka,unamuombea mwenzako kufa?”
“Kataka mwenyewe,au bado unampenda?”
“Tuachane na hayo,si nimekwambia unisubiri geto lakini”
“Siwezi kubaki mwenyewe kukusubiri,nimekuja kukuchukua tuondoke wote”
“Sasa hivi?”
“Sasa hivi ndio,kumbe saa ngapi?”
“Unadhani watanifikiriaje nikitoka pale?Italeta picha mbaya”
“Mimi hainihusu,wewe nenda kaage.Kwani wewe una mahusiano gani na Hajrath?Kama unampenda niambie ili nikuache naye,mimi sitaki kushea hata siku moja.Niambie hapahapa, chagua kimoja ubaki hospitalini tuachane ama tuondoke wote?”
Necka alizungumza na mwisho,akahitimisha na swali tata.Lililomfanya Ahmed,aishiwe pozi.Swali lilikuwa ni rahisi sana lakini jibu lilikuwa ni zito kulitoa.
“Ahmed nijibu,Mimi ama ubaki hapa?”
Necka Golden,akapigilia swali lake msumari wa nchi saba!Zaidi na hapo aliuliza kwa hasira za waziwazi,akimuangalia Ahmed machoni bila kukwepesha macho.
“Ahmed nijibu”
Hakuna siku aliyokuwa katika wakati mgumu kama hiyo,alikuwa ni mwanaume lakini siku hiyo alifyanta mkia kwani alitakiwa siku hiyo kunyoa ama kusuka.Akamtizama Necka Golden aliyekuwa mbele yake,akamkumbuka Hajrath, ambaye kwa wakati huo yupo kitandani anapigania uhai wake.Ndani ya moyo wake kukawa na nafsi mbili zinabishana, moja ikimwambia abaki hospitalini Hajrath anampenda ndiyo maana alitaka kujiua lakini nyingine ilimwambia hapana baki na Necka Golden,ndiyo chaguo lako.Vitu vingi sana vikawa vinapita ndani ya kichwa chake,akawa kama anatizama kaseti ya kusisimua ndani ya sekunde hizo chache.
“Ahmed,nijibu.Si naongea nawewe”
Necka akauliza kwa mara nyingine,hiyo ikamfanya Ahmed azinduke kutoka katika dimbwi la mawazo!
“Ngoja,nakuja.Naenda kuaga mara moja”
Ahmed,akasema.Nafsi ya pili ikachukuwa ubingwa,Necka Golden akashinda!Ahmed akaingia ndani ambapo huko alitoa dharura akidai kwamba anaenda hosteli kwake na angerejea baada ya muda mfupi,akaondoka zake.
Hazikupita dakika mbili,Necka Golden akaingia, nayeye akatoa sababu isiyokuwa na mashiko,jambo hilo lilifanya kila mtu aanze kuhisi kitu.Haikuwezekana hata kidogo Necka Golden afike hospitalini hapo watoke nje,alafu baada ya muda mfupi Ahmed arudi kuaga na baadaye Necka Golden.Hakukuwa na mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na minane,walijiongeza na walianza kuhisi nini kinaendelea ukichanganya na skendo iliyokuwa inavuma chuoni, kuna vitu vilipita ndani vichwa vyao lakini hawakutaka kuulizana kwa wakati huo kutokana na mazingira yaliyokuwepo.Mpangw’a akamsindikiza kwa macho Necka Golden,mpaka alivyopotelea kwenye korido ya hospitali hiyo,akashusha pumzi ndefu na kugeuka upande wa pili.
“Mpangw’a”
Sauti ya chini,ilisikika ikiita!Msichana mmoja mrefu kiasi akamsogelea,karibu zaidi na kukaa pembeni yake.
“Prisca,vipi?”
“Kumbe kweli?”
“Kweli nini?”
“Mhh,si kuhusu Ahmed na Necka”
“Wamefanya nini?”
Mpangw’a akajifanya hajui chochote,alielewa sana msichana huyo Prisca, anataka kumchimba.
“Don’t tell me hujui,kinachoendelea.Na nina uhakika sana!Hajrath alitaka kujiua kwa ajili yao”
“Una uhakika?Ebu acha hizo habari”
Sio kwamba Mpangw’a hakujua habari hizo,la hasha!Bali hakutaka kulisapoti jambo hilo kwa wakati kama huo wa majonzi,ilikuwa ni lazima kwanza wahakikishe Hajrath anakuwa katika hali nzuri, ndipo wazungumze mengine.

*****
Siku mbili zilipita,hali ya Hajrath haikuonesha matumaini yoyote yale.Hiyo haikufanya marafiki zake,wamtose na kumchinjia baharini! Ilikuwa ni lazima kila siku waambatane mpaka hospitalini ili kumjulia hali.Kilichowashangaza na kuweka alama ya viulizo vichwani mwao ni Ahmed,kutoonekana tena hospitalini hapo.Sambamba na Necka Golden pia alikata mguu kabisa,jambo lililozidi kuzua mashaka,hilo halikuwa na mjadala!Walilipitisha moja kwa moja ya kwamba watu hao wawili ni mtu na mpenzi wake.Siku iliyofuata wazazi wa Hajrath pamoja na kaka yake mkubwa waliwasili Jijini Arusha, wakitokea Dar es salaam,hali ya mtoto wao iliwatoa machozi.Kila mtu hakuamini,Hajrath alikuwa bado amevimba mwili mzima.Chanzo cha jambo hilo kiliwafanya washtuke zaidi,haikuwezekana hata kidogo mtoto wao atake kujitoa uhai.Sababu kila kitu walimpa,wakati mwingine walijinyima ili mtoto wao asome vizuri, kwa maana kwamba walimtumia pesa kila mwisho wa mwezi.Walivyojaribu kudadisi walishindwa,jibu hilo hawakuweza kulipata mpaka Hajrath mwenyewe,kifupi walikuwa katika kitendawili kikubwa sana kilichokosa majibu.
“Mlisema alikuwa wapi?”
Swali hilo liliulizwa zaidi ya mara sitini na kaka yake Hajrath,aliyeitwa Hussein.Aliuliza akiwa mwenye uzuni tele.
“Alikutwa Ngurelo”
Amney,alijibu.
“Kwanini alitaka kujiua sasa?”
“Kwa kweli,hata sisi jambo hilo tunashindwa kulielewa”
Maswali ya hapa na pale yalizidi,siku hiyo Hussein akawa kama shushushu anayetaka ripoti.Na kila alichokiuliza alijibiwa kiufasaha zaidi.Mwisho wa siku akaanza kuhisi ni lazima kuna jambo zito nyuma yake!

******
Wakati Hajrath akiwa mahututi kitandani,anapambana kukishinda kifo.Yeye Ahmed pamoja na Necka Golden usiku huo walikuwa Njeer’s Club,wanaruka majoka!Watu walikuwa wengi mno ndani ya club hiyo, ambayo ilikuwa ndiyo kwanza ina miezi kumi tangu izinduliwe.Mziki ulikuwa unapiga mno,wavulana kwa wasichana wameshikana viuno,wana bambiana.Wanacheza mziki,wanayarudi.Sio siri,ilikuwa ni furaha kubwa sana kwa Necka,ukizingatia aliweza kumshawishi Ahmed aingie ‘club’ jambo ambalo hapo awali lilikuwa gumu kutokea.
Robo tatu ya wadau wa ‘club’ hiyo walikuwa ni wanafunzi wa chuo cha Makumira,hilo lilikuwa wazi kabisa!
“Bebiiiiiiiiii,onjaaaa basi.Just oneee…Jamaaniii pleaseee,for the sake of love come on beibiiiii”
Necka Golden alikuwa anatema ung’eng’e kama mzungu vile,hii ndiyo ilikuwa sifa kubwa ya mrembo huyu.Hasa akiwa yupo mtungi,yaani amelewa pombe.Mkononi alikuwa ameshika glasi yenye mvinyo aina ya Jack Daniels, anamuhimiza Ahmed,aonje.Kwa nguvu ya penzi na ushawishi mkubwa,Ahmed akachukuwa glasi na kuiweka mdomoni.
“That’s maaaa Boiiiiiii”
Hapohapo Necka akamsogelea Ahmed midomoni na kuanza kumla denda.
“Ahmeeeeeeediiiiii,niweweee jembe langu”
Ilikuwa ni sauti iliyomshtua mpaka Necka Golden,Ahmed akageuka na kuona sura ya rafiki yake Gabriel.Akatabasamu kidogo!
“Gebooo!!”
“Siamini,hata wewee.Unakuja maeneo kama haya,dunia simama nishuke”
Mara ghafla ikawa shangwe,Gabriel akamtizama Necka Golden na kumgeukia Ahmed.
“Ndio shem sikuu hiziii?”
Gabriel akauliza.
“Yeah,ndio”
Kilichofuata hapo kilikuwa ni furaha,usiku ulikuwa mwingi lakini ndani ya club hiyo ambayo walikuwa wana kibali cha kupiga mziki mpaka asubuhi, ilikuwa kama ndio kumekucha vile.Mziki ulikuwa ukipigwa mno!Watoto wa Arusha walipandisha mori.
“Kakaaaaa,huyu ni demu wakooo?”
Gabriel akamuuliza Ahmed kwa mara nyingine,karibu na sikio lake.
“Ndiooo”
“Huyu ni Neckaaa?”
“Ndioo yeye,vipi kwanii?”
“Malaya huyuuu,anajiuza.Kama unanikubali mwanao mteme na huyuuu gashiii,atakuuua.HUYU NECKA GOLDEN NI MALAYAAAA KAKA”
Sijui ilikuwaje,haikujulikana kama Dj alizima mziki ama alitaka kubadilisha nyimbo kwani mziki ulizima ghafla na Gabriel alikuwa akimalizia sentensi yake ‘HUYU NECKA GOLDEN NI MALAYA KAKA’ kwa sauti kubwa ikafanya ieneee ‘club’ nzima.Necka alikuwa pembeni yake,maneno hayo yalipenya kama yalivyo!Akamgeukia Gabriel.
“Gabrieel,unasemaaa niniiii?”
Necka akauliza kwa shari huku akimsogelea Gabriel,mkononi alikuwa ameshika glasi ya pombe.
“Unasemajee?Wewe Mbwa”
Kufuatia sentensi hiyo,akam-mwagia Gabriel pombe usoni.Gabriel hakutaka kukubali,akarusha kofi lililompeleka Necka chini mzimamzima puu.Alivyoinuka alikuwa ameshika chupa,bila kuuliza chochote akampasulia nayo Gabriel Kichwani.Damu zikaruka kama bomba la maji lililotoboka,Gabriel akaenda chini huku damu zikiwa nyingi mno zinamvuja.Mambo yakawa tayari yameharibika!


Damu zilikuwa nyingi upande wa kaunta,zikatapakaa mpaka chini kabisa!Waliokuwa jirani na eneo hilo,wakaogopa wengine walikimbia, baadhi yao wakasogea karibu.Tukio hilo,likazua vurugu kuliko kawaida, badala ya furaha mambo yakawa kinyume chake,jambo hilo likafanya mziki upunguzwe sauti kutokana na kashkash kuibuka ghafla,mwishowe ukazimwa!Gabriel alikuwa chini anavuja damu nyingi sana,ameshika kichwa chake anahisi kizunguzungu kikali kutokana na damu kutoka kwa wingi.Ahmed alikuwa pembeni,alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa hajui achukuwe hatua gani aamini kitu alichokuwa anakiona mbele yake,ni wazi kabisa dalili mbaya sana zilikuwa mbioni kutokea siku hiyo usiku.
Necka Golden alivyoona jambo hilo aliogopa,akajua tayari ameshaua!Akatizama huku na kule na kuanza kupangua watu ili akimbie.
“Mkamateni huyo dada,pigeni simu polisi haraka sana”
Jamaa mmoja alisema kwa sauti.Tukio hilo lilikuwa la kutisha mno na halikuwahi kutokea ndani ya club hiyo tangu ifunguliwe.Kilichofanyika hapo ni meneja kutokea,haraka akapiga simu polisi na Necka Golden hakufika mbali,akashikiliwa.Dakika mbili baadaye,Deffender ya polisi kutoka Usariva ikawa imefika nje imepakia askari nane ndani.Askari watatu wakatua ardhini na kuzama ndani ya club ili kuangalia nini kimetokea,walichokiona hata wao walikiogopa.
“Mpakieni ndani ya gari,nani kafanya hivi?”
Aliuliza afande Ndomba,akiangalia huku na kule kwa hasira!
“Yule dada pale”
“Mpakieni kwenye diffenda nayeye,mvishe bangili sasa hivi”
Kama kawaida ya maaskari kuwa na mikwara na ndivyo walivyofanya kwa vitisho,Necka Golden akavalishwa pingu na kuanza kusukumizwa kutoka nje.Kimini alichovaa kiliwafanya maaskari wamuangalie kwa uchu wa matamanio.
“Wazazi wenu wanajua mnasoma,nyie mnakuja kugombania wanaume.Panda nyuma huko,ukanyee debe.Kesi ya mauaji itakuhusuu kunguni wewe”
“Nisa..meheeni”
Necka Golden alihisi kujuta,machozi yakaanza kumtoka, akiwa ndani nyuma ya Diffenda.Kichwani kwake picha ya milango ya gereza kufunguka nayeye kuswekwa ndani kifungo cha maisha ,ilianza kujijenga endapo Gabriel asingepona.Kilichomuuma zaidi ni baada ya kumuona Ahmed yupo nje ya mlango wa Club ametoka,macho yao yakagongana!Hapohapo Diffenda ikachomoka kwa kasi ya mkuki,mpaka kituo cha polisi Usariva!Diffenda ikapiga msele nje ya kituo,wote wakateremka!Pamoja na mtuhumiwa wao, Necka Golden.
“Humu ndani ya mkoba kuna nini?Njoo hapa.Afande Njau,chukua maelezo ya huyu dada.Kesho apelekwe gerezani”
Sentensi hiyo ilimfanya Necka atetemeke zaidi na kuona mwisho wake tayari umefika.Maelezo yake yakachukuliwa na kuamriwa aingie nyuma ya nondo.
“Naomba nipige simu”
Necka Golden akaomba.
“Upige simu wapi?”
“Nataka kuwaambia wazazi wangu kuwa nipo hapa”
“Baadaye,pita kule pumbavu”
Akili ya Necka ilimtuma moja kwa moja apige simu kwa Mr.Mwapongo, akiamini fika kwamba Mzee huyo ndiye aliyekuwa mwenye uwezo wa kutoa kitanzi kilichokuwa kinamkabili usiku huo.
Afande Ndomba tangu alivyomtoa Necka Golden club alimuangalia kwa jicho lingine la uchu,ndiyo maana alivyofika kwenye difenda akarudi tena kaunta ambapo kulikuwa na askari mwingine mwenye kazi ya kuandika maelezo.
“Yule dada yuko wapi?Niliyemleta hapa?”
“Yupo ndani”
Afande Ndomba,akatembea mpaka zilipokuwa nondo!Ndani yake kulikuwa na wanawake wengine, waliokuwa na makosa.
“Wewe,embu njoo hapa”
“Mimiii?”
Akauliza Mama mmoja, aliyekaa kushoto kabisa.
“Sio wewe, ebu weka matako yako chini.Wewe hapo.Njoo hapa”
Afande Ndomba alikuwa nje ya nondo!Anahitaji kuzungumza na Necka Golden,ambaye alisimama na kusogea karibu,kilichowatenganisha zilikuwa ni nondo zilizopita katikati yao!
“Vipi?Unataka kutoka?”
“Ndio afande”
“Una uhakika?”
“Sitaki kukaa huku afande,nisaidie nitoke.Naomba simu nizungumze na wazazi wangu”
“Subiri kwanza kabla hujafika huko.Mimi ninaweza kukutoa.Huku sio kuzuri,utanisaidiaje?”
“Nitakupa pesa afande”
“Sitaki pesa,jiongeze basi.Ili utoke humu,nishakwambia sio pazuri hapa!Fanya haraka,ama unataka kubaki?”
Afande alivyohitimisha na swali,akajifanya kutaka kuondoka lakini Necka akamuita akimsihisi kwamba atampa chochote anachotaka.
“Sawa subiri hapa”
Afande Ndomba,akachomoka mpaka mapokezi kwa niya moja tu.Kuchukuwa funguo za selo.
“Nipo kule chumba cha sindano,asiingie mtu”
“Poa”
Hizo ndizo zilikuwa tabia za maafande hawa,kufanya ngono na wanawake waliokuwa sero wakiwahaidi kwamba,wangewatoa.Siku hiyo Necka Golden akawa amefia kwa mpika supu!Kila kitu kikafanyika,kufuli likafunguliwa Necka akatolewa na kuingizwa ndani ya chumba kidogo kilichokuwa na godoro chini.Afande akafunga mlango na kuanza kuvua mkanda wa suruali yake kwa kasi!
“Vua basi,si unataka kutoka au?”
Afande akasema baada ya kumuona Necka amesimama,ameduwaa.
“Afande sikuwa nina maana hiyo”
“Acha utoto basi,pumbavu utarudi ndani sasa hivi na kesho uwende jela.Unatoa,hutoi?”
Hapo hakukuwa na njia nyingine.Ilikuwa ni lazima Necka Golden atoe rushwa ya ngono ili awe huru,alijifikiria mara mbilimbili kabla ya kukubali.
Mbele yake alikuwa ana vitu viwili vya kuchagua, apanue miguu yake awe huru ama abane abaki ndani na kesho apelekwe mahakamani.Hakutaka kuteseka na aliamini kupanua miguu yake na kutoa penzi ingebaki kuwa siri,mwenyewe akapandisha sketi yake juu na kulala chali juu ya godoro.
“Vua mpaka hiyo ya juu,nataka nione mpaka huko bwana!Kaa vizuri sasa”
Afande akasema,Necka akatoa nguo zake zote.Afande akapanda juu yake.Akatoa muwa wake na kuipanua miguu ya Necka Golden huku na kule,akaingia katikati na kutumbukiza muwa wake ndani ya ikulu ya Necka na kuanza kujisevia!

*****
Kitendo cha Gabriel kupigwa chupa ya kichwa,kilivuma kwa kasi ya moshi wa kifuu!Ndani ya chuo cha Makumira!Sambamba na habari za Hajrath kutaka kujiua kwa kumeza vidonge.Mbaya zaidi walisikia sakata hilo lililosababishwa na Necka Golden,jambo lililowaacha wanafunzi vinywa wazi.
“Yule demu mafia,sikutegemea jombaa”
Jamaa mmoja alikuwa anapiga stori,ilielekea nayeye alikuwepo ndani ya club hiyo, siku ya tukio.
“Ulisema ilikuwajee?”
“Si unajua Gebo,inshu zake za kuropoka na umbea umbea.Sasa kauvagaa mziki wa Necka”
“Kivipi sasa?”
“Necka alikuwa na Ahmed,Club hiyo jana usiku.Sisi tumeingia tumewakuta,si akajifanya kwenda.Kama kawaida yake,kuponda mademu”
“Alafu si alikuwa anamtaka Necka pia?”
“Sio la kuuliza hilo.Alafu ndiyo tabia yake,akichezea cha mbavu anaponda sasa jana alionja joto la jiwe”
“Huo usnitch,mwanaume gani anakuwa kama punga”
“Ndiyo hivyo,akaanza kuropoka na kumkandia Necka”
“Enheee….”
“Kudadeki,kama sinema ya kikorea vile.Ile chupa sijui yule demu aliiokota vipi kama Nikita.Nikasikia pwaaaaa,huku na kule Gebo chinii unaambiwa.Mziki ukazimwa mzee.Ilikuwa bonge la soo babuuuu”
Stori za aina hiyo ndizo zilitapakaa chuo kizima,kila mtu aliamini uvumi huo!
“Necka yuko wapi?”
“Kwa tetesi nilizosikia yupo Lockup,jana usiku alichukuliwa na Diffenda”
“Acha utanii mpaka wamwela walifika?!”
“Ndio nakwambia sasa,hapa nataka kuvaa kwanza nikamcheki Gebo hospital”
“Ngoja namimi nikajiandae,twende wotee.Oyaaa Kijipuu eeh”
“Alafu kaka hilo jina mimi silimaindi,tutazinguana kaka”
“Poa basi,Denis.Ukienda class utakuja na begi langu,Frida ana laptop yangu utamwambia akupe”
“Aya,nimekuelewa.Frida Damas?”
“Ndio kijipu”
“Acha Useng** basi”
“Aya basi kausha Denis Mnyamweziiiii”
Siku hiyo ilikuwa ni lazima wakamuone Gabriel,hospitalini ili wajue hali yake inaendeleaje.

*******
Kilikuwa ni kitendo cha dakika tano baada ya kupigwa chupa lakini Gabriel alipoteza zaidi ya lita moja na nusu za damu mwilini mwake.Alivyofikishwa hospitali iliyokuwa ya karibu!Akawa amepoteza nusu lita nyingine,shuka zima lililowa damu chapachapa,uso haukujulikana upo wapi.Manesi walitoka mkuku mkuku mpaka kwenye Diffenda iliyopaki nje.
“Kafanya nini huyu?”
Nesi mmoja akamuuliza askari.
“Mlevi tu,kapigwa na chupa.Tutakuja kesho kuyachukua maelezo yake”
Ripoti hiyo ndiyo waliyoandika manesi,Gabriel akafunguliwa faili lake.Akachunguzwa vizuri na daktari.
“Hatuwezi kumshona”
Dokta akasema na kuweka koti lake vizuri.
“Kwanini?”
“Amekunywa pombe,mpaka iishe”
“Lakini dokta,umeona hali yake?”
“Ndio na sidhani kama atafika asubuhi”
Dokta Sajo,alifananishwa na gaidi siku zote, kusema vitu vya namna hiyo ilikuwa ni kawaida sana kwake.Maneno hayo yalikuwa ya kutisha lakini kwake yalikuwa ya kawaida tu,hiyo ndiyo ilikuwa sifa yake kubwa sana!Hilo lilikuwa ni kweli kabisa kwamba Gabriel asingeweza kufanyiwa upasuaji wa aina yoyote ile kutokana na kiwango kikubwa cha pombe alichokunywa.
Kutokana na taaluma aliyokuwa nayo Dokta Sajo,ilitosha kabisa kuwa mwenye uhakika na jambo alilotabiri kwani saa tatu kasoro saba asubuhi, Gabriel aliaga dunia.Hilo lilithibitishwa na Dokta Sajo mwenyewe, baada ya kuhakiki vipimo vyote.
“Mfunikeni,apelekwe Monchwari.Andika Accident kwenye dirth certificate yake, muda ni saa tatu kasoro saba”
Huo ndio ulikuwa ukweli,Gabriel akafunikwa na shuka.Taratibu za kupelekwa monchwari zikaanza dakika hiyohiyo.

******
Mbali na Necka kutoa rushwa ya ngono ili atoke usiku huohuo bila kulala kituo cha polisi lakini badala yake,hakutoka mpaka kunakucha.Ilivyotimu saa mbili asubuhi akapewa simu.Ni jambo moja tu,alitaka kulifanya kumpigia Mzee Mwapongo ili amtetee ikiwezekana amtoe,lakini aliapia ni lazima angemkomoa afande Ndomba kwa unyama aliomfanyia wa kumpa uroda burebure.
“Nataka kumpigia anco wangu”
Necka Golden,alimwambia Afande huyo aliyekuwa zamu asubuhi hiyo mapokezi.
“Sawa,nakupa dakika mbili”
Alivyopewa simu tu,kitu cha kwanza kusaka ni nambari za Mr.Mwapongo,simu ikaita sana bila kupokelewa, akajaribu tena!Ikaita na kupokelewa.
“Necka,nilikwambia usinipigie simu.Mpaka nikutafute mimi,kuwa mwelewa nina mke,si nilikutumia pesa tayari”
Upande wa pili wa simu,ulisikika Mr.Mwapongo alikuwa kwenye laini anazungumza kwa sauti ya chini.
“Nina shida.Ni muhimu,nahitaji msaada wako”
“Sawa,nitafute baada ya dakika tano”
“Hapana sasa hivi”
“Siwezi,ngoja kwanza.Dakika tano,nipo na mke wangu.Hapa nimekuja seblen asije akashtuka,nitakupigia Necka”
“Jam…tititi”
Mr.Mwapongo akapotea hewani baada ya kukata simu.Hilo halikuwa na mjadala,alivyomfikiria mtu mwingine wa karibu ampigie akakosa,akarudishwa nyuma ya nondo.
Ilivyofika saa 4;15 asubuhi,akasikia kelele za maaskari, kutokea kaunta wakitaja jina lake,mwisho akasikia kitu kama ‘Gabriel amekufa’akasogea karibu na nondo ili kusikia vizuri huku akihisi kama tumbo linamuuma, japokuwa hakuelewa nila kuharisha ama uwoga.
“Huyo ana kesi ya mauaji. Yule kijana amekufa leo asubuhi.Kwahiyo asitolewe dhamana yoyote ile”
“Sawa afande”
Maaskari wakaondoka zao,Necka akahisi kuishiwa na nguvu, alielewa fika baada ya hapo kifungo cha maisha, kingemuhusu.Hakujuwa atamueleza nini baba yake mzazi, Mzee Golden Chande!Ambaye alikuwa mkali kuliko pilipili mbuzi,alitamani ardhi ipasuke aingie ndani imfunike kuliko kukutana uso kwa uso na Mzee Golden Chande.Mbali na hapo,alitamani kila kinachotokea kiwe ni ndoto,ashtuke!



Kila kitu katika maisha yake kilikuwa ni kama sinema fulani ya kihindi tena ya kusisimua,hakutaka kuamini kama kufumba na kufumbua mambo yangebadilika namna hiyo!Alitamani walau arudishe siku nyuma,abadilishe kila kitu lakini mazingaombwe hayo yasingeweza kutokea habadani!Ni kweli,alikuwa ana shtaka kubwa kuliko yote.Shtaka la mauaji,kesi hiyo ilikuwa ni nzito mno na hakukuwa na namna yoyote ile ya kudhaminiwa mpaka uchunguzi wa kina ufanyike!Hilo lilithibitishwa na Afande Mkebe,akimwambia waziwazi bila kukwepesha.Necka Golden alimwaga machozi ya uchungu siku hiyo, akiwa bado yupo mahabusu.Kifupi alijuta mno,kuingia club usiku ule!Mbaya zaidi mpaka inafika saa saba hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyeenda kumuona!
Tukio la Necka Golden,kuuwa liliwekwa kwanza chini ya kapeti ili wamtafute muhusika yoyote wa chuo cha Makumira, apewe habari hizo juu ya mwanafunzi wake.Jambo hilo halikuwa tatizo,wakafanikiwa kumpata Professor Shayo,mzee mkongwe ambaye alitunukiwa cheo hiko kutokana na kusoma sana na kuandika silabasi za chuo kizima na topiki zote madarasani kiujumla.
“ Kuna mwanafunzi wako,tumemshikilia”
Afande,akaanza kutoa maelezo baada ya salamu za hapa na pale.
“Mwanafunzi wangu?Wa Chuo gani?”
Ilibidi aulize swali hilo kwani Professa Shayo,mbali na kufundisha chuo cha Makumira alikuwa pia anafundisha vyuo vingine vingi.
“Makumira”
“Makumira?”
“Ndio”
“Mnamshikilia kwa kosa gani?”
“Ni hadithi ndefu kidogo lakini kifupi,ni kosa la mauaji”
“Murder case!?”(Kesi ya Mauaji)
“Ndio,tukaona tukutafute wewe.Ili tujue tutaanzia wapi?”
“Yaaani mtaanzia wapi kivipi?Mbona nashindwa kuelewa”
“Ni kwamba,inabidi uthibitishe kama kweli ni mwanafunzi wako”
“Afande,ninafundisha wanafunzi zaidi ya elfu tatu.Siwezi kuwatambua wote.Huyo mwanafunzi jina lake nani?Alifanya nini?”
Afande aliyekuwa zamu siku hiyo anamuhoji profesa Shayo,alipata kibarua kingine kipya cha kumuhoji mzee huyo aliyeonekana ni mtata wa kichinichini.
Badala ya kutumia dakika arobaini na tano, wao walitumia lisaa limoja na nusu kumaliza kila kitu na wakafikia muafaka ya kwamba wazazi wa Necka Golden, wapigiwe simu.Hilo ndilo suluisho lililobakia ili baada ya siku chache,faili la Necka Golden lisogezwe ngazi za juu na kesi yake ianze kusomwa!

*******
Hakuna mwanafunzi aliyekuwa tayari kuzipokea habari hizo za msiba wa Gabriel,kila mtu alisikitishwa sana!Kuna waliolia na wengine kupoteza fahamu kabisa lakini mwisho wa siku hakukuwa na kitu chochote, kilichoweza kubadilisha kifo hicho.Chuo Cha Makumira kilikuwa katika msiba mzito cha kufiwa na mmoja wa wanafunzi wao,siku mbili nzima wakatumia kuomboleza na siku ya nne ilivyofika mwili wa Gabriel ukawa umesafirishwa mkoani kwao Iringa, akapumzike kwenye nyumba ya milele,kifo cha Gabriel kilikuwa kama utani vile lakini ndiyo, ilikuwa safari yake ya mwisho duniani.
“Weee,mimi naamini malipo ni hapahapa duniani”
Jamaa mmoja alisikika akimwambia mwenzake, siku hiyo wakiwa wanajisomea usiku.
“Kivipi Jordan?”
“Unakumbuka Marehemu Gebo,alivyowagombanisha Hajrath na Ahmed?”
“Si ile siku kule Block C?”
“Ndio”
“Anhaaa,kumbuka pia Necka Golden,alikuwa anagogwa na Ahmed”
“Hizo si tetesi tu”
“Ah wapi,juzi hukuwepo mahakamani.Necka alikuwa na Ahmed club,ndio ule ugomvi ukatokea”
“Sasa unataka kusema nini kaka?”
“Malipo ni hapahapa duniani mzee.Walichomfanyia Hajrath ndio malipo yao hayo”
“Sio kweli,kifo kilipangwa bwana”
“Ndio nakwambia hivyo mimi”
“Ebu tusome,wiki ijayo pepa”
“Baadaye,utaniazima laptop yako.Kuna ile grup work nataka kuangalia”
Yapata wiki sasa,tangu msiba wa Gabriel kuisha.Sambamba na hapo Necka Golden alihukumiwa kifungo cha miaka kumi na mitano jela,kesi yake ilipungua makali sababu aliua bila kukusudia, vinginevyo kifungo cha maisha,kingemuhusu!

*******
Upepo ulikuwa mkubwa,hiyo ilifanya mpaka vumbi liwe jingi na kusababisha watu wasionane!Vitu vya ajabu vilikuwa vinapita mbele yake,hakuwa mwenye uhakika kama ni ndoto ama ni kweli.Kwani katika eneo hilo alikuwa peke yake,giza lilikuwa totoro!Ghafla akasikia sauti za bundi na ndege wa mwituni.
“Ha! Haa! Haaa! Haaa! Haaaaa!”
Sauti hiyo ya kucheka ilisikika ikijirudia,ilikuwa ni nzito mithili ya radi.Akazidi kuchanganyikiwa.Akahisi kama kuna kitu kimepita juu kwa kasi vuu!Hofu ikaanza kumtanda, baada ya kuona kitu cha ajabu mbele yake,alikuwa ni mnyama mwenye kichwa cha paka lakini masikio marefu,pembeni ana mabawa.Midomo yake ilikuwa ni mikubwa ya kutisha.
“Ha!Haa!Haaa!Haaaaa!”
Alivyocheka,akapanua mdomo hapo ndipo akaona meno marefu ya kiumbe hiko ambacho hakujua kinaitwaje.Kifupi aliogopa mno,akaanza kukimbia lakini hakuweza kwani alikuwa yupo palepale, mnyama huyo wa ajabu akaanza kucheka kwa sauti kubwa huku akitoa ulimi wake uliokuwa mrefu sentimita nyingi!
“Hauwezi kwenda popote popote pooopoooteeee wewe ni waaanguuu”
Sauti yake ilijirudia kama mwangi,akachanua mabawa yake na kutoa mikono yake yenye kucha ndefu na kuanza kumkaba,mara ghafla ukatokea mwanga mkali mno!Ukapiga eneo hilo,mnyama huyo akadondoka chini.
“Hajraaaaath”
Sauti hiyo ikasikika,Hajrath akashindwa kuona vizuri kwani ulikuwa ni mwanga mkali mno.Akashikwa kichwani.
“Umekishinda kifo,rudi duniani”
Mwanga ulizidi kuwa mkali.

*********
Ilikuwa ni katikati ya usiku,Nesi akiwa ndani ya wodi la mgonjwa ambaye zaidi ya mwezi mmoja,hakujitingisha wala kufanya chochote kile.Kitendo cha Mgonjwa huyo kujitingisha na kuchezesha vidole kilimfanya Nesi Warda,akimbie mpaka kwa daktari kumpa taarifa hizo.Jambo hilo likawa habari njema,dokta alivyofika tu.Akatabasamu,Hajrath alikuwa ameyafumbua macho yake,anatizama huku na kule!Akijaribu kuvuta kumbukumbu,ghafla picha ya mnyama wa ajabu pamoja na mwanga mkali vikaanza kujirudia ndani ubongo wake.Hakuelewa kama alikuwa yupo kwenye njozi ama ni kweli.
“Ha…pa wapi?”
Hajrath akauliza kwa taabu,sauti yake ilikuwa ya chini mno!Bado kumbukumbu hazikuwa zimekaa vizuri,zilikuja na kupotea kama saa mbovu!
“Upo Mount Meru hospital”
“Hospita..li?”
Hajrath akatulia kidogo,taratibu akaanza kukusanya tukio moja baada ya lingine.Akaona sura ya mwanaume Ahmed akiwa na Necka mara ya mwisho,akakumbuka alivyoenda duka la madawa na kujificha akitaka kujiua.Alivyofika hapo,machozi yakaanza kumtoka.Bado hakuwa mwenye uhakika kama yupo ahera ama amepona na kama amepona,ilikuwaje?Hicho ndicho kitendawili kilichokuwa kichwani kwake akashindwa kukitegua,siku hiyo!
Habari za Hajrath kufumbua macho yake na kuzungumza usiku huo, ulikuwa ni kama muujiza mkubwa kutokea!Wazazi wake muda wote walimshukuru Mungu kwa kufanya muujiza huo kwani tayari walishakata tamaa kabisa na muda wowote walikuwa tayari kupokea habari za msiba,kifupi walikuwa hospitalini tayari kurudi na mwili wa binti yao!

Afya ya Hajrath ilizidi kuimarika siku hadi siku,siku ya nne ilivyofika akawa anaweza kutembea mwenyewe, akizunguka na kufanya mazoezi na wagonjwa wenzake!Kitu kilichokuwa kinamsumbua siku zote ni mwanaume anayeitwa Ahmed,alijaribu kumtoa kabisa kichwani kwake lakini wapi,alishindwa.
“Hajrath,ilikuwaje kwani?”
Swali la namna hiyo halikuwa mara ya kwanza kuulizwa,kila mtu alitaka kujua chanzo cha yeye kutaka kujiua.Japokuwa aliulizwa,karibia na kila mtu lakini hakuwa tayari kutoboa siri,alihofia kuonekana mjinga na mpumbavu ama limbukeni wa mapenzi kwani wanaume wapo wengi.Ndiyo maana akapiga kimya!
“Pole mpenzi,nisamehee pia kwa yote yaliyopita ni shetani tu”
Siku hiyo sijui Erasto aliibuka kutokea shimo gani,akafika mpaka hospitalini na kumpa pole Hajrath.Hata yeye aliguswa na mkasa huo uliomkuta msichana anayempenda kwa dhati.
“Ahsante”
Hajrath,akaitikia kishingo upande.Ki ukweli alimchukia Erasto kuliko kawaida.Aliamini kwa njia moja ama nyingine yeye ndiye aliyesababisha mpaka Ahmed amteme.
“Nimekwambia ahsante,mkeo ajambo?”
“Tuachane na hayo,nimekuletea matunda.Yapo pale mezani”
“Aya”
Mawazo mengi yalimfanya akose raha ya maisha,japokuwa marafiki zake walifika kila siku kumuona lakini hiyo haikutosha.
“Hivi,naomba niulize kitu”
Siku hiyo Hajrath,ilielekea kuna jambo alitaka kuwauliza marafiki zake.Kilichowafanya marafiki zake wafurahi namna alivyochangamka, asubuhi hiyo.
“Uliza besti”
Amney,akadakia wote wakamtizama ili aseme anachotaka kuuliza.
“Necka Golden,sijamuona hapa.Yuko wapi siku hizi?”
Lilikuwa ni swali la mtego,Hajrath alitaka kupima maji.Akitegemea kuambiwa wapo na Ahmed ama asipewe jibu linaloeleweka.
Marafiki zake wakatizamana,kuna kitu alijifunza kutoka machoni mwao lakini hakuwa mwenye uhakika nacho,alichotakiwa ni kusubiri na kusikia atakachoelezwa,alikuwa yupo tayari kwa jibu lolote lile.
“Kwani ulikuwa hujui?”
Mpangw’a akadakia.
“Sijui nini?Siku zote nilikuwa hospitali.Nitajua nini mimi mwenzenu?”
“Yupo gerezani,amefungwa”
“Acha utani Mpangw’a,mimi nipo siriazi mwenzako”
“Khaa!Huamini au?”
“Nipo siriazi ujue,yupo wapi jamani?”
“Anachosema Mpangw’a ni kweli”
Amney,akatilia mkazo jambo hilo.Hapo ndipo taratibu walianza kumuelezea ilivyokuwa.Alishtuka zaidi baada ya kusikia Gabriel alifariki,moyo wake ulimuuma japokuwa hapo nyuma alimfanyia ubaya.
“Eeeh,Rest in Peace Gabriel.Kwanini lakini?”
“Ndio hivyo Hash,ya Mungu mengi”
Siku hiyo walizungumza hadithi nyingi na kupiga stori za hapa na pale,moyo ulimuuma tena Hajrath, alivyosikia baada ya wiki moja,mtihani wa kumaliza Semista ungeanza,aliumia mtima kwa sababu ilikuwa ni lazima arudie mwaka mwingine.
“Usiumie sana,tutakuwa wote.Nina vimeo vitatu mwenzangu.Nina Sap!Wala hainitii presha, Chuo sap ni sunaaa”
“Mimi ninayo moja,inabidi nirudie mwakani”
Hajrath alifarijika mno.Wakiwa katikati ya maongezi mlango wa wodi ukafunguliwa,kila mtu akageuka nyuma.Mtu aliyeingia alifanya kila mtu asiamini,alikuwa ni Ahmed.Moyo wa Hajrath ukalia paaa!Akahisi kama amepigwa na shoti ya umeme,kumbukumbu ya tukio zima akiwa na Necka Golden, likamjia kichwani ghafla.
“Habari zenu”
Ahmed,akasalimia lakini hakuna hata mmoja kati yao, aliyeitikia salamu hiyo!
“Hajrath pole Darling”
Sentensi hiyo,iliwatia kichefuchefu cha kutapika wodi nzima.Sio Hajrath peke yake, mpaka wakina Amney!
“Unaendeleaje?”
Ahmed,akataka kujua hali ya Hajrath.Matokeo yake ilikuwa ni kama anazungumza na sanamu!
“Amney,hali ya mgonjwa vipi?”
Ahmed,akamgeukia Amney na kumtupia swali.
“Mimi sio daktari”
Jibu hilo lilifanya Mpangw’a aliyekuwa pembeni acheke kwa sauti ya juu,jibu hilo kwake alilifananisha na kibonzo!Hiyo ilikuwa ndiyo tabia ya msichana huyu,kucheka cheka hovyo hata kama watu wapo siriaz!
“Lakini,ulikuwepo hapa”
“Acha unafki,umekuja kujua hali ya Hajrath ama kum-malizia?”
“Nimekuja kujua hali yake”
“Kama unavyomuona, ahsante”
“Mbona unakuwa hivyo?Hatupo hapa kugombana”
“Stoop,huna hata aibu!Mwanaume mzima,hovyoo!Na Mungu amekulaani,ile chupa ungepigwa wewe”
Siku hiyo Ahmed alipakwa shombo na Amney,akamchambua kila kitu!Akamsema,wala hakuogopa.
“Wewe wa kumfanyia Hajrath hivi?Ahmed wewe ni mnyama,mwanaume huna hayaaa hasidiii.Hivii umefuata nini hapa?Toka humu ndani”
Wakati maneno hayo yanatoka,Hajrath alikuwa anatiririkwa na machozi ya uchungu huku akimtizama Ahmed,mapendo aliyokuwa anampa hapo awali yalikuwa kama kwenye kioo sababu aliyaona kichwani!
“Ah…med”
Hajrath akaita huku kwikwi ikiwa imem-kaba kohoni.Kila mtu akamgeukia wakaacha kulumbana!
“Uli..taka nif..e ndi..o ufurahiii,nili..taka kujiua kwa aji..li yako kwanini lakii..ni?”
Bila kuulizwa siku hiyo, Hajrath akaanza kusimulia na kufunguka kila kitu kilivyokuwa,tangu alivyomfumania Ahmed na Necka Golden,ilikuwa ni simulizi ya kusisimua.Akahitimisha siku ambayo Erasto alitaka kum-baka chumbani,hakuna kitu chochote alichokiacha nyuma.
“Hajrath,nisamehee Mpenzi wangu.Sahau yaliyopita tugange yajayo.Nishajifunza,binadamu tunajifunza kutokana na makosa!”
“Nime…kusamehe la…kini ha..tuwezi ku..wa pa..moja te..na Ahmed,siwezi”
“Nadhani umemsikia,toka nje”
Amney,akapigilia msumari swala hilo.Ahmed akatimuliwa nje kama mwizi.Ni kweli,Hajrath aliamua kumfuta Ahmed ndani ya moyo wake,kifupi aliapia kutoka moyoni mwake kwamba, hatopenda tena!


Maisha ya Ahmed kuanzia siku hiyo,yalikuwa yenye huzuni mwingi.Mawazo yalimtawala kichwani kwake yakatafuna ubongo wake,kusoma tena hakuweza!Japokuwa mitihani ilikuwa inakaribia lakini yeye muda wote alibaki 'hostel' kulala na kumuwaza Hajrath tu,alihisi kujuta kwa kila kitu alichokifanya.
Aliumia mtima kiasi kwamba wakati mwingine alipitisha siku bila kula,akakosa 'apetite' kabisa ya kunywa hata maji.Kazi yake ilikuwa ni kumfuata Hajrath na kumuomba msamahaa lakini hakufanikiwa,vyuma vilikuwa vimekaza.Kila alipojaribu kumuimbisha hakufua dafu!Akajaribu kumtumia Mpangw’a ili asawazishe lakini alichomolewa na kutolewa nje kwani alionekana hafai,jambo alilomfanyia Hajrath lilitosha kabisa kuonekana yeye ni mnyama wa aina gani,hakuishia hapo.Akajaribu kwenda hospitali na maua pamoja na zawadi kedekede lakini vyote vilitupwa akarudi navyo,akili yake ikarudi nyuma kwa kasi ya ajabu, akakumbuka namna alivyoteseka kumpata Hajrath mara ya kwanza,akakumbuka nyimbo ambayo Hajrath anaipenda mno!Hapohapo akatabsamu na kwenda mjini kununua redio ndogo,akanyoosha moja kwa moja mpaka duka kubwa linalouza flash,akanunua pia.Akaingia moja ya studio ambayo walikuwa wana 'burn' nyimbo.
“Bro mambo vipi?”
Ahmed akamsalimia jamaa aliyekuwa bize na kompyuta yake,anabani cd.
“Fresh,kaka.Nambie”
“Nahitaji nyimbo moja hiviii”
“Nyimbo gani?”
“Inaitwa baby Don’t go,wameimba hawa mademu wanaitwa Close to you”
“Ngoja kidogo”
Jamaa aliyekuwa nyuma ya kompyuta akaanza kutafuta nyimbo hiyo,ilielekea nyimbo ilikuwa mbali sana, ndiyo maana ikachukuwa dakika mbili nzima kuipata.
“Nikuwekee kwenye flash ama simu?”
“Kwenye hii flash,shika”
Nyimbo ikawekwa kwenye flash,siku hiyo Ahmed akawa anajaribu zoezi hilo kwa mara nyingine ili tu asamehewe!Ki ukweli, alivyoanza kuisikiliza nyimbo hiyo ya mapenzi,ilimkumbusha vitu vingi sana nyuma!Mbali na Hajrath kupenda nyimbo hiyo bali alikuwa anaweza kuiimba yote mwanzo mpaka mwisho,akili yake ikasafiri kwa kasi ya umeme, akakukumbuka matukio mengi ya kimapenzi waliyokuwa wanafanya.
Hususani walivyokuwa kitandani,siku ya kwanza wanafanya ngono huku nyimbo hiyo ya taratibu ikiwa inatumbuiza asteaste.Hapo hakutaka kupoteza muda zaidi,akapanda daladala mpaka hospitali.
Ambapo huko aliruhusiwa kupita mpaka wodini.Alivyozama ndani bahati nzuri,akamkuta Hajrath amelala kitandani,amefumba macho yake.Alichofanya Ahmed ni kuchukua ‘headset’ za masikioni,akamvalisha Hajrath kisha kui ‘play’ nyimbo hiyo.
‘Baby,please don’t go,please don’t leave me!”
Sauti nyororo kutokea kwenye spika za redio kupitia ‘headphone’ zilisikika masikioni mwa Hajrath huku vinanda vya taratibu vikiendelea kutumbuiza,ilikuwa ni nyimbo nzuri ya kimapenzi.
‘In my dreams I know you’re always by my side,
Everywhere I go you linger in my mind,
I’ve been waiting so long for a special guy,
Then you came to lift me up and make me fly,
Baby don’t go,
I just want you here,
Right by you’re side,’
Mashairi ya nyimbo hiyo yaliingia ndani ya ngoma ya masikio ya Hajrath,yakapenya mpaka kwenye moyo wake.
Bado alikuwa kwenye usingizi mzito lakini mbele yake alimuona Ahmed,hakuwa ana uhakika kama ilikuwa ni njozi ama ni kweli,sio siri nyimbo hiyo ilikuwa ya mapenzi naya taratibu mno!Akaanza kutabasamu akiwa amefumba macho yake hivyohivyo,mara akaanza kuifatisha akiimba.Machozi yakaanza kumtiririka,yakapita pembeni ya macho na kulowanisha shuka!Taratibu akaanza kufumbua macho yake,mtu aliyemuona amesimama mbele yake,alifanya mapigo yake ya moyo yapige kwa nguvu.Mbele yake alimuona Ahmed amesimama kama mlingoti,mboni za macho yake hazikumuongopea!
“Hajrath,nisamehee”
Ahmed,akazungumza kwa hisia kali sana huku akimuangalia Hajrath aliyekuwa kitandani.
“Ahmed,tafadhali nenda”
“Nisamehee Hajrath ni ibilisi tu,naomba unipe nafasi nyingine.Sitoichezea”
“Siwezi Ahmed,naomba uwende.Sitaki kuumia tena,imetosha.Kuna makosa mengi sisi binadamu ya kufanya lakini sio kurudia yaleyale”
“Usiseme hivyo mpenzi”
“Tafadhali nenda,siwezi.Nenda tu”
Katika swala zima la misimamo msichana huyu alikuwa akiongoza na Ahmed alilijua hilo kwani alijua fika kabisa kuendelea kumuimbisha Hajrath, ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki.Kumsamehee Ahmed hakutaka tena alihofia kutendwa,hata kama angewekewa kisu shingoni siku hiyo,kifupi alikuwa keshamtoa ndani ya mtima wake kabisa,huo ndio ulikuwa msimamo wa Hajrath kwenye kila kitu,siku hiyo Ahmed akaondoka bila kuambulia chochote!

*********
Siku zilizidi kusogea adoado!Kwa kosa alilotaka kulifanya Hajrath ilikuwa ni wazi kabisa kama angepona ni lazima jela ingemuhusu,ndiyo maana polisi kila kukicha walijaribu kuuliza hali yake ili wamfungulie mashtaka.Mzee Mpilla, baba mzazi wa Hajrath hakutaka swala hilo litokee ndiyo maana alijitahidi kula sahani moja na mapolisi,akijaribu kuwashawishi ili faili hilo litupiliwe mbali.
“Sasa mzee,utasemaje tuongee hivi hivi?Sisi wakubwa watatuelewa vipi?Faili lishapanda juu tayari”
Afande mmoja wapo kati ya wawili alizungumza, akizunguka mbuyu.Kukaa sana mjini Dar es salaam, kulimfanya Mzee Mpila ajue nini wanahitaji askari hao,hivyo alijiongeza.
“Naelewa afande,mkono mtupu haulambwi”
“Ndio maana yake,utaulamba vipi?Ongea lugha nzuri Mzee,tukalichome moto hili faili liwe majivu”
Kilichokuwa kina maanishwa hapo ilikuwa ni pesa,ilikuwa ni lazima mzee Mpilla atoe kitu kidogo ili kesi hiyo izimwe.Haikuchukuwa siku mbili.Maaskari wakatembezewa shilingi milioni mbili ili waachane na kesi hiyo,hatimaye pesa ikaongea askari wakazibwa midomo.Kilichobaki kuanzia hapo ni kusubiri Hajrath aruhusiwe na madaktari ili wamchukuwe na kuondoka naye jijini Dar es salaam kwani muhula ulikuwa unaenda kuisha,hakukuwa na jinsi ya Hajrath kuendelea kubakia mkoani hapo!Siku nne baadaye madaktari wakatoa ruksa ya yeye kuondoka,akaandikiwa na dawa zitakazomsaidia akiwa nyumbani.Hakukuwa na muda mwingine wa kusubiri,siku iliyofuata wakapanda basi kwa safari moja tu,kuelekea jijini Dar es salaam!

******
Hali ya Hajrath ilizidi kuimarika siku hadi siku,akiwa nyumbani kwa wazazi wake!Kimara stop ova,wazazi wake walimuangalia kwa jicho la tatu,wakihakikisha binti yao anakuwa katika maangalizi mazuri.Walizidi kukaa naye karibu ili kujua ni jambo gani haswa lililompelekea mpaka atake kuutoa uhai wake,lakini yeye hakuwa tayari kutoboa siri hiyo kwa wazazi wake!
“Mama,yashapita sitaki kukumbuka”
Hilo ndilo lilikuwa jibu la Hajrath siku zote,endapo akikumbana na swali hilo kwa mama yake mzazi.
“Wewe ni mtoto wangu wa mwisho Hajra,kwanini ulitaka ku..”
“Maamaaaa”
Hajrath alimkatisha Mama yake,hata yeye hakutaka kabisa kukumbuka habari hizo.Alijisikia uchungu ajabu.Hakutaka kukumbuka yaliyopita kabisa,ilikuwa ni lazima asonge mbele.
“Anyway,baba yako amekununulia simu.Sijui utaenda kurenew line yako?”
“Hapana,nitanunua mpya”
“Aya,mimi nipo jikoni”
Hayo ndiyo yalikuwa maisha ya Hajrath siku zote na tangu awepo nyumbani hapo,ruti zake zilikuwa tatu tu.Kama hayupo chumbani, basi seblen ukimkosa hapo ni jikoni!Hakuwahi kutoka nje ya geti,lakini kwa siku hiyo, ilikuwa ni lazima atoke nje akatafute laini ya simu mpya.Ilivyotimu saa kumi ya jioni,akaoga na kuvaa kisha kutoka nje ambapo huko alinyoosha mpaka duka kubwa lililokuwa upande wa pili wa barabara.
“Nahitaji laini?”
“Laini gani dada?”
“Airtel,au nipe Tigo.Una voda?”
Hajrath alibabaika kidogo!
“Dada unahitaji laini gani?”
“Voda”
“Sawa,hizi hapa.Chagua namba”
Hajrath akapewa kadi nyingi za simu,akaanza kuchagua namba itakayomfaa na nyepesi kwake.Alivyoridhika, utaratibu wa usajili ukaanza mara moja,ambapo alitoa kitambulisho na usajili ukaanza dakika hiyohiyo!Akarudi nyumbani na kutulia tuli akijaribu kuingiza laini ya simu.
******
Japokuwa ujio wake ulikuwa wa ghafla tena kimya kimya lakini vijana wa mtaani hapo walilijua jambo hilo,kila mtu alimzungumzia Hajrath.Umbo la msichana huyo halikuwa la kawaida,alikuwa ana umbo lililochongwa vizuri kabisa,sio hivyo tu.Hajrath alijaaliwa kuwa na miguu mizuri iliyojaa,jambo hilo alilijua, ndiyo maana muda wote alikuwa anavaa sketi, kama ikitokea kuvaa suruali basi ni mara chache.Urembo wake ulizidi kuwatingisha vijana wa mtaani,jambo lililokuwa linawaogopesha ni kitu kimoja tu,kaka yake!Hakutaka mdogo wake huyo,azoeane na mwanaume yoyote yule,kuna siku alishawahi kupigana na mangi wa dukani kisa tu,alikuwa akimuongelesha kwa muda mrefu,sio hivyo tu.Walishawahi kutukanana na madereva wa pikipiki Kimara Stop ova,kifupi Hussein alimchunga dada yake na alikuwa mkali kana kwamba angekuja kumuoa yeye vile.
“Mimi leo,akija namtemea cheche”
Jamaa mmoja alisikika akimwambia mwenzake kwa majigambo.
“J4,kila siku hivyohivyo.Huna lolote,huwezi kabisa.Domo zege wewe”
“Acha dharau”
“Dharau wapi,nakuchana ukweli.Hata Asha hivyo hivyo,mpaka Makundi akamgonga,ukabaki unalia lia kama zoba”
“Sasa subiri.Yule mtoto mimi namwaga sumu.Siku moja hiyohiyo namkaza”
Yalikuwa ni mabishano makali baina ya vijana hao wakiwa vijiweni,hakuna msichana waliyemzungumzia isipokuwa Hajrath tu!Mbali na kumfukuzia kote wakitumia mbinu mbalimbali lakini hakuna hata mmoja kati yao, aliyeambulia chochote,kuna wengine walidhani wenda msichana huyo anapenda pesa,wakaingia kwa gia hiyo ya kutumia mavumba lakini wapi.Wanaume wengine, wakadhani wenda anapenda magari, wakaanza kumpigia misele wakitumia magari ya kifahali lakini walichomolewa na kutolewa nje.Msimamo wa Hajrath ulikuwa palepale,hakutingishwa, kilichowapa moyo zaidi wanaume ni jinsi alivyokuwa anatabasamu muda wote hasa akiwa anatongozwa,hapo waliamini wenda majibu yatakuwa mazuri.
“Lakini nakupenda Hajrath,mbona unanitesa hivyo?”
Siku hiyo ilikuwa zamu ya David Mwasha,kuchombeza huyu aliingia kwa gia ya kutembelea makalio yaani,gari.
“Nilishakwambia siwezi”
Hajrath akajibu huku akitabasamu,hiyo ilimpa imani David, akidhani wenda baadaye atakubaliwa akiendelea kukaza!
“Jaribu kunifikiria,kwani una boyfriend?”
“BIG NO”
“Sasa kwanini usinikubalie,nimehangaika nawewe kwa muda mrefu sana.Nikubalie nikuoneshe jinsi navyokupenda”
“Ujue,wanaume mna maneno matamu sana!Wote ni walewale,ni waongo.Hivi David,unataka kuniambia kwamba wewe huna demu?”
Hajrath akajibu kwa umakini kisha kuanzisha hoja ya kumchomolea David,siku hiyo alikuwa ndani ya gari la David siti ya mbele,amepewa lift.Kumpakia Hajrath ndani ya gari lake, ilikuwa ni kama bahati ya mtende,akiamini tayari kasha mnasa mrembo huyo!
“Sina demu”
“Yaani huoni hata aibu,sio kweli David.Kwanini unakuwa muongo nipe simu yako”
“Ninaye, lakini it’s complicated”
“Unaona sasa,tulia naye.Nina amini anakupenda”
Hajrath akazungumza sentensi hizo,kisha kuteremka kutoka ndani ya gari akimuancha Bwana David, anakula kwa macho kwani makalio ya Hajrath yalikuwa yanatingishika,hamsini hamsini Mia!

*******
Hatimaye chuo cha Makumira kikawa kimefunguliwa rasmi,wanafunzi walianza kufika mmoja baada ya mwingine.Hajrath akarejea chuoni akiwa amenawiri kuliko kawaida,uzuri wake ukawaka!Rangi yake ikazidi kung’ara,hiyo ilifanya wanaume wa chuo waanze kum-mezea mate wakijaribu kwa mara nyingine kumtongoza, wakiingia kwa gia ya kumpa pole nyingi na zawadi!Lakini njama zao hazikuzaa matunda hata kidogo wote walitoswa,wiki ya kwanza ilivyopita marafiki zake wakawa wameripoti chuoni ili kuendelea na semista nyingine!Alichotaka kukifanya kwa wakati huo ni kukichimba kitabu tu,wala sio kuwaza mapenzi.
Japokuwa moyo wake aliuhisi tofauti kila alipokuwa anamuona Mwanaume anayeitwa Florian Fredrick,huyu alikuwa mwaka wa tatu!Kuna vitu alikuwa anavihisi ndani ya mtima wake,kila alipojitahidi kupambana na hali hiyo ilishindikana kabisa,akahisi kama anajitesa!Siku hiyo ilibidi amfate Amney na kumueleza kila kitu.
“Huna lolote,sema unampenda Florian”
Amney,akamchana na kumpa makavu.
“Mimi sijasema hivyo, moja kwa moja”
“Kama unampenda mwambie tu,unaogopa nini sasa?”
“Sasa nitaanzaje?”
“Utaanzaje vipi?Siku hizi haki sawa!Wanawake tunatongoza kama kawaida,mimi mbona nishawahi kutongoza”
“Mimi naona aibu,sijawahi kufanya hivyo”
“Aibuuu?Kama unaona aibu,basi”
“Kwani unanishauri nini?”
“Mfate umwambie”
“Sijui kutongoza sasa!”
“Kwani yeye keshawahi kukutongoza?”
“Hapana,hajawahi”
“Mmmh,jaribu bahati yako”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kuna mademu wanamshobokea hatarii,usifanye mchezo na macho ya Florian.Wewe umempendea nini?”
“Hata sielewi,nimejikuta tu”
Siku zote ndege mjanja,hunasa kwenye tundu bovu!Hatimaye Hajrath akawa amenasa kwenye ulimbo.Hakuelewa aanze wapi, kumfuata Florian ambaye siku zote alionekana yupo siriazi na kauzu,mbali na hapo alikuwa ni mwanaume mzuri,mrefu kiasi,mweupe wa rangi mwenye macho makubwa ya duara muda mwingi ndevu zake alikuwa anazichonga kwa staili ya O,kifua chake kilikuwa kimetanuka kidogo kama cha mtu anayefanya mazoezi,hakuwa ana shobo na mwanamke yoyote Yule, chuoni hapo,alikuwa mkimya na mtaratibu,hakuonekana mara kwa mara!Usipomkuta darasani anajisomea vitabu basi hostel anaangalia movie!
“Mambo kaka”Siku hiyo Hajrath,akaukata mshipa wa aibu na kumfuata Florian!Moyo wake ulikuwa ukipiga mara mia mbili kwa sekunde.
“Fresh”
Florian akajibu na kuendelea kutoa macho yake juu ya kitabu cha hadithi nje kilichoandikwa ‘BEDROOM PROFESSIONALS’ilielekea kilikuwa kizuri,ndiyo maana alikuwa bize, kufungua kurasa moja baada ya nyingine.
“Naona unasoma kitabu”
Hajrath akaanza kujiongelesha na kujichekesha mwenyewe!
“Ndio”
“Kinahusu nini kitabu hiko?”
“Mambo mengi sana!Hususani mapenzi na harakati za maisha”
“Mtunzi wa Kitabu anaitwa nani?”
“Emmanuel F.Kway”
“Yule wa Story za Kway?”
“Ndio”
Hajrath alijaribu kumzoea kwanza Florian, hakutaka kuingia kichwa kichwa alitaka jambo hilo alifanye,hatua moja kwa nyingine.Alichogundua ni kimoja tu,Florian anapenda kusoma vitabu vya hadithi zilizotungwa na Emmanuel F.Kway.Kazi yake ikawa ni kuzunguka kwenye maduka ya vitabu,akanunua kitabu kinachoitwa 'MY VIRGINITY'.
“Hakuna kingine kilichotungwa na huyo Emmanuel F.Kway?”
“Vipo dada”
“Nipatie”
“Kipi sasa?Vipo vingi”
“Kwani vipo vingapi?”
“Vile pale angalia, kuna On my wedidng day,Sex Slave,Mahaba niue,Mchachuko,Daphine,Ab..”
“Nipe hivyo viwili”
Vitabu vikafungwa akalipa pesa,akarudi hostel.Siku iliyofuata,akamkuta Florian kwenye bustani akiwa anajisomea masomo ya darasani.
“Nimekuletea vitabu vya kusoma”
Hajrath akasema baada ya kutoa salamu kisha kumkabidhi Florian mfuko,furaha aliyoionesha mwanaume huyo haikuwa ya kawaida.Huo ndio ukawa mwanzo wa wao kujuana,mazoea yakajenga tabia.Hajrath nayeye akaambukizwa tabia ya kusoma vitabu.
“Kwenye vitabu kuna maarifa mengi sana”
Siku hiyo Florian alianza kujieleza,hakuelewa ya kwamba Hajrath anafanya yote hayo kwa ajili ya kuzuga na amemzimia kinoma!
“Ni kweli,sasa kwanini unampenda huyu Kway?Kuna wengine wengi wakina Eric Shigongo,Eddy Msulwa”
“Ndiyo Eric Shigongo,anatunga vizuri Eddy naye balaa wote nawasoma.Lakini jamaa,anakuja kwa kasi sasa hivi”
“Sema tu umemzoea”
“Inawezekana,hilo nalo neno”
Wakati Florian anajielezea,mawazo ya Hajrath hayakuwa hapo hata kidogo!Alikuwa mbali maili nyingi kihisia,alimuona Florian nayeye wakiwa fukwe za bahari wanachezea maji,wanakimbizana huku na kule.Kifupi,alimpenda mwanaume huyo balaa,mpaka mwenyewe alijishangaa amekuwaje!
Siku zilizidi kwenda na aliweka kila mtego ili atongozwe na Florian lakini wapi mwanaume huyo akawa hana habari naye.Akaona isiwe tabu,akaamua kujitosa siku hiyo ili amueleze ukweli.
“Florian,nakupenda sana!Haijawahi kuwa hivi.Nakupenda,usinifikirie vibaya”
Mapigo ya moyo ya Hajrath siku hiyo yalienda resi mno!Baada ya kutamka maneno hayo,jambo hilo lilimfanya Florian amtizame kwa mshtuko wa waziwazi kwani hakutegemea kusikia sentensi hiyo kutoka kwa Hajrath.



Wahenga waliosema kila ndege hutua mti aupendao,walikuwa sahihi kabisa kwani moyo wa Hajrath ulitua kwa Folorian Fredrick, ukavuta kiti na kukaa kitako!Alitokea kupagawishwa sana na mtanashati huyo,kila kukicha alifanya jitihada mbalimbali za kumnasa akitumia gia nyingi tofauti tofuati za kujifanya anapenda kusoma vitabu vya hadithi,lakini hilo halikufua dafu.Akaona isiwe tabu,ni bora afunguke kuliko kubaki na dukuduku hilo moyoni, sababu aliogopa kupata kiungulia.Kwa tamaduni za ki –Afrika, mtoto wa kike, kutongoza lilikuwa ni jambo la ajabu sana,hilo Hajrath alilitambua lakini hakutaka kujali.Ilimradi tu,anausikiliza moyo wake unataka nini.Ndiyo maana, siku hiyo jioni akaukata mshipa wa aibu kichwani na kumtamkia Florian maneno hayo,mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu baada ya kusema kilichokuwa kinamtesa ndani ya mtima wake siku nyingi,akahisi kutetemeka na kuishiwa nguvu kabisa!
“Nakupenda Florian,nakupenda sana.Usinichukulie vibaya”
Japokuwa neno ‘nakupenda’ halikuwa swali lakini siku zote lilihitaji jibu na ndiyo hiko alichokuwa anataka Hajrath.
Florian aliganda kidogo,akabaki anamtizama msichana huyo mrembo,maneno hayo alishindwa kuyaelewa vizuri sababu alimchukulia msichana huyo siku zote kama mdogo wake ama dada yake tu.
“Hata mimi nakupenda mbona”
“Sio kama unavyofikiria”
“Kivipi Hajra?”
Florian alihitaji ufafanuzi kidogo ingawa tayari alianza kuhisi ni upendo gani Hajrath anauhitaji.Hapo ndipo Hajrath,akapata kazi nyingine ngumu ya kujielezea!Akasema kila kitu, tangu mara ya kwanza alivyomuona na kuamua kutumia gia zote ili kumsogeza karibu,jambo hilo lilimshtua mno Florian kwani hakutegemea hata siku moja kama Hajrath wakati wote huo alikuwa mwenye niya kama hiyo.Huo ndio ukawa mwanzo wa Hajrath kumsumbua Florian,hakukoma!
Aliendelea kumgasi akimtumia meseji mbalimbali za mahaba usiku na kumpa zawadi, kama maua na kadi za mapenzi!Hazikuisha siku nne,Florian na Hajrath wakajikuta ndani ya kisiwa cha malavidavi,hakuna siku ambayo Hajrarth alisisimka mwili kama hiyo,baada tu ya kupigwa denda kwa mara ya kwanza na Florian.Sio siri alihisi kama damu yake imeacha kutembea,mwili wake umepararaizi.
“Florian”
Hajrath akaita huku akiwa amelegeza macho yake.
“Again”(Tena)
“What baby?”(Nini mpenzi)
“Kiss me please”(Nibusu tafadhali)
Hajrath akafumba macho yake,Florian akasogeza mdomo karibu,midomo yao ikagusana.Hajrath akafumbua mdomo wake,ulimi wa Floria ukapenya ndani,wakaanza kunyonyana ndimi kama makinda ya ndege,baada ya hapo kila mtu akamtakia mwenzake usiku mwema!Hajrath alikuwa ana hali mbaya siku hiyo,macho yake yalikuwa mekundu mno!Alivyofika hostel,hakuweza kutulia damu yake ilimwenda mbio,mwili wake ulichemka ajabu.Akaelewa nini maana yake,hapohapo akachukuwa simu na kumtafuta Florian kwenye laini.
“Halloo baby”
Hajrath,akaongea kwa sauti ya huba.
“Yes Darling”
“I’m horny”(Midadi imenipanda)
“You know my room,don’t you?”(Unajua chumba changu,si ndio)
“Yes I do”(Ndio,nakijua)
“Come”(Njoo)
“I can’t baby”(Siwezi mpenzi)
“Why?”(Kwanini)
“I’m scared”(Naogopa)
Hajrath hakuwa tayari kusimama na kwenda chumba anacholala Florian kwani kilikuwa karibu na Chuo,aliogopa kuonekana na wanafunzi wenzake!Alichofanya ni kusimama na kumuomba wakutane kwenye moja ya nyumba za wageni, zilizokuwa mbali kidogo na chuoni.Jambo hilo likafanyika kwani usiku huohuo,Hajrath alipata chumba akalipia pesa zake za ‘pocketmoney’!Akawa anamsubiri Florian kwa hali na mali,damu yake ilizidi kumwenda resi, kadri sekunde zilivyozidi kwenda mbele.Kifupi alijishangaa mwenyewe kwani kwenye swala la kufanya ngono na mwanamme kwa mara ya kwanza ilikuwa ni vigumu kwake,akamkumbuka Ahmed alivyokuwa akimzungusha kwa takribani mwezi kasoro!Iweje Florian?Hata siku tano hazijapita!Jambo hilo likazidi kufanya ajuwe ni kweli amekufa na kuoza kabisa mazima kwa mwanaume huyo!
“Ngo! Ngo! Ngoo!”
Chumba cha mlango wake kilisikika kikigongwa,akakaa vizuri ili kusikilizia kama ni kweli ama ni chumba kinachofuata,lakini chumba hiko kiliendelea kugongwa akili yake ikahisi ni lazima atakuwa ni Florian tu!Damu yake ikazidi kwenda kasi zaidi!Akatoka kitandani na kwenda kufungua,ni kweli!Alikuwa ni kama ametabiri vile kwani mbele yake alisimama Florian.Akajikuta anajificha nyuma ya mlango bila kupenda, haikujulikana kama ni aibu za kikekike ama mapozi.Alichofanya Florian ni kufunga mlango na ufunguo,akamfuata hukohuko nyuma ya mlango!
“Vipi?”
Florian akauliza kwa mapozi huku akimtoa Hajrath mikono yake aliyoiweka machoni.
“Baby bwaaaaaana”
Hapohapo Florian,akamkumbatia kwa nguvu kwa kama sekunde tatu nzima!Alivyojitoa akamsogelea midomoni, wakaanza kunyonyana ndimi.Hapo ndipo Hajrath,hakujiweza tena akalegea kabisa!Akawa tayari amemuachia Florian afanye anavyotaka,hilo ndilo kosa alilolifanya kwani hakuelewa ni saa ngapi alitupwa juu ya kitanda,anavuliwa nguo moja baada ya nyingine.Florian,alikuwa ni mwanaume mjanja!Hakutaka kuharibu mechi hiyo ambayo kwake ndiyo ilikuwa ya kwanza kuicheza na mrembo huyo,ndiyo maana akaanza kumyonya Hajrath shingo,akapitisha ulimi wake ndani ya sikio la Hajrath,hakuishia hapo!Mkono wake mmoja ukawa unafanya kazi ya kutomasa Maziwa ya Hajrath taratibu,hapo ndipo binti huyu,akahisi roho yake inaacha mwili.Kila alipoguswa sehemu ya mwili wake,akahisi kupagawa mno.
“Aaaaah,ashiiiiii..Aaaaaah yeeees”
Haikujulikana kama ni sauti ya kuigiza ama amekolea kwelikweli kwani Hajrath aliyafumba macho yake na kuanza kuvuta vuta mashuka huku na kule,raha aliyohisi haikuwa na mfano wake kamili.Vidole vya Florian,vilipita taratibu juu ya tumbo lake mpaka kwenye kitovu mwishowe vikafika mpaka kwenye mapango,akapitisha mkono wake ndani ya chupi.Akagusa kinyama laini kabisa,hapo ndipo Hajrath mwenyewe akainua mgongo wake na kuanza kushusha sketi aliyovaa kwani alihisi kama Florian anapata tabu,alivyotoa sketi.Akashuka kidogo na kushusha chupi.Florian,akaishika akamsaidia kuivua yote!Chini akabaki mtupu,haraka akatolewa nguo ya juu.Hiyo haikumaanisha kwamba waanze kuvunja chaga!Florian akawa anaendelea kuuchezea mwili wa Hajrath kama ameutengeneza yeye,kwa wakati huo Hajrath alitamani mechi ianze kwani alikuwa keshalegea kabisa!Hajiwezi tena,akili yake haifanyi kazi kabisa,yupo dunia nyingine ya raha!Aliendelea kufanyiwa mchezo huo mpaka alivyohisi kuna vitu kama majimaji vinaanza kutoka kwenye ikulu yake.Florian alivyogusa alilitambua hilo pia,akajaribu tena kupima oil, hapo ndipo alipoona tayari mgodi umeanza kutema madini,alichofanya ni kuipanua miguu ya Hajrath huku na kule.Akatoa nguo zake kwa kasi ya umeme na kushika muwa wake vizuri,uliokuwa mkubwa na mnene kama muhogo!Akaushika vizuri na kuutumbukiza ndani ya ikulu taratibu mno!Raha alizokuwa anahisi Hajrath,zilizidi kipimo kuna wakati alitamani kupiga kelele,hasa alivyobinuliwa na kuwekwa mbuzi kagoma kwenda majanini!Mtanange wa mechi hiyo ulidumu kwa takribani masaa mawili,ndipo walipopumzika.Kila mmoja,akiwa amemlalia mwenzake.Kilichofuata hapo ni kupeana maneno matamu,huo ndiyo ukawa mwanzo wa Hajrath kufungua moyo wake na kupenda kwa mara nyingine!

***********
Mapenzi ya Hajath na Florian,yaling’ara!Mwanzo ilikuwa ni siri lakini siku zote hakuna siri ya watu wawili,kila kitu kikawa wazi.Habari hizo zikavuma kwa kasi ya kimbunga.Kila mtu chuoni hapo, akawa anajua Hajrath na Florian ni mtu na mpenzi wake.Ingawa swala hilo lilikuwa ni kawaida chuoni hapo lakini wapenzi hao walitia fora,kwanza walipendezana!Cha pili walikuwa kama watoto mapacha,ukimuona Hajrath juwa basi Florian yupo pembeni kama sio mita moja!Waliongozana kama kumbikumbi.Kusoma walikuwa wote,kantini walikula pamoja.Hata wakati mwingine walitumia shuka na kitanda kimoja usiku.Hajrath aliogopa tena kufanya penzi hilo liwe siri,hakutaka kurudia kosa la mara ya kwanza,ndiyo maana alijiachia popote.Hiyo ilifanya mpaka asahau kama kuna mwanaume ama binadamu anayeitwa Ahmed.
“Yaani pale,umepoteza demu kaka”
Siku hiyo Ahmed aliambiwa kwani habari za Hajrath na Florian,alizisikia tu.Aliumia moyo lakini hakutaka kulionesha jambo hilo waziwazi,akajifanya kila kitu kipo kawaida lakini haikuwa hivyo kwani alichomwa ndani kwa ndani.
“Huna stori nyingine za kupiga?”
“Nakwambia ukweli,Yule manzii alikupenda ile kinyamaaa yaaani”
“Ndio,kila kitu kina wakati wake.Mwache mshkaji atambe!Ndio muda wake huu,ukifika wa mtu mwingine,ataachwa”
“Hivi unadhani,Florian ataachia lile goma kizembee.Unaota chalii angu”
Jamaa huyo,aliendelea kuongea maneno ya kuudhi mbele ya Ahmed na alizungumza kwa rafudhi ya kwao,Arusha!
“Time will tell”
“Aaah waaapi.Yule demu ngoja nikwambiee ukwelii aiseee!Uliponzwa na Marehemuu Geboo,Yule chalii kazi yake ilikuwa ndio hiyo kuharibu”
“Jembe,tuachane na hizo habari.Leo Manchester wanacheza!Tunaenda kucheki gemu wapi?”
Ahmed akajaribu kuizima mada lakini haikuwa kazi rahisi.
“Nachokwambia chaliii,Hajrath ni demuuu.Ebu kwanza vuta picha ile shepuu yake!Hivi ushawahi kumgonga yuleee?”
“Ndioo”
“Acha uwongoo,wewe hujawahi kuonja.Sasa hivi,Florian anafaidi ile kinyama”
“Oyaaaaaa,acha basi.Za wapi hizooo”
Ilibidi Ahmed,amnyamazishe kwa hasira za waziwazi tena kwa sauti.Mtima wake ulichoma mno!Alivyosimama hapo,hakugeuka nyuma.Akanyoosha mpaka Ngurelo getoni kwake.Huko alijitupa kitandani na kubaki akitafakari,sura ya Hajrath ikamjia kichwani.Habari zake na Florian,zikamtia wivu na kumchanganya akili,akajaribu kulala lakini wapi,usingizi ukawa ni kitu hadimu kupatikana.Hakujua ni kitu gani akifanye,japokuwa siku hiyo kulikuwa na mpira na aliipenda sana timu ya Manchester lakini hakujisikia kwenda,sababu alijua kabisa angejifosi tu wala asinge 'enjoy' kama siku zote!Hapohapo kuna wazo likamjia la ghafla,japokuwa hakuwa ana uhakika kama jambo analotaka kulifanya litazaa matunda kama mwanaume mtu mzima kama yeye,akachukuwa simu yake na kumtafuta hewani rafiki yake wa mwaka wa kwanza anayeitwa, Gipson Paul.
“Oyaa Gipson,shwari?”
“Shwari broo,niambie kiongozi”
“Una namba za Florian?”
“Florian yupi?Basket baller?”
“Sijui.Lakini Florian Fredrick”
“Anhaaa,yes ninazo broo.Unahitaji?”
“Ndio”
“Unataka ukamzingue nini kaka?”
Historia ya Hajrath na Ahmed,haikuwa siri chuoni hapo.Ilitapakaa kila kona, hivyo walijua sana kwa wakati huo Florian,ana mahusiano ya mapenzi na Hajrath!Wengine swala hilo walilibeza,kuna waliosema Ahmed kapokonywa tonge mdomoni,kila mtu akaongea lake.Kuna baadhi walienda mbali zaidi na kutengeneza timu!Wengine wakawa 'Team' Ahmed wengine 'team' Florian ikawa kama ligi ya mpira!Maneno ya chinichini yakatengenezwa na kusababisha bifu zito kati ya Ahmed na Florian Fredrick.Ndiyo maana Gipson Paul akahoji!
“Hapana,ili iweje?Nipe bwana,nitumie sasa hivi”
“Poa,simu yangu haina bando.Nipe dakika moja,nikanunue kifurushi”
“Si unitumie kwenye meseji za kawaida”
“Naenda kununua vocha”
“Poa,usisahau”
“Aminia,mshefa”
“Mia”
Dakika mbili baadaye,Ahmed akawa amepata namba za Florian,alivyosevu jina lake likatokeza WatsApp, moyo ulimuuma ajabu baada ya kuona ‘DP’ kuna sura ya Hajrath,yupo kwenye tabasamu, mbaya zaidi ameegamia kifua cha Florian,alitamani aipasue simu.

*******
Maisha ya Hajrath hayakutofautishwa na mtu aliyekuwa paradiso,Florian alimpa kila hitaji la moyo wake!Akamdekeza kama mtoto mdogo,akamtunza kama yai na kumlinda kama mboni ya jicho lake.Sio siri, katika wanaume ambao aliowahi kuwa nao katika mahusiano ya kimapenzi,hawakumfikia Florian hata robo,ilikuwa ni tofauti kama alivyodhani hapo awali akidhani wenda wanaume wote ni walewale,pata potea!
Muda wote Hajrath alitabasamu,akasahau yote ya nyuma.Mapendo ya Florian yakafuta makovu yote moyoni,mtima wake ukajawa na furaha!Sio yeye tu,hata marafiki zake Amney na Mpangw’a walikuwa wenye furaha pia.Ilikuwa ni lazima Florian akimuita sehemu Hajrath basi ni lazima Amney na Mpangw’a watakuwepo.Siku hiyo Florian,akaamua kuwatoa wote na kuwapeleka kwenye moja ya mgahawa mkubwa sana jijini hapo Arusha,akafanya kufuru kwa kuwalisha wote, wakatoshekwa na vyakula vingine wakabeba!
“Baby,hope ume enjoy?”
Florian akamuuliza mpenzi wake huku akimpangusa shavuni, ambapo kulikuwa na kipande cha nyama kimebaki.
“Thanks baby”(Ahsante mpenzi)
Haikuwa ahsante ya kawaida,bila aibu yoyote akasogea karibu na Florian,akamnyonya mdomo na kulana denda mbele ya kina Amney,tukio hilo lilifanya kila mtu aangalie chini,haikujulikana kama ilikuwa aibu ama haya, kwao!
“Nakupenda Hajrath”
“Mimi pia baby”
“Sasa,Amney!Tutaonana kesho chuo,njoeni nje niwakodie taxi mrudi hostel”
Matukio aliyokuwa anafanya Florian yaliwafanya marafiki zake na Hajrath,wamkubali sana!Kila sehemu waliyopita walimsifia.Hakuna msichana yoyote aliyemsogelea Florian kumtongoza kwani kesho yake angechambwa na kuogeshwa mvua za matusi na Amney kama sio Mpangw’a,ndiyo maana walimuheshimu Florian.Chuo kizima Hajrath na Florian walizungumziwa wakawa 'topic'.Siku hiyo baada ya Amney na Mpangw’a kukodiwa taxi ili warejee hostel!
Florian na Hajrath wakatafuta 'hotel' kubwa ya nyota tano,hiyo ilifanya Hajrath azidi kushangazwa na mapendo hayo.Kitu kilichokuwa kinamsumbua ni kimoja tu,ni wapi Florian anatoa pesa?Jambo hilo alitamani kumuuliza lakini hakutaka kufanya hivyo kwani haukuwa muda wake!

*****
Laiti kama angekuwa gari angemgonga Florian barabarani, amuue.Hakuna siku aliyojisikia uchungu kama siku hiyo kantini, alivyokuwa anakula chakula cha mchana,Hajrath alifika akiwa ameambatana na Florian,mbaya zaidi walikuwa wanacheka kimahaba!Akajifanya kuangalia chini ili kukwepa aibu,lakini hiyo haikusaidia sababu walikaa mbele yake.Ilikuwa ni wazi kabisa hawakumuona!Lakini yeye alilitafsiri tukio hilo kama kejeli na dharau na kuamini kwamba wanataka kumuumiza rohoo!
“Sasa baby,ndio kesho tunaenda!Si uliniambia hivyo?”
“Yeah,sijasahau.Kumbe wewe ni mzuri sana,sikuwa najua una macho mazuri”
“Kama yako,usiniangalie hivyo naona aibu baby”
“You are beautiful”(Wewe ni mrembo)
Maneno hayo yalisikika kutokea meza ya mbele yake,Florian na Hajrath walikuwa wakizungumza kimahaba!Moyo wa Ahmed uliuma ajabu,kilichomuumiza zaidi ni namna ambavyo Florian alivyopendeza!Mwenye mwili wa mazoezi,mrefu kwenda hewani.Kwa harakaharaka alimzidi kwa kila kitu,kuna jambo alilitafsiri,ya kwamba Hajrath alikuwa ana mchit na Florian kipindi wapo pamoja,haikuwezekana hata kidogo mapenzi yao yakolee namna hiyo, kwa muda mfupi!
Wivu ukachanganyika na hasira,akasimama wima kama mkuki na kuanza kutembea,akaivuka meza waliyokaa Hajrath na Florian,alivyopiga hatua nyingine saba.Akasimama na kugeuka,akarudi mpaka kwenye meza hiyo!Akawatizama kwa zamu!
“Nilijua tu”
Jambo hilo,lilimshtua Hajrath.Hakumuelewa Ahmed,anataka nini japokuwa ujio wake mahali hapo,ulimfanya ashtuke kidogo! Ingawa hakutaka kulionesha jambo hilo waziwazi,kwa nyodo na dharau,akampandisha juu mpaka chini na kumshusha kama mara tatu.Akabaki kimya na kumtizama mpenzi wake Florian, aliyekuwa mbele yake.
“Hajrath,yaani wewe wa kunifanyia mimi hivi?”
Ahmed,akauliza swali lililokosa majibu.Wakati huo Florian,alibaki kimya hakutaka kuongea chochote, kama mwanaume mwenye akili timamu na mwenye busara,hakutakiwa kutia neno sababu tu alijua historia kati ya watu hao wawili.
“Baby ngoja niwapishe”
Florian,akasimama ili awaachie faragha Ahmed na Hajrath.Alifanya hivyo kwa moyo mkunjufu kabisa na kusimama lakini Hajrath, akamshika mkono.
“Hapana,usiondoke baby”
Hajrath akasema nayeye akasimama wima!Akamsogelea karibu mpaka mdomoni,akatoa ulimi wake na kuanza kumnyonya denda Florian, mbele ya Ahmed!




Lilikuwa ni pigo lingine kubwa kuliko yote kwa Ahmed,kitendo hiko kilifanywa kwa kukusudiwa na Hajrath ili tu aache kumgasi na kumsumbua.Ndiyo maana, akafanya jambo hilo mbele yake,hakuishia hapo. Aliendelea kumnyonya ndimi Florian,akajitoa kidogo huku akirembua macho yake.
“Nakupenda Florian,nakupenda sana Mme wangu”
Maneno hayo alisema kwa sauti,akihakikisha kwamba yanamfikia Ahmed bila chenga!Adhma yake ilitimia sababu Ahmed alisikia na Moyo wake ukachoma kama pasi ya mkaa,akaumia kuliko kawaida.Akatamani kutupa ngumi lakini akashindwa sababu mwili wa Florian ulikuwa mkubwa,akaogopa kudhalilika mchana kweupe.Kilichokuwa kinaendelea ungesimuliwa ungedhani wenda ni mkanda wa sinema ama hadithi za kuandika lakini kila kitu kilichotokea kilikuwa halisi,sababu ndani ya kantini hiyo kuna wanafunzi walikuwepo na walishuhudia picha zima,kila mtu alijua kabisa kitakachotokea mbeleni kisingekuwa kitu kizuri kwani fahali wawili walikuwa wamekutana ndani ya zizi moja.
“Embu cheki.Wanavyopigana denda,kama ulaya vile!Maskini Ahmed”
Minong’ono ya chini kwa chini ilisikika,kila mtu akawa anasubiri misumbwi ama ugomvi utakaoanzishwa na Ahmed lakini matokeo yake,walimshuhudia anaondoka zake kutoka nje ya kantini.Umbali kutoka Kantini mpaka stendi ya mabasi siku hiyo kwake ilikuwa ni sawa na safari ya Dar es Salaam mpaka Kigoma,mwisho wa reli.Alijisikia aibu mno,akatamani ardhi ipasuke atumbukie ndani imfunike,kila mtu alimshangaa yeye,Ahmed alihisi kudhalilika kwa kitendo alichofanyiwa mbele ya kadamnasi,kila mtu aliyemwangalia akadhani wenda anamcheka yeye.Hakuwa ana raha hata kidogo!Picha ya Hajrath akimpiga denda Florian, ndiyo iliyopita kichwani,akavuka barabara upande wa pili, bila kuangalia magari,hiyo ilifanya akoswe koswe kugongwa.
Siku hiyo, hakutaka kuchukua daladala,aliona kama atachelewa kufika!Akatafuta pikipiki, ambayo ilimpeleka mpaka geto lake,Ngurelo!Huko akajitupa kitandani na kuanza kutafakari upya.
“Haiwezekani,lazima namimi niwaoneshe kazi.Mimi sio boya namna hiyo!Hajra hawezi kunidhalilisha kiasi hicho, nitamfunza adabu”
Alijisemea Ahmed akiwa kama mwenye kitu hatari anataka kukifanya,hakueleweka moja kwa moja kama anataka kulipa kisasi Kwa Hajrath ama anataka kumvimbia Florian.

*******
Swala la Hajrath kunyonyana ndimi na Florian,hadharani likageuka na kuwa kichwa cha habari ndani ya chuo cha Makumira.Kila mtu alilizugumzia kwa jinsi alivyolielewa,kama kawaida ya wabongo kila mtu ataongea la kwake.Penzi la Hajrath na Florian likazidi kupeta,wakawa maarufu ghafla.Hiyo ikapelekea mpaka wabatizwe majina Jay- z na Beyonce!Yaani Florian ni Jay- z,Hajrath ni Beyonce.Licha ya penzi lao kutingisha chuoni hapo na kuzungumziwa lakini wanaume hawakuacha kumpigia misele Hajrath, wakimtongoza na kutaka kuonja penzi lake,hawakujali kama yupo na Florian.Hiyo ni kawaida ya wanaume kwani walitaka kujua ni kitu gani haswa anapata Florian,mpaka akanasa kama gundi kwa Hajrath.
“Mike,si nilishakwambia.I have a boyfriend na ninampenda”
Huyo aliitwa Michael Mzuva,mwanaume aliyekuwa king’ang’anizi kuliko wote,siku hiyo ilikuwa ni zaidi ya mara kumi kuambiwa kitu hikohiko kimoja,hakukata tamaa hata kidogo, aliendelea kujipigia debe,akiamini ipo siku moja Hajrath angekuja kuwa wake,hata kama angeshea penzi na Florian, hakujali ilimradi tu,ampate msichana huyo mrembo sana!
“Hata mimi nina haki ya kukupenda ujue”
“Najua,lakini mimi sikupendi”
“Kwanini sasa?”
“Mbona unataka turudie tena mambo yale yale kama watoto,nitamwambia Florian ujue”
“Haaa! Unadhani namwogopa,mwambie tena itakuwa vizuri,ajue”
“Hivi wewe una wazimu?”
“Ndio,nina wazimu wa kukupenda Hajra”
“Niache nifanye course work”
“Leta nikusaidie”
“Ahsante,nitafanya mwenyewe”
Michael Mzuva,akapigwa cha mbavu lakini hakukoma,alizidi kumgasi Hajrath,hakuwa muelewa hata kidogo!Sio hivyo tu,wanaume wafanyabiashara walipishana na magari ya kifahari kutaka japo kulala naye usiku mmoja kwa kutangaza madau ya pesa lakini pesa zikaonekana sio kitu kabisa.
“Sawa,ahsante.Mimi sio Malaya,naomba uondoke”
“Unakataa,laki nne!Kwa usiku mmoja!Hutaki kulala maskini na kuamka tajiri?”
“Nimekwambia,sijiuzi”
“Sijasema hivyo Mrembo.Basi naweka laki tano,usiku mmoja tu.Hata kama usipoisha”
Thamani ya mwili wake ulikuwa ni zaidi ya pesa,hata kama angepewa nyingi kiasi gani, asingekubali kuvua nguo yake ya ndani na kupanua miguu,hakuwa tayari kuufanya mwili wake biashara.Hakuna kitu kinachomkera kama mwanaume kuingia na gia hiyo!
“Hivi,unanichukuliaje?”
Hajrath akamtupia Mzee huyo swali kwa ukali.
“Una maana gani?”
“Achana namimi.Tena unikome”
Hajrath akasimama na kurudi chuoni ambapo huko alinyoosha mpaka maktaba ili afanye kazi za chuo!Sio wanafunzi na wafanyabiashara peke yao, ambao walimtamani kingono mpaka walimu wanaomfundisha darasani,kuna wengine waliingia kwa gia ya kutaka kumpa alama nyingi lakini walitolewa nje!Kuna wengine walimuongezea max kwenye ‘coursework’ kisha baadaye kumuita ofisini lakini hao pia walipigwa vibuti,msichana huyu hakuwa wa kawaida!Bado alizidi kuonesha msimamo wake,uleule!Hakutetereshwa,alimpenda sana Florian, hakuwa tayari kumsaliti hata kidogo,aliridhika na kila kitu alichopewa!
“Umekula?”
“Hapana”
“Kwanini sasa?”
“Bado nasoma”
“Nenda ukale kwanza,utapata ulcers!”
“Nitakula tu”
“Nakuomba,au nije kukuchukuwa nikupeleke twende wote?”
“Hapana Ahsante,nitaenda tu”
“Fanya hivyo sasa hivi”
Mwanaume huyo alisikika upande wa pili simuni akimsihii Hajrath,huyu aliitwa Idris Hante,mwanafunzi wa mwaka wa tatu.Mmoja kati ya wanaume waliomsumbua ni huyo,lakini ilikuwa ni tofauti kwa wengine kwani Idris alikuwa wa kipekee kabisa,alikuwa ni mwanaume mcheshi, anayemjali kuliko kawaida.Mbali na hapo, alikuwa ana sauti nzuri yenye swaga,alimpagawisha zaidi anapotumia lugha ya kiingereza.Ungesikiliza sauti yake bila kumuona ungedhani wenda ni Mmarekani kumbe alikuwa ni Mtanzania,tena mpogoro!Idris alimfukuzia Hajrath kwa kipindi cha muda mrefu sana,jambo hilo lilimshangaza hata yeye kwani haikuwahi kutokea tangu aanze kutongoza wasichana!Ki ukweli, Moyo wa Hajrath ulihisi tofauti kabisa akiwa anazungumza na Idris,ndiyo maana alimsikiliza mwanaume huyo akatii amri zake.Hapohapo akasimama na kuelekea kantini huko alikula kisha kurudi tena maktaba kwa ajili ya kujisomea.
Licha ya kutengeneza ukaribu na Idris Hante lakini pia aliendelea kumpenda mpenzi wake Florian kuliko kawaida,walitembea pamoja na kwenda kumbi za starehe wote.Hiyo ilimfanya Hajrath ajihisi kama malaika wa peponi.Hazikupita hata siku saba bila ya wao kufanya tendo la kuzini,hilo lilizidi kumpagawisha zaidi Hajrath.Lakini kitu kilichokuwa kinamsumbua kichwa ni wapi Florian anatoa pesa nyingi za matumizi kama hizo,kila alipopanga siku ya kumuuliza alisahau na kushindwa kwani alivyomuona tu,aliishiwa pozi na mada zilizoongelewa zilikuwa ni mapenzi peke yake!Katika kudadisi sana akaja kugundua kwamba ana dada yake yupo nchini Marekani na huyo ndiye anafanya kila kitu,alikuwa akimtumia dolla kila baada ya wiki kuisha.
“Leo tena naenda westen Union,sista kanitumia pesa”
Hapo ndipo alipotegua kitendawili kilichomtesa siku nyingi!Kuanzia siku hiyo wakawa wanaongozana wote mpaka ofisi za Westen Union, kuchota pesa na ilikuwa ni lazima baada ya hapo,waende kujivinjari kwa kutumia pesa!Wakati yeye Hajrath anakula bata na kufanya matanuzi akiwa na asali wake wa moyo, huku nyuma Ahmed alikuwa anapambana na hali yake,moyo wake ukashindwa kusukuma damu ukapata kazi nyingine mbadala ya kusukuma penzi la Hajrath,kichwani alimuwaza Hajrath!Akawa kama teja aliyepata arosto,anazungumza mwenyewe.Jambo hilo kwa mara ya kwanza lilianza kama masihara lakini baadaye likaanza kuwa sugu,Ahmed wakati mwingine alizungumza mwenyewe!Na katikati ya maneno yake,alitaja jina Hajrath.
Kifupi akawa kama amepagawa fulani,kitu kilichowa staajabisha wenzake ni kitendo cha yeye kuanza kunywa pombe kali, kila siku iendayo kwa Mungu!
“Nipe pombe kali”
Siku hiyo alimwambia muhudumu wa baa,baada tu ya kuketi kitini.
“Pombe kali,zipo nyingi kaka.Unahitaji ipi?”
“Kali kuliko zote”
“Sawa”
Muhudumu,alivyoenda!Akafika na chupa kubwa ya Jack Daniels.Ahmed,akaitizama na kumuangalia muhudumu huyo, aliyevalia sketi fupi,anavutia mapaja yake yapo nje!Akabaki anamtizama na kumsindikiza kwa macho!Baada ya hapo,akamimina pombe kwenye glasi na kuanza kunywa,akiamini kwamba angetoa mawazo na 'stress'za mapenzi.Kila alivyokunywa pombe wivu ulizidi kumkaba kohoni.Akamkumbuka rafiki yake, Gabriel ambaye kwa wakati huo alikuwa tayari ametangulia mbele za haki,ghafla sura ya Necka Golden ikampitia kichwani,akahisi uchungu ajabu!Saa moja na nusu,ilimkuta akiwa eneo hilo la ‘Grocery’ analewa pombe,sambamba na chupa yake ya Jack Daniels, iliyokuwa ya pili tayari.Kichwa chake kilikuwa kizito,anahisi kizunguzungu kikali,ni wazi kabisa alijua kwamba hayupo vizuri na tayari pombe ipo kichwani.
Alivyoangalia pembeni,akamuona muhudumu aliyekuwa ana muhudumia yupo kandokando ya meza iliyokuwa pembeni yake.
“Psii psiiiiii”
Akamuita kwa staili na kupiga kimluzi na kunyoosha mkono hewani,alivyofika kwenye meza yake,akaanza kumuuliza maswali ya hapa na pale.Macho yake akiwa ameyatupa kifuani kwa muudumu na mara kadhaa, aliyashusha mpaka kwenye mapaja yaliyokuwa nje,akahisi kama jogoo wake anaanza kutuna.
“Umesema unaitwa naniiiiiii?”
“Eva”
Dada huyo,akajibu kwa mapozi.
“Nahitajiii tuooondoke wote leooo,tweendee getoo languuu.Tukazunguuumze vizurii nitaongea na bosiii wakoo”
“Sasa hivi ni muda wa kazi”
“At what timeee,unamalizaaaa?”
“Saa sita”
“Kwahiyo,nikusubiriiiii hapaaa?”
“Poa”
Pombe zilikuwa kichwani,zikaamsha na mengine.Akili yake ikahama,kichwa kingine kidogo ndio kilikuwa kinamuongoza,akawa yupo tayari asubiri mpaka usiku wa saa sita aondoke na muhudumu anayeitwa Eva,akalale naye!Kilichozidi kumuumiza moyo ni jinsi ambavyo Eve alikuwa akitolewa macho,hakupita meza tatu bila kuitwa na kutongozwa!
Saa 5;52 Usiku,akatembea kaunta na kumfuata Eva ili ajue jinsi watakavyoondoka wote!
“Kwani umejipangaje kaka?”
Eva,akauliza wakiwa wamesimama karibu na kaunta!
“Mimii ninaa pesaa bwanaaa,twende basiiii”
“Una shilingi ngapi?”
“Kumi na taanoooo”
“Kumi na tano?!Achana namimi”
“Twentiiiii”
“Ongeza hapo,tumalizane hapahapa”
Ahmed,midadi ilimpanda!Hakuwa yeye,pombe na akili za ngono zilimsukuma afanye anachotaka kukifanya kwa wakati huo,akabadilika kabisa!Akaingiza mkono mfukoni na kutoa noti ya shilingi elfu kumi.
“Shika hii,tukimaliza nakumaaliziaaaaa..Njoo basiii”
“Ongeza elfu tano”
“Nitakumaliziiaa, don’t woriiiiiii”
Siku hiyo hakutofautishwa na mtu anayenunua changudoa barabarani,biashara hiyo ya magendo ikaanza kufanyika eneo hilo bila mtu yoyote kugundua.Walivyofikia muafaka.Eva akaongoza upande wa choo cha kike,akageuka na kumpa ishara Ahmed,amfuate!Kama kondoo,anayeenda machinjioni.Akamfuata nyuma,walivyofika eneo hilo akamkuta Eveline,ameshika ukuta,ameinama kidogo sketi yake tayari ipo miguuni, ameishusha.Bila kuuliza Ahmed,akavua mkanda na kushusha suruali yake chini,akasogea karibu na kutoa muwa wake,akaishika miguu ya Eva vizuri na kuingiza tango ndani ya ikulu.Mechi ya siku hiyo,haikuhitaji refalii,ilikuwa ni bunda siliga.
“Maalizaaa basiiiiiiiii,harakaaa…aaa”
Eveline alilalamika kwani alikuwa kimaslai zaidi, hiyo ilifanya Ahmed,azidi kufanya tendo hilo kwa kasi mno!Huku mikono yake ikiwa imeshika kiuno cha Eveline,anafanya makamuzi.Ndani ya dakika kadhaa,akamwaga oil chafu lakini kabla ya kumaliza vizuri akasukumizwa,mbaya zaidi ndio alikuwa kwenye utamu.
“Wewe kaka vipi?Mambo hayo peleka kwa mkeo”
Eva,akaongea kwa hasira za waziwazi,kitendo cha kutaka kumwagiwa oil chafu, ndani ya ikulu kilimkera.
“Aaaah,umenikataaa stimuuuu”
“Nimalizie pesa yangu,niondoke”
Swala hilo,likaonekana kuwa gumu kidogo!Ahmed,akapandisha suruali yake vizuri akafunga mkanda,bila kujibu akawa anaondoka lakini alishikwa mkono.
“Nipe pesa yangu basi”
“Pesaaa gani?Achanaa na miiimiiii.Unanijuuaaa mimi weweee”
“Wewee kaka,nimalizie pesa yangu”
Ghafla,ukaibuka ubishani mkali baina ya Ahmed na Eveline,mhudumu wa baa hiyo,Ahmed akawa mbishi kumalizia salio lililobaki,Eveline akaanza kupayuka kwa sauti.Kwa nguvu za ajabu akamvuta Ahmed kwa ndani,akajishika kifuani!Kwa kuwa shati lake lilikuwa na vifungo ilikuwa ni rahisi kuvikata,kwa mara ya kwanza Ahmed hakuelewa nini maana ya tukio hilo.
“Ananibakaaaaaaaa,nisaidieniiiii”
Eveline,akaachia ukelele mkali wa sauti huku akimvuta Ahmed kwa nguvu upande wake,kutokana na kulewa pombe nyingi hakuwa mwenye nguvu za kujitetea akamdondokea Eveline kwa juu!Kilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua,haikujulikana watu walitokea wapi kwani walimgombania Ahmed kama mpira wa kona,wanaume wawili wakaingia ndani karibu na chooni,wakamshika Ahmed.Mmoja bila kuuliza akamtandika kibao cha mdomo,mwingine akamshushia ngumi kali ya tumbo.Kuna mwingine ndiyo kabisa,akaokota gongo kubwa la mti na kumpiga nalo Ahmed kichwani,puuu!



Mapenzi ya Hajrath na Florian,hayakutofautishwa na watoto mapacha!Ilikuwa ni kama wamezaliwa tumbo moja vile,mbali na hapo walikuwa ni marafiki wakubwa.Jambo la Hajrath lilikuwa la Florian na shida ya Florian ilikuwa ni lazima Hajrath aitambue zaidi na hayo, walikuwa wasiri katika shida zao, hawakuwa tayari kuyaanika matatizo yao kwa watu wengine, waliogopa vidudu mtu ambao wangetumia mwanya huo kutafuta sababu ama kuwagombanisha,hiyo ilifanya penzi lao lizidi kupasua miyamba.Kila mmoja alimuona mwenzake ni mpya!Kila Florian alipokutana na marafiki zake hakusita kuwaambia ‘Huyu anaitwa Hajrath,ni mke wangu’Alkadhalika kwa Hajrath,hiyo ilifanya kila mmoja wao ajisikie amani na furaha.Katika maisha siku zote, wanaopenda ufurahi ni wachache kuliko wanaopenda ufanikiwe,hivyo ndivyo ilivyokuwa hata kwa Hajrath na Florian.Wanafunzi wakaanza kuwapiga majungu na kuweka fitna ili penzi lao lichache waachane,lakini hawakufanikiwa kwani walikuwa wanatwanga maji kwenye kinu,yasagike.
“Florian hakufai,ana tamaa sana!Usimuamini shoga”
Siku hiyo Hajrath alikuwa akilishwa sumu ya maneno na mmoja wa wanafunzi wa Makumira,jambo hilo kwake akalitafsiri kama majungu.Akamtizama msichana huyo mdogo aliyefunga safari yake kuja kumueleza jambo la kipuuzi kama hilo.
“Ahsante,hauna kitu kingine cha kuongeza?”
“Sio hivyo da Hajra,nakwambia ukweli”
“Ili iweje?Nimuache au?”
“Hapana,sina maana hiyo”
“Basi niache na Florian wangu,ahsante kwa ushauri”
Wasichana mbalimbali waliofika kwa gia hiyo,aliwakata ndimi na kuwatoa dima.Tabia hiyo iliendelea lakini mwishowe,ikafika tamati.Sio siri, tangu walipoanza uhusiano na Florian miezi kadhaa iliyopita,Hajrath hakuwahi kuumizwa na mapenzi kama inavyotokea kwa rafiki zake,wakati wenzake walikuwa wanalalamika kunyanyaswa na kutendwa kwenye mapenzi kila kukicha yeye alikuwa anazidi kunawiri kadri siku zinavyozidi kwenda mbele.
Ilifika kipindi alifika mbali zaidi na kusema wanaume wote ni Malaya isipokuwa Florian Fredrick tu,peke yake!Japokuwa walifahamiana kwa kipindi cha muda mfupi lakini alikuwa ana kila sababu ya kusema hayo kwani alikuwa ana ushuhuda wa kuzungumza anayoyasema,ndani ya muda mfupi Florian, alimuonesha mapenzi mazito.Wakati mwigine alijilaumu ni kwanini hakujuana mapema na Florian!
“Hivi,kwanini hatukujuana mapema Darling?”
Hajrath akatupa swali siku hiyo usiku wakiwa ndani ya taxi, wanatoka kula chakula cha usiku kwenye moja ya hotel kubwa jijini hapo Arusha,alikuwa ana kila sababu ya kuuliza kitu kama hiko!
“Kwanini umeuliza hivyo baby?”
Florian akajibu kwa swali.
“Nakupenda sana Florian,naomba usiniache!Ukiniacha wewe,nitaamini wanaume wote ni sawa!Nakupenda,sijui kwanini sikukujua mapema”
“Kila kitu kina wakati wake Mke wangu”
Florian alipenda kumuita Hajrath ‘mke wangu,’japokuwa hawakufunga ndoa!
“Ni kweli love”
Hapohapo Hajrath akasogea karibu na mdomo wa Hajrath,akambusu mdomoni kisha kumlalia kifuani,dereva taxi kupitia kioo cha katikati aliliona tukio hilo sababu aliwaona abiria wake aliowapakia wakiwa nyuma!Safari ilizidi kuendelea lakini kabla hawajafika Hajrath aliomba gari lisimamishwe ili akatoe haja ndogo kwani alikuwa amebanwa na mkojo.
“Baby,tunakaribia kufika lakini”
“Hapana mkojo umenibana sana naomba nika susu”
“Okay, Chif Paki hapo mbele dakika moja”
Dereva akatii amri,akaweka gari kando karibu na baa moja wapo.Hajrath na Florian wakateremka!
“Mimi nakusubiri”
Florian,akakaa kwenye moja ya viti vya ‘Grocery’ waliyokuwa wameingia ili Hajrath aende kutoa haja ndogo,akawa anamsindikiza kwa macho!Jambo lililomfanya aangalie kando ni baada ya kuona wanaume na wateja mbalimbali wa ‘Grocery’ hiyo wanasimama na kuelekea upande wa chooni.Kabla ya Hajrath kufika msalani,alikumbana na lundo la watu walioweka duara,wengine walikuwa na magongo mikononi,vurugu ilikuwa kubwa!Akaogopa mpaka kuingia bafuni kujisaidia,neno alilosikia ni ‘Mbakaji’hakutaka kuuliza!Akaangalia mkusanyiko wa watu,Hajrath hakuwa mwenye tabia ya kuingilia mambo ya watu hususani vurugu kama hizo,lakini siku hiyo kuna kitu kilimwambia aende kutizama.Hapohapo,akapangua watu wawili watatu na kuchungulia.Moyo wake ukapiga kwa nguvu,hakuwa ana uhahika kama mwanaume aliyemuona ni Ahmed ama amem-fananisha!Ingawa alikuwa anavuja damu usoni lakini aliweza kumtambua,moyo ukamuuma ajabu!Kwa kasi ya mwewe akatoka mbio mpaka kwa Florian na kumvuta kwa nguvu,hakutaka kujua Florian angemfikiria vipi lakini alichotaka kukifanya ni kuyaokoa maisha ya Ahmed, kutoka mikononi mwa raia wenye hasira kali!
“Kuna niniii?”
Florian,ilibidi ahoji.Namna alivyovutwa, ilimuogopesha,ndiyo maana akauliza.
“Florian,please njoo.Ahmeeed anakufa”
“Unasemaje?Mbona sikuelewi yuko wapi?”
Kwa Hajrath,hakuwa ana uhakika asilimia mia moja kama jaribio lake lingefanikiwa kwani Ahmed na Florian walikuwa ni mafahari wawili, ambao hata siku moja wasingeweza kukaa zizi moja!
“Njoo,Florian ni huku”
Hajrath alirusha mikono huku na kule,huku akipiga piga miguu chini.Alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa!Florian,akasogea karibu mpaka kwenye kundi la watu lililokusanyika,akawapangua watu na kuingia kati.Hata yeye alivyomuona Ahmed amekaa chini anavuja damu nyingi,alipigwa na bumbuazi.Hakutaka kuuliza mara mbilimbili,akaingia kati kabisa na kusimama mbele yake na kuanza kuwasukumiza watu waliokuwa wanamgombania kama mpira wa kona!
“Oya kaa kandoo chariii,nitakupigaa betoo aisee!”
Pande moja la mtu,likampiga mkwara Florian kwa rafudhi ya kingarenaro.
“Hapana,hamuwezi kumpiga!Nipigeni mimi kwanza huyu namfahamu”
Florian alizungumza kwa kujiamini huku akiwatizama wananchi hawa wenye hasira kali, dhidi ya mbakaji Ahmed,hata yeye alikuwa mwenye hofu lakini hakutaka kulionesha jambo hilo waziwazi!Ndiyo maana alipiga mkwara mzito,Hajrath alikuwa pembeni, anashuhudia kila kitu,Ahmed alikuwa chini anahema na mwenye wasiwasi mwingi kama mtu mzima anayeoga nje!
“Nimesema hivi,kaeni kando.Kafanya nini kwani?”
Florian akataka kujua,ndipo kila mtu akasema kwamba alitaka kubaka!Kwa Florian hakutaka kushtuka moja kwa moja,hiyo ndiyo ilikuwa sifa kubwa ya mwanaume huyo,ilikuwa ni lazima kwanza atulize gasia hiyo kubwa ndipo mambo mengine yaendelee!Hapo ndipo mwanamke aliyekuwa anapiga kelele za kubakwa,akaitwa kando!
“Nataka kuongea na huyu dada,kaka kwani wewe ndio umebakwa?”
Florian,akamwambia jamaa mmoja ambaye alionekana ni mtata kuliko wote!
“Usinijibu hivyo,sawa?”
“Unataka nikujibu vipi sasa?Pisha mbele yangu.Nahitaji kuongea na aliyebakwa kama ndio wewe twende”
“Unasema nini wewe boyaa”
Florian,akasukumizwa lakini nayeye hakukubali akamkuda jamaa huyo shati na kumvuta kwa nguvu,jambo hilo lilimfanya Hajrath, amfate Florian kwa kasi na kumshika mkono!
“Baby please don’t!Nakuomba”
Kufuatia hapo,Florian akawa mdogo kwani alimsikiliza mpenzi wake Hajrath!Wakamchukua Ahmed na kumpeleka mpaka kwenye taxi,katika kumdadisi mwanamke huyo, ikagundulika kuwa hakutaka kubakwa bali kuna biashara ya ngono alikuwa anataka kufanya na Ahmed,alichofanya Florian ni kuzama mfukoni,akatoa noti nne za shilingi elfu kumi, tano.Kifupi ilikuwa ni shilingi elfu hamsini za kitanzania.Alivyorudi ndani ya taxi akamuamuru Dereva apeleke gari hospitali ya karibu.Hicho ndicho kilichotokea usiku huo lakini walivyofika hospitalini, walikataa kutoa matibabu kwani ilihitajika PF3 kutoka kituo cha polisi.
“Sawa,Hajrath.Wacha nikashughulikie PF3”
“Twende wote”
“Okay”
Harakaharaka wakaanza safari ya kuelekea kituo cha polisi kilichokuwa karibu,hapo walihojiwa maswali mawili matatu!Florian alivyoona analetewa gozigozi, ilibidi ajiongeze ili Ahmed,apatiwe karatasi hiyo maalum kwa haraka.Hapo ndipo, alipoifinyanga noti ya shilingi elfu kumi na kumkabidhi Afande mkononi bila wenzake kuona tukio hilo!
“Ulisema alifanya nini?Kavamiwa na wezi?”
“Ndio afande”
“Sawa,subiri hapo”
Pesa ikawa imepeleka mambo mbiombio,ndani ya sekunde mbili wakawa na karatasi mkononi,kwa kasi wakarudi hospitali.Wakati hayo yanatokea,Hajrath alikuwa anafikiria vitu vingi sana kichwani kwake,haikuwezekana hata kidogo kwa binadamu wa kawaida kufanya kitu kama hicho!Historia ya Ahmed na Florian ilikuwa ni mbaya na wasingeweza kupikika ndani ya chungu kimoja hasirani,lakini kwa Florian ilikuwa ni kinyume chake!
“Florian”
Hajrath aliita kwa sauti ya chini wakiwa katika hekaheka za kumtafuta daktari ili ampatie matibabu Ahmed.
“Yes”
“Thank you”(Ahsante)
“Not now”(Sio sasa hivi)
Siku hiyo Florian,alikesha hospitali akipambana na madaktari ili kuhakikisha hali ya Ahmed inarudi kwenye mstari,ilibidi tofauti zao aziweke kwanza kando!Siku hiyo,hawakuweza kumshona Ahmed kwani alitumia kiasi kikubwa cha pombe,japokuwa Florian aliwasihi madaktari watumie njia nyingine lakini hilo, halikuwezekana.
“Kamata hii basi,mtibu kaka yangu”
Florian,alijaribu kumpitishia Dokta noti ya shilingi elfu kumi ili kumlainisha.
“Hata ungenipa milioni kumi.Siwezi kukudanganya,kwa sasa hivi labda tutumie njia nyingine!Lakini sidhani kama nitafanikiwa wacha nijaribu”
Siku hiyo, Hajrath alilengwa na machozi,upendo aliouonesha Florian ulizidi kipimo chake!Shukrani alizompa hazikuweza kuelezeka kiwepesi.

Hatimaye kulikucha,pombe ndani ya mwili wa Ahmed iliisha.Hapo aliingizwa ndani ya chumba maalum,akashonwa kichwani nyuzi saba!Na matibabu yote yalitoka mfukoni mwa Florian,masaa matano baadaye akawa yupo kwenye hali yake ya kawaida!Kitu cha kwanza kukikumbuka ni raia wenye hasira mbaya, waliotaka kumuua na ilikuwa wazi kabisa asilimia mia moja,bila ya Florian kutokea na kumkingia kifua wenda zingekuwa ni habari nyingine nzito.Hivyo hakuwa ana hiyana, ilibidi amshukuru Florian.
“Umeyaokoa maisha yangu”
Ahmed,alisema siku hiyo baada ya Florian kutokeza wodini,kabla ya kujibu chochote Hajrath akawa amefika tayari.
“Usinishukuru Mimi,mshukuru Hajra”
Hivyo ndivyo Ahmed alivyofanya baada ya kupewa maelezo hayo,akatoa shukrani nyingi zisizokuwa na mwisho na Florian alihitimisha kuwa deni la hospitali tayari amelipa hivyo,anaondoka!Akatoa pole nyingi na kuondoka zake.

******

Ahmed,hakuwa mwenye kidonda kikubwa sana kiasi kwamba angeweza kuambiwa akae hospitali kwa siku mbili,ndiyo maana siku hiyo jioni yake akaruhusiwa huku akipewa dawa za maumivu ambazo zingemsaidia mbele ya safari, lakini walimsisitiza sana asitumie pombe kwani waliamini kwamba mgonjwa huyo alikuwa chapombe sababu tu,aliletwa hospitalini hapo akiwa amelewa hilo halikuwa tatizo hata kidogo.Alivyorudi kwake Ngurelo,alikitizama chumba chake!Hakuamini kwamba asingekiona tena,bado picha ya kupigwa na magongo ilimjia kichwani,akapitiliza mpaka mbele ya kioo kikubwa kilichosimama akajitizama,bandeji iliyokuwa kichwani kwake,ilimuogopesha mno!Na kichwa chake kilikuwa kinamuuma kupindukia,aliamini fika nyuzi alizoshonwa zinavuta.Akatembea mpaka jikoni akatafuta maji ya kunywa ili ameze dawa,akafanikiwa na baada ya hapo aliingia chumbani kwake,akajifungia na kulala!

Siku zilizidi kukatika na kusonga mbele kwa kasi ya ajabu!Kila aliyemuuliza Ahmed chanzo cha yeye kushonwa hakupewa jibu lililojitosheleza.
“Nilivamiwa na wezi,Usiku.Wakanipiga sana”
Hilo ndilo lilikuwa jibu la Ahmed siku zote,hakuwa tayari kutamka ukweli.Ilikuwa ni aibu kwake, kuweka mambo hadharani,cha ajabu na kilichomshangaza ni siri yake hiyo kutokuvuja!Siku zote,aliwahofia Hajrath na Florian kwani ndio hao peke yao waliojua ukweli wote wa yeye kutaka kumnunua bahamedi muuza pombe, matokeo yake akashindwa kumlipa pesa zake.Kifupi Hajrath na Florian,hawakutaka kumwaga mchele kwenye kuku wengi,waliendelea kumtunzia siri hiyo nzito Ahmed na hakuna mwanafunzi yoyote Yule aliyejuwa kwamba Florian ndiye aliyemkingia kifua Ahmed,hivyo ndivyo ilivyokuwa!
Maisha ya Ahmed tangu anusurike kupondwa na magongo baada ya kusingiziwa tukio la ubakaji,aliamua kubadili mfumo mzima wa maisha yake!Ilikuwa ni kama akili zake zimerudi na kukaa sawa,alivyokumbuka amebakisha semista moja ili ahitimishe masomo yake ya chuo kikuu.Ilimfanya awe bize na masomo,akajikita kwenye kitabu.Hakutaka kujihusisha tena kwenye swala zima la mapenzi, akakichimba kitabu kuliko kawaida,akawa mwenye usongo wa kupata alama za juu ikiwezekana ‘1st class’ kwa matokeo hayo aliamini angepata kazi nzuri na baadaye angekuwa ana maisha mazuri ambayo kila siku alikuwa anayaota kuyapata,hiyo ndiyo ahadi aliyojiwekea.Akasoma zaidi,matokeo ya ‘test’ yalivyotoka akawa amepata alama za juu,hiyo ilimpa moyo!Akazidi kukichimba kitabu zaidi,taratibu akaanza kumsahau Hajrath!Lakini siku moja akiwa jioni,ametoka kujisomea.Ghafla ujumbe ukaingia kwenye simu yake,juu ilikuwa namba ngeni.
‘Hi Ahmed,Mimi Hajrath.Usiku mwema,Love you’
Ulikuwa ni ujumbe,uliosomeka juu ya kioo cha simu yake, bado hakutaka kuyapa nafasi mawazo yake kwamba Hajrath,ndiye alituma meseji hiyo.Alikuwa ana kila sababu ya kuitupilia mbali meseji hiyo kwani alijua fika penzi la Hajrath na Florian ni sawa na kambale na tope!


Japokuwa alimuonesha mapenzi yote Florian na kumfanyia kila kitu ili ampe furaha lakini mawazo yake hayakuwa hapo hata kidogo,yalikuwa mbali maili mia moja!Alikuwa akimuwaza Ahmed tu,hospitalini kama ni mzima.Hakuacha kumuombea kimoyomoyo kwa Mungu wake ili apone haraka.Hakuelewa ni kwanini anamuwaza, wakati nafsi yake ilimchukia vibaya sana kwa matendo ya kinyama aliyomfanyia.Licha ya kujificha lakini Florian aligundua mabadiliko ya mpenzi wake,alipojaribu kumuuliza kulikoni alimpiga piga chenga na kuibua mada nyingine ilimradi tu,Florian asimfikirie vibaya!
“Naona haupo sawa”
Florian alisema siku hiyo wakiwa chumbani wamelala kitandani,Hajrath amempa mgongo anaangalia ukutani,wakati haikuwa kawaida yake hata kidogo.
“Baby,kuna course work naomba unisaidie”
“Ipi?”
Hajrath akaweka kanga yake vizuri kisha kusimama,jinsi alivyotembea hakutofautishwa na garika.Chumba kizima kilitetemeka,Moyo wa Florian ukaanza kumtetema!Akamuangalia Hajrath,akazidi kumshangaa jinsi alivyobinuka kwa nyuma kama kichuguu na ilikuwa ni lazima akitembea nyuma atingishike,mbaya zaidi siku hiyo, alivaa kanga moja!Japokuwa ndege alikuwa wake lakini siku hiyo Florian alijikuta anatumia manati kumuwinda.Kabla ya Hajrath kulifikia kabati ili atoe begi,Flaorian akafika kwa nyuma yake,haikujulikana kitandani ametoka saa ngapi,alichofanya yeye ni kuipitisha mikono yake kiunoni mwa Hajrath,ikatokea kwa mbele.Akanyonya Shingo,hapo Hajrath aliruka kwani alihisi kuna vitu vinatembea kwenye damu,ukizingatia siku hiyo kulikuwa na hali ya ubaridi fulani.Ndizi ya Florian taratibu ikaanza kusimama,hiyo ilifanya Hajrath ahisi kuna kitu kigumu kinamgusa!Akajua nini maana yake,maruani yake yakampanda.
“Beibiiiiiii”
Hajrath,akaita kwa sauti ya huba huku akigeuka nyuma,wakatizamana!Mwenyewe kama kondoo anayepelekwa machinjioni,akamsogelea Florian midomoni wakaanza kulana denda,mambo yakaanzia hapo kwani walitupana kitandani na kuanza kunyonyana ndimi huku wakishikana huku na kule!Uzuri kila mtu,alikuwa anajua ni wapi udhaifu wa mwenzake ulipo,hivyo ilikuwa ni rahisi sana kuchezeana!Hakuna siku Hajrath aliyopagawa kama hiyo,kitendo cha miguu yake kushikwa huku na kule kisha Florian kutoa ulimi wake na kuanza kudeki bahari,kilimpagawisha sio kitoto.Ndio maana akaanza kuhema juujuu huku akiwa amekishika kichwa cha Florian,ili asiache mchezo huo uliokuwa mtamu kuliko asali.Raha alizohisi hazikuwa na kipimo chake,Florian aliligundua hilo ndiyo maana akaongeza njonjo na madoido yote,kila ufundi aliutumia siku hiyo ili arudishe akili ya Hajrath kama kawaida,alivyohisi kama kuna vitu vinateleza.Hapohapo akaanza kuseti mitambo,akachukua mguu mmoja wa Hajrath wa kulia,akauweka begani kwake kisha kutumbukiza mashine kwenye mgodi ili uchimbaji uanze.
“Aaaaah aaaah aashiiii aaaah aaaa bebiiii,ilove youuu”
Hajrath alikuwa akiguna akiwa sikioni kwa Florian aliyekuwa juu yake yupo hoi,nayeye hakutaka kuwa gogo!Akaanza kukizungusha kiuno chake ingawa hakuelewa kama anapatia ama anabolonga kwani michezo ya mapenzi, alikuwa bado ni lena.Kitendo cha Miguu yake kuwekwa begani ndipo alipopagawa zaidi,Florian siku hiyo alijitahidi zaidi kunogesha mechi,akawa anatia mbwembwe nyingi ili mradi tu ampagawishe mpenzi wake.
“Aaahmee..d aaaahmed aaaaah aaaaaah”
Hakuwa ana uhakika kama alimsikia Hajrath vibaya ama ndio utamu kunoga, kwani katikati ya mchezo huo usiohitaji hasira Hajrath alianza kutaja majina yasiyoeleweka,lakini hiyo haikumfanya Florian asitishe mechi hiyo kwani alikuwa yupo karibu na goli,kilichobaki kwake yeye ni kupiga shuti kali mpaka nyavuni.Kwake kelele hizo zilikuwa kama za chura ambazo zisingeweza kumzuia tembo kunywa maji,ndio maana akampindua Hajrath na kupiga shuti kali la ajabu mpaka nyavuni,kisha hapohapo akalala kifuani kwa Hajrath.Alivyotuliza akili,akakumbuka jinsi Hajrath alivyokuwa analitaja jina ‘Ahmed’,akamezea kwanza na kuliweka kiporo!

********
Hakuelewa kama amerogwa ama ni pepo linamsumbua,Hajrath aliteseka na kulia na moyo wake!Tangu Ahmed apigwe na wananchi wenye hasira kali,mawazo yote yakahama!Akawa anatamani kumuona japo kwa sekunde moja tu,hiyo iliharibu mfumo wake mzima wa kufikiria,akawa anajisikia kukaa peke yake, apambane na hali hiyo.Mbali na hapo, alitaka kufanya juu chini ili Florian asije kugundua tatizo lake sababu aliamini kivyovyote vile ni lazima penzi lao lingeyumba kama sio mkataba wao wa mapenzi kuvunjika kabisa.
Siku moja akiwa peke yake akamkumbuka rafiki yake, Amney!Akajua huyo angekuwa suluisho la jambo hilo linalomtatiza kichwani,hapohapo akampigia simu.
“Njoo huku Garden,Amney”
Hajrath aliweka ‘heaphone’ masikioni, simu yake ipo juu mezani,anazungumza kupitia ‘headphone’ zake.
“Garden ipi?”
“Huku karibu na kantini”
“Sasa hivi?”
“Ndio,njoo sasa hivi”
“Poa,ngoja nimalizie kufanya hii research kidogo”
“Sawa,nakusubiri”
“Poa poa”
Dakika tisa baadaye,Amney alikuwa ametanda mbele yake!Akaketi pembeni ya rafiki yake kipenzi ili kusikiliza wito.
“Ushamaliza Couser work ya Mkude?”
“Bado”
“Kwanini sasa?”
“Florian,ananifanyia”
“Vipi,upo sawa?”
Amney,alikuwa ana kila sababu ya kuuliza,jinsi Hajrath alivyokaa ilimtia mashaka kidogo.Hakuwa yule ambaye anatabasamu kila wakati.
“Hapana”
“Nini tena?Florian kakufanya nini?”
“Hajanifanya kitu”
“Kumbe je?Unaumwa?”
“Hapana”
“Una shida gani sasa?”
“Ahmed”
Kufuatia jina hilo kutajwa,Amney akashusha pumzi nzito!Akamtizama rafiki yake kwa macho fulani ya mshangao unaotaka kujua kitu.
“Ahmed?Kafanya nini?”
“Ananitesa”
“Ebu,fafanua vizuri.Unanishangaza ujue”
Ilikuwa ni lazima siku hiyo,atoboe siri.Kila ilivyokuwa na tangu walivyomkuta Ahmed akiwa anashambuliwa kama mpira wa kona,hakuacha chochote nyuma kila kitu alikiweka bayana kwa Amney,alivyohitimisha akamtizama.
“Ahmed,alitaka kununua dada poa?”
Amney,akahoji!
“Hapana ni bahamedi wa baa”
“Ndio ni dada poa”
“Hapana,Amney.Usiseme hivyo!Jambo hilo lilinishtua sana”
“Achana naye,kwani si amepona?”
“Sina uhakika”
“Kwani hata akiwa sawa,akiumwa.Wewe inakuhusu nini?Umesahau alichokufanyia?”
“Sijasahau,lakini moyo unaniuma”
“Achana naye,Florian anakupenda!Anayekupenda,mpende.Shauri yako”
“Naelewa na keshaanza kuhisi”
“Hatari hiyo,jitahidi usimuwaze kabisa”
“Sawa,una namba zake?”
“Namba za nani?”
“Ahmed”
“Wewe za niniii?”
“Nina shida nazo tu”
“Mmmmh,sina uhakika kama ninazo!Ngoja niangalie”
Amney,akaanza kupekua simu yake kwenye majina, hatimaye akazipata hiyo ilikuwa ni bahati ya mtende kwa Hajrath.
“Naomba”
Kilichofuata hapo ni Hajrath kuzisevu namba za Ahmed.
********
Siku zilizidi kukimbia kwa kasi ya ajabu,test mbalimbali zilianza kufanyika na hiyo iliwafanya wanafunzi wawe ‘bize’, hawakwenda tena disco kama walivyozoea,kila mwanafunzi alijifungia chumbani kwake kujisomea,wenye tabia ya kuandika nondo ili wazitumie kwenye 'test' huo ndio ulikuwa wakati wao!
“Nabulele,mzigo wote huo!Hilo karatasi sasa utaliweka wapi?”
Jamaa mmoja,alikuwa akiandika kwenye karatasi,huyu aliitwa Nabulele!Chuo kizima walimtambua kwa tabia yake ya kuingia kwenye chumba cha mtihani na chabo na hata siku moja hakuwahi kukamatwa,walioiga waliishia kufumwa na kuchaniwa mitihani huku wengine wakiambiwa warudie semista,lakini ilikuwa ni tofauti kwa Nabulele, wengi walidhani anatumia kizizi cha bibi yake kwani hakuna mwalimu yoyote aliyewahi kumfuma,ndiyo maana siku hiyo alikuwa yupo bize kuandika ‘topic’ nzima kwenye karatasi hiyo ndogo!Alivyomaliza akamtizama rafiki yake.
“Yaani hii,naifinyanga naiweka huku.Hii ni power bank”
Nabulele akasema na kujitapa akiwaambia rafiki zake huku akionesha sehemu zake za siri,kumaanisha kwamba ataficha humo.
“Leo ndio unakamatwa”
“Bora punda afe,lakini mzigo ufike.Naenda kukaa karibu na Ahmed,nikiona gozigozi!Namuita anisaidie maana jamaa kichwa sana.Katika maisha lazima uwe na plan B bwana,sio unakaa kindezi”
Kweli,siku ya siku ilivyofika Nabulele alizama kwenye pepa,pembeni yake aliketi Ahmed ambaye muda wote alikuwa bize anajaza karatasi!Siku hiyo nusu chuo walikuwa wamegongana kufanya mtihani huo mmoja,ndiyo maana hata Hajrath pamoja na Florian, walikuwa ndani ya chumba hikohiko kimoja cha test!Mawazo ya Hajrath yote,yaliangukia kwa Ahmed aliyekuwa bize na kalamu yake anaandika, kila wakati alimpiga jicho,kwa Ahmed mtihani ulikuwa ni mrahisi mno!Alikuwa ni kama yeye vile ameitunga 'test' hiyo kwani alikuwa wa kwanza kumaliza.Jambo hilo, lilifanya macho ya wanafunzi wote yawe kwake.
“Write your index number”
Msimamizi wa mtihani,alimwambia Ahmed.Hapo ndipo alipogundua kuwa hakuandika namba ya jaribio hilo,akasogea mpaka pembeni ambapo kulikuwa na meza,bila kujua kwamba meza hiyo alikuwa Hajrath!Bila kupoteza muda,akaandika kwa haraka na kukabidhi karatasi huku nyuma akimuacha Hajrath,anamsindikiza kwa macho, jambo lililomkumbusha mbali ni marashi ya Ahmed,hakuelewa pia jambo hilo lilishuhudiwa na Florian, aliyekuwa kona ya kushoto!

*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG