Search This Blog

Saturday, February 6, 2021

RISE UP SEHEMU YA 1/10

 


RISE UP

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 1 KATI YA 10



Umasikini! Sio neno geni kabisa katika masikio ya watu wengi hususani katika nchi yetu hii ya Tanzania. Kila kukicha uta sikia watu wakilalama kwamba hali ni ngumu au kwa lugha ninyingine ni kwamba vyuma vimekaza. Ni kweli mimi ni mmoja wapo ambaye nina andamwa na upemi hadi kwenye mifuko yangu. Maisha ninayo ishi mimi, mke wangu, mwanangu pamaoja na mama yangu yote hutegemea ajira yangu ya ulinzi katika hii kampuni ya QX Security. Sio kazi yenye hata marupurupu ni kazi ambayo ina nifanya nizidi kuwa nauhasama na wauza maduka wa mtaani kwetu kwa maana kwa jinsi ninavyo kopa ime fikia wakati hata baadhi ya njia zenye maduka ninayo daiwa nime acha kuzipita na kama ni kizipita basi ni usiku sana muda ambao wauza maduka hao wana kuwa tayari wamesha funga maduka yao. Nikaanza kuitazama bunduki aina ya gobore niliyo ishika mkononi mwangu, bunduki ambayo ina ingia risasi moja tu na tume zibeba kama ushahidi kwa maana mimi toka niajiriwe kwenye kampuni hii ni mwaka wa tano sasa, sija wahi kuitumia kabisa kumlenga hata paka.

Nikatazama ukimya ulio tulia kwenye mtaa huu wenye maduka makubwa ya wahindi huku pembezoni kukiwa na benk kubwa ambayo walinzi wake ni askari wa FFU, ambao wezetu hawa wame jaaliwa kukabidhiwa bunduki za kisasa aina ya SMG.

‘Ngoja nijipumzishe kidogo’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitafuta moja ya kijieneo ambacho kime jificha kidogo, nikaiweka bunduki yangu pembeni kisha taratibu nika ishusha kofia yangu na kuufunika uso wangu na kuanza kuutafuta usingizi unao ninyemelea nyemelea, huku walinzi wezangu wa kampuni hii ninayo ifanyia kazi, wakiwa katika maduka mwengine. Hazikupita hata dakika ishirini, nikasikia mlio wa risasi aina ya SMG, ulio nifanya nikurupuke kwenye usingizi huo na kitu cha kwanza kukishika ni bunduki yangu. Mapigo ya moyo yakazidi kunidunda kwa spidi ambayo sio ya kawaida, kwa maana toka nianze kazi yangu ya ulinzi sikuwahi kukumbana na kisanga kama hichi. Risasi zikaanza kumimika katika mtaa huu wenye maduka yanayo tazamana. Nikachungulia kidogo na kuwaona askari polisi wawili wakiwa wamelala chini huku wakiwa wametulia tulia, ikiashiria kwamba wamesha tandikwa risasi na kufa. Nikaona watu kumi walio valia maksi kwenye nyuso zao huku wakiwa na nguo nyeusi wakiwamalizia kuwapiga risasi askari hao wawili walio lala chini. Walinzi wezangu wengine watatu nao nikawaona wakichapwa risasi huku wanaume hao wakisambaa mtaa huu wenye maduka tu. Wanaume wawili wenye bunduki kubwa zenye kutumia mikanda ya risasi, wakasimama mwanzo wa mtaa huu huku wengine wakisimama mwisho wa mtaa huu ambapo kuna jia ya kutokea kwenye mtaa huu. Kiufupi wame ufunga mtaa.

Jasho jingi likazidi kunimwagika huku nikiwa sielewi nini cha kufanya. Bunduki yangu kwa kweli haina ubora kabisa wa kupambana na majambazi ambao wana onekana wamejizatiti kwenye kila nyanja, kwani hata gari walizo kuja nazo sio vijigari mchwara ila ni Range Rover nne ambazo zote ni nyeusi. Majambazi kadhaa wakaingia benk huku wengine wakifungua duka moja baada ya jengine na mbaya zaidi katika mtaa huu maduka makubwa yana uza simu za kifahari pamoja na vito vya dhahabu kama cheni, saa, mikufu na kadhalika.

‘Allah nisaidie mimi’

Nilizungumza huku nikiendelea kujibaza kwenye kijipenyo hichi ambacho kime tenganisha kati ya duka moja na duka jengine na ni eneo dogo sana ambalo endapo wakipita na kutupia macho yao upande wangu basi wana weza kuniona. Nikahisi haja ndogo ikinilenga lenga kwa maana kuna mmoja wao ambaye ameshika tochi kubwa ameanza kumulika eneo moja baada ya jengine huku mkononi mwake akiwa ameshika mtutu wa bundiki wa maana.

‘Ehee mwenyezi Mungu, nikifa mimi ni nani ambaye ata ilea familia yangu’

Nilisali kimoyo moyo huku nikilia kwa uchungu sana.

‘Oya tayari tuondokeni’

Ilisikika sauti ya mmoja wao na kumfanya jamaa huyo ambaye amebakisha hatua kadhaa kunifikia, kughairi na kuingia kwenye moja ya gari na wakaondoka eneo hilo kwa mwendo wa kasi sana. Taratibu nikapata ujasiri wa kutoka eneo hilo, nikapita kwenye moja ya fremu ambayo wana uza vito vya thahabu, nikaona baadhi ya mikufu ya dhahabu kadhaa ikiwa ime angushwa chini. Kwa haraka nikaingia ndani ya duka hilo nika kusanya mifuku iliyo salia na nikaondoka eneo hili huku kikatiza mtaa huu kwa mwendo wa kasi sana huku bunduki yangu nikiwa nime iacha kwenye kiji eneo nilicho kuwa nime jibanza.

Nikafika katika nyumba yetu ambayo ndio nina ishi na familia yangu. Kitu cha kwanza kukifikiria ni wapi ambapo nita ficha cheni hizi ambazo ni za garama kubwa sana na kama nikifanikiwa kuziuza kwa baadhi ya masonara basi nita pata fedha. Nikazunguka hadi kwenye moja ya mti wa mmbilimbi ambao upo karibu kabisa na choo chetu cha nje. Nikachukua moja ya kipande cha mti na kufukua kwa haraka kijishomo ambacho nilipo weza kujiridhisha nika zifunga kwenye kitambaa changu kisha nikaziweka huku nikiangalia pande zote na kugundua kwamba hakuna mtu anaye niona. Nikazifukia vizuri kisha nikasimama huku nikiwaza ni nini nifanye.

Nafsi moja ina nishinikiza niweze kurudi eneo la tukio huku nafsi ngingine ikinishinikiza niweze kulala ndani.

“Rashidi”

Niliisikia sauti ya mama ikitokea chumbani kwake kwa maana chumba chake kina tazamana na eneo hili la uwani mwa nyumba yetu.

“Ndio mama”

“Ni wewe?”

“Ndio”

“Mbona upo hapa saa hizi ume toka kazini?”

“Ahaaaa……”

Nilishindwa kumjibu mama jibu la kueleweka kwa maana sio kawaida yangu mimi kurudi usiku kama huu wa leo. Mama akafungua mlango wa uwani na akatoka nje.

“Vipi mbona usiku huu”

Mama yangu alizungumza huku akiwa ameshika taa ya kuchaji kwa maana nyumbani kwetu hapa hakuna umeme.

“Tuta zungumza mama”

Nilizunhgumza huku nikiingia ndani na kumuacha mama akinitazama kwa mshangao. Nikasimama mlangoni mwangu, nika taka kugonga mlango ila nika sita kidogo mara ya kuuona mlango wa chumba changu ukiwa wazi kidogo. Nikausukuma na kuingia ndani, nikatoa simu yangu ya yenye kitochi na kumulika ndani hapa na kumkuta mwanangu mwenye miaka miwili akiwa amelala peke yake pasipo mama yake. Ika nibidi nitoke nje huku nikiwa na maswali mengi.

“Mama, mke wangu yupo wapi?”

“Mama Shamsa mbona ame lala humo ndani?”

“Hayupo mama?”

“Mmmm!!”

Ikamlazimu mama yangu kuingia ndani na kweli akajidhihirishia kwa macho yake kwamba mke wangu hayupo.

“Sasa ata kua amekwenda wapi?”

Mama aliniuliza huku akinitazama usoni.

“Sifahamu, nikuulize wewe?”

“Mimi sijui kwa maana nililala toka saa mbili usiku”

Nikapiga hatua hadi mlango wa mbele na kukuta ukiwa ume egeshwa, ina maana kwamba mke wangu alitoka na kuugesha mlango huu. Wasiwasi ukazidi kunijaa kwa maana sijui mke wangu ame kwenda wapi au ame kumbwa na jambo gani.

“Mpigie simu yake?”

Mama alizungumza na kweli nika mpigia simu yake, ikaanza kuita na baada ya kupiga mara mbili mfululizo ika pokelewa.

“Niambie mume wangu”

Mke wangu alizungumza kama mtu ambaye ame toka usingizini, kutokana nime weka loud speaker ika tubidi mimi na mama kutazamana.

“Vipi ume lala?”

“Ndio mume wangu, usingizi ulikuwa ume nipitia. Vipi mbona saa hizi ume piga simu kwema huko kazini?”

Mimi na mama ikatubidi tuzidi kujawa na mshangao. Ikanibidi kurudi chumbani kwangu kudhibitisha kwamba kweli mke wangu hayupo au ni wenge langu.

“Nime taka kukujulia hali tu mke wangu, vipi mama na mtoto wame lala vizuri?”

Niliuliza huku maumivu ya wivu wa mapenzi yakinitawala moyoni mwangu.

“Ndio, mwanao nime lala naye hapa pembeni ame nikumbatia mume wangu. Natamani unge kuwepo na kunikumbatia muda huu”

Maneno ya mke wangu yalizidi kunikasirisha. Mama akaanza kutingisha kichwa na kunisikitikia kwa maana mke wangu anacho kizungumza ni uongo kwa maana mtoto anaye mzungumzi ame muacha hapa na amelala peke yake.

“Ahaa sawa usiku mwema”

“Na wewe pia mume wangu, nina kupenda mwaaa”

Nikajikuta nikikata simu huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Kwa kweli, kati ya watu nilio kuwa nina waamini ni mke wangu. Sikuwahi kufikiria siku hata moja kama ana weza kunisaliti kwa namna yoyote ile.

“Ina maana mkwe wangu ana chepuka?”

Mama aliniuliza huku akionyesha kujawa na huzuni kubwa sana. Sikumjibu chochote mama zaidi ya kumsogelea mwanangu na kukaa pembeni ya kitanda.

“Mama”

“Bee mwanangu”

“Kazini tume vamiwa na majambazi. Walinzi wezangu pamoja na askari wawili wame uwawa kwa risasi”

Mama akastuka sana huku akinitazama usoni.

“Hawajakuumiza?”

“Hapana nilikuwa nime jificha mama”

“Ohoo Mungu wangu, sasa ita kuwaje?”

“Nime kimbia kuokoa maisha yangu mama. Sihitaji tena hiyo kazi”

“Mama akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu.”

“Rashidi?”

“Naam”

“Mola ameweza kukunusuru na mikono ya wauaji. Tafadhali mwanangu, acha hiyo kazi, fanya hata kazi nyingine. Kumbuka wewe ndio ninaye kutegemea, mwanao Shamsa naye ndio hivyo ana kutegemea ukiandoka wewe hapa duniani ni nani ambaye ata tusaidia isitoshe mama yako umri wangu ndio umesha kwenda hivi?”

Mama alizungumza kwa sauti ya unyonge huku naye machozi yakimlenga lenga. Nikajifikiria kwa muda kidogo kisha nika nyanyuka.

“Una kwenda wapi?”

“Subiri mama”

Nikatoka nje na kufukua kishimo nilicho weka cheni, nikazichukua na kurudi nazo ndani.

“Mama ficha hizi. Hizi ni cheni za dhahabu na niliziokoa wakati majambazi hao wana kimbia”

“Chidi mwanangu, usitake kuniambia ume shirikiana nao?”

“Hapana mama una nijua mimi mwanao. Sina hulka za wizi mama. Zifiche hizi, chochote kitakacho jitokeza tafadhali usije ukazitoa. Umenielewa mama”

Nilizungumza huku nikimshika mama yangu mkono wake wa kulia na kumkabidhi cheni hizo.

“Mwanangu najua ana hitaji kwenda shule. Tafadhali mama hakikisha kwamba huzitoi kwa mtu yoyote”

“Rashidi mwanangu una nitisha?”

“Sikutishi mama ila nina kuomba mama fanya kama nilivyo kuambia”

Mama akanitazama usoni kisha akanikumbatia kwa nguvu nyingi sana huku akilia mithili ya mtoto mdogo.

“Mama nina rudi kazini”

“Kufanya nini tena?”

“Sihitaji askari waweze kuja hapa nyumbani kwa tukio lililo tokea ni lazima askari wata hitaji maelezo kutoka kwangu”

Mama akanitazama kwa macho ya masikitiko.

“Nakuomba sana mama usimpe mtu hizo cheni, ukishindwa kukaa nazo wewe nenda kazifukie hata shamba alafu uta muambiana kumuonyesha muonyesha mjukuu ako Shamsa.”

“Nime kuelewa baba”

Mama akanikumbatia kwa mara ya mwisho kisha nika simama.

“Usije ukamuambia mama Shamsa kwamba nilirudi”

“Sawa”

“Na wala akirudi wala usionyeshe dalili yoyote ya kutambua kwamba ana tabia ya kutoka usiku”

“Sawa”

Mama alinijibu kwa msisitizo na ujasiri mkubwa, nikamshika mwanangu nywele zake na wala hakuweza kuamka, nikatoka ndani hapo na kuanza kukimbia kurudi katika lindo langu. Nikiwa karibu na eneo la kazini kwangu nikaona gari nyingi za askari zikiwa zime kusanyika katika eneo hilo. Nikatembea kwa kujiamini hadi walipo askari hao. Nguo zangu za ulinzi nilizo zivaa ziliweza kuwafahamisha askari hao kwamba mimi ni mmlinzi kati ya walinzi ambao wamekutwa ni maiti.

“Ulishuhudia tukio?”

Askari mmoja aliniuliza pasipo hata ya salamu?”

“Ndio”

Niliitikia kwa sauti ya kipole.

“Mkuu kuna mlinzi mmoja ameona tukio”

Askri huyo alizugumza na kumfanya mzee mmoja mwenye nyota mbili begani mwake kuja eneo tulilo simama. Akanitazama kuanzia juu hadi chini kwa macho makali sana yanayo tisha mithili ya macho ya Simba.

“Una itwa nani?”

“Rashidi”

“Rashidi nani?”

“Rashidi Pinda”

“Umetokea wapi muda huu?”

“Aha…majambazi walivyo vamia hapa niliweza kukimbia kwa woga?”

“Mpakizeni kwenye gari mpelekeni kituoni kwa mahojiano”

“Sawa mkuu”

Askari mmoja akanionyesha defender ya kupanda kisha tukaondoka eneo hilo kwa mwendo wa kasi sana. Tukafika kituo kikuu cha polisi na nika ingizwa kwenye moja ya chumba amabcho kina meza pamoja na viti viwili.

“Simu yako”

Askari huyo alizungumza huku akininyooshea mkono. Nikamkabidhi simu yangu kisha akatoka ndani hapa na kuufunga mlango kwa ndani. Nikakaa ndani hapa hadi nilipo anza kuona mwanga ukiinia katika dirisha dogo lilipopo juu ikishiria kwamba kume pambazuka tayari. Mlango ukafunguliwa na akaingia mwana dada mmoja marefu aliye valia suti nyeusi, shepu yake namba nane hakika ukiwa mwanaume lijari ni lazima umtamani. Akavuta kiti kilicho mbele yangu huku akinitazama kwa tabasamu pana usoni mwake.

“Rashidi Pinda, si ndio?”

“Ndio”

Mwana dada huyu ambaye hadi sasa hivi sifahamu ni nani akanielekezea simu yake na kunionyesha video iliyo rekodiwa na cctv kamera ikinionyesha nikiingia katika moja ya duka na kuchukua cheni za dhahabu na kutoka ndani hapo kwa mwendo wa haraka. Mapigo yangu ya moyo yakaanza kunienda kasi sana kwa maana sikufikiria nilicho kifanya kina weza kuonekana.

“Nime kuja kuzungumza na wewe kirafiki sana Rashidi endapo uta niambia ukweli na uwazi basi nita kusaidia kwa asilimia mia moja ila ukikataa sijui ni kitu gani ambacho kita kupata”

Mwana dada huyu mrembo alizungumza kwa upole sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Niambie wezako ulio shirikiana nao katika huu mpango wa kuvamia huu mtaa, wakauwawa askari polisi wawili pamoja na walinzi wezako watatu na kuiba mali nyingi sana, wapo wapi. Kumbuka ukweli wako Rashidi ndio uta kuweka huru la sivyo jela ita kuhusu”

Maneno ya mwana dada huyu yaanifanya nizidi kutetemeka mwili mzima kwa maana hata hao majambazi wenyewe siwajui ni kina nani na wala sifahamu wame tokea wapi na kitu kilicho niponza ni kuiba cheni za watu kwenye duka hilo la muhindi ambazo endapo nita ziuza basi nita toka kimaisha.



“Mi….imi….mi sijui”

Nilijibu huku nikiwa nime jawa na woga ulio ambatana na kigugumizi kikali sana. Mwadada huyu akatabasamu huku akisimama taratibu, akaliweka koti lake la suti vizuri kisha taratibu akanisogelea karibu yangu na akainama pembeni yangu huku akinitazama.

“Rashidi nahitaji kuzungumza nawe kirafiki kabisa. Ila mbona una nificha rafiki yangu, wewe nieleze ni wapi walipo majambazi wezako kisha nina kuhakikishia kwamba uta kuwa huru”

“Kweli dada yangu mimi sifahamu chochote”

Gafla nikastukia nikibamizwa uso wangu kwenye meza hii, wenge nililo lihisi hakika sikuwahi kukumbana nalo kwenye maisha yangu.

“Huwa sipendi mtu mbishi”

Mwanadada huyu alizungumza kwa sauti ya ukali kidogo huku akinishika kichwa changu kwa nyuma. Akanigongeza tena kwenye meza hadi damu puani zikaanza kunichuruzika. Akaingia askari mwengine wa kiume.

“Amesema chochote?”

Askari huyo alimuuliza mwana dada huyu.

“Hajazungumza chochote mkuu”

“Mpelekeni Pagatoni, ni hakikisha ana zungumza ukweli. Hatuwezi kuona askari wa jeshi la polisi Tanzania wana uwawa alafu mpumbavu mmoja aliye choresha mchongo ana kaa kimya.”

“Sawa mkuu”

Mwanadada huyu akanishika mkono wangu wa kulia eneo la kwapani, akaninyanyua juu, sikutarajia kuona mwanadada kama huyu akiwa na nguvu nyingi kiasi cha kuninyanyua. Akanitoa ndani hapa na kunikabidhi kwa askari wawili.

“Mpelekeni Pagatoni”

“Sawa mkuu”

Askari hao walimjibu mwana dada huyu na wakaanza kunipeleka katika eneo ambalo sijui ni eneo gani. Tukashuka ngazi zinazo elekea chini ya ardhi, eneo hili lina giza kiasi, tukafika katika chumba ambacho kina fivaa vya ajabu ajabu ambavyo leo hii ndio mara yangu ya kwanza kuviona.

“Mvueni nguo”

Mwana dada huyu alizungumza na askari hawa wawili wakatii amri hiyo.

“Jamani mimi sijui chocho…..”

Sikumalizia sentensi yangu, askari anaye nivua shati akanizaba kofi la shavuni upande wa kulia hadi nikahisi sikio langu lime poteza mawasiliano ya kusikia vizuri.

“Kaa kimya kunguni wee”

Askari huyu alifoka huku akiendelea kunivua shati. Sikuamini ninacho kiona kwa maana wamenivua nguo zangu zangu zote na nipo uchi kama nilivyo zaliwa. Nikafungwa mnyororo mmoja mkono wa kulia na mnyororo wa pili mkono wa kushoto. Minyororo hii ika ning’inizwa kwenye moja ya bomba lizizopo juu ya paa hili kisha askari hawa wakaanza kuvua minyororo hiyo na kujikuta nikianza kupanda juu taratibu huku mikono nikiwa nime ichanua kama mtu aliye sulubishwa msalabani. Mwanadada huyu akavua koti lake na kulining’iniza kwenye msumari wa mlangoni mwa chumba hichi.

“Hii ni nafasi yako ya mwisho Rashidi. Niambie wezako wapo wapi?”

“Haki ya Mungu dada yangu sijui, mimi ni mlinzi tu”

“Haya. Mwagieni maji”

Askari hawa wakachota maji kwenye moja ya pipa lililopo ndani hapa na kunimwagia mwilini mwangu. Hata dakika moja haikuisha nikaanza kuwashwa mwili mzima, hapa ndipo nikagundua kwamba maji haya ni maji ya upupu. Machozi yakaanza kunimwagika huku nikilia kwa uchungu sana kwa maana mwili wangu una washa na nina shindwa kujikuna. Askari huyu wa kike akachukua mjeledi wenye miba miba akaushika vizuri na kusimama mbele yangu.

“Sijawahi kuwa na huruma kwa mwanaume yoyote kwenye maisha yangu. Sasa leo uta kwenda kuzungumza”

Akanitandika mijeledi miwili ya haraka haraka. Yowe nililo lipiga hakika sikuwahi kulipiga kwenye maisha yangu, maumivu niliyo yapata hakika sikuwahi kuyapata kwenye maisha yangu.

“Sema wapo wapi wezako?”

“Sijui haki ya Mungu sijui dada muna nionea tu bure”

Nilizungumza huku nikilia kwa uchungu sana. Mwana dada huyu hakika hakuwa na huruma kabisa, akaendelea kunicharaza na mjeledi mwili mzima na kila sehemu alipo nipiga akatoka na vipande vya jama.

“Chumvi na pilipi”

Mwanadada huyu alizungumza na askari hawa wawili wakavaa gloves, wakafungua moja ya kopo na kutoa chumvi, wakaanza kunipaka mwilini mwangu hususani maeneo niliyo jeruhiwa na mjeledi. Maumivu niliyo yahisi hakika nikatamani ardhi ipasuke na inimeze. Chumvi hii ina pilipili ambayo ina yazidisha maumivu yangu.

“Cheni za dhahabu ume zipeleka wapi?”

Swali hili likanifanya nipate ujasiri kidogo kwa maana nipo tayari kufa ila nisisiema ni wapi zilipo cheni hizo kwani endapo nita ziuza basi mimi na familia yangu tuta kuwa na kijiunafuu cha maisha.

“Sijachukua mimi”

Nililia kwa uchungu sana. Mwanadada huyu akanipiga ngumi sita za tumboni na kukijuta nikitema damu.

“Mkuu uta muua”

Askari mmoja alizungumza kwa woga kidogo.

“Kaa kimya na wewe”

Mwana dada huyu alifoka, akatembea kwa haraka hadi kwenye meza iliyo jaa vifaa vya ajabu ajabu. Akachukua plaize na kinisogelea. Akayashika makend** yangu huku akiyaminya minya.

“Mkuu”

Askari wa pili aliita na kumfanya mwana dada huyu kumtazama kwa macho makali sana.

“Tumpe muda ata zungumza”

“Ohoo muna mtetea kwa sababu ni mwanaume mwenzenu si ndio?”

Askari hawa wanaonekana kushikwa na imani kidogo juu ya vitendo ninavyo fanyiwa.

“Hapana mkuu ila tumpe muda”

“Tokeni nje na nyinyi ni kina nani ambao muna nielekeza kazi mimi eheee?”

Askari hawa wa kiume wakajikuta wakikaa kimya.

“Nimesema tokeni”

Wakatoka ndani hapa na kuniacha na askari huyu ambaye sura yake haiendani kabisa na matendo yake. Akachukua vibanio viwili vya shuma ambavyo vina nyanya. Kimoja akanibana kwenye nyama ya mbavu yangu ya upande wa kulia kisha kibanio kingine akanibana kwenye kidole cha mguu wa kulia.

“Muna ua askari wa jeshi la polisi alafu muna taka tuwacheke chekee”

Alizungumza huku akipiga hatua hadi kwenye moja ya mashine iliyo kaa kama muundo wa stablaizer. Akaiwasha nikahisi mwili mzima ukitetemeshwa hadi nikahisi maini na moyo vikipasuka. Nikaanza kuona maruwe ruwe. Kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivyo kigiza kikaanza kutawala machoni mwangu na baada ya muda kidogo sikuweza kuona wala kusikia kinacho endelea.

***

Sauti ya mziki wa taratibu ikaanza kupenya masikioni mwangu. Nikayafumbua macho yangu na kuanza kuyaangaza katika chumba hichi, nikamuona mzee aliye valia koti yeupe akiwa amekaa kwenye moja ya kiti kilichomo ndani hapa huku akiminya minya computer yake. Nikajitazama mwili wangu na kukuta nikiwa nime valishwa nguo za rangi ya chungwa na nguo hizi ni maarufu sana kwa ajili ya wafungwa. Nikataka kujipapasa na mikono yangu miwili ila mkono wangu wa kushoto ume fungwa pingu iliyo unganishwa na kitanda hichi cha chuma.

“Ohoo ume amka”

Mzee huyo alizungumza mara baada ya kugeuka. Akasimama na kunifwata sehemu nilipo lala.

“Nipo wapi hapa?”

Niliuliza huku nikiwa nina tetemeka kwa woga.

“Kijana karibu sana upo gereza la Maweni, Tanga.”

Mzee huyu alizungumza huku akitabasamu usoni mwake.

“Tanga, Maweni?”

“Ndio na mimi ni daktari wako ninaye kutibu. Una wiki sasa toka uletwe hapa”

“Wiki!?”

Niliuliza huku nikizidi kushangaa kwa maana sijatarajia kama nina weza kufikishwa gerezani.

“Ndio, labda nikushauri jambo moja kijana wangu. Katika magereza ya watu hatari hapa Tanzania hili gereza ni namba moja. Ukiona mfungwa ume letwa huku basi tambua kwamba upo katika kundi la watu hatari.”

Maneno ya daktari huyu yakanifanya nizidi kuchanganyikiwa kwa maana sina kumbukumbu ni lini nime weza kuhukumiwa hadi kuletwa gerezani.

“Dokta nina ota, hapana nina ota?”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.

“Hapana hauoti na hichi unacho kiona ni sahihi. Nime jitahidi kukupa tiba na vidonda vyako sasa vimekauka. Majera yaliyo baki ni machache sana”

Daktari alizungumza huku akiiweka miwani yake sawa.

“Samahani”

“Bila samahani”

“Nililetwa hapa na kina nani?”

“Uliletwa na maofisa upelelezi wa jeshi la polisi ukiwa hoi binta abani. Na uliletwa hapa ukiwa na mejeraha yaliyo pewa matibabu ya awali ila baada ya hapo nika kushuhulikia na nimesha toa ripoti kwamba uta zinduka kati ya jana au leo. Namshukuru Mungu leo ume zinduka”

Hakika kwenye maisha hakuna kitu kibaya kama maisha kubadilika teka galfa tena ukiwa una majukumu ya watu wanao kutegemea kwenye maisha yao. Mlango ukagongwa na daktari akaruhusu anaye gonga kuingia, akaingia mwanaume mrefu aliye valia suti nyeusi na jinsi mnyoo wake ulivyo kaa kichwani, ina ashiria kwamba ni askari.

“Karibu afande”

“Nina shukuru dokta heshima yako”

“Nashukuru”

“Nina ona muhalifu wetu ameweza kuzinduka?”

“Ndio”

“Dogo una una jisikiaje?”

Nikashindwa hata kumjibu mwanaume huyu na nikabaki nikiwa nina mtumbulia macho kwani hadi sasa sielewi mambo yame kwendaje kwendaje hadi niwe gerezani.

“Dogo wewe jeuri sana ehee?”

“Hapana sio kijana jeuri. Ameziduka kutoka usingizini muda huu. Hivyo network zake bado hazijarudi vizuri”

“Ohoo basi akiwa vizuri uta nifahamisha nije kumuhoji maswali?”

“Sawa afande”

Mzee huyu alinitetea kisha afande huyu akatoka ndani hapa.

“Huyu ni mmoja wa maafisa polisi walio pewa jukumu la kukuchunga hadi pale utakapo zinduka. Kijana ni kweli ume shirikiana na majambazi?”

“Mimi na majambazi wapi na wapi dokta. Mimi ni mlinzi wa kawaida tu”

“Macho yako yana ukweli, ila sijui kwa nini wana shindwa kutambua ukweli ulimo ndani yako.”

Akaingia askari magereza mwenye nyota mbili begani.

“Nasikia ame amka?”

Alizungumza kwa sauti nzito na iliyo jaa mikwaruzo.

“Ndio kama dakika kumi na tano zilizo pita”

“Sasa ni wakati wa yeye kwenda kuonana na majambazi wezake. Muda wa kulala kwenye kitanda chako ume kwisha”

“Ila bado afya yake haijawa vizuri?”

“Dokta hili ni lijambazi kabisa, acha likapambane na wezake huko”

Askari huyu aliye panda hewani kwa urefu na kujazia misuli ya mwili wake alizungumza huku akinifungua pingu. Nikashushwa kitandani pasipo kupenda.

“Ngoja nimpatie dawa za kutuliza maumivu”

Daktari huyu alizungumza na kunipa kichupa kidogo.

“Kutwa mara mbili kidonge kimoja kimoja. Kimoja asubuhi kingine usiku”

“Nashukuru dokta”

Askari huyu akanipora kikopo hicho, akakifungua ndani na kutazama dawa zilizopo. Akakifunga na kunirudishia. Tukatoka ndani hapa huku miguuni nikiwa nime vaa ndala za umoja. Tukaanza kutembea kwenye kordo ndefu ambayo ina milango yenye bomba za chuma na kuna vyumba vingi. Kila eneo tunapo pita na askari huyu wafungwa wanachungulia huku wakishangilia.

“Mkuu mali mpya hiyo ilete huku”

Kelele za wafungwa walio jazia miili yao kwa misuli zilisikika kila eneo. Hakika gereza hili lina tisha kwa ndani, ni mara mia moja ukalipita kwa nje tu na sio kuingia ndani tena ukiwa kama mfungwa. Mlango wa moja ya chumba ukafunguliwa. Manjemba manne yaliyo jazia miili huku yakiwa tumbo wazi yakasimama huku yakitunisha vifua vyao.

Askari huyu akapenaa mkono na njemba moja, nika shuhudia akikabidhiwa noti ya elfu kumi iliyo kunjwa.

“Mali yenu huyo mzindueni usiku kucha”

Askari alizungumza huku akinisukumia ndani. Majamaa hayo yakanidaka huku yakionyesha dalili chafu za kingono.

“Mmmm mtoto mlaini kabisa”

Njemba moja ambalo ndio lilitoa pesa kwa askari magereza lilizunguma huku akijaribu kunishika makalio ila nikauwahi mkono wake.

“Una taka kufanya nini?”

Ilinibidi kujikaza kwa maana nikiwa legelege nita wapa nafasi ya kunifanya kitu kibaya.

“Ahaa dogo una koroma sio?”

Njemba moja lilizungumza huku likinisogelea na kuyachezesha maziwa yake yaliyo kaza kwa misuli itokanayo na mazoezi.

“Sihitaji ugomvi na mtu”

Nilitoa onyo huku nikijaribu kutoka katikati yao kwa maana wamenizingira.

“Oya toa boksi la condom”

Moyo ukanipasuka, hakika hivi vitu gerezani vina fanyika sana na wana ume hawaoneani huruma katika swala la kuingiliana kinyume na maumbile. Njemba moja ika toa boksi hilo la condom zilizo andika msd. Taa hatari ikawaka kichwani mwangu, kwani wakati ulio fika ni wakati wa kuilinda heshima yangu kama mwanaume niliya kamilika kila idara. Nikampiga kichwa njemba moja aliye simama mbele yangu na kikatua barabara kwenye pua yake na kumfanya ajishike pua yake huku akitoa mlio wa maumivu. Njemba aliye simama kulia kwangu nikampiga kisukusuku cha kooni mwake na kumfanya naye apate maumivu yaliyo mfanya ashike koo lake. Njemba aliye simama nyuma yangu akanikumbatia ili nisifanye fujo. Nikampiga kisukusuku kwa mkono wangu wa kulia na kikampata barabara kwenye sikio lake na kumfanya naye atoe mguno wa maumivu huku akiniachia. Njemba wa kushoto kwangu, nikamtandika ngumi ya kifua, akatabasamu kana kwamba ngumi hiyo haijamumpata.

“Piga nyingine mtoto mzuri”

Alizungumza kwa dharau huku akitunisha kifua chake. Nikaunyanyua mguu wangu wa kulia na kubamiza goti lake la mguu wa kulia hadi ukavunjika. Ukelele za mwezao ukawashangaza manjemba hawa, wakaanza kunishambulia na kunifanya niwe kama vile wameamsha mapepo yangu ya kupigana kwa maana katika maisha yangu yote ya kuanzia utotoni nilikuwa ni mtu mgomvi ambaye nina penda kupigana hata pasipo sababu ya msingi. Maisha hayo yalinifanya nijifunze kupigana nguvu za aina zote kuanzia ngumi za mtaani hadi ngumi za ulingoni. Kila siku mama yangu alikuwa akiletewa kesi zangu na mtu aliye nibadilisha na kunifanya niwe mtulivu na kuangalia familia ni mke wangu na ndipo nilipo amua kujikita sana kwenye maswala ya ulinzi kwa maana sikuwa na elimu ya kuajiriwa kwenye maofisi makubwa kwani niliacha shule nikiwa kidato cha pili.

Japo mwili wangu una majeraha ya maumivu ya kupigwa na askari wa kike, ila sikuhitaji kuwa mnyonge kwa manjemba hawa. Nikajitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha kwamba kila ninaye mpiga basi nina mvunja, tena sio kidogo nina mvunja kisawa sawa.

Kipondo nilicho watembezea manjemba hawa hawakuamini kwa maana miili yao ni miraba mine na mimi ukiniangalia ni mwembamba na nina kifua cha kawaida tu na wala sijajazia misuli kama wanaume hawa ambao wanatumia nguvu pasipo kutumia akili.

Njemba mmoja aliya salia akanikumbatia kwa mbele na kunibana kwa mikono yake miwili huku akininyanyu juu. Uso wangu una churuzika damu kwa maana kuikalisha minjemba mitatu iliyo shibiana kwa mazoezi kama wacheza myereka sio jambo la kitoto toto. Nikajitahidi kuitoa mikono yangu aliyo ibana na mwili wangu, nikafanikiwa kuichomoa mikono yangu na akabaki akiendelea kunibana mbavu zangu. Nikamkita vidole gumba kwenye macho yake na kummfanya aniachie huku akiweweseka. Nikambamiza teke la kifua hadi akajigonga kwenye nondo za mlango wa chumba hichi na akazimia.

“Si kila mwanaume ni mwanaume wa kumchezea mafala nyinyi”

Nilizungumza huku nikiwa nime simama katikati yoa.

“Usiniangalie mimi boya wewe”

Nilizungumza huku nikimkanyaga kwenye uso njemba mwengine ambaye yeye ndio alikuwa ametoa boksi la condom. Askari mmoja akapita eneo la chumba chetu. Akashangaa sana kuona manjemba yame lala chini huku yakigugumia maumivu. Akawaita askari wezake na akafika mkuu wao ambaye alinikabidhi katika manjemba hawa kwa hongo ya shilingi elfu kumi.

“Mtoeni”

Askari huyo alizungumza kwa ukali na askari walipo chini yake wakafungua mlango huu huku wakiwa wameshika virungu na wakaanza kunishambulia kwa kunipiga virungu, mateke huku wakiniburuta na kunitoa nje na sikuhitaji kupigana nao kwani wana weza hata kuniua na wakasingizia kwamba nilikuwa nina pambana nao ndio maana wakaniua.



Wafungwa wengi wanao chungulia katika milango hii ya nondo wakajawa na mshangao kuona nikipigwa kipigo ambacho wengi hawajajua sababu ni nini. Askari hao wakaninyua kwa nguvu na kuanza kunipeleka hadi kwenye chumba chembamba na kidogo ambacho kina dirisha dogo sana lililopo juu. Mlango wa chumba hichi ni wa chuma.

“Uta kula jeuri yako”

Mkuu wa askari hao wa gereza alizungumza kisha wakatoka ndani hapa na kuufunga kwa nguvu. Joto zito ambalo lipo ndani ya chumba hichi, likanifanya nimwagikwe na jasho jingi ambalo lina umiza majera ambayo bado hayajapona na yaliyo kuwa yemeanza kukauka yame toneshwa na kuanza upya. Giza lililomo ndani ya chumba hichi lina nifanya nishindwe kuona ni namna gani nilivyo jeruhuwa na manjemba hayo. Nikajipapasa kwenye mfuko wa suruali yangu na kwa bahati nzuri nikakikuta kikopo cha dawa ambazo nilipewa na daktari. Nikakifungua taratibu na kutoa vidonge viwili na kuvimeza pasipo hata maji.

‘Ehee Mungu ni kwa nini haya yanonitokea sasa hivi?”

Nilizungumza kwa uchungu, huku nikilia.

“Ukiletwa huku, Mungu hana msaada na wewe?”

Nilisikia sauti nzito kutoka upande wa pili na kujikuta niksikiliza kwa umakini.

“Hei”

Niliita huku nikisikilizia kama mtu huyo ana weza kuitikia.

“Ndio”

“Nani wewe”

“Una taka kunifahamu ili iweje?”

Sauti ya mwanaume huyo ilinijibu kwa ukali na ikanibidi nikae kimya. Hakika hali ya humu ndani japo nina jaribu kuizoea ila akili yangu haikubali kabisa kukaa humu ndani. Maumivu ya mwili yakatulia ila sikuweza kupata usingizi hadi asubuhi. Mlango wa chumba changu ukafunguliwa kwa chini sehemu ambayo ina weza kuruhusu sahani ya chakula kuingia. Kikaingizwa kikombe kikiwa na maji ya moto pamoja na kipande cha slesi ya mkate. Kutokana na njaa kali nika shukuru sana kuona chakula hicho kidogo. Nikayanywa maji hayo yote kwa mkupua kisha nikakitafuna kipande hichi ambacho hakika sikuweza kukihisi kama kime ingia tumboni mwangu kwa maana ni kidogo sana.

“Oya”

Nilisikia sauti ya mtu aliye nisemesha usiku wa kuamkia leo.

“Ndio”

“Una itwa nani?”

“Rashidi”

“Mimi nina itwa Ngoko”

“Mbona upo huku?”

“Kuna fala nilimchoma kisu kwenye mstari wa chakula juzi. Na wewe mbona ume letwa huku?”

“Nime singiziwa keshi ya ujambazi?”

“Sizungumzii kwa nini upo gerezani. Yaani nina zungumzia kwa nini upo kwenye hizi chamber huku?”

“Ohoo, kuna majamaa manne nime yapiga”

“Majamaa manne?”

“Ndio”

“Kwa nini ume yapiga?”

“Kuna askari mmoja aliniigiza kwenye room yao ili jamaa wanipakue. So nimeweza kuwavunja vunja wote”

“Mmmm!!!”

“Mbona una guna?”

“Hiyo mijama ndio mibabe ya hili gereza na inashirikiana na maaskari. Vipi wewe ni mgeni humu?”

“Ndio”

“Ndio maana walikupeleka ukakaribishwe”

“Ila wamenishindwa”

“Jamaa yangu wewe ni askari nini kwa maana hiyo mijaa haijawahi kupigwa na mfungwa yoyote humu ndani na nimijinyapara hiyo?”

“Hapana mwanangu mimi ni raia wa kawaida”

“Duu”

“Yaa”

“Aisee jiandae kwa vita na hawa maaskari na kuwa makini sana kwa manaa wana weza kukuwekea hata sumu”

“Duu”

“Ndio ume wagusa watu wao kwa maana watu wao hao ndio wana wasaidia kufanya biashara magendo ndani ya gereza”

“Biashara gani?”

“Ahaa kaka humu kuna biashara nyingi sana. Wana uza bangi, sigara, cocaine, wanauza chakula kizuri. Yaani humu ni kama upo kitaa ila kitaa cha wahuni mwanangu”

Ngoko akanieleza mambo mengi sana yanayo endelea ndani ya gereza hili, hakika kwa maelezo yake nikajiona kabisa ni lazima nita ishi maisha magumu na ya kuteseka.

“Je kuna mtu alisha wahi kutoroka?”

“Nina mwaka wa nane humu ndani ila sijawahi kuona mtu au kusikia kwamba kuna aliye toroka katika hili gereza mwanangu. Oya piga kimya wana wana kuja”

Ngoko ambaye yupo chumba cha pili alinieleza na kunifanya nikae kimya, milango yetu ikafunguliwa na tukamrishwa tutoke. Nikafungwa pingu mikononi mwangu pamoja na miguuni mwangu, hapa ndipo nikapata nafasi ya kumuona jamaa huyu ambaye naye ni mrefu na mwili wake ume jazia kwa misuli na ni mweusi sana. Akanishangaa mara baada ya kuniona nina mwili wa kawaida sana ambao sio wa kuzaniwa kwamba nina weza kuwapiga manjemba tena manne yaliyo jazia na kushiba. Tukaondolea eneo hili tena kwa ulinzi mkali wa askari walios hika mitutu ya bunduki. Tukagawanyishwa Ngoko akapelekwa eneo jengine huku na mimi nikipelekwa eneo jengine ambalo ni gorofani. Nikaingizwa kwenye moja ya ofisi ambayo kwa haraka niliweza kusoma kibao cha mlango na kufahamu kwamba ni ofisi ya mkuu wa gereza.

“Mkuu kijana mwenyewe ndio huyu?”

Mzee huyo alite valia nguo nzuri askari magereza huku begani mwake akiwa amechafuka kwa vyeo ambavyo sivifahamu.

“Musinitanie huyu mbau mbau ndio amewapiga na kuwavunja manyapara wangu?”

“Ndio mkuu”

Mkuu huyu aliye shika sigarete akavuta taratibu na kupuliza moto hewani.

“Kijana una itwa nani?”

Alizungumza huku akinyanyuka kwenye mkiti wake wa kifahari. Jinsi ofisi hii ilivyo jaa vitu vya thamani una weza kusema sio ofisi ya gereza.

“Nina itwa Rashidi”

“Rashidi nani?”

“Pinda”

“Ohooo wewe ni wale majambazi mulio vamia jijini Dar es Salaam ehee?”

“Mimi sihusiki nilikuwa ni mlinzi katika lile lindo. Wezangu walipo kuwa wana uwawa mimi niliweza kutoroka?”

“Kwa nini usinge baki na ukauwawa pamoja na wezako?”

Swali la mkuu wa gereza likataka kunifanya nimpe tusi ila kama kuna kitu kikanikaba kooni mwangu na kujikuta nikinyamaza kimya.

“Wewe si una ulizwa na mkuu. Jibu”

Askari ambaye aliniabidhi kwa manyapara alizungumza huku akinipiga kofi la mgongo. Dhairi askari huyu ana onekana kuto nipenda kabisa.

“Ilikuwa ni bahati yangu kuwa hai”

Nilizungumza kwa sauti ya upole.

“Andaa pambano nina hitaji kuona uwezo wake”

“Sawa mkuu”

Nikatolewa ndani ya ofisi hii huku nikiwa sielewi ni pambano gani ambalo nina andaliwa. Nikapelekwa hadi kwenye bwala la chakula ambalo lime jaa wafungwa. Kila ninapo katiza wafungwa wezangu wananiangalia kwa mshangao huku wakinong’onezana. Nikafunguliwa pingu na minyororo za miguu.

“Kula chakula chako cha mwisho kwa maana leo ndio siku yako ya kufa”

Askari huyu anaye nichukia alizungumza kisha akoondoka na kuniacha. Ngoko akaninyooshea mkono na kunipa ishara ya kumfwata katika sehemu aliyo kaa peke yake.

“Kachukue msosi pale ule jamaa yangu”

“Sawa”

Nikapanga mstari wa wafungwa wanao chukua chakula.

“Njoo ukae hapa”

Mzee mmoja alizungumza na kunipisha nikasimama mbele yake na watu wote walio kaa nyuma yake hawakuzungumza chochote.

“Hongera sana kija”

“Hongera ya nini?”

“Kwa kazi yako ya jana. Sifa zako zime samba kwa wafungwa wote humu ndani”

“Nashukuru”

“Una itwa nani?”

“Rashidi”

“Ohoo una jina kama la kijana wangu wa mwisho”

“Shukrani”

Nikachukua sahani moja kubwa, nikapakuliwa ugali mkubwa kiasi na nikajaziwa maharake ambayo yana elea elea kwa wingi wa maji.

“Tuta onana”

Mzee huyu alizungumza huku nikoondoka na kuelekea eneo alilo kaa Ngoko.

“Yule mzee ana semaje?”

“Amenipa hongera ya nilicho kifanya”

“Yule mzee ni mmoja wa wanajeshi walio asi jeshini miaka ya nyuma na alikuwa ni jambazi sasa ameingia hapa akiwa kijana hadi sasa amekuwa mzee wa miaka stini na kitu. Ile troops ya watu wanao mfwata kwa nyuma wale wote ni vijana wake. Wakitoka wale manyampara yeye ndio ana fwata kwa udon”

Ngoko alinieleza huku tukiendelea kula taratibu ugali huu wa dona.

“Humu gerezani kuna makundi ehee?”

“Hakuna gereza linalo kosa makundi dunia nzima. Kuna makundi ya wababe hadi makundi ya wanyonge. Vipi walikupeleka wapi?”

“Kwenye ofisi ya mkuu wa gereza”

“Duu huyo mzee ana roho mbaya. Amekuambiaje?”

“Alishangaa kwamba mimi ndio nime wapiga wala manyapara wake.”

“Hajakuandalia pambano?”

“Ameniandalia. Ume juaje?”

“Yule mzee ana endesha mradi wake wa mapambano ya siri sana yanayo fanyika kuanzia saa sita usiku. Hayo mapambano huwa ni ya mauaji. Yaani ni lazima mfungwa mmoja afe ndio anaye shinda ndio ana ishi. Isitoshe ana wapiganaji wake hao ni maalumu sana wanao toka nje ya eneo hilo la gereza kuna madoni wenye pesa zao wanao leta wapiganaji wao na wana beti pesa. Hivyo ndugu yangu leo jiandae”

Maneno ya Ngoko yakanipa wasiwasi, isitishe hali yangu ya kiafya sio nzuri.

“Kwa hiyo una taka kuniambia kuna mapigano ambayo sio rasmi?”

“Ndio wafungwa wanao ingia hapo ni wale wenye pesa. Ukitoa buku una ruhusiwa eneo la pambano. Wewe piga picha wingi wa wafungwa tuliomo humu ndani. Akikusanya buku buku ana zalisha bei ngapi?”

“Mmmm”

“Ndio hivyo kaka. Jiandae na leo wata kuandalia jamaa moja hivi lina ishi kama mfalme hapa gerezani. Hilo ndio piganaji lake ambalo ana litumia na ni jitu katili sana. Kumuua binadamu mwenzake ni sawa na binadamu kumkanyaga mende”

“Lipo wapi?”

“Hilo jamaa lina chumba chake peke yake. Yaani humo ndani ana tv flat, sofa, kitanda kizuri na ana letewa malaya wa kulala nao kila siku na halifanyi kazi yoyote zaidi ya kupigana tu”

“Mmmm!!”

Nikahisi haja ndogo ikinibana.

“Yaa kuna rafiki yangu ambaye nilikamatwa naye alimuaa kwa kumvunja shingo kwenye mapambano hayo. Yaani nina uchungu naye sema uwezo wa kupambana nalo ndio sina”

Ngoko alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Hakika hofo ya kufa ikaniawala kwa kweli maisha yangu yame vurugika kiasi cha kunifanya nishindwe kuelewa.

“Ubaya ni kwamba jamaa katika pambano lina ingia na silaha ya kisu alafu wewe mpinzani wake una ingia mikono mitupu. Hivyo ina kuwa ni rahisi kukuvamia na kukutoboa tobosa.”

“Ehee”

“Ndio hivyo mwanangu. Japo tume kutana muda mfupi sana ila nina kuonea huruma”

Mzee ambaye alikuwa ana niongelesha kwenye kwenye mstari wa chakula akafika eneo hili nililo kaa na goko wa wakatuzunguka. Mzee huyu akakaa kwenye kiti ambacho hakina mtu.

“Rashidi”

“Naam”

Mzee huyu alatazama pande zote kisha akausogeza mkono wake karibu na mkono wangu na kunikabidhi kiwembe.

“Ficha hiyo ndio silaha pekee itakayo kusaidia kuishi vizuri humu ndani”

Nikakiingiza mfukoni kiwembe hichi.

“Usikiingize mfukoni, nikikuambia ficha ni kwamba kiingize katikati ya mkunjo wa suruali yako”

Mzee huyu alizungumza kwa sauti ya chini chini, nikafasua eneo la kiunoni kwenye mkunjo wa suluali yangu na kukichomeka kiwembe hichi.

“Maisha mema”

Mzee huyu akanyanyuka na kuondoka na watu wake ambao nao wana onekana ni watu walio jizatiti kwa mazoezi.

“Naona nyota yako na nyota ya mzee zina endana”

“Kiasi”

“Kuwa makini kwa maana ukaribu wake kwako sio wa bure kuna siku ata hitaji ulipe wema alio kufanyia”

“Una maanisha nini?”

“Gerezani hakuna kitu cha bure ndugu yangu. Hivyo kuwa makini sana”

Kengele ika gongwa na wafungwa wakaanza kutawanyika.

“Muda wa kula ume kwisha. Tuna rudishwa geto”

Ngoko alizungumza huku tukiwatazama askari sita wakitufwata. Tukamrishwa kusimama na tuka fungwa pingu mikononi na minyororo miguuni. Tukarudishwa katika vyumba vyetu ambavyo ndio vyumba vya adhabu kwa mfungwa mkorofi kwa maana eneo hilo halina hewa ya kutosha na lina joto la kufa mtu. Kutokana na shibe ya ugali wa dona na maharage nikaikuta nikianza kusinzia na kausingizi kakanipitia na kulala fofo. Kelele za mlango wa chumba changu kugongwa gongwa zikanistua na kujikuta nikikurupuka kutoka usingizini. Mlango wa chumba uka funguliwa na mwanga mkali wa tochi ukanimulika usoni mwangu.

“Nyanyuka haraka”

Nilisikia amri hiyo iliyo zungumza kwa ukali na nika itii pasipo kushurutishwa. Nikatolewa ndani hapa huku nikiwa katika ulinzi mkali. Askari hawa wakiongozwa na askari ambaye hatupatani wakazidi unipeleka katika eneo ambalo lina onekana lipo chini ya ardhi. Kila jinsi tunavyo zidi kushuka eneo la chini ndivyo jinsi ninavyo sikia kelele za shangwe. Tukafika katika eneo kubwa sana ambalo limetengezwa kwama ukumbi wa ulingo wa mapambano. Eneo hili lina viti vingi sana na wafungwa walio kusanyika ndani hapo ni wengi sana. Askari hawa wakanisukumia katika ulingo mkubwa ulio zungushiwa nyanya ngumu zenye miba miba na ndani ya uliongo huo ulio kaa kama banda kubwa kuna sakafu ngumu sana kwa chini.

‘Ehee Mungu sasa ndio muda wangu wa kufa ume wadia nini?’

Nillimuuliza Mungu wangu kimoyo moyo huku nikishudia jinsi wafungwa wanavyo shangilia. Kwenye eneo moja lililo tengenezwa vizuri kama jukwaa nika muona mkuu wa gereza akiwa amekaa na baadhi ya watu wanao onekana ni matajiri. Ukumbi ukajawa na furaha sana mara baada ya jitu moja lenye futi kama nane au tisa likiingia huku likiwa limejazia kisasa sawa. Yaani yale manyapara niliyo pambana nayo kwa hili jitu ni mara mbili yake. Ukubwa wa mtu huyu ni sawa sawa na mpiganaji mmoja wa myereka wa zamani anaye itwa Andrew the Giant. Jitu hili lililo valia chupi tu likanyoosha mikono ju na kuufanya uliongo kulipuka kwa shangwe kiasi cha kunifanya nitamani kutoka ndani ya ulingo huu ila hilo haliwezekani kwani tayari jitu hili limesha ingia ndani ya ulingo na mlango wa banda hili umefungwa tayari kwa pambano kuanza.



Jitu hili kikawageukia mashabiki wake, likanyanyua mikono juu na shangwe zikazidi kutawala eneo hili. Nikapitisha pitisha macho yangu kwenye eneo hili na kumuona mzee aliye nipatia wembe akiwa amekaa kwenye moja ya eneo pamoja na watu wake. Askari mmoja akampa jitu hili kisu kirefu kama nch nane hivi, likanitazama kwa dharau kisha likatingisha kichwa na kumrudishia askari huyo kisu akishiria kwamba ata nimudu pasipo sihala. Likaniita kwa dharau kwamba nimpige ngumi, hakika sikujidanganya hata kumsogelea likaanza kunifwata kwa spidi huku likiwa lime tanua mikono yake. Akataka kunikumba ila nika mkwepa na akajizuia kwenye nyavu za banda hili, kigageuka huku likinitingishia kichwa pamoja na kidole kimoja cha mkono wa kulia akinishiria kwamba nisijaribu kumkimbia.

‘Nalifanyaje hili?’

Nilijiuliza huku nikimsoma jinsi anavyo kuja. Kufumba na kufumba akawa amesha nifikia, akanikumba kumbo ambalo nilijikuta nikirushwa futi kadhaa nyuma na kuangukia mgongo. Watu wakashangilia sana huku mimi nikisikilizia maumivu. Likanyanyua mguu mmoja juu na kuushusha karibu na eneo la kifuani mwangu. Nikabingirika kwa kasi na mguu huo ukakita chini hadi kishindo chake nikakisikia vizuri.

‘Mmmm’

Niliguna kimoyo moyo kwa maana sipati picha kama ninge kanyagwa na guu hili lililo shibiana kwa misuli. Nikanyanyuka kwa maana kulala kwangu chini kuna weza kuniletea madhara.

“ZUMO ZUMO ZUMO ZUMO”

Wafungwa waliendelea kulishangilia jitu hili nililo gundua kwamba lina itwa Zumo.

‘Lazima nijiokoea hapa’

Niliwaza huku nikimtazama jinsi anavyo kuja kwa kasi ili anikumbe kama mara ya kwanza, nikalipiga chenga ya mwili kwa kulikwepa huku nikiachia teka moja kwa mguu wangu wa kulia na mpiga eneo la nyuma la mguu wake wa kulia. Likasimama kama lime stuliwa, watu wote wakanyamaza kimya, taratibu likageuka huku likiwa limeikunja sura yake hadi nikaogopa. Hakika duniani kuna watu wana sura za kutisha. Likapiga kelele na kuwafanya watu waanze kushangulia. Likaanza kurusha mateke mfululizo kiasi cha kunifanya niyakwepe. Likanibamba kwa kunishika mkono wangu wa kushoto likaninyanyua juu na kuniweka begani mwake. Haki ya Mungu nikahisi kama dunia ina pinduka kichwa chini miguu juu, likaanza kuzunguka na mimi ulingoni hapa huku likiwa lime nibana kisawa sawa begani mwake. Likaninyanyua juu kwa mikono miwili kisha likaniachia mzima mzima. Nikajigeuza kwa haraka hewani na kutua kwa miguu miwili na kulifanya lisiamini. Nikampiga teke eneo la makend* yake na kumfanya aibane miguu yake huku macho yakiwa yame mtoka kwa maana eneo hilo hata uwe jasiri vipi ili ukipigwa ni lazima ujisikilizie kwanza. Nikajirusha hewani huku nikitanguliza miguu yangu miwili na ikapiga kwenye goti la mguu wake wa kulia na kulifanya lipige giti moja chini. Likataka kunishika kwa makono wake wa kulia, ila nikampiga ngumi kwenye vidole vyake vya mkono huo hadi nikasikia mlio wa jinsi mifupa ya vidole hivyo vinavyo vunjika. Likapiga ukelele ambao sasa hivi sio wa kufurahia ila ni kelele ya maumivu.

Askari mmoja akamuingizia kisu ambacho alikuwa amepatiwa kwa mara ya kwanza. Likanyanyuka likiwa na kisu hicho. Likajaribu kukirusha kwa mara kadhaa kisu hicho ambacho kina nipunyua punyua, ila jambo la kumshukuru Mungu hakijanipata. Nikakumbuka kiwembe nilicho kificha kwenye pindo la nguo suruali yangu, nikakichomoa na kukishika vizuri. Likarusha mkono wake wenye kisu, nikaudaka kwa maana kwa sasa ana tumia mkono mmoja, hukamcharanga vizuri sana kwenye eneo la kiungio kati ya mkono na kiganja. Damu nyingi zikaanza kumwagika kwa maana kiwembe hicho ni kikali. Shangwe zilizo kuwa zina tawala taratibu zikaanza kufifia, huku jitu hili likigugumia kwa maumivu. Nikaupiga mkono huo teka na kisu kikaanguka. Nika kiwahi kukiokota kisu hicho. Nikakimbia kwa kasi ya ajabu na kukanyaga nyavu hizi kwa hatua nne kuelekea juu, nikajigeuza kwa kasi hiyo hiyo na kutua mgongoni mwake huku mkono wangu wa kushoto nikimkaba kabali na mkono wangu wa kulia ulio shika kisu ukitua katika shingo yake huku nikia nimeitanguliza ncha ya kisu hicho kilicho zama karibia nusu na kusababisha damu kutoka kwa fujo kama bomba la maji lililo pasuka. Uso wangu wote ukajawa na damu huku nikiendelea kulikaba kisawa sawa jitu hili.

Likaanza kutumba huku likijaribu kunipigiza kwenye nyavu hizi. Nikakichomoa kisu hichi kisha nikakipitisha kwenye koromeo lake kwa nguvu zangu zote na kumzidishia hali mbaya jitu hili. Nikamuachia huku nikitua chini kwa miguu yangu miwili. Nikalishuhudia likipiga magoti mawili chini huku likwa limeshika koo la lake pamoja na eneo damu zinapo mtoka. Nikalisogelea huku nikiwa nimeyang’ata meno yangu kwa hasira. Nikakichomoa kisu hicho na kuanza mkumkita kita nacho kifuani mwake hadi jilalishuhudia likifumba macho na likaanguka chini na kulala chali huku damu zikiendelea kutapakaa kwenye sakafu ya ulingo huu. Hapakuwa na hata mtu mmoja aliye toa sauti yake kwa kushangilia, mwili mzima umelowana na damu, nikapiga kelele ya uchungu sana kwa maana toka kuzaliwa kwangu leo hii ndio mara yangu ya kwanza kumuua mtu. Mzee aliye nipatia wembe akaanza kupiga makofi yaliyo sikika ukumbi mzima. Akaskari karibia kumi wakaninyooshea mitutu ya bundiki ila mkuu wa gereza akanyoosha mkono na kuwapa ishara askari kushusha bunduki zao chini. Machozi yakaanza kunibubujika huku nikilitazama jitu hili, roho ya ushetani iliyo niiingia kwa muda moyoni mwangu, ikaanza kutoweka na kujikuta nikijisikia vibaya sana kwa kufanya kitendo hichi.

‘Ehee Mungu nisaidie mimi’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikishuhudia mlango wa banda hili ukifunguliwa wakaingia askari wanne wakiwa na bundika. Akaingia mkuu wa gereza huku akiwa haamini alicho kiona. Akalitazama jitu lake alilo kuwa ana litegemea, kisha akanitazmaa na mimi. Akatabasamu kwa dharau kisha akaninyooshea mkono mimi na kuwafanya wafungwa kushangilia kwa furaha.

“Mpelekeni katika chumba cha huyu kum** ukubwa wa bure lime angushwa na mtoto mdogo”

Mkuu wa gereza alizungumza kwa kejeli. Hapakuwa na askari aliye tamani kunishika kwa maana nime jawa na damu. Wafungwa wakazidi kunishangilia na nikaondoka ukumbini hapa.

“Wewe ni nani?”

Askari anaye nichukia aliniuliza huku akiwa ametangulia mbele na askari wengine wakinifwata kwa nyuma.

“Mimi ni jini”

Nilizungmza kwa kujiamini na kumfanyaa askari huyu kusimama, na mimi nikasimama huku wezake wanao nifwata kwa nyuma nao wakasimama. Akanigeukia na kunitazama usoni mwangu kwa macho yaliyo onyesha udhaifu wa kuniogopa.

“Usijaribu siku kunipiga kama ulivyo fanya jana. Nita kuvunja vunja kiungo kimoja baada ya kingine”

Nilizidi kumchimba mkwara askari huyu mara baada ya kugundua udhaifu wake. Hakujibu chochote zaidi ya kuongoza njia. Wakafungua mlango na wakanipa ishara ya kuingia katika chumba hichi kilicho tengenezwa vizuri kama chumba cha nyumbani kwa mtu tajiri. Nikajikuta nikishangaa kwa maana hata mtaani nilipo toka sijawahi kuingia kwenye chumba kama hicho toka nilipo zaliwa.

“Ukihitaji chochote kuna simu hapo uta piga”

Askari anaye nichukia alizungumza huku akinitazama kwa wasiwasi.

“Poa”

Askari wakatoka ndani hapa, nikaanza kukikagua chumba hichi huku nikitazama feniture za garama zilizo wekwa. Nikafungua mlango mmoja nilio uona na kukua ni choo na bafu kilcho tengenezwa kwa marumaru nzuri sana.

“Woo”

Nilizungumza huku nikitazama sink moja zuri la kuogea. Nikavua nguo zangu zote zilizo lowana chapachapa kwa damu. Nikafungua bomba linalo toa maji kwa mfumo wa mvua, nikasimama chini ya bomba hili na nikaanza kusikilizia jinsi maji yanavyo nimwagikia mwilini mwangu. Damu zote zikaniondoka mwilini mwangu, nilipo jiridhisha nikaanza koga kwa sababuni.

‘Maisha yana kwenda kasi sana’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikifikiria jinsi nilivyo pitia shida za siku hizi mbili. Nikatoka bafuni hapa, na kurudi chumbani huku nikiwa na furaha sana. Gafla mlango ukafunguliwa na wakaingia wasichana wanne walio valia vinguo vifupi huku wakiwa wamejazia makalio yao. Ikabidi nikiwahi kujifunika sehemu zangu za siri kwa mto wa kitanda. Akaingia mkuu wa gereza huku akiwa ameshika kipisi cha sigarete yake.

“Hongera sana Rashidi”

“Asante”

“Usiku wa leo nime kueleta warembo hawa. Uta kula nao bata hadi asubuhi alafu kukipambazuka tuta zungumza vizuri sana. Nina kutakia usiku mwema”

Mkuu wa gereza akatoka na kuufunga mlango. Wasichana hawa wakaanza kunisogelea huku wakinitomasa tomasa maungo yangu.

“No sijisikii”

Niliwaambia huku nikichukua moja ya shuka na kujifunga kiunoni mwangu. Nikapiga hatua hadi mlangoni na kuufunga kwa ndani.

“Hei mbona muoga hivyo. Tuta kupagawisha usiku kucha”

Msichana mmoja alizungumza kwa sauti laini na iliyo jaa ushawishi wa kimapenzi.

“Nime waambia kwamba sijisikii”

Nilizungumza kwa msisitizo na kuwafanya wasichana hawa kuanza kucheka kwa dharau. Wakaanza kuvua nguo zao na kubaki kama walivyo zaliwa. Wakaanza kupapasana miili yao na wakazidi kwenda mbali mara baada ya kuanza kunyonyana ndimi zao. Hakika mambo haya nilikuwa nikiyaona kwenye filamu za ngono, sasa leo nina jionea live live.

‘Kumbe hata Tz haya mambo yapo’

Nilijisemea kimoyo moyo huku nikisikilizia jinsi ninavyo pata msisimko wa kimapenzi.

“Njoo baby”

Msichana mmoja mweupe aliye jaliwa figa namba nane alizungumza huku akinifwata. Akanishika mkono na akanipeleka hadi kitandani na kunisukumia kitandani.

“Ngojeni kwanza, sitaki kufanya chochote”

“Wee kaka vipi. Yaani mbo** imekusimama alafu una sema hutaki kufanya chochote”

“Au una ogopa ukimwi?”

Msichana mwengine alizungumza huku akitoa pakti za condom.

“Nimeoa”

Nilijibu kwa kijikaza tu ila kusema kweli uchu ume nikamata kisawa sawa.

“Hahaaaa…..sasa ukitutomb** una hisi mke wako ata jua au?”

“Acha ushamba bwana”

Walinishambulia kwa maneno ambayo hakika yakanifanya niitoe hofu inayo nikabili na kujisemea kimoyo moyo liwalo na liwe kwa maana sidhani kama kuna mwanaume anayeweza kuushinda mtihani wa kukutana na wanawake wenye ushawishi mkubwa wa kimapenzi kama hawa, kuanzia midomoni hadi kwenye maumbo yao.

Wakaanza kunichezea kila mahali kiasi cha kunifanya nijisikie kama nipo dunia nyingine, wakanivisha condom na tukaanza kupeana mtanange wa kukata kwa shoka. Japo nimechoka kutokana na misuko suko niliyo ipitia ila sikushindwa kuwahimili wote wanne. Uhodari wangu sio kwenye kupigana ila hata kwenye mitanange ya kimapenzi nipo vizuri tena sana. Wasichana hawa kila jinsi muda unavyo kwenda ndivyo jinsi walivyo zidi kujawa na mishangao kwa maana hawakuamini kama nina weza kuwahimili kwa kiasi hicho. Dozi niliyo watembezea ikawachosha na wakalala fofofo. Kutona na uchovu nami nikapata usingizi burudani huku kiyoyozi cha AC kikitupepea vizuri sana.

Asubuhi wasichana hawa wakavaa nguo zao huku wakinisifia jinsi nilivyo wahimili. Wakashukuru kuwa nami katika usiku huo na wakaondoka. Akaingia askari na kunikabidhi nguo nyingine mpya kabisa za magareza.

“Mkuu ana kuhitaji ofisini kwake”

Askari huyu alizungumza kisha akatoka ndani hapa. Nikaoga vizuri kisha nikavaa nguo hizi nilizo letewa. Nikaongozana na askari huyu hadi katika ofisini ya mkuu wa gereza.

“Ohoo Rashidi karibu sana. Usiku wako ulikuwaje?”

Mkuu wa gereza alinisalimia kwa furaha sana.

“Salama”

“Aisee hongera sana”

“Asante”

“Umewaonaje wasichana wame kupe mambo matambu”

“Ndio”

“Safi. Aiisee nime penda sana upiganaji wako. Hembu nipe historia yako kwa ufupi ume jifunzia wapi hayo mambo?”

“Mtaani?”

“Mtaani!!?”

“Ndio”

“Ume zaliwa wapi?”

“Dar es Salaam na kukulia Dar es Salaam”

“Safi, sasa kuna huu mkataba hapa. Ukikubali kusaini basi uta ishi kama mfalme ila ukikataa uta ishi kama mfungwa”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akinionyesha karatasi moja.

“Zumo alikuwa ni mpiganaji wangu hodari sana. Aliniingizia pesa nyingi sana katika mapigano ya ulingoni. Sasa nina hitaji kukufanya na wewe uwe mpiganaji wangu na uniingizie pesa nyingi sana, alafu uta endelea kuishi kule Paradiso na uta pata starehe kwa wanawake wazuri wazuri, watoto wa Kitanga wanao jua kukata mauno kitanani eheee?”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akiwa na furaha kubwa sana.

“Alafu uta kuwa una toka outing za hapa na pale”

“Samahani”

“Bila samahani”

“Hadi sasa hivi sija hukumiwa kifungo chochote na sijui ni siku gani ambayo nita hukumiwa”

“Nisikilize Rashidi hadi una letwa hapa gerezani ni kwamba umesha hukumiwa kimya kimya”

“Una maanisha nini ikiwa mimi kama mfungwa nina haki zangu za msingi na nimesingiziwa tu kama nime fanya tukio la ujambazi ila siwajui wale majambazi”

“Rashidi ngoja nikupe siri moja”

Mkuu wa gereza akanyamaza akavuta fumba zito la sigarate yake kisha akautoa puani na akaisugua sugua sigara hiyo kwenye kijichombo cha kuzimia sigara kisha akanitazama kwa makini.

“Sio kila mfungwa anaye kuja hapa gerezani ana makosa”

“Asilimia sabini ya wafungwa wanao kuja hapa wengi wana kuja kwa kesi za kusingiziwa”

“Kesi yako wewe haikuwa haina haja ya kuletwa gereza la mbali na Dar es Salaam kama hili ikiwa kila kitu kina onekana kipo wazi”

“Una maanisha nini?”

“Ngoja nikpe siri ambayo ime kufanya wewe uwe hapa”

Mkuu wa gereza akaegemea kiti chake cha kuzunguka. Akashusha pumzi nyingi huku akinitazama kwa macho ya udadisi.

“Una mke mzuri sana, tena sana. Mke wako ana toka na kiongozi mmoja wa ngazi za juu na ameweza kutoa amri ya wewe kuletwa huku na amepanga ufilie huku ili aendelee kula bata na mke wako mama Shamsa. So kijana, kuwa mpole ufwate ninacho kuambia iliu uendelee kuishi au ulete ubishi uuwawe huku huku gerezani na mama yako pamoja na mwanao mdogo wa kike wafilie mikononi mwa huyo kiongozi. Chaguo ni lako bwana mdogo”

Maneno ya mkuu wa gareza yakanistua sana kiasi cha kujikuta nikiwa nime duwaa, picha kamili ya kumkoasa mke wangu nyumbani siku nilipo rudi, ikanitawala, sasa nikaanza kupata majibu ya kwa nini nilikuwa ninapewa adhabu kubwa ambayo sikuistahili na isitoshe mkuu wa gereza ana onekana ana ijua vizuri sana familia yangu niliyo iacha uraiani.



“Huyo kiongozi ni nani?”

Niliuliza kwa sauti ya msisitizo huku nikimtazama mkuu wa gereza.

“Hupaswi kumfahamu na nime kueleza hivi kwa sababu nina hitaji uwe mtu wangu la sivyo una kwenda kupoteza kila kitu. Tia saini hapo”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akinikazia macho, nikauchukua mkataba huu na kuusoma kwa umakini. Ni mkataba ambao hakika kwa asilimia mia moja una ninyonya kwa upande wangu kwa maana sinto pokea hata shilingi mia moja kwenye kila pambano nitakalo pambana ila nitakacho kipata ni maisha mazuri ya kuishi gerezani hapa, sinto fanya kazi ngumu, sinto lala kwenye vyumba wanavyo lala wafungwa wezangu kiufupi ni kwamba nita ishi kama nipo uraiani.

“Rashidi usiwe mjinga, ukaipiga teka nafasi hii ya dhahabu, wezako wana itamani sana

“Ni kwa muda gani nita kutumikia kama mbwa wako”

“Nime bakisha miaka mitatu nistafu. Nakupa ofa moja, nikistafu nita kufanyia mpango uta kuwa huru”

“Mama yangu na mwanangu wata ishije uraiani?”

“Hilo siwezi kulijibu kwa sababu, una tambua kabisa ume iba macheni ya dhahabu. Umebeshwa kesi ya ujambazi na uuaji, dogo fungua akili yako, hata tukisema leo tukuachie huru una kwenda kufa huko uraiani. Tulizana na mimi hapa kisha baada ya hapo ukitoka kuna connection nita kuwa nimesha kutengenezea maisha yako yatakuwa mazuri sana. Yaani kwa jicho la tatu nina ona kabisa una kipaji cha kupigana kick boxing na Boxing.”

Mkuu wa gereza alizungumza na kunifanya nianze kujichanganua maisha yangu ya nyuma. Japo miaka mitatu ni mingi sana kwa mama yangu na mwanangu ila ina bidi nijitengenezee mazingira ya kuhakikisha nikirudi uraiani basi nina anza kudili na kiongozi aliye niibia mke wangu alafu wengine walio nitesa kama yule askari mwanamke basi nao wana takesa.

“Rashidi Rashidi”

“Naam”

“Rudisha mawazo yako hapa”

Nikachukua kalamu na kusaini mkataba huu na kumfanya mkuu wa gereza kutabasamu.

“Kwa wiki uta kuwa na mapambano mawili jumamosi na jumapil. Hakikisha una jifua vizuri na una shinda kila pambano tume elewana?”

“Ndio”

“Una weza kwenda sasa”

Nikasimama huku nikimtazama mkuu wa gereza kwa macho ya udadisi.

‘Ipo siku yako uta zilipa pesa zote utakazo zichukua kwa jasho langu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitoka ndani hapa. Askari wakanirudisha ndani ya chumba changu, nikatazama simu ya mezani.

“Hii simu ina weza kupiga katika simu za kawaida?”

Nilimuuliza askari aliye nileta.

“Hapana, una wasiliana na watu wa humu humu ndani”

“Naomba unipekele kwa daktari”

“Sawa”

Askari huyu anaye onekana ni mpole alizungumza huku nikitangulia mbele.

“Una itwa nani afande?”

“Shemzigwa”

“Wewe ni msambaa?”

“Ndio”

“Sawa”

Tukafika ofisini kwa daktri, nikamsalimia mzee huyu akamuomba askari atoke ndani hapa.

“Hongera sana kijana. Jana niliweza kushuhudia pambano lako”

“Nina shukuru dokta, nina maumivu mengi sana mwilini mwangu”

“Hilo lazima litokee kwa maana kupambana na jitu ambalo halikuwahi kushindwa na mpinzani yoyote sio jambo la kawaida”

“Hivi ni kwa nini kuna endeshwa mashindano haramu kama haya?”

“Ahaa ni kutokana na tamaa za mkuu wetu. Pia serikali haitambui kama kuna ukumbi wa chini unao endesha mapigano ya kinyama kama haya”

“Mmm”

“Ndio”

Daktari alizungumza huku akinitazama majeraha yangu kwa maana nimesha vua shati.

“Ume pewa ofa ya kuishi kwenye chumba cha Zumo?”

“Ndio”

“Kuwa makini sana Rashidi?”

“Kwa nini?”

“Huyu mzee ataenda kukutumikisha vibaya sana na kukufanya ni mbwa wake. Kwenye kila pambana ana jivunia shilingi milioni mia moja na kwenda juu”

“Weee!!”

“Haki ya Mungu vile. Hivyo unapaswa kuwa makini tena makini sana la sivyo uta kufa ukiwa bado mdogo sana”

“Dokta nina kuomba unisaidie jambo moja”

“Jambo gani?”

“Nina omba unisaidie simu yako nimpigie mama yangu nizungumze naye”

Daktari akanitazama kwa sekunde kadha akisha akapiga hatua hadi mlangoni. Akaufunga kwa ndani kisha akatoa simu yake kwenye mfuko wa koti lake na kunikabidhi.

“Zungumza kwa sauti ya chini kwa maana hairuhusiwi kabisa kwa mfungwa kutumia simu”

“Sawa”

Nikaiingiza namba ya mama na kumpigia. Kwa bahati mbaya namba ya mama haipatikani kabisa hewani, nikajaribu kumpigia mara sita mfululizo ila hapatikani.

“Vipi?”

“Simpati hewani”

“Labda simu yake ita kuwa haina chaji”

Nikaka jifikiria kwa dakika kadhaa kisha nikaiandika namba ya mke wangu katika simu ya daktari. Nikaipiga namba hiyo na jambo la kumshukuru Mungu ikaanza kuita na baada ya sekunde tatu ikapokelewa.

“Haloo”

Niliisikia sauti ya mke wangu.

“Haloo”

Aliita tena ikabidi nijikaze

“Ni mimi”

Nilizungumza kwa upole.

“Hee wewe jambazi, muuaji umenitafutia nini?”

“Mke wangu ina maana hata wewe una amini hilo”

“Nisikilize Chid, umenichakaza vya kutosha. Sasa acha niendelee na maisha yangu, nimepata wanaume wanao jua kutunza wanauwe wenye pesa zao na wanao jua kujali. Yule panya wako nime muacha kwa mama yako na hamuto kaa kuniona wala kunisikia na usijaribu kunipigia simu tena kwa maana ukipiga, nina kuapia haki ya Mungu dini yangu Muislamu nita kufanyia kitu ambacho hujawahi kufikiria kwamba nita kufanyia”

Mke wangu alizungumza kwa ukali kiasi cha kunishangaza sana, hapa ndipo nika yaamini maneno ya mkuu wa gereza kwamba mke wangu ame chukuliwa na kiongozi mkubwa serikalini.

“Ila mke wangu”

“Nani ni mke wako. Yaani sijui nilifwata nini kwako, yaani ulinifubaza mwanaume wewe. Mtoto sikuwa na matunzo, sasa koma na ukomae sikuhitaji na wala sikutako tena. Tumeelewana na tena ukiendelea kunifwatilia mama yako na yule panya wako wa kike wata kufa”

“Hapana kwa kweli, mke wangu mbona ume badilika hivyo. Umekumbwa na nani?”

“Koma mwana haramu kum** mak** wee, masikini na fukara mkubwa wewe huna hadhi ya kuwa na mimi na sitaki unitafute”

Mke wangu akakata simu na kunifanya nimwagikwe na machozi yatokanayo na maumivu ya mapenzi. Kwa mara ya kwanza sikuwahi kutarajia kama ingetokea siku nikamwagikwa na machozi namna hii. Dokta aliweza kusikia kila kitu alicho zungumza mke wangu kwa maana kuna utulivu ndani ya chumba hichi.

“Wanawake”

Dokta alizungumza kwa sauti ya upole huku akinitazama.

“Sio wote ni wanyama. Ila wao ndio walituponza tukala tunda kipindi hicho cha Adam na Hawa na tukafukuzwa kwenye bustani ya Edern”

Daktari akaendelea kuzungumza kwa sauti ya upole.

“Natambua ame kuumiza, ila kuitwa fukara na masikini sio kwamba wewe ujikubali kwamba uta kuwa makini milele. Una mikono, una nguvu na una kipaji. Vitumie kwa sasa alafu baadae uta kuja kuelewa ni nini nina maasha.”

“Dokta nina weza kwenda?”

“Ngoja nikuchome sindano ya kukausha majeraha”

Daktari akanichoma sindano hiyo katika mkono wangu wa kushoto kisha nitatoka ndani hapo.

“Sasa hivi ni muda wa wafungwa kufanya nini?”

“Kupumzika”

“Nahitaji kwenda eneo wanalo pumzika”

“Sawa”

Nikatoka katika eneo kubwa ambalo lina viwanja tofauti tofauto vya kimichezo, vipo viwanja vya moira wa kikapu, vipi viwanja vya mpira wa tenes, kipo kiwanja cha mpira wa miguu, kiufupi gereza limejitosheleza kwa kila jambo.

“Hei”

Nilistukia nikiguswa kwa nyuma, nikageuka na kumuona Ngoko akiwa na furaha sana.

“Niambie mwanangu”

Nilizungumza kwa furaha kwa maana Ngoko ndio mtu niliye mzoea.

“Hongera sana kaka, ume fanikiwa”

“Yaa nime fanikiwa mwanangu”

“Aisee sikuweza kuhudhuria pambano lako ila nilikuwa nina sikia sifa za kwamba mwanangu ume fanikiwa kumuua Zuma”

“Yaa safi sana kaka”

Tukatafuta sehemu na kukaa. Ukimya ukatawala huku tukiwatazama wafungwa wezetu jinsi wanavyo cheza michezo mbalimbali. Wapo baadhi ya wafungwa macho yao yapo kwangu huku wakionekana kujadiliana mamno fulani.

“Vipi sasa hivi una ishi V.I.P ROOM?”

“Ndio”

“Daa mwanangu ume uchinja”

“Kwa nini?”

“Ahaa wewe mwenyewe una onaje kile chumba?”

“Kipo vizuri”

“Ila uso wako una onekana una huzuni. Kuna ishu ina kusumbua?”

Nikajifikiria huku nikiwa nimeinamisha uso wangu chini.

“Ndio mwanangu”

“Nini tena ikiwa maisha yamesha kuwa mazuri hapa gerezani kwa upande wako?”

“Mke wangu ana niumiza kichwa sana pamoja na familia yangu”

“Nini tena kime tokea?”

“Chanzo kikubwa cha mimi kuletwa huku gerezani ni kesi ya ujambazi ambayo nime singiziwa. Kumbe kuna kibopa mmoja wa serikalini ana mla mke wangu na yeye ndio amekandamiza hili jambo na mimi nika onekana kwamba ndio nilichongesha ramani ya majambazi kuvamia eneo langu la lindo na kuwaua askari wezangu pamoja na askari polisi”

“Duu mwana hicho ni kisanga”

“Yaa ni kisanga kaka. Hapa nime mpigia simu, amenitukana sana na kunipa vitisho vingi sana na ameweza kuniambia kwamba nikiendelea kumfwatilia basi mama yangu na mwanangu wata atawaua”

“Duu huja zaa naye nini huyo mwanamke?”

“Ajabu ni kwamba huyo mtoto ni wake aliye muweka tumboni miezi tisa”

“Duu!!”

“Hapa amenivuruga kwa kweli”

“Pole sana mwanangu kwa maana wana wake wa kipindi hichi wana penda pesa kuliko kuwapenda watu walio wazunguka”

“Sijui nitoroke nikamchinjilie mbali”

“Kaka kaka, hili gereza hakuna mfungwa aliye wahi kutoroka na ukitoroka ndugu yangu ume kwisha. Wanacho kifanya ni kwamba hawakufukuzi wewe, ila wana kwenda kumata mtu muhimu sana kwenye maisha yako kama mama, mtoto. Alafu ana pewa adhabu ya kufa mtu hadi wewe una jitokeza na ukirudishwa humu ndani basi kitanzi kina kuhusu”

“Duu”

“Yaa, bora ukaushe ndugu yangu”

Muda wa mapumziko ukaisha, kutokana leo ni jumapili, wafungwa hatufanyi kazi yoyote. Tukapata chakula cha mchana na usiku wafungwa tukakusanyika katika ukumbi sinema na tukaanza kutazama filama kuadhaa na ilipo timu saa tano kamili usiku wote tukaamriwa kuelekea katika vyumba vyetu vya kulala. Kila ninavyo jilazimisha kutafuta usingizi nina shindwa kwa maana mama yangu na mwanangu ni watu ambao wana niumiza kichwa. Sijui kwa sasa mama yangu yupo katika hali gani na mbaya sana ni kwamba mimi ndio mwanaye wa pekee na umri wake ume kwenda sana kiasi cha kuugua ugonjwa wa kisukari.

‘Lazima niwe tajiri’

Nilizungumza huku nikiwa na uchungu mwingi sana kwani njia pekee ya kulipiza kisasi ni lazima niwe na pesa.

Siku zikazidi kuyoyoma huku maisha ya jela nikiendelea kuyazoea. Kitu pekee ambacho nina imani kwamba kita nifanya niendelee kuishi vizuri hapa gerezani ni kupambana zaidi na zaidi ili kuhakikisha kwamba nina mfurahisha mkuu wa gereza. Nikapata kocha wa kunifundisha mbinu nyingi sana za kupigana mchezo wa boxing pamoja na kick boxing. Mzee Ulimbo ambaye ndio kocha wangu, ndio mzee ambaye alinipatia kiwembe kilicho nisaidia kumcharanga Zomo katika pambano la miezi sita iliyo pita.

Makali yangu ya kuwa mpiganaji hodari yakazidi kuongezeka na kila pambano la nje ya magereza haya niliweza kuvaa kinyago maalumu ambacho sio rahisi sana kwa mtu kuweza kuitambua sura yangu. Roho yangu haikuwa nzuri kama awali, kwani ukatili umenijaa ndani yangu na kila niliye pambana naye basi nilihakikisha nina mtoa maututi au nina muua kabisa. Jambo hilo likamfanya mkuu wa gereza kunipenda huku akizidi kujivunia pesa nyigi sana kwa mapambano anayo niandalia.

“Mkuu”

Nilimuita mkuu wa gereza huku tukiwa ndani ya gari lake tukielekea eneo la Pangani ambapo kuna pambano lime andaliwa na wazungu.

“Ndio Chid?”

“Nikishinda pambano la leo una weza kunipa nafasi moja”

“Nafasi gani?”

“Ya kumuona mama yangu pamoja na mwanangu?”

“Mmm ndio nita kusaidia katika hilo”

“Nina shukuru sana mkuu”

“Ila hakikisha kwamba una shinda?”

“Toka nilipo kuwa mpiganaji wako ni siku gani niliwahi kupigwa?”

“Hujawahi kabisa, ila nahitaji ushinde kwa maana huyu unaye kwenda kupigana naye ni mzungu kuna dola laki tano hapo zimewekwa mezani hivyo ukishindwa, siku yangu ina kwenda kuwa njema sana”

Nikamkata jicho la kona kwa maana hizo pesa anazo zipigia mahesabu naamini ipo siku nita fanikiwa kuzichukua na mimi nita kuwa tajiri.

Majira ya saa kumi na mbili jioni tukafika katika mji wa Pangani.Tukashuka kwenye gari hili binafsi la mkuu wa gereza huku tukiwa tuomeongozanana askari wake wawili walio valia nguo za kirai na wana linda nisiweze kutoroka. Nikaingizwa kwenye chumba cha maandalizi katika hoteli hii ya kitalii ambapo ndipo pambano linapo fanyika.

“Chid”

“Naam”

“Huyu unaye kwenda kupigana naye ni mtu hatari, ana jua karete, taikondo na kung fu. Kumbuka muna pigana kick boxing. Hakikisha kwamba una mmaliza”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akinikazia macho.

“Sawa”

Nikavaa bukta yangu ya kupambana nayo. Nikajifunga bandeji kwenye mikono yangu, pamoja vikanyagio vya miguu yangu kwa maana pambano hili ni la kupigana hadi kufa. Nikajifunga kinyago changu usoni na kukikaza vizuri kiasi cha kuto kuweza kuanguka hata nikipigwa vipi. Ilipo timu saa nne kamili nikaingia ulingoni, ulingo huu ambao ume zungushiwa banda kubwa la nyavu za senyenge silishangai sana kwa maana sio mara ya kwanza kupigana kwenye ulingo kama huu. Watu wote walio udhuria ndani ya uliongo huu wana onekana ni matajiri wenye pesa zao. Nikiwa katika kuangaza angaza macho yangu kwa watu walio kusanyika eneo hili, nikamuona mke wangu akiwa amevalia gauri zuri na la garama na pembeni yangu sikuamini macho yangu mara baada ya kumuona mwanaume huyo mwenye mahusiano naye ni makamu wa raisi.

***


Hasira na chuki vikanitawala sana moyoni mwangu, nikatamani kuchomoka ndani ya ulingo huu na kuwavaa ila siwezi kufanya hivyo kwani ulingo tayari umesha fungwa na mpinzani wangu amesha ingia ndani ya uwanja huu pamoja na refa wa pambano hili. Mpinzani wangu akaanza kuruka sarakasi kadhaa kwamakeke yaliyo nifanya nizidi kuijenga hasira yangu moyoni kwani mke wangu ambaye nilikuwa nina mpenda na kumjali kuliko kitu chochote leo hii ana maisha mazuri tena na mtu mkubwa tu serikalini. Nikamtazama kwa mara ya mwisho mke wangu hadi akajistukia kidogo na nikaona aki mnong’oneza makamu wa raisi. Kengele ikagongwa, mpinzani wangua akaruka hewani na kunipiga teke la kifua lililo nirusha nyuma kiasi na kuanguka chini. Watu wakampigia makofi, nikamtazama mkuu wa gereza jinsi anavyo nikazia macho. Mpinzani wangu akajirusha tena hewani na kunipiga teke la mgong’o na kunifanya nipate maumivu makali sana. Makamu wa raisi na mke wangu wakajumuika na watu wengine katika kupiga makofi ya kushangilia. Mkuu wa gareza akanipa ishara ya mkono kwamba ninyanyuke na nipambane.

Mpinzani wangu akajaribu kuleta shambulizi jengine la kunipiga kisukusuku cha mgongo ila nikabingirika na kisukusuku hicho kikagonga chini, nikampiga teke la kichwani na kumfanya aanguke chini huku akisikilizia maumivu ya kisukusuku chake pamoja na teke hilo. Nikasimama huku nikiruka ruka na kumtazama akinyanyuka taratibu. Mkuu wa gereza akazidi kunisisitizia kwamba nimalize mchezo mapema kwa maana mpinzani wangu ndio amesha legea. Nimtisha mpinazani wangu kama nina mpiga ngumi ya uso, akajikinga na mikono yake miwili, kwa kasi ya ajabu nikafyatua teke kwa mguu wangu wa kulia na kumpiga katika mbavu zake kiasi cha kuhisi kabisa kwamba nimevunja mbavu hizo za upande wa kushoto kwake. Ukelele alio utoa hakika haukuwa wa kawaida. Nikapiga teke la kifua na akajigongeza kwenye nyavu za ulingo huu zinazo nesa kidogo, kitendo cha kurudi mbele nikampiga tikitaka la kidevuni na kumfanya damu kumruka mdomoni mwake. Akiwa katika hali ya kuyumba yumba, nikakimbia kwa kasi kumfwata, mguu wangu wa kulia ukakangaga kidogo kwenye paja la mguu wake wa kushoto na kuruka juu kiasi, nikashka chini kwa pigo la kumpiga kisukusuka kwenye utosi wake na kumfanya atokwe na macho kwa maana pigo hilo lina vunja fuvu la kichwa hadi mishipa ya shingo. Kabla hajaanguka, nikamzunguka kwa nyuma na kumshika shingo yake na kukiweka kichwa chake katika baga langu huku nikimtazama makamu wa raisi pamoja na mke wangu. Nikabonyea chini kidogo na kuvunja shingo yake hiyo na hapo hapo akafariki dunia. Nikamuachia na akaanguka chini, mkuu wa gereza akwa wa kwanza kusimama na kupiga makofi, taratibu watu kadhaa nao wakaanza kupiga makofi wakiwemo wazungu ambao huyu ndio mpiganaji wao. Refarii akanifwata na kuhishika mkono wangu na kuunyanyua juu akiashiria kwamba nime shinda.

Mlango ukafunguliwa na taratibu nikatoka katika ulingo huu huku nikiwa katika uangalizi wa mabaunsa wanne walio jaa kisawasa. Nikarudi katika chumba changu cha kujiandaa, baada ya dakika mbili mkuu wa gereza na walinzi wake wakaingia huku akiwa na furaha sana.

“Safi sana Chidi yaani una juaa. Haki ya Mungu, wengi walidhania mechi ita kuwa ngumu alfu dakika saba tu ume imaliza. Safi sana wewe kiboko”

“Nahitaji kuonana na mama yangu na mwanangu”

“Hilo kesho tu nina waleta gerezani. Safi sana”

Mlango ukagongwa na mlinzi mmoja wa mkuu wa gereza akafungua.

“Mkuu makamu wa raisi na mke wake wapo hapa”

Macho yakanitoka huku mkuu wa gereza akionekana naye kustuka.

“Usizungumze chochote na usivue maksi yako”

Mkuu wa gereza alizungumza kwa sauti ya kunong’oneza. Makamu wa raisi akaingia ndani hapa akiwa na mke wangu pamoja na walinzi wake wanne walio valia suti nyeusi.

“Heshima yako mkuu”

“Nashukuru, bwana sehemu kama hizi sio za kupigiana saluti. Huku tume kuja kula bata na watoto wazuri kama hawa”

Makamu wa raisi alizungumza kwa sauti ya kebehi huku akiwa amemshika kiuno mke wangu. Hasira ambayo ime nijaa Mungu mwenyewe ndio anaye jua. Jambo la kumshukuru Mungu ni jinsi kinyago changu kimeifunika sura yangu na kubakisha macho tu, laiti kama mke wangu angeiona sura yangu nina imani angezimia.

“Nashukuru muheshimiwa huyu ni kijana wangu”

“Naona ana uwezo mkubwa sana. Ume mtoa wapi?”

“Ahaa ni kijana wangu wa mtaani. Nina jaribu kukikuza kipaji chake”

Mkuu wa gereza alizungumza kwa unyenyekevu mkubwa sana. Nikakunja ngumi mikono yangu yote kwa hasira kwani mkono wa makamu wa raisi una endelea kupapasa kila sehemu ya kiuno cha mke wangu na jinsi anavyo onekana ni mtu ambaye amelewa kwani kuna wakati ana shusha mkono wake hadi kwenye makalio makubwa ya mke wangu na kuyaminya kwa nguvu na mke wangu ana kazi ya kutabasamu tu.

“Una itwa nani kijana?”

Makamu wa raisi aliniuliza huku yeye na mke wangu wa kinitazama usoni.

“Anaitwa Mashushu”

Mkuu wa gereza aliwahi kujibu

“Mashushu, ndio jina la wapi hilo?”

“Ni watu wa bara huko?”

“Wewe ni Mngoni?”

Nikatingisha kichwa huku nikiendelea kuwatazama kwa hasira.

“Ahaa muheshimiwa, kijana wangu anapo kuwa ametoka kwenye pambano hususani la mauaji huwa ana kuwa katika wakati mbaya. Kama huto jali muheshimiwa nina omba tumpatie nafasi”

“Ahaa nime kuja kumpongeza tu. Baby”

“Bee”

“Hembu mpe zawadi”

Mke wangua kafungua kipochi chake na kutoa noti noti za shilingi elfu kumi kama thelathini hivi na akaanza kunirushia moja moja usoni mwangu tena kwa dharau kubwa sana. Mkuu wa gereza akanitazama jinsi mikono inavyo nitetemeka kwa hasira kisha akanipa ishara ya kutingisha kichwa kwamba nisifanya chochote.

“Waooo dogo hizi uta kwenda kunywa soda”

“Tuna shukuru muheshimiwa”

“Haya ngoja niwaache, mimi ngoja nikapate mambo matamu kutoka kwa mama watoto”

Makamu wa raisi akamvua karibu mke wangu, akamnyonya denda lililo nifanya nifumbe macho yangu huku machozi yakinibubujika kama ni dharau basi hii imezidi sana.

“Mmmm, tamu sana. Ndugu yangu kuna watoto watamu sana duniani. Kula nchi ndugu yangu”

Makamu wa raisi alimuambia mkuu wa gereza aliye baki akitabasamu kinamfki tu.

“Sawa sawa mkuu”

“Tuta onana, si una jua kesho nina dhiara ya kuja gerezani kwako. Hivyo andaa mazingira mazuri mazuri ya kuonekana kwenye tv. Nimekuambia kabisa kwani ilikuwa ni ziara ya gafla”

“Nashukuru mkuu kwa taarifa”

“Nime kujulisha tu”

Makamu wa raisi akaondoka chumbani hapa na walinzi wake huku akiwa ameking’ang’ania kiuno cha mke wangu kisawa sawa. Nikavua kinyago changu na kukitupa chini kwa hasira kali sana, katika siku ambazo mapigo yangu ya moyo yame nienda kasi sana ni siku ya leo.

“Hei hei Chidi.”

Mkuu wa gereza aliniita huku akinisogelea. Jicho nililo mtazama nalo yeye mwenyewe akajikuta akisita kunisogelea.

“Nahitaji kurudi gerezani sasa hivi”

“Sawa tuna fanya mpango uweze kurudi. Msaidieni kumkusanyia pesa zake”

Vijana wa mkuu wa gereza kwa haraka haraka wakakusanya pesa zangu na kunikabidhi. Nikazitazama pesa hizi huku nikikumbuka tukio la mke wangu kunimwagia pesa hizo usoni mwangu tena kwa dharau.

‘Ipo siku uta kuja kujuta’

Nilizungumza huku nikiziweka pesa hizi kwenye kibegi changu cha nguo. Nikabadilisha nguo zangu kabla ya kutoka wakaingia wazungu wawili mmoja akiwa ni mwanamke na mwengine akiwa ni mwanaume.

“Tume mpenda mpiganaji wako”

Mwanamke huyo alizungumza huku akinitazama usoni mwangu

“Nina shukuru sana”

Mkuu wa gereza alijibu huku akiwa na tabasamu.

“Tukihitaji kuzungumza biashara wasiliana nami muda wowote. Nipo nchini Tanzania hadi mwenzi ujao baada ya hapa nita Rudi nchini Marekani”

Mwanamke huyu alizungumza huku akimkabidhi bussines card mkuu wa gereza.

“Hapana matata kabisa tuta ongea”

“Mpiganaji wako he is very handsome boy”

Mwanamke huyu alizungumza huku akinitazama kwa macho ya ishara fulani ya kimahaba. Akatoka ndani hapa nasi hatukukaa sana tukatoka huku nikiwa nimevalia kofia niliyo ishusha chini kidogo kwenye uso wangu na sio rahisi kwa mtu kunifahamu. Tukaingia kwenye gari na walinzi hawa wa mkuu wa gereza.

“Nisubirini nina kuja”

Mkuu wa gereza akaondoka na kuniacha na walinzi wake hawa. Mmoja akiwa amekaa siti ya dereva na mwengine akiwa ameka siti ya nyuma na mimi. Kumbukumbu zangu zote zipo kwenye vitendo vya makamu wa raisi na mke wangu halali wa ndoa ya kiislamu. Hakika moyo wangu una uma kupita maelezo, akili yangu yote ina tamani kumuua makamu wa raisi ila kitu kinacho nizuia ni kwamba hadi leo hii sifahamu hali ya mama yangu na mwanangu. Laiti kama ninge fahamu wapo sehemu salama, haki ya Mungu leo ningeondoka na kichwa cha makamu wa raisi na isitoshe nipo gerezani hivyo sihofii kufungwa.

“Hata tuondokeni sasa”

Mkuu wa gereza alizungumza mara baada ya kuingia ndani ya gari akiwa na tabasamu pana sana. Safari ikaanza huku ukimya ukiwa ume tawala ndani ya gari hili. Sikuhitaji kufungua kinywa changu kwa maana hasira yangu ina endelea kuchemka ndani kwa ndani.

“Chidi”

“Naam”

“Umefanya kazi nzuri sana”

“Asante”

“Nime wasiliana na rafiki yangu mmoja yupo Dar es Salaam. Ameweza kuonana na mama yako na mwanao, kesho atawaleta uje kuoanan nao”

“Siwezi kuonana nao nje ya gerezani?”

“Hapana na ume sikia pale makamu wa raisi kesho ana ziara gerezani kwetu. Yaani ni bora alivyo lewa ameniambia kwa maana nilikuwa sijui chochote.”

“Nashukuru kwa hilo”

“Alafu yule mzee mshenzi sana. Ila Chid pambana mwanangu, ukifanikiwa kutoboa hii miaka miwili na nusu iliyo baki, nakuhakikishia kwamba uta fika mbali, kwa maana ana chukua mke wa mtu hivi hivi, yaani hata mimi roho imeniuma”

“Mkuu”

Dereva aliita kwa sauti ya chini kidogo.

“Naam”

“Una taka kuniambia kwamba yule mwanamke ni mke wa Chidi?”

“Yaaa, mwanangu hapa alikuwa na mke kisu sana yaani hadi watu wa juu wame muona sio mchezo”

“Naombeni hizo stori ziishe”

Nilizungumza kwa sauti iliyo jaa mikwaruzo itokanayo na hasira.

“Ohoo sahamahi”

Tukafika gerezani, tukiwa katika kutembea nika muibia mkuu wa gereza bussines card aliyo pewa pasipo yeye wala walinzi wake kuona chochote.

“Vipi Chidi tukuletee kikata kiu?”

“Sihitaji mtu yoyote leo. Nahitaji kuwa peke yangu”

“Hakuna shaka mzee”

Nikaelekea katika chumba changu. Nikalitupia begi la nguo kitandani, nikaufunga mlango huu kwa ndani kisha nikaingia bafuni na kuoga, nikarudi chumbani na kukaa kitandani. Nitoa pesa hizi ndani ya begi ambazo ni laki tatu. Nikatenga kiasi cha laki mbili na nusu kwa ajili ya kumpatia mama yangu na kiwango cha elfu hamsini kwa ajili ya kuwalipa wahuni wa humu gerezani ambao hawaogopi kufa, kuhakikisha wana fanya vurugu kipindi makamu wa raisi atakapo tia miguu yake eneo la ndani la gereza hili.

‘Lazima nimfanyie kitu sicho’

Niliwaza huku nikijizala kitandani na kupanga mipango ya namna gani ambavyo makamu wa raisi ana weza kudhalilishwa na wafungwa wezangu.

Asubuhi na mapema nikatembelea aneo wanalo fanya usafi kikundi cha wahuni wanao jiita Mamba. Wahuni hawa wapo sita na wote ni watu walio randuka kiakili kiasi cha kuogopwa na kila mfungwa hapa gerezani ila mimi pekee ndio ninaye weza kuzungumza nao kiustarabu kwa maana wana nikubali toka siku nilipo muua Zumo kikatili.

“Mwananaaaaa kula gwara”

Mmoja wao alizungumza mara baada ya kuniona. Nikapena nao tano wote sita kisha wakaacha kufanya kazi huku wakinitazama.

“Mwana niaje jana usiku ulitoka?”

“Yaa kuna ndezi mmoja wa kimarekani, nime mdanjisha”

“Woyoooooo pwaa pwaaaa, ndio maana tuna kukubalia aisee, hunaga kuremba alafu hujisikia wala huna uonevu, ila kuna lile jibupa ulilo liua, kum**a**eee zake likukuwa lina one asana watu”

Walizungumza kwa furaha sana.

“Sasa nisikilizeni wana”

“Ehee tuambie mkali wetu”

“Kuna chok** ana kuja leo hapa gerezani. Ni mtu mkubwa mkubwa serikalini ana kuja kututembelea. Sasa nina taka mumuonyeshe kwamba nyinyi ni mamba tena ni Black Mambaaaaa alafu nina watoa kitu cha hamsini, ishirini hii hapa na jiwe tatu mara baada ya kazi kuisha tumesomana”

“Mamaeee hilo limekwisha mwanangu, yaani Chidi eheee. Hilo umelileta kwa wenyewe si unajua sisi sio ndezi”

“Yaa nina wajua”

“Basi huyo chok** ata juta kwa nini ameleta msambwanda wake hapa gerezani. Je una taka tumtie mabeto au tumfanye nini?”

“Yaani mzalilisheni ni kiongozi wa serikali na ata kuwa na walinzi ila hakikisheni kwamba muna mzalilisha tume elewana”

“Usiofiee jemedari wetu kwa maana wewe ndio tuna kuelewa kuliko chok* yoyote humu ndani.”

“Mwake mwana”

Tukapeana tano na wavuta bangi hawa kisha taratibu nikaondoka huku nikiwa nimejawa na tabasamu kwa maana kasheshe atakalo kumbana nalo makamu wa raisi, ni Mungu mwenyewe ndio anaye jua.



“Hivi hawa jamaa una zungumza nao vipi?”

Ngoko aliniuliza huku tukielekea katika eneo lake la kufanya usafi.

“Kwa nini?”

“Una jua jamaa vichwa vyao wana vijua wao wenyewe.”

“Naona nyota zetu zime endana”

“Rashidi una mgeni”

Mmoja wa askari aliniambia huku akinitazama. Moyo wangu ukajawa na furaha kubwa sana nikiamini kwamba leo nina kwenda kuonana na mama yangu pamoja na mwanangu.

“Nakuja”

Nilimuambia Ngoko huku nikiondoka eneo hilo kwa mwendo wa haraka kumfwata askari anapo elekea. Nikaelekea katika eneo maalumu la kuzungumza na wageni wana watembelea wafungwa. Eneo hili lime tenganishwa na kioo kigumu kati ya eneo wanalo kaa wafungwa na wageni wanao tutembelea.

“Mgeni wangu yupo wapi?”

Nilimuuliza askari aliye nileta eneo hili. Askari hakunijibu chochote zaidi ya kufunga mlango wa chumba hichi. Mlango wa eneo la pili likafunguliwa. Sikuamini macho yangu mara baada ya kumuona mke wangu akiingia huku akiwa ana tembea kwa madaha. Nikaanza kumtazama kuanzia chini mpaka juu. Akavuta kiti ya usawa nilipo mimi na akakaa taratibu, akanitazama kwa macho ya dharau ambayo hapo awali sikupata kuyaona. Akachukua mkonga wa simu ulipo pembeni yake kwa maana ili tuweze kusikiana ni lazima tutumia mikonga hii ya simu. Kwa ishara akaniomba nichukue mkonga wa simu ili nizungumze naye. Nikachukua mkonga wa simu hiyo na kuuweka sikioni mwangu.

“Haloo Chid, nakuona unavyo zidi kupauka”

Sikumjibu chochote zaidi ya kumtazama kwa macho yaliyo jaa uchungu.

“Nimekuja na mume wangu, yeye ana pita huko kuwatembelea nyinyi wafungwa, mimi nikaona nipate muda wa kuzungumza na wewe”

“Mariam”

Nilimuita mke wangu kwa sauti nzito ambayo sikutarajia kama ina weza kunitoka katika koo langu hili.

“Ohoo nimesahau kukuambia jina langu kwa sasa sio Mariam tena. Nina itwa Anna na mwezi unao fwata nina kwenda kufunga ndoa nchini Ufaransa”

“Hivi umechanganyikiwa au umerogwa wewe?”

“Mtu aliye rogwa ana muonekano kama wangu. Yaani hata tukimuuliza mtu kwamba mimi na wewe ni nani aliye rogwa una hisi ata mnyooshea kidogle nani?”

Mke wangu alizungumza kwa dharaua kubwa sana hadi machozi yakanimwagika.

“Kwa nini una nifanyia mimi hivi, ni kwa nini una nifanya nipitie kipindi kigumu kama hichi ikiwa una jua mama na mtoto wetu”

“Weeee koma tena zungumza kwa sauti ya chini. Sina mtoto na wewe, hapa nilipo nina jiandaa kwenda kumzalia mume wangu mtarajiwa hivyo wewe sahau kama ulizaa na mimi. Alafu usinililie kinafki nilikuja kukupa tu taarifa kwamba nami nipo katika hili gereza nime kuja na mume wangu. Alafu kitu kingine endapo uta nisumbua, basi tambua maisha ya mama yako na huyo panya buku wako wa kike wapo mkononi mwangu. Nita wafykelea mbali”

Mke wangu mara naada ya kuzungumza hivyo akasimama, akachukua pochi yake ya garama, akavaa miwani ambayo alivyo ingia hapa ndani alikuwa ameishika mkononi kisha taratibu akaanza kutembea kuelekea nje. Furaha niliyo ingia nayo ndani hapa yote imeniishia.

‘Amepatwa na nini?’

Ndio swali lililo anza kunitawala kichwani mwangu kwa maana mwanamke huyu nilimkuta kwenye maisha ya chini sana, maisha ya kuuza kachori, japo mimi mwenyewe nilikwa na hali mbaya ila mwenzangu alikuwa na mbaya zaidi yangu. Nikaamua kuanza naye maisha na kuishi naye nyumbani kwetu, katika kipindi chote alikuwa ni mtu wa kuniheshimu kunijali. Japo nilikuwa ni mwanaume mkorofi na anaye ogopwa kitaani kwetu ila aliweza kunibadilisha hadi nikaachana na magenge ya wahuni ambao nilikuwa nina waongoza na kuamua kuwa mlinzi wa kuajiriwa na hadi tuna pata mtoto wetu wa kwanza Shamsa, aliendelea kuniheshimu na kunijali.

‘Kama ni pesa ina weza kumbadilisha mtu, mbona kuna kipindi wanaume wenye magari yao walikuwa wana mtongoza ila alikuwa ana wakataa. Amekumbwa na nini mama Shamsa’

Niliendelea kulalama huku machozi yakinimwagika. Taratibu nikasimama na kutoka ndani hapa, hata askari mwenyewe aliweza kuniona jinsi nilivyo vurugwa.

“Chidi kuna tatizo?”

Askari aliniuliza kwa sauti ya chini.

“Hakuna shaka”

Nilizungumza kwa sauti ya kukata tamaa. Nikakutana na rafiki yangu Ngoko, kunitazama tu usoni akatambua kwamba kuna tatizo.

“Vipi mbona una sura ya majonzi?”

“Usijali mwana”

Nilizungumza huku nikishusha pumzi nyingi. King’ora cha kukusanyika mstarini kikagongwa na wafungwa wote tukaanza kupanga mistari kwenye eneo maalumu la kusimamia. Nikaka katika mstari wa mbele, kabisa huku tukisubiria kutangaziwa tulicho itiwa. Akasimama mkuu msaidizi wa gereza.

“Leo tume pata ugeni wa makamu wa raisi. Hivyo nita hitaji muwe na heshima katika kila sehemu atakayo pita kwa ajili ya kututembelea. Tumeelewaa?”

Wafugwa wakaitikia.

“Viongozi wa sello tokeni mbele”

Viongozi wa vymba wakatoka mbele.

“Nyinyi ndio muta kuwa wawakilishi wa matatizo yaliyopo hapa gereznai kwa makamu wa raisi tuna elewa?”

“Ndio”

Baada ya maelekezo hayo tukaruhusiwa kutawanyika jambo lililo nifanya nikae kimya kwa sekunde kadhaa hukku nikipiga mahesabu ya haraka haraka.

“Chid”

“Eheee”

“Mbona umeshikwa na bumbuwazi?”

Ngoko aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Hakuna shaka”

Nikaanza kujipenyeza katikati ya wafungwa wezangu. Nikawaona jamaa wa kundi la Mambas.

“Aisee Chid kila kitu kipo fiti kali kiti”

“Poa wana naamini mume jiandaa vya kutosha”

“Vibaya sana, wewe mwenyewe uta tukubali”

“Kikubwa ni kuwa makini”

“Usijali hilo chalii wetu”

Nikaachana nao, nikatafuta sehemu na kukaa huku nikisubiria kwa hamu ujio wa makamu wa raisi. Ulinzi ukazidi kuimarishwa hadi sisi wenyewe tukaanza kuingiwa na hofu kwa maana askari magereza kidogo wakaka kando, hawa walio ingia ni wanajeshi wenyewe wakiwa wamevalia majaketi ya kuzuia risasi na makofia magumu. Kila mwanajeshi ana bunduki ambayo sifahamu ni bunduki za aina gani kwa maana sina ujuzi sana kwenye maswala ya silaha na hata kwenye kampuni yetu silaha ambazo tulikuwa tunapewa na kupewa mafunzo nazo ni magobore tu na wale wenye kiwango cha juu walikuwa wana fundishwa kutumia SMG.

“Mmm ina maana makamu wa raisi ana ulinzi mkubwa kiasi hichi?”

Ngoko aliniuliza kwa sauti ya kunong’oneza.

“Mambo yanabadilika ndugu yangu”

“Kweli aisee”

Baada ya lisaa moja makamu wa raisi akiwa ameongozana na walinzi walio valia suti nyeusi wapatao ishirini pamoja na askari magereza akiwemo mkuu wa askari magareza wakaanza kupita maeneo mbalimbali ya gereza hili huku wakiwa wameongozana na waandishi wa habari.

“Nahisi ata kuwa amekuja kukagua miradi ndani ya gereza hili?”

Ngoko alizungumza ila sikumjibu chochote kwa maana ninacho kikumbuka ni jinsi na namba ambayo makamu wa raisi alivyo kuwa ana mchezea chezea mke wangu jana usiku.

‘Ipo siku uta kuja kuingia mikooni mwangu wewe fala’

Niliwaza huku nikimtazama kwa mbali kwa macho yaliyo jaa hasira kali sana. Baada ya makamu wa raisi kuzunguka eneo zima, kikapigwa king’ora cha wafungwa wote kusimama mstarini. Tukatii na safari hii nikasimama eneo la katikati kwa maana endapo nitasimama mbele basi nina weza kujikuta nikifanya tukio ambalo sijalitegemea kulifanya kwa maana kwenye maisha hakuna kitu kinacho uma kama kuibiwa mke wa ndoa.

“Nime furahi sana kuwaona.”

Makamu wa raisi alizungumza huku akiwa na kipaza sauti.

“Nita hakikisha wenye mashauri yenu ambayo bado yapo mahakamani, yana sikilizwa kwa haraka kama ni kuachiwa huru basi muweze kuachiwa huru na kama kuhukumiwa basi muhukumiwe kwa kifungu cha sheria kwa maana nina sikia kuna baadi tenu mume letwa humu gerezani pasipo kusomewa mastaka. Polisi wakidai kwamba wana endelea kufanyia uchunguzi kesi zenu.”

Wafungwa wakashangilia.

“Tuta boresha mfumo wa malazi kwa maana nime tembelea kwenye baadhi ya vymba nime ona vina mapungufu mengi ikiwemo kuisha kwa magorodo na uhaba wa vitanda. Huduma za afya tuta ziboresha kuhakikisha kwamba muna kuwa na afya njema”

Wafungwa wakazi kushangilia gafla kifuko kilicho jaa kinyesi na mikojo kikatua kifuani mwa makamu wa raisi na kikampasukia kifuani mwake na kusababisha askari wake kumzunguka kwa haraka huku wakitazama ni nani aliye rusha kifuko hicho cha kinyesi. Kwa wingi wa wafugwa hawa ni jambo gumu sana kuweza kutambua ni nani aliye kirusha kwa maana kime rushwa katika kipindi wafugwa wote wakishangilia. Zikapigwa risasi mbili hewani na wafungwa wote tukalala chini huku mikono tukiwa tumeiweka katika visogo vya vichwa vyetu

“Nani aliye fanya upuuzi huu?”

Mkuu wa gereza alizungumza kwa kufoka sana. Makamu wa raisi akaondolewa eneo hili kwa kasi sana kwa maana hali ya hewa imesha haribika. Wanajeshi wakatuzunguka wafungwa wote huku waandishi wa habari wakiondolewa eneo hili.

“Kimetokea upande huu”

Mwanajeshi mmoja alizungumza na ikasababisha tulio kaa upande wa kulia turuhusiwe kutawanyika na walio kaa upande wa kushoto ambao wapo mia mbili hivi wakawekwa chini ya ulinzi.

“Ni kina nani walio rusha?”

Ngoko aliniuliza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.

“Sijui”

Nilimjibu kwa kifupi huku nikitafuta nafasi ya kuona ni wap makamu wa raisi ana pelekwa kwani kama tukio hilo likionekana kwenye tv ni tukio la aibu sana. Wafungwa wote tulio ruhusiwa tukaamrishwa kuingia katika vyumba vyetu huku wezetu ambao wame bakia nje hatujui wana fanywa nini.

“Chidi usitoke humu ndani kwako. Hayo ni maagizo ya mkuu”

Askari mmoja alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa”

Nikawasha tv na kuweka sauti ya chini sana, nikajaribu kutazama baadhi ya chaneli ila sikuweza kuona habari yoyote ya makamu wa raisi kutembelea gereza letu. Baada ya masaa mawili mlango wa chumbani kwangu uka gongwa, nikafungua na mkuu wa gereza akaingia.

“Hawa Mambas ni washenzi sana”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akikaa kwenye moja ya sofa. Nikastuka kidogo ila nikajitahidi kuficha mstuko wangu.

“Wame fanya nini?”

“Wao si ndio wame mrushia makamu wa raisi kile kinyesi”

“So wamekiri?”

“Yaa wao wenyewe wamekiri”

“Duu sasa wata pewa adhabu gani?”

“Una hisi kuna adhabu gani hapo zaidi ya kifo”

“Kifo!!?”

Niliuliza kwa mstuko sana.

“Ndio kifo na mbaya wame chukuliwa na wanajeshi. Yaani hao wana kwenda kuuwawa mbele ya safari, isitoshe imetazamwa rekodi yao wameonekana ni watu walio kuwa ni waalifu wakubwa sana. Hivyo ndio imesha kula kwao kwa maana lile ni tukio la kujaribu kumuua makamu wa raisi”

Nikajihisi uchungu sana kuwaingiza jamaa wa watu katika matatizo yanayo wagarimu maisha yao.

“Kwa maana kama ingekuwa ni silaga au bomu basi makamu wa aisi angekuwa amesha kufa muda huu”

“Duu”

“Ndio hivyo alafu kuna askari wana sema kwambe leo hii asubuhi walikuona una zungumza zungumza nao?”

“Ndio niliongea nao”

“Ulikua una ongea nao nini?”

“Mambo ya kawaida kuwapa salamu kw amaana jamaa wale ni waskaji zangu sana”

“Chidi, kama uliwaagiza wewe ni heri ukaa kimya kwa maana nina elewa kila kinacho endelea katika moyo wako. Hakuna mwanaume yoyote anaye weza kuibiwa mke wake na akashuhudia mbele yake kama jana pale hotelini alafu akaa asifanye chochote. Omba Mungu wasikutaje tu, nime zungumza kwa kuhisi hivyo kwa maana hisia zangu zime nituma hivyo. Endapo wakikutaja basi tambua makamu wa raisi ata kuua yeye mwenyewe kwa mkono wake mwenyewe, kwani hichi kitendo kime mkasirisha sana. Tumeelewana?”

“Ndio mkuu”

Nilijibu huku mapigo ya moyo yakinienda kasi sana kwa wasiwasi. Makamu wa raisi akanitazama kwa muda kidogo kisha akasimama.

“Mkuu vipi kuwaona mama na mwanangu?”

“Hilo jambo kwa sasa liache kwanza”

“Kwa nini mkuu?”

“Sio kwa nini mkuu? Bado wanajeshi na usalama wa taifa wana katika katiza humu gerezani bado wana fanya uchunguzi wa tukio lile. Una hisi kwamba familia yako ambayo mke wako mwenyewe ana taka kuingamiza”

“Umejuaje hilo?”

“Nimesikia kila maogezi yenu pale ndani. Kuna kamera inayo rekodi kila kitu. So una taka mama yako na mwanao waje kukuona muda huu alafu wakamatwe, fikiria mara mbili”

“Nime kuelewa ila si wapo salama?”

“Ndio”

“Basi nina omba nizungumze nao japo hata kwenye simu”

Mkuu wa gereza akanitazama kwa dakika mbili huku akionekana kutafakari jambo fulani akilini mwake. Akatoa simu yake na akaminya minya kwa sekunde kadha akisha akaiweka sikioni mwake.

“Ehee, vipi upo nao hapo?”

“Mpatie simu mama”

Baada ya sekunde kama tano hivi mkuu wa gereza akanikabidhi simu.

“Zungumza na mama”

Kwa haraka nikaichukua simu yake na kuiweka sikioni mwangu.

“Halooo”

“Rashid”

“Ndio mama ni mimi”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga.

“Ohoo mwanangu. Upo wapi na una endeleje baba?”

“Mama ni story ndefu. Ila vipi Shamsa yupo wapi?”

“Huyu hapa, Shamsa msalimie baba”

Kauli ya mama ikanifanya nizidi kujawa na uchungu moyoni mwangu.

“Shikamoo baba”

Sauti ya mwanangu ikausisimua mwili wangu wote, nikashindwa kujizuia na kujikuta nikilia kwa uchungu sana.

“Baba mbona una lia?”

“Hapana mwanangu. Una endeleaje?”

“Naendelea salama baba, mama upo naye hapo kwa maana bibi alisema umesafiri naye?”

Swali la Shamsa likanifanya nishushe pumzi ndefu sana kwa maana nina imani kwamba mama yangu alimdanganya mwanangu hivyo ili kumfanya asiwe ana tuulizia sisi mara kwa mara.

“Ndio mwanangu ila ametoka”

“Akija muambie nataka kuongea naye”

“Sawa mwanangu”

Japo mtoto wangu ni mdogo sana ila ni mtoto mwenye upeo mkubwa sana na kuishi uswalini nako kume msaidi sana kuchangamka katika kuongea.

“Mama muna endeleaje?”

“Mwanangu toka uondoke hali ni mbaya sana kwetu. Nyuma yetu ime pigwa X na tume pewa miezi mitatu tu tuondoke, hatujui tuende wapi mwanangu kwa maana wana sema wana hitaji kutanua barabara na sisi tupo eneo la ndani ya barabara hivyo tuta bomolewa”

Nikahisi mwili ukinyong’onyea kwa kuishiwa nguvu kwani nyumba hiyo ndio urithi wa pekee ulipo, endapo ita bomolewa ni wapi mama na mwanangu wata kwenda kuishi ikiwa mimi bado nina miaka miwili na nusu ya kukaa jela.



‘Ohoo Mungu wangu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikishindwa kujau nimjibu nini mama.

“Rashidi”

“Nina kusikia mama”

“Yaani hapa hata sielewi na nina hisi kisukari changu sasa kitaanza kunisumbua”

Mama alizungumza kwa sauti iliyo jaa majonzi.

“Mama usijali kila jambo lita kwenda vizuri, kwani kwa sasa mupo wapi?”

Kabla ya mama kunijibu chohote simu ya mkuu wa gereza ikakatika.

“Ime kata”

“Nahisi ni salio limekwisha. Uta zungumza nao baadae kwa sasa ngoja nikaangalie hao wapelelezi wa hili tukio wana semaje”

“Ila samahani sana mkuu nina kuomba sana tena sana uweze kumsaidia mama yangu na mwanangu”

“Usijali Chidi nita fanya kila liwezekanalo katika hilo”

Mkuu wa gereza akatoka ndani hapa na kuniacha nikiwa sijui nini cha kufanya. Nikakumbuka kiasi cha pesa nilicho nacho nikakitoa ndani ya begi na kutoka chumbani hapa ila askari mmoja aliyopo hapa mlangoni.

“Chidi sasa hivi wafungwa wote wapo ndani. Hakuna anaye rugusiwa kuonekana mazingira ya nje”

“Ila kuna…..”

Nikakatisha sentensi yangu kwa maana simuamini mtu yoyote kwenye swala la pesa. Mawazo yakazidi kuniandama kiasi cha kunifanya nijione ni mtu mwenye bahati mbaya sana. Jioni ya siku hii wafungwa hatukupata chakula kwa madai ya utovu wa nidhamu ulio weza kutokea na ikatubidi tulale pasipo kula chochote.

Asubuhi na mapema kama kawaida wafungwa wakasambaa katika maeneo yao ya usafi huku wanao kwenda kufanya kazi za nje wakipelekwa katika maeneo hayo ikiwa ni kupasua mawe huku nami nikielekea katika gym ya mazoezi kwa ajili ya kuendelea kujiweka fiti kwa kila pambano linalo kuja mbele yangu.

“Chidi mbona leo una mawazo sana”

Kocha wangu wangu wa mazoezi aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sipo sawa kocha”

“Kuna nini kinacho endelea?”

“Ni familia yangu kocha”

“Ime fanyaje?”

“Nyumba ya mama yangu ime pigwa X na ina karibia kuvunjwa, wanadai ipo eneo la barabara na walio ingia eneo la barabara hawalipwi fidia yoyote”

“Duuu pole sana”

“Nashukuru hapa nina shindwa kufahamu ni kitu gani kinacho endelea. Isitoshe mtoto wangu ni mdogo sana na kama unavyo fahamu juu ya mke wangu”

“Ila huyo mwanamke ni mbaya sana. Kama hata mwanaye wa kumzaa ana mfanyia mambo ya kipuuzi astahili kuwa mke”

Nikamuadhithi kocha kila kitu kilicho tokea kwenye pambano la juzi na namna nilivyo muona mke wagu akiwa na makamu wa raisi. Hadi nina maliza kumuelezea hayo kocha akatingisha kichwa kwa maana ni historia inayo umiza sana moyo.

“Chidi nisikilize mwanangu”

“Ndio”

“Jaribu kumsahau huyo mwanamke kwa sasa tutafute mbinu za jinsi gani tuna weza kuisaidia familia yako. Je ni rafiki yako yupi ambaye una muamini mtaani tukampigia simu awe ana itazama familia yako kwa ukaribu”

Nikatafakari kwa muda kisha nika mkumbuka Rama, mskaji wangu ambaye tulikuwa wote toka utotoni. Ni mskaji ambaye tumefanya mambo mengi sana ya kihuni ila jambo la kumshukuru Mungu sote tuliweza kupata kazi na kuoa, yeye amepata kazi katika kampuni ya kuuza mikate huku mimi nikipata kazi katika kampuni ya ulinzi.

“Nimemkumbuka mshaji wangu mmoja ana itwa Rama.”

“Una ikumbuka namba yake”

“Ndio”

Tukaondoa hapa gym hadi kwenye moja ya choo kilichopo katika jengo hili la gym. Akanipatia simu yake ya siri, nikaingiza namba ya Rama na simu yake ikaanza kuita, nikajawa na tabasamu pana sana kusikia simu ikiitwa.

“Oi niaje mwanangu”

Nilizungumza kwa sauti ya furaha.

“Haloo nani mwenzangu”

Nikaisikia sauti ya kike iliyo nistua sana hadi nikajikuta nikiitazama namba hiyo mara mbilimbili.

“Ni mimi Chid”

“Ohoo shemeji, habari za masiku”

“Mungu ana bariki, yupo wapi mshakaji?”

“Rafiki yako nipo naye hapa ila amepata ajali ya gari juzi. Amevunjika miguu yote miwili ila hivi sasa amejipumzisha kwa maana dakttari ame mpatia dawa ya usingizi.”

Nikashusha pumzi nyingi sana kwani matumaini yangu yote yameingia doa.

“Aisee pole sana shemeji”

“Tumesha poa shemu, jambo la msingi ni kwamba bado ana pumua.”

“Alipata ajali eneo gani?”

“Kibamba gari lao la mikate liligongana uso kwa uso na lori la mchanga. Tandiboy wake amekufa na yeye ndio amevunjika miguu yote miwili”

“Akiamka basi mpe pole”

“Sawa shemeji. Alafu wewe upo wapi, nina sikia upo gerezani”

“Ni kweli shemeji nipo jela nime bambikiwa kesi”

“Pole sana shemeji yangu”

“Nashukuru shem”

“Sawa”

Nikakata simu huku nikiwa sijui nini cha kufanya. Nikakumbuka kumpigia mama, kwa bahati nzuri simu yake leo nika ikuta hewani.

“Shikamoo mama”

“Marahaba mwanangu. Jana simu yako ilikata?”

“Ndio mama. Upo wapi?”

“Tupo hapa nyumbani mwanangu bado hali ni ile ile nime anzisha mradi wangu wa kuuza sambusa hapa nje”

“Sawa mama nisikilize kwa makini”

“Ndio”

“Zile cheni si unazo?”

“Ndio”

“Nina kuomba ukauze cheni mbili na kila cheni moja haipungui zaidi ya lilioni mbili. Najua ukiiza hizo uta pata kitu kama milioni nne au tatu. Jaribu kutafuta chumba sehemu tofauti na hapo fungua mradi na Shamsa muanzishe chekechea”

“Sawa baba hata mim nilikuwa nime fikiria kufanya hivyo sema nilikuwa nina ogopa kuuza hizi cheni pasipo idhini yako na isitoshe sikuwa nina fahamu bei kwani ninge uza hata laki laki”

“Sawa mama ila hizo ni cheni original kabisa na ni garama sana. Uza kwa siri sana na usikubali kupata madalali wa kukuonyesha ni wapi kwa kuziuzia.Kariakoo si una ijua vizuri mitaa ile”

“Najua mwanangu, mimi mwenyewe japo ni mzee ila nina ijua mitaa vizuri”

“Basi fanya hivyo”

“Sawa mwangu, ila nina hitaji kukuambia jambo mwanangu”

“Jambo gani mama”

“Hata ikitokea nime kufa leo. Usije ukadhubutu siku hata moja kurudiana na mama Shamsa, sio mwanamke na laiti kama ninge jua kwamba ana kuwa mnyama na mshenzi kama hivi wala nisinge kuruhusu kumuoa”

“Nimekuelewa mama na mimi kurudiana naye wala haito kuja kaa itoke”

“Sawa mwanangu. Kuwa makini huko ulipo”

“Usijali mama”

Nikakata simu na kumrudishia kocha. Kidogo sasa nikaaza kupata amani moyoni mwangu, tukaendelea na mazoezi ya hapa na pele na baada ya kumaliza nikaendelea na ratiba za kawaida.

“Chidi una itwa na mkuu wa gereza”

Askari mmoja aliniambia, taratibu nikasimama kwa maana nimekaa na kundi la washkaji wangu wa gerezani. Nikaongozana na askari huyu hadi ofisini kwa mkuu wa gereza.

“Chid Chid Chid”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Ndio mkuu”

“Kwanza kaa hapo”

Nikaa kwenye moja ya kiti kilichopo mbele ya meza yake.

“Sasa wale wazungu waliweza kunipigia leo. Wamesema kuna pambano la kukupima uwezo wako, endapo uta shinda pambano hilo, utakuwa umejikatia tiketi ya kuelekea nchini Marekani ukawe professional kick boxer”

Habari hiyo ikanistua sana na kunifanya nijawe na tabasamu pana usoni mwangu.

“Pambano lenyewe ni lini mkuu?”

“Leo usiku. Kule kule hotelini, yaani wameniambia wata nilipa dola milioni moja kwa ajili ya kukuachia wewe na uta kuwa chini yao na mimi nita kufanyia makaretee uweze kuondoka huku jela. Una onaje hiyo ofa mwanangu”

“Ni ofa nzuri”

“Usimuambie mtu yoyote hata kocha wako. Ukijitahidi kwenye hili pambano kesho huto rudi huku gerezani, fanya kweli mwanangu”

“Nime kuelewa, ila si nina weza kuondoka na familia yangu”

“Hayo uta zungumza na hao mameneja wako wapya mimi nikikamilisha makubaliano nao na wakanilipa changu basi mwanangu ndio ume tusua. Ila nita kushukuru sana kwa maana katika kipindi kifupi sana ume yafanya maisha yangu kubadilika sana”

“Nami nina shukuru kwa ukarimu wako”

“Usijali Chidi kwenye maisha ni kusaidiana, nenda kajiandae na saa kumi na mbili tuta ondoka hapa”

“Sawa mkuu”

Nikaondoka ofisini hapa huku nikiwa na furaha iliyopitiliza. Nikarudi chumbani kwangu na kujiandaa vizuri sana, huku nikiwa nina ifikiria ndoto kubwa sana ambazo ninazo kichwani mwangu. Nikamtafuta rafiki yangu Ngoko na kumpa kiasi cha elfu hamsini.

“Ya nini hii Chidi”

“Ni shukrani yangu ya kuwa rafiki yangu bora hapa gerezani”

“Ngoja kwanza. Una achiwa huru?”

“Hapana siachiwi huru ila nina weza leo nisirudi tena hapa jela rafiki yangu. Nina pambano la kufa na kupona ambalo lipo mbele yangu, hivyo niombee”

Ngoko akajawa na sura ya huzuni sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Kwa nini huyu mzee ana yaweka maisha yako rehani kwa ajili ya manufaa yake binafsi”

“Usijali ndugu yangu. Mungu ndio anaye jua nini kinacho kwenda kuutokea ila nina kuomba sana uweze kuwa mwema hivyo hivyo rafiki yangu na nikipata nafasi ya kurudi gerezani basi kesho tuta kuwa pamoja”

“Nina kuombea kwa mwenyezi Mungu akutangulie rafiki yangu”

“Nashukuru”

Tukakumbatiana na Ngoko kisha nikaachana naye na kuelekea kwa kocha wangu. Nikampatia kiasi cha laki moja hadi yeye mwenyewe akashangaa.

“Kocha leo ni siku ambayo nina hisi ita kuwa ya mwisho kuonana na wewe”

“Una maanisha nini Chidi”

“Kuna pambano ambalo mkuu wameniambia, ila nina pata hisia mbaya juu ya pambano hilo kwa maana hilo ni pambano la kufa na kupona”

Kocha akakaa kimya huku akinitazama usoni mwangu kwa sura ya huzuni.

“Chidi”

“Ndio kocha”

“Hakikisha kwamba una kuwa makini na una rudi hapa ukiwa salama”

“Niombee kocha”

“Usijali sala zangu zipo pamoja nawe”

“Nashukuru”

“Pia nina shukuru kwa kiasi hicho cha pesa”

“Usijali”

Nikaachana na kocha na kurudi chumbani kwangu. Majira ya saa kumi na mbili jioni tukaanza safari kama, huku mkuu wa gereza akiwa na walinzi wake. Tukafika Pangani majira ya saa mbili usiku na moja kwa moja nikapelekwa katika chumba changu cha maandalizi. Hazikupita hata dakika kumi wale wazungu wawili, mwanamke na manaume wakaingia ndani ya chumba hichi huku wakiwa wameongozana na mkuu wa gereza.

“Habari yako Rashidi”

Mwanamke huyu wa kizungu alinizalimia huku akinipa mkono wa kulia. Tukakutanisha mikono yetu, cha kushangaza mwanamke huyu akanipapasa kwa kidole chake katikati ya kiganja changu.

“Salama tu”

“Nina itwa Claudia. Huyu ni meneja wangu ana itwa Brian. Tumeweza kupenda upiganaji wako na uwezo wako. Baada ya pambano nina imani tuta zungumza yaliyo mengi na tuna imani kwamba uta shinda”

“Mungu abariki”

Taratibu Claudi akanisogelea na kuninong’oneza sikioni mwangu.

“Ukishinda, usiku wa leo utafurahia ushindi wako na mimi. Usiniangushe”

Claudia akaniachia huku akitabasamu. Mara baada ya Claudia kutoka ndani hapa meneja wake, mkuu wa gereza akanigeukia huku akiwa ameshika sigara yake kubwa.

“Chidi, watoto wa kizungu hawa. Ukishinda hakikisha na chumbani una kwenda kuwakilisha nchi vizuri. Mpige miti hadi achanganyikie, ukifanikiwa hilo nakuambia mwanangu uta kuwa umetoka kimaisha”

“Nimekuelewa mkuu”

Nikajiandaa kwa kuvaa bukta yangu ya kupigania, nikavaa kinyago changu cha kuficha sura kwa maana sihitaji sura yangu iweze kujulikana. Nikamaliza kujiandaa kwa kila kitu, gafla mlango ukafunguliwa na makamu wa raisi pamoja na mke wangu huku wakiwa wameongozana na walinzi wake wakaingia ndani hapa.

“Mkuu kumbe bado upo?”

Mkuu wa gereza alizungumza kwa woga kidogo.

“Yaa nipo bado nina endelea kula bata, si una jua Tanga ni tamu sana”

“Ni kweli mkuu”

“Naona mpiganaji wako amesha jiandaa vya kutosha”

“Ndio mkuu”

“Juzi uliniambia kwamba akiwa ana toka kwenye mapigano huwa ana kuwa na hasira na hawezi kuzungumza chochote?”

Makamu wa raisi alizungumza huku mke wangu akiwa amemlalia begani mwake.

“Ndio muheshimiwa”

“Basi leo nataka kuzungumza naye kwa maana leo nasikia pambano ni kali sana na mimi nina penda mapambano makali.”

Nikatazamana na mkuu wa gereza ambaye ana wasiwasi.

“Kijana una itwa nani?”

Kwa habati mbaya nikawa nimeshau jina ambalo mkuu wa gereza alimtajia makamu wa raisi ile siku.

“Eti una itwa nani kijana?”

Nikajifikiria kwa sekunde kadhaa.

“Mashushu”

Nilijibu kwa sauti nzioto sana ambayo ikamfanya hadi mke wangu kunitazama kwa makini sana kwa maana ni kwa mara kadhaa nilikuwa nina muigizia kwa kuzungumza kwa sauti nzito kipindi tukiwa katika mapenzi motomoto.

“Ohoo Mashushu, hembu vua basi nione sura yako kwa maana wapiganaji kama nyinyi muna weza kulifaa taifa kwenye kushiriki mashindo ya Olympic na ukatuletea medali ya dhababu au una semaje jamaa yangu?”

Mimi na mkuu wa gereza tukastuka sana kiasi cha kutazamana.

“Mashushu hembu nikione basi jamaa yangu. Vua kinyago chako”

Makamu wa raisi akazungumza kwa msisitizo kiasi cha kuwafanya walinzi wake kunisogelea na kutaka kunivua kinyago changu. Nikawazuia kwa ishara ya kuwaonyesha mkono wa kulia kwamba wasinishike na wakatii hilo. Nikamtazama mkuu wa gereza ambaye ana wasiwasi mwingi sana. Taratibu nikafungua mikanda ya kinyago changu huku nikiwa nime iinamisha sura yangu chini na taratibu nikaanza kukivua huku makamu wa raisi na mke wangu wakiwa na hamu kubwa sana ya kuiona sura yangu.

********



Gafla mlango ukafunguliwa na akaingia refarii na kwa haraka nikakakirudisha kinyago changu usoni pasipo mke wangu pamoja na makamu wa raisi kuiona sura yangu kwani nyuso zao wamezielekezea kwa refarii huyu.

“Jamani muda wa pambao umesha fika. Baada ya dakika kumi nitatoa ushindi kwa mpinzani wenu”

Refa alizungumza huku akitutazama kwa sekunde kadhaa kisha akatoka ndani hapa.

“Ohoo sawa Champion wetu nenda kapambane”

Makamu wa raisi alizungumza huku akinipiga piga begani mwangu. Macho ya mke wangu yana jaribu kuni dadisi mwili wangu, ila kutokana na alama za majeraha ambayo niliyapata kutokana na vipigo vya polisi pamoja na mapambao mbalimbali, vimeufanya mwili wangu kuwa wa tofuati kabisa naule mwili ambao mke wangu alikuwa amezoea kuuona. Makamu wa raisi, mke wangu na walinzi wake wakatoka ndani hapa na kuniacha mimi na mkuu wa gereza na vijana wake wawili.

“Huyu mzee ni jipu sana”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akiwa na hasira.

“Chidi upo tayari?”

Mkuu wa gereza aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Ndio”

“Twende”

Tukatoka ndani hapa huku nikiongozana na mkuu wa gereza pamoja na walinzi wake. Tulipo eneo la karibu na ulingo wakaniacha na wao wakatafuta siti za kukaa.

‘Ehee mwenyezi Mungu nina kuomba ukanisimamie kwenye hili’

Nilizungumza huku nikionyosha vidole vyangu viwili hewani huku nikiendelea kumuomba Mungu kimoyo moja. Nikaingia katika ulingo huu ulio zungushiwa nyavua na kuwa kama banda. Watu wote wakasimama na kuanza kupiga makofi. Mpinzani wangu, hana mwili wa kutisha ila ana onekana ni mtu wa mazoezi, kwa kumtazama kwa haraka haraka asili yake ni mtu wa China na kama sio chini basi ni Mjapani kwa maana watu hao wana fanana fanana sana. Refarii akatuita na tukasimama karibu naye huku tukitazamana.

“Pambano hili ni la kupigana hadi mmoja atakapo shindwa ndipo shindano litakapo isha. Mbinu zote zina ruhusiwa katika pambano hili hivyo ina wapasa kutumia kila aina ya uwezo wenu kuhakikisha una shinda pambano. Peaneni mikono”

Tukagongesheana ngumi na mpinzani wangu huyu anaye onekana yupo fiti kisawa sawa. Kengele ikagongwa na pambano likaanza. Mpinzani wangu akaanza kunishambulia kwa kasi sana kiasi cha kuninyima hata namna ya kufanya shambulizi lolote. Uwezo wake wa kunishambulia kwa mateke na ngumi, ukazidi kunipa wakati mgumu kwani ni kwa mara mbili mfululizo nikajikuta nikianguka chini kwa mateke yake.

‘Ehee Mungu nina fanyaje hapa?’

Nilijiuliza huku nikiwa nimelala chini kifudifudi nikimtazama mpinzani wangu anaye nionyeshea kidole cha kuniita niamke.

‘Chidi huwezi kushindwa. Huwezi kurudi jela tena hii ndio nafasi yako ya pekee ukivuka kikwazo hichi ume pita’

Nilijiambia nafsini mwangu mimi mwenyewe huku nikijivuta taratibu na kunyanyuka. Mpinzani wangu akaruka hewani huku akiwa ametanguliza mguu wake wa kulia mbele ambao amekusudia kunipiga teke la kifuani, nikamkwepa na akapita kama upepo.

‘Mmmm’

Nilijikuta nikiguna kwa maana laiti teke hilo lingenipata basi angenichangua kifua changu. Akiwa katika harakati za kugeuka, nikamzaba konde zito la ngumi eneo la shingoni mwake na kumfanya aweweseke huku akiwa hajielewi, nami nikapata wasaa wa kumtawala. Kila nilicho jaaliwa katika upiganaji wangu nikakitumia wakati huu, ngumi mateke, vichwa. Mpinzani wangu akaanza kuwa na wakati mgumu sana, nikamtandika ngumi mbili za jicho la kulia na kumfanya ashike jicho lake huku akizidi kuweweseka. Nikamchota mtama akaanguka chini, sikutaka kumpa nafasi kama aliyo kuwa ananipa yeye na kujivumilia chini nilipo anguka. Nikaanza kumpiga vigoti vya mbavuni mwake huku nikiamini kwa mapigo haya ya hapa chini nina kwenda kummaliza haraka sana. Gafla akanipiga ngumi sehemu zangu za siri, maumivu niliyo yahisi aisee yakanifanya nigairi kufanya kila kitu na kujishika sehemu zangu hizi za siri huku nikigugumia maumivu makali.

Mpinzani wangu akasimama huku uso ukiwa unachuruzika damu kwa maana kuna ngumi kadhaa nilimpiga usoni na kumpasua.

Akanipiga ngumi ya kichwani na kunifanya nianze kuhisi nyota nyota, macho yangu yakaanza kupata ungungu, hata mpinzani wangu siwezi kumuona vizuri.

‘Chidi mwanangu pambana. Huu ndio wakati wako’

Niliihisi sauti ya mama kwenye nafsi yangu. Nikastukia nikilala chali na mpinzani wangu akanikalia kiunoni mwangu na kuendelea kunishambulia kwa ngumi nzito nzito za usoni. Nikazidi kujikinga uso wangu kwa mikono.

‘Baba pigana’

Niliihisi sauti ya mwanangu Shamsa ikiniongelesha. Nikatupia jicho eneo alilo kaa mama Shamsa na nikamuona akiwa ametokwa na macho huku kila ngumi ninayo pigwa uso wake una kuwa una pata ishara ya maumivu. Mpinzani wangu akanipiga kabali moja takatifu, watoto wa mtaani tunaiita kabali ya mbao, ambayo ukiotewa kukabwa hiyo usipo jitutumua na kujitoa basi tambua kinacho fwata hapo ni kuzimia. Jicho likanitoka kwa maana jamaa ameibana shingo yangu kisawa sawa. Nikaanza kuitoa mikono yake huku nikifurukuta hapa chini kwa maana yeye amelala nyuma yangu huku miguu yake akiwa ameipitisha kiunoni mwangu na kuibana mbele ya kiuno changu. Nikafanikiwa kupata upenyo wa kuufikisha mkono wake mmoja kwenye eneo la mdomo wangu.

‘Usinitanie’

Nilizungumza kimoyo moyo kisha nikaanza kumng’ata mkono wake huo. Japo anajifanya haisi chochote, nikazidisha kuung;ata hadi damu zikaanza kumwagika. Uvumilivu wa maumivu ukamshinda na akajikuta akiniachia huku akibingirika pembeni. Nikaanza kuhema sana kwani kabari aliyo kuwa amenikaba ilikuwa ina nimalizia pumzi yangu.

‘Mungu nisaidie’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiwa nimechoka sana. Katika mapambano yangu yote niliyo pigana hayakuwa magumu kuliko hili. Hakika hili mpinzani wangu yupo vizuri na haitaji kunipatia nafasi ya kumshinda. Nikanyanyuka tartaibu huku nikihema sana, mpinzani wangu naye akanyanyuka na tukatazamana.

‘Ukiwa una pigana na mtu ambaye ame kuzidi maarifa. Ina bidi uhakikishe kwamba una pigana kuhuni, sheria za ulingoni na mbinu za ulingoni zote una ziweka pembeni na una pigana kihuni’

Niliyakumbuka maneno ya kocha wangu. Kupigana kuhuni ni zile ngumi za mtaani ambazo huna kujipanga wala kumkalia mpizani wako mikao ya kupigana. Mukishikana ni kukung’utana hadi atakeya shindwa basi ana kuwa ameshindwa. Mpinzani wangu akaanza kuyumba yumba huku akizunguka uwanja huu. Staili kama hizi niliwahi kuziona kwenye filamu za kina Jack Chaine.

‘Huyu fala mseng** kweli ananiletea maswala ya drunking master hapa’

Nilizungumza huku nikimtazama ata fanya nini, akaruka sarakasi hewani, kabla ya kutua chini nikamsindikiza kwa teke zito lililo mfanya aanguke chini kama gunia. Nimamvaa kuanza kumiga ngumi za kila aina. Nikazishika nywele zake ndefu ndefu na kuanza kuubamiza uso wake kwenye sakafu ya ulingo huu. Nikaushika mkono wake wa kulia na kuupitisha katikati ya mguu yangu nika uzungusha kwa nguvu zangu zote kwa kutumia miguu na nikasikia mifupa ikamvunjika. Mpinzani wangu akalia kwa nguvu sana huku akipiga piga mkono wake wa kushoto chini akiashiria kwamba ameshindwa na pambano. Refarii kwa haraka akaniachanisha naye huku akininyanyua mkono wangu wa kulia juu akishiria kwamba nime shinda. Machozi ya furaha yakaanza kunibubujika, hakika sijategemea kama nina weza kushinda pambano hili ambalo lilikuwa ni kali na zito kwa upande wangu. Watu wote uwanjani wakasimama na kuanza kunipigia makofi huku wengine wakishindwa kuficha furaha hususani Claudia ambaye ame kaa viti vya mbele kabisa. Mkuu wa gereza akaninyooshea dole gumba kwa mbali huku nikimuona naye akichuruzikwa na machozi ya furaha.

‘Nime fanikiwa, nimefanikiwa, asante Allah, asante Mungu’

Nilizungumza kimoyo moyo kwa furaha nyingi sana. Nikamtazama makamu wa raisi pamoja na mke wangu nao nina waona wana shangilia, nikamnyooshea kidole makamu wa raisi kisha nikakunja ngumi na kumfanya apige makofi akihisi kwamba nime mpa ishara ya kwamba nime shinda. Kumbe kimoyo moyo nina uchungu na hasira naye na siku nikibahatika kumshika mkononi mwangu, nita mvunja vunja hadi afurahi na roho yake. Nikamshuhudia mpinzani wangu akitolewa uwanjani hapa na wachina wezake wawili.

“Hongera sana kijana, nimekuwa refa katika mapambano mengi sana yana pita hata mia moja. Ila katika mapambano haya yako mawili, hususani hili la mwisho, nikiri sijawahi kuona mpambanaji kama wewe, hususani Mtanzania”

“Nashukuru sana”

“Endelea kuwa hivi, nina ona uta fika mbali sana”

“Asante refa”

Nikainama pande zote nne za ulingo huu ikiwa ni ishara ya kuwapa heshima watazamaji wote ambao ni watu na mapesa yao na ukitazama kwa haraka haraka hakuna kapuku hata mmoja aliye hudhuria. Nikatoka katika ulingo huu na kuanza kujikongoja kuelekea katika chumba cha maandalizi. Walinzi wa mkuu wa gereza wakanifwata huku nyuso zao zikiwa na furaha kubwa sana.

“Dogo hongera sana”

“Nina shukuru”

“Aisee kuna kipindi tulijua una shindwa bwana”

“Mungu tu amenisaidia”

Tukaingia ndani hapa.

“Naombeni muda wa dakika tano nisali kwa kuiepuka kifo kwa maana sikutegemea kama nita toka hai kwa mpinzani wangu”

“Sawa”

Walinzi wa mkuu wa gereza wakatoka ndani hapa na kuniacha peke yangu. Nikapiga magoti chini na kuanza kuswali kwa taratibu za dini yetu ya kiislam. Nikamaliza kiswali na nikawaruhusu walinzi hawa kuingia ndani hapa. Mkuu wa gereza akaingia ndani hapa akia ameongozana na makamu wa raisi, mke wangu na walinzi wake.

“Hongera sana kijana”

“Nina shukuru”

Nilimjibu kwa sauti nzito ambayo mke wangu alizidi kuidadisi.

“Aisee huyu dogo mfanyie mpango aingie jeshini. Na kule jeshini ata pata kuungana na timu ya jeshi inayo kwenda kushiriki mashindano ya Olympic ya mwaka huu”

“Nime kuelewa sana muheshimiwa”

“Mashushu, hii ni bussines card yangu. Ina namba nne hapo, moja ya kwanza ni ya kiofisi, hizo mbili zinazo fwata ni za hapa Tanzania na hiyo ya chini ni ya nchini Ufaransa kwamaana kule ndipo yalipo makazi yangu na huyu baby mama hapa”

“Shukrani sana muheshimiwa”

Nilizungumza huku nikizikariri namba hizo kwa haraka sana. Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba nina uwezo mkubwa sana wa kukremisha mambo.

“Ukiwa na shida yoyote, wewe nipigie alafu niambie muheshimiwa mimi ni mashushu basi nita kukumbuka”

“Asante sana mkuu”

“Haya niwatakie usiku mwema. Mimi na mke wangu tuna rudi Dar es Slaam usiku huu kwa ndege, hivyo hatuna muda wakuendelea kuka hapa”

“Asante mkuu kwa kuwa nami. Nina imani ipo siku tutakutana tena”

Nilizungumza huku nikimtazama makamu wa raisi pamoja na mke wangu kwenye nyuso zao.

“Yaa ni lazima tuta kutana”

“Pia hongera muheshimiwa”

“Hongera ya nini?”

“Una mwanamke mzuri sana. Mtunze, mjali na kumthamini kila wakati. Hakikisha asidondoshe chozi lake kwa ajili yako”

“Hahaa hilo haliwezi tokea. Nina mpenda sana ANNA wangu. Alafu mashushu wewe ni jasiri sana kwa maana hakuna mtu ambaye ameweza kunieleza hilo jambo siku hata moja. Ila asante sana na niwatakie usiku mwema”

“Nanyi pia”

Mke wangu akayatazama macho yangu kwa makini sana kisha akatoka ndani hapa. Nikaamini kuna kitu ata kuwa amekigundua machoni mwangu kwani, siwezi kuficha kila kitu, kama sura nime ificha ila macho ni ngumu sana kuyaficha, hususani kwa mwanamke niliye kaa naye kwa miaka zaidi ya sita sasa.

Claudia na meneja wake wakaingia ndani hapa.

“Kazi nzuri sana Rashidi”

“Nina shukuru”

Nilizungumza huku nikivua kinyago changu.

“Una weza kujiandaa na sasa tuka zungumza biashara”

“Hakuna shaka”

“Nina imani mkuu wako ata kuleta chumbani kwangu”

“Sawa”

Claudia na meneja wake wakatoka.

“Rashidi”

“Naam”

“Hongera sana na nina tamani uendelee kuwa nami ila ila bahati ime kuangukia. Ila katika historia yako kuna kitu nimejifunza hata vijana wangu munisikilize”

Mkuu wa gereza alizungumza na sisi wote watatu tukakaa kimya na kumtazama. Akavuta fumba la mosho wa sigarate yake kisha akanitazama.

“Sio kila tatizo ni tatizo, mengine yame kuwa ni madaraja ya kufanikiwa. Laiti kama lile tukio la kijambazi lisinge tokea kwenye lindo lako, na huyu jipu kama asinge kuchukulia mke wako na kukuagiza uletwe huku gereza la Maweni nina inamni kubwa sana, usinge weza kujua kipaji chako wewe ni nani na wala usinge pata nafasi kama hizi. Hivyo shukuru kwa haya matatizo yame kufanya leo hii, maisha yako yaende kubadilika kwa asilimia mia kubwa sana”

Mkuu wa gereza alizungumza na kunifanya nitingishe kichwa nikiamini alicho kizungumza.

“Yaani nina fananisha na kisha cha kwenye bibilia kinacho muhusu Yesu. Laiti kama binadamu tusinge kuwa na dhambi na maovu, basi asinge kuja duniani. Ila kutokana na maovu yetu akaletwa duniani kuokoa dhambi zetu na aliteswa msalabani na hadi leo jina lake lina abudiwa. Nina kuahidi Rashidi ipo siku watu walio kuwa wana kudharau wata kuabudu, wata ivaa picha yako kwenye nguo zako, wata kuweke kwenye profile zao za Whatsapp,Instergram, Twitter, Facebook na kwingineko na jina lako wata zidi kulitukusa. Jambo la msingi na kuzingatia hakikisha kwamba una kuwa naeshima kwa kila mtu, mpende kila mtu. Basi uta fanikiwa na utazungumziwa duniani kama wapiganaji hodari na mahiri. Umenielewa mwanangu?”

Mkuu wa gereza alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa hekima kubwa sana na leo ndipo nikagundua mzee huyu ana hekima sana japo ananidhulumu pesa zangu ila roho ya upendo ndani mwake.

“Nime kuelewa mzee wangu”

“Jiandae nikupeleke kwa Claudia meneja wako mpya”

Nikaingia bafuni, nikaoga haraka haraka, nikatoka ndani hapa na kukuta nikiwa nime wekewa suti mpya juu ya kitanda cha chumba hichi.

“Hii suti nilikununulia mchana, nina imani ita kutosha”

Mkuu wa gereza alizungumza huku akitabasamu. Toka nitoke tumboni mwa mama yangu, sikuwahi kuvaa suti na watu walio kuwa wakivaa suti kitaani kwetu tuna waita watoto wa kishua.

“Nina shukuu sana muheshimiwa”

Nikaivaa suti hii yenye rangi ya dark blue na shati jeupe.

“Imekukaa vizuri kama mzee amekupima vile”

Mlinzi mmoja alizungumza, huku akiniweka vizuri kola ya shati langu jeupe.

“Nashukuru”

Tukatoka ndani hapa na kuelekea katika chumba cha Claudia. Tukakaribishwa na meneja wake, mkuu wa gereza akapewa mkataba na akaanza kuupitia.

“Rashidi huu ni mkataba wa makubaliano ya kuuziana umiliki kati yangu na Claudia. Nime lipwa dola za kimarekani milioni moja. Nina tia saini hapa na kuanzia hivi sasa uta kuwa chini yake na yeye ndio ata kuwa ana kusimamia kwenye kila jambo na gerezani huto rudi tena. Sawa kijana wangu”

“Ndio mkuu”

Mkuu wa gereza akatia sahihi kisha Claudia akatia sahihi, meneja wake akatia sahihi, mlinzi mmoja wa mkuu wa gereza akatia sahihi na mimi nikapewa mkataba huu niupitishie macho ili nitie sahihi. Kutokana ume andikwa kingereza sikuhitaji kujisumbua kuusoma, nikatia sahihi yangu ya mcharazo kama dokta aliye kimbia chuo. Kisha nikamrudishia Claudia mkabata huo na akatabasamu sana huku akinitazama kwa macho yake ya kimahaba yaliyo nifanya niyakumbuke maneno ya mkuu wa gereza kwamba hata chumbani hapa ina nipasa niwakilishe taifa katika kumshuhulikia mwanamke huyu wa Kimarekani.



ENDELEA

Tukapeana mikono na mkuu wa gereza pamoja na walinzi wake kisha wakaaga na kuondoka eneo hili. Meneja wa Claudia naye akatoka ndani hapa na kuniacha na Claudia.

“Leo ina bidi tusherekee, ume pata uhuru wako”

CLaudi alizungumza huku akipiga hata hadi kwenye friji ndogo, akafungu na kutoa chupa mbili za bia.

“Una tumia hizi?”

“Hapana”

“Tumia bwana Rashid”

Claudia alizungumza kwa sauti ya kimahaba huku akifungua chupa moja na kunikabidhi. Akakaa pembeni yangu huku akinitazama.

“Ohoo pole ume umia sana. Je n ikupatia pain killer”

“Ikiwezekana”

Nilizungumza huku nikiiweka chupa hii ya bia mezani kwamaana kuchanganya pombe na dawa ni hatari sana. Claudia akanikabidhi vidonge viwili vya rangi ya pinki, akanipa chupa ndogo ya maji na nikavimeza. Ndani ya dakika tano maumivu yote niliyo kuwa nina yahasi yakatoweka.

“Rashidi ni kwa nini ulifungwa?”

“Nilisingiziwa kesi ya ujambazi ikiwa sijafanya kosa hilo”

“Ulishingiziwa?”

“Ndio”

“Kwani ulikuwa una fanya kazi gani?”

“Mimi nilikuwa ni mlinzi wa kampuni hizi za ulinzi.”

Nikaanza kumuadhithia Claudia kuanzia siku ya tukio hadi hapa nilipo.

“Aisee pole sana. Ni stori inayo gusa sana,”

“Nashukuru”

“Mimi nime vutiwa na wewe Rashidi, toka nilipo kuona siku ya kwanza, sikujali una kinyago usoni mwako. Ila nilivutiwa nawe. Ila mimi nipo ndani ya ndoa, nime olewa miaka saba iliyo pita, mimi na mume wangu hatujabahatika kupata watoto kabisa. Mimi na mume wangu tuna kampuni inayo husiana na maswala ya uwakala wa kutafuta wapiganaji wachanga, ambao tuna wakuza hadi kuwa ma professional wa ngumi za kupwa kabisa. Mume wangu ni tajiri mkubwa sana nchini Marekani.”

“Nashukuru kufahamu hili”

“Hata hii safari ya kuja Afrika ni kwa ajili ya kutafuta vijana wenye vipaji. Kuna mtu alinitumia clip yako hivyo nikawa na hamu ya kukuona na kwa bahati nzuri nime weza kuyashuhudia mapigano yako mawili. Naamimi uta kuwa mpiganaji mzuri sana. Kikubwa ni nidhamu hata unapo kuwa katika mahusiano na mimi hakikisha kwamba yana kuwa ya siri sana. Mume wangu asifahamu, tume elewana”

“Naweza kuuliza swali?”

“Uliza?”

“Je nisipo hitaji kuwa katika mahusiano na wewe?”

Claudia akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatabasamu.

“Rashidi”

“Naaam”

“Mimi ndio niliye kufanya uwe hapa kwa muda huu. Mimi ndio nita kufanya usahau umasikini na kuboresha maisha ya familia yangu. Ina kuwaje wewe ushindwe kuwa na mimi tena kisiri. Ukishindwa kuwa na mimi, nisiwe muongo, kila kitu kitaishi hapa na uta rudi gerezani”

Claudia akapiga fumba la bia hiyo kisha akasimama mbele yangu. Hapa ndipo nikajua kwamba nimesha kuwa mtumwa wa ngono kwa huyu mwanamke ambaye kwa haraka haraka umri wake una weza kufika miaka arobaini na ushee.

“Tumeelewana?”

“Ndio”

“Asubuhi tutaondoka na ndege kuelekea Arusha, mimi na wewe alafu Brian yeye ata kwenda Dar es Salaam kuonana na mama yako na tukiwa Arusha nita watafutia visa tukipata basi tuna kwenda nchini Marekani. Tume elewana”

“Ndio madame”

Nilizungumza kwa furaha kwa maana sasa maisha ya kuishi Bongo basi kwani nime jitahidi kupambana kwa miaka kadhaa kwa ajili ya kufanikiwa kimaisha ila sijafanikiwa.

“Naweza kukuomba kitu?”

“Niombe tu Chidi”

“Naomba niweze kumfahamisha mama yangu. Ili asishangae kuona ana tafutwa na mzungu, si una jua sisi wa Afrika kidogo bado tupo nyuma”

“Yaa ni kweli. Simu hiyo hapo tukifika Arusha nita kununulia simu mpya, nguo na kila kitu ambacho ana paswa kuwa nacho star kwa maana wewe una kwenda kuwa star”

“Nashukuru sana”

Nikachukua simu ya Claudia na kuiandika simu ya mama kwa haraka sana. Nikampigia na kwa bahati nzuri simu yake ikaanza kuita.

“Haloo”

Mama alizungumza kwa sauti iliyo jaa uchovu na usingi.

“Mama ni mimi Shikamoo”

“Marabaha Rashidi”

“Ndio mama”

“Mbona usiku sasa”

“Ni kweli kuna habari nina hitaji kukupatia”

“Habari gani?”

“Nime weza kupata mfadhali ambaye ana hitaji sisi wote watatu tuweze kuelekea nchini Marekani tukaishi huko”

“Ngoja kwanza, una ota au unacho kizungumza ni kweli?”

“Haki ya Mungu vile mama ni kweli”

“Usitake nipige kelele hapa”

“Kweli mama. Ila usimuambie mtu, kesho kuna mzungu ana itwa Mr Brian ana kuja kuwachukua na muta kuja naya Arusha”

“Sawa sawa mwanangu”

“Shamsa yupo wapi?”

“Amesha lala baba”

“Sawa asubuhi uta ni beep kwenye namba hii”

“Hakuna shaka mwanangu, mwenyezi Mungu azidi kukufungulia milango ya baraka na heri”

“Asante sana mama yangu”

Nikakata simu huku nikijawa na matumaini mapya ya maisha. Nikaiweka simu ya Claudia sehemu nilipo itoa na kwa haraka nikaitembea hadi sehemu alipo simama. Sikuhitaji kumuuliza maswali, nilicho kifanya ni kuanza kumnyonya denda huku chupa yake ya bia nikiitoa mkononi mwake na kuiweka pembeni. Nikamnyanyanyua Claudia na miguu yake akiipitisha kiunoni mwangu na kuibana kwa nyuma huku mikono yake akiipitisha mabegani mwangu na kuibana kwa nyuma.Tukaendelea kunyinyana denda, nilipo hakikisha kwamba nimerishika nikamlaza kitandani na kuanza kumvua gauni lake, nikaivua suti yangu hii na kuitupia pembeni. Nikaanza kumuonyesha mautundu ya uswahilini, sikuhitaji kumpaparikia mwana mama huyu, nikamuandaa kama nillivyo kuwa nina muandaa mke wangu. Taratibu Claudia akaanza kuomba nimpatie haki yake.

Nikamuweka mkao wa chura, na nikaanza kumpa dozi ambayo mkuu wa gereza alikuwa akini sisitizia kwamba nihakikishe kwamba nina wakilisha taifa. Nikambinua binua mwana mama huyu kila aina ya mkao ambao mingine akakiri kwamba ni migeni sana kwakena akazidi kukiri kwamba toka amjue mwanaume hajawahi kusugulia hadi akafika kileleni. Sifa zake zikazidi kuniongezea sifa na ujikuta nikizidisha mashambulizi hadi ikaifikia kipindi Claudia akaanza kuomba mapumziko kwa maana ana hisi pumzi ikimuishia. Nikampa mapumziko ya dakika kumi kisha tukaendelea na safari ghii nikajitahidi kufika kileleni mapema ili nisimchoshe akahisi kwamba nime mpania.

Usiku huu kwangu ni kama peponi, kwamaana ukiachilia kumfaidi mwana mama huyu ila nina lala kwenye chumba kizuri cha hoteli ambacho kwa mitaa yetu ya uswahili tumesha zoea gesti zetu bubu za elfu tatu tatu ambazo ukiingia na demu lazima ujue ni lazima waskaji wata kula chabo madirishani.

Asubuhi tukapata kifungua kinywa muruwaa, na baada ya hapo, Claudia akampatia maagizo Brian ya jinsi ya kuwasiliana na mama yangu na nikampigia mama na akazungumza na Brian. Jambo la kumshukuru Mungu Claudia na meneja wake wana zungumza kiswahili fasaha hivyo ni rahisi kuzungumza na watu kama sisi ambao shule tuliziona hazina umuhimu kwa kipindi hicho. Tukaianza safari ya kuelekea Arusha huku ikiwa ndio mara yangu kupanda ndege.

“Leo ndio mara yako ya kwanza kupanda ndege?”

“Yaaa, hapa karoho kana kwenda spidi kidogo”

Claudia akatabasamu.

“Usijali baby, uta zoea na yatakuwa ni masiha yako ya kawaida. Ukijitahidi na kufanya kazi kwa bidii uta ishi kama kina Mywether”

“Duu hao watu nina wasikia tu”

“Uta kutana nao kwa maana utakapo vuma watakuwa ni watu wa kawaida sana kukutana nao”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile”

“Nitafurahi sana”

Tukafika Arusha ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kufika. Tukaelekea kwenye moja ya hoteli ya kitalii, Claudia akapangisha vyumba vitatu. Ambavyo kimoja ni kwa ajili yetu na viwili ni kwa ajili ya mama, mjuu kuu wake pamoja na meneja wake. Tukakabidhiwa dereva wa hotelini pamoja na gari, tukatembezwa mji mzima wa Arusha, tukafanya manunuzi muhimu kisha tukarudi hotelini. Brian akatupatia habari njema kwamba ame onana na mama pamoja na mwanangu na wana fanya mpango wa kupanda ndege kuja Arusha.

“Claudia”

“Yes”

“Nashukuru sana kwa kila jambo ume yabadili maisha yangu sasa ndoto zagu zina kwenda kuwa kweli”

“Nami niahidi huto niangusha kwenye jambo lolote”

“Siwezi kukuangusha”

“Kweli?”

“Ndio”

“Nafurahi kusikia hivyo ila siku ukija ukabadilika uka nisaliti kwa mwanamke mwengine nikuahidi jambo moja tu. Nitakuua kwa maana nina wivu ulio pitiliza, ume nielewa”

“Ndio nime kuelewa”

Nilijibu kinyonge huku nikiyatazama macho ya Claudia yanayo onyesha dhairi kwamba ana maanisha anacho kizungumza. Majira ya alasiri Brian akafika hotelini hapa akiwa ameongozana na mama pamoja na mwanangu. Nikakumbatiana nao kwa furaha kubwa saka huku machozi yakitumwagika. Mama yangu akaashindwa kuyazuia machozi yake, hata mwanangu Shamsa naye akajikuta akilia kwa furaha kwa maana ni miezi ina karibia nane sasa sija kutana nao. Nikawatambulisha kwa Claudia na nika mshukuru sana Claudia na Brian kuweza kunisaidia kuiokoa familia yangu kutoka kwenye mikono ya mke wangu ambaye sijui ni shetani gani ambaye ame badilisha kwa haraka kiasi cha kutamani kunifanyia mambo mabaya. Usiku wa siku ya leo tukapata chakula kwa pamoja.

“Rashidi una mtotom mzuri sana”

Claudia alizungumza huku akiwa amekaa pembeni ya Shamsa.

“Nashukuru sana”

“Ahaa mkuu tuna weza kuzungumza kidogo?”

Brian alizungumza huku akisoma meseji iliyo ingia kwenye simu yake. Wakasimama kwa pamoja wakasogea pembeni na kuanza kuzungumza.

“Baba mama yupo wapi?”

Nikamtazama Shamsa na kumshika nywele zake ndefu na laini.

“Mama amekwenda kwa bibi wa kule ila bado haja rudi”

“Ahaa kwa hiyo ata rudi?”

“Ehee tuna kwenda huko, tuna panda ndege kama leo kisha naye ata kuja”

Mwanangu akazidi kujawa na furaha kwa umri wake hapaswi kujua machafuko aliyo yasababisha mama yake.

“Mwanangu sasa nina anza kuamini kwamba maombi yangu ambayo usiku na mchana nina omba yana kwenda kukubaliwa”

“Ndio hivyo mama.Mungu ana weza kukuletea mtu uka hisi ni sahihi, alafu akaondoka kwenye maisha yako uka umia sana ila kumbe Mungu ame kuandalia nafasi nyingine ambayo ni nzuri sana kwenye maisha”

“Ni kweli, ila jambo kubwa ni kumlea mwanao kwenye mazingira mazuri. Haijalishi ita kuwaje hakikisha mwanao ana ishi kwenye maadili ya kiafrika hususani Tanzania”

“Hilo usijali mama”

“Alafu kuna kitu kinacho endelea kati yako na huyu mzungu?”

Mam aliniuliza kwa sauti ya kunong’ona huku akitabasamu.

“Mamama”

“Mmm mimi mtu mzima mwanangu”

“Nita kuambia muda ukifika”

“Ila ana onekana ni mkubwa zaidi yako?”

Mama aliendelea kuni nong’oneza.

“Mama hilo lisikuumize kichwa nita kuambia muda na wakati utakapo fika.”

“Sawa baba”

Claudia akaniita kwa ishara, nikasimama na kuwafwata sehemu walipo simama.

“Rashidi hapa kuna habari ambayo sio nzuri kidogo”

“Habari gani hiyo”

“Brian mwambie”

“Ahaa nilipo kuwa Dar es Salaam niliweza kuwatafutia Visa zenu, mama na mwanao wao wamefanikiwa kupita na tuliwapatia hati za kusafiria na kila kitu chao kipo tayari. Ila kwa upande wako Visa ime kataliwa na inavyo oesha ni kwamba wewe bado ni mfungwa na ni muhalifu wa tukio la kijambazi”

Moyo wangu ukastuka, huku nikihisi kajoto kazito mwilini mwangu kwani kwa jinsi nilivyo pania kwenda nchini Marekani naona mambo yana ishia hapa hapa Arusha.

“Ohoo Mungu wangu”

“Ila kutokana tuna mtandao mkubwa sana. Ina bidi ulazimike kulikana jina lako, uukane uraia wako, ubadilishe dini na kumbukumbu zako za uhalifu zote zifutwe na uwe mtu mpya kabisa, kwani hili jambo la ujambazi na tena bado ni mfungwa kwa nchi ya Marekani huto weza kuingia hata kidogo”

Nikashusha pumzi nyingi na kuvuta tena pumzi mpya. Nikamtazama mwanangu ambaye ana kula chakula kitamu, nikamtazama mama yangu, ambao hawa ndio watu wanao nipa nguvu ya kuendelea kupambana na maisha haya na kuendelea kuishi nchini Tanzania nina weza kuwapoteza wote wawili kutokana na umasikini ulio kithiri.

“Hapa kwenye kubadili dini ina kuwaje?”

“Ili ukanyage nchini Marekeni ukiwa kama raisi wa kule, ina kubidi uwe Mkristo. Ukikubali tuna ondoka kesho mchana, ukikataa, sisi na wewe tuna ishia hapa Arusha na uta pambana na mamlaka ya vyombo vya usalama vya nchi yako kwa maaa wata kukamata na kukurudisha gerezani tena.”

Brian alizungumza pasipo kupindisha maneno huku akinitazama usoni mwangu kwa macho makali kiasi cha kunifanya nijawe na bumbuwazi kwani toka nime zaliwa nime kulia kwenye maisha ya Kiislamu, nime soma madrasa na kufaulu vizuri, sema balee ikanitenganisha mimi na dini yangu na kuwa kiongozi wa genge la wahuni, ila katika moyo wangu bado nina itumikia dini yangu ya Kiislamu na sifikirii kuibadilisha hadi nina kufa.



“Rashidi wakati ndio sasa hivi. Kuna watu ubalozini wana subiria jibu lako”

“Muna weza kunipatia dakika kumi nikazungumza na mama yangu?”

“Sawa zungumza naye”

Claudia aliniruhusu na kwa haraka nikamfwata mama na kumuomba tuzungumze kwa dakika chache.

“Kwema lakini?”

Mama aliuliza huku akionekana kujawa sura ya wasiwasi.

“Kuna katatizo kadogo ambako kametokea”

“Tatizo gani?”

“Hati zenu nyinyi wawili, zime kubalika na muna weza kusafiri kwenda nchini Marekani. Ila hati yangu mimi ime kataliwa kutokana na hii kesi ambayo nime bambikiwa na mume mpya wa mama Shamsa. Pia bado sija malizakifungo changu cha jela ambacho sija hukumiwa.”

“Mungu wangu sasa ita kuwaje hapo mwanangu?”

“Kuna mambo mawili nime ambiwa niweze kuyachagua?”

“Mambo gani hayo baba?”

Mama mara nyingi huwa upenda kuniita baba kwani mimi ndio mwananye wa pekee.

“Moja wameniambia niukane uraia wa Tanzania na niwe raia wa Marekani. Hilo ni jepesi ila jengine wanahitajinibadilishe dini yangu na niwe mkristo. Sasa mama nime kuwa muislamu toka mtoto, ulijihidi kunifukuza na kunihimiza kwenda madrasa. Leo ina kuwaje nije kuikana dini yangu niliyo kuwa na kuiabudu toka utotoni”

Mama akashusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu. Akanishika viganja vyangu vya mikono huku akinitazama usoni mwangu.

“Rashidi”

“Naam mama”

“Mungu amekuletea huu mtihadi sio kama ni bahati mbaya ila amekupa nafasi ya wewe kutoka hatua moja ama nyingine. Kuwa Muislamu au kuwa Mkristo, vyote ni sawa. Mungu tunaye muamini ni mmoja, japo tuna muita kwa majina tofauti, wezetu wana Yesu na sisi tuna Muhamad. Wote hawa walikuwa ni wawakilishi wa Mungu kwa nyakati tofauti tofuati na sehemu tofuati tofuati. Hata ukiitwa John huto pungukiwa na kitu, ila imani yako ipo hapamoyoni mwako. Hivyo sijaona tatizo na endapo jina uta badilisha basi uta kuwa mbali na maadui zako na hawato kujua weweni nani”

Maneno ya mama yakapenda moyoni mwangu na kichwani mwanangu yakaeleweka vizuri.

“Mwanangu Tanzania sio sehemu sahihi kwa sasa, nafasi ni hii ikipotea kila kitu kina kuwa kime kwisha”

“Nimekuelewa mama nina kupenda sana na nina kushukuru kwa ushauri wako”

“Ni jukumu langu”

Nikaachana na mama na kuwafwata Claudia na Brian.

“Vipi?”

Claudia aliunilia huku akinitazama usoni mwangu.

“Nime kubali”

“Ohoo asante Mungu”

Claudia alizungumza huku akishusha pumzi nyingi. Uso wake ukajawa na tabasamu.

“Maamuzi mazuri, wao wata tuletea jina la mtu ambaye ume fanana naye hivyo haito kuwa shida kwa historia yako kujulikana”

“Sija kuelewa hapo Brian ume sema kuna mtu ana fanana na mimi?”

“Ndio, kuna kijana mmoja ambaye ume fanana naye. Data kamili nita kupatia asubuhi”

“Sawa”

Mimi na Claudia tukarudi kwenye viti vyetu na kuendelea kula. Muda wa kulala ukawadia, mama na mjukuu wake wakaingia katika chumba chao huku mimi na Brian tukiingia katika chumba chetu. Usiku huu sikuwa na kazi ya nyingine zaidi ya kumtembezea kichapo kizito kwa Claudia hadi ikafikia muda akawa ana omba nikifika nchini Marekeni nimuoe na yupo tayari kuachana na mume wake. Yote katika yote nina fanya hivi ili niweze kupata njia ya kufinikiwa na ikiwezekana nije kuishi maisha ya kifahari ambayo hapo awali nikuwa nikitazamao kwenye tv kwa baadhi ya watu wenye mafanikio makubwa.

Asubuhi na mapema nikawa wa kwanza kuamka, nikafanya mazoezi ya viungo kama kawaida kwa maana nina penda kufanya maeozi sana. Baada ya kumaliza mazoezi katika gym ndogo iliyopo ndani ya hichi chumba chetu, nikaingia bafuni na kuoga.

“Za asubuhi mume wangu”

Claudia alizungumza huku akinipapasa papasa mgongoni mwangu kwa maaana nime kaa hapa kitandani hiku nikiwa nime mpa mgongo.

“Nimeamka poa, vipi wewe?”

“Mimi nime amka salama, ila haki ya Mungu jana ume jua kuninyooshea goti. Duuu yaani umenifanya vioungo vyamgu kurudi utotoni.”

“Kweli?”

“Kweli yaani, kuni kipindi ulivyo kuwa ume niinamisha nilihisi pumzi ikiniishia. Ila nilikuwa nina sikia utamu, ikanibidi nijikaze hivyo hivyo na kweli nime fanikiwa kimalizamechi. Kwa kweli wewe ni fundi”

“Usijali uta endelea kula raha hadi ushindwe wewe”

“Nashukuru sana Rashidi. Ila nina hofu sana”

“Hofu gani?”

“Endapo tuta kwenda nchini Marekeni nita kuwa sipati mambo matamu kama haya kwa maana mume wangu ana wivu sana na ana nibana snaa”

“Mmmmm”

“Ndio hivyo na ina bidi penzi letu liwe la siri sana kwamaana endapo ata fahamu kwamba mimi na wewe tuna mahusiano ata tuua”

Nikaanza kujawa na woga huku nikimtazama Claudia usoni mwake.

“Nina kuambia ukweli Rashidi, mume wangu ni mtu hatari sana, moja ana jihusisha na magenge makubwa ya wauza madawa ya kulevya kotoka Mexco na Colombia. Kiufupi ni loard of drugs, ambaye ana tumia muamvulia wa kuwa sponser wa wapiganaji kuficha siri zake. Ameswaka sana na FBI, CIA, ila wote hajafanikiwa kumkamata”

“Mmmm sasa kwa nini una niambia haya yote?”

“Nina kuambia ili utambue uhatari ulipo mbele yetu. Ingekuwani vigumu sana endapo ungejua mambo hayo kipindi ukiwanaye.Ila yote katika yote ina tupasa kuwa makini”

“Sawa mke wangu”

Niliitikia kwa sauti ya upole nailiyo jaa furahakbisa.

“Ila usiniogope kwa mana nina kupenda sana Rashid”

“Usijali, vipi Brian hawezi kwenda kusema chochote kw amume wangu, moj ni mtu wambu ambaye nina muamini kupita mtu yoyote’

“Sawa kama ni hivyo”

Claudi akashuka kitandani na kuingia bafuni, akaogoa, kisha akarudi chumbani. Mara baada ya yeye kuva nguo takatoka nje, nikakutana na mama pamoja na mwanangu nao wakiwa wamsha amka. Kwa pamoja tukapata kifungu kichwa.

Claudia aliita huku akimtazama mama yangu usoni.

“Beee”

“Marekeni tunapo kwenda ni nchiya fursa, je uta hitaji kufanya biashara gani ili tukifika tu nikufungulie ili usikae nyumbani?”

“Mmmm mimi kitu ninacho kiweza sana kuliko hata kuliandika jina langu ni kusuka ukili. Nina shuka mikeka, vikapu, mikoba kwa kutumia uwili”

“Waoo hiyo ni fursa nzuri sana kwa nchi ya Marekani. Watu wengi sana wata kuwa wana kuja kununua vitu vya asilimi kwako”

“Nashukuru sana kwa hilo”

“Tukifika Mungu bariki tuta jua ni nini cha kufanya.”

Brian akakatisha mazungumzo kwa kutusalimia huku usoni mwake akiwa amejawa na furaha.

“Leo sasa tuna weza kuondoka. Kila kitu kime kamilika, hati ya kusafiria hii, kitambulisho chako cha uraia wa Marekani hiki hapa nakuanzia hivi sasa uta kuwa una itwa Malcom X na habari njema ni kwamba hakuto kuwa na ulazima wa wewe kubadilisha dini yako”

“Ohoo asanteni sana”

Nilizungumza kwa furaha huku Brian akinikabidhi hati yangu ya kusafiria, kitambulisho changu cha utambulisho changu kinacho nionyesha mimi ni raia wa Marekani.

“Hizi ni picha za huyo kijana alikuwa ana itwa Malcom X alifarikikatika moja ya tukio la Kimbunga. Alikuwa akiishia Florida.”

Kwa kweli macho yakanitoka kwa maana huyu jamaa ana fanana na mimi kwa kila kitu. Hata nilipo mkabidhi mama picha ya kijana huyu akastuka kidogo, akanitazama kisha akatazama picha hizo.

“Musitake kuniambia huyu kijana sio Rashidi??”

“Sio Rashidi mama, binadamu dunianini wawili wawili.”

“Kweli ni wawili wawili, laiti kama angekuwaamepigia kwenye mazingira ambayo ni ya hapa Tanzania, ninge sema ni Rashidi ila kutoka naona magorofabasi huyu kijana amefanana sana na mwanangu.”

Udhibitisho wa mama ukazidi kunipa matumaini. Hata mwanangu Shamsa alipo tazama hii akakiri kwa kusema huyu ni baba. Maandalizi ya safari yakawadi, saa nane nchana juu ya alama tukapanda ndege ambayo moja ina elekea nchini Kenya.

“Ohoo asante Mungu”

Mama alizungumza huku akinishika mkono wangu wa kulia kwa furaha, kwani tayari ndege imesha acha ardhi ya Tanzania na kushika anga la kuelekea nchini Kenya.

“Kweli Mungu ametusaidia, kila kitu nina kiona kama ndoto kwenye maisha yetu mama”

“Ni kweli Rashidi”

Ndani ya masaa machache tukafika nchini Kenya, hatukukaa hata zaidi ya lisaa tukaunganisha kwenye ndege nyingine ya shirikla la Fly Emiraters na kuianza safari ya kwenda nchini Marekeni na kwa kipindi hichi, Claudi amekaa siti yangu ya pembeni. Akaendelea kunieleza mambo mengi sana kuhusiana na nchi ya Marekani, akanieleza juu ya jiji la Las Vegacy ambapo ndipo zilipo ofisi zao. Hakika Claudia ame kuwa mkombozi mkubwa sana wa maisha yangu na familia yangu. Baada ya mazaa zaidi ya kumi na nane tukafika nchini Marekani hii ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kwenye maisha yangu kufika. Asikuambie mtu, sisi huku Bongo tuna ingiza kuishi tu, ila huku watu ndipo watu wanapo ishi. Mama hata yeye mwenyewe ameshindwa kujizuia kajizuia katika kushangaa shanga magorofa makubwa na yaliyo kwenda hewani. Tukaingia kwenye gari moja ya kifahari ya milango sita ambayo siku zote nilikuwa nina waona maraisi wakipanda gari kama hizi.

“Tuna kwenda kwa mume wangu. Kisha kuna nyumba yetu ipo hapa hapa Las Vegacy muta ishi.

“Sawa sawa”

Tukafika kwenye jumba moja kubwa la kifahari. Jumba ambalo lina walinzi wengi kiasi cha kunifanya nijawe na hofu. Tukakaribishwa na mzee mmoja nne na mwenye kitambi kikubwa. Akanyona denda na Claudia kisha Claudia akatutambulisha kwamba huyo ndio mume wake. Kwa jinsi ya unene wa mzee huyu jinsi alivyo, kwa haraka haraka ana onekana ana kibamia na anashindwa kumridhisha mke wake ndio maana mke wake ame kubali mapigo yangu.

“Huyu ni Rashidi, kama nilivyo alivyo kueleza Brian basi ana julikana kwa Malcom X.”

“Karibuni sana”

Tukashangaa sana kwa mzee huyu kuzungumza kiswahili fasaha.

“Asante”

“Huyu ni mama yake na huyu ni mwanaye”

“Ohoo una binti mzuri sana”

“Asante sana”

“Mume wangu ana itwa DON”

“Tume furahi kukutana nawe bwana DON”

Mama alizungumza huku akipena mikono na mzee huyu.

“Asante sana”

Makaribisho haya hakika ni mazuri sana. Baada ya chakula cha usiku, tukapata wasaa wa mimi, Claudi, Brian na Bwana DON kuzungumza vizuri.

“Bwana Rashidi nina imani mke wangu ame weza kuingia mkataba na wewe”

“Ndio ndio”

“Alinitumia clip zako mbili za mapambano kwa kweli nilijawa na furaha na wewe ndio mtu ambaye kwenye biashara yangu nilikuwa nina mtafuta”

DON alizungumza kwa furaha sana.

“Ume kuja Marekani nina kuahidi nita kufanya uwe nyota itakayo tazamwa ulimwenguni mwote”

“Asante sana Don”

“Ni wapiganaji wengi san anime wafanya kuwa nyota, ila hakikisha kwamba katika maisha yetu tutakayo ishi mimi na wewe sihitaji ushindwe siku hata moja na katika kila pambano uta jipatia asilimia mbili ya mapato yaliyo patikana hadi pale garama tulizo kugaramia ziweze kurudi. Tumeelewana Rashidi?”

“Ndio nime kuelewa”

“Na angalizo jengine, mke wangu ni mzuri sana na ana vutia machoni mwa wengi. Tambua kwamba nime garamia, endapo uta onyesha dalili za kumtamani mke wangu au nikagundua una mahusiano naye basi kichwa chako kita kuwa na halali yangu na nikizungumza hivi sitanii kijana. Walio weza kumtamani mke wangu wote wamesha liwa na mamba katika kisima changu cha mamba. So muheshimu mke wangu upate matunda ya kuishi katika jiji la starehe kama hili.”

Maneno ya Don yakanistua sana kiasi cha kunifanya nitazamane na Claudia ambaye kwa jinsi nilivyo mpatia mambo ya kiswahili sidhani kama nita salimika kichwa changu kwa huyu DON.



“Nime kuelewa bwana DON”

“Sawa nina penda heshima. Leo uta pelekwa katika nyumba tuliyo kuandalia. Kesho jioni uta kuwa na pambano la majaribio. Nahitaji kukuona mwenyewe kama upo vizuri au laa.”

“Sawa sawa”

Baada ya mazungumzo haya nikaondoka nyumbani hapa kwa Don, mimi na familia yangu huku tukiwa tumeongozana na Brian anaye endesha gari. Tukafika katika moja ya nyumba nzuri sana ambayo nje tukakuta walinzi wawili walio valia suti. Tukashuka kwenye gari tukiwa na mizigo hii, walinzi hawa wakatusaidia kuingiza ndani. Brian akatuzungusha eneo zima la nyumba hii ya gorofa moja na kutuelekeza baadhi ya vitu ambavyo hapo awali hatukuwahi kuviona.

“Rashidi naomba tuzungumze”

Tukatoka nje ya Brian na tukakaa kwenye moja ya kibanda cha kupumzikia kilichopo katika bustani nzuri sana yenye maua ya kupendeza.

“Rashidi nina imani ume weza kumsikia DON alicho kizungumza?”

“Ndio ndio”

“Ana maanisha anacho kiongea. Najua nini kinacho endelea wewe na mke wake, ila tafadhali, mulicho kifanya nchini Tanzania kibakie kule kule nchini Tanzania ila sio hapa Marekani, hususani katika hili jiji la majajiri. Ata kuua kweli wewe na familia yako. Nikiwa kama mwanaume mwenzako nina kushauri kaa mbali sana na mke wake. Wanawake ni watu wa ajabu sana, watatumia njia ya kukushawishi na mwisho wa siku wewe ndio utakaye haribikiwa. Tuna elewana?”

“Ndio kaka, nina weza kukuuliza swali?”

“Ndio”

“Kwa nini wewe una ficha niliyo yafanya na mke wa Don nchini Tanzania?”

“Ni moja ya hali ya kuwa Royal kwa mke wa Don kwa maana mimi ndio mtu pekee anaye niamini. Nilicho kuambia wewe kitekeleze. Fanya maandalizi ya mapambano yoyote kwa maana huku kuna wapiganaji kweli kweli”

“Nashukuru”

Brian akatuaga mimi na mama kisha akaondoka na kutuacha na walinzi hawa. Hakika ndoto za kuishi maisha mzuri mimi na familia yangu sasa nina ziona zina timia taratibu.

Jioni ya siku iliyo fwata, Brian akaja kunichukua nyumbani hapa na moja kwa moja tukaelekea katika moja ya jengo moja kubwa ambapo nje tukakuta watu wengi wakiwa wame panga mstari ili waweze kuigia ndani. Mabaunsa wakatupisa, na kitendo cha kuingia ndani hapa mwili wangu uka nisimka kwani kuna watu wengi sana na kuna ulingo ambapo kuna pambano lina endelea.

“Huu ni ukumbi wa DON, kila siku kuna kuwa na mapambano na watu wengi sana huwa wana ingia ndani ya ukumbi huu”

“Ahaa sawa sawa”

Tukaingia katika ofisi moja kubwa, mithili ya seble. Nikamkuta DON, mke wake, walinzi pamoja na wanaume wengine kama sita hivi ambao kwa uvaaji wao wa suti nzuri pamoja na macheni ya dhahabu, wana onyesha kwambani matajiri wenye pesa ndefu sana. Katika ofisi hii kuna matv makubwa yanayo rusha pambano linalo endelea kwenye ulingo wenye banda lililo tengenezwa na nyavu ngumu sana.

“Karibu sana Malcom X”

DON alizungumza huku akiwa amejawa na furaha.

“Nina shukuru sana”

“Jamani huyu ndio yule Champion wangu niliye watumia Clip zake.”

“Mbona hana mwili wa mapigao?”

Tajiri mmoja alizungumza huku akinitazama kwa dharau kuanzia juu hadi chini.

“Kweli una muona ni mwemamba hana kifua kikubwa kama wapiganaji wako. Leo toa mpiganaji wako bora ambapane naye”

“Naweka dola milioni moja kwenye hilo pambano. Haki ya nani DON mpiganaji wako ana pigwa”

Tajiri huyo akazidi kuni nanga kwa dharau.

“Wewe jidanganye. Nina weka dola milioni moja akishinda mpigaji wako, una chukua zote”

Kwa kweli watu duniani wana pesa, yaani hayo ma milioni ya dola wanavyo yazungumza kama vile wana zungumzia buku la kibongo kumbe, hiyo pesa ukija nayo nchini kwetu Tanzania, ni sawa na biloni moja ambayo una weza ukafanya makeke mji mzima hadi watu wakakukoma.

Makubaliano yakafanyika kwa matajiri hao. Nikapewa lisaa moja kwa ajili ya maandalizi ya pambano hilo na Brian akanipeleka katika chumba ambacho wapo wapiganaji wengine na wote wamejazia miili yao na wana onyesha wana kula kisawa sawa.

“Boss huyo ni nani?”

Mpiganaji mmoja alimuuliza Brian.

“Ni mwenzenu”

“Mwenzetu? Mbona amepauka hana mwili mzuri wa kama mpigaji uliongoni?”

Mpiganaji huyu alizungumza kwa dharua na kuwafanya wapiganaji wote kuanza kunicheka kwa dharau. Ni kweli sina mwili wenye misuli, ila nina jimudu.

“Nyamazeni”

Brian alizungumza na wapiganaji wote wakaka kimya inavyo onyesha Brian ndio anaye wafwatilia wapigaji wote.

“Ana itwa Malcom X, ata kuwa mmoja wa watu walipo kwenye timu yetu kuanzia sasa”

“Sawa boss ila kwa huyu kimbau mbau, naona kama ume bugi”

“Killer huo sio utaratibu wa kukaribisha wageni. Muheshimuni mwenzenu na mumuunge mkono”

Brian alizungumza kwa kufoka.

“Sawa”

Wakanipokea kwa roho kishongo upande. Brian akanipatia funguo ya kufungua moja ya mlango wa kabati la chuma lililopo ndani ya chumba hichi kikubwa.

“Kuna kila kitu kwa ajili ya maandalizi yako ya ulingoni. Nime weka na kile kinyago chako”

“Ohoo asante sana”

“Ila usimuambie mtu yoyote kwamba una itwa Rashidi. Jina lako la kuingilia ulingoni, kujitambulisha kwa hawa watu wote ni Malcom X”

“Sawa nime kuelewa”

“Nenda kawahakikishie kwamba hatuja kuleta huku kutoka huko mbali kwa bahati mbaya”

“Nime kuelewa”

Brian akanitazama machoni kwa sekunde kadhaa kisha akatoka ndani hapa. Wapiganaji hawa wapatao ishirini na mbili, wote macho yao yapo kwangu. Nikafungua mlango wa kabati hili na kukuta vitu vyote vinavyo husiana na upiganaji vikiwa vime andaliwa vizuri. Nikavua tisheti yangu nyeusi, alama za makovu zilizo jaa mwilini mwangu zikanifanya nisikie miguno kutoka kwa wapiganaji hawa ambao miili yao kweli ni mizuri, na wakisimama mbele za watu ni lazima washangiliwe hususani wana wake. Nikabadilisha nguo zangu na kuvaa bukta yangu pamoja na kinyago changu nikakifunga vizuri usoni mwanangu.

“Hei, nina itwa Killer mimi ndio mpiganaji bora wa DON”

“Asante”

“Mbona una zungumza kinyonge nyonge kam mtu mwenye njaa”

Jamaa huyu mwenye miraba mine alizungumza huku akinigong’a gonga kifuani mwangu.

“Ndugu, nina fikiria pambano lilipo mbele yangu. Hivyo nina omba unipatie muda wa kujiweka tayari”

“Hahaaa fala wewe muoga ehee?”

“Sio muoga, ila nina hitaji muda wa kutulia”

Don, mke wake na walinzi wake wakaingia ndani hapa na kuwafanya wapiganaji hawa wote kumsalimia kwa kuinamisha vichwa vyao chini kidogokama wafanyavyo Wakorea, ni mimi pekee tu ndio nime simama nikiwatazama yeye na mke wake. Don akanifwata hadi sehemu nilipo simama huku akitabasamu.”

“Malcom”

“Ndio mkuu”

“Nime weka pesa zangu nyingi kwenye hili pambano. Huyo unaye kwenda kukutana naye sio mtu wa mchezo mchezo. Nahitaji uniletee pesa hapa”

DON alizungumza huku akinikazia macho.

“Sawa sawa”

Muda wote ambao Don ana zungumza macho ya Claudia yapo kwangu. Don akatoka ndani hapa na kuwafanya wapiganaji wengine kushangaa kwani nina zungumza na bosi wao kawaida sana. Muda wa pambano uka fika nikasindikizwa na walinzi wawili wa DON kuingia ulingoni, karibia watu wote waliomo katika ukumbi huu wakaanza kunizomea kwa kufanya BUUUUUUUUUUU………………….! Huku wakinyoosha vidole gumba chini.

‘Mungu nisaidie iondoe hofu moyoni mwangu’

Nilizungumza huku nikijiweka sawa. Mziki mkubwa ukaanza kusikika na nika anza kuona kundi kubwa likimleta mpiganaji anaye jifanya kurusha rusha ngumi na kuwafanya watu kushangilia kwa furaha sana. Akaingia uliongoni hapa na akaruka sarakasi tisa huku akinizunguka na kuwafanya watu wazidi kupiga kelele kwa vifijo.

“Leo katika pambano letu, tuna mleta kwenu mpiganaji mpya aliye valia bukta ya blue na kinyago cha blue Malcom X”

Mtangazaji alizungumza na watu wote wakazomea hadi nikajihisi hasira.

“Upande wa kushoto nina wapetea, mpiganaji aliye pigana mapigano tisini na tisa na hajapoteza pambano hata moja, mvunja viungo vya wapinzani, Alvando Torresssssssssss”

Mtangazaji alizungumza kwa mbwembwe nyinngi na watu wote wakaanza kushangilia kwa furaha huku mpiganaji huyo akiruka ruka hewani kwa machachari ya hali ya juu. Refa akasimama katikati yetu.

“Pambano hili ni la kupigana hadi mmoja aweze kusarenda. Mupo tayari?”

“Ndio”

Mpinzani wangu alijibu kwa haraka huku akinitemea mate usoni mwangu na kunifanya nikasirike na kutaka kumvamia ila refa akanizuia kwa maana pambano bado halijaanza.

“Malaya wa kike leo nina kwenda kukufir** mkund** wako nina kupiga ndani ya dakika mbili tu”

Jamaa akaongeza tusi lililo zidi kunikera sana. Ila nikakumbuka maneno ya kocha wangu ambaye aliniambia kwamba ukiona mpinzani wako ana kutukana au kuongea maneno ya kejeli ina maanisha kwamba ana cheza na akili yako na ukijifanya una tumia hasira kumvamia basi uta mpa nafasi ya yeye kukupiga sana kwani huto kuwa una tumia akili bali una tumia hasira. Nikavuta pumzi nyingi sana na kuishusha na kuifanya hasira yangu ishuke kwa uharaka sana.

“Malcom upo tayari?”

“Ndio”

Nikarudi nyuma hatua nne, kengele ya kuashiria pambano kuanza ika gongwa. Mpinzani wangu akaniyooshea kidole cha kati ikiwa ni ishara ya tusi. Akanifwata kwakasi sana huku akijaribu kurusha ngumi kadhaa, nikazikwepa kwa kasi ya ajabu ambayo hata yeye mwenyewe hakuitegemea. Akarusha mateke, na yote nikayakwepa. Akilini mwangu ninacho kifanya sasa ni kumsoma uwezo wake, na kitu kingine nina hitaji na mimi kumchezea akili yake. Toress akazidi kurusha makombora mazito mazito ila wepesi wangu uka zidi kumpa wakati mgumu. Nilipo hakikisha kwamba dakika mbili zime kishwa nikamuuliza.

“Dakika mbili za kunipiga zime isha una jipya?”

Swali langu likamfanya Toress kukasirika sana, akaruka hewani huku akijgeuza ili anipige teke la kifua, nikaudaka mguu hup alio utanguliza na kumbwaga chini kama mzito. Kelele zilzio kuwa zina pigwa na mashabiki taratibu zikaanza kupungua. Kwa kasi ya ajabu Torres akanyanyuka huku akinitazama kwa macho makali.

“Pigana”

Nilimuambia huku nikimpa ishara ya kumuita wa vidole viwili. Hakuna kiti kibaya kama kujiona bingwa alafu ukakutana na mtu mpya na akawa ana kudharua. Hichi ndio kitu anacho pambana nacho Torres kwa sasa kwani makombora yake ya ngumi na mateke vyote anavyo virusha kwangu nina vikwepa na hadi sasa hivi hajaingiza ngumi wala teke moja. Mara baada ya kumsoma vizuri sasa na mimi nikaanza kupeleka mashambulizi yangu ambayo kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi nilivyo zidi kumuhimili mpinzani wangu, ambaye mbinu sasa zime muishia. Ukumbi ukakaa kimya, mapigo yangu ninayo yapiga sasa ni kuhakikisha nina mvunja vibaya sana Torres. Mbavu zake leo hazikuwa na bahati kwani nilihakikisha upande wa kushoto na kulia nina vunja mbavu si chini ya tatu. Nikamvunja mkono wake wa kushoto pasipo huruma na kumfanya alie mithili ya mtoto mdogo.

Torres akakubali kushindwa pambano hili huku nikiwa nime mjeruhi vibaya sana. Nikasimama huku nikihema kwa hasira. Ukumbi mzima kila mtu yupo kimya hata refa mwenyewe ana onekana kushangaa jinsi pambano lilivyo isha kwa upande wa Torres. Refa akaninyanyua mkono wangu wa kulia juu, akiashiria kwamba nime shinda. Nikatoka ulingoni na watu taratibu wakaanza kupiga makofi. Nikarudi kwenye chumba cha wapiganaji ambao nao wenyewe walikuwa wakifwatilia pambano langu kwenye tv iliyomo humu chumbani. Kila mmoja akaka kimya huku wakinishangaa sana.

Taratibu nikavua kinyago changu, na kukakaa kwenye moja ya benchi huku jasho likinimwagika sana.

“Hongera sana”

Jamaa mmoja mweusi alinipa pongezi huku akininyooshea mkono wake wa kulia. Nikautazama kwa muda kidogo kisha nika ushika.

“Nashukuru”

“Pia samahani kwa kukudharua mara ya kwanza”

“Asante”

“Hongera”

“Hongera Malcom”

Kila mmoja akanipongeza kwa namna yake. DON akaingia ndani humu huku akicheka sana.

“Nilijua, nilijua na sija toa pesa yangu ya bureee. Safi sana Malcom”

DON alizungumza huku tukipeana mikono.

“Nina shukuru sana”

“Aisee ume mpiga mpiganaji ambaye alikuwa akiwaonea sana wapiganaji wangu. Aisee wewe ni mtu mwengine na sio kwamba ume mpiga, ila ume mvunja vunja kwa kweli wewe ni mashine. Mpigieni makofi”

Wapiganaji wote wakanipigia makofi.

“Aisee leo ni lazima nifanye part ya kukukaribisha. Tuta kula tuta kunywa na tuta furahia maisha”

DON alizidi kuzungumza kwa furaha sana. Claudia na Brian nao wakaingia ndani hapa huku nyuso zao zikiwa zimejawa na furaha sana.

“Mume wangu nilikuambia nina leta chuma ume jionea?”

“Yaa nime ona mke wangu, mwaaaa”

Don alizungumza huku akimyonya mke wake denda.

“Aisee yaani sijaamini kama Torres ume mpiga. Yaani utani utani tu umemchapa”

“Yaani mume wangu, nilikuambia huyu mtu sio wa mchezo. Ana uwezo mkubwa sana”

“Ni kweli kwa kweli”

Majira ya saa nne usiku, Don na walinzi wake, wapiganaji wake pamoja na mke wake tuka elekea katika ukumbi mmoja mkubwa sana ambao ume jaa warembo wengi walio valia chupi na sidiria huku wengine wakiwa wapo uchi kama walivyo zaliwa. Kila mpiganaji akajichagulia wasichana wake, wengine wanachukua wasichana wawili wengine wana chukua msichana mmoja, wengine watano. Yote katika yote ni kila mmoja aweze kufurahi kwa namna anavyo weza yeye mwenyewe.

“Chidy chagua demu wa kwenda kugonga. Au mambo haya Tanzania hayapo?”

“Ahaa….sikuwahi kuyashuhudia”

“Chugua bwana, hii club yote ni yangu”

Maneno ya DON yakamfanya Claudia kunitazama kwa jicho la wivu ambalo mume wake hakubahatika kuliona.

“Sawa mkuu, ila kidogo kwa leo nita hitaji kupumzika naona mwili una uma uma”

“Kuna chumba cha masaji kule. Hei”

DON akwaita wasichana wawili walio valia bikini ila vufuani mwao maziwa yao yapo wazi.

“Mchukueni champion wangu na mukamfanyie massage ya mwili mzima”

“Ahaa mkuu a….”

“Nenda bwana Malcom. Hii ndio Las Vegacy usione aibu.”

Wasichana hawa wakanishika mkono na kujikuta nikishindwa kujizuia. Tukaingia kwenye lifti na kupanda gorofani. Liti ikasimama kwenye gorofa ya sita kisha tukaingia katika moja ya chumba kinacho nukia manukato mazuri sana. Waichana hawa wakaanza kunifua nguo zangu huku wakinipapasa kila sehemu ya mwili wangu.

Wakanilaza katika kitanda kidogo cha futi kama nne hivi. Wakakanza kunimwagia mafuta malaini mgogoni mwangu huku wakiendelea kunionyesha manjonjo yao.

“Muna itwa nani?”

“Mimi naitwa Camika”

“Mimi nina itwa Martha”

“Ohoo muna majina mazuri sana”

“Asante”

Mlango wa chumba hichi uka funguliwa na sote tukatazama mlangoni kwani kumbukumbu zangu zina onyesha kwamba mlango huu tuliifunga muda ambao tuna ingia. Akaingia mwanamke aliye valia kinyago huku kiwa na vazi kubwa linalo buruzika hadi chini. Akawapa ishara wasichana hawa kutoka ndani hapa na wakatii pasipo kujibu chochote. Ikabidi nikae kitako kumtazama ni nani, taratibu akavua vazi lake hili pamoja na kinyago chake na nikajikuta nikistuka sana kwani huyu aliye ingia ni CLAUDI mke wa DON ambaye ni jana tu DON ametoka kuni chimba biti la endapo nita onyesha dalili ya kuwa nina mahusiano na mke wake basi kichwa changu kita kuwa halali yake.

ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

BLOG