Search This Blog

Saturday, February 6, 2021

RISE UP SEHEMU YA 8/10

  

RISE UP

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 8 KATI YA 10


Nilistuka kidogo mara baada ya kusikia sauti ya kitoto ikiniita nyuma yangu. Nikatambua kabisa motto huyu anaye niita amenifananisha na mlinzi ninaye fanana naye kidogo anaye itwa Jony. Nikageuka huku nikiwa na tabasamu, nikakutana na sura ya motto wa mama Shamsa.

“Wewe hujaondoka?”

Nikamfwata kisha nikachuchumaa pembeni yake.

“Ndio sijaondoka Ruben, una upo peke yako?”

Nilimuuliza mototo huyu kwa maana nina lifahamu jina lake.

“Nipo na dada yupo chumbani kwake”

“Ahaaa, una endeleaje?”

Nilizungumza huku nikimchunguza Ruben usoni mwake, kila aina ya sifa ambazo ninazo yeye pia anazo. Kutokana na nywele zake ndezo wanazo mfuga, nikachomoa nywele kadhaa kichwani mwake pasipo yeye kusikia maumivu yoyote.

“Mimi nipo vizuri. Leo pia tuta cheza mpira?”

Nikagundua kwamba huyu Ruben ana mahusiao mazuri na mlinzi huyo Jony.

“Ndio tuta cheza ila acha kwanza tuwakaribishe wageni”

“Sawa tano”

Mtoto akanipa tano kisha akakimbilia chumbani kwake. Nikachukua kitambaa mfukoni mwangu, nikaweka vipande hivi vidogo vya nywele kisha nikakifunga na kukikaza kitambaa hichi kisha nikakirudisha mfukoni mwangu. Nikatoka eneo la nyumba hii ya raisi, nikatazama jinsi eneo hili lilivyo kubwa. Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba nimefika wakati muafaka, wakati wa raisi wa Congo kuingia hapa ikulu huku akiwa ameongozana na mwenyeji wake pamoja na wake zao. Waandishi wa habari pamoja na watu wengi wengi wameambana na raisi huyu wa Congo huku walinzi wa raisi wa Congo karibia wote nina wafahamu kwani nilikuwa nao kwenye jeshi lake la mapinduzi. Kutokana ikuku hii nina ifahamu kutokana na kusoma kwenye ramani. Nikaingia katika libray(Maktaba) kuhakikisha kwamba hakuna ambaye ana niona na nina kaa hapa hadi ule muda wa wafanya biashara utakapo fika huku nikifwatilia kila kinacho endelea hapa ikulu kupitia simu yangu ya mkononi ambayo nime iunganisha na program inayo weza kudukua kamera zote pasipo mtu yoyote kuweza kulitambua hilo.

Baada ya vikao vifupi vifupi vya maraisi hawa wawili, ukafikia wakati wa wafanya biashara kuingia ikuku hapa kwa ajli ya kikao chao. Nikatoka maktaba hapa huku watu wengi wakiwa bize juu ya ugeni huu.

Wafanya biashara wote wakafika akiwemo Don na walinzi wake wachache. Kikao cha wafanya biashara kikaanza huku nikimuoma Caro na vijana wake wakiendelea kuimarisha ulinzi huku Caro akiwa ni miongoni mwa watu walio kaa katika eneo la wafanya biashara. Baada ya kama nusu saa ya kikao hichi kuanza, nikamuona DON akisimama na kutoka ukumbini hapa, nikaanza kumfwatilia kwa umakini na kumuona akielekea vyooni. Nami nikaelekea katika choo alicho ingia, kutokana na ubize wa watu hivyo hapakuwa na mtu aliye nitilia mashaka. Nikasimama eneo la kunawia mikono, nikamuona Don akitoka katika moja ya choo huku akifunga vizuri mkanda wake.

‘Huu ndio wakati mzuri’

Nilizungumza huku nikifunga mlango mkubwa wa choo hichi wa watu kuingia ndani hapa na kumfanya Don anitazame.

“Mbona una funga mlango?”

“Naamini tume kutana”

Niluzungumza kwa sauti yangu ya kawaida na kumfanya Don kustuka sana kwani hakutarajia kuniona wala kusikia. Nikachomoa bastola yangu huku nikifunga kiwambo cha kuzuia sauti ya risasi kutoka.

“Malcom?”

Don aliniita huku akirudi nyuma nyuma hadi akafika ukutani.

“Ndio ni mimi, nilikuwa nina usubiri muda kama huu, kwa maana nina nilikuwa nina hamu kubwa sana ya kuiona damu yako DON.”

Nilizungumza huku nikimnyooshea DON bastola ya kichwani mwake na pa kwenda zaidi ya kutetemeka huku akininyooshea mikono kama mtu anaye subiri kupokea upako kwa mchungaji wake.

“Malcom tu…u….ongee ndugu yangu”

Don aliniomba kwa sauti ya huruma huku akiendelea kutetemeka kwa woga, nikaikoki bastoka yangu huku kidole change cha pili kutoka kidole gumba nikikiweka taratibu kwenye triga kwa ajili ya kufyatua risasi ambayo ikitoka moja kwa moja ina piga kwenye paji la uso wa DON na kukichwangua kichwa chake.



“Hatuna cha kuzungumza mzee. Niliapa na nika kuambia nikionana na wewe ni lazima nikuue hivyo ni lazima ufe”

“Niambie una hitaji kiasi gani nina pesa Malcom nina weza nika kulipa kiasi chochote utakacho hitaji, ila nina kuomba uisamehe tu roho yangu”

Don alizungumza huku machozi yakimwagika, japo Don ni mtu mwenye roho mbaya ila nime tambua kwamba ni muoga sana na hakuna binadamu yoyote duniani ambaye ana weza kupenda kufa pale anapo kutana na adui yake ambaye ata hitaji kumuua.

“Una hisi pesa yako ina thamani kubwa kuliko roho yako”

“Najua haviendani kithamani ila nina kuomba sana ndugu yangu nina kuomba uweze kuniambia una hitaji kiasi gani?”

Nikakaa kimya huku nikimtazama DON usoni mwake.

“Hivi ulihitaji kiwais gani cha pesa kutoka kwa mke wangu?”

Don hakuweza kunijibu chochote zaidi ya kuendelea kutetemeka.

“Ulihitaji utajiri wa binti ambaye baba yake alipambana na kuupata. Najua una pesa nyingi sana ambazo hata idadi yake huwezi kuikumbuka si ndio”

Don akanijibu kwa kutingisha kichwa kwamba ni kweli kwa maana mtu huyu huingiza mamilioni ya dola kwa lisaa moja kwani uuzaji wake wa madawa ya kulevya ni karibia dunia nzima.

“Sasa uta nilipa kiasi gani hadi nikuache uwe hai”

“Dola bilioni kumi?”

“Siwezi kufanya upuuzi huo”

Nilizungumza huku mdomo wa bastola yangu ukiendelea kumtazama DON anaye endelea kutetemeka.

“Do…la milioni arobaini?”

“Bado”

“Do…la bilioni themanini?”

“Roho yako ina thamani kubwa Don hizo pesa haziwezi kuendana na roho yako”

“Do…la bilioni mia mbili”

Nikatabasamu kwa maana hizi ni pesa nyingi sana na hawezi kuingia kwenye akaunti moja na yeye pia hajaziweka kwenye akaunti moja.

“Una nitumiaje hizo pesa?”

“Nipatia akaunti mbili zinazo weza kuingiza hicho kiasi cha pesa”

“Ila una tambua hakuna nchi ambayo ina weza kupokea hicho kiasi cha pesa pasipo maelezo na muda wako wa kuishi ni mdogo sana”

“Zipo hizi pesa zina weza kuingia kupitia Black Makert na una weza kuzihifadhi nchi yoyote ile unayo hitaji nakuhakikishia kwamba zitakuwa salama na hauto iingia kwenye matatizo ya aina yoyote”

“Sawa nitumie”

“Alafu huto niua?”

“Wala sinto kugusa”

Don akatoa simu yake mfukoni.

“Ahaa wewe ni mjanja sana, nahitaji kujua kila unacho kifanya”

Nikamzunguka DON na nikasimama nyuma yake huku bastola yangu ikiwa katika usogo wake. Akaanza kuingia katika mfumo wa kibenki, nikamtajia akaunti yangu ya kwanza na kwa kupitia mifumo isiyo halali ya kuhamishia pesa ambayo ina patikana katika black makert(soko jeusi). Ambalo huusika na mambo mengi ya kihalifu ikiwa uuzaji wa silaha na utumaji wa pesa kama hizi.

“Ina chukua muda gani?”

“Dakika mbili tu”

Don alizungumza huku akitetemeka, pesa hizo zikaingia kwenye akaunti yangu ya kwanza kisha nikampatia akaunti ya pili na akaingiza posa hizo. Kwa kupitia simu yangu nika dhibitisha katika benki zote mbili kwamba kila akaunti imeingia kiasi cha dila bilioni mia moja, pesa ambazo kwa haraka haraka ukinisimamisha na matajiri wengine wanao pata pesa zao kihalali basi nina weza kuwa namba moja na kuwaangusha matajiri wote. Ila siwezi kuweka bayana juu ya pesa hizi kwa maana mashirika makubwa ya kipelelezi yana weza kuzifwatilia na endapo wata litambua hili basi maisha yangu yatakuwa ni ya kuwindwa kwani sina kampuni wala biashara ya kuniingizia kiwango hicho cha pesa. Nikampokonya DON simu yake kisha nikamuingiza kwenye choo kimoja na kumfungia kwa nje. Nikaichomkea bastola yangu kiunoni na nikatoka ndani hapa. Hapakuwa na aliye hisi chochote, nikaidumbukiza simu ya DON kwenye moja ya ndoo ya uchafu. Moja kwa moja nikaeleka hadi katika nyumba anayo ishi raisi, kwa jinsi nilivyo ingia ndivyo jinsi nilivyo anza kutoka. Nikalitoa begi langu lililopo chini ya kitanda, nikakiweka kitambaa hichi chenye nywele kadhaa za Ruben, nikakisogeza choo hichi cha kukaa kisha nikazama taratibu na nikakirudishia ili mtu asiweze kujua chochote. Nikazama ndani hadi nilipo ukuta mtungi wangu wa gesi katika tanki hili la maji taka. Japo umechafuka kwa kinyesi ila sikujali, nikauvaa mgongoni mwangu na puani kisha nikaanza kuingia kwenye bomba hili ambalo moja kwa moja likanipeleka hadi kwenye bomba kuu, nikaogelea na kuelekea nje kabisa na kutokea baharini. Nikaanza kupandisha juu na nikatokea katika usawa wa bahari nikaiona boti tuliyo jia. Nikaogela hadi ilipo, nikaingia ndani ya boti na kumkuta Shabani akiwa amezinzia.

“Hei”

“Mmmmmm aisee mbona una nuka mavi hivyo?”

Shabani alizungumza huku akiziba pua yake.

“Kazi baba”

“Khaaa….hembu vua bwana nime kula kuku mwenzako nisije nikamtapika.”

Nikavua suti hii, nikatoa paryumu ya kukata harufu ndani ya begi kisha nikaanza kujipulizia na ndani ya muda mchache harufu yote ikaisha.

“Aisee afafhali sasa. Ehee imekuwaje?”

“Sijamuua”

Nilijibu huku nikivaa nguo ambazo nilizivaa mara ya kwanza.

“Kwa nini sasa?”

“Pesa ndugu”

“Pesa ndio ime kufanya usimuue?”

“Ndio ila nita mtafuta sehemu nyingine ila cha kwanza ilikuwa ni sisi kuweza kupata pesa nyingi itakayo tuwezesha kuishi maisha mazuri hadi tuna kufa”

“Kiasi gani hicho amekulipa hadi umeshindwa kumuua?”

“Kaka tuta ongea, tundoke kwanza eneo hili”

Tukaanza kuondoka eneo hili. Tukafika ufukweni, tukakabidhi boti hii kisha tukaelekea eneo tulipo liacha gari letu na kuondoka.

“Ehee niambie ime kuwaje na umeingia haraka na kukutana naye haraka?”

“Yaaa nilikuwa nina mkaba hadi ameniingizia kiasi cha dola milioni mia moja”

Nilimdanganya Shabani kwa maana nikimtajia kiwango cha pesa halisi niliyo ingiziwa na DON atachanganyikiwa.

“Woooo aisee ni pesa nyingi sana”

“Yaa hapo nita kumegea hata kumi ndugu yangu”

“Kaka kweli?”

“Ndio”

“Aisee shukrani sana ndugu yangu”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuiona namba ya Jackline. Nikapokea na kuiweka sikioni mwangu.

“Mume wangu vipi upo salama?”

“Nipo salama, naona umenipigia kwa mfumo wa kawaida na sio video”

“Ndio mume wangu upo sehemu nzuri tukazungumza?”

“Ndio”

Nilizungumza huku nikimpa ishara Shabani ya kusimamisha gari, nikashuka ndani ya gari na nikasogea pembeni kidogo uli nizungumze naye kwa maana mazungumzo haya yana onekana yana umuhimu sana kwani sio kawaida ya Jackline kupiga simu ya kawaida mara nyingi tuna wasiliana kwa kupitia video call.

“Nimepokea simu kutoka kwa meneja wa beki ya FKB na LKB wameniambia kwamba akaunti zako zimeingizwa dola bilioni mia mia kila moja na pesa inapo toka haijulikani ila ime ingia, niambie imekuwaje kuwaje mume wangu?”

Swali la Jackline likanifanya nishushe pumzi kidogo.

“Simu nina imani zina weza kurekodiwa mke wangu nita kupigia video call”

“Sawa ila nina wasiwasi mwingi sana mume wangu”

“Usijali nita kueleza kila kitu”

“Sawa nina subiria nakuomba unipigie kabla huku hakujapambazuka”

“Usijali”

“Nakupenda Rashidi”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Nikakata simu na nikarudi ndani ya gari.

“Vipi kaka kwema?”

“Kwema mama watoto alikuwa ana hitaji kupata maelezo ya pesa iliyo ingia kwenye akaunti yangu.”

“Aisee kwa hiyo ana namba za siri za akaunti yako?”

“Hana ila yupo kwenye listi ya watu ambao ni warithi endapo nita kufa”

“Ahaa sawa sawa. Tuna elekea wapi sasa hivi?”

“Twende nyumbani kwako kwa zamani”

“Sawa”

Tukafika Kimara na kuelekea nyumbani kwa Shabani ambapo familia yake na mchepuko wangu wame hama.

“Ila kaka hivi huyo Don hato kurudi na kukuangamiza?”

“Kwa biti nililo mchimba sidhani kama ana weza kurudi na kufanya upuuzi wowote kwangu”

“Ina bidi uwe makini sana kaka kwa maana kama ametoa pesa yote hiyo ni lazima ata tafuta namna ya kukuua”

“Usijali, ngoja nizungumze na mke wangu”

Nikaingia katika chumba cha wageni na nikampigia simu Jackline na nikavaa wireless earphone ili mazungumzo yangu Shabani asiyasikie.

“Pole kwa kutawaliwa na wasiwasi mke wangu”

“Usijali mume wangu. Ehee pesa yote hiyo imetoka wapi mume wangu?”

“Kwa Don, amenilipa kiasi hicho ili niweze kumsamehe na nisimuue”

“Mungu wangu. Ametoa dola bilioni mia mbili kwa ajili ya uhai wake?”

“Ndio mke wangu”

“Na haujamuua?”

“Ndio hapo tuliamua kufanya makubaliano haya?”

“Sasa mume wangu kama ametoa kiwango hicho cha pesa hato kudhuru kwa kweli kwa maana ni pesa nyingi na imeingia kwenye benki hizo bila hata ya maelezo, yoyote na hawajui ime toka akaunti gani. Na isitoshe mume wangu, Don hawezi kukuacha ukaitumia hiyo pesa kwa amani ni lazima ata kujia na kukudhuru, hembu lifikirie hilo mume wangu”

“Usijali mke wangu kuwa na amani. Mimi hata nikifa una weza kuishia maisha mazuri wewe na familia nzima. Jambo la kufanya nina taka kuigawanyisha hiyo pesa, pesa zilizop kwenye akaunti moja nahitaji kuzigawa hawa kwenye akaunti za watoto. Kisha hayo mafungu mawili yaliyo salia nina hitaji uchukue fungu moja kisha mama naye nimuingizie fungu jengine”

“Sawa mume wangu ila pesa hizo kuzitoa kwenye ile zile benki na kuziingiza kwenye akaunti zetu za hapa Ufaransa ni lazima ziwe na maelezo mazuri?”

“Nalitambua hilo, kila mmoja nita andika maelezo kwa njia ya barua pepe na kila mmoja awe na hicho kiasi cha pesa nah ii iliyo salia nita jua namna ya kufanya”

“Sawa hivi Don ana kiwango gani cha pesa hadi akupatie pesa kiasi hicho?”

“Yule ni muuza madawa mkubwa hivyo ana uwezo mkubwa kuliko unavyo dhani na ana pesa nyingi sana ambazo hakuna anaye jua idadi yake ya pesa”

“Mmmm ila kuwa makini na huyo jamaa mume wangu”

“Usijali, ikifika jioni nita andika barua pepe hizo kuelekea kwenye benki moja wapo”

“Sawa mume wangu nina shukuru sana”

“Nawe pia nina shukuru mke wangu kipenzi, nina kupenda sana”

“Nina kupea pia mume wangu”

“Vipi Shamsa na wadogo zake ana endeleaje?”

“Anaendelea vizuri ni leo tu ametoka kukuulizia nikamuambia nita kupigia simu kukipambazuka”

“Sawa sawa kukipambazuka nita zungumza nao wote”

“Sawa mume wangu”

“Badae kwa maana huku ni mchana”

“Sawa kuwa makini mume wangu”

“Usijali”

Nikakata simu kisha nikatoka ndani hapa.

“Kaka ni sehemu gani wana toa huduma ya internet cafĂ©?”

“Ni sehemu nyingi sana wana toa hiyo huduma. Kariakoo kule na sehemu nyingi tu”

“Hembu twende nahitaji kuandika barua pepe kadhaa hivi”

“Kwa nini usinunue laptop na wi-fi una weza kufanya kazi sehemu yoyote ndugu yangu”

“Hilo nalo ni wazo zuri. Ile laptop yangu ya kwanza ilizama kwenye ajali ile ya gari pale Wami hivyo nimepata kajiuvivu hivi ka kununua pc nyingine ila kabla ya kwenda huko nahitaji tupite hospitalini nikapime DNA”

“Wewe ukapime DNA au?”

“Hapana nina vijinywele vya Ruben mtoto wa mama Shamsa hivyo nataka kumpima DNA ili nifahamu kama ni wangu au laa?”

“Mmm kaka lini umekutana naye kimwili?”

“Kuna siku nilimbaka, hivyo nina hisi kama ile siku aliondoka na mimba”

“Hahahaaaaa!! Una nichekesha sana, ulimkaje?”

Nikamuadithia Shabani tukio zima jinsi lilivyo tokea na namna nilivyo mteka mama Shamsa.

“Aise ni hatari sana kuna daktari nina mjua ana weza kutusaidia hili jambo kwa haraka. Tukimpatia kitu kidogo basi ana weza kutuhudumia kwa haraka na kutupatia majibu ya uhakika”

“Sawa”

Tukabadilisha nguo kwa maana kuna nguo kadhaa za Shabani aliziacha kwenye nyumba hii. Tukaingia ndani ya magari na kuondoka eneo hili. Tukafika hospitali ya Muhimbili na moja kwa moja tukaelekea katika chumba cha daktari ambaye ni rafiki wa Shabani.

“Shebyy karibu sana ndugu yangu”

“Shukrani sana dokta. Kutana na ndugu yangu ana itwa Rashidi”

“Habari yako Rashidi”

“Salama dokta”

“Rashidi huyu ana itwa dokta Malick”

“Nafurahi kukufahamu doka”

“Shukrani Rashidi, karibuni sana”

“Tuna shukuru sana, dokta ndugu yangu tuna shida ya jambo moja aise, tuna hitaji kupima DNA”

“Mume kuja na mtoto anaye paswa kupimwa hiyo DNA?”

“Hapana ila nina vipande vya nyele zake hapa nina imani DNA si ina weza kufanya kazi?”

Nilizungumza huku nikimtazama dokta Malick.

“Ndio ina weza kufanya kazi. Sasa ni nani ambaye ana pima DNA yake na mtoto?”

“Ni mimi”

Nilizungumza huku nikifungua kitambaa change, nikatoa nywele nilizo mchomoa Ruben kisha dokta akanipa kichupa maalumu na nika ziweka nywele hizo.

“Kabla sija pima ningependa kufahamu, huyo mtoto unaye taka kumjua kama ni wako au si wako ni wa mke wako wa ndoa au mchepuko kwa maana kwenye DNA kuna majibu ya aina mbili, awe ni mtoto wako au sio wako, sasa ni mara mia ukakuta ni mtoto wako kuliko ukakuta sio mwanao. Inakuwa ni tabu kidogo na watu wengi sana huwa wana fika hatua hadi ya kuwaua wake zao au michepuko wao. Je kaka Rashidi upo tayari kwa majibu yoyote?”

“Ndio nipo tayari kwa majibu ya aina yoyote”

“Sawa nita zipima na majibu mta kuja kuchukua kesho”

“Hakuna shaka ndugu”

“Shabani karibuni sana ndugu zangu”

“Tuna shukuru na malipo nita kuingiza kupitia simu”

“Nita shukuru sana ndugu yangu”

Tukaagana na dokta Malick na kutoka nje. Tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili.

“Kaka endapo ukakuta huyo dogo ni mwanao ita kuwaje?”

“Haki ya Mungu aisee yule mwanake ata teseka. Naamini ana jua kwamba mimi ndio baba wa mtoto ila ameamua kumbambikia mzee wa watu masikini”

“Haaahaha sasa uta mchukua au?”

“Ikiwezekana nita mchukua kwanza kuna demu wangu Fulani yupo Ghana naye ana mwanangu asiee na yeye nataka nimfwatilie. Nataka ninunua hata kisiwa niwajengee kila mmoja jumba leke la kifari wake hapo”

“Duu kaka hayo mawazo ya mbali sana ila ni jambo zuri. Kama Caro ana mimba, Itali una watoto, sijui Ghana una mtoto….”

“Uingereza nina mtoto, yaani ni mwendo wa kujaza dunia”

“Hahaaa…..”

Nikaitoa simu yangu mfukoni ambayo ina ita, nikaitazama na kuona namba ya Caro.

“Honey vipi?”

“Upo wapi mume wangu?”

“Nipo na Shabani tuna elekea Kariakoo. Vipi mbona una zungumza kama una wasiwasi”

“Mume wangu ikulu imevamiwa”

Kauli ya Caro ikanistua sana na kujikuta nikikaa kimya kwa muda huku nikisikilizia milio ya risasi ikirindima na hapa nikajua kwamba uvamizi huu wa sasa hausiani kabisa na uvamizi wangu kwa DON.



“Na….nani?”

Nililiza huku nikiwa nimeshikwa na kigugumizi.

“Hata sielewi hapa nina jitahidi kumuokoa raisi”

“Mungu wangu kwa hiyo ina kuwaje?”

“Nitakuambia”

Caro akakata simu na nikabaki nikiwa nimeshikwa na bumbuwazi.

“Vipi kaka kuna nini?”

Shabani aliniuliza huku akinitazama machoni mwangu.

“Anasema ikulu imevamiwa”

“Na nani?”

“Sijui na nina sikia milio ya risasi ikirindima eneo hilo”

“Du sasa ina kuwaje ndugu yangu?”

“Sijui tuelekee nyumbani kwa Caro tukarudishe hizi silaha kwanza”

“Sawa”

Tukaelekea nyumbani kwa Caro, nikarudisha sila zote kwenye chumba chake cha siri na jambo la kumshukuru Mungu kwamba sijatumia risasi hata moja. Hazikupita hata dakika ishirini, gari mbili nyeusi zikaingia nyumbani hapa kwa Caro kwa mwendo wa kasi sana na geti likafungwa. Wakashuka walinzi wa raisi pamoja na raisi mwenyewe na familia yake huku wakiongozana na Caro na wakaingia ndani hapa.”

“Kuna underground room ipo chini ardhi”

Caro alizungumza huku wakikimbilia kwenye moja ya chumba ambacho tuka nimfahamu hajawahi kuingia. Wakakimbilia ndani hapo humo huku hapa wakiwa wamebaki walinzi wawili wakiwa na bunduki. Baada ya muda kidogo Caro akatoka huku mkononi mwake akiwa ameshika bastola.

“Mke wangu ni nini kinacho endela?”

“Katika wafanya biashara walio ongozana na raisi wa Congo kulikuwa na magaidi hivyo ikulu ilianza kushambuliwa kwa ndani na walinzi wengi sana wame weza kuuwawa”

“Ila kumtoa raisi nje ya ikulu ni hatari sana?”

“Ndio ni hatari ila ni heri akakimbia nje ya ikulu kwa maana watu hawa wana onekana wameingia kwa njia ya chini yaani sielewi mambo yamekwendaje ila nakuomba tuzungumze”

Tukapandisha garofani, Caro akazima kinasa sauti cheka anahco tumia kuwasiliana na walinzi wezake.

“Mume wangu niambie ukweli una fahamu chochote kuhusiana na uvamizi huu?”

“Ina maana umesha anza kuto kuniamini?”

“Nina kuamini mume wangu ila ulikuwa na mpango wa kuingia ikulu sasa sijui kama ulikuja au laa?”

“Ndio nilikuja na nikamalizana na Don kisha nikaondoka sija mdhuru mtu wa aina yoyote. Sasa hao watu walio vamia huku nyuma nahisi walikuwa na ajenda yao wenyewe. Ehee hembu niembie imekuwaje kuwaje kwani?”

“Kikao cha raisi wetu na raisi wa Congo kilikuwa kina karibia kuisha. Galfa tukaanza kusikia milio ya risasi ikirindima. Jukumu langu ni kuhakikisha raisi ana kuwa salama, nikamtoa raisi kwa mlango wa dharura na tukaondoka ikulu. Hapa tumeliacha jeshi likipambana na wavamizi hao”

“Una jua ni jambo gumu san ikulu kuvamiwa na wana vamia wana hitaji nini?”

“Kwa sasa hilo sifahamu mume wangu ila jambo la msingi ni raisi kuwa hai na jeshi lita kuja hapa kuimarisha ulinzi”

“Sawa acha sisi tuondoke kama uanvyo fahamu mimi na kaka yako pamoja na mke wako hatupatani kabisa na wasije wakanihisi kama ni mimi bure”

“Usijali usindoke na ukiondoka wata kuhisi ni wewe. Tulia hadi pale hali itakapo tulia”

Gafla tukaanza kusikia milio ya risasi gatini jambo hili likatufanya kukimbilia dirishani na tukaona gari tatu nyeusi zikiwa zimepanga mstari mmoja huku wakipambaba na walinzi walipo getini huku watu hao sura zao zikiwa zimefunikwa.

“Hawa ndio walio vamia ikulu”

Caro alizungumza huku akivaa earophone masikioni mwake.

“Naomba silaha”

Nilizungumza, Caro akakimbila hadi kwenye shelfu iliyopo ukutani, akafungua na kutoa bastola moja pamoja na magazine mbili. Akanirushia kisha tukaanza kushuka kueleka chini. Tukawakuta walinzi wawili wakiwa wameelekezea bastola zao mlangoni huku Shabani akiwa amejibanza kwenye kwenye mlango wa kuelekea jikoni.

“Hakikisheni muna mlinda raisi”

Caro alizungumza huku akitangulia mbele. Nikapiga hatua za haraka hadi mlangoni, nikafungua mlango kidogo nikachungulia nje na nikashuhudia watu hawa wakimalizia mlinzi mmoja kwa kumpiga risasi na kuingia ndani hapa.

“Wana ingia ndani. Caro kajumuke na walinzi wengine kumlinda raisi acha niifanye kazi hii”

“Mimi na wewe ni kitu kimoja acha tupambane pamoja”

Caro alizungumza kwa kujiamini, kwa kasi ya ajabu nikafungua mlango na kuruka nje huku nikifyatua risasi kuelekea kwa majambazi wawili walio kuwa wametangulia. Risasi zangu zikawapata barabara vichwani mwao na wakaanguka chini na kufa. Nikakimbilia hadi kwenye moja ya gari na nikajibanza. Nikaanza kufyatua risasi kuelekea walipo majambazi hawa. Caro akakimbia hadi eneo nilipo na tukaendelea kusaidiana kujibu mashambulizi ya majambazi hawa.

“Niliende nikachukue silaha nyingine”

Caro alizungumza ikanilazimu kufyatua risasai na kuwafanya majambazi kutuliza mashambulizi huku wakiwa wamejibanza kwneye magari yao. Caro akaondoka eneo hili na kukimbilia hadi kwenye chumba chake cha kuhifadhia risasi. Baaada ya dakika tatu akatoka akiwa na bunduki kadhaa pamoja na bomu moja aina ya RPG. Akakimbilia hadi kwenye eneo la gari nililo jificha.

“Lete”

Nilizungumza huku nikilichukua bomu silaha hii ha bomu na kuiweka begani mwangu.

“Nilinde”

Nilizungu,za na Caro akafyatua risasi kuelekea walipo majambazi, nikanyanyua na kufyatua risasi kuelekea kati magari ya majambazi na gari mbili zikalifupuka. Nikaikokota AK47 chini na kuanza kufyatua risasi kuelekea nje. Nikakuta majambazi sita wakiwa wamekufa kwa bomu niliko lipua huku majambazi wawili wakiwa hoi mahutui.

“Nani amewagijaza”

Nilimuuliza jambazi mmoja anaye karibia kukata roho. Cara akasimama pembeni yangu huku akimtazama jambazi huyu.

“Nakuuliza nani aliye kutuma kutuma kwa maana huwezi kupona kwa jinsi ulivyo jeruhiwa ni heri kuzungumza tu ukweli”

“Ni jenerali Ngatuma”

Jambazi huyu alizungumza kisha akakata roho, jambazi aliye salia Caro akampiga risasi mbili za kifua na akafa.

“Huyo jenerali Ngatuma ndio yupi?”

“Ni jenerali wa sasa, ina maana ana hitaji kupindua nchi?”

Caro aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao.

“Sasa hivo sio muda wa kuuliza maswali. Muandae kaka yako tuondoke eneo hili kwa maana hao wanajeshi unao wategemea hawawezi kufika hapa sasa hivi kama wameagizwa na huyo jeneraliwao”

“Sawa”

Caro akakimbilia ndani kisha name nikakimbilia kwenye moja ya gari la walinzi ambalo limetobolewa tobolewa kwa risasi huku tairi zikiwa zime pasuliwa kwa risasi. Nikafungua mlango wa gari hii kisha nikaingia ndani, nikaisogea pembeni ili kupisha njia ya gari nyingine kuktoka. Nikachukua bunduki nyingine mbili zilzo kuwa kwenye eneo tulipo kuwa tumejibanza kwenye gari hili. Nikaingia ndani ya gari langu na nikaliwasha tayaru kwa kuondoka eneo hili. Wakaanza kutoka walinzi huku wakihakikisha usalama wa raisi. Kisha familia ya raisi ikatoka na kukimbilia ndani ya gari langu na kukaa siti ya nyuma. Caro akapanda siti ya mbele huku Shababi naye akikaa siti ya nyuma pamoja na raisi. Walinzi wakaingia katika gari jegine la Caro.

“Fungeni mikanda”

Niluzungumza huku nikimtazama mama Shamsa ambaye macho yake yamejawa na uwekundu utokanao na kulia kwa woga. Uzuri wa gari yangu ni manual, tukaondoka eneo hili kwa mwendo wa tahadhari sana huku tukizipita gari hizi za majambazi zinazo teketea kwa moto. Nikaingia barabarani kwa mwendo wa taratibu huku ukimya ukiwa umetawala ndani ya gari hili.

“Kwa nini una tusaidia?”

Raisi alizungumza huku akinitazama.

“Kaka hembu kaa kimya”

Caro alizungumza kwa ukali.

“Muache tu azungumze”

Nilizungumza huku nikiongoza mwendo wa gari hili huku nyuma tukifwata na gari walilo panda walinzi.

“Una kadi yoyote ya GPRS mwilini mwako?”

Nilimuuliza raisi.

“Ndio”

“Nikapungza mwendo wa gari hili na kulisimisha pembeni.

“Kwa nini umesimamisha gari baby”

Caro aliniuliza huku akinishangaa.

“Ipo eneo gani?”

“Hapa mkononi”

“Caro una kisu hapo?”

“Ndio”

Caro akachomoa kisu kidogo cha kukunjua kwenye buti zake.

“Hembu mkono wako”

Nilizungumza mara baada ya Caro kunikabidhi kisu chake. Raisi akanitazama kwa muda kidogo kisha akankabidhi mkono wake wa kushoto.

“Wapi?”

“Hapa”

“Raisi akanionyesha sehemu hiyo. Bila ya huruma nikamchana sehemu hiyo na kumfanya mke wake pamoja na mwanye kushanga. Nikamtoa kadi ndogo ambayo humuonyesha raisi eneo alipo. Nikaitupa kwenye gari la taka linali pita pembeni yetu kisha safari ikaendelea.

“Damu zina toka nyingi”

Raisi alizungumza huku akitazama eneo nililo mchana. Nikatoa kitambaa mfukoni mwangu na kumkabidhi na mke wake akamfunga kitambaa hicho mfukoni.

“Hujajibu kwa nini umenisaidia?”

“Sijakusaidia wewe nime msaidia Caro kama hutaki shuka kwenye gari langu na ujisaisie mwenyewe”

“Kaka si nilikuambia ukae kimya. Mtu mwenyewe hapo umri umekwenda. Wanajeshi wako wana kupindua alafu bado una leta jeuri hembu tulia Mungu akupiganie bwana akhaa una kera bwana”

Caro alifoka na kumfaya kaka yake akae kimya.

“Tuna kwenda wapi baby?”

“Nyumbani”

“Tanga?”

“Hapana”

Nilizungumza huku nikiwa makini barabarani kutazama gari zinazo tufwata nyuma na kuja mbele yetu. Majira ya saa kumi na mbili usiku tukafika katika jumba nililo nunua.

“Shabani rimoti ya geti unayo?”

“Ndio”

“Fungua”

Shabani akaminya rimoti na geti likafunguka taratibu. Tukaingia ndani kisha tukashuka katika magari.

“Kaka tuzungumze”

Shabani alizungumza huku tukisogea pembeni sehemu ambayo sio rahisi kwa watu kuweza kusikia.

“Kaka ume fanya nini ndugu yangu. Hawa washenzi ina kuwaje una waleta humu ndani, kumbuka hapa kuna familia zetu au una taka vita ihamishiwe hapa tuwapoteze tulio waleta huku?”

Shabani alizungumza kwa msisitizo.

“Nisamehe ndugu yangu najua nimefanya makosa ila hapa ndio sehemu ambayo kidogo ina usalama”

“Kaka bora ungeacha wafe wakupungizie kitabu cha dhambi. Kumbuka yule malaya alikuwa demu wako. Tuna jua tulipo mtoa. Na ni mara mbili alijaribu kukuua ila wewe umekuja kuwasiaida. Hembu niambie hiyo huruma umeitoa wapi ndungu yangu ehee?”

Shabani aliendelea kuzungumza kwa msisitizo huku dhahiri akionuesha kwamba hajapendezwa na jambo hili.

“Kaka usijali nita jua namna ya kulishuhulikia hili jambo”

“Kaka una yumba haki ya Mungu kumbuka una toka nje ya misimamo yako. Moja hatujiui ni kwa nini huyo jenerali sijui ni nani ana taka kumuua raisi, sisi tuna wababea beba achana nao bwana. Yaani nilijikaza sana kukaa karibu na mama Shamsa ila kusema ukweli nina mchukia yule mwanamke kuliko navyo hisi”

“Tuliza janzba kila jambo lita kuwa salana”

Nilizungumza huku nikimtazama mke wa Shabani pamoja na Tina wakiwa wamesimama katika mlango wa kuingilia huku wakishangaa ugeni huu wa kustukiza.

“Lolote litakalo tokea itakuwa ni juu yako. Mimi nimezungumza kama ndugu yako, isitoshe Caro na Tina una waweka kwenye hali gani. Yaani una taka kutengeneza kwa huyu mpuuzi alafu una haribu kwa wasichana wako., ahaaa….una boa kaka”

Shabani mara baada ya kuzungumza hivyo akaondoka eneo hili na kuelekea ndani. Caro akanifwata sehemu nilipo simama.

“Nashukuru mume wnagu kwa kunisaidia”

“Usijali, kabla sijaikaribisha familia ya kaka yako ndani, nina hitaji kujua mambo kadhaa kwa maana hapa nina ingia kwenye mambo yasiyo nihusu yasije yakaigarimu familia ya rafiki yangu”

“Sawa niulize tu mume wangu”

“Kwa nini jenerali amepindua serikali ya kaka yako?”

“Sijui mtu wa kumuuliza ni nyeye kwa maana hili jambo limetokea galfa sana na hata sisi wana usalama hatutambui chochote”

“Muite kaka yako”

Caro akamuita kaka yake kwa ishara na akatufwata hapa tulipo.

“Najua mimi na wewe hatuna historia nzuri, na haito kuja kutokea nika kuependa. Umepinduliwa tatizo ni nini baina yako wewe na huyo jenerali?”

“Una nihoji wewe kama nani?”

“Kama mtu niliye kuokoa”

“Una hisi kunileta hapa ndio uta taka kunitawala na kutaka kujua undani wangu. Ngoja nikuambie kijana nashukuru kwa msaada wako. Caro mimi bado ni raisi wa hii nchi. Una fwata amri yangu, mimi na familia yangu hatuwezi kukaa nyumbani kwa gaidi hivyo tuna ondoka. Ingia ndani ya gari na tuondoke sasa hivi. Nikiendelea kujificha ficha dhidi ya hawa watu wata ichukua nchi kiukweli ukweli”

“Kaka tulia kwanza usome ramani ya mambo yanavyo kwenda”

“Tuna ondoka na sio ombi ni amri”

Raisi alizungumza kwa msisitizo na akaondoka eneo hili, akaingia katika gari la walinzi yeye na familia yake.

“Mume wangu, samahani ila nipo kwenye majukumu ina omba nitimize majukumu yangu”

Caro alizungumza huku machozi yakimlenga lenga. Honi ikapigwa kutokea kwenye gari walilo panda raisi, familia yake na walinzi.

“Tafadhali kuwa makini mke wangu”

“Usijali mume wangu nita kuwa makini zaidi ya sana”

“Sawa”

Caro akakimbilia katika gari la walinzi, na wakaondoka nyumbani kwangu hapa. Nikaingia ndani huku hofu yangu kubwa ikiwa ni maisha ya Caro na mtoto wa mama Shamsa.

“Naomba namba ya yule dokta wa Muhimbili”

Nilimuambia Shabani mara baada ya kumkuta akiwa amekaa sebleni wakitazam taarifa inayo tangazwa kwamba kuanzia sasa hivi utawala wa nchi una ongozwa na jeshi na sio raisi tena.

“Shem wageni mbona wameondoka?”

“Wana dai kwamba hii sehemu sio salama”

“Baby upo salama lakini?

Tina aliniuliza.

“Ndio mke wangu”

Nikatoka nje na kumpigia daktari ambaye nilikwenda kupima vipimo vya DNA.

“Ndio dokta mimi ni Rashidi rafiki wa Shabani”

“Ohoo bwana Rashidi tena nilihitaji kunmpigia Shabani muda huu kwa maana sina uhakika kama kesho nita kuwepo nchini kama unavyo ona hali halisi ya kiuongozi ilivyo badilika na sisi wengine tume zoea kuongozwa kidemokrasia sasa inapo kuja swala la kijeshi tunao umia ni sisi wafanyakazi wa uma”

“Ni kweli, vipi majibu yametoka?”

“Ndio ndugu yangu Rashidi, hongera sana vipimo vinaonyesha DNA yenu ina fanana wewe na huyo mwenye nywele zake. Hivyo hongera sana ndugu yangu huyo ni mwanao na ni damu yako”

Macho yakanitoka huku nikikumbuka namna Ruben alivyo jawa na woga kipindi alipo kuwa ana ingia ndani kwa Caro nikakumbuka nanma alivyo kuwa amejikunyata mikononi mwa mama yake, jambo lililo nifanya damu yangu mwili mzima kunisisimka na kudhamiria ni lazima nimuokoa mwanangu kama hawa wengine wata hitajiu kufa acha wakefe ila mwanangu ni muhimu kuliko wao kwa sasa.



“Nashukuru dokta”

Nikakata simu huku nikiwa nimejawa na na furaha iliyo changanyikana na wasiwasi kwani sifahamu ni wapi Ruben alpo hadi sasa hivi. Nikarudi ndani kwa mwendo wa haraka kama mtu anaye wahi mshahara benki.

“Kuna nini mume wangu”

Tina aliniuliza huku akiwa na hali ya wasiwasi.

“Hakuna jambo sikinie hakuna mtu kutoka, Shabani uta walinda nina wahi sehemu mara moja. Tuna elewana?”

“Ila usalama upo ndugu yangu”

Nikamsogelea Shabani na nikamnong’oneza sikioni mwake.

“Dokta amesema vipimo vya DNA sawa, yule ni mwanangu hivyo acha kwanza nikakisake kidume changu. Hakikisha wana kuwa sala

ma hawa”

“Sawa kaka”

Nikashusha pumzi kidogo kisha nikatoa simu yangu mfukoni kisha nikaingia katika huduma za kibenki nikawaandikia email ya kuomba kuhamisha dola milioni kumi za Kimarekani kuingia katika akaunti ya Shabani iliyopoi nchini Tanzania. Japo ni kiwango kikubwa cha pesa ila benki wakanijibu kwa uharaka sana na kuniruhusu kuingiza pesa hizo.

“Kaka nina kuingizia mzigo ule tulio zungumza kwenye gari nitajie namba zako za benki”

“Ngoja kwanza kaka, ukizingiza sasa hivi na hali yenyewe hii. Nina hisi mabenki mengi yata fungwa na tuta kuwa tuna cheza pata potea. Wewe nenda, tuangalie hali ya nchi itakavyo kuwa kisha mambo mengine yatafwata”

“Sawa kaka nina shukuru”

“Kuwa salama”

“Sawa”

“Shem kuwa muangalizi kwa maana hao wanajeshi wanao pita na mavifaru yao huko mtaani wana wana ogopha sisi hatujazoea hayo mambo”

“Usijali shemeji nipo makini”

“Sawa”

Tina akanikumbatia na akanipiga busu la mdomoni kisha nikatoka ndani hapa. Nikaingia ndani ya gari langu, nikaligeuza na kuliweka sawa na kuanza kuondoka eneo hili. Nikampigia simu Caro na kwa bahati nzuri akwahi kuipokea.

“Upo wapi?”

“Kuna sehemu tumejificha mume wangu kwa maana kuna ulinzi kila sehemu tuna shindwa hata kutembea”

“Wapi niambie?”

Caro akanitajia eneo walipo, ambalo ni nje kidogo jiji la Dar es Salaa.

“Ina maana hawa jamaa walikuwa wamejipanga muda mrefu sana”

Nilizungumza huku nikipishana na magari kadhaa ya jeshi. Nikafika katika eneo walipo jificha nikawasiliana na Caro na akanifungulia geti na nikaingia ndani.

“Vipi mupo salama?”

“Yaani mume wangu wee acha tu”

“Ukimuuliza kaka yako ana semajaje?”

“Haeleweki. Una jua kaka kuna mambo mengi sana maovu ameyafanya ndani ya nchi. Nilimkanya sana na kumueleza kwamba hayo anayo yafanya ipo siku yatamrudi na kweli yana mrudi sasa hivi”

Nikatazama simu yangu ya mkononi na sasa hivi ina onyesha ni saa tano usiku.

“Sasa mume amua nini?”

“Hapa kuna watu tuna wasubiri na tuna ondoka nao na kukimbilia Madagascar kwa ajili kukaa huko kwa muda kwani hata mimi nikikamatwa nina weza kuuwawa kwani nimeweza kupewa majukumu ya sekta nyeti na kubwa kama NSS kiupendeleo”

“Mmmm kazi kweli kweli?”

“Yaani mambo yamebadikika sana tena kwa uharaka. Mbona ume kuja, umekuja kufanya nini mume wangu?”

“Nahitaji kuzungumza kitu na wifi yako, ukiachana ni adui yangu ila ni mama wa mwanangu nina liheshimu hilo hivyo tafadhali nina kuomba unipatie nafasi ya kuzungumza naye”

“Ngoja nikazungumze na naye”

“Sawa”

Caro akaingia ndani ya nyumba hii na baada ya muda akatoka akiwa ameongozana na mama Shamsa. Akatupisha na nikaanza kuzungumza naye.

“Ona sasa jinsi maisha yako yalivyo kuwa ya kikimbizi. Kweli nimeamini mwenyezi Mungu ana lipa waja wake hapa hapa duniani. Nakumbuka nilikuwa nina ishi kwa kuruka ruka sina amani na kwa ajili yako, nilipitia maisha ya tabu na shida kwa ajili yako.”

Nilizunguzma kwa sauti ya upole huku nikimtazama mama Shamsa machoni mwake jinsi alivyo mnyonge mithili ya kifaranga kilicho nyeshewa na mvua.

“Kwa hiyo ume niita uniseme?”

“Hapana sijakuja kukusema. Ila ninekuja kumchukua Ruben mwanangu”

Mama Shamsa akastuka huku akinitazama kwa macho ya mshangao.

“Ulihisi sinto jua. Tambua damu ni nzito kuliko maji na Ruben ni mwanangu. Sinto hitaji aweze kuishi maisha ya kikimbizi namna hii. NInacho kihitaji kwa hiyari yako, kamleta niondoke naye kwa maana kama ni kuwaua pia nina weza kuwaua na ita kuwa ni ishindi mkubwa sana kwa jenerali aliye wapindua.

“Rashidi sielewi una zungumza nini?”

“Una jua nini ninacho kizungumza. Au unataka nikamueleze yule mzee ili apate pigo jengine na afe kwa presha. Bwana kama amepokonywa nchi hilo ni pigo tosha aisee. Nina hitaji mwanangu”

Nilizungumza kwa ukali kidogo ila kwa sauti ya chini ambayo ni sisi wawili tu ndio tunao isikia. Mama Shamsa mwili mzima ukazidi kumtetemeka huku akiwa hajui nini cha kunijibu kwani nime mbana wakati mzuri.

“Hii ndio faida ya kuchagua pesa na kuacha mapenzi ya kweli. Una vuna ulicho kipanda. Namtaka mwanagu”

“Sio mwanao”

Mama Shamsa alijikaza tu kunijibu huku akiendelea kutetemeka. Nikachomoa bastola yangu kiunoni na nikaishika mkononi. Caro akasogea eneo hili kwa haraka mara baada ya kuona mambo yana haribika.

“Mume wangu kuna nini?”

Caro aliniuliza huku akiwa amejawa na mshangao mwingi sana.

“Mama Shamsa fanya nilicho kuambia”

Mama Shamsa akashindwa hata kuzungumza, wifi yake akashuhudia woga jinsi ulivyo mjaa mama Shamsa.

“Wifi ni nini kinacho kuogopesha?”

“Caro haya ni mazungumzo ya kifamilia kati yake na mimi hivyo nakuomba usiyaingilie tafadhali”

Nilizungumza kwa sauti nzito itokanayo na hasira iliyo nitawala.

“Ukitaka nikuache salama na uondoke na huyo mzee wako. Nina muhitaji mwanangu”

“Mwanoa gani tena baby?”

Caro aliuliza huku akiwa ametawaliwa na mshangao.

“Caro nina kuomba hili uliache kama lilivyo tafadhali”

“Ila mimi ni mpenzi wako nina paswa kujua mume wangu”

Nikamtazama Caro kwa macho makali.

“RUBEN ni mwanangu”

Caro macho yakamtoka kwa mshangao, kwani hili nililo lizungumza sidhani kama alilitegemea kutoka kwangu.

“Umesema?”

Caro aliuliza kwa msisitizo.

“Ruben ni mwanangu na mama yeka ni huyu kama ana bisha azungumze sasa hivi”

Mama Shamsa akaanza kuyumba na galfa akaanguka chini na kuzimia. Mimi na Caro tukabaki tukitazamana kisha taratibu Caro akachuchumaa na kumgusa shingoni mama Shamsa.

“Amezimia.”

Caro alizungumza huku akisimama.

“Rashidi nina hitaji kujua ulicho kizungumza una maanisha au?”

“Ndio nina maanisha. Wifi yako alinifwata kipindi sija kutana na wewe na wala sikufahamu. Aliniambia ili niweze kuishi kwa amani ni lazima nimpatie mtoto kwa maana mume wake ana hitaji mtoto na muda huo alikuwa tayari ameniteka. Hivyo sikuwa na jinsi zaidi ya kushiriki naye tendo la ndoa na matokeo yake ni Ruben. Hivyo nipo hapa kwa ajili ya kumchukua mwanangu niondoke zangu”

Nilibadilisha mada kidogo na kumfanya Caro kushusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu.

“Huyu mwanamke ni mshenzi kumbe ehee?”

“Kama aliweza kuniacha mimi mume wake wa ndoa una hisi kwamba ana shindwa kumsaliti mume wake. Na aliwatumia wana usalama vibaya kuniteka, kunipiga na kutaka kuniua kwa mara kadhaa. Unahisi ni kwa nini alitaka kufanya hivyo, ni kwa ajili ya kutunza siri hii”

“Masikini pole mume wangu. Sikumjua huyu mwanamke kwamba ni mbaya kiasi hichi japo nilikuwa nina muhisi ni mbaya na huyu ndio alimbadilisha kaka yangu. Alikuwa ana endekeza starehe kuliko kazi, wakati wa majukumu ya kitaifa, kaka yangu ana kuwa bize nay eye”

“Ndio hivyo hichi walicho kipata wana kistahili. Sipendi kukuona una toroka ukiwa na kiumbe change tumboni ila nina kuomba utakapo kuwa umefika sehemu unayo hisi ni salama. Wasiliana name kisha tujue nini cha kufanya”

“Sawa mume wangu, nina ombia jengine kwako”

“Ombi gani?”

“Nina kuomba niondoke na Ruben kwanza. Nitamtengenezea mazingira mazuri ya kukujua wewe kama ni baba. Hivyo tafadhali nina kuomba sana kwenye hili kama ni kuondoka niondoke naye kwani kumuacha na kumtenganisha mbali na mama yake tena kwenye kipindi kama hichi una weza kumuathiri akili yake na isitoshe yeye bado ni mtoto mdogo”

Caro alizungumza kwa sauti ya upole na unyenyekevu huku akinitazama usoni mwangu.

“Yeye na mdogo wake anaye kuja wote nita walea. Vizuri tafadhali mume wangu”

Nikakaa kimya kwa dakika kama tatu hivi nikitafakari ombi la Caro.

“Sawa ila nihakikishie kwamba una nijulisha kila sehemu ambayo uta kwenda”

“Usijali mume wangu nina kuhakikishia hilo”

“Sawa”

Mama Shamsa akanyanyuka na kukaa kitako.

“Tafadhali baba Shamsa usinipokonye na huyu tafadhali nakuomba”

Mama Shamsa alizungumza huku akilia. Nikavuta Caro karibu yangu na kumnyonya denda la nguvu kisha nikaingia ndani ya gari kabla sijafunga mlango nikashuka na kumfwata mama Shamsa sehemu alipo kaa.

“Nimewaacha huru wakati huu ila siku tukikutana ni lazima mulipe kwa mateso muliyo nipatia”

Nikarudi ndani ya gari na kuondoka eneo hili na kuanza safari ya kurudi nyumbani. Nikiwa nina karibia kufika nyumbani gari yangu ikasimamishwa na wanajeshi wawili. Tataratibu nikasimamisha gari huku nikichomoa bastola na kuzificha chini ya siti ya gari hili. Nikashusha kioo na mwanjeshi mmoja akasogelea kwenye kioo cha upande wangu.

“Shuka ndani ya gari”

“Kuna kosa lolote afande?”

“Una niuliza wewe kama nani, shuka ndani ya gari”

Mwanajeshi huyu alizungumza kwa ukali na taratibu nikafungua mlango na kushuka.

“Una hitajika na jenerali. Kaingie kwenye gari yetu”

Mwanajeshi huyu aliniamrisha huku akinionyesha gari lao.

“Ninaomba basi nifunge gari yangu”

Wakanipa nafasi ya kufunga gari langu vizuri kisha nikaingia katika gari lao na moja kwa moja tukaelekea hadi ikulu. Nikakuta wanajeshi wakiwa katika ujenzi wa maeneo yaliyo haribika. Nikapelekwa moja kwa moja hadi kwa jenerali Ngatuma.

“Karibu sana bwana Rashidi”

Nikastuka na kujiuliza kiongozi mkubwa wa jeshi kama huyu amelijuaje jina langu.

“Salama mkuu”

“Karibu ukae”

“Nashukuru sana”

Nikakaa kwenye kiti nilicho karibishwa.

“Naamini uta kuwa una shangaa ni kwa nini upo hapa kwa muda kama huu, si ndio”

“Ni kweli mkuu”

“Okay ipo hivi. Kuna wakati ulikuwa una shutumiwa kwamba ume husika na mauaji ya wanajeshi kwenye meli ya kijeshi. Nilikuwa nina hamu san ya kuonana na huyo mtu aliye husika na tukio hilo. Ila ulifika wakati ile amri ilitenguliwa na tukaambiwa hujahusika. Labda nianzie hapo nani amehusika kwenye tukio lile kama una fahamu”

“Kusema kweli mkuu aliye husika katika tukio lile ni mtu mmoja ana itwa DON naamini una mfahamu?”

“Sana tu nina mfahamu na ni muuza madawa ya kulevya mkubwa sana Duniani na sasa kila nchi ana sakwa na ahajapatikana”

“Ndio ana sakwa ila ni mtu mjanja sana”

“Una maanisha nini ni mtu mjanja”

“Leo hii kabla hamjapindua serikali alikuwa hapa ikulu”

“Nini?”

“Ndio Frenandes Philipe mdhamini wa uwanja mpya wa mpira yeye ndio DON amejifanyia upasuaji na kujibadilisha sura yake kabisa ndio maana imekuwa ni ngumu nyinyi kumjua. Ila raisi ana mfahamu, RPC wa mkoa wa Tanga ana mfahamu na hao walikuwa ni vibaraka wa wao kuhakikisha wana nitumia watu kwa ajili ya kuniua”

“Aisee kumbe”

“Ndio mkuu”

“Huyu mshenzi ata kuwa amesha kimbia nchini aisee. Ina bidi sasa hivi tuitangazie dunia kwamba tuna mtafuta yeye Frenandes Philipe”

“Litakuwa ni jambo zuri. Pia nina washukuru”

“Una tushukuru kwa sababu gani?”

“Kumuondoa raisi huyu madarakani kwani amenifanyia mambo mengi mabaya sana ambayo yaliniondoa maisha yangu kwenye ramani ya dunia na kuyahamishia kwenye ramani ya kuzimu.”

“Kivipi?”

“Mke aliye naye alikuwa ni mke wangu. Alinipokonya na akanitupia gerezani maweni na kusingiziwa kesi ya ujambazi wa mauaji yaliyo tokea pale Kariakoo, ikiwa nilikuwa ni mlinzi wa kawaida na nilishuhudia majambazi wakiwaua askari na walinzi wezangu wa maduka”

“Niliisikia hilo tukio nilikuwa nje ya nchi.”

“Ndio alimchukua mke wangu na akafunga naye ndoa”

“Aisee pole sana”

“Nashukuru mkuu”

“Ningependa ukawe balozi mzuri kwa wananchi kwa maana hatujapindua serikali kutokana na maslahi ya jeshi ila tume fanya hivi kutokana na uchafu mwingi ulio kuwa unafanya na serikali ya huyu mzee, wanajeshi walikuwa wana chukizwa kwa maamuzi ya kipumbavu aliyo kuwa akiyafanya”

“Nashukuru sana mkuu ila nilikuwa nina ombia moja”

“Omba kama lipo katika uwezo wangu nita lishuhulikia”

“Nina kuomba sana kama ina wezekana yule mdogo wake raisi ambaye ana itwa Caro asiuwawe tafadhali?”

Jenerali akashusha pumzi kidogo kisha akatingisha kichwa akimaanisha amekubaliana na jambo hilo.

“Ila kwa sasa asionekane nchini kwani ata uwawa. Akatafute pa kuishi hadi hali itakapo tulia ndipo aweze kuridi nchini”

“Nashukuru sana kwa moyo wako. Hakika wewe ni mtu mwema”

“Nashukuru kwa hilo bwana Rashidi. Vijana wangu wata kurudisha hadi lilipo gari lako”

“Sawa sawa”

Nikaondoka ofisini, nikaongozana na vijana walio nileta ikulu hapa na wakanipelekea hadi lilipo gari langu na nikarudi nyumbani.

“Aise nilikuwa na wasiwasi mkubwa sana. Nilihisi labda umekufa”

Shabani alizungumza mara baada ya mimi kushuka ndani ya gari.

“Mungu ni mwema nipo hai ndugu yangu, vipi wamelala?”

“Ndio, niliona nikusubirie hadi utakapo rudi kaka”

“Shukrani ndugu yangu.”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuona video call kutoka kwa Jackline nikaipokea.

“Mume wangu upo salama kweli?”

Jackline alizungumza huku akiwa ametawaliwa na wasiwasi mwingi.

“Nipo salmaa ndugu yangu. Mbona una onekana una wasiwasi, kwema lakini?”

“Kwema mke wangu”

“Nasikia serikali imepinduliwa, sasa wananchi wapo kwenye hali gani?”

“Wananchi wapo salama aliye pinduliwa ni raisi ambaye yeye alikuwa ana fanya mambo maovu kwenye nchi pia nina shukuru Mungu kwamba wamenirahisishia kazi yangu ya kumuangamiza yeye na yule mpuuzi mwezake”

“Waooo ina maana kazi imekwisha sasa mume wangu?”

Jackline alizungumza huku akitabasamu kwa furaha kubwa sana kwani kama ni adui yangu niliye mfwata nchini Tanzania amesha ondolewa madarakani ila kwa upande wa DON bado sina uhakika kama viya yangu mimi nay eye kama ime kwisha au laa.



“Mke wangu sina asilimia mia moja kama imekwisha au laa ila kutokana na pesa ambayo nimeichukua kwake sidhani kama ata kubali iweze bure namna hii”

“Hapo nimekuelewa mume wangu. Unarudi lini nyumbani sasa?”

“Mke wangu huku ndio nyumbani. Huku ndio asilili yangu najaribu kutengeneza mazingira kuhakikisha kwamba familia yetu ina hamia huku. Kwa sasa ngoja niandae mazingira ya familia yetu kuja kuishi huku. Ila nita rudi mara baada ya kila kitu kukipanga vizuri”

“Sawa mume wangu. Mimi nipo tayari kukufwata unapo kwenda”

“Nashukuru mke wangu. Naomba nipumzike kwa maana leo ilikuwa ni siku ndefu sana kwa upande wangu”

“Sawa mume wangu nikutakie usiku mwema”

“Nawe pia mke wangu. Nina kupenda”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Nikakata simu huku nikimtazama Shabani usoni mwake.

“Sasa kaka una hitaji familia yako kuhamia huku, ita kuwaje hawa vimada wako.”

“Ndugu kwani kuna wanaume wangapi wanao chepuka hapa hapa Tanzania na wake zao hawajui?”

“Ni wengi”

“Bais nami nitakuwa kwenye hao wengi”

Tukajikuta wote tukicheka. Tukaingia ndani na moja kwa moja nikapitiliza hadi jikoni. Nikakuta chakula , changua katika moja ya hotpot. Nikakala haraka haraka kisha nikaelekea chumbani, nikamkuta Tina akiwa amelala uchi pasipo kuwa na nguo hata moja na jinsi alivyo lala ni mtego tosha kwa mwanaume yoyote rijali, nikajikuta nikisisimka mwili mzima. Nikaingia bafuni na kuoga haraka haraka kisha nikarudi kitandani, sikuhitaji hata kujifuta maji, nikapanda na kumkumbatia Tina kwa nyuma na kumfanya astuke kidogo.

“Ni mimi”

“Baby umerudi?”

Tina alizungumza huku akijigeuza.

“Ndio mke wangu. Niambie”

“Safi vipi?”

“Poa”

Nilizungumza huku nikiushusa mkono wangu wa kulia hadi kwenye makalio ya Tina na nikaanza kuyatomasa taratibu. Tina hakuwa na hiyana taratibu akaanza kumchua chua jogoo wangu ambaye tayari alisha simama. Akajigeuza na akaanza kumnyonya taratibu. Baada ya kuridhika na maandalizi yake akamkalia na kuuanzisha mtanange huu wa kukata na shoka huku kila mmoja akijitahidi kuhakikisha kwamba ana mridhisha mwenza wake. Hadi tuna maliza mizunguko mitatu, tayari jua lilisha anza kuchomoza. Kutokanana uchovu kila mtu akapiwa na usingizi. Mlio wa simu yangu ukanistua, nikashuka kitandani na kuipokea.

“Haloo”

“Bado umelala mume wangu”

Niliisikia sauti ya Caro, nikaitazama namba vizuri na kuona ni namba kutoka nje ya nchi.

“Yaa si una jua jana ilikuwa ni siku ndefu sana”

“Kweli ni siku ndefu. Tumefanikiwa kufika Madagascar salama salmini ila kuna tatizo moja”

“Tatizo gani tena?”

“Akaunti zetu zote zime fungwa za Tanzania na nje ya Tanzania. Hivyo hapa tulipo hatuna pesa ya kutosha kujikimu mume wangu. Pesa iliyopo ni ya kujikimu siku mbili tatu hizi”

“Aisee poleni sana. Kiasi gani kina weza kutosha kwa kujikimu”

“Ahaa tukipata dola hata laki moja, itatusogeza huku tukiendelea kujipanga kukabiliana na maisha mapya”

“Sawa so nina weza kuwatumia pesa hizo?”

“Kama ina wezekana mumne wangu.”

“Fungua basi akaunti ya dharura”

“Sawa mume wangu ngoja nikifungua nita kuambia. Hii ndio namba nitakayo itumia huku”

“Sawa ngoja niisave hii namba”

“Poa nakupenda mume wangu”

“Nami pia”

Nikakata simu huku nikimtazama Tina anaye piga miyayo mingi.

“Nani huyo mume wangu?”

“Rafiki yangu”

“Sawa, saa ngapi sasa hivi?”

“Saa nne na dakika kumi na mbili”

“Duu muda umekwenda ngoja nikakuandalie chakula mume mume wangu”

“Sawa”

Tina akaingia bafuni, akaoga haraka haraka, akavaa nguo zake na akatoka ndani hapa.

‘Kweli maisha yana kwenda kasi leo hii Caro na kaka yake wamefulia?’

Nilizungumza huku nikiwa niemjilza kitandani. Hazikupita dakika kumia Caro akapiga tena simu.

“Honey”

“Niambie mke wangu”

“Ahaa nimesha fungua akaunti, nina kutumia namba ya akaunti na jina kupitia whatsapp”

“Sawa mke wangu”

“Poa poa”

Caro akanitiumia namba hiyo, nikaingia katika mfumo wa kibeki na nikatuma ombia la kutuma kiasi cha dola milioni mbili kuingia kwenye akaunti ya Caro na ombi langu likashuhulikiwa kwa haraka na pesa hiyo ikaingia kwa Caro. Caro akanipigia simu huku akiwa ametawaliwa na furaha sana.

“Hii yote ni yangu baby”

“Ndio ni pesa yako pia hakikisha una itumia vizuri kwa ajili ya watoto wangu”

“Asante sana mume wangu. Mungu akubariki”

“Amen hakikisha una fanya matumizi mazuri”

“Usijali mume wangu, nina imani ukija huku uta furahi na roho yako kwa maana nita piga biashara hadi ijizalishe mara dufu”

“Sawa mke wangu”

“Ngoja nifanye basi utaratibu wa nyuma kisha nita kutumia picha uone ni nyumba gani nina hitaji kuinunua”

“Poa poa”

Nikakata simu, nikaoga na nikatoka chumbani hapa. Nikasalimiana na kila mtu niliye mkuta sebleni.

“Kaka mali zote za mbaya wako zime binafsishwa na serikali ya sasa”

“Wee!!”

“Haki ya Mungu vile hiyo ndio habari inayo endelea kutangazwa sasahivi ifwatilie”

“Shem rafiki yako amechuja kama maji ya dibwi”

Nilizungumza huku nikicheka.

“Yaani jamani. Ila alicho kufanyia ana haki ya kupitia hicho anacho kipitia”

“Umeona eheee, wanawake muda mwengine sijui huwa muna tembelewa na majini ya mbuyu gani kwa maana munafanya mambo ya kipuuzi na mwisho wa siku muna umbuka kama huyu mwenzenu hapa”

“Mmmm mimi shem nina jitahidi kuoambana na hayo majini. Laiti kama ninge muacha mume wangu leo hii sijui ningekuwa wapi huko. Ila ona tulikula mihogo pamoja, tulipo pata tukala kuku pamoja ndio alipaswa kuwa na moyo huo”

“Jana alishindwa hata kushuka kwenye gari kwa aibu aliyo ipata”

Rashidi alizungumza huku akitabasamu kwa furaha.

“Yaani kweli maisha ni kama gwaride, wa kwanza ana weza kuwa wa mwisho na wa mwisho ana weza kuwa wa kwanza shem”

“Jamani tupo kwenye ukurasa mpya wa kimaisha. Ina tupasa tufikirie ni namna gani tutakavyo weza kutengeneza biashara zitakazo tuingizia pesa na kudumu vizazi hadi vizazi. Sasa hivi hatuna adui wa kutuwekea vikwazo tena”

Nilitoa wazo hilo huku Tina akiandaa vifungua kinywa mezani.

“Hilo nalo ni neon kaka”

“Hapo sehemu ume nena”

“Nasikiliza maoni yenu, je mungependelea tufungue biashara gani ambayo tuna weza kuimudu”

“Kaka mimi mabasi aisee. Napenda sana kumiliki mabasi”

“Ila jamani mabasi nayo yana changamoto zake na pia hayadumu kusema kwamba basi moja una weza kulitumia kwa miaka zaidi ya kumi au kumi na tano”

Tina alitoa wazo hilo kisha akatukaribisha mezani kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.

“Waoo leo maharage chapatti?”

“Ndio mume wangu. Nimewapikia mapishi ya kitanga leo, mujilambe hadi muchoke wenyewe”

“Aise hapo umetufikisha shem kwa maana hichi ndio chakula chetu tulicho kuwa tuna penda kula chule wakati wa mpumziko. Rashid una mkumbuka yule mama Kibonge aliye kuwa ana tuuziaga chapatti?”

“Namkumbuka sana”

“Aisee kuna siku nilishuhudia ajali yake pala Ubungo mataa daa”

“Mmmmm mambo ya ajali ya nini tena jamani. Tuna kula”

Shem alilamama.

“Vipi alikufa?”

“Ndio kaka”

“Duuu Mungu amlaze mahali pema peponi”

“Amen. Ehhee shem nirudi kwenye wazo lako, ni kweli biashara ya mabasi ina garama na changamoto nyingi sana ila mabasi haya endapo yatapata madereva wazuri, tutakuwa yanafanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara basi yana uwezo wa kuishi miaka mingi na pia haya yana jinunua”

“Hivi ni barabara ya wapi ina abiria wengi?”

“Dar to Mwanza. Dar to Arusha, Dar to Tanga. Kaka hii biashara ina pesa ndio maana una waona matajiri wanao ifanya hii kazi miaka nenda rudi mabasi yao yapo barabarani na kila baada ya muda wana toa mabasi mapya. Wao waweze sisi tushindwe tuna nini”

“Jamani wakina mama mume kunaliana na hii biashara?”

“Kama ina lipa shem tuifanye”

“Mimi nime ikubali honey”

“Sawa hiyo ni biashara namba moja imesha pita”

“Sasa honey tunaanza na mabasi mangapi?”

“Hiyo nayo pointi tuna anza na mabasi mangapi?”

“Kwa idadi hapo kaka ina tegemea tuna hitaji kuikamata barabara ya mikoa gani. Kama unavyo jua Dar es Salaam hapa ndio kitovu cha safari hivyo tuangalie na uhitaji wa mikoa mingine kama Mwanza kwa siku tuna weza kupeleka basi ngapi, Singida zina weza kwenda ngapi, Mbeya, Tanga. Moshi na Arusha kote tujapeleka mabasi. Ila ngoja nifanye uchunguzi wangu niangalie ni basi gani ambazo zina pendwa na abiria na basi gani ambazo zina dumu pia barabarani kwa maana kuna Mkorea, Mjapani na Mchina wote hawa wana tengeneza mabasi sasa kila mmoja ina bidi tuchague ni mabasi gani tuyalete kwa wingi”

“Sawa hiyo kazi naamini ipo kwa mtu sahihi na ita kamilika kwa muda sahihi”

“Ndio kaka”

“Ehee biashara nyingine, wamama muna mawazo gani?”

“Mimi nina wazo mume wangu”

“Wazo gani?”

“Biashara ya hoteli kusema kweli ina lipa na uendeshaji wa hoteli ni mzuri na una mpangilio. Kikubwa ni matangazo, kuajiri wafanyakazi wa kike wanao vutia, huduma nzuri nakuahidi mume wangu pesa ita rudi na ita ongezeaka maradufu”

“Tina ameniwahi, kwa kweli hata mimi mwenyewe nilikuwa nina penda tuwe na hoteli”

“Je tujenge hoteli ya mfumo gani, maisha ya kati au ya watu wa maisha ya juu?”

“Tuna changanya mume wangu. Japo ita kuwa ni 5 Star hoteli ila tuna weka uwiano wa vyumba vyenye hadi ya juu na vyumba ambavyo watu wana weza kulipia kwa usiku hata elfu themanini na kuendelea. Nimefanya kazi kwenye mahoteli nina ujuzi mkubwa juu ya hiyo biashara”

“Sawa eneo gani au mkoa gani tujenga hiyo hoteli”

“Kuan sehemu kama Arusha, wapo watalii wengi sana wana tembelea mkoa ule na tuna weza kujipatia pesa kupitia ujio wao kwa sababu za kitali. Dar es Salaam hapa ni jinni la biashara na uchumi wan chi hii ume shikiliwa na mkoa huu. Hivyo watu wengi sana hususani wafanya biashara wana weza kuitumia hoteli yetu na tukapata pesa. Yaani hii mikoa miwili mume wangu kama tukijenga hoteli, haki ya Mungu tuna piga pesa ya kufa mtu”

Leo ndio nimegundua uwezo mkubwa wa akili alio jaliwa Tina kipindi chote nimekaa naye ila hatukuwahi kuzungumzia maswala ya kibiashara ila leo hii nimeona kitu cha tofauti kwake.

“Okay je Tanga?”

“Tanga tuna weza kufungua pia hoteli ila mzunguko wake wa pesa sio kama Arusha na Dar es Salaam”

“Sawa nimekuelewa mke wangu. Tafuta picha za hoteli ambazo una fikiria tukijenga Tanzania ita pendaze, uta saidianana shemeji hapo”

“Sawa mume wangu”

“Wewe hatujasikia wazo lako ndugu yangu. Ni biashara gani una ihitaji?”

“Mimi nafikiria biashara ya kutengeneza kiwanda cha uzalishaji wa unga, mfuta ya kula, mchele, yaani vitu vyote vinavyo ligusa jiko la mwamamke, sijui nazi za pakti na makorokoro mengine tutengeneze. Una jua watu kusafiri sio muhimu, kwenda mahoteli makubwa pia sio muhimu, ila hapa kwenye kula ndio kila kitu. Watanzania wana penda kula vizuri, tukiwatengenezea ngano, sembe na dona safi, tuna pata wateja. Tukitengeneza sijui mafuta kama ya anizeti pia tuta piga pesa broo”

“Aisee umefikiria mbali?”

“Ndio, tukiwatengenezea maji safi ya kunywa tume, soda, juisi za chupa na boksi tume maliza. Wanao fanya hivyo wapo wachache ila na sisi tukaweka uwekezaji mkubwa. Kwanza tutata ajira nyingi sana kwa Watanzania pili tuta kuwa tuna lipa kodi nzuri serikali. Kiufupi tuta weza kubadilisha muonekano wa nchi”

“Kweli kaka hilo wazo ume litoa wapi?”

“Ahaa mrs wa Ufaransa baba yake ana makampuni makubwa ya kutengeneza hivo vitu. Basi wana piga pesa nyinngi sana. Sisi tukijitahidi tukatengeneza kahawa ile ya daraja la kwanza, sukari ya daraja la kwanza, tuna weza kushika soko la dunia”

“Ni kweli kaka hapo ume ongea cha maana”

“Nahitaji siku tuwe matajiri kwa pamoja. Mimi na Shabani tuna jua ni ndoto gani tulizo kuwa tuna zinazitamani, kama tumepata bahati ya kubutua mpira kama kombolela basi tubutue tuwaokoe wengine”

“Ni kweli kaka aisee. Tumetoka mbali”

“Sana, kipindi hicho hatuna mbele wala nyuma. Vibaka, wakorofi wa mtaa, shule ndio usisema kupigana na waalimu hadi leo tuna ishi kwenye jumba lenye hadhi kama hili kwa kweli sio jambo dogo”

“Ni kweli ndugu yangu”

“Sheby twende tukamuone mama Chausiku nahitaji kuzungumza naye”

“Sawa”

“Jamani fanyeni majukumu yenu na sisi tuna fanya ya kwetu kila kitu kiende kwa haraka na maisha yawe bora”

“Sawa sawa, mutuletee zawadi”

“Musijali”

Tukamaliza kula na kuondoka na moja kwa moja tukaelekea kwa mama chausiku na kama kawaida yake tukamkuta akikaanga mihongo.

“Yaani nyie watoto muna roho mbaya sana. Yaani ndio nini kuhama bila hata ya kuniaga, nina sikia tetesi tu kwamba mume hama?”

“Haha kwanza shikamoo”

“Marahaba hamjambo”

“Hatujambo mama. Naruhusiwa kuonja muhogo”

“Ndio una ruhusiwa”

Nikafungua deli la kuweka muhogo, nikachagua muhogo mmoja kisha nikaka kwenye benchi lililopo pembeni ya mama Chausiku.

“Ehee niambieni kwa maana nyinyi wana sio kwa ubaya mulio nifanyia”

“Hatujahama mama kila kitu kipo ndani. Ila tulikwenda sehemu kwa ajili ya mapumziko mafupi tu ya kifamilia. Ndio maana una ona tumeadimika siku mbili tatu hizi”

“Kwanza mumesikia raisi amepinduliwa?”

“Tumesikia”

“Ila bora yule baba alivyo pinduliwa kwa maana sio kwa aliyo kufanyia. Kweli Mungu atupi maombi ya mja wake”

“Umeona mama ehee?”

“Yaani sipati picha yule binti ana hali gani sasa hivi”

“Ana pambana na hali yake kwa kweli, kwa maana alicho kipanda ndio anacho kivuna”

“Na kweli aisee. Ila Rashidi nikuulize swali?”

“Niulize tu”

“Kwa nini usimsamehe mwenzako ukarudiana naye kwa maana kwa yule mzee najua alifwata pesa”

“Mama siwezi kudhubutu kufanya huo ujinga na pia una tambua kwamba nina mwanamke mwengine hivyo siwezi kurudia matapishi hata kwa bahati mbaya.”

Nilizungumza kwa msisitizo na hasira kidogo.

“Mmm nisamehe mwanangu.”

“Usijali mama yangu. Kilicho tuleta hapa ni kuja kusaidiana mama yangu. Tunazaliwa una tuona na tuma kuwa watu wazima na kupata watoto uliwasaidia pia wake zetu kijifungua.”

“Ni kweli”

“Tumeona kwa kidogo ambacho tunacho tukipige tafu mama yetu kwa maana kama unavyo ona hii biashara imedumu kwa miaka na miaka sasa. Tungependa uweze kutanua biashara yako je una hitaj mtaji wa kiasi gani ili biashara yako iongezeke au ufungue nyingine kubwa zaidi……”

Nikajikuta nikisitisha sentensi yangu mara baada ya kumuona Chausiku akitoka ndani kwao huku akiwa amependeza na kujazia mwili wake. Urembo alio kuwa nao utotoni umeongezeka mara dufu hadi akanifanya akili ikanihama na kuto kumchukulia kama dada na nikaanza kumtamani kimapenzi.



“Hee jamani Rashidi upoooo”

Chausiku alizungumza kwa furaha huku akinifwata na akanikumbatia kwa nguvu. Joto la mwili wake mlaini na ulio nona hakika ukanifanya nipate msisimko ambao kusema kweli ukazidi kuyaongoza mawazo yangu mabovu ya tamaa dhidi yake.

“Umekuwa mkubwa Rashidi”

“Hahaa hata wewe. Sema tumekuwa wakubwa sasa, niembie upo salama?”

“Nipo salama aisee. Pole nilisikia habari zako na mama alinihadithia. Pole sana”

“Nimesha poa na nilsiha sahau matatizo hayo. Ehee umerudi lini?”

“Nimerudi jana usiku”

“Aisee hongera sana nasikia umeolewa na muheshimiwa”

“Hahaa kawaida bwana”

“Mmmm ila maisha mazuri”

“Maisha ndio haya haya ya kuunga unga bwana”

“Haya bwana”

“Nasikia una mke wa kizungu na watoto mchanganyiko, hongera na wewe”

“Hahaaahaha ndio hivyo bwana. Ehee upo Dar hadi lini?”

“Wiki hii nzima kuna nyumba ya bi mkubwa nimekuja kusimamia ujenzi uishe kisha ndio nirudi Dodoma kwangu”

“Kumbe mama una jenga?”

“Ndio”

“Wapi?”

“Mbezi Mwisho kule makabe”

“Ahaa sasa una kwenda kuishi kwa wakishua”

“Hahaahaaha ndio hivyo bwana mwanangu”

“Tulikuwa tunazungumza na mama namna ya kumuongezea mtaji wa biashara yake. Si una jua maisha ni kusaidiana, mama zetu wametuzaa nasi ni jukumu letu ni kuwasaidia”

“Ni kweli. Ila Shabani upo kimya sana”

“Nakuona yaani umemuona Rashidi peke yake ila mimi nina nyoya ya mkaaa”

“Jamani nisamehe, si unajua wewe tunaonana mara nyingi ila unaendeleaje?”

“Ahaa mimi nina endelea salama hofu kwako?”

“Mimi nipo salama tu nina mshukuru Mungu ana nisaidia”

“Ehee mumehamia wapi jamani kwa maana nasikia mumehama bwana?”

“Hatujahama ila familia ipo sehemu kwa ajili ya ajili ya mapumziko”

Shababi alijibu na hakutaka kueleza ukweli wa sisi kuhama.

“Mama kama huto jail munaweza kutupeleka huko ilipo nyumba”

“Sawa hakuna shida mwanangu”

“Ila vijana munaonakana muna pesa. Kusukuma BMW X5 sio jambo la kaiwada”

Chausiku alizungumza kwa utani.

“Ahaa wapi, wewe naamini una endeshwa kwenye V8 sasa sisi na wewe nani mwenye pesa ndefu”

“Sasa yale si ya mume wangu”

“Kama amekuoa ni ya kwenu wote”

“Haya bwana mumeshinda”

Tukamsaidia mama Chausiku kuuza mihogo hii hadi ikaisha na tukaondoka eneo hili na kuelekea ilipo nyumba anayo jengewa na mwanaye.

“Waoo mumejitahidi”

Nilizungumza huku nikitazama nyumba hii inayo endelea kujengwa na mafundi.

“Ndio hivyo tuna unga unga si una jua pesa za kubana kwa mume hazitoshi kihivyo”

“Kwa hiyo hapa ina hitajika nini na nini?”

Nilizungumza huku tukiendelea kutazama nyuma hii iliyo fika maeneo ya dirishani.

“Hapa bado mambo mengi sana. Kwa hii wiki naamini nita isogeza sogeza hadi kuipaua bati kisha hata mama ana weza kuhamia ikiwa bado haijamilika kabisa. Kikubwa nahitaji kumtoa kule uswahili nimlete huku sehemu zilizo tulia, aje kuishi na wajukuu wake”

“Kwa hiyo hapa ina bidi ijengewe ukuta, kuingizwa umeme, kumalizia juu”

“Yaa”

“Una paua na nini?”

“Na bati, nilitamani kumuwekea m South ila ndio hivyo bajeti yenyewe ya kuunga unga”

“Hawa wanaojenga ni kampuni au ni mafundi wa kuunga unga?”

“Ni zile kampuni za ujenzi niliwapa milioni 15 kwa ajili ya kuanza kazi hapa nahitaji niwape milioni nyijngine kumi na tano ili kazi iweze kumalizika”

“Kwa hiyo ni milioni thelathini hii nyumba?”

“Ndio”

“Tuna weza kuidizaini ikawa kubwa kuliko hii”

“Una maanisha nini Chidi”

“Yaani namaanisha kwamba hichi kiwanja ni kikubwa. Una onaje hii nyumba ikavunjwa na ikapandishwa nyingine”

Mama Chausiku na Chausiku macho yawakatoka kwa mshangao.

“Nakuridishia milioni zako kumi na tano ulizio zitoa kwa mafundi, kisha tunashusha hapa hata gorofa moja”

“Rashidi hujaacha utani wako ehe?”

“Sio utani unajua mama yako ni kama mama yangu. Hivyo kuna hasara gani kuvunja nyumba hii ya vyumba vitatu tukapandisha gorofa ambayo tuna weza ku google na kumjengea mama.”

“Mmm!! Rashidi hicho unacho kizungumza upo serious au?”

“Nipo seriuso chausiku. Tuna mshushia mama nyumba kama ile ya jirani yake pale aliye jenga kwenye kiwanja cha mama yangu. Kitu kingine nilikuwa nimekuja kuzungumza naye nimfungulie biashara gani kubw ila hatukufika muafaka kutokana na ujio wako ulivuruga mazungumzo yetu”

“Mmmm kama nina anza kukuamini amini”

“Tatizo Chausiku bado una hisi yule Rashidi, kibaka wa mtaa ndio hadi mimi sasa hivi. Nimebadilika nimekuawa mtu mzima sasa na ninacho kizungumza nina kimaanisha. Ingia google, tafuteni nyumba za gorofa, tumuite injiani, atoe tathimini, hii ivunjwe tupandishe gorofa”

“Rashidi usije ukafanya kama jamaa mmoja hivi alikuwa na demu akamsomesha akamjengea wazazi wa mwanamke nyumba alafu demu akamkataa. Ila jamaa hakukata tamaa akawaambia wazazi wa mwanamke nataka kuwajengea gorofa munaonaje mukapisha mafundi kutokana wana mpendea pesa basi wakakubali kuhamia nyumba ndogo jamaa akavunja nyumba yote kisha akawaambia hayo ndio malipo ya usaliti, sasa isije na wewe ukatufanyia hivyo Rashidi”

Stori ya Chausiku ikatufanya tucheke kwa furaha.

“Ndugu yangu hawezi kuwafanyia hivyo”

“Yaani akifanya hivyo namuachia laana mimi ni kama mama yako Rashidi”

“Siwezi mama, wewe muiteni injiani mkuu”

Chusiku akamuita ijinia mkuu wa ujenzi wa nyumba hii.

“Kaka hembu msikilize huyu ndugu yangu mwaya”

“Eti fundi kwa mfano tukihitaji kusimamisha gorofa hapa ina wezekana?”

“Kwa eneo gani?”

“Yani tukivunja hiyo nyumba na kupandisha nyumba nyingine kubwa si ina wezekana?”

“Ndio ila munataka tuvunje hii tunayo jenga?”

“Ndio acha watafute nyumba ya gorofa ambayo wata hitaji ijengwe hapa na hii ivunjwe kabisa”

“Sawa”

“Fundi ngoja mara moja tuchague ila Rashidi nitakuamini kama unanirudishia milioni zangu kumi na tano nilizo zitoa”

“Nitajie namba yako ya benki”

Chausiku akanitajia namba yake ya benki na kumuingizia milioni kumi na sita.

“Hiyo iliyo zidi ni ya kutolea”

“Mshenzi wewe, pesa zote hizi umetolea wapi au ndio huyo mzungu?”

Chausiku alizungumza kwa furaha mara baada ya kiasi hicho cha pesa kuingia kwenye akaunti yake ya benki.

“Wewe una taka nyumba, acha maswali mengi”

“Mama tuchague aisee”

Wakaperuzi kama kwa dakika kumi hivi wakakubaliana nyumba moja nzuri ya gorofa, wakamuonyesha fundi nyumba hiyo.

“Ina wezekana kujengwa. Ina bidi tuandae ramani yake nzima kwa maana hatuwezi kujenga nyumba kwa picha ya nje, ni lazima iandaliwe ramani na wataalamu wa ofisini kwetu kisha ndio ijengwe.”

“Je kwa haraka haraka kwa kuitathimini hii nyumba ina weza kwenda bei gani?”

“Hiii kwa kuangalia si chini ya milioni mia tano mkuu. Ila ni bei ni ya makadirio hivyo ina weza kupanda au kushuka. Si munahitaji na hizi swimming pool?”

“Ndio”

“Sawa nita waomba munirushie hizo picha whatsapp kisha nami nikaae na timu ya wachoraji wangu wa ramani kisha tuta wapatia bei sahihi”

“Ina chukua muda gani?”

“Hadi kesho saa nane mchana kila kitu kita kuwa tayari na tutawapa ofa ya bure kuwavunjia hii nyumba tuliyo anza kuijenga”

“Sawa tuna subiri jibu lenu”

“Hakuna shaka mkuu”

Tukaagana nao na kuondoka nao eneo hili.

“Rashidi mwanangu hembu niambie ukweli pesa zote hizo umezipatia wapi?”

“Mama mimi ni mfanya biashara, ukiachana na majanga haya niliyo pitia”

“Aisee una jua bado sikuamini amini Rashidi”

“Utaamini kesho nitakapo walipa pesa yote mafundi”

“Mmmm haya bwana”

Simu ya Shabani ikaanza kuita.

“Ndio”

“Ahaa basi nita pitia hapo muda si mrefu”

Rashidi akakata simu na kunitazama.

“Vipi”

“Kuna jamaa nina kikao naye kidogo pale Ubungo basi uta nipitisha pale nahitaji kuzungumza naye juu ya ile biashara”

“Ahaa sawa sawa basi nitakupitisha”

“Kama huto jail Rashidi naomba unipeleke posta ila kama una ratiba nyingine nikuache uendelee?”

“No sina ratiba.”

“Kama muna ratiba nyingine basi mimi muniache nyumbani, saa kumi nina vikoba”

“Sawa mama”

Tukaanza kumpitisha mama Chausiku nyumbani kisha tukaelekea Ubungo, tukamuacha Shabani kisha sisi wawili tukaelekea Posta.

“Una kwenda kufanya nini Posta”

“Kuna rafiki yangu mmoja hivi naenda kuonana naye. Kuna biashara Fulani hivi nilizungumza?”

“Mmoja hivi, Fulani hivi, mbona una ficha ficha”

“Jamani Rashidi, okay ni mke wa waziri mkuu. Kuna biashara kama sisi wake wa wabunge na mawaziri huwa tuna ifanya. Tumechanga change na kuwekeza katika mradi wa kuuza vito vya dhahabu. Hivyo kila inapo fika mwisho wa mwaka kila mmoja ana pata gawio litokanalo na faidia Na gawio lako linategemea na kiasi cha pesa ulicho kiweka.”

“Ila leo sio mwisho wa mwaka?”

“Tulianzisha biashara mwezi kama huu miaka kama miwili iliyo pita hivyo leo ndio mwisho wetu wa mwaka ndio maana nilikuja Dar ili nikipata pesa hiyo niweze kumfanyia mama finishing ya nyumba yake”

“Ahaa hapo nimekuelewa”

“Yap”

“Ila mumeo ana faidi”

“Umeanza mambo yako. Bado hujaacha tu”

“Nazungumza ukweli, mumeo ana faidi sana. Mtoto umenona sijui kwa nini mdogo mdogo kipindi kile sikuwa na maisha mazuri ukashindwa kunikubalia”

“Ahaa zilikuwa akili za kitoto, isitoshe zile akili zenu za kihuni huni zilikuwa zinanifanya nina kuchukia sana”

“Ahaa….”

“Yaani kila ukipita ni Rashidi, Rashidi hadi nikawa nakuona mtu wa ajabu sana”

“Hivi una kumbuka ile siku niliyo kupiga busu hadi ukali”

“Hahaahaa yaani wewe”

“Yaani busu tu ukaangua kilio je ningezama chini ingekuwaje?

“Yaani sijui ningekufa. Ila nililia ile siku na nilikuwa naogopa balaa, mwili mzima ulitetemeka. Ila kuna siri moja ambayo ulikuwa huijui”

“Siri gani?”

“Siku ulipo muoa mama Shamsa roho yangu liniuma una jua hadi nililia”

“Ila wewe si ulikuwa una nikataa?”

“Yaani nilikuwa sikukutai kwa kuto kukupenda, nilikuwa nina kukataa kwa ajili ya matukio yako mara mumempiga mtu. Mara leo polisi wana kutafuta. Mara sijui mumeiba eneo gani na siku niliyo kuogopa zaidi ni ile siku nilipo washuhudia wewe Shabani na wale wezenu wawili mapacha mukimpiga mwalimu cha Mkono hadi mukamvunja jino”

“Haaa kumbe uliona?”

“Nilioan jinsi mulivyo mpiga mwalimu wa watu, nilikuwa nime jibanza kwenye ile mibuyu kule makaburini”

“Aise ile ndio ilikuwa tiketi yangu ya kuacha shule kwa maana sura yangu mwalimu cha mkono aliiona ila kija Rashidi na wale mapacha walifunika sura zao”

“Yaani mulivyo muacha amelala chini katulia nikajua mume ua aise nilitimua mbio”

“Hahaaa”

“Yaani niliogopa usiku kucha sikulala nikihisi muna umwa na siku ya pili nilitamani hata nisiende shule ila sikuwa na jinsi mama alinitimua nikaenda shule kilazima. Nikasikia Mwalimu Kikono kalazwa hospitali nikashukuru Mungu kwamba yupo kimya”

“Sema yule mwalimu alikuwa mnoko”

“Ila sio kwa kumpiga kule, yaani mulimchana chana na visu sijui inge kuwaje kama angekufa”

“Ila ilikuwa utoto”

“Yaani kuazi siku ile sikutaka hata kukubalia ombi lako”

“Hahaa”

“Wee nilikuogopa sana na askari jinsi walivyo kuwa wana kuja mara kwa mara pale nyumabni kwenu yaani ndio nilizidi kujawa na wasiwasi nikaona ukikamatwa una weza hata kunitaja na wewe”

“Alafu ile kesi mama alihonga sana hadi ikazima kimya kimya”

“Yaani ulimpa sana shida mama yako wewe”

“Ujana, ehee nikisema sasa hivi nirudishe sound zangu kwako uta nikubalia”

“Mmmm kwa sasa mambo yamebadilika sana Rashidi, nina mume nina watoto”

“Hata mimi nina mke nina watoto.”

“Mmmm ndoa yangu nina ipenda sana Rashidi”

“Hata mimi yangu nina ipenda”

“Simama hapo”

Chausiku alinionyesha moja ya mgahawa nikasimamisha gari eneo la maegesho.

“Eheee?”

“Naomba unisubirie Rashidi”

“Jibu langu”

“Jamani Rashidi”

“Ndio jibu langu, au sasa hivi una niogopa?”

“Sikuogopi”

“Ila?”

“Namuogopa mume wangu”

“Ana nini cha kukufanya umuogope?”

“Yaani Rashidi wala usisema, wee ngoja tu nionane na huyu mama”

“Niambie ana nini cha kukufanya una muogopa sana huyo mumeo”

“Rashidi mume wangu ni mtu hatari sana hivyo sipendi uje kuingia mikononi mwake kwa sababu ya kuniiba mimi, yaani ata tuua sisi sote wawili. Napenda sana kuwa na wewe ila ninapo mfikiria yeye nahisi kwamba dunia yetu mimi na wewe ina weza kuwa kuzimu, ni bora kila mmoja akazuia hisia zake na akafa nazo na ikabaki historia kwamba ulisha wahi kunipenda na mimi nilisha wahi kukupenda kwa siri tulipo kuwa watoto basi na si hapa ukubwani”

Chausiku mara baada ya kuzungumza maneno hayo akafungua mkanda wa siti ya gari na akashuka na kuniacha nikimsindikiza kwa macho jinsi msambwanda wake unavyo tingishika na kujikuta nikiimba kimoyo moyo. Hamsini hamsini mia.


ENDELEA

‘Siwezi kukuacha hivi hivi lazima nikupate tu, sijawahi kutongoza mwanamke kwa muongo mmoja khaaa!!”

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimtazama Chausiku jinsi anavyo zama ndani ya mgahawa huu.

‘Hata simba ni hatari ila mkewe ana chepuliwa na simba wengine.’

Nilizidi kuzungumz amaneno ya kunifariji. Nikaendelea kumsubiria Chausiku, nikawasha tv ndogo iliyomo ndani ya hili gari. Kila kituo cha chaneli kina onyesha namna wananchi wa Tanzania wanavyo toa maoni yao kutokana na swala la kupinduliwa kwa raisi ambaye alikuwa ana tumia madaraka vibaya na kufanya mambo ambayo wananchi walio mchagua hawakuyategemea. Baada ya dakika kama arobaini hivi, Chausiku akatoka ndani hapo na moja kwa moja akaingia ndani ya gari.

“Mbona ume chukua muda mrefu sana hadi kutoka”

Nilizungumza huku nikizima tv ya gari langu.

“Si una jua mambo ya kina mama, umbea kidogo”

“Ahaa hadi nyinyi wake wa viongozi muna umbea?”

“Wanapo kaa wanawake zaidi ya wawili, umbea haukosekani ndugu yangu. Ila nashukuru kilicho nipeleka nimekipata”

“Kwa hiyo tuondoke?”

“Ndio”

Nikawasha gari na taratibu tukaondoka eneo hili.

“Ehee niambie mume wako ni hatari kwa nini?”

“Mmmm kumbe bado una upo kwenye mazungumzo hayo?”

“Ndio kwa nini niyaache ikiwa bado nafukuzia mali yangu”

“Una jua Rashidi kwenye hili sekeseke la kumpindua raisi aliye pita. Mume wangu alichangia kwa asilimia kubwa sana. Hivyo mume wangu amependekezwa na huyu jenerali Ngatuma kuwa raisi ajaye hivyo tuna subiria miezi hii mitatu ya kijeshi iweze kumalizika kisha kampeni zifanyike kidemokrasia na mume wangu asimamishwe kuwa mgombania uraisi na kama uanvyo jua. Mtu akisha ingia ikulu basi nguvu yake sio ndogo ndio maana sihitaji tujichanganye kwenye mambo ambayo baadae yatakuwa na madhara kwetu. Kule ulichukuliwa mke na raisi aliye pinduliwa, safari hii ukimchukulia mke raisi wa sasa ata kuua. Mume wangu hapendi masihara kabisa hususani na wanao nifukuzia na hapa sipati picha akijua kwamba nina mjengea mama”

“Ina maana hatambui kama una mjengea mama yako?”

“Hatambui na mume wangu ni mtu mmoja mbinafsi. Kwao ana jenga ila kwa upande wangu wala hajali ndio maana najaribu kufanya fanya mitikasi yangu ya kina mama ambayo ana ijua nikipata pesa nina mjengea mama yangu.”

“Masikini pole, sasa ume mpendea nini mwanaume ambaye hata mama yako hamjali. Una jua nilishangaa sana mama alivyo niambia umeolewa na mbunge na bado yupo kwenye biashara yake ile ile na nyumba ile ile nilishangaa sana”

“Yaani mwenyewe ina niuma sana mama yangu kuendelea kuishi kwenye ule mtaa. Ila mume niliye mpata ndio hivyo”

“Una mpenda?”

Swali langu likamfanya Chausiku kukaa kimya kwa dakika kadhaa. Akavuta pumzi nyingi kisha akanitazama.

“Kwa nini umeuliza swali hilo?”

“Nimekuuliza kwa sababu, kama ni mtu anaye kupenda hawezi kuacha familia ya mke wake kuteseka”

“Ana nipenda ila tatizo ni ubinafsi”

“Hapana wewe ana unampenda. Hilo ndio swali langu?”

“Ndio nina mpenda”

“Macho yako yana danganya. Ina onyesha humpendi ila una ishi naye kwa sababu fulani”

“Sababu gani ikiwa mtu nina mwaka naye wa saba huu”

“Haijalishi una weza kukaa na mtu hata miaka ishirini ila moyo wako usimpende. Na kuendelea kuishi naye ikawa ni mateso tu kwako”

“Rashidi una ongea sana”

“Siongei sana ila nina kueleza ukweli”

“Haya nina mpenda ila sio sana”

“Kwa nini sio sana ikiwa mtu umezaa naye na muna watoto wangapi?”

“Boy and girl”

“Ina maana wawili?”

“Ndio”

“Ona sasa, umempendea pesa zake?”

“Rashidi mbona una nichimba chimba?”

“Nijibu”

“Ndio, maisha yangu yalikuwa ni magumu kama unavyo muona mama yangu. Nilivyo feli Form four wewe mwenyewe una jua sikuwa na pa kwenda zaidi ya kupigizana kelele na mama pale nyumbani. Ulivyo oa ndio kabisa nilizidi kukata tamaa kwa maana nilikuwa nina kuogopa ila moyoni nina kupenda na nikachelewa kufungua hisia zangu kwako. Hivyo nilivyo mpata yeye nikaona bora shida zangu zipungue na nivumilia mateso anayo nipatia”

“Mateso gani?”

“Ahaa ni ndoa Rashidi, usione watu wana ishi na hawa viongozi ukahisi wana furaha. Maisha wanayo pitia ni mungu mwenyewe ndio anaye jua.”

“Ina bidi tutafute sehemu tukae tuzungumzie hili”

“Tafadhali Rashidi sihitaji tuonekana kwenye hoteli yoyote. Mume wangu ana wapelelezi kila mahali”

“Kwa hiyo hutuwezi kuingai hoteli yoyote kisa yeye?”

“Ndio Rashidi wewe turudi tu kwa mama”

“Tunba kwenda hoteli”

“Rashidi uta niudhi, kama vipi naomba nishuke nikodi bajaji nirudi nyumbani”

Chausiku alizungumza kwa msisitizo huku akijifuta machozi usoni mwake.

“Poa siwezi kufanya jambo litakalo kuumiza”

Nilizungumza huku nikiendelea kuendesha gari hili taratibu kutokana na wingi wa foleni ya jiji hili la Dar es Salaam.

“Ila samahani”

“Samahani ya nini?”

“Kukukatalia kwenda hotelini. Sihitaji upate matatizo zaidi”

“Ina maana mumeo ana kutesa sana”

“Tuiache hiyo mada Rashidi”

“Niambie mumewako ana kutesa sana?

“Nimesha kuambia mbona”

“Okay, sasa dawa yake ina chemka”

“Dawa gani?”

“Kukuchukua wewe”

“Hahaa Rashidi una hitaji kufa ehee?”

“Sihitaji kufa ila lazima apate maumivu kama unayo yapitia wewe. Unajua tukiachana na hisia za kimapenzi kati yetu. Wewe ni sawa na mdogo wangu ndio maana nimechukua jukumu la kumuangalia mama na kumfanyia kitu kama mwanaye wa kumzaa. Hivyo hata wewe ni lazima nichukue uangalizi juu yako”

Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya Chausiku kunitazama kwa macho yaliyo jaa huzuni. Nikatoa kitambaa mfukoni mwangu na kumkabidhi kwa ajili ya kujifuta machozi”

Taratibu akajifuta machozi.

“Asante”

“Usijali”

Ukimya ukatawala kati yenu. Sikutaka kumsemesha chochote Chausiku kwa sasa huku akilini mwake nikiwa nina jaribu kupanga mipango ya kudili na mume wake. Nikatoa simu yangu mfukoni na kumpigia Shabani.

“Kaka’

“Niambie ndugu yangu”

“Tuna karibia kufika Ubungo hapa. Bado upo?”

“Ahaa…nimeondoka muda kidogo ndugu yangu, nimeelekea Sinza na huyu jamaa kama ina wezekana una weza kuelekea tu home kwa maana bado mizunguko ipo mingi mingi”

“Poa poa kaka”

Nikakata simu na kuirudisha usoni.

“Mke wako ni raisi wa wapi?”

“Ufaransa”

“Mama na Shamsa ndio wana ishi huko?”

“Ndio”

“Vizuri”

“Nilitamani siku mama aende kule sema mambo yaliingiliana”

“Aliniambia na nilimfahamisha mr anitafutie hati ya kusafiria kwa ajili ya mama ila akaingilai huku na kule na mambo yakachelewa”

“Kwa hiyo hakukusaidia kwa chochote?”

“Ndio”

“Yaani una mwanaume wa ajabu sana”

“Ahaa ndio maisha hayo”

Tukafika Kimara kwa mama Chausiku. Kabla Chausiku hajashuka ndani ya gari nikamshika mkono wake wa kulia.

“Chausiku”

“Bee”

“Hisia zangu bado zipo kwako, nilipo kuona nisiwe mnafki, hisia zangu ziliweza kufufuka upya. Nilijaribu kuzizika kwenye kaburi la sahau ila kwa bahati mbaya zimefufuka tena. Tafadhali Chausiku fikiria kuhusiana na hili”

Chausiku akashusha pumzi nzito. Kwa haraka nikamsogelea na kumnyonya denda zito kwa dakika kama mbili hivi na nikamuachia na kumfanya ashushe pumzi nyingi.

“Nahisi leo pia uta lia”

Chausiku akatabasamu huku akinitazama usoni mwangu.

“Chausiku nina kupenda”

“Najua hilo Rashidi ila ndio hivyo tumesha chelewa kwenye haya maisha”

“Ila tuta nafasi ya kutengeneza background yeyu”

“Kivipi Rashidi ikiwa mimi na wewe kila mtu ana familia. Ukiachilia familia tu tuna watoto, kwa nini tuwadhulumu watu wengine haki ya furaha yetu kisa hisia zetu. Sidhani kama wanao wata furahia kuona una watafutia mama mwengine na mimi sidhani kama watoto wangu wata furahi kuona nina watafutia baba mwengine labda itokee mwana familia mmoja kwenye familia zetu amefariki hivyo tuna weza kufanya hivyo vitu ila kwa sasa tafadhali Rashidi tuache hili jambo”

Chausiku alizungumza kwa hisia kali sana.

“Nikuulze swali”

“Niulize”

“Una nipenda bado?”

“Rashidi bwa….”

“Niambie una nipenda bado?”

“Ndio nina kupenda”

“Kama ni hivyo endelea kunipenda na mimi nina kupenda. Kesho acha tushuhulike swala la mama kisha mambo mengine yatafwata”

“Sawa”

“Ila bado mumeo nina mfikiria hawezi kukutesa na watu kama sisi tupo”

“Usiazishe vita na yule mwanaume ata kupoteza Rashidi”

“Kama ni pesa nina pesa nyingi kuliko yeye, ila anacho nizidi yeye ni kujulikana na connection ila kama utakubali kushirikiana nami kwenye hili ninalo liwazia basi itakuwa ni nafasi ya wewe kuishi kwa Amani”

“Una maanisha nini?”

“Mumeo anakwenda kuwa raisi si ndio?”

“Ndio”

“Kama ameshindwa kukuheshimiu wewe mke wake uliye mzalia watoto wawili, ataweza kuwaheshimu Watanzania mamilioni atakao waongoza”

Chausiku Akaka kimya huku akiendelea kunisikiliza kwa umakini

“Kama atachukau madaraka hato kuwa na muda na wewe wala familia yako. Ili kuweza kumkatisha kasi yake basi ni kudili na watu wake wanao hitaji kumpatia nguvu, ni heri akasimama mwengine kuliko yeye.”

“Rashidi”

“Naam’

“Familia yangu ina malengo na mume wangu alikuwa na malengo ya kufikia kuwe raisi wa nchi hii hivyo tafadhali kwa madhaifu yake ambayo nimesha yazoea nakuomba usije ukayatumia kukatisha ndoto zake. Kama ni kuteseka ni mimi ndio nina teseka na nimesha zoea. Tafadhali nina kuomba sana Rashidi kama una nipenda basi acha haya mambo yaende kama yanavyo kwenda”

“Chausiku acha upuuzi na huo unao ongea ni ujinga. Kwani hakuna mwanaume ambaye ana kukupa furaha. Mimi na wewe tumejuana kwa miaka mingi sana na huu ni mwaka wa ngapi. Tumecheza kombolela pamoja kwa nini nikuache uteseka kwa nini nikiuache maisha yako yaliyo baki uishi kwa mateso. Eheee?”

Nilizungumza kwa kufoka hadi Chausiku akaanza kutetemeka kwa woga.

“Nina kupenda na una lijua hilo. Kwa nini nikiache una teseka na wewe ndio mwanamke wa kwanza kukupenda katika moyo wako na wazazi wetu walikuwa na ndoto kuona mimi na wewe tuna kuwa mke na mume ila maisha tu yametugawanya ila kama tumekutana tena ni wakati wa sisi kujipanga upya. Na safari hii siwezi kukubali wala kuona kitu chcohote kina simama mbele yetu ni lazima uwe wangu”

Nilizungumza kwa hasira na kwa msitizo hadi Chausiku akaanza kutetemeka kwa woga kwa maana ana zifahamu vizuri hasira zangu.

“Rashidi”

“Hakuna cha Rashidi, wewe ni wangu na huwezi kulikwepa hilo”

“Nisikilize basi ninacho kuambia”

“Sema”

“Kunikasirikia sio solutiokn na sipendi kuiona hasira yako”

Chausiku alizungumza kwa sauti laini na iliyo jaa mahaba mengi. Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama machoni mwake.

“Nakuomba nifikirie juu ya ombi lako?”

“La kukutongoza kwa mara ya ishirini au?”

“Hahaaa”

“Ndio kwa maana toka nimeanza kukutongoza, kukufukuzia ukienda kuoga mara ya ngapi hii”

“Haya bwana mimi nazungumzia juu ta hizi ndoa zetu. Kwa mwanaume wewe kukimbia familia ni rahisi ila mimi ni mama ambaye wanagu nimewaweka miezi tisa tumboni na nina jua uchungu wao”

“Sawa wewe kaa na fikiria upange nini cha kufanya”

“Sawa”

Chausiku yeye mwenyewe akanisogelea na tukapiga denda la hisia kali kwa dakika zaidi ya tano kisha tukaachiana.

“Nakupenda sana Rashidi”

“Nakupenda pia chausiku wangu”

Chausiku akafungua mkanda wa siti ya gari na akashuka.

“Hutaki kumuaga mama mkwe wako mtarajiwa”

Nikajikuta nikitabasamu. Nikashuka ndani ya gari na kuingia ndani, tukastuka sana kumkuta mama Chausiku akiwa na mwanaume ambaye simfahaumu ila nilipo mtazama Chausiku nikamuona akistuka.

“Mume wangu ume kuja saa ngapi mbona hujaniambia?”

Chausiku alizungumza kwa kubabaika huku akionyesha uso wa wasiwasi. Hapa ndipo nikamtambua huyu jamaa vizuri.

“Nimekuja muda kidogo”

“Rashidi karibubu ukae”

Mama Chausiku alizungumza ika nibidi kukaa kwenye moja ya sofa.

“Rashidi huyu ni mume wangu. Baby huyu ni Rashidi kaka yangu”

“Una kaka mbona hujawahi kuniambia”

“Ahaa huyu ni mtoto wa rafiki yangu ambaye tulikuwa ni amajirani zetu kabla ya hilo eneo kuuzwa na kujengwa hiyo gorofa hapo nje. Ni kijana niliye mlea mimi mwenyewe hivyo ni kama mwanangu wa kumzaa”

Mama Chausiku ikabidi aingilie kati haya mazungumzo.

“Ohoo ndio ulikuwa umeongozana na mke wangu muda wote huo?”

“Jamani mume wangu huyu ni ndugu yangu”

“Hata kama ni ndugu yako sio kuzunguka naye mji mzima hadi watu wananipigia simu wamekuona sehemu fulani fulani. Unajua kabisa sipendi ushenzi na sitaki uwe karibu na mtu yoyote. Kwanza huyu sura yake sio ngeni huyu si ndio yule gaidi wa Al-Shabab?”

Mume wa Chausiku alizungumza kwa ukali bila kujali uwepo wa mama mkwe wake wala uwepo wangu, jambo lililo nifanya hasira yangu ianze kuchemka taratibu huku nikimtamani sana huyu jamaa ni mtie mitama ambayo itamfunza heshima huwezi kwenda ukweni na kujifanya mtawala wa kwa kila mtu.



“Shemeji”

Niliita kwa sauti ya upole kidogo.

“Kaa kimya sizungumzi na wewe. Jiandae na tuondoke sasa hivi sitaki upuuzi”

Mume wa Chausiku alizungumza kwa ukali sana.

“Chausiku hakuna kuondoka”

Nilizungumza kwa kujiamini na kumfanya kila mtu kustuka.

“Una semaje wewe boya”

Mume wa Chausiku alizungumza huku akisimama kwa jazba na kunisogelea.

“Mkwe mkwe”

Mama Chausiku alijaribu kumzuia mkwe wake kwa sauti ila tayari jamaa alisha nikaribia. Akajaribu kunipiga ngumi ya uso ila nikaupangua mkono wake, nikiwa hapa hapa kwenye kochi nikampiga mtama ulio muangusha chini.

“Jamani achene ugovi, achene jamani”

Mama Chausiku alilalama huku Chausiku naye akiwa amejibanza kwenye moja ya kona huku akitetemeka kwa woga. Mumwe wake akanyanyuka na kurusha Makonde mfululizo, nikayakwepa yote nikamtandika ngumi moja ya mbavu uliyo mfanya ayumbe huku akitoa mguno wa maumivi makali kwa maana upiganaji wake umenikumbuka zama zangu za mapambao ya ulingoni tena mapambano ya kifo. Jamaa akachomoa bastola kiunoni mwake, kabla hata hajafanya chochote nikaruka hewani na kuipiga teke kwa mguu wangu wa kulia na kuifanya iangukie mbali.

“Jamani achene, Rashidi mwangu achaaa”

Mama Chausiku alizungumza huku naye akiungana na mwanye kwenye kulia. Mkwe wake hakutaka kuacha ugomvi huu alio uanzisha pasipo sababu ya msingi. Akajarubu kurusha teke nikainama chini na nikampiga ngumi nzito iliyo tua kwenye sehemu zake za siri na kumfanya aanguke chini na kujishika sehemu zake za siri huku akilia kwa uchungu sana.

“Ukihitaji usiumie zaidi, ondoka humu ndani na kuanzia hivi sasa Chausiku sio mke wako. Tuna elewana?”

Niliuzungumza huku nikiiokota bastola yake nikaikoki na kumuelekezea kichwani mwake.

“Umenielewa wewe mbwa?”

Niliuzungumza kwa msisitizo huku jasho likinitiririka, japo ni pambano dogo ila nimetumia uwezo mkubwa sana kijilinda ili nisiumizwe na huyu mpumbavu.

“Ndio”

“Rashid…….”

Chausiku alitaka kuzungumza kitu ila nikaweka kidole kimoja mdomoni mwake nikiashiria kwamba akae kimya hili halimuhusu kabisa.

“Sasa nikuone una ikabili hii familia au una nyanyua mkono wako kumpiga Chausiku nitakacho kufanya ni sawa sawa nilicho wafanya wengine. Pumbavu sana wewe, una kazi ya kumfokea mwanamke kama una mfokea mwanaume mwenzako. Chausiku niangalie”

Chausiku aliniangalia huku mwili ukimtetemeka.

“Una mpenda huyu fala?”

Taratibu mume wake akageuza sura na kumtazama Chausiku aliye shikwa na kigugumizi cha kuzungumza.

“Sema una mpenda?”

Chausiku akatingisha kichwa akimaanisha kwamba hampendi.

“Lete kalamu na karatasi akuandikie talaka hapa”

“Talaka!?”

Jama alihamaki

“Usisjhange, leo una mpata talaka. Una kazi ya kumtesa binti wa watu una hisi hana wazazi yeye. Sasa kwenye talaka yako kuna kipengele cha yeye kuishi na wanaye sasa ukifanya ujinga hata hilo unalo liwaza kichwani mwako halito kuwa”

“Bwana shemeji nakuomba tuzungumze kama wanaume, nimejua nime kosea ila kumpa talaka mke wangu hiyo itakuwa ngumu bwana shemeji”

Mume wa Chausiku alizungumza kwa sauti ya upole na unyonge huku akijitahidi kukaa kitako na mikono yake ikiendelea kuwa sehemu zake za siri.

“Chausiku una shangaa nini, ingia ndani chukua kalamu na karatasi uje hapa. Ndoa ya kiislamu broo ina vunjika muda wowote na nina taka umpatie talaka nne ili akili zikukukaa vizuri kichwani mwako, olewe akiachika huko ndio umrudie mpuuzi mmoja wewe”

Nilizungumza huku kwa msisitizi na kumfanya Chausiku kukimbilia ndani na baada ya dakika akatoka akiwa na kalamu pamoja na karatasi akaviweka mezani. Nikaa kwenye moja ya sofa huku nikiwa baso nimeishika bastola yale na kuielekezea kwake.

“Usikae chini suti yako ikaendelea kuchafuka. Kaa juu kochi ambalo hujachangia hata shilingi mia moja”

“Mama nisamehe kwenye hili kwa maana huwezi kuwa na mkwe ambaye hana mchango wowote kwenye maisha yako na ya mwanao. Hivyo mzee shika peni na karatasi hiyo hapo uanze kuandika hichi kipengele ambacho ni muhimu ukileta upuuzi uta ujua ugaidi wangu na nita kuchangua kichwa hapa hapa au nita kwenda kukuulia sehemu ambayo hakuna atakaye iona maiti yako”

Mume wa Chausiku akaanza kutetemeka, jeuri kiburi vyote vimeyayuka mithili ya barafu juani.

“Andika, mimi hapo uta jaza jina lako na sitaki kulijua jina lako. Nina achana na mke wangu wa ndoa Chausiku. Jukumu la kulea watoto na kuwasimamia ata ishi nao na mimi nita toa pesa za matumizi kama inavyo paswa. Hayo mengine uta yajua mwenyewe huko mbele mambo ya talaka ila niliyo yazungumza yaandike”

“Ila shemeji…..”

“Mzee hakuna cha shemeji. Wewe una weza kunifokea mbele ya mama yangu. Tana kwetu, mtaa nilio zaliwa, angalia hapo dirishani kwenye hilo gorofa kabla halijajengwa ndipo nilipo zaliwa. Unatuchimba mkwara kwa sababau wewe ni mbunge au?”

Nilimfokea mume wa Chausiku na akakaa kimya.

“Tena mke wako amenisimulia majanga yote unayo mfanyia. Una mnyanyasa una mnyanyapaa. Mbunge una tembele mshangingi, mama yako mkwe una muacha ana endelea kupika mihogo. Unajiita wewe ni mwanaume, aisee kama nikiwa hai na nime rudi kwenye nchi yangu. Sinto ruhusu hii familia yangu iteseka kwa maana huyo mke wako unaye muona anazaliwa nina muona, sasa ndoa yetu ime fika mwisho. Andika kabla sijakakuua”

“Mke wangu nitete basi kwa mumeo”

“Hata mimi nimeyachoka maisha yako. Nilikuwa nina ishi kwa ajili ya wanangu tu ila upendo ulisha kwisha kwako siku nyingi. Mwanaume malaya una niletea hadi wanawake nyumbani alafu una taka kuniita mimi mumeo. Aisee siwezi kuendelea kuishi hayo maisha, niache usije ukaniua maradhi mengi sasa hivi”

“Kumbe alikuwa ana kuelea hadi wnaaume ndani?”

Mama Chausiku aliuliza kwa mshangao.

“Ndio mama”

“Kwa nini usinge niambia”

“Mama hata ninge kuambia ungefanya nini kwa mfano. Mwanaume ana roho mbaya, mpigaji, una hisi ungemtoa kirahisi kama hivi. Mwanaume ana lala na bastola chini ya mto wa kitanda kweli huyo ni mwanaume wa kuwa naye mimi”

Chausiku alizungumza huku akilia kwa uchungu.

“Andika aisee”

Mume wa Chausiku akaanza kuandika taratibu talaka hii.

“Ongeza karatasi kuwe na kopi mbili”

Chausiku akaingia ndani na akarudi na karatasi nyingine. Mume wake akamaliza kuandika karatasi ya kwanza na akahamia kwenye karatasi ya pili.

“Andika kama ulivyo andika huku”

“Sawa shemeji”

Alijibu kwa woga huku akiendelea kuandika. Akamaliza kuandika, nikazipitia karatasi zote na kuziona zina fanana maandishi.

“Tia sahihi, mpe Chausiku atie sahihi. Mimi shahidi natia sahihi na kuanzia sasa ndoa hakuna. Nenda sehemu yoyote hii ndoa haiwezi kurudi na kesho. Watoto wa Chusiku waleta Dar es Salaam. Mwanaume mshenzi una kazi ya kumuingizia mdogo wnagu wanawake wezake hadi ndani alafu tukuchekee tu kisa una pesa. Aisee, tulizaliwa masikini, mama zetu waliuza miago na chapati kutulea hadi tukafika hapa. Usilete utani kabisa nah ii familia na nikuambie tu, ulibugi kwenye familia siyo, ulimjua Chausiku na mama yake ila hukujua back up iliyopo nyuma yao.”

Nilizungumza kwa kujiamini, Chausiku akatia sahihi na mumewe akatoa sahihi.

“Karatasi moja yako na nyingine ni ya Chausiku. Angalizo, ukihisi kama hili lililo fanyika ni upuuzi au ni maigizo, na ukajaribu kumdhuru yoyote kati yetu au watoto wa Chausiku nitakacho kufanya huto imalizia miezi mitatu ya kusubiria ili uwe raisi wa hii nchi. Umenielewa?”

“Ndio”

Nikachomoa magazine ya bastola hii, nikatoa risasi zoze pamoja na risasi iliyo kwenye chamber. Nikaigawanyisha bastola hii vipande vipande na nikachukua spring inayo iwezesha risasi kufyatuliwa na kutoka kwa kasi ndani ya bastola.

“Hii nabaki nayo na hivi nenda navyo ondoka sasa hivi”

Akakusanya vitu nilivyo vitoa kwenye bastola zikiwemo na risasi kisha akaondoka eneo hili huku nikimsindikiza akatoka nje na kutokemea kwa miguu kwenye mtaa huu.

“Rashidi, Mungu wangu huyu mwanaume ata rudi tena ana ata tufanyia kitu kibaya Rashidi nina hofu hata ya kuendelea kuishi hapa. Tafadhali tuondoke”

Chausiku alizungumza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi.

“Kama ni hivyo kusanyeni vitu vya muhimu niwapeleke tunapo ishi sasa”

Chausiku na mama yake wakaondoka sebleni hapa na baada ya muda wakatoka wakiwa na mabegi. Tukaingiza mabegi ndani ya gari na kufunga nyumba hii kisha tukaondoka. Moja kwa moja niakelekea katika nyumba ninayo ishi na familia ya Shabani.

“Karibuni jamani ni suprize gani,. Wifi umekuja?”

Mke wa Shabani alizungumza kwa furaha huku wakipokea mizigo.

“Ndio wifi yangu tumewafanyia suprize”

“Ni kweli”

“Jamani hawa ni wageni wetu na tuta ishi nao hadi pale watakapo sema tumechoka”

“Aisee mwangu Rashidi hapa ume panga au?”

“Tumenunua na ndugu yangu”

“Aisee kweli nyinyi ndio marafiki. Toka utotoni hadi ukubwani”

“Ndio hivyo mama, jisikieni mupo nyumbani na salama”

“Tina mkwe wangu una endeleaje?”

Chausiku akanitazama usoni kwa macho ya kuiba kidogo.

“Salama mama karibuni sana”

“Nashukuru”

“Huyu ndio wifi yetu.”

Chausiku aliuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Ndio”

Nilijibu huku nikitabasamu ila najua jibu langu lime urarua moyo wa Chausiku.

“Tina huyu ndio mwanangu Chausiku”

“Nashukuru kukufahamu wifi”

“Nashukuru”

Wakakumbatiana. Haukupita muda mwingi Rashidi akarudi na kwapamoja tukajumuika kupata chakula cha usiku na tukiwa wawili nikamueleza kila kilicho tokea katika siku ya leo.

“Ila kaka hapo huoni kama uta kuwa na changanya mafaili?”

“Kivipi?”

“Chausiku anakupenda alafu upo na Tina huoni kama ita kuwa ina muumiza sana”

“Nalijua hili ila natafuta namna ya kulitatua”

“Usitake kuniambia kwamba una muacha Tina”

“Tina siwezi kumuacha kwa maana huyu demu ana madini kichwani”

“Umeona ehee?”

“Yaa ila cha kufanya nita wapasukia ukweli wote wawili. Ikiwezekana niwe na wake wao wawili, huku Jackline akiwa ndio mke mkubwa”

“Kwa mfano wamekubali je huyo mzungu wako ata kukubalia?”

“Hapo ndipo ninapo pawazia kwa maana Jackline ni mtata balaa”

“Ila kuwa makini kaka, usije ukapoteza familia unayo ipenda kwa ajili ya mepenzi si unajua kwamba mwanamke akisema imekwisha ana maanisha kweli?”

“Ndio kaka”

“Sawa mimi nikutakie kila laheri”

“Nawaona muna punga upepo”

Chausiku alizungumza huku akitufwata kwenye kibanda hichi cha kupumzikia.

“Yaa kidogo”

Shabani alijibu huku akinyanyuka.

“Una kwenda wapi sasa na wewe?”

“Naongeza kinywaji”

Shabani alizungumza huku akimuonyesha Chausiku chupa ya bia iliyo isha. Shabani akaondoka na Chausiku akaka kwenye kiti kinacho tazamana na kiti changu.

“Una mwanamke mzuri”

Chausiku alizungumza huku akiweka glasi ya juisi mezani.

“Hata wewe ni mzuri”

“Nikuulize swali Rashidi”

“Niulize?”

“Hivi una wanawake wangapi kwa maana niliye taarifiwa ni mzungu na yupo huko Ufaransa na huyu vipi?”

“Pia ni mwanamke wangu”

“Rashidi una nijibu kirahisi una jua ni jinsi gani ninavyo jisikia moyoni mwangu. Naumia kwa majibu yako, una jua fika kwamba nina kupenda na nina kuhitaji kwenye maisha yangu. Wewe una mwanamke mwengine una hisi nita jisikiaje”

“Ila hatukujua kama tuta fikia hapa. Kipindi nina anza mahusiani na yule binti wewe upo ndani ya ndoa na ndoa yako leo ndio imevinjika.”

“Najua na nina lielewa hilo. Ila nisiwe muongo, siwezi kuishi na mke mwezangu ndani ya nyumba moja”

“Kwa hiyo una takaje?”

“Kama mama ata baki hapa basi acha abaki, mimi nita tafuta hoteli au nyumba yoyote ya kupanga niishi huko na wanangu. Ila kukaa hapa sinto weza”

Chausiku alizungumza huku akionekana akimaanisha.

“Chausiku”

“Bee”

“Nina mpango wa kumjengea mama sasa hivi. Hili ninalo lizungumza sio ombi ni amri, huto kwenda kuishi sehemu yoyote zaidi ya hapa nyumbani kwangu hadi pale nyumba ya mama itakapo kamilika.”

“Ila Rahis…”

“Hakuna cha ila. Au unataka mume wako arudi na kukuua si ndio?”

Nilizungumza kwa kufoka japo kwa sauti ya chini ila ukali wangu ukamfanya Chausiku kuwa mpole na mnyonge kidogo.

“Ila Rashidi nitasikia wivu nikiwaona muna lala pamoja?”

“Vumilia kwa maana nita lala na wewe pia”

“Rashidi”

“Nimemaliza. Kuanzia hivi sasa wewe ni mke wangu na nina mamlaka juu yako, tuma elewa?”

“Ndio”

Chausiku alijibu kwa sauti ya unyonge huku akinitazama usoni mwangu.

“Jiandae nahitaji tukalale hoteli”

“Leo”

“Sasa hivi”

“Kwenye hilo hapana Rashidi”

“Kwa nini?”

“Nimeachana na mwanaume leo hii hii na leo hii hii tukalale wote. Una hisi mama atatuchukuliaje. Isitoshe Rashidi hapa nilipo nipo kwenye siku zangu hivyo hata tukienda huko hotelini hatuto fanya chochote.”

Nikamtazama Chausiku kwa sekunde kadhaa. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama kwa muda kidogo kisha akanitazama usoni mwangu.

“Si upokee”

“Jamaa ana piga”

Chausiku alizungumza huku akinigeuzia simu yake na nikaona namba ya mume wake.

“Poke na weka loud speaker”

Chausi akafanya kama nilivyo muagiza.

“Nisikilize wewe mwanamke. Umenikana mbele ya huyo kaka yako mseng** na ukajiona mnanja kukubali kusaini hii talaka feki. Sasa nina kuhakikishia nita kuua wewe, wanao, mama yako na huyo mseng** kaka yako. Na nikiwa raisi hakuna hata mmoja wenu nita muacha hai, subiri muone”

Maneo ya ukali yakamfanya Chausiku kuanza kutetemeka kwa woga hadi simu ikamponyoka na kuanguka chini kwa maana woga umemfanya hadi nguvu za mikono kumuishia.



Kwa haraka nikaiokota simu ya Chausiku na kuanza kuizungumza.

“Ukijaribu kufanya unacho kifanya. Nina kuhakikishia ikulu huto iona, na utaisikia kwenye bomba”

“Hahaahahaa hadi kufika huwezi kuniangusha mpuuzi wewe na nina kuambia nita kuonyesha mimi ni nani”

Mume wa Chausiku alizungumza kwa dharau kisha akakata simu.

“Rashidi wanangu itakuwaje MUNGU wangu!!”

Chausiku alizungumza huku akiwa amepagawa kisawa sawa.

“Hei Chausiku nisikilize”

Nilizungumza huku nikimshika Chausiku mikono yake na akanitazama machoni mwangu huku machozi yakimbubujika.

“Wanao nyumbani uliwaacha na nani?”

“Na dada wa kazi”

“Mpigie simu”

“Alafu nimuambiaje”

“Umuulize juu ya watoto”

Chausiku akaikwapua simu yake kiganjani mwangu na kuanza kuitafuta namba ya dada wa kazi, akaipata na kumpigia simu.

“Halima Halima”

“Upo wapi?”

“Watoto?”

“Sasa nisikilize Halima wachukue watoto na uwapeleke kule kwa mama Fatuma sasa hivi”

“Wewe fanya kama nilivyo kuambia nipo njiani nina kuja kuwachukua hakikisha kwamba hupokei simu za baba yako wala kumueleza upo wapi. Umenielewa”

“Nina kuja usiku huu huu”

Chausiku akakata simu na akasimama.

“Rashidi ina bidi niende Dodoma sasa hivi”

“Huwezi kwenda peke yako ni lazima twende pamoja”

“Sawa fanya basi hivyo”

Tukatoka katika kibanda hichi, na kuingia ndani.

“Shabani tuna kwenda Dodoma sasa hivi”

“Kuna nini?

“Tuna kwenda kuchukua watoto wa Chausiku, mr wake ana hitaji kuwadhuru, nipatie bastola”

“Vipi tuongozane?”

“Hapana baki hapa uwalinde hawa.”

“Sawa kaka”

“Usimuambie mtu yoyote kama tumekwenda Dodoma”

“Sawa”

Tukatoka ndani na kuingia ndani ya gari. Tukaondoka nyumbani hapa kabla hata hatujafika mbali, simu yangu ikaanza kutoka, nikaitoa mfukoni na kuona namba ya Tina.

“Hei”

“Baby muna kwenda wapi mbona muna ondoka?”

“Kuna tatizo limetokea hivyo nita kwenda kulishuhulikia. Kaa ndani na usimuambie mama asijae akapata preshe”

“Niambie mume wangu ni nini?”

“Wewe subiri turudi”

“Sawa mume wangu kuwa makini”

“Usijali”

Nikakata simu na safari ikazidi kusonga mbele. Tukaingia kwenye moja ya sheli, nikajaza gafi mafuta tanki nzima na safari ikaendelea kusonga mbele.

“Rashidi ongeza kasi”

Chausiku alizungumza huku akihangaika hangaika kwenye siti yake.

“Aisee nina tembea na spidi mia mbili, nikienda zaidi ya hapa tuna kufa. Au una taka usiwaone wanao?”

“Sawa basi endesha tu unavyo weza”

Safari ya kufika Dodoma ikatuchukua masaa matano na nusu kwa maana njiani nilijitahidi kuhakikisha kwamba nina endesha gari kwa uwezo wangu wote kuhakikisha tuna fika mkoani Dodoma. Chausiku akanielekeza hadi kwenye nyumba ya rafiki yake ambaye alimpa maagizo mfanyakazi wa ndani kuelekea na watoto.

“Ngoja nimpigie simu”

Chausiku alizungumza huku akiminya minya simu yake kisha akaiweka sikioni.

“Fatuma shosti yangu nimesha fika nipo hapa nje.”

“Ndio shosti nimesha fika”

“Haya”

Chusiku akakata simu.

“Mlinzi ana tufungulia geti”

Hazikuisha hata dakika mbili geti hili kubwa likafunguliwa na taratibu nikaingiza gari ndani na ya uzio wa nyumba hii ya gorofa. Tukashuka ndani ya gari na rafiki yake huyu akatupokea.

“Karibuni sana”

“Nashukuru, vipi wanangu na dada wapo salama?”

“Ndio wapo salama wame lala, ehee imekuwaje shosti yangu kwa maana naona mupo juu juu?”

“Yaani ni stori ndefu shosti yangu.”

“Kwanza karibuni ndani hapa nje baridi jamani”

Tukaingia ndani na akatukaribisha vizuri.

“Ehe niambie ime kuwaje?”

“Kwanza nikutambulishe huyu ana itwa Rashidi ni mmoja wa kaka zangu nilio kuwa nao toka nikiwa mdogo hadi kufikia umri fulani kabla ya maisha hayajatutengenisha na kuwa mbalimbali.”

“Nashukuru kukufahamu Rashidi”

“Asante”

“Rashidi huyu ndio Fatma rafiki yangu kipenzi, siri yake siri yangu. Pia amekuwa ndio mshauri wangu mkubwa sana hususani kwenye maswala yangu haya ya ndoa.”

“Nashukuru”

“Fatma hapa nilipo tumbo la uzazi lina nicheza shosti yangu. Tafadhali nina kuomba nikawaone kwanza wanangu namaini roho yangu ita tulia”

“Sawa wapo chumbani una weza kwenda kuwaona”

“Rashidi nina kuja”

Chausiku akanyanyuka na kupandisha ngazi za kueleka gorofani na kutuacha sebleni hapa na Fatma aliye valia gauni la kulalania ila zito ambalo lina chora vizuri umbo lake namba nane.

“Una tumia kinywaji gani?”

“Hapana nipo vizuri”

“Usione aibu kaka, hapa ni kama nyumbani kwako”

“Usijali”

“Una jua sisi Wagogo ni wakarimu sana hivyo sio vyema mtu akaja nymbani kwangu na akaondoka bila hata ya kutia baraka. Uta nisamehe, ila nina kuomba nikakueletee maji ya kunywa”

Fatma alizungumza kwa sauti ya kunibembeleza hadi nikajikuta nikikubali.

“Una hitaji ya baridi au ya moto”

“Ya moto”

“Sawa”

Fatma akanyanyuka na kuanza kuelekea jikoni. Nikapa wasaa wa kuangalia umbo lake hili lililo umbwa na kuumbika. Kusema kweli ni mwanamke mwenye sifa nyingi sana na maombo yao kidogo hayapishani na umbo la Chausiku, sema alicho mzidi chausiku ni kalio lililo nona.

‘Kweli wanawake wazuri ni wengi’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimsindikiza Fatma hadi akaingia jikoni. Akatoka ndani humo akiwa na glasi ya maji, akanikabidhi huku akipiga goti kidogo jambo ambalo ni nadra kuwaona kwa wanawake hususani hawa wa sasa.

“Karibu”

“Nashukuru”

Fatma akaka alipo kuwa amekaa.

“Vipi umeoa?”

Swali la Fatma likanifanya nimtazame na kuona jinsi alivyo yalegeza macho yake.

“Ndio na nina watoto watatu”

“Hongera sana”

“Nashukuru sana vipi wewe?”

“Mimi nimeolewa, ila mume wangu yupo Afghanistani kwa kazi maalumu ya kiusalama”

“Ohoo”

“Yaa yeye ni mwanajeshi kule wale walinda amani sasa ana cheo kikubwa kidogo amekwenda na vijaan wataka ahuko kwa miaka miwili”

“Sawa sawa. Watoto je?”

“Ninao wawili na wote wapo shule za bweni”

Chausiku akashuka kwenye ngazi za gorofa hili huku uso wake ukiwa umejawa na tabasamu pana.

“Rashidi mume wangu kwa kweli nina kushukuru wangu nime waona usiku huu”

Chausiku alizungumza kwa furaha sana.

“Mume!!”

Fatma aliuliza kwa mshangao.

“Ndio ni mume wangu”

“Na yule gaidi wako vipi:?”

“Ndio ukae sasa nikusimulie mambo yalivyo kuwa shosti yangu yaani siamini kama nime toka kwenye lile tanuri la moto. Yaani watui wasione haya majumba yana mambo mengi sana”

Chausiku akaanza kumuadithia Fatma kila kitu kilicho tokea.

“Mmmm ila mume wako una mjua sio mtu wa mchezo mchezo”

“Ndio nia mjua ila hapa nina unafuu”

“Sasa nimuite Rashidi Shem au kaka?”

“Shemeji yako bwana, huo ukaka umekuja kutokana na kuficha ficha”

“Sawa, shemeji mume wa zamani wa bi shosti ni mtu hatari sana. Mtu mwenyenguvu na ushawishi mkubwa kwenye serikali ya sasa na ana mpango wa kugombania uraisi je ita kuwaje akipata uraisi si ata waua nyinyi au hilo wezangu hamjalifikiria?”

“Tumelifikiria ila ni lazima kujilinda na kwa sasa sio wakati wa kusema ni namna gani ambavyo tuna hitaji kukabiliana naye”

“Mmmm ila nina mashaka kwenye hilo shemeji”

“Wala usijali kila jambo litakaa kwenye mstari”

“Kusema kweli mimi nina waombea mema”

“Amen. Fatma rafiki yangu nina kuomba tuondoke hapa usiku huu huu kwani endapo mume wangu akaja hapa kwako na kutukuta humu basi balaa lake naamini una lijua”

“Mmm ila muda ume kwenda ndugu zangu. Laleni na saa kumi na moja au mbili muna ondoka n ahata akija kwangu ana jua hapa ni nyumbani kwa nani hivyo lazima aje kwa heshima”

Fatma alizungumza kwa kujiamini

“Mmmm kama moyo wangu una sita vile”

“Usiwe na wasiwasi rafiki yangu. Wewe una jua jinsi jamaa anavyo muagopa mr”

“Rashidi una ushauri gani?”

Tupumzike kwa maana tukirudi usiku huu Dar tuna weza kupata ajali na mwili wangu ume choka nilikuwa na siku ndefu sana”

“Sawa mume wangu”

“Naamini Chausiku wewe sio mgeni na nyumba hii. Hivyo una weza kwenda kuandaa chumba kwa ajili ya Mr hapa”

“Usijali hivi ule udi wako upo?”

“Ndio una taka kuchoma muda huu?”

“Ndio best”

“Inagia pale chumbani kwangu kuna kichomeo kina mkaa bado utaukuta juu ya meza”

“Sawa”

Chausiku akaelekea chumbani na kuniacha na Fatma kwa mara nyingine.

“Rashidi”

“Naam”

“Sema rafiki yangu amekuwahi na sihitaji kuuvunja urafiki wetu kwa starehe ya muda”

“Una maanisha nini?”

“Kusema kweli umenivutia toka nilipo kuona pale nje. Sasa Chau alivyo nitambulisha wewe ni kaka yake kidogo nilikuwa na matumaini ya kukupata, ila mambo yamebadilika na siwezi kukupata tena kwa maana umesha nyakuliwa mdomoni mwangu”

Nikatabasamu huku nikimtazama Fatma machoni mwake.

“Tukiachana na hayo yote unayo yazungumza kwa nini mume wa Chausiku muna muogopa sana?”

“Ana pesa na amemwaga pesa nyingi sana kuhakikisha kwamba raisi ana tolewa madarakani.”

“Kwa hiyo pesa ndio ime mfanya raisi aliye pita ametolewa madarakani?

“Ndio Rashidi”

Nikatabasamu kwa maana kama pesa imeweza kumuwezesha mume wa Chausiku kupewa nafasi ya kugombania uraisi basi pesa hiyo hiyo ina weza kumuondoa madarakani na akakosa hata ubunge alio nao sasa hivi.



“Sawa sawa, hivii una namba ya huyu jenerali anaye iongoza nchi sasa hivi?”

“Ndio ninayo namba yake ni shemeji yangu yule”

“Je una weza kunisaidia kunikutanisha naye?”

“Sawa basi asubuhi tuta wasiliana naye tuone ni namna gani tuna weza kuonana”

“Nashukuru kwa hilo shemeji”

Chausiku akashuka kutoka gorofani.

“Tayari mume wangu twende tukalale”

Chausiku alizungumza huku akinitazama machoni. Nikamtazama Fatma akatabasamu kidogo, nikamugaa na kuelekea chumbani. Taratibu Chausiku akanikumbatia kwa nguvu na kwa hisia kali. Tukaanza kunyonyana denda na tukaangukia kitandani, kila mmoja akamvua mwenzake nguo na ndani ya mdua mchache tukaanza mtanange ulio jawa na matamanio makubwa sana. Mtanange huu kila mmoja amepania kushinda kwani kila mmoja ana hakikisha ana jituma kadri anavyo weza yeye mwenyewe. Hadi tuna maliza mtanange huu, kila mtu ameridhika vya kutosha.

“Upo vizuri sana Rashidi”

“Hata wewe sio kwa mauno hayo”

“Yaani una jua ni siku moja tu yule mwanaume amenikojoza ila wewe umenikujoza hadi nimechanganyikiwa kwa kweli”

“Kwa nini sasa alikuwa hakufikishi kileleni?”

“Ahaa akipanda dakika saba hamaliza ana shusha mzigo na akilala ndio mazima”

“Kwa hiyo kwa kipindi chote hicho ulikuwa una ishi kwenye mateso hayo?”

“Ndio Rashidi nilikuwa nina tesaka sema ndio hivyo nita fanyaje sasa wakati ndio mume niliye pewa na Mungu”

“Pole”

“Asante mume wangu”

Baada ya mapumziko ya dakika kama kumi tukarudi ulingoni, safari hii ikiwa kila mtu amesha msoma mpinzani wake hivyo ni piga ni kupige, ila kutokana na ujuzi na maujanja niliyo pewa haikuwa kazi rahisi kwa Chausiku kushinda kwenye mzunguko huu nilicho kihakikisha ni kutumia kila mbinu kuhakikisha kwamba ana nyoosha mikono juu. Tukamaliza mtanange huu ulio dumu kwa dakika zaidi ya arobaini. Chausiku moja kwa moja akalala fofo, kwani amechoka sana. Nikaingia bafuni nikaoga nikavaa nguo zangu na nikatoka chumbani hapa na kukaa sebleni. Majira ya saa kumi na moja alfajiri nikamuona Fatma akishuka kwenye ngazi huku akiwa amevalia night dreasing yake.

“Shem hujalala?”

“No huwa mara nyingi nina pendelea kuamka mapema sana ni saa kumi na moja sasa”

“Ahaa sawa sawa, mimi ngoja nichukue maji jikoni”

Fatma akaanza kuelekea jikoni huku akitembea mwendo wa mitego na mara kwa mara ana geuka nyuma kuniangalia. Akasimama katika mlango wa jikoni akaniisha kwa ishara ya kidole. Nikameza fumba zito la mate kisha nikasimama na kumwata. Akanikamata mkono wangu kwa haraka na kunivutia ndani, akaanza kuninyonya denda.

“Shem nimeshindwa kuvumilia, nimesikia jinsi ulivyo kuwa una mtomb** chausiku, tafadhali nipatie hata kimoja tu.”

Fatma alizungumza huku akifungua zipu yangu na akaingiza mkono ndani ya zipi yangu na akamtoa jogo wangu ambaye tayari alisha anza kusimama kama mnara wa babeli. Nikampandisha kigauni chake hichi juu na kumuinamisha na akashika ukuta. Taratibu jogoo wangu wakapenya katika kitumbua chake na kumfanya Fatma kutoa mguno mkali wa kimahaba. Nikaaaza kumpelekea moto wa kasi sana kuhakikisha kwamba nina kidhi haja zake ndani ya muda mfupi na kufanya hivyo pia nina weza kumtumia Fatma kama silaha yangu ya siri kuhakikisha mume wa Chausiku hajanyagi ikulu. Fatma akalalama vya kutosha huku akijitahidi kuendana na mapigo yangu ila akashindwa kwani mapigo yangu sio ya kawaida. Japo nilisha piga mechi mbili muda mchache ulio pita ila nilitumia dakika ishirini kuhakikisha kwamba nina maliza mechi hii huku Fatma akiwa amechoka kisawa sawa.

“Asante sana Rashidi, ngoja nikalale, sijawahi kutombv** kama hivi”

Fatma alizungumza huku akishusha kigauni chake, akaninyonya denda kidogo kisha akatoka jikoni hapa. Nikafungua friji hili kubwa la milango miwili, nikaanza kitazama minywaji na matunda yaliyo pangwa ndani ya friji hili, nikachukua ndizi moja pamoja na kinywaji cha kunipa nguvu mwilini kisha nikatoka ndani hapa na kukaa sebleni na kuanza kula taratibu.

‘Ila kuna haja gani ya kutimia pesa nyigi na watu wengi kumzuia mume wa Chausiku ikiwa nina uwezo wa kumuua na asijue mtu yoyote?’

Niliwaza akilini mwangu.

‘Lazima nikabiliane naye kihuni kabla ya kutumia nguvu ya pesa’

Niliendelea kuwaza akilini mwangu.

“Honey”

Sauti ya Chausiku ikanistua na kunitoa kwenye dimbwi la mawazo. Akanifwata nilipo kaa akanipiga busu la mdomioni.

“Nilikuwa nakutafuta chumbani”

“Niliamka muda mrefu kidogo”

“Ahaa vipi lakini umeamka salama?”

“Nipo salama mpenzi, hapa nina waza waza jinsi ya kukabiliana na jambo lililopo mbele yetu. Vipi lakini watoto wamesha amka?”

“Bado wamelala”

“Ahaa”

“Shikamoo dada”

Binti mdogo kiasi wa kike alimsalimia Chausiku.

“Marabaha, mume amkaje?”

“Salama dada “

“Rashidi huyo ndio dada wangu wa kazi”

“Ohoo nashukuru kwa kukufahamu dada”

“Nashukuru shikamoo”

“Marahaba.”

“Dada andaa kifungua kinywa kwa ajili ya watoto. Tuna safari ya kuelekea Dar”

“Sawa dada”

Mfanyakazi huyu wa ndani akaingia jikoni na kutuacha hapa jikoini. Baada ya dakika ishirini Fatma akajumuika nasi hapa sebleni huku akiwa amejikausha kimya kana kwamba asubuhi hatujafanya chochote.

”Shemaji nimewasiliana na jenerali ameniomba tuongozane ikulu leo hadi saa kumi tuwe timefika ofisini kwake.”

“Shukrani sana kwa hiyo tuna ongoza na pamoja leo?”

“Ndio”

“Muna safari ya wapi wajameni?”

“Ohoo tulisahau kukuambia mke wangu. Jana nilimuomba shemeji hapa aweze kunikutanisha na jenerali wa jeshi ambaye kwa sasa ndio anaye ongoza nchi. Hivyo ndio amesha wasiliana naye”

“Ahaa sawa, asante rafiki yangu kwa kumsaidia mume wangu kwa maana hili swala naona limemnyima usingizi hadi akaamua kuamka mapema”

“Usijali mimi na wewe ni ndugu, shida yako ni yangu na yangu ni yako hivyo kwenye hili tutasaidiana hadi dakika ya mwisho”

“Asante sana ndugu yangu”

Watoto wa Chausiku mara baada ya kuamka wakanisalimia na nikatambulishwa kwao kama mjomba. Baada ya kupata kifungua kinywa tukaondoka mkoani Dodoma na kurudi jijini Dar es Salaam. Simu ya Chausiku ikaanza kuita.

“Yule injinia ana piga”

“Mpokelee”

Chausiku akapokea simu hiyo.

“Ndio injinia”

“Aha mumemaliza?”

“Basi nipo njiani. Nikifika nyumbani tutakuja hapo ofisini kwenu”

“Sawa nashukuru sana”

Chausiku akakata simu.

“Wamesha maliza kupiga tathimi na kuchora ile ramani”

“Ni jambo zuri basi tuta pita ofisini kwao”

“Anko Rashidi”

Mtoto wa kwanza wa chausiku aliniita huku akiwa amekaa siti ya nyum yeye, Fatma, dada wa kazi pamoja na mfanyakazi wa ndani.

“Naam”

“Una endesha gari vizuri si kama baba ana penda kukimbiza gari kama nini”

“Kweli”

“Ndio yaani una weza hata kuona maeneo ya nje vizuri, ila baba yeye akiendeasha yaani kama muna paa hivi”

“Kuendesha gari kwa kasi sio salama una weza kupata ajali”

“Ni kweli yaani akinindesha huwa nina ogopa kama nini”

“Pole”

Tukafika jijini Dar es Salama majira ya sa anane mchana na moja kwa moja tukafikizia nyumbani kwangu na kupokelewa vizuri tukapata chakula cha mchana. Kutokana ratiba yetu ni ngumu tukaondo nyumbani na moja kwa moja tukalekea ofisini kwa wakandarasi.

“Shosti tuingie ofisini hapa kuna hawa wakandarasi kuna nyumba shemeji yakoa na hitaji kutujengea hivyo tumekuja kuingia nao mkataba.”

“Ahaa sawa”

Tukashuka ndani ya gari na kuingia ndani ya ofisi ya wakandarasi hawa. Injinia mkuu ambaye ndio mmiliki akatupokea vizuri na tukaingia naye kwenye moja ya ukumbi kwa ajili ya kufanya kikao kidogo. Wakatuonyesha ramani nzima ya nyumba jinsi inavyo kuwa mfumo wa 3D.

“Ni nyumba nzuri shemeji”

Fatma alizungumza kwa maana naye tumeingia naye kwenye kikao hichi.

“Shukrani sana shemeji. Injiania ni kiasi gani kina hitajika”

“Hadi iishe kabisa mkuu ni shulingi bilioni moja pointi mbili yale makadirio ya awali kidogo yalikuwa sio sahihi kwani kuna vitu vingi vimeongezeka”

“Duuu”

Chausiku aliguna huku akinitazama usoni mwangu.

“Ndio madame tusamehane kwa maana ile siku yalikuwa ni makadiria ya machoni tu”

“Ila hiyo pesa si tuna kabidhiwa tu funguo nyumba ikiwa ime kamilika”

“Ndio madame, kama unavyo iona ndivyo jinsi tutakavyo wakabidhi, na tuna wapatia ofa kuingiza na feniture mpya kabisa hivyo mutatupatia machaguzi ya feniture munazo zihitaji nanyi mutazikuta ndani ya nyumba yenu”

“Hadi mutukabidhi ita garimu muda gani?”

“Miezi sita mkuu”

“Malipo si nina weza kuyafanya yote sasa hivi?”

Chausiku na Fatma macho ya mshangao yakawatoka.

“Ndio mkuu hakuna shaka”

“Naombeni namba yenu ya benki tumalizane, tuandikishane mkataba kisha kazi ifanyike kikamilifu, si una jua sisi binadamu una weza kusema utalipa kidogo kidogo una weza kukumbwa na matatizo mambo yakawa sio mambo”

“Ni kweli mkuu”

Nikahamisha kiasi hicho cha pesa kwa kampuni hii ya ujenzi kisha tukaandikishana mkataba na tukaondoka ofisini hapa na moja kwa moja tukaelekea ikulu. Tukamshukuru Mungu tukaruhusiwa kuonana na raisi kwa kupitia mgongo wa Fatma.

“Karibuni sana shemeji”

“Nashukuru, naona ofisi imekukubali shemeji yangu”

“Hahaaa mimi mwanajeshi bwana, mambo haya ya kisiasi mimi siyawezi bwana. Shemeji nawe umekuja karibu”

“Asante sana shemeji”

“Mume wako nilionana naye jana usiku.”

“Ohoo”

“Ndio ila sikujua kama leo ungekuja. Kijana karibu naamini ni majuzi tu ndio tume onana”

“Ni kweli muheshimiwa raisi”

“Hivi ni Rashidi ehee?”

“Ndio Rashidi, huyu ni mdogo wangu”

“Ohoo shem Chausiku kumbe Rashidi ni ndugu yako”

“Ndio tumekua pamoja na tumecheza pamoja”

“Aisee safi sana. Ehee karibuni”

“Ahaa shemeji, Rashidi kidogo alikuwa na mazungumzo nawe hivyo kama ina wezekana tuwapishe muzungumze pamoja”

“Sawa”

Fatma na Chausiku wakatoka ofisini hapa kwa raisi na kutuacha sisi wawili hapa.

“Niambie kijana”

“Safi muheshimiwa. Ahaa labda niende moja kwa moja kwenye ombi lililo nileta kw amaana nina imani una majukumu mengi sana ya kikazi”

“Sio sana kwa maana tuna waandaa wana siasa waje kuwa viongozi wa hii nchi bwana. Mdogo wako hajakuambia kama shemeji yako ana chukua nchi”

“Ameniambia na hilo kidogo ndio lililo nileta”

“Ehee niambie kijana shida yako”

“Najua ni maswal mazito kigo kuyaingilia kama tayari yalisha pangwa. Ila naamini yana wezekana kwani hakuna kitu kinacho shindikana kwenye haya maisha”

“Ni kweli aisee”

“Sasa muheshimiwa najua shemeji ametoa dau kubwa sana hadi kupatiwa nafasi ya kuwa mtu atakaye ingia kwenye kinyang’anyiro cha uraisi?”

“Nani amekuambia?”

“Mke wake, na maswala kama haya una jua fika mume hawezi kumficha mke”

Jeneali Ngatuma akaka vizuri huku akinitazama kwa macho ya udadisi.

“Naamini hilo ni kweli?”

“Sijajua ni kwa nini jamaa amekuwa ni mzembe kiasi hicho hadi siri nyeti kama hizi ameamua kumueleza mke wake”

“Ni kweli na hiyo ina onyesha dhairi kwamba hana sifa ya kuongoza nchi na isitoshe nchi kama nchi ina hitaji kiongozi mwenye koo la kutunza siri”

“Yaa ni kweli”

“Jamaa hana uwezo wa kuongoza nchi kwani hata familia yake mwenyewe hawezi kuiongoza.

“Hivyo?”

“Ndio hana uwezo wa kuongoza familia yake ni mtu mwenye hasira na maamuzi mabaya nay a haraka sana. Sasa nchi ikiwa na kiongozi kama huyo ina kuwa nit aby kidogo muheshimiwa”

Jenerali Ngatuma akashusha pumzi.

“Ila jama nina muonai ni mnyenyekevu sana na mwenye hekima?”

“Ni kwako tu na si kwa wengine, ana roho ya kikatili ambayo haifai. Mimi sio mnafki ila ni jambo la heri kutahadharishana mapema, una weza ukampa madaraka n ahata wewe mnywewe aka kufanyi vitu vibaya na ogopa sana kiongozi anaye tumia nguvu ya pesa kitaka mali ni mtu mbaya sana muheshimiwa”

“Aisee ila ndugu huyu jamaa alisha tuingiza kwenye kifungo ambacho tumeingia na kutoka kwake sidhani kama ni kazi rahisi na sina budi kumkabidhi nchi”

“Kifungo gani muheshimiwa raisi?”

Jenerali Ngatuma akashusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu kwa macho yaliyo jaa masikitiko hadi nikahisi kwamba hicho kifungo walicho bananishwa kwa kweli sio kidogo na kutoka kwake ni shuhuli.




“Huyu jamaa alitupatia pesa kiasi cha dola milioni 100 za kimarekani katika kuhakikisha tuna tengeneza mpango na kitengo maamlumu cha kumpindua raisi kisiri sana kwa maana ili uweze kutekeleza jambo kubwa kama lile lina hitaji pesa ambayo una weza kuwalipa vijana hata ikitokea ya kutokea basi wana pesa ya kukimbilia mbali. Hivyo zoezi likikamilika kama tulivyo panga na kilicho salia ni kwamba ni yeye kumkabidhi madaraka katika kipindi cha miezi mitatu ya serikali hii ya mpito”

“Dola milioni mia moja?”

“Ndio”

“Akirudishiwa na wewe uka simama kama raisi hapo utajisikiaje?”

“Una maanisha nini?”

“Yaani tukimpatia pesa na wewe ukasimama kwenye nafasi ya uchaguzi na kuwa raisi wan chi hii”

“Ndugu yangu hivi una jua tuna zungumzia dola milioni mia moja sio pesa ndogo aise”

“Najua ni pesa nyingi”

“Sasa nani wa kuitoa kwa maana hicho kiasi cha pesa mimi sina kwenye maisha yangu”

“Akitokea mtu wa kukitoa je uta kubali kuwa raisi”

“Mmmm mbona una nitafutia uhasama na mtu ambaye nimeoanga naye hili jambo kuanzia moja hadi sasa hivi tupo kwenye mafanikio”

“Nalitambua hilo ila usimame wewe kama raisi yeye hawezi kuongoza nchi”

“Mmmm hilo ni jambo gumu sana Rashidi, siwezi kuwa msali kwake na ni mtu wangu wa karibu na tumetoka naye mbali. Ukiachana na pesa tu, ila ana maono makubwa sana juu ya hii nchi. Kitu cha kukusaidia wewe ni kwamba nita kaa kimya na kujifanya hatujazungumza chochote dhidi yake kwa maana akifahamu, wewe na mdogo wako maisha yenu yatakuwa hatarini”

Jenerali Ngatuma alizungumza kwa msisitizo na kunifanya nishushe pumzi nyinngi huku nikimtazama usoni mwake.

“Ndio samahani kwa kila kitu ila hilo unalo taka kulifanya haliwezekani”

“Saw animekuelewa na nina shukuru kwa kila kitu”

“Nashukuru nawe pia”

Nikasimama na kuagana na jenerali Ngatuma kisha nikatoka ofisini hapa huku akili yangu ikiwa ina jaribu kuchanua mafaili ya faili la mpango wa matumizi ya pesa na sasa kinacho fwata ni kuhakikisha kwamba nina tafuta plan B.

“Vipi mbona kama huna furaha?”

Chausiku aliniuliza huku akinitazama usoni.

“Nendeni mukaage tuondoke”

Wakaingia ofisini kwa jenerali Ngatuma na mimi nikatangulia kwenye gari. Baada ya dakika tano wakatoka na tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili taratibu.

“Nahitaji kuelekea Magagascar”

“Lini?”

“Muda huu”

“Nini?”

Chausiku aliniuliza kwa mshangao mkubwa.

“Ndio nipeleke hadi uwanja wa ndege muta rudi nyumbani kwa ndege”

“Madagascar una kwenda kufanya nini?”

“Nina muda mchache juu ya kulisuluhisha hili swala acha nielekee Madagascar, nikirudi muta jua kila kitu nilicho kwenda kukifwata kule.”

Chausiku na Fatma wakatazamana, moja kwa moja nikaelekea hadi uwanja wa ndege. Nikatoa hati yangu ya kusafiria ambayo nina tembea nayo kwenye wallet yangu.

“Kwa hiyo ndio una safari kweli?

Chausiku aliniuliza kana kwamba nina mtania.

“Ndio nina safari. Rudini nyumbani na hakikisheni kwamba muna kuwa salama”

“Lini sasa una rudi?”

“Kati ya siku mbili hizi”

“Sawa”

Nikakumbatiana na Chausiku, kisha nikapeana mkono na Fatma kisha moja kwa moja nikaelekea eneo la kukata tiketi, nikakata tiketi ya ndege inayo ondoka saa moja na nusu usiku. Muda wa ndege ninayo panda kuondoka ikawadia, nikajumuika na abiria wengine kuingia ndani ya ndege, Safari ikaanza huku akilini mwangu nikimfikiria Caro kwani yeye ndio mtu anaye ifahamu nchi hii ya Tanzania vizuri na ana weza kunisaidia kwenye mpongo wa kusitisha zoezi la mume wa Chausiku kuingia madarakani. Nikaweka alarm katika simu yangu ya kulala masaa mawili, kwani nia uchovu mwingi sana. Taratibu nikailaza kidogo siti ya ndege hii na taratibu nikaanza kuutandika usingizi. Arlam ikaniamsha baada ya masaa mawili na nikazinduka kutoka usingizini. Baada ya masaa matatu ya kusafiri angani, tukafika Antananarivo Madagascar. Nikiwa hapa uwanja nikalipia simu maalumu ambazo humuwezesha mgeni kumpigia mwenyeji wake, kwani wageni wengi huwa wakiingia katika nchi hii huwa sio wote wana kuwa na laini za mitandao ya simu za nchi hii. Nikaingiza namba ya simu ya Caro na nikampigia simu. Simu yake ikaanza kuita na baada ya muda kidogo ikapokelewa.

“Haloo”

Niliisikisa sauti ya Caro akizungumza kwa uchovu kidogo.

“Ni mimi”

“Rashidi?”

“Ndio, nipo uwanja wa ndege. Nielekeze nyumbani nije”

“Sawa”

Caro a kanielekeza eneo wanapo ishi, nikakakata simu na kuingia kwenye moja ya taksi na kumpa address namba ya nyumba ambayo Caro ana ishi na jina la mtaa. Dereva akaingia address namba hiyo kweye tv ndogo iliyopo pembeni yake ambayo ina onyesha ramani ya eneo tunalo hitaji kwenda na baada ya dakika tukaletewa ramani ya kufika katika nyumba ya Caro. Safari ikaanza huku dereva akifwatisha ramani hiyo.

“Ni mara yako ya kwanza kuwepo hapa Madagascar?”

Dereva aliniuliza kwa sauti ya uchangamfu.

“Yaa”

“Karibu sana kisiwani kwetu”

“Nina shukuru”

Nilimjibu kwa ufupi ufupi dereva huyu kwani akili yangu hapa ilipo ina waza mambo mengi sana. Tukafika katika nyumba ya kifahari yenyue geti kubwa kiasi.

“Ni hapa mkuu”

“Kiasi gani?”

“Dola ishirini”

Nikatoa dola mia na kumkabidhi dereva.

“Weka chenchi”

Nilizungumza huku nikishuka kwenye gari hili.

“Shukrani sana tajiri”

Dereva taksi alizungumza kwa furaha. Nikapiga hatua hadi getini na taratibu geti hili linalo tumia umeme likafunguka kidogo usawa wa mimi kuingia. Nikatazama kamera zilizo fungwa nje ya geti hili kisha nikazama ndani. Nikamuona Caro akinikimbilia kwa kasi, akanikaribia na kunirukia kwa furaha na akanikumbatia kwa furaha huku akinipiga mabusu mengi mfululizo.

“Karibu sana mume wangu”

Caro alizungumza kwa furaha.

“Nashukuru, mbona umepungua mwili vipi kuna tatizo?”

Nilizungumza huku nikimtazama Caro namna alivyo pungua kiasi.

“Kwa kilicho tokea nilkikuwa ni lazima nipungue mume wangu”

“Pole sana”

“Karibu sana ndani mume wangu”

“Nashukuru, hili jumba lote una ishi peke yako?”

“Hapana naishi na kaka, walinzi wake, wifi na mtoto. Shukrani sana mume wangu kwa maana pesa uliyo tupatia ndio nilifanikiwa kununua nyumba hii kisha nyingine nikafungulia miradi kadha kwa ajili ya kutengeneza pesa”

“Sawa sawa mke wangu hilo ni jambo zuri sana kwenye maisha”

“Karibu ndani mume wangu naona tuna piga story nje”

Tukaingia ndani, ukimya wa nyumba hii una weza kuhusia watu hawaishi.

“Watu wamelala nini?”

“Muda mrefu sana wame lala”

“Okay, nina njaa mpenzi wangu niandalie basi msosi hata kidogo”

“Una taka kula nini mume wangu?”

“Chochote ili mradi tumbo liweze kushiba”

“Sawa mume wangu nakuandalia chakula upendacho, twende chumbani kwanza ukaoge mwili upate nguvu”

“Sawa”

Tukaelekea katika chumba anacho ishi Caro. Caro akaanza kunivua nguo, uvumilivu ukatushinda na kujikuta tukiazama katika penzi nzito huku kila mmoja akihakikisha kwamba ana mpatia mweza wake haki roho ina penda. Kitu ambacho nina kishangaa kwangu ni uwezo wa kufanya mapenzi wanawake watatu ndani ya masaa yasiyo zidi ishirini nane na kila mmoja nikamuhimili kwa kiwango kile kile kama nilicho mpatia Chausiku.

“Ahaa sasa ngoja nikakupikie kwa maana shibe yangu na mimi ikwisha si kwa kunitomb** huku”

Cauther alizungumza huku akihema sana.

“Nasubiri madigo diko yako”

Nilizungumza huku nikiyatomasa tomasa makalio ya Caro. Akashuka kitandani, akajifunga tengene na kutoka chumbani hapa. Nikachukua simu ya Caro iliyopo mezani, nikaingiza namba ya Shabani na nikampigia simu.

“Kaka za muda”

“Salama aisee, nimesikia umekwenda Madagascar?”

“Yaa ilikuwa safari ya galfa kidogo, si unajua changamoto iliyopo mbele yetu”

“Vipi umefikia kwa bi mama au?”

“Yaa nimefikia kwake”

“Wana endeleaje?”

“Ahaa…nimeonana naye peke yake ila naamini wana kwenda salama”

“Okay so ni swala la kifamilia ndio limekupeleka au kuna maswala mengine?”

“Tuta zungumza nikirudi”

“Sawa ndugu yangu”

“Ila wapo salama hao?”

“Yaa wapo salama kabisa”

“Poa poa kaka nikutakie usiku mwema”

“Nawe pia ndugu yangu”

“Poa”

Nikakata simu, nikawasha tv iliyomo hapa chumbani, nikasubiria hadi Caro alipo rudi na chakula.

“Nimepika ugali wa nguvu, najua utakupa nguvu ya kunishuhulikia tena”

“Hivi huku hawa sakamki wapo?”

Niuliza huku nikichukua samaki mmoja aina ya dagaa na kuanza kumtafuna.

“Yaa wapo wengi sana si una jua hawa wezetu wana wamezungukwa na bahari hivyo uvuvi upo kila mahali”

“Ahaa sawa sawa”

Caro akaninawisha maji na tukaanza kula.

“Ruben ana endeleaje?”

“Ahaa yupo salama, watu tuna jitahidi kuzoea mazingira mapya na maisha mapya”

“Hujaulizwa pesa umetolea wapi?”

“Waliuliza kwa maana akaunti zetu zote zimefungwa si za nje ya nchi wala ndani ya nchi. Nikawachana ukweli kwamba laiti ingekuwa sio wewe tungekuwa omba omba wa kukaa mahotelini na mwisho wa siku pesa ingekata”

“Wakasemaje?”

“Wana cha kusamea zaidi ya kujisikia aibu. Yaani mume wangu usimfanyie mtu ubaya kwenye haya maisha. Kwa maana hakuna anaye fahamu kesho yake. Ona walivyo kuwa wana kuwinda ili wakue ila sasa hivi hapa tulipo. Yaani maisha kweli ni ya kushuka na KUPANDA”

Nikapiga matonge kadhaa huku nikifirikia maisha ya nyuma niliyo kuwa nina fanyiwa na mama Shamsa pamoja na mwanaume wake.

“Baby mbona upo kimya”

“Hapana kuna mambo kidogo nilikuwa nina waza”

“Mambo gani?”

“Ahaa tuachane nayo yamesha pita”

“Niambie tu mume wangu, kwa maana sio kwa ukimya huo. Najua una hasira dhidi ya kaka yangu na yule malaya wake. Ila tafadhali wasamehe kwa maana dunia imesha wapiga na hawana cha kufanya, heshima imeshuka sasa hivi kaka yangu ukimuona ndio amezidi kuwa mzee. Hata pesa ya saluni wana niomba mimi”

“Duu”

“Wee acha tu. Tule bwana, tufikirie maisha yetu na huyu mtoto wetu ajaye”

Kwa kutumia mkono wangu wa kushoto, nikalishika shika kidogo tumbo la Caro ambalo tayari limesha anza kuchomoza kutokana na ujauzito wake.

“Kaka yako amesha tambua?”

“Ametambu nini?”

“Kwamba Ruben sio mwanaye?”

“Sidhani, hapa ni juzi juzi tumetoka kumpima sukari ina panda si mchezo, sasa kama akijua kwamba na huyu mtoto anaye muita kidume chake sio mwanaye, ana kufa”

“Hahaaa ila ni haki yake kufahamu kwa maana Ruben ata mzoea huyo mzee kama baba yake kumbe baba yake nipo hapa.”

“Kwa sasa hembu tuliache hili mume wangu kwa maana sihitaji msiba mwengine hapa. Kwani kupoteza mali vyeo na kila kitu tulicho kuwa tuna miliki nchini Tanzania ilikuwa ni msiba tosha kwetu. Sasa akifa na huyu naweza kupungua saidi ya hapa mume wangu.

“Sawa”

Tukaendelea kupata chakula hichi huku tukitazama tv. Tukamaliza kula na Caro akaninawisha mkono kisha akatoa vyomgo na akarudi akiwa amebeba mzinga wa wyne na glasi mbili. Akamimina wyne hii kisha akanikabidhi glasi yangu, tukagonganisha chiaz.

“Kwa maisha ya mtoto wetu”

Caro alizungumza huku akitabasamu.

“Hivi na unywaji huo mtoto kweli hato kuwa mlevi?

“Hahaha hawezi kwa maana si kwamba nina kunywa kulewa, nina kunywa kidogo kidogo.”

“Sawa”

“Ehee uongozi mpya upo vipi?”

“Wananchi wengi sana wame ufurahia na wameupenda”

“Nina ona kwenye tv. Kwa kweli kaka alichokwa na wananchi”

“Ilikuwa akachokwa namna ile?”

“Sio wewe tu ulifanyiwa mabaya, wapo wengine nina imani walifanyiwa mabaya na wakachoka”

“Una mjua jamaa mmoja ambaye ana itwa nani vile?”

“Ni nani?”

“Hembu simu yako”

Caro akanikabidhi simu yake na nikampigia simu tena Shabani.

“Ehee”

“Hivi mume wa Chausiku ana itwa nani jina lake maarufu la uongozi?”

“Nundu”

“Poa poa”

Nikakata simu.

“Aisee ungenipa nizungumze na shem”

“Kesho. Huyu jamaa ana itwa Nundu una mfahamu?”

“Yule mbunge na mfanya biashara?”

“Ndio”

“Namjua vizuri ni rafiki yangu sana”

“Ana taka kusimamishwa kuwa raisi wa nchi ya Tanzania”

“Mungu wangu nani ana taka kufanya upuuzi huo. Jamaa kwanza mpiga madili kama kaka, ana roho mbaya na chafu. Hafai kabisa kuwa raisi yule jamaa”

“Hivi una jua yeye ndio aliye endesha mpango mzima wa kumtoa madarakani kaka yako?”

“Nini……?”

Caro aliahamaki sana huku macho yakimtoka kwa maana huyo ambaye amesema ni rafiki yake amemgeuka na kuwafanya sasa waishi kama wakimbizi katika nchi wasio kuwa na mmlaka wala vyeo vya aina yoyote kama walivyo kuwa navyo nchini Tanzania.



“Ndio yule jamaa ndio ana husika na kupanga mbinu yeye na jenerali Ngatuma, akawafadhili dola milioni mia moja na kutekeleza mpango wa kuipindua serikali ya kaka yako”

“Shenzi kumbe alikuwa ana nizunguka yule mpuuzi.”

“Ana kuzunguka kivipi?”

“Una jua nilikuwa nina mchukulia kama broo na hata siku ya mwisho ikulu ina pinduliwa nilikuwa naye ikulu, na nilinana naye dakika tano kabla ya tukio kutokea. Sasa kumbe yeye ndio yupo nyuma wa haya yote”

Caro alizungumza huku akionekana kupagawa.

“Ndio yupo nyuma na mpango wao waliupanga kwa kipindi kirefu sana hadi kumpindua kaka yako”

“Rashidi mume wangu hapa ni lazima tufanye kitu. Mshenzi yule hawezi kuendesha nchi.”

“Sasa una taka kufanya nini?”

“Chochote tu mume wangu ilimradi kuhakikisha hachukui madaraka na huyo Ngatuma mshenzi, madaraka amepewa na kaka yangu alafu ana msaliti shenzi yake”

Caro alilamama huku akionyesha dhairi kwamba amekereka kwa hili lililo tokea.

“Ndio hivyo mambo yalivyo mke wangu binadamu wana badilika”

“Asubuhi hili ni lazima tulizungumze na kaka yako”

“Ila kumbuka mimi na hao watu wawili picha haziendi”

“Mume wangu wakati huu ni wakati wa kusimama pamoja kwa ajili ya nchi. Nina kuomba tofauti ziweze kukaa pembeni tushuhulike na hili jambo”

Nikamtazama Caro machoni mwake, taratibu akavishika viganja vyangu.

“Tafadhali mume wangu nina kuomba sana tusaidiena kwenye hili”

Caro alizungumza kwa sauti laini na nyororo. Akaaanza kuninyonya denda, taratibu nikamvua tenge lake, nikamnyanyua na kumlaza kitandani, huku tukiendelea kunyonyana denda, nikaususha ulimi wangu taratibu hadi katika maziwa yake na kunza kuuchezesha kwenye chuchu hizi zilizo anza kusimama kama namba moja. Caro akazidi kutoa miguno ya kimahaba, nikausha ulimi wangu hadi katika kitumbua chake na kuanza kukinyonya taratibu na kumfanya Caro kutoa miguno mingi ya kimahaba.

“Baby nipe”

Caro alizungumza huku akininyanyua kichwa change. Taratibu nikauanzisha mtanange hukuu huku nikiupeleka taratibu, sihitaji kutumia nguvu wala kasi kubwa kama nilivyo mzoesha Caro.

“Baby ongeza kasi”

Caro alilalama, nikamgeuza kwa haraka na mimi nikalala chali kisha akanikalia kiunoni mwangu.

“Mmmmm”

Caro alilamaa huku mikono yake miwili akiita kifuani mwangu na akaanza kuzungusha kiuno chake. Viganja vyangu nina kazi ya kukatiza maeneo mbalimbali ya mwili wa Caro kuanzia katika chuchu zake hadi kwenye makalio yake haya malaini.

“Baba nak….o…..ko…..j…o……..a’

Caro alizungumza huku akiongeza kasi ya kuzungusha kiuno chake kwa haraka nikamlaza kifua chake kifuani mwangu kisha nikapata muhimili mzuri wa kujumuika naye kwenye kasi hii ya kufika kileleni mwa mlima.

“Nakuja”

Nilizungumza kwa sauti nzito ya na yakimahaba.

“Njooo tu baby”

Caro alizungumza na sote tukajikuta tukimaliza mtanange huu kwa wakati mmoja huku kila mmoja akiwa amejawa na furaha.

“Mke wangu wewe mtamu sana”

“Asante mume wangu hata wewe mtamu, yaani una jua kunikuna hadi nina kunika”

“Naamini hapo mtoto nimempa masiko mpya”

“Hahaaahhahaa chizi wewe”

Caro alizungumza hukua kishuka juu yangu, akaanza kuelekea bafuni. Nikashuka na kumfwata.

“Ndio hapo kama alikuwa ana takiwa kuwa na masikio kama yako basi ameyapata masikio yangu”

“Hahaaa hembu niache mimi”

Tukaoga kwa pamoja na tukarudi kitandani. Taratibu nikamkumbatia Caro kwa nyuma.

“Baby”


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG