Search This Blog

Saturday, February 6, 2021

RISE UP SEHEMU YA 9/10

  

RISE UP

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 9 KATI YA 10


“Naam”

“Kama tukifanikiwa kumzuia Nundu asiingie madarakani ni nani una pendekeza awe raisi?”

“Wengi tum bona wapo viongozi wazuri. Waziri mkuu pia ni mtu ambaye ana weza kuwa raisi kwa sababu yule mzee nimekaa naye kwa kipindi kirefu na nimeweza kuona uwezo wake wa kuongoza na hekima aliyo kuwa nayo.”

“Kwa nini hujampendekeza kaka yako?”

“Mpuuzi yule hawezi”

“Hahaa kwa nini una muita mpuuzi?”

“Ni mpuuzi kwa sababu, kipindi nilipo kuwa nina mshauri na kumlalamikia, hakunisikiliza zaidi ya kumsililiza huyo mpuuzi mwenzake ambaye alikuwa ana tumia walinzi wa kiserikali kwenye kuteleleza mambo yakibinafsi, sasa acha kwanza wapate walicho kipanda”

“Kazi kweli kweli”

“Ndio, ila jamaa kama ametoa dola milioni mia moja na hato kuwa kiongozi ita kuwaje mume wangu?”

“Mimi nilikuwa na wazo”

“Wazo gani?”

“Tumuue kabla ya uchaguzi”

“Mmmm mume wnagu yule jamaa ni mchawi balaa. Watu wa Kigoma hao wamesha lala ndani ya ziwa hawauliki kirahisi, wengine wana meza irizi kabisa”

“Mmmm hakuna ambaye hafi mbele ya risasi”

“Mume wangu sema haupo kwenye system ila kuna watu ni wachawi. Unampiga risasi mtu hafi ana kimbia aisee asikuambie mtu mume wangu”

“Hivi ina wezekanaje mke wnagu au ndio yale maswala ya Kinjikitile Ngwale na watu wake kwenye vita ya maji maji”

“Ohooo sasa wale kidogo uchawi wao ulikuwa haujaendelea. Ila hawa wa sasa mume wangu kuna watu ni washirikina usipime. Sasa yule jamaa alipataga ajali kwenye gari yake, yaani gari ilipondoke pondeka na dereva wake alikufa hapo hapo ila yeye alichubuka tena mkononi tena kama vile amekwaruzwa na kucha”

“Duuu”

“Jamaa ndio ni mwanga kikweli kweli. Yaani asikuambie mtu, sasa hapa nina pata picha kwa nini kina jenerali walimgeuka kaka, Una weza kuta alisha wapiga kimbora kila wanacho ambiwa wao wana fwata tu kama mazuzu”

“Na inaonyesha huyo jenerali ana muogopa balaa”

“Hivyo ehee?”

“Ndio”

“Duu sasa hapa ina bidi tuwe na plan za ziada”

“Una Manisha?”

“Kama na yeye ana tumia njia za kuzimu na sisi twende huko huko. Una hisi tuna weza kukabiliana naye kiurahisi hivyo”

Nikamuachia Caro taratubu na nikakaa kitako kitandani na kumtazama.

“Una maanisha?”

“Mume wangu usijifanye kama hujui. Kama mtu nina kuambia akipigwa risasi hafi, una hisi kwa hali ya kawaida tuta muweza. Tukishangaa tuna weza kujikuta kimasira jamaa ana chukua nchi na mambo yana haribika. Ila ngoja kwanza mume wangu nina swali, kwa nini umelifwatilia swala la huyu jamaa kuingia madarakani na kuchukua nchi”

“Ipo hivi yule mama muuza mihogo una mjua’

“Mama Chausiku?”

“Ndio, mwanaye Chausiku ndio mke wa jamaa”

“Wee yule dada black beuty fulani hivi ndio mke wa Nundu?”

“Ndio huyo huyo”

“Jamaa alisha wahi kunitambulisha siku moja tu mke wake. Ila anamuweka siri sana mke wake?”

“Ndio hivyo sasa jamaa ana mnyanyasa sana yule mwanamke na ana mletea wanawake wengine hadi nyumbani kwake. Na mwisho wa siku kuna siku alitaka kumpiga viabao mbele yangu na mama yake na nikaliingilia kati na nikamdhibiti jamaa kwa maana alisha chomoa bastola alitaka kutuua”

“Mungu wangu, sasa mtu kama huyo kweli akipewa nchi si mambo yana weza kuwa kama kwa Gadafi”

“Yaani nilicho kifanya baada ya kumdhibiti nikamuamrisha kumpa talaka mke wake na akafanya hivyo nikiwa nimeshikia bastola”

“Mmmm alikubali kweli?”

“Ndio hapo nilisha kuwa nimempa kipigo kizito kidogo hivyo alikosa kwa kukimbilia na akaandika talaka na baada ya hapo alitaka kuwaua watoto wa Chausiku ika bidi niende kuwachukua Dodoma na kuwarudisha nyumbani kwa Shabani.”

“Aisee sasa jamaa na pes azote hizo alishindwa nini hata kuacha kumjengea mkwe wake?”

“Jamaa ni mbinafsi wa kutupa na hilo ndio lilinifanya niweze kusimama upande wa Chausiku na akanielezea mipango yake mingi kuhusiana na jamaa na nikaonana na jenerali na kwa bahati mbaya woga umemfanya ashindwe kunisaidia kwa lolote”

“Masikini pole kwa huyo dada”

“Ndio hivyo ina tupasa kumzuia mapema sana kwani alitoa ahadi kama akipata uraisi ata hakikisha mimi, mama Chausiku, Chausiku mwenyewe na wanaye sote ana tuu”

“Hilo ndio tatizo la viongozi wa kiafrika. Wakipataga madaraka basi akili zina waruka na mwishowe wanajikuta wakitumia madaraka yao vibaya kuwadhuru wasio na uwezo”

“Ndio aliyoo yafanya kaka yako”

“Tulale mke wangu kukipambazuka nina imani tutakuwa tumesha pata jibu la nini tufanye”

“Sawa mke wangu”

Baada ya muda mfupi usingizi ukampitia Caro, ila kwa upande wangu, usingizi hauninyemelei kabisa. Asubuhi, Caro akawa wa kwanza kutoka chumbani hapa, baada ya nusu saa akarudi na kunieleza kwamba tayri amesha niandalia chai.

“Watu wamesha amka?”

“Wote wameamka wapo sebleni kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.”

“Umewaambia kwamba nipo?”

“Hapana nataka uwafanyie suprize”

“Poa”

Nikajiandaa na tukatoka ndani hapa. Mama Shamsa na mume wake macho yakawatoka huku wakinitazama kwa mshangao mkubwa sana.

“Karibu mume wangu”

Caro alizungumza huku akivuta moja ya kiti kilichopo kwenye meza hii ya chakula. Nikakaa huku nikiwatazama mama Shamsa na mume wake.

“Ruben mambo”

Nilizungumza huku nikimshika shavu Ruben ambaye ni mwanangu.

“Shikamoo”

“Marahaba mtoto mzuri. Hujambo?”

“Sijambo”

“Habari zenu”

Niliwasalimia mama Shamsa na mume wake. Hapakuwa n ahata moja aliye nijibu zaidi ya kuendelea kunishangaa.

“Jamani si munasalimiwa?”

Caro alizungumza.

“Salama”

Raisi mstafu alijibu kwa unyonge.

“Mume wangu alikuja jana usiku kututembelea”

“Poleni nilikuja kuwasalimia bila ya kuwapa taarifa nilikuja kutazama nyumba ambayo mke wangu ameinunua ina muonekano gani”

Mama Shamsa akainamisha kichwa chini kwa kuona aibu.

“Umeipenda ehee mume wangu?”

“Ndio ni nyumba nzuri, kubwa na tulivu”

“Karibu hapa ni kwako na hili ni jasho lako mume wangu kipenzi kakika bila wewe leo hii sijui tungekuwa tuna maisha gani.”

“Musijali maisha ya bina damu yana badilika muda wowote, wa chini ana kuwa juu na waliye juu ana kuwa chini. Sipati picha kama leo hii ningekuwa nimekufa kwenye lile gereza la kule Congo au kule kwenye nyumba za mateso Lushoto Tanga kwenye msitu wa Khandekamaa sijui inge kuwaje?”

Nilizungumza maneno amnayo moja kwa moja nina tambua kwamba yata mtesa mama Shamsa na mume wake.

“Ina bidi usamehe tu mume wangu, saba mara sabini”

Caro alinijibu huku akitabasamu.

“Jamani mbona muna onekana hamuna furaha kabisa juu ya uwepo wangu hapa?”

“Ahaaa karibu”

Raisi mstafu alizungumza kwa sauti ya unyonge sana.

“Nashukuru muheshimiwa raisi, sijakuja kuwaondolea furaha yenu kwenye hii nyumba. Yale yaliyo pita ya kunichukulia bibie huyu kwa kutumia cheo chao cha madaraka na mimi kwenda kupigana ulingoni kule na kupitia maisha magumu, yoye nina shukuru kwa maana leo hii Mungu amenisimamisha na kunipandisha juu na kuwa imara kuliko nilivyo kuwa pale awali. Huyo mkeo ata baki kuwa mama wa wanangu tu na si kingune endelea kuwa naye”

Kauli yangu ikamfanya mama Shamsa kunyanyua uso wake na kunitazama huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana.

“Samahani ume sema wanao?”

Raisi mstafu alizungumza na kumfanya mama Shamsa macho kumtoka huku akinitazama na midomo yake ikianza kutetemeka huku akitamani kuniomba nisizungumze ukweli ulipo kati yangu, yeka na huyu mtoto Ruben kwani raisi mstafu akifahamu ukweli tu sidhani kama maisha yake yataendelea kuwa karibu na mzee huyu.




“Ndio wanangu, una hisi mimi nina ubaguzi, Shamsa ni mwanangu wa kwanza na huyu ni ndugu yake japo mama mmoja na baba tofauti au una taka hadi watoto wawe na matabaka?”

Niliuzungumza huku nikitabasmau nikamuona mama Shamsa jinsia kishusha pumzi nyingi na kunitazama.

“Jamaani hayo sio ya kuzungumzia sasa hivi. Tunye chai kisha tuangalie ni nanma gani ya kumzuia Nundu”

Caro alizungumza huku tukiendelea kupata kifungua kinywa.

“Nundu yupi?”

Raisi aliuliza.

“Nundu yule mbunge”

“Amefanya nini?”

“Yeye ndio yupo nyuma ya mpango wako wa wewe kutolewa madarakani. Yeye amemlipa Ngatuma dola milioni mia moja na wakashirikiana kukupindia madarakani”

Raisi Macho yakamtoka huku akiwa kama haamini kama anacho kisikia.

“Wewe umejuaje?”

“Umesahau mimi ni nani au una hisi mimi kukaa hapa Madagascar nimepoteza connection zangu zote?”

Caro hakutaka kumueleza kaka yake ukweli wa chanzo cha habari hizo kwani ana weza asiniamini kwani uhasama kati yetu bado upo.

“Mshenzi yule nita mkata masikio”

“Una mkataje ikiwa sasa hivi huna nguvu ya kipesa wala nguvu ya madaraka”

“Lazima nifanye jambo. Nita wasiliana na Obote anipatie msaada”

“Wa….?”

Caro aliuliza huku akimtazama kaka yake.

“Kuipindua serikali na nichukue madaraka tena”

“Alafu?”

“Alafu nini ikiwa nimetolewa hata sijamaliza muhula wangu wa kwanza”

“Kaka siku zote nina kuambia ukweli na ukweli uta baki kuwa huru. Kipindi ulipo kuwa na mke wako wa kwanza mambo yalikuwa yamenyooka hivi”

Caro alizungumza huku akimyoosha mkono wake wa kulia akionyesha ishara ya mambo hayo jinsi yalivyo kuwa wamenyooka.

“Ila ulivyo mwaga mke wako wa ndoa ambaye alikuvumilia toka ulipo kuwa una anza maisha na kijistulia hadi kuwa makamu wa raisi matokeo yake ndio haya. Kiufupi huna sifa ya kuongoza nchi huo ndio ukweli na sio mara ya kwanza kukuambia. Hujiulizi kwa nini ulivyo pinduliwa wananchi walishangilia kupinduliwa kwako. Alafu leo hii una jidanganya ohoo Obote atanisaidia kuipindua, mzee kaa ule maisha yako yaliyo baki usitake ufe mwanao akashindwa kukufaidi, umri umesha kwenda.”

Caro alizungumza bila ya kuogopa na kumfanya mama Shamsa kuwa mnyonge sana.

“Kuna wananchi wangapi walikuwa na madua mabaya kwako kama Rashidi hapa, ukichiliana na madua mabaya tu walikuwa wana kuwinda ili wakudhuru ni wangapi? Kama ni wengi ulio wafanyia mabaya usijaribu kurudisha miguu yako Tanzania uta kufa. Mimi nina kuambia ukweli kwa sababu ni ndugu yako, sikufichi wala sikuonei huruma kwenye ukweli”

“Kwa hiyo?”

“Kwa hiyo nini…..Nundu ana taka kuchukua nchi hapa ndio nina jadili na mume wangu tujue namna gani ya kufanya kumzuia kwa maana dada yake Chausiku amemtonya kwamba huyu nundu ni mtu mbaya sana na hafai kuongoza nchi”

“Samahani Chausiku yupo?”

Mama Shamsa aliniuliza kwa suati ya unyonge.

“Ndio, yeye ndio aliye nisindikiza uwanja wa ndege kuja hapa”

“Jamani nime mmiss”

“Mpigie”

“Utanipatia namba yake jamani”

Mama Shausiku alizungumza huku akijichekesha.

“Kwa hiyo nani muna hisi ana weza kusimamishwa kuwa raisi?”

“Tukuulize wewe ambaye ulikuwa raisi watu wako si unawajua. Tafuta mtu atakaye kuokoa kwenye kifungo chako hichi cha ukimbizini”

“Nipeni muda wa kufikiria na kutafakari”

“Sawa huo muda ukisha patikana huyu Nundu tuna mfanyaje?”

“Ina bidi aangushwe”

“Anaangushwaje mtu mchawi kama yule”

“Kuna mtaalamu mmoja nita waelekeza yupo Kigoma huko ndio tunapo kwenda viongozi karibia wote. Mzee huyo yupo vizuri”

“Nundu sio ndio kwao huko?”

“Ndio ila mzee ukimueleza umegizwa na mimi basia wafanyia vitu”

“Nani sasa wa kumuua nundu”

“Mimi nita muu”

Nilizungumza na kuwafanya watu wote wanishangae.

“Nini?”

“Mume wangu hili swala ukijichanganganya nawe uta kuwa mkimbizi kama sisi?”

“Nilisha zoea kuwa mkimbizi. Hivyo ni bora kuwa mkimbizi kwa mara nyingine ila nchi iwe mikono salama”

Raisi akanitazama kwa sekunde kadhaa.

“Tuna weza kuzungumza”

“Ndio zungumza”

“Kama wanaume”

Nikamtazama Caro machoni mwake.

“Ndio”

“Sawa nina kuomba tuzungumze”

“Si mumalize kula kwanza”

“Mimi nimeshiba, nina kwenda bustanini”

Raisi akasimama na kuondoka eneo hili.

“Kifungua kinywa chako ni kitamu mke wangu”

Nilizungumza huku nikimpiga busu Caro mdomoni mwake.

“Asante mume wangu kipenzi”

Nikasimama.

“Bustani ipo wapi?””

“Ukitoka mlango huo wa jikoni mkono wako wa kushoto”

“Shukrani”

Nikafwata maelekezo na nikamkuta raisi akiwa amekaa kwenye moja ya kibanda kati ya vibanda viwili vilivyopo eneo hili. Nikaka kwenye moja ya kiti na nikakunja nne huku nikimtazmaa mzee huyu.

“Ahaa najua mimi na wewe hatupatani na nimekufanyia mambo mengi sana maovi ambayo kama binadamu nimekaa chini na kutafakari sana ni kwa nini ile siku uliamua kutusaidia na kama ingekuwa ni kutua basi ungesha tuua muda mrefu ila leo hii tumepata kifungua kinywa pamoja. Nimejisikia ni mkosaji na nina jutia sana kuhusiana na yale yote niliyo kufanyia, hivyo nina kuomba sana ndugu yangu uweze kunisamehe”

Nikatabasamu kwa dharau huku nikimtazama mzee huyu.

“Hivi ungekuwa ikulu leo hii ungeniomba msamaha?”

Swali langu likawa gumu kwa mzee huyu na akabaki akiinamisha kichwa chini.

“Nilikuwa fukara, tena masikini wa kufanya kazi ya ulinzi na kulipwa laki na ishirini kwa mwenzi. Mungu alinijalia kunipatia mtoto mzuri na mke mzuri. Ila ukanipokonya mke mzuri kutokana cheo chako na mali zako. Ukanisingizia kesi ambazo nyingine hazikuwa na hata mantiki huku siku hadi siku ukiendelea kumla mke wangu hadi imefikia wakati nilitamani kujiua. Leo hii kirahisi tu una niomba msamaha, unajua ni maisha gani niliyo pitia hadi kufika hapa. Una jua ni damu za watu wangapi nilizimwaga ili kuitetea roho yangu. Alafu sasa hivi kirahisi tu una niambia nisamehe. Mzee usilete siasa kwenye maisha yangu, kama uliweza kunipokonya mke basi sasa hilo ulifanikiwa kirahisi sasa hivi ni muda wa kuchukua kila kilicho kuwa changu kutoka kwako na endapo utajaribu kuvuka mstari wangu kwa mra nyingine nita kuua. Nikutakie mapumziko mema ya kuzeeka vizuri ukisubiria siku zako za kufa kwa kudra za mwenyezi Mungu”

Nilizungumza huku nikisimama.

“Rashidi”

“Nini mzee”

“Kila binadamu ana makossa na kila binadamu ana haki ya kusamehewa?”

“Aisee kwa bahati mbaya mimi sio Mungu. Mungu pekee ndio ambaye anaye samahe hata mtu ukitoka kuua sasa hivi ukatubu ana kusamehe. Sasa mzee wangu siwezi kukusamehe, laiti ungeniomba msamaha wakati ulipo kuwa madarakani hapo sawa ila kwa sasa haupo madarakani, ume fulia, umeishiwa alafu una niomba msamaha. Yaani kwa akili ya kawaida kabisa tu mtu ana tambu kabisa kwamba una omba msamaha kutokana huna cha kufanya mzee. Hivyo siwezi kukusamehe kwa sasa”

Nikaondoka eneo hili na kumuacha raisi akinitazama kwa macho yaliyo jaa masikitiko. NIkarudi sebleni.

“Mke wangu nahitaji kwenda mjini”

“Sasa hivi?”

“Ndio una weza kuniazima gari yako”

“Ndio ila kwa nini tusiende wote mume wangu au una ufahamu huu mji?”

“Kuna google map ita nielekeza”

“Ila una onekana kama hauna furaha kaka amekueleza nini?”

“No ni mazungumzo ya kawaida. Nahitaji kutafuta baadhi ya vitu, nitarudi muda si mrefu”

“Ila mume wangu nchi hii ipo vizuri sana katika maswala ya kuzingatia leseni za udereva barabarani ita kuwaje askari wakikumata. Wewe subiri nionge haraka haraka tukazunguke wote”

Ikabidi nimkubalie Caro kuondoka naye. Nikaka kwenye moja ya sofa na Ruben akanifwata.

“Anko”

Ruben aliniita na kumfanya mama yale kunitazama.

“Niambie anko”

“Wewe ni mwanajeshi?”

“Kwa nini una niuliza hivyo?”

“Siku ile nilikuona na bastola?

“Hahaaa bastola ni kwa ajili ya kunilinda”

“Uta ninunulia na mimi?”

“Una taka bastola?”

“Ndio”

“Sawa nikirudi kutoka mjini nita kununulia”

“Sawa anko”

Ruben akaniponyoka mikononi mwangu na kukimbulia gorofani.

“Wewe”

Nilimuita mama mama Shamsa mara baada ya kumuona akielekea gorofani. Akasimama na kunitazama kwa ishara nikamuita na akakaa kwenye sofa linalo tazamana na sofa langu.

“Mara ya mwisho kuongea na Shamsa ni lini?”

Mama Shamsa akakosa jibu la kunipatia kwani alisha mkana mwanye ili kuolewa na huyu mzee.

“Mbona hunijibu?”

“Sikumbuki na nina hisi ata kuwa amesha nisahau”

“Nahitaji mwanangu sasa aweze kujua ndugu zake wengine”

“Una maanisha nini?”

Nikatazama eneo zima na kuona hakuna mtu anaye fwatilia mazungumzo haya.

“Nina hitaji kuondoka na mwanangu akawajue ndugu zake wengine”

“Lakini Rashidi si tulisha zungumza hili?”

Mama Shamsa alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyonge mwingi sana.

“Tulizungumza nini?”

Nilimuuliza kwa msisitizo huku nikimkazia macho.

“Juu ya Ruben?”

“Kwamba?”

“Honey tundoke nimesha maliza”

Caro alizungumza huku akishuka kwenye ngazi kwa kasi.

“Waoo umependeza mke wangu.”

Niliuzungumza huku nikisimama, nikamsogelea Caro na kumsamisha kwa kumgeuza geuza kuangalia gauni lake hili alilo vaa na kumfanya aonekane mzuri sana.

“Asante mume wangu”

Caro akaninyonya denda pasipo kujali uwepo wa mama Shamsa eneo hili.

“Wifi kama kuta kuwa na jambo lolote la kuongeza kwenye friji basi uta nijlisha”

“Sawa wifi”

Tukatoka ndani hapa na kuingia katika gari lake aina ya Range Rover.

“Una zipenda hizi gari ehee?”

“Sana tu mume wangu, ndio maana hata ile iliyo zama pale wami roho yangu iliniuma sana”

“Pole mke wang”

“Nilisha poa na kusahau. Ehee tuna kwenda wapi?”

“Sehemu yoyote iliyo tulia nahitaji kutuliza kichwa change na mupata mawazo mapya”

“Huhuhu kwani kaka amekuambiaje?”

Caro alizungumza huku tukitoka eneo hili taratibu.

“Mambo tu ya kuniomba msamaha. Nimemuuliza kwa nini asiniombe msamaha kipindi kile alipo kuwa madarakani, ananiomba msamaha kipindi hichi akiwa hao”

“Mume wangu hawa watu wawili sio wa kuaminika kabisa. Hivyo wewe wasikilize tu ila ishi nao kwa akili sana”

“Najua hili mke wangu ndio maana sihitaji kujiweka nao karibu. Ila mke wangu nahitaji kuondoka na mwanangu safari hii. Ruben ina bidi amjue dada yake Shamsa na ndugu zake wengine. Haya maswala ya kuficha ficha hivi mambo yana weza kua mabaya huko mbeleni”

“Ni jambo zuri ila nakuomba awajue ndugu zake baada ya mimi kujifungua hichi kiumbe tumboni.”

“Mmm”

“Ndio mume wangu nina kuomba kwa maana kama uta kwenda kuwatambulisha basi ukawatambulishe wote”

“Sawa kwa sababu ume omba nime kukubalia”

“Nashukuru kwa hilo mume wangu”

Kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi nilivyo anza kuitilia mashaka moja ya gari iliyopo nyuma yetu.

“Hiyo gari ya blue ina tufwatilia sisi au?”

Nilimuuliza Caro huku nikigeuka nyuma na kutazama gari hii aina ya BMW X5.

“Nime waona muda mrefu ila sidhani kwa maana huu msongamano wa magari ni mengi”

“Hembu simamisha kwenye moja ya duka tuone kama wata simama au laa”

“Sawa”

Baada ya mwendo wa kama dakika tano, Caro akasimamisha gari kwenye moja ya duka. Gari linalo tufwatilia nalo likaismama mita kadhaa kutoka lilipo gari letu.

“Umeona wamesimama”

“Mmmm sasa wata kuwa ni kina nani mume wangu”

“Sijui kwani kuna mtu anaye jua mupo nchini hapa?”

“Hapana”

“Kama sio watu wenu basi wata kuwa ni watu wangu”

“Kina nani sasa?”

“Nina maadui wengi bado sasa cha kufanya wewe ondoka na gari acha mimi nishuke”

“Una kichaa nini Rashidi, yaani uingie kwenye hatari alafu mimi nikimbie. Umesahau mimi ni nani au?”

“Ishu sio wewe ni nani, ishu ni wewe na mwanangu wa tumboni kuwa salama. Hujui kama una kwenda kuitwa mama au una hisi una uwezo kwa kuhimili mikiki mikiki mikiki yamapigano. Endapo uta pigwa mangumi ya tumboni uta nieleza nini juu ya mwanangu ajaye”

“Rashi….”

“Ondoka”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama Caro machoni mwake.

“Sasa utarudije?”

“Kwani nilikujaje”

“Nina shuka nina ingia humu dukani, ondoka baada ya kama dakika moja ukiona watu hawa wana nifwatilia moimi na kama ni wewe basi nita kodisha taksi na tuta wawinda wao”

“Haya bwana mume wangu”

Caro akanibusu mdomoni mwangu kisha nikashuka na kuingia kwenye dula hili kubwa la nguo huku nikiw amakini kuhakikisha nina tazama wanao ingina ndani hapa. Nikawaona wanne walio valia suti nyeusi wakingia ndani hapa na moja kwa moja nikajua wana nifwata mimi. Nikajifanya nikizunguka kwenye duka hili kubwa na nikamuona Caro akiondoka eneo hili na gari. Mwanaume mmoja akanifwata huku mkono wake ukiwa ndani ya koti lake la simu akionyesha kwamba ana hitaji kunishambulia kwa bastola. Kabla hata hajanishambulia nikamuwahi kwa kumpiga teke la kifua na akanguka chini. Wezake wakanifwata na kuanza kunishambuliwa, kutokana nina jimudu hawakuwa na changamoto yoyote kwangu. Galfa mwanamke mwenye nywele ndefu na aliye valia miwani nyeusi akaingilia ugomvi huu na akanisaidia kuwazimisha watu hawa wanne ndani ya muda mfupi.

“Heloo baby Rashidi”

Nilijikuta nikishangaa mara baada ya kumuona Leticia akinitazama huku akivua miwani yake na kuziweka sawa nywele zake ndefu ambazo zimechanguka kutokana na mpambano huu mkali.



“What the fuc**. Leticia una fanya nini hapa?”

“Nilikuona ulipo kuwa una ingai ndani hapa ila nilipo waona watu hawa wakikufwatilia nikaona nikusaidie. Tuondoke kabla polisi hawajafika hapa”

“Ngoja”

Nikachuchumaa na nikampapasa mmoja wa watu hawa na nikachukua wallet yake nikaifungua ndani na kuona vitambulisho kadhaa. Tukatoka ndani hapa na kuvuka upande wa pili wa barabara, tukaingia kwenye gari la Leticia na kuondoka kwa kasi eneo hili.

“Una fanhya nini hapa Madagascar?”

Nilimuuliza Leticia huku nikimtazama nyuma ili kuona kama kuna gari ina tufukuzia au laa.

“Nipo mapumzikoni nimeachana na kazi ya uskari”

“Kwa nini?”

“Nimechoka kupokea oder za wakubwa hivyo kwa sasa nina fanya kazi kama mtu huru”

“Ni vizuri, una onekana mzuri vile vile”

“Hahaaa kawaida yangu kujitunza ili mtu asinitambue nilikuwa nani, ngoja tuelekee kwenye nyumba niliyo panga kwa mdua”

“Okay”

Tukafika katika nyumba ambayo Leticia amepanga.

“Karibu na ujisikie nyumbani”

“Nashukuru una ishi peke yako?”

“Yaa nina wiki ya tatu sasa toka nianze kishi hapa. Aisee hujaacha kuandamwa na majanga?”

“Wee acha tu”

Nilizungumza huku nikifungua wallet ya mmoja wa watu tulio wapiga. Nikatoa kitambulio na kimoja ya kitambulisho cha mtu huyu kinaonyesha yeye ni mwana usalama wa nchi hii ya Madagascar”

“Ni mpelelezi”

Nilizungumza huku nikimkabidhi Leticia kitambulisho hicho, kisha akakipiga picha kwa kutumia simu yake, akawasha laptop yake na kudhibitisha kama kweli huyu jamaa ni mwanausalama au laa.

“Yaa ani mpelelezi wa kitengo cha nchi hii”

“Sasa kwa nini waa nifwatilia?”

“Hujaingia kinyume na sheria katika nchi hii?”

“No sijaingia na wala sasa hivi siishi maisha hayo ya kiuhalifu tena”

“Au wametumwa?”

“Na nani?”

“Sijui nikuulie wewe maadui ambao upo nao”

“Yaani hata sielewi”

“Don na wewe mume malizana vipi?”

“Kwanza una jua kwamba Don amebadilisha sura yake?”

“Weee”

“Ndio amebadilisha sura na sasa hivi ana sura bandia”

“Ebwana ehee kwa hiyo sura yake ya sasa una ifahamu?”

“Vizuri sana”

“Sema nipo njie ya kazi ila ningekuwa ndani ya kazi ningejitahidi kumsaka. Ehee tuachane na hizo habari, nime kumbuka heka heka zako balaa”

“Kweli”

“Ndio, nahihitaji unipe mambo matamu mpenzi wangu”

Leticia alizungumza huku taratibu akinisogelea akanikalia mapajani mwangu huku tukitazamana kisha taratubu tukanza kunyonyada ndimi, ndani ya muda mfupi sote tukajikuta kama tulivyo zaliwa na kuanzisha mtange wa kukata na kushoto na ukadumu kwa zaidi ya dakika arobaini hadi kufika tamati.

“Utamu wako haujaondoka Leticia”

“Kweli?”

“Yaa wewe bado mtamu sana”

“Asante mpenzi wangu hata wewe utamu wako umeongezeka.”

Tukaoga kwa pamoja kisha nikavaa nguo zangu na Leticia akajifunga tenge.

“Umesema kwamba una fanya kazi wewe kama wewe, kivipi?”

“Yaani sasa hivi kama mtu ana hitaji nimfanyie kazi yake basi nina mfanyia kazi yake kwa mfano akihitaji nika kuue mtu ana nilipa change nina ifanya kazi kisha maisha yanakwenda.”

“Duu hatari sana”

“Ndio hivyo ndio maana nimeakua kuja kuishi mbali sana na Brazil. Vipi wewe una fanya kazi gani?”

“Mimi nipo bado nina zunguka zunguka kama tiara, upepo unapo kwenda nami ndipo ninapo kwenda”

“Waooo kwa hiyo hauna shuhuli ya msingi?”

“Ndio”

“Unaonaje tukaunda kikosi kazi cha mimi na wewe tukashirikiana kwenye maswala haya”

“Hapana Leticia hayo sio maisha ya mwanamke mzuri kama wewe kuishi. Una paswa kuanzisha kazi yako ambayo ita kuingizia kipato halali”

“Kama kazi gania mbayo nina weza kuifanya Rashidi, ikiwa maisha yangu mengi nimeishi kwa kushika silaha na kupambana na wahalifu wengi”

“Sawa kama ume amua kufanya hivyo. Kwa sasa kuna kazi moja nahitaji unisaidie”

“Kazi gani?”

“Kuna mtu inabidi kumuua. Kama unavyo tambua kwamba nchi ya Tanzania kiongozi wake amepinduliwa hivyo kuna mpuuzi mmoja ana kwenda kuchukua madaraka hivyo ina bidi tumshuhulikie”

“Yupo Tanzania?”

“Ndio”

“Sawa hakuna shaka tuta dili naye”

“Leo sinto lala hapa kuna sehemu nina hitaji kuelekea kuna watu nina hitaji kukutana nao”

“Sawa hakuna shaka, kwa sababu umepajua nyumbani nitakupatia namba yangu, muda wowote ukinihitaji uta nipigia”

“Sawa wasa”

Nikaka nyumbani hapa kwa Leticia hadi majira ya saa moja usiku nikarudi nyumbani kwa Caro kwa kutimia usafiri wa taksi.

“Mume wangu umenipatia wasiwasi kama nini?”

Caro alizungumza huku akinikumbatia.

“Kwa nin”

“Kwa lililo tokea, yaani ingekuwa si hii mimba na amri yangu ninge kufwata”

“Usijali nipo salama”

“Umewafahamu ni kina nani wale watu

“Ndio kogtambulisho cha mmoja wao kina onyesha kwamba ni wana usalama wa nchi hii”

Nilizungumza huku nikimkabidhi Caro kitambulisho cha mmoja wa wanaume niliye naye.

“Sasa kwa nini wana kufwata wewe?”

“Sijui au ndio ile ishu ya ugaidi?”

“Mmm ni ya muda mrefu sana na nchi kama nchi si ilisha kutangaza kwamba upo salama na huna kosa lolote”

“Basi ina bidi nirudi nchini Tanzania haraka iwezekanavyo na vipi uliwaeleza kwamba nimepatwa na tatizo”

“Hakuna”

“Sawa”

Tukaingia ndani kwa pamoja kwani mazungumzo haya tumeyafanya tukiwa tumekaa kwenye moja ya kibanda cha kupumzikia.

“Alafu kaka amenielekeza mzee ambaye tuna paswa kwenda ili tuweze kumshinda Nundu”

“Wewe kwenye hili nita kuomba uweze kukaa kandao. Nina hitaji kulishuhulikia mwenyewe”

“Kwa nini sasa mume wangu?”

“Kwa sababu ya mtoto wetu”

Caro akakosa poiti ya kuzungumza.

“Kwa hiyo uta kwenda mwenyewe?”

“Ndio wewe nipatie namba yake”

“Sawa”

Caro akanitajia namba ya mzee huyo kisha kwa pamoja tukaingia ndani. Tukajumuka familia nzika katika kula chakula cha usiku.

“Caro”

Raisi Mstafu aliita huku tukiendelea kula.

“Bee”

“Asubuhi nilizungumza na mume wako na nikamuomba masamaha ila ilikuwa ngumu kwa yeye kunielewa, nina kuomba umueleze kwamba msamaha wangu ninao muoma una toka moyoni, labda wewe ata kuelewa”

“Kaka Rashidi mwenyewe si huyu hapa ana kusikia na kama mtu kukusamehe kwa wewe ulicho kifanya na huyo mwanamke juu yake sio rahisi kama munavyo fikiria. Laiti ingekuwa ni mimi ningekuwa nimesha wamaliza siku nyingi wala nisinge weza kukaa na nyinyi meza moja ila mtoto wa watu ana jikaza tu kuishi nasi hapa na laity ingekuwa sio mimi angesha wadadavua. Hivyo mpeni muda”

Caro alizungumza maneno ya kumkatisha tamaa kaka yake.

“Mzee”

“Ndio Rashidi”

“Kwanzani kushukuru”

Kila mtu akanitazama hata mama Shamsa naye akaacha kula na kuniangalia kwa mshangao kidogo.

“Kwa sababu gani una nishukuru?”

“Una jua kipindi ulipo mchukua huyo mwanamke niliumia sana na ulipo nipeleka jena ndio niliumia zaidi. Ila nilipo kuja kugundua kwamba nina paswa kuishi maisha mapya basi nilihakikisha kwamba nina ishi maisha mapya na kupambana kuhakikisha kwamba nina pata pesa na nguvu ya kupambana na maadui zangu na leo hii nipo hapa. Ila kama usinge mchukua huyo mwanamke basi sasa hivi ningekuwa bado mlinzi wa kazi za watu”

“Mmmm”

Mama Shamsa akaguna kwa sauti ya chini.

“Ila mume……”

“Shiiii”

Nilimnyamazisha Caro mara baada ya machale kunicheza. Nikanyanyuka kwa haraka na kukimbilia eneo kuwashia taa za hapa sebleni na nikazima taa na giza likatawala. Nikajibanza dirishani na kuchungulia nje, nikawaona watu wanne walio valia nguo nyeusi wakiruka ukuta wa nyumba hii na kuingia ndani huku mikononi mwao wakiwa na silaha.

“Caro pandisheni juu haraka sana”

Nilizungumza huku Caro, kaka yaka na mama Shamsa wakiwa tayari wamesha simama.

“Nakuletea silaha”

Caro alizungumza huku wakikimbilia juu gorofani ambapo ndipi vilipo vyumba vya kulala. Nikamuona mmoja wa watu akifungua pin ya bomu la machozi na kulirushia ndani ya seble hii na likapenda kupitia katika dirisha la kioo. Kwa haraka nikaliokota bomu hili linalo toa moshi mwingi wa machozi na kulirushia nje na kusababisha watu hawa kuanza kushambulia dirishani hapa kwa risasi zisizo na idadi huku bunduki zao zikiwa zime fungwa viwambo vya kuzuia sauti jambo lililo fanya shambulizi kuwa la kimya kimya.

“Kamata hiyo”

Caro akaniriushia bastola moja huku naye akiwa na nyingine Akakimbilia kwenye ukuta nilio jificha.

“Wapo wangapi?”

Caro alizungumza kwa sauti ya kunong’oneza.

“Wapo wanne”

Tukasikia namna wanavyo badilisha magazine za bunduki zao. Jambo hili likanipa nafasi ya kufanya shambulizi la harala sana kwa kuftua risasi kadhaa zilizo wapata wote wanne na wakanguka chini.

“Nenda njuu kachukue familia tuondoke eneo hili”

“Sawa”

Caro akapandisha gorofani. Sikuhitaji kufungua mlango huu wa sebleni, kwa haraka nikatimia mlango wa jikoni kufungua na kutoka nje. Gafla nikakutana na watu wawili walio valia ninja wakimalizia kuruka ukuta na kutua chini kwa upande huu wa mlango wa jikoni. Mmoja wao akaruka juu na kunipiga teke la kifua lililo niyumbisha na kurudi nyuma. Kabla sijajipanga vizuri akaipiga teke bastola yangu na ikaangukia pembeni. Wakachomoa panga zao zinzo meremeta, na wakaa tayari kwa mapambano. Watu hawa wenye ujuzi mkubwa wa kuyimia panga hizi wakanza kunishambulia huku wakitumia mbinu mbalimbali. Jambo ninalo mshukuru Mungu mimi mwenyewe ni nunda ambaye nimeshindikana. Japo sina upanga ila nina jitahidi kadri ninavyo weza kukwepa mapigo yao na kwa kutumia miguu yangu na mikono yangu nina weza kupigana nao kisawa sawa. Mlio wa risasi ukasika nyuma yangu na watu hawa wakaanguka chini.

“Umeumuia mume wangu?

Cauther aliniuliza huku akinishika mkono.

“Hapana hawa watu ni hataris ana, familia ipo wapi?”

“Hapo sebleni”

“Tuondokeni”

Nilizungumza huku nikitangulia mbele kwa umakini wa hali ya juu. Tukaingia ndani ya gari familia nzima huku Mama Shamsa akiwa amembeba Ruben. Nikawasha gari hili na kuliweka sawa,nikaliendesha hadi getini kwa mwendo wa kasi kisha nikafunga breki na kuzima taa za mbele nikashuka ndani ya gari huku bastola ikiwa mkononi, nikatoka kupitia geti dogo na kuchungulia nje na kuona hali ya barabara hii ikiwa na ukimya. Nikafungua geti kisha nikarudi ndani ya gari na tukaondoka kwa mwendo wa kasi.

“Naomba simu yako”

Nilimuambia Caro na akanikabidhi simu yake. Nikampigia Leticia katika simu yake.

“Rashidi hapa”

“Vipi hii ni namba yako”

“Hapana sio namba yangu ula wale watu wamenifwatilia hadi nyumbani nilipo kaa”

“Weee hii ishu ipi seriously sana”

“Ndio hivyo nina kuja nyumbani kwako sasa hivi na famil……”

Kabla hata sijamalizia sentensi yangu nikastukia lori kubwa likutubamiza upande wangu wa dereva na kuifanya gari hii kubingirika mara nne mfululizo huku kelele zikitawala ndani ya gari hili. Mawenge mawenge yakanitawala kichwani mwangu huku hata macho yangu sioni vizuri.

“Haloo Rashidi, Rashiiiiiiiiiiiiiiiiiii”

Niliisikia sauti ya Leticia ikitoka kwenye simu iliyo anguka upande wangu huku gari hii ikiwa imelala ubavu, nikamuangalia Caro na kumuona akiwa ametulia tuli, nikegeuka nyumba na kumuona mama Shamsa na mwanaye wakiwa wapo kimya huku raisi ambaye amekaa siti ya nyuma yangu, simuoni vizuri. Gari mbili zikasimama kwa haraka pembeni ya gari letu.Taribu nikaiokota simu ya Caro na kuiingiza mfukoni mwa suruali yangu, nikajaribu kuitafuta bastola yangu ila kwa bahati mbaya siioni. Watu hawa wakafungua mlango wa gari hili, wakanitandika na kitako cha bunduki kidhwani na giza nene likanitawala.

***

“Ni nini unafanya?”

Niliisikia sauti ya raisi mtafu kwa mbali sana, nikafumbua macho yangu taratibu na kumuona raisi mstafu akiwa amesimama na Don pembeni yake huku kichwani mwake akiwa amefungw bandeji. Ila staili hii niliyo ning’izwa ni kichwa chini miguu juu.

“Una jua huyu mpuuzi amechukua kiasi gani kwangu?”

“Sasa ndugu yangu kama kiasi alicho kichukua ndio kina kufanya usababishe ajali kwa familia yangu nzima?”

“Vijana wangu hawakutambua kwamba nifamilia yako. Wao waliniambia yupo na familia yake na nilikuwa nina itamani sana familia yake ndio maana niliwapa amri ya kuhakikisha wana wakamata wote. Ila pia shukuru Mungu hujakufa na wala mke wako, mwanao na mdogo wako hamjakufa. Shida yangu ni huyu mtu hapa”

“Ila Don achana naye hana faida kwetu”

“Nakuuliza una hitaji kurudi madarakani au hutaki?”

Mazungumzo haya yote yakiendelea nina jifanya nimefumba macho yangu na sisikii kinacho endelea.

“Nina hitaji”

“Basi kaka kimya na isitoshe huyu si adui yako si ndio? Sasa una mtetea wa nini acha anzinde ili nikimuua ajue kwamba ana uwawa na mimi”

Nikalitazama eneo hili kwa kona za macho yangu na kuona mashine nyingi na kwa haraka haraka nikatambua kwamba eneo hili ni eneo la kiwanda.

“Amechukua kiasi gani?”

“Dola bilioni mia mbili”

“Una pesa hiyo yote?”

“Nina trions of dollar mzee, japo hakuna benki inayo jua hizo pesa zipo wapi”

“Ndio maana kijana alikuwa na dharua?”

“Ndio maana yake najua rogo yako haijabadilika. Kama una taka kumuua nafasi yetu ni hii. Wewe ni rafiki yangu ulinisaidia kipindi nina tafutwa na ukanipa eneo kwenye nchi yako. Sasa hivi ni wakati wa mimi kurudisha fadhila kwako. Niambie una taka tumpe adhabu gani gani unayo hisi ina faa?”

“Najua wana hisi kwamba sijui, ila wameshindwa kujua mimi ni mtu wa aina gani. Yule Ruben sio mwanangu na ni mtoto wa huyu mshenzi ila nimejikausha kama sifahamu chochote. Na huyu mshenzi alimtomb** mke wangu kipindi nikiwa nimesha muoa ndio wakampata yule mtoto. Sasa nahitaji hiyo mbo** yake ikatwe kwa maana ni dharau kubwa kumjaza mimba mke wangu wa ndoa na kumjaza mimba mdogo wangu wat umbo moja hiyo ndio adhabu ninayo hitaji aipate”

Kauli ya raisi mstafu ikanistua kidogo na kujikuta nikishusha pumzi za taratibu huku nikianza kutafuta kufikiria namna gani ninavyo weza kuepukana na adhabu hizi za hawa mashetani wawili.



ENDELEA

“Sawa akizinduka tutampatia adhabu hiyo kwa maana raha ya adhabu ni kuhakikisha mtu ana shuhudia jinsi anavyo ipokea”

“Hapo umenena jambo”

Nikawaona Don na raisi wakitoka ndani humu huku wakiwa wameongozana na walinzi. Geti kubwa la kuingilia ndani ya kiwanda hichi likafungwa.

‘Hawa wazee waseng** kweli’

Nilijikuta nikitukana huku nikijitrazama jinsi walivyo niacha uchi kama nilivyo zaliwa. Tataraibu nikaanza kujigeuza ili kuifikia Kamba iliyo ifunga miguu yangu kwani kitu walicho kikosea wao ni kunifunga miguu na kuiacha mikono yangu ikiwa huru. Zoezi la kuifungua kama hii ngumu iliyo funga mikono yangu haikuwa kazi ngumu kwangu. Nikafanikiwa kujifungua kamba hii, kisha nikatua chini taratibu kwa kwa kutumia mikono yangu huku nikimbingirika kama tairi. Nikachuchuchumaa huku nikijitazama mwili wangu ili kuona kama kuna majera yoyote ambayo yapo mwilini mwangu. Kwa bahati nzuri ajali ilivyo tokea sikuumia sana kama ilivyo kuwa kwenye ajali ya kwanza nchini Tanzania. Nikanyata hadi kwenye moja yam ashine ya kiwanda hichi, nikachunguza eneo zima na bahati nzuri hakuna mtu yoyote aliyomo humu ndani. Nikatembea kwa haraka hadi kwenye moja ya chumba kwa bahati nzuri nikakuta mavazi ya mafundi, nikavaa moja ya overall, nikavaa na buti, nikatachukua moja ya spana kubwa kisha nikaanza kutembea kuelekea mlangoni. Nikajaribu kufungu geti hili ila kwa bahati mbaya nikakuta likiwa limefungwa kwa nje. Nikafikiria kwa muda kidogo kisha nikatazama madirisha ya vioo yaliyo juu kidogo kwenye kuta za kiwanda hichi. Nikafikiria namna ya kupanda ili nitoke upande wa pili wa kiwanda hichi. Nikachukua moja ya bomba kubwa la chumba na nikaliegemesha ukutani kisha taratibu nikaanza kupanda kuelekea kwenye moja ya dirisha ambalo kioo chake kimefunguliwa. Nikafanikiwa kufika katika dirisha hili kisha nikachungualia nje.

‘What is fuc**”

Nilijikuta nikishangaa kuona ukuta wanje ukiwa ni mrefu sana kuliko ukuta huu wa ndani na kama nikijaribu kuruka basi kitakacho fwata ni miguu yangu kuvunjika vunjika.

“Lazima wata ingia tena, siwezi kuhatarisha viungo vyangu”

Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikirudi ndani, nikashuka kupitia bomba hlii hili na nikalilirudisha nilipo litoa bomba hili. Nikafuta eneo moja ambalo lina niwezesha kuangalia mlangoni kila anaye ingia na anaye toka na aneo hili sio rahisi sana kwa matu kuweza kuniona. Nikaa eneo hili baada ya dakika kama ishirini na tano hivi mlango ukafunguliwa, wakaingia walinzi wawili wakiwa na bunduki zao mikononi.

“Amekwenda wapi?”

Walinzi hawa walihamaki huku wakikimbilia katika eneo ambalo nilikuwa nimefungwa na kuning;inizwa. Nafasi hii walio niachia walinzi ikanifanya nikimbie kwa kasi na kimya kimya hadi katika geti hili na nikatoka nje kwa tahadhari kubwa sana. Nikaona wafanyakazi wengi wakiendelea na majukumu yao katika kiwanda hichi kikubwa.

‘Ni kiwanda cha nini hichi?’

Nilizungumza huku nikiendelea kushangaa shangaa. Mlio wa king;ora ukaanza kunguruma eneo zima la kiwanda hichi, nikawaona wafanyakazi wakikimbilia kwenye eneo la wazi na wakakusanyila Nami nikakimbilia na kukusanyika nao. Nikachukua moja ya kofia ngumu zinazo fanania na wafanyakazi hawa. Mkuu wa wafanyakazi hawa akasimama huku akiwa ameshika kipaza sauti.

“Kazi leo imekwenda vizuri hivyo kila mtu ata pokea pesa yake na tuta onana kesho asubuhi”

Wafanyakazi wakaanza kushangilia na kutawanyika. Walio anza kupokea mishahara yao ya siku wakaanza kutoka eneo hili, nikaambatana na wafanyakazi hawa ambao ni ngumu kunitambua kwamba mimi sio mfanyakazi mwenzoa. Nikaugeka nyuma na kusoma jina la kiwanda hichi kikubwa kisha nikaendelea kuifwatisha barabara hii huku nikiwa nimeongozana na wafanyakazi wengine. Nikamuona mmoja wa wafanyakazi nilio ongozana nao akizungumza na simu.

“Samahani una weza kuniazima simu yako?”

“Sawa”

Akanikabidhi simu yake nikaingiza namba ya simu ya Leticia kisha nikampigia.

“Ni mimi?”

“Ohooo Mungu wangu. Rashidi toka jana nina kutafuta”

“Ndio nipo maeneo ya kiwanda cha DRX,”

“Napafahamu nisubirie kwenye kituo cha mabasi nina kuja kukufwata”

“Sawa nimeazima hii namba”

“Usijali”

Nikakata simu na kumrudishia jamaa huyu na nikamshukuru kisha nikaendelea kutembea hadi tukafika kwenye kituo cha mabasi. Nikatafuta eneo la kukaa na baada ya dakika kumi na mbili nikaliona gari la Leticia likisimama upande wa pili wa barabara. Nikavuka barabara na nikaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili.

“Upo salama mpenzi wangu?”

Leticia aliniuliza huku nikivua kofia hihii.

“Sipo poa”

“Pole sana ilikuwaje?”

“Muda ule tulipo kuwa tuna zungumza lori lilitugonga na kusababisha ajali na kuna watuw alitutekea na kunizimisha. Nilipo zinduka nilijikuta kwenye moja ya godauni la kile kiwanda huku yule raisi pamoja na Don wakizungumza kuhusiana na namna gani wanavyo weza kunipatia adhabu kubwa nitakapo zinduka”

“Una taka kuniambia kwamba Don ndio ana husika na hili?”

“Ndio ana husika kwa asilimia mia moja pamoja na yule aliye kuwa raisi wa nchi ya Tanzania”

“Mmmmm, sasa ina kuwaje?”

“Tufike nyumbani nita jua nini cha kufanya”

Tukafika nyumbani kwa Leticia, akanihudumia kwa kunishona jerala langu la mguuni ambapo nimechanika sehemu kubwa kidogo kutokana naa jali niliyo ipata na damu ilinitoka hadi ikakauka yenyewe.

“Rashidi”

“Naam”

“Haya maisha yataisha lini?”

“Una maanisha nini?”

“Lini utawaangusha maadui zako kwa maana una ishi pasipo kuwa ana amani. Una cheka siku mbili una lia siku tatu na nina kumbuka ulisha wahi kuniambia wewe ni baba na una mwanamke wako ambaye najua ata kuwa sasa ni mke wako. Huoni kama wana kuhitaji, huoni kama wana kuwa wana hamu na wewe. Kwa mwaka una onana nao mara ngapi?”

Nikashusha pumzi kidogo huku nikimtazama Leticia machoni mwake.

“Niambie”

“Ina weza kupita hata mwaka sija onana nao”

“Kwa nini Rashidi ehee? Ni wakati wa wewe kumaliza hili swala, kipindi kile nilikuwa na hamu kubwa sana ya kuzaa na wewe ila nilijiona nita teseka na kumtesa mwanangu kwa maisha yale niliyo kuwa naishi hadi leo. Nikuombe kitu”

“Ndio”

“Nahitaji hii game tuimalize sasa mimi na wewe. Adui yako sasa hivi ni adui yangu nahitaji huu mchezo uishie. Umenielewa?

“Ndio”

Leticia akamaliza kunishona kisha akanifunga bandeji yenye dawa.

“Nahitaji kulala kukiweka sawa kichwa change”

“Hakuna shaka”

Nikaingia chumbani na nikajibwaga kitandani.

‘Ni kweli sasa ina bidi kuimaliza huu mchezo’

Nilizungumza kimoyo moyo na baada ya muda mfupi usingizi mzito ukanipitia na nikalala fofofo.

“Hei mpenzi amka chakula kipo tayari”

Leticia aliniamsha huku akiwa amekaa pembeni ya kitanda.

“Saa ngapi sasa hivi?”

“Saa tatu usiku”

“Aisee muda ume kwenda”

“Kiasi pia nilitaka kukuamsha saa moja ila nilikukuta una koroma sana ina onyesha ulichoka sana”

“Ni kweli”

“Oga uupe mwili nguvu kisha tujadili jambo”

“Jambo gani?”

“Kuhusiana na hawa wazee wawili ambao ni maadui zako, nimejaribu kufanya upelelezi wangu na nimesikia wametoka nje ya nchi hii”

“Nini?”

“Oga kwanza”

Nikaingia bafuni nikaoga kwa haraka kisha tukajumuika na Leticia mezani.

“Ehee niambie”

“Baada ya wale wazee kukukuta umetoroka ndani pale ndani waktambua moja kwa moja kinacho fwata ni moto wa kuotea mbali hivyo wametoroka”

“Umejuaje hayo yote?”

“Mimi nilikuwa askari mpelelezi hivyo nina jua namna ya kumfwatilia muhalifu yoyote pasipo yeye kujua. Kumlipa mtu kwa ajili ya kunipa taarifa yeti kama hizo sio jambo gumu kwangu. Hivyo nilifanya kila niwezako kupata hiyo bahari. Ulipo kwenda kulala mimi nilikwenda kufanya kazi hiyo na nikapata taarifa hizo.”

“Wameelekea nchi gani?”

“Tiketi zoa zina onyesha kwamba wana elekea Dubai ila siwezi kuamini moja kwa moja kama wataelekea Dubai ila nina imani kwamba wana kwenda Dubai”

“Wameondoka na nani?”

“Wameondoka na familia ya raisi, mkewe, mwanaye pamoja mdogo wake”

“Waliondoka wakiwa kama wametekwa au?”

“Hapana wakiwa huru tu. Picha zao hizi hapa nilizinasa wakati wana ondoka”

Leticia alinionyesha picha zilizo pigwa zikiwaonyesha raisi, Don, mama Shamsa, Ruben na Caro wakiwa uwanaja wa ndege wakiondoka.

“Umezipata wapi hizi picha”

“Kama nilivyo kuambia nina watu wangu na nilisha wapa habari juu ya hawa watu wawili hivyo waliweza kunipatia picha hizo walipo kuwa wana ondoka”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama Leticia usoni mwake.

“Nini tuna fanya?”

“Rashidi hii vita yako ina bidi sasa tutumie akili na tusipoteze muda. Nimeweza kuwaomba watu wangu ninao juana nao kuhakikisha wana nipatia destination ya ndege hiyo itakapo tua kwenye kila kiwanja na waweza kunipatia details za kila abiria anaye shuka uwanjani hapo”

“Aisee una onekana umejipanga sana kwenye kazi zako?”

“Kipindi ambacho nilikuwa kazini nilitengeneza connection nyingi kila nchi na kwa kila mtu ambaye niliamini ata nisaidia. Ni sawa na hata nilivyo fanya kwako kwa maana nina imani kama ningepatwa na tatizo mimi ungenisaidia.”

“Yaa ningekusaidia tu”

“Basi hivyo ndivyo nilivyo wekeza kwa watu wengine kama wewe”

“Sawa”

“Hivyo tusubirie majibu kwa watu hao kwa maana kwa jinsi ndege ilivyo ondoka hadi sasa hivi haijatua sehemu yoyote ile”

“Sawa nashukuru sana Leticia kwa msaada wako. Niazime simu yako nipige nchini Tanzania”

“Sawa”

Leticia akanipatia simu yake na nikampigia Shabani.

“Niambie ndugu yangu”

“Salama, hujanitafuta kaka kwema?”

“Mungu ni mwema ana saidia, ujenzi wa nyumba ya bi mkubwa umeenza?”

“Ndio ndugu yangu umesha anvza. Vipi sauti yako ina onyesha kama ni mtu mwenye maumivu fulani hivi?”

Nikashusha pumzi nyingi sana kwa maana Shabani ni mtu anaye nijua vizuri.

“Nilipata ajali”

“Mungu wangu, ajali ya nini tena?”

“Kama ile niliyo ipata Ubungo ndio niliyo ipata hapa nchini hapa”

“Aisee ilikuwaje?”

Nikamuadhithia Shabani kila kilicho tokea kuanzia tulivyo vamiwa nyumbani na kutekwa na Don na jinsi nilivyo toroka na kusaidiwa Leticia.

“Sasa kaka ina bidi ufanye jambo kwa maana ukiwa mzembe tuta kupoteza aisee”

“Ndio nina jitahidi vipi Chausiku na wanaye wana sumbuliwa?”

“Hapana usalama upo wa kutosha”

“Naomba uwalinde ndugu yangu”

“Usijali kwenye hili. Kuna lile swala la biashara ndugu yangu una onaje tukaanza kulifanya mapema huku ukiendelea kushuhulika na maswala hayo ya Don na raisi”

“Hapo umezungumza jambo. Bejeti ni kiasi gani?”

“Kwa kampuni ya mabasi au?”

“Kuanzia hoteli na miradi yote?”

“Bado sijajua juu ya hoteli ila ya mabasi nimefahamu kuyaingiza nchini hadi kuyasajili na kuanza kuanza kufanya kazi ina tugarimu kama 4.5 bilioni shilingi?”

“Ambazo kwa kukadiria ni dola kama mbili na na usheee?”

“Ndio kaka?”

“Sawa sasa nita hamisha kiasi cha pesa kwneye akaunti yako. Hakikisha kwamba usimamizi wake una kuwa mzuri na mambo yana kwenda kama tulivyo panga”

“Usijali kaka nita simamia kila jambo”

“Poa hembu nitajie akaunti yako inayo weza kupokea kiwango kikubwa cha pesa”

Shabani akanitajia akaunti namba yake nikainakili pembeni kisha nikakata simu.

“Nataka kumuingizia dola milioni kumi”

“Samahani ume sema?”

“Dola milioni kumi”

“Unayo hiyo pesa na mbona ni pesa nyingi sana hiyo umeitoa wapi?”

“Kwa Don”

“Kivipi?”

Nikamuelezea Leticia namna nilivyo pata pesa hiyo kutoka kwa Don.

“Aisee sasa kama una pesa kiasi hicho hapa ndipo nakumbuka ule ushauri wako ulio niambie nianzishe biashara kumbe ningepata udhamini”

“Hhaaahaa ndio hivyo niazime laptop yako nihamishe pesa”

Leticia akanikabidhi laptop uake niakingia katika mfumo wa pesa nikamahimisha kiasi cha dola milioni ishiri katika akauti ya Shabani kisha nikampigia simu.

“Ndugu imefika?”

“Aisee hichi ninacho kiona ni kweli au?”

“Ni kweli, kumi hapo ni yako na kumi nyingine ingiza kwenye mradi wa mabasi kisha hizo hoteli nita zijenga nikiwepo”

“Shukrani sana ndugu yangu Mungu akubariki”

“Amen, hakikisha mambo yanakwenda”

“Usijali kaka yata kwenda”

“Poa wasalimie wote”

“Alafu ndugu kuna jambo moja nataka kukuambia kuhusiana na Tina”

“Jambo gani tena?”

“Nahisi huyu binti ni mjamzito?”

“Weee”

“Ndio ana kila dalili ya kuwa mjamzito na mama Chau aliniambai hili jambo leo na nililidhibitisha kwa kumuona akitapika”

“Upo nyumbani?”

“Yaa”

“Hembu naomba umpatie simu”

“Dakika moja”

Nikanyanyuka na kutoka nje ili nizungumze na Tina vizuri.

“Huyu hapa”

“Haloo”

“Niambie mume wangu”

“Una jisikiaje?”

“Namshukuru Mungu nipo vizuri”

“Una mimba”

“Nani amekuambia?”

“Niambie ukweli?”

“Najisikia nina dalili hizo mume wangu ila sijapima”

“Basi asubuhi Sheby ata kupeleka hospitali sawa”

“Sawa mume wangu, mpe simu Shabani”

“Ndio kaka”

“Kesho umpeleke hospitalini huyo”

“Sawa ndugu yangu nita lifanya hilo, ngoja kwanza naona Chausikua na kuja huku ana kimbia sijui kuna nini”

“Shabani Shabani kaka yangu mume wangu ameuwawa, nipelekea nikauone mwili wake”

Nikastuka sana mara baada ya kusikia mume wa Chausiku ameuwawa, na swali moja ninalo jiuliza kama mimi nipo huku, Caro na familia yake wapo nje ya nchi ni nani amehusika na kifo cha Nundu.



“Ameuliwa wapi na nani?”

Nilimsikia Shabani akiuliza kwa msisitizo.

“Sijui wewe nipeleke maiti yake ipo Muhimbili.”

“Sawa kaingie kwenye gari. Kaka una nisikia?”

“Nakusikia vizuri”

“Ngoja nikalishuhulikie hili”

“Poa nipatie ripoti ya kila kinacho endelea”

“Sawa kaka si kwa namba hii?”

“Ndio kwa namba hii hii?”

“Poa poa

Nikakata simu huku nikimtazama Leticia machoni mwake.

“Kuna nini?”

“Yule jamaa tuliye panga kumuua ameuwawa?”

“Weee?”

“Ndio sasa sijui ni nani amehusika na kifo hicho.”

Nilizungumza huku tukirudi ndani kwani Leticia alitoka ndani wakati nilipo kuwa nina Zungumza na Maulidi.

“Au atakuwa na maadui wengine zaidi yaw ewe?”

“Labda kwa maana mtu anapo kuwa na amadui wengi basi , lazima ashuhulikiwe. Baada ya nusu saa Shabani akapiga simu.

“Ndio ndugu yangu”

“Kaka ni kweli kamaa amefariki amepigwa na risasi ya kichwa na imetoboa upande wa pili na ubongo wote umefumuliwa.”

“Mmmm”

“Ngoja nikutumie picha kwa maana Chausiku ameuona mwili wa mume wake amezimia”

“Hembu nituimie”

Picha kama ishirini na mbili hivi zikaingia katika simu, kupitia mtandao wa whatsapp. Nikazifungua na tukaanza kuangalia moja baada ya nyingine.

“Huyu aliye tekeleza hili ni sniper”

Leticia alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Kwa nini?”

“Hiyo risasi iliyo mpiga sio ya bunduki hizi za kawaida kama pistor, smg au shory gurn. Kwa maana bunduki hiyo imeipenyeza kwenye paji la uso na kutoka nje na kuacha tundu hilo sio jambo la mchezo.”

Simu ikaita tena na nikaipokea.

“Ndio Sheby"

"Upo karibu na tv?”

“Ndio”

“Hembu washa tv aisee,”

“Kuna nini?”

“Nchi imepinduliwa tena”

“Nini?”

Nilizungumza huku nikiangaza angaza ni wapi ilipo rimoti. Nikaiwasha tv hii na kutafuta cheneli ambayo ina weza kurusha taarifa hiyo.

“Kuna nini?”

Leticia aliniuliza maera baada ya kuoniona nikibadilisha badilisha chaneli hizi.

“Nasikia nchi imepinduliwa tena”

“Ohooo hembu weka bbc”

“Ni namba ngapi?”

“229”

Nikaweka cheneli hiyo na kweli tukakuta matangazo ya uongozi jenerali Ngatuma kupinduliwa na aliye tekeleza hilo ni waziri mkuu wa serikali ya raisi aliye tolewa madarakani.

“Tanzania ni nchi imara na haiwezi kuchezewa na wapuuzi wenye uchu wa madaraka na wanayo itakia mabaya. Nafasi ya raisi Francis ita endelea kama kawaida na atatolewa madarakani kwa mujibu wa kikatiba, moja kushindwa kwenye kura au muda wake wa uraisi utakapo kwisha. Hivyo nina waomba wananchi wote wa Tanzania kuendelea kuwa na amani kwani nchi ipo katika mikono salama kuanzia hivi sasa na wanajeshi wote walio iasi nchi adhabu yao ni kifo na hakuna atakaye pelekwa kwenye mahakama yoyote duniani. Asanteni na Mungu aibariki Tanzania”

“Huu ni mpango wa DON”

Nilijikuta nikizungumza huku nikizima tv hii.

“Adui yetu hajapiga hatua pekee ila amepiga msamba si kwa kasi hii aliyo kwenda nayo”

Maneno ya Leticia yakanifanya nishushe pumzi nyingi huku nikiwa sijui ni kitu gani kimetokea kwa uharaka hivi hadi karata niliyo kwua nina itegemea kuchanika.

“Tuna fanyaje kwa maana jamaa ana rudi madarakani?”

“Sijui cha kufanya Leticia kichwa changu kimeyumba”

“Tulia wewe sio wa kushindwa kirahisi namna hiyo. Fikiria nini cha kufanya”

Leticia mara baada ya kuzungumza hivyo akaingia jikoni kisha akarudi na mzinga wa wisky pamoja na glasi mbili. Akanikabidhi glasi moja akanimiminia wisky kiasi kidogo kisha na yeye akajimiminia kiasi chake. Tukagonga chease kisha kwa pamoja tukanywa kiasi hichi cha pombe hii kali hadi ikaisha. Akaongeza kiasi kingune kwenye kila galsi.

“Fikiria nini tufanye Rashidi?”

“Lazima tuukate mzizi”

“Ambao ni DON si ndio?”

Leticia aliuliza.

“Ndio ni DON”

“Hati yako ya kusafiria unayo?”

“Ilipotea kwenye ajali”

“Basi tuta elekea kwa mtaalamu mmmoja hivi akakutengenezee passport yako kisha tuta elekea nchini Tanzania nina imani tukiwa Tanzania tuta jua nini cha kufanya?”

“Nimekuelewa”

Tukaendelea kunywa pombe hii kali ha vichwa vyetu vikalewa kisawa sawa. Uchokozi wa kimapenzi alio uanzisha Leticia tukajikuta tukizama kwenye dimbwi kubwa la mapenzi huku kila mmoja akifurahia penzi la mwenzake.

Asubuhi na mapema, tukaelekea kwa mzee ambaye ana tengeneza hati za kusafikria kwa njia za magendo. Akanitengenezea hati yangu ya kusafiria, tukamlipa kiasi alicho kihitaji na majira ya mchana tukakata tiketi ya ndege kwa ajili ya kurudi nchini Tanzania. Majira ya saa tisa alasiri tukaingia ndani ya ndege na safari ya kurudi nchini Tanzania ikaanza. Tukafika uwanja wa ndege wa JKN kitu kilicho badilika kidogo ni ulinzi wa wanajeshi wanao katika katika katika kiwanja hichi.

“Nahitaji nikae hotelini ili niwe huru kufanya upelelezi wangu”

Leticia alizungumza huku tukutoka nje ya uwanja huu.

“Hutaki kufikizia kwangu?””

“Sinto kuwa huru wewe mwenyewe una fahamu kazi hii jinsi unavyo endeshwa. Laiti kama ungekuwa una ishi mwenyewe hapo sawa”

“Nimekuelewa, una hitaji hoteli ya ina gani?”

“Yoyote ila ningependa hoteli ya kawaida kwani ita nipatia uhuru wa mimi kuifanya kazi yangu kiufasa. Ni lazima nipeleleze ni namna gani mambo yanavyo kwenda kwenye hii nchi na tuta kuwa tukionana mara kwa mara”

“Sawa”

Tukaingia ndani ya taksi na moja kwa moja tukaelekea hadi kwenye hoteli ambayo niliona ni eneo zuri kwa Leticia kukaa, baada ya hapo nikaelekea nyumbani kwangu. Nikamlipa dereva taksi kiasi anacho nidai kisha nikashuka ndani ya taksi hii, nikaminya kengele ya getini kisha geti likafunguliwa. Tina akanikumbatia kwa furaha huku akinipiga mabumsu mfululizo.

“Ohoo asante Mungu umerudi mume wangu”

“Una endeleaje?”

“Nipo vizuri japo kuna huzuni huzuni humo ndani. Mume wa dada Chausiku amefariki”

“Duu”

“Ndio hivyo ameuwawa”

“Vipi wewe na mwanangu ajaye mupo salama?”

“Namshukuru Mungu tupo salama, shem alinipeleka hospitalini na kweli nimekutwa na mimba”

Tukaingia ndani na nikawakuta kina mama wengi baadhi yao ni kutoka mtaani kwangu nilipo kulia. Shem akanifwata na tukasalimiana na moja kwa moja tukeleka jikoni.

“Vipi Chausiku yupo wapi?”

“Chumbani yupo na madaktari kidogo presha ina msumbua”

“Okay msiba upo hapa?”

“Hapa?”

“Hawa ni rafiki wa mama wamekuja kumfariji tu. Ila walisha zika kwa taratibu za kiislamu. Wamezika eleo saa nne asubuhi”

“Okay, Sheby yupo wapi?”

“Ametoka mara moja?”

“Kuna mpya gani ukiachana na msiba?”

“Hakuna mpya shemeji yangu ila hongera kwa kumjaza Tina”

“Hahaaa shukrani”

Nikasalimia na wamama hawa kisha nikaeleka chumbani kwa Chausiku, nikamkuta akiwa amelala kitandani huku ametundikiwa tripu ya maji na pembeni yake yupo nesi.

“Hababri”

“Salama”

“Mgonjwa ana endeleaje?”

“Hali yake kidogo ni nafuu kwa sasa tofauti na jana”

Nikaka pembeni ya kitanda hichi huku nikimtazama Chausiku machoni mwake.

“Hei una jisikiaje?”

“Afadhali kidogo”

“Uta kuwa salama mshkaji wangu sawa”

“Nashukuru, nesi naomba utupishe kidogo”

Nesi akatoka ndani hapa na nikabaki na Chausiku.

“Rashidi”

“Naama”

“Una weza kujua ni nani ambaye amehusika na kifo cha mume wangu?”

“Kwa kweli sijui, jana nilipo kuwa nina zungumza na Sheby ndio nilisikia hiyo taarifa uliyo kuwa una muambia ndio maana leo nimerudi”

Chausiku akanitazama machoni kwa sekunde kadhaa kisha akanitazmaa mkononi mwangu ambapo nimefunga bandeji.

“Umefanyaje hapo mkoni?”

“Nilipo kuwa Madagascar nilipata ajali ya gari nikaumia hapa mkononi”

“Pole”

“Nashukuru mpenzi wangu. Nani alikupatia taarifa ya kifo cha mumeo?”

“Ni mlinzi wake na aliniambia kwamba emedunguliwa alipo kuwa ana shuka ndani ya gari lake na akafariki hapo hapo”

“Duu pole sana”

“Nashukuru Rashidi, japo yule mwanaume nilikuwa simpendi ila kusema kweli nilipo ona na maiti mwili wangu wote ulijawa na ganzi kubwa sana na nikajikuta nikishiwa nguvu kabisa na kuzimia”

“Pole ila kama unavyo sikia nchi ime pinduliwa tena”

“Na nani?”

“Kwani huna habari?”

“Sijui chochote mimi”

“Masikini pole sana, nchi imepinduliwa na aliye kuwa waziri mkuu na serikali iliyo ondolewa madarakani ina rudi tena na yule jenerali Ngatuma naye ame uwawa hivyo kwa asilimia mia moja mume wako ame uwawa na watu walio ipindua serikali””

“Si wata niua na mimi?”

“Kwa nini wakuue?”

“Si mke wa msaliti?”

“Hapana huna hatia yoyote itakayo kufanya wewe kuuwawa. Hivyo kuwa na amani”

“Naogopa Rashidi”

“Usiogope. Ngoja nikabadilishe nguo”

“Sawa”

Nikatoka ndani hapa na kuingia chumbani kwangu. Nikamkuta Tina akiwa amevalia kanga moja, taratibu akaifungua kanga na ikadondoka chini.

“Nina hamu na wewe mume wangu. Nimeshindwa kuvumilia”

Tina alizungumza huku akinisogelea taratibu, tukaanza kunyonyana denda na nikamlaza kitandani taratibu.

“Ila kuna msiba mke wangu”

“Sinto piga kelele, nifanye taratibu taratibu”

Tina alizungumza huku akifungua zipu ya suruali yangu. Akamshika jogoo wangu na tartaibu akamchomeka katika kitumbua chake. Taratibu tukaanza mechi hii huku kila mara Tina ana jizuia kutoa sauti, hadi tuna maliza kila mtu jasho lina mwagika kisawa sawa. Tukaoga pamoja kisha Tina akaniandalia nguo za kuvaa. Tukatoka chumbani hapa na nikakutana na Shabani katika kordo moja kwa moja tukatoka nje na kukaa kwenye kibanda cha kupumzikia.

“Ehee niambie ndugu yangu”

“Aisee hali ndio kama hii mambo yana kwenda haraka sana”

“Yule mshenzi ana rudi tena madarakani tuna fanyaje?”

“Mmmm kusema kweli ni shuhuli pevu ndugu yangu na yule chagudoa mwanamke si bado yupo naye?”

“Ndio wapo wapamoja”

“Mmmm hii vita ya safari hii kaka ina bidi tufanye maamuzi magumu kufa au kupona”

“Ni kweli. Vipi umepata basi ngapi?”

“Nimeagizia basi ishirini kwanza na hizi ndio picha zake zina chorwa na nimesha fungua kampuni ya basi hizo na nimenunua godauni moja na nyumba moja ambayo ndio zita kuwa ofisi za mabasi yetu”

Shabani akanionyesha picha za mabasi yanayo endelea kuchorwa namna tunavyo hitaji yawe.

“Ni mazuri”

“Yaa ni mazuri nimepanga yawe yana kwenda Dar to Mwanza, Mbeya. Iringa, Tanga na Nairobi”

“Kazi nzuri ndugu yangu. Nimepoteza simu yangu hivyo baadae nahitaji tueleke madukuani nikanunue nyingine”

“Usijali kaka”

“Nimechoka sana”

“Umechoka nini?”

“Maisha tu yaani natamani kama nifenife””

Hahaaa cha ujinga ndugu. Kwa nini una kata tamaa mapema?”

“Kaka kuna kipindi nikiwa kama binadamu nakosa hamu ya kuishi. Nina pesa, nina wake wazuri nina watoto wazuri ila sitamani kuishi kabisa, natamani Mungu anichukue hata sasa hivi ili hizi dhahama ziweze kuniepukia”

Nilizungumza kwa sauti ya upole huku hali ya kukata tamaa ikiwa imenitawala moyoni mwangu.

“Nikuulize kitu?”

“Niulize”

“Nini kimetokea kwa maana sijakuzoea kukuona una kata tamaa mapema hivyo?”

“Shabani”

“Ndio kaka”

“Katika maisha yangu nimepitia mambo mengi sana, Katika yote hayo asilimia themanini ni mabaya. Sijapitia mazuri ya kusema yamenifurahisha. Najua nita kuwa na mwisho mbaya”

“Una maanisha nini?”

“Nimeua watu wengi sana, nimefanya mambo mengi sana mauvu. Una hisi nini kinacho kwenda kufwata mara baada ya uovo huo wote nilio ufanya? Nita kufa na sijui nita kufanye ndugu yangu. Nahitaji kufanya jambo la mwisho kisha baada ya hapo nita jua nini cha kufanya?”

“Jambo gani?”

“Nahitaji kumuua DON na baada ya kumuua DON nami nita jiua?”

Shabani macho yakamtoka kwa mshangao kwa maana hajategemea kama nita zungumza jambo kama hili ila kusema ukweli nina tamani maisha yangu yafike tamani ili niweze kupumzika kwani niliyo fanya hadi sasa nina amini kwamba nimetosheka.




“Kaka narudia kukuambia wewe ni mpambanaji, japo sijui ni changamoto gani ulizo zipitia kiuhalisia, ila umenihadithia na kweli ni mambo magumu sana kama binadamu una weza kukata tamaa mapema sana. Ila kumbuka kwamba nipo hapa ndugu yako, tulipita kwenye mengi na mengi tulisaidiana, mazuri na mabaya. Siwezi kukubali kukuona una kata tamaa kirahisi namna hiyo”

Shabani alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwanagu. Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama Fatma anaye kuja eneo hili huku akiwa amevalia baibui.

“Shemeji habari yako”

“Salama habari yaw ewe?”

“Namshukuru Mungu umerudi lini?”

“Mida hii ndio nime ingia, msiba umenirudisha nyumbani”

“Aisee ni kweli, tuna weza kuzungumza kidogo?”

“Ohoo ngoja niwapishe”

Shabani akasimama na akaondoka eneo hili, Fatma akaka kwenye kiti alicho kuwa amekalia Shabani.

“Niambie”

“Nime kumiss Rashidi”

“Hilo ndio ulilo taka kuniambia au kuna jengine?”

“Jengine ni jinsi uongozi wa nchi ulivyo badilika kwa haraka sana”

“Nimesikia”

“Sasa kama adui yako ana rudi madarakani ita kuwaje?”

Swali la Fatma likanifanya nishushe pumzi kidogo huku nikimtazama machoni mwake.

“Nani adui yangu?”

“Si raisi anaye rudi madarakani, najua ni adui yako kwa sababu amemchukua mke wako wa ndoa”

“Wewe una mawaza gani?”

Nilirahisisha mada hii kwa kumuuliza swali Fatma ambalo kwa kweli nina hitaji kusikia maoni yake.

“Mawazo yangu nahitaji tumpe nguvu waziri mkuu awe raisi”

“Una maanisha nini?”

“Rashidi siasa ni mchezo wa Karata. Utakapo zichanga karata zako vizuri una weza kufanikiwa kwenye mambo mengi sana. Waziri mkuu aliwezeshwa na somebody Frenandes Philipe pesa za kuweza kupanga mipango ya haraka haraka na wakamuondoa adui yao ambaye ni ngatuma pamoja na shemeji yeyu au kwa lugha nyingine X shemeji. Huyu waziri mkuu aendapo ana pewa nguvu na mtu wa kando ana uwezo kuwa raisi na isitoshe sasa hivi yeye ndio anaye ongoza nchi”

“Ila kama amewezeshwa na huyo Frenandes huoni kama atakuwa ni kibaraka wa huyo Frenandez kwa maana kitu pesa kina mfanya mtu kuwa mtumwa maisha yake yote”

“Najua ata kuwa mtumwa ila poit yetu kwa nini asiwe mtumwa kwetu. Ngoja nikupe sifa za huyu mzee, moja ni mtu anaye penda sana totos wazuri wenye matako makubwa. Mbili ana penda sana pesa na pombe, kiufupi ni mtu wa bata.”

“Mungu wangu mtu kama huyo kweli akipewa nchi ana weza kufanya kile ambacho wananchi wana kihitaji akifanye?”

“Haijalishi Rashidi, usiangalie kundi la watu wengi. Jiangalie wewe na usalama wako na familia yako, kwa maana huyu mzee mimi ni rafiki yangu sana na kiufupi yupo hapa kiganjani mwangu. Amenitongoza sana ila nina mchomolea na pia ana muogopa sana mume wangu. Ndio maana ana kuwa na heshima na mimi, hivyo huyu tukimchorea ramani ana pita tunapo taka sisi”

“Una mjua huyo Frenandes Philipe?”

“Namjua kivipi?”

“Una mjua ni nani?”

“Sijui ila nasikia ni mfanya biashara wa Kimexan?”

“Huyo Frenandes Philipe ndio adui yangu mkubwa. Jina lake halisi anaitwa DON kama una umeshawahi kusikia Mungu wa madawa ya kulevya ndio huyo DON a.k.a ni Frenandes Philipe”

“Mungu wangu kumbe ndio yeye!!?”

“Ndio ni yeye hivyo alipo ingia huyo makamu wa raisi hato weza kutoka. Ni mara kumi aliye ingia kwa Nundu kuliko kwa DON. Mtu pekee niliye fanikiwa kutoka mikononi mwa DON ni mimi na pia bado ana nisumbua na kaa unavyo ona hizi bandeji ni moja ya ajali niliyo ipata nikiwa Madagascar na nimeponea chupuchupu kuuwawa na huyo mtu. Hivyo vita yangu ni mimi na DON. Huyu raisi ni kama tawi tu”

Fatma akashusha pumzi nyingi sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Nimepata wazo”

“Wazo gani?”

“Kwa nini tusimtafute mtu mwengine mwenye nguvu kwenye chama chao tukamuwezesha kuchuana na raisi huyu anaye rudi madarakani”

“Kwani uchaguzi si baada ya miaka kama miwili, una taka tukae miaka miwili tukiwatazama tu?”

“Hapana huyu aling’olewa madarakani kwa sababu ya kutokuaminiwa. Ili aweze kurudi ni lazima kwanza chama chake kumpigie kura kisha bunge likae na limpitishe. Nina wabunge wengi ninao juana nao na wenye kuweza kunisaidia kwenye hili. Akikosa kura ya chama chaka au akipata, basi bungeni tuna kwenda kumbamiza”

“Hivi Fatma una jua mimi sio muumini kabisa wa Siasa?”

“Najua hili Rashidi, ila kwa sasa ndio kadi tuliyo nayo mkononi. Ukitaka kumuua huyu mzee, kumbuka kuna usalama wa taifa, wata kutafuta na kukudhuru au una taka kutangazwa kuwa gaidi kama ilivyo kuwa kipindi cha kwanza”

“Ina onekana Profile yangu ume isoma sana ehee?”

“Nisiwe muongo ni kweli nilikusoma kwa namna ninavyo jua mimi na kukuelewa mambo mengi”

“Kwa nini umefanya hivyo?”

“Kwa sababu nimekupenda Rashidi, hajalishi nina mume au ni mpenzi wa Rafiki yangu ila nimekupenda kwa maan moyo wangu una haki ya kuchagua ninacho penda na ninacho kihitaji”

“Ila wewe ni mke wa mtu?”

“Najua ila wewe ni mume wa watu”

Nikajikuta nikitabasamu kwa maana Fatma ana onyesha ujasiri ambao sikuutegemea kutoka kwake.

“Wewe ni nani kwanza kwa maana ina bidi tujuaje kabla ya kwenda mbele kwa maana nina kujua kwa jina la Fatma tu na rafiki wa Chausiku hayo mengine siyajui kwako?”

“Hahahaaa, mimi majina yangu ni Fatma Makwega. Kwetu ni Morogoro, mtoto wa mwisho na watatu katika familia ya mzee Makwega. Baba yangu alikuwa jenerali wa jeshi miaka ya huko nyuma, kaka yangu ni mkurugenzi wa shirika la umeme, dada anaye nifwatia ni muhasibu mkuu wa B.O.T. Mimi ni mdananda”

“Una maanisha nini kusema mdananda?”

“Baada ya kumaliza PHD yangu kwenye maswala ya uhasibu, niliingia jeshini, nikapiga kazi kwa miaka mine na huko ndipo nilipo kutana na mume wangu na tukafunga ndoa tulipo kuwa huko huko jeshini. Kutoka akili yangu haikuwa kabisa kwenye maisha ya kuajiriwa, niliamua kuchana na jeshi na kufanya biashara pamoja na kuingia kwenye siasa ambapo huko nilitengeneza connection nyingi sana kwa maana mume wangu alisha wahi kuniambia kwamba ndoto yake ni kuwa raisi. Hivyo ili nitimieze ndoto za mume wangu ni lazima nihakikishe nina tengeneza mazingira mapema kabla yay eye kuwa raisi”

“Ngoja kwanza, mume wako bado ana ndoto za kuwa raisi?”

“Hadi ana ingia kaburini anazo.”

Nikaka akimya kwa muda kidogo.

“Usitake kuniambia mume wangua arudi achukue nafasi hii?”

“Una miaka mingapi?”

“Arobaini na nane. Usinione mrembo mrembo nimekula maisha hii baby Face ndio ina nifanya nionekane mdogo.”

“Una sifa za kugombania uraisi”

“Mimi?”

“Ndio jeshini umepita na una jua maswala ya usalama wa nchi hii. Una ijua siasa ya nchi hii na wana siasa wengi wapo mikononi mwako. Why tusiitumie hiyo nafasi. Kipindi cha kwanza ukagombania na ukawa wewe na kipindi cha pili cha uongozi ukamuachia mume wako”

“Mmmm?”

“Usigune, kwa sababu hatuwezi kuwekeza kuwekeza kwa mtu ambaye hatujui huko mbele ata tufanyia vimbwanga gani si una jua madaraka yana vimbisha kichwa. Ila wewe nina weza kuwekeza kwako”

“Ngoja nizungumze na mume wangu kwa maana sikuwa na malengo wala mawazo hayo?”

“Akisema hapana utaacha hii nafasi iende?”

“Ni mume wangu n anime umbwa kuwa chini yake na sio juu yake”

“Basi zungumza naye nipatie jibu”

“Naenda kuzungumza naye sasa hivi. Nipe dakika kumi”

“Sawa”

Fatma akasimama na akaondoka eneo hili na nikabaki nikimtazama jinsi wezere lake linavyo tingishikia kiasi cha kunifanya nishushe pumzi nyingi.

‘Aisee kumbe usili lijua ni sawa na usiku wa giza. Demu kumbe ni mjeda, ukiingia vibaya vibaya ana kuvunja?’

Nilizungumza huku nikimtazama Fatma akifungua mlango wa gari lake aina ya Toyota VX V8. Baada ya dakika kama saba Fatma akatoka na kurudi nilipo.

“Naona uso una furaha?”

“Sana, mr amekubali niweze kugombania hiyo nafasi na nimemueleza wazo lako la kwamba mimi nina kwenda kumsafishia njia. Miaka mitano sio mingi, nikipiga mitano na yeye ana kuja kumalizia kumi ya mwisho”

“Umeona ehee?”

“Ndio sasa hapa ina bidi tuanze kufikiria nje ya boksi Rashidi. Siasa yetu moja ina hitaji pesa, na mbili ina hitaji kuwa black mail watu tunao fanya nao kazi”

“Una maanisha nini kwenye kuwa black mail?”

“Kila binadamu ana udhaifu wake. Hawa wanachama ambao nikizungumza nao na kulipitisha jina langu lisimame kwenye kinyang’anyiro cha uraisi, wana weza wakala pesa na kura nisipate. Chakufanya ni kuhakikisha kwamba kila mmoja tuna pata profile yake, yenye mazuri na mabaya yake ambayo ana hisi ni ya sirini. Ili anapo kula pesa yetu ajue na sisi tunayajua yake. Hii ita saidia kuua mawazo yake ya kiherehere cha kutaka kutoka kwenye mikono yetu”

“Hapo ume nena jambo. Kiasi gani kina hitajika hadi wewe kuingia ikulu?”

“Kwa makadiria ya haraka si chini ya dola millioni mia”

“Mia moja!??”

Nilizungumza huku macho yakinitoka.

“Ndio haziendi zote ila hapo tutakuwa na nguvu ya kumnunua yoyote yule tunaye mtaka. Rashidi ukiachana na nguvu ya Mungu, kitu kingine chenye nguvu hapa duninia ni pesa mpenzi wangu”

“Una nihakikishia ukipata pesa hiyo una weza kuingia madarakani?”

“Kwa asilimia mia moja Rashidi”

‘Nina pesa nyingi haramu hii hii ndio ina fanya hizi njia za haramu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimtazama Fatma usoni mwake.

“Nakuhakikishia nita kuwa mbwa wako kuanzia kwenye ngono hadi kuwenye lolote utakalo hitaji ndani ya nchi hii”

“Sitaki kukufanya kuwa mbwa wangu kwa sababu sipo hivyo. Nitakacho kihitaji ni kumfyekelea mbali DON pamoja huyu Kenge wake”

“Sawa hayo tu?”

“Ndio”

“Usijali yatafanikiwa kwa maana kama ni ushawishi kwenye chama ninao na nguvu ndani ya chama ninao cha kufanya ni mimi kuanza harakati za kulipandisha jina langu liwe kileleni zaidi”

“Ila ninavyo sikia siasa ni mchezo mchafu. Uta uwawa?”

“Kwa kuniroga hawato weza kwa maana mimi mwenyewe ni mchawi hahaaa. Kirisasi siwezi kuuliwa kizembe kama nundu kwani nita lipa serikali na wata nipatia walinzi maalumu kama raisi kabla ya kuingia madarakani na baada ya kuingia madarakani wata kuwa ni walinzi wangu moja kwa moja.”

“Fatma una ongea kwa kujiamini usije ukanieletea mapicha mapicha sinto kuelewa?”

“Rashidi kama una taka nikudhibitishie kwamba sinto kuangusha wala kukubadilikia wewe twnede nikakuonyeshe”

“Ukanionyeshe nini?”

“Wewe twende tu sehemu kama huto jali”

Nikajifikria kwa muda kisha tukaeleka hadi katika gari la Fatma, tukaondoka eneo hili na tukafika kwenye nyimba moja iliyopo maeneo ya Mbezi Beach.

“Karibu hapa ni kwangu, nyumba hii nimeinunua kwa ajili ya kutuliza akili na ninapokuwa nimechoka au ninapo kuwa na shuhulizangu Dar es Salaam huwa nina penda kuja kukaa hapa, sipendelei sana kukaa hotelini kwani usalama wa hotelini ni mdogo kuliko unapo kuwa nyumbani kwako kama hapa”

Fatma alizungumza huku tukitazama mazingira ya nyumba hii ambayo ni nzuri sana.

“Mume wako wana fahamu una nyumba hapa?”

“Hapana, sio kila jambo ninalo lifanya mume wangu afahamu kwa maana kuna maisha baada ya kuachana”

“Eti ehee?”

“Ndio”

“Wewe si ndio mtu uliye niambia umezaliwa kuwa chini yake na ana amri juu yako?”

“Ndio kwenye swala kama la uraisi sio swala la mimi kumdanganya kwa maana siwezi kuwa raisi wa kujificha na nikiwa raisi nita kuwa bosi wake hivyo ni lazima nimueleze hiyo ili ajiandae kisaikolojia. Kwani akiachana kuwa mume nyumbani ila ofisini nita kuwa bosi wake”

“Nimekuelewa”

Fatma akaingiza namba za siri kwa ajili ya kufungua mlango wa nyumba hii kisha tukaingia ndani. Fatma akavua baibu lake kisha akavua suruali aliyo ivaa ndani ya baibui hili na akabaki akiwa na chupi pamoja na sidiria.

“Rashidi siku ile tuliiba iba. Leo nifanye chochote unacho kihitaji kunifanya nikiwa kama mwanamke wako”

Nikatazama umbo hili namba nane la Fatma. Japo sipo kwenye mood ya kufanya mapenzi ila nikajikuta niki nikiapwa na msisimko wa ajabu sana dhidi yake. Nikamsogelea na kumshika moja ya kalio lake na nikaliminya kwa nguvu.

“Kwa nini unataka nikutomb**?”

“Kwa sababu un ambo** tamu”

Fatma alizungumza huku akiyarembua macho yake. Tukaanza kunyonyana denda kwa hiais kali sana, nikamlaza katika sofa lililo hapa sebleni, nikamvua sidiria yake na nikaanza kuyanyonya maziwa yake.

“Oohoooiiii….aiiiisii…..tamu”

Fatma alitoa miguno iliyo zidi kunipandisha morali. Nikaanza makaratee yangu ya kumnyonya kila sehemu ya mwili wake. Kusema kweli mwana mama huyu amejazia, tena amajiazia kisawa sawa sawa na kila sehemu ya mwili wake ni laini na inayo lete msisimko.

“Una ninyonyo…..o…nya vi….zu….ri baby…..”

Fatma aliendelea kulalama, nilipo jiridhisha na oparesheni yangu ya kumuandaa, nikaanza kumpa vitu adimu na safari hii hata naye ana jituma kisawa sawa huku akionekana ana hitaji kunikomoa ila kutokana na uzoefu wangu nilio nao kwa wanawake, komoa yake ikageuka kibao kwake na ikawa mputemte mpute huku jasho likilowanisha miili yetu kana kwamba tume toka kuoga. Kutokana na siku mbili hizi kutumika sana kwa wanawake hawa ikanichukua lisaa zima kumaliza mzunguko huu.

“Ungeniua Rashidi”

Fatma alizungumza huku akishema sana.

“Kwa nini?”

“Ahaa si kwa kunipekesha huku. Wewe mwanaume huchoki, yaani kasi uliyo anza nayo ina ongeza kila muda”

“Ndio uweze kuona tofauti ya sisi wanaume, mimi sio kama hao wengine”

“Wewe utakuwa ume chanjiwa aisee”

“Hahaa sijui ila hivyo ndivyo nilivyo”

“Ila asante kwa maana una nifikisha hadi kilele cha kilimanjacho na huniachi njiani”

“Usijali”

“Una njaa nikupikie?”

“Kama ita wezekana”

“Twende chumbani kwa maana si kwa kukukaribisha huku”

Fatma akandaa chakula na kwa pamoja tukala na kwa pamoja tukaanza kula.

“Ni wanaume wangapi umewaleta hapa kwako?”

“Hakuna wewe ndio mtu wa kwanza na wa mwisho kuijua hii nyumba”

“Una uhakika?”

“Haki ya Mungu vile dini yangu muislam, siwezi kukuongopea Rashidi.”

“Sawa ehee nime ratiba ya matumizi ya hizo dola milioni mia zita tumia vipi”

“Lazima niunde timu ya kunisaidia kwenye kampeni. Lazima nita kuwa na kampeni meneja pamoja na wasaidizi wengine. Kuta kuwa na matangazo kwa njia ya mabango, redio, tv na sasa hivi dunia ina kwenda kasi sana tuta weza kwenye mitandao ya kijamii ambapo huko kuna watumiaji wengi sana. Ukiachana na huko kwenye kampeni. Kuna hapa kuharibu jina la huyu mzee aliye mchukua mke wako. Ni lazima tuunde kashfa kubwa itakayo mchafua hadi chama kimuone hana manaa na atupiliwe mbali”

“Kashfa ya mke wangu ina tosha?”

“Hiyo ni ya kawaida sana kwa maana hakuna ushahidi wowote juu ya hilo n ahata kama utakuwepo ushahidi, mwanamke akikukataa basi hakuna kitu. Ina bidi tupate kitu ambacho kitakuwa ni mwiba sana, mwiba utakapo mchoma ata kuwa hoi”

Nikaka kimya kwa muda ksha nikakumbuka jambo moja zuri na kujikuta nikitabasamu.

“Mbona una tabasamu”

“Una jua maadui wakiungana mara nyingi huwa wana huko nyuma walisha tendeana majanga. Sasa nina janga la huyu kenge ambalo huyo rafiki yake wa sasa alinisaidia”

“Jambo gani?”

“Nina picha za nguno za huyu mzee pamoja na mke wangu. Niliwaahidi kuziweka kwenye mtandao kipindi ni makamu wa raisi ila wakaniwahi kunipiga pin nikashindwa kuziweka sasa wakati wa kuzitumia umefika je hiyo sio sindano?”

Fatma akanipa mkono ikiwa ni ishara ya kunipongeza kwani kwa udhaifu huo wa kuchafuliwa kwenye mitandao kwa video na picha za ngono basi hakuna mwananchi hata mmoja atakaye muamini na kumpigia kura.



ENDELEA

“Hapo mshikaji wangu ume nena. Na tuna weza kutengeneza video ya wewe kutoa shutuma kwa huyo mzee na kuelezea maovu yote aliyo yafanya na watu anao shirikiana nao. Dunia ita kuamini na isitoshe bado ana endelea kuyawinda maisha yako”

“Umeona ehee”

“Ndio siasa mbona kitu kirahisi, usione hawa viongozi wana ongoza ongoza, nao wana watu wao wana waogopa ambao ukiwazingua tu wana wadondosha chini”

“Etie ehee?”

“Ndio mambo ya siasa hayo mpenzi wangu. Wewe iandae hiyo video”

“Alafu mdogo wake aniliambia kuna watu alisha wahi kuwafanyia mabaya tukiwapata kama kumi na wakitoa ushahidi juu yake basi kila kitu kita kuwa kime muangukia?”

“Yule Caro?”

“Ndio”

“Una mfahamu kumbe?”

“Sio kumfahamu tu ana mimba yangu”

“Mamae walai mwanaume wewe. Hahaaaaaa”

“Yaa sitaku kukuficha kwa maana sihitaji maisha ya aina hiyo?”

“Aisee kumbe umetugonga wengi ehee, alafu sote sisi watatu ni marafiki hususani mimi na yeye”

“Dooo ndio hivyo”

“Sawa, hiyo sio ishu kwa maana kila mmoja ata jiachia kwa wakati wake. Na mimi sijui nikubebee mimba?”

“Kama una taka kuuwawa na mumeo beba mimba, hato jali ni raisi au laaa”

“Haaa nakutania, kwa hapa nilipo fika sihitaji kufunga funga pampas za watoto”

“Kwani una watoto wangapi?”

“Watatu, wote wapo Uingereza wana soma, wamepisha miaka miwili miwili ndio maana una niona ni mrembo kwa maana nilizaa fasta fasta sasa hivi nina somesha.”

“Hongera sana”

“Nashukuru. Hivyo mpenzi hatuna muda wa kusubiri ina bidi hili swala la inabidi tulishuhulikie haraka iwezekanavyo”

“Sawa deal done”

Nafurahi kufanya kazi na wewe kwa maana ni muelewa na una jua nini nafanya”

Tukaoga pomoja kisha tukaondoka nyumbani hapa na nikamuomba Fatma anipitishe kwenye hoteli alipo Leticia kisha yeye akaondoka. Nikapandisha hadi gorofa ya sita kilipo chumba cha Leticia. Nikaminya kengele ya mlangoni mwake.

“Nani?”

“Mimi”

Leticia akafungua na nikaingia ndani.

“Aisee nchi yenu ina joto sana”

“Pole ndio Dar es Salaam ila sio nchi nzima kwa ni kuna maeneo yana baridi kali kuliko hata Brazil”

“Mmmm kweli?”

“Ndio Kilimanjaro huko na maeneo mengine mengi. Vipi toka ume fika ume toka?”

“Hapana, sijazunguka”

“Sasa kuna jambo nahitaji unishauri”

“Jambo gani?”

Nikamueleza Leticia mpamgo mzima nilio zungumza na Fatma.

“Mmmm dola milioni mia moja ni nyingi sana hata Marekani sidhani wagombea uraisi wake wana ttumia kiasi hicho kikubwa cha pesa. Na jambo jengine usiwaamini wana siasa kwa maana wote ni waongo”

“Kwa hiyo tusiende na plan hiyo twende na plan ya kuwaangamiza DON na huyu panya mwenzie?”

“Sijasema usitishe plan hiyo ila ina bidi ungalie mpenzi wangu kwa maana dola milioni mia ni kiasi kikubwa sana cha pesa kwa maana ni utajiri wa mtu na mwenine hajaufikia, na isitoshe hiyo pesa kwa pesa a hapa Tanzania ni nyinngi sana tena sana. Cha kufanya wewe simamia jinsi ya matakwa ya pesa hizo zinavyo hitajika na kutimia. Usitoe pesa kwa sababu unayo na umeipata kwa uraisi. Ila ikiisha je ita kuwaje, ikiwa wewe ni baba ambaye una hitaji kuwaachia wanao urithi na pia una hitaji kujijenga kiuchumi kwa maana pesa inayo kaa tu bila kujizalisha na ina inatoka tu, ni mbaya sana”

“Nimekuelewa mpenzi wangu”

“Kwa hiyo hatuna haja ya kumsaka DON?”

“Ina bidi tuwe na plan mbili, hii ya kisiasa mimi na wewe ytuendelee kuiangalia kama ilivyo ila ikibuma sisi tuna itekeleza yetu na huyu anaye chukua pesa yangu akinizingua hato kuwa na bahati kwani ata kufa.”

“Sawa baba wewe ndio mwenye maamuzi na wewe ndio unaye jua namna gani una weza kumuongoza huyo raisi wako”

“Vipi vyakula havijakupa shida?”

“Hapana havijanipa shida kabisa. Nipo sawa kabisa na nivitamu sana”

“Sawa nilipita kukujulia hali yako kwa sasa kuna sehemu nina elekea”

“Poa mpenzi hujapata simu kwa maana kuna wakati nita tamani kukupigia ila nita kukosa hewani.”

“Nikinunua nita kujilisha”

“Sawa”

Nikaondoka hotelini hapa na kurudi nyumbani kwangu kwa usafiri wa bodaboda.

“Una onekana una furaha uso wa huzuni wote umekwisha, kuna mpya gani huko?”

Shabani alinizungumza huku tukipeana tano.

Naye nikamshikisha nililo ongea na Fatma.

“Mmmmm dola milioni mia aisee hapana ni pesa nyingi sana hiyo”

“Ngoja tuone”

“Sio tuone Rashidi, hiyo pesa una nunua mji aisee na una kuwa na mji wako, hembu jaribu kufikiria upya juu ya hiyo pesa kwa maana ina tusaidia kujenga hata hoteli nne zenye hadithi ya nyota tano”

“Sawa nita likifikiria”

“Ila ana nguvu hiyo ya kuwa raisi au ana taka kukutumia kama daraja kufika malengo yake?”

“Ahaa lengo langu ni kumuondoa DON kabisa kwenye hii dunia na kuipoteza nguvu yake?”

“Sasa mtu kama Don hawezi kuwekeza nguvu yake Tanzania. Kuna maeneo ya kumbana kama uliniambia muliweza kwenda Mexco na kudili na kundi lake huko ndipo kwenye nguvu yake ya kiuchumia Rashidi. Ila hizi siasa za hapa bongo ni ubabaishaji mtupu. Mimi ni ndugu yako na nita kueleza ukweli kwenye kila jambo, huyu demu amejua una pesa hivyo ana taka kuzichukua kirahisi kaka. Hakuna mfanyabiashara yoyote duniani wala mtu yoyote duniani umuombe hicho kiasi hicho cha pesa kirahisi rahisi alafu hakuna return y ahata shilingi mia hapana kaka. Kumbuka hiyo ni dola milioni mia moja sio buku wala shilingi milioni mia ya Kitazania”

Rashidhi alizungumza kwa msisitizo.

“Una nishaurije sasa?”

“Cha kukushauri ni kwamba huyu mama, wewe msaidie kufikia hapo anapo taka, ila usimpe dolar milioni mia. Cha kumueleza yeye ajaribu kupanga finance budget yake ailete mezeni tuta kuwa na muhasibu ata ipitia akiipitisha ita pita. Kaka hiyo pesa uliyo ipata kwa DON sio kama hujaitolea jasho, umeitiolea jasho kwa mapambamo ya ulingoni uliyo kuwa una pigana ndugu yangu ukiyaweka rehani maisha yako, ndio maana umeipata sasa hivi. Hivyo usitake jasho lako lipotee kirahisi namna hiyo”

“Nashukuru sana ndugu yangu kwa ushauri wako”

“Ni jukumu langu kukueleza ukweli kwa maana kama una mapesa haya yote una kata tamaa je ukiwa kapuku, kajamba nani una dhani uta kuwaje si utajirusha gorofani ufe”

“Hahaaahaa”

“Usicheke kaka, hawa wanawake ni nyoka. Ungekuwa kapuku asinge kupa kum** yule. Ila ameona una pesa ndio maana amekuja na mipango yake ya ajabu ajabu”

“Ila hilo la kuwa raisi mimi ndio nimemshauri?”

“Kaka hawa watu wana akili wanapo anzisha mada wana jifanya kama vile wana jitoa na hawataki kuwa wao ila ukwagusia tu kidogo wana jaa.”

“Na wewe ni mwanasiasa nini?”

“Kaka shida zinapo zidi una fanya chochote ili watoto wale. Nimeingia huko kwenye mavyama vyama yao hivyo najua sana mbinu zao. Washenzi hao wee acha tu”

Nikajikuta nikicheka kwa sauti ya juu kwa maana Shabani ana onekana hajafurahishwa na hili jambo kabisa.

“Poa kaka ina bidi nifikirie”

“Na usisahau Tina ni mjamzito, Caro ni mjamzito, sijui huko kwa wengine ambao hujaniambia kama hujajaza mimba nyingine. Hao wote wana hitaji urithi, ohoo maisha mafupi haya kaka”

“Poa poa ndugu yangu ngoja nikapumzike kwa maana muda umekwenda”

“Poa ndugu yangu usiku mwema”


“Nawe pia?”

Nikapitiliza hadi chumbani kwangu na nikajitupa kitandani, hazikupita hata dakika tano usingizi mzito ukanipitia. Asubuhi na mapema nikaamka, nikamtazama Tina aliye lala pembeni yangu, nikajiangalia mwili wangu na kuonan nikiwa sina nguo hata moja kwani wakati nina lala nililala na nguo pamoja na viatu vyangu. Nikaingia bafuni nakuanza kuoga huku kichwa change kikiwaza mambo mengi sana ambayo ina bidi niyafanye.

‘Kwani mafunzo niliyo yapata Beirut mbona siyatumii?’

Nilijiuliza swali huku maji ya bomba hili la mvua yakiendelea kunimwagikia mwilini mwangu.

‘Nilifundishwa kuwa jeshi la mtu mmoja, sasa ina kuwaje nina kuwa mzembe hivi. Kama ningekuwa sina hii pesa inge kuwaje juu ya hawa watu?’

‘Huyu mzee hata akitakiwa kurudi madarakani akiuwawa wata sema watu walio kuwa wameipindua serikali wameamua kumuondoa tu?’

‘Ndio, hii ni nafasi aisee, siwezi kuiachia. Siasa ina matokeo mawili, kushinda na kushindwa, sijawahi kuona droo ya siasa na hata ikitokea ni lazima mmoja ashindwe.’

‘Nimepata wazo’

Nikamaliza kuoga na nikatoka bafuni, nikavaa haraka haraka na nikatoka nje.

“Mwanangu”

Mama Chausiku aliniita akiwa jikoni.

“Mama umeamka?”

“Ndio mwanangu una endeleaje?”

“Salama shikamoo”

“Marahaba, pole bwana jana sikukusalimia”

“Usijali najua ulikuwa na mambo mengi sana. Vipi mkono umefanyaje?”

“Ahaa niliumia kidogo nilipo kuwa safari”

“Ahaa sawa baadae mchana mama yako ana kuja pamoja na mke wako. Wana kuja msibani”

“Mungu wangu, mke wangu gani?”

“Si mzungu?”

“Kwa nini hawajaniambia?”

Walikutafuta hewani wakakukosa, na nilizungumza nao kuhusiana na msiba wakasema wata ondoka hivyo hadi saa nane wata kuwa hapa. Wanakuja na wajukuu zangu wote”

“Ohoo sasa huyu Tina ina kuwaje?”

“Na nilisha zungumza naye na kumueleza kwamba mke wako ana kuja na amenielewa”

Nikajikuta nikishusha pumzi kwa maana mziko wa Jackline nina ujua vizuri.

“Ume sema saa ngapi wana kuja?”

“Saa nane mchana, hivyo saa saba ina bidi niwe uwanja wa ndege. Ikiwezekana twende wote kuwapokea”

“Sawa ngoja nina mizunguko kaza akisha nitawahi kurudi, kama ita shindikana nao…..”

“Hakuna cha kushindikana Rashidi. Yule ni mama yako na mke wako wa ndoa, kwa nini una ona kama ni watu baki tu?”

“Sija maanisha hivyo mama”

“Ila umemaanisha nini?”

“Sawa mama tuta kwenda wote”

“Sawa, nina andaa chai”

“Nita kuja kunywa. Shabani ameamka?”

“Hapana, kwa maana mimi leo ndio wa kwanza kuamka”

“Nahitaji funguo ya gari hiyo BMW”

“Mama Shikamoo”

Nilisikia sauti ya Fatma nyuma yangu.

“Marahaba mwanangu umemkaje?”

“Nimeamka salama mama. Za asuhuhi shem”

“Salama za wewe?”

“Fatma huyu ni mdogo wako sio shemeji yako.”

“Ohoo”

“Ndio”

“Samahani Fatma naomba tuzungumze mara moja”

Nilizungumza huku nikitangulia kutoka nje kwa maana mama Fatuma ana hitaji kuanzisha mada nyingi nyingi. Tukasimama nje nikatazama mazingira kama yana ruhusu kuzungumza hichi ninacho taka kumueleza.

“Umeniambia ulikuwa ni mwanajeshi?”

“Ndio, huniamini?”

“No sio ishu ya kukuamini. Mimi nina shida ya bunduki”

“Ya kazi gani?”

“Nahitaji kuingia mzigoni kuifanya kazi yangu. Huyu mzee siwezi kumuacha hai, ni lazima nimuue kwa mkono wangu ili iwe njia rahisi sana kwa wewe kuingia ikulu. Kwani hata ukimuangusha kumbuka ana uchu wa madaraka ata watu wenye nguvu wata mfadhili na hapa tutakuwa tuna cheza maswala ya kidalipo, yatakuwa ni mambo ya kuongoza kwa wiki wiki muna pinduana”

“Ila Rashidi kweli una weza kuifanya hiyo kazi?”

“Nisikilize wewe ni mwanajeshi, ila mimi ni zaidi ya mwanajeshi, nimepita mafunzo yote na hapa unapo niona nime kamilika. Nina weza kuoendesha mission ya kwangu mimi peke yangu na ikafanikiwa.”

“Mmmmm hilo sijawahi kulijua?”

“Huwezi kulijua kwa maana hata uki google huwezi ona”

“Hahaaa sawa niambie una hitaji bunduki gani na nita hitaji unidhibitishie kwamba wewe ni mkali kwa kutumia hizo bunduki.”

“Usijali, nahitaji M4 Carbine moja pamoja na Beratta m9 pistol”

“Zina patikana”

“Pia nitahitaji na bunduki nyingine ya ziada”

“Bunduki gani?”

“McMillan TAC-50”

“Duu kwa kuongea hivyo ona onekana wewe sio mwenzangu kabisa”

“Nisaidie hizo”

“Sawa kuna mshkaji wangu, yupo Bagamoyo, acha niwasiline naye ikiwezekana twende sasa hivi”

“Fanya hivyo basi”

“Basi ngoja nimpigie na nibadilishe nguo si una ona nimevaa mavazi ya kulalia haya”

“Poa”

Fatma akaingia ndani na baada ya dakika kumi akatoka akiwa amevalia suruali pamoja na tisheti huku chini akiwa amevaa raba. Akanirushia funguoa, tukaingia ndani ya gari lake na kuondoka nyumbani hapa.

“Jamaa yupo”

“Yeye ni nani?”

“Ahaa yeye ni mtaalamu wa hizo silaha. Ni mzee mtu mzima amezeeka hivyo amenunua ranch yake kubwa huko Bagamoyo anaishi mwenyewe”

“Sawa”

Tukaendelea na safari hii hadi tukafanikiwa kufika katika eneo la mzee huyu ambalo limejitenga kabisa na makazi ya watu. Tukapokelewa na mzee huyu mwenye kipara cha uwaraza. Fatma akanitambulisha kwake.

“Nahitaji kumuona kama ana weza kuzitumia tusije tukawa tunampa silaha kubwa mwanafunzi”

Fatma alizungumza huku akitabasamu.

“Kwa hiyo nimpeleke kiwacha cha mazoezi?”

“Ndio”

Tukaingia katika gari aina ya Jeep ya mzee huyu na tukaelekea eneo lenye uwanja mkubwa sana.

“Hapa ndipo ninapo fundishia watu kutumia silaha. Tuna anza na bunduki gani hapa kijana?”

Mzee alizungumza huku akinitazmaa machoni mwangu.

“Zote”

Nilizungumza huku nikichukua M4 Carbine, nikatoa magazine na kuikuta ikiwa imejaa risasi, bastola nikaichomeka kiunoni mwangu huku McMillan TAC-50 nikivaa mkanda wake na ikaning’inia mgononi.

“Nita kuwa nina simamisha target moja baada ya nyingine ili uwe una lenga. Sawa”

Mzee alizungumza na nikamjibu kwa kutimia kidole ngumba nikimaanisha sawa. Akaanza kusimamisha vibao maalumu ambavyo vimekaaa kama watu walio shika bunduki huku vingine vikiwa na duara na nina paswa kulenga katikati. Kwa kasi ya ajabu nikaanza kuwaonyesha uwezo wangu wa kutumia bunduki huzi kwa kumshambulia adui yangu. Risasi katika M4 Carbine zikaisha nikahamia katika bastola nikamaliza risasi zake kisha nikatumia McMillan TAC-50, kudungua vibao vilivyopo mbali sana hadi nina maliaza Fatma na mzee huyu wanapiga makofi kwani ndani ya muda mfupi sana nimeweza kushambulia vibao hivi na hakuna risasi hata moja iliyo anguka au kupiga pembeni ya target niliyo wekewa.



“Kwa kipindi kirefu sana sijawahi kuona mtu mwenye uwezo kama wako. Umejifunzia wapi?”

Mzee huyu aliniuliza huku akinitazama machoni mwangu. Nikashusha pumzi nyingi huku nikitazama tagert nilizo zilenga.

“Ni mafunzo yangu binafsi”

“Una taka kuniambia ulijifunza mwenyewe?”

“Ndio kwa maana wapo wanao fundishwa ila hawawi kama mimi. Hivyo kasi ya mtu hutegemea na jitihada zake, mwalimu ata atakuambia wapi kwa kulenga ila si kukusaidia kulenga”

“Aisee wewe kiboko, nimehesabu saa yangu hapa umetumia dakika moja na sekunde ishirini”

Fatma alizungumza huku akinitazama

“Weee”

“Ndio nilikuwa nina tazama saa yangu ya mkononi hapa”

“Kazi nzuri sana kijana. Wewe ni hazina ya taifa hili endapo uta tumika vizuri basi uta kuwa ni miongoni mwa vjana wa usalama hatari sana”

“Nashukuru mzee”

Tukarudi nyumbani kwa mzee huyu, nikamlipa kiasi cha pesa alicho niuizia cha bunduki hizi pamoja risasi kisha tukaondoka na kuianza safari ya kurudi mjini.

“Una uhakika una weza kumuua raisi?”

“Kwa nini una uliza?”

“Kwa maana naona mpango wako ume badikika haraka sana?”

“Uwezo huo ninao na wewe kaa usubirie uone”

“Sawa”

“Umefikia wapi kwenye maswala ya kiushawishi kwenye chama chako?”

“Aha..naendelea vizuri na wazo langu nimesha lipenyeza kwa baadhi ya viongozi wa chama na wana ona nina faa. Ila wana hitaji pesa kidogo ili kuzidi kuwaweka sawa, si una jua siasa bwana na pesa ni kama kurwa na doto”

“Sawa nimekuelewa. Leo mke wangu na mama yangu wana kuja?”

“Wapi hao?”

“Mke wangu wa ndoa kabisa anakuja”

“Waooo nitafurahi kumuona”

“Eti ehee?”

“Yaa nita rufahi kumuona mke wako wa ndoa”

Tukafika nyumbani kwangu, nikakutana na Shabani akiwa anaingia katika gari.

“Silaha zangu nina omba unitunzie”

“Sawa”

Nikashuka katika gari hili la Fatma na kuingia katika gari la alilo panda Shabani.

“Niambie ndugu yangu”

“Salama aise, kutokuwa kwako na simu kuna weza kukukosesha habari za haraka”

“Kweli aisee kuna mpya gani?”

“Mama aliniambia jana usiku kwamba mke wako na mama wana kuja leo. Sasa nikashindwa kukupatia habari kwa maana tayari ulisha ingia chumbani kulala”

“Mama Chau aliniambia asubuhi hii yaani hapa hata sielewi ita kuwaje kwa mwanamke huyu Tina”

“Ila ameniambia kwamba tayari alisha mpanga Tina na uzuri Tina ulisha mueleaza juu ya hali yako kwamba una mke. Vipi umezungumza na Tina?”

“Bado”

“Ongea naye kudhibitisha kwamba atatulia akimuona mke wako kwani asije akaanza kuleta mawenge na mwisho wa siku ukajikuta ukipoteza bara na pwani”

“Ngoja nikaongee naye. Una elekea wapi?”

“Naelekea kwenye ile ofisi yetu ya mabasi mafundi wana itengeneza kwa mfumo ambao nilihitaji uwe.”

“Nisubirie twende pamoja”

“Sawa kaka”

Nikashuka ndani ya gari na nikaingia ndani, nikasalimia na Chausiku, shemeni pamoja na Tina kisha nikakamuita Tina chumbani kwa ajili ya sisi kuzungumza.

“Ulienda wapi mume wangu?”

“Bagamoyo kuna vitu nilikwenda kununua na Fatma”

“Sawa. Najua una wasiwasi kusikia kwamba mke wako ana kuja”

Tina aliwahi kuizungumzia mada hii.

“Usijali, kuwa na amani mume wangu, mimi wala sina tatizo kwenye hilo. Nita wapisha chumba hadi pale atakapo amua kuondoka”

Tina alizungumza kwa sauti ya unyonge na iliyo jaa huzuni kubwa. Kwa saikolojia ndogo tu ana onyesha dhairi kwamba hajafurahishwa na ujio wa mke wangu.

“Umeridhika?”

“Ndio nimeridhika kwa maana siwezi kubadilisha ukweli kwamba wewe ni mume wa mtu na una familia yako”

“Sawa nimekuelewa?”

“Ila nakuomba jambo moja Rashidi”

“Jambo gani?”

“Tafadhali nina kuomba sana uwe unanipatia haki zangu za kimsingi kama mwanamke wako. Aisije akaja mke wako ndio ukanitelekeza kabisa na kuniacha na kuto kunijali kabisa”

“Usijali kwa hilo”

“Kama yakinishinda nita kwenda kuishi Tanga kwenye ile nyumba”

“Nani ata kuangualia?”

“Mama yangu ata kuja”

“Alafua nakumbula nilikuambia kwamba unitambulishe kwa wazazi wako sijui iliishia wapi?”

“Rashidi sikukukatalia ila ubize wako na mambo yako mengi ndio maana hadi leo hatujafanya chochote”

“Sawa tuta panga. Sasa hivi kuna sehemu nahitaji kwenda baadae”

“Umekunywa chai sasa?”

“Chai nita kunywa”

“Sawa mimi ngoja nitoe nguo zangu nita kuwa nina lala chumbani kwa Chausiku”

“Sawa”

Tina akanisogelea, akaninyonya denda kidogo kisha akaniachia.

“Naamini nita kuwa nina miss sana fujo zako za kitandani”

“Usijali mke wangu, kila jambo litakwenda vizuri”

“Sawa”

Nikatoka ndani hapa.

“Rashidi Rashidi”

Chausiku aliniita huku akinifwata nje.

“Niambie”

“Upo bize sana?”

“Yaani wee acha, vipi hali yako?”

“Namshukuru Mungu sasa hivi nipo vizuri. Nina mazungumzo kidogo na wewe sijui una muda?”

“Mmmm ya nina dakika chache tuongee”

“Twende tukakae pale kibandani nisije nikaanguka kwani bado sipo sawa sawa”

Tukaka kwenye kibanda cha kupumzikia.

“Ehee niambie mpenzi”

“Aha Fatma aliniambia kwamba una taka kumsaidia awe raisi ni kweli?”

“Alinishirikisha kwenye wazo la yeye kuwa raisi, nikamuambia nita mpa support”

“Kabla ya kumsaidia mtu niulize kwanza mimi”

“Una maanisha nini?”

“Yule ni rafiki yangu, dada yangu, siri yake siri yangu. Ila kwenye hiyo nafasi ya uraisi sidhani kama ana weza kufiti”

“Unataka kuniambia hana sifa au vigezo vya yeye kuwa raisi?”

“Hana”

“Ehee hayo nayo mapya. Au una muonea wivu?”

“Simuonei wivu ila jua tu hana sifa hizo”

“Niambie kwa nini?”

“Wewe chunguza kabla ya kumsaidia, utakapo pata mwanga wa kujua kwa nini hana uta niambia ulicho kiona. Ila kwasasa siwezi kukuambia hadi ujionee wewe mwenyewe”

“Mmmm sawa mpenzi”

“Ni hili tu kwa sababu wewe nimekujua toka nikiwa mdogo nay eye nime nikiwa nimesha balehe na mavuz** yangu hivyo kati yenu mmoja wenu akiharibikiwa nitakaye umia sana ni wewe kwa maana upo moyoni mwangu na nina kujua”

“Nashukuru ila ningependa kujua japo jambo moja tu juu ya Fatma”

“Ni msaliti na kigeugeu. Mtu wa aina hiyo sio wa kuwekeza kwake kwa maana ikitokea mwengine ana uwezo wa kumfanyia makubwa zaidi yako ana weza kukuacha kwenye mataa. Wewe chunguza kabla ya kufanya maamuzi yako binafsi.”

“Sawa asante”

“Poa nasikia wifi yangu leo ana kuja?”

“Ya mama amenieleza kwamba ana kuja”

“Namshubiria kumuona kwa hamu mzungu wetu na vitoto vyetu”

“Hhaahaa haya bwana”

Nikanyanyuka na moja kwa moja nikaeleka katika gari na nikaondoka nyumbani hapa.

“Mbona una mawazo sana?”

Shabani aliniuliza mara baada ya kuniona nikiwa nimekaa kimya sana.

“Kichwa kina mambo mengi tu. Tupitie duka la simu”

“Sawa, ulienda wapi na yule demu?”

“Bagamoyo, kuna bunduki nilikwenda kuzinunua kwa ajili ya kazi ya kumuwinda raisi pamoja na DON.”

“Una muamini sana Fatma ehee?”

“Kwa nini?”

“Demu yule nikimtazama naona kama simuelewi elewi. Naona kama ni machepelele fulani ambaye sidhani kama una paswa kumshirikisha kwenye ishu kubwa kama hizo?”

“Ahaa ngoja tuone”

“Kaka nikuulize swali?”

“Niulize?”

“Ni muda gani umejuana na Fatma?”

“Nimejuana naye ile siku ambayo nilimpeleka Chausiku Dodoma kuchukua wanaye na siku ile ile nikamla mzigo”

“Hembu nakuomba uweze kumuondoa kwenye mipango yako ndugu yangu. Ana weza kukuletea madhara makubwa sana”

“Usija nitafanya hivyo ndugu”

“Fanya hivyo kaka, kwa maana naona ana kuja kwa kasi sana ambayo mwisho wa siku isije ikatuletea madhara”

“Nimekuelewa”

Tukafika katika duka moja la simu.

“Karibu tajiri”

Muuza duka alizungumza kwa furaha huku wakipeana mikono na Shabani.

“Salama sana ndugu yangu nianimbie”

“Fresh tu ndugu, yangu nimeleta mzigo mpya na asubuhi hii ndio nimeufungua”

“Aisee hambu nitazamie simu moja kali sana. Chidi wewe ni mpenzi wa simu gani?”

“Samsung?”

“Sio iphone?”

“Iphone ni za wadada na wanamama, ila Samsung ni simu za wanaume?”

“Wewe ni mtu wa tatu nina kusikia ukizungumza hivyo boss. Una hitaji note au S?”

“10 Plus”

Nikanunua simu hii kisha tukaondoka eneo hili, tukapita kwa wakala na nikasajili line kwa kutumia kitambulisho cha Shabani.

“Nahitaji nikutambulishe kwa demu wangu mmoja hivi anaitwa Leticia”

“Mwengine?”

“Yaa huyo ni Mbrazi”

“Ndio huyo uliye kuwa naye huko Brazil?”

“Ndio”

“Aisee kazi kweli kweli. Ila kumbuka mke wako ana kuja leo?”

“Nakumbuka ila huyo hana tatizo”

“Sawa”

Tukafika hotelini alipo Leticia. Akatukaribisha chumbani kwake. Nikamtambulisha Shabani kwake.

“Nashukuru kukufahamu shemeji”

“Nawe pia Shabani nafurahi kukufahamu. Ahaa Baby afadhali umekuja”

“Ehehe niambie?”

“Leo saa nane mchana raisin a familia yake wana kuja uwanja wa taifa na watapokelewa kwa mapokezi ya heshima sana”

“Duuu”

Nikatazamana na Shabani machoni mwake.

“Mbona muna tazamana kuna nini?”

“Leo hii mama yangu mzazi, wajukuu zake na mkwe wake wana kuja majira hayo ya saa nane wakitokea nchini Ufaransa”

“Sawa ila ujio wao hauwezi kuvuruga mpango nilio nao. Kwani raisi ana kuja na kupokelewa na waziri mkuu kisha yeye na mke wake wata kuwa kwenye gari la wazi. Watapita mitaani na kuwapungia wananchi mikono kwa kumkaribisha tena nyumbani. Nina ona hii iwe ndio nafasi ya kumdungua akiwa ndani ya gari lake la wazi”

“Aiise kama vile ulikuwa kwenye mawazo yangu. Nilikuwa nimepanga kabisa kumuua raisi akiingia tu Tanzania sema sikuwa na full detail za safari yake”

“Ndio hivyo tuna masaa manne ya kujiandaa.”

“Silaha unayo sasa?”

Leticia akavuta brufcase iliyopo chini ya kitanda. Akaifungua na nikaona bunduki iliyo tengenishwa tenganishwa vifaa vyake.

“Nimejiandaa kwa kila kitu”

“Umeitoa wapi hii?”

“Nilisha kuambia nime wekeza kwa watu Rashidi. Hivyo ninapo kuwa sehemu ninapo hitaji kufanya kazi basi kazi yangu nina itekeleza kwa umakini na uhodari wa hali ya juu”

“Ndio maana nakupenda. Shabani, nenda nyumbani muambie Fatma akupatie mizigo yangu uniletee hapa hotelini”

“Mpigie simu kwa maana ana mambo mengi, kama unavyo jua mimi na yeye kama damu zimepishana hivi”

“Sasa simu mpya hii sina namba yake”

“Ngoja nimpigie Chausiku”

Shabani akampigia simu Chausiku kisha akanikadhi simu hii.

“Chau ni mimi”

“Niambie Rashidi”

“Fatma yupo?”

“Yaa tena ana taka kutoka”

“Mpatie simu”

“Dakika moja ngoja nimfwate juu”

Nikasubiria kwa sekunde kadhaa kisha nikasikia sauti ya Fatma.

“Ni mimi”

“Niambie Rashidi”

“Safi, namuagiza Shabani nipatie ule mzigo wangu”

“Upo mbali sana?”

“Sio mbali sana ila mpatie mzigo”

“Sawa nina msubiria”

“Poa”

Nikakata simu na Shabani akaondoka hotelini hapa. Leticia akaanza kunionyesha ramani ya eneo ambalo msafara wa raisi una pita.

“Najua kifo chake kita washangaza wengi sana ila hatuna jinsi ni lazima tumuue”

“Nimekuelewa”

Leticia akanivuta tisheni na kuninyonya denda la kibabe.

“Nahitaji uni tomb** kama vile huto nitomb** tena kwani baada ya tukio hili leo. Mimi na wewe hatuto onana kwa kipindi kirefu kupisha uchanguzi wa tukio lifanyike. Hivyo tuagane kabisa hapa kitandani”

Leticia mara baada ya kuzungumza maneno hayo akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine kuhakikisha mtanange huu wa leo una kuwa ni wa kukata na shoka.




Kila mmoja akafanya kadri ya uwezo wake kuhakikisha tuna ridhishana. Hadi tuna maliza mtanange huu, Leticia akanikumbatia kwa nguvu sana huku akishusha pumzi nyingi.

“Rashidi nina kupenda sana”

Leticia alizungumza kwa sauti ya upole na laini sana.

“Nakupenda pia mke wangu”

Taratibu akaniachia huku akinitazama usoni mwangu.

“Najua siwezi kuwa mke wako. Ila kwa hichi ambacho umeniachia kitakua ukumbosho kwenye maisha yangu pale nitakapo maliza hii mission yangu”

Leticia alizungumza huku akinitazama machoni mwangu.

“Kipi nilicho kuachia?”

“Ujauzito wako”

“Unataka kuniambia ume nasa?”

“Mimi ni mwanamke na mayai yangu hayana shida yoyote hivyo kushika mimba sio sio jambo la gumu kwenye maisha yangu”

“Kama una mtoto wangu nina kuomba hii kazi niifanye mimi mwenyewe?”

“Rashidi, nimesha andaa mazingira ya kazi hii hivyo acha niikamilishe”

“Mimi pia nina taka kuifanya?”

“Hapana Rashidi. Wewe nenda kaipokee familia yako ili kuepusha kustukiwa. Hakikisha familia yako ina kuwa salama”

“Nahitaji ukisha fanya hii kazi una kwenda wapi?”

“Nita potea kwa muda hadi nikijifungua ndio nita kutafuta”

“Una hitaji nikuingizie kiasi gani kitakacho kusaidia kwenye kipindi utakacho kuwa mwenyewe?”

“Chochote utakacho kiona kina faa”

Mlango ukagongwa ikatibidi kujifunga mataulo.

“Nani?”

“Mimi”

Tulisikia sauti ya Shabani. Nikafungua mlango na Shabani akaingia nadani hapa.

“Ohoo nimejuja wakati mbaya?”

“Hapana niambie”

“Mzigo upo kwenye gari, nimeshindwa kupanda nao”

“Shukrani ndugu yangu katusubirie ndani ya gari”

“Poa”

Shabani akatoka ndani hapa. Tukaingia bafuni na kuoga, baada ya kumaliza, nikavaa nguo zangu huku Leticia naye akivaa suruali yeusi, shati jeupe. Kisha akavalia baibui na akajifunga ninja.

“Umekuwa muarabu sasa?”

“Yaa”

Baada ya kila mtu kujiandaa Leticia akabeba kila kilicho chake ndani ya chumba hichi kisha tukatoka. Tukakabidhi funguo mapokezi na kuondoka.

“Ukisha fanya tukio una elekea wapi?”

“Kuna gari ina nisubiria sehemu, na nitaelekea hadi baharini na kupanda boti itakayo nipeleka moja kwa moja eneo ambalo nitakuta ndege zile zinazo tua ndani ya maji na nitaondoka zangu Tanzania mazima”

“Umejipanga?”

“Kwa sababu najua hili litakuwa ni msaada mkubwa sana kwako”

“Sawa mke wangu”

Leticia akatuelekea hadi sehemu ambayo ana hitaji tumepeleke.

“Sijakuingizia bado pesa”

“Niingizie”

Leticia akanitajia namba za akaunti yake, nikamuingizia kiasi cha dola milioni moja.

“Shukrani mume wangu. Shemeji tuta onana pajapo makaliwa ya Mungu”

“Amen”

Tukanyanyona denda na Leticia kisha akashuka ndani ya gari pamoja na mabegi yake. Tukamshuhudia akiingia kwenye moja ya gari lililo kuwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara na akaondoka eneo hili huku akielekea barabara ya kushoto kwetu.

“Huyu demu mafia kweli”

Nilizungumza huku nikilitazama jinsi gari hilo likikunja kona nyingine.

“Kwa nini?”

“Hataki niifanye kazi kumuua raisi kwa sababu ana hitaji kuifanya yeye mwenyewe”

“Una muamini ana weza kuifanya?”

“Ndio nina muamini”

“Basi muache aifanye sisi tuwe mashuhuda”

“Yaa ngoja tuone”

“Hizi silaha nazo ina kuwaje?”

“Turuidi tu nyumbani, muda wa kwenda kuwapokea wageni basi tuta kwenda”

“Sawa sawa”

Tukarudi nyumbani, bunduki hizi nikazihifadhi kwenye chumba cha siri ambacho kipo chini ya ardhi na chumba hichi ni mimi na Shabani pekee ndio tuna kifahamu.

“Nilikuwa nina watafuta sana”

Chausiku alizungumza huku akitutazama mimi na Shabani.

“Kuna nini?”

“Tusaidiane jamani kwenye kuandaa maandalizi ya kuwapokea wageni?”

“Ehee”

Shabani aliguna kidogo.

“Kwani si wana kuja msibani jamani au kuna haja ya kupamba nyumba?”

Nilimuuliza Chausiku.

“Ni wazo la mama yako mkwe hilo”

“Aaha wana kuja sio watu wanao taka mambo mengi. Kikubwa andaeni chakula kizuri basi”

“Wana kula chakula cha asili kama ugali?”

“Kwa Jackline ana kula ila sijajua kwa wanaye kama wamewazoesha chakula hicho”

“Sawa”

“Mama kwani yupo wapi?”

“Jikoni”

“Sawa nina kuja kumuona”

Chausiku akaondoka.

“Kaka ubadili hayo mavazi”

“Kwa nini?”

“Kama mke wako ana ijua harufu yako, basi akikukuta na hayo mavazi ata jua dhahiri kwamba ume toka kuchepuka”

“Sawa ndugu yangu”

Nikaingia jikoni na kukuta wamama wakishuhulika na maandalizi ya mapishi.

“Mama nakuomba”

Tukasogea hadi sebleni.

“Nasikia kuna maandalizi makubwa?”

“Ndio mwanangu, kumbuka mkwe wangu ana kuja”

“Ila mama sioni haja ya haya mambo yote. Kumbuka wanao kuja ni wana familia isitoshe wana kuja msibani”

“Najua ila ukaribu kwa mgeni Tanzania sisi ni jambo la kawaida sana. Hivyo wewe jiweke tayari muda wa kwenda kuwapokea wageni utakapo fika basi tuna kwenda kuwapokea”

“Sawa sawa”

“Rashidi tuna weza kuzungumza?”

Tina alizungumza huku akinitazama.

“Ndio”

Tina akatangulia kutoka nje kwa ajili ya sisi kuzungumza.

“Niambie”

“Rashidi mimi nina omba niweze kuondoka kwa kweli. Sina ujasiri wala moyo wa kuweza kumuona mke mwenzangu. Najua una weza kuchukulia kirahisi sana hili jambo ila kusema kweli lina niumiza na hii hali yangu nina weza kujikuta nina fanya vituv ya ajabu ambavyo uta vichukia huko mbeleni. Tafadhali nina kuomba sana uniruhusu niondoke”

“Ila Tina kumbuka hali yangu ina hitaji uangalizi wa karibu sana”

“Najua Rashidi, nita ajiri hata mtu au nita ishi na mama yangu. Nina kwenda Tanga utakapo kuwa una hitaji kuzungumza na mimi basi uta kuja”

Tina alizungumza kwa sauti ya upole huku akinitazama machoni mwangu.

“Hutaki kumuona mama yangu?”

“Natamani sana kumuona ila moyo wangu una niuma Rashidi. Hakuna mwanamke duniani anaye mpenda mumewe na akamuona akiwa na mwanamke mwengine. Japo najua ni mke wako wa ndoa kabisa ila nami nina moyo tena wa nyama ambao nitaumia Rashidi”

Tina alilama huku machozi yakimlenga lenga. Kusema kweli nikajikuta moyo wangu ukijawa na huzuni kubwa sana huku nikimtazama binti huyu kwani hichi kwa kweli ni kipindi kigumu kwake.

“Nimewasiliana na mama na amesha tangulia Tanga hivyo mimi nikiondoka muda huu nita kutana naye na tuta kwenda kwenye ile nyumba kule”

“Ila sidhani kama usalama kule uta kuwa ni mzuri kwako na mama?”

“Usijali hakuna litakalo tudhuru”

“Sawa, sasa uta waagaje watu katikati ya shuhuli?”

“Nilisha zungumza na wifi pia nikaonge na mama na wote wama ridhia hilo”

“Basi nita kuja Tanga ndani ya siku mbili hizi”

“Sawa mume wangu, nashukuru kwa kunikubalia”

Tina akanikumbatia kwa furaha kisha akaniachia.

“Mizigo yangu ya nguo tayari nimesha iandaa hivyo ningependa unisindikize Ubungo”

“Sawa”

Tukaingia ndani, nikamuita kwa ishara mama Chausiku na akanifwata sehemu nilipo simama.

“Umezungumza na Tina juu ya swala la kuondoka?”

“Yaa aliniomba ushauri nami nikaona afatwe kile ambacho ana ona ni sahihi kwake. Kwa maana kweli mke wako ana kuja. Ata lala kwenye kitanda alicho kuwa anal alia yeye huoni kama itamuumiza kwa asilimiua kubwa sana, isitoshe ni mjamzito, usije ukafanya mimba yake ikatoka bure”

“Mmmm sawa”

“Hata kama ingekuwa ni wewe Rashidi, anakuja mume wa mtu wako na ana lala kwenye kitanda ambacho una lala wewe ungejisikiaje kwa mfano?”

“Vibaya”

“Basi ndio hivyo hata kwa yeye upande wake ana jisikia vibaya”

“Sawa mama acha basi nimpeleke Ubungo”

“Sawa harakisha saa nane ina karibi na foleni hizi si unajua”

“Yaa”

Nikapandisha gorofani, nikakutana na Tina katika kordo akiwa na mabegi yake. Nikasaidiana naye kubeba mabegi haya hadi nje.

“Vipi mbona na mabegi?”

Shabani aliuliza.

“Tina ana safari ana elekea Tanga mara moja”

“Kwema lakini?”

“Kwema shem wala usijali”

Shabani akaniangalia kwa muda kama vile ana hitaji kuniuliza kitu ila akakausha.

“Sawa shem safari njema”

“Asante shemeji”

Tukaingai ndani ya gari na tukaondoka nyumbani hapa. Ukimya ukatawala ndani ya gari huku kila mtu akiwa hana cha kusemesha mwenzake.

“Najua nimefanya maamuzi ya haraka, ila nina kuomba unisamehe sana Rashidi”

“Kikubwa ni wewe na mwanangu aliyopo tumboni muwe salama”

“Nakupenda sana Rashidi, nimekuzoea ila sina jinsi, ili nisikuudhi ndio maana nime amua kufanya hivi”

“Naelewa Tina. Ukifika nitahitaji kuzungumza na mama kwa kutumia video call”

“Utakubali nikupigie muda wowote?”

“Ndio wewe ni mke wangu, mbona una nijeka kama mchepuko”

“Mimi ni mchepuko”

“Kivipi ikiwa dini yangu ina ruhusu kuoa hata wake wanne. Ishu ni kwamba Jackline yeye akufahamu wewe. Ila nikikaa naye chini nita yaweka mambo sawa. Umenielewa?”

Nilizungumza kwa ukali

“Nisamehe sipendi kukasirika”

“Una niudhi, unavyo jiweka chini chini. Ungekuwa ni mchepuko ninge kugongea huko nje nje na usinge ishi na mimi hapo nyumbani”

“Naomba unisamehe mume wangu”

“Nimakusamehe. Nakupa sasa kazi moja, nenda Tanga, tafute eneo zuri ambalo wazo lako la hoteli una hisi linaweza kukamilika na ujenzi wa hoteli uanze haraka iwezekanavyo. Maisha yenyewe mafupi haya nina weza kufa nikakuacha wewe na mwanao hamuna kitu”

“Sawa mume wnagu”

Tukapita kwenye moja ya benki nikatoa kiasi cha milioni nne na kumkabidhi Tina.

“Hizi tumia vizuri, zitakusaidia kwenye kipindi hichi kifupi ambacho sipo nawe. Umenielewa”

“Sawa mume wangu”

Tukafika Ubungo, nikamkatia tiketi Tina katika banasi yaendayo mkoani Tanga. Nikasubiria hadi muda wa basi hilo kuondoka nami nikaondoka stendi hapa. Nikampigia simu Chausiku.

“Ndio Rashidi”

“Hembu mpe simu mama”

“Huyu hapa”

“Rashidi”

“Sasa mama una onaje ukakodisha bodaboda ikakuleta hadi hapa Ubungo, nikisema nirudi tena huko, kisha tueleke Airpot ina weza kula kwetu, leo kuna foleni na isitoshe nina sikia kuna msafara sijui wa raisi”

“Mimi hao bodaboda siwaminigi jamani”

“Shani si yupo?”

“Ndio”

“Basi muambie akuitie bodaboda wake anaye muamini, mimi utanikuta Ubungo hapa”

“Sawa”

Nikatafuta moja ya mgahawa katika eneo hili la Ubungo, nikaagizia agizia juisi ili kupoteza poteza muda ili nimsubirie mama Chausiku.

“Kurudi kwake sidhani kama ana weza kuongoza nchi tena”

Niliwasikia wanaume wawili walio kaa pembeni yangu wakizungumza huku tukitazama habari ya ujio wa raisi na watu wana ombwa kujitokeza barabarani kwa ajili ya kumpungia mkono.

“Siasa ni mbaya sana. Watu wana penda madaraka kuliko sisi wananchi”

“Umeona ehee, ila si atapigiwa kura na bunge”

“Sasa una hisi bungeni hato pitishwa kama, ameweza kurudishwa kwa mtutu basi ata pita hata kwa mtutu tu huko bungeni”

Simu yangu ikaanza kuita.

“Ndio mama”

“Upo wapi, nimesha fika hapa Ubungo na bodaboda”

Nikamuelekeza mama Chausiku nilipo, nikalipia juisi hii niliyo kunywa kisha nikatoka nje na kumkuta mama Chausiku akinisubiria. Tukaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza.

“Ila Rashidi mwanangu upunguze”

“Nipinguze nini mama?”

“Umalaya. Nahisi nikitumia neon hilo lita kuingia vizuri akilini. Nimemuonea sana huruma Tina kuondoka”

“Ila sio makossa yake. Isitoshe hawa wamekuja tu galfa, sasa nita fanyaje?”

“Ila shukuru Mungu yule binti ana kupenda. Ila ingekuwa ni mimi aisee mbona ningekaa na ningefanya vituko balaa, tena nina mtoto wako tumboni, ndio ungekoma kabisa”

“Hhaa watu wameumbwa tofauti mama”

“Ni kweli, ila wakati mwengine una paswa kuwa makini mno huko unapo pita pita kuna maradhi mwanangu wee haya”

“Nimekuelewa mama”

Tukafika uwanja wa ndege. Ulinzi tulio ukuta hapa kwa kweli si wakawaida. Tukasimama eneo ambalo wageni ndipo wanapo tokea.

“Saa nane ndio hii”

Mama Chausiku alizungumza huku akitazama saa yake ya mkononi.

“Yaa ndio sasa”

Nilizungumza huku nikiangaza angaza eneo hili. Saa nane dakika ishirini, nikamuona mama, Jackline pamoja na wanangu watu wakitoke eneo hili. Shamsa akawa wa kwanza kuniona, akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu, wadogo zake nao wakanikimbilia na kunikumbatia kwa furaha.

“Mumekua wakubwa wanangu”

Nilizungumza huku nikiwatazama. Jackline naye akanikumbatia na bila aibu yoyote akaanza kuninyonya denda lililo wafanya waswahili wezangu kuduwaa kwani kwa mila za Kitanzania hivi vitu vinafanyikia chumbani na sio hadharani kama hapa uwanja wa ndege.


Taratubu tukaachiana ndimi zetu.

“Nimefurahia sana kukuona mume wangu”

“Hata mimi nime furahia kuona mke wangu. Watoto wetu wamekua wakubwa sasa”

“Yaa sasa wamerudi nyumbani”

Mama akatanua mikono yake na taratibu nikamsogelea na kumkumbatia kwa nguvu.

“Karibu sana nyumbani mama”

“Nashukuru mwanangu. Naona misuli imeongezeka kuwa mikakamavu?”

“Mbona nilikuwa hivi hivi”

“Hapana sasa ime ongezeka”

“Hahaha nashukuru mama yangu. Nikawabeba wanangu hawa mapacha na tukaanza kutembea kuelekea lilipo gari. Tukaingia ndani ya gari huku wakati huu Jackline akikaa siti ya mbele huku wanangu na bibi zao wakikaa siti ya nyuma.

“Leo kuna ulinzi mkubwa sana kuna nini Rashidi?”

Mama aliniuliza huku tukiondoka taratibu eneo hili.

“Nchi ilipinduliwa sasa yule raisi aliye pinduliwa leo hii ana rudi nchini”

“Ndio yule yule?”

Mama aliniuliza kwa shauhuku kubwa.

“Ndio huyo huyo”

“Ehee kazi ipo kweli kweli”

Tukafika eneo ambapo magari yote yamesimamishwa kupisha msafara wa raisi. Ikatulazimu na sisi kusimamisha gari letu pembeni. Jackline akanishika kiganda change cha mkono wa kulia.

“Vipi maisha ya hapa Tanzania mume wangu?”

“Ahaa joto jingi ila Mungu ana tusaidia”

“Baba nimetoa wimbo mpya”

“Weee”

“Usikilize”

Shamsa akanikabidhi ipod yake, nikaanza kuusikiliza wimbo huu hadi nikajikuta nikishangaa uwezo mkubwa sana wa kipaji chake.

“Huyu ni wewe?”

“Ndio ni mimi baba”

“Kuna yule dj wa Marekani alihitaji kumsainisha kwenye lebo yake ila nikamuambia hadi nizungumze na baba yake kwa maana nisinge fanya maamuzi ya kipeke yangu peke yangu”

“Dj gani?”

“Dj Khalid”

“Aisee hilo ni dili kubwa mke wangu angesainishwa tu”

“Usijali nafasi bado tunayo mume wangu. Ipo siku ata sainishwa, sasa hivi huwa namsisitizia kwanza kwenye masomo kwa maana una jua kipaji bila elimu ni sawa na kujaza pipa kwa kifuniko cha chupa”

“Ni kweli aise”

“Rashidi hembu na mimi nimsikilize mkukuu wangu”

“Ngoja niuweke tuusikie wote”

Nikachomoa earphone na sote tukaendelea kuburidika na wimbo huu. Tukaendelea kusubiri kwa dakika kama arobaini, hivi gari za polisi zikaanza kupita kwa mwendo wa kasi kisha zikafwatia pikipi kama ishirini hivi za askari wa usalama barabarani huku pikipiki hizi za rangi nyeupe zikiwa zime chora umboa la V katika utembeaji wake wa mwendo wa taratibu. Zikaanza kupita gari za walinzi huku zikiwa nazo kwenye mwendo wa taratibu. Ikafika awamu ya gari ya raisi, tukamuona raisi akiwa na mke wake wakiwa wamesimama kwenye gari hilo huku wakipingia wananchi mikono. Nikamuona Shamsa akimuangalia kwa umakini mama yake, kisha akajikausha kimya, nikatazamana na mama zangu hawa kwa maana wana jua ni namna gani Shamsa alivyo mkumbuka sana mama yake. Gari hili likapita huku zikifwatia gari nyingine za walinzi. Nikamtazama Shamsa na akajikausha kimya kana kwmaba hajaona chochote. Baada ya msafara huu kutokomea, gari zikaruhusiwa kuendelea na safari zake. Nikaendelea kuendesha kwa taratibu gari hili katika foleni hii ndefu. Majira ya saa moja kasoro usiku tukafika nyumbani na tukapokelewa na Chausiku, mke wa Shabani, mwanaye pamoja na wamama wawili ambao walikuwa hapa nyumbani kwa ajili ya kumfariji mama Chausiku na mwanaye.

“Hii nyumba ni yako mume wangu?”

“Yaa nimei inunua”

“Aisee umejitahidi mume wangu. Kumbe ume fanya mambo ya maana?”

“Kama nipo na mke mwenye akili ya biashara, nina achaje na mimi kufanya mambo ya maana”

“Hahaha ni kweli aisee.”

Furaha ikatawala kwa kila mmoja huku Shamsa na wadogo zake wakionekana kujawa na furaha sana kuliko mtu yoyote. Kila mara nina jaribu kuingia kwenye mitandao ya kijamii kuperuzi ili niona kama raisi ame uwawa ila kwa bahati mbaya hakuna taarifa kama hiyo.

‘Ina maana hajamuua au?’

Nilijiuliza swali lililo kosa majibu.

“Shem”

“Ndio shem”

“Sheby yopo wapi?”

“Alitoka muda mrefu. Hembu mpigie simu”

“Sawa. Baby ngoja nimpigie yule rafiki yangu uliye zungumza naye siku ile tulipo kuwa kwa mama Chausiku tukila mihogo”

“Sawa mume wangu”

Nikaondoka sebleni hapa na nikatoka nje kabisa. Nikampigia Shabani, simu yake ikaanza kuita na baada ya muda kidogo ikapokelewa.

“Kaka upo wapi?”

“Nipo njiani nina kuja ndugu yangu si umesha fika home?”

“Ndio tume fika toka saa moja hivi”

“Sawa”

Nikakata simu kwa maana mazungumzo ya mpango wa kumuua raisi sio ya kuzungumza kupitia simu kwani ni rahisi kusikilizwa na vyombo vya usalama.

“Baba”

Niliisikisa sauti ya Shamsa nyumba yangu nikageuka na taratibu nikachuchumaa ili niwe sawa naye kwa kimo.

“Niambie malkia mrembo wangu?”

“Kwa nini mama ameamua kuwa na yule mzee?”

Swali la Shamsa likanipa kigugumizi kilicho nifanya nishindwe kumjibu hapo hapo.

“Ahaa….hata mimi sija jua mwanangu”

“Au kwa sababu yeye ni raisi?”

“Labda mwanangu”

“Namchukia sana mama. Alinikana, nakumbuka vizuri”

Kauli ya Shamsa ikaniumiza sana moyo wangu na nikajukuta nikimkumbatia.

“Nataka kuwa mtu maarufu dunia nzima ijue ubaya akio ufanya kwako na kwetu sote”

“Ila mwanangu ina bidi umsamehe kwani kuna wakati binadamu huwa tuna telezaga kutokana na mambo ya kidunia”

“Mimi siwezi kumsamehe, najuta ni kwa nini nilizaliwa na mwanamke kama yeye. Mimi mama yangu sasa hivi ni Jackline, ameweza kunipenda kwa moyo wake mmoja, amenifunza yaliyo mazuri na kunikanya kwa mabaya. Amenipatia kila ninacho kihitaji. Amekuwa mama mzuri kwangu na kwa wadogo zangu. Ila mama yangu mzazi ana nikana kwa ajili ya pesa na uchu wa pesa. Haki ya Mungu baba nina mchukia mama, namchukia”

Shamsa alizungumza kwa jazba hadi akaanza kulia. Taratibu nikamkumbatia, nikamnyanyua na nikambeba hadi kwenye boneta ya gari na nikamkalisha.

“Usilie mwanangu”

Nilizungumza huku nikimfuta machozi kwa kutumia viganja vyangu. Kitu kingine nilicho kigundua kwa Shamsa, ni uwezo wake mkubwa wa kukumbuka mambo ya nyuma.

“Nilikuwa na hamu kubwa sana ya kurudi nyumbani, nahitaji niwe mkubwa ili nimuonyeshe mama kwamba alikosea kunisaliti tena hadharani na kuniambia mimi sio mwanaye”

“Mwanangu yamesha pita hayo. Yaache, ipo siku Mungu ata mlipia”

“Kwani ili mtu awe raisi ana paswa aweje?”

“Awe ni mwema, asiwe na kashfa. Ana namiaka arobaini na kitu. Kuna sifa nyingi nyingi ambazo sizifahamu sana”

“Kwani wewe hupendi kuwa raisi?”

“Mimi, hapana mwanangu sina sifa hizo. Baba yako niliacha shule nikiwa kidato cha pili na kuanzia hapo sijawahi kuingia shule kabisa.”

“Ila si shule zipo una weza kusoma?”

“Kwa sasa nimewaachi nyinyi mwanangu someni sana ili muje kutimiza ndoto na malengo yenu. Mimi kwa sasa nina watengenezea njia ya kiuchumia na maisha mazuri”

Nikamuona Jackline akija eneo hili.

“Naona muna zungumza”

“Yaa mwanao alikuwa na yake anahitaji kunishirikisha”

“Mama nina muomba baba awe raisi ila hataki”

Shamsa akaamua kuzungumza mwenyewe.

“Raisi?”

Jackline aliuliza kwa mshangao.

“Ndio”

“Eehe umefikiria nini mwanangu hadi kumshauri hivyo?”

“Nimependa kumuona ana kuwa raisi ili wale maadui zake wanao msumbua aweze kuwashuhulikia”

“Shamsa mwanangu, raisi ana kuwa ni kiongozi wa watu. Hivyo raisi akitumia cheo chake vibaya kwa kuwahukumia watu hato pendwa na watu. Sawa mwanangu”

Jackline alizungumza kwa sauti ya upole huku mkono wake mmoja akiwa ameupitisha kiunoni mwa Shamsa.

“Sawa mama, ngoja niingie ndani”

Nikamshusha Shamsa kwenye bonet hii ya gari na nikamnyanyua Jackline na kumpandisha. Taratibu tukanyonyana denda.

“Una nitia nyeg** baby”

Jackline alizungumza kwa sauti ya mahaba.

“Leo nahisi hatuto lala”

“Yaani nilivyo na hamu na wewe. Yaani hapa nilikuwa natamani ndege iweze kufika haraka sana”

“Ila vipi baba ana endeleaje?”

“Ana endelea vizuri, ameelekea New York kuna maswala yake ya kibiashara amekwenda kuyafwata huko”

“Sawa sawa”

“Ila amesema akitoka New York ata unganisha hadi South Africa kisha ata kuja hapa Tanzania kujumuika nasi kwenye mapumziko haya”

“Sawa sawa mke wangu ana karibishwa, hapa ni kwake”

Tukaona gari la Shabani likiingia ndani hapa.

“Shabani huyo ana fika”

Shabani akasimamisha gari lake pembeni ya gari hili akashuka na kwa furaha akasalimiana na shemeji yake.

“Karibuni sana”

“Tuna shukuru, tumekaa masaa mengi sana kwenye ndege”

“Poleni sana”

“Tuna shukuru sana shemeji, Kumbe ni mcheshi sana wewe?”

“Sana, yaani tabia za ndugu yangu hapa zina endana kabisa na mimi ndio maana tumekuwa pamoja toka tulipo kuwa vijana wadogo sana”

“Aisee ni vizuri sana”

“Yaani Shabani tulikuwa tuna kaa mtaa mmoja. Kwao hapa na mimi kwetu hapa. Hivyo toka watoto tuna cheza mpira pamoja”

“Ndio maana wanao wana penda sana kucheza mpira.”

“Weee”

“Haki ya Mungu wana penda mpira sana, kuna siku nilisha wapeleka kwenye academy ya PSG. Wakataka kusajiliwa kabisa ila nikawaambia umri wao ni wadogo snaa na pia hadi nizungumze na wewe”

“Aisee kaka umezaa majembe”

“Hahaaa nakumbuka yake mambo yangu ya kupiga chenga. Kipindi hicho naitwa Ronaldo yaani wee acha maisha yana mambo megi sana”

“Kumbe uliitwa hadi Ronaldo?”

“Ndio ila yule Ronaldo Mbrazi sio huyu wa sasa”

“Hahaa natakani kama ningekuona unavyo cheza”

“Uta niona siku”

“Kaka unikumbushe tuongee jambo”

“Ngoja niwapishe shemeji”

“Hapana sio muhimu sana”

“Hapana una jua wanaume wanapo zungumza ujue kuna jambo la muhimu. Baby nipo ndani”

Jackline akanipiga busu la mdomo kisha akaondoka eneo hili.

“Aisee una nyota ya watoto wakali. Unawatolea wapi hawa aisee?”

“Humu humu duniani ndugu. Aisee umesikia chochote juu ya ishu ya raisi?”

“Hata mimi nilikuwa nataka kukuuliza vipi umesikia kwa maana naona kimya tu”

“Una taka kuniambia Leticia hajafanya kazi?”

“Nikuulize wewe kwa maana ndio mtu wako. Hivi ulimpa pesa?”

“Ndio”

“Kiasi gani?”

“Dola milioni moja”

“Jamaa wewe, yaani huna huruma kabisa na pesa yako. Hizo si pesa nyingi sana kaka?”

“Ni mjamzito, ana mimba yqangu hivyo nina gawa urithi mapema sana”

“Duuu sasa, raisi hajauwawa ina kuwaje hapo kaka?”

“Ndio nataka kujua, au binti wa watu amekamatwa?”

“Sidhani kama angekamatwa ningetambua”

“Sasa tuna mpataje?”

“Kwani huna namba yake?”

“Tena umenikumbusha”

Nikaiandika namba ya Leticia ambayo nimeikremisha akilini mwangu kisha nikaipiga. Kwa bahati mbaya namba yake haipatikani.

“Vipi?”

“Hapatikani”

“Duu sasa tuna fanyaje, hii ni hatari sana mzee akirudi madarakani ikiwa familia yako ipo hapa. Je uta weza kuilinda wasiidhuru kwani lazima wata angalia udhaifu wako ambao ni familia yako?”

Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikimtazama Shabani machoni mwake.

“Yaani bora ile kazi ninge ifanya mimi mwenyewe aise”

“Sasa sio wakati wa kujutia ni wakati wa kufikiria nini cha kufanya ndugu yangu kwani kama ni maji ndio yamesha mwagika”

“Una nishaurije?”

“Ina bidi tujipange kujilinda, tulimuacha adui akaingia kwenye zone yake hivyo sidhani kama tuna weza kumkabili kirahisi sana hayo”

Nikaegemea gari hili huku nikiwa na mawazo mengi sana kwa maana sasa maji yanataka kuzidi unga.

“Nahitaji kuifanya hiyo kazi mimi mwenyewe usiku huu”

“Una kichaa wewe. Mke wako, wanao, mama yako wapo ndani una taka kwenda kujiingiza kwenye matatizo yasio na msingi. Hembu kuwa na akili broo, usifanye vitu kihisia, fanya vitu kwa akili wewe ni mwanaume ndugu yangu sio mwanamke anaye ongozwa kwa hisia.”

Shabani alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.

“Rashidi tuna familia, tuna wake, ina bidi kufikiria kama wanaume. Tufikiria nje ya boksi juu ya hili”

“Au ni msaidie Fatma kuwa raisi?”

“Huko ni kuishiwa maarifa na maamuzi kama mwaname. Yule damu hatufai na hapaswi kuwa kwenye mipango yetu. Yule tumemjua hata mwezi haujapita why aingie kwenye maisha yetu. Sisi wawili tuna paswa kukaa chini na kutafakari nini cha kufanya, na tukulipata safari hii hakuna kurudi nyuma amza zao ama zetu. Sawa kaka”

Shabani alizungumza kwa msisitizo na nikajikuta nikitingisha kichwa kwani rafiki wa kweli ni yule anaye chukulia matatizo yako kama yake na ana kusaidia kwenye wakati wowote uwe wakati war aha, huzuni au shida.




“Ngoja nikapumzike nikamka nina imani nita pata jibu la nini nifanye”

“Sawa kaka”

Tukaingia ndani pamoja, nikamtambulisha Maulid kwa watoto wangu hawa wa kiume kisha kw apamoja tukajumuika mezani kupata chakula cha usiku, kisha mimi na Jackline tukatangulia kuelekea chumbani huku nikimuacha Chausiku akitutazama kwa jicho kali ambalo ndani yake limejaa wivu. Kitendo tu cha kuingia ndani, Jakcline akanidandia na kuanza kuninyonya denda hoku mikono yake akiwa ameipitisha mabegani mwake na miguu yake ameipitisha kiunoni mwangu. Kutokana ni mwepesi haikuwa shida wangu kumbeba na kumuhimili. Nikaufunga mlango kwa ndani kisha taratibu nikatembea hadi kitandani huku tukiendelea kunyonya. Tukavuana nguo kwa haraka haraka na Jackline akakaa mkao ambao nina upenda, tukaanzaisha mechi hii kwa kasi ya ajabu huku kila mmoja akionyesha ujuzi wake.

‘Haki ya Mungu ipo siku nita fia kiunoni mwa mwanamke, si kwa kuwatomb** huku’

Nilizungumza hukimoyo moyo huku nikiwa katika kasi ya kutafuta goli la kwanza kwa maana hizi mechi mfululizo zimefanya waarabu wangu kuwa mbali sana na geti la kutokea. Jackline akafanya kila anacho kiweza hadi nikamaliza mzunguko wa kwanza huku yeye kwa upende wake akiwa tayari amesha funga magoli manne kwenye mzunguko huu tu wa kanza.

“Ahaa nilikuwa nina hamu sana na wewe mume wangu. Yaani hapa nimekuwa mwepesi sasa”

“Kweli?”

“Ndio mume wangu yaani umenisukugua kisawa sawa.”

“Nashukuru kwa kuja mke wangu kwa maana nyeg** zingeniua?”

Nilizungumza kana kwamba sijafanya chochote toka mara ya mwisho kukutana kimwili na mke wangu kumbe ni shetani niliye vaa ngozi ya kondoo.

“Pole mume wangu. Nipo hapa uta nichoka wewe mwenyewe”

“Vipi biashara lakini?”

“Zina kwenda vizuri mume wangu na sasa hivi baba ana taka kufungua kampuni ya ndege za abiria. Ndio dili analo kwenda kulifanya New York na Africa kusini”

“Aisee itakuwa ni kampuni kubwa sana?”

“Ndio amewekeza pesa nyingi sana na ndege zake zita kuwa zina safari dunia nzima”

“Amenunua ndege za aina gani?”

“Ametengenezewa na kampuni ya Air Bus pamoja na Boeing hivyo hapa kwenye miezi miwili ijayo kampuni ina anza kufanya kazi kwa maana yupo hatua za mwisho. Ngoja nikuonyeshe picha za hizo ndege”

Jackline akachukua simu yake na kuanza kunionyesha picha za ndge hizo.

“Aiee ni nzuri na kubwa sana?”

“Yaa ana taka kuleta ushindani na Fly Emirates na KLM”

“Aisee ame nunua ndege ngapi?”

“Ameanza na ndege mia moja”

“Mia moja!!?”

Niliduwaa kwa maana sisi huku tuna pambana na mabasi wezetu wana pambaa na kampuni za ndege.

“Ndio ndege mia moja na bado nyingine mia zina tengenezwa kwenye miaka miwili hii ijayo.”

“Aise kumbe baba mkwe ana pesa nyingi hivyo?”

“Yaa hiyo ni ndoto yake aliyo kuwa nayo toka alipo kuwa na miaka ishirini na moja. Amekuja kuitimia akiwa na miaka sabini sasa”

“Duu kweli ina bidi uishi katika ndoto zako”

“Ndio hivyo mume wangu. Ehee niambie ilikuwaje Don akakuingizia pesa zote zile. Una jua dola bilioni mia sio mchezo mume wangu?”

“Yaa ni stori ndefu, kama unavyo jua mimi na DON mfarakano wetu. Sasa niliweza kumbananisha na nilikuwa nime dhamiria kumuua kabisa na akaniomba tuzungumze biashara. Akanipandishia dau hadi dola bilioni mia moja nikaona sio dili dogo. Najua Shamsa na ndugu zake wana weza kuzitumia hadi kufa kwao”

“Yaani umefanya la maanaa kuziingiza kwenye benki za Sweeden ila ungeingiza Marekani, lazima FIB wangekuwinda kutaka kujua pesa yote hiyo ina toka wapi?”

“Yaa ndio maana niliamua kuhakikisha zina kwenda Sweeden kwani kule ndio kuna machimbo ya matajiri wote”

“Hivi Don ana pesa kiasi gani hadi kukupa hizo zote ambazo hata baba hajazifikisha japo ni tajiri ila baba hana utajiri wa pesa hizo”

“Nilimsikia DON akisema ana pesa zina fika dola trilioni moja””

“Mungu wangu”

“Kwa DON siwezi kushangaa kwa maana jamaa ni drugs dealer wa maana. Tofauti na hawa wote ulio wahi kuwasikia sijui kina Pablo, Jamaa ana pesa, ana ingiza pesa kwa sekunde na pesa yake hajaweka benki ndio maana hawezi kukamatwa. Vile viwanda vyake kadhaa ndio vina angaliwa tu, ila upande wa pili ana pesa”

“Mmmm sasa kwa nini mume wnagu usinge mmega hata nusu kwa nsu?”

“Mke wangu sikujua hili mapema. Ila siku ile alipo fikisha dau hilo nikaona ina nitosha mimi na wangu umasikini ndio kwa heri hiyo”

“Sio mbaya. Sasa mume wangu, haya umemuacha DON hai huoni kama ana weza kukurudia na kukudhuru?”

“Hilo ndipo nina jaribu kulitafutia namna ya kulishuhulikia kwa maana lazima nihakikisha nina pambana naye hadi dakika ya mwisho. Cha kwanza ilikuwa ni kupata nguvu ya pesa kisha baada ya hapo nita kuwa na uwezo wa kufanya chochote na kwa wakati wowote na nisinge tumia pesa yako ua ya baba kukabiliana na DON kwa maana hizo pesa zenu ni za biashara. Ila hii pesa niliyo ipata kwa short cut ndio itakayo mtoa roho”

Nilizungumza huku Jackline akiwa amekilaza kichwa chake kifuani mwangu na mkono wangu mmoja wa kulia ukiwa katika makalio yake nikiendelea kuyapapasa taratibu tukisubiria mzunguko wa pili wa mechi hii.

“Na mpambae wake ambaye ana mpatia nguvu ni huru raisi anaye taka kurudishwa madarakani”

“Huyu tuliye pisha msafara wake?”

“Ndio na yule nikiisha muondoa basi DON kwa Tanzania hato kuwa na nguvu kubwa kwani tayari nimesha mjua wapambe wake wengine wadogo wadogo.”

“Ina bidi safari hii mume wangu tufanye kweli, tusimpe nafasi ya kumkamata hata mmoja wetu kwenye hii familia yetu”

“Nakuahidi mke wangu nita hakikisha kwamba sote tuta kuwa salama”

“Nakupenda hapo mume wangu. Vipi hujafungua biashara yoyote hadi sasa hivi”

“Kwa sasa tumeanza na biashara ya mabasi ambayo Shabani ana simami”

“Waoo ni jambo zuri sana hilo mume wangu”

“Nashukuru na pia tuna mpango wa kujenga hoteli zenye hadhi ya nyota tano ambazo zita kuwa katika mikoa mitatu ya kibiashara. Hapa Dar es Saalam, Arusha kwa ajili ya utalii na nyingine kati ya Mwanza au Tanga”

“Ahaa sawa mume wangu ila kuna msimamizi kwenye hizo hoteli kwa maana biashara ya hoteli ina hitaji umakini wa ahali ya juu sana. Sasa kama utakuwa hujapata wasimamizi wa uhakika ni bora ukafungua moja kwanza alafu ukasikilizia, ukiona ina kwenda vizuri basi wewe uta fungua nyingine. Ila kama kuna usimamizi mzuri una weza kujenga nyingine. Kikubwa ni kuhakikisha kwamba hiyo pesa una izalisha na kuitakatisha, hata siku ukiamua kufwatiliwa basi una weza kuwaonyesha vyanzo vyenye thamani ya pesa unayo miliki mume wangu”

“Sawa mke wangu nime kuelewa”

“Pia kwa kutumia kampuni mpya ya baba tuna weza kufungua tawi hapa nchini Tanzania na ndege zake zikawa zina tua hapa na tuna pata wateja wengi na ukisaidia katika kuwekeza hilo na wewe una kuwa una ingiza asilimia fulani kwa maisha yako yote ambapo shirika lita kuwa lina fanya kazi”

“Sawa mke wangu nime kuelewa na pia nilifikiria kufungua kiwanda cha utengenezaji wa mafuta ya kula, unga wa mapishi na bidhaa nyingine za jikoni ila zinazo husiana an kula tu”

“Hilo ni wazo zuri mume wangu. Jambo pa msingi ni kutazama kwanza sera za kufanya biashara kama hiyo ni rafiki kwenye nchi yako. Una jua kuna nchi zina kodi nyingi hivyo una wesza kujikuta una kiwanda kama hicho alafu wewe una pokea asilimia stini na asilimia arobaini ina ingia kwenye makodi ya kiserikali. Mwisho wa siku garama za uendeshaji wa kiwanda zina kuwa ni kubwa kwa upande wako wewe muwekezaji na mwisho wa siku una funga biashara kutokana na hasra hivyo una kuwa umepoteza kazi na pesa pia”

“Kweli nina mke mfanya biashara. Una jua mambo mengi”

“Hahaa baba yangu alinifundisha hivyo toka utotoni. Hata mimi nimesha ipandikiza hiyo roho kwa watoto wetu. Japo wana vipaji ila ni lazima wawe na elimu kubwa juu ya biashara, kwanza ya kile wanacho kifanya pia kwenye vitu vitakavyo waingiza pesa nyingi zaidi ya hizi tunazo tafuta sisi. Hivyo hata leo hii hatupo duniani, kwa kile nilicho kipandikiza kwa Shamsa basi ata weza kujiongoza mwenyewe bila kudhulumiwa na mtu yoyote”

“Ndio maana ana maswali mazito sana tofauti na umri wake”

“Kwa watoto wa miaka nane ni haki yake kuwa na ufahamu mkubwa wa kiakili kwa maana dunia sasa hivi ina kimbia haitembei na haimsubirii mtu. Kila siku kuna mambo mengi yana gunduliwa na vitu vya zamani vina achwa na vitu vipya vina chukua nafasi kwa mafano mzuri, soko la simu. Zamani ilikuwa ili uwasiline na mtu aliyopo mbali ilikuwa ni lazima umtumie ujumbe kupitia Fax. Ila sasa hivi wewe mwenyewe una ona, mimi nipo Ufaransa wewe Tanzania ila tuna onana kupitia simu za mkononi. Hivyo maisha yame badilika mume wangu”

“Ina bidi unipige msasa wa kibiashara sasa?”

“Usijali mume wangu nipo na wewe uta jua mambo mengi sana, ila kwa sasa ngoja nikupige msasa wa huku”

Taratibu Jackilne akageuka kisha akapanda juu ya kifua chngu huku kicha chake akikielekezea alipo jogoo wake na kitimbua chake kikiwa karibu kabisa na uso wangu. Tukaanza kunyonyana maungo yetu na kufanuya raha kutawala kati yetu. Baada ya kila mmoja kuridhika, taratibu Jackline akamkalia jogoo wangu humi mikono yake akiiweka kifuani mwangu na akaanza kukata mauno kana kwamba ni mtoto wa kizaramo.

Pindua piundua zinazo endelea hapa kitandani una weza kuzifanisha na vita ya pili ya dunia iliyo muondoa Adolf Hitler madarakani. Kwani kila mmoja na pombana kwa ajili ya ishindi. Tukahamia katika sofa mara naada uya kuona uwanja wa kitanda haututoshi.

“Nakupenda sana Rashidi”

Jacklie alilalama huku sote tukiendeleza jaramba hili linalo tufanya tumwagikwe na jasho japo A/C ina fanya kazi.

“Nakupenda pia mke wangu”

“Wewe mtamu mume wangu”

“Kweli?”

“Yeaha. Wewe mtamu baby ooo…..aiis……a…:

Jacklie alizidi kulama na kunifanya nizidi kuongeza makeke, kwani hakuna jambo zuri kwenye mitanange kama hii ukisifiwa na mpenzi wako, ina kufanya una cheza hata zaidi ya uwezo wake. Utofauti wa kuto sifiwa na mpenzi wako kuna poteza ladha ya mtanange, ndio maana wanaume wakipata michepuko inayo wasifia hata kama ana kibamia basi ana hamia huko na kumuacha mke wake anaye subiria mechi iishe ageukie upande wa pili wa kitanda na alale.

“Una kum** tamu mke wangu”

“Kweli?”

Jackline aliniulza kwa sauti laini na iliyo jaa mahaba.

“Ndio baby…..vip….nikojo……e?”

“Kojoa baby nakusubiria tumalize mapamoja”

“Kweli”

“Yes baby”

Nikamkunja kisawa sawa Jackline kwenye sofa hili hadi likaanza kusogea, Sote kwa pamoja tukamaliza mechi hii huku tukihema na kutawalia na furaha kubwa. Jackline akanikumbatia huku akinipiga mabusu mfululizo.

“Una nijulia mume wangu”

“Hata wewe mke wangu na una nihimili”

“Lazima nikuhimili mume wangu kwa maana hakuna tembo anaye shindwa na mkonga wake”

“Hahaa”

“Yaaa kipindi cha kwanza ndio ulikuwa una nionea. Ila sasa hivi ahaa tuna kwenda sambaba hadi dakika ya mwisho”

“Hongera mke wangu”

“Hongera kwako mume wangu umenifanya niwe hodari kitandani”

“Hahahaha”

Taratibu nikamnyanyia Jackline na kuingia naye bafuni. Tukagoba na kurudi kitandani.

“Ngoja nitandike kitanda mume wangu kwa maana ona shuka lilivyo changuka”

“Sawa mke wangu”

Ikatubidi tushuke kitandani. Tukasaidiana kutandika shuka kisha tulalala huku nikimkumbatia Jackline kwa nyuma. Usingizi ukatupitia sote kwani si kwa uchovu huu. Nikafumbua macho yangu mara baada ya kusikia kelele za watoto wangu. Nikatazama pembeni na simuoni Jackline, mwanga wa jua unao ingia dirishani una ashiria kwamba kume pambazuka. Nikatazama pembeni na kuona trake suit ambayo ni nimpya kabisa. Nikavaza suruali yake, kisha taratibu nikapiga hatua hadi dirishani. Nikamuona Shabani akicheza mpira na watoto wote huku furaha ikiwa ime tawala.

“Umeamkaje mume wangu?”

Jackline aliingia ndani hapa huku akiwa ameshika kikombe.

“Salama mke wangu”

“Nimekueletea kahawa, ni siku nyingi sana sijakutengenezea kahawa”

“Hii ndio ile ninayo ipenda?”

“Yaa ndio hiyo nimekununulia nyingi sana”

“Waoo asante mke wangu”

Nikapokea kikombe hichi, Jackline akanipiga busu la mdomoni. Nikaionya kahawa hii na kusikilizia ladha yake inayo nichangamsha sana.

“Ohoo nzuri sana mke wangu”

“Asante mume wangu. Ahaa kuna nguo mpya nyingi nimekuja zazo nimezipanga kwenye hilo kabati hapo, hivyo ukihitaji nguo, viatu, saa, niwani mikanda vyote nimekupangia humu ndani mume wangu”

“Nashukuru mke wangu”

Nikapiha hatua hadi kwenye kabati hili kubwa lililo jengewa ukutani. Nikatazama nguo hizi na kujikuta nikitabasamu kwa furaha.

“Nashukuru mke wnagu”

“Usijali mume wangu, nilikufanyia shooping ya nguvu nikiamini kwamba uta kuwa una hitaji hivi vitu. Kuna hizi raba air force, Jordan, Fila. Kuna suti hizi, saa hizi”

“Waoo hizi saa ni dhahabu?”

“Yaa, una hisi nita kununulia vitu feki mume wangu”

Nikazitazama saa hizi kumi na tano ambazo zote ni mpya.

“Asante mke wnagu japo sijakupatia zawadi ila nakuahisi nita kupatia zawadi”

“Usijali mume wangu.Mimi ni wako, cochote utakacho nipa kwangu ni zawadi”

“Nashukuru”

“Oga kwanza kisha ndio utoke nje mume wangu. Nimeweka mataulo mapya humo bafuni na zile sabuni unazo zipenda”

“Zile zinazo nukia vizuri?”

“Ndio mume wangu”

Nikainywa kahaja hii haraka haraka, kisha nikavua suruali hii na nikaingia bafuni, Jackline akasimama mlangoni mwa bafu hili huku akinitazama kwa macho malegevu.

“Baby, nilizungumza na raisi wa Marekani akaniambia kwamba Don amepoteweka na wana imani ata kuwa amekufa. Sasa sijajua umekutana naye vipi?”

“Mshenzi yule, amejifanyia oparesheni ya uso na amebadilisha muonekano wake wote. Amejichonga kama Michael Jackson sema huyu yeye amebadilisha sura kabsia na pia ana tumia kitambulishi kingine na jina jengine”

“Weeee”

“Ohoo, kuna watu ambao wata shindwa kumjua Don ila sio mimi. Nikikaa kwake kama mbwa nikifanta mambo hatari ya kuhatarisha maisha ili mradi apate pesa yeye hivyo sio rahisi mimi kushindwa kumfahamu yeye, yaani hata niamshwe usiku wa manane”

“Aisee kweli amekukaa moyoni”

“Ndio hivyo mke wangu. Yaani alishangaa hata yeye nilivyo mgundua akiwa kwenye muonekano wake huyo ndio maana ilikuwa rahisi kwa mimi kupiga pesa niliyo taka ili nimuachwe hai”

Nilizungumza huku nikiendelea koga kwa sababu hii ambayo ni miongoni mwa sabani garama duniani ambayo kopande chake kimoja kina uzwa dola elfu 2800,

“Baby hii sabuni ina itwaje aisee?”

“The Bader Hassoun and Sons, imetengenezwa Lebanon hiyo.”

“Hivi hakuna sabuni garama tofauti na hii?”

“Bado aisee mume wangu, hiyo wametengeneza na vumbivumbi la dhahabu, Oliva Oil, material yake mengine nime yasahau.”

“Hii sabuni ukiogea hadi nongo za miaka kumi nyuma zina toka”

“Hahaa chizi kweli mume wangu kweli mtu akae na nong’o za miaka kumi?”

“Ndio mke wangu, ohoo sababi zetu hizi za mia mia una hisi zina toa nongo”

“Haha hata bwana mume wangu, kikubwa nina penda moyo wako uridhike.”

“Asante mke wangu, wewe huogi?”

“Nimesha oga, watoto wapo na baba mdogo wao huko wana cheza mpira”

“Nimewaona wanavyo burudika”

“Kwa hiyo mume wangu umesema Don amebadisha sura?”

“Ndio mke wangu”

“Ana itwa nani?”

“Philipe Frendando”

“Mungu wangu”

Jackline alistuka sana akatoka bafuni hapa na baada ya dakika akarudi bafuni hapa akiwa na simu yake.

“Huyu hapa baby?”

Jackline akanionyesha picha yake akiwa amepiga yeye na Don hukuw akipeana mikono na ina onyesha wakiwa kwenye kikao cha kibiashara na kupeana mikono huku kuna ashiria kwamba kuna makubaliano ya kibiashara wamaingia jambo ambalo likanifanya nipate kigugumizi cha kumjibu Jackline kwani sasa Don amekutana na mke wangu bila ya yeye kumfahamu.



“Ndio huyu mume wangu?”

“Ndio”

“Ohoo Mungu wangu tumesha liwa baby”

“Una maanisha nini?”

Jackline akatoka bafuni hapa ikanibidi kuoga haraka haraka kisha nikatika huku nikiwa nimejifunga taulo kiunoni. Nikamuona Jackline akiwa amekaa kitandani huku akiwa amejiinamia chini.

“Mke wangu niambie nini kimetokea?”

Nilizungumza huku nikikaa pembeni ya Jackline.

“Mwenzi ulio pita nilikutana na huyu Philipe Frenando. Tuliingia ubia kwenye kiwanda changu kile cha kutengeneza Soda. Nilikuwa nina hitaji kupata msambazaji katika bara la America Kaskazini na tulito tenda ambayo makamponi mengi sana yalipileta cv zake na kampuni ya Philipe ikashinda. Huwezi amini nimeingia naye mkataba wa dola milioni mia tatu. Sijajua kabisa kwmaba ni DON mume wangu?”

Jackline alizungumza huku akimwagikwa na machozi.

“Na mbaya zaidi nilimkaribisha hadi nyumbani kwetu. Akala chakula cha usiku na sisi”

“Mungu wangu”

Nikajikuta nikishusha pumzi nyingi sana.

“Niasamehe mume wangu”

“Hapana mke wangu hukujua chochote, hivyo huna haja ya kuniomba msamaha”

“Sasa amesha jua mazingira ya familia yangu”

“Usijali kama alikuwa na mpango wa kuwaangamiza angesha waangamiza ila najua DON yupo kwa ajli ya kuniwinda mimi. Ila maswala yote si yalifanyika kika kisheria?”

“Maswala gani?”

“Ya hiyo biashara yenu?”

“Ndio”

“Basi usiwe na shaka kila kitu kita kwenda sawa”

“Mume wangu…”

“Niamini mimi mke wangu na kuna jambo moja nahitaji unishauri”

“Jambo gani?”

Nikamueleze Jackline mpango wa kumsaidia Fatma kuwa raisi.

“Mume wangu hatuwezi kutumia pesa yetu kwenye siasa epuka sana siasa, kama ni kumalizana na maadui zetu tumalizane nao kijasusi na sio kutumia pesa. Mume wangu kuna watu wana fanya kazi miaka hata hamsini ila dola milioni mia moja hawafikishi kabisa”

“Sawa mke wangu, kwani nilishindwa kufanya maamuzi nikihitaji ushauri wako kwani wewe ndio mshauri wangu wa mwisho”

“Nakupenda mume wangu, na nina malengo makubwa na wewe na familia yetu. Tambua pesa ndio nguvu ya binadamu mume wangu. Leo hii usipo kuwa na pesa ukawa masikini, tajiri anaweza kununua haki yako na wewe ukanyimwa haki yako. Mfano mzuri ni kwa mama Shamsa, sahamani nimetolea mfano huo ila ungekuwa na hii pesa kipindi upo naye, asinge kusaliti wala kuondoka maishani mwako”

“Sawa mke wangu nimekuelewa. Nakupenda sana”

“Nakupenda pia Rashidi wangu”

Nikamkumbatia Jackline kwa muda kidogo kisha akaniomba nivae nguo tutoke chumbani hapa. Baada ya kuvaa tukaelekea sebleni. Nikasalimiana na watu wote nilio wakuta hapa ikiwemo mama yangu.

“Rashidi njoo tuzungumze mwanagu”

Mama alizungumzungumza huku akinyanyuka na tukatoka nje. Tukakaa kwenye kibanda cha kupumzikia.

“Ehee habari za masiku?”

“Salama tu mama, niambie”

“Namshukuru Mungu. Umejitahidi jumba ni kubwa sana kama sio lako vile”

“Hahaaa nashukuru sana mama yangu”

“Ehee nimesikia nyepesi nyepesi kwamba kuna mwanamke umejaza ujauzito huko?”

“Nani amekuambia?”

“Unahisi kwamba dunia ina siri na binti huyo hadi picha nimeiona”

Nikashusha pumzi kidogo huku nikimtazama mama.

“Yaa ni kweli”

“Sasa kwa nini ameondoka hapa”

“Sasa mama una hisi ni rahisi sana kwa yeye kukaa hapa na Jacline akiwepo?”

“Hivi mwanangu una wanawake wangapi kwa maana kuna yule wa Ufaransa uliniambia kipindi kile ana itwa nani yule?”

“Fiifi”

“Ehee yupo wapi kwa maana yule sasa hivi mtoto wake atakuwa ni mkubwa?”

“Kabla sijatekwa niliambiwa kwamba Fiifi amerudi kwao nchini Ghana na nilipewa namba yake ila kwa bahati mbaya ndio mambo yalikuwa vile”

“Yaani mwanangu una majanga. Ehee mwengine ni nani ambaye ana mtoto wako au ujauzito wako. Nazungumza hivyo kwa maana nahitaji kukusanya wajukuu wangu niwajue mapema na wajuaje mapema kwani nilikuzaa wewe peke yako, sasa umenitanulia familia yangu”

“Ahahaa kuna mdogo wake raisi ana itwa Caro ana mimba yangu?”

“Raisi gani?”

“Yule tuliye pishana naye jana?”

“Kwa hiyo baada ya kukuibia mkeo ukaona ukamjaze mimba mdogo wake?”

“Ndio mama malipo hapa hapa duniani”

“Hahahaha jamani kweli nimezaa”

“Ndio hivyo mama alininyanyasa na mimi nikampatia”

“Amesha jifungua?”

“Hapana hajajifungua bado”

“Ehee mwengine?”

“Mwengine ni mkweo wa kwanza”

“Nani?”

“Mama Shamsa”

“Nini?”

“Ndio mama Shamsa ametuzalia mtoto wa kiume?”

“Wa kwako?”

“Ndio”

“Wewe!!”

Mama akajawa na mshangao mkubwa sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Niambie una nitania Rashidi yaani kwa maovu yote uliyo tufanyia bado ume kwenda kumtia mimba nyingine hivi una akili wewe?”

Mama alizungumzaa kwa kufoka kidogo

“Ila mama subiri nikuadithie jinsi ilivyo kuwa usifoke tu kwa sababu hujui ilikuwaje?”

“Yaani yule mwanamke kwangu ni shetani. Mwanamke asiye na huruma hata kwa mtoto aliye mzaa kwa uchungu na kumuweka tumboni miezi tisa wewe hujaliona hilo tu.”

“Sasa mama nisikilize”

“Ehee niambie ilikuwaje?”

“Hiyo siku mama Shamsa alinitumia walinzi wake na wakaniteka. Walinipeleka mashambani huko kwa lengo la kutaka kunia”

“Una ona sasa”

“Si unisikilize sasa mama”

Mama akakaa kimya huku akinikata jicho moja kali.

“Ilikuwa hivi. Baada ya kuzinduka nilimkuta na walinzi wake na alitaka kuniua kwa manyanyaso makali sana. Ila nilifanikiwa kuwavamiwa walinzi wake na kuwau wote na baada ya hapo akabaki yeye mwenyewe, nilitaka kumuua ila adhabu niliyo iona ni nzuri ni kumbaka”

“Mpuuzi kweli wewe, hiyo nia dhabu au mulikuwa muna tamaniana. Una mbakaje mwanamke ambaye alikuwa mke wako.”

Nikaka kimya kwani mama anaonekana kucharukwa kwa kweli ana onyesha kuwa na chuki ya wazi wazi na mama Shamsa.

“Na huyo mtoto ana umri gani?”

“Ana enda mwaka wa nne”

“Sasa nahitaji umchukue, sihitaji alelewe na yule shetani. Ata mpandikiza chukio mtoto wako na atakuchukia wewe mwenyewe. Umenielewa?”

“Ndio mama”

Mama akatazama saa yake ya mkonini.

“Sasa hivi ni saa mbili, saa nne tuna elekea kule alipo kwenda Tina”

“Mama Tina yupo Tanga lakini?”

“Kwani Tanga ni mbinguni. Una mgari mkubwa huo si tuna kwenda na kurudi leo hii hii, sawa”

“Sawa”

“Tuna kwenda sisi wawili, nahitaji kumuona huyo mwanamke umenielewa”

“Sawa mama”

“Kabla ya kwenda huko tupite madukani tumnunulie zawadi”

“Mama kwani ni mke wa raisi tuna kwenda kumuona si…..”

“Ni mkwe wangu na ana mjukuu wangu tumboni. Japo nimeishi ulaya siwezi kusahau mila na desturi za kishwahili. Kumpelekea mkwe zawadi ni jambo la muhimu. Una nielewa?”

“Sawa mama”

“Jiandae na umuambie mkeo”

“Sawa”

Mama akanyanyuka na kuondoka, kweli mama yangu amebadilika, sasa hivi sio yule mama wa kimasikini kama miaka kadhaa ya nyuma. Hata uzee haujamla kama kipindi kile alivyo kuwa akizeeka kutokana na shida. Nikatoa simu yangu na kumpigia Tina.

“Vipi?”

“Salama mume wangu za wewe?”

“Namshukuru Mungu sanamani bwana jana sikukupigia kukuuliza ume fikaje?”

“Usijali kwa maana najua ulikuwa na bibi”

“Mama amefika?”

“Ndio amefika”

“Basi nina kuja na mkweo”

“Weee?”

“Ndio ametaka kuja kukuona leo hii hii na hapa tuna ondoka saa nne”

“Mungu weee naogopa. Haki kunifokea?”

“Kwa sababu gani?”

“Mmmmm, labda nime muiba mume wa mkwe wake wa ndoa”

“Hamna haji kwa sababu hiyo. Ana hitaji kuonana na wewe”

“Tuwapikie nini?”

“Chochochote”

“Sawa mume wangu”

“Baadae”

“Poa”

Nikakata simu, nikamuona Fatma akija eneo hili ikanibidi kuto kunyanyuka na kumsubiria. Akaingia katika kibanda hichi.

“Umeamkaje Rashidi”

“Salama, niambie”

“Safi aisee. Una mke mzuri”

“Nashukuru, jana ulikuwa kwenye msafara wa raisi?”

“Ndio na tulimpeleka hadi hotelini”

“Hoteli gani?”

“Serena”

“Anakaa hapo kwa muda gani?”

“Kwa siku kama nne hivi, ana subiria bunge kupiga kura ya kumuamini au kuto muamini”

“Okay”

“Vipi mpango wako mbona haujautekeleza?”

“Upi?”

“Si  wa kumuua?”

“Una hisi kwamba ni rahisi kama hivyo?”

“Najua sio rahisi ila ulisema uta muangamiza na nikasubiria sana kwa hamu kumuangamiza, ila imepita kimya kimya na hapa ninavyo ongea pesa nyingi sana ime mwaga kwa wabunge wampigie kura ya kumuamini na kurudisha madarakani”

“Okay”

“Ina bidi sasa tuwanunua hao wabunge na wampige chini na wakimpiga chini tuna rudisha mjadala kwenye chama na ina bidi tuweze kutafuta mgombea mwengine na tayari nimesha penyeza jina langu na kuna backup kubwa sana nitakayo ipata nyuma yangu kuhakikisha kwamba nina kuwa raisi”

Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikimtazama Fatma usoni mwake.

“Una wanunua kwa kiasi gani hadi uwaamini?”

“Kila mmoja ukimpatia bilioni moja hachomoi”

“Fatma hembu ngoja kwanza kuna jambo nilishuhulikie kwa sasa, kuna mahali nina mpeleka bi mkubwa hivyo hayo mambo mengine tutaongea nikirudi”

“Sawa, ila una onekana kama huna raha?”

“Ndio mambo ni mengi sana kwa sasa, hivyo hembu niache kwa wakati huu”

“Sawa Rashidi, hongera kwa mapacha una fanana nao yaani mtu hawezi kubisha kama ni wanao”

“Nashukuru”

Nikanyanyuka na kuelekea kwenye kiwanja wanacho cheza wanangu na Shabani. Wanangu wote wakanikimbilia na kunikumbatia kwa furaha. Nikasalimiana nao na wakarudi kiwanjani.

“Niambie ndugu yangu”

“Safi aisee. Nina kwenda Tanga na bi mkubwa?”

“Vipi kwema?”

“Yaa anata kwenda kumuona Tina”

“Ohoo tatizo hilo?””

“Yaani wee acha. Nakuonba uwatazame tazame hawa kipindi nikiwa sipo”

“Sawa kaka”

“Mimi ngojan ikajiandae”

“Sawa”

Nikarudi ndani, nikanywa chai na Jakcline na nikamueleza juu ya safari yangu na mama ila sikumuambia tuna kwenda Tanga kwa ajili ya kuonana mke mwenzie, zaidi nikamueleza kuna rafiki wa mama wa siku nyingi ana kwenda kuonana nao. Jackline hakuwa na kipingamizi wala maswali juu ya safari hiyo kwani nilimuambia tuna rudi leo hii hii. Nikajiandaa na mama naye akawa tayari, na tukaondoka nyumbani hapa. 

“Kariakoo kuta kuwa na nguo nzuri, twende huko kisha wakati wa kwenda Tanga tuna pita ule njia ya Bagamoyo”

“Sawa mama”

Ukimya ukatawala ndani ya gari hili. Tukafika Kariakoo na mama akaniomba nimsubirie kwenye moja ya sheli na yeye akaingia kwenye maduka haya. Baada ya nusu saa akarudi akiwa na begi kubwa.

“Kuna nini, mbona begi kubwa hilo mama?”

“Ni zawadi za mkwe wangu”

“Sawa”

Safari ikaanza rasmi huku gari ikiwa imejaa mafuta ya kutosha.

“Umesha muona huyo mwanao?”

“Yupi?”

“Wa ibilisi”

“Ndio”

“Ana fanania na wewe au mama yake?”

“Mimi”

“Ulifanyie kazi hilo nililo kuambia nahitaji huyo mtoto sitaki alelewe”

“Nimekuelewa mama”

“Na leo nahitaji ukamuhalalishe huyo Tina”

“Una maanisha nini?”

“Yaani leo hii hii nina toa mahari na leo hii hii muna funga ndoa. Kanzu na kila kitu cha ndoa kipo ndani ya hilo begi hivyo nalo hilo lielewe mapemaa sio tuna fika huko una anza kubabaika babaika”

Nikajikuta nikipigwa na mshangao mmoja mtakatifu kwani sikupanga kabisa kumuoa Tina kwa siku ya leo ila naona mama amechachamalia jambo ambalo sijui kama wazazi wa Tina wana weza kulikubali ikiwa sisi ni Waislamu na wao ni Wakristo.



“Masihara hayo mama”

“Haki ya Mungu una kwenda kumuoa huyo mwanamke, au unapenda unavyo zaa za nje ya ndoa KUmbuka watoto wa nje ya ndoa ni haramu?”

Nikamkata jicho moja kali mama hadi akajistukia mwenyewe kwani hata yeye mwenyewe amenizaa nje ya ndoa tena na mume wa mtu. Sikutaka kuongea chochote zaidi ya kuendelea kuendesha gari hili kwa umakini wa ahali ya juu. Ukimya ukatawala ndani ya gari hili, na nikazidi kusonga mbele, nikatoa simu yangu mfukoni na nikampigia Shabani.

“Ndugu”

“Niambie”

“Wapo salama hao?”

“Ndio wapo salama vipi?”

“Aisee nitafutie ramani ya hoteli ya Serena na niambie familia ya raisi imekaa upande gani na gorofa ya ngapi”

“Sawa kaka”

Nikakata simu.

“Mama”

“Abee”

“Hivi una jua mimi sasa hivi ni mtu mzima?”

“Ndio”

“Hivyo tafadhali wakati una zungumza jaribu kuchagua maneno ya kuongea na mimi, sipendi kukuvunjiua heshimiwa. Kwenye hili la maamuzi ya kumuoa Tina au kuto muona mimi ndio msemaji wa mwisho, si wewe wala mtu mwengine yoyote yule. Kama utatoa mahari, itolewe na sio kuoa. Siwezi kumvunjia sheshima Jackline nikafanya maamuzi ya kipumbavu ikiwa wewe una jua ni wapi Jackline amenitoa. Amefanya kila kitu kwa ajili yangu, yako na Shamsa. Ingekuwa mama wa Kiswahili niambie Shamsa sasa hivi angekuwa na hali gani kama siofanyakazi wa ndani. Ila amempa maisha, amempa mwanga amempa kila kitu ambacho hata mimi mwenyewe nimeshindwa kumfanyia ikiwa mimi ni baba yake. Alafu kirahisi tu una sema kwamba nikaoe ili mtoto atakaye zaliwa asiwe haramu. Sasa kama atazaliwa akiwa na chapa usoni mwake kwamba ni haramu basi acha iwe hivyo ila sio kumzalilisha mke wangu wa ndoa”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama mama usoni mwake.

“Sawa yaishe na usikimbize gari kwa mahasira yako, tusije tukafa bure”

“Nipo makini”

Majira ya saa saba mchana tukakanyaga ardhi ya jiji la Tanga. Nikampigia simu Tina kabla sijafika nyumbani.

“Vipi”

“Safi mume wangu mumefika wapi?”

“Tupo Kwa Minchi hapa. Vipi, nfani kuna kila kitu?”

“Nilifanya shooping ndogo tu mume wangu”

“Sawa”

Nikakata simu, nikaendesha gari hadi kwenye moja ya super makert,. Nikanunua vitu vyote vinavyo paswa kuwa katika jiko la mwanamke huku tukisaidiana na mama kwenye kuvichagua kwa maana yeye ndio ana jua nini mwanamke ana paswa kuwa nacho jikoni. Tukaelekea katika nyumba ninayo ishi.

“Kumbe ni mtoto wa kishua ehee, si kwa jumba hili”

Mama alizungumza huku tukisubiria geti lifunguliwe.

“Nyumba yangu hiyo”

“Weee?”

“Ndio nimeinunua na nilikuwa nina ishi naye hapa kabla ya kwenda kuishi naye Dar”

“Waooo kweli nimezaa kidume. Umewekaza hadi raha kweli yale maneno yako uliyo kuwa una niambia mama vumilia ipo siku nita kuwa tajiri leo yametimia”

“Ndio hivyo mama kuishi kwenye ndoto zako ni jambo muhimu haijalishi uta pitia nini au utapita wapi ilimradhi ufikeishe malengo yako”

Geti likafunguliwa na Tina.

“Waoooo”

Mama alizungumza huku akimtazama Tina aliye jipamba kisawa sawa.

“Ni mwanamke mzuri aisee”

Nikasimamisha gari eneo la maegesho. Tina akatufwata hapa akamsalimia mama huku akipiga goti moja chini.

“Shikamooo mama”

“Marahaba mwanangu, haujambo?”

“Sijambo mama, karibuni sana nyumbani”

“Nina shukuru sana.”

Tina akanikumbatia, nikampiga busu la mdomo.

‘Jamani mbele ya mama’

Tina alininong’oneza.

"Kawaidia mbona hiyo”

“Mmmmm naona aibu mwenzi. Mama karibuni sana ndani”

“Nina shukuru mwanangu”

Tina na mama wakaingia ndani, nikashusha mizigo na kuingiza ndani. Nikasalimiana na mama Tina ambaye yeye na mwanaye wamefanana kiasi kwamba huwezi kubisha kwamba ni tu na mama yake.

“Karibuni sana jamani”

Mama Tina alizungumza kwa furaha.

“Nashukuru sana mama yangu. Kuna mizigo ngoja nikamalizie kuishusha”

“Tina saidiana na mwenzako”

Tukatoka nje na Tina.

“Umefanana na mama yako?”

“Yaa mama kajizaa. Ila mume wangu mbona mavitu mengi hivyo”

“Si una jua mama mkwe wako, yaani ametaka kukuona leo nikawa sina jinsi”

“Nimefurahi kwa hilo amenithamini. Alafu baby ningeomba utuwekee walinzi. Yaani toka lile tukio la majambazi litokee nimekuwa muoga kama nini kuishi hapa, na ukiangalia mimi na mama ni wanawake”

“Ohoo pole sana mke wangu. Kuna kampuni gani ya ulinzi ambayo una ijua ni nzuri?”

“Ngoja nita kwenda hotelini pale nilipo kuwa nina fanya kazi nitawauliza wale walinzi wao wanawachukua kampuni gani”

“Mpigie basi bosi wa ile hoteli?”

“Sina namba yake, nilibadili namba”

“Okay nimekumbuka basi tuta enda. Twende tukawasikilize hao kina mama”

“Alafu nimekumbuka kitu mume wangu. Hatuwezi kuanza clinic hadi wewe uwepo”

“Una maanisha nini?”

“Yaani sheria za siku hizi ni lazima baba wa mtoto aliye tumboni naye aende clinic na mke wake, tupimwe kisha ndio huduma zina anza kwangu”

“Mmmm”

“Mbona una guna”

“Naona utaratibu mpya huo”

“Mbona upo huo mume wangu. Kwani Shamsa alivyo zaliwa hukwenda na mama yake hospitalini?”

“Hata sikumbuki”

“Basi mambo yamebadilika hivyo mume wangu”

Baada ya kumaliza kuingiza mizigo yote tukarudi sebleni na kuwakuta wazazi wetu wakicheka kwa kufurahi kana kwamba ni watu wanao fahamiana kwa kipindi kirefu sana.

“Rashidi nimezungumza na mkwe wako hapo. Ina bidi kesho twende kwa wakwe zako tukatoe mahari”

Nikatabasamu huku nikimtazama mama usoni mwake.

“Mama huyu ndio mume wnagu mtarajiwa ana itwa Rashidi. Rashidi huyu ndio mama yangu mzazi ndio mama Christina”

“Nashukuru sana mama yangu kwa kukufahamu?”

“Nashukuru hata mimi pia”

“Tina huyu ndio mama yangu naamini leo ndio mara ya kwanza kumuona. Ana ishi nchin Ufaransa

“Nashukuru kukufahamu mama na karibu nyumbani”

“Asante nime karibia mkwe wangu. Kweli mwanagu amejua kuchagua chombo cha ukweli. Kwa kweli wewe ni mzuri sana”

“Asante sana mama yangu”

“Namuomba mwenyezi Mungu ajalie uweze kuzaa mjukuu wangu mwema na mwerevu”

“Asante sana mama. Ngoja niwaandalie chakula kwani ni wakati sasa wa kula huu”

“Sawa mwanangu”

Tina akaondoka sebleni hapa na kutuacha sisi watatu.

“Baba unajishuhulisha na nini?”

“Ahaa mimi ni mfanya biashara mama yangu”

“Oohoo sawa sawa mwanangu. Nimezungumza na baba Tina ameomba sana tuweze kwenda nyumbani kwani mimi ni mama tu siwezi kupokea mahari. Hivyo kwa mila na desturi zetu ina bidi muje na mshenga ndio tuna weza kuwapokea”

“Sawa mama hilo halina shida”

Tina akaanda chakula kisha kwa pamoja tukajumuka mezani na tukaanza kula.

“Waooo chakula ni kitamu sana. Mwanangu una weza kupika sana”

“Nashukuru sana mama”

Tukamaliza kula kisha mama na Tina wakaingia ndani kwa ajili ya kupeana zawadi zao.

“Una umri gani?”

“Mwezi ujao nina fikisha miak thelathini”

“Ni umri mzuri kwa kijana kuanzisha familia”

“Ni kweli mama”

“Umesomea maswala gani”

“Una maanisha nini mama?”

“Yaani ukiachana na biashara umesomea nini?”

“NImesomea biashara mama”

“Ahaa sawa sawa mwanangu. Mungu awatangulie”

“Amen”

Mama akatoka chumbani na kurudi sebleni hapa.

“Mazazi mwenzangu kuna zawadi nimezileta zipo chumbani”

“Ohoo ngoja nikazione mzazi mwenzangu”

Mama Tina akanyanyuka na akaondoka sebleni hapa.

“Ila maama si tunakuja na kugeuza, hiyo safari ya kesho ita kuwaje?”

Nilizungumza kwa sauti ya chini chini.

“Kwani kuna ubaya gani tukalala hapa siku moja”

“Ila kumbuka mke wangu yupo Dar nimemuacha mwenyewe?”

“Amekaa mbali na wewe kwa kipindi gani hadi uhofie leo.”

“Ila alikuwa kwao, ila huku ni kwetu, lazima niwe mwenyeji na nimtembeze sehemu nyingi nyingi”

“Bwana weee. Acha tutoe mahari tummilikia huyu binti. Wewe huoni binti amesimama vizuri yule.”

“Mama”

“Hakuna cha mama, nimeongea na rafiki yangu ni mzee mzee yupo Lushoto na nimemuelezea hiyo familia ya binti na ameifahamu. Hivyo yupo tayari kuwa mshenga”

“Sawa kwenye kutoa barua pamoja na mahari kwani lazima niwepo?”

“Wewe ndio lazima uwepo”

“Mama una yakimbiza sana haya mambo nina mambo mengi sana ya kufanya”

“Mimi nataka kuiwahi hii mimba, mtoto akizaliwa faini ita kuwa kubwa zaidi”

“Mama kwani shida ni pesa. Kuishi maisha yetu haya una ogopa faini. Mbona faini ni jambo la kawaida tu”

“Kesho tuna kwenda kutoa mahari kwa wakwe zako. Tutaondoka wote wanne”

“Amesema ni Lushoto hapo juu?”

“Ndio”

“Basi tuondokeni leo. Kesho asubuhi tuna fanya yaliyo tetu kisha tuna ondoka”

“Sasa hilo ni jambo la kumuuliza mkwe wako kama ina wezekana”

“Mama yaani una penda kukurupusha watu hiyo tabia umeitoa wapi?”

“Mume wangu huwa ana penda kuyapeleka mambo chap chap ndio maana sasa hivi ana kwenda kufungua kampuni ya ndege, sasa wewe kuwa lazy lazy uone matokeo yake”

“Daaa, yaani uta nifanya……”

Nikaikatisha sentesi yangu mara baada ya kumuona Tina akitoka ndani hapa akiwa amevalia gauni moja zuri lililo mkaa vizuri mwilini mwake.

“Mama nashukuru san anime pendeza ehee?”

“Sana mkwe wangu, yaani una vutia sana. Mwanangu hajakosea kukuchagua aisee”

“Tina jiandae twende kwenye ile hoteli tuulizie walinzi ina kuwaje kuwapata”

“Sawa baby”

Tina alizungumaza kwa furaha

“Yaani kusema kweli damu yangu na huyu binti zimeendana sana”

Mama alizungumza huku akimtazama Tina akiondoka sebleni hapa.

“Na Jack je?”

“Zimeendana sana ila wewe mwenyewe umedumisha mila za kiafrika za kuazaa zaa sana hivyo mimi nikiwa kama mama sipaswi kuleta ubaguzi kwa wakwe zangu wote ina bidi niwapende na hiyo ndio kawaida yangu hata kipindi kile tulipokuwa tuna ishia na mama Shamsa. Mama mkwe akauridi sebleni hapa.

“Mama samahani”

“Bila samahani baba yangu”

“Hivi tuna weza kwenda Lushoto leo, kesho asubuhi tukatoa mahari na nikawahi kikao Dar es Salaam kwa maana kuna wafanya biashara kutoka Dubai kesho nina hitaji kuonana nao”

“Ina wezekana baba yangu. Pole sana kwa mihangaiko mwanangu”

“Asante”

“Wafanya biashara siku zote huwa wana kuwa bize hadi mambo ya muhimu wana yasahau”

Mama alizungumza huku akinitazama”

“Tayari mume wangu”

Tukawaaga wamama hawa na kuondoka nyumbani hapa.

“Haki ya Mungu mume wangu nina kupenda sana na nina shukuru sana kwa mama mkwe kunipenda na kunikubali kwa kiasi hichi. Yaani nilihisi mama mkwe ana kuja kunifokea au kunisema vibaya kumbe ni mwanaa mama mmoja mcheshi sana”

“Mzee ndivyo alivyo”

Tukafika katika hoteli ambayo Tina alikuwa ana fanyia kazi, tukapokelewa vizuri na wafanyakazi wezake na akasalimiana nao kwa furaha.

“Jamani umenenepa”

“Maisha tu shosti yangu. Una kula nini jamani?”

“Vyakula hivi hivi”

“Yaani, huyu ndio shemeji yetu?

“Ndio ni mume wangu mtarajiwa”

“Waooo hongera sana. Karibu sana shemeji”

“Nashukuru sana.”

“Vipi mumekuja kulala?”

“Hapana, tumekuja kumuulizia meneja.”

“Meneja yupo ofisuni kwake, karibini sana”

“Tuna shukuru”

Tukaingia ofisini kwa meneja wa hoteli hii naye akajawa na furaha kumuona Tina, tukatambulishana na moja kwa moja Tina akazungumza kilicho tuleta hapa.

“Kampuni ina itwa J.I.M.S ofisi zao zipo hapo barabara ya kumi”

“Tuna shukuru sana”

“Ngoja niwape namba ya mkurugenzi wao”

“Asante sana”

Tukaga na kuondoka, tukafika katika ofisi za kampuni hii ya ulinzi. Tukajaza fomo na tukaomba ulinzi wa walinzi wanne. Wawili wata kuwa wana linda asubuhi hadi saa kumi na mbili na wengine wana ingia saa kumi na mbili hadi asubuhi. Nikalipia kiasi kinacho paswa kuliowa kwa huduma ya ulinzi huu, tukapewa walinzi wawili wa kuanza nao na tukaongoza na gari lao hadi nyumbani kwangu. Nikawaonyesha mazingira ya nje ya nyumba hii na kazi ikaanza haraka sana. Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuiona namba ya Shabani.

“Niambie kaka?”

Nilizungumza huku nikisogea eneo ambalo nina weza kuzungumza bila mtu yoyote kusika”

“Salama ndugu yangu. Vipi mumefika salama”

“Ndio kaka tumefika salama. Ehee niambie umefikia wapi?”

“Nimefanikiwa kupata full details za wapi alipo lala mzee na ramani ya hoteli nzima. Kama ina wezekana ndugu yangu hii kazi tuifanye leo hii hii kwani nasikia kesho ana hamia mjengoni”

Nikajikuta nywele na minyweleo vikisimama kwa kunisisimka, kwani nafasi ya pekee kumua raisi ni leo na kesho mama amepanga kwenda kutoa mahari ya Tina kitu ambacho kina nifanya nibaki njia panda.



“Sawa nina kupatia jibu soon, nitumie hiyo ramani ya jengo kwenye simu yangu”

“Poa kaka

Nikakata simu huku nikishusha pumzi nyingi. Nikajifikiria kwa dakika kadhaa kisha nikaingai ndani.

“Mama nakuomba mara moja”

Tukatoka nje huku mama akinitazama.

“Nina hitaji kurudi Dar es Salaam haraka iwezekanavyo. Si una weza kuendesha gari?”

“Ndio ninaweza ila ngoja kwanza. Una kwenda kufanya nini?”

“Kuna kazi muhimu sana ambayo imetokea. Inanipasa kuifanya usiku huu huu”

“Lakini wewe mwanangu kwa nini una kuwa hivyo. Si unajua kesho ina umuhimu na wazazi wake wanataka kukuona?”

“Kwani huyu ni nani yake si mama yake, ameniona yeye inatosha. Ataniona siku nyingine bwana mama. Kwa sasa nakuomba nikafanye kazi yangu. Kwa sasa nahitaji nikatekeleze majukumu yangu muhimu. Nahitaji kupanda ndege hapo nampigia simu Shabani ata nipokea uwanja wa ndege”

“Yaani una nitia aibu wewe, hizo kazi huwezi kuzisogeza mbele tukamaliza hili”

“Kati ya milioni mia na kwenda kutoa mahari kipi kina manufuaa?”

Mama macho yakamtoka huku akinitazama kwa kunidadisi.

“Rashidi”

“Naam”

“Usisahau mimi ni mama yako. Una nidanganya?”

“Mama nakudanganya nini, unahisi mali hizi zote mama zimekujaje kujaje ehee?”

“Kama ni kweli Mungu akubariki ufanikiwe ila kama ni uongo huto fanikiwa”

“Mama”

“Nakuambia ukweli kama una nidanganya huto fankiwa na si unajua baraka za mama ndio muhimu kwa mwanaye yoyote””

Nikashusha pumzi huku nikimtazama mama usoni mwake.

“Sawa nenda”

Mama alizungumza huku akianza kutembea kuelekea ndani.

“Mama ngoja kwanza”

“Ehee niambie”

“Iko hivi una tambua kwamba nina maadui zangu na maadui ninao wawinda ni DON pamoja n raisi aliye mchukua mama Shamsa. Wiki kazaa nilipo kuwa nchini Madagascar waliniteka na kutaka kuniua ndio maan auna ona hapa mkononi badi nina kidonda kinacho elekea kupona kutoana ajali waliyo nisababishia. Hivyo wamekuja nchini Tanzania. Raisi huyu ana hitaji kurudishwa madarakani, na alitaka kunia dhahiri. Isitoshe mwaangu Ruben naye yupo mikono ambayo sio salama. Raisi ametambua kwamba Ruben sio mwanaye japo mama Shamsa hajalitambua hilo”

“Ulijuaje?”

“Walipokuwa wameniteka, nilizimia. Hivyo baada ya kuzinduka nilimuona yeye na DON wakizungumza na akakiri kabisa kwamba ana taka kuniua kwa mateso tena nikiwa nimezinduka. Nikamsikia akisema kwamba anajua kabisa Ruben sio mwanaye na ata hakikisha kwamba nina jutia kwa nini nime tembea na mke wake pamoja na mdogo wake na kuwapatia ujauzito. Sasa mtu kama huyo ikiwa yupo sambaba na Don ambaye alisha fika hadi nyumbani pasipo nyinyi kujua, hapa una hisi ni nini kinacho kwenda kutokea mama”

“Una maana gani alifika nyumbani?”

“Kuna siku ambayo Jackline alikuja nyumbani na mfanya biashara anaye itwa Philipe Frenandes?””

“Ndio nakumbuka ilikuwa ni part ndogo na tulipata naye chakula cha usiku”

“Sasa huyo Philipe Frenandes ndio Don”

“Mungu wangu!!”

Mama alihamaki.

“Ndio hivyo adui amesha ingia kwenye biashara za mke wangu. Sijui ata kuwa ana fikiria nini au ana mpango gani ila kwa sasa ni mwendo wa kupigana naye. Mbaya zaidi mupo na mimi hapa nchini Tanzania, hivyo ana weza kumdhuru, ni lazima nihakikishe kwamba adui yangu nina muwahi kabla hajatuwahi”

Mama kaka kimya kwa muda kidogo.

“Kwa hiyo Dar una kwenda kufanya nini?”

“Nina kwenda kumuua yule raisi kabla hajarudishwa nadarakani”

“Una weza ukalifanya hilo mwanangu?”

Mama aliniuliza kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Ndio mama nina weza”

“Kaifanya kikamilifu kidume change. Hakikisha kwamba safari hii ushindwi na hukamatwi wala kugundulika. Kwa mateso aliyo tupitisha mpige risasi ya mbili za miguu kwa niaba yangu”

Maneno ya mama yakanipa ukakamavu wa hali ya juu.

“Nashukuru sana mama yangu”

“Hakikisha una fanya hivyo”

“Usijali mama yangu”

Mama akanikumbatia kwa nguvu na hapa nikazidi kuhisi upendo wa mama. Nikamuachia mama kisha kwa pamoja tukarudi ndani.

“Mama, nimepata dharura kidogo hivyo nina omba niondoke. Naomba Tina na mama wanisindikize uwanja wa ndege niwahi kuelekea Dar es Salaam”

“Kwema huku baba?”

“Ndio kwema mama”

Tina akataka kuzungumza jambo ila akajizuia. Baada ya kuaga, tukaondoka nyumbani hapa na Tina pamoja na mama yangu.

“Kuna nini mume wangu, nilitaka kukuuliza mbele ya mama pale ila nikahisi utajibu kwa maelezo mengi”

“Kuna ishu nina kwenda kufanya na Sheby hivyo ina bidi niondoke usiku huu huu”

“Sawa mume wangu”

“Ngoja nimpigie simu Sheby”

Nikampigia simu Shabani.

“Kaka”

“Nipo njiani nina enda airport naomba unipokee kwenye airport ya Dar.”

“Poa kaka hakuna shaka, ramani uliiangalia?”

“Sijaifungua bado ila nikiwa angani nita ifungua na kuiangalia kwa umakini mkubwa.”

“Sawa hakikisha una icheki kaka kwani kama nikutekeleza hili jambo tutekeleze usiku huu huu”

“Usijali ndugu yangu”

“Una rudi na mama?”

“Hapana mama nina muacha huku”

“Sawa kaka”

Nikakata simu na safari ikaendelea. Tukafika kiwanja cha ndege, nikafanya utaratibu wa kukodi ndege ndogo binafsi na nikafanikiwa kupata ndege moja.

“Rashidi”

“Ndio mama”

“Nahitaji uwe makini sawa”

“Usijali mama yangu”

“Safari hii narudia usifanye makossa”

“Usijali mama utapata matokeo hivi karibuni”

“Sawa mwanangu”

Nikakumbatiana na mama kisha nikamsogelea Tina, nikamkumbatia na nikamnyonya denda.

“Usinisahau mume wangu”

“Usijali siwezi kukusahau”

Mara baada ya kuachana nao nikaingi ndani ya ndege hii na tukaondoka uwanjani hapa. Tukafika jinini Dar es Salaam majira ya saa tatu usiku, nikatoka nje ya uwanja na nikaingi akatika gari alilo kuja nalo Shabani.

“Vipi zile bunduki umekuja nazo?”

“Hapana nimeziacha nyumbani, si unajua ulinzi sasa hivi ni mkubwa sana una weza kusimamishwa na askari alafu gari likafanyiwa uchunguzi na mambo yakawa sio mambo”

“Sawa sasa sihitaji Jackline atambue kwamba nipo Dar”

“Kwa nini?”

“Hii kazi nahitaji kuifanya kimya kimya”

“Kaka yule ni mke wako, anapaswa kujua ishu kubwa kama hii, ili likitokea la kutokea ana ondoka na wewe au ana kusaidia kwa namna nyingie”

Nikajifikiria kwa muda kisha nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba nimekubaliana na wazo la Shabani. Tukafika nje ya nyumba yangu.

“Tusiingie ndani. Kachukue mzigo na muambie Jackline aje anikute hapa, nikiingia ndani watoto wana weza kutupotezea muda”

“Sawa kaka”

Shabani akashuka ndani ya gari baada ya dakika tatu, Jackline akatoka ndani huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Nikakumbatiana naye.

“Sijaamini shem alivyo niambia kwamba upo hapa nje. Vipi mbona hauingii ndani?”

“Usijali mke wangu, leo nahitaji kuikamilisha ile kazi”

“Kazi gani?”

“Kumuua yule raisi”

“Usiku huu?”

“Ndio mke wangu”

“Umejiandaa lakini?”

“Ndio mke wnagu nimejiandaa kwa kila jambo”

“Ndio maana nina kupenda mume wangu upo tayari kwa kila jambo na wakati wowote tu”

Shabani akatoka ndani hapa akiwa na begi la mgongoni, akafungua mlango wa siti ya nyuma ya gari kisha akaingiza begi hili.

“Nakuomba ukae tayari na watoto lolote litakalo jitokeza basi mutakuwa tayari kunifwata kule nitakapo kwenda. Sasa hivi sihitaji kuwaacha peke yenu. Nakwenda kuifanya kazi ambayo aitaisaidia familia yetu. Sawa mke wnagu”

“Usijali mume wangu, nina kuelewa sana”

“Tukimalizana na huyu ni zamu ya Philipe”

“Sawa mume wangu, hakikisha una kuwa salama”

“Asante mke wangu”

Tukaondoka nyumbani hapa, tukiwa ndani ya gari nikapata sasa wakati mzuri wa kuitazama ramani ya hoteli nzima ya Serena.

“Hatuwezi kumuua tukiwa gorofa ya pili kwa kumdungua”

“Sidhani kwani hiyo ni hamsini kwa msini una weza kukuta vioo vina bullet proof risasi ikashindwa kupenya au unaweza asisimame dirishani tuna mpataje”

“Hilo nalo ni wazo zuri ila kuingia ndani ya hoteli na kufanya shambulizi ina weza kuwa hatari zaidi ya kumdungua. Kama chumba chake ni hichi basi tuta muua kupitia hapa hapa dirishani”

“Sawa kaka”

Tukafika kwenye moja ya gorofa linalo tazamana na hoteli ya Serena. Tukapandisha juu ya gorofa hili.

“Kuna baadhi ya vifaa niliongezea”

Shabani alizungumza akatoa darubini na akanikabidhi. Nikaanza kutazama dirisha la chumba anacho ishi raisi.

“Naona kuna ukimya”

Nilizungumza huku nikitazama dirisha hilo.

“Au wamelala?”

“Sasa hivi ni saa sika kasoro ila nina ona taa bado ina waka”

Nilizungumza huku nikitazama eneo la chini katika hoteli hii na kuona jinsi walinzi wanavyo katiza katiza. Nikafungua begi hili na kutoa bunduki yenye uwezo wa kushambulia kwa masafa marefu. Nikaikoki vizuri na kuielekezea kwenye dirisha hilo.

“Akifa huyu mshenzi nita shukuru sana”

Nilizungumza huku tukiendelea kusubiria kama ata katiza kwenye dirisha nifanye shambulizi kisha tuondoke. Tukaka eneo kwa lisaa moja na nusu hadi tukajikuta tukikata tamaa.

“Kaka hembu cheki kule”

Shabani alizungumza huku akinipoa darubini hii. Nikatazama eneo la dirishani nikaona kuna mtu akishuka kwa kutumia kamba ngumu akitokea juu kabisa ya dirisha.

“Hembu shika”

Nikainyanyua bunduki hii ambayo nayo ina lensi yenye uwezo wa kumvuta mtu kwa karibu. Nikamvuta mtu huyu kwa ukaribu sana na nikagundua ni mwanamke ila alivyo valia amevalia kama ninja.

“Leticia”

Nilizungumza huku moyo ukiwa umejawa na furaha. Nikaielekezea bunduki hii chini na kuwaona walinzi wakiendelea kuwa bize na mambo yao.

“Ni yule demu kwa Kibrazil?”

“Ndio”

“Kumbe bado yupo”

“Tushuhudie shuhuli”

Nikamuona Leticia akiingia katika dirisha la chumba cha raisi. Galfa taa zikazima hivyo kinacho endelea ndani ya chumba hicho mimi na Shabani tukabaki kimya. Baada ya dakika kama kumi hivi nikamuona Leticia akitoka dirishani, akadanida kamba yake na kupanda juu ya jengo hilo na akapotelea gizani.

“Aisee tuondoke”

Niliuzungumza huku nikiifunga bunduki hii. Tukaondoka na kuiongia ndani ya gari na taratuibu tukaondoka eneo hili.

“Aisee atakuwa amemuua kweli?”

“Hata sijui ndugu yangu”

“Ngoja tukasikilizie aise kwa maana hii show imepigwa na mtu mmoja”

Nilizungumza huku nikimtazama Shabani jinsi anavyo endesha gari hili kwa mwendo wa kawaida. Tukafika nyumbani hapa. Nikakutana na Fatma akielekea katika gari lake.

“Vipi mbona juu juu?”

“Nimepokea habari kuna uvamizi umetokea hoteli alipo lala raisi”

“Duu”

“Ngoja nikacheki hali halisi iliyo toke. Baadae”

“Tuongozane?”

Nilimuuliza Fatma akanitazama kwa muda.

“Sawa twende”

“Poa, Sheby muambie wife nimetoka”

“Sawa kaka”

Tukaingia katika gari na kuondoka eneo hili.

“Wanasemaje?”

“Wanasema raisi amevamiwa yeye na mke wake ndani ya chumba chao cha kulala. Ikiwa ulinzi ulikuwepo wa kutosha na hakuna aliye ingia wala kutoka ndani ya hoteli”

“Sasa amevamiwa vipi?”

“Yaani hapo ndio nina jiuliza imekuwaje”

“Sasa huo ndio ushindi kwako”

“Ahaa wapi, hii ishu itakuwa ni kubwa”

Simu ya Fatma ikaanza kuita na akaipoke.

“Ndio mwenyekiti”

“Muhimbili ehee?”

“Sawa nina kuja huko”

Fatma akaendelea kuendesha gari hili kwa mwendo wa kasi sana.

“Raisi amepelekwa Mhimbili hivyo ina bidi twende huko”

Fatma alizungumza huku mwendo wa gari hili ukizidi kuongezeka. Tukafika hospitali ya Muhimbili na kukuta ulinzi ukiwa ni mkali sana. Moja kwa moja tuaelekea kwenye eneo ambalo raisi amepelekwa, nikamkuta mama Shamsa, Caro pamoja na watu wengine wakiwa kwenye kordo hii. Caro akanikumbatia na kunibusu huku akilia.

“Vipi mpenzi?”

“Kaka ametaka kuuwawa”

Caro alizungumza huku akilia kwa uchungu sana. Nikamuona mama Shamsa akitetemeka kwa woga huku mikono yake ikiwa ina damu.

“Usijali hali yake ita kuwa salama”

Caro akandelea kunitazama hadi Fatma akanitazama kwa jicho la wivu.

“Kweli mume wangu?”

“Ndio”

Nikamkalisha Caro kwenye eneo alilo kuwa amekaa. Nikamtazama mama Shamsa naye akanitazama kwa macho ya wasiwasi na woga mwingi. Sikutaka hata kuzungumza naye nikatafuta sehemu nikasimama huku nikiwatazama walinzi walipo eneo hili.

“Huyu kumbe ni demu wako pia”

Fatma alizungumza kwa sauti ya chini huku akiwa amesimama mbele yangu. Kabla hata sijamjibu mlango wa chumba alicho ingizwa raisi ukafunguliwa. Daktari akatoka huku akivua gloves zake, akavua miwani yake na kuwafanya watu wote kusimama mbele yake ili kumsikiliza ni nini anacho kizungumza.

“Tumejaribu kadri ya uwezo wetu kuyaokoa maisha ya raisi wetu, ila kwa bahati mbaya raisi wetu amefariki majira ya saa kumi usiku na dakika tano. Poleni sana ten asana”

Kauli ya daktari huyu ikanifanya nishushe pumzi nyingi sana huku moyo wangu ukiwa umetawaliwa na furaha kubwa sana kwani nilicho kuwa nina kihitaji sasa kimekamilia. Adui aliye salia ni DON pekee.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG