Search This Blog

Saturday, February 6, 2021

RISE UP SEHEMU YA 3/10

  

RISE UP

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 3 KATI YA 10



Nikamuona Jackline akitoka katika chumba cha baba yake. Akaniita kwa ishara na nikamfwata.

“Njoo nikutambulishe rasmi kwa baba ila samahani kwa hali aliyo kuwa ameionyesha pale awali”

“Usijali mke wangu”

Tukaingia ndani na muda huu kidogo baba mkwe hayupo katika hali ya hasira.

“Rashidi una mpenda kweli mwanangu?”

“Ndio baba”

“Hujafwata utajiri wake?”

“Hapana kwa maana mapenzi sio pesa kwani pesa zina kuja na kutoweka”

“Sawa, nina kushukuru kwa yote uliyo yafanya na pia kuwa na mwanangu katika kipindi chote cha matatizo”

“Nashukuru nawe pia.”

“Nina hitaji kuzungumza na mama yako pamoja na hao mashehe ikiwezekana waweze kuletwa hapa”

“Sawa baba ngoja niwapigie walinzi wawalete”

Jackline aliuzngumza na akatekeleza jambo hilo.

“Kazi yako ni nini kijana?”

“Mimi ni mpiganaji wa ulingoni”

“Unapigana ngumi za aina gani kwa maana mwanangu ni mpiganaji kick boxer?”

“Mimi pia nipo kwenye kick boxer na ngumi za mtaani”

“Ohoo safi sana”

“Baba wanajiandaa na wanakuja”

Jackline alizungumza mara baada ya kumaliza kuzungumza na simu.

“Sawa, Jack ameniadithia historia yako na amenielezea juu ya hao kina DON”

Nikamtazama Jackline usoni mwake.

“Ila usiwe na shaka, jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba nime amka na madakari wameniambia vyakula vya lishe vita nisaidia kuujenga mwili ndani ya wiki moja kisha wata niruhusu kurudi nyumbani. Rashid najua mwanangu hapa ni mjamzito”

“Ndio baba”

“Nitahitaji umlinde kwa namna yoyote na usiogope vita iliyopo mbele yetu kwa maana ulitumwa kutuangamiza ila nikuhakikishie kwamba sasa tuta wageukia wao”

Baba mkwe alizungumza kwa msisitizo na dhairi sasa nikaanza kuona picha yake halisi kwamba naye na kina DON ni wale wale tu.

“Hakuna shaka baba”

Baada ya nusu saa mama, mjukuu wake pamoja na mashehe wakafikishwa hospitalini hapa na baba mkwe. Kwanza baba mkwe akaomba azungumze na mama peke yake na watu wote tukaa nje.

“Vipi shehe wangu majibu mumesha pata?”

“Ndio shehe”

“Wameona ana mapacha?”

“Wamesema kwamba ni mjamzito tu. Nina imani siku zitakavyo kwenda huko mbeleni ndio wata gundua kama ni mapacha au laa”

Nilizungumza na Shehe huku tukiwa tumesimama mita chache kutoka sehemu alipo kaa Jackline pamoja na Shamsa.

“Sawa sawa”

“Alafu shehe kuna jambo moja lina nisumbua”

“Jambo gani?”

Ikabidi nimuelezee shehe uhusiano wangu na DON na nikamuelezea vitisho alivyo nifanyia.

“Shehe wangu huo ni mtihadi?”

“Tena sio mdogo shehe, hivi watu kama hawa hatuwezi kuwasomea albadili wakafilia mbali?”

“Hahaha hapana shehe wangu. Jambo kubwa ni kumuomba mwenyezi Mungu aweze kutuepusha nao hao wabaya kwa maana hao watu wana nguvu kutoka kuzimu”

“Nguvu kutoka kuzimu?”

Niliuliza kwa mshangao. Mama akatoka katika chumba cha baba mkwe na kumuita shehe na kijana wake na wakaingia kwa pamoja ndani hapao huko. Nikaka pembeni ya Jackline huku walinzi wakiwa wamesambaa katika kordo hii ndefu.

“Baba yako ana onekana sio mtu wa masihara kabisa?”

“Yaa sio mtu wa masihara. Ni mkali sana ndio maana wame mlisha madude dude hadi ina onekana ni saratani”

“Mmmm kweli ata nikubali?”

“Mbona amesha kukubalo na amefurahi kwamba ana kwenda kupata wajukuu”

“Alafu mke wangu kuna jamb o muhimu sana una paswa kulifahamu”

“Jambo gani hilo mume wangu”

“Kuna mtu nina hisi katikati ya walinzi wako ana peleka habari nyeti kwa DON”

“Mmmm kwa walinzi wangu sidhani, kwani kume tokea nini?”

“Kuna muda DON alinipigia nikiwa hapa nje. Akaanza kunifokea sijui nimeleta mashehe wamemuombea baba hadi amezinduka. Akanipa maagizo ya kumsambaratisha baba mkwe la sivyo aya wasambaratisha nyinyi nyote kisha animalizie na mimi”

Jackline akashusha pumzi nyingi huku akinitazama,

“Sasa ni nani ambaye ata kuwa amejua hili jambo?”

“Sijui mke wangu kwa maana amenipigia simu muda si mrefu cheki, ni dakika thelathini nzilizo pita”

Nilizungumza huku nikimuonyesha Jackline, muda ambao DON alinipigia.

“Mume wangu ina bidi tuwe makini sana kwa maana haya mambo ni mapana kuliko tunavyo yachukulia”

“Usijali mke wangu, nita hakikisha kwamba nina kulinda wewe na wanangu wanao kuja”

“Una maanisha nini kusema wanangu wanao kuja?”

Jackline alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Shamsa na huyo anaye kuja na watakao zaliwa ni lazima nihakikishe nina walinda. Sawa mke wangu”

“Nashukuru sana Rashidi wangu nina kupenda sana, umenifanya niwe mwanamke ambaye nilikuwa nina wazia siku nije kuishi maisha haya”

“Nashukuru mke wangu. Baadae nita hitaji kukuomba kitu”

“Kitu gani baby”

“Sio vizuri mtoto akakisikia”

Baada ya dakika ishirini, mashehe na mama wakatoka ndani ya chumba hichi huku wakiwa na nyuso zilizo jaa furaha.

“Shehe wangu nashukuru sana kwa maana kwa kazi hii naona mwenyezi Mungu ameamua kunyoosha mkono wake wa heri.”

“Una maanisha nini shehe?”

“Mzee bwana ametupa dola milioni moja ya kimarekani kwa pesa zetu za kibongo ni sawa na kama bilioni mbili na amehiadi kutuwezesha kujenga msikiti mkubwa sana ambao Afrika nzima haujawahi kutokea. Na kingine alicho tufurahisha zaidi ni kwamba ameomba abadilishe dini na tumemsilimusha ndani hapo”

Jackline macho yakamtoka kwa mashangao kwa maana kusikia baba yake amebadilisha dini ni jambo la mshangao.

“Baba yangu au mwengine ndio amebadilisha dini?”

“Baba yako, kwa muujiza wa mwenyezi Mungu ameamua kubadili dini na amesema akipona ata kuja nchini Tanzania na sisi tutakuwa wenyeji wake. Anahitaji kuendelea kuishi kwenye maisha ya kumcha Mungu sasa”

“Anayo yazungumza shehe ni kweli kabisa”

Mama aliunga mkono shehe. Mimi na Jackline pamoja na Shamsa tukaingia ndani hapo.

“Wooo muna mtoto mzuri sana”

Baba mkwe alizungumza huku akimtazama Shamsa usoni mwake.

“Tuna shukuru sana baba”

Nilijibu huku nikiwa nina furaha.

“Baba ni kweli umebadilisha dini?”

“Ndio mwanangu. Nina jua sija kushirikisha ila kwa hii nafasi ambayo Mungu amenipa na kuishi tena, sihitaji kurudi kwenye yale maisha ya kikatili, dhuluma na roho mbaya. Sasa hivi nina hitaji kuishi kwa kumpendeza Mungu.”

“Wooo ni jambo zuri baba. Ila kuna hawa kina DON wana mtishia mume wangu na kumuambia kwambwa watatumaliza”

“Hao lazima tushuhulike nao, kuwa mwema kwangu siwezi kuacha familia yangu iteseka ni lazima nihakikishe kwamba nina dili na mmoja baada ya mwengine”

“Na harusi yenu ambayo DON ana hitaji kuifanya ni ya kifahari sihitaji ifanyike kwa pesa zake. Nikitoka hospitalini nita panga mimi ifanyike vipi na wapi. Sawa”

“Sawa baba”

“Rudini nyumbani muka mpumzike”

Tukaagana na baba mkwe na tukarudi nyumbani.

“Niambie mume wagu ulikuwa una niambia kuna jambo una hitaji tuzungumze nyumbani”

Jackline alinisemesha huku tukiwa tuna ingia ndani kwetu.

“Vita hii ya DON nina hisi ina wenda kupamba moto. Nina hitaji tufanye jambo moja”

“Jambo gani baby”

“Nahitaji kupata mafunzo ya kijasusi. Nahitaki niwe fiti zaidi ya hapa nilipo kwa maana kama unavyo jua nilipita mafunzo ya ulinzi tu wa kawaida na na kikwetu kule ni ngazi ya chini sana kuwa mlinzi wa madukani”

“Ahaa hilo halina shida mume wangu ila utayaanza mara baada ya daktari kukuruhusu kufanya”

“Usijali mke wangu”

“Ila mume wangu usije ukamueleza DON kwamba ume kataa kuifanya kazi yake”

“Ila mke wnagu nina hisi jamaa kama vile ananitazama kila ninapo kwenda”

“Najua lazima aweke watu wake wa kukufwatilia.”

“Ila nikikamilika nita muua mimi mwenyewe”

“Mmmm”

“Usigune ila hiyo ndio anahadi ninayo kuambia”

Majira ya sala ya saa mbili usiku, mashehe wakaanza kunisomea kisomo cha kwangu peke yangu. Kisomo changu kikadumu kwa masaa mawili na kikaisha.

“Mwanao ata kuja kuwa mtu mkubwa sana huko mbeleni, shehe wangu”

“Kweli?”

“Ndio nina ona nyota yake ina nguvu sana”

“Je mimi?”

“Nisiwe muongo shehe. Kuna mitihadi mingi hapo mbeleni nime iona. Ila mwenyezi Mungu nina imani ata iepushia mbali. Wala usiwe na shaka na hofu”

“Asante sana”

“Nashukuru, ila itahidi na shemeji basi ahamie kwenye dini hii”

“Naamini siku mwenyezi Mungu atakapo mshushia rehema zake basi ata badilisha kwa moyo wake mwenyewe.”

“Mungu amuongoze katika hilo”

“Amen”

Baada ya siku mbili shehe na msaidizi wake wakaondoka na kurudi nchini Tanzania huku wakiwa wameingiziwa kiwango cha pesa ambacho baba mkwe amewapatia na Jackline naye akawapatia kiasi cha dola laki moja ikiwa kama shukrani kwa kazi waliyo ifanya.

“Mmm mama siku mbili hizi nina kona una safari za hospitalini kwenda kumtazama baba mkwe na nina kuona ni mwenye furaha sana?”

Nilimuuliza mama huku nikimtazama usoni mwake, akatabasamu kwa maana katika kipindi cha maisha yangu niliye ishi naye sijawahi kumuona akiwa na furaha ya kwake binafsi na furaha ambazo huwa ana zipitia ni furaha za mimi kumfurahisha au mjukuu wake.

“Mwanangu nime penda”

Kauli ya mama kidogo ikanistua.

“Una maanisha nini mama?”

“Una kumbuka siku ile baba mkwe wako alivyo niita peke yangu katika chumba alicho lazwa?

“Ndio”

“Aliweza kunieleea hisia zake, hapo awali nilihisi kwamba ana nitania, ila kadri jinsi ninavyo kaa naye hospitalini nami nimejikuta nikizipokea hisia zake na moyo wangu ume funguka kwake”

“Toba!!”

Nilihamaki huku nikitabasamu.

“Haki ya Mungu Rashidi mwanangu.”

“Jackline ana lifahamu hili?”

“Hapana na wewe sikupanga kukueleza na wala usimueleze mpenzi wako. Baba yake mwenyewe ana hitaji kuzungumza yeye mwenyewe.”

“Ila mama nyote umri ume kwenda?”

“Rashidi, mapenzi hayana umri, rangi wala dini”

“Nalijiua hilo, maana yangu ni kwamba kuwa makini mama kwa maana kwa sasa sinto pendelea uje upate ujauzito kwa maana sijui mtoto wenu ataniita mimi nani, Shamsa sijui ataitwa nani?”

“Hilo haliwezi kutokea mwanangu. Kama ni kukutafutia mwenzako, ningefanya kipindi hicho nikiwa bado msichana mdogo. Ila nilivyo kufungua wewe nilionekana kwamba kizazi changu kina shida hivyo wakakitoa kabisa ndio maana ulibaki kuwa wewe kama wewe kwenye maisha yako yote.”

“Sawa mama mimi nina kubariki kwenye mapenzi yako mapya kikubwa nina penda upate raha mama yangu”

“Nashukuru mwanangu”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni mwangu na kukuta ni namba ngeni. Nikamtazama mama usoni mwake kwa sekunde kadhaa.

“Vipi mbona hupokei”

Sikumjibu chochote mama zaidi ya kunyanyuka eneo hili na kusogea pembeni na kuipokea simu hiyo.

“Haloo”

“Mambo Rashidi, mimi ni Fiifi”

“Ohoo mambo vipi?”

“Safi Rashidi nina mazungumzo muhimu na wewe je una dakika kadhaa tuzungumze?”

“Ndio niambie”

“Rashidi nime jaribu kukuficha hili jambo hili nina ona ni heri nika kambia ukweli. Nina MIMBA yako”

Nikastuka sana na mapigo yangu ya moyo yakaanza kunienda kasi sana kwa maana endapo hili jambo Jackline akilifahamu sijuo ni kitu gani kita tokea kwangu na familia yangu.




“Hilo unalo lizungumza ni kweli Fiifi?”

“Haki ya Mungu vile sikutanii. Ila nina tambua kwamba upo kwenye mahusiano yako na upo kazini sihitaji kukuharibia, nita mlea mwanangu mimi mwenyewe na…..”

“Fiifi nisikilize. Nitahitaji kuonana na wewe ana kwa ana tulizungumze hili”

“Hakuna shaka Rashidi”

“Nashukuru, tuta wasiliana na nita kuambia ni wapi uwee kufika”

“Sawa”

Nikakata simu huku nikishusha pumzi, nikatazamana na mama huku nikirudi kwenye kiti nilicho kuwa nime kaa.

“Vipi mbona una onekana kuwa na wasiwasi”

“Hakuna tabu mama”

“Kweli?”

“Ndio”

“Sasa mimi nina kwenda kujiandaa, niende hospitalini”

“Poa”

Mama akaondoka eneo hili. Nikaanza kumtafakari Fiifi, nikakumbuka mtanange tulio ufanya, siku ya kwanza kumtoa usichana wake ndio siku ya kwanza kwa yeye kuupata ujauzito. Nikampigia simu Jack.

“Kaka umenitupa ndugu yangu”

“Samahani kwa hilo, una endeleaje lakini?”

“Nina mshukuru Mungu bado nina endelea kupambana”

“Upo wapi?”

“Nipo mjini”

“Naomba uje kunichukua”

‘Sasa hivi?”

“Ndio”

“Poa nina kuja”

Nikakata simu na kuelekea chumbani na kukumkuta Jackline akiwa amelala. Hali yake hi ya mjamzzito ina mfanya awe ana choka mara kwa mara.

“Hei baby”

Nilizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba.

“Niambie mume wangu”

“Safi. Mke wangu nina hitaji kutoka mara moja, kuna sehemu nina elekea Jack ana kuja kunichukua”

“Wapi baby”

“Mjini”

“Sawa mume wangu nenda na walinzi”

“Hapana nita kuwa na Jack”

“Ila Jack mume wangu sio watu wa DON”

“Usijali, hakuna tatizo lolote litakalo tokea”

“Sawa mume wangu mimi acha niendelee kulala, kwa maana sijisikii kufanya chochote”

“Poa mke wangu pumzika”

“Sawa usichdlewe kurudi”

“Poa”

Jack akafika nyumbani hapa na tukaondoka.

“Kaka ina kuwaje mbona mkuu ana niambia nikufwatile kila nyendo”

“Una maanisha nini Jack”

“Mku ume mfanya nini kwa maana ana niambia kwamba nikutazame sana au umesha badilisha plan nini?”

“Usijali ndugu, Plan ipo pale pale?”

“Malcom mwanangu kuwa makini”

“Poa poa nahitaji tukutane na Fiifi”

“Umeongea naye?”

“Ndio”

Tukaifka katika mgahawa anao fanya kazi Fiifi, kwa bahati nzuri tukamkuta.

“Karibuni niwahudumie nini?”

Fiifi alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Nime kuja kuzungumza nawe Fiifi”

“Sio muda huu, nipo kazini”

Fiifi alizungumza huku akionekana kabisa kwamba hana furaha ya kuniona hapa.

“Tafadhali, dakika moja tu”

“Sina muda hup”

Fiifi akaondoka hapa na kutiacha mimi na Jack tukiwa na mshangao.

“Kaka vipi kuna nini kinacho endelea?”

“Dogo ana mimba”

“Mimba?”

“Ndio”

“Duuu hongera sana kaka kwa maana mtoto ni baraka”

“Ni kweli, ila nahitaji kuzungumza na Fiifi ni muhimu sana asije akavuruga mpango wote ambao umenileta hapa Paris”

“Ngoja”

Jack akanyanyuka na kuelekea eneo la ndani ya mgahawa huu. Wanaume wawili walio valia suti wakafika eneo hili, mmoja akaka kwenye kiti alicho kuwa amekaa Jack na mwengine akiwa amekaa kiti cha pembeni yangu. Aliye kaa pembeni yangu, akaniwekea bastola mbavuni mwangu.

“Tulia kama ulivyo. Una iona ile gari nyeusi pale?”

“Ndio”

Nikajibu huku woga mwingi sana ukiwa umenitawala.

“Twende taratibu”

Nikanyanyuka huku nikiwa na wasiwasi mwingi sana. Tukaingia ndani ya gari hili, ambapo nika kuta mwanamke mmmoja wa kiafrika. Gafla akanikita sindano ya shingoni nikajaribu kufurukuta, ila sikumaiza hata dakika nikahisi viungo vyangu vikipoteza nguvu na mwishowe nikajikuta nikipitiwa na usingizi mzito sana.

***

Ubaridi mkali sana una penya kwenye mwili wangu, ukanifanya nifumbe macho yangu taratibu. Giza lililopo katika eneo hili kikanifanya nishindwe kutambua ni wapi nilipo. Nikajipapasa mwilini mwangu ni akujikuta nikiwa na boksa tu.

‘Nipo wapi?”

Nilijiuliza swali ambalo hata jibu lake sikuweza kulipata kabisa. Taratibu taa za ndani hapa zikaanza kuwaka na hapa ndipo nika gundua kwamba nipo kwenye kontena la kuhifadhia nyama ambazo kwa kuzitazama vizuri ni nyama za nguruwe. Ubaridi wa eneo hili ni mkali sana kiasi cha kunifanya nizidi kutetemeka. Mlango ukafungukiwa na wakaingia wanaume wawili walio valia mavazi kama mafundi gereji. Wakanunyanyya na kunitoa eneo hili huku wakiniburuza.

Wakaniingiza kwenye chumba cha kawaida ambacho hakina kitu chochote.

“Nipo wapi?”

Nilijikaza kuwauliza wanaume hawa, ila hawakunijibu chochote. Jambo baya zaidi ni kwamba katika chumba hichi hakuna dirisha hata moja. Nikaka ndani ya chumba hichi kwa dakika kadhaa mlango ukafunguliwa, moyo ukanistuka sana mara baada ya kumuona makamu wa raisi akiingia huku akiwa na walinzi wake wawili.

“Ni wewe mpu…..”

Kabla sijanyanyuka mlinzi wake mmoja akanipiga teke la kifuani na kuniangusha chini.

“Rashidi ulijaribu kuvuka mstari kuniletea upuuzi mbele ya raisi wangu”

Makamu wa raisi alizungumza huku akichuchumaa taratibu.

“Ulitaka kuniharibia njia yangu ya kueleka kwenye ndoto zangu za kuwa raisi. Sasa kwa mtu kama wewe siwezi kukuchekea siku hata moja ni lazima nihakikishe kwamba nina kushuhulikia kisawa sawa”

Nikatabasamu huku nikimtazama makamu wa raisi usoni mwake.

“Hahahahhaaaa”

Nikacheka kwa dharau huku nikisikilia maumivu ya teke nililo pigwa kifuani mwangu.

“Una cheke?”

“Nina cheka kwa maana najua huwezi kuniua na usihisi kwamba zile picha ninazo mimi mwenyewe. Jiulize nilizipataje na mpiga picha aliingia vipi pale hotelini mukiwa faragha”

Nilizungumza kwa kujiamini huku nikimtazama makamu wa raisi usoni mwake.

“Ohoo”

“Yaa hakuna cha ohoo. Hata ukiniua sasa hivi zile picha zita eneoe duninai kote na sidhani kama kuna mtu ata weza kukuchagua”

“Mtoeni na mpelekeni kwa wengine nina imani kwa sasa hato weza kutoroka kama Maweni”

Walinzi wa makamu wa raisi wakaninyanyua na kunitoa ndani hapa. Tukatembea kwenye kordo hii ndefu. Nikaingizwa kwenye ukumbi mkubwa wenye manjemba yaliyo jazia miili yao huku katikati ya ukumbi huu kukiwa na pambano linalo endelea. Njemba mmoja mwenye miraba minne ana pigana na jemba jengine ambalo kwa muonekano tu lina tisha sana. Kila ambaye nina mtazama kama ana mwili kama wangu, nina kosa.

“Una nizibia”

Njema moja lilizungumza huku likinivuta pembeni na kuniagusha chini. Ikabidi nitafute sehemu ambayo haina mtu na nikakaa.

“Hapa nipo wapi?”

Nilimuuliza moja ya njemba ambalo lipo pembeni yangu, akanigeukia na kunitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatazama ulingoni. Shangwe zikazidi kupamba moto ndani ya ukumbi huu huku manjema hayo yakizidi kupondana hadi moja likakubali kushindwa na pambano likaishia hapa.

“Twende”

Njemba nililo liuliza swali, likanyanyuka na nikaanza kumfwata kwa nyuma. Kila njemba lina nitazama mimi. Tukaingia katika moja ya chumba ambacho kina vitanda viwili vya chuma na magodoro yake ni membamba na watoto wa uswahili huwa tumezoa kuviita ni ulimi wa mbwa.

“Lala ni usiku sasa hivi”

Njemba hilo likanirushia blangeti kisha likapanda kitandani na kulala. Nikajilaza taratibu huku nikiwa sielewi hili gereza ni la aina gani kwa maana sijaona askari wala mlinzi wa aina yoyote.

“Hapana nipo wapi?”

“Dogo lala”

Njema hilo lilizungumza kwa sauti nzito na hazikupita hata dakika kumi likaanza kukoroma kiasi cha kunifanya nikose kabisa usingizi. Hadi kuna pambazuka sikuweza kulala, hapa ndipo nikaanza kuyakumbuka maneno ya shehe kwamba kuna matatizo mengi yatanijia mbele yangu.

“Dogo amka”

Taratibu nikaamka na kukaa kitako.

“Twende”

Ikabidi nifwate amri kwa maana sielewi ni kitu gani kinacho endelea. Tukatoka katika uwanja mkubwa ambao ume jaa mawe. Hapa ndipo nikawaona askari walio valia mavazi meusi huku wakiwa na bunduki. Tukafika kwenye moja ya meza iliyo jaa nyundo kubwa.

“Chukua nyondo moja hapo”

Nikachukua moja ya nyundo na njema hili likabeba nyundo yake. Tukafika kwenye moja ya jiwe kubwa na njema hili likaanza kupasua.

“Una shangaa shangaa nini dogo pasua jiwe”

‘Ehee Mungu wangu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikipasua jiwe hili. Wafungwa wengine nao wapo kwenye kazi hii ya kupasua mawe huku ulinzi ukiwa ni mkali sana katika hili gereza. Ila jambo la kunishangaza ni kwamba wafungwa tuna vaa bukta.

“Hili gereza lipo wapi?”

Ilibidi nimuulize njemba hili kwa maana uvumilivu umenishinda.

“Hapa ni nchini Congo”

“CONGO!!!!”

“Ndio una shangaa nini?”

Nikahisi nguvu zikiniishia mwili mwangu kwa maana sijategemea hata siku moja niweze kurudi barani Afrika tena gerezani.

“Hili ni gereza la waalifu watukutu duniani.”

Njema hili lilizungumza huku likinitazama usoni mwangu.

“Ina maana walifu wote walioletwa ndani hapa ni watukutu?”

“Ndio, gereza lipo msituni na ulinzi wa hapa ni mkali sana kiasi kwamba endapo utatoroka uta uwawa. Kwani hadi una letwa hapa hukuwa una fahamu?”

“Sikuweza kufahamu chochote”

“Pole nina itwa Roma”

“Rashidi”

Tukapena mikono na Roma. Kisha tukaendelea na shuhuli ya kupasua mawe. Ukafika muda wa kupata kifungua kinywa. Tukapanga mstari kwenye foleni. Katika uchunguzi wangu nilio ufanya, hakuna mfungwa mwembaba zaidi yangu mimi peke yangu. Wafungwa wote wamejazia miili yao. Tukapewa kipande cha mkate, kiazi kitamu kimoja pamoja na chai. Tukatafuta moja ya meza mimi na Roma na tukaa.

“Roma huyu ni nani?”

Njemba moja lilikaa pembeni yangu huku akiweka kikombe cha chai na shani ya chakula mezani.

“Ni kijana mpya”

“Dogo nini kime kufanya uje kwenye hili gereza la kifo?”

“Nilitaka kumuua makamu wa raisi”

“Makamu wa raisi?”

Roma aliniuliza kwa mshangao.

“Ndio”

“Wa nchi gani?”

“Tanzania”

“So mpango wako haukufanikiwa?”

“Ndio, ila siwezi kukaa hapa gerezani nina hitaji kuondoka”

“Huwezi kutoroka kwenye hili gereza”

“Hivi mbona sioni askari zaidi ya kule nje?”

“Katika hili gereza kuna kamera zinazo onekana na kamera za siri. Hivyo askari wana kaa nje tu huko ndipo endapo mfungwa ana fanya chochote ana uwawa kwa kupigwa risasi na kufa. Hivyo mdogo wangu Rashidi huto weza kutoroka kabisa ndani ya hili gereza.”

Maneno ya Roma yakanifanya nitazame eneo hili tuliko kaa na kweli nikaona kamera kadhaa zikiwa zime fungwa.



“Una taka kuniambia kwamba hakuna hata mfungwa mmoja aliye wahi kutoroka ndani ya hili gereza?”

“Hakuna nina mwaka wa ishirini na sita sasa sijaona”

“Kwa hiyo maisha ni ya kuishi na bukta tu na boksa?”

“Ndio hili gereza halina sare. Hivyo wafungwa wote tuna ishi hivi kutokana na kuhofiwa kuficha silaha. Wafungwa wengi walio ingia magerezani hapa wana tokana na makosa ya kivita hususani mapinduzi katika nchi za Afrika”

Roma alizungumza kwa sauti ya chini huku tukiendelea kula. Tukamaliza kula chakula na tukarudi katika kazi ya kupasua mawe.

“Haya mawe tunayo yapasua yana fanya kazi gani?”

“Kuna malori ambayo huja kubebe hizi kokoto na kuzipeleka kwenye makampuni makubwa huko ya kutengenezea saruji na majumba makubwa”

“Hayo malori huwa yana kuja muda gani?”

“Majira ya usiku sana na huwa wanakuja na wafanyakazi wao kubeba. Muda huo wafungwa wote huwa tunakuwa tume fungiwa ndani. Hiyo yote wana ogopa wafungwa kutoroka”

Gafla tukaanza kusikia king’ora chenye sauti kali sana. Wafungwa wote tukaacha kufanya kazi na kulala kifudi fudi.

“Usinyanyue kichwa”

Roma aliniambia.

“Kuna nini?”

“Hicho ni king’ora cha hatari, nahisi kuna wafungw awana gombana”

Kutokana eneo hili tulipo ni kilimani kidogo, nikageuka upande wa kushoto, nikaona manjemba wawili wakipigana. Sikuamini macho yangu mara baada ya kuona askari wakiwapiga risasi mfululizo manjemba hayo mawili na wakaanguka na kufa.

‘Mungu wangu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikishuhudia jinsi manjemba hayo yanayo kata roho. King’ora hicho kinanyamaza na tukaanza kusimama mmoja baada ya mwengine.

“Haya ndio maisha ya hapa gerezani. Ukijifanya mjuaji tu una kufa”

“Duuu”

“Ndio hivyo”

Muda wa mchana ukafika tukapata chakula na wafungwa tukupata muda wa kupumzika huku wengine wakioga.

“Mkuu wa hili gereza ni nani?”

“Kwa miaka yangu yote niliyo ishi hapa sijawahi kumuona”

“Kweli”

“Ndio sijawahi kumuona”

“Hivi hapa kuna mapambano?”

“Ndio yapo mapambano ya usiku. Ila yana kuwa weekend kama jana, siku hizi za kawaida hakuna mapambano yoyote. Ila leo kuna jambo moja hatari”

“Jambo gani?”

“Kuna shindano moja linaitwa Last Man stand. Wanachukuliwa wafungwa ishirini, majira ya saa moja usiku wana ingiwaza msituni wakiwa hawana silaha wala kitu chochote. Katika msitu kuna wanaya wa kila aina na wakali sana ambao kumuua binadamu ni kitu cha kawaida. Endapo uta fanikiwa kufika mwisho wa msitu huo ambapo kuna kuwa na mabomu na askari wenye silaha wanao wasubiria, ukiwapita na kukimbia basi una kuwa huru ila ukishindwa una uwawa. Wafungwa huwa wan apana nafasi ya kutazama kwenye tv kubwa zilizopo hapa gerezani.”

“Kwa hiyo Roma una taka kuniambia kwamba huko msituni kuna kamera?”

“Ndio kuna kamera, mimi nina hisi huwa wana fanya kama tv Show moja ambayo ina waingizia pesa nyingi sana kwa kuyagarimu maisha ya watu”

Nikashusha pumzi huku nikiwa nina waza huo msitu.

“Je kabla ya kuingizwa msituni kunamaelekezo wanayo patiwa watu?”

“Hakuna chochote zaidi ya kwamba muna pangwa mstari mmoja kisha muna anza kukimia. Leo uta ona hilo shindano”

Shahuku kubwa ikanijaa sana ya kuweza kuona jambo hilo. Majira ya saa kumi na mbili, wafungwa wote tukasimama kwa mistari iliyo nyooka katika uwanja mkubwa sana uliopo hapa gerezani. Askari walio valia mavazi meusi huku wakiwa wana bunduki, wapatao mia mbili wakatuzunguka. Askari mmoja mwenye kipaza sauti akasimama kwenye jukwaa huku akiwa na kipaza sauti. Akaamrisha tuanza kuhesabu namba, akaanza kuhesabu mfugwa wa kwanza, hadi wa mwisho huku namba yangu mimi ikiwa ni mia tisa na moja, huku namba ya mwisho ikiwa ni elfu mbili na mia tano.

“Namba nitakazo zitaja zitoke mbele”

Askari huyo aliamua na akaanza kutaja namba za watu na wakaanza kutoka mbele. Alipo fika mtu wa kumi na tisa akanyamaza kidogo, kisha akoanekana kama akinong’onezwa na askari mwengine.

“Namba mia tisa na moja pita mbele”

“Nikastuka sana, Roma aliye somama nyuma yangu, akanigusa begani na taratibu nikamgeukia.

“Pole sana ndugu yangu”

Roma alizungumza huku akiwa amejawa na huzuni. Nikapita mbele na kupanga mstari na wezangu walio itwa.

“Sasa nyinyi watu ishirini, leo ndio mume ingia kwenye kipindi chetu cha Last man Stand. Hakikisha kwamba una fanikiwa kutoroka msituni na kuwatoroka askari. Ukifanikiwa katika hilo, upo huru ukishindwa una kufa. Muna robo saa ya kujiandaa”

Askari sita wakatuelekeza sehemu ya kuelekea na taratibu tukaelekea katika chumba hicho. Kila ninaye mtazama usoni mwake ana onekana kujawa na huzuni.

“Eti ina kuwaje?”

Nilimuuliza jamaa mmoja aliye kaa karibu yangu.

“Hakuna aliye ingia katika msitu huo na kupona”

Jamaa huyu alinijibu kwa sauti iliyo jaa huzuni kubwa sana. Muda wa mapumziko ukaisha, tukapakizwa kwenye karandika huku tukiwekwa chini ya ulinzi mkali. Kwa mwendo wa kama dakika kumi hivi karandika hili lililo sindikizwa na magari mawili yaliyo jaa askari, yakasimama na tuka amrishwa kushuka. Nikawa mtu wa tano kushuka kwenye karandika hilo. Eneo hili tulipo ni kilimani, na chini ya kilima hichi ndipo ulipo msitu na hapa hadi kufika msitu huu kuna nyasi fupi ambazo hakuna eneo ambalo mtu ana weza kujificha. Tukaamrishwa kupanga mstari mmoja.

“Ukiogopa kuingia katika msitu huo una pigwa risasi na kufa.”

Askari mmoja alizungumza kwa sauti ya juu. Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi sana kwa maana msitu huu ukiutazama kwa macho ya kawaida una onyesha dhairi kwamba una tisha.

“Moja, mbili, tatu kimbia”

Askari wakaanza kupiga risasi hewani huku wakicheka, kwa kiwewe cha riasi hizo zikatufanya kila mmoja kuanza kushusha kiporomoko hichi kwa kasi sana.

‘Mungu nisaidie’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikianza kuingia katika msitu huu ulio shonana kwa miti mirefu. Mwanga wa mbalamwezi una tusaidia kuweza kuoana mbele. Nikasimama huku mwili mzima ukinisisimka, wezangu wawili walio kuwa nyuma yangu wakanipita kwa kasi. Nikatazama nyuma yangu nikaona chui wawili wakitufwata kwa kasi ya ajabu. Mimi mwenyewe nikajikuta nikianza kuchanganya miiguu yangu kwa kasi na hata wezangu wawili walio nipita, nikawapita. Chui hawa wanao onekana kuwa na njaa kali sana wakazidi kutukimbiza, nikamshudia mwezangu mmoja akirukiwa na chui mmoja na kuangushwa chini. Ukelele alio utoa nikatamani sana kumsaidia, ila nikajikuta nikishindwa kabisa.

Mwezetu mwengine akarukiw ana chui huyo na mimi nikazidi kuchanja buga huku nikizidi kusonga mbele. NIakfika kwenye moja ya mti nikasimama huku nikihema kwa maana nime kimbia kwa kasi takribani nusu saa pasipo kusimama. Nikainama huku nikijitahidi kuvuta pumzi. Nikaanza kusikia kimlioa ambacho mara nyingi huwa wana toa majoka makubwa. Nikageuka upande wangu wa kushoto nikaona joka kubwa na lenye unene wa kutisha likiniangalia huku likitoa ulimi wake nje.

Nikakaza macho huku nikilitazama jinsi linavyo ninyemelea. Joka hili likanirukia, nikalikwepa na kubamiza kichwa chake kwenye mti huu. Joka hili lenye futi kama thelathini hivi, lakajigeuka kwa kasi na kuanza kunifwata sehemu nilipo angukia. Ujasiri mkali ukanijaa kwa maana hapa nikiweka woga tu basi nita kuwa kifo cha kutafunwa na joka hilo.

Nikafanikiwa kuokota mti ulio chongeka kidogo mbele. Joka hili likajirusha ili kunidaka shingo yangu, ila nikalikwepa huku nikimkita eneo la mbavuni mwake na mti nilio ushika. Joka hili likaanza kujivirigisha huku damu zikiruka. Sikuhitaji kulisubiria lipate nafasi ya kunishambulia, nikaokota kipande cha jiwe na kuliwahi eneo la kichwani mwake na kuanza kuliponda kwa nguvu zangu zote hadi nikafanikiwa kulia. Nikasimama huku damu nyingi zikiwa zimetapakaa mwilini mwangu. Nikiwa katika kuangaza angaza, nikaona kamera moja ikiwa ime fungwa juu ya mti. Nikaitazama kwa macho makali, kisha nikaanza kukimbia kusonga mbele. Nikafanikiwa kuona majani ambayo ujipaka mwilini huwa yana nuka vibaya sana na hakuna mjama hata mmoja ambaye ana weza kukushambulia. Nikaanza kuyachuma kwa haraka, huku mwengine nikiyatafuna na kujipakaza mwilini mwangu. Harufu mbaya na kali ya majani haya sikujali kwa maana ni bora kuwa hai kuliko kuona kinyaa cha harufu mbaya ya majani haya. Nikahakikisha kwamba nime jipaka mwili mzima kisha nikaanza kukimbia huku wezangu karibia wote nime potezana nao.

Njiani nika kutana na wanyama wengine wakali, ila hapakuwa na mnyama aliye weza kunisogelea kwa maana nina nuka vibaya na hii ndio pona yangu. Ndani ya masa matatu na nusu huku nikiwa nina kipimbia pasipo kupumzika nikafanikiwa kufika mwisho wa msitu huu. Kabla sijatoka, nikaona magari karibia sita yaliyo washa taa kuelekea msituni hapa na katika eneo hili nililo simama hadi kuelekea kwenye magari yayo kuna mita mia moja na ni tambarare. Eneo ambalo niliambia kwamba lime tegeshwa mabomu ya ardhini.

‘Nikitoka wata niua. Acha nijibanze hapa hapa’

Nilizungumza huku nikiwa nime jibanza kwenye maja ya mti. Joka moja kubwa, likakatiza pembeni ya miguu yangu na halijanidhuru kiasi cha kunifanya nimuombe Mungu harufu ya majani haya isiishe. Nikaona kamera yenye mfumo wa drone ikiwa imesimama juu yangu huku inavyo onyesha kuna mtu ana iendesha.

“Hamuwezi kuniua nyinyi wana haramu. Malayaa nyinyi, jina langu ni Rashidi Pinda na nikitoka hapa makamu wa raisi nina kuapia nita kuuaaaaaa”

Nilizungumza kwa hasira kali sana huku nikiitazama kamera hiyo ambayo sio rahisi kuisogelea. Muda ukazidi kuyoyoma hadi jua likaanza kuchomoza. Nikachungulia na kuwaona askari wakishuka kwenye magari yao na kukimbilia katika eneo hili nilipo mimi.

“Shitii”

Nilizungumza huku nikiwatazama jinsi wanavyo katika katika eneo hilo la mabomu. Nikaukremisha mtindo wao wa kupita. Kisha nikaanza kutokomea kuingia msituni zaidi ili kama ni kunifwata wanifwate ndani ya msitu. Nikaanz akusikia milio ya bundiki ikirindima ndani yam situ huu, huku kelele za kuuwawa kwa askari hao na wanayama wakali zikisikika.

‘Muosha huonywa, kenge nyinyi’

Nilizungumza huku nikikimbilia eneo walipo askari, nikamkuta askari mmoaja kiwa ameviringishwa na joka kubwa huku akilia kwa chungu. Nikaokota bunduki yake na kuanza kujibanza kwenye miti kwa maana sio askari wote walio ingia katika msitu. Kuna askari kama sita wamesalia nje yam situ. Nikatoa magazine ya bunduki hii na kukuta ikiwa imejaa risasi za kutosha. Nikairudisha magazine hii na kuanza kusonga mbele huku nikiw amakini sana, nikaona askari wengine wakiwa wana tafunwa na simba wenye njaa kali. Nikawaona askari sita wakiwa wamesimama kwa umakini huku bundiki zao zote wakizielekezea ndani ya msitu huu. Nikanzaa kufyatua risasi kuelekea kwa askari hao. Shambulizi hili la gafla nililo wafanyia likawachanganya askari hawa na wakaanza kurudi nyuma pasipo mpangilio. Waili wakakanyaga mabomu yaliyo tegwa ardhini na yakalipuka na wakachanguliwa vibaya. Nikamuona askari mmoja akikimbila yalipo magari. Nikafumba jicho moja ya kumtungua risasi ya mgongo na akaanguka chini. Nikaanza kutoka ndani ya msitu huu huku nikiwa nime pona peke yangu.

Kwa umakini mkubwa sana nikaanza kupita katika eneo hili ambalo lina mabomu. Nikafanikiwa kufika kwenye magari yahaya polisi ina ya Ford Ranger. Nikaingia kwenye moja ya gari na kwa bahati nzuri nikakuta funguo ikiwa ina ning’inia katika sehemu ya kuendeshea. Nikawasha gari hili na kuanza kuifwata barababa hii ya vumbi.

Nikaingia kwenye moja ya kijiji ambacho kina nyumba chakavu za udongo. Nikasimamisha gari hili, kisha nikashuka huku nikiwa na bunduki. Wamama walio niona, wakakimbia huku wakionekana kuniogopa. Nikafungua mlango wa nyuma ya gari hili na kwa bahati nzuri nikafanikiwa kuona ramani. Nikaifungua na kuitazama.

“Sasa hapa nilipo ni wapi?”

Nilijiuliza huku nikiangaza angaza. Nikatazama eneo nililo toka nikaona gari tatu za polisi zikija kwa mwendo wa kasi sana. Kwa haraka nikaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili huku nikiwa sitambui ni wapi ninapo elekea.

“Ehee Mungu nisaidie”

Nilizungumza huku nikikata kona kadhaa za barabara hii iliyopo pembezoni mwa mlimza mkubwa huku pande wa pili kukiwa na makorongo ambayo endapo gari litapinduka na kuingia katika korongo hilo basi hato pona. Nikatazama katika kioo cha pembeni na kuona gari za polisi zikizidi kunisogelea, jambo lililo nifanya nitishike sana. Wakaanza kunisahambulia kwa risasi zilizo piga nyuma ya gari hilo na kunifanya nichachawe sana. Nikakunja kushoto katika njia ndogo na kuachana na barabara kubwa. Njia hii japo ni nyembeba kiasi ila ina gari linapita. Nikafika katika moja ya kijiji chenye nyumba nyingi nyingi.

“Samahani hii barabara ina kwenda hadi wapi?”

Nilimuuliza jamaa mmoja aliye simama pembeni ya barabara.

“Broo huko mbele kuna ngome ya waasi”

“Waasi”

“Ndio na endapp uta fika huko huto weza kutoka salama”

Nikatazama nyuma na kuona gari za polisi zikishusha kilima huku zikija kwa kasi.

“Nashukuru”

Nikatia gia na kuzidi kuifwata barabara hii nyembamba ambayo magari mawili hayawezi kupishana. Nikakiacha kijiji hichi na kuingia kwenye msitu na nikazidi kusonga mbele. Galfa risasi mbili zikapiga kioo cha mbele ika katika sita ya pembeni yangu na kunifanya niiname chini huku nikifunga breki za gafla. Nikachungulia na kuona kundi kubwa la wanajeshi ambao hawajavalia sare za kueleweka wakijitokea mzituni na kulizunguka gari hili huku wakiniamrisha nishuka ndani ya gari hili huku nikiwa nimenyoosha mikono juu jambo lililo nifanya niishiwe na matumaini ya kuishi kwa maana nimeokoka kwenye msito wa wanyama wakali sasa nime angukia kwenye mikono ya wanajeshi na sijui ni kitu gani wata nifanya.



Taratibu nikafungua mlango wa gari hili na kushuka huku mikono yangu ikiwa juu. Gafla nikasikia kitu kizito kikinigonga nyuma ya kisogo changu na nikaanguka kifudifudi huku taratibu giza likianza kunitawala machoni mwangu na haikuisha hata dakika moja nikapoteza uwezo wa kufahamu ni kitu gani kinacho endelea.

***

Harufu kali ya kinyesi ikanistua na kunifanya nifumbue macho yangu. Giza totoro lililopo katika eneo hili, likashindwa kunifanya niweze kuona vizuri hili eneo, ila nilicho jigundua ni kwamba, nusu ya mwili wangu upo ndani ya shimo ambalo ndio lina kinyesi huku mikono yangu ukiwa ime fungwa juu na kunifanya niwe nina ning’inia kama nyama buchani. Harufu hii ikanifanya nijihisi vibaya sana kiasi cha kunifanya nijihisi kutapika, ndani ya muda mchache nikajikuta nikitapika mfululizo. Ila kwa giza la eneo hili siwezi hata kuona nini ninacho kitapika. Njaa kali ikazidi kunikung’uta tumboni mwangu, nikakaa katika hali hiiya kuning’inia kwa masaa kadhaa kadhaa hadi nikoona mwanga hafifu wa juua ukipenyenyeza katika mlango wa choo hichi.

‘Ehee kumbe hichi ni choo?’

Nilizungumza huku nikiangaza uchakavu wa choo hichi. Lisaa moja mbeleni mlango ukafunguliwa na wakaingia wanajeshi wawili wakiwa na bundukia aina ya SMG mikononi mwao. Wakaikata kama niliyo ning’iniziwa na kunivuta nje ya chohoo hichi huku nusu ya mwili wangu ikiwa ime jaa kinyesi na wao wala hawahisi kinyaa cha aina yoyote. Wakanisukumiza kwenye uwanja wenye vumbi la kutosha, nikaona wanajeshi baadhi wakifanya maeozi huku wengine wakilinda eneo hili. Akasimama mwanaume mmoja mwenye ndevu nyingi usoni mwake mithili ya Osama Bin Laden. Ila ni mweusi na ana mwili mkubwa kama wa Iddi Amin Dadaa. Mwanaume huyu amevalia mavazi safi ya kijeshi huku akiwa na vyeo vingi vinavyo ning’inia na mkononi mwake amashika sigara kubwa ambazo huwa mara nyingi huvutwa na watu matajiri na sio rahisi kuzikuta katika maduka ya kawaida.

“Mnyanyueni na mukamchape maji”

Nikanyanyuliwa na wanajeshi wawili hawa wakaanza kuniburuta huku kila mmoja akiwa ameshika mkono wake. Wakanifikisha kwenye dibwi moja la maji machafu.

“Jinawishe huko”

Mmoja alizungumza huku wakinisukumia ndani ya dimbwi hili. Hakika kwa jinsi nilivyo choka, mwili wangu hauna hata nguvu ya kusimama vizuri, nikajitahidi kujinawisha ila nikahisi kushindwa. Mwanajeshi mmoja akanipiga teke la kifua na kuanguka chini.

“Nawa”

Alifoka huku akininyooshea bundiki. Kwa kiwewe nikaanza kunawa mwili mzima tena haraka haraka.

“Nanyuka na tembea”

Nikajikaza kiume huku nikihisi maumivu ya kifua changu. Nikaanza kutembea japo ni kwa kuyumba yumba ila ina jikaza kutembea. Tukaingia kwenye moja ya bafu kubwa, wakaniamrisha nisimame kwenye ukuta, mmoja wao akanipa ishara ya kuva boksa yangu ambayo ime chafuka sana. Nikaivua na nikabaki kama nilivyo zaliwa. Mwanajeshi mmoja akachukua mpira wa maji mkubwa mithili ya mipira inayo tumika na vikosi vya zima noto. Mwezake akafungulia maji kwenye koki na yakaanza kutoka kwa wingi na kwa kasi kubwa. Akaanza kunimwagia maji hayo mbayo kwa kweli, sina nguvu ya kuyastahimili zaidi ya kujikuta nikianguka chini huku yakiniumiza kisawa sawa.

“Hahahaaaa toa mkono kwenye makend** wewe”

Mwanajeshi anaye nimwagia maji hayo alizungumza mara baada ya kuniona nimeweka viganja vyangu kwenye sehemu zangu za siri. Mwanajeshi huyu akaona nina mletea ukaidi, akanipiga maji ya uso, nikashindwa kuvumilia na kujikuta nikijiziba uso wangu kwa viganja kwa maana maji haya yana nguvu kunwa na yana umiza sana mwili. Akayaelekeza maji haya kwenye sehemu zangu za siri na kujikuta nikiishusha viganja vyangu tena. Ikawa kama mchezo, nikiweka viganja sehemu za siri ananipiga na maji haya usoni mwangu, nikiweka viganja usoni, anaipiga sehemu za siri hadi nikajaribu kugeuka na kuwapa mgongo.

“Geuka mbele”

Mmoja wao alifoka kwa hasira huku akinifwata sehemu nilipo. Akanipika mateke mazito ya mgongo hadi nikageuka bila kupenda. Mchezo wao ukaendelea kwa dakika kama kumi hivi hadi akaingia mwanjeshi mwengine ambaye ana onekana ana cheo kidogo kikubwa kuwapita wao.

“Mkuu ana muhitaji huyo mtu”

“Sawa mkuu”

Wanajeshi hawa walizungumza kwa heshima.

“Simama”

Nikajaribu kusimama ila nguvu zime kwisha na sina uwezo kabisa wa kusimama.

“Nimesema simama”

Nikashika ukuta huu unao teleza kutokana na maji. Nikajikaza kiume huku mwili, ukinitetemeka na njaa kali ikizidi kunikung’uta tumboni mwangu. Tukatoka ndani hapa huku nikiwa uchi kabisa, tukatembea kwenye kordo moja ndefu kidogo ya nyumba hii. Nikaingizwa kwenye moja ya chumba na nikakalishwa kwenye kiti cha chuma. Mikono na miguu yangu ika fungwa na pingu katika kiti hichi. Akaingia mwanajeshi ambaye nilimuona pale awali. Akanitazama kwa macho yake makali yaliyo yaa uwekundu mithili ya mvuta bangi aliye bobea.

“Ni nani amekutuma?”

Aliniuliza swali ambalo ni jepesi ila jibu lake sina.

“S…i…jatumwa na mtu?”

Akatoa ishara kwa kijana wake mmoja. Mtetemeko ninao upata nina ufananisha kama nilio upate kipindi nime kamatwa nchini Tanzania kwa kosa la kusingiziwa kwamba nime waua askari kwenye lindo langu na sura ya askari yule wa kike aliye nipiga shoti bado nina ikumbuka. Kelele zangu hazikusaidia kupunguza maumivu ya shoti hii ninayo pigwa.

“Zima”

Alizungumza na shoti ikazimwa, kwani kiti hichi kime unganishwa na nyaya za umeme. Akavuta pafu kubwa la sigara kisha akautoa mocha wake puani na kunitazama.

“Una itwa nani?”

“Ra…Rashidi”

“Wewe ni raia wa nchi gani?”

Nikafirikia kwamba nime tokea nchini Ufaransa au Marekani, wana weza kuniua, wakihisi kwamba mimi ni mpelelezi wa mashirika makubwa kama FBI na mengineyo.

“Ta…tanzania”

Nilijibu huku nikitetemeka, moja kwa maumivu ya shoti niliyo pigwa na mbili kwa njaa kali sana niliyo nayo.

“Tanzania eneo gani?”

“Dar…..Dar.”

Akanitazama kwa umakini sana kama mtu anaye nidadisi.

“Kwa nini ulikuja eneo hili ukiwa na gari la polisi?”

“Ni….i…litoroka kwenye gereza moja na…na….na tulipe….elekwa kwenye msitu wenye wanyama wakali. Wezangu waliliwa na mimi nika fanikiwa kutoroka”

“Wewe ume toka kwenye ule msitu?”

Aliniulza huku akionyesha kwamba ana fahamu vizuri juu ya msitu huo.

“N…dio”

“Askari hawakuuua?”

“Ni….li…waua”

“Hembu nileteni laptop yangu”

Mwanajeshi akatoka ndani hapa na baada ya dakika tatu akarudi akiwa na laptop.

“Nitafutie kipindi cha juzi jumatatu cha wale washenzi”

Mwanajeshi huyo akaanza kuminya minya laptop hiyo kisha akamuwekea video mkuu wake. Ninacho kisikia kutoka katika video hiyo ni sauti za vilio vya wezangu wakitafunwa na wanyama wakali. Mkuu huyu akanitazama kwa jicho la kuiba kisha akaendelea kutazama. Nikajawa na matumaini kidogo mara nilipo sikia sauti yangu nikiwatukana waandaaji wa kipindi hicho. Akatazama kipindi hicho hadi alipo anza kusikia milio ya bundiki ikirindima. Akanigeuzia laptop hiyo na nikajiona jinsi ninavyo waua askari kadhaa wa gereza hilo.

“Ina onyesha una mavuzo fulani ila sio ya kijeshi. Wewe ulikuwa ni nani nchini Tanzania?”

“Nilikuwa mlinzi wa kampuni hizi za ulinzi”

“Kampuni gani?”

“QX Security”

“Ingia kwenye mtandao wa hiyo kampuni. Jina lako ni Rashidi nani?”

“Rashidi Pinda”

Kijana wake akatafuta kwa dakika kdhaa.

“Huyu hapa ila profile yake inaonyesha amefukuzwa kazi kwa kosa la ujambazi kwa kuwaangamizi askari wa kikosi cha FFU pamoja na walinzi wezake.”

“Una taka kuniambia wewe ni jambazi?”

“Hapana nilisingiziwa tu mkuu. Sija waua”

“Nani alikusingizia?”

“Makamu wa raisi alikuwa na mahusiano na mke wangu. Hivyo wakanibambikizia keshi hiyo na akafunga naye ndoa na wakanisweka gereza la Maweni Tanga na nilipo jaribu kutoroka, nikajikuta nipo kwenye gereza hilo la minjemba”

Mkuu huyu akanong’onezana na kijana wake na sijasikia ni nini wanacho ongea.

“Sawa hatuto kuua”

“Ohoo nina shukuru sana, asante sana”

Nilizungumza kwa furaha toka moyoni mwangu.

“Ila uta kuwa ni miongoni mwetu sisi. Endapo uta jaribu kutoroka hapa, tuta kutafuta na tuta kuua. Mpeni nguo, viatu, pamoja na chakula, kuanzia kesho asubuhi uta jumuika na wengine katika mfunzo ya kijeshi.”

“Sawa, ila nina weza kuuliza swali?”

Mkuu huyu akanitazama kidogo kisha akatingisha kichwa kwa kuniashiria kwmaba niulize.

“Hivi nyinyi ni kina nani?”

Wakatazamana na kijana wake.

“Sikia jinsi unavyo endelea kukaa hapa basi uta tufahamu sisi ni kina nani ila kwa sasa, kula, kisha utaonyeshwa chumba cha mapumziko.”

“Nashukuru”

Nikaletewa nguo za kijeshi mpya pamoja na mabuti. Niavaa na nikatoka ndani hapa na mmoja wa wanajeshi ambao walikuwa wana nitesa.

“Mseng** una bahati sana wewe, na sijui kwa nini ume achwa hai”

Jamaa huyu alizungumza huku akionekana kunipania sana. Sijahitaji kumjibu chochote zaidi ya kuongozana naye. Tukaingia jikoni na kukuta wapishi wakipika chakula.

“Mpeni msosi”

“Huyu ni mpya?”

“Ndio”

Nikachukua moja ya sahani na kupakuliwa ugali mkubwa na maharage yaliyo chemswa tu pasipo kuungwa. Kutokana na njaa kali, sikuhitaji kuremba. Nikaanza kuutandika ugali huu japo ni wa moto, ila una pita kooni bila ya shida yoyote. Wanajeshi hawa wana nishangaa tu, ndani ya dakika kumi nikamaliza kula.

“Naweza kuongezwa?”

“Mamaee walai, ugali wote ule una taka kuongezwa?”

“Mpeni bwana”

Mwanajeshi mwengine ambaye ni mpishi alinitetea. Nikatengewa ugali mwengie wa wastani na nikaendelea kula hadi nikashiba ndii.

“Maji ya kunywa”

Wanajeshi hawa wakatazamana kisha mmoja akanichotea maji ya kunywa kwenye pipa moja na kunikabidhi jagi lililo jaa maji. Nikaanza kuyafakamia maji haya hadi nikayamaliza.

“Duu!!”

Mwanajeshi mmoja aliguna huku wakinishangaa. Nikasimama na tukatoka na mwanajeshi huyu na kuingia naye kwenye bwalo kubwa lenye vitanda kama mita mbili hivi ambavyo ni vya gorofa. Tukatembea hadi kitanda cha mwisho kabisa.

“Kitanda chako ni hichi kuanzia hivi sasa. Ila kila anaye lala kwenye hichi kitanda lazima afe”

Mwanajeshi huyu alinionyesha kitanda hichi kilichopo juu, kisha akaondoka. Kutokana ni mtu ambaye amejawa na chuki na mimi toka nilipo asubuhi, sijayajali maneno yake, nikapandisha ngazi na kulala chali huku nikisikilizia shibe jinsi inavyo nitawala. Uchovu na shibe vikanitawala na mwishowe usingizi umzito ukanipitia na nikalala fofofo.

Kelele za watu wanao zungumza huku wengine wakicheka zikanistua usingizi. Nikaona wanajeshi wengi wakiwa ndani ya bwalo hilo ambalo ndio sehemu ya kulala.

“Wewe ni mgeni?”

Mwanajeshi aliye simama pembeni ya kitanda hichi aliniuliza huku akinitazama machoni mwangu.

“Ndio”

“Karibu, nina itwa Razaro”

Alizungumza huku akinikabidhi mkono wa kulia, nikautazama kwa sekunde kadhaa kisha nani nikampa mkono wangu wa kulia ikiwa ni ishara ya kusalimiana.

“Nina itwa Rashidi”

“Wewe ni muislamu?”

“Ndio”

“Ohoo sawa. Twende tukapate chakula cha usiku”

“Sasa hivi ni saa ngapi?”

“Saa mbili”

Nikashuka kitandani hapa na kujinyoosha viungo.

“Tusikilizane”

Razaro alizungumza kwa sauti kubwa na wanajeshi wengine wote ndani ya bwalo hili wakanyamaza na kila mmoja akasimama kumsikiliza ni nini ana hitaji kuzungumza.

“Tuna ndugu yetu huyu ana itwa Rashidi. Nina hitaji tumpatie ushirikiano, ni mgeni”

Wanajeshi walio karibu yangu wakanikaribisha kwa kunipa mikono.

“Mimi ndio dom leader hivyo nikiwa ndani ya hili bwalo mimi ndio mkuu wao”

Razaro alizungumza huku tukitembea kuelekea nje.

“Ahaa sawa sawa. Ahaa nina weza kukuuliza swali”

“Uliza tu”

“Nyinyi ni kina nani?”

“Kwani ulivyo ingia hapa hukuelezwa sisi ni kina nani?”

“Hapana”

Razaro akanitazama machoni mwangu kwa sekunde kadhaa huku akiwa amesimama.

“Nani aliye kuingiza hapa?”

“Mkuu mwenye ndevu nyingi na mweusi”

Razaro akatabasamu kidogo kisha akarudi katika sura yake ya ukauzu.

“Yule ndio kiongozi wetu. Hii ni kambi ya wanajeshi tuliyo iasi serikali iliyopo madarakani. Na sisi tume uteka huu mji wa Goma hivi sisi hapa ndio watawala na kila majeshi ya serikali yanavyo jaribu kuingia au kupigana nasi huwa tuna watandika kisawa sawa na kuutetea mji wetu. Hivyo ina kupasa kuwa tayari kwa lolote na muda wowote kwa maana vikosi vya serikali na umoja wa mataifa vina uwinda sana huu mji”

Maneno ya Razaro yakanifanya nijawe na bumbuwazi kwa maana nimeingia kwenye jeshi la waasi pasipo mimi mwenyewe kupenda na nita piga vita ambayo hata hainihusu kwa maana mimi ni Mtanzania na nina na hawa ni wa Congo ambao kwao vita ni jambo la kawaida sana kitu ambacho kwa Tanzania sikuwahi kukisikia wala kukiona kabisa toka nilipo zaliwa hadi hapa nilipo fika.



“Ahaa?”

Nilijibu huku nikitabasamu kwa woga. Tukaingia katika holi kubwa la chakula na kukuta wanajeshi wengi wakiendelea kula. Tukapanga mstair na kupatia chakula chetu. Tukakaa kwenye moja ya meza na kuanza kula taratibu. Wingi wa wanajeshi hawa wana weza kufika elfu mbili na kitu.

“Kula ushibe kwa maana kesho asubuhi ni muda wa mazoezi magumu”

Razaro alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa sawa”

Tukamaliza kula na kurudi kwenye bwalo la kulala. Nikapanda kitandani kwangu na wala sijamaliza dakika kumi, usingizi mzito ukanipitia. Kelele za mabati yanayo gongwa kwa pamoja, zikanistua sana kiasi cha kunifanya nikae kitako kitandani. Nikawaona wanajeshi wezangu wakiruka vitandani kwao jambo ambalo likanitisha kidogo.

“Rashidi amka muda wa mazoezi”

Razaro alizungumza huku akivaa shati lake. Nikachukua shati langu nikashuka kitandani, uzuri ni kwamba nimelala na viatu pamoja na suruali. Tukatoka ndani hapa huku tukikimbia, kigiza kilichopo angani kidogo kinanipa mashaka, na kujiuliza muda huu ni saa ngapi kwani. Tukakimbilia hadi kwenye uwanja mkubwa na hapa ndipo nikatambua kwamba kambi hii ya jeshi ina wanajeshi wengi sana. Tukaanza kuamrishwa kukaa katika vikundi vikundi.

“Wale wageni waje huku”

Mwanajeshi mwengine mwenye umri mkubwa kiasi aliamrisha na ana onyesha kwamba ndio mkuu wa maeozi. Nikawafwata wezangu ambao ni wageni na tukasimama katika eneo letu, nikahesabu wezangu na kukuta ni kumi na moja huku mimi nikiwa mtu wa kumi na mbili. Wengine wakatawanyika huku wakielekea katika majukumu wanayo yajua wao wenyewe.

“Simama wimaaaa”

Mkuu huyu aliamrisha na sote tukasimama kwa ukakamavu huku tukiwa tumepanga mistari miwili yenye watu kumi na mbili. Akaanza kupita kuanzia mbela hadi akafika nyumba ambapo ndipo nilipo. Akanitazama kwa muda kidogo kisha akanizaba kofi zito la shavu hadi nikahisi wenge. Akaniongeza kofi jengine na akasababisha hasira yangu kuanza kunipanda taratibu.

“Kwa nini una ndevu?”

Alininiuliza kwa ukali.

“Sijui mkuu”

“Hujui ikiwa vipi kidevuni mwako?”

“Mkuu mimi nimekuja jana”

“Ohoo kwa hiyo ulivyo ingia hapa hujajua sheria?”

“Ndio”

“Ukiongea na mimi piga magoti”

Mzee huyu alikoroma huku akinishika bega langu na kunikandamiza chini hadi nikapiga magoti pasipo hiyari yangu.

“Nyoosha mikono juu kenge wewe”

Nikanyoosha huku machozi yatokanayo na hasira yakianza kunilenga lenga.

“Nyinyi wengine kamalizeni kazi yangu ya jana”

Wezangu hawa wakatawanyika na nikabaki peke yangu katika huu uwanja ulio jaa vumbi.

“Bingiria”

“Nini!!?”

Niliuliza kwa mshangao. Akanisukumiza kwa teke na nikaanguka chini, akachomoa mkanda wa suruali yake na kuanza kunitandika nao huku akinisisitiza kwamba nibingirie kwenye vumbi hili tena la udongo mwekundu kama wa mkoa wa Morogoro. Nikatii amri huyo huku nikiendelea kutandikwa.

“Twende twendeeee”

Alizungumza huku akinipiga na mkanda huu.

“Mkuu nina tii kwa nini una nipiga”

“Una semaje wewe kenge?”

“Nina tii acha kunichapa?”

“Jeuri wewe ehee?”

Akanipiga teke la kwanza likatua mgongoni, teka la pili nikaudaka mguu wake na kwa kasi ya ajabu nikamzusha mguu huo na akaanguka kifudifudi, akajaribu kuchomoa bastola yake kiunoni ila nikamzuia kwa kuvunja vidole vya kiganja chake cha kulia na kumfanya apige yowe. Nikawaona wanajeshi wawili wenye bunduki wakija eneo hili kwa kasi kubwa. Nikamtandika mgumi sita za uso za haraka haraka hadi wanajeshi hawa wanafika eneo hili na kuninyooshea bunduki zao, pua ya mkuu wetu ina mwaga damu huku ikiwa imepinda kwa maana ngumi karibia nne nime mpiga puani mwake.

“Mka…ate…ni”

Alizungumza kwa shida na nikatii amri ya kunyoosha mikono juu. Mwanajeshi mmoja akanipiga na kitako cha bunduki mgongoni mwangu na nikaanguka chini. Wakaanza kunishambulia kwa mateke, sikuhitaji kupigana nao na cha zaidi ni kujilinda wasiniumize shemeu zangu za siri na usoni. Mlio wa bunduki iliyo pigwa hewani ikawafanya wanajeshi hawa kuacha kunishambulia.

“Muna fanya nini?”

Nikageuka nyuma taratibu na kumuona mkuu wa jeshi hili akifika eneo hili.

“Mkuu amemshambulia mwalimu wa mazoezi”

“Ime kuwaje hadi umeshambuliwa na wewe?”

Mkuu huyu aliuliza huku akimtazama mwalimu wa mazoezi kwa macho makali.

“Mkuu huyu kijana hatufai?”

“Hujajibu swali”

“Ni…limuambia abingirike kwenye vumbi, nikawa nina mchapa mkanda akanishambulia”

“Aligoma ulipo muamrisha kubingirika?”

“Hapana”

“Kwa nini ulikuwa una mchapa?”

“Ni jeuri mkuu”

“Mchukueni mwalimu wenu akapewa huduma ya kwanza.”

Mwalimu huyu akaondokelewa eneo hili na vijana wake na nikabaki eneo hili na kijana huyu.

“Kwa nini ume mshambulia?”

“Muheshimiwa aliku….”

“Kwanza ukizungumza na mimi nyanyuka”

Tartaibu nikanayanyuka huku mwili mzima ukiwa umejaa vumbi.

“Alinipiga vibao viwili akidai kwamba nina ndevu. Sasa mimi ni mgeni sikuelewa sheria za hapa zipo vipi. Akaanz akunipiga mateke na kuniaamrisha nibingirike na mwisho wa siku hasiri ikanipanda kama binadamu nikampima nguvu, ila nikaona hana uwezo huo kama nilivyo kuwa nina muona”

“Rudia umesema hada nini?”

“Uwezo huo mkuu”

“Una taka kuniambia mwalimu wangu hana uwezo wa kufundisha hili jeshi?”

“Naweza kusema ndio au hapana”

“Dogo una niletea siasa. Ndio au hapana maana yake ni nini?”

“Maana yake ni kwamba kwenye mapigano naweza hisi hana uwezo. Ila kimbinu za kijeshi labda ana weza kuwa ni mkali kwa maana mimi sio mwanajeshi na nilikuwa mlinzi mgambo ambaye mafunzo yetu ni ya kiwango kidoo sana”

“Ohoo. Hivi una jua adhabu ya kukataa kumtii mkubwa wako ni nini?”

“Ahahaa?”

“Ni kifo”

Nikastuka sana huku nikimtazama jamaa huyu ambaye kusema kweli hajabarikiwa kuwa na sura nzuri hata kidogo.

“Usinitumbulie macho, adhabu yako ni kifo. Ila kutokana ni mgeni nita kupa nafasi moja ya mwisho”

“Ohoo nashukuru sana mkuu mandevu”

Nilizungumza kwa furaha huku nikiwa nimeinama kiheshima.

“U…umenii.taje?”

Aliniuliza kwa ukali kidogo nna kujikuta nikinyanyua uso wako ngukumtazama.

“Rudia ume niitaje?”

“Mkuu mandevu”

Akakunja sura hadi nikahisi moyo una pasua kifua kwa jinsi unavyo nienda kasi kwa wasiwasi. Gafla akaanza kucheka kwa nguvu hadi nikamshangaa.

“Wewe ndio mtu wa kwanza kuniita hilo jina. Nime nipenda”

“Kweli?”

“Ndio, ila nina itwa jenerali Obote. Sinto hitaji kusikia ukinyanyua kinywa chako kuniita mandevu”

“Nisamehe mkuu sinto zungumza tena”

“Adhabu yako ya kifo ita amuliwa kwenye pambano la leo. Utapigana na kijana wangu, mlinzi wangu namba moja. Akikupiga, nita kwenda kukudumbukiza kwenye kisima cha mamba, wata kutafuna na kukugawanya vipande vipande hadi utakuwa historia. Ila endapo uta mpiga, basi nita jua nini cha kufanya”

“Asante sana mkuu”

Akaniatzama kwa macho yaliyo jaa udadisi kisha akaondoka eneo hili huku mikono yake akiwa ameikweka nyuma.

“Obote”

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitazama mambo wanayo yafanya wanajeshi wengine. Kutokana sijapangiwa kazi yoyote nikamfwata mwanajeshi mmoja.

“Broo vipi?”

“Poa”

“Bafu hapa lipo wapi?”

“Wewe ni mgeni?”

“Ndio”

“Unaona kule”

Akanionyesha jengo lililopo mbali kama mita mia mbili hivi.

“Ndio”

“Yale ndio mabafu na vyoo”

“Sawa nashukuru”

Nikaondoka na kuelekea katika mabafu na vyoo hivi. Nikakuta wanajeshi wengine wakifanya usafi, nikasalimiana nao.

“Naweza kuoga kidogo?”

“Huoni kama nina fanya usafi au?”

Mwanajeshi mmoja mwenye mwili mkubwa alizungumza huku akinitazama kwa macho makali.

“Poa samahani broo, nita subiria hadi mukimaliza”

“Oya tukimaliza milango yote ina fungwa na hakuna mtu kuoga wala kuny**”

Jamaa huyu alizungumza kwa ubabe na wanajeshi wengine wanaonekana kumtii.

“Ila broo, nina oga mara moja tu”

“Dogo una zingua. Umekja na una taka kumtawala kila mtu nsi ndioa.”

“Hapana”

“Ila?”

“Si munaona mavumbi yalivyo nijiaa washkaji nina omba tu”

“Oya sepa kabla hatujakufanya kiti kibaya”

Wakanikatalia katukatu nikaona isiwe shida kwani kukaa hivi na vumbi sinto kufa wala kupungua mahali popote. Muda wa kupata chakula cha asubuhi ukawadia, nikawa miongoni mwa wanajeshi wana kwenda kupata kifungua kinywa.

“Rashidi vipi mbiringo ume kukuta nini?”

Razaro aliniuliza huku akinishangaa jinsi nilivyo jawa na vumbi mwilini mwangu.

“Kubiringirika”

“Wee acha tu ndugu yangu”

“Nimesikia umepiga mwilimu?”

“Aliniudhi”

“Mkuu amekuambiaje?”

“Ameniambia kwamba amenipatia adhabu ya kifo”

“Duu, ila mbona upo kawaida kama huna hofu ya kifo”

“Kanipa pambano la kupigana na mlinzi wake namba moja endapo nikipigwa nina uwawa na nikimpiga ata fikiria nini cha kufanya”

“Aisee bora ukubali kuuwawa kwa risasi kuliko kuuwawa na huyo jamaa. Kwanza ana tisha ana roho mbaya na ana uwezo mkubwa sana wa kupigana”

“Weee!!”

“Haki ya Mungu vile kwa nini nikufiche. Sisi wote tuna muogopa ni mtu mbaya kwa kweli”

“Anapigana staili gani?”

“Zote unazo zijuia wewe. Karete, ndondi, taikondo. Kiufupi ni mtu aliye kamilika na kwa mara kadhaa amekuwa akimuokoa mkuu kwenye majanga mengi hususani ya kuvamiwa”

“Liwalo na liwe, kufa ni kitu cha kawaida sana”

“Broo usiseme hivyo?”

“Kufa kwa kupigwa risasi ni aibu kubwa sana kwa mwanaume. Bora nikafie ulingoni ili nionekane kweli mimi shujaa”

“Haya”

Tukamaliza kula na nikajumuika na Razaro katika kusimamia shamba moja kubwa la mahidi, linalo limwa na wananchi walio tekwa na jeshi hili. Wananchi hawa kwa kweli wana teseka na wana teswa vibaya na wanajeshi hawa.

“Kwa nini wana watesa wana nchi?”

Nilimuuliza Razaro huku nikimtazama usoni mwake.

“Hawana faida hawa. Kazi yao ni kutuchoma kwa wanajeshi wa serikali. Ila wata jua umuhimu wetu siku Obote takapo chukua nchi na kuwa raisi”

“Ila hawa ni waafrika wezetu?”

“Rashidi unapo kuwa hapa ina bidi kuwa na roho ya kinyama acha kuwa na roho ya kike kike”

Razaro alizungumza huku tukimtazama mwanajeshi mwenzetu jinsi anavyo mpiga mateke mzee mmoja aliye jaribu kupumzika kwa kuchoka.

“Mwanangu acha bwana”

Nilizungumza huku nikimfwata mwanajeshi huyo ila nikajikuta nikisiama mara baada ya mwanajeshi huyo kuninyooshea bundiki.

“Usiingilie biashara zangu”

Mwanajeshi huyu mweusi kama chungu cha uketo alizungumza kwa ukali huku akinitazama machoni mwangu.

“Poa”

Nikarudi nyuma hadi sehemu alipo simama Razaro. Nikazidi kupata uchungu mara baada ya kumuona mwana mama mmoja akipigwa na wanajeshi wengine ambao ni vijana wadogo ambao kwa kukadiria ni kama miaka kumi na sita au kumi na saba hivi.

“Kuua kwetu ni jambo la kawaida sana, kwa maana hata sisi kuuwawa ni jambo la kawaida sana. Hivyo usishangae kila kinacho endelea Rashidi”

Sikumjibu chochote Razaro zaidi ya kuimezea hasira na machungu ninayo yapata kutokana na kuteswa kwa wananchi hawa.

‘Ina bidi nitafute nguvu. La sivyo hawa wnanchi wata zidi kuuwawa’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikikunja ngumi mikono yangu yote miwili. Tukashinda shambani hapa hadi majira ya jioni na wananchi hawa wakarudishwa kwenye magareza yao yenye ulinzi mkali kisha tukarudi kambini.

“Ina bidi ule mapema kwa ajili ya pambano lako”

Razaro alinishauri na akanifanyia mpango wa wapishi, wakanipatia chakula cha kutosha, nikala mapema huku nikiwa na mawazo mengi sana kuhusian ana familia yangu, hususani mama yangu na mwanangu.

‘Ila wapo sehemu salama, japo najua wata kuwa na wasiwasi mkubwa sana na mimi. Ila makamu wa raisi, haya mateso ninayo tapitia kisa mke wnagu nina kuapia haki ya MUNGU nita hakikisha siku nikikukamata mkononi mwangu nita kukamuaa kama mafuta ya alizeti yanavyo kamuliwa’

Niliwaza huku nikiliminya kwa nguvu tonge la ugali hadi likaanza kujitokeza kwenye upenyo wa vidole vyangu. Nikamaliza kula na nikajiandaa kisaikolojia kwamba muda wa mimi kwenda kuyaokoa maisha yangu ume wadia. Wanajeshi wakatangaziwa kwamba usiku wa leo kuna pambano kati ya mlinzi wa raisi na mwanajeshi mgeni.

“Ulingo hvii upo wapi?”

Nilimuuliza Razaro huku nikimtazama usoni mwake.

“Uta uona tu”

Muda ukafika wa kuelekea ulingoni. Nikaingi katika bwala la chakula na kukuta likiwa limetengenezewa ulingo katikati huku wanajeshi wakikaa kwa mtindo wa kuzunguka ulingo huu. Nikawa wa kwanza kuingia ulingoni huku wanajeshi wengi wakinizomea. Nikamtazama bwana Obote eneo alilo kaa na kumuona akivuta sigara yake kubwa. Kijana wake aliye simama nyuma yake akapia hatua hadi karibu ya ulingo huu huku akinitazama kwa macho makali. Akavua shati lake na kumrushia mmoja wa mwanajeshi ili alishike. Akachezesha kifua chake kisha akaingia ulingoni. Kengele ikagongwa kuashiria kwamba pambano limeanza. Nikamfwata kwa kasi mwanajeshi huyu na nikampiga ngumi za uzito wangu wote kifuani mwake. Ila cha kushangaza hajatikisika wala hajaonyesha dalili kama ameumia zaidi alicho fanya ni kunipa ishara kwamba niendelee kumpiga ngumi nyingine huku usoni mwake akiwa amejawa na tabasamu la dharau linalo ashiria kwamba ngumi ninazo mpiga si chochote kwake.


*************************************************

Hofu ikanitawala kidogo ila nikajitahidi kuhakikisha kwamba hofu ina nitoka kwani ikiendelea kunitawala ndio mwanzo wa kupigwa shindano hili. Jamaa huyu akanisisitiza nimpige ngumi nyingine kwa maana haumii. Nikatazama katikati ya mipaja yake na nikaona upenyo mzuri wa kuweza kupitia teke. Nikamtisha kama nina mpiga ngumi ya uso akarudisha uso nyuma. Nikampiga teka zito la sehemu za siri na kumfanya ajikunje huku akitoa mguno wa maumivu. Kuinama kwake kukanipa nafasi ya kumpiga kigoti cha kichwani na akaanguka chini, nimrukia na kumpiga kisukusuku cha kifuani na kumfanya azidi kuguumia kwa maumivu makali sana. Akajaribu kujitutumua ili anyanyuke ila nikazidi kumtandika ngumi mfululizo za usoni mwake, hadi nikampasua eneo la juu ya jicho la kulia na damu nyingi zikatawala usoni mwake. Nikanyanyuka huku nikimtazama jinsi anavyo jaribu kusimama huku dhairi akiwa amejawa na hasira. Akaanza kunishambulia kwa hasira na ninacho kifanya ni kumkwepa huku nikimpiga mapigo ambayo hayatarajia. Kwa asilimia mia moja watu wote humu ndani hakuna hata mmoja ambaye aliamini kwamba nina weza kumpiga huyu mbabe wa wababe. Kadri jinsi muda unavyo kwenda ndivyo jinsi nilivyo jikuta nikimzidi kimbinu na hali ikazidi kuwa mbaya. Kitu ambacho jamaa huyu alikikosea toka mpambano huu una anza ni kunidharau na kunipa mimi nafasi ya kufanya ninacho taka huku akiamii ana pigana na kibonde. Nikazidi kuwadhihirishia kwamba mimi sna mazoezi ya kijeshi ila nina kipaji cha kupigana. Kipaji ambacho ni watu wachache sana huwa tuna barikiwa. Nikampiga kabali moja takatifu, akaaribu kujitoa kabali hii ila nikazidi kumkaba hadi nikaanguka nay echini. Taratibu akaanza kulegea hadi akatulia tuli na kuzimia. Nikanyanyuka huku mwili ukiwa umelowana na jasho, watu wote ndani hapa wametulia kimya. Obote akasimama huku akinitazama, akaanza kupiga makofi na kuwafanya wanajeshi wengine nao kuanza kupiga makofi ya kunipongeza. NIkashuka ulingoni na kumsogelea Obote alipo simama.

“Mkuu nime kamilisha kazi yangu”

“Hongera sana. Sasa nenda kaoge upumzike na kesho asubuhi uta patiwa mavazi mapya na nita kupa nafasi”

“Shukrani sana mkuu”

Nikatoka ukumbini hapa na kurudi katika bweni letu la kulala. Razaro akawa mtu wa kwanza kuingia ndani hapa huku uso wake ukiwa ume jawa na furaha sana.

“Hongera sana”

“Nashukuru”

“Vipi huja umia?”

“Maumivu tu kwa mbali”

“Aisee pole sana. Aisee ume mpigaje pigaje yule jamaa?”

Wanajeshi wengine wakaingia huku kila mmoja akinipongeza kwa kazi niliyo ifanya. Nikaanza kupata marafiki wapya ambao kwa siku ya jana sikuweza kuwapata. Kila mmoja ana niuliza siri ya kumpiga jamaa yule huku wengine wakiniuliza mimi ni nani kwani.

“Jamani ndugu zangu naombeni nikaoge tuta zungumza kesho”

“Sawa sawa”

Nikaelekea bafuni nikaoga na nikarudi bwenini kwa ajili ya kujipumzisha.

“Rashidi”

Razaro aliniita huku nikiwa nimelala kitandani kwangu ambapo ndio kitanda cha juu.

“Ndio kaka”

“Wewe una mafunzo ya kijeshi?”

“Hapana”

“Ila mbona ume weza kumpiga jamaa?”

“Mimi ni mpiganaji, nina pigana ngumi za ulingoni na ngumi za mtaani”

“Ndio maana, una jua jaa hajaweza kupigwa na mtu hata mmoja hapa kambini”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu. Leo wewe ume weka rekodi”

“Basi ni jambo la kumshukuru Mungu”

“Ila ukipata nafasi kwa mkuu usitusahau ndugu yangu”

“Usijali”

Tukazungumza mambo mawili matatu na usingizi ukatupitia sote wawili. Asubuhi na mapema nikaletewa mavazi mengine ambayo yana nyota mbili begani, kwa kweli sitambui utambuzi wa vyeo vya kijeshi hivyo nina jioanea mapicha mapicha.

“Ukisha maliza kuva ina bidi twende ofisini kwa mkuu”

“Sawa”

Nikabadilisha nguo na kuvaa hizi nilizo letewa kisha nikaondoka bwenini hapa na mwanajeshi huyu aliye niletea nguo na kuelekea ofisini kwa mkuu. Nikaingia ofisini kwa mkuu na kumsalimia.

“Kaa bwana Rashidi”

“Nashukuru”

“Una jua ni kwa nini nimekupandisha cheo?”

“Hapana?”

“Kwa sababu ume mpiga tena na kumzimisha mtu ambaye nilimtegemea sana na kumuamini kwamba ni chuma ila wewe ume kuja kumzimisha hahaaa sijapata kuona”

“Nashukuru mkuu”

“Nahitaji uwe mshauri wangu. Hususani nikiwa katika harakati za kwenda kuichukua hii nchi na niwe mtawala”

Nikakaa vizuri kwenye kiti kwa maana kuwa mshauri wa kiongozi huyu anaye onekana ana tumia nguvu pasipo akilini jambo kubwa sana kwangu japo na mimi sina elifum kama ile ambayo wanashauri wengi wa viongozi wamekuwa wakiipata.

“Hilo halina shaka mkuu”

“Safi, nikupe stori fupi kidogo ili tuweze kwenda sawa. Miaka sita iliyo pita nilifukuzwa na raisi huyu aliyopo madarakani. Nilikuwa ni jenerali wa jeshi. Alinifukuza kazi mara baada ya mimi na yeye kupisha kiitikadi. Yeye ana iongoza nchi kwa matakwa yake na sio kwa matakwa ya wananchi. Hata zikipigwa kura na akashindwa bado tume za uchaguzi zina mtangaza yeye kama mshindi. Familia yake ina ishi kama pepoini ila wananchi wana ishi kama kuzimu. Hivyo nilipo fukuzwa nikaona hapa, nikaanzisha jeshi langu kwa maana kuna wanajeshi walikuwa wakinisikiliza na kuniamini mimi. Kitu nilicho kifanya ni kuingia msituni na kuwafua wanajeshi wangu kwa ajili ya kufanya mapinduzi. Tulijaribu kufanya mapinduzi mara moja ila tulishindwa na wanajeshi wangu wengi wakauwawa. Ila nime jipanga upya sasa nina hitaji kumtoa madarakani moja kwa moja”

“Sawa sawa mkuu. Kwanza pole kwa kuwapoteza vijana wako”

“Nimesha poa. Hembu nipe mpango wako, nini nifanye”

“Kuna mapinduzi ya aina nyingi hususani katika nchi. Kuna mapinduzi ya kutumia nguvu ndio hayo uliyo yafanya na mwishowe uka shindwa. Kuna mapinduzi ya kutumia akili”

“Ehee nipe sasa jinsi ya kutumia akili”

“Nina imani raisi kuna watu ambao wana mpa nguvu?””

“Yaa wapo wanao mpatia nguvu”

“Siku zote ukitaka kuuvunja mti mkubwa, endapo uta kata matawi kuna asilimia kubwa sana kwa mti huo kuweza kuchepua matawi mengine na ikawa ni kazi ya kujinga. La kukushauri hapa ni kukata mizizi inayo shikilia mti na endapo una baki mzizi mmoja, hata ukiwa peke yako basi una weza kuusukuma mzizi huo na ukaanguka chini”

“Aiisee kichwa chako kipo very smart sasa nina anza kupata picha”

“Nashukuru kama ume elewa mkuu. Mizizi ni hao watu wanao mshikilia raisi. Tuanze na hao, tuna waua katika fifo vya kutumia akili. Kwani kuna njia zaidi ya elfu moja za kuweza kumuangamiza mtu”

Nikamuona Obote akikaa vizuri kwenye kiti chake na kuendelea kunisikiliza kwa umakini sana.

“Tuna weza kuwaua kwa ajali, sumu, kuwagombanisha wao kwa hao hususani kwenye biashara. Kuwabambikia kesi naa wakafungwa na huyo raisi wao. Sasa hapa ina bidi uchague tuanze na njia ipi?”

“Mmmmm ngoja nikupe listi ya watu saba wenye nguvu hapa nchini na ndio wanao mpa kiburi huyo kiongozi kwa maana wana nufaika kupitia uovu wake ana ufanya”

“Sawa nipatie”

Jenerali Obote akafungua laptop yake na kuanza kunionyesha watu hao ambao wote ni mawaziri wa nchi hii.

“Kila mmoja unaye muona hapo ana nguvu kwenye hii serikali”

“Sawa, hawa tuta waua taratibu, nipatie usiku wa leo niweze kupanga huyu afe vipi na huyu afe vipi na akibakia raisi, basi ni raisi kuiteka ikulu na kumtoa madarakani na kujitangazia uraisi”

“Sawa sawa”

“Sawa chukua muda wa kutosha”

“Ila ukiachana na hilo, nina wazo moja au ushauri”

“Niambie tu Rashidi. Nitapenda uwe una niambia ukweli na wala usiniogope”

“Sawa. Kuna wananchi wale ambao wameshikiliwa mateka kule mashambani.”

“Ndio ndio nina watambua”

“Wana teseka sana, wana pugwa na wana nyanyaswa sana. Kumbua kwamba una hitaji kuingia kwenye hii nchi na kuwaongoza hawa wananchi. Endapo wata poteza imani na wewe huku ambapo bado hujawa kiongozi wa nchi basi siku ukiingia madarakani, wata jiunga na wata kupindua kama unavyo panga kwenda kumpindua huyu”

“Nime kuelewa”

“Wale wananchi ina bidi wapate matunzo mazuri, ina bidi waweze kutengenezewa mazingira mazuri ya hata kukupenda wewe. Wana pigwa na kuumizwa sana, jaribu kulitazama hilo”

“Nime kuelewa basi nita hakikisha wana ishi mamisha mazuri”

“Nashukuru kwa kunisikiliza”

“Kuwa na amani kwa maana sasa hivi wewe ndio mshauri wangu”

“Asante. Nina ombi moja”

“Ombi gani?”

“Nina omba baada ya kuyamaliza mambo yako naomba unisaidie kudili na adui yangu”

“Huyo makamu wa raisi wa Tanzania?”

“Ndio”

“Usijali tuta dili naye kimya kimya”

“Kitu kingine nina penda sura yangu iwe ya kificho sinto penda sura yangu ifahamike hata tutakapo kuwa tuna toka na kuelekea sehemu yoyote basi ningependa kuifunika sura yangu”

“Hilo halina shaka. Chukua laptop yangu kawapitie hao watu na mchana uweze kunirudishia”

“Sawa”

Nikatoka ndani hapa nikiwa na laptop ya Obote. Nikaomba ofisi ili niweze kuifanya kazi yangu, kitu cha kwanza kukifanya ni kuingia kwenye mtandao wa Facebook, nikaitafuta akaunti ya Jackline na kukuta akiwa ameposti picha zangu huku akitangaza dau la Euro milioni tano kwa mtu yoyote atakaye fanikisha kuniona, nikiwa hai, Huku wingi wa posti zikiwa ni za kumuomba Mungu aweze kunilinda sehemu yoyote nilipo. Nikatamani kumtumia meseji kwa akaunti yangu hii mpya niliyo ifungua ila nikajikuta nikisita.

‘Ina bidi nimalize mission yangu’

Nilizungumza huku nikiachana na maswala ya kuitazama akaunti ya Jackline na nikaanza kumfwatilia kiongozi mmoja baada ya mwengine katika mtandao hadi nikafanikiwa kuwatambua vizuri wao na familia zao. Nilipo maliza kazi yangu nikamrudishia Obote laptop yake.

“Kesho nitakupatia plan ya kuwua”

“Sawa, kuna sehemu nina hitaji tuelekee mchana huu kapate chakula kisha twende”

“Sawa mkuu”

Nikajumuika na wanajeshi wengine kupata chakula cha mchana huku wengi wao wakionekana kunipigia saluti kwa maana nime pata cheo kikubwa kuliko wao.

“Ndugu yangu kuna msemo mmoja unalala masikini na una amka tajiri ndio wewe”

Razaro alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Hahaa ni mambo ya kawaida haya ndugu yangu. Yana pita tu”

“Ina onekana bosi amekukubali sana”

“Tuachane na hayo ndugu yangu. Kuna vitu nina hitaji uwe una nisaidia kama unavyo jua mimi ni mgeni na nchi hii ya Congo”

“Sawa ndugu yangu mimi na wewe tupo pamoja”

“Sawa nita kushirikisha baadae wakati wa kulala”

“Poa ndugu yangu”

Majira ya saa tisa mchana tukaondoka eneo hili na Boaz katika gari lake aina ya Range Rover Sport. Huku mbele ikiwa ime tangulia gari iliyo jaa wanajeshi aina ya pic up huku nyuma napo kukiwa na gari aina ya pic up iliyo jaa wanajeshi.

“Tuna kwenda wapi mkuu”

“Nina kuonyesha jinsi nilivyo tawala mji huu”

“Ahaa”

“Yaa japo kuna vikosi vya serikali vina jaribu kuleta unoko unoko wa kujaribu kuchukua maeneo ila wana shindwa kwa maana tuna wahimili”

Tukapita kwenye mojaya mji ambao ume jaa majumba mengi yaliyo haribiwa vibaya kwa mabomu.

“Unapo kuwa na haya ya kutawala eneo hususani Afrika ni lazima utumie mabavu na ndio nilicho kifanya”

Obote alijisifia huku akivuta sigara yake hii.

“Kwa hiyo huku kote kulikuwa na mapigano?”

“Ndio kuyatoa majeshi ya serikali haikuwa kazi rahisi”

Safari ikazidi kusonga mbele huku nikiendelea kuonyeshwa baadhi ya maeneo ambapo kila sehemu ulinzi una imarishwa na wanajeshi wa Obote.

“Nina ona wananchi wana endelea na shuhuli zao?”

“Ndio kwa maana wame kubali kuishi chini ya sheria yangu basi kila mtu ata ishi kwa amani. Tukafika katika moja ya gorofa majira ya saa moja usiku.

“Hapa kuna night club tuingie tule bata kidogo kabla ya kurudi kambini”

“Sawa mkuu”

Nikachukua kitambaa na kujifunga usoni mwangu, nikavaa kofia yangu huku nikiwa katika vazi hili la kijeshi ambalo limenipendeza sana kwa haraka haraka una weza kusema mimi ni mwanajeshi kumbe ni ngekewa tu ime niangukia. Ndani ya ukumbi huu kuna wasichana wa kila aina huku asilimia kubwa ya wasichana wapo uchi kabisa huku wengine wakiwa wamevalia bikini.

“Rashidi furahia maisha”

Tukaa kwenye moja ya sofa huku wanajeshi wakizunguka. Wakachaguliwa wasichana kadhaa walio wazuri na kuanza kutukatikia mauno.

“Ahaa mimi sihitaji”

Nilizungumza huku nikimtoa mapajani mwangu msichana mwenye makalio makubwa anaye nikatikia mauno.

“Rashidi usione aibu”

Obote alizungumza huku akimpiga vibao msichana mmoja kwenye makalio yake.

“Usijali mkuu nipo poa”

“Au una taka kwenda kumpa mambo kwa maana kuna vyuma eneo hili”

“Hapana nipo sawa tu”

“Sawa pata kinywaji”

Nikaagizia maji huku nikiwa makini sana kuhakikisha kwamba nina kuwa salama eneo hili kwani nime ongozana na mtu ambaye nina imania na maadui kila sehemu na muda wowote ana weza kushambuliwa. Ikatimu saa nane usiku na tukaondoka eneo hili huku Obote akiwa amelewa sana.

“Rashid”

“Ndio mkuu”

“Yaani wana wake wa Kikongo wana kum** tamu sana. Kwa nini hujataka kumtomb** mmoja?”

“Hapana mkuu ipo siku nita waonja”

“Yaani nime tomb** wanawake wanne aisee ni watamu sana”

Nikatabasamu tu kwa maana matukio hayo yote nimeyashuhudia jinsi Obote alivyo kuwa akiwatafuna wasichana hao ambao wana onekana ni malaya.

“Ina bidi sasa hivi nioe kwa maana si una jua nikiingia ikulu ni lazima niwe na mke”

“Ume pata mwanamke wa kuoa?”

“Nita tatufa kati ya vigori mtaani”

“Ahaa ni jambo jema”

“Simamisheni gari”

Obote alizungumza na gari likasimamishwa. Akafungua mlango wa gari na akashuka, akasogea pembeni ya barabara na akainama huku akianza kutapika.

“Mkuu vipi?”

Nilimuuliza huku nikiwa nime inama pembeni yake.

“Pombe nime kunywa nyingi sana”

“Pole mkuu”

“Ngoja nijitapishe”

Gafla tukaanza kusikia milio ya risasi ikianza kurindima jambo lililo tufanya sisi wote tuanze kuchanganyikiwa kwa maana ni hatari ambayo hatujaitarajia majira kama haya ya saa nane usiku.


“Ina tokea wapi milio hiyo?”

Obote alizungumza huku akisimama wima. Wenge lote la pombe limemtoka

“Naona ina tokea upande ule wa kaskazini”

Mwanajeshi mmoja alizungumza huku tukitazama kwenye vilima vilivyopo upande wetu kwa kaskazini.

“Wasilianeni nao tujue kuna nini kimetokea”

Obote alizungumza huku sote tukirudi katika magari na kuondoka eneo hili.

“Nini kinacho endelea?”

Mwanajeshi aliye kaa siti ya mbele alizungumza kwa kutumia simu ya upepo.

“Kuna wanajeshi wamevamia. Wanajeshi wa umoja wa mataifa, tuna jaribu kuwazuia?”

Nikamtazama Obote usoni mwake.

“Wamewazi au?”

“Hapana tume wazidi, ila tuna omba msaada zaidi”

“Sawa jeshi lina kuja hapo”

Mwanajeshi huyo alizungumza na Obote akamrisha wanajeshi walio karibu na upande huo kueelekea eneo la tukio.

“Washenzi wana jifanya wana taka kuurudisha huu mji kwenye mikono yao. Rashidi asubuhi nahitaji unipatie mbinu za kuwateketeza haraka iwezekanavyo”

“Sawa mkuu”

Tukarudi kambini huku Obote akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana kwani bado mapambano yana endelea. Nikaelekea bwenini na kukuta wanajeshi wengine wakiwa wamelala. Nikavua nguo zangu na nikabakiwa na bukta ya ndani na nikapanda kitandani. Akili yangu ikajawa na mawazo mengi hususani kwa shida ambazo Jackline na familia yangu wana zipitia kwa sasa. Hadi kuna pambazuka hata lepe la usingizi halikunipitia. Mara baada ya kujiandaa nikaelekea ofisini kwa Obote na nikamkuta akiwa na mlinzi wake niliye mpiga ulingoni.

“Mkuu huyu amepandishwa cheo?”

“Kaa kimya”

Obote alimkanya mlinzi wake huyo kwa ukali kidogo, nikamsalimiana nao japo mlinzi huyo hajaitikia salamu yangu ila sijajali hilo kabisa. Nikaanza kumueleza mbinu za jinsi ya kuweza kuwamaliza wanao mpa nguvu raisi wa nchi hii, mmoja baada ya mwengine.

“Wewe ni genius, sikuwahi kufikiria hili jambo siku hata moja. Umeona mwenzako ni kichwa?”

Obote alimuambia mlinzi wake huyo ambaye dhairi anaonyesha kuchukizwa na nafasi niliyo ipata.

“Kazi hii ina anza leo. Tuna anza na huyu waziri wa ulinzi, niandalie makomandoo wanao weza kufianya kazi hii”

“Sawa”

Mlinzi huyu akatoka na kutuacha sisi wawili.

“Naona kijana haamini kama ume mpa kichapo. Hapa alikuwa ana niomba niandae pambano la marudio”

“Ume mkubalia?”

“Hapana nime muambia amepigwa hakuna marudio. Kwa maana alipoteza yeye mwenyewe”

“Sawa”

Mlinzi huyu wa Obote akarudishi jibu kwamba makomandoo wapo tayari. Tukatoka ndani hapa na kuelekea katika chumba cha mkutano. Nikawaleza mbinu ya kumuu waziri wa ulinzi, kila mmoja akaifurahia mbinu hiyo na maandalizi ya utekelezaji yakaanza. Makomandoo hawa watano wakaondoka kambini hapa majira ya saa nane usiku na kuelekea eneo alipo waziri wa ulinzi.

“Ina bidi tukae kwenye tv kwa ajili ya kusikia habari za kifo chake”

Obote alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana. Baada ya lisaa moja makomandoo hao wakatutaarifu kwamba wamesha fika eneo alipo waziri wa ulinzi.

“Sawa ifanyeni kazi kwa umakini”

“Hakuna shaka mkuu”

Obote akakata simu hii ya mezani na tukaendelea kutazama tv. Baada ya nusu sana simu ya mezani ikaanza kuita. Sote watatu tukaitazama kwa sekunde kadha akisha Obote akaipokea.

“Ndio”

“Sawa kazi nzuri”

Obote alijibu huku tabasamu pana likiwa lime mtawala usoni mwake. Akakata simu na kutugeukia.

“Kazi tayari waziri wa ulinzi amesha uwawa na vijana wana rudi kambini”

Obote alizungumza kwa furaha, hazikupita hata dakika ishirini, tv ya taifa ikatangaza habari ya kifo cha waziri wa ulinzi kilicho tokea kwa ajali ya gari lake kufeli breki na kupata ajali mbaya iliyo muua yeye na dereva wake.

Obote akanisifu sana kwa, mbinu niliyo itoa ya kukata breki za gari la waziri huyo na dunia nzima imeamini kwamba ajali hiyo ime tokea kwa breki za gari lake kufeli.

Kadri siku zinavyo zidi kwenda ndivyo jinsi ninavyo zidi kupata nafasi katika kikosi hichi cha Obote huku makomandoo hawa wakinipatia mafunzo makali sana huku mipango ya kuwapunguza mawaziri wenye nguvu kwenye serikali ikizidi kuendelea taratibu. Ndani ya miezi kumi na mbili, mawaziri wote wenye nguvu katika serikali ya DRC tumewaua kwa vifo ambavyo vyote hatukuhusishwa kama magaidi. Wapo walio kufa kwa vifo vya ajali, wapo walio kufa kwa vifo vya kujinyonga wao wenyewe huku wakiandika kwamba wameamua kujinyonga ila ukweli ni kwamba tuliwalazimisha kujinyonga kwa kuhofia kuwawa familia zao. Wapo walio jipiga risasi, wapo walio jirusha magorofani na walifanya hivyo mara baada ya kuyatambua madhaifu yao. Rashidi ambaye kipindi cha nyuma nilikuwa sijui chochote, sasa hivi nipo vizuri sana. Mafunzo niliyo yapata kwa mwaka mzima katika kambi hii ya waasi yamenifanya niweze kujitegemea mwenyewe.

“Leo ni siku ambayo tuna kwenda kuiteka ikulu. Leo ndio siku ya kuipindua hii serikali, kwa pamoja tuna imani tuna weza”

Obote alizungumza mbele ya wanajeshi wake wote huku mpango wa kuipindua ikulu, tukiwa tumesha upanga miezi saba nyuma huku kukiwa kumetengenezwa njia maalumu ya ardhini ambayo hutokea ikulu. Ramani na mipango yote ya jinsi gani ambavyo tuna weza kuingia ikulu niliipanga mimi. Hapa ndipo ninapo jigundua kwamba nina kipaji kingine ambacho hapo awali sikuweza kukijua. Kipaji cha kuweza kutengeneza mpango na mpamgo ukafanikiwa. Ni watu wachache sana wenye uwezo wa kutengeneza mipango tena ya matukio kama haya ikakamilika kama walivyo panga.

“Chidi nina omba tuzungumze”

Obote alizungumza mara baada ya kushuka jukwaani. Tukaingia ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo.

“Ehee niambie mkuu”

“Kwa nini hutaki nikupatie uongozi kwenye serikali yangu ikiwa ni mengi sana ume weza kunisaidia ndugu yangu?”

“Natambua kwamba ni mengi tumefanya na kuwepo hapa na ukanipatia nafasi ume weza kunifanya niweze kujijua kwamba mimi ni mtu wa aina gani. Natamani sana kuwa katuika ufalme wako, ila nina omba sana niwee kushika njia yangu kwa maana kuna watu nina hitaji kudili nao kwa asilimia mia moja. Tafadhali ndugu yangu, utakapo kuwa una hitaji ushauri wangu basi nitatengeneza njia ya kuwasiliana mimi na wewe”

“Sawa ndugu yangu. Ila ningependa nikupatie hata uwaziri mkuu”

“Hahaa hapana kaka. Una jua nina adui na huyu panya ambaye kwa sasa ni raisi Tanzania. Nina hitaji kudili naye vizuri sana. Nikiwa waziri wako mkuu ata tafuta chokochoko za kukuondoka madarakani”

“Sawa”

Obote akaridhika na ombi langu. Msaada mkubwa sana wa kijeshi tuna upata kutoka katika nchi ya Russia na wame msaidia Obote kuanzia pesa, silaha pamoja na wanajeshi makomandoo walio tupatia mafunzo ya ziada. Majira ya saa kumi na mbili ikaanza safari ya kutembea katika njia iliyo chini ya ardhi kuelekea katika ikulu ya raisi. Uzuri ni kwamba ya siri wanajeshi kama hamsini hivi eneo la karibu sana na ikulu na hapa ndipo kuna njia hii ya siri inayo elekea hadi ikulu. Mimi na Obote pamoja na walinzi wake ndio tuna ongoza harakati hizi huku wanajeshi wengine wakiwa wana jiandaa kwa ajili ya kuvamia mji mkuu ambapo ndipo ikulu ilipo na endapo tuta fanikiwa kuishikilia ikulu basi raisi hato kuwa na ujanja.

Tukafika eneo la chini kabisa ya ikulu. Obote akatoa ramani niliyo ichora inayo onyesha jinsi gani ambavyo ikulu ipo kwa juu. Mtaalamu wa I.T akafungua laptop yake na kutuonyesha mazingira ya juu yanayo rekodiwa na CCTV kamera za ikulu hii jinsi alivyo zidukua. Baada ya maelekezo mawili matatu aliyo tatoa Obote, tukapandisha ngazi kuelekea eneo la juu la ikulu, ambapo lina tokea katika moja ya stoo ya kuhifadhia chakula. Kijana wa I.T akazinatisha kamera zote za ikulu na walinzi walipo katika chumba maalumu cha kuongozea kamera hizo hawakugundua chochote kwa maana wana ona hali ya kawaida tu. Tukaanza ikulu taratibu majira ya saa mbili usiku. Tukaanza kazi ya kuwaua walinzi wa ikulu kimya kimya hadi wakakabaki wachache. Mimi na Obote pamoja na mlinzi wake. Tukaingia katia eneo analo ishi raisi na familia yake na tukawakuta mezani wakiwa wana kula chakula cha usiku. Kuingia kwetu kukawastua sana na kumfanya raisi na familia yake kujawa na woga mwingi sana.

“O…oobote?”

Raisi alibabaika huku tukiwa tume wanyooshea bunduki.

“Kaa chini”

Obote alizungumza huku akisogea eneo la meza hiyo.

“Ona munavyo ishi kifahari. Yaani raisi una tumia kikombe kilicho tengenezwa kwa dhahabu kwa kunywea mvinyo huku wananchi wako wakiwa katika hali ya mateso na njaa iliyo kithiri?”

“Obote mimi na wewe ni ndugu kumbuka tulipo toka?”

“Ohoo nakumbuka ulinifukuza tena ukataka kuniua shenzi wewe”

Obote akamtandika riasi ya kichwa jamaa mmoja aliye kaa pembeni ya mke wa raisin a akaanguka chini na kufa. Mke wa raisi na mabinti wawili wanao fanan wanao onekana ni mapacha wakazidi kulia kwa uchungu. Obota akachukua kipande kimoja cha nyama ya kuku na kuaza kutafuna.

“Mmmm tamu sana. Yaani muna ishi kama peponi”

“Obote niambi nini una taka mimi nipo tayari kufanya”

“Ninacho kihitaji ni roho yako na ikulu. Nikikuacha hai uta nirudi”

Obote akawapiga risasi mabiti hawa wawili na wakafariki.

“Naona una mke mzuri sana, mrembo, amejazia na ana kila sifa ya kuwa mwanamke mzuri.”

Obote alizungumza huku akifungua vifungo vya shati la mwana mama huyu, raisi akataka kunyanyuka ila nikampa ishara ya kumtahadharisha kwamaba kinyanyuka tu nina muuua. Obote akamnyanya mwana mama huyu anaye tetemeka kwa woga huku akiendelea kulia kwa uchungu mwingi. Akamuinamisha mezani kifudi fudi.

“Obote mke wangu hana lolote la kufanya juu ya hili”

“Shiiiiiiii…..”

Obote alizungumza huku akipandisha gauni la mwana mama huyu juu.

“Mfungeni kamba huyu kenge”

Mlinzi wa Obote akamfunga pingua raisi katika nondo ya dirisha la hapa ndani na kumfanya asiwe na ujanja wa aina yoyote. Obote akafungua zipu ya suruali yake na kumtoa jogoo wake na kumzamisha katika kitumbua cha mwana mama huyu anaye lia kwa uchungu sana, japa anajaribu kujitahidi asibakwe ila kwa nguvu alizo nazo Obote hakika mwana mama huyu hajaweza kabisa kufua dafu. Raisi akajaribu kujitoa katika pingu hiyo ila ana shindwa na ana mshuhudia jinsi mke wake anavyo bakwa na Obote.

Japo nimejawa na roho ya kikatili ila kwa kitendo hichi na kilio hichi cha huyu mwana mama nikajikuta nikimuonea huruma.

“Mkuu mmalize tu”

“Acha nijilie huyu mwnamke una jua alikuwa ni demu wangu, ila jamaa alinipiku na kumchukua, kutokana alikuwa na nguvu ya pesa na kila kitu. Acha nimle”

Obote alizungumza huku akiwa amezishika nywele za mwana mama huyu huku akiendelea kumbaka. Nikamtazama raisi na kumuona jinsi macho yanavyo mtoka, macho yamekuwa mekundu, na mishipa ya mwili mzima imejichora vizuri kwenye ngozi yake.

“Acha nimle mkund**”

Obote alizungumza huku akimtazama raisi. Nikamshuhudia jinsi anavyo mfir** mama wa watu na kumfanya alie kwa uchungu sana.

“Mery una kumbuka ulivyo nisaliti kisa pesa ehee?”

Obote alizungumza huku akiendelea kufanya kitendo hicho cha kinyama.

“Unakumbuka wewe malaya?”

Obote alizungumza huku akiendelea kumsukumiza jogoo wake kwa mwana mama huyu.

“Sasa hii ndio adhabu munayo paswa kupata malaya kama nyinyi”

Mimi na mlinzi huyu wa Obote tukabaki tukishuhudia mchezo huu hadi mwisho. Obote akachomoa bastola yake na kupiga mwana mama huyu kichwani na damu zikatapakaa katika meza hii iliyo jaa vyakula vya kila aina. Obote akamfuta futa jogoo wake aliye jaa kinyesi cha mwana mama huyu kisha akamrudisha ndani ya suruali yake na kufunga zipu. Akachukua tishu aliyo jifutia jogoo wake na kumsogelea raisi.

“Kula mav** ya mke wako. Ni matamu sana ehee?”

Obote alizungumza huku akimsokomeza raisi tishu hiyo mdomoni mwake.

“Yaani miaka yote hiyo niliyo kuachia yule malaya hukuwahi kumla mkund** kwa maana mkund** wake leo ndio nime utoa bikra”

“Obote bora uniue kuliko dharuahu hii”

Raisi alizungumza kwa suati nzito iliyo jaa uchungu.

“Huhuhuhu….sikuui broo. Ila kuna vijana wangu wata kubaka kama nilivyo mfanya mke wako na baada ya hapo wata kuua wao”

Nikahisi ni utani ila Obote akawaruhusu wanajeshi wanne walio nje ya mlango kuingia ndani hapa.

“Vipi mume maliza kazi nje?”

“Ndio mkuu ikulu ipo mikononi mwetu”

“Najua muna uchu sana, mshuhulikieni jamaa”

Wanajeshi hawa wakaanza kumvua nguo raisi.

“Mkuu tumuue tu”

Nilishauri huku nikimtazama usoni mwake.

“Acha vijana washerekee bwana Rashidi”

Wananjeshi hawa wakamvua nguo raisi kwa mbinde huku Obote akirekodi kwa kutumia simu yake. Bila ya huruma wakaanza kumuingilia kinyume na maumbile raisi ambaye amejitahidi kadri ya uwezo wake kuhakikisha anal inda heshima yake ya kuwa mwanaume ila hajaweza kwani sio rahisi kuwashinda nguvu wanajeshi wanne tena wenye mazoezi makali. Wanaume wote wanne wakamuingilia raisi hadi akazimia huku damu nyingi zikimtoka sehemu ya makalio yake.

“Hongereni sasa, muna weza kuendelea na kuimarisha ulinzi”

Raisi tukamuacha eneo hili huku akiwa amefungwa pingu. Tukaikagua ikulu nzima na kujirdhisha hakuna aliye salia.

“Hichi ni chumba cha siri ehee?”

Obote alizungumza huku tukiwa katika eneo hilo chini ya chumba cha raisi.

“Yaa sijui kuna nini”

Nilizungumza huku nikitazama mlango huu wa chuma.

“Kamlete yule mshenzi aje kututolea namba za siri”

Mlinzi wa Obote akaondoka eneo hili na kupandisha juu. Baada ya dakika mbilia karudi huku akiwa ana mburuta raisi ambaye yupo hio bintaabani.

“Hei hei wewe fala tuambie neno la siri la hili eneo?”

“Sijui”

Obote akampiga risasi ya mguu raisi na kumfanya alie kwa uchungu mwingi sana.

“Sema kabla sijakuua?”

“Mimi ni wakufa tu sikuambii”

Obote akataka kumpiga risasi ya kichwa ila nikamzuia. Nikachuchumaa huku nikimtazama raisi.

“Najua uta kufa, hilo halina kificho. Ila una onaje ukaafanya jambo moja tu la mwisho kwa ajili ya wanachi wanao baki. Ukituambia neno la siri la eneo hilo basi uta kwenda kwa amani huko unapo kwenda?”

“Nenda kamtomb** mama yako”

NIkanyanyuka huku nikiwa nimejawa na hasira kwani katika vitu ninavyo vixhukia ni kutukaniwa mama yangu. Nikamnyanyua raisi kwa nguvu na kuushika mkono wake wa kulia na kuubandika eneo la pembeni ambalo kabla ya kuingiza namba za siri ni lazima ubandike mkono. Alama ya tiki la kijani lika onekana ikiashiria kwmaba mkono huo ni sahihi katika kufungua eneo hilo. Nikatulia kwa sekunde kadhaa huku nikitazama batani hizi za kuingizia neno la siri.

“Una fanyaje Chidi?”

“Huyo kenge hawezi kutuambia neno la siri. Ila main key imesha funguka kilicho baki ni kujua neno la siri Je una tambua tarehe za wanaye kuzaliwa au miaka yao?”

“Ndio”

Obote alijibu na akanitajia namba miaka ya watoto wa raisi kuzaliwa. Nikaziingiza ila zikagoma.

“Mwaka wake wa kuzaliwa?”

Obote akanitaji, nikaingiza nazo zikakataa.

“Fuc**”

“Hii ni ya tatu na ya mwisho nikiingiza ina goma na mlango huu hato funguka”

“Wewe mpuuzi seme neno la siri”

Raisi akamcheka kwa dharau Obote ambaye amemfokea. Nikamtazama raisi machoni mwake na nikagundua jambo, nikakumbuka jinsi alivyo kuwa ana pata tabu alivyo kuwa ana pata tabu jinsi mke wake alivyo kuwa ana bakwa.

“Ana mpenda sana mke wake. Nitajie tarehe mwezi na na mwaka alio zaliwa mke wake”

Obote akanitaijia nilivyo mueleza. Nikamuona raisi ametoa macho hapa nikapata uhakika kwamba hizi ndio namba za siri za kufungulia mlango huu. Nikaanza kuingiza mwenzi wa mke wake, nikaingiza mwaka wa mke wake na nikaingia tarehe aliyo zaliwa mke wake. Lock ya mlango huu ikafunguka na kutufanya tujawe na furaha, Obote akausukuma mlango huu mlubwa na mzito wa chumba. Hatukuamini macho yetu mara baada ya kuona vibunda vya dola za kimarekani vikiwa vimepangwa vizuri kuanzia sakafuni hadi kukaribia eneo la juu ya chumba hichi huku kukiwa na vipande vingi vya dhahabu ambavyo navyo vimepangwa vizuri kuanzia chini hadi juu ya chumba hichi kitu ambacho kikatufanya tujawe na furaha kubwa sana kwani mali hizi zitamsaidia Obote katika kuitengeneza serikali yake mpya.



Obote akaingia ndani ya chumba huku akiwa ameatawaliwa na furaha kubwa sana. Akajirusha juu ya maburungutu haya ya pesa yaliyo pangwa kama kitanda.

“Hahahahahahaaaa”

Obote alicheka huku akiendelea kugara gara juu ya pesa hizo.

“Jaama alikuwa ana kula maisha”

Obote akanyanyuka huku akiwa ameshiak vibunda vya pesa akanirushia mimi na mlinzi wake.

“Za kujipoza machungu ya kazi”

“Asante”

Nilizungumza huku nikiweka vibunda hivi wilivi vya pesa mfukoni mwangu.

“Hii sehemu tuta kuwa tuna ifahamu sisi watatu, sinto hitaji mwanajeshi mwengine tofauti na sisi aifahamu”

“Sawa mkuu”

Tokatoka nja ya chumba hichi. Obote akamtazama raisi huyu ambaye yupo hoi sana kwani kwa vitendo alivyo fanyikwa hana hata nguvu ya kusimama. Obote akachomoa bastola yake kiunoni na kumsogelea raisi, akachuchumaa pembeni yake.

“Una kumbua nilikuambia ita fika siku ya anguko lako una kumbuka?”

Raisi hakumjibu chochote Obote.

“Basi leo ndio ume anguka tena mikononi mwangu. Ngedere wewe”

Obote akampiga risi ya mguuni raisi akalia kwa uchungu na maumivu makali, Obote hakuishia hapo, akachomoa kisu chake katika buti la mguu wa kulia. Akamshika jogoo wa raisi na kumkata taratibu.

“Ulimla demu wangu kutokana ulikuwa na pesa sasa furahia”

Obote akamtenganisha jogoo wa raisi na kiwiliwili chake, kwa jinsi damu zinavyo mtoka raisi na maumivu ya mguu wake, akazimia.

“Nina hitaji ashuhudia jinsi ninavyo jitangaza kwamba mimi ndio raisi mpya wa DRC Congo. Wakiamka asubuhi wata kuta kila kitu kime badilika.”

“Ila mkuu hali yake ni mbaya huyu”

Mlinzi wa Obote alizungumza.

“Kwa hiyo?”

“Ni bora tumpige risasi afe”

“Nahitaji aone nimechukua nchi, mtoeni”

Tukamburura raisi huku tukipandisha ngazi na kukea katika chumba cha raisi cha kulala. Tukamtoa hadi sebleni na kumlaza chini. Tukapokea ripoti kwamba mji mkuu wa Kinsasha tumeutawala sisi na wanajeshi wengiwa serikali wame jisalimisha wao na silaha zao. Maandalizi ya kwenda moja kwa moja kwenye televishion yakaanza kufanyika.

“Kila kitu kipo sawa mkuu”

Mwanajeshi mmoja alimuambia Obote na tukaelekea katika ukumbi wa matangazo ulipo hapa Ikulu. Obote akakaa kwenye moja ya kiti ambacho ndio hukualia raisi pale anapo hutubia taifa. Obote akapewa ishara kwamba aanze kuzungumza kwa maana sasa yupo mubashara kwenye luninga.

“Ndugu zangu wa jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo. Ni matumaini yangu mupo salama na furaha tele. Wana Congo wengi tuliteseka katika kipindi cha uongozi wa raisi aliye pita. Raisi ambaye hakuhitaji kutoka madarakani kwa kipindi cha miaka ishirini sasa. Wana nchi tuliishi kwenye umasikini ulio kithiri na mateso. Leo hii nina watangazia rasmi ya kwamba mimi ndio raisi mpya wa nchi hii ya DR Congo.”

Obote alizungumza na wanajeshi walipo katika chumba hichi wakaanza kushangilia.

“Niwaahidi jambo moja. Nita hakikisha uchumi wa nchi una panda juu zaidi na zaidi na kila mwana nchi ana jivunia kuwa Mcongo. Nita hakikisha nchi ina ongozwa kwa misingi ya haki na demokrasia. Wananchi muta piga kura kila baada ya miaka mitano na niwaahikishie kwamba muda wangu wa kuondoka madarakani nita ondoka kikatiba kama katiba itakavyo ruhusu mimi kuondoka. Nita tengeneza serikaali ya kusikiliza wananchi, nita tengeneza serikali yenye kuwajali wananchi, miundo mbinu nita iboresha, kuanzia hospitali, barabara, maji, umeme naa kadhalika. Nita hakikish DRC itakuwa ni nchi salama, haito kuwa nchi ya vita na mauaji tena. Mungu ibariki DRC asanteni”

Matangazo yakaishiahapa na yakaanza mazoezi ya kuitoa miili ya walinzi wote wa ikulu walio uwawa. Obote akamfwata raisi aliye pita na kumuonyesha matangazo ya yeye kujitanga kuwa raisi.

“Umeona. Mimi ndio raisi mpya wa DRC”

“Una niua ila ipo siku na wewe uta uliwa tena kikatili na kinyama kama hivi”

Maneno ya raisi yakamchukiza sana Obote akachukua kisu chake na kuanza kumkita kita tumboni hadi utumbo uka mtoka. Hakika kuna watu wana ukatili mkubwa sana hapa duniani na sidhani aliyo yazungumza Obote ata weza kutimia hata moja kwa wananchi. Usiku wa siku hii ni sherehe kwa wanajeshi wote. Hadi kuna pambazuka mitaa ya jiji hilo la Kinsasha, lime tawaliwa na wananchi wanao furahi kupinduliwa raisi wao.

“Kweli watu wana kupenda nina ona huko mitaani ni jina lako na picha zako ndio zina tamba”

“Yaa wana nchi walitamabi hata haya mapinduzi yangetokea miaka ya nyuma”

“Ila ndugu yangu nikukumbushe tu. Ina idi ufanye kama vile ulivyo waahidi wananchi usijaribu kuenenda kinyume nao”

“Usijali Rashidi, nime fanya ukatili mkubwa sana kwa watu wapuuzi kama hawa ila ukweli wangu ni kwamba nina uchungu mkubwa sana na hii nchi na nikuahidi kwamba ndani ya miaka mitano ita kuwa mbali sana”

“Mimi nina kutakia kila la heri kwa maana kufanikiwa kwako, kwangu ni furaha ndugu yangu”

“Ila Rashidi nikumbie jambo moja”

“Ndio”

“Mungualikuleta kwa sababu maalumu kwenye haya maisha yangu hususani kwenye nchi hii kwa sababu maalumu. Bila ya mipango yako sidhani kama ninge kuwa hapa kwa maana nilicho kuwa nina fanya mimi ni kutumia nguvu pasipo akili”

“Basi usitumie nguvu kuwaongoza watu.”

“Usijali ndugu yangu”

“Nita kaa hapa wiki moja na nita hitaji kuelekea nchini Tanzania. Nina hitaji kwenda kuikamlisha mission yangu”

“Je utahitaji vijana?”

“Hapana kwa jinsi nilivyo patiwa mafunzo sidhani kama kuna haja ya kuwa na vijana”

“Sawa ndugu yangu ila kukiwa na tatizo lolote nijulishe”

“Usijali ndugu yangu”

Siku zikazidi kusonga mbele huku baadhi ya vyombo vya habari vya kidunia vikilaani juu ya mapinduzi yaliyo fanyika nchini Congo huku vyombo vingine vikifurahishwa kwa mapinduzi hayo. Kelele za vyombo vya habari havikuweza kumuumiza akli Obote zaidi alicho kuwa ana kihakikisha ni kuanza kutaifisha mali zote zinazo milikiwa na viongozi wa serikali iliyo pita ambayo walikuwa wana ishi kama wapo peponi na ufisadi ulitawala kisawa sawa. Jitihada anazo zifanya Obote ndani ya wiki moja kuhakikisha nchi ina rudi kwenye mstari hakika sio mimi peke yangu niliye zipenda hata wananchi wa nchi hii wame zipenda. Obote akaimarisha ulinzi kwenye mipaka yote ya nchi nzima DRC. Akayaomba majeshi ya umoja wa mataifa kuondoka majeshi yao nchini kwa maana sasa wana weza kujitawala wao wenyewe na wakakubali kufanya agizo hilo kuepuka migogoto isiyo ya kilazima.

“Ume bakisha siku mbili za kukaa hapa ndugu yangu nina tamani sana kama unge baki kwa wiki nyingine”

“Hapana nina mambo mengi sana ambayo nina hitaji kuyafanya ndugu yangu. Ila nitakuwa nina kuja kutembea”

“Sawa ina bidi ufungue akaunti nikuingizie japo kiasi cha pesa kitakacho kusaidia katika maisha unayo kwenda kuyaanza”

“Sawa”

Taratibu za kufungua akaunti hazikumaliza hata dakika kumi zikakamilika. Obote akaidhisha na kuagiza niingiziwe dola kaki tano. Nikamshukuru sana kwa maana kwa maisha ya Tanzania ni pesa nyingi sana. Nikafanya maandalizi yote ya kuelekea nchini Tanzania, hapo sinto tumia usafiri wa ndege ila nitatumia usafiri wa boti katika ziwa Tanganyika na kuingilia mkoa wa Kigoma na hapa ndipo nitakapo anzisha safari yangu ya kuelekea jijini Dar es Salaam.

“Ndugu katika watu ambao wata kusaidia katika serikali yako mmoja wako ni Razaro. Mpe nafasi ata kusaidia kukufikisha mbali?”

“Razaro yupo vuzuri ehee?”

“Ndio ana upeo mubw”

“Una jua sijakaa naye ila kwa sababu yako nita mpa hata uwaziri”

“Nashukuru sana ndugu yangu”

Jambo ninalo mshukuru Mungu ni kwamba Obote ana nisikiliza sana kuliko hata wanajehsi wake alio kuwa nao kwa kipindi chote na pia ana niheshimu sana,

Siku ya kuondoka nchini DRC ikawadia. Kila mwanajeshi niliye muaga akasikitika sana na wapo ambao walishindwa kuyazuia machozi yao kwa maana nime ishi nao kama ndugu zangu. Kipindi nime kuwa kiongozi wao niliondoa matabaka katikati yao kwani ukiachilia matakaba ya kivyeo ila kulikuwa na matabaka ya kikabila ambayo nilihakikisha jeshi lina kuwa moja na tuna malengo moja ndio maana ikawa ni rahisi sana kwa sisi kuipindua nchi kwani hapakuwa na wasaliti katikati yetu. Obote akanipatia rubani wa Helcopter na nikasafiri hadi katika mji wa Kahiba. Nikapanda boti iliyo andaliwa maalimu kwa safari ya kunifikisha Ujiji Kigoma. Safari hii ika tugarimu masaa nane kuanzia saa mbili usiku hadi saa kuumi usiku. Nikafika Kigoma saa kumi na moja kasoro asubuhi. Moja kwa moja nika elekea katika Hoteli iitwayo Kigoma Hilltop. Nikapangisha chumba kwa siku tatu, hii yote nina hitaji kufanya upelelezi wa namna nchi ya Tanzania kwa sasa inavyo ongozwa na raisi huyu mpya ambaye hapo awali alikuwa ni makamu wa raisi. Nikalala kwa masaa manne kwa maana nina uchovu mwingi sana na nime pitia matatizo mengi sana.

‘Sasa nipo nyumbani’

Nilizungumza huku nikiwa nime lala chali huku nikitaza paa la juu la chumba hichi nilicho lala. Nikashuka kitandani na kuingia bafuni huku saa ya ukutani ikionyesha sasa hivi ni saa tano asubuhi. Nikatoka chumbani kwangu hapa huku nikwa nime vaa pensi pamoja na tisheti. Chini nina kobazi za kawaida na mkono wangu wa kulia nime shika simu aina ya Samsung S10+. Kwa haraka haraka mtu akinitazama hawezi kuhisi kama mimi ni mwanajeshi niliye fanya kazi kwa jeshi la waasi Congo. Nikatafuta moja ya eneo lililo tulia na kujitenga huku likiwa limeelekea katika ziwa hili Tanganyika.

“Karibu”

Muhudumu mmoja wa kike alizungumza huku akiwa amesimama pembeni yangu.

“Nashukuru, brake fast yenu ipo vipi?”

“Ahaa huwa tuna penda kumsikiliza mtena kwani brake fast yetu ni bure”

“Ohoo sawa. Muna chapati, maharege na mhogo ya kukaanga?”

“Yes ipo”

“Basi ningependa kuletewa na kahawa”

“Sawa karibu sana”

“Asante”

Nikakunja nne huku nikisikilizia hali nzuri ya hewa ninayo ipata katika eneo hili. Nikaanza kuperuzi kwenye mitandao ya kijamii huku nikitumia akaunti feki ninayo jiita Hadija Sadick. Nime fungua kwa majiya ya kike kwa maana sihitaji kujulikana kama uwepo wangu upo, kwani kwa mara kadha nime kuwa nikiitembelea page ya Jackline na kuangalia anacho kipost. Nikaingia katika ukurasa wa instergram wa Jackline na kukuta akiwa amepost picha za watoto wangu wawili ambao ni mapacha huku pembeni yake akiwepo mwanangu Shamsa ambaye kwa sasa amekuwa mrembo kweli kweli.

‘Zawadi ya pekee ambayo umenipatia Rashidi mume wangu ni hawa watoto. Nina imani kwamba bado upo hadi japo vyombo ya usalama vya nchi yangu vina dai kwamba uta kuwa umekufa. Ila nikuahidi nita hakikisha nina fanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba una patikana. Nina kupenda wanao wote watatu wana kupenda mume wangu’

Maneno haya ya Jackline aliyo yaandika kwa lugha ya Kifaransa ambayo kwa kukaa kwangu DRC nilijifunza na nina izungumza kiufasaha, yakanifanya machozi yanilenge lenge. Nikatamani kumpigia video call ila nikashindwa kwani hatari ya mimi kujalikana nipo hai basi ina weza kuwasumbua wao hususani wanangu ambao bado ni wadogo na wana hitaji kulelewa katika mazingira mazuri na salama. Nikaiperuzi page hii ya Jackline na kukuta picha nyingi sana akiwa na familia nzima.

‘Nita rudi kwenye familia nisubirini’

Nilizungumza kimoyo moyo. Muhudumu akaniwekea nilivyo muagiza pembeni yangu.

“Karibu sana”

“Nina shukuru”

“Je ungependa nikueletee na nini zaidi?”

“Hivi hivi vina tosha”

Muhudumu akaninawisha mkono na nikaanza kula taratibu. Nikaingia mtandao wa YouTube na kuanza kufwatilia kampenzi za makamu wa raisi huku kila mkoa anao kwenda ana mtambulisha mke wangu kama ndio mke wake halali. Nikamaliza kupata kifungua kinywa na kurudi chumbani kwangu, nikachukua kofia na kuondoka hotelini hapa kwa usafiri wa Taksi.

“Leo nahitaji uzinizungushe karibia mji huu mzima”

“Usijali kaka ni wewe tu”

“Ehee raisi mpya munauonaje uongozi wake?”

“Daa jamaa ana piga kazi aisee, yaani kwa hii miezi kadhaa aliyo ingia madarakani amepiga kazi kisawa sawa”

“Eti ehe?”

“Ndio kaka. Ila huyu mzee amenichosha kwenye jambo moja tu”

“Jambo gani?”

“Ameoa binti mdogo sana yaani eti yeye ndio first lady. Yani nina shindwa kuelewa sijui kwa nini hawa dada zetu wana kuwa wana wapenda vizee kama wale”

“Ndugu yangu ni pesa ndio ina wapagawisha mademu kwa kiasi hicho”

“Aisee ni kweli ndugu kwa maana yule demu kwa mahesabu ya haraka haraka sidhani kama ana fika miaka ishirini na saba au nane”

“Ukisikia ng’ombe hazeeki maini ndio huyo kauli ndugu yangu”

“Kweli aishee, mzee ana kula bata”

Dereva taksi alizungumza na kunifanya moyo wangu uzidi kujawa na hasira na maumivu makali juu ya mama Shamsa na raisi.

“Ehee kaka nikupeleke wapi na wapi?”

“Wewe nitembeze mji mzima, sehemu zenye maeneo mazuri wewe nitembeze kwa maana ninacho kihitaji mimi ni kupumzisha akili yangu”

“Wewe ni mgeni hapa Kigoma ehee?”

“Yaa”

“Ume tokea wapi?”

“Dar es Salaam”

“Aisee Dar nina tamani siku moja niweze kufika”

“Kwani huja wahi kufika jijini Dar es Salaam?”

“Toka nizaliwe mwanangu”

“Kwa nini sasa ikiwa ni nchi moja ya Tanzania?”

“Kule sina ndugu, so nitafikia wapi?”

“Sio kila mtu anaye fika jijini Dar es Salaama ni lazima awe na ndugu wengine hawana ndugu na wana piga maisha na wana tusua”

“So una nishauri niende Dar es Salaam kwa maana nina sikia wanao kwenda kule lazima watusue kimaisha?”

“Dar ndio mpango mzima. Ila angalizo, Dar es Salaam ni jiji la watu wasio na huruma, mwenye pesa ana zidi kupata zaidi na asiye kuwa na kitu ana zidi kukosa zaidi hivyo kuwa makini sana ndugu yangu.”

“Usijali kaka wewe Dar una piga ishu gani?”

“Nina biashara zangu za hapa na pale”

“Ahaa ila zina kuingizia pesa?”

“Yaa ndio maana tuna maisha mazuri kama hivi, tuna kuja mikoani kama hivi kupumzisha akili.”

“Aisee ni kweli, ahaa kuna nini leo?”

Dereva alizungumza mara baada ya kufika kwenye moja ya barabara na kukuta foleni kubwa.

“Au ajali?”

“Hapana kungekuwa na ajali watu wote wangekuwa wamekimbilia huko, si una jua Tanzania yetu”

“Yaa naijua”

“Ngoja nikaulize”

“Sawa”

Dereva akashuka ndani ya gari na kuelekea mbele kwa ajili ya kuuliza. Baada ya dakika kama tano hivi akarudi na kuingia ndani ya gari.

“Kuna nini?”

“Daa nasikia raisi yupo hapa Kigoma. Hivyo barabara zime fungwa ili kusubiria msafara uweze kupita”

Taratibu nikajikuta nikijawa na tabasamu kwani nime kuja katika muda muafaka wa kumpata adui yangu kama nikimaliza leo, sinto kuwa na hata ya kukaa hapa Tanzania, nita rudi zangu DRC na huko ndipo nitakapo ondokea kuelekea nchini Ufarans ilipo familia yangu.



“Daa viongozi wetu bwana jau sana”

Dereva alizungumza na kunifanya nitoke kwenye dimbwi la mawazo kwa maana kichwa changu kwa sasa kina panga mipango ya jinsi gani ya kumkabili adui yangu.

“Ume sema?”

“Nimesema viongozi wetu jau kweli”

“Kwa nini?”

“Ona raia tulivyo simamishwa barabarani. Hapa kama una mgonjwa kwenye gari si ana kufika isitoshe una ambiwa wamesimamishwa sasa ni lisaa lime, ila bado hajapita.”

Dereva taksi alilalama huku akionekana kukerwa na foleni hii.

“Raisi ana ziara hapa Kigoma?”

“Sijajua kwa kweli mara nyingi mimi huwa sio mfwatiliaji sana wa mambo ya viongozi”

“Ngoja nikaangalie na mimi”

“Poa kaka uta nikuta hapa”

Nikavaa kofia yangu vizuri na kuishusha nusu uso na taratibu nikashuka ndani ya gari. Nikasimama pembeni ya barabara huku nami nikisubiria gari hizo za msafara kupita. Askari wa usalama barabarani, wamesambaa kila sehemu kuhakikisha kwamba hakuna chombo chochote cha usafiri kinakatiza barabarani. Nikatoa simu yangu mfukoni na kujifanya nina rekodi rekodi. Hazikupita dakika kuni na tano gari za msafara zikiongozwa na gari ya polisi yenye king’ora zikaanza kupita eneo hili kwa mwendo wa kasi sana. Nikarekodi kuanzia gari ya kwanza hadi gari ya mwisho na kuna gari kama nne hivi ambazo zina fanana na moja ya gari hizo ni ya raisi. Wananchi wakaanza kutawanyika huku magari yakiruhusiwa kuiendelea na safari zao, nikarudi kwenye taksi.

“Hapa kuna maduka yanayo uza laptop?”

“Ndio lipo duka la muhindhi mmoja ana computer na laptop za kila aina”

“Nipeleke”

Foleni ikapungua na sisi tukaaza kuondoka eneo hilo. Kwa mwendo wa dakika ishirini tukafika kafika gorofa moja refu ambapo chin kuna maduka mengi. Dereva akanionyesha dula la muhindi huyo na nikaingia ndani ya duka. Nikatazama laptop zilizo wekwa katika makabati ya vioo.

“Boss hii Mackbook Air bei ngapi?”

“Ni dola elfu moja mia nne mkuu”

Muhindi huyu alinijibu huku akinitazama usoni mwangu. Sikutaka kujibizana naye, nikatoa kibunda che dola mia mia nilicho kifunga vizuri. Nikahesabu kiwango cha pesa anacho kihitaji muhindi huyu na kumpatia. Nikapewa laptop niliyo ihitaji ikawekwa ndani ya boksi, nikakabidhiwa risiti na kurudi kwenye gari.

“Ahaa sasa hivi ninahitaji unipitishe dula la nguo”

Nilimuambia dereva na tukaondoka eneo hilo. Tukafika katika moja ya duka, nikashuka na kuingia dukani, nikanunua suruali nyeusi ambayo ni ina futika vizuri tofauti na jinzi. Nikanunua tisheti jeusi pamoja na swete lenye kofia ambalo nalo lina rangi nyeusi. Nikamlipa muuzaji huyu na kuingia katika dula la viatu, nikanunua raba nyeusi. Nina nunua viti vyenye rangi hii kwa ajili ya kazi ambayo nina imani nikiifanya usiku nikiwa na mavazi hata ni ngumu sana kwa mtu kuweza kuniona gizani. Nikaingia duka la jirani ambalo lina uza nguo za kike. Nikaulizia baibui na kwa bahati nzuri nikapata.

“Mke wangu ana mwili kama huu wangu je hili lita nitosha?”

Nilimuuliza mwana dada huyu.

“Yaa ni saize sawa”

Nikamlipa kiasi alicho hitaji kisha nikarudi ndani ya taksi nikiwa na mifuko yangu.

“Turudi hotelini”

“Sawa kaka”

Tukafika hotelini.

“Kiasi gani kwa mizunguko yote?”

“Bosi ni wewe tu”

“No taja ni bei ngapi kwa maan anime chukua muda wako wa kutosha”

“Ukinipatia elfu sabini ita pendaza mkuu”

“Una uhakika kwa maana naona tumetembea umbali mrefu. Sasa wewe chukua hii”

Nikampa dereva laki moja na kumfanya atbasamu hadi nikamuona pengo la upande wa kulia ambalo kwa muda wote sikuweza kuliona.

“Asante sana kaka”

“Sasa nina hitaji namba yako ya simu”

Dereva akanitajia namba yake na nikainakili kwenye simu yangu.

“Nitakupigia nikikuhitaji. Una funga saa ngapi?”

“Ahaa kaka mimi kazi masaa yote nipo kazini, wewe nipigie muda wowote”

“Poa”

Nikaachana na dereva na moja kwa moja nikaelekea chumbani kwangu. Nikajaribisha nguo zote nilizo zivaa kisha nikafungua laptop niliyo inunua na nikaanza kuteingiza programs ninazo zifahamu ambazo kijana wa I.T katika jeshi la Obote alikuwa akinielekeza jinsi ya kuzitumia. Kwa kipindi cha miezi sita aliweza kunifundisha mambo mengi sana. Nikamaliza kazi yangu ya kungiza program ninazo zihitaji. Nikaiingiza video niliyo irekodi kwa simu katika laptop hii. Nikaipeleka mbele hadi ikafik katika gari nne zinazo fanana ina ya Range Rover Vorge. Nikaanza kuzi scan katika moja ya program niliyo iingiza na nikagundua gari ya nne kutoka nyuma ndipo alipo raisi, mke wake pamoja walinzi wake wawili huku mmoja akiwa ni dereva ambao wao wamekaa siti ya mbele.

“Zimeelekea wapi?”

Nilizungumza huku nikizi track gari hizo kwa masaa manne yaliyo pita zilikwenda wapi na wapi. Kutokana teknolojia ime kua haikuwa kazi ngumu kwa mimi kujua gari hizo zilienda wapi na wapi.

“Shit”

Nilijikuta nikijilaumu kwa maana baada ya mizunguko ya raisi, hatua ya mwisho gari hizo zime elekea uwanja wa ndege na hadi ninavyo zungumza hivi sasa raisi hayupo tena mkoa wa Kigoma.

“Ina bidi nielekee Dar”

Nilizungumza huku nikiingia katika shirika la leri Tanzania, nikatazama ratiba ya treni za umeme ambazo zinaanzia safari yake hapa Kigoma kuelekea Dar es Salaam.

“Duu hadi kesho saa mbili asubuhi. Poa nita ondoka kesho”

Nilizungumza mwenyewe huku nikiifunga laptop hii. Roho ya kisasi ikaendelea kunishawishi nijiulize namna gani nina weza kupanga karata zangu vizuri ili kama ni adui basi niweze niweze kupambana naye kwa maneshabu ya hali ya juu. Nikatoka nje ya chumba changu na kuelekea eneo la swimming pool, nikatafuta moja ya kiti nikakaa huku nikiendelea kuperuzi peruzi mitandaoni huku nikifwatilia kazi za raisi huyu.

“Aha habari yako”

Muhudumu mwengine wa kike alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Nikavua earphone niliyo iweka sikioni mwangu.

“Ohoo salama niambie”

“Safi, nikuhudumie nini?”

“Ahaa….una juisi ya pera?”

“Ndio”

“Naomba unipatie”

“Sawa”

Muhudumu akaondoka na nikaendelea kuperuzi. Baada ya dakika tano muhudumu akarudi na glasi ya juisi, akaniweka pembeni yangu, nikamshukuru kisha akaondoka zake.

“Huyu ni nani?”

Sauti ya ukali ya mwanamke ikanifnaya nitazame upande wangu wa kushoto na kumuona mwana dada mmoja mrembo akiwa na mpenzi wake.

“Nakuuliza huyu ni nani ambaye ume piga naye picha hizi. Kwa hiyo siku zote ninavyo toa pesa zangu na kukugaramia una kwenda kuwahonga malaya zako si ndio?”

Mwanamke huyo alifoka na kumfanya mwanaume huyo kukaa kimya.

‘Duu jamaa marioo’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiufwatilia ugomvi huu kwa ukaribu sana kwani wapo karibu na mim.

“Sasa kuanzia hivi sasa mimi na wewe basi. Ondoka sihitaji kukuona Juma. Yaani nina funga safari kutoka huko ninapo toka, nina kuja hapa kwa ajili yako alafu una wasichana wabaya wabaya ambao ukiwasimamisha na mimi ni sawa na mbingu na ardhi?”

Dada huyu akazidi kufoka.

“Baby”

“Koma usiniite Baby. Kwanza toa chip yako kwenye hii simu na nirudishie simu yangu. Mpuuzi wewe, nina kuhudumia kuanzia kula yako, kuvaa, huna mbele wala nyuma alafu unaniletea using** kum** mak*** wewee”

Dada akaizidi kumporomoshea matusi jamaa wa watu ambaye umasikini ndio una mfanya awe mnyonge.

“Ongea taratibu basi”

“Nini kum** wewe niongee taratibu. Okay ondoka kabla sijakuzalilisha na usidhubutu kunipigia simu wala kunitafuta. Mbwa wewe”

Dada huyu alizungumza huku akitoa line ya mwanaume huyo kwenye simu na kumrushia usoni. Taratibu jamaa akanyanyuka huku akiwa mnyonge mithili ya mwanaume aliye fumaniwa na mama mkwe wake. Akapita mbele ya kiti nilicho kaa na akapotelea kwenye mlango wa kutokea eneo hili. Dada huyu akainama chini na kuanza kulia hadi nikamuonea huruma kwa kweli mapenzi yana umiza. Akasimama, hapa ndipo nikapata nafasi ya kuiona shepu yake ya namba nane. Kiuno chake chembamba kiasi kimebeba makalio na hispi zilizo shoneana. Kifuani ana chuchu kubwa kiasi, kiufupi huyu mwanamke ni mzuri. Akatembea taratibu hadi ukingoni mwa swimming pool hili. Akajirikiria kwa sekunde kadhaa kisha akajidumbukiza na kuzama chini.

‘Asije akataka kujiua huyu?”

Nilizungumza huku nikiiweka simu yangu mezani. Nikavua tisheti yangu na kubaki na pensi, nikavua koboza na kusogea karibu ya swimming pool hii. Nikachungulia chini na kweli nika muona dada huyu akifurukuta. Nikajitosha kwenye maji na kuzama chini, nikaogelea hadi eneo alipo kwa maana swimming pool hii ni refu kwenda chini na ni kubwa. Nikamshika kiunoni na kuanza kupanda naye juu.

“Niache, niache bwana nife”

Dada huyu alizungumza huku akijitahdii kujitoa mikonini mwangu. Kwa jinsi nilivyo mkaba hakuweza kurufukuta kabisa.

“Acha upuuzi wewe. Una taka kufa kijinga namna hii?”

Nilizungumza kwa kufoka huku nikimkumbatia kwa nguvu mwana dada huyu. Akanitazama kwa sekunde kadhaa machoni mwangu.

“Sikujui hunijui, hata nikifa maisha yangu yana kuhusu nini wewe?”

Sikutaka kumsikiliza zaidi ya kufanya jitihada za kumtoa kwenye swimming pool hii na kwa bahati mbaya eneo hili tulikuwa watatu, mimi na wao tu. Nikamkalisha juu ya kingo za swimming pool hii.

“Una taka kufa si ndio?”

Nilimuuliza kwa ukali huku nikimkazia macho.

“Ndio”

Nikatoka katika swimming pool hii na kumnyanyua juu.

“Twende”

Nilizungumza huku nikimshika mkono mwana dada huyu na kumnyanyua juu. Nikaanza kumvuta na yeye akaanza kunifwata. Tukafika eneo ambalo kwa chini kuna maji ya ziwa Tanganyika kwa maana hoteli hii ime jengwa pembezoni kabisa mwa ziwa hili na ipo juu ya kilima kirefu kidogo.

“Ruka kule kwenye yale majabali ili ufe vizuri usitake kuwapa kesi za kipuuzi. Wewe una kuwa na mwanaume ambaye una mlisha una mvisha una mnywesha alafu unaitwa ni mwanaume. Hivi nyinyi wanawake wa Kitanzani nani kawaroga. Una muonga mwanaume na una tarajia muda wake na nguvu zake azipeleke wapi kama sio kuwa na mwanamke anaye muona ana mfaha na wewe ukaw akitega uchumi tumia akili wewe. Kama huna wazazi, huna majukumu wala watu wanao kutegemea ruka ufe.”

Nilizungumza kwa kufoka hadi mwana dada huyu akaanza kutetemeka.

“Rukaaa ufee, nitatoa maelezo polisi kwamba umemfumania mpenzi wako na ukaruka kwenye korongo huko ukafa”

Nikazidi kumfokea mwana dada huyu kwa maana katika kipindi hichi ambacho nime kaa na wanajeshi waasi swala la kufa ni la kawaida sana kwangu kwani kwa mara kadhaa tuliingia katika mapambano ya majeshi ya serikali na vikosi vya majeshi ya umoja wa mataifa na nilishuhudia watu wakifa huku na mimi nikiua ili nibaki kuwa hai.

“Wanawake wapumbavu wenye akili ndogo kama nyinyi ndio munatanguliza uzuri wa sura na maumbo yenu pasipo kujua thamani ya maisha yenu. Tumia akili acha kutumia sifa ya matako yako makubwa hayo. Ruka nakusubiria nikushuhudie una kufa”

Taratibu mwana dada huyu akaka chini na kuangua kilio, nikatambua dhahiri kwamba maneno yangu yamemchoma na kumuumiza. Nikamtazama kwa sekunde kadhaa kisha nikaanza kuondoka eneo hili na kumuacha akiwa an alia. Nikakaa kwenye kiti changu huku pensi yangu ikiwa imelowana maji. Hazikupita hata dakika tano mwana dada huyu akarudi kwenye meza yake huku akinitazama kwa macho makali. Akakusanya vitu vyake na akanza kupita mbele yangu. Akapiga hatua tano kisha akarudi na kusimama mbele ya kiti changu.

“Sijawahi kuona mwanaume katili kama wewe kwenye maisha yangu”

Mwanadada huyu alizungumz akwa hasira kisha akatema mate pembeni na kuondoka eneo hili. Nikabaki nikitabasamu tu kwa maana mawazo yake ya mapenzi yanamchanganya. Nikanywa kinywaji changu hichi kisha nikamuita muhudumu na kumlipa pesa yake na nikarudi chumbani kwagu. Nikatazama filamu kadhaa kwenye mitandao hadi ikafika saa mbili usiku, nikatoka chumbani na kueleka katika mgahawa. Nikaagiza nyama choma na ndizi za kuchoma na muhudumu akaniletea chakula kama nilivyo muagiza. Kitu ninacho kipenda kwenye hoteli hii huduma zao zipo haraka sana na wana jali wateja kwa ubora wa hali ya juu. Nikamaliza kula, nikalipia chakula hichi, nikanunua maji ya chupa kubwa na kurudi chumbani kwangu. Kutokana asubuhi nina hitaji kuwahi kituo cha treni, nikalala mapema.

Saa kumi na mbili asubu nikamka, nikaoga na kujiandaa haraka haraka. Nikampigia simu dereva taksi na sa moja kamili akafika hotelini hapa. Nikabeba mizigo yangu na kutoka chumbani kwangu, nikakabidhi funguo huku nikimuambia muhudumu nina ondoka na chumba changu wana weza kukikodisha kwani nime ondoka kabla ya siku zangu kuisha. Nikaingia ndani ya taksi na moja kwa moja tukaeleka hadi katika stesheni ya treni. Nikakata tiketi na nikaingia ndani ya treni. Nikaitafuta siti yangu, nikaweka begi langu lenye nguo chache katika eneo maalumu la mizigo kisha nikaa katika siti yangua mbayo ni ya dirishani. Nikaifungua laptop yangu na kuendelea kutazama filamu ya Mission Impossible Rogue Nation ambayo usiku niliishia robo.

“Wewe”

Nikanyanyua uso wangu na kumtazama dada ambaye jana nilimuokoa kutoka kwenye swimming pool. Mkononi mwake ameshika tiketi huku akitazama namba ya siti ambayo anapaswa kukaa.

“Karibu”

“Yaani siku yangu leo pia ina vurugika”

Alizungumza huku akiingiza begi lake sehemu ya mizigo kisha akaka siti ya pembeni yangu.

“Pole”

“Hivi kwa nini wewe kaka una roho mbaya?”

“Hiyo ndio salamu?”

Nilizungumza kwa ubabe kidogo.

“Mmmm….Okay habari yako kaka mwenye roho mbaya?”

“Salama dada usiye jielewa”

“Ehhh Mungu ndio maana nilisema siku yangu imekuwa mbaya”

“Itaachaje kuwa mbaya ikiwa hujui thamani ya mtu unaye zungumza naye. Hivi una hisi jana ungekufa leo hii ungekuwa umepanda hii treni wewe?”

“Kwani mimi ni wa kwanza kufa?”

“Sio wa kwanza kufa ila ukifa umekufa no kurudi. Mshepu wako huo una kwenda kuwa chakula cha funza. Tena funza wata kufaidi kishenzi kwa maana watakavyo kula mtako huo”

Nilizungumza huku nikitabasamu.

“Hivi weee kaka una mke kweli?”

“Sina na sitaki kwa maana kwua na mke asiye na akili kama wewe ni balaa tupu. Yaani akili zako zote zipo matakoni una hisi kwamba tako ndio kila kitu.”

Nilizidi kuzungumza kwa utani hadi mwana dada huyu uso wake ukajawa na hasira ya waziwazi.

“Okay nina itwa Chidi”

“Sijakuuliza jina lako na sihitaji kulijua”

“Haya”

Nikavaa earphone zangu nilizo zichomeka katika laptop na kuendelea kutazama filamu hii. Safari ikaanza taratibu huku kila mtu akiwa binze na mambo yake. Baada ya dakika ishirini za safari dada huyu akanichomoa earphone ya sikio langu la kushoto na kunifanya nimtazame.

“Nina itwa Irene”

“Kwani nime kuuliza”

“Hee weee kaka mbona mswahili hivyo. Nime tulia na hasira zangu zime isha, naongea kwa wema alafu una nishushua jamania. Kaka wengine sio wapaoje?”

“Tupo hivi hivi, dawa ya jeuri jeuri. Poa kama hasira yako ime kwisha nami yangu imesha kwisha. Nashukuru kukufahamu Irene”

Tukapeana mikono huku sote tukitabasamu.

“Pole kwa mambo ya jana”

“Ahaa…sitaki hata kuyakumbuka kwa kweli, jana ingekuwa sio wewe sasa hivi ningekuwa nimesha fanya maamuzi ya kipuuzi”

“Kwa nini una maamuzi ya haraka?”

“Ndio nilivyo umbwa aisee. Yaani hadi ofisini kwangu wafanyakazi huwa wana niogopa”

“Kwani una fanya kazi gani?”

“Nipo serikalini kitengo nyeti”

“Kitengo gani hicho nyeti kuliko nyeti zetu tulizo nazo”

“Hahaaa yaani wewe. Mimi nipo kitengo cha siri cha kumlinda raisi. Kiufupi mimi ni usalama wa Taifa katika kitengo cha kumlinda raisi kwa siri sana. Wewe je una fanya kazi gani?”

Nikatabasamu huku nikimtazama Irene usoni mwake kwani nilikuwa nina jiuliza ninapo fika Dar es Salaama nita weza vipi kukabili raisi, sasa nime ipata karata ya siri ambayo kwa kweli nikiicheza vizuri basi raisi hana chake.



“Ahaa mimi ni mfanya biashara tu wa kawaida. Ila mara nyingi sana watu ambao ni usalama wa taifa huwa hawajisemi hadharani, hiyo ni kutokana na usiri wa kazi yao?”

Nilimuuliza Caro huku nikimtazama usoni mwake.

“Hayo mambo ni ya kizamani.”

Caro alizungumza huku akitoa kitambulisho chake na kunipatia. Macho yakanitoka kwa maana Caro ametoke kuniamini na kuzoea kwa uharaka sana.

“Hongera sana”

Nilizungumza huku nikimrudishia Caro kitambulisho chake.

“Nashukuru kwa kukufahamu”

“Usijali, una jua sijawahi kukutana na mwanaume jasiri na mbabae kama wewe. Wanaume karibia wote ambao ninaandamana nao kazini na ninao kuwa nao kwenye mahusianoa wengi wao wana kuwa ni waoga. Wana niogopa, ila wewe jana uliniburuta kama mtoto aisee una jua nilijishangaa sana”

“Haahhaa kwa hiyo una taka kuniambia wanaume wana kuogopa”

“Weee sana, na ukitegemea na cheo changu basi ndio usiseme”

“Hahaaa sawa sawa. So una ishi Dar au?”

“Yaa naishi Mokocheni”

“Sawa”

“Wewe je?”

“Kimara”

“Sawa sawa”

Safari ikazidi kusonga mbele huku kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi mimi na Caro tuna zidi kuzoeana kiasi cha kwamba tukapanga tukifika Dar es Saalam nikapajue kwake kwanza kisha ndio twende kwangu. Katika mazungumzo yetu sikutaka kumgusia kabisa kuhusiana na maswala ya usalama wa nchi hii au raisi. Nikajitahidi sana kumpigisha stori za kawaida ambazo zina mfurahisha na kumchekesha. Uzuri ni kwamba jiji zima la Dar es Salama nina lifahamu hivyo kupata nyumba ya fasta fast ya kupangisha kwangu haito kuwa shida kubwa. Tukafika jijini Dar es Salaam. Tukatoka kituoni na kumkuta dereva wa Caro akimsubiria. Tukapokewa mizigo yetu na dereva akaiingiza ndani ya gari.

“Juma”

“Ndio mkuu”

“Huyu ni rafiki yangu ana itwa Chidi au Rashidi. Rashidi huyu ni dereva wangu ni mwak wa pili sasa ana niendesha”

Caro alitutambulisha mara baada ya kuingia ndani ya gari.

“Nashukuru kukufahamu kaka”

Nilizungumza kwa uchangamfu mkubwa sana.

“Hata mimi nina shukuru”

Tukafika nyumbani kwa Caro. Nikaguna kimoyo moyo kwa maana ni jumba moja kubwa la kifahari huku nje kukiwa na gari za kifahari nne, Range Rover Sport, Toyota VX V8, Ferrari na Astorn Martin.

“Waooo ni nyumba nzuri sana Caro. Hii ni yako?”

“Ndio ni yangu, karibu ndani”

Tukaingia ndani huku dereva akiingiza mizigo yetu ndani.

“Nina ishi peke yangu. Ila nina wadada wa kazi wawili huwa wana fika asubuhi kufanya usafi na kuondoka, getinin ina walinzi wanne. Wawili wana ingia asubuhi na wawili wana ingia usiku”

“Sawa sawa”

“Juma una weza kuelekea ile sehemu niliyo kupa maelekezo kwenye simu”

“Sawa bosi”

Juma akaondoka na kuniacha na Caro. Akaandaa chakula cha mchana kisha akanialika mezani kwa ajili ya kula. Tukaanza kula taratibu huku ukimya ukitawala kati yetu.

“Kama unge kufa ndizi nyama hizi tamu ningezilia wapi mimi”

“Hahahaa Chidi una vituko kweli?”

“Haki ya Mungu vile”

“Ila una jua mimi nina hasira Chidi kwa maana Daa sipendi mwanaume kucheza na hisia zangu na huwa nikipenda nina penda kweli”

“Ngoja kwanza wewe kabila gani?”

“Mkurya”

“Ndio maana”

“Ndio maana nini?”

“Haaa hamjijui. Muna hassia sana”

“Ni kweli. Yule kijana ni Mungu tu ndio alinizuia kumfanya kitu kibaya ila nilipanga nimpige kisawa sawa ila nika muheshimu”

“Anapajua hapa kwako?”

“Hapana kijana mwenyewe nime muona Facebook, huwa nina funga safari kwenda Kigoma, nina tuliza mizuka yangu kisha nina rudi Dar”

“Dar na cheo chako hicho kweli una tongozwa na wanaume wa Facebook?”

“Hakunitongoza ila mimi ndio nilimtongoza. Ngoja nikuambie kitu kimoja Rashidi. Mimi wanaume wana niogopa kwa sababu moja, mimi ni mtu ambaye nina enda direct kwenye point. Mwanaume akisema ohoo mimi nakupenda akajifanya kunihonga basi nina mleta hapa kwangu, uta kuta badala ya kunitongoza ana ywea kwa maana nipo vizuri nina kila kitu ambacho mwanaume ana paswa kuwa nacho. Mbili mimi ndio nikimpenda mtu basi sijivungi nina mueleza ukweli, akikataa basi ila sijawahi kumueleza mwanaume kama nina mpenda akanikatalia”

“Hahaa hadi sasa hivi umesha kuwa na wanaume wangapi?”

“Wengi sana Chidi kwa maana hii kazi yangu kama nina hitaji kupata labda details kwa mtu anaye hiajika na serikali ambaye ni mwanaume basi lazima nitumwe mimi. Mtu akiangalia hii shepu na huu msambwanda lazima adate mamaye”

“Hahahahaaa”

“Yaa una mpa mtu show moja ya kibabe yeye mwenyewe ana mbela na kuanza kuropoka ropoka”

“Hahaaa sasa kwa nini yule kijana alikuzuzua?”

“Yule fala nilimpenda, hilo ndio tatizo. Ila hawa wengine nina pita tu kama upepo, yaani hata siwaweki moyoni”

Tukamaliza kula na kurudi sebleni huku akilini mwangu nikiwa makini sana nisijichanganye uhalisia wangu alafu mambo yanitokee puani.

“Ehee biashara yako wewe ina dili na nini?”

“Mara nyingi huwa nina nunua vitenge Uganda nina leta Dar es Salaam nina sambaza kwenye maduka ya jumla”

Nilitandanga kwa maana kazi hiyo haija haja ya kuonyesha duka.

“Ohoo ni biashara nzuri sana. Vipi ina lipa?”

“Kiasi chake tuna pambana hivyo hivyo”

“Ni kweli Chidi kwenye maisha hakuna kitu kizuri kama kutafuta pesa yako hususani ukiwa ni mwanaume. Ila ukisubiria uwe marioo kama yule mseng** ndio yale mambo kanunua simu kampa mume walivyo achana kampokonya”

“Hahaa ila chizi kweli wewe. Si ungemuacha akajipige picha na demu wake”

“Nyoo simu ya milioni mbili, kweli nimuachie akapige na kademu kabaya tena wapo kitandani.”

“Hahaa”

Simu ya Caro ikaanz akuita akaichukua mezani alipo kuwa ameiweka na kuipokea.

“Mkuu heshima yako”

“Ndio nimesha rudi Dar es Salaam”

“Nije sasa hivi ehee?”

“Sawa nina kuja”

Caro akakata simu.

“Sasa Rashid, raisi ameniita ikulu, ngoja nikajimwagie fasta niende. Uta baki hapa hadi nirudi tafadhali usiondoke”

“Yaani nibaki jumba zima peke yangu?”

“Kwani kuna ubaya gani. Nina kwenda kuongea tu na mkuu kisha nina rudi.”

“Poa ita kuwa ni vyema ukanipatia namba yako ya simu”

“Hivi sikukupa ehee?”

“Hukunipatua”

“Basi nina kupa, njoo nikuonyeshe chumba ama uta kuwa ume choka una weza kulala.”

Tukaelekea kwa pamoja hadi goforani, akanionyesha chumba kilicho andaliwa vizuri na ndipo yalipo wekwa mabegi yangu.

“Poa mimi nita pumzika kidogo”

“Hakuna shaka, ngoja nikajiandae”

Cauther akatoka ndani hapa. Nikakichunguza chumba hichi kwa umakini sana kama kina kamera au laa, kwani kwa mtu ambaye ni mpelelezi ni ajambo la kawaida sana kufunga kamera za siri katika vyumba vya nyumba zao hususani vyumba vya wageni. Nilpo hakikisha kwamba chumba kipo salama, nikavua nguo zangu zote kisha nikaingai bafuni, nikaoga kisha nikajifunga taulo na kutoka chumbani hapa. Kabla hata sijapanda kitandani, mlango ukagongwa.

“Chidi”

Nikafungua mlango na kutazamana na Caro. Akapigwa na bumbuwazi la sekunde kadhaa huku akiniazama vizuri kuanzia usoni hadi kifuani .

“Hei”

“Ahhaa hizi ndio namba zangu”

Caro akanipatia kikadi chenye namba za simu, nikaagana naye na akaondoka. Nikajilaza kitandani huku nikitafakari mambo mengi sana kuhusiana na namna gani ninavyo weza kuhakikisha kwamba nina muingia adui yangu pasipo yeye kushtuka. Kitu ambacho nita nigarimu ni sura yangu.

‘Nitawezaje kubadilisha sura yangu ikiwa karata yangu muhimu imesha nitambu?’

Niliendelea kuwaza akilini mwangu hadi usingizi ukanipita. Sauti ya mlango unao gongwa ikanifanya nifumbua macho yangu, giza totoro lime tawala ndani ya chumba hichi, nikashuka kitandani na moja kwa moja nikatembea hadi ilipo swichi na kuiwasha. Nikafungua mlango wa chumba hichi na kumkuta Caro akiwa amejifunga tenge moja mwilini mwake.

“Mambo Chidi”

“Safi, aisee kumbe nime lala sana ehee?”

“Yaa nilirudi nikakugongea ila nikaona ume lala nikaamua nikuache hadi nitakapo maliza kuandaa chakula cha usiku”

“Ohoo saa ngapi sasa hivi?”

“Ni saa tatu usiku”

“Daa”

“lla ume lala salama?”

“Yeah”

Tukatazamana na Caro kwa sekunde kadhaa. Macho yake tu yana onyesha kwamba ana uhitaji wa jambo fulani kutoka kwangu. Nikamtazama taratibu jinsi tenge hilo alivyo lifunga kimitego kwani nusu ya mapaja yake yote ipo wazi.

‘Mimi mwanaume’

Nilizungumza huku nikimshika Caro mkono wake wa kushoto na kumsogeza karibu yangu. Chuchu zake zikakita kifuani mwangu uzuri ni kwamba nime mpita urefu kidogo. Nikausogeza mdomo wangu taratibu na nikaugusisha na lipsi zake na Caro akatulia kimya. Nikaupenyeza ulimi wangu taratibu katikati ya lipsi zake, taratibu Caro akafumba macho yake na hii ikawa nafasi yangu nzuri ya kuanza kumnyonya denda. Hisia kali zikapita katikati yetu na taratibu tukaanza kuingia ndani ya chumb hichi huku nikiufunga mlango. Nilivua tenge la Caro na likaanguka chini, huku nami nikivua taulo na kulitupia pembeni. Nikamlaza Caro kitandani huku nikiendelea kumnyonya denda. Nikashusha mdomo wangu hadi katika chuchu zake zilizo jazia vizuri. Nikaendelea kuzinyonya na kumfanya Caro kutoa miguno mfululizo ya kimahaba. Nikaipanua miguu yake na kuanza kumnyonya kitumbua chake.

“Aiiissiiiio….oo…a..iiia….”

Caro alilalama kiasi cha kunipandisha midadi kwani nina zaidi ya mwaka mzima na miezi yake simjui mwanamke na katika jeshi la waasi wa DRC nilijitahidi kujiweka biza kwa kujifunza mambo mengi sana ili kuyatoa mawazo ya kutembea na mwanamke.

“Nitie baby”

Caro alilalama mara baada ya kuzidiwa. Nikampaka mate jogoo wangu na taratibu nikamzamisha katika kitumbua chake.

“Aiiiiiii……ooooooo”

Caro alilalama huku akimsikilizia jogoo wangu aliye nona na mwenye urefu wa kutosha akisafiri katika kitumbua chake. Nikaanza kumpiga bokora za kisawa sawa, bakora za kutoa uchu wangu wa karibia mwaka mzima. Caro akafika hatu ya kulalama kuomba kupumzika ila bado nikazidi kumtandika bakora hadi nikamaliza mzunguko wa kwanza.

“Tuendele?”

“Hapana Rashidi, mshenzi una tomb** wewe haaaa. Sijawahi kutomb** hivi”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile. Yaani ume kojoa bado mbo** ime simama!!?”

Caro aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mwingi sana.

“Ndio, maana nakuambia niunganishe cha pili”

“Hapana kwa kweli, hapa kum** yote ina waka moto. Ehee ngoja nipumzike kwanza, uta nitomb** baade mpenzi”

Caro alizungumza huku akihema mithili ya mtu aliye kimbia umbali mrefu pasipo kupumzika. Tukapumzika kwa dakika kumi tu, uvumilivu ukanishinda, nikaanza kumchezea tena Caro hadi akalegea na safari hii kazi niliyo anza nayo ndio niliyo maliza nayo na dakika arobaini zilinitosha kabisa kumaliza mzunguko huu wa pili huku Caro naye katika dakika hizo arobaini akienda mizunguko mitatu.

“Rashidi asante sana. Haki ya Mungu nime pat ambo** sahihi inayo weza kunikuna hadi sehemu ambayo sijawahi kukunwa”

“Sehemu gani?”

“Mmmm naijua mwenyewe, una jua wengi walio nipitia walikuwa na vimb** vidogo vidogo au hata kama ana kubwa basi hawezi kuitumia. Ila wewe kweli mwanaume mashine yaani una isokomeza hadi kuna sehemu ina gonga, tiii, tiii, tiii”

“Hahaaa”

“Yaani hapa najiona mwepesi kama nimezaliwa jana. Yaani tuna kula kisha tuna rudi na kuendelea, leo nataka tupeane mambo hadi kila mmoja aridhike”

“Ila huu mtanange wa pili umejitahidi kwenda na kasi yangu kuliko wa kwanza”

“Wee wa kwanza ni sawa na gari jipya. Si una jua unapo pata gari jipya lazima kwanza ulisome na kulizoea, ukienda nalo pupa lina kuua. Ila ukilizoea sasa ndio una jua niende na spidi mia, mia mbili”

“Hahaa”

“Kweli, ila nisiwe mnafki wala muongo wewe una jua kutomb**. Una jua kumfanya mwanamke aende na mapigo yako, yaani umenikunja hukujali ukubwa wa umbo langu au kalio langu, ila ume nipelekesha kama ulivyo kuwa una nivuta kwenye swimming pool”

“Hahaa poa tuoge bwana tule. Nikija nikupe vitatu vya kulalia”

“Mmm vitatu nita vimudu, kama hivi ni dakika thelathini na je hivyo vingine si vitakuwa masaa”

“Acha woga”

Tukaoga kwa pamoja huku tukiwa tayari tumefungua ukurasa mpya wa mapenzi. Kitu cha pekee ambacho nina kiangalia kwa upande wangu ni kuhakikisha kwamba nina mpagwisha Caro kwa kadri ninavyo weza ili hata nitakapo hitaji kupata baadhi ya taarifa kuhusiana na raisi basi iwe ni jambo rahisi kwake kunipatia.Tukashuka sebleni huku kila mmoja akiwa amejifunga taulo. Tukala wali nyama aliyo pika Caro.

“Aisee wewe ni fundi kwenye mapishi?”

“Kweli?”

“Mama vile wewe fundi una jua kupika”

“Nashukuru, nita kuwa nina kupigia madiko diko hadi uchoke wewe mwenyewe”

“Haha nita shukuru sana”

“Hivi Rashidi una mchumba?”

“Hapana sina”

“Kweli?”

“Yaa kweli sina”

“Usinidanganye Rashidi nahitaji kutulia na wewe sawa kwa maana kile nilicho kuwa nina kitafuta kwa wanaume nime kipata kwako.”

“Usijali, ume kipata tena kwa mtu sahihi.”

“Kama ni hivyo nita muambia kaka kesho ikiwezekane nikakutambulishe kabisa. Nimetokea kutekwa na penzi lako Rashidi”

Nikatabasamu huku nikimtazama Caro kwani katika kumi na nane zangu amesha ingia.

“Nashukuru, kaka yako yupo mkoa gani?”

“Ohoo kaka yangu yupo hapa hapa Dar es Salaam, nilisahau kukuambia kaka yangu ndio raisi wa hii nchi”

Nikajikaza kuzuia mstuko wangu kwani kaka wa mke wangu ndio adui yangu aliye nipokonya mke wangu halali wa ndoa na kunipitisha kwenye maisha ya mateso ambayo sikutarajia kuyapitia kwenye maisha yangu siku hata moja.



“Waoo hongera sana Caro, kumbe raisi ni kaka yako?”

“Yaa ni kaka yangu wa tumbo moja. Yeye ndio wa kwanza na mimi ni wasabi kuzaliwa kwenye familia yetu na ndio mtoto wa mwisho”

“Sawa sawa. Nimeona kaka yako ame funga ndoa na mwanamke mwengine”

“Yeah ni kweli. Yule wifi yetu wa kwanza alikuwa ana zingua, waliachana kabisa kipindi ni makamu wa raisin a akampatia talaka na akavuta chuma kingine kibichiii”

“Haahaa”

Nilijichekesha kwa kujiakaza tu ila ukweli roho ina niuma sana.

“Kaka yangu ni mzee wa totos. Sasa yule naona ndio kampa mambo matamu hadi akaamua kumuoa kabisa”

“Sawa sawa”

Sikutaka mada hiyo iweze kuendelea kwa maana nina weza kushikwa na hasira inayo weza kumfanya Caro kujua kinacho niumiza. Tukamaliza kula na tukapiga mechi ya kibabe hapa hapa sebleni. Hakika usiku huu nikajitahidi kardri ya uwezo wangu kumridisha Caro. Asubuhi tukapata kifungua kinywa Caro akaniaga ana elekea kazini kwake nami nikamueleza ratiba yangu ya kuanzia saa nne asubuhi.

“Basi uta tumia ile Range Rover mume wagu”

“Mmm ila ni gari la kifahari sana hakuna aliye wahi kuniona na gari kali kama hilo”

“Acha zako Rashidi. Kwani wakikuona na gari hilo wata fanya nini, wata kuua?”

“Hapaa”

“Sasa, wewe tumia kila kitu changu sasa ni chako mume wangu wala usijibane bane unapo hitaji chochote kutoka kwangu”

“Sawa mpenzi ila mimi sio marioo”

“Hahaa jamani mume wangu sijakuita hivyo bwana”

“Poa”

Tukanyonaya denda kisha Caro akaingia kwenye gari linalo endesha na dereva wake na akaondoka eneo hili. Nikajiandaa kwa kila kitu majira ya saa nne nikaondoka nyumbani hapa kwa Caro nikiwa na gari lake. Nikaelekea moja kwa moja hadi ilipo kuwa nyumba yetu, nikashangaa sana kukuta gorofa moja la kifahari likiwa lime jengwa hapa huku kijumba chetu cha udongo kikiwa hakipo.

‘Ehee nani tena kashusha mjengo huu uswahilini huku?’

Nilijiuliza huku gari langu nikiwa nimelisimamisha mita chache kutoka lilipo jumba hilo. Baadhi ya nyumba za majirani nazo zipo kama nilivyo ziacha, kiufupi kilicho badilika ni jumba hili tu. Nikiwa nina endelea kutafakari nikaona watoto wa wiwili wa kiarabu wakitoka katika geti la jumba hilo huku wakiwa na vibaskeli vidogo. Nikavaa miwani yangu nyeusi pamoja na kofia, nikashuka ndani ya gari na nikatembea hadi kwa mama Chausiku ambaye ana biashara ya kuuza vifungua vinywa, vya kila aina.

“Habari”

Nilizungumza kwa sauti nzito kidogo.

“Salama kaka habari”

Nikagundua kwamba mama Chausiku hajanifahamu bado.

“Safi, nahitaji mihogo ya elfu kumi naweza kupata?”

“Ndio kaka yangu ila ni ya kusubiria, sijui una weza kukaa pale kwenye benchi.”

“Sawa”

Nikaka kwenye bechi lililopo hapa huku nikiendeleakuwatazama watu ambao kwa asilimia tisini nina wafhamau kwa maana ndio mitaa yangu ya kujidai.

“Hili jumba ni zuri ni jumba la nani?”

Nilizungumza huku nikimtazama mama Chausiku.

“Ni jumba la Muhindi mmoja, alinunua eneo hili kutoka kwa binti mmoja alikuwa ameolewa na kijana mmoja ana itwa Rashidi ila ninavyo sikia kwamba Rashidi alikuwa ni jambazi hivyo alikamatwa na kufungwa jela huko.”

“Kwa hiyo mke wake ndio aliuza hili eneo?”

“Ehee, yule binti sasa hivi ameolewa bwana na raisi wa awamu hii”

“Wee”

“Ndio na mama mkwe wake na mjukuu wake nasikia wameondoka kwenye mazingira ya kutatanisha”

“Duu”

“Yaani yule binti mshenzi sana, ila nina sikia kwamba mpango mzima wa hadi mume wake kusingiziwa kesi ni kutokana na huyo mke wake. Yaani yule kijana alikuwa ni mtu mwema sana, alikuwa mcheshi sana. Ila ndio hivyo wana wake wa Kitanzania sisi tukimpata mwenye pesa basi yule masikini mwenzatu tupo radhi hata kumtoa kafara ili mradi tu tuishi maisha mazuri”

“So una taka kuniambia kwamba jamaa alibambikiwa kesi?”

“Ndio, mimi huyo kijaa nina mjua toka alipo kuwa kijana mdogo kwa maana ni rika la mwanagu Chausiku. Japo alikuwa ni mkorofi ana magenge yake ya mtaani ila sikuwahi kusikia Rashidi ni jambazi na dakika za mwisho alikuwa ni mlinzi sijui kwenye kampuni gani ile”

“Duu pole yake”

“Yaani wanawake sisi wabaya sana.”

Mama Chausiki akaanza kutoa mihogo hiyo ndani ya sufuria.

“Una kula hapa au nikufungie?”

“Nifungie”

Mama Chausiku akaniwekea mihogo hiyo mia moja ndani ya mfuko mwusi.

“Kachumbari je?”

“Niwekee”

“Akaiweka na nikamlipa elfu kumi.

“Nashukuru sana baba yangu”

“Usijali, nita kuwa nina kuja kununua mihogo mara kwa mara”

“Asante sana”

Kwa mwaka muda mrefu nilio kaa mbali na huu mtaa karibia watu wengi hawajaweza kunifahamu kwani hadi mwendo wa kuembea nime badilisha. Nikaingia ndani ya gari huku hasira ikiwa imenijaa moyoni mwangu.

“Huyu malaya ameuza eneo la mama yangu. Anajua mama yangu alifanya kitu gani hadi akalipata hili eneo. Lazima nimuonyeshe mimi ni nani?”

Nikawasha gari na kuondoka eneo hili, nikatafuta nyumba ya kupanga katika mtandao na kw abahati nzuri nikapata nyumba eneo la Mbezi beach. Nikawasiliana na daliali, nikakutana naye na moja kwa moja tukaelekea katika nyumba hiyo. Nikalipa kodi ya mwaka mzima kisha nikaondoka eneo hili, nikapita katika maduka yanayo uza bidhaa za ndani ya nyumba. Katika siku hii hii nikajaza vitu vyote vinavyo hitajika ndani ya nyumba hii na majira ya jioni nikarudi nyumbani kwa Caro huku mchana nikishindia kula mihogo ya mama Chausiku.

“Baby am home”

Caro alizungumza huku akinifwata, tukakumbatiana huku tukipigana mabusu ya mdomoni.

“Pole na kazi mke wangu”

“Nina shukuru mume wangu. Vipi wewe mizunguko ime kwendaje?”

“Ime kwenda safi. Samahani sikukupigia simu”

“No hata mimi nina omba samahani kwa maana leo kuna mambo fulani ya kiusalama yaliniweka bize sana, nikahisi kwamba nikirudi uta kuwa umekasirika”

“No sijakasirika. Leo ninge penda sana twende kwangu”

“Woooo sawa, acha nioge kishwa twende”

“Ila habari njema ni kwmaba kule Kimara leo nime hama na nimehamia hapo Mbezi beach”

“Why umehama Kimara?”

“Ilikuwa ni plan yangu kabla hata hatujaonana, leo nime ona niikamilishe”

“Sawa hakuna tatizo itakuwa jambo jema tukaenda kuzindua nyumba mpya”

“Hahaa yaa”

Caro akaoga na kubadilisha nguo. Tukaelekea katika nyumba hii niliyo panga, japo sio ya gorofa ila ni nzuri sana na ipo pembezoni mwa habari.

“Waooo nimepapenda sana hapa mume wangu”

“Kweli?”

“Ndio, pametulia na huu upepo wa bahari basi una nifurahisha sana”

“Nashukuru kwa hilo kama ume pambena nilihisi uta hitaji jumba la gofora”

“No mimi kama ume nijua ni mtu ninaye penda kuishi maisha ya kawaida sana. Hata lile gorofa pale nilinunua kutokana na ile hulka ya kisichana kwamba rafiki azangu wakija wakute nina jumba zuri. Una jua zile wasichana, tuna penda kuonekana sana”

“Yaa ni kweli”

“So rate yake hapa ni bei gani?”

“Dola elfu mbili na mia tano kwa mwezi”

“Sio mbaya. Una onaje tuka ongea na huyo mwenye nyumba tukainunua kabisa iwe yako”

“Mmmm acha nikae kae kwanza. Nikiyapenda zaidi mazingira basi tuta mshawishi ila nisipo yapenda basi tita jenga au kununua sehemu nyingine”

“Sawa mume wangu nime kuelewa. Alafu leo nime zungumza na kaka na kumueleza juu ya mahusuano yetu amefurahi sana kwa maana alikuwa kila siku ana nisisitizia kwamba nielewe na nizae mapema kwa maana umri ndio una kwenda hivyo”

“Kuzaa ni swala la majaliwa ya mwenyezi Mungu na ndoa ni jambo muhimu na uamuzi mzuri kwenye maisha ya kila binadamu”

“Ni kweli, na pia nilimueleza kuhusiana na utofauti wa kidini kati yetu. Akanishauri kwamba ili kuto kuwa na mgongano wa maneno au maamuzi, ina bidi tufunge ndoa ya bomani, nikammuambi nita zungumza na wewe ukikubali mimi sinto kuwa na kipingamizi chochote.

“Naomba muda nilifikirie hilo jambo”

“Sawa mume wangu mimi sina neno”

Kadri siku zinavyo zidi kwenda ndivyo jinsi Caro alivyo zidi kukolea kwenye penzi langu na jambo la kumshukuru Mungu katika kipindi cha wiki mbili hizi za mahusiano yetu. Kaka yake amesafiri kikazi na kuelekea nchi za nje. Katika kipindi cha wiki mbili hizi kila siku nilijaribu kumdadisi kwa umakini sana Cauther kusuniana na kaka yake huku kisingizio changu kikubwa ni kwamba nina muogopa kwa maana kaka yake ni mtu mkubwa ndani ya nchi hii.

“Ngoja nikuambie mume wangu. Kaka yangu ni mkali pale anapo kuwa kazini. Ila kwenye maswala ya kifamilia ni mtu poa sana. Ni mtu anaye penda kujali na kuheshimu mawazo ya kila mtu. Una jua yeye kwetu ndio baba na mama, wazazi wetu walifariki miaka mingi sana hivyo yeye alitusomesha, akatulea hadi wengine tumefikia hapa hivyo usiwe na woga bwana”

“Mmm sikutarajia maishani mwangu kama ipo siku nita kuja kuwa namahusiano ya kimapenzi ma mdogo wake raisi”

“Ndio hivyo Mungu amekuletea. Alafu uzuri ni kwamba kaka yangu mara nyingu sana huwa hapendelei sana kutuweka front kama wadogo zake Ndio maana kweye maswala yake ya kisiasa amekuwa yeye kama yeye na sisi ni ngumu sana kujulika.”

“Hicho ndio kitu ambacho nina kipenda. Mara nyingi huwa sipendelei mapenzi yetu yajulikane kama ya wasanii hawa wa Bongo. Siku ya kuachana kila mtu ana kuwa na aibu kwa upande wake”

“Umeona ehee”

“Yaa. Vipi ana rudi lini?”

“Wiki ijayo, akitoka China katika dhiara yake ana rudi moja kwa moja Tanzania. Safari hii sikuambatana naye kwa maana kuna mambo ilinipasa kuyashuhulikia”

“Sawa mke wangu na pia tumepata muda wa kukaa pamoja na kujuana”

“Umeona ehee”

Maelezo ambayo Caro aliyo kuwa akinipatia kuhusiana na kaka yake kwangu ni msaada mkubwa sana, huku taratibu nikiendelea kupanga mpamgo wa kumuua raisi mara tu atakapo kanyaga nchini Tanzania. Katika muda ambao Caro ana kwenda kazini na hususani nikiwa nyumbani kwangu, ni nafasi yangu nzuri sana kuendelea kutengeneza mpango wangu madhubuti wa kumuua kaka yake na mke wake. Nikafanikiwa kuipata ramani nzima ya uwanaja wa taifa katika mtandoa unao itwa dark web. Mtando huu una tumiwa mara nyingi na wahalifu wa kidunia, mtandao ambao endapo ukibainika ume ingia basi mashirika makuu ya kijasusi kama FBI, Interpol na mengine lazima yakusake kuhakikisha kwamba wana kukamata. Katika mtando huu una weza kununua kila kitu cha kihalifu kwa bei ndogo sana.

Nikaanza kuikremisha ramani nzima ya uwanja wa ndege. Nilipo hakikisha kwamba nime ielewa vizuri, nikaifuta katika laptop yangu kwa ajili ya kulinda siri zangu. Caro akarudi mchana jambo ambalo sio la kawaida yake.

“Mume wangu nina safari ya kuelekea Arusha, nita kaa siku nne”

“Kuna nini?”

“Ni mswala ya kikazi”

Kutokana nina jua baadhi ya mambo ya kazi yake yana hitaji usiri, sikuhitaji kumuhoji sana Caro.

“Ila mume wangu mimi ndio nitakuwa nina kutafuta kwenye simu. Samahani kwa hilo si una elewa kazi zetu”

“Ndio mke wangu”

“Nita omba uweze kunisindikiza uwanja wa ndege kwa maana ina bidi niondoke saa tisa hii”

“Poa jiandae”

Kutokana hapa kwangu kuna nguo baadhi ya Caro. Akajiandaa na tukaianza safari ya kuelekea uwanja wa ndege.

“Yaani mume wangu nina waza mambo mengi sana”

“Mambo gani?”

“Hii kazi yangu sio ya kutulia sehemu moja. Hadi kuna muda nina hisi una weza kuniacha ukachoka kuvumilia”

“Wala usijali. Mimi ni muelewa kwa maana hata mimi kama nikianza safari zangu za Uganda, Congo zina weza kukufanya uwe una choka kunisubiri”

“Siwezi kuchoka”

Tukafika uwanja wa ndege. Caro akakutana na wafanyakazi wake wanne, nikakaa hadi nikawashuhudia wakipanda ndege nami nikapata muda wa kudhibitisha kile kiti nilicho kikremisha kwenye ramani ya uwanja huu ni sahihi. Maeneo yote ambayo ni rahisi kwa raia wa kawaida kupita bila ya tatizo lolote nika gundua kwamba ni sahihi na ramani niliyo isoma. Nikaondoka uwanjani hapa huku akili yangu ikzidi kwenda kasi sana. Nikamkumbuka Obote, nikafika nyumbani kwangu, nikaeleke eneo la ufukweni ambapo kuna upepo mwingi sana ambao hata kama ikokea kume fungwa kinasa sauti kinacho weza kunasa sauti umbali wowote basi hakiweza kunsa mazungumzo haya. Nikaweka mfumo katika simu yangu ambao mazungumzo yangu haya hayawezi kunaswa wala kurekodiwa na mtando huu wa simu ninao utumia. Nikampigia Obote huku nikiwa nimekaa kwenye jiwe kubwa lililopo hapa ufukweni na uzuri ni kwamba katika ufukwe huu hakuna watu wanao utumia.

“Hahari za siku ndugu yangu”

“Salama Rashidi ume nitupa”

“Sijakutupa ndugu yangu, ila nilikuwa nina tengeneza mazingira mazuri ya kuwepo hapa nchini”

“Ehee niambie ume fikia wapi?””

“Ahaa nina endelea kufanya upelelezi wangu ila nina jambo moja ambalo nina hitaji kujua”

“Niambie tu ndugu yangu”

“Hivi nina weza kupata daktari anaye weza kunifanyia oparesheni na kuniwekea sura bandia?”

“Ndio wapo wengi sana na ninao wafahamu. Kuna daktari mmoja bingwa yupo nchini Canada akam uta hitaji nita kuunganisha naye”

“Nita shukuru sana ndugu yangu kwa maana ninahitaji sura nitakayo weza kuifanyia kazi huku nikiwa nimebaki katika sura yangu ya kawaida”

“Samahani sijakuelewa kidogo. Una hitaji sura ya kuvuka au sura ambayo uta kaa nayo kwa muda mrefu.?”

“Nahiyaji sura ambayo nina weza kuvaa na kuivua”

“Ngoja kwanza ndugu yangu nina kupigia baada ya dakika kama tano hivi”

“Sawa kaka”

Nikakata simu huku nikimsubiria Obote anipigie. Baada ya dakika tano kweli Obote akanipigia.

“Aisee ndugu yangu wewe ni kijukuu cha mtume”

“Kwa nini?”

“Nime pokea habari haapa kwamba raisi wa nchini kwako. Kesho kutwa ata pita nchini kwangu kwa kuja kunipa pongezi akitokea chini hivyo uchaguzu ni wako. Umalize kazi yako akiwa hapa DRC au usubirie akirudi nchini Tanzania”

Nikatabasamu huku furaha ikinijaa moyoni mwangu kwani kama nikimuua hapa nchini Tanzania ita niwia ugumu sana kwa mimi kutoka hapa nchini ila nikimuulia nchini DRC basi ita kwua ni msala wa Obote na serikali yake.



“Kaka nini kuja hapo ni nyumbani”

“Karibu sana”

“Nashukuru”

Nikakata simu na kuanza kushangulia kwa furaha zote. Nikarudi nyumbani kwangu na kuanza kuweka vitu muhimu katika begi langu la nguo. Nikaanza kupiga mahesabu ya haraka hara kwa safari ya kutoka China hadi DRC ina garimu masaa mengi sana kuweza kufika.

‘Ina bidi niende hadi Kigoma kwa ndege ya kukodi’

Niliwaza kimoyo moyo. Nikiwa katika dimbwi la mawazo simu yangu ikaanza kuita, nikaitazama na kukuta ni Caro.

“Honey”

“Niambie mume wangu”

“Safi vipi?”

“Safi tume fika”

“Pole kwa safari”

“Nashukuru na pia wala sio safari ndefu”

“Mke wangu nina safari ya kuelekea Uganda, kuna mzigo umeingia kwa wale wauzaji wezangu. Hivyo nime pigiwa simu kama lisaa na nusu lililo pita hapa ndio nina fikiria niondoke na ndege au basi”

“Ahhaa ni biashara ya haraka?”

“Ndio mke wangu”

“Basi ondoka na ndege. Ukitumia basi ita kugarimu masaa mengi sana”

“Sawa mke wangu”

“Ila kuwa makini mume wangu”

“Usijali nipo makini sana”

“Sawa nikutakie safari njema”

“Nashukuru. Funguo nina iacha pale nilipo kuwa nime iweka”

“Poa mume wangu, kama nikiwahi kurudi uta nikuta nyumbani kama ukiwahi kurudi basi nita kukuta nyumbani”

“Poa mke wangu, ninakupenda”

“Nina kupenda pia mume wangu”

Nikakata simu, nikafunga nyumba yangu na nikaondoka pasipo kutumia gari. Nikafika eneo la waendesha pikipiki, nikapanda pikipiki na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza. Nikafika uwanja wa ndege, nikamlipa dereva kisha nikaelekea katika moja ya shirika la ndege ndogo. Nikafwata hatua zote za kukodisha ndege binafsi na safari ya kuelekea mkoani Kigoma ikaanza mara baada ya kumaliza kuwalipa kila walicho kihitao. Majira ya saa mbili usiku, nikafika wanja wa ndege Kigoma. Nikatoka uwanjani na nikakodisha taksi ambayo moja kwa moja ikanipeleka hadi katika ziwa Tangayika. Nikakodisha boti ambazo zina fanya safari haramu ambazo hupita maeneo ambayo hakuna kizuizi cha askari wa majini hususani askari wa nchi ya Tanzania. Safari ikaanza huku njiani nikiwasiliana na Obote na akaniahidi nikifika tu ufukweni nita kuta helicopter na wanajeshi wata nipokea. Safari ikatugarimu masaa nane na nikafika ufukweni, nikapokelewa na wanajeshi ambao nina fahamiana nao vizuri. Tukaingia ndani ya helicopter na safari ya kuelekea ikulu ikaanza.

Saa moja asubuhi tukafika ikuku, na moja kwa moja nikaelekea eneo analo ishi raisi hapa ikulu na kumkuta Obote akiwa na mlinzi wake.

“Karibu sana Rashidi”

“Asante sana ndugu yangu”

Tukasalimiana kwa kukumbatiana, nikakumbatiana pia na raisi huyu.

“Naona Tanzania kume kupenda. Una ng’ara na una pendeza”

“Hahaa kiasi chake. Ehee niambie huyu mjinga ana kuja kweli?”

“Ndio na tayari mapokezi yake yata fanyika hapo kesho”

“Aisee hii ni golden chance kwa kweli, sihitaji kuipoteza”

“Usijali. Ila una paswa kuwa makini makini tena sana. Kumbuka endapo ata fia hapa nchini kwangu basi kuna uwezekano wa asilimia sabibi ya nchi za umoja wa Afrika kuniwekea vikwazo na tukarudi katika vita jamboa ambalo kwa sasa sihitaji kulizikia katika nchi yangu”

Obote alizungunmza kwa msisituizo.

“Usijali ndugu yangu, nita jua nini cha kufanya”

“Rashidi nakusisitizia hili kwa maana una elewa haya mambo yanavyo kwenda. Sihitaji nchi yangu kuingia doa, nimesha anza kutengeneza urafiki na baadhi ya nchi za Kiafrika na kama umeona jamaa amejuja basi tambua kwmaba nime tengeneza mahusiano mazuri”

“Usijali ndugu yangu. Vipi ametuma wapelelezi wake?”

“Ndio ametuma tumu ya wapelelezi wake wakiongozwa na binti mmoja anaye itwa Caro”

“Caro”

“Ndio ni mmoja wa walinzi wake wa siri sana. Aisee ni mtoto bomba sana, yaani nina mmezea mate kweli kweli”

Nikashusha pumzi kwa maana sihitaji wajue chochote kwamba mimi na Caro tuna mahusiano.

“Okay”

“Jana usiku waliripoti hapa ikulu. Hivyo maandalizi ya eneo ambalo raisi ata lala na kufikia tayari yamesha andaliwa.”

“Ana kaa kwa muda gani?”

“Ameniambia ata kuwa na ziara ya siku mbili kwa maana ana hitaji kuboresha mahusiano ya Tanzania na DRC yazidi kuwa mazuri”

“Okay sawa sawa”

“Ume jipanganye kwenye kazi yako?”

“Nita kupa jibu mara baada ya kutambua watu alio ongozana nao wana uwezo gani na uimara gani”

“Sawa nina kuelewa mr plan”

“Hahaa”

Nikapata kifungua kinywa pamoja na Obote, nikakabidhiwa chumba changu hapa hapa ikulu. Kwa kupitia Obote kila nilicho muuliza kuhusiana na eneo ambalo raisi ata fikia na kutembelea hakusitia kuniambia. Nikiwa katika upelelezi wangu nika muona Caro akiwa emongozana na vijana wake.

‘Huyu mwanamke mshenzi kweli. Kwa hiyo alinipiga changa la macho?’

Nilizungumza huku nikiwa nimekaa kwenye moja ya eneo ambo lipo karibu kabisa na hoteli ambayo raisi ata lala.

‘Nita muonyesha kwamba mimi ni nani?’

Nikaingia ndani ya gari alilo nipatia Obote na nikarudi ikulu.

“Ndugu yule daktari nina weza kumpata kweli?”

“Duu tena una bahati. Ameingia asubuhi ya leo hapa DRC na nimepanga majira ya jioni nikutane naye”

“Basi muombe nionane naye ikiwezekana nitengenezewe sura ya bandia. Si una jua adui yangu ana nifahamu na pia nita hitaji kuwa mshauri wako wa karibu kwa adui yangu. Nina jua kuna baadhi ya mambo ata hitaji kukushawishi kwa ajili ya manufaa yake binafsi”

“Usijali”

Obote akanyanya mkonga wake wa simu na akampigia daktari amabaye baada ya dakika hamsini akafika ikulu hapa akiwa na vifaa vyake vya kazi kw amaana Obote tayari alisha mueleza katika simu. Hatkuhitaji muda wa kupotea na kazi ya kutengenezewa sura ya bandia ambayo daktri ameniambia kwamba haifananii na mtu yoyote, ikaanza. Mara baada ya sura hiyo kumaliza kutengezwa katika kifaa ambacho daktari ana kijua mwenyewe, akaanza kunibandika sura hii kwa kutumia gundi ngumu sana ambayo sio rahisi kwa mtu kuweza kuijua kwamba nina sura bandia. Hadi inafika saa moja usiku kazi ikakamilika, si Obote tu aliye nishangaa kwa kubadilika hata wanajeshi wengine nao wakakiri kwamba nime badilika.

“Ume kuwa tofauti kabisa ndugu yangu. Kwa sura hii kwa kweli hakuna anaye weza kukufahamu”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile. Ndio maana nilikuambia kwamba hii huyu daktari sio wa kawaida.

“Nashukuru sana ndugu yangu”

Nikapiga picha za passport size kwa jaili ya kutengenezewa kitambulisho changu kama raisi wa DRC pamoja kitambulisho kinacho nionyesha kwamba mimi ni mshauri wa raisi. Huku jina ninalo litumia ni Sudy S. Sudy.

“Naamini sasa umesha pata wazo la nini una hitaji kukifanya?”

“Yaa nime pata na nina imani kwamba kama ni kumuua basi hato fia kwenye nchi yako. Ila ata fia akiingia nchini Tanzania”

“Eehee niambie”

“Nita hitaji sana tena sana umuombe raisi wa Tanzania uitazama ndege yake ili nawe ikiwezekana ununue ndege kubwa kama ndege yake. Baada ya hapo mimi nita tengeneza kikombe maalumu cha raisi kwa maana katuka ndege raisi kuna vikombe maalumu kwa ajili ya raisi kunywea chai au kahawa. Katika kikombe hicho, nita kiwekea bomu maalumu ambalo hakuna hata mty atakate wazia kwamba bomu hiko lime wekwa ndani ya kikombe. Nita itrack ndege, ikisha tua tu katika uwanja wa ndege Dar es Salaam basi nita ilipua ikiwa katika run way. So sio wewe wala nchi yako itakayo husika katika ajali hiyo.”

“Aisee wewe ni genius kwa hiyo plan nime kuelewa. Sasa hivyo vikombe una vifahamu?”

“Ndio, nilisha fanya upelelezi wangu wa ndege nzima ya raisi hadi kufahamu kikombe hicho”

“Kukiingiza uta kiingizaje ndani ya ndege hiyo kwa maana ulinzi una weza kuwa ni mkali sana”

“Hilo niachie mimi”

“Sawa”

Tukapata chakula cha usiku na nikaingia ndani kwangu na kuanza kukagua picha moja baada ya nyingine, niliyo piga maeneo tofauti tofauti ambayo raisi wa Tanzania ata pita. Nikaitazama picha ya Caro akiwa katika eneo nililo muona.

‘Haya bwana mama mpelelezi’

Katika kipindi cha makomandoo kutoka Russia walivyo kuja hapa DRC kutupa mafunzo, nilijiunga nami kwenye kitengo cha utengenezaji wa mabomu. Hivyo nilijifunza kutengeneza mabomu ya kila aina.

“Kikombe kina weza kugundulika”

Niliwaza huku nikichanganyua nini nifanye.

“Bomu la kalamu ni zuri zaidi”

Nilizungumza huku nikitabasamu. Nikaingia katika mtandao na kutafuta kalamu inayo tumiwa na raisi wa Tanzania na nikazipata picha kalamu hizo. Nikatoka ndani kwangu na kuelekea moja kwa moja ndani kwa Obote. Nikamgongea na akaniruhusu kuingia ndani.

“Samahani ndugu yangu nime kusumbua”

“Wala usijali ehee niambie’

“Aisee hizi kalamu hapa Congo nita zipatia wapi?”

Nikamuonyesha Obote picha ya kalamu hizi. Akazitazama kwa sekunde kadhaa.

“Nahisi ninazo mbili ofisini kwangu. Moja ni mpya kabisa sija zitumia”

“Kweli?”

“Ndio, ila ni za nini?”

“Nahitaji kutengeneza bomu la kalamu. Bomu ambalo raisi yeye mwenyewe ata ingia nalo ndani ya ndege pasipo yeye mwenyewe kujua”

“Plan ya kikombe ime kufa?”

“Yaa ime kufa”

“Basi twende nikakupatie”

Tukatoka ndani hapa na kuingia ofisini kwa Obote. Akanipatia kalamu ambayo ina fanania na kalamu inayo tumiwa na raisi wa Tanzania.

“Shukrani sana ndugu yangu”

“Usijali”

Nikarudi chumbani kwangu na nikaanza kutengeneza bomu hili huku vifaa vyote nikiwezeshwa na Obote. Hadi kuna pambazuka ndio nina kamilisha kazi hii inayo hitaji umakini na maarifa ya hali ya juu sana. Bomu hili nime litengeneza kwa mifumo miwili ya ulipukaji. Mfumo wa kwanza, endapo kifuniko cha kalamu hii kikifunguliwa basi lina lipuka na mzinga wake sio wa kitoto. Mfumo wa pili ni kulilipua kwa kutumia simu yangu ya mkononi hata kama itakuwa mbali sana na mimi. Mlango wa chumbani ukagongwa, nikasimama na kuufungua.

“Za asuhi ndugu yangu Sudi”

“Hahaaa ua niita Sudi”

“Ina bidi nilizoee jina lako jipya”

“Karibu ndani”

“Nashukuru”

Obote akaingia ndani hapa.

“Naona kitanda hakijaguswa”

“Sijalala kabisa ndugu yangu. Nimefanikiwa kutengeneza bomu hili”

Nikamuonyesha Obote kalamu hii na jinsi bomu linayvo fanya kazi na endapo likilipuka basi lina lipuka kwa uwezo gani.

“Aisee ina bidi awe makini sana kwa maana akifungua kalamu na yupo na sisi tume kwenda baba”

“Hahaa hawezi kwa maana nina imani nita ichanganya”

“Rashidi, tusije na sisi tuka fumuka na bomu lako”

“Hahaaa usiwe muoga ndugu yangu”

“Ingieni”

Obote alizungumza na wakaingia wasichana wawili wakiwa wameshika mifuko maalumu ya kuhifadhia suti.

“Raisi ata fika hapa saa nne asubuhi hivyo saa tatu ina bidi tuwe timesha fika uwanja wa ndege. Jiandae utachagua suti moja kati ya suti hizi mbili”

“Sawa kaka”

“Wata kuhudumia kwa kila kitu unacho hitaji. Sasa hivi ni saa kumi na mbili asubuhi. Hakikisha hadi saa tatu una uwa umesha maliza maandalizi yako”

“Sawa”

Obote akatoka ndani hapa na wasichana hawa wakavua nguo zako na kubaki kama walivyo zaliwa.

“Ahaa jamani sihitaji kufanya mapenzi asubuhi hii. Wekeni suti hizo hapo na tokeni hapa ndani”

Nilizungumza kwa kujikaza kwani akili yangu sasa hivi ina fikiria kazi iliyopo mbele yangu japo kama mwanaume jasiri nina tamani kweli kuwalala hawa wasichana kwa maana maumbo yao yamechongeka kisawa sawa.

“Usiku mutakuwa wageni wangu sawa”

Niliwaambia wasichanna hawa huku wakivaa nguo zao na wakatoka ndani hapa. Nikajipumzisha kwa lisaa moja na saa mbili kamili nikaamka. Nikachagua suti ya kuvaa, nikachagua suti hii nyeusi, nikaingia bafuni na nikaoga kisha nikajiandaa. Nikaiweka lakamu hii katika mfuko wa ndani wa koti la suti, nikabeba na vitambulisho vyangu na kutoka ndani hapa. Tukapata kifungua kinywa na Obote na saa tatu kasoro tukaondoka ikulu huku msafara ukiwa ni mrefu sana na wa magari ya kifahari na ulinzi ni mkali sana. Ukimya ume tawala katika gari hili nililo panda mimi, Obote, mlinzi wake pamoja na dereva.

“Mbona una mawazo kaka”

Nilimuuliza Obote huku nikimtazama usoni mwake.

“Nina muwaza yule demu”

“Demu gani?”

“Yule mlinzi wa raisi wa Tanzania, anaye itwa Caro. Unajua ain aya wanawake wale mimi ndio ninao wapenda”

“Weee”

“Haki ya Mungu vile”

“Daaa sasa ina kuwaje?”

“Ndio nina fikiria leo kwenye halfa ya chakula cha usiku nikae nay echini nimpe maneno matamu matamu. Akikubali nina oa”

“Jitahidi ndugu yangu kwa maana kwenye upande huo sihitaji kuingia sana”

“Hahaa nina kujua hependi mademu ndio maana hata leo hii wale uliwafukuza”

“Hahaa nipo kikazi kaka”

“Sawa”

Tukafika uwanja wa ndege na kukuta wananchi wengi wakiwa wamefika kwa ajili ya kumpokea rasi wa Tanzania. Ngoma za asili zina pigwa na wacheza ngoma ambao wamevalia kiasilia huku wanajeshi walio valia sare nzuri wakiwa wamesimama kwenye mistari sita iliyo nyooka. Raisi Obote akawapungia mikono wananchi wote walipo eneo hili kisha tukaaa kwenye jukwa maalumu lililo andaliwa kwa ajili yetu.

“Rashidi”

“Ndio kaka”

“Kumbuka kwamba nita kutambulisha kwa jila la Sudi S. Sudi”

“Sawa kaka”

Tukaendelea kuburudishwa na ndoma hizi za wana sanaa huku mimi nikiwa nime kaa kiti cha nyuma ya raisi Obote. Muda wa raisi wa Tanzania kufika nchini Congo ukawadia, ndege kubwa mithili ya ndege ya raisi wa Marekani, ikaanza kutua kwa kasi katika uwanja huu. Shangwe zikazidi kutawala katika kiwanja hichi.

“Aisee jamaa ana ndege kubwa”

Obote alininong’oneza sikioni mwangu huku tukiwa tuna elekea katika zulia jekundu.

“Ndio hivyo ndugu yangu”

Nikamuona Caro akiwa na walinzi wezake huku wakiwa makini sana kuhakikisha kwamba raisi ana kuwa salama. Ndege ikasimama eneo la zulia jekundu, ngazi ndefu zikawekwa usawa wa mlango wa ndege ya raisi. Baada ya maandalizi yote kukamilia raisi wa Tanzania akatoka ndani ya ndege hiyo huku akiwa amemshika mkono mke wake. Akafika ngazi ya chini na akapokelewa na mwenyeji wake huku wakipena mikono na kukumbatiana. Mke wa raisi ambaye ni mama Shamsa akakabidhiwa zawadi ya maua na mabinti wawili walio andaliwa kwa kazi hiyo na maua hayo akamkabidhi mlinzi wake. Raisi Obote akaanz akumtambulisha raisi wa Tanzania kwa makamu wake wa raisi wake kisha akafika kwangu.

“Huyu ni mshauri wangu namba moja ana itwa Sudi S. Sudi”

Nikapeana mkono na raisi wa Tanzania ambaye ni adui yangu kisha kipaeana mkono na mke wake na kujikuta hasira ikianza kunitawala kifuani mwangu kwani mwanamke huyu kwa kweli amevuruga maisha yangu kwa kiwango cha hali ya juu sana hadi nikatamani kujilipua pamoja naye kwa kutumia kalamu hii iliyopo mfukoni mwangu.



Nikatabasamu kujitahidi kuzuia hasira yangu. Nikauachia mkono wake na raisi Obote akaendelea na utambulisho kwa viongozi wengine alio ambatana nasi. Sisi wengine tukarudi katika sehemu za kukaa huku raisi Obote na raisi wa Tanzania wakikagua vikosi vya jeshi vilivyopo hawa uwanja wa ndege. Watu wote tulio kaa tukasimama na nyimbo za mataifa yote mawili zikapigwa kisha, viongozi wote wakaingia ndani ya magari huku mimi nikipanda katika gari jengine tofauti na gari la raisi na safari ya kuelekea ikulu ikaanza huku akilini mwangu nikipangilia mambo mengi ya kumfanya huyu raisi. Tukafika ikulu, raisi Obote na raisi wa Tanzania wakaingia katika ofisi ya raisi kwa ajili ya mazungumzo ya wao peke yao huku walinzi wa Obote na walinzi wa raisi wa Tanzania wakiwa nje ya ofisi hiyo kuimarisha ulinzi. Baada ya dakika kumi za mazungumzo wakatoka ndani hapa kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa habari. Muda wote haya yakiendelea macho yangu yapo makini sana kwa walinzi wa Tanzania hususani Caro ambaye ni mwanamke wangu.

“Nchi yetu ya Congo imepata ugeni mkubwa sana, kwanza nimshukuru ndugu yangu raisi Ibrahim kwa kweli ni ameonyesha ni jinsi gani na namna gani ambavyo ana penda kuhakikisha kwamba ujirani wetu kati ya DRC na Tanzania una zidi kuimarika.”

Raisi Obote alizungumza huku akimtazama raisi Ibrahim.

“Ni mambo mengi sana ambayo nime zungumza naye na tumepanga kushirikiana kwa nchi hizi mbili ikiwemo kuongeza ulinzi katika ziwa Tanganyika kwa maana ni watu wengi sana wana litumia ziwa hilo kwa kusafirisha silaha, kuvuka kuingia nchi moja hadi nyingine kinyume na taratibu na pia uvuvi haramu. Hivyo nimkaribishe ndugu yangu kwa ajili ya kuzungumza mambo kadhaa.”

Raisi Obote mara baada ya kuzungumza mambo hayo. Raisi Ibrahim akaanza kuzungumza.

“Nina furaha kubwa sana kwa kuwa hapa. Ni watu wengi wana chukulia mapinduzi ya nchi ya CONGO kama uasi ila kwa jinsi ninavyo muelewa ndugu yangu Obote, ni mtu sahihi wa kuiongoza hii nchi kwa maana ana iongoza nchi hii kwenye misingi na taratibu na nina imani kwa asilimia kubwa kwamba ata wavusha wananchi wa DRC kutoka hapa walipo na kuwapeleka katika maisha ya juu ambayo kila mwananchi ata yarufahia.

“Nimekuja DRC ukiachana na kumpongeza tu ndugu yangu raisi Obote. Ila pia kwa pamojana nina imani tuta endelea kudumisha urafiki kati ya Congo na DRC kwa haya machache nina penda sana kuwashukuru kwa kunikaribisha vizuri na nina imani kwamba ziara yangu ya siku mbili itaenda vizuri. Asanteni sana”

Msemaji wa serikali wa ikulu akakaribisha maswali mawili kutoka kwa waandishi wa vyombo vya habari kutoka mashirika mbalimbali ndani na nje ya nchi ya Congo.

“Mimi nina itwa Amina Rajab, kutoka shirika la BBC London. Swali langu ni kwako raisi Obote. Katika kuipindua serikali iliyo toka madarakani. Katika habari za ndani tume sikia kwamba ulimbaka mke wa raisi aliye pita mbele ya mume wake na ukamuua je hilo ni kweli?”

Swali hilo likanistusa sana nikamtazama raisi Obote na kumuona akitabasamu.

“Hhahaaa hizo ni propaganda zinazo endelea kutengenezwa na vyombo vya magaribi. Ila ukweli ni kwamba raisi aliye pita madarakani alikimbia yeye na familia yake baada ya kuona ikulu ime vamiwa na hajauwawa na tukio la kidhalilishaji kama hilo halijawahi kutokea kabisa. Swali jengine”

Kwa jinsi Obote alivyo jibu swali hili, amelijibu kisiasa ila kw ajinsi ninavyo mfahamu ni dhairi kwamba swali hili lime mchukiza seme tu ana onyesha kujikaza.

“Nina itwa Mandingo nime okea shirika la utangazaji la taifa. Muheshimiwa raisi ni lini tuta mfahamu first lady kwa maana Wacongo wengi tuna tamani sana kuweza kumfahamu”

“Hahahaa niombeeni kwa Mungu, atakapo patikana kila mtu ata mfahamu. Asanteni sana”

Baada ya mazungumzo ya waandishi wa habari kuisha. Tukajumuika katika meza ya chakula huku ni watu wachache sana kutoka katika serikali ya nchi hii ya Congo kupata nafasi ya kula na maraisi hawa wawili.

“Chakula ni kitamu sana”

Raisi Ibrahim alizungumza huku akiendelea kula.

“Shukrani sana ndugu yangu”

“Ina bidi uoe shemeji”

Mke wa raisi Ibrahim, mama Shamsa alizungumza.

“Hahaaa usijali shemeji, safari nyingine utakapo kuja uta kutana na mke mwenzio. Tena nina penda sana kuoa huko Tanzania”

“Wooo ni wazo zuri sana ndugu yangu. Karibu sana upate mke Tanzania kwa maana ni nchi ambayo ina wanawake wazuri kama hawa”

“Hahaa ni kweli hata mimi mwenyewe nina ona. Alafu kuna msichana mmoja nime muona kati ya walinzi wako wa kike, nisiwe muongo kwa kweli nime mpenda sana tena sana”

“Nani huyo?”

Raisi Ibrahim alizungumza huku akitabasamu.

“Anaitwa Caro”

“Ooohooo alafu nilishindwa kukuambia Caro una jua ni mdogo wangu wa tumbo moja”

“Weee!!”

“Haki ya Mungu vile ndio last born katika familia yetu.”

“Aisee kwa hiyo undugu una weza kuzidi kuunganishwa?”

“Ndio tena ni jambo zuri sana. Ukimuoa nina imani hata yeye mwenyewe atajawa na furaha kubwa sana.”

Mama Shamsa akamnong’oneza mume wake.

“Ila kabla ya yote ita bidi tuzungumze naye kisha tukukutanishe naye”

“Hakuna shida ndugu yangu. Mimi nipo tayari kwa lolote lile. Nimempenda sana Caro”

“Usijali ndugu yangu kila jambo lita kwenda vizuri”

Kwa upande mmoja roho yangu ina niuma sana kuona kila mwanamke ninaye kuwa naye ana chukuliwa na raisi, ila kutokana nina familia yangu, kidogo wivu kwa Caro ni mdogo kuliko ulivyo kuwa kwa mama Shamsa ambaye nilimpenda kwa moyo mmoja pasipo kuiona hatari iliyo kuwa mbele yangu.

“Sawa tuta lizungumza hili”

Tukamaliza kupata chakula cha mchana na tukaingia katika kikao cha kujadilia kuhusiana na maswala ya kushirikiana katika ulinzi wa kulinda ziwa Tanganyika huku tulio ingia katika kikao hichi tukiwa ni washauri wa mariai pekee na hata walinzi wa maraisi wabebaki nje.

‘Hapa ni lazima nimbadilishie kalamu’

Niliwaza kimoyo moyo huku nikitazama jinsi viongozi wanavyo jiandaa kwa ajili ya mazungumzo.

“Serikali yako raisi uliye mpindua tulijaribu kuzungumza naye ila kwa bahati mbaya hatukuweza kufikia muafaka kwa kipindi kile nilikuwa ni makamu wa raisi kama una kumbuka”

“Nina kumbuka ndugu yangu”

“Nina imani kwa pamoja tuna weza kuzifikisha ndoto za nchi zetu katika maeneo amayo yana paswa kufika”

“Ndio ndugu yangu. Nchi yangu ya Tanzania ipo tayari kutoa wanajeshi mia mbili wa majini katika kuimarisha ulinzi”

“Hata mimi nita toa idadi hiyo hiyo, pia tupige marufuku uvuvi haramu una endelea na kwa kipindi cha mwaka mmoja tuhakikishe tuna acha samaki wana zaliana na wana kuwa ni wengi”

“Hilo halina shaka lime pita. Pia nimepata wazo moja, una onaje wanajeshi wetu wakawa wana pata mafunzo ya kijeshi hii ita zidi kuimarisha ulinzi wa nchi zetu mbili.”

‘Mkuu hapo una jiingiza kingi. Watatuma wapelelezi wao ambao ni wanajeshi wata idadisi hii nchi na wata zoa kila aina ya mali iliyopo ndani ya nchi yako’

Nilimshauri kwa kumnong’oneza Obote.

“Hilo la wanajeshi wetu kushirikiana ni jambo zuri, ila ninge penda sana tupeane muda katika hilo”

“Hakuna shaka ndugu yangu. Nina jambo moja ninge penda kulifahamu kwa maana lilitokea kipindi cha nyuma kidogo.

“Ndio ndio”

“Kuna muhalifu wangu mmoja nilimleta hapa nchini kwako ila kwa bahati mbaya alitoroka gerezani na ina sakikika kwamba alikamatwa na viana wako kipindi bado mupo porini, je una lifahamu hili?”

“Hapana kijana ana itwa nani?”

“Rashidi”

“Sina habari hizo ila kwa vijana wote wanao kamatwa waliuwawa”

Nikajikaza kuto kuonyesha mstuko wangu.

“Sawa samahani kwa kukuuliza swali hilo ambalo kwa namna moja ama nyingine ni nje ya mada yetu”

“Usijali ndugu yangu”

Kikao hichi kifupi kikamalizika na raisi Ibrahim akaelekea katika eneo la kupumzika kabla ya halfa itakayo fannyika usiku.

“Mshenzi bado nipo kichwani mwake yule”

Nilimuambia Obote mara baada ya kuingia ofisini kwake.

“Kwani hilo la mke tu ndio ana kufanya akuwinde hivyo?”

“Ndio”


ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

BLOG